Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live

Taarif ya Evra kujiunga na kikosi cha Man u

$
0
0
Moja ya story ambazo hazikutegemewa sana ni story za kwamba Patrice Evra atajiunga na Manchester united club ambayo amecheza kwa muda mrefu na kupata mafanikio.
 
Ukweli ni kwamba Evra atasepa Juventus lakini sio kwa ajili ya kwenda kucheza Manchester United. Wakala wake Federico Pastorello amesema kwamba sio swala la kuficha kwamba Evra ataondoka Juventus, tutaona ndani ya siku chache zijazo.

Habari zinasema kwamba Manchester United inaweza kumpa Evra nafasi ya kuanza career ya kuwa kocha. Inategemewa kwamba mwishoni mwa msimu huu ndio itakua mwisho wake na ataacha kucheza soka la mashindano.

Uhusiano wake mzuri na Paul Pogba na Antoine Griezmann unampa sababu nyingi Evra kuwa kwenye timu ya Jose Mourihno. Griezmann bado ni chaguo la Jose Mourihno na pia kuna mchezaji gani ambaye hatapenda kuanza kuwa kocha akiwa chini ya Jose Mourihno kocha mwenye mafanikio.

Azam ayapewa ubingwa kombe la Mapinduzi 2017

$
0
0
Wakati michuano ya Kombe la Mapinduzi ikiingia katika hatua ya nusu fainali huku bingwa mtetezi timu ya URA ya Uganda wakifungashwa virago, tayari timu ya Azam imetabiriwa kuchukua ubingwa wa michuano hiyo kwa mwaka huu.
Kikosi cha Azam FC

Mtu wa kwanza kufanya hivyo ni nahodha wa URA, Jimmy Kulaba, ambaye amesema kuwa baada ya wao kutupwa nje, timu pekee yenye uwezo wa kunyakua kombe hilo mwaka huu ni Azam FC ya Dar es Salaam.

Jimmy alitoa utabiri wake jana usiku mara baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Taifa Jang'ombe ambao ulimalizika kwa URA kufungwa bao 1-0, na kuvuliwa rasmi ubingwa wa micuano hiyo.

Jimmy amesema kwa jinsi alivyokiona kikosi cha Azam kilichoshinda mabao 4-0 dhidi ya Yanga, anaona hakitakuwa na mpinzani katika timu zote nne zilizotinga nusu fainali.

Jimmy Kulaba

"Azam wa kikosi kizuri, wachezaji wake ni wazoefu, wanajitambua na wako serious na kazi, natamani kuona Azam wanakuwa mabingwa wa Mapinduzi"

Azam wanakutana na Taifa Jang'ombe katika moto wa nusu fainali ya kwanza utakaopigwa kesho Jumanne saa 10 jioni, wakati mchezo wa pili wa nusu fainali utazikutanisha Simba na Yanga saa 2 usiku.
Je, utabiri huu utatimia, tusubiri

Rais Magufuli Atembelea ''Kijiwe Chake'' Chato Kuongea na Mafundi Viatu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika benchi la kibanda cha kupigia kiwi (Shoe Shine) pamoja na wakazi wengine wa Chato katika eneo maarufu kama Stendi za zamani Chato mkoani Geita. Kibanda hicho cha Kiwi ndicho Rais Dkt. Magufuli alichokuwa akisafishiwa viatu vyake kabla ya kuwa Rais, pia ni sehemu ambayo alikuwa akipenda kukaa na kubadilishana mawazo na wakazi wa Chato wakati akiwa mapumzikoni kipindi cha Nyuma.

Rais ameongea na ''vijana wa kijiwe'' kuhusu hali ya maisha na matarajio yao katika utawala wake.

''Vijana wa kijiwe'' wamemshukuru sana kwa kuwatembelea na ''kupiga story'' lakini pia wameshangaa sana kwa sababu hawakutegemea kama angeweza kuwatembelea tena baada ya kuchaguliwa kuwa Rais wa Tanzania.

Wamemuomba asiache kuwatembelea kila anapopata nafasi ya kufika Chato ili waendelee kumueleza hali halisi ya maisha na mafanikio yao kama walivyokuwa wanafanya kabla hajachaguliwa kuwa Rais wa Tanzania.

Rais amewaambia serikali yake inafanya kila linalowezekana ili kuwajengea mazingira bora zaidi ya kupata kipato halali lakini pia waendelee kuchapa kazi halali.

Video: Udhalilishaji wa Mwanamke Kuchapwa Viboko Hadharani na Wanaume, Serikali ichukue Hatua

$
0
0
Nimeiona hii clip ikizunguka mitandaoni.Inamuonyesha mwanamke wa makamo ya kati akitandikwa viboko vya kutosha tu makalioni na wanaume wenye nguvu zao.

Inaonekana ni "adhabu" dhidi ya mwanamama huyu,hata anapotaka kupinga kuchapwa;Wazee wa Kimila wanaamuru vijana waje wamkamate ili atege kalio na achapwe sawasawa.

Lafudhi za wazee hawa inaonekana ni wale wa "Kanda Maalumu".Huu ni ukatiri mkubwa sana dhidi ya akina Mama.Katika zama hizi kumchapa mwanamke viboko,tena vya makalio kwa idadi kubwa,si ni udhalilishaji tu,bali ni unyama na kinyume cha haki za binadamu.

