Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live

Taaruki Iliyotokea Bank ya CRDB Mbagala Leo..Baada ya Wateja Kuzaniwa Majambazi Kwa Kukaidi Agizo la Kuacha Kutumia Simu Wakiwa Bank

$
0
0

POLISI wamelazimika kufyatua mabomu ya machozi ili kuwatawanya watu waliojikusanya mbele ya Benki ya CRDB tawi la Mbagala - Rangi Tatu, baada ya mtu mmoja aliyekuwa akiongea na simu ndani ya benki hiyo kukaidi maagizo ya polisi ya kuacha kufanya hivyo mapema leo mchana wa Machi 11, 2016.


Kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo, watu watatu mmoja akiongea na simu na wengine wawili waki-chat ndani ya benki hiyo, waliagizwa na mlinzi wa benki kuacha kufanya hivyo lakini wakakaidi.


Baada ya mlinzi kuona hivyo alitoa taarifa kituo cha polisi Mbagala - Maturubai, na hapo polisi wakiwa ndani ya gari lao maarufu kama defender, waliwasili kwenye eneo hilo na kuamuru watu hao ambao wanaelezwa kuwa wateja, kutoka ndani ya benki hiyo.


Hata hivyo palitokea mabishano baada ya mmoja wao kukaidi amri ya polisi na kuanza kupigana nao.

 

Kuona hivyo watu walianza kujaa na polisi bila kufanya ajizi wakafyatua mabomu ya machozi kutawanya watu na kuwadhibiti 'wateja' hao wabishi na hatimaye kufanikiwa kuondoka nao.


Hali hiyo ilizua tafrani huku watu wakidhani kuwa palikuwepo na tukio la ujambazi, kwani ni mwezi uliopita umbali wa mita chache kutoka kwenye benki hiyo, palitokea tukio baya ya uvamizi wa benki ya Access ambapo watu saba waliauawa, wakiwemo polisi.

Mwanafunzi Auawa Kwa Ugomvi wa Chaja ya Simu....Apigwa na Chuma Kichwani

$
0
0
Watu wawili wamefariki dunia mkoani Dodoma katika matukio mawili tofauti likiwemo la mwanafunzi wa chuo cha serikali za mitaa Hombolo, Basil Msabila (24) kuuawa kwa kupigwa na chuma kichwani na mwenzake aitwaye Charles Makele (19) kwenye ugomvi wa kugombea chaja ya simu.

Akizungumza na waandishi wa habari, kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa amesema kuwa tukio hilo lilitokea Machi 6 mwaka huu katika chuo cha serikali za mitaa kilichopo Hombolo katika Manispaa ya Dodoma.

Amesema uchunguzi wa awali unaonesha kuwa chanzo cha tukio hilo ni ugomvi wa kugombania chaja ya simu ambayo ni mali ya marehemu katika chumba cha bweni ambapo wanaishi wanafunzi wanne.

Katika tukio la pili mtu mmoja mwanaume ambaye hakufahamika jina lake mara moja aliuawa na watu wenye hasira katika eneo la kisasa lililopo katika Manispaa ya Dodoma baada ya kukutwa akivunja dirisha la mtu.

Aidha ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Dodoma kutojichukulia sheria mkononi na kutofanya mauaji ya kikatili dhidi ya watu kwa tuhuma nyepesi kwa kisingizio cha watu wenye hasira kali

WAZIRI Mkuu Majaliwa Afurahishwa na Ushindi wa Lulu Michael na Richie Tuzo za Filamu...Akutana nao Kuwapongeza

$
0
0
Party bado inaendelea. Washindi wa tuzo za AMVCA, Elizabeth ‘Lulu’ Michael na Single ‘Richie’ Mtambalike wamekutana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Ijumaa hii jijini Dar es Salaam.

Wawili hao walishinda tuzo hizo Jumamosi iliyopita jijini Lagos Nigeria. Lulu alishinda kipengele cha filamu bora ya Afrika Mashariki huku Richie akishinda tuzo ya filamu bora ya Kiswahili.

Lulu ameshare picha Instagram na kuandika: Mapema Leo Na Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa..! ”

Hii imekuwa ni wiki ya sherehe kwa washindi hao.

