Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Shilawadu Kazini!! Utata Waibuka Juu ya Mtoto wa Ray na Chuch Hans,Ray Akana Hana Mtoto Hivyo Asichuriwe ..!!!

$
0
0
ray-4
Ray na Chuchu.
UTATA mzito umeibuka kuhusiana na mtoto aliyezaliwa na msanii wa filamu Bongo, Chuchu Hans ambapo mashabiki wengi wametaka kujua kama mtoto huyo ni wa Vincent Kigosi ‘Ray’ au nani na kwa nini kuna usiri mkubwa juu ya kuzaliwa kwa mtoto huyo?

Ishu ya mimba awali kulikuwa na usiri mkubwa sana kuhusiana na ujauzito wa Chuchu ambapo mara kadhaa alipobanwa na mwandishi wetu alikana kuwa na mimba huku Ray naye akidai hajui lolote kuhusiana na ujauzito wa mpenzi wake huyo.

”Mimi sina ujauzito, watu wanasema tu na kama unataka kuhakikisha, nitakuja hapo ofisini kwenu mnipige picha,” alisema Chuchu lakini kila alipoombwa kuonana na mwandishi wetu alikuwa akichenga. Hata hivyo, kwa kuwa ujauzito haujifichi baadaye ilikuja kubainika kuwa, Chuchu ana mimba kubwa ya kujifungua wakati wowote.ray-6
Taarifa za kujifungua siku chache baadaye zilivuja taarifa kuwa, Chuchu kajifungua mtoto wa kiume lakini cha ajabu bado wahusika hao waliendelea kuwa wasiri na hata walipopigiwa simu kuulizwa, walitofautiana kwenye majibu yao.

Msikie Ray mara baada ya Chuchu kudaiwa kujifungua, paparazi wetu alimpigia simu Ray lakini katika hali ya kusha-ngaza, alionesha kutojua lolote.

“Unanipa hongera ya nini? Mimi sina mtoto bwana, hizo habari naziona tu mitandaoni, msinichurie,” alisema Ray.

Chuchu akubali

Wakati Ray akisema hana mtoto, Chuchu alikiri kujifungua mtoto wa kiume huku akim-shukuru Mungu kwa kumzalia mpenzi wake salama.ray1

Madai mazito

Hata hivyo, wakati kukiwa na taarifa tofauti kuhusiana na kujifungua kwa Chuchu, mtu wa karibu wa mastaa hao aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini alimwaga ubuyu akisema:

“Chuchu kajifungua ila inadaiwa mtoto si wa Ray na ndiyo maana amekuwa mgumu sana kuzungumza. Sura ya mtoto inaonekana haipo kwa Ray wala Chuchu, sasa katika mazingira hayo si unajua mwanaume lazima ustuke.

“Maana unaweza kujishebedua kuwa mpenzi wako kakuzalia mtoto, kumbe si wako. Kwa hiyo ishu ni je, mtoto huyo ni wa Ray au kuna baba mwingne, nadhani Ray akijiridhisha kuwa ni damu yake, atafunguka.”
Kufuatia madai hayo kuwa mtoto si wa Ray, mwandishi wetu alizungumza na Ray tena lakini safari hii alionesha kuna kitu anachokificha kwani alitoa maneno ya kushangaza akisema:

“Mimi watu wananiambia Chuchu kajifungua mbona bado na aliyesema kuwa mimi sijui kama mtoto ni wangu ni nani? Mbona watu wanatunga sana maneno, unajua sio kila mtu anapenda kuweka wazi mambo yake jamani, haya ni maisha yangu, muda wa kuongea ukifika nitasema.”
ray-5
Chuchu naye ajikoroga

Kuhusiana na madai kuwa, mtoto aliyejifungua si wa Ray, Chuchu alijikoroga katika kutoa maelezo kwani safari hii alikana kujifungua akisema, eti muda huo alipokuwa akiongea na mwandishi wetu alikuwa hospitalini akijisikilizia.

“Kwani Ray alishakana kuwa mtoto si wake? Mbona mimi sijajifungua ndio kwanza nipo hospitali, kuhusu kuficha mimba mwanzo hatukutaka kwa sababu ya mambo binafsi sasa ndio tumeamua kuweka wazi ujauzito na mtoto akipatikana tutaweka wazi. Hapa nipo Muhimbili, natarajia mtoto lakini bado.”
Kuna kitu kinafichwa

Kufuatia utata huo uliopo kuhusiana na mtoto huyo aliyezaliwa, inaonekana wazi kuna kitu kinafichwa ambapo wapo wanaosema labda wanatafuta kiki na wengine kusema huenda ni kweli kuna utata juu ya baba wa mtoto.
ray-3 NB

Kujifungua kwa mwanamke ni jambo la heri hivyo hakuna sababu ya Chuchu na Ray kuendelea kulifungafunga na badala yake wawe wawazi ili pongezi ziweze kuwamiminikia kwa wakati muafaka.


Mahakama Yaridhia Umeya wa Mtoto wa Marehemu Sitta Manispaa ya Kinondoni..!!!

$
0
0

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemtambua Benjamin Samweli Sita (pichani) kuwa meya wa Kinondoni. Hukumu hiyo imetolewa leo baada ya mahakama kutupilia mbali hoja za upande wa pili Ukawa waliofungua kesi kupinga matokeo ya ushindi huo.

