Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Sifa na Udhaifu za Wanaofikiriwa Kuziba Cheo cha Dk. Slaa Chadema leo...

$
0
0
Kitendawili cha nani atavaa viatu vya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa, aliyeshika wadhifa huo kwa miaka 11, kitateguliwa leo jijini hapa baada ya kikao cha Baraza Kuu la chama hicho, lakini tayari sifa na udhaifu wa majina yanayopewa nafasi kubwa vimewekwa hadharani.

Wanaotajwa kuwa na sifa ya kurithi nafasi ya Dk. Slaa ni waliokuwa wasaidizi wake wa karibu Naibu Katibu Mkuu Bara, John Mnyika na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu.

Vikao vya Kamati Kuu vinaendelea jijini Mwanza kuandaa agenda za Baraza Kuu ambalo litakutana leo kwa ajili ya kujadili majina mawili ambayo yatawasilishwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe.

Vyanzo mbalimbali kutoka ndani ya chama hicho vinaeleza kuwa Mnyika ambaye ni Mbunge wa jimbo la Kibamba huenda asifikiriwe sana katika nafsi hiyo kutokana na ukaribu wake na Dk. Slaa.

Imeelezwa kuwa hata Dk. Slaa alipotangaza kuachana na siasa, Mnyika hakuonekana katika majukwaa na vikao mbalimbali ikiwemo kikao cha Kamati Kuu, kilichopitisha jina la Edward Lowassa kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa 2015.

Wadadisi wa masuala ya kisiasa wanasema Mwalimu hawezi kuvaa viatu vya Dk. Slaa licha ya kufanya naye kazi tangu mwaka 2014 hadi Oktoba 2015, kwani licha ya kukaimu nafasi hiyo hakuweza kuendesha chama kama mtendaji mkuu kwa kiwango kilichotarajiwa.

Wachambuzi hao wanasema Mnyika na Mwalimu moja kwa moja wanapoteza imani ya wajumbe wa Baraza Kuu na hata Mwenyekiti akipeleka majina yao, kuna uwezekano wa kukataliwa kwani Katiba inawaruhusu kufanya hivyo.

Mwingine anayeonekana anaweza kuvaa viatu vya Dk. Slaa ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, ambaye pia ni mwanasheria wa chama.

Lissu anaelezewa kuwa amekitumikia chama hicho kwa uaminifu, kujitoa kwa muda mrefu kwa nguvu zote bila kujali maslahi anayoyapata na hajaonyesha dalili za usaliti.

Lakini Lissu anatajwa kuwa anapungukiwa sifa kutokana na kuwa na maamuzi ya haraka kwa mambo mbalimbali.

Mwingine anayejadiliwa miongoni mwa wavaaji wa viatu vya Dk. Slaa ni aliyegombea ubunge jimbo la Morogoro Mjini, Marcossy Albany, ambaye ana faida ya kufuta dhana kwamba chama hicho kinaongozwa na viongozi kutoka mikoa ya kanda ya kaskazini.

Mratibu wa chama hicho Kanda ya Ziwa, Robert Bujiku, naye anatajwa tajwa ikiwa ni mkakati wa kuongeza misuli ya chama kwa kanda ya ziwa.

Mwanachama mwingine anayetajwa ni Fredreck Sumaye, ambaye sifa yake kuu ni kujitoa kuingia upinzani bila kujali atakachopata na alitembea kwenye kampeni nchi nzima kumpigania aliyekuwa mgombea urais aliyekuwa akiungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wannachi ( Ukawa), Edward Lowasa.

Sifa nyingine ya Sumaye ni kwamba hana makundi na hana tuhuma za ufisadi, lakini wakati vikao hivi vinaendekea Sumaye yupo nchini India kwa matibabu.

"Unajua Mwenyekiti amepewa mamlaka na Katiba ya kupendekeza majina mawili kwenye Baraza Kuu ambalo lina hiyari ya kukubali au kukataa majina husika, hadi sasa ni siri kubwa kwa Mwenyekiti hadi leo atakapotamka majina ya waliopendekezwa," kilisema chanzo chetu na kuongeza:

"Dk. Slaa alikuwa na misuli ndani ya chama, alikijenga kwa muda mrefu hadi ngazi ya chini, wengi wa wanachama wetu wameingia na kumkuta Dk. Slaa hivyo kwa sasa kupata mtu mpya ambaye atavaa viatu vyake siyo jambo jepesi.

"Ni lazima kufanya upembezi kuona mtu makini, mvumilivu, mwenye bidii ambaye atakuwa daraja na mwenye uzoefu katika suasa."
Baadhi ya wanachama na viongozi waliozungumza na Nipashe, walieleza sifa wanazoona zitafaa kwa mrithi wa Dk. Slaa kuwa ni uvumilivu na kufuata nyayo za mtangulizi wake kwa kuwa tayari kubeba lawama na kukijenga chama katika misingi inayotakiwa.