Kuna wizara mtambuka,Kama Wizara ya Mambo ya Ndani ya ndugu yangu Mwigulu Nchemba pia Wizara ya Dada Ummy Mwalimu na Kituo cha Haki za Binadamu cha Madam Hellen Kijo Bisimba.Likemeeni jambo hili na wahusika wachukuliwe hatua na iwe fundisho kwa wengine wenye mila hizi za ajabu ajabu.

Haya Hapa Maisha Magumu Ya Ney Wa Mitego

$
0
0
Kisa cha NEY WA MITEGO kulala saluni miaka mitatu na kijue kisa cha NEY WAMITGO kutolipa nauli kutoka mbeya kuja dar. 

Tazama Video:

Download Application ya UDAKU SPECIAL Kwenye Simu yako Kutoka Google Play Kusoma Habari Kirahisi

$
0
0
Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 


Au Kama Unayotayari Bonyeza Hapa Ku Update Uweze Kupata Ikiwa na Muonekano Mpya

Hiki ndicho kinamliza Aika wa Navy Kenzo

$
0
0
Zikiwa zimeshapita siku kadhaa toka kundi la Navy Kenzo waweze kuipeleka mtaani Album yao ya 'AIM' amabayo ina jumla ya ngoma 11 wasanii hao wameonyeshwa kusikitishwa na kuvunjwa moyo na baadhi ya watu ambao wamekuwa wakizivujisha ngoma hizo

Watu waliowanyooshea vidole zaidi ni Bloggers ambao wamekuwa wakichukua nyimbo zao kwenye Album na kuziweka kwenye mitandao ya kijamii.

Akizungumza kwenye kipindi cha Bongo fleva Top 20 Aika alisema kitendo cha baadhi ya watu hususani bloggers kuchukua nyimbo hizo kwenye album na kuziweka mitandaoni kinakuwa kinawavunja moyo kwani kinasababisha biashara yao kupunguza kasi na kuharibu mauzo ya album hiyo mtaani.

Mbali na hilo Aika alisisitiza kuwa anatambua bloggers huenda wanajua wana wa'support' kwa ku-upload nyimbo hizo kwenye mitandao ya jamii ili kusaidia album kuuzika lakini huenda wengine hawajui kile wanachofanya kinawaharibia wao soko la album yao mtaani.

MaDj Wa Sauzi Waufagilia Muziki Wa Bongo

$
0
0
Siyabonga Sibeko ‘DJ Capital’ (kushoto) na Lutendo Kungoane ‘Dj Sliqe’ (kulia) wakizungumza na Waandishi wa Habari jana

WACHEZESHA disko ‘ma DJ’ maarufu Afrika Kusini Siyabonga Sibeko ‘DJ Capital’ na Lutendo Kungoane ‘Dj Sliqe’ wamesema kwamba muziki wa Tanzania uko juu kwa sasa.

Wakizungumza na Waandishi wa Habari jana katika hoteli ya New Africa, Dar es Salaam ma DJ hao wa Redio na Telesheni nchini Afrika Kusini walisema Tanzania imepiga hatua kubwa kimuziki.

“Kwa sasa huwezi kuzungumzia nchi zinazofanya vizuri kwa kiwango cha juu kimuziki Afrika bila kuitaja

Tanzanja,”alisema Dj Capital na kuongeza; “Afrika Kusini, Nigeria, Ghana, Tanzania na Kenya hizo ndizo nchi za Afrika zinazofanya vizuri katika muziki wa kisasa,”alisema.

Kwa upande wake DJ Sliqe’ alisema kwamba anavutiwa zaidi na wasanii wawili wa Tanzania kwa sasa, ambao ni Diamond Platnumz na Vanessa Mdee.

“Ni wasanii wengi wa Tanzania wanaofanya vizuri kwa sasa, lakini mimi upande wangu nawapenda zaidi hao wawili,”alisema.

Wawili hao, wote ni Ma DJ wa kituo cha Redio cha Touch Central cha Johannesburg, Afrika Kusini wakati DJ Capital pia anafanya kipindi cha Club 808 cha Televisheni ya ETV nchini humo.

Wawili ambao wamekuja nchini kwa ziara ya wiki moja kujifunza zaidi kuhusu muziki wa Tanzania, pia ni Ma DJ wa kumbi za disko nchin kwao.

“Tumekuja hapa kujigunza na kukutana na wasnaii kwa sababu sisi pia ni watayarishaji wa muziki,”alisema Capital.

Video: Mtazame Rais Magufuli Akifurahi na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Chato Alikosoma

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amefanya ziara ya kushtukiza katika Shule ya Msingi Chato,ambapo ndipo aliposoma kuanzia darasa la kwanza hadi la saba na kuzungumza na walimu na wanafunzi wa shule hiyo.

Tazama  Video hii kuona ilivyokuwa

Video: Eric Omondi alivyoirudia Movie ya ‘The Gods must be crazy’

$
0
0
Eric Omondi ni mchekeshaji kutoka Kenya ambaye anakupa uhakika wa kucheka  ukimsikia au kumtazama

Msanii huyu kairudia movie ya ‘The gods must be crazy’ na ameeiita ‘The Gods are not crazy we are’.

