Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

Kijana: Ukipenda Jimama au Mwanamke Mwenye Pesa Uvumilie Vipigo/Kugombezwa Hadharani

$
0
0
Wale vijana wenzangu mnaopenda majimama (kulelewa) mkubali makofi, makonzi sometimes mitama hadharani, pia hata kufokewa hadharani.

Maana wengi wa hawa majimama wana stress za kutosha lakini usisahau ndo yanayowaweka baadhi ya vijana mjini kwa kila kitu, la muhimu ukishagombezwa we jidai kujichekesha tu ili mambo yaishe.

Pia nawasihi sana baadhi vijana tusiwapende hawa majimama tutafute maisha yetu, tusipende maisha ya bure kwani tunaweza kupata madhara mengi ikiwemo magonjwa UKIMWI na kukosa vijana wa kujenga taifa.

Nawasilisha.

Watuhumiwa wanne wa Amboni wakamatwa na wananchi wakishirikiana na JWTZ

$
0
0
Wananchi wa Mleni, Amboni mkoani Tanga, kwa msaada wa askari wa JWTZ, wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wengine wanne wanaotuhumiwa kwa ujambazi na ambao walikuwa wamejificha katika mapango ya Mleni huko Amboni Tanga.

Kwa mujibu wa ITV,wananchi waliwaona watuhumiwa hao na kisha wakawaapigia simu askari hao wa JWTZ ambao walikuja kuwakamata na kisha kuwakabidhi Polisi.

Mkuu wa Operation na Mafunzo wa Jeshi hilo,afande Chagonja ameahidi kuwa, raia waliosaidia kukamatwa kwa wahalifu hao watapewa zawadi,zawadi ambayo ameifananisha na "takrima".

Watuhumiwa hao wameelezewa kuwa ni wenye asili ya "kiarabu" na "kisomali" na kwamba walikamatwa wakiwa wamedhoofika kwa njaa.

CHANZO: ITV

Johari Akiri Kumpora Kimapenzi Mwigizaji Ray Kutoka kwa Mainda

$
0
0
STAA wa sinema za Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amekiri kwamba wakati anaingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na nyota wa fani hiyo, Vincent Kigosi ‘Ray’ alijua yupo na nguli wa filamu, Ruth Suka ‘Mainda’, Johari Amekiri Baada ya kuulizwa na Gazeti moja maarufu ....

Jack Patrick Aandika Barua Akiwa Gerezani Kuhusu Mapenzi ya Diamond na Zari , Vanessa na Jux na Aunty na Iyobo

$
0
0
Wakati akiendelea kutumikia kifungo akiwa jela huko Macau, Hong Kong nchini China, modo maarufu Bongo, Jacqueline Fitzpatrick Cliff  ‘Jack Patrick’ amenena mazito juu ya Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na mwandani wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Juma Khalid ‘Jux’, Vanessa Mdee, Aunt Ezekiel na Moze Iyobo.

BARUA KUTOKA CHINA
Jack aliyekamatwa nchini humo kwa msala wa madawa ya kulevya ‘unga’ mwaka 2013 kisha kufungwa miaka sita kwenye Gereza la Macau, hivi karibuni alilitumia gazeti hili barua nzito akionesha kushtushwa na vitu fulani vya mastaa hao.

MIMBA YA AUNT
Moja kati ya mambo yaliyomshtua Jack ni mimba ya mwigizaji Aunt Ezekiel ambaye ni mke wa mtu, Sunday Demonte anayodaiwa kupachikwa na mcheza shoo wa Diamond, Moze Iyobo.
Hata hivyo, katika skendo hiyo, Jack aliwataka watu wamuache Aunt apumzike kwani mapenzi hayachagui hasa kama ana furaha.

“Nimeshtushwa na udaku special Lol! Sasa Aunt ameamua kutulia na Iyobo…acha apumzike mapenzi hayachagui as long as ndiyo furaha yake, that’s okey,” aliandika Jack.

DIAMOND, ZARI
Mbali na mimba hiyo ya Aunt inayoelekea kuzaa matunda muda si mrefu, modo huyo alionesha kushtushwa na penzi la staa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz na Zari akishangaa ilikuwaje hadi jamaa huyo akaachana na Wema Sepetu kisha kutua kwa mrembo huyo mwenye maskani yake nchini Afrika Kusini na Uganda.