"Chama chenyewe kina taratibu zake, miongozo yake, kanuni, Katiba na sifa hivyo ndiyo hufuatwa katika kumpata kiongozi wa nafasi hiyo," alisema Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Profesa Baregu na kutaja sifa anazoona zinafaa kuwa ni:

“Moja, awe mwenye uelewa mpana siyo anajua mambo ya Chadema tu, bali vyama vingine na kwenye uwanja wa siasa kwa ujumla akiwa na uzoefu mpana na mvumilivu kwa kuwa madonge ya kiasiasa yanayotupwa mengi yanaelekezwa kwa Katibu Mkuu.”

See The Cool App That Every Tanzanian Should Have On Their Phones

$
0
0

Good News! Sasa Blog yako ya Udaku Special Ipo Google Play Store.

Download Udaku Special Blog Android Application CLICK HERE From Play Store

Au Bonyeza hii picha hapa chini

Hapa Nakuletea Picha na Kinachoendelea Kwenye Mkutano Mkuu wa Chadema wa Kutangaza Katibu Mkuu Mpya wa Chama Hicho...

$
0
0
Mambo yanaendelea vizuri ukumbini mpaka sasa Katibu Mkuu anayesubiriwa kwa hamu kubwa atatangazwa rasmi leo Endeleeni kuwa na subira


#LiveUpdates..

Mwenyekiti wa Chadema taifa Freeman Mbowe anasema umoja wao ndani ya UKAWA ulisaidia kujenga mtengamamo wa kitaifa tofauti na chaguzi zilizopita.

Mbowe: Usiku Hotel ya gold crest ilivamiwa na polisi wakimtaka Ester Bulaya, viongozi wa Chadema wakapambana na polisi.. Kama umeingia chadema na unaogopa kulala ndan bac umekosea njia.

Mbowe: Sasa uchaguzi ndani ya Chadema utafanyika mwaka 2017, uchaguzi mkuu wa chama ni October 2018..

Mbowe: Migogoro mingi ndani ya Chadema imepelekea kuanguka kwa chama, hivyo itashugulikiwa kwa haraka.

Mbowe: Kuiua Chadema kuna gharama kubwa..

Mbowe: Mchakato wa kumpata katbu wa Chadema kuna mambo yake... Ebu ngoja tuache nitasema badae..

Mbowe: Jambo ambalo hatutalivumia ndani ya Chadema ni swala la rushwa kwani rushwa linagawa taifa, sasa swala la rushwa lililelewa na CCM na sasa inataka kuingia Chadema.

Mbowe amewanyooshea vidole wale wanaotumia mitandao ya kijamii..

Mbowe: Kuna majimbo kama Iringa, Rukwa, Arusha Chadema waliachiwa kwa aslimia mia moja na Ukawa hvyo amewataka wajumbe wajitafakari kwanini wameshindwa kuchukua ushindi wa kutosha ktk majimbo hayo.

Mbowe: Mkutano umeazimia kufupisha uongozi ndani ya Chadema, ili kujipanga na kupata nafasi ya kujianda vyema ktk uchaguz mkuu.

Mbowe: Changamoto zilizopo ndan ya ukawa hakuna haja ya kuyakimbia bali ni kupambana nayo.

Mbowe: Kutukana na kuchafua chama

Mbowe: Waraka wa kukamatwa kwa Ester Bulaya umetoka kwa spika wa bunge.

Wajumbe wamekubali mabadlko hayo kwa kauli moja..

Mbowe: Nawashauri tunapokuwa popote lazima tukatae nchi yetu kugawa vipande vipande. Kama kuna kosa tunalifanya Chadema ni kushabikia kuligawa taifa.

Mbowe: Wanaovuruga Viti Maalum ni wanaume kuliko wanawake.. Wanaume wana interest na viti maalumu kwa kiasi kikubwa nchi hii na kuharbu utaratbu

Mbowe: Watu walidhani kuondoka kwa Slaa chama kitakufa..

Mbowe: Watoto wangu walikuwa wa kula sana maharage, sasa siku moja wakala nyama, jirani akasema umeona Lowassa kaja Chadema.. Lowassa hakutoa hata senti tano kununua chama.




Mama Diamond Afanya Kufuru...Akarabati Nyumba Kwa Mil 100 na Kununua Mtaa Mzima

$
0
0

KUFURU! Mama wa staa mwenye jina kubwa Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kasimu ‘Sandra’ amedaiwa kufanya kufuru ya aina yake kwa kununua mtaa mzima, Tandale-Uzuri jijini Dar na kuikarabati nyumba yake aliyokuwa akiishi zamani kwa kutumia takriban shilingi 100 Milioni

Chanzo chetu makini ambacho kilifuatilia ishu nzima tangu nyumba hiyo ilipoanza kukarabatiwa, kimesema kwamba kwa kipindi kirefu ‘bi mkubwa’ huyo amekuwa akifika nyumbani hapo asubuhi na kuondoka jioni akisimamia ujenzi sambamba na binti yake, Esma.


