Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

Boss Ananitaka Kingono, Nipo Njia Panda Naomba Ushauri

$
0
0
Katika harakati za kutafuta kazi nilibahatika kufika ofisi moja maeneo ya Mwenge (Dar es salaam) kwangu ilikua faraja kubwa sababu kiukweli nilikua nahangaika sana na hali ya ugumu wa maisha na sikutaka kabisa kuwa tegemezi kwa mtu yoyote (wakiwemo wazazi) niliamini kunipa elimu ni mtaji muhimu na tosha na lilikua jukumu langu kuandaa maisha yangu mwenyewe na kujitegema

Nilipofika pale niliomba kuonana na boss ila nikaambiwa haiwezekani labda ningekua na appointment, kutokana na uzoefu hii kauli nilikua nimekutana nayo mara kadhaa hivyo ilikua hainisumbui sana, nikamwambia yule receiptionist kuwa nilikua na appointment (kiukweli sikua nayo na nakiri nilidanganya na nilikosea ila sikuwa na namna mbadala) akaniuliza nimwambie we ni nani nikasema mwambie (tax consultant)

Waliongea mawili matatu then nikaruhusiwa kuingia nadiriki kusema shida ni mwalimu mkubwa sana kwani sikuwa na woga wowote kuonana na yeyote na kujinadi, baada ya mazungumzo na mahojiano ya kama dakika sita yule manager (mwanamke) akaniambia alhamisi niende nikafanye interview na kutokana na intro niliyoitoa hiyo siku (Jumanne).

Haikua kazi kwangu kupata hiyo kazi hata baada ya interview ya alhamisi, tulikubaliana terms za kazi na mshahara then nikapewa mkataba. Nilifurahi sana nikijua sasa mipango yangu itaenda vema (kwakweli mshahara ulikua mzuri tu) hadi nikaanza kupangilia biashara ndogondogo ili kuinua uchumi wangu.

Nilianza kazi wiki iliyofuata na wafanyakazi wenzangu walikua watu wema sana kwangu hivyo nilifanya kazi kwa furaha na ufanisi sana mpaka hali ilipokuja kubadilika.

MABADILIKO

Baada ya wiki moja mambo yalianza kubadilika pale ofisini, mara kwa mara boss alikua na vikao visivyokua na mbele wala nyuma na mimi na akawa mkali kwa wafanyakazi wenzangu especially wa kike na taratibu wakaanza kuniogopa.

Siku moja aliniita ofisini (ilikua Ijumaa) na akaniambia nifunge mlango nilishtuka sababu normally ukiingia ofisini lazima ufunge mlango cha kushangaza akaniambia ni-u lock nikafanya alivyotaka,

Hakuna cha maana alichoniambia zaidi ya story za kifamilia tu oooh mara mumewe (aliekuwa meneja kabla hajaumwa) anasumbuliwa na kisukari na presha na anapata taabu sana mi nikawa msikilizaji tu na aliongea muda mrefu hadi jua likazama na watu waliondoka ofisini alibaki mlinzi tu.

Aliongea mengi na mwisho akaniambia anataka nimsaidie (ngono) kitu ambacho kilinishtua kidogo ukizingatia ni mtu mzima rika la mamaangu, nilimbembeleza kuwa hapo si pahali salama ili tu aniache siku hiyo ili nikajipange jinsi ya kuepukana nae na kuikabili ile hali.

Alinikomalia sana hadi kunivamia physically na alionekana wazi alikua desperate for sex ila nilifanikiwa kumpanga na akanielewa baada ya hiyo siku ofisi nzima wakahisi nilizini na yule boss hivyo kukawa na minong'ono mingi na sikuwa na namna ya kuwaaminisha vinginevyo.

Tangu hapo ni wiki ya pili sasa huyu mama ananisumbua sana, ananiahidi mambo mengi kama nitakubali kusex nae na ni dhahiri nikimtamkia kuwa SITAKI nitapoteza kibarua kwani ye ndo meneja hapa na ndo anaajiri na kusitisha ajira,

Leo hii (Jmosi) kanipigia simu na kuniambia kesho saa saba ana kikao na mimi cha kikazi ila location naona hata aibu kuisema. Wakuu najua kuna watu humu wakike na kiume ambao wamekutana na hali kama yangu,

Naipenda kazi na sina pa kushikilia kwa sasa lakini pia sitaki kuisaliti imani yangu na msimamo kwa kupenda vitu vya dezo na kufanya uzinzi na mtu wa rika la mama yangu, ni dhambi kubwa na pia ni kinyume cha maadili ya jamii yetu lakini pia nikifikiria matokeo ya kuachishwa kazi (na mipango niliyokwisha iweka kichwani kwangu) roho inaniuma sana nabaki nikiwaza na kuwazua bila kujua haswaa nishike wapi.

Msimamo wangu ni kutokulala na huyu mama no matter the consequences ila naomba mnipe chakula cha akili ili akinifukuza kazi basi niwe nimeimarika kisaikolojia kwa ushauri wenu na nisitetereke sana kisaikolojia.

