Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

HII NDIO SABABU KWANINI VENESSA MDEE HATAONEKANA KWENYE SHOW MPYA YA TV1

$
0
0
Kuna taarifa zilianza kupatikana kupitia vyanzo mbalimbali vya habari kwamba msanii ambae pia ni mtangazaji wa 102.5 Choice FM Dar es salaam Vanessa Mdee ataonekana kwenye show mpya katika kituo cha Television cha TV1.
V money anapenda kukufahamisha kwamba hatoonekana kwenye show hiyo, yani hajaichukua hiyo kazi kutokana na ratiba yake (V) kumbana kutokana na mipango yake ya sasa pia ya kusafiri kuendeleza muziki wake.
Imekua ngumu kwa sasa sababu ameamua kufocus zaidi kwenye muziki hivyo atashindwa pia kuhimili kuifanya hiyo kazi ambayo pia inaratiba kubwa ya shooting.

YALE MABILIONI YALIYOFICHWA USWISS YAANZA KUCHOTWA KIMYA KIMYA

$
0
0
Dar es Salaam. Mabilioni ya shilingi yaliyowekwa na Watanzania katika benki za Uswisi yameanza kuhamishwa kimyakimya.

Ripoti ya Benki za Uswisi ya 2012 inaonyesha kuwa fedha zinazotoka Tanzania zimepungua kwa karibu Sh.36.4 bilioni ikilinganishwa na zilizokuwapo 2011 nchini humo, lakini haielezi sababu ya kupungua kwake.

Taarifa za kuhamishwa kimyakimya kwa fedha hizo ambazo zinaaminika kuwekwa na Watanzania waliowahi kuwa katika utumishi wa umma, imekuja wakati ambao Serikali inasubiriwa kutoa taarifa yake kuhusu vigogo walioficha fedha nchini humo, ambazo zinaaminika walizipata kwa njia zisizo halali.

Awali, kiasi cha fedha kilichotajwa kufichwa katika benki hizo ni Sh.327.9 bilioni (Dola za Marekani 204.96 milioni), lakini taarifa mpya ya 2012 inaonyesha kuwa kiasi hicho kimepungua hadi Dola za Marekani 182.2 milioni (Sh.291.5 bilioni).

Kiasi hicho cha fedha kinaweza kujenga barabara ya lami yenye urefu wa kilomita 300 ambao ni sawa na kutoka Morogoro hadi Iringa.

Akizungumzia ripoti hiyo, Balozi wa Uswisi nchini, Olivier Chave alisema: “Hadi mwisho wa 2012, fedha zilizopo kutoka Tanzania zimebaki Faranga za Uswisi 160 milioni (Dola za Marekani 182.2 milioni) na siyo zile za awali ambazo ni Faranga za Uswisi 180 milioni (Dola za Marekani 327.9 milioni)……. hivyo ndiyo kusema kuwa fedha hizo zinapungua,” alisema Chave na kuongeza:

“Inawezekana ni kutokana na kelele za vyombo vya habari hasa Mwananchi, pengine wenye fedha wameamua kuzihamishia kwenye benki za nchi nyingine. Sisi Serikali ya Uswisi tunapochapisha ripoti kama hizi kuonyesha jumla ya fedha kwa nchi zote duniani, haimaanishi kuwa fedha zote hizo ni haramu.”

Alisema ni makosa kwa vyombo vya habari kuendelea kuonyesha kwamba ni Uswisi pekee kunakofichwa fedha chafu, kwani zipo nchi nyingine ambako watu wa mataifa mbalimbali huweka fedha zao ambazo zimepatikana kwa njia haramu.

Benki za Uswisi zimekuwa zikidaiwa kutumika kuficha fedha chafu kutoka maeneo mbalimbali duniani kutokana na usiri wake katika kutunza taarifa za wateja.

Ripoti hiyo inaonyesha kuwa Kenya inaongoza kwa nchi za Afrika Mashariki kwa kuwa na kiasi kikubwa cha fedha ambacho ni karibu Sh.1.6 trilioni ikifuatiwa na Uganda Sh.376.7 bilioni, kisha Tanzania Sh.291.5 bilioni.

Rwanda ina Sh.55.1 bilioni na Burundi Sh.42.2 bilioni.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alipoulizwa jana kuhusiana na taarifa hizo mpya alisema suala hilo la fedha zilizopo Uswisi si la kuzungumza kwenye vyombo vya habari.
“Hili jambo ni jambo nyeti sana kwa sababu kazi tuliyopewa kuchunguza suala hili bado hatujamaliza, kwa hiyo kuanza kulizungumza kwenye vyombo vya habari kunaweza kuathiri kazi hii,” alisema Jaji Werema.