 Nyumba hiyo kabla ya kukarabatiwa.


“Mama Diamond noma, kateketeza shilingi milioni 100 na bado nasikia ameshafanya mchakato wa kununua nyumba za jirani ili mtaa mzima uwe wao,” kilisema chanzo chetu.

Chanzo hicho kimezidi kutiririka kuwa mama Diamond anataka kuifanya nyumba hiyo kuwa bora zaidi kwani mbali na kuiboresha, kuna mpango wa kutengenezwa swimming pool (bwana la kuogelea).

 Ikiwa inakarabatiwa


Mara baada ya kupenyezewa ubuyu huo, gazeti hili lilifika kwenye nyumba hiyo na kuzungumza na mama Diamond aliyekuwa bize kusimamia ujenzi.



“Jamani! Taarifa hizi mmezitoa wapi tena? Kweli nimekarabati nyumba yetu iwe bora zaidi. Hayo mambo ya gharama na mipango mingine ni siri labda mje mmuulize Diamond akirudi Marekani lakini ukarabati huu mnaouona ndio nimeusimamia mimi na mwanangu Esma,” alisema mama Diamond.

FREEMAN MBOWE Afunguka Kwa Mara ya Kwanza Kuhusu Ujio wa Lowasa Chadema, Adai Hakulipa Hata Shilingi Moja

$
0
0
Mwenyekiti wa Chadema-Taifa Freeman Mbowe  amesema, Edward Lowassa, aliyekuwa mgombea wa chama hicho kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na kuungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), hakutoa hata senti moja alipojiunga na chama hicho.

Mbowe amezungumza hayo kwenye Mkutano wa Baraza Kuu la Chadema linaloendelea hivi  sasa Jijini Mwanza.

Amesema kuwa, pamoja na kuwepo kwa kauli nyingi kwamba, Lowassa alimwaga pesa kabla ya kujiunga na chama hicho, ukweli unabaki kuwa hakutoa pesa yoyote kama ilivyokuwa ikidaiwa.

“Watoto wangu walikuwa wanakula sana maharage, sasa siku moja wakala nyama, jirani akasema umeona Lowassa kaja Chadema,” amesema Mbowe.

Akizungumzia migogoro ya kichama iliyokuwa imejitokeza kwenye uchaguzi uliopita Oktoba 25 mwaka huu Mbowe amesema, kuna kila sababu kushughulikia migogoro hiyo kwa haraka.

“Migogoro mingi ndani ya Chadema imepelekea kuanguka kwa chama, hivyo itashugulikiwa kwa haraka,” amesema na kuongeza; “Uchaguzi mkuu wa chama ni Oktoba 2018.”

Amewaeleza wajumbe wa mkutano huo kwamba, harakati za kisiasa hasa kukikuza chama ni gharama kubwa, jambo ambalo chama kinajitahidi kukabiliana nalo.

Amesema kwamba, pamoja na mambo yote ndani ya chama hicho lakini suala la rushwa haliwezi kuvumiliwa hata mara moja.

Akifafanua kauli hiyo amesema, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeishi kwa kulea rushwa na kwamba, hali hiyo ndio imekifikisha hapo kilipo sasa.

Amesema, hali hiyo inaelekea kuingia Chadema jambo ambalo linaweza kusababisha kupasuka kwa chama hicho endapo halitashughulikiwa.

“Jambo ambalo hatutalivumilia ndani ya Chadema ni swala la rushwa kwani rushwa inagawa taifa, sasa swala la rushwa lililelewa na CCM na sasa inataka kuingia Chadema,” amesema.

“Kuna majimbo kama Iringa, Rukwa, Arusha Chadema waliachiwa kwa asilimia mia moja na Ukawa lakini kwanini wameshindwa kuchukua ushindi wa kutosha katika majimbo hayo?” amehoji.

Akizungumzia changamoto za Ukawa, Mbowe amekiri kuwepo na kwamba hakuna sababu ya kuzikwepa.

“Changamoto zilizopo ndani ya Ukawa hakuna haja ya kuzikimbia bali ni kupambana nazo,” amesema.

Akizungumzia umoja wa kitaifa amesema kwamba  Chadema hakikubaliani na mtu yoyote anayetaka ama kushabikia kauli za kuligawa taifa.

“Nawashauri tunapokuwa popote lazima tukatae nchi yetu kugawanyika vipande vipande. Hatukotayari kufanya kosa kama hilo wala kushabikia kuligawa taifa ,” amesema.

Mh. Estar Bulaya Achiwa Huru...Kweli Kuwa Mpinzani Inahitaji Moyo...

$
0
0
Mh Estar bulaya mbunge wa bunda akiwa kwenye office ndogo za bunge jiji daresalam baada yakuachiwa huru na mda huu anaelekea airport kwa ajiri ya safari yakwenda mwanza kwenye kikao cha kamati kuu..

