Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Sio Kila EX Wako Anayeomba Mrudiane Anamaanisha! Wengine Huomba Kurudi Ili Wakutesti Tu

$
0
0

Sio Kila EX Wako Anayeomba Mrudiane Anamaanisha! Wengine Huomba Kurudi Ili Wakutesti Tu Jinsi Ulivyo Mbulula,Jinsi Usivyo Na Msimamo Na Jinsi Ulivyo CHEAP Na Huna Misimamo Wala Future.
.
Jitu Mmeachana Miezi 6,Leo Linakutesti Lirudishe Majeshi,Na Wewe Ulivyo Kiazi,Upo-Upo Tu,Ina Maana Miezi Yote Hii Ulikuwa Umeganda Unasubiria Rehema Zake Ama?? Kurudia Matapishi Ya EX Ukitegemea Amebadilika Ni Sawa Na Kupika Sufuria La Makande Kwa Mshumaa,Utaambulia Masizi Tu..
.
Kipi Kipya Kakiona Kwako Hadi Arudi??Nini Kilimshinda Huko Nyuma Ambacho Leo Anakiweza Anataka Kurudi??Akafie Mbele Huko.
.
KUWA NA MSIMAMO,Ukisema Its Over Umaanishe,Sio Unakuwa Na Hisia Zinapepea Tu Kama Bendera Ya Katibu Kata Wa Kishumundu... Mtu Kama Hajielewi Achana Nae,Siku Akijirudisha Mwambie Kwanza Akapimwe Minyoo Ya Kinyarwanda.
.
Umekazana Kuwaambia Marafiki Zako 'Siku Hizi Hakuna Mapenzi Ya Dhati Watu Wote Majanga Tu',Nani Amekwambia Hayapo?? Yapo Sana Ila Wewe Unatumia Mbinu Tofauti..
.
Huwezi Kusoma Degree Ya Law Halafu U-Apply Kazi Ya Chief Accountant Wa Bodi Ya Tumbaku...Kila Siku Utasingizia Balance Sheet Haina Jurisprudence..Lawyersl

Mmenielewa! Acha Kudate Watu Wasiojielewa,Usidate Kwa Sababu Uko Lonely,Usiwe Desperate Kuingia Mahusiano Kwa Sababu Shosti Zako Wanakusimulia Walivyopelekwa Ruwenzori Waterfalls..
.
Ingia Kwenye Mahusiano Pale Moyo Wako Ukiwa Tayari Na Mtu Uliyemfia Kihisia Na Amekuwa Approved Na Veins,Auricles,Na Aorta Za Moyo Wako Kwamba He/She Is Really The One.. Unadate Na Mtu Ambaye Mustakabali Wake Mwenyewe Haujui,Ukimuuliza Anataka Kuwa Wapi Ndani Ya Miaka 5 Ijayo Anakwambia Mungu Anajua Dont Worry,Halafu BBM Na Instagram Unajiita Baby Ake Mie Iam In Love..

Utaishia Kufua Boxer Hadi Kucha Zinukie Gololi! Mbwa Kamwe Hashughuliki Na Kesi Za Paka Kufungiwa Kabatini.Date The Right Person,With Right Reasons,In A Right Time Uone Kama Mapenzi Hayapo...
.
Nikipanic tena nitarudi

Mwenyekiti Chadema Ahukumiwa Miezi Nane Jela Bila Faini,Kisa Hiki Hapa..!!!

$
0
0
 
VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akiwemo Kaimu Mwenyekiti wa Mkoa wa Lindi na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama, Selemani Mathew na Katibu wa Chadema Kijiji cha Nyangamara ‘A’ mjini Lindi, wamehukumiwa kifungo cha miezi minane jela bila ya faini kutokana kufanya mkutano bila ya kibali cha Jeshi la Polisi katika kijiji hicho wilayani Lindi.

Viongozi hao waliohukumiwa ni kati ya viongozi sita waliokamatwa na kutuhumiwa kufanya mkutano bila ya kibali cha Jeshi la Polisi nchini.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Lindi, Muhini alitoa hukumu hiyo baada ya kusikiliza mashtaka pande zote mbili na kubaini viongozi hao walitenda kosa la kisheria.

Tukio lililotokea Aprili 3, mwaka jana kwa viongozi na wanachama kwa pamoja kufanya mkutano bila ya kibali cha Jeshi la Polisi wilayani Lindi.

Alitaja kifungu cha sheria kilichovunjwa ni Kipengele 74(1) na 75 kinachozungumzia Mwenendo wa Makosa ya Jinai kinachosomeka kwa pamoja na sheria ya Jeshi la Polisi.

Alisema washitakiwa wengine wanne wanaachiwa huru, kwani walibainika hawana hatia. Hao ni Bashiru Rashidi, Hassani Mchilima, Abdallah Mmasikini na Isimael Kupilila.

Akizungumzia hukumu hiyo, Mratibu wa Wanawake wa Chadema Mkoa wa Lindi, Sina Kikuwi alisema mahakama haikutenda haki kwa watuhumiwa hao.

Alisema taarifa walikuwa nayo kwenye vikao hivyo vya ndani havihitaji kibali, bali kutoa taarifa ambazo zilishatolewa katika mamlaka husika.

Selemani Mathew aliwahi kuwa D
iwani wa Vijibweni wilaya ya Kigamboni jijini Dar es Salaam kwa tiketi ya CCM. Aligombea katika Jimbo la Mtama mkoani Lindi mwaka juzi, ambapo katika kura za maoni za CCM alishindwa na Nape Nnauye.

Baadaye alihamia Chadema ambako alikuwa mgombea ubunge wa chama hicho, lakini pia alishindwa na Nape ambaye sasa ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Umesikia Jinsi ACT Wazalendo Walivyomjibu Polepole wa CCM,Wamuumbua Kwa Kauli hii..!!!

$
0
0

Chama cha ACT-Wazalendo, kimemjibu Katibu Itikadi na Uenezi wa CCM, Hamphrey Polepole kwa kumueleza kuwa kazi chama cha siasa ni kuhangaika na matatizo ya wananchi.

Juzi, Polepole aliwataka wapinzania kuacha  kutumia matatizo ya wananchi kujinufaisha kisiasa huku akitolea sakata la njaa na tetemeko la ardhi liliotokea Bukoba.

Akizungumza na wanahabari jana (Jumatano) katika Makao Makuu ya ACT-Wazalendo, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma kwa chama hicho, Ado Shaibu amesema  kukabiliana na matatizo ya wananchi  ndiyo mtaji sahihi wa kisiasa.

"Chama cha siasa lazima kishughulike na matatizo ya wananchi, kisichojishughulisha na matatizo ya wananchi kitakufa,"amesema Shaibu.

Kaimu Jaji Mkuu Mpya Atoa Ahadi ya Kesi Kuendeshwa Kwa Kutumia Kompyuta..!!!

$
0
0

KAIMU Jaji Mkuu mpya wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma ameahidi kuweka mkazo katika matumizi ya Tehama katika kuendesha kazi za Mahakama kuhakikisha haki inapatikana kwa haraka.

Jaji Juma alitoa ahadi hiyo baada ya kuapishwa, tukio lililofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam jana.