JUMA Jux Afunguka Kuhusu Aliyekuwa Mpenzi wake Jack Cliff Kujihusisha na Madawa ya Kulevya..Adai Hakujua

$
0
0
Mwimbaji wa Juma Jux Amefunguka kuhusu aliyekuwa mpenzi wake mrembo Jack Cliff kujihusisha na madawa ya kulevya mpaka akajikuta anakamatwa huko Macau China, Jux Amesema kipindi chote alichokuwa naye hakuwahi kujua wala kuhisi kuwa mpenzi wake huyo anabeba madawa ya kulevya...

“Lakini huwezi amini sikuwahi kutambua kama Jackie Cliff anafanya mambo hayo mpaka alipopata matatizo hayo ndiyo najua mimi, hivyo ilinipa wakati mgumu sana mimi kiasi kwamba nilikuwa sijielewi,” aliongeza.

Wimbo wa Nay wa Mitego Shika Adabu Yako Wavuka Mipaka...Mwanamuziki Amani wa Kenya Adai Anaupenda Sana..Asema Haya

$
0
0
Shika Adabu Yako ya Nay wa Mitego inaweza ikawa imefungiwa na BASATA, lakini imefanikiwa kuwafikia watu wengi ndani na nje, shukrani kwa mitandao ya kijamii.


Na sasa muimbaji wa Kenya, Amani, amedai kuwa yeye ni shabiki mkubwa wa wimbo huo.

“Naipenda sana,” alisema Amani kwenye kipindi cha Mseto cha Radio Citizen.

Amesema mstari uliomchekesha zaidi ni ule wa Ommy Dimpoz japo alisema staa huyo wa ‘Wanjera’ achukulie poa tu aliyoambiwa.

Amani anadai mstari mwingine anaoupenda ni ule Nay anasema wasichana wa mjini siku hizi hawavai nguo za ndani.

Mtazame mrembo huyo akiungolea wimbo huo.

ALI KIBA na Sauti Soul Wanakuletea Video Mpya ya Wimbo Walioshirikiana Unaitwa Unconditionally Bae...Ali Kiba Kafunika Balaaa

$
0
0
Mabibi na mabwana Sauti sol kutoka  Kenya wametuletea video ya wimbo wa Unconditionally bae waliyomshirikisha Alikiba kutokea Tanzania

Unaweza ukaitama hapa chini nimekuwekea mtu wangu wa nguvu

LADIES: Hizi ni Dalili 11 Mpenzi Wako Anataka Akufanye Uwe Mke Wake...Soma Hapa

$
0
0
Ukiotea story kwenye vikao vya wanawake, utasikia wakisema wanaume wanaooa siku hizi wamekuwa wachache. Kwamba wengi tunapenda kuwachezea tu. Lakini wapo wanaume ambao wanataka kutulia na mwanamke mmoja na kumfanya awe mke wake. Sasa utajuaje kuwa boyfriend wako anakupenda kiasi cha kutaka uwe mke wake?

1. Huweka mipango ya baadaye

Anapoanza kuzungumza mipango yake ya baadaye, ni ishara kuwa angependa ajue mtazamo wako na mtazamo wako una uzito kwake.

2. Unaalikwa kwenye kila tukio

Unakuwa mtu wa pili kwenye kila matukio muhimu. Hii inamaanisha kuwa anakuona una umuhimu kwenye maisha yake. Anataka kukutambulisha kwa familia yake na kukufanya ujisikie kuwa na wewe ni sehemu yake.

3. Yuko Makini

Kama mpenzi wako anazingatia muda, ni lazima anakukubali sana. Pindi mwanaume anapokuwa kwenye uhusiano serious, atahakikisha kuwa mwanamke wake hamsubiri. Atahakikisha unajua kama atachelewa na hatokuchomesha mahindi.

4. Kuna ongezeko la ukaribu

Itaonekana kama mlipoanza kuwa pamoja. Mwanaume wako atakuwa karibu zaidi, kukushika mkono wakati unapika au kutumia muda kukufanyia massage wakati ukifanya kazi.

5. Anakumisi

6. Anakuona wewe pekee

Hawezi kukufanya ujisikie wivu kwa kuonesha kutamani wasichana wengine hata kama mkiwa sehemu yenye watu wengi

7. Anataka muishi pamoja

8. Hufunguka mambo mengi kwako

9. Hakimbii unapokuwa kwenye wakati mgumu

10. Hakuchoki

11. Anasema kuwa anataka kukuoa

Maneno Haya ya LULU MICHAEL Yamewagusa Wengi Sana....'Usishindane na Mtu Shindana na Wewe Uliyekuwa Jana Usiwe Leo'