“Heh! Kwani Diamond aliachana na Wema tena?” Alihoji Jack na kuongeza:
“Sasa Zari si anakaa South Africa ‘Sauzi’? Wanaonana vipi na Platnumz? Mh! Wala hawatadumu maana mapenzi ya mbalimbali. Labda kama Nasibu (Diamond Platnumz) atahamia South.


KAJALA Vs WEMA
Pia video queen huyo wa Ngoma za Nataka Kulewa (ya Diamond), She Got A Gwan (ya Marehemu Ngwea) na Kamugisha (ya Linex) aliulizia lile bifu zito la Wema na Kajala Masanja kama lilikwisha kwani mastaa wa Bongo Movies walishazoeleka kugombana na kupatana.

Bifu hilo ni lile la Wema kumtuhumu Kajala kumchukulia bwana’ke (CK) huku akisahahu kwamba alimlipia Sh. Milioni 13 ili asiende jela miaka mitano baada ya kukutwa na hatia ya kuuza nyumba iliyowekwa kizuizini na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.“Ya Kay (Kajala) na Wema naona mwishowe watarudisha urafiki tu. Ya Bongo Movies nimeshayazoea huwa wako hivyo kila muda, kawaida yao.”

JUX, VANESSA
Jack alipofika kwenye ishu ya kusalitiwa na staa wa Bongo Fleva, Jux akidaiwa kuwa kwenye malovee na sexy lady wa muziki wa Kizazi Kipya, Vanessa ‘Vee Money’, aliandika ishu hiyo kwa hisia zaidi huku akijilaumu mwenyewe kwa kosa alilofanya.


“Ya Jux na Vanessa nimeamua tu kuyaacha coz nipo jela siwezi kumzuia kufanya lolote then ni makosa yangu yaliyofanya hayo yote kutokea.“Sijui hata kama itakuja kutokea tena kuwa wote tena mimi na yeye, that chapter closed already, nahesabia muda mfupi tu now nitatoka lakini sina chochote cha kufanya nionane naye,” alimalizia kuandika Jack.

Jack Patrick alihukumiwa kifungo hicho mwaka jana lakini taarifa zilieleza kuwa endapo ataonesha nidhamu gerezani ataachiwa mapenzi hivyo hatakaa jela miaka yote sita.
GPL

Mrembo Huddah Monroe Asema Kazi yake ya Kuwapa Raha Wanaume Inalipa..Aonyesha Kadi ya Range Rover Analomiliki

$
0
0
Mrembo Huddah Monroe
Mrembo wa Kenya Huddah Monroe Amejitokeza na kuwaponda wale waandishi wa Habari Bloggers wanaosema gari aina la Range Rover analoendesha kwa sasa ameazima kwa mtu na kusema kuwa kazi anayofanya (Socialite ) ya Kutoa Escort kwa kuwapa raha wanaume na kuhuzuria events mbali mbali inamlipa sana kiasi hawezi azima gari ...Huddah Ameweka Mtandaoni kadi ya gari hiyo ambalo ni la gharama sana kwa mtu wa kawaida ikionyesha jina lake halisi kama mmiliki halali wa Ndinga hiyo matata
Kadi ya Gari aina ya Ronger Rover ikionyesha jina halisi la Huddah

Ubuyu huo Warembo wa  Bongo mpo?

Diamond, Ommy Dimpoz, January na wengine walaani mauaji ya albino

$
0
0
Mauaji ya mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja, Yohana Bahati huko Chato yamewaumiza watu wengi si Tanzania tu bali dunia nzima.

Kifo cha kusikitisha cha mtoto huyo aliyekutwa amekatwa miguu na mikono kimeandikwa na mashirika yote makubwa ya habari duniani na hivyo kuipa Tanzania sifa mbaya.

Wananchi wamelaani vikali kitendo hicho na kuitaka serikali kuchukua hatua kuhakikisha haviendelei tena. Hivi ndivyo mastaa wa Tanzania nao walivyoungana na wananchi wengine kueleza waliyonayo moyoni.

