Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Kamati Saidia Stars na TFF Wasutana na Kuonyooshea Vidole Mchana Kweupe....

$
0
0
Kamati ya Saida Taifa Stars ishinde imemaliza kazi na kuvunjwa rasmi jana, lakini nyuma yake imeacha maswali mengi kuliko majibu kuhusu utendaji na uhusiano wake na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Rais wa TFF, Jamal Malinzi aliunda kamati hiyo ili kuhamasisha Stars iishinde Algeria na kufuzu hatua ya makundi kusaka tiketi ya kucheza Kombe la Dunia mwaka 2018, badala yake Stars ikaishia kufungwa jumla ya mabao 9-2.
Jambo kubwa lililozua mkanganyiko ni suala la usafiri wa ndege kwa ajili ya Stars kwenda Algeria kwa ajili ya mchezo wa marudiano.

Awali, kamati hiyo chini ya Mwenyekiti Farough Baghozah, ilidai kupata udhamini kutoka kwa Kampuni ya Fastjet waliotoa punguzo la gharama za tiketi kwa wachezaji kufikia dola 700 (Sh. Milioni 1.4) kwenda na kurudi kwa mtu mmoja.

Hata hivyo, wakati kamati hiyo ikiandaa mipango ya usafiri kupitia Fastjet, TFF ikaja na mipango yake na kuamua kutumia ndege ya Uturuki (Turkish Airways) kwa gharama ya dola 1,200 (Sh.milioni 2.5) kwa mtu mmoja.
Isitoshe, ilielezwa kuwa Fatjet ingetumia muda mfupi (saa nane) hadi Algeria, wakati ndege hiyo ya Uturuki ilisafiri kwa saa 11 hadi Algeria.

Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Michael Wambura jana alisema wakati akizungumza na waandishi wa habari kuwa suala la mabadiliko ya usafiri liliamuliwa na TFF wenye mamlaka safari ya timu hiyo.

"Kamati ilifanya kazi yake, lakini mwisho wa siku TFF iliamua timu isafiri na ndege nyingine," alisema Wambura.

Aidha, alipoulizwa kama hakukuwa na mawasiliano baina ya Kamati na TFF kuhusu usafiri, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Farough Baghozah alisema kwenye vikao vya kamati hiyo kulikuwa na viongozi wa TFF na walikuwa wakifahamu kila kilichokuwa kikiendelea.

"Siwezi kumnyooshea kidole mtu, lakini kulikuwa na watu wa TFF kwenye kamati, tulishangaa na maamuzi yaliyotoka," alisema Baghoza.

Baghoza alisema walishafanya utaratibu (booking) Fastjet na uamuzi wa TFF kukataa kutumia ndege hiyo, umeingiza gharama kamati ya Sh. Milioni 75.

"Gharama hii ya kufuta safari ambayo tayari ilishaandaliwa, tunalazimika kulipa sisi kama kamati,” alisema Baghozah.

Alisema kuwa kamati hiyo ilifanikiwa kukusanya Sh. milioni 120, ambazo walizitumia kwa ajili ya kambi ya timu hiyo nchini Afrika Kusini pamoja na kukaa hotelini jijini Dar es Salaam wakati wakisubiri mchezo dhidi ya Algeria.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa aliikosoa kamati hiyo akidai haikuwa inafanya kazi kwa uwazi na kwamba mambo mengi hayakuwa na ukweli.

"Hiyo (Kamati) iseme ukweli. Ni jambo la kushangaza tuache kutumia usafiri wa bei nafuu na kwenda wenye gharama kubwa. Ukweli ni kwamba, Fastjet hawakutoa punguzo lolote kama kamati inavyodai, ila walikuwa wanatafuta abiria," alisema Mwesigwa.

“Hatukutaka aibu ya kushindwa kusafisha timu kwa kutegemea Fastjet ambayo hatukuwa na uhakika nayo.”
Akiikosoa zaidi kamati hiyo, Mwesigwa alidai kuwa kamati hiyo haikuwahi kuonyesha mkataba wowote wa makubaliano na Fastjet kuhusu kuipunguzia gharama na TFF.
“Sisi hatuwezi kukubali taarifa za mdomoni, tulitaka mambo yafanyike kimaandishi,” alisema na kuongeza:

“Kama kamati ingeonyesha mkataba waliosaini na Fastjet, tungeacha kutumia Ndege ya Uturuki, lakini hilo halikufanywa, sasa kwanini tuweke mategemeo kwenye kazi zisizo na uhakika?”

KINACHOSHANGAZA
Taifa Stars ina mdhamini, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) wenye jukumu la kuigharamia timu katika mambo mengi, lakini hapohapo kamati inadai imetumia Sh milioni 120 walizopata kutoka kwa wadau mbalimbali.

Awali, Kamati ilidai ilihitaji zaidi ya Sh.bilioni 1 kwa ajili ya gharama zote katika mechi mbili za Stars dhidi ya Algeria, lakini imeshindwa kupata hata robo ya fedha hizo.

Bado kamati hiyo ikifahamu haina fedha, ilitoa ahadi ya Sh. Milioni 500 kwa timu kama ingeiondoka Algeria kwenye michuano hiyo. Kama Stars ingefanikiwa, hizo milioni 500 ziketoka wapi?

Viongozi Waliojiuzulu Chadema Warejea Tena

$
0
0
Joto la utawala wa Rais John Magufuli limebadili utendaji kazi wa makatibu wakuu wa wizara mbalimbali waliozoea kukaa ofisini na sasa wanafanya kazi nje ya ofisi na kusikiliza kero za wananchi kwenye maeneo yao.

Wakati hilo likifanyika, Ikulu jijini Dar es Salaam imesema katibu mkuu au mtumishi yeyote wa umma atakayeshindwa kwenda na kasi na mabadiliko ya utendaji kazi katika serikali ya awamu ya tano ajiondoe.

Tamko hilo linalotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alipohojiwa jana  kuhusu kutokuwapo kwa makatibu wakuu wa wizara kadhaa kwenye ofisini zao wiki iliyopita.
 
Makatibu wakuu wa Wizara kadhaa wamelazimika kuzifunga ofisi zao na kuelekea mikoani kusikiliza kero za wananchi.

