Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live

JPM Sio Mtu wa Mchezo.. Afunguka"Huyo Nitalala Naye Mbele Mwenyewe"

$
0
0
Rais Magufuli amewataka Wakulima na Wafugaji kuacha vitendo vya kupigana na kwamba katika serikali yake hakuna mtu aliyeko juu zaidi ya mwingine na kusisitiza kwamba watanzania wote ni sawa kwani ndiyo waliyomchagua.


Akizungumza na wananchi wa Morogoro akiwa njiani kuelekea Msamvu Raid Magufuli amesema kwamba kamwe vitendo vya kupigana visirudie katika serikali yake na kwamba wale watakaokiuka watashughulikiwa.

Aidha ameongeza kuwa anataka wakulima na wafugaji waishi kwa kuheshimiana kwani yeye anachokihitaji ni amani.

Pamoja na hayo, Rais Magufuli amewashangaa Wafugani kuwalisha ng'ombe mazao ya wakulima ilhali kuna majani ya kutosha na wanaposhtakiwa wanaamua kutumia gharama kubwa kuhonga hata kufikia hatua ya kuuza ng'ombe.

"Mimi nimekaa kwa wamasai Monduli, nimechunga mpaka ng'ombe za wamasai nikiwa JKT Makuyuni. Ni watu wazuri tu. Sasa kwanini wamasai wa huku wanachukia mali za wengine wakulima? Nataka niwaaeleze nitalifuatilia hili.

Pamoja na hayo ameongeza "Kama yupo mmoja ambaye analiisha kila siku anajifanya ana mali huyo mimi ndiye ntalala naye mbele mwenyewe".

Mtazame hapa chini


"Huyo nitalala naye mbele mwenyewe" - JPM

HATARI Sana...Waziri wa Mambo ya Ndani apigwa risasi

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani Pakistan, Ahsan Iqbal (59) amejeruhiwa baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana wakati akiwa katika mkutano wa kampeni za uchaguzi katika jimbo la Punjab.


Kwa mujibu wa vyanzo vya habari mbalimbali vinasema kuwa Waziri huyo amejeruhiwa katika bega lake la kushoto kufuatia risasi moja kumpata ambazo zilikuwa zikifyatuliwa na kijana ambaye mpaka sasa hajafahamika.

Hata hivyo msemaji wa huduma za uokoaji Jam Sajjad Hussain amedai kuwa Waziri huyo alifanikiwa kuingizwa kwenye gari yake na kutoka katika eneo hilo aliloshambuliwa  na kumpeleka hospitali kwa matibabu zaidi.

Mbali na hilo mtoto wa Waziri huyo amesema kuwa baba yake hajapata majeraha makubwa ambayo yanatishia maisha yake hivyo ni majeraha ya kawaida ambayo anaendelea kutibiwa na madaktari.


UBISHOO Wamponza...Atumbukia Mtoni na Kufariki Akijipiga 'Selfie'

$
0
0

Kijana mmoja ambaye hakujulikana jina mara moja nchini Nigeria amefariki dunia baada ya kutumbukia mtoni wakati akijaribu kujipiga picha kwa simu maarufu kama 'Selfie'.


Tukio hili limetokea eneo la Nembe katika mji wa Bayelsa, ambapo kijana huyo alikua anajaribu kupiga picha ya mwisho ya kumbukumbu katika chuo cha mafunzo ya usalama NYSC.

Wakisimulia tukio hilo baadhi ya mashuhuda wamesema kwamba mtu huyo aliteleza kwa bahati mbaya wakati walipokuwa amesimama eneo la “Jetty” katika mto huo na kutumbukia mtoni.

Mwili wa kijana huyo ulipatikana dakika 30 baada ya kuzama na hakuna taarifa za kumtambulisha mtu huyo.

Mamlaka za mji huo zimeshindwa kumtambua mtu huyo na hakuna ndugu wala jamaa ambaye amekwisha jitokeza hata baada ya picha za mtu huyo kusambaa katika mitandao ya kijamii.

