Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Mashindano ya Big Brother Africa yavunjwa

$
0
0
Kama ulikuwa unasubiria kuona mashindano ya Big Brother Africa basi pole sana sababu kwa mwaka huu hayatakuwepo.


Mashindano ya Big Brother yametokea kuwavutia watu wengi kutokana na kukutanisha washiriki wanaotoka mataifa mbalimbali ya Afrila, huku Tanzania ikionekana kufanya vizuri kwenye mashindano hayo.

Taarifa zilizotolewa na waandaaji wa mashindano hayo kupitia M-Net wamesema kwa sasa wanajiandaa kuweka mikakati ili kuboresha mashindano hayo hapo mwakani.


“We wish to thank Big Brother Africa fans far and wide for their continues support over the past edition and promise that the shw will go on, on Dstv, with new and excting productions in store from M-Net,” wamesema.

Mpaka sasa taji hilo la Big Brother linashikiliwa na Idris Sultani aliyefanikiwa kushinda mwaka jana na kupata zawadi ya fedha kiasi cha dola laki tatu.

Kauli ya Louis van Gaal baada ya Ubingwa wa Kombe la FA kwa Man United

$
0
0
Baada ya kufanikiwa kutwaa Kombe la FA akiwa na Man United, Louis van Gaal amezungumza kauli ya kujivunia, licha ya kuwa kibarua chake kipo mashakani kuchukuliwa na Jose Mourinho kwa siku za usoni, licha ya kuwa mchana wa May 21 2016 ulianza kwa headlines zisizo njema kwake.

Van Gaal ameripotiwa na Metro na AS kuwa atafukuzwa na Man United nafasi yake kuchukuliwa na Jose Mourinho, hiyo ilikuwa ni saa kadhaa kabla ya BBC na Sky Sports kuziongezea nguvu taarifa hizo, kwa kuripoti habari kama hizo katika tovuti zao.

Louis van Gaal amekuwa akiandamwa na tetesi zinazohusu hatma ya kibarua chake, aliongea kauli zya kujivunia kama hana hofu na habari zinazoendelea.‘Hii ni furaha kubwa kwa klabu na mashabiki na kwangu pia ambaye nimefanikiwa kushinda taji hili nikiwa katika nchi nne tofauti ni makocha wachache wanaoweza kujivunia hilo, hivyo nina furaha sana na jambo hili”

Rais Magufuli Alichelewa Kumng'oa Kitwanga -Lema

$
0
0
Lema ambaye ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani ya nchi ameyasema hayo katika mahojiano maalum na EATV kuhusu maamuzi ya Rais kumng'oa Waziri Kitwanga katika wadhifa wake ambapo Lema amebainisha wazi kwamba Rais alipaswa kutengua uteuzi wa waziri huyo baada ya kuandamwa na kashfa ya ufisadi kwa kampuni ambayo ana ubia nayo ambayo ilipewa kazi ya kufanya manunuzi na kuweka mashine za kuhifadhi alama za vidole katika vituo vya polisi nchini.

''Bunge lilipuuzia maoni ya kambi rasmi ya upinzani kuhusu suala la Waziri Kitwanga kuhusika katika kampuni iliyopewa kazi ya kuweka mashine katika vituo vya polisi, kama Rais alikuwa na nia njema angemsimamisha mapema kupisha uchunguzi, hii ya kuja kumsimamisha kwa maadili ya unywaji pombe ni issue ndogo ukilingnisha kashfa ya lugumi''-Amesema Lema.

Aidha Mbunge huyo ameeleza kuwa wakati wa Bunge la katiba pombe ilikuwa inauzwa bungeni hivyo kitwanga kusimamishwa kachukuliwa kama sample tuu kwakuwa wabunge na mawaziri wanaokunywa pombe wakati wa kazi ni wengi zaidi.

Profesa Muhongo Aichana Mikataba ya IPTL, Songas na Agreco........Asema Haina Tija Yoyote kwa Taifa

$
0
0
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amesema mikataba yote ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na kampuni za kufua umeme siyo mizuri na haina manufaa yoyote kwa Taifa.

Profesa Muhongo alisema hayo juzi wakati akijibu hoja ya kuongezeka kwa deni la Tanesco iliyotolewa na Msemaji wa Kambi ya Upinzani katika wizara hiyo, John Mnyika.

Kambi ya upinzani imekuwa ikisema mikataba ya Tanesco haina tija kwa Taifa na imekuwa ikiliua shirika hilo. Katika hotuba yake, Mnyika alisema Tanesco imekuwa ikiilipa IPTL Sh300 milioni kwa siku kama gharama za uendeshaji.

Profesa Muhongo alikiri kwamba ni kweli deni la Tanesco ni kubwa na limesababishwa na uongozi dhaifu, rushwa, wizi na mikataba mibovu ambayo Tanesco imeingia.

Alisisitiza kwamba hakuna mkataba unaolinufaisha Taifa.

“Lazima niseme ukweli, mikataba yote ya Tanesco siyo mizuri. Tumekuwa tukiwalipa Songas gharama za uendeshaji Dola 4.6 milioni; IPTL tunawalipa Dola 2.6 milioni; Agreco tunawalipa Dola 2.0 milioni. Hakuna mkataba wenye manufaa kwa Taifa,” alisema Profesa Muhongo na kuahidi kwamba wizara yake itachukua hatua ili kulinusuru shirika hilo na mzigo huo wa madeni kila mwezi.

Alisema wizara yake imeanza utaratibu wa kufanya tathmini ya utendaji wa wafanyakazi wa Tanesco ili kuhakikisha wanatoa huduma bora.

Alisema tathmini hiyo inafanywa kwa mameneja wa Tanesco kwa kuangalia wameingiza kiasi gani na wameunganisha wateja wangapi.

“Kila baada ya miezi mitatu tunafanya tathmini ya mameneja wetu na mwezi wa sita tutafanya tathmini ya pili. Wapo ambao walishindwa kukidhi vigezo katika tathmini iliyopita, wameondolewa,” alisema waziri huyo.