Aliwaomba Watanzania kuvuta subira juu ya jambo hilo akisema kamati yake inaendelea kufuatilia na taarifa itawasilishwa.

VITA DHIDI YA MAJANGILI INAHITAJI UJASIRI NA SIO BUNDUKI NA MAGARI MAPYA

$
0
0
Sina budi kumpongeza Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, kwa jitihada zake za kukabiliana na ujangili nchini.

Ama kwa hakika, najua kwamba anaumiza kichwa kufanya kila awezalo kuhakikisha ujangili unakwisha au unapungua nchini.

Katika jitihada hizo, hivi karibuni kupitia wizara yake, alitoa bunduki 500 aina ya AK 47, za kivita mahsusi kwa ajili ya kupambana na ujangili pamoja na magari aina ya Landcruiser.

Waziri alisema bunduki hizo pamoja na magari vitapelekwa katika mapori ya hifadhi nchini kwa ajili ya kuwasaidia askari wa wanyama pori kufanya vyema kazi yao.

Hata hivyo vita ya ujangili wa meno ya tembo haina tofauti sana na ile ya dawa za kulevya.

Ni mtandao mpana ambao umejipanga vyema ili kuhakikisha meno ya tembo yanapatikana kwa uhai au umauti. Mtandao huu si wa Watanzania pekee, mtandao huu unahusisha raia wa nchi za nje hasa Bara la Asia. Na wengi wanaokamatwa, ni raia wa Hong Kong na Thailand.

Kwa mfano, ripoti iliyotolewa Juni 2013 na Taasisi ya Ulinzi wa Tembo Tanzania (TEPS), inaeleza Bandari ya Dar es Salaam ni kituo kikuu barani Afrika kinachotumika kusafirisha pembe za tembo kuelekea China, Vietnam, Japan, Ufilipino na Thailand.

Hivyo basi wakati tukiendelea kuleta bunduki za kivita, magari na kuongeza askari, lazima tujue nani anawalea raia wa China wanaokamatwa na pembe za ndovu na wale wanaohusika katika mtandao huu huko China, Vietnam, Ufilipino na Thailand.

Kwa sababu, hakuna mfanyabiashara anayeweza kufanikiwa katika biashara bila kuwa na wateja. Kama wateja wakubwa wa pembe za ndovu na faru ni raia wa Bara la Asia, basi tujue kabisa kiini cha msiba wetu kinaanzia huko.

Wakati huo huo, hatuna budi kuangalia urafiki wetu na nchi hizo hasa China kwani inaelekea ni wa mashaka hasa pale wanapokaribishwa kuwekeza huku wakitumia fursa hizo kutuharibia mustakabali wetu.

Uchunguzi uliowahi kufanywa na gazeti hili uliwahi kugundua kwamba mtandao wa ujangili una watu wake katika Bandari ya Dar es Salaam, ambao hushiriki kuipitisha mizigo ya pembe za tembo bila kugundulika.

Kinachozua maswali, ni kwa nini makontena mengi yanapita katika bandari hizo bila kugundulika, lakini hushikwa katika bandari nyingine kama Vietnam, Thailand, China na Ufilipino?

Kwa mfano, Januari 2009, mzigo mkubwa wa pembe za ndovu uliondoka salama Bandari ya Dar es Salaam, lakini ulikamatwa Machi 5, Vietnam katika Bandari ya Hai Phong.

Wakati huo huo, hebu tujichunguze na sisi wenyewe kuhusu utendaji wetu, usiri, kubebana, kuoneana haya na kile kinachoaminiwa na Watanzania wengi eti demokrasia.

Majangili wengi wanaokamatwa au kujulikana kabisa kuwa wanafanya ujangili huo, husitiriwa na kuonewa haya kwa sababu tu ya majina yao makubwa, vyeo serikalini na wakati mwingine wanaonekana wana umuhimu kwa nafasi zao serikalini.

Mwenendo huu unasababisha ujangili kuendelea kukolea mithili ya moto wa kifuu kwa sababu majangili hayo yanafahamu fika kwamba, hayataweza kufanywa lolote au hata ikitokea akawepo anayejaribu kufanya lolote basi, atapewa kitu kidogo, kama wasemavyo waungwana ‘penye uzia, penyeza rupia.”