Hali ya viongozi hao kuhama jiji na kwenda mikoani imeleta mabadiliko ya utendaji kazi wao baada ya miaka ya nyuma kuzoeleka kutumia muda mwingi ofisini na kuacha kazi za nje kufanywa na waziri, naibu au watendaji wengine.

Baadhi ya wizara ambazo zilitembelewa na kukuta ofisi za katibu mkuu zikiwa zimefungwa ni Uchukuzi, Tamisemi, Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano na Ujenzi.

Baadhi ya wafanyakazi wa wizara hizo ambao hawakutaka majina yao yatajwe, walisema mabosi wao kwa sasa inakuwa nadra kuonekana ofisini wakifanya kazi kwa kuogopa kuonekana wazembe.

"Hatujawahi kuona katibu anakwenda mikoani kama ilivyo sasa, kila siku anakwenda huku na kule kuangalia miradi na kero za wananchi," alisema mmoja wa wafanyakazi wa moja ya wizara  hizo.

Hatuna Muda na Katibu Mkuu Goigoi-Sefue
Akitoa kauli ya serikali, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alisema kuanzia sasa katibu Mkuu na mtendaji wa serikali ambaye anafanya kazi kwa kusuasua ajiondoe mwenyewe.

Alisema tayari amefanya kikao na makatibu wote kuwaeleza suala hilo na atakayerudi nyuma hatakuwa na nafasi katika serikali ya awamu ya tano.

"Jambo hilo tumekubaliana kwenye kikao, serikali ya awamu ya tano haitakuwa na utani kwa wale watakaoonekana hawaendi na kasi ya Rais, sasa wanatakiwa kuchagua kama wanataka kuendelea na nafasi  zao au la," alisema Sefue

IKULU: Katibu Wa Wizara ambaye ni Goigoi Ajiondoe Mapema

$
0
0
Joto la utawala wa Rais John Magufuli limebadili utendaji kazi wa makatibu wakuu wa wizara mbalimbali waliozoea kukaa ofisini na sasa wanafanya kazi nje ya ofisi na kusikiliza kero za wananchi kwenye maeneo yao.

Wakati hilo likifanyika, Ikulu jijini Dar es Salaam imesema katibu mkuu au mtumishi yeyote wa umma atakayeshindwa kwenda na kasi na mabadiliko ya utendaji kazi katika serikali ya awamu ya tano ajiondoe.

Tamko hilo linalotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alipohojiwa jana  kuhusu kutokuwapo kwa makatibu wakuu wa wizara kadhaa kwenye ofisini zao wiki iliyopita.
 
Makatibu wakuu wa Wizara kadhaa wamelazimika kuzifunga ofisi zao na kuelekea mikoani kusikiliza kero za wananchi.

Hali ya viongozi hao kuhama jiji na kwenda mikoani imeleta mabadiliko ya utendaji kazi wao baada ya miaka ya nyuma kuzoeleka kutumia muda mwingi ofisini na kuacha kazi za nje kufanywa na waziri, naibu au watendaji wengine.

Baadhi ya wizara ambazo zilitembelewa na kukuta ofisi za katibu mkuu zikiwa zimefungwa ni Uchukuzi, Tamisemi, Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano na Ujenzi.

Baadhi ya wafanyakazi wa wizara hizo ambao hawakutaka majina yao yatajwe, walisema mabosi wao kwa sasa inakuwa nadra kuonekana ofisini wakifanya kazi kwa kuogopa kuonekana wazembe.

"Hatujawahi kuona katibu anakwenda mikoani kama ilivyo sasa, kila siku anakwenda huku na kule kuangalia miradi na kero za wananchi," alisema mmoja wa wafanyakazi wa moja ya wizara  hizo.

Hatuna Muda na Katibu Mkuu Goigoi-Sefue
Akitoa kauli ya serikali, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alisema kuanzia sasa katibu Mkuu na mtendaji wa serikali ambaye anafanya kazi kwa kusuasua ajiondoe mwenyewe.

Alisema tayari amefanya kikao na makatibu wote kuwaeleza suala hilo na atakayerudi nyuma hatakuwa na nafasi katika serikali ya awamu ya tano.

"Jambo hilo tumekubaliana kwenye kikao, serikali ya awamu ya tano haitakuwa na utani kwa wale watakaoonekana hawaendi na kasi ya Rais, sasa wanatakiwa kuchagua kama wanataka kuendelea na nafasi  zao au la," alisema Sefue

Je Kasi ya Magufuli na Watendaji Wake Ndio Mwanzo wa Udikteta? Ama ni Kasi Inayotakiwa Katika Taifa Hili ?

$
0
0
Mwalimu Nyerere once a time alisema kama nigetaka kuwa dicteta ningeweza. hivi sasa watanzania tumepata upofu wala hatuoni tena. nimewahi kusema kwenye post zangu kuwa IPO siku watanzania watamkumbuka Rais Kikwete.

kwanini niseme ivo, twende pamoja na kama unamatongotongo kanawe,na kama umemeza viroba kaa mbali na hii post,only great thinkers.

1. VITISHO NA HOFU
ukubali au ukatae magufuli sasa anaogopwa na amejaza hofu wananchi haswa wafanyakazi na wafanyabiashara. kumbekeni Adolph Hitler alishinda uchaguzi wala hakupindua serikali pia alipata public sympathy hata pale alipokesea. tazama sasa hata hii post kuna watu watakosoa bila kujali relevance yake.

2. KUVUNJWA KWA HAKI ZA BINADAMU.
hivi sasa unaweza kuweka polisi bila kushtakiwa mfano. hivi jeuri ya Paul Makonda yakumweka MTU kizuizini bila kumpeleka mahakamani ni uvunjaji wa haki za binadamu. sasa ivi kila mkuu wa wilaya anaamua tu kwa ubabe hats bila kuangalia haki za binadamu.