FREEMAN Mbowe "Imeniwia Vigumu Sana Kumpa Pole Mbunge Heche Kwa Kifo cha Mdogo Wake"

$
0
0
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amefunguka na kusema kuwa kwa siku kadhaa zilizopita amekuwa katika wakati mgumu na kushindwa kuelewa neno gani anaweza kumpa Mbunge wa jimbo la Tarime vijijini, John Heche kufuatia kifo cha mdogo wake Suguta ambaye alifariki kwa kuchomwa kisu na askari

 Mbowe amesema kuwa kifo ambacho kilimpata mdogo wake na Heche kinaumiza sana ndiyo maana kwa siku kadhaa amekosa maneno mazuri ya faraja kumpa kiongozi huyo wa CHADEMA

"Ni siku ya 3 sasa toka ulimpozika mdogo wako, nimefikiria kwa muda mrefu, maneno gani nitumie kukupa pole lakini imeniwia vigumu sana kuyapata maneno hayo kutokana na aina ya kifo kilichokatisha maisha ya kijana mdogo kabisa katika Taifa. Tunafundishwa ya kwamba tushurukuru kwa yote,liwe baya au zuri, sawa tunashukuru lakini kwa kifo cha aina ya mdogo wako kinauma na kuumiza sana, bora mtu akiumwa inakuwa ni rahisi mnasema ni kazi yake Mungu hakuna anayeweza kuipinga na huwa ni kipindi kigumu kuliko wakati mwingine wote wote katika maisha yetu wanadamu pale tunapoondokewa na wapendwa wetu lakini kwa kifo cha aina ya mdogo wako ni maumivu zaidi" 

Aidha Mbowe alitumia wakati huo kutoa pole kwa familia ya John Heche kufuatia kifo cha mdogo wake huyo

"Nakupa pole sana Kamanda Heche John katika kipindi hiki kigumu, Mungu akupe nguvu wewe, familia, ndugu, jamaa na marafiki, pole kwa mara nyingine kamanda, apumzike kwa Amani Kamanda Suguta"

MSANII Harmonize " Bora Ningesikia Mbosso Ndio Anatembea na Sarah ila huyu Mwarabu Fighter Naanzia Wapi Hata Kumuuliza?"

$
0
0


MSANII Harmonize amefunguka kumwogopa Mwarabu Fighter Baada ya kuenea Udaku kuwa Baunsa huyo wa Diamond anatoka kwa siri na Girlfriend wake kwa siri
_
Regrann from @harmonize_tz - Mara 10 ningesikia @mbosso_ anakula mzigo ningemsubiri pale @thelifeclub_1 tarehe 13/5/ na #kipanga yani ile anaingia tuu....!!! nikamuulia hapo hapo sasa mtu kama huyu hivi unaanzaje hata kumuuliza mana hata kucheka kwenyewe kwa msimu jamani Mungu huyu daah.....!! 😓😓

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

IRAN Yasema Marekani itajuta ikijitoa mkataba wa nyuklia.....Ufaransa Yahofia Kuzuka Vita

$
0
0
Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema kwamba endapo Marekani itajiondoa kwenye mkataba wa nyuklia kati ya nchi yake na mataifa yenye nguvu duniani, basi Marekani itajutia maisha yake yote.

"Ikiwa Marekani itaondoka kwenye makubaliano ya nyuklia, mutaona hivi karibuni watakavyojutia kuliko ilivyowahi kuwatokezea kwenye historia," alisema mwanamageuzi Rouhani kwenye hotuba yake ya jana (Jumapili 6 Mei) akiwa kaskazini mwa Iran.

"Trump anapaswa kujua kuwa watu wetu wameunganika, utawala wa Kizayuni (Israel) unapaswa kujuwa kuwa watu wetu wako kitu kimoja," alisema Rouhani.

"Leo, mirengo yote ya kisiasa nchini Iran, ama iwe kulia au kushoto, wahafidhina, wanamageuzi na watu wa mrengo wa kati, wote wameungana," aliongeza.

Rais Donald Trump wa Marekani ametishia kujiondoa kwenye makubaliano hayo wakati utakapofika muda wa kusainiwa upya tarehe 12 Mei, akiwataka washirika wa Ulaya "kuyarekebisha makosa makubwa yaliyomo" ama sivyo arejeshe upya vikwazo dhidi ya Iran.

Mkataba huo wa nyuklia ulisainiwa mwaka 2015 kati ya Iran na Uingereza, China, Ufaransa, Ujerumani, Urusi na Marekani, wakati huo ikiongozwa na Barack Obama.