Haiwezekani kuumaliza ujangili kwa risasi pekee au kwa maneno kuwa ‘tuna majina 40 ya majangili’ la hasha. Hii haitoshi, kwa serikali yenye ujuzi na ufahamu wa kiintelijensia kama Tanzania. Itakuwa aibu ya karne iwapo tembo na faru watamalizika na kizazi kijacho kikawafahamu wanyama hao kwa picha pekee.

0715-773366

CONGOLESE APLCS MAI-MAI CAPTURE 4 TANZANIAN PEACEKEEPERS

$
0
0
CONGOLESE APLCS MAI-MAI CAPTURE 4 TANZANIAN PEACEKEEPERS
The Congolese militia of the Alliance for a Free and Sovereign Congo (APCLS), under the command of General Janvier Buingo Karairi, have captured four Tanzanian peace keeping soldiers serving within the United Nation Intervention Brigade,  after heavy fightings in Lukweti, Masisi terrotory, sources within the Office of the Governor of North-Kivu Province told AfroAmerica Network.

APCLS Ambush Kill 18 FARDC Soldiers; North Kivu Governor Julien Paluku Asked to Mediate

The APLCS captured the Tanzanian troops after heavy fightings in Lukweti,  20 km towards Walikale, from the city of Nyabiondo, in Masisi territory. APCLS troops have been battling the Congolese army FARDC over the last few months. The Tanzanian troops were captured when they fell in ambush, while trying to reinforce the FARDC position that was surrounded. During the ambush, 18 FARDC soldiers were killed and an undetermined number injured.  Although APCLS was accused by UN Group of Experts in the January 23, 2014 report S2014/42  of collaboration with other armed groups, it appears the ambush was solely conducted by APCLS troops. APCLS fighters are primarily of Hunde ethnic origin and are often allied with Hutus and Nyangas, against Rwandan-backed Congolese militias, such as Raia Mutomboki and Mai-Mai Nduma Defense Forces of Cheka aka Sheka Nteberi.

  According to the sources with the Office of the North-Kivu Governor, when Martin Kobler, the Head of MONUSCO,  learned of the capture, he contacted the Governor of North Kivu, Julien Paluku Kahongya,  to request that he intervene with the APCLS mai-mai leaders and Hunde elders, to have the 4 Tanzanian soldiers released. The Governor asked the head of Security, Miganda, to lead the negotiations. AfroAmerica Network tried to contact Miganda to enquire about the status, without success.  However, the sources said Miganda was already in contact with General Janvier, to negotiate the release.

Martin Kobler, MONUSCO Head Seeking A Peaceful End to Conflict in the Kivus.

The capture of the Tanzanian peacekeeping troops comes as Martin Kobler was engaged in a media charm to have the humanitarian and military crisis in North-Kivu resolved peacefully. On March 5, 2014 he held a meeting in Goma with representatives of armed groups and officials of the DRC government to find ways to resolve the conflict.

During the meeting, Martin Kobler proposed the representatives of the armed groups to convince those among their commanders accused of crimes in front of the International Criminal Court (ICC), to surrender. He promised that if these leaders do so, he would himself provide air transportation from Eastern DRC to the Hague.  The representatives of armed groups gave a commitment to convince their commanders. In return, the DRC official promised to report to President Joseph Kabila, so that he supports the initiative.

According to sources close to MONUSCO and the DRC government officials, DRC President Joseph Kabila agreed with the  principle and promised to give an official response no later than March  8, 2014.  Specifically, Joseph Kabila was asked to agree to support a disarmament and resettlement of Rwandan combatants on DRC territory.