Itakumbukwa kuwa, siku ya uchaguzi huo, polisi waliwakamata baadhi ya viongozi na wajumbe wa UKAWA sambamba na ongezeko la wajumbe batili upande wa CCM.

CHADEMA na Ukawa walifungua kesi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kupinga ushindi Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta huku walalamikaji wakiwa ni Mustapha Muro (aliyekuwa mgombea Meya Manispaa ya Kinondoni) na Jumanne Amir Mbunju (aliyekuwa mgombea Naibu Meya wa Manispaa hiyo) wote wakiwakilisha na Wakili wa CHADEMA, John Malya.

Kesi iliyofunguliwa dhidi ya Afisa Utawala wa Manispaa ya Kinondoni, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Samweli Sita (aliyetangazwa kuwa Meya) na Manyama Mangaru (aliyetangazwa kuwa Naibu Meya).

Ubuyu Mpya!! Meneja wa Diamond Atangaza Ujio wa Tamasha la Diamond Are Forever 2017,Litafanyika Uwanja wa Taifa

$
0
0
Meneja wa Diamond Platnumz, Sallam SK aka ‘Fundi Mitambo’ ametangaza ujio mpya wa tamasha kubwa la Diamonds Are Forever 2017 ambapo safari hii litafanyikia katika uwanja wa Taifa.

Muimbaji huyo alifanya tamasha hilo kwa mara ya kwanza nchini mwaka 2012 katika ukumbi wa Mlimani City show ambayo ilihudhuriwa na watu wengi kwa kiingilio cha Tsh 50,000.

Sallam akizungumza live na mashabiki katika mtandao wa Istangam (Insta Live) alisema show hiyo ipo kwenye maandalizi na itafanyika uwanja wa Taifa.

“Mjiandae na Diamonds Are Forever 2017, Diamonds Are Forever 2017 is back,” Sallam aliwaambia mashabiki. 

Meneja huyo alidai safari hii tamasha hilo litafanyika uwanja wa taifa ili kuwapa fursa watu wengi zaidi ya kuudhuria.

Hata hivyo hakuweka wazi ni lini au mwezi gani tamasha hilo litafanyika.

Kuhusu Issue ya Njaa,Warioba Afunguka ,Adai Nchi Ina Njaa Kali,Aitaka Serikali ya JPM kugawa Chakula Haraka

$
0
0
 
WAZIRI Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba, amesema zipo kila dalili ya nchi kukumbwa na upungufu wa chakula, hivyo wanasiasa bila kujali itikadi zao, wanapaswa kuungana kubuni mikakati na hatua za kuchukua kudhibiti hali hiyo.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mwenyekiti huyo wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba alisema si sahihi kuendelea kubishana kuwa nchi ina njaa au haina, wakati dalili zinaonesha uwezekano wa kukumbwa na upungufu wa chakula.

“Watanzania tuwe pamoja kulikabili hili kama tulivyokuwa tukifanya huko nyuma. Hili ni suala la kitaifa, ni lazima tuungane kujua wakati huu tunafanya nini na hali ikiharibika tufanye nini, tusilifanye suala hili kuwa la kisiasa,” alionya Jaji Warioba.

Alisema nchi kukumbwa na upungufu wa chakula ni jambo la kawaida na si jipya, kwa vile limekuwa likitokea miaka ya nyuma kutokana na sababu mbalimbali, ikiwamo mvua kutonyesha kwa wakati.

Huku akieleza jinsi Rais wa Awamu ya Kwanza, Julius Nyerere alivyokuwa akihimiza wananchi kulima na kuhifadhi chakula ikitokea nchi inakumbwa na upungufu wa chakula, alitaja mambo manne yanayopaswa kufanyika ili kukabiliana na kadhia hiyo.

Sakata la nchi kukumbwa na njaa liliibuka katika maeneo mbalimbali huku vyombo vya habari vikiripoti taarifa za wananchi kushindia maembe na mifugo kufa, kutokana na ukame.

Wanasiasa na wasomi walizungumzia jambo hilo na kuitaka Serikali kuchukua hatua za haraka huku viongozi wa dini wakienda mbali zaidi na kuwataka waumini wao wafanye hija, mfungo, mikesha na maombi ili kunusuru hali hiyo.

Jumatatu wiki hii, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema Serikali itagawa tani milioni 1.5 za chakula zilizobaki msimu uliopita katika maeneo yenye uhitaji mkubwa ili kupunguza kasi ya ongezeko la bei za vyakula nchini, lakini akakana taarifa kuwa nchi ina njaa.

Wakati Majaliwa akitoa ufafanuzi huo, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles Tizeba, alisema Serikali kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), katika mwaka wa fedha wa 2016/17 imepanga kununua tani 100,000 za chakula, na hadi Januari 8, wakala huyo alikuwa amenunua tani 62,087 za mahindi.

Lakini jana, Jaji Warioba alisema licha ya nchi kujitosheleza kwa chakula kuna baadhi ya maeneo yana upungufu unaosababisha utegemezi wa chakula kutoka sehemu zingine za nchi.