Chini ya makubaliano hayo, vikwazo vilipunguzwa kwa masharti ya Iran kutokuunda bomu la nyuklia, lakini Iran inasema haioni mafanikio ya ahadi hizo licha ya kutimiza masharti ya mkataba.

Mara kadhaa, Rouhani amekuwa akirejelea msimamo wa nchi yake kupinga kuzuiliwa nchi yake kuunda makombora yasiyo ya kinyuklia, na hilo amelizungumzia pia kwenye hotuba yake ya Jumapili.

Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa (kushoto) anaamini kuwa Marekani haina sababu ya kujitoa kwenye mkataba wa nyuklia wa Iran.

Naye Trump amekuwa akiukosoa mkataba huo, akitaja baadhi ya vifungu ambavyo anasema vinaondoa vikwazo vya nyuklia kuanzia mwaka 2025.

Macron aonya dhidi ya vita
Katika jitihada za kuyaokoa makubaliano hayo, Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amependekeza hivi karibuni kwamba mkataba huo utanuliwe kuyashirikisha masuala kama hayo yanayolalamikiwa na Trump, na pia kuondoa kikomo ya muda wa Iran kuruhusiwa kuunda makombora mengine na pia kuangalia dhima ya Iran kwenye eneo la Ghuba na Mashariki ya Kati.

Hatua ya Iran kumuunga mkono Rais Bashara al-Assad, kupitia kundi la Hizbullah la Lebanon, na pia kuwaunga mkono waasi wa Kishia nchini Yemen kumeongeza mzozo kati yake na mataifa ya Magharibi.

Licha ya hayo, jana Rais Macron ameonya kwamba kunaweza kuzuka vita endapo marekani itajiondoa kwenye makubaliano hayo.

"Tunaweza kuibuwa mambo mengine mapya. Kunaweza kukawa na vita," Macron ameliambia gazeti la kila wiki la Ujerumani, Der Spiegel, ingawa ameongeza: "Sidhani kama Donald Trump anataka vita."

ROMMY Jones Kusuka Twende Kilioni ili Afanane na Wema Sepetu

$
0
0
Rommy Jones amuahidi Wema Sepetu kwamba na yeye ataenda kusuka nywele mtindo wa twende kilioni ili afanane na Wema Sepetu.

Uamuzi huo wa Rommy Jones umekuja mara baada ya Wema kupost picha akiwa amesuka nywele kwa mtindo huo.

Kauli ya Rommy imeibua maswali mengi sana kwa wadau mbalimbali wengine wakimuunga mkono wazo lake huku wengine wakimkandia vibaya sana.



TIMU ya Yanga Hoi Kwa Waarabu...Yachapwa 4 Bila

$
0
0
Wawakilishi wa Tanzania katika kombe la  shirikisho Afrika (Caf Confederation Cup) Yanga wameanza vibaya hatua ya makundi baada ya kufungwa mabao 4-0 kwenye mchezo wao wa kwanza wa makundi dhidi ya USM Alger ya Algeria.

Yanga ikicheza ugenini bila nyota wake wengi wa kikosi cha kwanza ilianza kuruhusu goli la kwanza dakika ya nne lakini hadi kipindi cha kwanza kina malizika Yanga ilikuwa nyuma kwa magoli 2-0.

Kipindi cha pili Yanga ikaruhusu tena goli la mapema ndani ya dakika 10 za kwanza na kuifanya USM Alger kuongoza kwa magoli 3-0, wakati mchezo ukiwa kwenye muda wa nyongeza beki wa Yanga Andrew Vicent alimfanyia madhdambi mchezaji wa USMA na mwamuzi kuamuru ipigwe penati ambapo golikipa wa USM Alger aliifungia timu yake goli la nne.

Matokeo ya mechi nyingine za Kundi D, Rayon Sports imetola sare ya kufungana goli 1-1 dhidi ya Gor Mahia ya Kenya. Kwa maana hiyo, USM Alger inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi tatu ikifuatiwa  na Gor Mahia pamoja na Rayon Sports zenye poini mojamoja baada ya kila timu kucheza mechi moja.


MAJIBU ya Michael Wambura Ukimwambia Aachane na Soka

$
0
0
Kama unakumbuka vizuri aliyekuwa makamu wa Rais wa TFF Michael Wambura alifungiwa maisha kujihusisha na soka, maamuzi ambayo yalitangazwa na kamati ya maadili ya TFF baada ya kujiridhisha na tuhuma ambazo zilikuwa zikimkabili Wambura.