Haya Hapa Matokeo ya Mechi ya Yanga na APR ya Rwanda iliyofanyika Jioni ya Leo Huko Rwanda

$
0
0

YANGA SC imejiweka kwenye nafasi nzuri ya kuingia hatua ya mwisho ya mchujo ya Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji APR katika mchezo wa kwanza wa raundi ya Kwanza jioni ya leo Uwanja wa Amahoro, Kigali, Rwanda.
Asante kwa wafungaji wa mabao hayo, beki Juma Abdul Jaffar kipindi cha kwanza na kiungo Thabani Scara Kamusoko kipindi cha pili na Yanga sasa watahitaji hata sare mchezo wa marudiano ili kusonga mbele.

Hizi Hapa ni Tofauti Kati ya Mwanaume na Mvulana Katika Mahusiano ya Kimapenzi....

$
0
0
Hebu tutizame mambo kadhaa yanayomtofautisha mwanamume na mvulana kwa faida ya jamii yetu.

Ushauri kwa wanaume.

Dear men,
1. Kuwa na wanawake wengi hakukufanyi uwe mwanaume halisi, bali inakufanya uwe mvulana na kuna tofauti kubwa kati ya mwanaume na mvulana.

2. Mwanaume halisi anae mwanamke wake mmoja tu katika maisha yake. Hata ikitokea anao wengine ni wake wa ndoa na heshima yake kwa mwanamke wake haitaisha.

3. Kuwa vizuri kitandani hakukufanyi uwe mwanaume halisi. Mwanaume halisi ni yule ambae kamwe hakimbii majukumu yake.

4. Haikuhitaji kuvaa mlegezo na kutembea mabarabarani ukidhani utawavutia wanawake. Ukweli ni kwamba wavulana wadogo ndio huvaa mlegezo na wasichana wadogo wasiojitambua ndio hupenda wavaa milegezo.

5. Usiwatumie wanawake na kuwaacha. Kumbuka sheria ya "karma" what goes around must come back around.

6. Kama hutaki kumfanya awe mkeo, usimpe mimba au usimtongoze kabisa.

7. Usitii kichwa chako kidogo cha huko chini kila muda. Muda mwingi kichwa kidogo hutupeleka katika njia isiyo. Acha kichwa kikubwa kitawale kichwa kidogo.

8. Sio kila kitu unachokiona ndani ya sketi kinafaa kukikomalia ukile, sketi nyingine zimejaa nyoka ambao wanaweza wakakuuma. Jaribu ku control sex desire.

9. Usimtamani mwanamke kwa ajili ya umbo lake, maziwa yake na makalio. Hivyo vitu ni packaging tu na siku zote package huweza kuharibika.

10. Mheshimu mwanamke na kamwe usimpige hata kama ni mke wako.

11. Mwanaume wa kweli kamwe hasengenyi. Kama wewe ni msengenyaji jiweke katika kundi la wavulana.

12. Tumia muda wako mwingi kuhangaika kutafuta pesa. Mwanaume wa kweli na aliyekua kiakili hutumia muda wake mwingi kuplan na kufikiria jinsi ya kufanikiwa kiuchumi. Wanaume wapumbavu hutumia muda wao mwingi kuwaza jinsi ya kulala na wanawake mbalimbali.

13. Siku zote utafurahiwa kama utakuwa una mafanikio kiuchumi. Hakuna hata mtu mmoja atakayesheherekea kwa kuwa unao mademu wengi. Ipi faida umalize nguvu zako kujijenga kiuchumi au umalize protini yako kwa wanawake tofauti tofauti?

Kuwa mwanaume mwenye busara. Ambae ungependa Mwanao wa kiume aje kuwa kama wewe.

Wasalaam mie mkulima wa matikiti.

Wamechanganyikiwa...DALILI Zote za Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kuukosa Umeya wa Jiji la Dar es Salaam

$
0
0
DALILI zote za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuukosa Umeya wa Jiji la Dar es Salaam zimedhihiri na sasa wamechanganyikiwa, anaandika Mwandishi Wetu.

Taarifa kutoka Ofisi ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam zinaeleza kwamba, CCM inaelekea kushindwa kupiga ‘bao la mkono’ kwenye uchaguzi wa Meya wa Jiji hilo kutokana na mazingira kukaa vibaya.
Leo Juma Gaddafi, Katibu wa Siasa na Uenezi wa Mkoa wa Dar es Salaam amekutana na baadhi ya waandishi katika Ofisi ya CCM Mkoa huo huku akionesha hofu ya chama hicho kushindwa kutetea nafasi hiyo.

Taarifa kutoka kwenye kikao hicho zinaeleza kwamba, CCM mpaka sasa imekata tamaa ya umeya kutokana na mazingira magumu yaliyotengenezwa na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Si hivyo tu, katibu huyo ameonesha kuchukizwa na kile alichokieleza udhaifu wa Isaya Mngurumi, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala na Mkurugenzi wa Manspaa ya Kinondoni kwa kushindwa kuhimili wajumbe wa Ukawa kwenye chaguzi za umeya wa wilaya hizo.

