Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live

Sipendi Comedi za Kibongo Kwa Asilimia Kubwa zinazalilisha Wanawake

$
0
0
Mwigizaji wa kike wa filamu Ligth butterfly Mushi ‘Light’ amefunguka kwa kusema kuwa hapendi kuigiza Komedi kwa sababu ni udhalilishaji hasa kwa wanawake, anasema kuwa aliwahi kuchaguliwa kucheza Komedi ya Inye lakini baadae aligundua kilichofanya achaguliwe ni maumbile yake.



“Tunaigiza filamu hakuna udhalilishaji lakini kuna Komedi tuliwahi kucheza ilikuwa inataka wasanii wa kike wawe na maumbile makubwa yaani makalio, kuchesha makalio sasa huo si uchekeshaji ni udhalilishaji, hicho ndio kilinifanya nichukie Komedi,”anasema Light.

Light anasema kuwa waandaaji wasiangalie tu maslahi yao tu pia waangalie waigizaji nao maisha yao baadae wakiwa na familia zao na wakiangalia filamu zao za Komedi zilizotolewa siku za nyuma watakuwa katika hali gani, hali ambayo inamfanya asipende kuigiza Komedi

VIJIMAMBO: Simu ya Mwanaume Naiona Kama Bomu-Lulu

$
0
0
Siku hizi sio kitu cha ajabu kusikia au kuona wapenzi wamegombana na kufikia hadi kuachana kisa simu za mikononi. Wapo wanaoishi kwenye dhana ya simu ya mkonomni ya mpenzi wako ni simu yako na wapo wanaoishi kwenye dhana ya kila mtu na simu yake na mambo yake hakuna kuchunguza simu ya mwenzio.

Mrembo na mwingizaji, Elizabeth Michael “Lulu” ameweka wazi mtanzamo wake kuhusu simu ya mpenzi wake kwa kusema yeye hawezi kuipekuwa kwani anaiona kama ni bomu.

Lulu aliandika hayo kwenye ukurasa wake kwenye mtandao wa INSTAGRAM mara baada yakuweka picha ya mtoto akilia ikiwa na maadishi ya lugha ya kingereza yakiwa na maana  kuwa hiyo ilikuwa ni baada ya kupekua simu ya mwanaume na kupata kile alichokuwa anakitafuta....

Lulu aliiandikia picha hiyo (tazama hapo juu);

“Hii inaitwa MWANA UKOME......Simu Ya Mwanaume naiona kama BOMU...!”

Wewe je simu ya mwenzi wako unaichukuliaje?

KENYA:15 Reasons Why You Should Not Marry A Nairobi Woman

$
0
0
1. She believes she is a doll

2. When she is single her net pay is ksh.20,000 but her rent is 15,000,Transport.5000,clothing 5000 and food 10,000.You will probably marry a whore.

3. She’s never happy without wealth.

4.  Equality dominates her thinking.

5. She only says “thank you” when she sees money on the table.

6. If you run broke,nothing will stop her from cheating.

7. Artificial nails,artificial hair,artificial skin colour,artificial hips,artificial breasts.

8. Drinking is part of her diet.

9. At age 8: You take her to bed and tell her a story.

10. At age 18: You tell her a story and take her to bed.

11. At 28: You don’t need to tell her a story to take her to bed.

12. At 38: She tells you a story and takes you to bed.

13. At 48: You tell her a story to avoid going to bed.

14. At 58: You stay in bed to avoid her story.

15. At 68: If you take her to bed, that will be a story.

Rais Ateuwa Wakuu wa Wilaya Wapya, Paul Makonda na Fredrick Mwakalebela Ndani

$
0
0
RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya kwa kuwateua Wakuu wapya 27, kuwahamisha vituo vya kazi 64 na wengine 42 amewabakisha kwenye vituo vyao vya kazi vya zamani.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa OWM TAMISEMI leo mchana (Jumatano, Februari 18, 2015) Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema mabadiliko hayo yamesababishwa na kuwepo kwa nafasi wazi 27 ambazo zilitokana na wakuu wa wilaya watatu kufariki dunia; kupandishwa cheo wakuu wa wilaya watano, kupangiwa majukumu mengine wakuu wa wilaya saba na kutenguliwa kwa uteuzi wa wakuu wa wilaya 12.