Baadaye Wambura alikata rufaa kwenda kamati ya maadili ya rufaa ambako maamuzi yalibaki vilevile, inawezekana wadau wengi wanatamani kujua Wambura atachukua hatua gani au amekubali kutumikia hukumu yake?

Jumamosi ya Mei 5, 2018 Wambura akiwa ndani ya kipindi cha Clouds 360 cha Clouds TV ametoa msimamo wake juu ya hukumu iliyotolewa na kamati ya rufaa ya maadili na hatua atakazochukua.

“Kuna mtu akila vijiko viwili vya wali anashiba, kuna mwingine akila kilo moja ya ugali hashibi. Kama mtanzania nina wajibu wangu na bahati nzuri sisi wakati tunakua tulitunzwa, tumelelewa na kusomeshwa na serikali, kuacha ile elimu niliyosomeshwa na serikali ikapotea bure bila kuwasaidia wengine nadhani ni dhambi ambayo sistahili kuibeba.”

“Sisemi kwamba lazima niwe kiongozi, lakini mchango wangu kwenye mpira si dhani kama utakuwa umeishia hapo. Tangu 2004 sikuwahi kuwa kiongozi lakini mchango wangu katika mpira umeleta mambo mengi.”

“Nikisema niachane na mpira je, wale watu walionichagua wapo tayari kuachana na mimi?  Kuna aina mbili za watu, kuna watu ambao wanatamani uongozi lakini hawachaguliki. Ukimpeleka kwa wananchi wapigie kura hawamchagui, mimi nikipelekwa kwenye kura nachagulika, maana yake watu wanaopiga kurawananiamini.”

Faiza Anasa Mimba Nyingine Amwaga Chozi Hadharani

$
0
0
Faiza Anasa Mimba Nyingine  Amwaga Chozi Hadharani
UTAMU wa ubuyu hauchagui mtoto wala mtu mzima, wote ni twende tu! Mwigizaji wa sinema za Kibongo ambaye ni mzazi mwenza wa Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) anayetumikia kifungo cha miezi mitano jela, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Faiza Ally amejikuta akimwaga machozi laivu!

Kwa mujibu wa msambaza ubuyu wetu, hivi karibuni Faiza alinasa ujauzito mwingine wa mtoto wa tatu huku mtoto wake wa pili akiwa na umri wa miezi nane tu kisha ukachoropoka. Chanzo hicho kilitiririka kuwa, Faiza alianza kuumwa bila kujua anaumwa nini baada ya kuwa anatumia dawa akiamini ni za kuzuia ujauzito, kumbe zilikuwa ni za kuharibu mimba.



Ilisemekana kwamba, Faiza alifikia hatua ya kutumia dawa hizo akiamini hatapata mimba kwa kuwa baba wa mtoto wake wa pili alikuwa amekuja Bongo kwa kuwa ni raia wa Marekani. Kiliendelea kutiririka kuwa, Faiza alikuwa haelewi, lakini kila alipotumia dawa hizo alipata maumivu makali na kuanza kuona mabadiliko makubwa kwenye mwili wake, hasa wakati wa hedhi.


Ilisemekana kwamba, kufuatia hali hiyo, ilimlazimu Faiza kwenda kuonana na daktari ili kujua ni kitu gani kinamsumbua. “Alipoamua kwenda hospitalini alikuwa hajui tatizo ni nini kwenye mwili wake. Kila alipokuwa akitumia dawa hizo zilimfanya ajisikie vibaya mno.

“Pale kwenye Hospitali ya AAR ndiyo waligundua kuwa alikuwa na ujauzito ila ulishaanza kutoka na kubaki masalia ambayo ilibidi asafishwe,” alitonya mtoa ubuyu wetu. Mpashaji huyo alizidi kuweka wazi kuwa, baada ya kugundulika kwamba alikuwa na ujauzito, lakini ukawa umeharibika kutokana na dawa hizo, madaktari waliamua kumsafisha ili kumrudisha kwenye hali yake ya kawaida.



Baada ya gazeti hili kupata ubuyu huo lilimtafuta Faiza ili kufafanua zaidi kuhusu ishu hiyo ambapo mambo yalikuwa hivi;

Ijumaa Wikienda: Pole sana Faiza na kuumwa?


Faiza: Asante.