3.KUVUNJWA KWA UTAWALA WA SHERIA.
KUNA uvunjaji wa sheria wazwazi huku wananchi wakichekelea. mh magufuli binafsi alidai atavunja nyumba ambayo inazuia bomba la maji hata km kesi IPO mahakamani kisha watu wanachekelea hii no hatari. kuna bomoa bomoa ambazo zinaendelea hata km kuna pingamizi la mahakama zinavunjwa tu kwa jeuri. pia polisi mwanza walivunja sheria kuzuia kuagwa kwa mawazo.chekeleeni lakini lilikufika u will understand the rule of law what does it mean?. kuna mkuu wa wilaya geita amefukuza kaxi daktari bila kufata utaratibu wa Sheriakupitia kwa mwajiri yani mkurugenzi. OK just laugh and enjoy but it will b u one day

4.UBABE NA JEURI.
BAADJI ya viongozi sasa wamejawa na ubabe na jeuri ambayo ni sifa ya madikteta. hatuitaji viongozi wababe. tunataka mifumo iliopo wazi kuanzia mtaani hadi wilayan km sio taifa. MTU anawezeje kufuta likizo ya mtumishi ambayo ni haki yake km so jeuri na ubabe nothing else u can say.

Conclusion.
Naomba tuangalie mifumo ya uongozi na utawala wa nchi yetu. kuliko magufuli kuwafukuza watu kila siku tatizo sio watu ni mfumo. napendekeza katiba mpya ipigiwe kura ili ianze kutumika. tuache ubabe na vitisho. Magufuli asipowekewa check n balance na kamati kuu believe m he will be a dictator .

By  Assadsyria3

Hili la Wakuu wa Mikoa/Wilaya Kufuta Likizo ni Kuweka Watu Vizuizini ni Ukiukwaji wa Sheria!

$
0
0
Siungi mkono na sitothubutu kuunga mkono matamko ya wakuu wa mikoa ya Tanga na Kilimanjaro kufuta likizo za watumishi wa umma kwa mwezi huu wa December bila kutolewa ufafanuzi wa kisheria! Hizi ni dalili za utawala wa kimabavu na usiotumia weledi na maadili ya kazi! Likizo za watumishi wote wa umma zipo kwa mujibu wa sheria! Mfanyakazi yeyote yule wa umma aliyeajiriwa na anayelipa kodi serikalini ana haki ya msingi kabisa ya kupata likizo ya siku 28 kwa kila mwaka wa utumishi! Hata waalimu huwa hawaendi likizo pale ambapo wanafunzi wamefunga shule! Wao huwa na likizo zao ambazo zipo kwa mujibu wa sheria!

Mkuu wa wilaya kuweka watumishi wa umma kifungoni bila kuwa na maelezo yoyote ya kuridhisha ni dalili za utawala wa kimabavu hatuongozi nchi kwa "Presidential decree" Kiasi kwamba kila kiongozi anaweza kufanya maamuzi kwa kutamka tu na kisha akawa haojiwi! Kumuweka mtu korokoroni ni lazima kuna kosa na ni lazima mahakama iamue haki! Huwezi kumfunga mtu kwa muda kadhaa bila kuwepo na maelezo yoyote kisheria! Mahakama ina kazi gani?

Kumekuwa na tabia zinazoenda kinyume kabisa na maadili ya utumishi wa umma za viongozi kutoa matamko kandamizi na yasiyofuata taratibu za utawala bora kwa lengo tu na wao waonekane wamo kwenye list ya machachari! Waonekane kuwa na wao wamo!

Tunatakiwa watu wajitume ndiyo, tunataka watu wawajibike ndiyo! Lakini tusifanye hivyo kwa kutumia mfumo kandamizi ambao naona unahasisiwa ndani ya Taifa! Hatupo tayari kuona hilo! Watu wafuate taratibu, kanuni na maadili ya utumishi wa umma!

Enzi za utawala wa Kikwete kuna D.C aliwahi kuwachapa waalimu viboko na watu wakapaaza sauti! Nadhani tusipokemea haya kuna wengine watafanya hivyo na kwa hurka ya utawala wa sasa huenda wakaungwa mkono! Ni lazima tujue kuwa sisi tumeshakubali kuwa nchi ya kidemokrasia na nilazima tufuate kanuni za utawala huo!

Tumeona Zanzibar mtu anafuta uchaguzi kinyume kabisa na taratibu watu wanaunga mkono! Hizo ni dalili za utawala mbovu kabisa! Naomba ieleweke kuwa siungi mkono wizi wala uzembe kazini ila katika kuwajibishana ni lazima zitumike kanuni na sheria halali!!

Nafasi za Kazi EQUIT BANK, Application Deadline 4th December, 2015

$
0
0
EQUITY BANK

EMPLOYMENT OPPORTUNITY


Ingia Kwenye Hii Website ya Ajira AJIRAYAKO.COM Kusoma Hizo Nafasi za Ajira

Au Bonyeza HAPA

Socialite CORAZON Teases Kenyan Men After Being “Eaten” By a Ugandan Tycoon

$
0
0

Kisii’s s3xiest socialite, Corazon Kwamboka, has decided to tease Kenyan men days after landing in the Country from Uganda, where she had gone to satisfy a youthful tycoon.

Just feast your eyes on this.




Sakata la Makontena: Mwigulu, Saada Mkuya, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Wanatakiwa Wawe Ndani

$
0
0
Ni jambo la kusikitisha kuwepo upotevu wa kiasi kikubwa cha pesa kwa ukwepaji kodi wa makontainer 349 yenye thamani billion 80 wakati wenye dhamana ya kulinda mali hizi zisipotee wakina Mwigulu Nchemba, Saada Mkuya, Katibu Mkuu wizara ya fedha wakiwa nje bila kuchukuliwa na hatua yoyote kama walivyo wenzao sita walioachishwa kazi na kuwekwa chini ya uchunguzi, haiwezekani makontiner idadi kubwa kama hii ipotee billa wakuu hawa kujua lolote, tunaiomba serikali iwafuatilia na kuwawajibisha mara moja, hivyo hivyo katika uongozi wako Mh. Tingtinga untakiwa kuwafyeka wote. Vivyo hivyo tnataka taarifa sahii ya maandishi kuonyesha kama fedha zlizoamriwa kulipwa kutoka kwa wana-ESCROW kama zimelipwa kwa wakati.
Jamii Forums

Taarifa Sahihi Kuhusu Habari ya Kukamatwa Mabunda ya Hela Kwa Afisa wa TRA zilizozagaa Mtandaoni