Hata hivyo, Waziri Mkuu alisema, Rais Kikwete amewabadilisha vituo vya kazi wakuu wa wilaya 64 na kuwabakiza kwenye vituo vyao vya zamani wakuu wa wilaya 42.

Wakuu wa Wilaya wapya 27 walioteuliwa ni Mariam Ramadhani Mtima anayeenda Ruangwa; Dk. Jasmine B. Tiisike anayeenda Mpwapwa; Pololeti Mgema (Nachingwea); Fadhili Nkurlu anayeenda Misenyi; Felix Jackson Lyaniva anayeenda Rorya na Fredrick Wilfred Mwakalebela anayeenda wilayaya Wanging’ombe.

Wengine na vituo vyao kwenye mabano ni Zainab Rajab Mbussi (Rungwe); Francis K. Mwonga (Bahi); Kanali Kimiang’ombe Samwel Nzoka (Kiteto), Husna Rajab Msangi (Handeni), Emmanuel J. Uhaula (Tandahimba); Mboni Mhita (Mufindi); Hashim S. Mgandilwa (Ngorongoro); Mariam M. Juma (Lushoto); Thea Medard Ntara (Kyela); Ahmad H. Nammohe (Mbozi); Shaban Kissu (Kondoa) na Stephen Zelothe (Musoma).

Wengine ni Pili Moshi (Kwimba); Mahmoud A. Kambona (Simanjiro); Glorius B. Luoga (Tarime); Zainab R. Telack (Sengerema); Bernard Nduta (Masasi); Zuhura Mustafa Ally (Uyui); Paulo Makonda (Kinondoni); Mwajuma Nyiruka (Misungwi) na na Maftah Ally Mohamed (Serengeti).

Wakuu wa Wilaya saba ambao uteuzi wao umetenguliwa lakini watapangiwa kazi nyingine ni Brig. Jenerali Cosmas Kayombo aliyekuwa Simanjiro; Kanali Ngemela E. Lubinga (aliyekuwa Mlele); Juma S. Madaha (aliyekuwa Ludewa); Mercy E. Silla (aliyekuwa Mkuranga); Ahmed R. Kipozi (aliyekuwa Bagamoyo); Mrisho Gambo (aliyekuwa Korogwe) na Elinas A. Pallangyo (aliyekuwa Rombo).

Waziri Mkuu pia aliwataja Wakuu wa Wilaya 12 ambao uteuzi wao umetenguliwa kutokana na sababu za umri, kiafya na kuimarisha utendaji Serikaini na wilaya zao kwenye mabano kuwa ni James K. Ole Millya (Longido); Elias Wawa Lali (Ngorongoro); Alfred Ernest Msovella (Kongwa); Danhi Beatus Makanga (Kasulu); Fatma Losindilo Kimario (Kisarawe); Elibariki E. Kingu (Igunga); Dk. Leticia Moses Warioba (Iringa); Evarista N. Kalalu (Mufindi); Abihudi M. Saideya (Momba); Martha J. Umbulla (Kiteto); Khalid J. Mandia (Babati) na Elias Goroi (Rorya).

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA.
JUMATANO, FEBRUARI 18, 2015.

Rais wa Chuo cha CBE Ndani ya Ufisadi Mkubwa , Abambwa na Mamilion ya Pesa Chumbani Kwake

$
0
0
KIMENUKA! Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo cha Biashara (CBE), Ramadhan Kirungi amejikuta akiwa korokoroni ya Kituo cha Polisi cha Daraja la Salenda jijini Dar baada ya kudaiwa ‘kufoji’ saini ya benki ya wanachuo na kuchota shilingi milioni 31.

Kwa mujibu wa chanzo makini, wizi huo unadaiwa kubainika baada ya makamu wake, Godfrey Modest kutumwa benki kwa ajili ya kutoa fedha ambazo cheki yake ilishasainiwa.“Yule makamu aliporudi chuoni alimweleza mhusika, akashagaa sana na hakuamini kilichotokea ndipo walipoamua kumkamata rais huyo.

“Walipokwenda kumkagua kwake walimkuta na shilingi milioni 16.5 keshi zilizosalia zikiwa zimefungwa katika mafungu matatu,” kilisema chanzo chetu kikiomba hifadhi ya jina lake.