Kuhusu suala la umeme vijijini, Profesa Muhongo alisema Hazina imetoa Sh70.2 bilioni kwa ajili ya kumalizia utekelezaji wa awamu ya pili ya mradi wa umeme vijijini, unaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (Rea).

Jambo hili lililalamikiwa na wabunge wengi wakisema wakala huyo anashindwa kutekeleza majukumu yake kwa sababu fedha zake hazitolewi na Serikali.

Walishauri fedha za Rea ziwekwe katika akaunti yake maalumu bila kupitia Hazina. Hata hivyo, Profesa Muhongo alilihakikishia Bunge kwamba miradi yote iliyobaki katika awamu ya pili ya Rea itakamilika kufikia mwisho wa mwezi ujao.

Alisema miradi ya Rea haitatetereka kwa sababu ya Shirika la Changamoto za Milenia la Marekani (MCC) kusitisha kutoa misaada kwa Tanzania akisema Serikali imejipanga kusimamia miradi ya maendeleo bila kutegemea misaada ya wahisani.

“Tumeanzisha Mamlaka ya Udhibiti wa Mafuta (Pura). Wakala huyu atakuwa na jukumu la kusimamia mikataba yote ya mafuta na atasimamia pia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC),” alisema Profesa Muhongo.

Kuhusu suala la migodi kutolipa kodi, waziri huyo alisema ni kweli mingi hailipi na kusema ameanza kusimamia suala hilo na kuwa wote lazima walipe kodi.

Alisema Serikali pia itawalipa fidia wakazi wa Lindi katika eneo ambalo kitajengwa kiwanda cha kupakia gesi (LNG). Alisema fedha zipo na vijana wakasome Veta ili wapate ajira katika kiwanda hicho.

Ali Kiba, Diamond Platnumz Kimenuka Hatari...

$
0
0
Kimenuka! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia mafahari wawili wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kudaiwa kutupiana vijembe vya kufa mtu baada ya kuwepo kwa madai ya Kiba kuhujumiwa.

Kwa mujibu wa chanzo makini, ili kuweka hujuma ya kibiashara, hivi karibuni, pamoja na kukanusha mara kadhaa kutokuwa na tatizo na Kiba, Diamond alidaiwa ‘kutengeneza’ kwa makusudi penzi la mwigizaji Jacqueline Wolper Massawe na msanii wa Wasafi Classic Baby (WCB), Rajabu Abdulhan ‘Harmonize’ kisha kuvujisha video ya uhusiano huo mpya siku ambayo Kiba alikuwa akiuachia wimbo wake mpya wa Aje (Jumamosi iliyopita), lengo likiwa kuhamisha upepo mashabiki kutoka kwenye wimbo mpya na kujali mapenzi ya wawili hao.

“Ni hujuma ya kibiashara, Diamond na uongozi wake wameamua kumfanyia Kiba ili wimbo wake ukose kiki kwa watu,” kilidai chanzo chetu.


VIJEMBE VYATAWALA
Hata hivyo, kwa mujibu wa mmoja wa mameneja wa Kiba ambaye hakupenda jina lichorwe gazetini, amemtupia vijembe Diamond kwa kudai licha ya hujuma hizo lakini hawawezi kumgusa Kiba.
“Wanajisumbua, kizuri huwa kinajiuza chenyewe na huwezi kuzuia mafuriko kwa mikono. Wameingiza kiki zao lakini msimu huu hazifui dafu. Wimbo (Aje) umepokelewa vizuri na una mafanikio makubwa hadi sasa.


AZUNGUMZIA MKATABA
“Kuonesha kwamba Kiba amekubalika, ndani ya muda mfupi baada ya wimbo huo kuruka hewani, amelamba mkataba na kampuni ya kimataifa ya Sonny Music. Sasa hapo ndipo utakapoona Ngoma ya Kiba imekubalika kiasi gani, hawamuwezi huyu,” alisema meneja huyo.

KEJELI SASA!
Kama hiyo haitoshi, meneja huyo alizidi kutupa vijembe kwa Diamond kwa kueleza kuwa Kiba ni mkongwe hivyo kamwe hawezi kulingana naye kimuziki.

“Diamond hamuwezi Kiba, ameanza kuimba wakati Diamond bado hajawa msanii. Ameshafanya mengi kwenye huu muziki kuliko huyo Diamond, unakumbuka dili la One 8, Kiba aliungana na mastaa wakubwa katika project iliyokuwa chini ya msanii mkali duniani, R-Kelly (Robert Sylvester Kelly), Watanzania wanajua,” alisema meneja huyo.

KIBA HUYU HAPA
Alipoulizwa Kiba kuhusiana na vijembe na kejeli hizo anazodaiwa kuzitupa kwa mpinzani wake (Diamond), alisema ishu hiyo isiitwe vijembe badala yake ieleweke kwamba ndiyo ukweli.
“Siyo vijembe wala majungu. Huo uliosikia ndiyo ukweli wenyewe,” alisema Kiba.
TEAM DIAMOND WAJIBU MAPIGO
Kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii, wafuasi wa Diamond waliojipa jina la Team Diamond walicharuka kusikia msanii wao amehusishwa na hujuma za ‘kumuua’ Kiba kibiashara.
“Hana lolote huyo, Diamond ameshafanya makubwa sana ndani ya muda mfupi kumzidi yeye ndiyo maana anatapatapa kwa sababu nani asiyejua kuwa Diamond yupo fasta katika kuona fursa kuliko Kiba?
“Wolper na Harmonize wapo penzini kwa matakwa yao na si kwa kumuua Kiba, hana jipya,” aliandika mmoja wa wafuasi wa Diamond kwenye Mtandao wa Kijamii wa Instagram.


DIAMOND ANASEMAJE?
Jitihada za kumpata Diamond ili azungumzie suala hilo hazikuzaa matunda kufuatia simu yake ya mkononi kutopatikana hewani hadi tunakwenda mitamboni lakini meneja wake, Babu Tale alipoulizwa kuhusu suala hilo, alicharuka:

Risasi Jumamosi: Tale tuambie, hivi kuna ukweli wowote kwamba Diamond na timu yako mlipanga kumzima Kiba alipokuwa anatambulisha ngoma yake mpya kwa kutupia video inayoonesha uhusiano wa Wolper na Harmonize?