$
0
0
Habari zilizosambaa mitandaoni kuhusiana na mabunda ya noti za dola ya Kimarekani kuwa zimekutwa nyumbani kwa mmoja wa watuhumiwa wa mtandao wa wizi bandarini na TRA sio za kweli,  
Ukweli ni kwamba mabunda hayo ya noti yalikamatwa huko jijini York, Portland, Marekani Mwezi Septemba mwaka 2010, na sio hapa Dar es salaam, Tanzania kama ambavyo wadau wengi wa mitandao hasa ya Whatsapp na Instagram wanavyovumisha.
Tumelazimika kutoa habari hii ili kuokoa wadau wetu wengi katika vuguvugu hili la uvumi wa mitandaoni ambayo hupelekea kazi kuwa ngumu kwa wengi wetu tunaotafuta na kutoa taarifa za uhakika na ukweli. Maana samaki mmoja akioza wote huonekana wameoza.
 Vile vile hii ni kuwafumbua wale wote wanaohusika kusimamia na kutekeleza sheria ya mitandao wawe macho na kuanza kuchukua hatua madhubuti ili kupunguza kama si kuondoa kabisa tabia hii mbaya ya kusema uwongo kila kukicha.

Taarifa Kutoka Azam Kampuni ya Bakhresa Kuhusu Kuhusishwa Kwnye Makontena 349 Yaliyotolewa Bandarini Bila Kulipiwa Ushuru

$
0
0
Kumekuwa na taarifa zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii kuwa kampuni ya Bakhresa inahusika na upotevu wa Makontena 349 yaliyoripotiwa hivi karibuni kuwa yametolewa bandarini bila kulipiwa ushuru. Taarifa hizo zilitolewa na Waziri Mkuu wakati wa ziara yake ya Bandari ya Dar es salaam hivi karibuni.
Uchunguzi wetu umeonyesha kuwa si kweli kuwa kuna makontena yenye bidhaa zilizoingizwa na kampuni hio ama ni miongoni mwa makontena yaliyohusika katika sakata hilo. Isipokuwa kumetokea upotevu wa makontena yaliyoingizwa nchini na baadhi ya wafanyabiashara katika eneo la kuhifadhia makontena(ICD) linalomilikiwa na kampuni hiyo la Azam ICD.
Aidha imebainika kuwa kuna uchunguzi unaofanywa na mamlaka ya mapato nchini TRA, huku kukiwa na ushirikiano na uongozi wa Kampuni hiyo (SSB Group of Companies) kuhakikisha wale wote wanaohusika na upotevu huo wanachukuliwa hatua na kodi yote ya serikali inalipwa na wamiliki wote wa makontena yaliyohusika katika upotevu huo wanawajibishwa.

SSB Group of Companies

Corporate Affairs Department

November 29, 2015

RED ALERT: Two High Walue ISIS Terrorists Arrested While Planning a Terror Attack in Kenya

$
0
0

Kenya’s security agencies have foiled an imminent and deadly terror attack by Iranian trained terrorists after they arrested two Kenyans suspected to have been recruited into an Iranian terror cell to carry out attacks targeting both locals and foreigners in the country.

The two, Abubakar Sadiq Louw (69) and Yassin Sambai Juma (25), were arrested as they tried to recruit Kenyans into the terror group to help them stage an attack on the Kenyan soil.

Inspector General of Police, Joseph Boinnet, addressed the media on Saturday morning and confirmed the arrest of the two Kenyan terrorists who were trained in Iran.

Upon interrogation, Boinnet noted that the two terrorists disclosed their mission and their targets in Kenya.

They also revealed they were instructed to recruit more Kenyans into the ring, especially school children.


The two travelled back into the country from Iran where they met their handlers who trained them in many things on how to stage a terror attack as well as resist interrogation when arrested.

Boinnet said the police were still interrogating the suspects with an aim of squeezing more Intel from them.

It is not clear which terror group the two terrorists belong but reliable sources intimated that they belong to ISIS.



Johnie Walker Wazindua Kampeni Mpya ya 'Furaha Itakufikisha Mbali'

$
0
0
PIC NO 2 & 2c.  Mkuu wa masoko bidhaa za pombe kali za Diageo-Serengeti Breweries Limited(SBL) Stanley Samtu (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (Hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya ya Johnnie Walker iliyopewa jina la “Furaha itakufikisha mbali” yenye lengo la kuhamasisha watu kuwa na utamaduni wa kupenda na kufurahia kile wanachokifanya katika kujiletea maendeleo binafsi. (Kushoto) ni Meneja Chapa (pombe kali) wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Shomari Shija na (kulia) ni Dj maarufu kutoka Ireland Frank Jez. “Johnnie Walker” ni chapa maarufu ya pombe kali inayosambazwa na Kampuni ya bia ya Serengeti hapa nchini.


Mkuu wa masoko bidhaa za pombe kali za Diageo-Serengeti Breweries Limited(SBL) Stanley Samtu (katikati) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (Hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya ya Johnnie Walker iliyopewa jina la “Furaha itakufikisha mbali” yenye lengo la kuhamasisha watu kuwa na utamaduni wa kupenda na kufurahia kile wanachokifanya katika kujiletea maendeleo binafsi. (Kushoto) ni Meneja Chapa (pombe kali) wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Shomari Shija na (kulia) ni Dj maarufu kutoka Ireland Frank Jez. “Johnnie Walker” ni chapa maarufu ya pombe kali inayosambazwa na Kampuni ya bia ya Serengeti hapa nchini.


Mkuu wa masoko bidhaa za pombe kali za Diageo-Serengeti Breweries Limited (SBL), Stanley Samtu (kushoto), Meneja Chapa (pombe kali) wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Shomari Shija (kulia) na Dj maarufu kutoka Ireland Frank Jez (katikati) wakionyesha bidhaa mbalimbali za Johnnie Walker wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya ya Johnnie Walker iliyopewa jina la “Furaha itakufikisha mbali” yenye lengo la kuhamasisha watu kuwa na utamaduni wa kupenda na kufurahia kile wanachokifanya katika kujiletea maendeleo binafsi. “Johnnie Walker” ni chapa maarufu ya pombe kali inayosambazwa na Kampuni ya bia ya Serengeti hapa nchini.


