Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

BABY MADAHA "DIAMOND NI WA "HAPA HAPA" MIMI WA INTERNATIONAL"

$
0
0
Baby Madaha amesema kamwe hawezi kucheza ligi moja na Diamond Platnumz. Akiongea na kipindi cha Hot Mix cha EATV Ijumaa hii, muimbaji na muigizaji huyo wa ‘The Gal Bladder’ amesema Diamond ni msanii ‘wahapahapa’ huku yeye akifahamika kimataifa zaidi

Aliongeza kuwa pamoja na kufanya muziki, yeye pia ni muigizaji mzuri wa filamu wakati Diamond ni muimbaji peke yake na hivyo kamwe hawezi kuwa level moja na hitmaker huyo wa Roho Yangu.

Kwa muda sasa, mafahari hao wamekuwa wakirushiana madongo huku Baby akisema Diamond hajui kuimba kulinganisha na msanii kama Ali Kiba.

JOHN MNYIKA "NIMEMTUMIA BARUA WAZIRI WA MAJI PROF.JUMANNE MAGHEMBE KUMSHAURI AJIUZULU"

$
0
0
Waziri wa Maji Prof. Maghembe Ajiuzulu,Dawasa/Dawasco warejeshe huduma ndani ya wiki moja katika maeneo yaliyokuwa yakipata mgao wa maji kabla

Nimemtumia ujumbe Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe kumshauri ajiuzulu kutokana na kujirudia rudia kwa matatizo ya maji katika Jiji la Dar Es Salaam kinyume na maelezo yake ya uongo aliyoyatoa bungeni tarehe 4 Februari 2013.

Aidha, Wenyeviti wa Bodi na Watendaji wakuu wa Mamlaka zinazohusika na huduma ya maji jijini (DAWASA na DAWASCO) watoe maelezo kwa umma juu ya sababu za kweli za matatizo ya maji kujirudia rudia katika Jiji la Dar Es Salaam.

Pia, wajieleze kwa umma ni kwanini wananchi wasipendekeze Rais awachukulie kwa uzembe, kuisababishia hasara Serikali, kuathiri uchumi wa nchi na maisha ya wananchi kwa kukosa maji mara kwa mara ambayo ni huduma ya msingi ya
binadamu na malighafi muhimu katika uzalishaji.

Itakumbukwa kwamba tarehe 4 Februari 2013 niliwasilisha hoja binafsi bungeni juu ya hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa maji katika jiji la Dar Es Salaam, nikipendekeza Bunge kuingilia kati kuweza kuisimamia Serikali kuchukua hatua za haraka.

Iwapo hoja hiyo ingejadiliwa na maazimio yote kutekelezwa matatizo ya maji katika Jiji la Dar Es Salaam mpaka hatua ya sasa yangekuwa yamepungua katika maeneo mbalimbali kutokana na hatua ambazo nilipendekeza zichukuliwe.

Hata hivyo, badala ya kuunga mkono hoja hiyo ambayo ingeisaidia Wizara yake na kurekebisha udhaifu uliokuwepo na hivyo kumrejeshea imani kwa umma ambavyo ilikuwa imepungua; Waziri Maghembe akaamua kinyume cha kanuni za Bunge kutoa hoja ya kuondoa hoja niliyowasilisha.

Katika hatua hiyo nilijaribu kutumia kanuni za Bunge kuweza kutoa ufafanuzi juu ya uongo wa Waziri Prof. Maghembe na hatua ambazo Bunge lilipaswa kuchukua. Hata hivyo Naibu Spika wa Bunge Job Ndugai aliamua kukiuka kanuni kumlinda hali ambayo ilichochea vurugu bungeni.

Mara baada ya kurejea bungeni tarehe 10 Februari 2013 nilihutubia wananchi na kuwaeleza kusudio la kuandaa maaandamano kwenda Wizara ya Maji iwapo katika kipindi cha ndani ya wiki mbili Waziri Prof. Maghembe asingejitokeza kutoa maelezo kwa umma kuhusu masuala yote ambayo alipaswa kuyajibu bungeni juu ya hatua za haraka zilizopaswa kuchukuliwa.

Ndani ya wiki hizo mbili Waziri Maghembe alijitokeza mara mbili kuzungumzia masuala ya maji Dar Es Salaam; kupitia mikutano ya CCM ikiwemo katika kata ya Goba jimboni Ubungo na katika mkutano wake na wafanyakazi DAWASA na DAWASCO tarehe 21 Februari 2013 na kueleza hatua za haraka ambazo angesimamia zichukuliwe.

Hata hivyo, baada ya wiki moja bila ya Waziri wa Maji na Wizara kwa ujumla kuonyesha kwa matendo kuisimamia kwa karibu EWURA, DAWASA, DAWASCO na Manispaa ya Kinondoni kuchukua hatua za haraka ambazo nilizieleza kwenye hoja binafsi, niliamua kuchukua hatua zaidi.

Nilitangaza kuongoza maandamano ya wananchi tarehe 16 Machi 2013 kwenda Wizara ya Maji ili kupata majibu na kuisimamia Serikali kuchukua hatua za haraka. Hata hivyo maandamano hayo yalizuiliwa na Jeshi la Polisi kwa sababu zisizo za msingi na kuombwa kukata rufaa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani.