Diamond

Ndugu zangu! nafkiri ni Muda wa kubadilika sasa…Tuacheni fikra potofu, za Kipuuzi na ukatili Usio na Maana.. Hivi inamaa unataka kuniambia na hao kina Bill gates Mzee wa kuku, Carlos Slim, Amancio Ortega , Bakhresa na Matajiri wakubwa Duniani pia Walitajirika kupitia Ukatilii huu wa Ma Albino…??? Juhudi na Utendaji wako wa Kazi ndio utao kufanya Uendelee na kufikia Hayo Malengo unayoyataka… Tuache kujidanganya na Kuwatesa Ndugu zetu wasio na Hatia.

Ommy Dimpoz

Tanzania inazidi kupata sifa mbaya kimataifa kila kukicha. Ufisadi, rushwa na sasa mauaji ya albino wasiokuwa na hatia yamerudi tena. Inasikitisha kuona kwamba kuna binadamu yupo radhi kumuua binadamu mwenzake ili apate utajiri. Hii haikubaliki hata kidogo.

Naungana na watanzania wote walioumizwa na mauaji ya mtoto Yohana Bahati wa huko Chato kulaani vikali kitendo hicho. Serikali ichukue hatua madhubuti kulinda usalama wa ndugu zetu hawa. ‪#‎PingaUkatiliHuu‬ ‪#‎StopAlbinoKillings‬

Lady Jaydee

Sio vizuri Sio vizuri kabisaaa Nadhani sote tunafahamu fika Kuwa sio vizuuuuuri Ila kwanini tunaendelea kufanya Wakati tunajua sio vizuri Tafadhali Angekuwa mwanao? Angekuwa kaka /dada yako? Angekuwa mdogo wako? Ungejiskiaje? Kumbuka tu kuwa, sio vizuri. Full stop.

Zahir Zorro

Tazama Watoto hawa walivyo wazuri, Sera ya kujua Albino inaleta LAANA. Kubwa sana ktk Tanzania. Hivi Tujiulize anae faidika ni nani??

Peter Msechu

#Nihakiyakekuishi HUYU NI BINADAMU KAMA WEWE MWENYE MAUMIVU KAMA WEWE MWENYE MOYO WA NYAMA KAMA WEWE INAUMA SANA KUONA BAADHI YA WAPUMBAVU WACHACHE WANAMGEUZA BINADAMU MWENZAO BIASHARA KWA KUTOA UHAI WAKE HII NI DHAMBI KUBWA SANA SANA MUNGU ANACHUKIZWA SANA NA KITENDO HIKI KINAVYOENDELEA HAPA TANZANIA.. TUNAJITIA LAANA WENYEWE BILA KUJUA TUTASHINDWA KUFANIKIWA NA TAIFA KUZOROTA SABABU YA ROHO HIZI ZINAPOANGAMIA BILA SABABU WATANZANIA WENZANGU TUUNGANE KWA PAMOJA TUKEMEEE MAUAJI HAYA #TEAM #TUPENDANEEE

January Makamba

Mauaji ya ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi, yaani albino, ni ukatili usio na mfano. Serikali haipaswi kuwa na huruma katika kuwasaka na kuwaadhibu wanaofanya vitendo hivi. Ni muhimu pia kuweka utaratibu wa kuwalinda wenye ulemavu wa ngozi dhidi ya tishio la kutekwa na kuuwawa. Elimu kwa umma ni muhimu. Wanaofanya haya matendo wapo ndani ya jamii yetu. Tuweke utaratibu wa malipo kwa wasamaria wema wanaotoa habari kuhusu wahusika wa biashara ya viungo vya binadamu. Na tuweke utaratibu wa kuwalinda watoa habari hizi. Hili ni tatizo la kisheria lakini pia ni tatizo la imani za ushirikina na uchawi ndani ya jamii. Ni lazima kuyakabili mambo haya mawili kwa pamoja. #TanzaniaMpya @TanzaniaMpya #StopAlbinoKillings

Henry Mdimu

Ni kweli mimi ni Albino, nimejikubali na nimeishi maisha yangu yote bila kujali nilivyo. Sijawahi kutumia hali yangu kupata kitu kwa huruma, nimeyapigania maisha yangu na nimepiga hatua. Leo hii naongea nanyi nikiwa Baba, Mume, Mwandishi Mwandamizi, Blogger, na mengine mengi, lakini hali yangu sasa inaanza kunikwaza. Haya mauaji jamani, nimejiteua kuwa Balozi, nitatetea, na kusimama mbele ya wenzangu wote wenye hali kama hii, kama ni wanasiasa ama wafanyabiashara, wanataka kutuua kwa maslahi binafsi, mwaka huu HAPANA. Wanaoniunga mkono mikono juu

Picha: Huddah Monroe Achefua Tena Watu Mtandaoni, Atupia Picha Akiwa Mtupu Kitandani

$
0
0
Huddah Monroe ameshajikubali kuwa ni ‘good girl gone bad’ na ndio maana haoni tatizo kuweka picha akiwa kitandani kama alivyozaliwa.