Tale: “Siyo kweli. Hilo swali ni la kipuuzi. Sikiliza, ngoja nikuunganishe na bosi wako ili asikie unavyoniuliza. Nakata halafu nakupigia.
Hata hivyo, Babu Tale hakufanya hivyo na alipopigiwa tena, simu yake haikupatikana.

WOLPER AFUNGUKA
Gazeti hili halikuishia hapo, lilimtafuta Wolper ili kujua kama ni kweli ametumika kumfifisha Kiba kimuziki ambapo alisema si kweli kwani penzi lake na Harmonize limetoka katika mioyo yao.
“Hakuna kitu kama hicho. Sisi tumependana wenyewe wala hatujashinikizwa na mtu yeyote kuvujisha penzi letu eti ili kumfanya fulani afifie! Kama imetokea limevuja wakati ambao huyo Kiba naye ametoa wimbo itakuwa tu imetokea lakini si kwamba tumedhamiria,” alisema Wolper huku simu ya Harmonize ikiita bila kupokelewa.

Ugomvi wa Diamond na Kiba ni wa muda mrefu ambapo huwa na msimu kwani kuna wakati unachachamaa kama sasa na kipindi kingine unapoa na hakuna anayejua hatima yao.

Chanzo: Global Publishers

Sura Nne za Rais Magufuli Baada ya Kutumbuliwa Charles Kitwanga

$
0
0
JAMII ya Watanzania imetakiwa kujifunza sura za Rais John Magufuli, kutokana na hatua yake ya kutengua uteuzi wa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga.

Akizungumza na gazeti hili jana kuhusu hatua hiyo ya Rais Magufuli, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania, Johnson Minja, alisema Rais ametuma salamu kwa sura nne kupitia utenguzi huo.

Sura ya kwanza kwa mujibu wa Minja, alisema Rais amewakumbusha watumishi wote wa umma kwamba uadilifu ni jambo muhimu mahali pa kazi, na wanapaswa kuheshimu na kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia muda na sio kutumia muda huo vibaya.

Pili, Minja alisema Rais ametuma salamu kwa walio karibu yake, kwamba uswahiba wao hauhusiani na kazi ya nchi, hivyo suala la kufahamiana si kigezo cha kiongozi avunjaye maadili kuachwa, bali wanapaswa kutambua nchi inaongozwa kwa Sheria na Katiba.

Akizungumzia sura ya tatu ya uamuzi huo, Minja alisema Rais amewakumbusha Watanzania kuwa haangalii muda gani amemteua kiongozi au muda gani ametumikia nafasi aliyopewa, bali kinachoangaliwa ni utendaji kazi wake kwa Taifa.

Aidha sura ya nne, imeelezwa kwamba Rais ameoneshwa kuwa haendeshwi kwa siasa za vyama kwa kuangalia wanasiasa watasema nini, hasa wakati huu wa uwepo wa Sakata la Kampuni ya Lugumi, na kusema alichoangalia ni kosa limetendeka muda gani.

“Kwa kweli Rais kaonesha ukomavu wake, ameonesha ni Rais mwenye msimamo, bila kusita amefanya uamuzi sahihi, hakuangalia vyama vya siasa vinasema nini, bali aliangalia maadili ya utumishi wa umma yanasema nini na kuchukua hatua,” alisema Minja.

Watumishi wengine
Kwa upande wake Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mchambuzi wa habari, Kitila Mkumbo, alisema uamuzi huo wa Rais ni hatua muhimu, na amefanya jambo kubwa na sahihi hivyo mawaziri wengine wanapaswa kuwa makini.

“Ni hatua kubwa, Rais amefanikiwa kuvuka hili, ameonesha uwezo wake wa kufanya uamuzi na sio kuangalia sura kwa minajili ya urafiki, au kufahamiana, ukiwa kiongozi unapaswa kujitambua hadhi yako na nafasi yako kwa jamii,” alisema Profesa Mkumbo.

Alisema hatua hiyo inaashiria kwamba taasisi nyingine za Serikali zitafanya kazi zake mapema badala ya kumsubiri Rais afanye kila kitu.

Profesa Mkumbo alitoa mfano kwenye utenguzi huo na kusema Bunge lilikuwa na uwezo wa kumzuia asiingie ndani ya ukumbi ule kwa hali yake ya ulevi, ili asiiaibishe Serikali kama ambavyo imeonekana, lakini hawakuchukua hatua hadi Rais alipochukua.

“Sasa ni wazi kwamba Sheria za Kazi na Vileo maeneo ya kazi zitaanza kufanya kazi, ili kila mtumishi ajitambue na kufahamu wajibu aliopewa ni dhamana na anatakiwa kutekeleza kwa kuzingatia maadili,” alisema Profesa Mkumbo.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Benson Bana alisema cheo ni dhamana na kwamba katika nafasi aliyokuwa nayo ndani ya Baraza la Mawaziri tena kwenye wizara nyeti, alipaswa kuwa mfano wa kiongozi mwenye uadilifu na haiba yake ifanane na hicho chombo.

“Rais katuma salamu nzito kwa wengine na taasisi za umma, imetufundisha kuwa Rais akikupa wadhifa, usimuangushe, huyu kamuangusha Rais na Serikali, alipaswa kuwajibishwa na amewajibishwa kwa wakati, bila kushinikizwa,” alisema Dk Bana.

Alisema wananchi wanapaswa kumuelewa Rais na kuacha kuzungumza maneno yasiyo na maana kwani Kitwanga alipaswa kuwajibishwa kwa kosa alilotenda kwa wakati huo la ulevi na Rais amechukua hatua.

Dk Bana alisema kwa hatua hiyo ya Rais, ni wazi kwamba wale wote wenye wadhifa katika utumishi wa umma, wanapaswa kuheshimu na kuzingatia misingi ya Maadili ya Utumishi wa Umma na kama misingi hiyo huwezi kuitekeleza, ni bora waache kazi mwenyewe.