Itazame hapo chini

Hatua 10 za Kumchagua Mchumba

$
0
0
Wengi wamejikuta wakiitwa wahuni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na makundi ya wanaume au wanawake. Hata hivyo wachunguzi wa masuala ya mapenzi wanasema idadi kubwa ya wapenzi si kigezo sahihi cha kupima tabia ya mtu na kumhusisha na uhuni.

Watalaam hao wanataja safari ya kupata chaguo halisi la mwanaume/mwanamke wa maisha ndiyo inayowaponza wengi kiasi cha kujikuta wameingia katika kashfa ya kuwa na uhusiano na dazeni ya wapenzi.

Wanasema msichana/mvulana anayeingia katika uwanja wa mapenzi kwa kuwa na hisia za kufanya ngono, hukosa umakini wa nani anafaa kuwa mpenzi wake kutokana na kukosa elimu ya uhusiano kutoka kwa wazazi wake.

Kwa mantiki hiyo, bila upembuzi wa kina, mtu asiye na elimu ya jinsi ya kumpata mpenzi wa kweli hujikuta ameangukia kwa mwanaume/mwanamke asiyemfaa, ambapo baadaye huamua kuachana na huyo na kwenda kwa mwingine kujaribu bahati tena ya kupata penzi la kweli.

Zinatajwa zawadi, hitaji la kusaidiwa kimaisha, mvuto wa kimahaba na mazoea kuwa ni vichocheo vinavyowaangusha wengi kwenye mapenzi na wasiowafaa.

Ukweli ni kwamba mtu aliyenaswa kwa ‘ujinga’, huwa hakatwi kiu ya penzi na mwanaume/mwanamke asiye chaguo sahihi la maisha yake. Hivyo hufikia maamuzi ya kujiingiza katika uhusiano mpya mara 2,3,4,5 na kujikuta wakiambulia wanaume/wanawake wale wale wasio sahihi kwake.

Mwanamnke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Suzzy aliwahi kuniomba ushauri, akasema amechoka kuchezewa, maana kila mwanaume anayempata anakuwa si chaguo lake. Lakini kibaya zaidi kuachia ngazi au kutemwa huku akiwa tayari ameshafanya mapenzi na wanaume hao.

Nia ya swali lake ilikuwa ni kuniomba njia za kumtambua mwanaume mkweli bila kufanya naye mapenzi? Aliuliza hivyo huku akiwa na hoja kuwa wanaume wengi hawako tayari kuwa na uhusiano na msichana bila kufanya naye mapenzi na wakati huo huo huficha tabia zao chafu wakilenga kumnasa wamtakaye.

Binafsi nafahamu kuwa kuna wanawake/wanawake wengi ambao hujiingiza katika mapenzi kwa kutekwa na hadaa za mwili na kujikuta wanacheza mchezo wa kitoto wa pata potea.

Ni madhumuni ya somo hili kufundisha vigezo vya kumpata mwanaume/mwanamke halisi wa maisha, bila kufanya naye mapenzi. Njia hii ina faida kwa pande zote mbili yaani kwa mwanamke na mwanaume kwani kuacha au kuachwa bila kufanya mapenzi ni bora kuliko kuwa muonjaji, tabia ambayo huathiri kisaikolojia na ni hatari kwa afya.

Ifuatavyo ni njia ya kisaikolojia ambayo mwanamke anaweza kutumia kumpata mwanaume mwenye kumfaa bila kufanya naye mapenzi tena ni jibu sahihi la kuondokana na mchezo wa kubahatisha kwa wanaume wanaosaka wapenzi wa kweli na si taksi bubu ambazo mchana huweka namba za njano usiku nyeusi.

KWANZA- Ni ya mwanamke/mwanaume mwenyewe kujifahamu na kufahamu vigezo vya mpenzi anayemhitaji katika maisha yake. Ifahamike kuwa kila mwanaume ana wake na kila mwanamke anaye wake wa maisha pia. Hivyo asiyekufaa wewe anawafaa wengine, kinachotakiwa ni wewe kujitambua kwanza ili umtambue umtakaye.

Wanawake/wanaume wengi hawafahamu wanahitaji wapenzi wa aina gani, hivyo wanajikuta kama watu wanaoingia sokoni bila kujua wanataka kununua nini? Ndiyo maana wengi wameangukia kwa matapeli wa mapenzi, wakachezewe na kuumizwa moyo bure.

PILI- Ni kuketi chini na kuorodhesha vigezo stahili vya mwanaume/mwanamke unayemtaka. Baada ya hapo orodhesha tena kasoro za mwanaume/mwanamke unazoweza kuzivumilia na zile ambazo huwezi kuzivumilia kabisa. Hii inatokana na ukweli kwamba mwanadamu hajakamilika, ana upungufu wake.

TATU- Anza kumsaka kwa kutumia milango ya fahamu. Cha kufanya hapa ni kuruhusu macho yawaone wanaume/wanawake na kuwatathmini kwa maumbile yao ya nje na kisha kupata majibu kutoka moyoni juu ya kuvutia kwao ambako hutambulika kwa moyo kurithika na mwili kusisimka.