$
0
0
Siku utakayojua kusudi La wewe kuwepo duniani pengine ndo siku utakayojua umepoteza muda kiasi gani kufatilia mambo ya wengine,kujilinganisha na wengine,au kufanya mambo yasiyo na faida ktk maisha yako,Hakuna aliyekuja duniani kwa bahati mbaya ipo sababu ya uwepo wako…fanya jitihada za kujua hyo sababu…ukishajua Tu utakuwa busy sana kuhakikisha unafikia malengo uliyokusudiwa automatically utajikuta unakuwa busy na mambo yako wala Huna muda na watu,utajikuta huyumbishwi na maneno wala mazingira magumu Yoyote….usipojua kusudi la wewe kuishi utajikuta una spend asilimia kubwa ya maisha yako katika maisha ya wengine😉wakati unaowafatilia wanafika kwenye malengo Yao ww Bdo umekwama tu..!
Mabadiliko hayana Muda maalum…Mabadiliko yanahitaji Utayari wako Tu..!
Tulale Salama…!
#RuleNumber1(YOU VS YOU)usishindane na mtu shindana na wewe uliyekuwa jana usiwe leo😊

Elizabeth Michael ‘Lulu’  @ elizabethmichaelofficial on instagram

Mwimbaji CHRIS BROWN Avurugwa...Amtukana Matusi ya Kila Aina Donald Trump Mgombea wa Urais Marekani..

$
0
0
Mgombea huyo ambaye amekuwa akiibuka kidedea kwenye kura nyingi za maoni za chama chake, Republican anachukiwa na jamii ya watu weusi na latino nchini humo kutokana na sera zake za kibaguzi.

Kupitia Instagram, Chris ameandika:

F*CK TRUMP AND F*CK THE PIGSpigpigpigpig! TO SEE THIS EVIL SHIT IS SO WRONG! GOD WILL HAVE HIS REVENGE! TRUST ME! WITHOUT OUR BLACK CULTURE, ASIAN CULTURE, LATIN CULTURE, MUSLIMS, AND ANY RACE THAT YOU DONT APPROVE OF HELP YOU TO BE WHO THE F*CK YOU ARE. NOT TO MENTION WE ARE THE MOST CREATIVE,OPPRESSED, resilient, And HARD WORKERS, without out us your just another simple minded scared little man. WHEN MAKE FASHION, WE MAKE WHITE ARTIST WANNA BE US, White girls singing R&B OLD VIBE SONGS and its the best thing since sliced bread? BRANDY AND BEYONCE SING CIRCLES AROUND YALL CLONES! until the poeple in these power positions start showing humility and a actual love for everyone in AMERICA and the whole world. Ain’t nobody stupid my nigga. People are so afraid to say shit because y’all just find a way to kill our leaders!!!! WHO THE F*CK U THINK CLEANS YOUR HOTELS AND WORKS HARD TO FEED A WHOLE FAMILY. US”! YOU A BITCH,, ALWAYS BEEN A P*SSY! I ain’t running for no political offices nor don’t I want to be apart of the devision of (Devil)race. FIRST THING YALL do IS BRING GOD IN it. DONT PLAY WITH POWERS U don’t understand. Ok… Ok…ok… ALL JOKES ASIDE,……F*CK TRUMP! #FU*CKTRUMP

Kim Kardashian Shares New Adorable Photo of Saint West......

$
0
0
Kim Kardashian just shared this beautiful photo of her son, Saint West and captioned it: "You're the sun in my morning babe"

TIMU ya Newcastle Yamtangaza Huyu Kuwa Kocha Mpya Baada ya Kumtimua Steve McClaren

$
0
0
Rafael Benitez ameteuliwa kuwa kocha mpya wa klabu ya Newcastle kufuatia kufutwa kwa aliyekuwa kocha wa kilabu hiyo Steve McClaren.

Benitez amewahi kuzinfundisha timu za Liverpool,Chelsea,Real Madrid,Intermilan na Valencia anaichukua timu hiyo ikiwa imesalia pointi moja kushushwa katika jedwali la ligi ya Uingereza huku kukiwa kumebakia mechi kumi pekee.
Benitez ametia saini kandarasi ya miaka mitatu na kuwaleta makocha Fabio Pecchia,Francisco de Miguel Moreno na Antonio Gomez Perez.

JOYCE KIRIA Amchimba Mkwara Mume Wake...Atishia Kumpiga Chini Asipofanya Haya

$
0
0
Mtangazaji wa Kipindi cha ‘Wanawake Live’ kinachorushwa kupitia Televisheni ya East Africa, Joyce Kiria amefunguka kuwa hata kama mumewe wa ndoa hatakuwa mchapakazi atampiga chini na kuendelea na maisha mengine.