“Wakurugenzi hawakuwa majasiri katika kupamba na vitisho vya wajumbe wa Ukawa na kuwa wakweli. Walishindwa kutoa tafsiri sahihi ya wajumbe halali wanaotakiwa kupiga kura katika uchaguzi wa meya wa jiji,” amelalamika Gadafi.

Kwenye mkutano huo Gadafi amedai kwamba wakurugenzi hao walifanya upotoshaji wa tafsiri sahihi kuhusu uwepo wa wajumbe wa CCM walioonekana kutokuwa wajumbe halali.
“CCM imesikitishwa na upotoshaji uliofanywa na wakurugenzi hao hasa kwa kuwavua uhalali wa kupiga kura baadhi ya wajumbe wetu,” amesemea na kuongeza;

“Wakurugenzi wa Manispaa za Ilala na Kinondoni wamekula matapishi yao, haiwezekani uchaguzi wa awali wawakubali wabunge viti maalum kama wajumbe halafu uchaguzi wa jiji waseme hawastahili kupiga kura.”

Gaddafi amedai kwamba, Ukawa ndio walikuwa wa kwanza kuuvuruga uchaguzi huo kwa kuwa walitumia njia ya vitisho na kuwafanya wakurugenzi wafanye maamuzi kulingana na mashinikizo yao.

Amedai kwamba, licha ya CCM kuonekana kuwa chanzo cha kuvuruga uchaguzi huo lakini chama hicho hakina sababu hata moja ya kufanya hivyo isipokuwa ni utaratibu wanaoshinikiza ufuatwe na kuwa wana mgombea bora na anayekubalika.

“Wajumbe wa Ukawa ndiyo walianza kukiuka taratibu za upigaji kura kwa kupiga picha kura walizopiga na kumuonesha mmoja kati ya viongozi wao.

“Uchaguzi hupigwa kwa siri, iweje Ukawa wawalazimishe wajumbe wao kupiga picha kura walizopiga? Ina maana wanaogopa wajumbe wao wasije wakaipigia kura CCM,”amesema.
Jumla ya wajumbe wa mkutano wa kumchagua Meya wa Jiji ni 161. Kwa upande wa Kinondoni kuna wajumbe 58 ambapo CCM wapo 20 na ukawa 38.

Temeke jumla ya wajumbe 49, CCM wapo 31 na ukawa 18 na Ilala jumla ya wajumbe 54 huku CCM wakiwa 23 ukawa 31.

Chanzo: Mwanahalisionline

Je Unajua Kuwa Mchekeshaji Masanja ni Mchungaji wa Kanisa...Hapa Anaelezea Jinsi Alivyoupata Uchungaji Huo......

$
0
0
Mchekeshaji wa kundi la Orijino Komedi, Masanja Mkandamizaji amefunguka na kuzungumzia jinsi alivyoupata uchungaji wake.

Masanja ambae kwa sasa anaendesha huduma ya ‘Street Gospel’, amekiamba kipindi cha Uhondo cha EFM kuwa imani yake ndio imemfanya kuwa mchungaji.

“Uchungaji upo wa aina mbili, kuna wa kuoteshwa na wakusomea. Kwa mfano ukiangalia mapadri wa Roman hakuna Padri aliyeoteshwa, wote wamesomea. Hata mimi sasa hivi nasomea uchungaji, lakini pia mimi nimekuwa nikiishi maisha ambayo yamenipelekea kuwa hivi, Kanisa lilikuwa ni sehemu ya maisha yangu, kabla ya kuokoka na baada ya kuokoka,” alisema Masanja.

Aliongeza, “Hudama yangu ambayo naiendesha sasa hivi ni Street Gospel na kazi yetu sisi ni kuhubiri mitaa ya mungu, kwa hiyo tunahubiri kwenye mitaa ya ulimwengu. Pia tuna kanisa letu linaitwa AGT lipo Kariakioo,”

Bunge Laeleza Sababu za Bulaya Kukamatwa Mwanza Usiku Nakumsafirisha Hadi Dar

$
0
0
Bunge laeleza sababu za Bulaya kukamatwa Mwanza usiku nakumsafirisha hadi Dar


Imetiamia MBOWE Amtangaza Dk. Vicent Machinji Kuwa Ndio Katibu Mkuu Mpya wa Chadema

$
0
0
DAKTARI Vicent Machinji ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kupitishwa na Baraza Kuu la Chadema, katika kikao chake kilichokaa jijini
Katika Kikao hicho cha Baraza Kuu, Freeman Mbowe alitangaza jina la Dk. Machinji na kuungwa mkono na wajumbe wa baraza hilo, hivyo anajaza nafasi iliyoachwa na Dk. Willibrod Slaa, aliyejienguwa ukatibu mkuu wa chama hicho.

Jina la Dk. Machinji halikuwa miongoni mwa wanachama wa Chadema ambao walikuwa wanatarajiwa kumrithi Dk. Slaa kwani waliokuwa wanatabiriwa kukatia kiti hicho ni Salum Ally Mwalimu, Frederick Sumaye, Benson Kigaila, John Mnyika, Dk. Marcus Albanie na Prof. Mwesiga Baregu.