Baada ya habari hizo kutua kwenye Gazeti la Amani, mapaparazi wetu walimtafuta msemaji wa chuo hicho, Leonidas Tibanga ambaye alikiri kutokea kwa wizi huo na kuongeza kuwa hatua zimechukuliwa na mtuhumiwa alikamatwa na kupelekwa polisi huku uchunguzi zaidi ukifanyika.“Ni kweli wizo huo umetokea na hivi ninavyozungumza na wewe, mtuhumiwa yupo polisi lakini uchunguzi zaidi unaendelea,” alisema Tibanga.

Faiza Ally: Hapa Bongo Hakuna Staa Mwenye Figa Kali Kama yangu

$
0
0
Mzazi mwenziye na Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi aka Sugu Faiza Ally Amejigamba kwa kusema hapa Bongo hakuna staa yoyote Bongo mwenye figa kama yake ya kuweza kuvaa bikini na kujiachia kama yeye..Wengi wamejaa minyama nyama tu wakijiachia ni kichekesho ...Amesema ukitaka kujua wewe ni mrembo kiasi gani vaaa bikini na ujiachie......
Je Mdau kuna ukweli ?

Jack Wolper Kubadili Tena Dini , Safari Hii Aopoa Muuza Magari Muislam

$
0
0
Eti Anataka kubadili Dini Tena na kuurudia uislamu upya ! limeandika gazeti la VISA , Ni baada ya kupata mwekezaji wa mwili wake mwenye imani ya Kiislam....Habari za Mjini zinatiririshwa na...
wambea wake kuwa muiagizaji huyo wa kichaga kwa sasa anawekwa mjini na jamaa mmoja mwenye pesa chafu ambae ni muuza magari anampa kila kitu Wolper ndio maana kwa sasa katulia tuli hana shobo na mtu ila tatizo ndio hiyo Dini tu ambayo inasemekana yupo radhi kuibadilisha kama jamaa atakuwa serious kufanya ndoa ...

Mwigizazi Lulu Michael Kuihama Bongo, Sasa Kuhamia Kenya

$
0
0
Habari za chini ya kapeti zilizoifikia Udaku Special Blog kuhusu mwigizaji Lulu Michael zinasema huenda siku za karibuni akahamia nchini kenya kikazi baada ya Kituo kimoja kikubwa cha Television kuvutiwa naye na kuamua kumpa kazi ya Utangazaji ..
Bila kutaja jina la kituo hicho cha Televion myetishaji wetu alisema mwakilishi wa Kituo hichi alitua hapa nchini kuweka mambo sawa..Inasemekama kituo hicho kilisha onyesha nia ya kumchukua muda mrefu na ndio maana Lulu Akawa Bize sana na Masomo ya kujifunza kingereza ili asije akaaibisha akienda huko kwa Kenyata

Kortini kwa Tuhuma za Kununua "Malaya wa Buguruni Rozana"

$
0
0

WATU wanne wamefikishwa katika Mahakama ya Jiji kwa tuhuma za kununua machangudoa katika eneo la Buguruni Rozana jijini Dar es Salaam. Watuhumiwa hao waolifikishwa Jumanne ya wiki hii katika mahakama hiyo ni Antidius Severian (25), Yaham Mihamed (24), Ally Hassan (35) na Mohamed Hamis (27).

 Wakisomewa mashtaka na wakili wa Serikali, Ramadhan Kalinga mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Bernard Mpepo, alidai kuwa Februari 14, mwaka huu katika eneo la Buguruni Rozana watuhumiwa hao walikamatwa na askari mwenye namba E.7882D/CPL wakifanya manunuzi ya madada poa hao huku wakijua ni kosa kisheria.

Hata hivyo, washtakiwa hao walikana kosa hilo, ambapo Hakimu Mpepo, alisema dhamana kwa watuhumiwa hao ipo wazi ambapo aliwataka kila mmoja kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja atasaini dhamana ya Sh 200,000.

Watuhumiwa hao walishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kurudishwa rumande hadi Februari 24, mwaka huu kesi itakapotajwa tena.

Ugaidi Tanga: Wasomali Wawili Watiwa Mbaroni

$
0
0

JESHI la Polisi nchini kwa kushirikiana na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), limewatia mbaroni watuhumiwa wawili wanaodaiwa kuwa na asili ya Somalia katika msako unaoendelea dhidi ya kundi la wahalifu wa silaha mkoani Tanga.

Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Jeshi la Polisi mjini hapa, kimeiambia Mpekuzi kuwa watu hao walikamatwa jana saa 5 asubuhi katika eneo la Kijiji cha Amboni Mafuriko, baada ya kuonekana katika eneo hilo wakiwa wanashangaa na hawajui wanakokwenda.

Baada ya kuonekana kwa watu hao, wananchi wa kijiji hicho kilicho jirani na Kijiji cha Mleni ambako kundi la wahalifu wa silaha lilijificha, walitoa taarifa kwa polisi ambao walifika na kuwatia mbaroni.

“Ni kweli leo (jana) saa tano asubuhi huku eneo la Kijiji cha Amboni Mafuriko kuna watu wawili wenye asili ya Somalia walikamatwa baada ya wananchi kuwaona na kuwatilia shaka, na hivyo kufanikisha kukamatwa,” kilisema chanzo hicho.

Wakati huohuo, jeshi hilo linawashikilia watu wawili ambao ni wafanyabiashara na waumini wa dini ya Kiislamu wa Jumuiya ya Answar Suni mkoani hapa kwa tuhuma za kuhusishwa na tukio la kufadhili vikundi vya uporaji wa silaha dhidi ya polisi.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, ndugu wa watuhumiwa hao walidai ndugu zao wamekamatwa na polisi siku tatu zilizopita.

“Kuna ndugu zetu wawili wameshikiliwa kwa mahojiano kwa zaidi ya siku tatu na hatujawahi kuwaona kila tukiwapelekea chakula na dhamana imekataliwa, hivyo hali hiyo inatupa wasiwasi mkubwa,” alisema mmoja wa ndugu wa watuhumiwa hao ambaye hakutaka jina lake litajwe.

Mbali na matukio ya kukamatwa watu hao, hali ya ulinzi katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo imeimarishwa, hasa katika wodi ambayo askari waliojeruhiwa kwenye tukio la Amboni wamelazwa wakiendelea na matibabu.

Mpekuzi  ilimpotafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Fraser Kashai pamoja na Kamishna Mkuu wa Operesheni na Mafunzo nchini, Paul Chagonja, wote walisema wapo katika kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama.

Diamond Amnunulia Pete na Cheni za Gharama Mpenzi Wake Mpya Zari the Lady Boss

$
0
0
Mapenzi Moto moto ya Mwanamuzi Diamond kwa Mpenzi wake mpya bado yanaendelea ku make headlines baada ya kumnunulia Pete na Cheni ya mkononi Zari the lady boss , Kama picha inavyoonyesha hapo zote ni za dhahabu pure ila gharama zake hatukuweza kujua kwa haraka ...

Zari Ameweka picha hiyo na kuandika maneno haya ..Woke up to some 24 carat eish. Thank you Boo, xoxo...#QueenTingz..

Zari Ashutumiwa Kuiga Kila Anachofanya Wema Sepetu, Hata Hili la Pete ya Dhahabu Mashabiki wa Wema Wanasema Kaiga

$
0
0
Cheni na pete alizojinunuliwa Wema Sepetu siku za Nyuma
Baada ya Zari Kupost Picha Akionyesha Pete na Cheni ya Dhahabu aliyonunuliwa na Mpenzi wake Diamond Kama zawadi huko Instagram limezuka jambo mashabiki wa Wema wakisema Anamwiga mtu wao kila anachofanya ...Jisomee hapa huyu ni Shabiki mkubwa wa Wema Amendika hivi :

Mtaawapili
"Bibi zaituni acha tabia zako za copy na kupaste sio kila anachofanya wema na lazima ufanye utaumbuka bure.....nyie team nyoko nyoko ebu tafuteni kitu cha kufanya au mwambeni huyo bosslady awape kazi ya kufua ile sidiria kauka ni kuvae mfyuuuuu.hivi nyie mnajuwa kama wema anapenda gold sana na anazo nyingi mno.alipokuwa ck alipelekwa dubai kununuwa gold tu Google utaona .kama mtakumbuka vizuri wema na domo walikuwa china walinunua gold za gram 50 kila mtu🙌.watu wanasema eti cheni ya wema ni fake ni ule mkeka wa elfu 50 nyoooooooo kwenye upande wa madini wema ana fanya kweli cheni ya sio fake muulizeni vizuri wajinga tukitaka kujuwa wema wapi walinunuwa gold kasmani jewellery mitaa ya kitumbini tel 2557562.... nenda kaulize bei zake kama ujatoka bila kuagaaa tena ata yule mjela jela anayo @dainakavishe ebu wape bei za gold kiasi gani"