Jaji Juma awali alikuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania na atashika nafasi hiyo mpaka hapo Rais Magufuli atakapofanya uteuzi wa Jaji Mkuu.

“Katika kuwahudumia wananchi katika kutoa haki na kwa haraka tutatumia teknolojia ya habari ili haki iweze kupatikana haraka kuliko sasa,” alisema Jaji Juma.

Alisema alipata nafasi ya kusoma sera ya Tehama iliyotolewa Mei mwaka jana ambayo inatoa picha ya nchi miaka 20 ijayo kuonesha nchi inatakiwa kwenda wapi ambapo na mahakama inatakiwa kutekeleza.

“Mpango wangu ni kwamba, kesi zinasajiliwa katika mtindo huo ili kuhakikisha haki inapatikana haraka na kwa uwazi zaidi ya ilivyo sasa,” alisema Jaji Juma na kuwapongeza majaji wakuu waliomtangulia ambao waliweka msingi wa mabadiliko katika mahakama ikiwa ni pamoja na kuweka mpango mkakati unaosaidia katika utendaji kazi.

“Sheria nyingi zimebadilika, fedha nyingi zimepatikana na vilevile mpango mkakati wa mahakama, sasa ni kuutekeleza mpango huo ….. wao wameshamaliza kazi yao sasa ni kupunguza maneno”, alisema Jaji Juma.

Aidha alimshukuru pia Rais John Magufuli kwa kumuamini na kumteua katika nafasi hiyo ili aweze kuwahudumia wananchi katika kutoa haki. Rais Magufuli juzi alimteua Jaji Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania kuchukua nafasi ya Jaji Mohamed Chande Othman ambaye amestaafu.

Katika tukio hilo, Jaji Mkuu mstaafu alisema katika mambo ambayo hata yasahau katika kazi zake ni pamoja na kubadilisha watumishi wa mahakama kutambua kuwa ni chombo ambacho kinawajibika kwa wananchi.

“Hili ni jambo ambalo lipo na linaendelea katika kuhakikisha kwamba mahakama ni chombo ambacho kinatoa haki na pia kwa wakati kwa Watanzania wote,” alisema Othman na kuongeza kuwa Mahakama iko kwenye kasi ambayo Serikali ya Awamu ya Tano inaitaka na kuwataka watendaji wanaobaki kuongeza kasi hiyo.

Inasikitisha Sana:Auawa na Kutupwa Chini ya Daraja,Kisa Hiki Hapa..!!!!

$
0
0

MKAZI wa kijiji cha Sakalilo kilichopo mwambao wa Ziwa Rukwa wilayani Sumbawanga, Kalitus Jacob (44) ameuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kisogoni kisha mwili wake ukatupwa chini ya daraja la Mumba na watu wasiojulikana.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa, George Kyando alisema tukio hilo lilitokea Januari 16 mwaka huu, saa 12:00 jioni katika kijiji cha Sakalilo “Kabla ya tukio, alionekana akiwa kilabuni na wake zake wawili wakinywa pombe, aliwaaga na kuondoka na hakurudi tena hadi alipokutwa akiwa amekufa. Chanzo cha mauaji hakijajulikana na juhudi za Jeshi la Polisi zinaendelea ili kubaini kiini cha mauaji hayo,” alieleza Kamanda Kyando.

Alisema kuwa mwili wa marehemu umekabidhiwa kwa ndugu zake kwa ajili ya maandalizi ya maziko yake baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu.

Alisema watuhumiwa hawajakamatwa huku uchunguzi unaendelea ili kuweza kuwabaini waliohusika katika mauaji hayo.

Hatarii!! Prof lipumba na Sumaye Wakutana Uso kwa Uso Kwenye Kampeni,Washambuliana Kwa Maneno Mazito..!!!!

$
0
0

Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Frederick Sumaye wamekutana kwenye kampeni za uchaguzi wa diwani wa Kata ya Kahumulo huku kila mmoja akirusha vijembe kwa chama cha mwenzake.

Wakati Lipumba akiielezea Chadema kuwa imepoteza mwelekeo kwa kumkaribisha waziri huyo mkuu wa zamani na mwenzake, Edward Lowassa, Sumaye amesema CUF haiwezi kuwakomboa wakazi wa Kahumulo.

Wawili hao walikuwa katika kata moja wakiwanadi wagombea udiwani wa vyama vyao katika mikutano miwili tofauti ya uchaguzi mdogo uliopangwa kufanyika Jumapili ijayo.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa kumnadi Ntalikwa Ishatala uliofanyika Kata ya Kahumulo, Profesa Lipumba amesema Chadema ni chama kilichopoteza mwelekeo kwa kuwa kimebeba mafisadi waliohama CCM.

Wakati Profesa Lipumba akiishambulia Chadema, Sumaye alikuwa eneo jingine akimnadi mgombea wa chama hicho kwenye kata hiyo, Dotto John.

Waziri huyo mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu amesema CUF na CCM ni vyama ambavyo havina mtazamo wa kuikomboa Tanzania.

Aibu ya Mwaka Hii!! Amber Lulu Abambwa Akidendeka Live na Njemba Nnje ya Ukumbi,Tazama Picha Hapa +18..!!!

$
0
0
amber-lulu-5
DAR ES SALAAM: Video Queen mwenye vituko kila kukicha, Lulu Euggen ‘Amber Lulu’ Jumapili iliyopita alibambwa usiku wa manane  akifanya vitendo vichafu na msanii wa tamthiya ya Kelele aliyejulikana kwa jina moja la Talik, nje ya ukumbi wa Catalunya uliopo Mwenge Jijini Dar.

amber-lulu-6amber-lulu-1amber-lulu-7amber-lulu-8amber-lulu-4Video Queen huyo alikuwa ni mmoja wa waalikwa kwenye sherehe ya kuzaliwa staa wa Bongo Muvi Irene  Uwoya, ambapo baada ya kuingia na kupata ulabu kiasi cha kutosha, alitoka nje na kukaa pembeni ya gari akiwa na msanii huyo huku wakipigana mabusu mdomoni bila kujali wapita njia.

“Nyie huyu Lulu atakuwa amepagawa kabisa maana hata haogopi kabisa kama watu wanapita na kuwaona wanachofanya, na wakati huyu sasa hivi anajinadi yuko na Young D” alisikika kijana mmoja akizungumza.

Licha ya binti huyo kuhusishwa na Young D, zipo tetesi pia zinazomtaja msanii wa Hip Hop, Roma Mkatoliki kuwa pia anatoka naye kimahaba.

Mwandishi wa habari hii alimsogelea Lulu na kutaka kujua kulikoni kufanya mambo hayo hadharani, ambapo aligeuka mbogo na kutaka aachwe aendelee na mambo yake.“Dada yangu nakuheshimu, naomba uniache, tena uniache kabisa, hakuna aliyenilipia nauli ya kuja hapa hata mara moja,” alisema Lulu.Katika pati hiyo iliyohudhuriwa na mastaa kibao, waalikwa walikunywa na kula kwa muda wote kuanzia saa amber-lulu-3Wakijiachia kima-lovee.

Ubuyu wa Moto Moto: Zari Alianzisha Tena na Hamisa Mobeto,Aanika Ukweli wote Juu ya Diamond Kuchepuka na Mobeto..!!!