Ijumaa Wikienda: Tumepata habari kuwa ulikuwa mjamzito, hilo limekaaje?



Faiza: Ndiyo…ni kweli nilikuwa na ujauzito.



Ijumaa Wikienda: Sasa ilikuwaje wakati una mtoto mdogo?



Faiza: Ilitokea tu bahati mbaya!



Ijumaa Wikienda: Eeh!



Faiza: Unajua mimi sikai na baba mtoto wangu hivyo mara nyingi tunatumia dawa ya kuzuia mimba, lakini tuliyokuwa tukitumia ilikuwa siyo ya kuzuia ni ya kuharibu mimba hivyo ujauzito huo ulipoingia kwa bahati mbaya na kutumia dawa hizo, ukatoka. Lakini haukutoka vizuri, ndiyo nikawa ninajisikia kuumwa hadi nilipochukua uamuzi wa kwenda hospitalini.



Ijumaa Wikienda: Kwa hiyo kama isingekuwa ni hiyo dawa kuharibu na mimba imeingia bahati mbaya ungezaa?



Faiza: Ndiyo maana Mungu angekuwa amepanga. Mimi siwezi kutoa ujauzito hata siku moja.



Ijumaa Wikienda: Lakini si ulisema watoto wawili wanatosha?



Faiza: Ndiyo ilikuwa hivyo, lakini mimba imeingia bahati mbaya, nisingeweza kufanya lolote zaidi ya kusubiri kulea tu kwa mara nyingine.



Ijumaa Wikienda: Kwa hiyo hospitalini wakafanyaje?



Faiza: Walinisafisha na sasa ninaendelea vizuri.



Ijumaa Wikienda: Polesana Faiza.



Faiza: Asante

Waziri wa Pakistani Anusurika Kifo Baada ya Kupigwa Risasi

$
0
0
Waziri wa Pakistani Anusurika Kifo Baada ya Kupigwa Risasi
Waziri wa Mambo ya Ndani Pakistan, Ahsan Iqbal (59) amejeruhiwa baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana wakati akiwa katika mkutano wa kampeni za uchaguzi katika jimbo la Punjab.


Kwa mujibu wa vyanzo vya habari mbalimbali vinasema kuwa Waziri huyo amejeruhiwa katika bega lake la kushoto kufuatia risasi moja kumpata ambazo zilikuwa zikifyatuliwa na kijana ambaye mpaka sasa hajafahamika.

Hata hivyo msemaji wa huduma za uokoaji Jam Sajjad Hussain amedai kuwa Waziri huyo alifanikiwa kuingizwa kwenye gari yake na kutoka katika eneo hilo aliloshambuliwa  na kumpeleka hospitali kwa matibabu zaidi.

Mbali na hilo mtoto wa Waziri huyo amesema kuwa baba yake hajapata majeraha makubwa ambayo yanatishia maisha yake hivyo ni majeraha ya kawaida ambayo anaendelea kutibiwa na madaktari.

Simba Haikamatiki Yasubiri Point Moja tu Kuwa Bingwa

$
0
0
Simba Haikamatiki Yasubiri Point Moja tu Kuwa Bingwa
Ligi Kuu Tanzania bara imeendelea leo Jumapili ya May 6 2018 kwa michezo minne kuchezwa katika viwanja mbalimbali Tanzania bara, mchezo kati ya Simba dhidi ya Ndanda FC  uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Simba ambao wanatajwa kuwa na safu nzuri ya ushambuliaji msimu huu kuliko vilabu vingine leo wamefanikiwa kupata point tatu kwa ushindi finyu wa goli 1-0 goli ambalo lilifungwa na Emmanuel Okwi dakika ya 44.

Irene Uwoya na Dogo Janja Wasaka Mtoto Usiku Kucha

$
0
0
Irene Uwoya na Dogo Janja Wasaka Mtoto Usiku Kucha
MKALI wa Bongo Movies, Irene Pancras Uwoya na mumewe, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ ambaye ni msanii wa Bongo Fleva, wamesema kuwa, wapo bize kwa sasa na wamekuwa wakikesha kumsaka mdogo wake Krish ambaye ni mtoto wa mwanamama huyo aliyezaa na mumewe wa awali, marehemu Hamad Ndikumana ‘Kataut’.



Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Ijumaa Wikienda, mastaa hao walifunguka kuwa, kwa kipindi hiki cha mvua ndiyo muda sahihi wa kusaka mtoto hivyo wanalifanyia kazi suala hilo kwa nguvu zao zote.