Meneja Chapa (pombe kali) wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Shomari Shija (wa kwanza kulia) na Dj maarufu kutoka Ireland Frank Jez (katikati) kwa pamoja wakiwa na mabalozi wa pombe kali ya Johnnie Walker Chiku Ally(wa kwanza kushoto) na Judith Mbowe(wa pili kulia) wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya ya Johnnie Walker iliyopewa jina la “Furaha itakufikisha mbali” yenye lengo la kuhamasisha watu kuwa na utamaduni wa kupenda na kufurahia kile wanachokifanya katika kujiletea maendeleo binafsi. “Johnnie Walker” ni chapa maarufu ya pombe kali inayosambazwa na Kampuni ya bia ya Serengeti hapa nchini.

Chapa maarufu ya pombe kali inayosambazwa na Kampuni ya bia ya Serengeti Breweries “Johnnie Walker” imezindua kampeni mpya iliyopewa jina la “Furaha itakufikisha mbali” siku ya leo katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam ikiwa na lengo la kuwahamasisha watu kuwa na furaha katika kila wanachokifanya kwa vile furaha huleta maendeleo na sio kinyume chake kama wengi wanavyodhani.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye uzinduzi wa Kampeni hiyo katika hoteli ya Serena, Mkuu wa kitengo cha Masoko pombe kali wa Kampuni ya bia ya Serngeti (SBL) Stanley Samtu alisema “Kama chapa, Johnnie Walker imesimama daima kwenye upande wa maendeleo. Imekuwa hivyo kwa miaka takribani 200 tangu mwanzilishi Johnnie Walker alipoanza ufundi wake. Uzoefu umetufundisha kwamba maendeleo hayatakiwi kuwa safari ya kupanda tu na isiyo na kikomo bali tunaweza kupiga hatua na kufurahia katika malengo tunayoweza kuyafikia kila kukicha. Hiyo ndio maana halisi ya kampeni hii ya Furaha itakufikisha mbali zaidi”.
Kufurahia kile unachokifanya ni sehemu kubwa na muhimu ya kufanikiwa na kuwa na maendeleo. Katika juhudi za kufikisha ujumbe kwa wahusika, Johnnie Walker inategemea kuwamulikia baadhi ya nyota katika fani mbalimbali waliojizolea umaarufu kutokana na mafanikio walioyafikia. Hawa ni pamoja na Sheria Ngowi wa tasnia ya mitindo, Dj Frank Jez kutoka Ireland na Dj Peter Mo. Vijana hawa wote wamebobea katika kile wanachokifanya na wamekuwa mfano wa kuigwa nchini. Wamekuwa sehemu ya dunia ya watu ambao wanaaamini kuwa chanya siku zote katika kazi ni moja kati ya vitu viliyowasaidia kufika mbele zaidi katika fani zao.

Soma Nafasi za Ajira Katika Magazeti ya Leo....Zipo za Serekali na Mashirika Binafsi

Waziri Mkuu: Tumedhamiria Kuwatumikia Watanzania...Tutahakikisha Mapato Ya Taifa Yanatumika Kwa Maslahi ya Watanzania Wote

$
0
0
WAZIRI MKUU Majaliwa Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuhakikisha kila kinachokusanywa kama mapato ya nchi kinatumika kwa maslahi ya Watanzania wote na si kwa manufaa ya wachache.
Alitoa kauli hiyo jana mchana (Jumapili, Novemba 29, 2015) wakati akifunga maadhimisho ya miaka 20 ya Dayosisi ya Pwani ya Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) kwenye ukumbi wa PTA, viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

“Serikali imeanza kukabiliana na upotevu wa mapato ya Serikali na kuepuka matumizi yasiyo ya lazima ya fedha za umma. Nia yetu ni kuhakikisha kila kinachopaswa kukusanywa kama mapato ya nchi, kikusanywe na kitumike kwa masuala ya msingi kwa ustawi wa Watanzania wote na si kwa watu wachache,” alisema.

Akifunga maadhimisho hayo kwa niaba ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu alisema Serikali imedhamiria kupambana na maovu yote na kuondoa kero zinazowaumiza wananchi wa kawaida.
 “Wako watu wanaoamini kwamba hatuwezi, nawaomba waondoe hiyo dhana. Wako watu wanaodhani kwamba kwamba utawala huu ni wa watu wapole, nao pia waondoe hiyo dhana,” alisema huku akishangiliwa na mamia ya waumini waliohudhuria sherehe hizo zilizoanza Novemba 27, 2015.

“Tunawaomba Watanzania wote mtuunge mkono kwenye vita hii na mtuwezeshe kuifanya kazi hiyo. Tunaomba waumini wote mtuombee katika sala zenu za kila siku ili tuweze kuongoza kwa haki na kuwaletea Watanzania wote maendeleo,” aliongeza.

Akinukuu kitabu cha Mithali sura ya 29 mstari wa pili, Waziri Mkuu alisema: “Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi, bali mwovu atawalapo, watu huugua. Mtuombee viongozi wenu tuwe waadilifu na wenye kutenda haki. Nasi tutaendelea kuwa waadilifu ili watu wetu wasigue,” alisema.

Aliwataka viongozi wa kanisa hilo waendelee kuisaidia Serikali katika kujenga kundi la watu wenye maadili mema ili walisaidie Taifa kuwa na watu waadilifu na hivyo kupunguza kero nyingi zinazoikabili jamii.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na waumini wa kanisa la hilo kutoka mikoa mbalimbali, Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT, Askofu Silas Kezakubi alisema Kanisa hilo litaendelea kumuombea Rais Dkt Magufuli na viongozi wenzake ili wawe na afya njema, wawe na hekima na kuahidi kwamba wataendelea kuwaweka chini ya ulinzi wa Mungu siku zote.

Alisema wao kama kanisa wanaamini kwamba Serikali ya awamu ya tano ina nia ya kuwatumikia wananchi kwa bidii na uadilifu lakini akasisitiza kuwa siri ya bidii na uadilifu inapatikana kwenye neno la Mungu.

Akisoma risala ya kanisa hilo, Askofu wa AICT Dayosisi ya Kibaha, Askofu Charles Salalah alisema kanisa halina budi kushirikiana na Serikali kwa sababu wote wanawahudumia watu walewale isipokuwa katika malengo tofauti.