Nilikata rufaa lakini toka wakati huo mpaka anaondelewa katika nafasi yake Waziri Dr Emmanuel Nchimbi alikwepa kuchukua hatua dhidi ya aliyekuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni Charles Kenyela kwa kuvunja sheria, kusababisha hasara na kuwanyima haki ya msingi wananchi ya kufikisha ujumbe kwa Serikali.

Maandamano hayo yangefanyika na hatua kuchukuliwa matatizo yangepungua tofauti na ilivyo sasa, hivyo Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Pereira Silima anapaswa kueleza umma lini rufaa hiyo itashughulikiwa maandamano yaweze kufanyika wananchi wapate majibu ya hatua za haraka nilizopendekeza ndani na nje ya Bunge.

Zaidi ya nusu mwaka umepita toka Waziri Prof. Maghembe atoe ahadi ambazo ameshindwa kusimamia utekelezaji wake na hivyo kupaswa kujiuzulu. Iwapo Waziri Prof. Maghembe hatajiuzulu nitaeleza hatua zaidi ambazo nitachukua.

Wakati hatua hizo zikisubiriwa, natoa mwito kwa DAWASA na DAWASCO kuhakikisha kwamba katika kipindi kisichozidi wiki moja huduma za maji zinarejea katika maeneo ambayo yalikuwa yakipata mgawo wa maji.

Wenu katika uwakilishi wa wananchi,

John Mnyika (Mb)
10/01/2014

SIKILIZA/DOWNLOAD WIMBO MPYA WA LADY JAY DEE- HISTORIA

$
0
0
Lady Jay Dee aka Binti Commando/ Anaconda ameachia wimbo mpya unaoitwa Historia, wenye ujumbe wa kijamii unaohamasisha watu kujituma ili kuhakikisha kuwa hawabaki kuwa ‘Historia’ kabla siku haijafika, isiwe 'alikuwa nazo' ni bora kuwa 'anazo'.
“Utakubalije uwe historia kabla siku yako haijafika?” Anaimba Lady Jay Dee.
Usikilize hapa:

HUWEZI AMINI HUYU JAMAA AJAOGA WALA KUGUSA MAJI KWA MIAKA 60

$
0
0
Amoo Hadji, an 80-year-old Iranian man, has not taken bath for 60 years, according to the city website Bavanat.com.

His skin is scaly, you can barely see his eyes and he smells to high heaven. The reason for it is as simple as that: he has just refused to take a bath for sixty years now.

Hadji leads a fairly primitive life, with his most prized possession being a three-inch steel pipe that he smokes animal dung with.

Living in the village of Dezhgah (city of Farashband in Fars province of Iran), he seems to blend in with his surroundings.





LIGI KUU UINGEREZA::MANCHESTER UNITED WAICHAPA SWASEA GOLI 2 BILA

$
0
0
Manchester United halted their three-match losing streak as second-half goals from Antonio Valencia and Danny Welbeck eased the pressure on beleaguered manager David Moyes.
At Old Trafford, where Swansea won for the first time in last weekend's FA Cup tie, the Welsh side were unable to repeat their heroics as United rediscovered the form that earned them six straight wins before that awful start to 2014.


NINA DATE NAE WEEK YA PILI SASA..ANANIULIZA NINA MPANGO GANI WA NDOA

$
0
0
Habari ya mwaka ndugu,naam kama ilivyo ada tena kwa mara nyingi ni true story
Kuna mdada nina date naye week ya pili sasa ,tangia nimemjua kwa ukaribu its about mwezi na nusu ,jana ameanza kubadilika tofauti na alivyokua mwanzo,baada ya kumuulizia (just inquisitive) sana amekuja na swali Nina mpango gani na yeye?
Kiukweli hii issue imeniacha mdomo wazi imenistua honestly two weeks?hata sijamjua kiundani,nikafanya categorisation zangu ananiuliza nina mpango naye gani?
Kwa utafiti nilioufanya haraka haraka nimeshtukia kuwa rafiki zake wengi wameolewa na mara kadhaa ndani ya mwezi mmoja na nusu niliojuana naye amewahi kuniaga anaenda send off,na wedding party kadhaa
Swali sasa kwa wanaukumbi walioa au ma single pia, hivi ndani ya week mbili tatu unaweza kuweka promise ya ku engage au oa?Au ndo dunia ya digitali
Hapa nazungumza baada ya kubanwa sana nina mpango gani niliahidi RING ENGAGEMENT ambayo tarehe wala mwezi sijaweka clear kwa sababu machale yamenicheza huyu mtu anaji pretend na anatafuta pa ku fulfill marriage ambition yake(hii ndo tafsiri yangu) so far mambo kama haya ndo yanatunga mimba na kuzaa mauti ndani ya ndoa baadae na moyo wangu hauko radhi kabisa

Naomba kuwasilisha,mnipe mawazo ,experience ,knowledges zenu nanyi wana board huenda nami pia nimekosea
Tiririka

WALIOTANGAZA NIA YA URAIS CCM MTEGONI

$
0
0
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umeshauri Kamati ya Maadili ya CCM kuwaonyesha mlango wa kutokea wote walioanza kampeni za kugombea urais, ubunge na nyingine kinyume cha maadili ya chama.

Umesema wagombea hao ambao umewaita wasio rasmi, wameonywa mara kadhaa na viongozi wa chama ikiwamo kupitia kwenye vyombo vya habari, lakini wameshindwa kujitambua na kujirekebisha.