“Tupo bize kidogo, tunasaka mtoto maana si unajua watu wanaangalia matunda ya ndoa kwa jicho la tatu hivyo sisi tunaangaika na hilo sasa hivi,” alisema Dogo Janja.



Kwa upande wa Uwoya alisema kuwa, yeye kama mwanamke anatakiwa kumzalia mumewe mtoto na hivyo kwa hivi sasa yeye na mumewe wapo katika harakati hizo kwa sababu Krish ameshakuwa mkubwa.



“Mke lazima amzalie mumewe na mimi na mume wangu sioni tunachosubiri kwa sasa maana Krish ni mkaka mkubwa na anahitaji mdogo wake,” alisema Uwoya.

Hofu Kubwa Imezuka Makao Makuu Yanga Kisa Yondani

$
0
0
Hofu Kubwa Imezuka Makao Makuu Yanga Kisa Yondani
SIKU chache baada ya beki wa kati wa Yanga, Kelvin Yondani, kumtemea mate beki wa Simba, Asante Kwasi na suala hilo kupelekwa katika Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho ya Soka Tanzania (TFF), hofu kubwa imezuka makao makuu ya klabu hiyo.



Yondani alimtemea mate Kwasi hivi karibuni katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliozikutanisha Yanga na Simba katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.



Wapenzi na mashabiki wa timu hiyo, wamejawa na hofu ya kumkosa mche­zaji huyo katika mechi zao zote za ligi kuu zilizobakia, jambo ambalo wanaamini kuwa linaweza kusababisha wakamaliza ligi hiyo wakiwa katika nafasi ya tatu ambayo wanashika sasa wakiwa na pointi 48, nyuma ya Azam yenye pointi 49, pamoja na Simba ambayo kabla ya mechi yake ya jana ilikuwa na pointi 62.



Jana, Jumapili Championi Jumatatu lilizungumza na baadhi ya mashabiki wa Yanga makao makuu ya klabu hiyo kuhusiana na suala hilo la Yondani na baadhi yao walionyesha hofu hiyo.



“Tunasubiri tuone ni adhabu gani atakay­opewa lakini hofu yetu tuliyonayo sasa ni kwamba tunaweza kumkosa katika mechi zetu zote zilizobakia na ukizingatia ni mchezaji muhimu sana katika kikosi chetu msimu huu,” alisema mmoja wa mashabiki hao ambaye alijitambulisha kwa jina la Salum Juma.



Shabiki mwingine wa timu hiyo ambaye alijitambuli­sha kwa jina na Emmanuel Temba, alisema: “TFF inatakiwa kutenda haki katika hilo, kama ni adhabu basi aadhibiwe kwa mujibu wa kanuni lakini siyo kwa ajili ya kutaka kumkomoa kutokana na mashinikizo ya baadhi ya watu wasiotutakia mema.



“Bado tunamhitaji sana Yondani katika mechi zetu za ligi zilizobakia lakini pia katika michuano ya ki­mataifa, kwa hiyo wasitoe adhabu ambayo inaweza kusababisha asionekane tena uwanjani mpaka mwisho wa ligi.”



Hata hivyo, kwa mujibu wa kanuni ya 37 ya ligi kuu inayozungumzia udhibiti wa wachezaji, adhabu kubwa ambayo Yondani anaweza kukumbana nayo kutokana na kosa hilo ni kifungo cha mechi tatu pamoja na kulipa faini ya Sh 500,000.

Pesa Yamkwamisha Christian Bella

$
0
0
Pesa Yamkwamisha Christian Bella
AMA kweli vimekosa grisi! Mkongwe wa Muziki wa Dansi, Christian Bella ‘Obama,’ amesema ukata amemfanya abadili utaratibu wa kufanya shoo zake kwa juma. Amesema Sasa atakuwa anafanya shoo moja badala ya shoo nne hadi tano alizokuwa akifanya awali.

Akizungumza na Over Ze Weekend, Bella anayebamba na Ngoma ya Shuga alisema kuwa, atakuwa akifanya onesho kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi ndani ya Kiwanja cha Mzalendo Pub Kijitonyama Jijini Dar.