Mrembo huyo wa Kenya amepost picha kwenye akaunti yake ya Facebook akiwa kitandani huku akiwa amejifunika na shuka sehemu ndogo tu ya mwili wake kuficha sehemu ny*ti.

Mashabiki wake hawakusita kumchana.

Dnt you fear God?oh I like your beauty and en everything mash Allah but this idea of being naked subhanallah stop it.You are a good girl hudda you can change if you want,” aliandika Shankaroon A. Mohammed.

Wajameni u mean ur whoring for real?? Oh my… please stop proving ppl right n be decent now that uv achieved what u wanted… n be quiet, if not for anything else then respect your clientèle. This is wrong,” ameandika Brenskie La’femme.

Dully Sykes Alaumu Wasanii Ambao Hawakuja Kumzika Baba yake

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Dully Sykes, ameshangazwa na kitendo cha wasanii wengi kutojitokeza katika mazishi ya baba yake mzazi, Ebby Sykes

“Nilitegemea kwakuwa tunampumzisha baba yangu hapa hapa Dar es Salaam, wangekuja wasanii wengi ambao ni marafiki zangu, lakini hali ilikuwa tofauti kabisa,” .

“Sijui walijua nitakuja kuwaomba fedha zao, mimi nilishapata michango mingi kutoka kwa watu wengine mbalimbali, ukweli wasanii tuache roho za kimasikini,” alisema.

Sykes aliendelea kusema amegundua asilimia kubwa ya wasanii wamekuwa wakipendana wakati wa raha tu, lakini inapofika muda wa matatizo kila mmoja hukimbia.

Diamond Atoa Sababu za Kushindwa Kuhudhuria Msiba wa Baba yake Dully Sykes

$
0
0
Diamond Platnumz ni miongoni mwa marafiki wa karibu wa msanii Dully Sykes ambaye weekend iliyopita alimpoteza baba yake mzazi Ebby Sykes, lakini hakuweza kuhudhuria msiba huo kutokana na sababu ambazo amezitoa leo.

Diamond ambaye wakati msiba huo unatokea alikuwa Zanzibar na mpenzi wake Zari, ameelezea sababu zilizomfanya kushindwa kuhudhuria mazishi.

“Watu waliniona niko zanzibar lakini walikuwa hawajui nimeenda kufanya nini,” Diamond

ameiambia 255 ya XXL ya Clouds FM. “Usiangalie kila unachokiona Instagram ukajua mtu labda kwasababu alikuwa anafanya starehe.

Niko katika kipindi ambacho sio kizuri kwangu mimi na familia yangu kwasababu kuna vitu ambavyo siwezi kuvizungumza lakini, na siwezi kuviweka kwenye media ndo maana watu wengine wanaweza kuniona nacheka lakini […kwanza mama yangu anaumwa na anaumwa sana sijawahi kulizungumza hili ndo nalizungumza hapa, hapa ninapoongea na wewe yupo India, kuna vitu vingi vinaendelea, siwezi kusema nilikuwa Zanzibar nafanya nini

Haya Mengine Saba ya Yamoto Band Kwenye BBC Dira ya Dunia

$
0
0

Tuliziona pichaz Yamoto Band pamoja na story za wao kwenda zao London, Uingereza kupiga show, siku ya leo FEB21 muda mfupi baadaye watakuwa na show, watu wetu hawa saa chache zilizopita walikuwa kwenye Interview na mtangazaji Charles Hillary kwenye BBC Dira ya Dunia.

Swali la kwanza kuulizwa ilikuwa wapi lilikozaliwa jina la Yamoto Band? ;”Ukiachana na vitu vya motomoto ambavyo tunavitoa ni jina ambalo lilibeba nyimbo yetu ya kwanza.. Yamoto Band ni zao la Mkubwa na Wanae, kituo ambacho kinalea watoto wenye vipaji..“– Aslay.