Alisema kanisa hilo linahubiri maadili mema na bidii katika kazi kwa vile linaamini kuwa maendeleo hayadondoki kutoka juu wala hayaoti kama uyoga bali yanapatikana kwa watu kufanya kazi.

Akisisitiza kuhusu uadilifu, aliwataka wazazi kudumisha ndoa zao ili watoto wapate malezi mema kutoka kwa baba na mama na kwamba baba na mama wasipokaa vizuri, watoto hawawezi kuwa waadilifu.

“Wazazi tunao wajibu wa kupanda mbegu bora ya uzalendo kwa watoto wetu. Endapo tutapanda mbegu mbaya ya kuwagawa watoto wetu kwa itikadi tofauti, ni lazima tujue kuwa tutavuna tunachopanda.”

“Tukumbuke kuwa tunalo Taifa moja tu la Tanzania. Hata kama watoto wetu watakuwa na upenzi na vyama vyao, ni lazima tuwalee katika misingi ili wakue wakijua Taifa letu ni moja tu. Ndiyo maana tunaweka mkazo kwenye familia kwa sababu maadili mema yanaanzia nyumbani,” alisisitiza.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM
JUMAPILI, NOVEMBA 29, 2015.

Lowassa na Mbowe Watua Katika Eneo Ambalo Mauti yalimfika Mwenyekiti wa Chadema Geita Alphonce Mawazo

$
0
0
M/Kiti CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe akifatana na alikuwa mgombea urais wa chama hicho Mhe. Edward Lowassa pamoja na viongozi mbalimbali wakitazama eneo ambalo Alphonce Mawazo alifanyiwa kitendo ya kinyama cha kukatwakatwa mapanga na watu wanaosemekana ni wafuasi wa CCM ikiwa ni umbali mchache kutoka kutuo cha polisi na ofisi za CCM katika barabara kuu inayoelekea Geita kutokea Busanda.



Wataalam Wanashauri: Tuwapige Wake zetu Angalau Mara Moja Kila Mwezi

$
0
0
Wataalam wa mahusiano wanashauri ili mahusiano yadumu vizuri na kwa muda mrefu inabidi mume amuonye mkewe kila siku, amkalipie kila wiki, ampige kofi angalau mara moja kila mwezi, ampige kibano cha maana kila mwaka na amrudishe kwao angalau mara moja kila baada ya miaka mitano. Kwa kufanya hivi uamsha ari na upya wa penzi.

Nchi kama Marekani ambao kufanya domestic violence ni kosa kubwa sana ni moja ya nchi zinazoongoza kwa talaka duniani maana wanawake wanaota mapembe na kuona wenzi wao hawawajali lakini sehemu kama mara ni vigumu sana ndoa kuvunjika.

Kazi kwenu waoaji na waolewaji kuokoa ndoa zenu

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Leo Tarehe 30 Novemba..Ikiwemo ya Mali za Vigogo TRA Kuibua Mapya

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Leo Tarehe 30 Novemba

Njia 10 Zinazotumika Kukwepa Kodi Bandari ya Dar es Salaam

$
0
0
Wakati Serikali ikikunjua makucha yake dhidi ya wote waliohusika katika kashfa ya kupitisha makontena 349 kwenye Bandari ya Dar es Salaam bila ya kuyalipia kodi, imefahamika kuwa idadi hiyo ya makontena ni sehemu ndogo tu ya mamia ya mizigo yanayovushwa kinyemela kila uchao na kuikosesha serikali mabilioni ya fedha.

Hata hivyo, wakati serikali ya Rais Magufuli na Waziri Mkuu wake, Kassim Majaliwa, ikiendelea kutafuta suluhu ya kudumu kuhusiana na ukwepaji kodi, imebainika kuwa kazi hiyo siyo lelemama kwani zipo njia zaidi ya tisa zinazotumiwa kukwepa kodi katika Bandari ya Dar es Salaam.

Mosi, ni kupitia mwanya utokanao na mfumo wa zamani wa malipo usiohusisha ule wa sasa wa kielektroniki, maarufu kama ‘E-Payment’.
 
Kwamba, wafanyabiashara wengi hutumia mfumo huo wa zamani unaohusisha matumizi ya karatasi zilizojazwa kwa mkono na hivyo kuwezesha ujanja wa kubadili taarifa kwa manufaa ya mitandao ya wakwepaji wa kodi.

“Tatizo lililopo ni kwamba mfumo wa E-Payment ni mpya (umeanza Julai) na umefungwa kwenye benki moja tu iliyopo ndani ya eneo la Bandari… ule wa zamani unaendelea kutumiwa na wajanja hucheza na maandishi ya kujaza kwa mkono kuhujumu mapato ya serikali,” chanzo kimeeleza.

Njia ya pili ya kuhujumu mapato bandarini hapo, imetajwa kuwa ni ya kushirikiana na maafisa wa benki. Hii ina uhusiano mkubwa na njia ya kwanza inayohusisha matumizi ya mfumo wa malipo wa zamani usiokuwa wa kielektroniki.
 
Mfanyabiashara anaweza kuandikiwa kodi sahihi anayotakiwa kulipa, lakini anashirikiana na wafanyakazi wa benki anayokwenda kuweka fedha kwa kuhakikisha kuwa baada ya kufanikiwa kuondoa kontena bandarini, maafisa wa benki husika husitisha malipo hayo kwa kuondoa fedha husika kwa madai kuwa fedha ziliingizwa kwenye akaunti husika kimakosa.

“Huwa kuna ushirikiano wa karibu kati ya maafisa wa benki na mfanyabiashara husika. Baada ya kontena kutolewa bandarini, hamisho la fedha (transaction) huondolewa katika mfumo kwa maelezo kuwa halikuwa sahihi,” chanzo kimedai, huku kikisisitiza kuwa ushirikiano huo huhusisha pia watu wa Bandari na TRA ambao mwishowe hugawana malipo kadri wanavyokubaliana.

Tatu, ni mwanya wa uvushaji wa makontena yenyewe yasiyolipiwa ushuru kupitia mageti maalum yanayofahamika kwa kazi hiyo, hasa geti Namba 3 ambalo chanzo kimedai ndilo linaongoza kupitisha mizigo ya ‘dili’.

“Kwa ujumla yapo mageti matano ya kupitisha bidhaa mbalimbali, baadhi yakiwa ni ya kupitihia mafuta, nafaka na magari.
 