NIMEMFUMANIA MKE WA RAFIKI YANGU KIPENZI GUEST HOUSE AKIWA NA NJEMA JINGINE

$
0
0
Katika hali nisioitegemea tumegongana ana kwa ana gest mi na shemeji yangu wa karibu ambae mme wake tunafanya kazi pamoja. mimi nikiwa nampeleka mgeni wangu kwenye chumba alichofikia mara ghafla chumba chumba cha pili mlango ulifungulia na kikatokea kichwa tu kugeuka tukagongana ana kwa ana huyo shemeji yangu ilichukua takriban sekunde 30 kukodoleana macho na baada kutoa salam sauti ya chini mimi niliingia chumba cha mgen wangu kumuaga na kumtakia safari njema wakati natoka huku mwili ukiwa umekufa gan kwa kutoamin nilichokiona kwa shemeji yangu na kutambua alienipokea zamu ya lindo saa 12 jion mke wake ana madudu niliishiwa nguvu kabisa, alikuja mhudum wa ile gest akaniitia chemba baadae akaja jamaa ambae sikuweza kumtambua kutokana na mazingira na kunieleza kilichotokea muda mfupi uliopita anaomba iwe niifanye kuwa siri kwanza ametokanae mbali isitoshe ni mzazi mwenzie na akanikabidhi elfu 70 ambayo mi nilikataa kuipokea huku nikimwambia kwasasa nahitaji kuwahi nyumbani mambo mengine tutawasiliana kwa simu ili kukwepa ushaidi niliondoka lakin hatua chache baadae ilipigwa simkuingalia ilikuwa ya shemeji yangu akinisihi lile suala anaomba liwe siri kwa gharama yoyote ile na nimpe muda mfupi mtu wake anafanya michakato ya hela soon nitapata kwa njia ya m-pesa. kubwa kwangu jamaa tumetokanae mbali sana urafiki kwetu ni zaidi ya ndugu tumesoma shule ya msingi moja tumeachana sec. tumeingia depo pamoja na kupangiwa kituo kimoja yaani kama bahati tu hofu yangu ni kwamba asikie hii isue najua alaf sikumpa taarifa atanionaje mimi? mpaka sasa natambua kwamba ameoa na ana watoto wawili huyu jamaa ameniambia kwamba ni mzazi mwenzie nashindwa kuelewa na proces zote za uchumba mi nilihusika na sikuambia kama amezaa, katika nyakati tofauti nimeingiziwa kwa mpesa zaidi mil. 1.2 kwa saa 17
nifanyeje?

KUPOTEA KWA NDEGE YA MALAYSIA NI MAAJABU..WATUMIA MPAKA WAGANGA WA KIENYEJI

$
0
0
Karibia Week Sasa kama Si week, lakini hakuna alamu yoyote ya ndege ya Malaysia Airlines, haijulikani kama imedondoka au imezama baharini na kama ingezama mabaki yangeonekana au hata kama ingelipuliwa mabaki nayo yangebaki, sasa sijui imepotelea wapi! Kila nikifuatilia nakutana na still missing!
Wakati ambapo China imepeleka angani satellite 10 kuitafuta ndege ya Malaysia Airlines iliyopotea, serikali ya Malaysia imewaomba waganga wa kienyeji kusaidia zoezi hilo.
Mganga maarufu nchini humo Ibrahim Mat Zin anayejulikana kama ‘Raja Bomoh Sedunia Nujum VIP’ alifanya tambiko kwenye uwanja wa ndege Kuala Lumpur Jumatatu hii kusaidia kuitafuta ndege hiyo ya MH370. Anadaiwa kuitwa na viongozi wa juu wa serikali.
“Nadhani ndege bado ipo angani ama ilianguka baharini,” alisema Ibrahim Mat Zin.