Kuhusu ishu ya mtu anayewaandikia nyimbo zao; “Mara nyingi sana tunaandika wenyewe lakini tunashare idea na bosi wetu Mkubwa Fella.. Tunakaa naye na tunashare idea“– Aslay.

Hapa wanaongelea utofauti wa Yamoto Band na band nyingine; “Vitu vingi vishafanyika, uongozi wetu unataka sisi tuwe wapya ndio maana bendi unaona iko tofauti kwanza tuna umri mdogo.. nyimbo zetu zina dakika tatu nne tofauti na bendi nyingine..“– Maromboso.

Band nyingi zinavunjika, unadhani hii itatokea kwa Yamoto?; “Sisi tumekaa ni zaidi ya miaka minne tuko pamoja kabla ya Yamoto Band kujulikana tunajua nini maisha halafu tumetoka katika maisha magumu.. Sio rahisi leo unishawishi kwa vitu vidogo milioni mbili milioni tatu wakati tunategemea mamilioni mengi baadaye“– Aslay.

Ni nini siri ya umoja wao?; “Tumekaa muda mrefu sana kwenye tundu moja kwa hiyo tumeshazoeana hata tabia zetu.. Tumeshakuwa kama ni ndugu sasa na sio marafiki tena“– Bella.
Hapa Charles aliomba kuambiwa maana ya ‘Kupwelepweta‘; “Kupwelepweta ni kitu ambacho hakikutoshi, kama mimi nivae koti lako lazima linipwelepete…“– Aslay.

Hii ni sauti ya Interview yao yote nimerekodi BBC Dira ya Dunia, play kuisikiliza.

Msanii wa Vichekesho Atia Aibu Dodoma, Nyeti zake Zaonekana Wazi Akiwa Jukwaani

$
0
0
Mchekeshaji maarufu hapa Tanzani Masai nyotambafu ambaye kwa sasa na Presenter wa Star Tv kwenye kipindi cha MINI BUZZ Ambapo kwa sasa wapo Dodoma kw ajili ya maandalizi ya vipindi vyao ambavyo vinaruka kila siu kupitia luninga hiyo... Siku ya jana Masai aliibuka ndani ya kiwanja cha matei lounge na kufanya bonge la show ambapo hakifanikiwa kumaliza show kutoka na mbwembwe zake kumpoza..

Kwenye picha hapo tazama suruali aliyovaa hapo ni Model halafu anaenda kupiga msamba wewe unadhani kitatokea nini hapo?? Hapo ndipo alipobugi step Gafla tulisika Chaaaaaa........ Masamba alioupiga ulifanya aishiwe pozi na kutulia kama dadkika kadhaa akiwa hajui cha kufanya lakini alifanikiwa kujiogeza na kuvuta miguu yake na kujizogeza mpaka nyuma ya kibanda na kusimama huku akiwa amebana miguu na kuanza kutembea robo hatua... Ila tuligundua kwamba Msanii huyo alikuwa hajavaa nguo ya ndani na kuhofia nyeti zake kuonekana... Kiukweli masai alikuwa kwenye wakati mgumu sana mpaka mijasho kumtoka mwili mzima na badae alifanikiwa kutoka eneo hilo na kwenda kuvaa nguo ya ndani pamoja na suruali..tukio hilo lilitokea Matei Lounge Dodoma

Malick: Sijaona Mwanamke Mrembo Kama Rose Ndauka toka Nimeachana Naye

$
0
0
Bwana Malick Bandawe  amefunguka kwa mara ya kwanza kuwa tangu atengane na mzazi mwenziye, Rose Ndauka bado hajatokea wa kumtetemesha.

Akimzungumzia Rose, Malick alisema kuwa huko nyuma alipomuona Rose alimtetemesha na kuamua kuingia mzimamzima mpaka kufikia hatua ya kupata naye mtoto lakini mpaka sasa hajatokea kama yeye.

“Unajua mambo yanapotokea lazima kukubaliana nayo na huwezi kulazimisha. Tangu uhusiano wetu usambaratike, hajatokea kama Rose,” alisema Malick.