$
0
0
Mwanamitindo Hamisa Mobeto.
DAR ES SALAAM: Kimenuka tena! Ndiyo unavyoweza kusema baada ya mzazi mwenza wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kutupia picha ya hereni kwenye Mtandao wa Kijamii wa Snapchat huku akitupa dongo kwa kusema aliyesahau vitu vyake aende akavitoe, bifu limeibuka upya mitandaoni.
 
zari
Mzazi mwenza wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
 
Baada ya kutupia picha ya Snapchat hiyo, mashabiki mbalimbali wa mtandao huo walijiongeza na kuoanisha na picha ya Mwanamitindo Hamisa Mobeto kwa kufananisha hereni alizovaa siku za nyuma zikifanana na hizo alizodai Zari zimesahaulika kwenye chumba cha Diamond, nyumbani kwake, Tegeta-Madale jijini Dar.

Mbali na mashabiki hao kujiongeza, mjadala mzito uliibuka pia wakidai ugomvi wa Zari na Mobeto si rahisi kumalizika maana kati yao hakuna anayeweza kuwa mpole na kumwachia mwenzake atambe. “Hili lazima ni dongo kwa Mobeto, yaani hawa, hauwezi kupita muda hawajazinguana, kweli mapenzi yanauma lol…” aliandika mmoja wa mashabiki wanaotumia mtandao huo wa Snapchat.     Staa wa Bongo fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na mpenzi wake Zari .

Mjadala ulikuwa mkubwa huku kila mmoja akimtetea anayempenda hadi mashabiki hao kufi kia hatua ya kutukanana mitandaoni. Kuna ambao walimtetea Zari lakini wengine walikuwa upande wa Mobeto.

Risasi Jumamosi lilimtafuta mwanamitindo huyo ili aweze kufungukia hayo madai ambapo alisema ameziona lakini hakutaka kufunguka kama ni zake au la: “Nimechukizwa na kitendo hicho. Kitendo hicho kimenifanya mimi nitukanywe sana matusi ya nguoni kwenye mitandao ananitafuta sana Zari lakini ipo siku atanipata,” 
alisema Mobeto.

 Hii si mara ya kwanza kwa wawili hao kuingia kwenye bifu ambapo inadaiwa penzi la Diamond ndilo linalowatia ‘uchizi’ hata kuwafanya w a k w a r u z a n e k i l a mara

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Kutoka Bagamoyo , Anarudisha Mapenzi na Kusafisha Nyota

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI, (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 48 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI:

SHEKH SHARIFU RASHIDI ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji na n.k, anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, pia anatoa pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali kulingana na nyota yako, anaouwezo mkubwa wa kutumia jina la muhusika kwa kutatua tatizo lako, anaouwezo wa kumrudisha mtu aliepotea kimiujiza, pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo,

WASILIANA NAE KWA SIMU NA WHATSAPP NO: 0718-668347. 0685-224047, 0767-204308 na 0627-251404 au follow@shekh_sharifu_rashid, Email:shekhsharifurashid@gmail.com

Mh,!! Shilole na Nuh Mziwanda Wamerudina au Hawajarudiana?Nuh Mziwanda Amefunguka Haya Juu ya Swali Hilo

$
0
0
nuhumziwanda.png
MSANII wa Bongo Fleva anayetamba na Wimbo wa Jike Shupa, Naftari Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ amesema kuwa japo kuna tetesi zinaenea mtaani kwamba amerudiana na aliyewahi kuwa mpenzi wake, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ suala hilo halina ukweli wowote ndani yake na wala hafikirii kabisa kurudiana na mwanadada huyo.


Tetesi za Nuh kurudiana na Shilole zilianza kuvuma baada ya kusambaa kwa kipande cha video kilichowaonesha wakipatanishwa wakati wakiwa kwenye safari za Tamasha la Fiesta na watu kujiongeza kuwa wamerudiana.

“Kilichotokea ni kwamba mimi na Shilole tumeondoa tofauti zetu za kibinadamu ambazo tulikuwa nazo baada ya kuachana.

Lakini kuhusu kurudiana hahitakuja kutokea hata siku moja na siwezi kurudi nyuma kwenye hili maana nina mpenzi wangu ninayempenda,” alisema Nuh.

Pitia Vichwa Vya Magazeti ya Leo 19/1/2017...!!!

Laana Tupu!! Kaka Mtu Akamatwa kwa Kumbaka na Kumtoa Usichana Dada Yake wa Miaka 4..!!!

$
0
0
 

 
 YAWEZEKANA ikawa  ni  moja ya  sababu ya  mvua  kuchelewa kunyesha  mkoani Iringa tofauti  na  ilivyozoeleka  miaka  mingine  ni  kutokana na laana kama hizi  baada  ya kikosi  maaalum kinachoongozwa   mkuu  wa  wilaya ya Iringa  Richard Kasesela  kwa  kushirikiana na OFM kufanikiw kumkamata  kijana Emmanuel Mkiwa  (19) kwa tuhuma  za kumbaka mara kwa
mara mdogo wake  wa miaka (4)


 
 
LAA
Afisa  maendeleo ya  jamii Manispaa   ya  Iringa  Josephina Mwaipopo  akiwa na mtoto aliyebakwa
Imedaiwa kuwa kijana  huyo  ambae  ni mwenyeji  wa mtaa  wa Omary  Matrekta kata ya  Mtwivila  katika  Manispaa ya  Iringa alikuwa akiishi nyumba  moja na babake pamoja na wadogo  zake watatu  wawili  wa  kiume na mmoja ni  mtoto   huyo  wa  miaka 4  ambaye alitelekezwa  na mamake  mzazi kutokana na mambo ya  kifamilia kati  yake baba  wa  mtoto .
 
Mashuhuda wa  tukio   hilo  lililotokea January 16 majira ya  saa 2 usiku walimweleza  mwandishi  wa  OFM  Iringa  kuwa kijana   huyo mara  kwa mara  alikuwa  akimbaka  mdogo wake  huyo  ambae baba  mmoja  na mama tofauti kabla  ya  mtoto   huyo kuwaeleza majirani   kuwa kakake  huyo amekuwa akimkandamiza na  kijiti sehemu  zake  za  siri (Akimbaka)
 
Kutokana na  maelezo ya  mtoto   huyo ndipo taarifa  za  raia  wema  hao zilipofikishwa kwa mkuu  wa  wilaya  na OFM na  kuamua  kufika  katika eneo la  tukio na  kufanikiwa  kumkamata kijana   huyo  na baba mzazi wa  watoto  hao  Shukuru Mkiwa kwa malezi mabaya  ya  watoto.
 
Akizungumza baada ya  kukamatwa  kwa  kijana   huyo  mkuu  wa  wilaya ya  Iringa Richard  Kasesela   pamoja na  kuwashukuru raia wema  kwa  kufikisha taaarifa  ya  kunyanyaswa  kwa mtoto   huyo  bado  alitoa wito kwa wananchi  wengine  ambao  wanataarifa  za  kunyanyaswa  kwa  mtoto yeyote  katika  wilaya ya  Iringa  kutoa taarifa  ili  wahusika wakamatwe  na  kufikishwa  katika  vyombo  vya sheria.
 