Nafasi ya Katibu wa Chadema ilikuwa wazi tangu Dk. Slaa alipoondoka Chadema muda mfupi baada ya chama hicho kumpitisha Edward Lowassa aliyetokea CCM kuwa mgombea urais wa chama hicho na kuungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili Ya March 13, Ikiwemo ya Lowassa Kujipima na Magufuli....

Tuhuma ya Kugushi Cheti Yamuondoa Kigogo Baraza la Taifa la Elimu ya Vyuo vya Ufundi( NACTE)

$
0
0
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la  Elimu ya Vyuo vya Ufundi( NACTE),Dr. Primus Nkwera amejiuzulu nafasi yake.

Uamuzi wa kujiuzulu  kwa  Dr. Nkwera ulitangazwa katika ofisi  kuu  za Baraza  hilo  zilizopo  Mikocheni  Dar es Salaam juzi na Mwenyekiti  wa  Bodi,Mhandisi Steven Mlote na kusababisha  baadhi  ya  wafanyakazi  kuangua  kilio.

Akizungumza katika kikao cha dharura cha wafanyakazi wote wa baraza hilo,Mlote alisema Dr. Nkwera amejiuzulu  ili  kulinda  hadhi  ya Nacte kutokana  na  habari iliyoandikwa na Gazeti la Dira ikimtuhumu mambo mbalimbali.

Gazeti  hilo la Dira la Jumatatu tarehe 07/03/2016 toleo no.405 lilimtuhumu Katibu Mtendaji wa NACTE, Dr.Primus Nkwera  kughushi vyeti vya shahada ya uzamivu  baada ya kusomeshwa na serikali Afrika Kusini na kufeli.

Mlote alisema kwa mujibu wa Dr. Nkwera, nafasi hiyo haipaswi kushikwa na mtu mwenye tuhuma  ya  aina  yoyote, na ametafakari na kuona ajiweke kando na uongozi wa Nacte ili uchunguzi ufanyike akiwa pembeni.

"Tumetumia muda mwingi kutafakari hoja  ya  Dr. Nkwera na hatimaye tumekubali kujiuzulu kwake kwa shingo upande," alisema Mlote na kuongeza:

"Kazi kubwa iliyofanywa na Dr. Nkwera akiwa kiongozi wa Nacte inafahamika na kila mmoja, vilio na machozi ya wafanyakazi wenzake yanadhihirisha kuwa kujiuzulu kwake kunaacha simanzi kubwa.

"Najua mmepata mshtuko mkubwa, lakini Dr Nkwera hajafa, yuko hai na huyu bado ni mtumishi wa serikali. Alichofanya ni kuamua kuachana na ukatibu utendaji.

"Tutaendelea kumtumia itakapobidi kwa ushauri.Wakati mwingine lazima mkubaliane  na  hali  hii, lakini pia  endeleen kuchapakazi kwa ufanisi kama  kawaida kana kwamba bado mko na Dr. Nkwera."

Kutokana  na  kujiuzulu  kwake, Mlote alisema bodi imemteua Mkurugenzi wa Mitaala wa Nacte, Dr Adolf Rutayunga kukaimu nafasi hiyo  wakati taratibu nyingine zikiendelea.

Akizungumza na wafanyakazi hao, Dr. Rutayunga alisema viatu alivyoviacha Dr. Nkwera ni vikubwa kwake, lakini  akaahidi kuendeleza yote  aliyoyaacha.

Huu Hapa Ndio Wasifu wa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dr.Vincent B. Mashinji

$
0
0
WASIFU WAKE KWA UFUPI.

JINA: Dr.Vincent Mashingi

UMRI: Miaka 43
KABILA: Msukuma

TAALUMA: Daktari bingwa wa binadamu (MMED) na Daktari wa Falsafa (PhD).
ELIMU:

1981 - 1987 Elimu ya Msingi (Shule ya msingi Iligamba)

1988 - 1992 Elimu ya Sekondari (St.Pius seminary)

1992 - 1994 A-Level PCB (Mzumbe High School).

1995 - 2001 Chuo Kikuu cha Makerere (Degree ya Udaktari MD)

2003 - 2005 Chuo Kikuu Kishiriki Muhimbili (Shahada ya pili - udaktari bingwa (MMED Anaesthesiology).

2004 - 2004 Chuo Kikuu Kishiriki Muhimbili (Astashahada ya Utafiti)

2008 - 2010 Evin School of Management (Shahada ya Uzamili (Masters) ya Public Relations (CSR)

2007 - 2010 Blekinge Institute of Technology (Shahada ya pili (Masters) ya Usimamizi wa biashara, MBA)

2010-2010
University of Carlifonia - Anderson School (Stashahada ya Management Development)

2008 - 2008 University of Maryland School of Medicine (Astashahada Human Virology)

2010 - 2016 Chuo Kikuu Huria Tanzania (Shahada ya uzamivu (PHD) ya Uongozi.
UZOEFU WA KITAALUMA,

2001 2002, Daktari wa mazoezi - Intern doctor (Hospitali ya taifa Muhimbili).