UVCCM umedai wagombea hao wasio rasmi katika kampeni zao tayari wameanza kusababisha kutoweka kwa mshikamano ndani ya chama, kwani wamekuwa wakipita nchi nzima kushawishi kwa fedha na rushwa nyingine mbalimbali makundi ya jamii ili kuungwa mkono.

Mkuu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi Taifa, Paul Makonda alisema Kamati ya Maadili ya CCM ina wajibu wa kutafsiri hasira ya wanaCCM dhidi ya kampeni hizo ambazo zinakijeli chama, uongozi wa nchi uliopo na kuleta nyufa.

“Tunachokiona sasa ni tofauti kabisa na malezi na makuzi yetu ndani ya chama, kwani tayari baadhi ya wanaCCM bila uoga wala aibu wameshajitangaza ni wagombea urais, ubunge, udiwani na nafasi nyingine za kupigiwa kura, wameanza kampeni za kishindo za rushwa na vishawishi mbalimbali nje kabisa ya utaratibu, kanuni na maadili ya chama,” alisema Makonda na kuongeza:

“Watu hawa waonyeshwe mlango wa kutokea, tusipoziba ufa huu sasa tujiandae kujenga ukuta mwakani kwa gharama kubwa kupindukia.”

Makonda alisema kwa sababu mwaka huu kuna mchakato wa chaguzi mbalimbali zitakazohitimishwa mwakani na ushaguzi mkuu, mshikimamo wa hali ya juu unahitajika ndani ya chama.

“Kwa sasa ilani ya CCM ya mwaka 2010 imewekwa pembeni, kinachonadiwa ni ilani binafsi za kumwaga fedha nchi nzima, kusambaza elimu kama njugu, bila kueleza vyanzo vya mapato ya Serikali zao za kusadikika,” alisema. Alisema hatua hiyo ni ukiukwaji mkubwa wa sheria za chini, maadili, miiko ya chama.

pamoja na Serikali kwa ujumla ambapo ipo wima katika kuhakikisha kuwa ilani ya CCM ya mwaka 2010 inatekelezwa kwa ufanisi mkubwa.

Alisema CCM inataratibu zake za kupata viongozi na wote tunazijua, kufanya kinyume na taratibu hizi ni uasi, upungufu wa busara, na ukosefu wa sifa ya uongozi.

“ Hivyo vijana wa CCM tunamuunga mkono Mwenyekiti wa CCM taifa Dk Jakaya Kikwete, Makamu Mwenyekiti, Philiph Mangula na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama Nape Nnauye waliokemea tabia hii mpya hatarishi kwa chama chetu ya kuhaha kupata uongozi nje ya taratibu na kutumia vishawishi vyenye sura ya rushwa vitakavyokitia doa chama,”

Makonda alisema kuwa maadili na kanuni za chama ni kuwaunganisha wanaCCM wote kuwa kitu kimoja, hivyo dalili zozote nje ya tunu hizo ni usaliti, uasi ambao hauna budi kupigwa vita kwa nguvu zote kwa vijana.

WASOMI WANENA:CHADEMA WAJICHULIA KIFO WAO WENYEWE

$
0
0
*Wasomi ndani, nje ya chama wakitabiria anguko
*Wasema kisipochukua hatua kitafika 2015 kikiwa dhaifu
SAFARI ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuelekea katika uchaguzi mkuu wa 2015 imeelezwa kuwa ni yenye kutia shaka na kimetabiriwa kufika mwaka huo kikiwa dhaifu.

Mwenendo wa matukio ambayo umma umeendelea kuyashuhudia ndani chama hicho wiki hii, msingi wake ukiwa ni kuvuliwa uongozi Zitto Kabwe na kuvuliwa uanachama kwa Dk. Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba, ndiyo yaliyoibua hisia za namna hiyo miongoni mwa umma na jamii ya wasomi walioko ndani na nje ya chama hicho.

Tayari baadhi ya wasomi na wanasiasa wenye ushawishi hapa nchini, wakiwemo viongozi wa kada mbalimbali, wamekwisha kukaririwa kwa nyakati tofauti wakieleza kuona hatari ya kifo inayokikabili Chadema, kutokana na uamuzi wake huo wa kuwavua uanachama makada wake wawili na kutishia kuchukua uamuzi kama huo kwa Zitto.

Ndani ya Chadema na katika Kamati Kuu ya chama hicho, baadhi ya wajumbe wake nao wamekaririwa kutoa kauli zinazoonyesha kuona hatari ya kifo inayokikabili chama chao.

Mbunge wa Iringa Mjini, Mchugaji Peter Msigwa,  amekaririwa ndani ya Kamati Kuu ya chama hicho hivi karibuni, akisema kuwa ni heri chama hicho kipoteze Uchaguzi Mkuu wa 2015, lakini Zitto aondolewe.

Mbali na Msingwa, miongoni mwa wasomi wanaoheshimika hapa nchini, na makada wa chama hicho, Mabere Marando na Profesa Mwesiga Baregu, nao wametoa kauli za kukionya chama hicho juu ya uamuzi wake huo na kueleza hatari wanayoiona mbele.

Marando amesikika ndani ya Kamati Kuu ya chama hicho akisema kuwa, anaona mwelekeo ule ule wa NCCR-Mageuzi kuipata Chadema.