MZUNGU AFUMANIWA GESTI AKIWA NA MWANAFUNZI

$
0
0
NI kweli duniani kuna mambo na mambo yenyewe hufanywa na binadamu! Mzungu mmoja ambaye jina lake halikupatikana, amejikuta mikononi mwa polisi kufuatia kunaswa gesti akiwa na denti, OFM wa Ijumaa walikuwepo.
Mzungu baada ya kunaswa na OFM akiwa na denti gesti.
Tukio hilo la aina yake kwa mwaka 2014, lilitokea saa saba usiku wa kuamkia juzi katika gesti hiyo iliyopo Msasani jijini Dar es Salaam.
DENTI AKWEPA SHULE
Awali ilidaiwa kuwa, mwanafunzi huyo wa kidato cha tatu, anayesoma katika shule moja ya sekondari jijini Dar, (jina tunalihifadhi kwa maadili) alikuwa akikwepa shule jambo lililokuwa likimuumiza kichwa mama yake mzazi (jina lipo).
Mzungu akitahamaki baada ya tukio hilo.
Katika kufuatilia, mzazi huyo alibaini kwamba, binti yake alikuwa amebanwa na Mzungu huyo na ndipo alipofikiria njia ya kumnasa.
OFM YASHIRIKISHWA
Habari zaidi zinasema kuwa katika kupanga mkakati huo, mwanamke huyo alipata jibu kwamba ni lazima Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ washirikishwe.
Ilikuwa saa 3:45 usiku wa Machi 11, 2014, Kamanda wa OFM alipokea simu kutoka kwa mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la mama Zakia, mkazi wa Tegeta jijini Dar es Salaam.
Mzungu akiomba msamaha.
Mama: Haloo, hapo ni Global Publishers?
Kamanda: Ndiyo mama, unasemaje?
Mama: Jamani naombeni msaada wenu maana nyinyi ni kiboko hamuwezi kuyafumbia macho maovu. Mimi ni mjane najisomeshea mwanangu, kwa sasa yupo kidato cha tatu.
Namsomesha kwa shida sana lakini sasa nimegundua kuna Mzungu anamrubuni mpaka wakati mwingine haendi shule.
Mzungu na denti wakiwa kitandani.
Hivi karibuni nilianza kumtilia shaka, nikachukua simu yake akiwa amelala, nikaipekua na kukuta meseji za mapenzi za mtu ambaye simfahamu.
Lengo langu ni kumkomesha huyu mtu ili iwe fundisho kwa wengine.
Kamanda: Oke mama, nimekuelewa, tunakuahidi kukusaidia, kinachotakiwa ufuate taratibu za kisheria kwanza. Katoe ripoti polisi maana huyo ni mwanafunzi kisha wasiliana na mjumbe au mwenyekiti wa mtaa.
Mama: Ahsante sana mwanangu, nitakujulisha.
Mzungu na denti wakivaa nguo.
MJOMBA MTU AJULISHWA
Kwa sababu ni mjane, mwanamke huyo aliwasiliana na kaka yake ambaye alianza kumfuatilia denti huyo kila alipokuwa akienda, hasa nyakati za jioni, ndipo za mwizi arobaini zikatimia.
DENTI AONEKANA AKIPANDA GARI YA MZUNGU
Siku ya tukio, mjomba huyo alifanikiwa kumuona mpwa wake akipanda ndinga ya Mzungu huyo.
Mjomba huyo, haraka sana aliwasiliana na Kamanda wa  OFM, wakakutana na kuanza kulifuatilia gari hilo kila lilipokuwa likikatiza.
WATINGA KLABU
Mwisho wa safari ya wawili hao ilikuwa kwenye klabu moja ya usiku iliyopo Masaki, Dar ambako walitumia muda mwingi kujirusha hadi mishale ya saa saba usiku.
MZUNGU MBELE, OFM, MJOMBA NYUMA
Baada ya wawili hao kutoka klabu, msafara wa kwenda gesti ulianza ambapo Mzungu huyo akiwa na denti, bila kujua wanafuatiliwa, walikwenda hadi kwenye gesti hiyo.
OFM na mjomba mtu nao walikuwa nyuma yao huku tayari wakiwa wameshawasiliana na askari ambao walifika kwenye gesti hiyo na kuunganisha nguvu.
MHUDUMU AWEKWA MTU KATI, AGONGA MLANGO
Ili kumweka mtu kati Mzungu huyo, ilibidi mhudumu wa gesti hiyo atonywe kisa chote ambapo alikubali kwenda kugonga mlango wa chumba walichoingia wapenzi hao.
MZUNGU, DENTI LAIVU!
Mzungu ndiye aliyefungua mlango na kukutwa kama alivyozaliwa huku denti akiwa juu ya kitanda.
Kwa hasira, mjomba alimchapa kofi mpwa wake ambapo Mzungu huyo aliomba apigwe yeye kama suala la kupigana litaendelea. Hata hivyo, hakupigwa.
MZUNGU AJITETEA
Katika utetezi wake, Mzungu huyo alisema anashangaa kuvamiwa wakati denti huyo ni girlfriend wake, utetezi ambao haukukubalika.
OFM YAWAACHA
Kwa kuwa OFM walikuwa na majukumu mengine usiku huo, baada ya zoezi hilo kukamilika waliondoka eneo la tukio na kuwaacha askari na mjomba mtu  wakiendelea kumhoji Mzungu huyo.
Stori: Issa Mnally na Richard Bukos
GPL

LULU: ...SIFANYI TENA KOSA, NIKIPATA MIMBA NAZAA TU!

$
0
0
Stori: Shakoor Jongo

STAA wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kuwa kama siku yoyote atapata ujauzito kwa bahati mbaya, hatafanya kosa tena, atazaa tu. Katika mahojiano maalum na gazeti hili juzikati, Lulu alisema kwa sasa yuko tayari kuolewa ili awe na familia yake ila si kwa sharti la mwanaume husika kumwambia amzalie kisha ndiyo amuoe.

