Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Zijue Sababu Sugu Zinazochangia Kuachwa Mara kwa Mara

$
0
0

Hivi ulishawahi kujiuliza ni kwa nini kila siku wewe umekuwa ni mtu wa kuachwa na kila mpenzi unayempata?

UBABE WAKO

Ubabe ni chanzo kikubwa cha mifarakano katika uhusiano wa kimapenzi. Utakuta mwanaume ni mbabe kupitiliza kwa mpenzi, mchumba au mkewe, mwanamke au mwanaume asifanye jambo dogo, ameshamtolea bonge la tusi, asifanye hivi kapewa teke! Hili ni tatizo. Kila siku utaishia kubadilisha wanaume au wanawake kwa sababu ya tabia zako za ubabe. Mapenzi hayahitaji ubabe bali lugha yenye mnato na mvuto kwa mwenza wako.

UZURI WAKO

Baadhi ya wapenzi ambao wanajifahamu kuwa wao wamebarikiwa, wamejaliwa kuwa na umbo au sura nzuri, basi kila kitu anachokifanya, anafanya kwa kujishebedua, akiamini kuwa mpenzi wake hana cha kumfanya kwa sababu ameumbika vizuri au kwa sababu yeye ni mtanashati. Tabia hiyo ya kujiona mzuri, humfanya kuleta uzuri ule hadi faragha, jambo ambalo halistahili. Wewe nani amekuambia uzuri wako ni muhimu kwenye sita kwa sita? Pale panahitaji kazi tu na si mbwembwe kama zako, ndiyo maana unaweza kumkuta msichana mrembo au kijana mtanashati lakini hadumu na mpenzi anayempata kwa sababu ya tabia yake ya umimi.

KUTOKUJIWEZA FARAGHA

Shindwa kazi yoyote, shindwa chochote katika dunia hii ila usishindwe kumpa huduma nzuri, yenye kumridhisha faragha mpenzi wako. Kama utakuwa unaweza kufanya mambo mengine vizuri lakini faragha unakuwa hujiwezi, hili ni tatizo kubwa sana, tatizo ambalo unatakiwa kulitafutia utatuzi mapema. Uvivu au kutokujituma unapokuwa faragha na mweza wako inaweza kuchangia kwa asilimia kubwa zaidi kuachwa na kila mpenzi unayekuwa naye. Mbaya zaidi uvivu wa faragha haubebwi na uzuri, elimu, umri, fedha, ustaa, wadhifa au umaarufu ulionao katika jamii.

URITHI WAKO

Mali za urithi nazo ni tatizo sana kwani utakuta mtu anatumia urithi wake kumnyanyasa mpenzi wake. Kwa mfano, mwanamke aliachiwa nyumba na wazazi wake na anakuwa na uhusiano na mpenzi wake, anaamua kuishi kwenye nyumba yake lakini utakuta anajisahau nakutaka kumpanda kichwani mpenzi wake. Anajikuta akisahau kuwa yeye ni mwanamke na mwenziye ni mwanaume pamoja na kwamba walikubaliana kuwa wataheshimiana na kupendana kwa dhati! Hilo jipu uchungu. Lazima jamaa atakukimbia kwani ataona kama unamnyanyasa kutokana na kipato, elimu, uwezo wako na kadhalika. Hivyo unapaswa kuwa makini sana na sababu hizo ambazo nimeziandika hapo na sababu hizi ni kwa wanawake na wanaume.

MAJIVUNO/KUJISIKIA

Hili pia ni tatizo kwenye uhusiano, haiwezekani wewe uwe ni mtu wa kujisikia au kujivuna kuwa wewe ni bora kuliko mweza wako, mtu unaishi naye, ‘unashea’ naye kila kitu lakini unamdharau, haipendezi na kwa tabia hiyo huwezi kudumu na mpenzi kwa muda mrefu kwani kila mtu atakuwa anakukimbia kwa sababu anajua hujui thamani ya kupenda. 

Article 1

$
0
0

Muigizaji wa filamu nchini Aunty Ezekiel amedai kuwa hamkubali Harmo Rappa kwa kuwa hana kipaji cha muziki.

Wakati akijibu maswali ya mashabiki Jumatano hii kupitia mtandao wa Facebook wa EATV katika kipindi cha Kikaangoni, Aunty alisema rapper huyo anatumia nguvu nyingi sana kujitangaza lakini hana kipaji muziki.

“Simkubali Harmo Rappa maana hana kipaji cha muziki anatumia nguvu nyingi sana,” amesema Aunty.