Ni kutokana na hilo, matukio ya hivi karibuni kabisa ya kutekwa na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa chama hicho Wilaya ya Temeke, Joseph Yona, lakini pia kuzuka vurugu ndani ya Kamati Kuu na lile la wafuasi wa chama hicho walio katika pande mbili zinazopingana, kupigana nje ya Mahakama Kuu ya Dar es Salaam, ambako Zitto alikuwa akitafuta haki yake ya uanachama, yanafananishwa na yale yaliyopata kutokea ndani ya chama cha NCCR-Mageuzi kati ya miaka ya 1990 na 2000.

Inaelezwa kuwa miongoni mwa mambo ambayo yalichangia chama cha NCCR-Mageuzi, ambacho kilikuwa chama kikuu cha upinzani nchini kupoteza nguvu zake wakati huo, ni migogoro ya kiuongozi ambayo ilisababisha watu kutwangana hadharani, kama ilivyo sasa kwa Chadema.

Tayari Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, amekitaka Chadema kujiepusha na vurugu na uvunjifu wa amani wakati kinapotatua mgogoro wake na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wake, Zitto Kabwe.

Wakati hayo yakitokea, huko Kigoma baadhi ya wananchi nao wamekaririwa wakieleza kufedheheshwa na kauli iliyotolewa na baadhi ya viongozi wa Chadema ya kumuita Mbunge wao kuwa ni Mbunge wa Mahakama na wametamka bayana kwamba iwapo Zitto atatimuliwa, chama hicho kisahau kuungwa mkono mkoani humo.

Askofu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana anayetoka Mkoa wa Kigoma, Dk. Gerald Mpango, ambaye amekuwa mpenzi mkubwa wa siasa za mageuzi na ameshiriki mikakati mingi ya kuijenga Chadema, amesikika akisema kuwa hatua ya kumtoa Zitto haitakiacha salama chama hicho, licha ya kuwahi kufanya hivyo kwa Dk. Amani Kabourou na David Kafulila.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                      

Wasomi ambao wameelezea matukio yanayotokea ndani ya Chadema, wameonyesha shaka kama chama hicho kitaweza kufanya vizuri katika uchaguzi mkuu ujao na kuonya kuwa kisipotafuta suluhu mapema, kuna dalili za kuanguka.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Prosper Ngowi, aliliambia Gazeti hili kwamba nyakati hizi si sahihi kwa chama hicho kuweka kipaumbele migogoro.

“Katika hili naweza kusema kuwa hiki si kipindi kizuri kwa Chadema kulumbana, kwasababu kama tunavyofahamu kuwa tunaelekea katika kipindi cha uchaguzi mkuu mwaka 2015, nilitarajia Chadema kama chama kikubwa cha upinzani kingetumia muda huu kujiimarisha zaidi kiweze kufanya vizuri katika uchaguzi wa 2015.

“Priority (kipaumbele) yao kwa sasa kilitakiwa kiwe kuangalia namna nzuri ya kuweka mikakati imara ya kuongeza madiwani, kuchukua viti vingi zaidi katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu, lakini pia kushinda majimbo mengi zaidi na ikiwezekana hata katika nafasi ya urais,” alisema Profesa Ngowi.

Alisema anashangazwa na kitendo cha sasa cha kuweka malumbano kama kipaumbele chao, hali ambayo inawadhoofisha katika kupanga mikakati imara ya ushindi.

“Wataalamu wa masuala vya vyama vingi wanasema kuwa kila lengo kubwa la chama cha upinzani, ni lazima katika kutafuta hiyo dola kuwe na mipango ya muda mrefu, sasa naona kama Chadema, moja ya chama kikubwa cha upinzani wameacha kufanya hilo kwa sasa na wameweka nguvu kubwa katika kutafuta migogoro, jambo ambalo linaweza kuwaangusha,” alisema Profesa Ngowi.

Alisema mgogoro uliopo kwa sasa hawezi kusema mshindi ni nani, bali busara inapaswa kutumika kumaliza tatizo lililopo kuweza kupata mwelekeo mzuri kuelekea mwaka 2015.

“Naweza kusema kuwa bado wana nafasi ya kusuluhisha hadi kufikia uchaguzi wa serikali za mitaa na kuelekea uchaguzi mkuu ujao,” alisema Profesa Ngowi.

Kwa upande wake, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria (OUT), Profesa Peter Maina, alisema mambo yaliyojitokeza yataifikisha Chadema 2015 ikiwa dhaifu.

Alisema mgogoro uliojitokeza mpaka Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto kukimbilia Mahakamani, umetokana na uongozi wa chama hicho kushindwa kutumia busara kutatua mgogoro huo mapema.

“Niseme tu kwamba kuna watu ndio wameufikisha huu mgogoro hapo ulipo, ilikuwa rahisi kutumia busara kuumaliza pale wenzake na Zitto (Dk. Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba) walipokiri kuandaa waraka na kusema ulikuwa siyo kwa nia mbaya.

“Lakini kuna watu wazito ndani ya Chadema kama kina Profesa Safari, Mabere Marando na wengine walipoona jambo hili inasemekana waliomba suluhu ya haraka, lakini inaonekana kuna watu upande wa chama hicho hicho hawataki suluhu na matokeo yake ndiyo haya ya kupelekana Mahakamani,” alisema Profesa Maina.

Alisema kitendo cha kulumbana nyakati hizi ni kusababisha  chama hicho kuingia katika uchaguzi mkuu kikiwa dhaifu.