Akizungumza na mwandishi wa habari, Joyce, ambaye leo anazindua rasmi kampeni yake ya ‘Mwanamke Piga Kazi’ inayofanyika katika Viwanja vya Leaders jijini Dar, alisema kuwa kwa kipindi ambacho tupo nacho sasa hivi lazima kupiga kazi.

“Kwangu, hata kama mume naye atakuwa mzembe wa kupiga kazi nampiga chini kabisa maana sasa hivi tunakimbizana na kazi ya kupiga kazi kwa nguvu ili tuwezeshe kusonga mbele zaidi,”  alisema Joyce.

Pia mtangazaji huyo aliongeza kuwa anawaomba wanawake wengi wajitokeze kwani hakutakuwa na kiingilio chochote, lengo ni kuja kujifunza mbinu za kujikomboa kama wanawake na kujiamini katika kufanya kazi.

Katibu Mkuu Mpya CHADEMA Huyu Hapa!

$
0
0
Wananchi hapa wanasubiri ujio mkuu leo.Ujio wa Katibu mkuu wa Chama chenye ufusi mkubwa nchini cha Chadema.

Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Freeman Mbowe ndiye atakayesimama leo mbele ya Baraza Kuu kutegua kitendawili kinachosubiriwa kuteguliwa na mamilioni ya wafuasi ndani na nje ya nchi.

Tayari majina kadhaa yasiyopungua kumi yamekuwa yakibashiriwa kwamba moja kati ya hilo ndilo litakalopita katikati ya moshi mweupe pale kwenye ukumbi wa Gold Crest.

Hekima na busara nyingi za Freeman Mbowe zimesababisha mpaka leo jina hilo kuwa siri kuu.Hata hivyo uchunguzi wa kuaminika kutoka kwa watu wa karibu na washauri wakuu wa Freeman Mbowe unasema Katibu mkuu mpya atakuwa ni mpenda chama na wananchi,kiongozi asiyeyumbishwa,mtetezi wa Katiba ya chama na jasiri asiyeyumbishwa atakayekuwa na uwezo wa kutamka jambo na nchi inasimama.

Waandishi wa habari wa ndani na nje ya nchi wamefurika kwenye viunga vya ukumbi huu kujiandaa kuwa wa mwanzo kurusha jina la Katibu mkuu mara litakapotangazwa.

Tunatarajia kabla siku ya leo kuisha tuwawekee hapa jina la Katibu Mkuu mpya Chadema mara baada ya Moshi mweupe kuonekana.

Kinachomsumbua Rais Mh. John Pombe Magufuli ni Mikataba Mibovu iliyoikuta...Je Tuko Tayari Kumsaidia?

$
0
0
Msaidie Rais wako atawale.

Wengi waweanza kuhoji Mh. huyu aliahidi hiki na kile katika kampeni mbona bado hajatekeleza?

Kwenye vyanzo vya mapato Bandalini,kodi za wafanyabiashara wakubwa na wadogo anazikusanya ila kwenye vyanzo vingine kama kwenye migodi ya madini na viwandani amekuta ni madudu
Amekuta serikali imeingia kwenye mikataba mibovu ya kinyonyaji. Ninavyosema mikataba mibovu ni mibovu kwelikweli, mtakumbuka zile miswada iliyokuwa inapitishwa chapu chapu usiku wa manane na wabunge 33? Miswada hii imezarisha sharia mbovu kweli kweli. Mikataba hiyo mibovu inaleta madhara kwa nchi nzima navyosema nchi nina maana watu wake na siyo ardhi kwani ardhi haina uhai.

Kila Mh. Rais anavyochungulia kwenye vyanzo vya mapato makubwa kama ya kwenye migodi ya madini na gesi asilia anakuta kuna mkataba mbovu.

Afanyeje sasa?

Kwa wale wapenzi wa Simba Sports Club nitawakumbusha club chenu kilishiriki mashindano ya club bingwa Africa mwaka 1974, waliwatoa Linale ya Lethoto, wakawatoa Mufurila wanderlers ya Zambia, wakapangiwa Heaths of Oak ya Ghana. Mchezo wa kwanza walichezea Ghana pamoja na kushinda 2- 1 kulikuwa na mchezaji mmoja anaitwa Mohamed Pollo alikuwa anasumbua sana, kidogo tu kesha fika kwa Mambosasa golikipa, kidogo tu kawapita mabeki wote kafika kwa kipa Mambosasa na alikuwa anafanikiwa kuokoa hatari hizo.