NNE - Kuanzisha safari ya kuchunguza tabia za nje na za ndani kivitendo. Hapa suala la ukaribu baina ya mwanaume na mwanamke linahitajika. Msingi unaotajwa hapa ni kujenga mazoea ya kawaida yasiyokuwa na masuala ya kimapenzi na ngono. Kutambuana, dini, viwango vya elimu, kabila na makundi ya marafiki ni mambo ya kuzingatia.

Katika uchunguzi huu mwanamke/mwanaume anayetafuta mpenzi hana budi kupitia na kumlinganisha huyo aliyempata na vigezo alivyojiwekea. Zoezi hili liendane na kuweka alama ya pata kila anapobaini kuwa mwanaume/mwanamke anayemchunguza amepata moja ya vigezo vyake. Lakini pia aweke alama ya kosa kwa kila kasoro anayoivumilia na ile asiyoivumilia.

TANO - Ajipe muda wa kutosha kati ya miezi sita na mwaka kumchunguza huyo mwanaume, kisha aketi chini na aanze kujumlisha alama za vigezo alivyovijiwekea na jinsi mwanaume huyo alivyopata au kukosa.

Ikibainika mwanaume aliyechaguliwa amepata zaidi ya nusu ya alama ya vigezo vilivyowekwa, basi ujue kuwa anafaa. Kuhusu alama chache alizikosa anaweza kusaidia kuzikamilisha polepole wakati wa maisha ya ndoa.

Lakini angalizo kubwa kabisa ni kwamba mwanaume/mwanamke akionekana kuanguka katika kasoro zisizoweza kuvumilia kwa zaidi ya alama tatu. Yaani kwa mfano ni mlevi, mwizi, muongo, mbishi na katika hizo kashindwa 3, huyu hafai, ni vema akawekwa kando kwani huwezi kubeba kero 3 kwa pamoja katika maisha.

SITA - Kusajili mapenzi yenye malengo yanayotekelezeka. Lazima baada ya kuchunguzana kwa kina wapenzi watengeneze muongozo wa mapenzi yao. Wasiwe kama wanyama, lazima mipango ya wapi wametoka walipo na wanapokwenda.

Hata hivyo watalaam wanasema lazima wapenzi wapime umakini wao kwa vitendo. Kama wamekubaliana kuoana, suala la mume kwenda kujitambulisha kwa wakwe na hatua ya kuiendea ndoa ionekane. Usiri usiwepo tena. Kila mmoja amuone mwenzake kama sehemu ya maisha yake na mara zote wasaidiane kwa ukaribu.

SABA - Ni vema ndugu wakashirikishwa ili kuwapa nafasi na wao ya kuamua kama mapenzi hayo ni budi yakaendelea au yakasitishwa. Ni ukweli ulio wazi kwamba licha ya wengi kupuuza maamuzi ya ndugu kwa madai ya kuwa hawana nafasi kwa wapenda nao, lakini uchunguzi unaonesha kuwa wapenzi wengi huacha kutokana na sumu za ndugu hasa pale wanapokuwa wameonesha kutounga mkono uhusiano wa wanaotaka kuoana

NANE - Hatua hii ni ya kuweza kuzungumzia ufanyaji mapenzi, hapa nina maana kama wapenzi wamejizuia kwa muda mrefu na wanahisi kuchoka wanaweza kujadiliana kuhusu hilo na kuamua ufanyaji huo wa mapenzi una lengo gani, kama ni kuburudisha miili basi suala la afya na uzazi salama litazamwe.

TISA - Kutimizwa kwa ahadi ya kuoana ni hatua ya tisa ambayo nayo si busara ikachukua muda mwingi kutekelezeka, kwani ucheleweshaji mwingi wa ndoa nao huvunja moyo na mara nyingine umewafanya wengi kutoaminiana.

KUMI - Kuamua kuwa mwili mmoja kwa kuvumilia na kuwa tayari kukabiliana na changamoto zote za maisha ukiwemo mkwamo na dhiki ambazo huchangia sana ndoa nyingi kuvunjika. Hapa pia ni wajibu wa wanandoa kuchukuliana udhaifu na kusaidia, kuwa tayari kujifunza na kujali zaidi upendo kuliko hisia za mwili ambazo wakati mwingine hudanganya na hivyo kumfanya mwanandoa asivutiwe na mwenzake.

Mwisho ni kwamba kanuni hizi huwafaa watu wazima mapenzi ya kitoto hayawezi kujenga misingi hii imara mara nyingi ni kudanganyana, kuharibiana maisha, kupeana mimba na maradhi.

Wafanyabiashara ya ‘Unga’ Wabadili Mbinu

$
0
0
Wafanyabiashara wa dawa za kulevya wamebuni mbinu mpya kwa kusafirisha na kuingiza nchini, vibashirifu (kemikali zinazotumika kutengeneza dawa ya kifua) aina ya ephedrine kisha kuvitumia kutengeneza kokeni na heroini.

Kamanda wa Polisi, Kikosi cha Dawa za Kulevya, Mihayo Msikhela alisema jana kwamba wafanyabiashara hao husafirisha kemikali hizo kutoka Bara la Asia na wanapozifikisha nchini huzitumia kutengeneza dawa hizo za kulevya.