GPL

Penzi la Wema Sepetu na Ommy Dimpoz, Kumbe Dimpoz ni Boya tu Nyuma ya Pazia kuna Kigogo

$
0
0

HABARI ya mjini ni kwamba, lile penzi linalonadiwa la Mbongo-Fleva, Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ na mwigizaji Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ limejaa magumashi, ikidaiwa kuwa jamaa huyo kawekwa kama boya tu, nyuma yake kuna kigogo mzito serikalini ndiye anayekula vinono, Risasi Jumamosi limetonywa.


Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika, Dimpoz ameagizwa na kigogo huyo awe mpenzi kivuli wa Wema ili kuzuga watu wasishtukie mchezo kama yeye ndiye anayesukuma gududumu la malovee kwa Madam.

“Kutokana na unyeti wa kazi yake, jamaa hataki kujitokeza ‘front’ ndiyo maana ameamua kumtumia Dimpoz kama kanyaboya huku yeye akiendelea kula vyake,” kilisema chanzo hicho.Kikizidi kumwaga ubuyu, chanzo hicho kilidai kigogo huyo ndiye anayedhamini safari zote za Wema na Dimpoz nje ya nchi ikiwemo ile ya juzikati nchini Marekani ambayo ilibuma.

“Jamaa ana pesa chafu, amemnunulia Wema viwanja viwili kimoja kipo Tabata na kingine Kigamboni, Dar, ndiye anayemwezesha Wema katika shughuli zake za kila siku.“Kigogo huyo ndiye chanzo cha Wema kummwaga Diamond, alimpotezea kwa sababu ya maslahi zaidi, hata kwenye bethidei ya Wema mwaka jana, kigogo huyo ndiye aliyegharamia vitu kibao hadi kusababisha Diamond ahoji,” kilisema chanzo chetu.

Jitihada za kumsaka kigogo huyo ili azungumzie ishu hiyo hazikuzaa matunda lakini alipotafutwa Dimpoz na kusomewa tuhuma hizo, alijibu:“Watu watambue kuwa uhusiano wangu na Wema upo kwa ajili ya ‘project’ zangu, niacheni please niinjoi maisha yangu kuhusu huyo kigogo muulizeni vizuri Wema mwenyewe,” alisema Dimpoz.

Mwanahabari wetu alipomvutia waya Wema, alijibu kwa kifupi na kukata simu:
“Ujue sasa hivi mimi sitaki malumbano na mtu, najua kila mtu siku hizi anaongea kila anachojisikia, naomba niachwe na maisha yangu, unayoyasema hayana maana,  wanasema kwa sababu hakuna anayemjua mpenzi wangu wa sasa sina muda wa kubishana.”

Hivi karibuni, wakiwa Sauz, Wema na Dimpoz, picha zao wakiwa kimahaba zilivuja mitandaoni hivyo kuibuka gumzo kuwa huenda kwa sasa nao wanatoka.

Lowassa Azidi Kushawishiwa na Watu Mbali Mbali Atangaze Nia Ya Kuwania Urais

$
0
0
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Kishapu mkoani Shinyanga, Shija Ntelezu, ameungana na baadhi ya wana CCM wengine kumuomba Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa, ajitokeze kutangaza nia ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juzi, Ntelezu alisema kwa niaba ya wana Kishapu wenzake anamuomba Lowassa baada ya kumaliza adhabu aliyokuwa akitumikia yeye na wenzake watano ni wakati mwafaka hivi sasa wa kutangaza rasmi nia yake kugombea nafasi hiyo ili ampokee kijiti Rais Jakaya Kikwete.

Mwenyekiti huyo alisema kwa kadri anavyomfahamu Lowassa ni mmoja wa viongozi wachapa kazi wazuri hapa nchini na mwenye uwezo wa kutoa maamuzi magumu yanapohitajika kutolewa na kwamba ndiye kwa sasa anayeweza kumrithi Rais Kikwete na kuendeleza kasi ya kusukuma kasi ya maendeleo aliyoyaanzisha.

Alisema wakati taifa likielekea kwenye mchakato wa uchaguzi mkuu, Oktoba mwaka huu ni muhimu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikawa makini kuhakikisha kinamteuwa mgombea mwenye uwezo wa kukabiliana na wagombea wengine kutoka vyama vya upinzani.