“Ndiyo maana tumekuwa na mikoa ambayo inasikifika kwa uzalishaji chakula. Lakini mwaka huu kwa dalili hizi na mambo yanayoambatana na mabadiliko ya tabianchi, inaonekana kutakuwa na upungufu wa chakula kwa sehemu kubwa,” alisema.

Aliongeza, “hii inatokana na mvua kutonyesha kama inavyotarajiwa. Hili si jambo jipya limewahi kutokea miaka ya nyuma.”

Alisema kwa kuwa kuna dalili za upungufu wa chakula ni lazima kujiandaa kukabiliana na hali hiyo, ikiwamo kuhadharisha wananchi.

“Pia lazima kusaidia wananchi kutumia njia zitakazowawezesha kupata mazao. Hilo linapaswa kufanywa na Serikali na watu wa kada mbalimbali. Hapa wananchi wanaweza kupewa elimu au mbegu zinazostahimili ukame,” alisema.

Alisema, “bado tuna muda maana kuna sehemu ambazo zinapata mvua za vuli. Licha ya mvua kutonyesha kama ilivyozoeleka, wananchi washauriwe kuzitumia vizuri, ni wajibu wa Serikali kusaidia wananchi hata kama wanahitaji mbegu.”

Kwa mujibu wa Jaji Warioba, nchi inapokumbwa na upungufu wa chakula, wananchi pia wanapaswa ama kulima au kuhifadhi chakula na si kusubiri Serikali ishughulikie suala hilo.

“Nakumbuka mwaka fulani nchi ilikumbwa na upungufu wa chakula, Serikali iliwataka wananchi walime. Nakumbuka Nyerere aliwaeleza wananchi walime, la sivyo tutakufa na watu walilima kila mahali,” alisema na kuongeza:

“Wenye uwezo wanunue chakula na kukitunza. Haifai tuanze kulumbana, maana mwisho wa siku Serikali itajitahidi kuziba pengo la upungufu kama upo,” alisema.  

Aliongeza kuwa viongozi bila kujali vyama, jambo la kwanza wanalopaswa kufanya ni kuhimiza wananchi watumie mvua zinazonyesha sasa kupanda mazao, pili, kutathmini hali ilivyo na kama itatokea waamue watafanya nini.

Alisema si sahihi kuendelea kubishana kuwa nchi ina njaa au haina njaa, wakati dalili zinaonesha uwezekano wa kukumbwa na upungufu wa chakula.

“Watanzania tuwe pamoja kulikabili hili, kama tulivyokuwa tukifanya huko nyuma. Hili ni suala la kitaifa hivyo ni lazima tuungane,” alisema.

Hatarii!! Mvua Kubwa Yanyesha Nyumbani kwa Magufuli na Kuua Mmoja..!!!

$
0
0

NYUMBA 49 zimeezuliwa na kubomolewa huku Neema Masunga (27) akipoteza maisha kwa kupigwa na radi kutokana na mvua iliyoambatana na upepo na radi kunyesha kwenye machimbo ya Matabe kijijini Bwanga wilayani Chato mkoani Geita.

Katika tukio hilo, la juzi nyumba 11 zilibomolewa na 38 kuezuliwa mapaa na kusababisha familia kukosa mahali pa kuishi na wengine kulazimika kujihifadhi kwa majirani.

Tukio hilo lilitokea saa mbili usiku baada ya mvua iliyoambatana na upepo mkali na ngurumo za radi kunyesha kwa nusu saa.

Mwenyekiti wa eneo hilo, Jackson Kusekwa alisema marehemu Neema ameacha watoto watano, mmoja akiwa wa wiki mbili.

Alisikitishwa na tukio hilo lililotokea kwenye kipindi kigumu cha njaa kwa waakzi wa Matabe baada ya mazao waliyolima yakiwamo mahindi kukauka kwa jua.

Alisema Neema alipoteza maisha baada ya kupigwa na radi akiwa chumbani akimnyonyesha mwanawe huyo ambapo radi ilimrusha hadi sebuleni na kufariki dunia.

“Radi ilimrusha hadi sebuleni na mtoto akabaki chumbani…imeharibu sana nyumba kwani imepasuka, kwa ujumla tuna hali mbaya sana, wananchi kwa sasa wanaishi kwa shida wengine wamehamia kwa majirani ili kujihifadhi baada ya nyumba zao kubomolewa,” alisema Kusekwa.

Mmoja wa wanakijiji, Abel Charles alisema baada ya hali hiyo wananchi walikusanya mabati yaliyoezuliwa na katika harakati hizo walipata taarifa za mtu kufariki dunia na ndipo wananchi walijikusanya na kwenda eneo la tukio na kushuhudia mwanamke huyo akiwa amepoteza maisha.

Mama mzazi wa marehemu, Mariam Masunga (78) alisema, binti yake amemwachia watoto hao na mdogo kabisa anayehitaji msaada kwani hata yeye kwa umri wake alikuwa akimtegemea mwanawe huyo.

“Naomba msaada wa kulea watoto hawa...mimi sina uwezo, kwani nimezeeka katika maisha yangu nilikuwa namtegemea mwanangu ambaye sasa amefariki dunia, naiomba Serikali inisaidie,” alisema Mariam huku akiangua kilio.