"Hili Namba 3 ndiyo hutumika kupitisha makontena ya bidhaa zenye thamani kubwa na wengi wasiolipa kodi hulitumia hili,” chanzo kilieleza kabla ya kufafanua kuwa awali, hilo geti Namba 3 halikuwa na mfumo wowote wa kuangalia kama kontena husika limelipiwa au la na ndiyo maana lilikuwa likitumika zaidi kupitisha makontena yasiyolipiwa kodi.

Njia ya nne ya kuhujumu kodi ya mapato ni ya kuwatumia watu wanaoendesha bandari kavu (ICD’s). Inaelezwa kuwa hivi sasa kuna bandari kavu 12, ambazo kila meli inapoingia hujulikana kila mzigo husika unapelekwa kwenye bandari ipi kati ya hizo.
 
Hata hivyo, inaelezwa kuwa kinachofanyika ni kwa baadhi ya makontena yanayotolewa bandarini ili yapelekwe bandari kavu kabla ya kukombolewa na wahusika huishia kupelekwa kwa wafanyabiashara wenye makontena na hivyo kuikosesha mapato serikali.

“Awali kwenye ICD’s kulikuwa na askari wa mmiliki wa ICD’s na siyo wa TPA… huyu alikuwa akiangalia malipo ya bosi wake tu ambayo ni gharama za kuhifadhi mzigo na hivyo TPA na TRA huambulia patupu,” chanzi kimeeleza, kikiongeza kuwa hivi sasa walau kuna nafuu kwani kwenye ICD’s kuna walinzi wa TPA lakini hilo limefanyika baada ya watu kuwa tayari wameshaiba sana.

Njia ya tano inayotumiwa kukwepa kodi ni ya kubadili taarifa, hasa kupitia watu wenye wajibu wa kufanya tathmini. Kwamba, badala ya mzigo kukadirwaa kodi kwa kiwango sahihi, wahusika ambao zaidi huwa ni watu wa TRA hukadiria fedha kidogo baada ya kujihakikishia kuwa nao wanapewa mgawo na wafanyabiashara.

“Hapo utakuta kontena la kodi ya milioni 80, mteja anaambiwa alipe milioni 40 tu … na wakati mwingine kiasi hicho pia hakiandikwi balki huandikwa cha chini zaidi kama milioni 5 tu…hii ni njia nyingine inayoligharimu taifa mabilioni ya fedha,” chanzo kimeeleza.

Njia ya sita inayofanikisha ukwepaji kodi ni mtandao mpana wa baadhi ya vigogo wa maeneo mbalimbali Bandarini na TRA, ambao hawa huhakikisha kuwa wanakuwa na timu ya vijana wao wa kazi karibu katika kila eneo ili kufanikisha mipango yao.

“Hii ndiyo njia kubwa ya hujuma. Kama utakumbuka aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, alisambaratisha baadhi ya mitandao kwa kuwagusa vigogo 27…  ile ilikuwa kuvunja mtandao uliokuwapo. Hilo lilisaidia kiasi, lakini sasa ipo pia mitandao mingine ambayo uchunguzi ukifanyika utabaini kuwa mambo yameanza kurudi kama zamani,” imeelezwa.

Njia ya saba ya ukwepaji kodi ni kwa baadhi ya vigogo wa Bandari na TRA kuanzisha kampuni zao za uondoaji mizigo bandarini. Inaelezwa kuwa hizi hutumiwa sana kufanikisha ‘dili’ za ukwepaji kodi na ndiyo maana haishangazi kusikia kuwa kuna makontena zaidi ya 300 hayaonekani kwenye kumbukumbu za TRA.

Njia ya nane ya ukwepaji kodi ni kuonyesha kuwa kontena linapelekwa nje ya nchi, kwa mfano Malawi, wakati ukweli ni kwamba huishia hapahapa nchini.

“Utakuta kontena linadaiwa kupelekwa Malawi, lakini linachukuliwa na gari kukuu linaloonekana wazi kuwa haliwezi kufika hata Kibaha… njia hii pia hutumiwa sana kuikosesha serikali mapato,” chanzo kingine kilisema

Njia ya tisa ya ukwepaji kodi  ni ucheleweshaji wa makusudi wa utoaji makontena. Kwamba, mteja anapotaka kutoa mzigo wake kwa kufuata njia halali zilizopo, huishia kuzungushwa kila uchao ili akubali kutoa rushwa na mwishowe kulipishwa kiwango pungufu cha kodi au kulipa fedha zisizoingia kabisa kwenye mikono ya TRA.

Njia ya kumi ni ubabaishaji unaofanyika katika kuorodhesha idadi ya makontena inayotolewa bandarini kwenda kwenye bandari kavu. Hapa, kama makontena yanayotolewa ni 12, basi huandikwa kuwa ni 10 na mengine mawili huishia kuondolewa bila ya kuwa na kumbukumbu zake kwa ajili ya kulipiwa kodi.

Pamoja na kuwapo kwa njia zote hizo, chanzo kimedai kuwa sababu kubwa ya kufanikiwa kwa ukwepaji kodi ni mtandao mpana unaoundwa na vigogo mbalimbali na ndiyo maana taarifa mbalimbali za wakaguzi wa ndani na wa nje katika Bandari ya Dar es Salaam huishia kubaki kwenye makabrasha bila ya kuwapo kwa utekelezaji wowote wa vitendo juu ya yale yanayopendekezwa na wataalamu.

Chanzo: Nipashe

Moto Wa Magufuli Watua Kwa Bakhresa.......TRA Yazuia Makontena Yake Bandari Kavu, Kampuni Yake Yahusishwa na Ukwepaji Kodi

$
0
0
KAMPUNI ya Said Salim Bakhresa (SSB) inachunguzwa na vyombo vya dola kwa tuhuma za kushiriki kukwepa kodi na hivyo kuikosesha serikali mabilioni ya fedha kutokana na makontena yaliyohifadhiwa kwenye bandari yake ya nchi kavu (ICD) ‘kupotea’ bila kulipiwa kodi.