Mwishowe Mambosasa akachoka akawabwatukia mabeki wake kwa nini wanamwachia winga Mohamed Pollo kila saa anasumbua? Wanafanya kazi gani? Beki wa kati merehemu Omary Cogo Mruya akamwuliza kipa Mambosasa ambaye naye ni marehemu " unaweza kudaka penati? Kipa Mambosasa akasema sawaaa kuliko mnamwachia tu Pollo anatamba.

Basi mpira uliofuata Mohamed Polo akapangua ngome kama kawaida yake kufika kwa Chogo akamkata kiroho mbaya ikawa penati, Chogo akamwambia Mambosasa haya penati hiyo. Mungu siyo Athuman penati kupigwa Mambosasa akaipangua na kwa rafu ile Mohamed Polo akawa amadhibitiwa.

Turudi kwenye mada Mh. Rais Kakuta mamikataba mabovu ya kinyonyaji kwenye vyanzo vya uhakika vya mapato hasa kwenye migodi ya madini,sasa je! aivunje ? Wanasheria mko teyari kusimama kwenye mahakama za duniani kutetea? WANASHERIA MKO TAYARI KUMSAIDIA RAIS ATAWALE?
WEEKEND NJEMA.

By Ebaeban

Baada ya Esther Bulaya Kukamatwa Mwanza..Kamanda wa Polisi Adai Hati ya Kukamatwa Imetoka Ofisi ya Bunge na Anatakiwa Kusafirishwa Kwenda Dar es Salaam

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Bunda,Ester Bulaya amekamatwa na Jeshi la Polisi  jijini Mwanza na kulazimika  kulala  rumande baada ya kunyimwa dhamana.

Polisi walivamia Hoteli aliyofikia mbunge huyo na kumkamata majira ya saa 7 usiku na kisha  kumpeleka  kituo cha kati cha Jijini Mwanza akiwa ameambatana na Mhe. Halima Mdee (Mb) , Joyce Sokombe (Mb) pamoja na Wakili John Malya.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Justus Kamugisha amesema  hati ya kukamatwa kwake imetoka ofisi ya Bunge na kwamba Mbunge huyo anashikiliwa kama mtuhumiwa ambaye anatakiwa kusafirishwa kwenda Dar es Salaam.

Wabunge hawa pamoja  na  uongozi  wa  juu  wa  CHADEMA  Wako  jijini  Mwanza  kwa  ajili  ya  kikao  cha Baraza  Kuu  la  chama  hicho kinachofanyika leo katika Hotel ya Gold Crest

CCM Yawatupia Lawama Wakurugenzi Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar ......Yadai Wanawahujumu ili UKAWA Washinde

$
0
0
Wakati waziri wa nchi ofisi ya Rais, Tamisemi na utawala bora George Simbachawene akitoa muda wa uchaguzi wa mameya kukamilika ifikapo machi 25 mwaka huu,Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Juma Simba “Gadafi” amemuomba Waziri  huyo kuangalia upya  utendaji kazi wa wakurugenzi wa Manispaa za Ilala na Kinondoni, akidai wamevuruga uchaguzi wa meya na naibu wake.

Akizungumza na wanahabari jana, Simba alisema CCM imefikia hatua hiyo baada ya kutoridhishwa na utendaji kazi wa wakurugenzi hao, ikiwamo kushindwa kutafsiri vyema vifungu vya sheria vilivyosababisha kuondolewa kwa majina ya wajumbe wao kwa madai kuwa hawana sifa za kushiriki uchaguzi huo.

“Wakurugenzi hawakuwa majasiri katika kupambana na vitisho vya wajumbe wa Ukawa na kuwa wakweli. Walishindwa kutoa tafsiri sahihi ya wajumbe halali wanaotakiwa kupiga kura katika uchaguzi wa meya wa jiji,” alilalamika Gadafi.

Kwenye mkutano huo Gadafi alidai kwamba wakurugenzi hao walifanya upotoshaji wa tafsiri sahihi kuhusu uwepo wa wajumbe wa CCM walioonekana kutokuwa wajumbe halali.