“Huu ni wakati wao wa kutafuta suluhu, naamini chama hakitakufa, lakini kitafika katika uchaguzi mkuu kikiwa dhaifu, hakitakuwa na nguvu kama ya awali, lazima viongozi wa Chadema wafahamu kuwa wakati mwingine haraka haina faida, uharaka uliotumika kushughulikia mgogoro haukuwa na faida.

“Kwa mfano, angalia Katibu Mkuu wa chama, Dk. Willibrod Slaa alivyofanya kipindi kile, badala ya kusuluhisha mgogoro, yeye anakwenda jimboni kwa Zitto kufanya mkutano, hapa inaonekana dhahiri hakuwa na nia ya kuleta suluhu, bali kuendeleza mgogoro, nafikiri busara hazikutumika toka awali na ndiyo maana leo hii mgogoro umekuwa mkubwa,” alisema Profesa Maina.

Katika hatua nyingine, Profesa Maina alisema kauli ya mwasisi wa chama hicho, Edwin Mtei, ya kusema Zitto hatakiwa ndani ya Chadema, inakiumiza zaidi chama, kwani haionyeshi demokrasi katika chama.

“Kauli ya Mtei inazidi kuonyesha nia ovu waliyonao baadhi ya watu ndani ya Chadema, kusema Zitto akatafute chama siyo maneno ya kuonyesha ukomavu kidemokrasia, niseme kwamba Mtei yeye anakiumiza zaidi chama, huu siyo wakati wa kulumbana ni wakati wa kutafuta suluhu kurudisha heshima ya chama.

Akizungumzia kitendo cha Zitto Kabwe kukimbilia Mahakamani alisema mbunge huyo amefanya hivyo kujikinga kutokana na hatua zilizopangwa kuchukuliwa dhidi yake.

“Kitendo cha Zitto kukimbilia mahakamani si kitendo cha ajabu bali amekwenda sehemu aliyoona haki itatendeka dhidi yake, unapoona mambo yanafanywa na mpinzani wako na unaona unaweza usitendewe haki una haki ya kwenda Makahamani kwahiyo wanaosema kwamba Zitto amekosea si kweli kwasababu yeye si mtu wa kwanza kwenda Mahakamani,” alisema Profesa Maina.
Mtanzania

LINEX "NATUNGA NYIMBO KWA AJILI YA MAHARUSI..SPECIAL WEWE NA MPENZI WAKO"

$
0
0
Wasanii wa Tanzania kwa sasa wamekua na mbinu nyingi za kujiongezea kipato mbali na kipato wakipatacho kwa sasa ambacho ni showz na kuuza miito ya simu lakini kwa sasa wengi wanajaribu kufikiria upande mwingine wa kuweza kupata shilingi,Miongoni mwa hao ni Linex.

Linex leo kwenye ukurasa wake wa Facebook ameandika ujumbe ambao unawahusu wachumba wanaotegemea kuoana ambapo yeye katangaza rasmi kujihusisha na utungaji wa nyimbo ambao utakuhusu wewe na mwenzi wako,Ujumbe wake kwenye Facebook ulisomeka hivi.

MTOTO WA MAREHEMU WHITNEY HOUSTON AOLEWA KWA NDOA NA KAKA YAKE

$
0
0
Stori inaamplfy kwamba mtoto wa mwimbaji staa Marehemu Whitney houston, Bobbi Kristina amevunja mapendekezo ya familia yake ya kutoolewa na kijana ambae ni kama kaka yake, mshkaji ambae alilelewa toka mdogo na Whitney na wao wote kuishi nyumba moja.
Pamoja na kushupaliwa kutoolewa, Bobbi ambae ana umri wa miaka 20 amethibitisha kuolewa na boyfriend huyu aitwae Nick Gordon ambae wamekua mapenzini kwa miaka kadhaa ambapo sasa hivi kama wanajipanga kuja na show yao ya TV.

GARI AINA YA TOYOTA NADIA 2000 MODEL INAUZWA KWA BEI POA

$
0
0
Toyota nadia 2000 model just arrived from Japan.
Fully duty paid
Comprehansive insurance
Color silver
Call/whatsapp 0768570703
Bei inaanzia Mil 10 Maelewano yapo .

RAIS KIKWETE ATANGAZA KUWA KESHO JUMATATU NI SIKU YA MAPUMZIKO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza kuwa kesho, Jumatatu, Januari 13, 2014, itakuwa ni Siku ya Mapumziko (Public Holiday) kwa Watanzania wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.


Rais Kikwete ameutangaza uamuzi huo mjini Zanzibar ambako leo ameungana na Watanzania na Wazanzibari wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, mwaka 1964.


Mapinduzi hayo yaliyoongozwa na mwasisi wa Zanzibar na Taifa la Tanzania, Hayati Abeid Amaan Karume yalifanikiwa kuung’oa madarakani utawala dhalimu wa Sultan na kuwawezesha kwa mara ya kwanza katika historia Waafrika walio wengine kujitawala ndani ya nchi yao wenyewe.


Yalikuwa ni Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofungua njia ya kuzaliwa kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar – miezi mitatu baada ya Mapinduzi hayo – Aprili 26, 1964.


Naye Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein ametangaza kuwa kesho itakuwa Siku ya Mapumziko Tanzania Visiwani kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.


Rais Shein alitangaza mapumziko hayo wakati alipohutubia wananchi kwenye Uwanja wa Michezo wa Amaan mjini Zanzibar katika kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi.

WEMA SASA MAMA KIJACHO KITUMBO HAKIFICHIKI...GUESS WHO IS THE BABA KIJACHO!