Asanteni


Faida Ama Uzuri wa Kuoa Single Mothers na Wadada Over 35 years

$
0
0

Ndoa nyingi zina changamoto lakini nimegundua ukioa single mother au dada ambae ni 35+ hawa watu mara nyingi huwa ni wife materials ukilinganisha na hawa wenye age ya 20-35.

*Hawa watu wana commitment sana katika ndoa zao.
*Wanakuwa washapitia changamoto nyingi zinazohusisha mahusiano so huwa hawasumbui.
*Wengi wamekomaa kiakili na wanajua jinsi ya kuhandle mume na familia kwa ujumla
wana mazuri mengi.

Kama hujaoa ukipata watu wa namna hii usipoteze fursa.

Hamisa Mobetto “Sijaonana na Lulu Toka Atoke Jela, Yupo Kwenye Maisha ya Mtoto Wangu Nitaruhusu Amlee

$
0
0
Mwanamitindo Hamisa Mobetto amejibu baadhi ya maswali aliyohojiwa na Ayo TV ikiwemo swala la kuonana na muigizaji Elizabeth Michael a.k.a Lulu baada ya kutoka gerezani huku ikiwa Lulu anasemekana kuwa mapenzini na mwanaume aliyezaa na Hamisa mtoto wa kwanza.

Bonyeza PLAY hapa chini kumsikiliza Hamisa Mobetto akiyajibu yote.


Hamissa Mobetto Aingia Mkataba Mnono na Kiwanda cha Kutengeneza Nywele

$
0
0
Hamissa Mobetto Aingia Mkataba Mnono  na Kiwanda cha Kutengeneza Nywele
Maisha yameanza kumnyookea mwanamitindo Hamisa Mobeto kwa kuvuna kweupee shilingi milioni 5.7 kwa mwezi (zaidi ya milioni 60 kwa mwaka) leo Agosti 8, 2018, baada ya kuingia mkataba wa mwaka mmoja wa kuwa balozi wa kiwanda kinachotengeneza nywele (rasta) cha Prima Afro, kilichopo Tabata, Matumbi jijini Dar.



Kwa mujibu wa chanzo ambacho ni rafiki wa karibu na mwanamitindo huyo, waandaji waliangalia ni mtu gani anaweza kuwatangaza zaidi miongoni mwa mastaa na kuona Mobeto anafaa zaidi yao.




“Amewapiga bao mastaa wenzake wengi, ama kweli mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Mobeto hivi karibuni amesemwa sana mitandaoni, kuanzia kipindi cha ile bethidei ya mtoto wake, Daylan hadi hii ya juzijuzi na Zamaradi, kumbe Mungu alikuwa na mipango naye, ona sasa amevuna mkwanja mrefu,” kilisema chanzo.

Chanzo kiliendelea kumwaga data kuwa, Mobeto ameingia mkataba kwa njia ya dola ambapo amelipwa kiasi cha dola za Kimarekani 2,500.


“Hajataka tu kusema ni mkataba wa kiasi gani lakini ni dola za Kimarekani ambapo sasa ukichukulia dola 2,500 kwa pesa za Kibongo ni kama shilingi milioni 5.7 hiyo ni kwa mwezi, ukifanya kwa mwaka mmoja alioingia atakuwa amevuna kiasi cha shilingi milioni 68.4 kwa nini asiwe na kismati ikiwa wenzake hawajavuna pesa hizo ndani ya mwaka huu,” kilitia nukta chanzo hicho.



Mara baada ya kusaini mkataba huo, Mobeto alisema kuwa, hakujua lakini kumbe walikuwa wakimchunguza nguvu yake kwenye mitandao ya kijamii.

“Baada ya kunichunguza, walinifuata ofisini kwangu tukazungumza, nikausoma mkataba na kuangalia masharti yao na kiwango wanachotaka kunilipa niliporidhia tukapanga siku ambayo ni leo nikasaini,” alisema Mobeto.

Majibu ya Tume ya Taifa kwa Ubalozi wa Marekani Yawaibua Tena CHADEMA

$
0
0
Chadema kimesema Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) inapaswa kulaumiwa kwa kuvuruga uchaguzi mdogo uliofanyika Agosti 12, 2018,  kuorodhesha  baadhi ya matukio iliyodai yalilenga kuwakandamiza wagombea wa chama hicho na wanachama.

Jana Alhamisi Agosti 16, 2018 chama hicho kilitoa taarifa kwa vyombo vya habari na kubainisha kuwa baadhi ya maeneo wagombea wake walienguliwa katika mazingira ya kutatanisha, hata walipojaribu kuhoji hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.

Majibu ya Tume ya Taifa kwa Ubalozi wa Marekani Yawaibua Tena CHADEMA
Chama hicho kimesema  taarifa iliyotolewa na NEC kujibu tamko la Ubalozi wa Marekani  kuhusu uchaguzi huo mdogo,  haiakisi  ukweli wa mambo na badala yake ilipotosha kuhusu kilichotokea kwenye mchakato wa uchaguzi huo.