Misingi ya Nyerere
Kwa upande wake Mhadhiri mwingine wa Chuo hicho, Dk Bashiru Ally, alizungumzia suala hilo kwa kurejea misingi ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kuwa katika mambo muhimu aliyoyajenga ni misingi ya utaifa na maadili ya utaifa.

Alisema kiongozi ni hadhi na ni nafasi ya heshima na kila kiongozi awe wa ngazi yoyote kuanzia Serikali za Mitaa hadi urais, anapaswa kutambua kuwa cheo ni dhamana na kina masharti na maadili yake.

“Ni mara ya kwanza kwa rais kuonesha ukali, ulevi ni jambo baya, linatakiwa kukemewa kwa nguvu zote, ujumbe huu uende kwa taasisi zote serikalini na kwa umma, pia walevi popote walipo hizi salamu ziwafikie,” alisema Dk Bushiru.

Alisema kosa alilofanya Kitwanga lipo kwa watumishi wengi wa umma na kwamba kwa hatua hizo za Rais, Katibu Mkuu Kiongozi anapaswa kupeleka salamu kwa taasisi zilizo chini yake kuwakumbusha kwamba utumishi wa umma unakwenda sambamba na maadili.

Swali kurudiwa
Kutoka bungeni, kitendo cha Kitwanga kujibu swali akiwa mlevi, kimesababisha Serikali kutakiwa kujibu upya swali hilo bungeni, huku akimkasirisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Aidha, imefahamika kuwa watu wengi ‘walishitukia’ kuwa mbunge huyo wa Misungwi mkoani Mwanza hakuwa ‘sawasawa’ wakati akijibu swali bungeni Ijumaa asubuhi mjini hapa.

Taarifa ya Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, Ikulu, Gerson Msigwa juzi kuhusu kutenguliwa uteuzi huo wa Kitwanga ilikuwa na aya mbili tu.

Kuitwa na Waziri Mkuu
Lakini baada ya hali hiyo kutokea, inaelezwa kuwa baada ya kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni, Kitwanga aliitwa ofisini kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye awali alikuwamo bungeni.

Inaelezwa Waziri Mkuu alikuwa amekasirika sana kutokana na kilichofanywa na waziri huyo na hakuwa yule aliyezoeleka miongoni mwa watu wake.

Kilichoendelea kati yao hakikufahamika, lakini kuna kila dalili alizungumza na Dk Magufuli kutokana na kitendo cha uvunjifu wa maadili ya utumishi kilichofanywa na Kitwanga, na kusababisha rais kutengua uteuzi wake.

Katika taarifa yake juzi usiku saa chache baada ya kutimuliwa Kitwanga, Waziri Mkuu Majaliwa alisema uamuzi uliofanywa na Dk Magufuli umefuata kanuni za utumishi wa umma ambao unakataza mtumishi kulewa akiwa kazini.

Kwa kawaida, maswali bungeni hujibiwa na naibu mawaziri kwa kila wizara, na endapo wizara haina naibu, hujibiwa na waziri husika. Na endapo wote hawapo, huteuliwa naibu waziri mwingine kujibu.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yussuf Masauni hakuwapo bungeni juzi na imefahamika kuwa yuko safarini kikazi katika moja ya mikoa nchini.

Kwa mujibu wa Naibu Spika Dk Tulia Ackson, swali la Minja lilikuwa: “Askari wa Jeshi la Polisi na Magereza wanaishi katika nyumba chakavu zisizokuwa na hadhi, ikilinganishwa na kazi zao wanazozifanya kwa jamii? Je, serikali ina mpango gani wa kuwaboreshe askari makazi.”

Akitoa majibu ya mwongozo huo juzi usiku kabla ya kuahirisha Bunge, Dk Ackson alisema ilibainika kuwa si kwamba swali la Minja halikujibiwa kikamilifu na Waziri, ila majibu yake hayakutoa mchanganuo wa nyumba ngapi zitajengwa kwa upande wa askari wa Jeshi la Magereza.

“Kwa kuzingatia Mwongozo ulioombwa na Mheshimiwa Mbunge, na uzito wa swali lililoulizwa kiti kimeamua kuelekeza swali hilo lirudiwe kuulizwa katika kikao cha tarehe 23 Mei, 2016. “Ili serikali iweze kutoa majibu kwa ufasaha zaidi ikiwa ni pamoja na kutoa mchanganuo wa nyumba ngapi za Askari Magereza zitajengwa, na katika maeneo gani,” alisema Naibu Spika.

Kitwanga aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) na Nishati na Madini anakuwa waziri wa kwanza kutimuliwa katika Serikali ya Awamu ya Tano.

SOURCE: Habarileo

PAUL Makonda Azitaka Benki zimwambie Waliokuwa Wanapokea Mishahara Hewa

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Dar, Paul Makonda amezitaka benki nchini zishirikiane na serikali ili kubaini akaunti zilizokuwa zikiingiziwa mishahara hewa pamoja na kuwabaini wote waliohusika katika malipo hayo.

Makonda akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake amezitaka bank 6 zikiwemo NBC, CRDB, NMB, CDB na zingine kutokana na swala la watumishi hewa waisaidie serikali ya mkoa wa Dar kufanya mambo matatu.

1) Kusimamisha matumizi ya akaunti za watumishi hewa mpaka pesa hizo zitakaporudishwa

2) Kuwataja watu wanaochukua pesa kupitia account hizo ambazo zimefunguliwa kwenye benki zao na watumishi wanaojulikana ni hewa ili polisi wachukue hatua pamoja na kufikishwa mahakamani.

3) Kama pesa hizo hazijachukuliwa maana yake ziko bank kwa sababu hiyo makonda amezitaka bank hizo kurejesha pesa za wananchi.

Makonda amezitaka benki hizo kukamilishwa mambo hayo ndani ya siku 21 na amezipatia benki hizo majina na namba zote za akaunti za watumishi waliyokuwa wananufaika na mfumo huo na amesema itasaidia pia kwa watumishi wa mabenki ambao siyo waaminifu.