Kasesela alisema  kuwa uchunguzi   uliofanywa baada ya  vipimo katika  Hospitali ya  Rufaa ya  mkoa  wa  Iringa umeonyesha mtoto   huyo kashaondolewa usichana wake   na  hivyo kulazimika  kulazwa  kwa  matibabu katika Hospitali   hiyo huku akiahidi kumsaidia mtoto  huyo  kumsomesha .
 
Alisema kuwa yawezekana  moja ya  sababu ya  mvua  kuchelewa  kunyesha katika mkoa  wa Iringa  ni  pamoja  na matukio ya  kinyama kama haya ya ubakaji  watoto na  kuwa  hatakubali kuona mbakaji  anaendelea   kuishi uraiani wilaya ya  Iringa kwani tayari  mkuu  wa  mkoa  wa  Iringa Amina Masenza  kupitia  kikao  cha makati ya  ushauri ya  mkoa (RCC) aliagiza wabakaji wote wasakwe kwa udi na uvumba na yeye ameanza
kutekeleza agizo hilo.
 
Japo alisema alishangazwa  na hatua ya baba  mzazi wa  kijana  huyo kumficha mbakaji ndani na  kudanganya  kuwa  hayupo wakati  kijana wake  alikuwepo  ndani hivyo  mzazi  huyo  kukamatwa pamoja na kijana wake yeye kwa  kosa la  kumchifa  mharifu  na kijana wake kwa kosa la ubakaji .
 
“Hiki  ni  kikosi  kamili  ambacho kitaendelea  kuendesha  misako  mbali mbali kwa kushirikiana na oparesheni  Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers hivyo kwa  yeyote  anayejua  wapi  mtoto anafanyiwa vitendo  vya kikatili piga  simu hii mwandishi wa OFM Iringa 0754 026 299 tutakufikia ulipo na
kuchukua  hatua”
 
Jeshi la  polisi  mkoa  wa Iringa  kupitia kwa  kamanda wa  polisi  mkoa (RPC) Julius Mjengi limethibitisha  kukamatwa kwa mtuhumiwa   huyo na  kuwa baada ya  upalelezi  atafikishwa mahakamani  huku  likiwataka  wananchi  kuendelea  kufichua  waharifu  zaidi

Maiti Iliyozikwa na Baadae Kukutwa Kitandani Nyumbani, Yazikwa Tena kwa Ulinzi Mkali wa Polisi

$
0
0

Maiti ya mtoto Haruna Kyando (9) ambayo ilikutwa nyumbani muda mfupi baada ya wananchi kutoka makaburini kumzika, imezikwa kwenye makaburi ya Isanga chini ya ulinzi wa askari wa Jeshi la Polisi nchini, huku waombolezaji wakiaga mwili huo kwa kufunuliwa jeneza eneo la kichwani makaburini hapo.
 

Aidha, Mchungaji wa Kanisa la Bonde la Baraka, ameingizwa lawamani kwa kupotosha umma.maiti6Haruna aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifafa tangu udogo wake, alikutwa na wazazi wake Jailo Kyando (36) ambaye ni muosha magari na mkewe, Anna Elieza (32) akiwa amefia usingizini Jumatatu wiki hii nyumbani kwao Mtaa wa Igoma A, Kata ya Isanga jijini Mbeya.


Kilichowapa taharuki wakazi wengi jijini hapa ni baada ya ndugu, jamaa na marafiki wa familia ya Haruna walipotoka makaburini siku hiyo walikokwenda kuzika, waliporejea nyumbani waliukuta mwili wa mtoto huyo ukiwa umelazwa kwenye godoro, pale pale ulipowekwa wakati walipokuwa wakiuandaa kuuweka kwenye jeneza.maiti2
Jeneza baada ya kufukuliwa kutoka kaburini.
Hatua hiyo ilizua taharuki kubwa kiasi cha wananchi kutaka kufahamu ni kitu gani kilichozikwa ndani ya jeneza na ndipo Jeshi la Polisi lilipoingilia kati, kuzuia kufukuliwa kwa kaburi husika.



Hatua hiyo ilisababisha vurugu na hatimaye saa tatu za usiku siku hiyo hiyo ya maziko ya awali, Polisi wakalazimika kutumia mabomu ya machozi, kutawanya watu waliofurika katika makaburi ya Isanga wakishinikiza kaburi lifukuliwe.maiti11
Mwenyekiti wa Mtaa wa Igoma pamoja na Baba wa Marehemu wakifunua jeneza kuhakikisha kama kulikuwa na mwili wa marehemu.
Lakini juzi baada ya kukamilishwa kwa taratibu husika, ikiwemo kupatikana kwa kibali kutoka mahakamani, saa nne na nusu asubuhi, Polisi Mkoa wa Mbeya walifika eneo la makaburi alipozikwa marehemu na kusimamia shughuli nzima ya kufukua kaburi hilo.



Shughuli hiyo iliyodumu kwa muda wa nusu saa kama ilivyokuwa siku ya kwanza, ilihudhuriwa na mamia ya wakazi jijini hapa waliotaka kujua nini kilichozikwa ilhali mwili ukiwa umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kwa wakati huo.maiti1
Jeneza lililofukuliwa likiwa halina kitu ndani yake.
Nusu saa baadaye jeneza la mtoto huyo lilitolewa nje ya kaburi na ndipo Mwenyekiti wa Mtaa wa Igoma A, Fredy Mwaiswelo alipofunua jeneza na kukuta ndani kukiwa tupu, hali iliyoashiria mwili wa marehemu haukuwekwa ndani ya jeneza wakati wanakwenda kuzika.


Kutokana na hali hiyo, Polisi kwa kushirikiana na baadhi ya vijana, walibeba jeneza hilo na kuelekea nalo katika Kituo cha Polisi kwa ajili ya uchunguzi zaidi kabla ya kuwakabidhi tena wanandugu mwili ili kuendelea na taratibu za maziko kwa mara nyingine.

Baada ya ndugu kukabidhiwa mwili, jeshi hilo pia lilisimamia maziko yaliyofanyika upya saa 10 jioni katika kaburi lile lile la awali, lakini tofauti na awali, kabla ya kuzika ulifanyika utaratibu wa ndugu, jamaa na marafiki waliohudhuria, kuuaga mwili wa marehemu uliokuwa ndani ya jeneza lililofunuliwa upande wa kichwani.

Kutokana na mkanganyiko uliojitokeza, baadhi ya ndugu na majirani wa Mtaa wa Igoma, walisema tukio hilo linaweza kuwa na sura mbili kwa maana ya hujuma iliyofanywa kwa makusudi, ikilenga maslahi binafsi ya mtu inayohusishwa na imani za kishirikina au bahati mbaya ya kuusahau mwili wa marehemu.

Walisema inaweza kuwa hujuma kutokana na kawaida ya misiba kabla ya maziko, lazima ndugu watoe heshima za mwisho kwa marehemu, lakini kwa msiba huu haikufanyika pamoja na baadhi ya ndugu kutohudhuria mazishi.