 Tayari Mamlaka ya Mapato (TRA) imepiga marufuku SSB kuingiza makontena katika bandari hiyo kavu ambako ndiko kunadaiwa kufanyika kwa vitendo hivyo vya ukwepaji wa kodi kutokana na baadhi ya makontena kupotea katika mazingira ya kutatanisha.

Katika barua iliyoandikwa kwenda kwa Meneja Mkuu wa SSB iliyosainiwa na Wolfgang Salia kwa niaba ya Kamishna wa Ushuru na Forodha wa TRA, inaeleza kuwa usitishwaji huo unatokana na kampuni hiyo ya Bakhresa kuchunguzwa kwa tuhuma za kuwepo madai ya kujihusisha na ukwepaji wa kodi kwa baadhi ya kontena zilizoingia na kutoka kwenye ICD yake.

Kwa mujibu wa barua hiyo, vitendo hivyo vya ukwepaji wa kodi vimefanywa kinyume cha Sheria ya Ushuru wa Pamoja wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Mwaka 2004 na hivyo kuikosesha Serikali mapato.

“Unafahamu kwamba uondoaji wa bidhaa kutoka eneo linalodhibitiwa na forodha, ambalo kodi na ushuru wa serikali haujalipwa ni kinyume na sheria kwa mujibu wa Sheria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Usimamizi wa Forodha ya mwaka 2004 na kanuni zake kwa vile husababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

“Kwa sababu hiyo, imeamuriwa kukuzuia kupeleka makontena katika bandari yako kavu kuanzia tarehe ya barua hii, hadi suala hili litakapotatuliwa. Pande zote zinazohusika zinapaswa kutii amri hii.

“Kutokana na sababu hizo, tunasimamisha upelekaji wa makontena katika bandari yako kavu. Usitishaji unaanza mara moja. Hata hivyo utoaji wa bidhaa zilizopo katika bandari hiyo tajwa utaendelea,” ilisema sehemu ya barua hiyo iliyoandikwa Novemba 17, mwaka huu.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Walipa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Richard Kayombo alipoulizwa juu ya suala hilo jana, alikiri kampuni hiyo kuchunguzwa, lakini akagoma kuzungumzia kwa undani kwa kuwa suala hilo liko kwenye uchunguzi.

“Mimi siwezi kulizungumzia suala hilo kwa sababu liko kwenye uchunguzi na wanaofanya uchunguzi huo ni state organ (vyombo vya dola). Katika hatua hiyo, mimi siruhusiwi kusema lolote,” alisema Kayombo.

Meneja wa Kundi la Makampuni ya Said Salim Bakhresa, Said Mohamed alipotafutwa kuzungumzia suala hilo, alisema yeye hahusiki na masuala ya ICD badala yake mambo hayo aulizwe Meneja wa ICD aliyemtaja kwa jina moja la Khan. “Mimi niulizie unga umekosekana... Sihusiki kabisa na mambo hayo,” alisema Mohamed.

Hata hiyo, Mohamed aligoma kutoa mawasiliano ya Khan, akisema: “Hiyo namba mimi hapa sina, wewe mtafute tu huko ICD atakupa maelekezo zaidi.”

Habari zilizopatikana jana pia zilieleza kuwa mmoja wa wafanyakazi wa SSB anayeishi maeneo ya Kinyerezi (jina tunalihifadhi), alivamiwa na kundi la maofisa wa Serikali kuanzia asubuhi hadi jioni na kufanya upekuzi kwake.

“Tangu asubuhi hawa jamaa wamekuja hapa wakamchukua mjumbe wa eneo hili na kwenda naye kufanya upekuzi, hadi sasa hivi wanaendelea kufanya kazi hiyo,” alisema Tito Bagule, mkazi wa eneo hilo.

Tayari Rais John Magufuli ameshamsimamisha Kamishna Mkuu wa TRA, Rished Bade kutokana na tuhuma za uzembe na rushwa na kusababisha upotevu wa makontena zaidi ya 349 yenye thamani ya Sh bilioni 80.

Upotevu huo umegundulika baada ya makontena hayo kuonekana kwenye mifumo ya Mamlaka ya Bandari, lakini haimo kwenye mifumo ya TRA.

Kabla ya kusimamishwa kazi, Bade alikiri kupotea kwa makontena hayo, wizi ambao alisema unafanywa kati ya bandari kuu na bandari kavu (ICD) ya Ubungo.

Alisema kutokana na upotevu wa kontena hizo mmiliki wa bandari hiyo ameamriwa kulipa faini ya Sh bilioni 12.6 na hadi sasa alishalipa Sh bilioni 2.4.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Diwani Athuman, amesema tayari jeshi hilo limeanza upelelezi kuhusu kashfa ya upotevu wa makontena iliyobainishwa hivi karibuni na kusababisha baadhi ya vigogo wa TRA kusimamishwa kazi.

Pamoja na upelelezi huo, alisema wameanza uchunguzi wa mali za wafanyakazi wote waliohusishwa na kashfa mbalimbali TRA kama ilivyoagizwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ili kubaini kama zinaendana na kipato chao halisi.

 Akizungumza na mwandishi wetu jana, Diwani alikiri kuwa jeshi hilo linawashikilia watumishi wanne kati ya watano wa TRA ambao jeshi hilo liliagizwa liwakamate na kuwahoji kuhusu sakata la upotevu wa kontena 349.

“Tuliagizwa tuwakamate watumishi watano, mpaka sasa tumewakamata wanne, mmoja ndio tupo kwenye utaratibu wa kumkamata, lakini kikubwa ni kwamba tumeanza upelelezi, kama tulivyoagizwa,” alisisitiza DCI Diwani.

Breaking News: Sheikh Issa Ponda Ashinda Kesi ya Uchochezi na Kuachiwa Huru

$
0
0
Mahakama ya hakimu mkazi Morogoro imemuachia huru Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda aliyekuwa akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi baada ya mahakama kutoridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka na hivyo kuonekana hana hatia

Makosa yaliyokuwa yakimkabili ni mawili ambayo ni kushawishi watu kutenda kosa, pamoja na kutoa matamshi yanayoumiza imani ya dini nyingine.

Hakimu wa kesi hiyo Mary Moyo amesema ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka haukujitosheleza hivyo mahakama hiyo imemwachia huru na rufaa iko wazi endapo upande wa mashitaka hautaridhika na hukumu hiyo.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>