“CCM imesikitishwa na upotoshaji uliofanywa na wakurugenzi hao hasa kwa kuwavua uhalali wa kupiga kura baadhi ya wajumbe wetu,” alisemea na kuongeza;

“Wakurugenzi wa Manispaa za Ilala na Kinondoni wamekula matapishi yao, haiwezekani uchaguzi wa awali wawakubali wabunge viti maalum kama wajumbe halafu uchaguzi wa jiji waseme hawastahili kupiga kura.”

Gaddafi alidai kwamba, Ukawa ndio walikuwa wa kwanza kuuvuruga uchaguzi huo kwa kuwa walitumia njia ya vitisho na kuwafanya wakurugenzi wafanye maamuzi kulingana na mashinikizo yao.

Alidai kwamba, licha ya CCM kuonekana kuwa chanzo cha kuvuruga uchaguzi huo lakini chama hicho hakina sababu hata moja ya kufanya hivyo isipokuwa ni utaratibu wanaoshinikiza ufuatwe na kuwa wana mgombea bora na anayekubalika.

“Wajumbe wa Ukawa ndiyo walianza kukiuka taratibu za upigaji kura kwa kupiga picha kura walizopiga na kumuonesha mmoja kati ya viongozi wao.

“Uchaguzi hupigwa kwa siri, iweje Ukawa wawalazimishe wajumbe wao kupiga picha kura walizopiga? Ina maana wanaogopa wajumbe wao wasije wakaipigia kura CCM,”alisema.

Gavana wa Benki Kuu Tanzania, Beno Ndulu Usiwe Mbishi..'Gavana Ambaye Hajui Idadi ya Wafanyakazi Wake Anawezaje Kujua Usalama wa Hazina Yetu?'

$
0
0
Gavana Ndullu aliingia ofisini mwaka 2008 akichukua nafasi ya Balali wakati huo Us$1 ilikuwa sawa na tshs 1100/= leo hii us$ 1 ni sawa na tshs 2182/= na haonyeshi kuwa anazo mbinu mpya za kusimamia soko letu la fedha. Wakati akikabidhiwa ofisi ya umma riba za mabenki zikiwa 8% hadi 12% leo hii riba za mabenki ziko 25% hadi54% na haoni haja ya kuingilia kati yeye kwake sawa tu. Hapana hatuwezi kwenda kwa mtindo huo.

Leo anaambiwa ahakiki invoice aone kama ziko sawa anaonekana kusitasita, inamaana anajua madudu yapo ila hataki kuwa mhanga wa hayo madudu kama alivyo hepa yale madudu ya escrow.

Ukweli uchumi wetu hauwezi kuimarika kama tunae Gavana asiyekuwa na weledi wa kusimamia hazina yetu. Gavana ambaye hajui idadi ya wafanyakazi wake anawezaje kujua usalama wa hazina yetu? Mbele ya media wenzie walikiri wapo watumishi kanyaboya halafu yeye anasema tumwambie ni nani kweli?

Chanzo:Eddy/Jamii Forums

Lulu Michael Afungukia Madai ya Kutoka Kimapenzi na Dj Majay....Adai "Mchumba Hatangazwi, Ndoa Ndiyo Inatangazwa,"

$
0
0
Mshindi wa tuzo ya AMVCA 2016, Elizabeth ‘Lulu’ Michael amefunguka na kuelezea mahusiano yake na CEO wa EFM, Dj Majay baada ya hivi karibuni kuonekana kuwa karibu zaidi.

Akizungumza katika kipindi cha Friday Night Live cha East Africa Television Ijumaa hii, Lulu alisema kama ni kweli yupo kwenye mahusiano ya kimapenzi na Majay basi mashabiki wake watasikia taarifa za ndoa.

“Ninaweza nikasema ndio wakati sio kweli na ninaweza kusema hapana wakati ni kweli, lakini kikubwa zaidi kimaadili ya kitanzania, kimaadili niliyofundishwa mimi, mchumba hatangazwi, ndoa ndiyo inatangazwa,” alisema Lulu.

Aliongeza, “Kama ni kweli ndoa itakuja na watu wataona, lakini siwezi kutangaza wakati bado hatuna mikakati ya ndani zaidi.”

Kiba Amlipua Jokate...Adai Hakuwa na Mpango wa Kudumu Naye Kimapenzi....

$
0
0
Staa anayesumbua na wimbo wa Lupela, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ amedaiwa kumlipua Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ kwa kusema hakuwahi kuwa na mpango wa kudumu naye penzini, Risasi Jumamosi linakupa ubuyu kamili.