VIDEO:

Wanawake Mbele ya Pesa, Mimba na Ukimwi ni Matokeo tu

$
0
0
Kama ulikuwa huwafamu vizuri hawa ndugu zetu, mama zetu.
Usitenge muda kuwafahamu, sababu utaweza kuwa chizi
Pesa wananusa kama sisimizi anavyo nusa sukari ipo wapi
Ukiwa na pesa ya kutosha utaweza kuwachanganya kijiji kizima
ukifulia kijiji kizima wanakuacha, utaanza kuonekana kama kituko

Aliye umba pesa Mr pilato kweli kaziloga. 
Ukiwa na pesa, wanawake wanacho itaji ni pesa yako tu. 
utumie condom, usitumie shauri yako
pesa imewatoa ufahamu kabisaaaaa

Lulu Michael na Gigy Money Wacharuana....

$
0
0
MASTAA wawili wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Gift Stanford ‘Gigy Money’ wamejikuta wakiingia kwenye mtifuano mkali baada ya kutoleana maneno machafu.

Chanzo makini kilieleza kuwa ishu ilianzia kwa Gigy ambaye alisema mwanadada Lulu hajui kuvaa anavaa matangazo, hii ni baada ya kuulizwa na kituo kimoja cha runinga kwamba ataje mastaa kumi wanaojua kuvaa ambapo Lulu alimjibu kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa Instagram kuwa bora asijue kuvaa lakini hawezi kuvaa matambara kama yeye.

“Yaani Gigy alikasirishwa sana na kitendo cha Lulu kumwambia anavaa matambara alijikuta akipaniki na yeye akaendelea kushilikilia msimamo kwamba anavaa nguo za matangazo hivyo ni bora yeye anayevaa matambara anayonunua mwenyewe kuliko yeye,” kilisema chanzo.

Baada ya kupata maelezo ya chanzo, paparazi wetu alimtafuta Gigy na kumuuliza kulikoni ambapo alisema amekasirishwa sana na kitendo cha Lulu kumwambia anavaa matambara wakati yeye alizungumza kama anavyoona kwani mavazi anayovaa hayaendani na mazingira.

“Matambara ni ya kwangu na haya ni maisha yangu siyo yeye anayevaa nguo za matangazo eti anajiona naye anavaa maana naona Lulu ameunda na kampeni na makundi kwa ajili ya kunishambulia, mimi ni jeshi la mtu mmoja hawaniwezi,” alisema Gigy Money.

Ili kuleta mzani wa habari, gazeti hili lilimtafuta Lulu lakini mpaka linaenda mtamboni simu yake ilikuwa ikiita tu bila kupokelewa.

Chanzo:GPL

PICHA:Kijana Ashambuliwa na Simba Baada ya Kuingia Katika Uzio wa Simba Hao Katika Hifadhi

$
0
0
A man who str!pped n@ked and entered a lion enclosure in a Chilean zoo has survived the incident, but the lions were killed.

Santiago authorities confirmed that the two lions were put down as they severely mauled the 20-year-old man who had broken into their cage early on Saturday.


The man, who has been named by local media as Franco Luis Ferrada Roman, was taken to a nearby hospital for treatment and was said to be in grave condition.

The young man broke into the enclosure, took off his clothes and jumped into the middle, horrifying other visitors who witnessed the attack.

Once inside, the lions reportedly immediately pounced on him and began to ‘play’ with him.
At this point, zookeepers intervened in the attack and shot the two lions in order to save his life.

The director of the zoo, Alejandra Montalva, said: ‘We believe that this person entered as a visitor and paid for his ticket.

One witness, Cynthia Vasquez, told Chilean radio station Bio Bio that the security personnel at the zoo were slow to react and that the animals did not attack the man as soon as he entered the enclosure.

‘He entered the enclosure from above and the lions started to play with him, and then after they attacked him,’ she said.

She also said the man was ‘shouting things about Jesus’She criticised the actions of the security personal, saying ‘first they threw water, evacuated the people and only later did they fire shots’.

Timu za Tanga Zaipa Mkono wa Kwaheri Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania

$
0
0
Klabu ya African Sports imeungana na vilabu vingine vya Tanga (Coastal Union na Mgambo JKT) kuipa mkono wa kwaheri ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara baada ya kuchapwa bao 2-0 na Mtibwa Sugar kwenye mchezo wa mwisho wa ligi uliochezwa kwenye uwanja wa Manungu Complex, Turiani, Morogoro.

African Sports na Mgambo JKT zote zilikuwa zikihitaji ushindi kwenye mechi zao za leo huku zikiombea mabaya timu za Ruvu JKT na Kagera Sugar ili zenyewe ziwe na uhakika wa kusalia VPL.

Lakini mabo yalikuwa tofauti baada ya Ruvu JKT kuichapa Simba kwenye uwanja wa taifa huku Kagera Sugar wakipata sare ya kufungana bao 2-2 dhidi ya Mwadui FC.

Kwenye uwanja wa Azam Complex, Mgambo imeshuka daraja kwa kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Azam FC. Mgambo iliyokuwa ikihitaji ushindi kwenye mchezo wa leo imejikuta ikishindwa kupata ushindi kwa mara nyingine mbele ya Azam ambao sare hiyo imewafanya wamalize kwenye nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Yanga.

Simba waliokuwa wakiwania nafasi ya pili wamechapwa na Ruvu JKT na timu hiyo iliyo chini ya kocha wa zamani wa Simba King Kibadeni imenusurika kushuka daraja.

Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi

$
0
0
Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MEDIA ambayo ipo chini ya Reginald Mengi.
Wanachama na mashabiki wamefikia hatua hiyo baada ya kukasirishwa na kitendo cha Reginald Mengi kutumia vyombo vyake vya habari kuandika habari za uongo na uchochezi kuhusu Yusuph Manji ili kuivuruga Yanga. Mengi ambaye pia ni mwanachama wa Yanga anaonyesha kutofurahishwa kwake na uwepo wa Manji katika klabu ya Yanga.


SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 23, Ikiwemo ya Spika Afichua Wabunge Wavuta Bangi na Unga

$
0
0


SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 23, Ikiwemo ya Spika Afichua Wabunge Wavuta Bangi na Unga

Watumishi HEWA Waziponza Benki...Benki za Dar es Salaam Zalimwa Barua Kurejesha Mamilioni ya Shilingi

$
0
0
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametoa siku 21 kwa benki zilizokuwa zikitumika kuweka mishahara ya watumishi hewa, kurejesha fedha hizo serikalini ; au kubainisha waliokuwa wakitumia akaunti hizo, kuchukua fedha.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Makonda alisema benki ndio pekee wanaoweza kusaidia mkoa, kutambua wahusika waliokuwa wanatumia akaunti hizo pamoja na wale waliokuwa wanachukua fedha hizo.

Alisema watu hao wasipopatikana, inamaanisha fedha bado zipo katika benki hizo, hivyo zinapaswa kuzirudisha serikalini zifanye maendeleo kwa wananchi.

“Tayari tumeshaziandikia benki hizo barua na kuwapatia majina na akaunti na kuwataka kutuwasilishia majina ya wahusika, waliohusika na akaunti hizo ili kusaidia kutambua mtandao mzima wa wahusika wa suala la watumishi hewa ambao wameigharimu serikali,” alisema Makonda.

Alitaja benki hizo pamoja na fedha wanazodai kuwa ni benki ya NMB ambayo inadaiwa zaidi ya Sh bilioni mbili, CRDB zaidi ya milioni 400, NBC zaidi ya milioni 141, DCB milioni 85, Standard Chartered zaidi ya Sh milioni mbili na Community Benki zaidi ya milioni 100.

“Hakuna mtu anayeweza kutumia akaunti ya mtu bila kufuata taratibu za kibenki, hata kama mtu amefariki kuna taratibu za kufuata ndipo apate akaunti, naamini benki hizi zitasaidia kuwatambua wahusika wote,” alisisitiza.

Aidha, alizitaka benki hizo kufunga huduma za akaunti hizo ;na zisifanye malipo yoyote mpaka fedha hizo zitakapopatikana.

Mpaka sasa, Mkoa wa Dar es Salaam umebainika kuwa na watumishi hewa 283, ambao wanadaiwa kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 3.6 ambazo zilitumika kuwalipa mishahara.

Jamaa Aliyejitosa Zoo Aliwe na Simba Laivu Alikuwa Anadai Mwisho wa Dunia Umefika...

$
0
0
Inasikitisha kwakweli, ameokolewa.... na simba walioanza kumla waliuwawa. aliingia kwenye jumba la simba akavua nguo na kuwadandia badae akachenjiwa...kwenye nguo zake kimekutwa kikaratasi-suicide note...kwamba mwisho wa dunia umefika kwahiyo anajiwahi.....ana miaka 20...inaonekana alikua muumini maana alikua akimtaja yesu....walioshuhudia wamesema....nchini Chile.


TanzaniteOne Yamvaa Mbunge James Ole Millya, Yamtuhumu Kupotosha Bunge na Umma Bila Kufanya Utafiti

$
0
0
Lema Akiwa na  James ole Millya
KAMPUNI ya Sky Group Associates inayomiliki mgodi wa tanzanite wa TanzaniteOne, imesema Mbunge wa Simanjiro, James ole Millya amepotosha Bunge na umma juu ya suala zima la ununuzi wa hisa kwa kampuni hiyo.

Akichangia bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini mwishoni mwa wiki, Millya alisema Sky Group Associates iliyonunua hisa kwa Kampuni ya TanzaniteOne na kumiliki kitalu C Mirerani wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara, haikufuata taratibu za ununuzi wa hisa hizo na kuwatuhumu baadhi ya mawaziri kuwa walihusika katika kupindisha taratibu.

Aliwataja mawaziri hao kuwa ni George Simbachawene na Jenista Mhagama, ambaye hata hivyo alikanusha madai hayo ; na ametaka taratibu za Kibunge zimlamzishe Millya, kukanusha au kuthibitisha madai yake.

Mbali ya hilo, mbunge huyo aliituhumu kampuni hiyo kwa kuwafukuza kazi wafanyakazi 201, bila ya kufuata utaratibu na kwamba inawanyanyasa .

Akizungumza na mwandishi wetu, Mwanasheria wa kampuni hiyo, Kisaka Mnzava alisema uongozi umesikitishwa na kauli ya Millya, kwa kusema alitoa kauli bila kufanya utafiti wa kina.

Mnzava alimtaka mbunge huyo, kujiridhisha kwa kufanya utafiti wa kina namna hisa za TanzaniteOne zilivyouzwa kwa Sky Group, inayomilikiwa na wazawa kwa asilimia 100.

Alisema wamiliki wa hisa wanajulikana na kama anahitaji kuwafahamu, anapaswa kwenda Mamlaka ya Usajili wa Leseni za Kampuni (Brela) kujiridhisha.

Alisema hakuna waziri wala kiongozi yeyote mwingine wa serikali, anayemiliki hisa katika Sky Group Associates.

Alisema kampuni imeshalipa kodi yote ya serikali, na kampuni hiyo sio ya mfukoni, kama anavyodai mbunge huyo.

Mnzava alisema shughuli za uzalishaji zinasimamiwa kikamilifu kati ya Sky Group na serikali kupitia Shirika la Madini la Taifa (Stamico), ambao ni wabia wa mgodi huo, na kwamba hakuna madini yanayoibwa kama mbunge huyo alivyosema.

Alisema hakuna njia ya mkato, iliyofanywa katika ununuzi wa hisa ; na hakuna waziri yeyote aliyehusika katika kusaidia kupindisha taratibu, kwani kila kitu kipo wazi.

Alisema Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu), Jenista Mhagama hana ndugu na mtu anayefanya kazi TanzaniteOne.