2002 - 2003, Mtafiti wa kujitegemea (Freelance Researcher).

2003 - 2005, Daktari (Hospitali ya Taifa Muhimbili)

2005 - 2006, Daktari bingwa (Hospitali ya Regency).

2006 - 2008, Msimamizi wa mradi (Shirika la kimataifa la afya IMA World Health)

2008 - 2016, Mshauri wa tiba (TB and HIV), Shirika la afya la Kimataifa la IMA WorldHealth.

NB:
Msaada kwa wafuasi wa chama chakavu ambao definately watakua wanaona "mapichapicha" kwenye elimu ya Katibu Mkuu mpya wa CHADEMA. Ili kuwasaidia wanaweza kukariri kwamba GS mpya wa CHADEMA ana degree 1, Masters 3, Certificate 2, Diploma 1 na PhD 1.

Dr.Mashingi ndiye Katibu Mkuu wa chama cha siasa msomi kuliko wote duniani. Hapa Mbowe kacheza kama "Messi" na "Ronaldo" kwa wakati mmoja.!

Mwanamuziki JUX Afunguka Jinsi Alivyomshawishi Venessa Mdee Mpaka Kumkubali Kimapenzi..Adai Haikuwa Kazi Raisi

$
0
0
MKALI wa Miondoko ya RnB Bongo, Juma Jux, amesema wakati anaanza kumsarandia kimapenzi staa mwenzake, Vanessa Mdee ‘V Money’ alihangaika sana na haikuwa kazi rahisi.

Jux alisema ili kuhakikisha anamweka mtoto Vanessa kwenye ‘line’, alianza kwa kuomba kidani cha mkononi.

“Siyo mchezo, nilizunguka kweli. Nilianzia kwa kuomba kidani, akawa haelewi somo, nikahangaika kweli lakini mwishoni nilifanikiwa na nipo naye hadi leo,” alisema Jux.

Katibu Mkuu Mpya Chadema Aleta Taharuki Ndani ya CCM...

$
0
0
Chama cha Mapinduzi kilikuwa kimejipanga vyema kabisa na lundo la tuhuma na kashfa mbalimbali kwa watu kadhaa ambao walikuwa katika list yao kuwa watakuwa wateule wa Ukatibu mkuu wa Chadema.

Habari za uhakika zilizopatikana toka ndani ni kuwa kitengo cha propaganda cha ccm kwa muda wa miezi minne kilipewa jukumu la kufanya kazi hiyo ya kutafiti kasoro za mmoja mmoja kwa wale watu sita ambao wao walisema panga pangua lazima awe mmoja wao.

Kasoro na kashfa hizo zilikwishaandaliwa makala kila mtu na yake ikitegemea nani atatangazwa. Project hii iligharimu fedha nyingi zilizotengwa na chama.

Lakini kitendo cha Chadema kuja na jina geni kabisa kwao ni sawa na kupigwa knock out dakika ya kwanza ya round ya kwanza. Hawakutegenea na wamepigwa butwaa.

Wapo viongozi ambao walikuwa na kikao cha siri hotelini maeneo ya Mikocheni wakisubiri jina litajwe walionekana wakitawanyika usiku wakiwa wameinamisha vichwa chini.

Hata kwenye mitandao ya jamii ambako watu walikesha wakisubiri wachangiaji wengi waliokuwa wanasubiri kuiponda Chadema kwa yale majina waliyokuwa nayo wamechanganyikiwa na kumshambulia Dr Vicent bila mpangilio maana hawamjui.

Chadema kumbe inajua kucheza na siasa za CCM kwa nini haikamati dola kwa mbinu hizi? Hilo ni swali katika mada nyingine

Chanzo: Jamii Forums

Donald Trump – WENGER Can Go To Hell, I am Ready to Pay The New Arsenal Coach for 50 Years

$
0
0
US tycoon and GOP presidential aspirant Donald Trump has said that Arsenal manager Arsene Wenger belongs in hell for failing the club and fans.

Trump, the number one Arsenal supporter said Wenger is a disgrace to the club and that he’s bankrupt of ideas needed to take the club forward.

Speaking in North Carolina during the GOP Presidential nomination campaigns, Trump, the Republican front runner said Arsenal fans are tired of Wenger and its time they got someone else to manage the club.

“I am a number one supporter of Arsenal FC and as a real GUNNER, I expect us to humiliate other minor clubs. Arsene Wenger has hurt so many souls worldwide, including myself. This man runs the club like his own property and he does whatever he pleases with it. How could Manchester beat us? As if that is not enough, Swansea hammered us and the best we could do is hit the woodwork three times. Wenger is a clown, a masquerade and an original version of fake” Said Trump.