Aidha, Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Chato ambaye ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Shabaan Ntarambe alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa alituma wajumbe wa kamati yake kufuatilia kabla ya kutoa taarifa hizo.

“Nimemtuma OCD (Mkuu wa Polisi Wilaya) kufuatilia hilo tukio; ni kweli limetokea akishatoka huko nitatoa taarifa baadaye,” alisema Mkuu wa Wilaya.
 
NB:Wilaya ya Chato Iko Mkoa wa Geita anapotoka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dk John Pombe Joseph Magufuli.

Nay Bwanaa!! Eti Nayeye Kaamua Kutaja Wasanii Wake Watano Wanaomkuna..!!!

$
0
0

Rapa Nay wa Mitego ameweka wazi wasanii watano wakali wa hip hop ambao amekuwa akiwasikiliza na kuwakubali siku zote kutokana na kazi zao katika muziki wa hip hop Tanzania. 

Nay wa Mitego alisema hayo kwenye kipindi cha Planet Bongo na kusema msanii wa kwanza ambaye yeye anakumbali na kumuheshimu ni Mr 2 maarufu kama '2 Proud' kwani huyo ndiye aliyemfanya yeye kuanza kuimba na anatamani kuona anaendelea kufanya muziki siku zote kwani akiwa anasikiliza kazi zake mpaka leo huwa anafurahi.

Mbali na Mr 2, Nay wa Mitego alisema rappa wa pili anayemkubali ni Fareed Kubanda, wa tatu ni Mr Blue, wa nne ni Mwana FA na rappa watano ni Nay wa Mitego mwenyewe ambaye anajua mashabiki zake wanataka nini na kuwapa muziki mzuri siku zote. 

Ommy Dimpoz Afunguka Skendo ya Kuwekwa Kinyumba na Jimama Maeneo ya Mbezi

$
0
0
Msanii wa muziki wa bongo fleva Ommy Dimpoz amekanusha tetesi zilizozagaa kwamba amewekwa ndani kimapenzi maeneo ya mbezi  na jimama ambalo lina mahusiano naye kumapenzi.

Akiongea kupitia eNEWZ ya EATV, Ommy amesema kwa sasa anaishi Mikocheni Dar es Salaam na hajawahi kuwekwa ndani na mwanamke yeyote kwa kuwa anasema mpenzi wake wa sasa ni mchina na hajawahi kuwa na mahusiano na mwanamke wa kizungu na kwamba hizo ni story za watu ambao waliamua kuvumisha.

Hata hivyo Ommy amesema kwa sasa anajenga nyumba yake maeneo ya Mbezi na Kigambona hivyo hana nyumba ambayo amepangisha au kupangishiwa Mbezi na mambo yatakapokuwa wazi atamuweka wazi mpenzi wake.

Ebwana Weee!! Umesikia Alichokisema Said Fella Juu ya Mziki wa Taarabu na Mipango ya Kundi Lake la Yah TMK Taarab?

$
0
0
Meneja ambaye amejizolea umaarufu mkubwa kutokana na mchango wake wa kuinua vipaji vya wanamuziki wachanga hadi kuwa maarufu, Saidi Fella ‘Mkubwa Fella’ amedai muziki wa taarab haujakufa kama baadhi ya watu wanavyodai.

Mkurugenzi huyo wa Yamoto Band ambaye ameingia kwenye muziki wa taarab kwa kuanzisha bendi ya ‘Yah TMK Taarab’ amedai hakuna ukweli wowote kwamba muziki wa taarab umekufa.

“Mimi siamini kwamba muziki wa taarab umekufa, mashabiki wapo wanazaliwa kila siku wanataka muziki mzuri,” Mkubwa Fella alikiambia kipindi cha Jahazi ya Sham Shama ya ITV.

Fella amesema yeye pamoja na bendi yake hiyo wamejipanga kuleta ushindani mpya kwenye muziki wa bendi kwa kuachia kazi nzuri.

“Ukija kwenye Yah TMK Taarab utapata kila kitu, sasa hivi tupo chimbo tunaanda kazi nzuri, kwa sababu ingawa tuna watu ambao wanamajina makubwa au wana uwezo mkubwa lakini mashabiki hawataki majina, wanataka kazi, kwahiyo sisi tumejipanga vizuri na tunakuja kutoa burudani kwa sababu mashabiki wapo wengi wanataka kazi,” alisema Fella.

Umeipata Hii ya Toleo Jipya la Simu ya iPhone 8,Eti Itakuwa na Uwezo wa Kutambua Sura za Watu..!!

$
0
0

Toleo lijalo la simu za Apple, iPhone 8, itakuja na uwezo wa kutambua sura za watu.

“Other features appear to include some form of facial/gesture recognition supported by a new laser sensor and an infrared sensor mounted near the front-facing camera and, as expected, should also finally include wireless charging,” alisema, Timothy Arcuri toka kampuni ya utafiti ya Cowen and Company.

Simu hizo zinatarajiwa kuzinduliwa September mwaka huu na zinatarajiwa kushuka bei zake kwa asilimia 30 hadi 50.