“Mashabiki wangu najua wengi mnapenda tufanye makamuziki mara kwa mara lakini kutokana na vyuma kukaza nawaomba tufanye kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi ndani ya kiwanja hiki,” alisikika Bella akiwa jukwaani kiwanjani hapo huku akishangiliwa na umati wa mashabiki walio-furika.

Msikiti Washambuliwa Afghanistan Wakati wa Swala

$
0
0
Msikiti washambuliwa Afghanistan wakati wa swala
Maafisa kutoka Mashariki mwa Afghanistan wanaarifu kuwa watu kumi na nne wamekufa na wengine na kadhaa walijeruhiwa katika mlipuko kwenye msikiti katika jimbo la Khost.

Wamearifu kuwa mripuko huo ulitukia wakati watu walipokuwa wamejumuika kwa swala za adhuhuri.Mashuhuda wanaarifu kuwa msikiti huo ulikuwa ukitumika pia kama kituo cha usajili wa wapiga kura.

Kulikuwa na mashambulio kadhaa katika miji mingine tangu msimu wa usajili wa wapiga kura ulipoanza mwezi uliopita kwa uchaguzi wa bunge mwezi wa Oktoba mwaka huu, na mpaka sasa hakuna kundi lolote lenye msimamo mkali lililo jitokeza na kukiri kuhusika kwake.

Ingawa kundi la wanamgambo wenye msimamo mkali limetekeleza mashambulizi kama hayo hapo awali.Mnamo tarehe 22, mwezi wa nne , shambulio katika kituo cha kuandikishia wapiga kura katika mji mkuu Kabul liliua watu hamsini na saba.

Shambulio la mjini Kabul tayari kundi la wanamgambo wa dola ya kiislamu walikiri kuhusika nalo, ingawa mamlaka za Kabul zimetoa angalizo kwa watu kuwa wasijihusishae na uchaguzi ujao, ambao unaarifiwa kuwa ni mtihani muhimu wa uaminifu wa Rais Ashraf Ghani.Miongoni mwa waliojeruhiwa wanasadikiwa kuwa katika hali mbaya . Kumekuwa na matukio ya kushambulia vituo vya kupigia kura tangu msimu huo ulipoanza mwezi uliopita kuelekea uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika nchini humo mwezi wa October,kwa uchaguzi wa wabunge.

SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumatatu

Alikiba Yamkuta ya Daimond Naye Kupelekwa Mahakamani Kisa Matunzo ya Mtoto

$
0
0
Alikiba Yamkuta ya Daimond Naye Kupelekwa Mahakamani Kisa Matunzo ya Mtoto
MFANYABIASHARA wa mitumba Hadija Hassan amefungua kesi ya madai ya matunzo ya mtoto dhidi ya msanii nguli wa muziki wa kizazi kipya, Ali Kiba maarufu kama King Kiba.

Katika kesi hiyo, Hadija anadai jumla ya Sh. milioni 1.41, ikiwamo Sh. 950,000 za ada na Sh. 460,000 za matumizi ya mtoto wa miaka mitano (jina limehifadhiwa kwa sababu za kisheria na kimaadili).

Hadija ambaye ni mfanyabiashara wa mitumba amefungua kesi ya madai hayo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam akidai matunzo kwa mlalamikiwa ambaye ni mzazi mwenzie -King Kiba.

Kwa mujibu wa hati ya madai iliyowasilishwa mahakamani hapo, mlalamikaji anadai kuwa Januari, 2013 katika Hospitali ya Mikocheni, jijini Dar es Salaam alizaa mtoto wa kike ambaye baba yake ni mlalamikiwa.

Alidai kupitia hati hiyo kwamba mlalamikiwa anatakiwa kumhudumia mtoto huyo kwa mahitaji yote muhimu ikiwamo chakula, nguo, elimu na matibabu.

"Kutokana na Sheria ya Watoto ya mwaka 2009, mdaiwa anatakiwa kutoa huduma kila mwezi, chakula Sh. 150,000, matunda Sh. 50,000, chakula cha ziada Sh. 50,000, michezo na burudani za watoto Sh. 100,000, nguo Sh. 60,000 na matibabu Sh. 50,000 ambapo jumla ni Sh. 460,000," alidai mlalamikaji kupitia hati hiyo.

Aidha mlalamikiwa anatakiwa kulipa ada ya shule kwa muhula Sh. 950,000, na anadaiwa aliacha kutoa matunzo hayo kwa mtoto tangu Januari, mwaka huu hivyo anaiomba mahakama imwamuru mdaiwa kutoa matunzo hayo ya Sh. 460,000 kila mwezi na ada.