Taarifa hiyo iliyotolewa na ofisa habari wa chama hicho, Tumaini Makene inasema NEC imeshindwa kusimamia uchaguzi uwe huru na haki, kutokana na ama kutokuwa na uwezo au kufumbia kwa makusudi hila na njama zilizokuwa zikifanyika kuharibu na kuvuruga uchaguzi huo.

“Jamii ya watanzania, jumuiya ya kimataifa na dunia nzima iliona na kushuhudia kupitia njia mbalimbali za upashanaji habari ikiwemo vyombo vya habari na mitandao ya kijamii jinsi ambavyo NEC ilishindwa kusimamia uchaguzi uwe huru na haki,” ilisema.

“Mathalani  wagombea udiwani wa Chadema katika kata tano Tunduma walinyimwa fomu zao za kugombea kwa makusudi kabisa kisha fomu hizo wakapewa watu wengine (wanaodaiwa hawajulikani).”

Imesema, “kwa kutumia mbinu za kijinai zinazohusisha kughushi. Kama hiyo haitoshi wagombea wetu wakaanza kusakwa na kukamatwa na polisi na kubambikiwa tuhuma za jinai.”

Mbali na hoja hizo, Chadema imesema imeshangazwa na namna NEC ilivyohoji Marekani ilitumia utaratibu gani kupata taarifa ilizotoa kuwa uchaguzi uligubikwa na vitendo vya vurugu na ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi.

“Swali hilo la NEC linaibua swali jingine,  je mamlaka zilizoharibu na kuvuruga uchaguzi huo zilifanya hivyo kwa sababu zilijua hakuna waangalizi wa kimataifa? Je zilifanya hivyo kwa sababu zilijua habari za matukio hayo hazitaufikia ulimwengu ambao hautakaa kimya,” imesema taarifa hiyo.

Agosti 15, 2018 NEC iliutaka ubalozi huo kuthibitisha inachokieleza juu ya uchaguzi huo, ikisema uchaguzi mdogo huwa hauna waangalizi wa kimataifa na kuhoji ubalozi huo umetoa wapi taarifa hizo na hayo iliyoyaona ni kwa kutumia utaratibu upi na sheria ipi.

Mume Auawa na Wananchi Baada ya Kumuua Mke Wake kwa Mundu

$
0
0
Mume Auawa na Wananchi Baada ya Kumuua Mke Wake kwa Mundu
Mkazi  wa kijiji cha Kinku  tarafa ya Mungaa wilaya Ikungi , Singida, Editha Kanisi (49) ameuawa kwa  kukatwa kwa  kisu cha kukatia majani, (mundu) shingoni na kichwani na mume wake Joseph Wilbroad (53).

Baada ya Joseph kufanya mauaji hayo wananchi wenye hasira kali nao walimshambulia kwa silaha na kumuua.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana   Agosti 16 Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ACP Sweetbert  Njewike alisema tukio hilo limefanyika  Agosti 15 mwaka huu usiku saa mbili huko katika kijiji cha Kinku.

Alisema kuwa tukio hilo lilitokea  usiku wakati  wanandoa hao wakijiandaa kulala na uliibuka mzozo mkali baina yao huku kila mmoja akimtuhumu mwenzake kuwa si mwaminifu kwenye ndoa.

“Kila mmoja alimtuhumu mwenzake kutokuwa mwaminifu katika ndoa yao,”alisema.

Akifafanua zaidi alisema malumbano hayo yalisababisha mwanaume kuchukua kisu cha kukatia majani kiitwacho mundu na kumkata mke wake shingoni na kichwani.

Alisema Editha alijaribu kukimbia lakini alipotoka nje ya nyumba yao alianguka chini na kufariki dunia papo hapo.

 “Watoto wao baada ya kuona mama yao kaanguka chini, walianza kupiga kelele za kuomba msaada na majirani walifika mara moja kwenye eneo la tukio na wakamwomba Joseph afungue mlango,” alisema Kamanda huyo

"Joseph alikaidi kufungua mlango na ndipo walipouvunja kwa nguvu.Walipofanikiwa kumkamata Joseph,walimpiga kwa silaha za jadi na kusababisha kifo chake,”aliongeza.

Alisema uchunguzi zaidi na msako mkali unaendelea kuwasaka waliohusika na mauaji ya Joseph.

UN Yataka Kuachiwa Huru Mwanaharakati wa Haki za Bidamu Aliyefungwa

$
0
0
UN Yataka Kuachiwa Huru Mwanaharakati wa Haki za Bidamu Aliyefungwa
Bodi ya umoja wa mataifa UN,imetaka kuachiliwa huru kwa mwanaharakati wa haki za binadamu wa Bahraini Nabeel Rajab aliyefungwa kwa madai ya kufanya makosa ya kueneza habari za uongo na kukashifu mamlaka za kiserikali.

UN inasema kuwa hukumu ya Nabeel Rajab ilifanyika kinyume cha sheria na ilikiuka uhuru wake binafsi wa kujieleza.