Baada ya Mtaawapili kutoa huo UBUYU haya ni Maoni ya Mashabiki walicomment kwenye shutuma hizi:

maskio_popo

Si ajabu kajinunulia mwenyewe hiyo mibat yake alafu et tanx boo,hao ndo wale wanaowapaga ela mwanaume akalipie mahari kwao


mtoto_mzuriii

Ataiga mpka akome apeleke mbele huko mitende yakeee


chamiy8

Hahaha yule bibi mpimbavuu leo tilimuanda morning jioni kanunua ha haha hataki kushindwa mamaeee sasa atajuta hamfikii wema wetuu kwa gold namuaminia wema pekeyakee

kimbwi22222

Saaana hakuna fake hapo hata me nnayo ....3.6 mil hizoo.....hakuna ubishi wema wetu hatariiiiiiiiiii......wengine wanaiga...mtapasuka msambaaaa eeh

Local Business Becomes Member of International Trade Association

$
0
0
 Credit & Debt Masters Company Limited, located in Dsm, Tanzania, has become an international member of ACA International- the Association of Credit and Collection Professionals which brings together more than 5000 members world wide. Credit & Debt Masters Company Limited is dedicated to advancing quality and professionalism in the credit and collection industry.

Ommy Dimpoz: Wema Siyo Mpenzi Wangu

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva, Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, amesema anashangazwa na uvumi unaoendelea kuwa yupo katika uhusiano na mwigizaji wa filamu, Wema Sepetu.
Akielezea kuhusu picha zilizosambaa kwenye mitandano ya kijamii, Ommy Dimpoz, alisema walikuwa Afrika Kusini kwa mapumziko ndipo picha hizo zilipopigwa.

“Tunapiga picha nyingi sana na Wema hata uki-google utaziona, hii siyo mara ya kwanza, lakini sijui kwanini hizi zimetengeneza taswira nyingine kwa mashabiki,” alisema.

Ommy alisisitiza kuwa yeye hajawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Ex wa rafiki yake, na kuwa yeye na Wema walikuwa wakifahamiana hata kabla ya Wema kuanza mahusia ya kimapenzi na Diamond. Hivyo kuacha kwao haiwezi kumpelekea yeye awe mbali nao kwani hayo ni mambo yao binafsi.

Japokuwa Ommy anaamni kuwa kwenye pitapita za kimaisha inawezekana mtu akawa na mahusiano ya kimapenzui na Ex wa rafiki yake, kwani hicho kitu kinawezekana.

“Ku-date na Ex wa rafiki yangu, kwa mimi hapana lakini kuhusu maswala ya mapenzi lolote linaweza kutokea kwasababu umesha sema Ex kwahiyo it means hawapo kwenye mahusiono tena kwahiyo inaweza ikatokea huko mbele mbele maisha yameendelea  watu wakaja kukutana , kwa huyo vitu hivyo vinawezekana”  Dimpoz alieleza.

Picha za wawili hao wakiwa katika pozi tofauti zimeendelea kuwa gumzo na kuzua maswali mengi kwa mashabiki, kutokana na ukaribu aliyonao Ommy Dimpoz na aliyekuwa mpenzi wa zamani wa Wema, Nasib abdul ‘Diamond’.

Wema Amuumbua Kajala!

$
0
0

UBUYU: Gazeti la udaku la Amani, limeripoti kuwa mrembo na mwigizaji wa Bongo Movies ,Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ amedaiwa kumuumbua shosti wake wa zamani, Kajala Masanja kwa kumwaga ‘ubuyu’ kwamba amefilisika baada ya kigogo maarufu kama CK anayedaiwa kuwa ndiye mpenzi wake, kuyumba kiuchumi.

Kigogo huyo aliyewahi kuwa na uhusiano na Wema kisha kumwagana naye, imedaiwa kuwa ile jeuri ya kununua magari ya kifahari, kumiliki biashara mbalimbali mjini, kwa sasa ameangukia pua kwani hawezi tena kujitutumua.

Kwa mujibu wa chanzo makini kilicho karibu na Wema, baada ya kuhamishia majeshi kwa Kajala, Wema hakufurahia hivyo aliposikia uchumi umeyumba, amefurahia sana kufuatia ule msemo wa ‘adui muombee njaa.’