Ijumaa: Kwani kwa sasa si una mpenzi? Lulu: Ndiyo ila bado sijapanga swala la kufunga naye ndoa. Ijumaa: Kwa hiyo umesema ukipata mimba kwa bahati mbaya hutofanya misteki lazima uzae, unaweza kuniambia ni misteki gani? Lulu:

Nadhani maswali yako uliyoniuliza nimekujibu kiufasaha kabisa hilo siwezi kulijibu. Ijumaa linahisi kosa ambalo Lulu hatalirudia tena ni la kutoa mimba, kitu ambacho hataki kukizungumzia.
GPL

MADAHA AKOMALIA NDOA NA MENEJA WAKE

$
0
0
Stori: Gladness Mallya

MWANA DADA kutoka kiwanda cha muziki na filamu Bongo, Baby Madaha ameonekana kukomalia kuolewa na meneja wake, Joe Kairuki huku akidai kuwa, mwanume huyo ni mume sahihi kwake.

Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Baby Madaha ‘Queen of Swaga’ alisema kutokana na uhusiano wake na Joe kuelekea kwenye ndoa, mara nyingi amekuwa akila bata zake nchini Kenya ambako ndiko mchumba wake huyo anakotokea.

“Mimi sijui kwamba ni mume wa mtu kwani sijawahi kumuona huyo mwanamke ila ninachokijua Joe ana mtoto na hajafunga ndoa na aliyezaa naye tena wanaishi nchi tofauti kwa hiyo sioni shida kuwa naye na mipango ya ndoa ipo,” alisema msanii huyo.
GPL

AVRIL CONFIRMS THAT SHE IS TAKEN (ENGAGED)

$
0
0
Love is a beautiful thing and feeling loved back is just a burst of beautiful colors. Avril, an RnB artist, who is among the top beautiful sassy divas from Kenya has finally found her prince. Avril has confirmed that she is engaged to her Kenyan based South African business man.

In the past we have witnessed Avril, just like any other woman engage in a roller coaster of relationships, but hey everyone has to YOLO ones in a life time right? Okay after kissing many frogs Avril finally met her charming prince. She had this to say  about her relationship “we had come to Nairobi for business when he was introduced to me by his contacts. We became friends before the affair turned into a beautiful relationship. Now, I am engaged to him,”. Its definitely clear that Avril has fallen head-over-heels for her man.

We still don’t know the fiances name but hopefully we shall know it soon. As the two continue planning for the wedding and going for adventures around Africa, its time we got an official invite. And for those who snoozed on their chances allow me to say, sorry guys she’s now taken.

BODA BODA WAVAMIA MAKAO MAKUU YA CHADEMA KINONDONI

$
0
0
Jengo la makao makuu ya CHADEMA yaliyopo mtaa wa ufipa Kinondoni yameviwa ma vijana waendesha boda boda wa jijini Dar muda huu wakitaka waonane na viongozi wa chama hicho kuwaeleza kero na manyanyaso wanayoyapata kutoka kwa maofisa wa jiji pamoja na askari polisi katika utekelezaji wa mujukumu yao ya kujipatia riziki.

Kutokana na hali hiyo tayari polisi wameshazingira eneo zima la makao makuu ya CHADEMA kwa ajili ya tahadhari ya jambo lolote

WEMA NA DIAMOND HAPATOSHI YADAIWA WAZICHAPA KISA VICTORIA KIMANI

$
0
0
Inasemekana lakini ....Habari kutoka Segment ya U-Heard ya Sudi Brown wa Clouds FM imehabarisha kuwa Wema na Diamond Jana walikwaruzana baada ya Wema kuhisi kuwa Diamond anatoka na Mwanamuziki wa Kenya Victoria kimani ..hii ilitokea Diamond na Victoria walipokuwa Studio wakifanya wimbo inasemekana Diamond hakumwaga Bi Wema , Wema aliona tu kwenye Instagram kuwa mida hiyo Diamond yupo na Victoria ndio ikabidi awafungie Safari na kuzua Timbwili la haja , Inaonekana Wema aliona Wivu baada ya kuwa na Tetesi kuwa Diamond anatoka na Mwanadada huyu kutoka Kenya...


"MPENZI TUJENGE NYUMBA MBILI TUKIACHANA KILA MTU ACHUKUE YAKE"

$
0
0
Chonde jamani baadhi ya kina mama/dada/wasichana mbona mna roho kama za ajabu hivi.

Unawezaje kumwambia mumeo tena wa ndoa maneno kama hayo? mweeee!

Maneno haya kaambiwa mwanaume na mkewe wa ndoa wiki moja iliyopita.

Kwa sasa jamaa hamuamini kabisa mkewe akihofia huenda huyu mwanamke atakuja kumuua kwa sababu ya mali.