Hadi sasa Nabeel amekwisha tumia miaka mingi tu gerezani tangu alipokuwa akiongoza harakati zake za kidemokrasia mwaka 2011.Lakini serikali kwa upande wake inasema kuwa mashitaka ya Rajab yalitolewa katika mfumo wa uhuru na uwazi.

Nabeel Rajab, mkuu wa kituo cha haki za binadamu cha Bahrain Center for Human Rights (BCHR) na makamu katibu mkuu wa taasisi ya kimataifa ya haki za binadamu ya International Federation of Human Rights (FIDH), amekuwa akishikiliwa tangu june mwaka 2016.

Mwezi Februari mwaka huu alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela kutokana na kutoa ujumbe kupitia ukurasa wake wa Twitter ulikuwa ukipinga kile kinachodaiwa kuwa ni mateso wanayoyapata wafungwa wa Bahrain na vitendo viovu vya jeshi la Saudia wakishirikiana na muungano wa wapiganaji wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Yemen

Hata hivyo hukumu hiyo ilikuja huku akiwa anatumikia kifungo cha awali cha miaka miwili gerezani baada ya kukutwa na makossa ya kueneza habari zinazodaiwa kuwa ni za uongo.

Shirika la Human Rights Watch limesema kuwa taarifa kutoka kwa wanafamilia wa Rajab,zinasema kuwa anaishi katika mazingira magumu,anafungiwa katika chumba kichafu,chenye wadudu ambacho ukubwa wake si zaidi ya futi kumi,lakini pia afya yake imedhoofu na anasumbuliwa na ugonjwa wa ngozi ambapo anahitaji matibabu.

Mhasibu Ahukumiwa Kifungo cha Miaka Mitano Jela

$
0
0
Mhasibu Ahukumiwa Kifungo cha Miaka Mitano Jela
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu miaka 5 jela aliyekuwa Mhasibu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Kijitonyama, Gryson Mnyawami baada ya kupatikana na hatia ya kosa la wizi wa zaidi ya Shilingi Milioni 9 akiwa mtumishi.

Hukumu hiyo, imesomwa na Hakimu Mkazi Mkuu Janeth Mtega ambapo amesema upande wa mashtaka kupitia mashahidi wake 5 wameweza kuthibitisha pasipo kuacha shaka kuwa mtuhumiwa ametenda kosa la wizi.

Hata hivyo, kabla ya kusomwa kwa hukumu hiyo, Hakimu Mtega alitaka mwendesha mashtaka kueleza kuhusu kumbukumbu za mshtakiwa kama anamakosa mengine ama la.

Mwendesha Mashtaka, wakili wa Serikali, Janeth Magoha ameekeza kuwa hakuna kumbukumbu za makosa kwa mshtakiwa, hili ni kosa lake la kwanza.

“Sina kumbukumbu za mshtakiwa, ila naomba mahakama itoe adhabu kali kwa kuwa kitendo cha wizi alichofanya akiwa kama mtumishi wa umma ni kibaya, kinaitia hasara kubwa Serikali, pia suala la wizi katika Chuo cha ustawi limekuwa likitokea mara kwa mara Kitendo cha yeye kudhulumu wanafunzi siyo haki kwani ile ni hela ya walipa kodi,” alisema.

Katika utetezi wake, mshtakiwa Mnyawami, aliiomba mahakama hiyo kumpunguzia adhabu, kwani awali alikubali kulipa fedha hizo taratibu lakini taasisi ndiyo ilimkatalia.

“Dada yangu ni mgonjwa na mama yangu ni mjane na wote wananitegemea,”.

Katika mashtaka yake, anadaiwa May 31, 2014 katika Chuo cha ustawi wa jamii kilichopo Kijitonyama wilayani Kinondoni mtuhumiwa akiwa ameajiriwa kama Mhasibu wa Chuo hicho aliiba sh, 9,714,000 mali ya muajiriwa wake ambayo ameipata kutokana na nafasi yake kazini hapo.

Wanasiasa Wanaong'ang'ania Kukaa Kwenye Chama Kimoja kwa Muda Mrefu Bila Kuhama ni ‘Manungayembe’ – Mwita Waitara

$
0
0
Wanasiasa Wanaong'ang'ania Kukaa Kwenye Chama Kimoja kwa Muda Mrefu Bila Kuhama ni ‘Manungayembe’ – Mwita Waitara
Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Ukonga kwa tiketi ya CHADEMA, Mwita Waitara amedai kuwa wanasiasa wanaong’ang’ania kukaa kwenye chama kimoja kwa muda mrefu hao ni Manungayembe’.


Mwita Waitara kushoto kwenye picha.
Waitara amesema kuwa ukiona mwanasiasa kwa miaka yote haoni mafanikio wala maendeleo kwa kupinga kila kiongozi anayeingia madarakani basi ujue huyo ni Nungayembe.

Akifafanua kauli hiyo kwenye kipindi cha Jahazi cha Clouds FM, Mwita amesema kuwa kuna viongozi kuanzia awamu ya Mwinyi walikuwa wanaipinga serikali, awamu ya Mkapa hivyo hivyo, awamu ya Kikwete wanapinga na ya Rais Magufuli wanapinga tu ujue hao ni Manungayembe kwani mwanasiasa wa kweli ni lazima abadilike kuendana na mazingira.