Hata hivyo Harmo amemchana Mose Iyobo ambaye ni mzazi mwenzake na Aunty katika wimbo wake mpya ‘Kiboko ya Mabishoo’ ambao amemshirikisha Juma Nature.

Ukweli Juu ya Freemason na Illuminant Kuhusika na Kifo cha Michael Jackson(Sehemu ya Pili)..!!!

$
0
0

Rais w CBS Records Walter Yetnikoff aliwatishia MTV na kuwaambia “Sitawaletea tena video na ninakwenda hadharani na **** kuwambia watu kwamba hamtaki kuonesha video za watu weusi"

Nafasi ya Walter iliwafanya MTV waanze kurusha vidio ya ‘Billie Jean’ na ‘Beat it’.

Bahati mbaya ni kuwa Thriller ilikuwa ni kama barabara ya kumfanya Michael kuwa kikaragosi cha Illuminati, kuanza kumtumia Michael na kipawa chake kuingiza maono ya kishetani kwa umma. Safari hiyo ilikuwa ni muhimu kufanyika kabla hawajamfanya Michael kuwa ‘White Man’ yaani kabla hawajampatia ugonjwa wa vitiligo ulio badilisha ngozi yake.

Dada yake na Michael, Latoya Jackson alikuwa na haya ya kusema kuhusu kifo cha kaka yake.

"I believe Michael was murdered," she said. "I felt that from the start. Not just one person was involved, rather it was a conspiracy of people. He was surrounded by a bad circle. Michael was a very meek, quiet, loving person. People took advantage of that. People fought to be close to him, people who weren’t always on his side."

"He had needle marks on his neck and on his arms and more about those will emerge in the next few weeks," she said. " I cannot discuss that any further as I may jeopardize the investigation. I can, however, say that I have not changed my mind about my feeling that Michael was murdered."

"I am going to get down to the bottom of this," she said. "I am not going to stop until I find out who is responsible. Why did they keep the family away? It’s not about money. I want justice for Michael. I won’t rest until I find out what and who killed my brother." 

Yaani kwa kiswahili.....

"Namini Michael aliuwawa, nilihisi hilo tokea mwanzo, sio mtu mmoja tu alihusika pasi na shaka ni kikundi cha watu, alizungukwa na kundi baya, Michael alikua mkimya na mpole na mwenye upendo,kwaio walitumia nafas hio vibaya kwake,,watu walipigana kua karibu nae,sio kila mara watu walikua upande wake. Alikua na majeraha ya sindano kwenye shingo na kwenye mikono,japo siwezi kuzungumzia hilo kwa kina nitaharibu upelelezi, lakini siwezi kamwe kubadili msimamo wangu na ninachoamini kwamba Michael walimuua. Sitapumzika hadi nihakikishe nani alihusika, kwanini wameitenga familia, sina shida ya pesa,nataka haki itendeke kwa Michael, sitapumzika.hadi nijue nani alimuua kaka.yangu".

Michael Jackson alifahamu kuwa Illuminati wanataka kumuua. Mwili wake ulipatikana na majeraha kadha ikiwemo shingoni na magotini, pia inaonesha kuwa alidondoka sakafuni kabla ya kifo chake, yaani alikuwa akipambana dhidi ya muuaji kuokoa uhai wake.

Latoya alipoulizwa ni nani aliyemuuwa Michael alijibu ....

“Doctor unaye muona, anaye tajwa kama msababishi wa kifo, ni kinga, yupo nyuma yake watu waliotaka Michael Jackson afe.”

Wakati wa shitaka la mara ya pili la Michael lililomalizika Juni 13 2005, wazazi wa Michael walimuita rafiki yake na Michael Dick Gregory, ambaye alikuwa ni rafiki mzuri wa Michael, walimuomba amtembelee Michael maana hayupo vizuri hata kidogo.

Baada ya siku chache Gregory alirudi na Michael kwenye jumba lake la Neverland. Michael alimkumbatia na kumuambia tafadhali usiniache wanataka kuniuwa.

Gregory akamuuliza Michael lini ilikuwa mara yake ya mwisho kula maana anaonekana kudhoofu, Michael akamjibu, “ wanataka kuniuwa kwa sumu”, akamuuliza ni lini mara ya mwisho amekunywa maji, Michael akamjibu, “Wanataka kuniua”

Gregory akamchukua Michael na kwenda naye kwenye hospitali ya karibu lakini mbali na Neverland bila kumuarifu mtu yeyote kwamba anakuja hapo na Michael Jackson, na akatundikiwa dripi kutoka 11:30 jioni mpaka 11:30 asubuhi na siku iliyofuata kwa masaa 24 akawa kwenye drip bila kupumzika, Dr. Aliyekuwa akimuhudumia akasema lau asingefika kwa wakati basi masaa mengine 12 angelikufa.