Wakiwa sebuleni baada ya kula mwanamke-ghafla tu-akamwambia mumewe eti wajenge nyumba nyingine ya pili ili ikitokea huko mbeleni wakiachana basi kila mmoja awe na nyumba yake kwani hii nyumba wanayoishi sasa mwanaume alijenga kabla ya kumuoa yeye.

Mwanamke anahofia hatapata kitu ikitokea atakufa au wakiachana huko mbeleni.

Mshikaji kaja niambia afanyeje, maana anahofia huenda huyu mwanamke anaweza kuja kumtoa roho kama watakuja kuwa na mali.

Sababu ya hofu hii, mshikaji anafikiria hata kukiuza kiwanja chake kilichopo bunju alichokuwa anapanga kuanza ujenzi mwezi wa nane.

Hivi jamani mkeo akikwambia maneno kama haya, na ndo hivyo ushamuoa kwa ndoa ya kanisani utafanyaje?

DIAMOND ASHIKA NUMBER MOJA TOP TEN CHAT YA NYIMBO ZA AFRICA..TRACE TV

$
0
0
Toka nimeanza kufatilia hii chati ya TRACE TV, kituo cha ufaransa ambacho kimeshika hata nchi za Afrika kwa kucheza muziki wenye viwango kutoka kila kona ya dunia, sijawahi kuona msanii wa Afrika Mashariki alieshika nafasi ya kwanza kwenye Top10.
Siku zote nilizoea kuona Wasouth Africa na Wanigeria ndio wanaishika namba 1 ila sasa Mtanzania Diamond ameivunja hiyo rekodi kupitia single yake ya ‘number 1 rmx’ ambayo kamshirikisha Mnigeria Davido

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO MPYA WA GODZILA FEAT..MARCO CHALI-YOU AND I

$
0
0
Download wimbo mpya wa Godzilla akimshirikisha Producer Marco Chali, wimbo unaitwa "You and I"

BAADA YA RIHANNA NA DRAKE KUONESHA LIVE MAPENZI YA CHRIS BROWN NAE AFANYA HIVI

$
0
0
Last week it was reported that Karrueche had finally given up on her relationship with Chris Brown after discovering that he was still secretly longing for Rihanna. Well, now that Rihanna and Drake are official, Chris took to Twitter last night to say Karrueche will always be his heart...then he deleted it..

TANZANIA HAIMO KATI YA MAJESHI IMARA ZAIDI KATI YA NCHI 7-KENYA IMO

$
0
0
Mtandao wa Globalfirepower.com -  umeainisha nchi 7 zenye majeshi imara zaidi Afrika na hii ndio tathimini yao, lakini Tanzania haimo ila kenya ndo wamo.

Egypt: Ina watu zaidi ya milioni 83

Kila mwaka watu 1.5 ,milioni hufikisha umri wa kujiunga na jeshi la nchi hiyo.

Ina Tanks: 5000

Helicopters za kijeshi: 200

Ndege za kivita: 863

mine warfare: 28

Serviceable airports: 84

Budget ya jeshi kwa mwaka ni $4 bilioni.

2: Ethiopia ni ya pili.

Ina idadi ya watu-milioni 84.

watu milioni 2 hufikia umri wa kujiunga na jeshi kwa mwaka.

ina Tanks: 300
Armored vehicles: 1200
Aircrafts: 147
Helcopters: 68

Budget ya jeshi kwa mwaka ni $ 300 milioni.

3. SOUTH AFRIKA.

Ina watu milioni 51

Watu milioni 1 hufikisha umri wa kujiunga na jeshi.
Jumla ya Tanks: 250
Magari ya kivita:1590
Rocket projectors:240
Frigators:4
Submarine:3
Defence budget kwa mwaka: $ 5 milioni.

4. NIGERIA.
Ina watu milioni 160.
watu milioni 3.5 hufikisha umri wa kujiunga na jeshi.
Ina Tanks: 363
Magari ya kivita: 1400
Ndege za kivita: 294
Helcopters: 84
53 serviceable Airports.
Defence budget ni: $ 2.2 bilioni.

5. ALGERIA.
Ina jumla ya watu: 37 milioni.
watu laki 672,000 hufikisha umri wa kujiunga na jeshi.
Ina zaidi ya Tanks: 1000
Magari ya kivita: 1800
Ndege za kivita:400
Helcopters: 136
Submarines: 3

12 coastal crafts
Defence budget: $8 bilioni.