Akizungumza  nyumbani kwake jana pamoja na kukanusha tuhuma za kuhusisha tukio hilo na imani za kishirikina, baba wa marehemu alisema mkanganyiko uliojitokeza wakati taratibu za kuuandaa mwili zikifanyika pamoja na uzushi uliofanywa na mchungaji, ambaye alisema hamjui kwa jina, ndiyo vilivyokuza jambo hilo.

Alisema kama ilivyo kawaida baada ya majirani kupata taarifa za msiba wakiwa nyumbani hapo, walichanga fedha na kutuma watu kwenda kununua jeneza.

“Wananchi walichanga hela wakanunua jeneza likaletwa nyumbani. Waliobeba jeneza walilisukumiza tu kwenye chumba wakatoka, sisi tukaendelea na taratibu nyingine za mazishi. Baadaye akaja mwenyekiti akasema toeni mwili wa marehemu nje, wakatoa meza nje wakatuma vijana waende kuchukua mwili wa marehemu ndani. Waliopeleka jeneza ndani na waliokwenda kulichukua ni watu wengine. Jeneza likawekwa juu ya meza tukaendelea na mahubiri,” alisema Kyando.

Alisema baadaye walikwenda kuzika na baada ya kuzika walirudi nyumbani kisha wakala chakula na kunawa maji, kama ilivyo desturi ya misiba mingi mkoani hapa.

“Tumenawa maji tukakaa. Baada ya kukaa kuna mgeni akaingia katika chumba tunacholala ambapo awali ndipo tulimlaza mtoto kwenye kigodoro, alipoweka begi akakuta kuna blanketi. 

“Alipolifunua akashtuka akasema kuna nyoka watu wakaanza kukimbia ndani. Baadhi ya watu wenye roho yenye hasira wakaamua kuingia ndani wakahakikishe kuna nini,” alisimulia.

“Walipoingia ndani ndipo wakakuta ni mwili wa mtoto yaani marehemu. Waliposema ni mtoto wakipaza sauti watu wakajaa ndani. Ndipo waumini wa yule mchungaji wakaanza kumpigia simu yule mchungaji baadaye akarudi.”

Alisema baada ya mchungaji huyo kufika, aliingia ndani na waumini wake na kuanza kuomba.

“Walipoomba kwa muda mrefu ndipo mchungaji huyo alipotoka nje na kushika MIC na kuuambia umati kuwa mtoto baada ya kuombewa amehema mara mbili na ndipo watu wakaanza kulumbana,” alieleza.

“Kama siyo mchungaji kuzusha yale wala yasingekuzwa mpaka kwenye mitandao kiasi hiki. Sisi tunaamini walioagizwa kuchukua mwili walichukua jeneza tupu pasipo kuwekwa mwili ndani yake na kwa kuwa baada ya kutolewa jeneza hatukuingia ndani hivyo tuliuacha mwili nyumbani tukaenda kuzika jeneza peke yake,” alibainisha.

Akizungumzia suala la imani ya familia hiyo, Kyando alisema awali yeye na familia yake yenye watoto wawili, walikuwa wakisali katika Kanisa Katoliki, lakini kutokana na matatizo ya degedege yaliyokuwa yakimsumbua mwanawe wa kwanza, mkewe aliamua kumpeleka mtoto huyo kwa mchungaji wa Kanisa la Bonde la Baraka ili aombewe ikiwa ni sehemu ya kuhangaikia afya ya mtoto.

“Tulikuwa tunasali Roma, lakini kutokana na matatizo ya mtoto, mama yake akaamua aanze kusali Kanisa la Bonde la Baraka ili aombewe. Hapo mimi nikaacha kusali na ndiyo sababu hata katika ibada ya maziko ya mtoto ikabidi tulishirikishe kanisa walikokuwa wanasali mama na mtoto,” alisema Kyando na kuongeza:

“Watu wamezungumza maneno mengi sana, siwezi kubisha japo ni ya uzushi ila wameongea kutokana na walivyosikia, ila ukweli naujua mimi na namwachia Mungu.”

Naye baba mkubwa wa marehemu, Saulo Kyando alisema jambo lililotokea lilikuwa la kawaida na kilichotokea ni kukosekana kwa uratibu makini wa msiba huo.

“Hili jambo lilikuwa la kawaida sema kilichokosekana ni mtu ambaye angeliweka jambo sawa, angekuwepo mtu wa kusimamia kila hatua yasingefikia hapa,” alisema Saulo.

Imefichuka Aisee:Hizi ndio Sababu za Okwi Kuamua Kuvunja Mkataba Wake na Klabu ya Denmark..!!!

$
0
0


MSHAMBULIAJI wa zamani wa Simba na timu ya Taifa ya Uganda, Emmanuel Okwi amevunja mkataba wa kuichezea klabu ya Sonderjyske Fodbold ya Denmark baada ya pande zote mbili kufikia makubaliano.

 Okwi amefikia makubaliano ya kuvunja mkataba na uongozi wa klabu hiyo baada ya kutopata nafasi ya kutosha kuichezea tangu alipojiunga nayo mwaka 2015 akitokea Simba.

Mtandao huo ulimnukuu Mkurugenzi wa Soka wa klabu hiyo, Jorgen Haysen, akisema maamuzi hayo yamefikiwa baada ya Okwi (24), kushindwa kupata nafasi ya kucheza kwa muda mrefu.

“Okwi hajapata muda wa kutosha kucheza kwenye timu yetu, na hata matarajio ya kupata muda zaidi wa kucheza hayajaongezeka.

Hivyo basi tumekubaliana kuuvunja mkataba huu. Tunamtakia kila la heri," alisema Haysen kwenye taarifa ya mtandao huo maarufu wa michezo.

Okwi alisaini mkataba wa miaka mitano na alitegemewa angekuwapo kwenye kikosi hicho mpaka mwaka 2020.

Nyota huyo pia amewahi kuzichezea klabu za SC Villa ya Uganda , Etoile de Sahel ya Tunisia na Yanga. 

Kwa muda mrefu tangu kuanza kwa msimu huu wa Ligi Kuu mara kwa mara Okwi amehusishwa kutaka kurejea kwenye kikosi cha Simba japo viongozi wa timu wamekuwa wakikanusha taarifa hizo.

Walimu Wamuamulia Mkuu wa Mkoa Aliyeagiza Washushwe Vyeo vya Ualimu Mkuu,..!!!

$
0
0

CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT), kimesema kitamburuza mahakamani yeyote atakayetekeleza agizo la mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendegu la kuwavua vyeo walimu wakuu wa shule 63 mkoani humo kutokana na matokeo mabovu ya wanafunzi, kwani hana mamlaka ya kinidhamu kwa walimu.

Kauli hiyo ilitolewa jana Dar es Salaam na Rais wa CWT, Gratian Mukoba, Alisema kuwa kauli hiyo ya Mkuu wa Mkoa ni ya kisiasa na haitekelezeki, kwani kwa mujibu wa sheria, Tume ya Maadili ya Walimu ndiyo yenye wajibu wa kufanya hivyo.

“Mkuu huyo wa Mkoa hana Mamlaka kwa mujibu wa sheria za nchi kwa hiyo anachofanya anakiuka sheria, anavunja sheria. Kwa hiyo sisi tumesikia tamko tunasubiri kuona utkelezwaji wake,” alisema Mukoba.