Hivi karibuni, Jokate alizungumza na wanahabari wa Global Publishers na kudai amemchoka mpenzi wake huyo hivyo ameamua kumuacha rasmi Kiba ambapo habari hiyo ilichapwa jana kwenye Gazeti la Ijumaa.

Chanzo kilicho karibu na Kiba kimeweka bayana kuwa mkali huyo hakuwa na mpango na penzi la Jokate lakini alilazimika kuwa naye karibu kwa shughuli za kikazi (muziki).

“Tunamshangaa Jokate kusema eti amemchoka Kiba leo wakati anajua kitambo tu Kiba hakuwa na mpango naye. Kiba alilazimika ‘ku-fake’ penzi kwa sababu walikuwa wanafanya kazi za pamoja, hakuwa na jinsi.

“Jokate mwenyewe anajua kwamba Kiba hakuwa na mpango naye. Nafikiri kajitokeza kwenye ‘media’ ili aonekane yeye ndiyo kamuacha Kiba kumbe mwenzake hata hakuwa na mpango wa kuwa naye,” kilisema chanzo hicho.
Gazeti hili lilimtafuta Kiba katika simu yake ambapo alidai hapendi sana kuanika mambo yake binafsi kwenye vyombo vya habari lakini mmoja wa mameneja wake aliyeomba hifadhi ya jina, alifafanua suala hilo.

“Kiba hakuwa na mpango na Jokate na ndiyo maana kila siku tunapokuwa kwenye kazi zetu hapendi umtajie ishu za Jokate hata kidogo na alikuwa akisisitiza kweli lakini sisi tulikuwa tunalazimisha waendelee kwa sababu tulikuwa tunafanya kazi za pamoja,” alisema meneja

Chanzo:Global Publishers

Gavana BOT Afunguka Kuhusu Watoto wa Vigogo Walioajiriwa Bank Kuu...Adai Hakuna Jipya Kama Wanasifa Kwanini Wasiajiriwe?

$
0
0
Hatimaye Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Prof. Benno Ndulu amefunguka kuhusu hatma ya watoto 14 wa vigogo wanaodaiwa kuajiriwa kwa kubebwa katika taasisi hiyo nyeti kwa mustakabali wa taifa kiuchumi.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Prof. Ndulu alisema orodha hiyo, ambayo mwandishi alimsomea kuanzia mwanzo hadi mwisho, haina jipya.

Prof. Ndulu alisema hakuna ubaya wowote kwa mtu mwenye sifa kuajiriwa na BoT, bila kujali jina lake.
Kuanzia juzi na jana, orodha ya majina ya watu 14 wanaotajwa kuwa ni watoto wa vigogo waliopo BoT ilikuwa ikisambazwa kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii.

Mjadala katika mitandao hiyo ilikuwa huenda wapo watakaoguswa katika kutekeleza agizo la Rais John Magufuli aliyeitaka BOT kupunguza wafanyakazi wake wasiokuwa na shughuli muhimu za kufanya kutoka jumla ya wafanyakazi 1,391.

Rais Magufuli alitoa agizo hilo juzi baada ya kufanya ziara ya ghafla kwenye benki hiyo na kutoa maelekezo kadhaa kwa uongozi wa juu, akiwamo Gavana Prof. Ndulu.

Majina ya watoto hao wa vigogo ambayo yamesambaa kwenye baadhi ya mitandao, yameendelea kuibua maswali mengi kuhusu hatma yao BoT.

Wengi wa wachangiaji wanadai kilichowapatia ajira ni ushawishi wa majina makubwa ya wazazi wao katika medani za uongozi nchini na siyo sifa za kuajiriwa kwenye taasisi hiyo.

Alipoulizwa suala hilo jana, Prof. Ndulu hakutaka kuzungumzia kwa kina, lakini alisema majina hayo siyo mapya na kwamba yalishaandikwa na kujadiliwa mara nyingi hapo kabla.

“Hayo majina kwani kwako wewe ni mapya? Mbona yameshaandikwa na kujadiliwa sana hayo… mimi nasema hakuna jipya hapo,” alisema Prof. Ndulu na kuongeza:

“Hivi ukiwa na jina kubwa halafu ukiwa na akili ama sifa za kufanya kazi fulani, unataka kuniambia usipewe hiyo kazi kwa sababu una jina kubwa?”

Kwa kauli, ni dhahiri tafsiri Prof. Ndulu ana maana kwamba watu hao wenye majina makubwa walipata kazi kwa sifa zao na siyo majina ya wazazi wao kama inavyovumishwa kwenye kurasa za mitandao mbalimbali ya kijamii.