SWALI LA MSINGI: NANI HASA NI WAASISI WA MAPINDUZI?

$
0
0
Kwenye historia ya Mapinduzi tufundishwayo shuleni, hayati Sheikh Abeid Amani Karume ndiye anayekua mioyoni mwetu kama muasisi na kinara wa Mapinduzi yaliyofanyika Zanzibar tarehe 12 Januari 1964. Pamoja naye, Abdulrahman Babu, Thabit Kombo Jecha, Abdallah Kassim Hanga na wengineo pia wanajulikana kama waasisi wa Mapinduzi.

Lakini hata hivyo, tunavyoendelea kukua na kudadisi zaidi haswa tukisikiliza stori za wazee wetu waliokuwepo wakati wa Mapinduzi, tunasikia majina mengine ambayo hayatajwi sana kwenye mapambano dhidi ya utawala dhalimu wa Kisultani uliodumu kwa miaka 133 visiwani Zanzibar. Jina kama John Okello ni miongoni mwa majina ambayo yamesahaulika katika kuyapa sifa.

Katika stori hizo, tunaambiwa kwamba viongozi waandamizi wa ASP na vyama vingine, hawakuwepo Zanzibar usiku wa Mapinduzi. Pia, tunaambiwa kwamba, Sheikh Abeid Amani Karume alikuwa ni 'muoga' wa vita kiasi cha kukimbia Zanzibar wakati Mapinduzi yakifanyika. Inasemekana kwamba, Mapinduzi ya Zanzibar yalifanyika kwa nguvu ya vikundi vidogo vidogo mbali mbali ambavyo havikuwa na mpango mmoja. Vikundi vyote vilitumia advantage hiyo baada ya vijana wa Okello wakiongozwa naye, kuteka kituo cha Polisi cha Ziwani na kuchukua silaha za rashasha.

Wakati haya yote yakitendeka, Karume alikuwa Dar-es-salaam huku vijana wengine wasio wa ASP wakishughulika na Mapinduzi. Tunaendela kuambiwa kuwa, baada ya Mapinduzi kufanyika, Okello ndiye aliyemuamuru Karume kurudi Zanzibar na kumpa urais. Najiuliza maswali mengi kuhusu stori hizi.

Je, ni kweli kwamba hayati Sheikh Abeid Amani Karume ndiye muasisi wa Mapinduzi Zanzibar? Je, stori nzima ya mapambano yaliyodumu kwa saa tisa ya John Okello na vijana wake 200 ni propaganda? Nani aliyefyatua risasi ya kwanza kuashiria kuanza kwa mapinduzi? Nani aliyesimama kidete mstari wa mbele kupigania haki ya Wazanzibari dhidi ya utawala wa Sultan Jamsheed? Je, Okello alikuwa na nguvu gani hadi kumuamuru Karume kurudi Zanzibar? Hayo yote yanabaki kuwa ni maswali ambayo majibu yake yote yapo kwa wazee wetu waliohusika moja kwa moja na Mapinduzi.

Sasa, wazee wanaondoka, nini ambacho vijana tunakibeba kutoka kwao kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar ilhali shuleni tunafundishwa tofauti na stori wanazotupa? Nakaribisha maoni yenu.

PUB YA AUNT EZEKIEL CHALI, ASHINDWA KUIENDESHA

$
0
0
Stori: Shakoor Jongo
PUB iliyoibuka kwa muda mchache na kukamata ‘taito’ kubwa Bongo ya mwigizaji Aunt Ezekiel, Demonte imefungwa ghafla, haitoi huduma tena.

Imedaiwa kuwa, pub hiyo iliyopo maeneo ya Mwananyamala, jijini Dar, imefungwa kutokana na mhusika kushindwa kuiendesha.

“Imefungwa, nasikia gharama za vinywaji na wafanyakazi aliowaajiri zilikuwa juu akaona bora afunge,” alisema rafiki wa Aunt aliyeomba hifadhi ya jina lake.

Paparazi wetu alishuhudia pub hiyo ikiwa imefungwa kwa zaidi ya miezi kadhaa, alipomtafuta Aunt, hakupatikana hadi tunakwenda mitamboni.
GPL

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA CHADEMA KUHUSU TUHUMA DHIDI YA FREEMAN MBOWE

$
0
0

KUHUSU TUHUMA DHIDI YA M/KITI WA TAIFA, FREEMAN MBOWE

Kama mojawapo ya mikakati ya baadhi ya watu wanaotaka kuhamisha mjadala wa makosa yanayowaandama ya utovu wa maadili na usaliti dhidi ya chama, hivi karibuni, Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe amezushiwa tuhuma zisizokuwa na ukweli wowote zikilenga kumchafua kwa nafasi yake ya uongozi na kuipaka matope taasisi anayoiongoza.

Tuhuma hizo ni pamoja na;
1. Kwamba Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa mwaka 2005 eti alichukua fedha kutoka kwa Mbunge wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono kiasi cha sh.Milioni 40 ili Mwenyekiti Mbowe asifanye kampeni katika jimbo hilo.
2. Mwaka 2008, eti Mbunge Mkono alimpatia Mwenyekiti wa Chama Taifa, sh. Milioni 20 kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa Tarime, kisha akazitoa kwenye chama kama mkopo na akalipwa.
3. Mwaka 2010, wakati wa uchaguzi mkuu Mbunge Mkono eti alimpatia Mwenyekiti wa Chama Taifa sh. Milioni 200 kwa ajili ya kampeni za mgombea urais.
4. Mwaka huo huo wakati wa uchaguzi mkuu, eti Mwenyekiti wa Chama Taifa, alipokea sh. Milioni 100 kutoka kwa Rostam Aziz kwa ajili ya kampeni.