“Hivi vibashirifu aina ya ephedrine mara nyingi vinatumika kutengenezea dawa za kifua lakini hawa wafanyabiashara haramu wanabadilisha mfumo wake. Wanachofanya wanachanganya na kemikali nyingine ambazo wanatengeneza dawa aina ya heroini na kokeni,” alisema.

Pia, alisema wafanyabiashara hao hununua kemikali hizo bila kuwa na kibali cha Serikali na hudanganya kuwa zitatumika kutengeneza dawa za kifua

Askofu Mokiwa Aendelea Kung’ang’aniwa

$
0
0
Mvutano wa uongozi katika Kanisa la Anglikana, umechukua sura mpya baada ya Askofu Mkuu wa kanisa hilo, Dk Jacob Chimeledya kutishia kuweka hadharani nyaraka zinazoonyesha ubadhirifu anaodaiwa kufanya Askofu wa Kanisa hilo Jimbo la Dar es Salaam, Dk Valentino Mokiwa, endapo ataendelea kung’ang’ania madarakani.

Dk Chimeledya alibainisha kuwa iwapo Dk Mokiwa ataendelea kung’ang’ania madarakani, ataweka hadharani mambo ambayo alidai asingependa waumini wake wala Serikali kuyajua kwa ajili ya kulinda heshima ya kanisa hilo.

Wakati Askofu Chimeledya akiyasema hayo, Askofu Mokiwa amesema atazungumza na wanahabari leo kutoa ufafanuzi wa tuhuma hizo dhidi yake.

Msemaji wa Askofu Mokiwa, Yohana Sanga alisema atazungumza na kujibu maswali yote ambayo wengi wametaka kuyajua kutoka kwake baada ya kuamuriwa kujiuzulu.

Awali, Askofu Chimeledya alimuamuru Askofu Mokiwa kujiuzulu kwa kile alichodai amevunja misingi ya kanisa.

Jana, Askofu Chimeledya aliwataka waumini wa kanisa hilo Dayosisi ya Dar es Salaam kuacha kulalamika kwani askofu wao hakuonewa.

Korti yaamuru Washtakiwa wa Mauaji ya dada wa Bilionea Msuya Wakatibiwe

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru washtakiwa wa kesi ya mauaji ya Aneth Msuya, wakatibiwe baada ya kukubaliana na madai yao kuwa walipigwa wakiwa mahabusu katika kituo cha Polisi.

Miriam  ambaye ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo ni mjane  wa bilionea Msuya,  aliyekuwa mfanyabiashara wa madini ya tanzanite. Bilionea Msuya pia aliuawa kwa kupigwa risasi Agosti, 2015 eneo la Mijohoroni, kando mwa Barabara ya Arusha–Moshi, mkoani Kilimanjaro.

Uamuzi wa Mahakama kwa washtakiwa  kwenda kutibiwa unatokana na malalamiko yao waliyoyatoa kupitia kwa wakili Peter Kibatala kuwa walipokuwa mahabusu, waliteswa kwa kupigwa na kulazimishwa kukubali kutenda kosa hilo katika maelezo yao.

Mbali na madai ya washtakiwa hao kuteswa na kuomba Mahakama ifanye uchunguzi na iagize watibiwe, pia Wakili Kibatala alidai hati ya madai ina kasoro za kisheria.

Mahakama ya Kisutu katika uamuzi wake uliotolewa na Hakimu Mkazi Godfrey Mwambapa ilikubaliana na madai ya washtakiwa hao.

Q Chief Amwagia Sifa Mpenzi Wake ‘ni Wanawake Wachache Wenye Moyo wa Chuma Kama Wako’

$
0
0
Msanii wa muziki Q Chief ameshindwa kuzuia hisia zake mtandaoni na kuamua kumwagia misifa mpenzi wake.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo Sungura, amedai mwanamke hiyo ni mwanamke wa pekee kutokana na uvumilivu wake.

“Soon tunatimiza miaka miwili katika uhusiano wetu umekuwa mvumilivu mwenye hekima ni wanawake wachache sana dunia hii wenye moyo wa chuma ulionao tumepita rough roads tumevuka vikwazo vingi tumepitia kila aina ya changamoto but most important tumepigana vita zote na kushinda sisi ni wababe wa vita love you honey, soon utatoka juani na utajikuta kivulini naamini maana Mungu wetu yu mwema nakizuri zaidi anatupenda sana,” aliandika Q Chief Instagram.

Muimbaji huyo ambaye ameweza kupambana na kuachana na matumizi ya Madawa ya kelevya, mapema mwaka 2016 alionekana akivalisha pete msichana huyo.

Watanzania Tujifunze Haya Kutoka kwa Rais Magufuli

$
0
0
Kuna msemo ambao una tupa moyo sana sisi wanadamu kwa namna moja au nyingine ndivyo ninavyoweza kusema, Msemo huo ni ule usemao hakuna mkamilifu zaidi ya Mungu pekee katika dunia hii na umuhimu wa kitu huwezi kukiona mpaka pale kitu hicho kitakapoondoka machoni pako.