ORODHA YENYEWE
Orodha ya watu wanaodaiwa kuwa ni ya watoto wa vigogo, na ambayo Prof. Ndulu alisema siyo mpya kwani ilishaandikwa na kujadiliwa sana hapo kabla ni pamoja na Pamela Lowasa, anayedaiwa kuwa ni mtoto wa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowasa.

Wegine ni Filbert Sumaye anayedaiwa kuwa ni mtoto wa Waziri Mkuu mstaafu katika serikali ya awamu ya tatu, Fredrick Sumaye na Zaria Kawawa, anayedaiwa ni mtoto wa aliyewahi kuwa Waziri Mkuu katika serikali ya awamu ya kwanza, Marehemu Rashid Mfaume Kawawa.

Mwingine ni Harriet Lumbanga anayedaiwa ni mtoto wa aliyewahi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi wakati wa utawala wa serikali ya awamu ya tatu, Marten Lumbanga.

Aidha, orodha hiyo pia ina jina la Salama Ali Hassan Mwinyi anayedaiwa ni mtoto wa aliyekuwa Rais wa awamu ya pili, Alhaji Hassan Mwinyi; Rachel Muganda anayedaiwa ni mtoto wa aliyekuwa Balozi katika serikali ya awamu ya nne, Alexender Muganda.

Salma Omar Mahita, katika orodha hiyo anadaiwa kuwa ni mtoto wa aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi wakati wa utawala wa awamu ya tatu, IGP mstaafu Omar Mahita.

Wengine ni Justina Joseph Mungai anayedaiwa kuwa ni mtoto wa aliyewahi kuwa Waziri wa Elimu na Utamaduni katika serikali ya awamu ya tatu, Joseph Mungai.

Pia yumo Keneth Nchimbi anayehusishwa na kada wa CCM aliyewahi kuwa kigogo wa Jeshi la Polisi John Nchimbi.

Blasia William Mkapa, anadaiwa kuwa ni mtoto wa Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkpa katika orodha hiyo yenyep ia jina la Violet Phillemon Luhanjo, ambaye anadaiwa kuwa mtoto wa aliyewahi kuwa Katibu Mkuu kiongozi wakati wa serikali ya awamu ya tatu na nne, Phillemon Luhanjo.

Liku Kamba anadaiwa kuwa mtoto wa aliyekuwa kada wa CCM wa muda mrefu, Kate Kamba.

Wengine wanaotajwa katika orodha hiyo ni Thomas Mongela anayedaiwa kuwa mtoto wa kada mashuhuri ndani ya CCM; aliyewahi kushika nyadhifa mbalimbali zikiwamo za ubunge, Getrude Mongela.

Jina la Jabir Abdalah Kigoda linadaiwa kuwa ni mtoto wa aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara katika serikali ya awamu ya nne, marehemu Abdalah Kigoda.

KUPUNGUZA WAFANYAKAZI 
Juzi, miongoni mwa maagizo aliyoyatoa Rais Magufuli wakati wa ziara yake ya kushtukiza, ni pamoja na kumtaka Gavana Ndulu kupitia upya orodha ya wafanyakazi wa benki hiyo na kuwaondoa ambao hawana ulazima wa kuwapo.

Rais alielezea kushangazwa kwake na kitendo cha BoT kuwa na wafanyakazi wanaofikia 1,391.

Alipoulizwa kuhusu kupunguza wafanyakazi BoT kama ilivyoagizwa na Rais Magufuli, Prof. Ndulu alisema hayo yatafanyika baada ya vikao vya ndani na kwamba baada ya hapo, Benki Kuu itatolewa taarifa rasmi ya matokeo ya maagizo ya Rais.

Prof. Ndulu alisema si vyema, na wala haamini kuwa ni busara kuzungumzia masuala yanayowahusu wafanyakazi wa BoT kwa vyombo vya habari na badala yake, masuala hayo yatazungumzwa kwenye vikao vya ndani vya menejimenti ya benki hiyo.

“Haya ya kuwaondoa baadhi ya wafanyakazi tutayazungumza kwenye vikao vya ndani kisha tutaandaa na kutoa tamko," alisema Prof. Ndulu.

"Mambo haya si ya kuyazungumza kwenye vyombo vya habari, hata wewe masuala ya wafanyakazi wenu hamyaweki magazetini holela holela tu.

"Nomba niachieni nafasi jamani.”
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live




Latest Images