Idara ya Habari ya CHADEMA, inapenda kutaarifu umma yafuatayo;
1. Hakuna ukweli hata mmoja katika tuhuma hizo. Ni uongo na uzushi uliopangiliwa kama moja ya mikakati ya watu wenye malengo ya kutaka kuilaghai jamii kwamba viongozi wa CHADEMA hawana tofauti na wale wa CCM na kwamba chama hiki kikuu cha upinzani kinachobeba matumaini ya Watanzania katika kupigania haki zao na kupinga kila aina ya ufisadi, kionekane hakina tofauti na chama kilichoko madarakani, ambacho kimepoteza ushawishi kwa wananchi.

2. Matokeo ya uongo huo ni kutaka kuisaidia CCM na kugeuza mjadala.

3. Idara ya Habari ya CHADEMA inapenda kuuambia umma wa Watanzania wote, hususan wanachama, wapenzi, mashabiki wa CHADEMA na wapenda mabadiliko nchini kwamba,Mwenyekiti wa Chama Taifa, ameshawasiliana na mawakili walifanyie kazi suala hili kwa ajili ya kuchukua hatua za kisheria.

4. Kwa uhakika tunapenda kuiambia jamii ya Watanzania wote, hususan wanachama, wapenzi, mashabiki wa CHADEMA na wapenda mabadiliko wote nchini, kwamba; Chama wala Mwenyekiti wa Chama Taifa, mahali popote na wakati wowote, hajawahi kupokea msaada wa fedha hizo kutoka kwa waliotajwa kwa malengo yaliyosemwa.

5. Tungependa kuwaambia waliozusha tuhuma hizo, ni vyema kama wanapenda kutunza heshima kidogo waliyobakiza katika jamii kutokana na kuelemewa na mzigo wa tuhuma za utovu wa maadili na usaliti dhidi ya CHADEMA, badala ya kugeuka kuwa mabingwa wa kupika uongo, wajibu masuala ya msingi yanayowaandamana kuhusu mikakati yao ya kuhujumu CHADEMA na viongozi wake, ambayo iwapo chama kisingeibaini na kuchukua hatua za kinidhamu, ingesababisha kuua ndoto na matumaini ya Watanzania kufanya mabadiliko ya kimfumo na kiutawala, kwa kuiondoa CCM madarakani.

6. Taarifa kuhusu baadhi ya tuhuma katika mkakati huo ambazo zimemlenga Mwenyekiti wa Chama Taifa, kwa kuhusisha shughuli zake binafsi za uwekezaji, zitajibiwa kupitia taasisi husika.

Imetolewa leo Dar es Salaam na;

Tumaini Makene

Ofisa Mwandamizi wa Habari- CHADEMA

AIBU:MPIGA CHABO MAARUFU AKAMATWA AKIPIGA CHABO WAPENZI GESTI

$
0
0
Stori: Chande Abdallah na Denis Mtima, Mwanza
NI aibu kubwa! Mpigachabo maarufu nchini, Andrea Masangu (29) amenaswa akiwa kwenye uvungu wa kitanda akiwapiga chabo wanandoa, Ijumaa Wikienda lina mkasa wote mkononi.

Tukio hilo lilitokea Januari 10, mwaka huu, ndani ya Gesti ya Riverside, Stendi ya Nyegezi jijini hapa ambapo kijana huyo aliingia kwa kuruhusiwa na mhudumu wa gesti hiyo katika mtego makini uliotegwa na Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers na mwishowe kujikuta akiumbuka.

OFM WAPOKEA MASHTAKA
Wiki moja nyuma, mtu mmoja alipiga simu kwa OFM jijini Dar akidai yeye ni msomaji wa Magazeti Pendwa ya Global. Akasema ameamua kupiga simu ili kumshtakia Andrea akidai amekuwa na tabia iliyoota sugu ya kupiga chabo wapenzi wanapokuwa gesti.

“Mimi naitwa…(akataja jina lake), napiga simu kutoka jijini Mwanza. Kuna bwana mmoja anaitwa Andrea, amekuwa na tabia ya kuwachungulia (kuwapiga chabo) wapendanao wanapokuwa gesti.
“Mbaya zaidi, huyu jamaa nasikia huu mtindo anao siku nyingi sana. Amekuwa akienda hata nje ya Mkoa wa Mwanza kwa ajili hiyo,” alisema mtoa habari huyo.

Akaongeza: “Kuna watu wanasema kuwa hata Tabora, Dodoma wanamjua kwa tabia hiyo. Hebu OFM njooni Mwanza.
Ijumaa Wikienda: Usipate tabu, hukohuko Mwanza kuna OFM wametokea hapa makao makuu. Nawapa namba yako ili mshirikiane.
Mtoa Habari: Mtakuwa mmefanya jambo la maana sana.

KAZI YAANZA
Ndani ya dakika tano tu, OFM waliopo Mwanza wakapewa namba za mnyetishaji wetu, kazi ikaanza.
OFM Mwanza, walimtafuta mtoa habari huyo na kukaa naye meza moja ambapo walipanga mipango.
Miongoni mwa mipango hiyo ilikuwa ni pamoja na kutoa taarifa kwenye kituo cha polisi jijini Mwanza ambapo maafande walijipanga.