Hata hivyo, kauli hiyo haijaeleweka kuwa amemulenga nani. Mwita alijiengua CHADEMA na kutangaza kujiunga Chama tawala cha CCM kwa kudai kuwa anaunga mkono juhudi za Rais Magufuli.

Mwita pia ameteuliwa na Kamati Kuu ya Halmashauri ya Taifa ya CCM kugombea Ubunge kwenye jimbo hilo la Ukonga na ameahidi kuchukua jimbo hilo kwa kishindo akidai kuwa anakubalika na wananchi wa jimbo hilo wameanza kukielewa Chama cha Mapinduzi.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Wema Sepetu Anunua Ugomvi wa Hamisa Mobetto na Zamaradi

$
0
0
Wema Sepetu Anunua Ugomvi wa Hamisa Mobetto na Zamaradi
Wakati bifu baina ya mtangazaji wa runinga, Zamaradi Mketema na mwanamitindo Hamisa Mobeto juu ya gauni la kushona likishika kasi, mrembo Wema Isaac Sepetu ameibuka na kununua ugomvi huo. Ishu nzima ilianzia Jumanne ya wiki hii ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zamaradi aliandika waraka mrefu wa kurasa tatu ukieleza namna alivyosikitishwa na Mobeto kwa sababu ya gauni alilovaa katika arobaini ya mtoto wake aitwaye King Salah iliyofanyika mwishoni mwa Julai, mwaka huu nyumbani kwake maeneo ya Bunju B jijini Dar.

Katika waraka huo, Zamaradi alionesha kusikitishwa na maneno yanayosambaa mitandaoni kuwa alipewa mshono na Mobeto kwa lengo la kushonewa, lakini akauchukua na kwenda kuushona kwa mtu mwingine huku akimwaga chati zote za WhatsApp walizokuwa wakitumiana.

Hata hivyo, kwa upande wa Mobeto naye aliibuka na kupinga vikali waraka huo. Wakati hayo yakiendelea, Wema kupitia ukurasa wake alinunua ugomvi kwa kuandika; Tuendelee ama tusiendelee’ ambapo swahiba wake wa karibu ambaye ni mbunifu wa mavazi, Martin Kadinda aliingilia kati kwenye komenti na kuandika; ‘Tusiendelee’.

Muda mfupi mara baada ya Wema kusema hayo, aliambulia maneno machafu kutoka kwa mashabiki tofauti wakimlaumu; “Ni bora ungekaa kimya kuliko kuingilia mambo yasiyokuhusu*** wee,” alikomenti shabiki mmoja huku wengine wakishadadia.

Meneja wa Wema, Neema Ndepanya naye hakukaa kimya, aliingilia kati na kumkingia kifua Wema kwa kuandika waraka wake. “Kiki za kuchafuana zilishapitwa na wakati, hakuna kitu kibaya duniani kama kuwa mnafiki, yaani nachukia mtu anajifanya kila wakati anaonewa yeye tu,” aliandika.

Baada ya kuyaona hayo yakiendelea mitandaoni, Ijumaa lilianza kwa kumsaka mnunua ugomvi, Wema ambaye simu yake iliita bila kupokelewa, likampigia simu Neema na alipopatikana alisema hajamkingia kifua Wema na hayupo upande wa mtu yeyote.

“Sasa unaniuliza mimi kwani ndiyo Zamaradi, Wema au Hamisa si uwapigie wahusika mimi ni mpenzi mtazamaji tu kama wewe sihusiki na chochote na wala sipo upande wa yeyote kati yao. Kama watu wametafsiri vingine ni shida yao mimi simo kabisa si unajua kila mtu anaandika kitu anachojisikia eeh basi nimejisikia tu kuandika mtu akisoma vizuri ataielewa, lakini ukikurupukia kuisoma lazima ulete maana nyingine,” alisema Neema.

Nape Nnauye "Sheria zipitiwe Kudhibiti Hama Hama Kwenye vyama vya Siasa"

$
0
0
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amesema ipo haja ya kupitiwa upya kwa sheria inayosimamia thamani ya kura hasa katika kipindi hiki cha wabunge na madiwani kuhama vyama vyao.

Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Agosti 16, 2018 katika ofisi ndogo za Bunge visiwani Zanzibar katika mafunzo ya siku mbili ya kamati ya uongozi, makamu wenyeviti wa kamati za Bunge pamoja na wajumbe wa tume ya utumishi wa Bunge.

Amesema pamoja na uwepo wa wimbi kubwa la wanasiasa kuhama, wapigakura wanatakiwa kupewa thamani yao kwa kuwa wakati wa uchaguzi wao ndio uhitajika kupiga kura kuchagua wawakilishi wao.