“Sisi Kishapu tunaamini iwapo CCM itamsimamisha mgombea jasiri mwenye uzoefu wa kiuongozi ambaye pia ana historia nzuri ya uchapaji kazi hapa nchini ambaye haitokuwa kazi kubwa kumnadi kwa wapiga kura nafikiri Lowassa anatosha kwa nafasi hiyo hivi sasa, yapo mambo mengi makubwa aliyafanya wakati wa uongozi wake,”

“Utumishi wa Lowassa unafahamika hapa nchini kuanzia ndani ya chama hadi Serikalini, kwa sisi wa Shinyanga tunamfahamu zaidi maana aliwahi kuwa mtendaji wetu enzi ya TANU, lakini kikubwa tunachokikumbuka ni jinsi alivyowezesha kutufanikishia mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria,” alieleza Ntelezu.

Alisema ni muhimu vikao mbalimbali vya uteuzi ndani ya CCM vikawa makini katika kufikia maamuzi yake na wajumbe wake wasikubali kuyumbishwa na maneno ya watu wasiokitakia mema chama hicho na kwamba kimchunguze kwa umakini kila mgombea aliyejitokeza bila ya kumpaka sifa mbaya za uongo.

Mwenyekiti huyo alifafanua kuwa ushauri wao wa kumtaka Lowassa agombee nafasi hiyo ya urais si kwamba wana CCM wengine waliojitokeza hawana sifa hizo, bali ni muhimu kumpa kipaumbele mtu mwenye uzoefu mkubwa wa kiutendaji ndani ya serikali na chama.

“Ushauri wetu usichukuliwe kwamba wana CCM wengine waliokwisha tangaza nia hawafai au hawana uwezo na hakuna anayewalaumu, maana ni haki yao ya kikatiba, lakini tunaangalia ni yupi miongoni mwao mwenye uwezo zaidi atakayeweza kukivusha chama chetu kwa urahisi kwenye uchaguzi mkuu ujao,” alieleza.

Akifafanua kuhusu uwezo wa Lowassa Ntelezu alitaja baadhi ya mambo makubwa aliyoyafanya alipokuwa waziri katika wizara mbalimbali nchini na pale alipokuwa waziri mkuu na kutaja baadhi ya shughuli kubwa kuwa ni pamoja na maamuzi ya ujenzi wa sekondari za kata ikiwemo ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Lowassa pamoja na makada wengine watano, Frederick Sumaye, William Ngeleja, January Makamba, Bernard Membe na Stephen Wassira juzi walimaliza rasmi kifungo cha miezi 12 walichopewa na kamati kuu ya CCM ikiwa ni adhabu ya kukiuka kanuni na taratibu za chama hicho na kuanza kampeni za kuwania urais kabla ya wakati.

Mkuu wa Kituo cha Polisi Afungwa Jela Miaka 30 kwa kosa la Kumbaka Mahabusu

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa ya Njombe, imemhukumu aliyekuwa mkuu wa kituo cha Polisi Ilembula kifungo cha miaka 30 jela, baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka  mtuhumiwa aliyekuwa ndani ya mahabusu.

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Augustine Rwezile, baada ya mshtakiwa huyo James Nyambenga kukiri kosa hilo mahakamani, ambapo mshakiwa huyo anadaiwa kumtoa msichana huyo kwenye chumba cha mahabusu alikokuwa anashikiliwa na kumbaka.

Mwanamke huyo ambae ni mhudumu wa bar alikuwa anashikiliwa kwenye mahabusu ya kituo hicho kwa tuhuma za uzururaji.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Rwezile amesema ushahidi uliotolewa na upande wa mlalamikaji na vielelezo vya daktari aliyempima msichana huyo viliweza kuithibitishia Mahakama kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo.

BAADA ya Kupewa Talaka Jack Pentezel Afunguka na Kusema Haya Kuhusu Ndoa Hiyo iliyobuma

$
0
0
BAADA ya kupewa talaka na aliyekuwa mumewe, Gadna Dibibi, mwigizaji Jacqueline Pentezel ‘Jack Chuz’ ameamua kufunguka na kuweka wazi kuwa hayuko tayari kuolewa tena.

Jack alisema, kwa muda aliodumu kwenye ndoa ameshaona raha na karaha yake hivyo suala la kuolewa tena sasa hivi halipo akilini mwake.