Aidha, Mukoba alisisitiza kuwa wanaamini kuwa agizo la mkuu huyo wa mkoa haliwezi kutekelezeka kwa kuwa lilitolewa kinyume cha sharia.

Mukoba alieleza kwamba ikiwa litatekelezwa, huyo atakeyekuwa amelitekeleza watamfikisha mahakamani kwani mkuu wa mkoa hana mamlaka ya kumwandikia mtu barua.

Mukoba alisema kwa mujibu wa sheria ya utumishi wa umma ya mwaka 2002 na kanuni zake za mwaka 2005 na Sheria ya Utumishi wa Walimu ya mwaka 2005 na kanuni zake za mwaka 2016, mkuu wa mkoa siyo mamlaka ya nidhamu.

Aliongeza kuwa kwa mujibu wa sheria za nchi hata Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Waziri Mkuu, Waziri, Mkuu wa Mkoa, Wilaya ama mtu yeyote hana mamlaka ya nidhamu juu ya mwalimu.

Alibainisha kuwa kabla mkuu wa mkoa kutoa tamko hilo, alitakiwa kufanya utafiti ili kujua sababu za wanafunzi wa Mkoa wa Mtwara kufeli, kwani kuna sababu nyingi zinazoweza kuchangia matokeo mabovu ya wanafunzi.

Alitaja baadhi ya sababu hizo zinazoweza kuchangia matokeo mabovu kuwa ni mazingira magumu ya walimu kufundisha, mila na desturi za jamii ya watu wa Mtwara ambazo bado hazijaipa elimu kipaumbele na hali ya umasikini.

Alisema kuwa hatua za kinidhamu huwa zina utaratibu wake na kufafanua kuwa lazima kuundwe tume ya kufanya uchunguzi pamoja na kumpa nafasi mwalimu husika kujitetea ili kubaini kama  ana kosa ambalo linaweza kufanya aadhibiwe.

Alisema Katiba ya Tanzania inakataza mtu yeyote kuhumumiwa bila kusikilizwa.

Akizungumzia suala hilo, Waziri Kivuli wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Suzan Lyimo alipinga kitendo cha mkuu huyo wa mkoa kuwashusha vyeo walimu kutokana na Shule za Serikali kufanya vibaya katika matokeo ya mitihani, huku akisema hakuna Sheria yeyote nchini inayompa mamlaka hayo.

“Nashangaa ametoa wapi mamlaka hayo, hata kama angekuwa na mamlaka amejiridhisha kiasi gani kwamba walimu wamechangia wanafunzi kufeli, lakini pia suala la uadilifu wa watumishi hawa linapaswa kuwa chini ya Afisa Elimu sasa ni ajabu kuona RC anaigilia,”

“Kila mtu anafahamu jinsi gani Mtwara hali ya miundombinu ya elimu ilivyo katika mikoa ya pembezoni, shule hazina madarasa ya kutosha, walimu wachache bado wanawacheleweshea mishahara halafu wao bado wanakuwa wahanga wanafunzi wakifeli,” Alisema Suzan.

Duh:Tazama Picha za Hekalu la Mbwana Samatta Analojenga Huko Kigamboni,Ni zaidi ya Hekalu la Diamond..!!

$
0
0
Staa wa Tanzania katika Soka,Mbwana Samatta,ameamua kujenga Hekalu lake kimya kimya Maeneo ya Kigamboni,Imefahamika.


Samatta ambaye anakipiga katika Ligi ya Ubeligiji ,inasemekana ameamua kujenga Hekalu hilo mara baada ya kubomoa iliyokuwa nyumba yake ya awali maeneo ya Kisarawe II.





Noma Sana,Alichokisema Kajala Baada ya Video ya Mwanae Kusambaa Akingonoka Kwenye Gari na Mtu Mzima,Tazama Hapa Livee

$
0
0
kajala
Katika mitandao mbalimbali ya kijamii ipo video iliyosambaa ambayo inamuhusu binti mdogo wa chini ya miaka 18 akifanya mapenzi na mtu mzima ndani ya Gari.
paula-2
Paula Paul katika akiwa na watumishi wa Kajala Entertainment
Awali ilisemekana kuwa katika video ile  binti aliyeonekana ni Paula Paul ambaye ni mtoto wa staa wa  Filamu Tanzania Kajala Masanja ‘K’.kajala-2
Kajala na mwanaye Paulapaula
Paula katika pozi
Kupitia mtandao wake wa Instagram, Kajala amekanusha vikali taarifa juu ya video hiyo na kusema kuwa yule si Paulapaula
Puala na wazazi wake.
“Hey everyone….jamani mimi sina shida na mtu kama akinichukia au akinisema mimi kwa kitu chochote kile…kwasababu najua binadamu kuongea mmezoea..ila katika kuongea kwenu,kuingilia na kujudge my life naomba msimuingize mtoto wangu…sijawahi kumuomba mtu anisaidie kulea hata siku moja…mimi nimeona kuna video insambaa mnasema ni mwanangu na mnajua kabisa sie paula huyo ila ilimradi tu mfurahishe roho zenu…nilinyamaza…ila sasa naona mnakoelekea ni 

pabaya..mnahisi yeye hana moyo? Au mnahisi haumii?.mwanangu anasoma na sitaki mumchanganye na mambo yenu ya kipuuzi…vitu vibaya mnavyo muombea mwanangu viwarudie wenyewe…leave my daughter alone jamani…give us a break..fanyani tu mambo yenu yatakayofanya mpate faida katika maisha”, ameandika Kajala.kajala

Eheeh!! Eti Kofii Olomide Kupiga Show Kwenye Bethidei ya Jack Pemba,Hivi Ndivyo Itakavyokuwa..!!!

$
0
0
Koffi-Olomide
PESA inaongea! Msanii nguli wa Bolingo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Koffi Olomide ‘Mopao’ anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye sherehe ya siku ya kuzaliwa (bethidei) ya pedeshee mwenye jina kubwa Bongo, Jack Pemba inayotarajiwa kufanyika Februari 3, 2017 nchini Uganda.
koffi-olomide-2Hii imethibitishwa na Koffi mwenyewe kupitia kipande cha video kinachosambaa mitandaoni kikimuonesha  akiwahakikishia mashabiki wake kwamba atakuwepo kwenye bethidei hiyo.koffi-olomide-bling-bling2Koffi Olomide ‘Mopao’.
Mopao anaonekana akiwa nyumbani kwake huku akionesha magari kadhaa ya kifahari na kumshukuru Jack Pemba kwa kile alichomfanyia ingawa hajaeleza wazi ni jambo gani amelifanya Jack Pemba kwa Mopao.Jack-Pemba (1)Jack  Pemba
JACK PEMBA NI NANI?
Jack  Pemba ni kijana raia wa Kitanzania anayeishi nchini Uganda, ambaye aliibuka na kupata umaarufu mkubwa mwishoni mwa miaka ya 2,000, baada ya kuwasili akitokea Uingereza, inakosemekana ana mke mzungu na watoto.auntjackEnzi hiozo, Jack Pemba na Aunt Ezekiel.
Akiwa Bongo, Jack Pemba ambaye ni mkali kwa ‘totoz’ aliingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na mwigizaji wa Filamu Bongo, Aunt Ezekiel, ambaye kwa sasa amezaa na dansa wa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Mose Iyobo lakini wakaachana miezi michache baada ya kutoelewana.