Amebainisha kuwa licha ya Katiba ya nchi na sheria mbalimbali kutominya fursa ya mwanasiasa kuhama chama kimoja na kwenda kingine, bado thamani ya mpiga kura inapaswa kuenziwa

“Siwezi kupingana na Katiba kuhusu hamahama za wanasiasa lakini ni vyema thamani za wapiga kura ikatambulika vyema,” amesema Nape.

Katibu huyo wa zamani wa Itikadi na Uenezi wa CCM, amesema ni vyema kukawa na sheria ambayo itampa mamlaka mbunge au diwani anayehama chama baada ya uchaguzi, aendelee kuwa na nafasi hizo katika chama anachokwenda.

Amesema jambo hilo likifanyika litaokoa kiasi kikubwa cha fedha kinachotumika katika chaguzi ndogo kwenye maeneo ambayo mbunge au diwani amehamia chama kingine.

Zifahamu Faida 6 za Juisi ya Tangawizi, Halafu Nenda Kajaribu Uone Ajabu Yake..!!!

$
0
0
Tangawizi ni kati ya viungo mahili vinavyochochea ladha nzuri katika vyakula vya aina mbalimbali na hivyo kuwavutia walaji kula chakula husika.

Tangawizi pia inapowekwa kwenye vyakula vigumu kama nyama huifanya ilainike na hivyo kuweza kuiva kwa haraka zaidi.

Leo nataka kukueleza msomaji wangu kuhusu hizi faida nyingine za kutumia juisi ya tangawizi kama ifuatavyo:-

1. Hutumika kama kituliza maumivu.

2. Husaidia kuboresha mmeng'enyo wa chakula tumboni

3. Huthibiti shinikizo la damu

4. Huboresha afya ya kinywa

5. Hukinga matatizo ya ngozi hasa chunusi

6. Husaidia kukuza nywele (kulinda afya ya nywele)

Download Hii Application Kwenye Simu yako Ujifunze Mambo ya Mapenzi na Kusoma Vimbwaga Vyake...Usipitwe

Mbwana Samatta Kaamua kweli Europa League...Atupia Goli

$
0
0
Club ya KRC Genk ya Ubelgiji inayochezewa na mtanzania Mbwana Samatta leo iliingia uwanjani kucheza game yake ya marudiano ya kuwania kucheza hatua ya Makundi ya UEFA Europa League dhidi ya Lech Poznan ya Poland.

KRC Genk ikiwa ugenini nchini Poland katika game ya marudiano baada ya game ya kwanza nyumbani Luminus Arena kupata ushindi wa magoli 2-0, leo tena wamepata ushindi mwingine wa magoli 2-1.

Magoli ya KRC Genk yalifungwa na Mbwana Samatta dakika ya 19 na Trossard kwa mkwaju wa penati dakika ya 45 wakati goli pekee la Lech Poznan lilifungwa na Cywka dakika ya 50. Hii ni game ya pili mfululizo Mbwana Samatta anaifungia goli KRC Genk

Serikali: Kila Mtanzania Atapaswa Kumiliki Laini Moja ya Simu, Ukitaka ya Pili Unaomba TCRA

$
0
0
DAR: Serikali imesema itaanza kudhibiti umiliki holela wa 'line' za simu na hivyo chini ya usajili wa 'line' kwa alama za vidole mtu akitaka kusajili 'line' zaidi ya mbili itabidi ajaze fomu ya kueleza kwa nini anataka 'line' ya pili.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Atashasta Nditiye aliyeeleza kuwa katika udhibiti huo watashirikiana na NIDA kupitia vitambulisho vya Taifa.

Amesema kuwa mtu akitaka kusajili 'line'ya pili ya simu Kampuni za simu zitamuona na kujua kuwa tayari ana 'line' ya kwanza, hivyo lazima atajaza fomu maalum kueleza kwa nini anataka 'line' ya pili.

Aidha, Naibu Waziri amesema kuwa kabla ya mwaka huu kuisha 'line' za simu zitaanza kuuzwa kwenye maduka rasmi na mtu anayesajili atachukuliwa alama za vidole na picha yake

VIDEO:

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0

KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa,

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako.

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada .

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI , PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA

Bifu la Young Dee na Amber Lulu Lafikia Hapatoshi

$
0
0
Bifu la Young Dee na Amber Lulu Lafika Pabaya
MSANII wa Muziki wa Bongo Fleva, Lulu Eugen ‘Amber Lulu’ amejikuta akiingia katika bifu zito na msanii mwenzake, David Genzi ‘Young Dee’ baada ya kumtolea maneno ya shombo katika ukurasa wake wa Instagram kwa kusema kwamba rapa huyo hawezi kuoa kwa sababu hicho si kitendo rahisi na ukiangalia yeye mwenyewe sasa hivi anatamani

kuolewa, hivyo kumtaka afanye muziki bila kutengeneza kiki kama anaweza. Maneno hayo ya Amber Lulu yalitokana na picha ya harusi iliyokuwa ikisambaa mitandaoni, huku watu na mastaa mbalimbali wakidai kuwa rapa huyo ameamua kuoa kimyakimya bila kumualika mtu yoyote

Akizungumza na Vijistori Mitandaoni, meneja wa Young Dee alisema kuwa; “Young Dee hawezi akabishana na mtoto wa kike halafu hata hivyo huyo Amber Lulu hawezi akafanya muziki mzuri bila kufanya kiki na tena ukiangalia kiki zake nyingi ni lazima amtaje Young Dee, kwa sababu anajua kuwa brand kubwa hivyo anaona akimtumia lazima atoboe,” alisema meneja huyo.