Msajili wa Vyama Ashikilia Msimamo wake Wa Kumtambua Profesa Lipumba kama Mwenyekiti wa CUF

$
0
0
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amesema hana hofu ya kuchafuliwa kutokana na tuhuma zinazotolewa dhidi yake, huku akisema msimamo wake uko palepale na kwamba anamtambua Profesa Ibrahim Lipumba kama Mwenyekiti wa CUF na Maalim Seif ni Katibu Mkuu.

Kauli ya Jaji Mutungi imekuja baada ya taarifa na kauli za matusi na kejeli zilizomuhusisha yeye na ofisi yake kusambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii baada ya kuidhinisha zaidi ya Sh300 milioni za ruzuku kwenda kwenye akaunti ambayo kamati ya uongozi ya CUF ilidai siyo ya chama hicho.

Taarifa za msajili kuingiza fedha hizo kwenye akaunti hiyo na baadaye kutolewa kwa njia ambayo inaonekana kutia shaka zilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, Julius Mtatiro ambaye alilinganisha suala hilo na uchotwaji wa zaidi ya Sh300 bilioni zilizokuwa kwenye akaunti ya Tegeta Escrow.

Kupitia taarifa yake jana, Jaji Mutungi alisema kuna mbinu zinazopangwa na wanaojiita Kamati ya Uongozi ya CUF ambayo ofisi yake haiitambui, huku akisisitiza kumtambua Profesa Lipumba kama mwenyekiti wa CUF na Maalim Seif kuwa Katibu Mkuu.

Jaji Mutungi ambaye mwishoni mwa mwaka jana alifunguliwa kesi Mahakama Kuu na bodi ya wadhamini wa CUF ikiiomba itoe amri ya kubatilisha barua ya mlezi huyo wa vyama vya siasa inayomtambua Profesa Lipumba kuwa mwenyekiti wa CUF, alisema kauli zinazotolewa mitandaoni zina lengo la kuchafua ofisi yake.

“Tayari mbinu hizo zimeanza kutekelezwa na viongozi wa kamati hiyo kwa kusambaza habari za kudhalilisha katika vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ya kijamii kama Facebook na mingineyo,” alisema. 

Msajili huyo alisema moja ya mkakati huo ni taarifa iliyosambazwa juzi na Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Habari wa CUF,, Mbarala Maharagande ya kejeli, matusi, tuhuma na dhihaka kwake.

Jaji Mutungi alisema hivi karibuni, Maharagande alizungumza na waandishi wa habari huku akidai kuwa ofisi ya msajili inasababisha mpasuko ndani ya chama hicho na ndiyo maana imetoa ruzuku kwa Profesa Lipumba.

Licha ya tuhuma hizo, Jaji Mutungi alisema kwamba haogopi kuchafuliwa akizingatia ukweli kwamba yeye ni mtumishi wa umma na anafanya kazi zake akiwatumia wananchi kwa mujibu wa sheria za nchi.

Alisema kamwe hawezi kuyumbishwa na matusi wala kejeli zinazotolewa dhidi yake pamoja ofisi anayoiongoza.

“Nimezipata hizo taarifa kwamba kuna baadhi ya watu wamepanga kupambana nami kwa kunichafua, japo naendelea kuzifanyia kazi lakini waache wanichafue, wala siogopi lolote,” alisema. 

Hata hivyo, Jaji Mutungi alisema mjadala wa ruzuku ya CUF aliyotoa kwa chama hicho ameshaufunga na anashangazwa na maneno yanayozidi kusambazwa na watu wanaojiita viongozi wa CUF.

Alipotafutwa  kuzungumzia tuhuma hizo, Maharagande aliendelea kusisitiza kuwa kauli iliyotolewa wakati alipofanya mkutano na vyombo vya habari ipo hivyo na kwamba waliitisha mkutano kumjibu msajili ambaye alifanya mkutano na waandishi wa habari siku moja kabla kuhusu masuala ya CUF.

Darassa Ana Fursa ya Kuingiza Mamilioni ya Shilingi Kwa Show za Kenya

$
0
0
Akiwa anajitayarisha kutoa album yake mwaka huu wa 2017, rapper Darassa hivi sasa ana uwezo wa kujiunga na wanamuziki wa kuimba wa Bongo Flava nguli Diamond Platnumz, Rais CEO wa kampuni ya muziki Africa WCB na hasimu wake wajadi kimuziki si mwingine bali ni Mfalme wa Bongo Flava Africa Alikiba, kwa kuwachuna Wakenya mamilioni ya pesa kwa hiyari yao kupitia ufanisi wake kimuziki na umaarufu unaozidi kupanda kila uchao hapa nchini Kenya.


Nikianzia na mjini Mombasa uswahilini hapa, nakupatia hali halisi jinsi ilivyo. Nakutembeza katika mitaa kadha wa kadha ambapo mashabiki wa muziki wa kizazi kipya wameupokea wimbo wa rapper Darassa ‘Muziki’ kwa taadhima na heshima kubwa. Kuanzia kitongoji cha Lights, Soko Mjinga, Kisauni, Mwandoni, Mtopanga, Bombolulu, Bamburi hadi kuvuka ng’ambo ya pili ya Ferry Likoni mpaka Ukunda nyimbo, ‘Muziki’ inatamba kwa kasi zaidi ya mawimbi mazito baharini.