Wasomi hutumia kauli ‘Time will tell’ wakiimaanisha muda utaongea. Kwa kipindi kirefu sana Watanzania tumekuwa tukiipinga rushwa kwa kiasi kikubwa ambayo ilikuwa kansa ya maendeleo kwa nchi yetu. Lakini Mungu alisikia kilio chetu na kusema kilio cha rushwa katika taifa la Tanzania kimefika mwisho kwa kutupatia rais wa awamu ya tano Dkt John Pombe Magufuli. Simaanishi kwamba marais wa nyuma waliopita hawakuipinga rushwa hapana nawaona waliifanya kwa nafasi yao na muda walioupewa kulitumikia taifa hili.

Rais Magufuli tangu aingie madarakani amefanya vitu vingi sana kwa muda mchache. Si kweli kwamba yote anayoyafanya wengine wetu wanaweza wakayachukia lah hasha! kwasababu katika maisha pia huwezi kupendwa na wote na pia sio kila kitu unachokifanya watu wote watakipenda.

Ziara za Rais Magufuli

Rais huyu akiwa katika ziara sehemu mbalimbali za Tanzania au nchi jirani watu wengi wamekuwa wakitaka kujua kazungumzia nini katika hotuba yake na watu hutulia katika vituo mbalimbali vya televisheni kujua nini kimesemwa katika hotuba hio. N pia baada ya hotuba hiyo kuisha katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania watu wanakuwa wakirudia kile alichokisema na kumpongeza kwa alichokisema huku wengine wakionyesha kufurahishwa na hotuba za rais huyu.

Utumbuaji majipu

Hili neno la kutumbua majipu hupenda kulitumia Rais huyu popote atakapokuwa hata akiwa katika ziara fulani au akifanya ziara ya kushtukiza sehemu ambapo akifika katika eneo hilo akiona kuna mapungufu au kuna matumizi mabaya ya fedha yeye humtumbua mtu huyo kwa kutaka asimamishwe kazi mara moja bila kutaka kusamehewa na hutumia kauli ‘Mtu akitumbuliwa hapa Dar es Salaam asije akafikiri akienda mkoa mwingine atapata kazi katika serikali hii. Hilo halipo ukifutwa kazi Dar es salaam umefutwa moja kwa moja.’ Kauli hii nadhani inawapa umakini watendaji hao sambamba na kufanya kazi kwa ufanisi kuogopa kutumbuliwa.

Baadhi ya wapinzani kusifia jitihada zake katika kupambana na rushwa

Baadhi ya viongozi wa vyama pinzani nchini wamekuwa wakifurahishwa sana na hali ya rais huyu kupinga rushwa nchini na niliwahi kumnukuu akisema, Rushwa ni kansa kwa maendeleo ya nchi.Hapa ukitaka kujua rais huyu anaichukia rushwa ukichukua ugonjwa wa Kansa jinsi ulivyo na unavyowatesa watu ndivyo utakavyoelewa ni jinsi gani amekuwa akichukizwa na baadhi ya watu ambao mpaka leo wanapenda rushwa.

Safari ya serikali kuhamia Dodoma
Ni miaka mingi tulikuwa tukisikia kuwa makao makuu ya Tanzania yapo Dodoma, lakini viongozi mbalimbali wa nchi hii wanaishi Dar es Salaam, jambo ambalo miongoni mwa watu walikuwa wakijiuliza. Ni jambo gumu sana kumhamisha mtu eneo alilokuwa akiishi siku zote au miaka yote kumpeleka sehemu ambayo huenda alikuwa akienda katika matembezi yake ya kawaida. Lakini Rais Magufuli ameweza kuwatoa baadhi ya viongozi akiwemo Waziri Mkuu na kuwahamishia Dodoma ikiwa ni sehemu ya kutaka viongozi wahamie katika makao makuu hayo. Yeye na makamu wake Bi Samia Suluhu nao wana mpango baadaye kuhamia huko.

Rais Magufuli na Kutetea wanyonge

Rais Magufuli amekuwa akiwatetea wanyonge kwa kiasi kikubwa huku akichukizwa na baadhi ya vitendo vya baadhi ya viongozi kutumia madaraka yao vibaya na kutaka viongozi wengine wajiondoe madarakani kama watashindwa kuwatetea wanyongee katika taifa hili. Katika awamu hii wanyonge wamekuwa ni watu wenye furaha ikiwemo kuachiwa huru wamachinga kufanya biashara zao. Akienda sehemu mbalimbali, amekuwa akiwatia moyo wanyonge huku akisema kuwa hata yeye ni mtoto wa mkulima hivyo matatizo ya wakulima anayatambua vilivyo. Watu wenye ulemavu wa miguu na wenye changamoto mbalimbali amekuwa akitoa sehemu ya mshahara wake kuwasaidia chochote kwaajili ya kuendesha maisha yao ya kila siku.

Serikali ya awamu ya tano

Hata katika vitabu vya dini kuna neno husema itii mamlaka iliyo juu yako. Hili lipo katika serikali hii wengi wao wamekuwa wakimtii Rais Magufuli anapotoa maagizo na baadhi yao kufuata yale anayoyataka. Kufanya ziara za kushtukiza katika maofisi mbalimbali ni kitu ambacho viongozi wa awamu hii wanakifanya. Wamekuwa si wa kukaa ofisini, wamekuwa wakuzunguka kila mahali kwaajili ya ziara ili kujua hali za wamanchi wao na changamoto wanazokutana nazo kwa namna moja au nyingine,sambamba na kuwatatulia changamoto hizo na kwa viongozi wanaofanya vibaya wamekuwa wakiwasimamisha kazi bila kuogopa.