“Wema amefurahi sana, anawaambia marafiki zake kuwa malipo ni hapahapa duniani, Wema alimlipia Kajala dhamana ya sh mil. 13 ili asifungwe kwa msala wa kutakatisha fedha uliokuwa ukimkabili lakini akamgeuka na kumchukulia bwana wake, ule si ubinadamu kabisa,” kilisema chanzo hicho.

Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kuwa, Kajala ana nuksi kwani CK alipokuwa na Wema alikuwa na mafanikio na kupata fedha kila kukicha lakini alipohamia kwa Kajala mambo ndiyo yakaharibika.
“Kajala ana nuksi, CK alipokuwa na Wema walikuwa wanapata fedha nyingi kila wakati lakini kwa Kajala wamefilisika kwelikweli,” kilisema chanzo na kuongeza:

“Madam mwenyewe amemshangaa sana CK kuishiwa fedha wakati alikuwa mtu wa kucheza na dola nyingi kila kukicha na aliwekeza fedha zake katika miradi mbalimbali.”

Jitihada za kumpata CK ili azungumzie ishu ya kuyumba kiuchumi hazikuzaa matunda lakini kwa mujibu wa mmoja wa watu ambao wanafanya naye kazi, kigogo huyo ameporomoka kiuchumi kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kufanya magumashi ya fedha kazini hadi kufikia hatua ya kutaka kufukuzwa kazi.

“CK hayuko vizuri kazini, ana majanga kibao, ile jeuri aliyokuwa akifanya na Wema na Kajala ilikuwa ni fedha za magumashi sasa kimemnukia kazini,” kilisema chanzo hicho ingawa mwenyewe alipotafutwa kwenye simu hakupatikana.
Wakati mwanahabari wa Amani akiendelea kuichimba habari hiyo, alifanikiwa kunasa ‘clip’ ya sauti ya Wema iliyoonesha dhahiri kwamba mrembo huyo amefurahishwa na kitendo cha wawili hao kukalia kuti kavu.

Sauti hiyo ya Wema inasikika akizungumza na shosti yake kumueleza jinsi gani Kajala ameumbuka maana alifikiri kutembea na shemeji yake ameula kumbe matokeo yake ameangukia pua kwani mwanaume amefilisika.“…Kajala sasa hivi anaendesha Noah (Toyota) ile yenye mastikamastika nakwambia…” ilisikika sehemu ya clip hiyo.

Paparazi wa Amaani alimvutia waya Wema ili aweze kufunguka zaidi kuhusiana na sakata hilo namna ambavyo amefurahia, simu yake iliita bila kupokelewa.Hata hivyo, mwandishi wetu alikwenda nyumbani kwake, mtaa wa Bwawani-Kijitonyama jijini Dar zaidi ya mara tatu kwa nyakati tofauti lakini hakufanikiwa kumpata baada ya mlinzi kudai amelala.

Mwanahabari wa Amani alimvutia waya Kajala ili kusikia naye anasemaje baada ya kudaiwa kuanguka kiuchumi, simu yake iliita bila kupokelewa lakini hata hivyo, rafiki yake wa karibu ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alikanusha madai ya kufilisika.“Kajala hajafilisika na hawezi kufilisika, hayo yatakuwa maneno ya watu tu,” alisema rafiki huyo wa Kajala.

Wema na Kajala waliwahi kuwa mashosti wa damu kabla ya kugombana ambapo chanzo kilitajwa kuwa ni CK,  mwaka jana walidaiwa kupatana lakini baadaye ikaelezwa kuwa bado wanaendeleza bifu.

Download Official Iyanya and Diamond Platnumz - Nakupenda (I Love You)

$
0
0
Haya Sasa Huu ndio official Wimbo wa Diamond na Mwanamuziki Iyanya Kutoka Nigeria Unaoitwa Nakupenda (I love you ) Unaweza Kusikiliza ama Kuudownload Kupitia Link hiyo hapo chini ..
Kazi Kwako ..Usikilize alafu uniambie kama umekubamba ama la...... Huu Hapa:

Uteuzi wa Paul Makonda Kuwa Mkuu wa Wilaya Wapingwa Kila Kona.....Anatuhumiwa Kumpiga Warioba na Kumtusi Lowassa Hadharani

$
0
0
Uteuzi wa Makonda ambao umefanywa na Rais Kikwete, unaonesha kuwashitua wengi; hali ambayo imefanya watu wengi kumbeza hasa kupitia mitandao ya kijamii.