Akizungumzia kufukuzwa kwa wafanyakazi 201, mwanasheria huyo alisema waliofukuzwa kazi ni wafanyakazi hatari kwa mustakabali wa kampuni, kwani ni wachochezi na wenye hila za kutaka kuihujumu kampuni hiyo ili ilete maafa.

Alisema kugoma ni kosa kisheria na kama mgomo haukufuata taratibu, sheria lazima zichukue taratibu.

Msichana Azitanulia Dola Milioni 3.3 Alizowekewa na Benki Kimakosa

$
0
0
Msichana mwenye umri wa miaka 21 na raia wa Malaysia, aliyezitanulia dola milioni 4.6 za Australia ambazo ni takriban dola milioni 3.3 za Marekani alizowekewa kimakosa na benki, anadai alidhani aliwekewa kwenye akaunti yake na wazazi wake ambao nao ni matajiri.


“Wazazi wangu hunipa hela nyingi sana,” anasema Christine Lee Jia Xin kwenye utetezi wake kuhusu swali la kwanini alidhani anaweza kuwa na fedha zote hizo,” gazeti Sydney Morning Herald limeripoti Jumapili ya May 22.

Lee anadaiwa kutumia mamilioni kwa kununua mikoba ya gharama kubwa, vidani vya thamani, nguo pamoja na kupanga kwenye nyumba za kifahari kwa miezi 11 kuanzia 2014 na 2015 kwa kutumia fedha alizowekewa kimakosa na benki ya Westpac. Katika tukio moja msichana huyo alitumia  A$300,000 kwa siku.

Benki hiyo ilikuja kugundua kosa lake pindi Lee alivyohamisha $1.15m kwenda kwenye akaunti yake ya PayPal kwa malipo ya mara 14 kwa siku moja April 7 mwaka jana, Herald limeandika.

Msichana huyo anadai sasa amebakiza A$4,000 tu.

Mwanafunzi huyo wa mwaka wa tatu wa kozi ya chemical engineering alishtakiwa May 5 mwaka huu kwa kupata fedha hizo kimakosa na kukaa kimya. Lee Jiaxin alikamatwa na polisi akijaribu kuondoka na ndege kwenda kwao Malaysia kwa passport ya dharura.

Westpac ilipewa mamlaka na mahakama mwaka jana kukamata mali zake zote, kumtangaza amefilisika na kuchukua hati yake ya kusafiria. Benki hiyo iliweza kuwapata PayPal wakarudisha A$1.15m.

Baada ya Lee kuacha kwenda mahakamani wala kupokea simu, polisi walitoa hati ya kukamatwa March 6, 2016.

Boyfriend wa msichana huyo, Vincent King alimwekea dhamana ya $1,000 kumtoa jela baada ya kukamatwa May 4. Anadai hakujua kilichokuwa kikiendelea kwa mpenzi wake.

Hakimu amedai itakuwa ngumu kumshtaki kwa kosa la jinai kutokana na benki kumpa yenyewe fedha hizo.

Picha: Nyota Ndogo Afunga ndoa na Mchumba wake Raia wa Denmark

$
0
0
Muimbaji wa Kenya, Mwanaisha Abdalla maarufu kama Nyota Ndogo amefunga ndoa weekend hii.

Muimbaji huyo wa ‘Watu na Viatu’ sasa ni mke halali wa mchumba wake Henning Nielsen raia wa Denmark.

“My great day love you all
I thank Allah
#wedding
#love
#world,” ameandika.

Nyota Ndogo mwenye makazi yake mjini Mombasa ameshare picha hizo akiwa na mume wake kwenye Instagram.

“I love my husband Henning Nielsen
#myday
#we,” ameandika kwenye picha nyingine aliyoipost kwenye mtandao huo.


Muimbaji mwenzake wa Kenya, Akothee amempongeza kwa kuandika: akotheekenya Congratulations mrembo I wish you a happy life with your family @nyota_ndogo.”

Huyo anakuwa mume wake wa pili baada ya kuachana na mume wake aliyezaa naye watoto wawili.

Usiyoyajua Kuhusu Bia ya Tanzania Iliyopachikwa Jina la Utani la ‘Ukawa’

$
0
0
 “Nipatie Ukawa hapo”, “lete Ukawa chapu chapu” hayo ni maneno utakayoyasikia siku hizi ukiingia baa mbalimbali za mtaani jijini Dar es Salaam.

Mbali na maneno hayo pia utawasikia vijana wakisema, “Naenda kujiunga, najiunga cha buku (Sh1, 000) halafu nakuja”. Kama huelewi wanachozungumza wanywaji hao, unaweza kujiuliza Ukawa ni nini au mtu anapoenda kujiunga anajiunga na nini.

Ukisikia baa watu wanasema leta Ukawa basi ujue hiyo ni bia aina ya Pilsner Lager na ukisikia mtu anaenda kujiunga ujue basi anaenda kunywa bia aina ya Eagle Draught, ambayo wateja hukinga glasi kwenye mtungi maalumu.

Kwa nini inaitwa Ukawa?
Watumiaji wa kinywaji hicho wanaeleza kwamba ni kutokana na gharama yake kuwa nafuu na ndiyo maana inaitwa jina hilo ambalo ni maarufu kutokana na Umoja wa Katiba ya Wananchi, unaojumuisha vyama vinne vya upinzani vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD.

Wanaeleza kuwa kutokana na Ukawa sera yao kuwa ni mabadiliko na maisha nafuu kwa wananchi na Pilsner inauzwa Sh1,500 tofauti na bia nyingine zenye ujazo sawa zinazoanzia Sh2,300 na kuendelea, wanaona imekuwa nafuu kubwa kwao na ndiyo maana wakaiita Ukawa.

“Hii bia bwana ni nzuri na ni nafuu, yaani hawa jamaa wametufaa sana na ndiyo maana tunaiita Ukawa kwa kuwa inatia matumaini kwa kutupunguzia gharama za unywaji,” alisema Kiongozi Njau alipokuwa akijipatia bia ya yake ‘Ukawa’.