Mbali na Pwani ya Kenya, sehemu za nyanda za juu na Ziwa Victoria hadi Kisumu na Kenya yote kwa jumla. Kituo cha redio maarufu zaidi nchini cha Citizen, kupitia kipindi cha Mambo Mseto kinachoendeshwa na mtangazaji anayependwa sana na vijana Afrika Mashariki Mzazi Willy M Tuva, huwa kipimo kamili cha ni mwanamuziki gani anayetamba kwa sana Afrika Mashariki katika msimu fulani kwa kupitia requests zinazotumwa na mashabiki kwa kuitisha nyimbo za wasanii wanaowakubali.

Msimu huu Darassa ameivunja rekodi kwa jinsi nyimbo yake ya Muziki inavyoombwa kwa sana si radio Citizen pekee bali hadi vituo vingine mbalimbali hata vile vinavyotangaza kwa lugha ya jamii fulani ama lugha ya mama hapa Kenya.

Kimtazamo mji wa Mombasa ndio kitovu cha mafanikio kwa wasanii wengi wa Bongo Flava kutamba nchi Kenya wanaobobea na waliobobea na kufifia kimuziki. Nikiwataja baadhi tu wakiwemo Mr Nice ‘’Mzee wa Fagilia, Mr. Blue jamaa la ‘Mapozi’, Ray C ‘Mrembo wa Wanifuatia nini’, Lady Jaydee ‘Dada wa Siku hazigandi’, Proffessor Jay ‘Nguli wa Zali la Mentali’, Ferooz ‘Kigogo wa Starehe.’ Alikiba, ‘Jamaa wa Cinderella’, Diamond Platnumz ‘Raisi wa Kamwambie’ Yamoto Band ‘Vijana wa Nitakupelepweta’ na wengine wengi.

Hii inapelekewa na sababu ya kuwa watu wanaoishi katika pwani ya Kenya wengi wao hutumia Kiswahili na tokea jadi kabla ya muziki wa kizazi kipya kuiteka nyara anga ya muziki wa pwani nchini Kenya wamekuwa wakipenda sana muziki wa Taarabu ambao asili na chimbuko lake ni nchi ya Tanzania hivyo wa pwani wanajua utamu wa Bongo Flava kabla kusambaa sehemu zengine za nchi ya Kenya.

Kwa sasa wimbo, Muziki umekuwa kama wimbo wa taifa. Unaongoza kwa kuwa wimbo unaoitishwa na kuchezwa zaidi na Asilimia zaidi ya themanini ya vituo vya redio hapa nchini Kenya.
Unapoingia kwa matatu(Daladala), kuna msemao unaopewa abiria mwenye maneno mengi na utingo chambilecho pale mtu anapolalamikia nauli imepanda unajibiwa na mstari katika wimbo ‘Muziki’ (Acha maneno weka muziki). Kwakweli Darassa ametia watu wengi skuli(shule), sasa kazi ni kwake…mashabiki nchini Kenya wana kiu na hamu ya kumuona LIVE. Sasa kama soko limefunguka, kaka Darassa wangojani?

Makala ya: Changez Ndzai (Kenya)

Darasa Asideal na Muziki Kwa Sasa, A Deal na Kukuza Brand Yake

$
0
0

Producer wa muziki anayekuja juu kwasasa hapa nchini
ambaye anafanya kazi katika studio za Mj Records,
Daxo Chali amefunguka kupitia kipindi cha Bongo.Home
cha @timesfmtz na kudai kwa sasa @darassacmg asiumize
tena kichwa kutoa wimbo mkali wa kuuzidi #muziki
.
.
"Darassa yupo vizuri darassa amepata hit song unajua hits song aliyopata darassa kwa wasanii inatokeaga mara moja sana mimi mziki nafananisha na kama zigo ushaelewa, zigo ni ngoma ambayo imehit sana kwa muda mfupi tu ikahit ikachukua mwaka mzima ay akaja akatoa remix ikahit mwaka mzima" alisema
@daxochali .
.
"so darassa level aliyofikia sasa hivi kashapata hit song ya namna kama ile au sio anachotakiwa sasa hivi asideal sana na muziki adeal na kukuza brand yake ajibrand sasa kwamba ifike stage kama Diamond sasa hivi hajali sana akiingia studio sijui natoa ngoma ya aina gani ni ile brand yake sasa ndio inauza so darassa kashafika level ya kutoa hits 3 mfululizo atafute brand sasa, yani brand yake ndio iuze sasa hivi anavyovaa anavyokaa watu wanavyomzunguka maisha yake" ameongeza
.
.
Daxo Chali ni ndugu na Producer mkongwe nchini ambaye
pia anafanya kazi katika studio za master J inayojulikana
kama MJ Records ambayo ilianza kufanya kazi za wasanii
miaka ya nyuma zaidi toka game ya muziki inaanza hapa
nchini....

KARIBU KUTOA MAONI YAKO HAPA⤵

Roma Awatolea Uvivu na Kuwapa za Uso Nay wa Mitego na Madee Kwa Ugomvi Wao Usio na Mbele wala Nyuma

$
0
0

Mwana Hip Hop mkali Roma amewafungukia Madee na Nay wa Mitego kwa Ugomvi wao wa Kugombania nani ni Rais wa Manzese..