Si kwamba serikali zilizopita zilikuwa hazina mazuri, hapana na wala si kwamba serikali hii haina mapungufu, hapana bali kwa namna moja au nyingine wanafanya vizuri katika kuliongoza taifa hili. Kikubwa ni kuwaombea ili Mungu awajaze hekima na maarifa katika kuliongoza taifa hili huku akiwapa pumzi na nguvu za kutosha kwasababu kuongoza nchi ni kitu kikubwa ambacho waweza kuona ni kitu cha kawaida kwa hali ya ubinadamu. Kikubwa tujitupe tufanye kazi kwa bidii zote ili tuweze kupata vipato vyetu kihalali.

BY: Emmy Mwaipopo

Pata Kifaa Chenye Uwezo Asilimia 99% wa Kuongeza Ukubwa wa Uume....

$
0
0

Handsome up ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa uhakika na bila madhara. Inapatikana kwa @200,000/=tu. PIA kuna Gely ya kupaka @ 120,000/= na Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa kwa wanaume @120,000/=.
Na spray ya kuchelewesha kufika kileleni kwa mwanaume @120,000/=
NB.Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON $ CO. Wasiliana nasi kwa no (+255) 0767447444 au
0714335378.
Follow us
@Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr

List ya Waliotabiriwa kifo 2017: Malkia Elithabeth na Robert Mugabe Wapo

$
0
0
Hapo chini utaona listi ya watakaokufa mwaka 2017, Watu maarufu zaidi ya 50 wamechaguliwa na jopo la watabiri kuwa watakufa mwaka huu. Kuna sheria za kuchagua watu watakaokufa kama ifuatavyo: Mtabiliwa kifo lazima awe maarufu kiasi ya kwamba huyo mtu akifa lazima vyombo vya habari vya uingereza vitamtangaza; na vigezo vingine kadhaa akionekana mgonjwa au ukimuona unajua huyu!

Malkia Elizabeth II ameshatabiriwa mara moja akadunda huo Mwaka sasa hivi pia katabiriwa kuwa atadanja mwaka huu 2017.. mume wake Prince Philip nae Ametabiriwa 2017 pia.

Raisi wa zamani wa Marekani Jimmy Carter mwenye Miaka 93

Bwana Mugabe Miaka 93 naye Masikini wamemtabilia 2017 ndio the end - Kaandikwa Dictator alishatabiriwa mara 3 before

Pia katika list hiyo Billionea Mwenye Familia tajiri kabisa Rockefeller mwenye miaka 102 nae amatabiriwa 2017 atakufa...

Desmond Tutu naye pia Mubarak

Katika list ya Mwaka 2016 Fidel Castro alikuwepo na Nusu walio orodheshwa walikufa na wengine ndio wamesogea mwaka huu kwa kukomaa huku Wanateseka.. inasikitisha Sana


Below you will find DeathList 2017, a list of 50 celebrities selected by an expert committee for their likelihood to die during 2017. There are a few rules to DeathList summarised as follows: Candidates must be famous enough such that their death is expected to be reported by the UK media;Candidates cannot be famous solely for the fact they are likely to die in the near future and only 25 candidates can reappear from the previous year’s list. 2016 was billed as the year of the celebrity death by some and, although DeathList 2016 started strongly, it hit a very lean period from June to November and ended with a final score of 12, two below the all time record of 14. Has the big celebrity clear-out of 2016 made the task more challenging for 2017 or will the rate of celebrity deaths continue apace? Only time will tell...


Rank Prev Year Appear Name Age Description Discuss
1 10 15 Kirk Douglas 101 Actor
2 28 9 Vera Lynn 100 Singer
3 6 11 Billy Graham 99 Evangelist
4 18 3 Lord (Peter) Carrington 98 UK Politician
5 15 5 Peter Sallis 96 Last of the Summer Winer
6 16 5 Prince Philip Duke of Edinburgh 96 Casual rascist
7 41 5 Denis Norden 95 Comic / TV Presenter
8 3 Pierre Cardin 95 Fashion Designer
9 37 4 Stan Lee 95 Marvel comics
10 4 10 Olivia De Havilland 101 Actress
11 7 6 Herman Wouk 102 Author
12 1 Tony Booth 86 Actor
13 20 5 Bob Dole 94 Politican
14 1 Leah Bracknell 53 Actress
15 23 2 Jimmy Carter 93 Ex US President
16 1 Gord Downie 53 Tragically Hip Singer
17 29 3 Leslie Phillips 93 Comedy Actor
18 4 Robert Mugabe 93 Dictator
19 8 4 Javier Perez de Cuellar 97 Ex UN Secretary General
20 39 13 Jake Lamotta 96 Boxer
21 1 King Michael of Romania 96 King of Romania
22 1 Betty White 95 Golden Girl
23 1 Nobby Stiles 75 Footballer
24 2 Queen Elizabeth II 91 Queen
25 1 Jill Gascoine 80 Actress
26 1 Bob Barker 94 The Price is Right
27 26 2 Doug Ellis 93 Ex-Aston Villa Chairman
28 27 5 George Bush Senior 93 Former President of USA
29 1 Honor Blackman 92 Actress
30 1 Ian St John 79 Footballer
31 1 Hugh Hefner 91 Playboy
32 1 David Prowse 82 Darth Vader
33 6 Jerry Lewis 91 Comedian
34 1 David Rockefeller 102 Billionaire
35 31 2 Sandy Gall 90 TV news reporter
36 1 Pope Benedict XVI 90 Former Pope
37 50 3 Bruce Forsyth 89 Entertainer
38 32 9 Fats Domino 89 Singer
39 4 Hosni Mubarak 89 Former Egyptian President
40 34 3 Desmond Tutu 85 Archbishop
41 1 Emperor Akihito 84 Japanese Emperor
42 1 Gay Byrne 83 Broadcaster
43 36 2 Glen Campbell 81 Country Singer
44 1 Liz Dawn 78 Vera Duckworth
45 49 2 John Noakes 83 Blue Peter Presenter
46 3 Valerie Harper 78 Rhoda
47 21 4 Joost van der Westhuizen 46 Rugby player
48 13 2 Mary Tyler Moore 81 Actress
49 1 Errol Christie 54 Boxer
50 6 Ian Brady 79 All round Mr Nice Guy