Njau na wenzake ambao walikuwa wamejaza chupa za Pilsner mezani huku wakipiga kelele na kueleza furaha yao kuwa bei hiyo ya Sh1,500 ambayo ni rahisi kuimudu inawapunguzia mzigo wa kunywa vinywaji ambavyo havina kiwango.

Ilianzaje kuitwa Ukawa?
Njau alisema wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana mmoja wa wagombea wa Ukawa, mkoani Kilimanjaro aliingia baa na kutaka kuwanunulia kinywaji watu waliokuwapo katika baa hiyo.

“Sasa huyo jamaa akajiuliza hawa wako wengi nitawanunulia bia ipi ambayo haina gharama sana, ndiyo akanunua Pilsner zikawekwa mezani, basi wanywaji wakaanza kuimba Ukawa, Ukawa, Ukawa, ndiyo ikawa hivyo tena hadi leo inaitwa Ukawa,” alisema.

Victor Temba, mnywaji mwingine wa bia hiyo alisema, “ukiwa na Sh10,000 unakunywa Ukawa zako sita na unabakiwa na ‘buku’ (Sh1,000) au ukiwa na Sh5,000 unakunywa zako tatu na ‘jelo’ (Sh500) linabaki la nauli, unataka nini tena?

Alisema wameiita Ukawa kwa kuwa ni bia ambayo wananchi wanaweza kumudu kuinunua.

“Sijui hicho kiwanda kilifikiria nini? Yaani kimeileta wakati muafaka kama vyama vya Ukawa vilivyojiunga na kutupa matumaini wakati wa kampeni,” alisema Temba.

Mmoja wa wauzaji wa bia hiyo eneo la Mabibo External jijini Dar es Salaam, Dickson Mwarabu alisema Ukawa inanyweka na watu wa ngazi tofauti tofauti.

“Ninauza Ukawa kama sina akili nzuri, inapendwa kwa kuwa ni nafuu na iko vizuri. Mimi mwenyewe huwa naipiga ikifika jioni. Hainitii hasara katika faida ninayopata kila siku,” alisema Mwarabu.

Ofisa uhusiano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ambayo ndiyo inazalisha Pilsner, Abass Abraham alisema bidhaa hiyo imesajiliwa kwa jina la Pilsner, hivyo kama watumiaji wameamua kuipa jina lao ni sawa, lakini kisheria na kibiashara jina la bidhaa hiyo litabaki kuwa Pilsner.

Alisema bia hiyo inauzwa Sh1,500 na inatengenezwa kwa asilimia 100 na malighafi za ndani.

“Tunajivunia ubora na ladha ya Pilsner. Ni bia pekee Tanzania inayotengenezwa kwa kufuata utaratibu ulioanzia Jamhuri ya Czech mwaka 1840,” alisema Abraham.

Wanaojiunga je?
Wakati wateja wa SBL wanafurahi na Ukawa, wenzao wa Tanzania Breweries Ltd (TBL) wanafurahia “kujiunga” kwa kunywa bia ya Angle Draught inayouzwa Sh500 kwa glasi.

Vinnie Msewa alisema kuwa kutokana na bia hiyo kuuzwa kwa kupimwa, wanaweza kupata kipimo cha Sh500 kwenda juu, hivyo ni rahisi kwao kuimudu.

“Naenda kujiunga kaka baada ya hapo nitapiga Ukawa mbili mambo yanakuwa poa,” alisema.

Hata hivyo wauzaji wa bia hiyo hawakupenda kuzungumzia jinsi wanywaji wanavyojiunga kwa kupata vipimo vya kinywaji hicho.

Meneja Masoko wa TBL, Fimbo Butallah alisema bia hiyo huzalishwa na kuwekwa kwenye mitungi ambayo imeondoa gharama ya kuweka kwenye chupa, ndiyo maana wanywaji huweza kuipata kwa bei rahisi.

“Tulifanya utafiti tukagundua watu wengi wanatamani kunywa bia, lakini hawana uwezo wanaishia kunywa vinywaji visivyo halali kama gongo,” alisema Butallah.

Alisema baada ya utafiti huo waliamua iwe inauzwa kati ya Sh600 kwa glasi ya ujazo wa mililita 300 na kwa mililita 500 ni Sh1,000 jijini Dar es Salaam ambako kwa mtu hupata kinywaji hicho kwenye glasi kwa gharama nafuu.

“Imewasaidia watu kuacha kunywa vinywaji visivyo halali. Tumewaangalia watu wenye kipato cha chini. Bia hii inatengenezwa asilimia 100 na mtama unaolimwa hapa Tanzania,” alisema.

Wenye Ukawa wanasemaje?
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Chadema, Tumaini Makene akizungumzia suala la bia hiyo kuitwa Ukawa alisema, “Kwanza inaeleza kuwa Ukawa inaongoza na CCM inatawala kwa kuwa ukiongoza watu unaishi kwenye mioyo na akili zao.” Alisema Ukawa ilipofikia leo iko kwenye mioyo ya watu na akilini mwao.

“Kwa namna wananchi walivyokata tamaa, wamepata matumaini na Ukawa kwa kuwa iko mioyoni mwao. Inaonyesha Ukawa iko juu.”

Makene alisema ni watu kutafuta uhafadhali wa mambo katika maisha. “Tunafurahi kuwa kuonwa sisi ndiyo tumaini lao yaani wanaona Ukawa ndiyo wenzao.”

Mawaziri na Wabunge Wamiminika Kumpa Pole Kitwanga

$
0
0
Wabunge mjini Dodoma wamiminika nyumbani kwa aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Charles kitwanga ,mawaziri na wabunge wamechukua hatua ya kwenda kumuona aliyekuwa waziri mwenzao na alisikika waziri mmoja akisema kuwa

" hili si jambo la kucheka kwani hii ni kama ajali ya kisiasa iliyomtokea mwenzetu kwani toka atenguliwe nafasi yake hayuko sawa lakini tunaimani atakuwa sawa tu, ndiyo maana tumekuja kumpa pole na kumfariji" alisikika waziri mmoja.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images