Ameandika haya:

BY @roma2030 - Oyaaaaah!! Sililizeni Nyie
Mnatuchosha Bana na Vimaneno maneno vyenu kila saa kwenye Radio Zetu....Ili Mradi tu Mvikikishe #vinyimbo vyenu mlivyoachia!!!
Mbona #Sisi_Tumetulia_tu. Na tumeachia Dude.
😉😉😉😉😉😉😉😉 #SASA_NASEMAJEEEEE
Nyie Si Mnaigombania #MANZESE!!??? Sasa nataka Nyote wawili Madee na Nay
Mlitamke hilo neno MANZESE atakayelitamka vizuri kwa kulipatia ndio
MWENYE MANZESE YAKE.😂😂 Aaaaf Andaeni #Pambano mimi #Refa

Diamond Kanyakua Tena Tuzo Nigeria, Usiulize ni Tuzo Gani Wewe Bofya Hapa!

$
0
0
MKALI wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ameshinda tena tuzo za Too Exclusive zinazotolewa nchini Nigeria katika kipengele cha Msanii Bora wa Mwaka 2016 ambacho hutolewa kwa msanii asiyekuwa wa nchi hiyo (Nigeria) ambaye anafanya vizuri kwa bara zima la Afrika..

Katika tuzo hizo, wengine waliokuwa wakiwania vipengele mbalimbali ni  Wizkid, Tekno na Tiwa Savage, Kiss Daniel, Simi na wengine kibao.

Obama Awaaaga Wananchi wa Marekani kwa Barua Hii..!!!

$
0
0

Muda Mfupi Uliopita Aliyekuwa Rais wa Marekani Barack Obama aliwaandikia barua wananchi wote wa Marekani kwa kuwashukuru kwa kipindi chote alichokuwa Rais wao.

Obama katika barua hiyo ameweka wazi furaha yake kwa kumaliza miaka yake 8 ya kukaa madarakani .


Duh!! Matonya Afunguka Jinsi Walivyopanga Kumzika Gigy Money Akiwa Hai..!!!

$
0
0

Matonya
Matonya.
WAFUATILIAJI wa burudani hususan katika Muziki wa Bongo Fleva watakuwa wanazifahamu nyimbo kama Vaileth, Anita, Taxi Bubu na Dunia Mapito ambazo zilifanya poa katika chati na sehemu mbalimbali za starehe. Mkali wa ngoma hizo alikuwa ni Seif Shaban maarufu kama Matonya. 

Jamaa huyu ni mmoja wa wanamuziki wakongwe wanaoendelea kulisongesha katika gemu la muziki wa Bongo Fleva ambapo anapoibuka na ngoma mpya huwa gumzo. Kama utakumbuka miaka miwili iliyopita alikuwa akitesa na Ngoma ya Mule Mule aliyomshirikisha Rich Mavoko, akafunga mwaka jana na Sugua Benchi na sasa amefungua mwaka na ngoma mpya ya Hakijaeleweka ambapo ndani ya ‘kideo’ chake yumo muuza nyago Gigy Money.matonya
Gigy Money na Matonya
Juzikati Matonya alitimba ndani ya Ofisi za Global Publishers zilizopo Bamaga-Mwenge jijini Dar na kupokelewa na Global TV Online kisha kufanyiwa mahojiano katika Kipindi cha Exclusive na katika makala haya anafunguka zaidi;matonya-1
Matonya
 Showbiz: Hongera kwa kazi zako, lakini ujio wako safari hii upo kasi sana. Umefunga mwaka na Sugua Benchi na umefungua na Hakijaeleweka, kwa nini umetoa ngoma haraka hivi kwa kipindi kifupi?

 Matonya: Ujue maisha yanabadilika! Mashabiki wangu walikuwa wamemiss sana kumsikia Matonya kila mara akiwa na nyimbo tofauti. Hivyo mipango yangu ni kuwafurahisha kwa kutoa nyimbo nyingi na kwa haraka zaidi.gigy_money
Gigy Money
Showbiz: Kuna utofauti gani kati ya Matonya wa zamani na sasa?

 Matonya: Matonya wa zamani na sasa ni watu wawili tofauti. Mfano ukiangalia video ya wimbo wangu huu mpya wa Hakijaeleweka ni tofauti na za nyuma. Nimeonesha maisha ya watu wengi wasivyothamini mtu wa pembeni hadi anapoondoka (kufariki) ndo’ wanajua thamani yake. Nimeonekana nipo makaburini nasali kwa uchungu kitu ambacho sijawahi kukifanya katika video zangu za nyuma.

 Showbiz: Unaweza kutuambia ilikukosti kiasi gani maandalizi ya hii video?

 Matonya: Nashukuru haikutukosti kiasi kikubwa video hii japo siwezi kukitaja kwa sasa lakini kuna vitu vidogovidogo kiukweli vilitukosti kama vile kuna sehemu za makaburini ilibidi tukodi kisha tusubirie hadi vibali yaani process ilikuwa ndefu sana.
 matonya
Matonya
 Showbiz: Katika video yako kuna video queen Gigy Money ameonekana kubadilika kimavazi, sijui unaweza kutuambia ilikuwaje?