Pamoja na mambo mengine, mlalamikaji anaomba malipo ya kwanza yatolewe mapema baada ya hukumu, na pia anaiomba mahakama imwamuru King Kiba kumsomesha mtoto, kumnunulia nguo na matibabu ikiwamo kumtafutia bima ya afya.

Pia mlalamikaji anaomba mahakama imwamuru Kiba kulipa gharama za matunzo Sh. 460,000 kuanzia Februari 2017 mpaka siku itakapotolewa hukumu na gharama za kesi ziwe kwa mdaiwa.

Mbali na maombi hayo, Hadija anaomba mahakama itoe amri nyingine yoyote itakayoona inafaa kwa manufaa yake. Kesi imefunguliwa kwa msaada wa Kituo cha Wanawake cha Msaada wa Kisheria (WLAC).

BWANA HARUSIAli Kiba, ambaye jina lake la kuzaliwa ni Ali Saleh Kiba amefunguliwa madai hayo ikiwa ni siku chache tangu afunge ndoa iliyopendeza mjini Mombasa Kenya.

Nyota wa kibao cha 'Seduce Me' Kiba aliuacha rasmi ukapera baada ya kufunga ndoa na mpenziwe kutoka Kenya, Amina Khalef, mwezi uliopita.

Harusi hiyo ya kukata na shoka ilifanyika katika msikiti wa Ummul Kulthum na ilihudhuriwa na rafiki wa mwanamuziki huyo, Gavana wa Mombasa Ali Hassan Joho.

Msanii huyo ambaye Mei 20, 2016 aliingia mkataba na kampuni ya kimataifa ya Sony Music kwa mujibu wa mtandao wa kompyuta wa Wikipedia, alijizolea umaarufu kupitia albamu yake ya 'Cinderella'.

Kutana na Mtaalam Sharif Hamad Kalala Mchambuzi wa Nyota za Binadamu na Tiba Asili

$
0
0
KUTANA NA SHARIF HAMAD KALALA NI SHARIFU MCHAMBUZI WA
NYOTA ZA BINAADAMU NA NI MWENYE UPEO MKUBWA KUTAFITI MATATIZO YAKO KABLA YA KUTOA USHAURI WAKE WA TIBA AlJALISHI MBALI ULIKO TIBA YAKE UMFIKIA YEYOTE MWENYE UITAJI POPOTE
DUNIANI.

 SHARIF HAMAD KALALA NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA QUR-AN, DAWA ZA ASILI ZA MITI SHAMBA PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.

ANATIBU KWA NJIA YA SIMU KWA KUTOA
MAELEKEZO NAMNA YA MATUMIZI YA DAWA UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-

 KUFANIKISHA NDOA KWA UNAYE MPENDA KWA HARAKA. KUMRUDISHA MPEZI NDANI YA MASAA 12 TU.
 ULIJALI (NGUVU ZA KIUME) NDANI YA /IKI MMOJA TU
MIGUU KUWAKA MOTO KUTAFSIRI NDOTO MFARAKANO WA WANANDOA MFARAKANO KAZINIKUPANDISHWA CHEO NDANI YA SIKU SABA 7 TU.
KUTOA PETE YA BAHATI KUTOA MAJINI MACHAFU IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA. KUPATA MAFANIKIO YA MALI BILA YA MASHARTI. KUPANDIKIZANYOTA YA KUBASHIRI KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA KWENYE BIASHARA. ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA KUMUOA AU KUWA NAYE. ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA
KWA NJIA YAMSUKULE
NAO UWEZO WA KUUA KESI SUGU NA MPYA NDANI SIKU 7 TU.
MENGINEYO MENGI ZAID YALIYO KUWA SUGU PIGA KWA WALE WALIYO ANGAIKA SEHEMU MBALI MBALI SHARIF HAMAD KALALA NI SULUISHO. ENDAPO UTAMSIKILIZA KWA YALE ATAKAYO KUSHAURI NA KUKUPA
ELEKEZI.
 TIBA NI KWA DINI ZOTE POPOTE ULIPO NJE NA NDANI YA NCHI.

MOBILE +255 -673 025 376
WhatsApp +255-757 069 066
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live




Latest Images