“Arsenal has become a punching bag for every team. Can you imagine that some teams like Manchester United and Chelsea can beat us home and away?”

“This man Wenger belongs either in hell or in Holywood acting horror movies. As an actor, and given his pathetic old figure, the thriller movies he stars will sell worldwide unlike when he masquerades as a football manager.Arsenal needs to be revamped. If it is money the club lacks, I am ready to pay a new coach for 50 years as long as Wenger goes and leaves Arsenal in peace. If Wenger was to lead the children of Israel to the promised land, they could spend 40 years doing nothing but again end up in Egypt” Added Trump.
Just recently, Trump adviced Man United and Chelsea to form 1 team and beat Arsenalafter Arsenal humiliated Manchester United 3 goals to 0 in the first leg of English Premier League.

Mkuu wa Mkoa Wa Dar es Salaam Ampa ONYO Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniphace Jacob

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki, amemtaka Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniphace Jacob, kuacha malumbano ya kisiasa na badala yake ajikite kufanya kazi.

Onyo hilo Sadiki limekuja baada ya Meya Jacob kukaririwa akisema manispaa hiyo ina uwezo wa kukabiliana na uamuzi wa serikali wa kutoa elimu ya bure bila kuhitaji fedha zinazotolewa na utawala wa Rais John Magufuli.

Halmashauri ya wilaya ya Kinondoni inaongozwa na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambao ni mwamvuli unaojumuisha wabunge na madiwani kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Chama cha Wananchi (CUF).

Sadiki alisema hahitaji malumbano na kiongozi huyo ambayo hayana tija.

"Mimi sipendi malumbano yasiyo na tija baina ya viongozi," alisema Mkuu wa Mkoa na kuongeza; "unapokataa msaada kama huo wa kupunguza mapungufu katika sekta ya elimu, wanaoathirika ni watu waliowachagua."

Serikali imepanga kutumia Sh. Bilioni 137 kugharamia elimu bure katika miezi sita ya kwanza ya Rais wa tano, Magufuli.

Kiasi cha Sh. bilioni 18.77 kilitumwa kwenye akaunti za shule za Msingi na Sekondari za halmashauri zote hapa nchini na vyombo vya usimamizi wa mitihani kwa kila mwezi wa Januari na Februari, kwa ajili ya wanafunzi kusoma bure.

Pesa zilizogawanywa kwenye akaunti za shule za Msingi na Sekondari katika halmashauri zote ni Sh. bilioni 15.7 kila mwezi na Sh. bilioni 3 kila mwezi kwenye akaunti vyombo vya usimamizi wa mitihani katika Halmashauri zote hapa nchini.

Mkuu wa Mkoa alisema fedha hizo zitapelekwa katika Manispaa zote na ametoa agizo kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni kutumia fedha hizo katika matumizi yaliyokusudiwa na si vinginevyo.

Sadiki alisema kwa sababu Rais Magufuli ni kiongozi wa wote, ana haki ya kutoa kwa wote bila kuzuia wala mipango yake kukataliwa.

"Yule ni mkuu wa nchi, hata kama wanakusanya fedha za kutosha, zipo taratibu za matumizi ya fedha hizo," alisema Sadiki.

Kwa mujibu wa Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mipango wakati akitoa taarifa ya kuanza kwa utumaji wa fedha za elimu bure Januari 6, mwaka huu, walimu wakuu wa shule zote za Msingi na Sekondari katika halmashauri zote hapa nchini wanatakiwa kuweka wazi matumizi ya fedha hizo katika mbao za matangazo kwa kila shule, ili kila mzazi aweze kujua kiasi gani kimetumika.

Sadiki alikuwa akizungumza wakati akipokea msaada wa ahadi ya ujenzi wa madarasa 12 katika mkoa wa Dar es Salaam kutoka kwa Wamiliki wa Malori Tanzaznia(Tatoa), yenye thamani ya Sh. milioni 300.

Mkoa wa Dar es Salaam, alisema Sadiki, una upungufu wa vyumba vya madarasa 7,223, lakini pia uhitaji wa madawati 66,000.

"Yapo maeneo mengi ya kujenga shule, nawaomba wadau wetu muendelee kuhamasisha kupata shule nzima kwani shule nzima inahitaji madarasa kuanzia 22," alisema.

Mshindi wa Big Brother Idris Sultan Atuhumiwa Kuvaa Saa Feki na Kuringishia Watu Mtandaoni...

$
0
0
Page maarufu ya Fake Watch Busta kutoka Mtandao wa Instagram imeibuka na tuhuma kuwa mshindi wa Big Brother Africa 2014 amevaa saa feki , mtandao huo ambao kazi yake ni kuweka wazi mastaa wanaovaa saa feki umeandika haya na kuambatanisha picha hiyo hapo juu....
From @fakewatchbusta - Big Brother Africa winner @idrissultan with the worst fake Richard Mille skull i've ever seen  Skull has meth teeth and ate too much  That Hublot is missing some gold paint on the lugs as well
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images