SIKU YA TUKIO
Siku ya tukio, Andrea alikwenda kwenye gesti hiyo na kumuuliza mhudumu kama kuna wateja wa ‘shot’ taimu’ wataingia, akajibiwa wapo njiani.
Akaomba alipe shilingi elfu mbili (2,000) ili atangulie kuingia yeye kwenye chumba ambacho mhudumu huyo atahakikisha anawaingiza wapendanao hao.

OFM WAJULISHWA, WAINGIA
OFM walijulishwa kuwa mpiga chabo huyo amewasili na tayari ameingia chini ya kitanda kwenye gesti hiyo, nao wakamchukua OFM mwanamke na kutinga naye sanjari na Polisi wa Dawati la Jinsia Jiji la Mwanza.

OFM WAMCHEZEA MCHEZO
Ndani ya chumba hicho, wapendanao (mke na mume) hao walifikia kitandani. Lakini ili kujiridhisha kama kweli Andrea alikuwa uvunguni, OFM mwanaume alijifanya ameangusha pesa chini, alipoinama kuiokota akamuona kiaina lakini hakuonesha kushtuka.

Ndipo OFM hao ‘wapendanao’ walianza kuchojoa nguo za juu na kuzitupa chini kana kwamba walikuwa tayari ‘mchezoni’ ili kumshawishi Andrea aendelee kuamini na kufurahia dhamira yake chafu.

OFM NJE YA GESTI
Nini kilibaki hapo kama si OFM waliokuwa chumbani kuwajulisha kwa simu wenzao waliokuwa nje na polisi?
Chumba kilivamiwa, Andrea akajikuta yuko chini ya mikono ya sheria akionekana ameingilia faragha.

ETI AKAJITETEA!
Baada ya kutolewa chini ya kitanda, Andrea aliwekwa mtu kati na kuhojiwa kulikoni kuwa mpiga chabo wa kiwango kile?
Andrea alianza kwa kuomba msamaha na kuahidi kuacha kabisa tabia hiyo. Alikiri amekuwa akichungulia watu wengi sana wanaofika katika gesti za jijini Mwanza.

“Jamani nimekoma, ni shetani tu, naacha kabisa mambo haya ‘haki  ya Mungu’ kuanzia leo sifanyi tena.
“Kweli nimewachungulia watu wengi sana na sijapata faida yoyote, sijui shetani gani aliniingia,” alilalama Andrea na kuongeza kuwa hayupo peke yake bali ana marafiki zake wengi ambao hufanya kama anavyofanya yeye.

Soo hilo liliisha kwa Mshauri Nasaha wa Taasisi ya Farijika, Aisha Mtumwa kumrekebisha kisaikolojia Andrea sambamba na kumpa onyo kwamba akirudia tena atatupwa rumande kwa kosa la kuingilia faragha ya watu.
GPL

TAZAMA JINSI MAGAZETI YA KITANZANIA YANAVYO TUCHANGANYA..JIONEE MWENYEWE HAPA

$
0
0
Huku amefumba macho! Hayo ni magazeti mawili ya jana yaliyokuja na takwimu mbili tofauti juu ya idadi ya tembo iliyobaki. Takwimu zenye kuzidi kutuchanganya ' Sisi watu wa Nchi ya Kusadikika'.
Maana, kwenye moja ya meza za magazeti, mwananchi baada ya kusoma taarifa hiyo nilimsikia akitamka kwa kukata tamaa; " Sasa hao 13 elfu waliobaki si watamalizika mwaka huu!"
Na ukweli unapatikana wapi?
Kwenye ukurasa wa pili wa The Guardian la leo inasomeka, kuwa ripoti inaeleza kuwa tembo 13,084 ndio waliobaki kwenye mfumo wa ekolojia kwenye hifadhi za Selous na Mikumi. Hapo hawajajumlishwa tembo wa Ruaha Rungwa na kwingineko.
Hata hivyo, idadi ya tembo inapungua kwa kasi kama tusipofanya jitihada za dhati kuukabili ujangili.

TAKUKURU (PCCB) YATOA MAJINA YA WALIOFUDHU KUFANYA MCHUJO WA KWANZA...CHEKI HAPA

$
0
0
The following applicants have been shortlisted for the Aptitude Test after meeting the basic requirements as per our advertisement on Monday 30th September and 2nd October 2013 in the Daily News and Nipashe Newspapers respectively.

The Test will be held on 17th January, 2014 at PTA Hall situated at Sabasaba Grounds (Kilwa Road) scheduled as follows;-

(i) Investigation Officers - Starting at 9:00am
(ii) Assistant Investigators - Starting at 12:00pm


BONYEZA HAPA KUSOMA MAJINA

TOFAUTI NA KUIGIZA HIKI NICHO KINGINE ANAFANYA DR CHENI

$
0
0
 Dr.CHENI ambaye yeye tofauti na uigizaji pia ni mshehereshaji(MC) amekuwa kivutio kikubwa sana katika shughuli za masherehe ya kutosha, Cheni ameuambia mtaandao wetu kuwa huwa anapokea simu nyingi sana za kumhitaji kufanya sherehe kama MC na yuko tayari wakati wowote anapohitajika maana yeye yupo kwa ajili ya jamii
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images