Arusha: Lema 'Aendelea Kuongoza' Akiwa Mahabusu

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA) ambaye yuko mahabusu katika Gereza la Kisongo anaendelea kutenda na kumudu kazi zake akiwa mahabusu. Taarifa za kuaminika zinaonesha kuwa Lema huombwa mawazo, maelekezo na ushauri kabla ya kufanyika jambo lolote Arusha.

Mambo yote yafanyikayo kwa kujadiliwa au kuamriwa na Baraza la Madiwani la Arusha ambalo linadhibitiwa na CHADEMA yanahusisha mawazo na melekezo ya Mbunge Lema. Taarifa zinaonesha kuwa Lema yu katika afya njema na mwenye ari kubwa ya kutenda kazi.

Lema, Mbunge wa kwanza wa upinzani jimbo la Arusha Mjini aliyeweza kutetea kiti chake cha Ubunge, anahusishwa na kuhusika na kila jambo jimboni Arusha katika kulipanga, kulijadili na kuliamua. Lema anatajwa kuwa ni mmoja wa Wabunge machachari wa upinzani nchini.

Yuko mahabusu baada ya kukosa dhamana katika mahakama huko Arusha katika kesi zake mbili za jinai. Bado Lema anapambania kupata dhamana huku akiendelea na kesi zake za jinai.

Mwafaaaaaaa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Ujangili wapungua Tanzania

$
0
0
WIZARA ya Maliasili na Utalii, imesema vitendo vya ujangili nchini vimepungua kwa mwaka uliopita ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Hali hiyo imetokana na kuwapo kwa ushirikiano wa vyombo vya ulinzi na usalama, mamlaka husika na wananchi katika kutoa taarifa na kufanikisha kukamatwa wahalifu wa ujangili wa tembo.

Hayo yalisemwa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Gaudence Milanzi jana mjini hapa, alipotoa hotuba yake ya kufungua kikao cha mafunzo ya siku tano kwa watendaji wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (TAWA) na wakuu wa mapori ya akiba.

Alisema, ujangili umepungua na ukamataji wa meno ya tembo unaofanyika kwa hivi sasa unatokana na ujangili wa zamani ambayo baadhi ya wahalifu huo walikuwa wameyahifadhi kwa ajili ya usafirishaji kwenda katika masoko.

“Watu watasema, mbona ukamataji wa meno ya tembo unaendelea endapo ujangili umepungua? Meno haya ni yaliyokuwa yamehifadhiwa kwa kitambo na yanakuwa katika njia ya usafirishaji kwenda nje ya nchi na si meno mapya ya tembo,” alifafanua Milanzi.

Hata hivyo, alisema licha ya kupungua kwa ujangili tofauti na miaka ya nyuma, lakini bado unaendelea kufanyika kwa kiwango kidogo na kutokana na hali hiyo juhudi za pamoja zinahitajika katika suala la ukamataji na udhibiti kwenye maeneo ya hifadhi za taifa.

Alisema, “kazi ya sasa kwa mamlaka kwa kushirikiana na nyingine ni kazi ya kuhakikisha majangili hawawezi tena kuingia ndani ya mapori ya hifadhi kwa ajili ya kuua wanyamapori hasa tembo. Na hii itasaidia kukomesha biashara hii haramu,” alisema Milanzi.

Katibu Mkuu huyo aliwataka watendaji wa mamlaka hiyo na nyingine zinazosimamia rasilimali za hifadhi za wanyamapori kuongeza nguvu katika vita dhidi ya ujangili kwani mafanikio ya serikali yameanza kuonekana katika suala zima la mapambano ya vita vya ujangili.

Mwenyekiti wa Bodi ya TAWA, Hamis Semfuko, kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu alisema kuwa ujangili, uharibifu wa mazingira na uvamizi wa mifugo na kujenga makazi ndani ya mapori ya hifadhi ya akiba ni mkubwa na mifugo mingi inatoka nje ya Tanzania.
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live




Latest Images