6. KENYA.
Ina jumla ya watu milioni 43

watu laki 839,000 hufikisha umri wa kujiunga na jeshi.
Tanks: 186
Self propelled guns: 30
Ndege za kivita: 148
Helcopters: 78
194 serviceable airports.

Defence budget: $ 5 bilioni.

7. LIBYA.

Ina watu milioni 6
watu laki 116,000 hufikisha umri wa kujiunga na jeshi.
Tanks:500
Magari ya kivita:2500
Self propelled guns:400
Rocket projectors:800
AT Weapons: 1050
Ndege za kivita: 600
Helcopters: 121
Defence Budget: $880 milioni.

PENZI LA HUDDAH NA MUSTAPHA KWISHNEY "MUSTAPHA IS NOT MY CLASS" HUDDAH

$
0
0

After all the racket surrounding the Huddah-Mustapha relationship, things have now taken a totally different an anticipated direction. Earlier today, speaking exclusively to Ghafla! Huddah declared that there’s in fact nothing between her and the ‘Lenga Stress’ hit-maker.

In a lengthy statement sent to us, Huddah states emphatically that Colonel Mustapha is not in her class nor her level and everyone knows that she can never date him…only in his dreams!

Huddah says,

"I don't know Mustafa, I don't know where he lives. And the first time I met him was at the photo session and when we went for KTN interview. When I heard he is all over doing interviews without me saying how much we are dating has trashed my name coz Mustafa and Ogopa DJs are a sinking ship that was only looking to rise using my name.

I went ahead, called Lucas of Ogopa Djs and ordered him not to release the song or else I'll take legal action. And that's why it never got released.

I just wanna make it clear that Mustafa is not my class, not on my level and everyone knows I can't date him apart from his 300fans. Even Mwanaisha asked in the interview, "you are known to be on top of ur game, why Mustafa?" I just laughed coz I was told what to say at the interview until shit hit the fan."

Since it was prudent to give both Mustapha and Ogopa DJs a right of reply, we reached out to them for the same.

However, if you’ve been keenly following this mini-‘telenovela’, you should know by now that Ogopa never answer phone calls and so the same was witnessed today. After several phone calls and text messages, we got no response.

All the same, we reached out to Colonel Mustapha. And it appears he’s been taking notes from his producer because 6 phone calls later, no answer was forthcoming.

With our hands tied, there’s little we could do than to let the public be the judge.

TB JOSHUA" NDEGE YA MALAYSIA IPO CHINI YA MAJI BAHARINI WATAIPATA HIVI KARIBUNI"

$
0
0
“The plane concerned is deep inside the sea. Some of the particles will be seen on the surface of the sea any moment from now.May their souls rest in peace. We pray the Lord gives the family and loved ones the strength to bear the loss. Our prayer and love are always with them, the nation of Malaysia and other countries who had passengers on this flight.”However,US Counter-terrorism officials now suspect that the plane flew for a total of five hours based on data automatically downloaded and sent back to Rolls Royce - the manufacturers of the Boeing 777's engines.
They are now pursuing the astonishing possibility that the plane and its 239 passengers was diverted to an undisclosed location 'with the intention of using it later of another purpose.The pilot or somebody else turned the planes' transponders off to avoid detection and flew it to another location

NAZIZI AFA KIMAPENZI NA PRODUCER WA KIBONGO...AACHANA NA MUME WAKE

$
0
0
Hivi karibuni, mmoja wa waasisi wa hip hop nchini Kenya, Nazizi, alithibitisha kuwa ameachana ma mume wake kutoka Tanzania, Vinny, na wapo katika harakati za kupeana talaka Naziz na Vinny wana mtoto mmoja wa kiume. Msanii huyo, ambaye ni member wa kundi la hip hop la Necessary Noize, amekufa kimapenzi na Mtanzania mwingine tena, producer Herry Sappy, anayefanya shughuli zake za kimuziki kwenye studio ya Home Boyz Productions ya Kenya. Kwa mujibu wa bongo5.com, Nazizi amethibitisha kuwa na uhusiano na Herry Sappy tangu Valentine’s Day, Februari 14, na uhusiano wao ni wa dhati Chini hapa ni picha za wapendanao hao, pamoja na moto wa Nazizi na aliyekuwa mume wake.
Nazizi na Herry Sappy wakimbusu mtoto wa rapper huyo
Nazizi na Herry Sappy wakimbusu mtoto wa rapper huyo
Nazizi na aliyekuwa mumewe, Vinny, wakati mapenzi yalipokuwa
Nazizi na aliyekuwa mumewe, Vinny, wakati mapenzi yalipokuwa
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images