Utaona hapo kuwa Juni 2005, illuminati walikuwa wakifanya jaribio la kumuuwa Michael tena, lakini lilishindikana, lakini Juni 2009 walifanikiwa kutekeleza azma yao baada ya kumtumia mtu ambaye Michael alimuamini zaidi, Daktari wake, Conrad Murray. 

Michael alikuwa na nguvu za kutosha, dokumentari kadhaa zimetolewa zikimuonesha wiki kabla ya kifo chake, alionekana yuko safi, na akifanya maandalizi ya ‘tour’ yake ya London aliyoipatia jina la ‘THIS IS IT’, Tetesi ni kuwa kwenye Tour hiyo Michael kati ya mengi aliyo kuwa nayo ilikuwa ni kuufumbua macho ulimwengu kuhusiana na madhila na ubaya wa Illuminati, lakini jamaa nao walishaiona hatari hiyo na hawakuwa na muda wa kupoteza, ndipo daktari ambaye pia ni Freemason alipochukua jukumu hilo zito la kumuangusha King of Pop.

MWISHO....!!!

JPM: Serikali Haitatoa Chakula Bure kwa Wenye Njaa..!!!

$
0
0

Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameendelea kusisitiza kuwa kuwa Serikali haitatoa chakula cha msaada kwa watakaopatwa na njaa ilihali wanaweza kuzalisha chakula katika maeneo yao.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo jana katika ziara yake mkoani Pwani, wakati akizungumza na wananchi wa Somanga, Nangurukuru na Mchinga Moja, ikiwa ni ziara yake katika mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara.

Amepokea kero za wananchi katika maeneo hayo na kufanya kazi kwa bidii ikiwemo kuzalisha mazao ya chakula cha kutosha

"Najua mmezoea kusikia maneno mazuri mazuri kuwa hakuna atakayekufa kwa njaa, sasa mimi nasema usipofanya kazi, usipolima mazao na kupata chakula wakati mvua inanyesha Serikali haitatoa chakula cha bure kwa wenye njaa, ni lazima tufanye kazi, sasa hivi mvua zinanyesha limeni mazao ya chakula" amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Pia Rais Magufuli amezungumza na wananchi wa Ikwiriri na kupokea kero zao ambapo amewaagiza Mamlaka ya Maji katika Mji huo kuhakikisha mradi wa maji uliojengwa na kukamilika tangu mwaka 2015 kwa gharama ya Shilingi Bilioni 5, unaanza kutoka maji kabla ya mwisho wa Mwezi huu na pia amepiga marufuku utozaji wa ushuru kwa wafanyabiashara wadogowadogo wa mazao.

Aidha, Mhe. Dkt. Magufuli amewaagiza viongozi wa Mkoa wa Lindi kushughulikia migogoro ya wakulima na wafugaji iliyoanza kuibuka mkoani humo na ameahidi kutoa Shilingi Milioni 20 kusaidia ujenzi wa Zahanati ya Somanga.

Aliyegombea Ubunge Chadema Aokotwa Ameuawa Kinyama...!!!

$
0
0

Kada wa Chadema katika Jimbo la Hai mkoani Kilimanjaro, Anitha Swai ameuawa katika tukio lililogubikwa na wingu zito.

Taarifa za awali zilizopatikana usiku huu zimedai kuwa Anitha ambaye aligombea ubunge wa viti maalum mwaka 2015, alitekwa nyara wilayani Rombo na kuuawa maeneo ya TPC nje kidogo ya mji wa Moshi.

Vyanzo mbalimbali vya habari vimedokeza kuwa mara ya mwisho mwanasiasa huyo alionekana akiwa na watu wawili wilayani Rombo siku ya Jumatatu, Februari 27 na kuaga wanaelekea Arusha.

Hata hivyo, tangu siku hiyo Anitha hakuonekana hadi maiti yake ilipogunduliwa leo (Alhamisi) jioni maeneo ya TPC huku gari lake likiwa limetelekezwa maeneo ya Bomambuzi mjini Moshi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa amethibitisha kuokotwa kwa mwili huo, lakini amekataa kuthibitisha kama ni wa kada huyo wa Chadema.