Amber Lulu naye huyu apa; “Niliongea vile kwa sababu najua Young Dee hawezi akatoa wimbo bila kufanya kiki, anadanganya watu kuoa wakati yeye mwenyewe anahitaji mtu wa kumuoa, halafu ukiangalia kiki ni kubwa kuliko wimbo anaotaka kuutoa yani kiufupi siku hizi muziki wake ushakufa labda ajipange upya,” alisema Amber Lulu.

Wamiliki wa Televisioni Waongezewa Msalaba Mwingine

$
0
0
Wamiliki wa Televisioni Waongezewa Msalaba Mwingine
KAMPUNI zinazomiliki minara ya kurusha matangazo ya televisheni zimetoa siku 30 kwa wamiliki wa vituo vya televisheni nchini kulipa gharama za kila mwezi vinginevyo zitaondolewa katika minara hiyo.

Kampuni hizo za minara zimesema televisheni za ndani kwa muda mrefu zinapatiwa huduma hiyo bila kulipia, jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Zimesema utaratibu uliowekwa kisheria unawataka wamiliki wa kituo cha televisheni kulipa Sh. milioni 2.4 kwa mwezi kwa kila mkoa au kanda ambayo inapata matangazo ya kituo husika.

Wawakilishi wa kampuni za Agape, Star Media na Basic Transmission, waliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam walipozungumza na waandishi wa habari.

Katika mkutano huo, Mch. Vernon Fernandos, mwakilishi wa kampuni ya Agape, alisema kuwa tangu mwaka 2010, televisheni za ndani (local channels) zimegoma kulipa gharama za kurusha maudhui yake.

Alisema katika kipindi chote, sheria ilikuwa inazitaka televisheni za ndani kulipia gharama za kurusha maudhui, lakini hilo halikufanyika kwa miaka nane sasa.

"Tunatoa mwezi mmoja kwa televisheni zote kulipa gharama za kurusha maudhui wanayoandaa na baada ya kipindi hicho kumalizika, wakigoma kulipa tutakaa na Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano (TCRA) na wamiliki wa televisheni hizo na kuziondoa zisionekane," alisema.

"Baada ya kuondolewa kuonyeshwa bure, itamlazimu mtumiaji wa mwisho ambaye ni mwananchi anunue king'amuzi cha kampuni hizo, ili kupata matangazo ya televisheni hizo."

Alisema hadi sasa kampuni hizo tatu zina minara 47 ya kurusha matangazo kwa nchi nzima inayotumiwa na televisheni za ndani 34.

Aliongeza kuwa kila televisheni ina leseni ambayo inaonyesha inatakiwa kurusha matangazo katika eneo gani na la ukubwa gani.

Kwa mujibu wa Fernandos, televisheni za kitaifa ambazo zinaonekana mikoa yote pia zitatakiwa kulipa gharama kulingana na ukubwa wa eneo ingawa alisema bado kuna nafasi ya mazungumzo ili kuwapunguzia bei ya kurusha kwa kila mwezi.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Kampuni ya Star Media, Justin Ndege, alisema kwa muda wa miaka nane wamekuwa wakipata hasara kwa kuwa televisheni za ndani zimegoma kulipa.

Alisema kampuni hizo zimetumia mtaji mkubwa katika uwekezaji na wanaona sasa ni wakati mwafaka kwa televisheni hizo kulipa gharama kwa mujibu wa sheria.

WIZARA YAJITOSA

Wakati hayo yakijitokeza, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji imesema itaingilia kati mvutano uliopo kati ya TCRA na kampuni zinazorusha chaneli za televisheni nchini.

Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Stella Manyanya, alisema mkoani Pwani jana, kuwa wizara yake inalichukulia umuhimu suala hilo kwa kuwa ni la biashara na uwekezaji.

Katika ziara ya Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kwenye kiwanda cha kuchakata matunda na vinywaji baridi cha Kampuni ya Bakhresa mkoani Pwani, Manyanya alisema watahitaji kujua zaidi na kuona suala hilo linapatiwa ufumbuzi wa haraka.

"Sisi tunalichukulia suala hili kama la biashara, tutapenda kulifahamu zaidi…je, TCRA na wamiliki wa ving'amuzi hawawezi kukaa pamoja na kutatua tatizo hili? Sisi ni viwanda, biashara na uwekezaji, hivyo kuna uwekezaji na biashara hapo na tuna wajibu wa kulifuatilia," alisema.

Aliwataka wamiliki wa ving'amuzi nchini kutokuwa na mazoea ya kukimbilia mahakamani kwa kuwa suala kama hilo linazungumzika.