Baadhi ya wanaobeza, wanadai kwamba Makonda hana sifa ya kuongoza wilaya kubwa kama Kinondoni, ambayo ina changamoto na migogoro mingi ya ardhi.

Makonda ambaye ni Katibu wa Chipukizi na Uhamasishaji wa UVCCM, jina lake limekuwa kubwa hivi karibuni baada ya kutuhumiwa kumpiga  Jaji Warioba wakati wa  mdahalo ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere.

Pia, kujitokeza kwake hadharani kumpinga Edward Lowassa, kuliongeza jina hilo kuwa maarufu.

Wakizungumza na Mpekuzi  kwa nyakati  tofauti, baadhi ya wasomaji wa mtandao huu, wamedai kuwa uteuzi huo wa Rais ni mzuri ila  alikosea kumweka wilaya ya  Kinondoni yenye matatizo chungu mzima ya kiutendaji ikiwemo migogoro ya mipaka, ardhi, wafanyabiashara ndogondogo na mambo mengine ya ndani.

“Tunampongeza Rais kwa kuteua wakuu wapya wa wilaya, ila kwa huyu Paul Makonda kumweka Kinondoni, ameteleza. Hii wilaya inahitaji mtu mwenye uzoefu mkubwa katika uongozi na uadilifu” alisema Sued Musa.

Naye  Albert Chenza  wa  Dar  alikuwa  na  haya ya  kusema: "Ma-DC kama Makonda wapo kwa ajili ya CCM kutetea maslahi ya CCM au wapo kwa ajili ya wananchi kuwasaidia wananchi?
 
"Ikumbukwe DC ndiye Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya na DSO akiwa katibu wake, sasa mtu kama Makonda ambaye yupo tayari kufanya vurugu yoyote kutetea maslahi ya CCM leo kupewa u-DC wa Kinondoni tutegemee nini uchaguzi mkuu wa Oct 2015?
 
"Ikitegemea kuna mvutano kati ya wapinzani na CCM ambao vyombo vya usalama vinatakiwa kuleta haki na amani, wapinzani wategemee kupata haki au NGUVU zao ndo itakuwa haki yao? Hakika nuru ya amani inafifia Tanzania.
 
"Hii ni kama tupo disco la kukesha ambalo inatolewa CD hii inawekwa ile na zote unahitaji unywe panadol kuzisikiliza." Alisema  Albert  na  kuongeza:

"Ni dhahiri sasa Mzee Warioba na Taasisi ya Mwalimu Nyerere wamemjua adui yao halisi ni nani. Aliyekua mstari wa mbele kumshambulia na kumfanyia fujo Mzee Warioba amepongezwa rasmi  kwa  kupewa  ukuu  wa  wilaya.
 
"Pia imeendelea kujidhihirisha sasa kuwa Ukitaka U-DC wewe mtukane Lowassa kama Nape Nnauye, Mrisho Gambo na Makonda  walivyofanya.
 
"Na pengine atakayekua jasiri vya kutosha na kumchapa angalao vibao viwili usoni anaweza kupata Ukuu wa Mkoa au Ubalozi kabisa"
 
Sailas Kassa Edward  yeye  anamaoni  tofauti  kidogo, na hapa  anaanza  kwa kumpongeza Makonda: "Siku ya jana (juzi) Rais kikwete alifanya uteuzi wa wakuu wa wilaya ambapo moja ya wateule ni paul Makonda.
 
"Inanishangaza sana kutoka jana(juzi) mpaka leo(jana) watanzania wamekuwa wakilalamika kupitia mitandao ya kijamii wakikosoa uteuzi wa ndgu makonda.
 
"Mimi binafsi nampongeza kwa nafasi aliyopata nadhani katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania haijampa rais mamlaka ya kuwatenga watu bali kila mtu ana haki ya kuongoza na pia kuongozwa.
 
"Kwa watanzania itafika hatua kila mtu mwenye intrest za chama cha mapinduzi hamtaki apate nafasi je nani ana haki na nani hana?
 