 Matonya: Kikubwa nilitaka kubadilisha mazingira ya Gigy kwa maana watu wengi wamezoea kumuona kwenye video na nje ya video akiwa katika mavazi ya nusu utupu. Nimejaribu kumbadilisha na kuonesha jamii kuwa ukiishi na wanawake kama hawa wanaweza kubadilika.

Najivunia sana kwani kwa upande wa video, Gigy ameweza kufunika kwa kiasi kikubwa kutokana na mavazi ya heshima aliyoyavaa mwanzo hadi mwisho yaani sasa hivi kwa walioiona video hii wakimuona Gigy alivyo wanaweza kuleta hata ng’ombe, mbuzi au hata wakajenga ghorofa kwa ajili ya kumchumbia.Gigy-money-(5)
Gigy Money
Showbiz: Ugumu gani mliupata wakati mnatengeneza video?

Matonya: Dah! Ujue wakati tunatengeneza kwanza, tulitaka Gigy adumbukizwe (azikwe) katika kaburi lililochimbwa kwa mujibu wa ‘skripti’. Kabla ya kufanyika video, Gigy alinipigia simu na kuniuliza nguo zipi sasa anaweza kuzikiwa nazo lakini tukawa tumebadilisha idea hiyo na kuonesha tayari ameshazikwa na kaburi limetengenezwa.

 Showbiz: Kwa sasa nani anasimamia kazi zako za muziki?

 Matonya: Namshukuru Mungu nina mameneja watatu, wa kwanza Kapasta 4 Real, James na Hilton ambaye yupo Nairobi kwa ajili ya kunisimamia nje ya mipaka.Gigy money (6)
Gigy Money na Mwanahabari.

Showbiz: Unazungumziaje janga la madawa ya kulevya lililowakumba wasanii wengi kwa sasa?

Matonya: Kiukweli hali inatisha na vijana wengi wanaangamia lakini wa kuwaokoa ni sisi wasanii pamoja na jamii. Ni lazima tushirikiane kwa pamoja kuweza kutatua janga hili. Kama tunaweza kushirikiana katika kuingia studio na kutoa nyimbo kali kisha kushirikiana na media basi hata hili la kuwaokoa vijana wenzetu tukishirikiana tunaweza kuliepuka.

Zitto: Angalieni Hali ya Wanafunzi, Jirani yao Chato Inajengwa Airport ya zaidi ya TSh Bilioni 50

$
0
0

Mwanasiasa Machachari Zitto Kabwe ameweka picha hiyo hapo juu kwenye ukurasa wake wa Facebook na kuandika yafuatayo:

Watoto wa Shule ya Msingi Mnyala katika kata ya Nkome Wilaya ya Geita.
Jirani yao Chato inajengwa Airport ya zaidi ya tshs 50bn

Mwana FA: Muziki wa Ma Group Ulishafeli, Hauwezi Kurudi Tena

$
0
0
Mwana Fa amadai kwa sasa muziki wa ma group hauwezi kulipa tena kutokana na hali ya uchumi wa muziki kwa sasa, ametolea mfano wa ma group ya muziki ya Marekani waliyokuwa wameyaiga kama D12 yalivyokufa na wasanii wake kubaki solo kwa kuwa ma group kiuchumi haulipi

Muda Wapita Tena Bila Jammeh Kuondoka Madarakani Gambia

$
0
0
Jammeh alikuwa ameomba apewe hadi saa 16:00 (saa moja jioni Afrika Mashariki) kufanya uamuzi kuhusu iwapo ataachia madaraka au la.

Makataa ya kwanza ya kumtaka aachie madaraka kufikia saa sita mchana yalikuwa yamepita.

Taarifa zinasema makamu wa rais wa zamani wa Gambia, Isatou Njie-Saidy, yupo ikulu ambapo anashiriki mazungumzo ya dakika za mwisho.

Marais wa Mauritania na Guinea wanajaribu kumshawishi Jammeh kuondoka.

Baada ya Majeshi Kuingia Gambia,Rais Yahya Jammeh Akubali Yaishe,Atangaza Kukimbia Nchi..!!!

$
0
0

Kiongozi wa zamani wa Gambia, Yahya Jammeh amekubali kuachia madaraka na amesema anaondoka nchini humo kwenda kuishi uhamishoni.

Taarifa za kuondoka kwa kiongozi huyo aliyetawala Gambia kwa miaka 22 zimetolewa na rais anayetambuliwa na jamii ya kimataifa Adama Barrow kupitia mtandao wake wa Twitter.

Barrow ametangaza hayo baada ya mazungumzo ya saa kadha yaliyonuiwa kumshawishi Jammeh kukubali matokeo ya uchaguzi.

Mataifa ya Afrika Magharibi yamewatuma wanajeshi Gambia na kutishia kumuondoa Jammeh madarakani kwa nguvu iwapo angekaidi amri ya kuachia madaraka kwa hiari.

Barrow amekuwa nchini Senegal kwa takriban wiki moja. Aliapishwa kuwa rais mpya wa Gambia katika ubalozi wa Gambia mjini Dakar Alhamisi iliyopita. Ametambuliwa na jamii ya kimataifa kama kiongozi mpya wa Gambia.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images