"Tunaamini bila nyie nchi haiwezi kwenda na tunapenda Watanzania wapate habari, pia nina hakika serikali ni sikivu na imekuwa ikitatua kero nyingi zinazogusa Watanzania, hivyo hata suala hili litapatiwa ufumbuzi karibuni," alisema.

Mjumbe wa kamati hiyo na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tabora, Hawa Mwaifunga, alitaka ufafanuzi kutoka kwa uongozi wa Kampuni ya Azam Media kuhusu kuzuiwa kwao kurusha chaneli za ndani kupitia king’amuzi cha Azam TV.

"Mimi naomba kujua na kupata sababu nini kilitokea hadi mmezuiliwa kurusha chaneli za ndani?" Mwaifunga alihoji.

Akijibu swali hilo, Mkuu wa Uhusiano na Masuala ya Ndani wa Kampuni ya Bakhresa Group, Hussein Sufiani, alisema chanzo cha zuio hilo ni mabadiliko ya sheria.

Alisema kuna haja kwa serikali kupitia upya na kuzifanyia marekebisho sheria ili ziendane na wakati uliopo.

"Kama sheria mpya hazitambui sheria za zamani, basi kuna haja zibadilishwe ili ziendane na za sasa," Sufiani alisema.

Wiki iliyopita, TCRA ilitishia kuzinyang'anya leseni kampuni za Multichoice Tanzania Limited na Simbanet Tanzania Limited kwa kukiuka masharti ya leseni zake kurusha maudhui ya nje na kuuza maudhui ya ndani kwa muundo wa malipo ya kabla.

Lugola Atoa Amri kwa Polisi Kuwakamata Wanafunzi Watoro

$
0
0
Lugola Atoa Amri kwa Polisi Kuwakamata Wanafunzi Watoro
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewapa wiki moja Jeshi la Polisi Wilaya Bunda, kuwakamata wanafunzi watoro, wazazi wa wanafunzi watoro pamoja na watu waliowarubuni wanafunzi wa kike ambao wameacha shule wilayani humo.

Lugola ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, wilayani Bunda, Mkoa wa Mara, alisema inamsikitisha sana idadi kubwa ya wanafunzi wilayani humo wameacha masomo yao na kurubuniwa wanaume ili waweze  kuolewa huku Serikali ikitangaza elimu bure kuanzia shule za msingi mpaka kidato cha nne.

Akizungumza na mamia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa mpira wa miguu wa Busambara, Kijiji cha Busambara, Kata ya Kitengule, wilayani humo, Lugola alisema kiwango cha wanafunzi kuacha masomo inatisha, hivyo serikali haiwezi kukaa kimya, lazima kuhakikisha wanafunzi hao wanasoma ili waje kuwa viongozi wa nchi.

“Mkuu wa Polisi wa hapa Bunda, nawapa wiki moja, mtumie elimu zenu za upelelezi mliofundishwa, wakamateni, wachunguzeni, wahojini ndugu,  jamaa, majirani mtawawapata wote wanaowarubuni watoto hawa, halafu mushughulike nao,” alisema Lugola.

Pia Lugola aliongeza kua,  kuna sheria zinazoshughulika na wanafunzi watoro na pia zipo sheria zinazoshughulika na wazazi wa wanafunzi watoro, pia zipo sheria zinazowashughulikia wanaume wanaowarubuni wanafunzi, hivyo haiwezekani wanafunzi wa kidato cha tano wakatae masomo, na wengi wao wanaokataa masomo ni wasichana.

Aidha, Lugola alisema ujenzi wa sekondari mbili za kidato cha tano na sita unaendelea ambapo katika kata za Nansimo na Muramba katika Jimbo lake la Mwibara zitanaanza kuchukua wanafunzi mwaka ujao watakao fanya mtihani wa kidato cha nne mwaka huu.

“Tunaendelea kuweka miundombinu katika shule hizo ili ziweze kuchukua wanafunzi wa kidato cha tano katika maeneo haya na hatutarajii wanafunzi kukosa shule wamalizapo kidato cha nne,” alisema Lugola.

Hata hivyo, Lugola pia aliwataka polisi nchini kuwakamata waendesha magari na bodaboda ambao hawafuati sheria za barabarani ikiwemo baadhi ya bodaboda uvunja sheria kwa makusudi kwa kupakia abiria wanne na kuendelea ambapo ni hatari kwa usalama wa dereva na abiria hao.

“Idadi kubwa ya polisi wanafanyakazi kwa umakini na uaminifu mkubwa, ila wachache sana ndio wenye tabia hizo mbaya, nawataka askari hao wafuate sheria na pia kuendelea kuzikamata kama ni magari au bodaboda au wananchi wowote ambao wanavunja sheria za nchi,” alisema Lugola.

 Waziri Lugola yupo katika ziara jimboni kwake kwa kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuwaunganisha wananchi kupitia Bonanza lake la michezo ya mpira wa miguu ambalo linashirikisha kila kata wakitoa washindi mbalimbali ambao anawapa zawadi pamoja na kuingia moja kwa moja katika mashindano ya kugombea Kombe la Kangi.
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live




Latest Images