"Nimejaribu kuchunguza haya yote yanatoka wapi mpaka makonda anakuwa gumzo mtaani nikagundua kuwa wapenzi wa Edward Lowassa wameumia sana kuona makonda anakuwa mkuu wa wilaya hasa ukizingatia anafichua mbinu na hila za Lowassa na makundi yake. "

Mwanamke Amuua Mwanamke Mwenzake kwa Kummwagia Mafuta ya taa na Kumchoma Moto baada ya Kumfumania na Mumewe

$
0
0
Mkazi wa kijiji cha Ibosa, kata ya Nyakato, Bukoba Vijijini, Amelia Richard (50) anatuhumiwa kumuua mwanamke mwenzake kwa kummwagia mafuta ya taa na kumchoma moto baada ya kumfumania na mumewe.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera,  Henry Mwaibambe  alitaja tukio hilo ni  la Februari 15, mwaka huu saa 3 usiku katika kijiji cha Ibosa kata ya Nyakata Bukoba vijijini.

Alimtaja aliyeuawa ni  Pelagia Martin (46) aliyeunguzwa mwili mzima. Kamanda alisema mwanamke huyo alicheleweshwa kufikishwa Hospitali ya Mkoa hadi kesho yake; Februari 16 baada ya wanafamilia kuomba wayamalize bila kwenda Polisi.

Makubaliano ya wanafamilia hao yalitokana na kile kilichoonekana kwamba  Amelia alimfumania Pelagia akiwa na mumewe,  Richard Bulebo (57) ndani ya nyumba yao.

Kwa mujibu wa Kamanda, Februari 16 walipoona hali ya majeruhi inazidi kuwa mbaya, ndipo walifika katika Kituo cha Polisi mjini Kati wakiomba msaada.

Polisi walimpeleka majeruhi huyo Hospitali ya Mkoa lakini alifariki kabla ya kupatiwa matibabu. Polisi inamshikilia Amelia na Bulebo kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo.

Mzee Yusuph kuoa tena mke wa watatu,Wake zake watupiana vijembe mtandaoni

$
0
0

Mwimbaji mahiri wa muziki wa Taarab nchini ambaye pia ni mkurugenzi wa kundi la Jahazi Modern Taarabu,Mzee Yusuph anatarajia kuoa tena mke wa tatu hivi karibuni huku wake zake wawili wakiwa kwenye bifu zito wakitupiana vijembe mtandaoni.

Akipiga stori na Uheard na Soudy Brown alisema kuwa anatarajia kuoa mke huyo ambaye anaishi huko visiwani Pemba,na kwamba mipango ikiwa tayari kila kitu kitakuwa hadharani.

Hivi karibuni wake zake wawili ambao ni Malkia Leila Rashid ambaye pia ni mwimbaji wa kundi hilo na mke wake mdogo aitwaye Chiku wamekuwa wakirushiana vijembe kwenye mtandao wa kijamii wa ‘WathsAAp’ kwa kuandikiana ‘Status’ za vijembe.

Habari zinasema kuwa wake hao wamekuwa kama chui na paka na mzee Yusuph hana mpango wa kuwapatanisha kwa kuwa hakuna hata mmoja aliyeonyesha chuki kwa mwenzake akiwa na nao.

‘’Waache tu warushiane vijembe tena ndiyo vizuri na dawa yao nawaletea mke wa tatu na wala sina mpango wa kuwapatanisha,"alisema Mzee Yusuph.

Joseph Kusaga: Clouds FM haina chama! Akanusha Clouds kununuliwa na Rostam Aziz

$
0
0

Clouds fm wamekana kuwa shutuma zinazotolewa kwenye social media hasa jamiiforums kwamba wao CCM sio za kweli.

Akihojiwa CEO wa clouds katika kipindi power breakfast, amesema wao kama radio hawana chama kwa sababu hata sheria TCRA haziruhusu.

Pia kwenye uchaguzi wa mwaka huu wagombea wote watapewa nafasi sawa.

Ameendelea kusema kuwa wafanyakazi wachache kuwa CCM haimaanishi clouds yote ni CCM.

Pia clouds imekanusha habari zilizozagaa kuwa radio imenunuliwa na Rostam Aziz, ameongeza kuwa hizo ni propaganda za kuichafua radio hiyo.

Amesema kama wakiuza radio watatangaza kwasababu radio ni yao,na hawamuogopi mtu.

Wakati wanamuhoji nimesikia wanamuita Joh (labda ndiye Joseph Kusaga) sina uhakika na majina mengine,wanomfahamu watatujuza.
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live


Latest Images