Jack Pemba ni maarufu miongoni mwa wanamuziki, kwani ni mmoja kati ya mapedeshee wanaofahamika kwa kutunza kiasi kikubwa cha fedha jukwaani, huku akizawadiwa kwa kuimbwa kwenye nyimbo.Capture Jack Pemba alivyoosha gari lake jipya kwa mvinyo.
TUJIKUMBUSHE

Mwaka jana, Jack Pemba alifanya sherehe ‘bethidei’ ya kufuru wakati akisherekea kutimiza umri wa miaka 42, iliyofanyika kwenye Hoteli ya Speke Resort Munyonyo iliyopo pembezoni mwa Ziwa Victoria, nje ya Mji Mkuu wa Uganda, Kampala.
Capture 3Katika sherehe hizo, kiasi cha shilingi milioni 100 za Uganda ziliteketea, katika sherehe iliyohusisha wageni wapatao 100 ambapo keki kubwa ilikatwa huku waalikwa wakiburudishwa laivu na bendi ya muziki.Katika kile kinachoonekana kama kulibariki gari lake jipya, Range Rover Sport 2016, katika video nyingine, Jack Pemba alionekana akiliosha na mvinyo (Champagne) unaotajwa kuwa ni miongoni mwa mivinyo ghali huku akilifuta gari hilo kwa kutumia noti za dola ya Marekani.

Watu wameanza kujiuliza kwa kuwa ameshazoeleka kufanya kufuru kubwa kwenye sherehe mbalimbali, mwaka huu itakuwaje kwenye bethidei yake? Pia ni kiasi gani cha pesa amemlipa mwanamuziki ghali barani Afrika, Mopao Koffie, hadi akakubali kuwa Special Guest wa Birth Day Party yake? Tusubiri, muda utatuambia! Wenyewe wanasema, Time Will Tell!!!

CHADEMA Kuliburuza Mahakamani Jeshi la Polisi kwa Kukinyima Chama Hicho Uhuru wa Kufanya Kampeni

$
0
0

CHADEMA kuliburuza Mahakamani Jeshi la Polisi kwa kukinyima chama hicho uhuru wa kufanya kampeni za uchaguzi wa udiwani.

Katika uchaguzi mdogo wa kata ya kiwanja cha ndege Jeshi la Polisi lilitumia mabomu ya machozi na kuwakamata wanachama kadhaa wa CHADEMA.

Kama Ulikuwa Hujui, Hawa Ndiyo Vigogo Wauza Madawa ya Kulevya Walioitikisa Dunia ..!!!

$
0
0

madawa sauzi (3)

Labda ulikuwa miongoni mwa watu waliosikia taarifa ya kukamatwa kwa muuza madawa ya kulevya nchini Mexico, Joaquín Guzmán Loera AKA “El Chapo Guzmán”, na ukajiuliza kuhusu wauzaji madawa ya kulevya ambao waliwahi kutokea katika dunia hii.

Wapo wengi ambao walikuwa wauzaji wa madawa ya kulevya, mabilionea ambao mwisho wao ulikuwa mbaya kama Pablo Escobar. Kama ulikuwa huwajui, hii hapa chini ni orodha ya wauzaji madawa ya kulevya hatari ambao wamewahi kuwepo katika dunia hii mpaka sasa.

frank-lucas-aka-superfly

FRANK LUCAS AKA Superfly

Unapowazungumzia wauza madawa ya kulevya ambao wamewahi kuishi katika hii dunia basi hutoweza kuliacha jina la mshikaji huyu, Mmarekani, ‘bitozi’, bilionea ambaye utajiri wake mkubwa ulitokana na uuzaji wa madawa ya kulevya.

Jamaa alivuma sana miaka ya mwishoni mwa mwaka 1960 na mwanzoni mwa mwaka 1970. Jamaa alikuwa na washikaji wengi waliokuwa wakipiga biashara hii haramu. Kila siku, alisafirisha madawa ya kulevya kupitia kwenye majeneza ya watu aliokuwa akiwaua na washikaji zake.

Mwaka 1975, jamaa alivamiwa nyumbani kwake, ndani ya nyumba tu kukakutwa kiasi cha dola laki tano (zaidi ya bilioni moja), kwa kipindi hicho, kilikuwa kiasi kikubwa sana cha fedha. Jamaa alipokamatwa, akafungwa gerezani miaka 75 kwa kesi zaidi ya 100 za madawa ya kulevya.DEA agents bring Jamaican gang leader Christopher "Dudus" Coke From Westchester County Airport to a waiting vehicle, Thursday, June 24, 2010, in White Plains, New York. (AP Photo/David Karp)

CHRISTOPHER COKE AKA: “Dudus”

Jamaa alikuwa mpiga dili mkubwa tu kwenye biashara ya madawa ya kulevya. Alikuwa Mjamaika, mwenye sura ya kipole, kusaidia watu ambapo baada ya kugundulika kwamba anafanya biashara hiyo, hakutaka hata kutafutwa, mwenyewe akajipeleka polisi mwaka 2010.

Mshikaji aliingiza kiasi kikubwa cha fedha, mpaka kukamatwa kwake alikuwa ameingiza kiasi cha dola bilioni 30 (zaidi ya trilioni 60) ambapo kwa sasa tungesema kwamba yeye ni tajiri wa 18 duniani.

Japokuwa alikuwa na ubaya wake wa kufanya biashara hiyo haramu lakini mshikaji alikuwa mtu wa watu. Alikuwa akijenga hospitali, kufanya biashara nyingine na kuwaajiri watu wengi, aliwasaidia masikini na kuwafurahisha kwa kuyaboresha mazingira yao japokuwa upande wa nyuma, aliteketeza vijana kwa kuwauzia biashara hiyo.

griselda-blanco-aka-the-cocaine-godmother

GRISELDA BLANCO AKA: “The Cocaine Godmother”

Unaweza kumchukulia poa tu kwa sababu ni mwanamke lakini ni lazima ujue kwamba kwa watu waliokuwa wakifanya biashara ya kulevya kwa kiasi kikubwa huwezi kumuacha huyu mwanamke.

Alikuwa mtu wa dili, mbali na uuzaji wa madawa hayo, pia alikuwa muuaji mzuri tu ambaye kwa kipindi chote cha kufanya biashara yake, aliwaua watu 200 kwa risasi, tena kwa mkono wake mwenyewe.

Baada ya kufanya biashara hiyo kwa miaka kadhaa, akakamatwa na kufungwa miaka 20 gerezani, ila cha kushangaza sasa, akiwa hukohuko nyuma ya nondo, michongo yake ya biashara ilikuwa ikisonga kama kawa.