“Katika ndoa lazima kuwe na mabaya na mazuri, hata hivyo siwezi kusema ndoa ni chungu hapana, ila mimi kwa sasa hivi nimeona nipumzike kwanza sitaki tena ndoa labda kwa hapo baadaye nitakapojipanga tena upya,” alisema Jack.

Jack alidumu na mumewe huyo kwa miaka miwili na nusu kabla ya kupewa talaka hivi karibuni huku chanzo kikiwa ni kusalitiana katika mapenzi.

Mwanamke Ashikwa na Hamu Kupitiliza Afuata Wanaume Barabarani na Kuomba Wambake..Video

$
0
0
Embu Pata picha wewe mwanaume Mwanamke mzuri kama huyu amekufuata barabarani na kutaka akupe bure bure ..utafanyaje ...embu angalia video hii hapa chini jinsi huyu mwanamke anavyofuata Wanaume barabarani akitaka wamfanyiezie kitu mbaya  baada ya kushikwa hamu kupitiliza..Hii imetokea huko Nigeria:
VIDEO HII HAPA CHINI:

Kuacha Usagaji Unaofanyika Shule za Kike, Hili ni Lingine la Kusikitisha Linalofanyika Kwenye Shule Nyingi za Boarding-Video

$
0
0
Kuacha mambo ya usagaji ambayo yamekuwa yakiripotiwa sana kwenye shule za boarding za wasichana sasa limeibuka hili la Wanafunzi kutesana hasa wale wa kidato cha juu kuwatesa wa kidato cha chini ..Kwenye video hii wanafunza hawa wanampa kichapo cha mbwa mwizi mwanafunzi mwenzao huku akiwa hana uwezo wa kujitetea...Habari tulizozipata inasemekana baada ya video hiyo kuvuja na walimu kuiona wanafunzi kadhaa waliohusika walifukuzwa shuleni  hapa ..hii imetokea huko South Africa...Video ya kusikitisha hii hapa chini:

Picha Mbali Mbali za Msichana Mwenye Umbo Matata Anayesemekana Kateuliwa Kuwa Mkuu wa Wilaya

$
0
0
Jana Siku Nzima Msichana huyu anayejulikana kama Nice Chande ama @mwakalicious24 amepaishwa sana kwenye mitandao ikisemekana kuwa Rais kamchangua kuwa Mkuu wa Wilaya ...Watu wengi waliguswa hasa kutokana na umbo lake matata ....Bado hatujapata ukweli wa jambo hili lakini haraka haraka nimeangalia majina ya wakuu wa Wilaya wapya sijaona jina lake labda awe anatumia jina jingine ...Jionee Picha zaidi Hapa Chini:






Precision Kuuza Ndege Zake..Kisa na Mkasa Huu Hapa

$
0
0
SHIRIKA la Ndege la Precision linatarajia kuuza baadhi ya ndege zake na kubakiza ndege sita kupunguza mzigo wa madeni yanayoikabili Kampuni hiyo kwa sasa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo, Michael Shirima alisema Dar es Salaam jana kuwa hatua hiyo imefikiwa kutokana na uchakavu wa ndege hizo na hali ya uchumi wa kampuni.

“Kampuni iko katika mazungumzo na mwekezaji ili kukamilisha makubaliano ya kununua ndege zenye madeni na kisha kuzikodisha kwa kampuni nyingine… makubaliano haya yanatarajiwa kufikiwa mwishoni mwa robo ya kwanza ya mwaka huu,” alisema Shirima.

Alisema pamoja na kufikia hatua hiyo kampuni haijakata tamaa kwa kuweka jitihada ya kutafuta mtaji mkubwa kupitia kwa wanahisa wa sasa au wawekezaji wasio wanahisa.

Awali akiitoa taarifa katika mkutano mkuu wa mwaka wa Tatu wa wanahisa, Shirima alisema mazingira ya biashara yalikuwa na ushindani huku kukiwa na hofu juu ya usalama duniani kote.

Pia alisema thamani ya fedha za kigeni hususan Dola ya Marekani imeendelea kukua ikilinganisha na shilingi ya Tanzania hivyo kusababisha akiba hafifu ya fedha za kigeni na hasara kwa biashara ambazo matumizi yake mengi yanategemea fedha hizo.
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live




Latest Images