Mwaka 2004 akatolewa gerezani lakini ilipofika mwaka 2012, akauawa kwa kupigwa risasi na mshikaji aliyekuwa akiendesha pikipiki. Huo ukawa mwisho wake, akazikwa ingawa bado anajulikana kama mfanyabiashara mkubwa wa biashara hiyo haramu.mellylee-freeway-rickross-4

Rick Ross AKA: “Freeway”

Siyo huyu unayemjua wewe! Siyo yule jamaa mwenye mwili mkubwa, mwanamuziki wa Kimarekani, achana na huyo, mshikaji mwenyewe alilichukua jina la Rick Ross kutoka kwa huyu jamaa.

Mwili mdogo, mtanashati, alipenda kutabasamu lakini nyuma ya tabasamu lake, jamaa alikuwa ‘mbaya’ kwenye biashara ya madawa ya kulevya.

Jamaa alianza kufanya biashara hiyo miaka ya 1980. Alianza kama ‘punda’ yaani mbebaji lakini baadaye akajizatiti na kuwa na biashara yake mwenyewe. Jamaa alikuwa akiuza mzigo wa dola milioni 3 (zaidi ya bilioni 6) kila siku iendayo kwa Mungu. Mshikaji alikuwa akiuza kilo 400 kila wiki.arturo-beltran

Arturo Beltrán Leyva AKA: “Boss of Bosses”

Kama washikaji wa hapo juu, hata huyu mwana alikuwa nuksi kwenye uuzaji wa madawa ya kulevya. Mshikaji alikuwa na kundi lake liitwalo Beltran Leyva Cartel, kundi lililosumbua sana nchini Mexico.

Kulikuwa na kesi nyingi dhidi ya kundi hilo, watu walikuwa wakiuawa, wanawake walibakwa, walisafirisha sana silaha kwenda sehemu mbalimbali, wengine waliteswa na kutekwa. Kwa kifupi, kundi hili lilikuwa hatari zaidi kuliko makundi mengine yaliyowahi kutokea huko.

Jamaa aliuawa na wanajeshi wa majini mwaka 2009 katika majibizano ya kurushiana risasi na wanajeshi hao.

felix

Felix Mitchell AKA: “The Cat”

Jamaa alikuwa si kitoto, huyu ni miongoni mwa wauza madawa ya kulevya wakubwa waliowahi kutokea duniani. Alikuwa na kundi lake liitwalo 69 Mob. Jamaa alikuwa akipiga dili za chinichini, ilikuwa vigumu kukamatwa kwani alikuwa mjanja kupindukia.

Alipokamatwa, alifungwa jela miaka mingi tu ila wakati akiwa ametumikia kifungo kwa miaka miwili, kuna jamaa hukohuko jela akamuua kwa kumchoma kisu, hiyo ilikuwa mwaka 1986 na mazishi yake yalihudhuriwa na watu wengi, sawa na mazishi ya aliyekuwa mwanaharakati, Martin Luther King Jr.amado-carrillo-fuentes

Amado Carrillo Fuentes AKA: “Lord of the Skies”

Alikuwa Mmexico aliyekuwa akifanya biashara ya madawa ya kulevya kwa kiasi kikubwa. Hakuwa mkuu wa kitengo, aliajiriwa na bosi wake aliyeitwa Rafael Aguilar Guajardo ila akaamua kumuua na kushikilia yeye hicho kitengo.

Ndiye muuzaji pekee wa madawa ya kulevya aliyekuwa akiingiza kiasi kikubwa nchini Marekani kuliko mtu yeyote.

Alikuwa bilionea, mwenye kupenda watu na kusaidia masikini. Hakuwa na utani katika biashara hiyo, aliua wote aliohisi kwamba walikuwa watu wabaya katika biashara yake.

Alitumia ndege zake kusafirisha madawa ya kulevya kwenda nchini Marekani mara nne kwa siku. Kumkamata haikuwa kazi nyepesi kwa sababu alikuwa akibadilisha sura yake kwa kuvaa sura ya bandia.

Mwaka 1997 alipokuwa akifanyiwa upasuaji wa kuwekewa sura ya bandia katika Hospitali ya Santa Monica nchini Mexico, dawa zilizidi hivyo kufariki dunia na baada ya siku mbili, wale madaktari waliofanya upasuaji huo wa kumuwekea sura ya bandia wakakutwa wameuawa kinyama na miili yao kutupwa.

escobar

Pablo Escobar AKA: “The World’s Greatest Outlaw”

Huyu jamaa alikuwa kiboko, ni Mcolombia aliyekuwa akiuza madawa ya kulevya kwa kiasi kikubwa. Alikuwa katili, kuua watu waliokuwa kinyume naye ilikuwa ishu ndogo sana kwake.

Hakutaka mchezo, hakuwahi kuweka fedha benki, alikuwa akizihifadhi ndani na wakati mwingine zilikuwa zikiliwa na panya. Kuna kipindi mtoto wake alikuwa akiumwa, alizitumia dola za Kimarekani kumuwashia moto, eti kupoza baridi lililokuwa likimpiga,  kitu kilichowakasirisha sana Wamarekani, waliona wamedharauliwa sana mpaka noti yao kuchomwa moto.

Alikuwa na utajiri mkubwa na mwaka 1989 alitangazwa kama tajiri wa saba duniani akiwa na utajiri wa dola bilioni 25 (zaidi ya shilingi trilioni 50). Jamaa alikuwa akimiliki 4/5 ya soko kubwa la madawa ya kulevya duniani.

Jamaa alikuwa akisafirisha tani 15 za madawa ya kulevya kila siku barani America. Jamaa aliua majaji 30 waliokuwa wakisimamia kesi zake na polisi 400 ambao walionekana kimbelembele kumfuatilia kwenye mishe zake na pia aliilipua ndege aina ya Avianca Flight 203 ambayo ilikuwa ikimbeba waziri mkuu wa kipindi hicho nchini Colombia.

Kwa kifupi, jamaa alikuwa na pesa ndefu kiasi cha kuiambia serikali yake kwamba imuache afanye mishe zake kwani angelipia deni la dola bilioni 20 (zaidi trilioni 40) lililokuwa ikidaiwa, ila serikali ikakaata na kumuua.

el-chapo

Joaquín Guzmán Loera AKA “El Chapo Guzmán”

Hapa ndipo kwenye kazi sasa. Huyu anaonekana kama mwamba wa biashara hii ya madawa ya kulevya. Ni Mmexico mwenye mkwanja mrefu ambapo amekuwa akiupata kupitia biashara yake haramu.

Alikuwa mtu anayetafutwa kwa nguvu zote kabla ya kukamatwa. Aliwekeza nguvu kubwa katika biashara hii, Wamarekani na Wamexico walimtafuta lakini hawakumpata.

Wakati wakiwa na uchungu naye, wakafanikiwa kumpata na hivyo kufungwa nchini Mexico. Kutokana na fedha alizokuwa nazo, inasemekana kwamba aliwahonga askari magereza na kutoroka kwa kupitia katika bomba la choo, unaamini hilo?

Wamarekani walikasirika sana, wakaahidi kumtafuta, kweli wakaingia mzigoni. Hawakuchukua muda sana, wakamnasa na hivyo kuiambia Serikali ya Mexico kwamba watamfunga wao wenyewe ili wamuonyeshee kwamba wao si watu wa mchezo, kweli wakamfunga na mpaka leo hii yupo gerezani akiendelea kutumikia kifungo chake ambacho hakikuwekwa wazi ni cha muda gani.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>