"Ni kweli kuna tukio hilo, lakini ninachoweza kusema bado hajatambuliwa na mwili wake umepelekwa KCMC ili ndugu waweze kuutambua," amesema.

Hata hivyo, Diwani wa Viti Maalumu wa Kata ya Mawenzi mjini Moshi, Hawa Mushi amethibitisha kuwa aliyeuawa ni kada wa chama chao, lakini chanzo na nani waliohusika hakijajulikana.

Hawa amesema taarifa zilizothibitishwa ni kuwa mwili wake ulipatikana maeneo ya TPC huku simu iliyopatikana katika gari yake ndiyo iliyosaidia kumtambua.

Makatibu Wakuu Sasa Kuiona Dar kwa ‘Kubip’..!!!

$
0
0

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi amewaagiza makatibu wakuu wote wa wizara kuhakikisha wanakuwapo Dodoma wakati wote na wakienda Dar es Salaam iwe ni kwa shughuli maalumu.

Balozi Kijazi aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na makatibu wakuu hao kwenye kikao cha kikazi.

Alisema japokuwa bado kuna watumishi wamebakia Dar es Salaam, lakini wao wanatakiwa kujipanga kuhakikisha shughuli zote zinafanyika kwa ufanisi katika miji yote miwili.  Alisema wizara zote hadi jana zilikuwa zimeshahamia mkoani Dodoma.

“Niwatake makatibu wakuu muwepo Dodoma muda wote na si kuchungulia tu, tuwepo hapa. Mtakuja Dar es Salaam kama kuna majukumu muhimu tu,” alisema Balozi Kijazi.

Alisema amemuagiza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu kuandaa taarifa ambayo ataiwasilisha katika Baraza la Mawaziri ili litoe uamuzi ni wapi mji huo wa kiserikali utajengwa.

Alisema hivi sasa watakuwa katika majengo ya muda, wakati suala la kuwa na mji wa Serikali (government city) likiendelea kuzungumzwa.

Balozi Kijazi alisema kila wizara itaendelea kutumia majengo waliyopangiwa, wakati wakijipanga kujenga yao katika mji wa kiserikali.

Mti Wenye Miaka 600 Wapatikana Nchini...!!!

$
0
0

Mtafiti wa viumbe hai na mazingira kutoka Chuo Kikuu cha Bayreuth cha nchini Ujerumani, Dk Andrew Hemp ameelezea sifa za mti ujulikanao kama Mkukusu kuwa unaweza kuishi kati ya miaka 200 hadi 300, lakini ulioonekana nchini una miaka 600.

Akiuzungumzia mti huo ambao unapatikana katika Kijiji cha Tema wilayani Moshi, mtafiti huyo amesema mti huo ambao ni mrefu kuliko yote barani Afrika una urefu wa mita 81.5 na uko katika eneo lililopo kwenye Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (Kinapa).

Dk Andrew amesema kwa mujibu wa utafiti mti huo una uwezo wa kuishi miaka hiyo kwa kutunzwa na kuhifadhiwa.

Amesema kwamba katika utafiti walioufanya barani Afrika waligundua miti mirefu 31, lakini Mkukusu wa Moshi ndiyo mrefu kuliko yote na una umri wa miaka 600 hivi sasa ukiwa umevuka kiwango cha juu cha maisha ya miti ya aina hiyo.

Tayari Serikali imeiagiza Kinapa kuboresha miundombinu ya barabara ili kuweza kuufikia mti huo iwapo watalii watataka kwenda kuuona.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadiki amesema mti huo utasaidia kuongeza mapato kwa kasi kwa kuwa ni kivutio kipya cha utalii ndani ya mkoa huu.

Mtoto wa Marehemu Komba Aibuka na Haya Kuhusu Baba Yake,Aaamua Kutunga na Wimbo Kabisa...!!!

$
0
0

Ikiwa sasa ni takriban miaka miwili tangu aliyekuwa Mkurugenzi wa Tanzania One Theatre (TOT), Kampteni John Komba, kufariki Dunia, Mtoto wake Gerald John Komba, ameibuka na kutoa wimbo wa kuiunga mkono Serikali katika mapambano yake mapya dhidi ya dawa za kulenya nchini Tanzania.

Gerald aliyezaliwa mwaka 1986 jijini Dar es salaam, amesema, ameamua kutoa wimbo huo wenye maudhi ya kwaya, ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya kifo cha Baba yake, Marehemu John Komba aliyefariki  Dunia, Februari 28, 2015 katika Hospitali ya TMJ, Mikocheni jijini Dar e Salaam, alikopelekwa baada ya kuzidiwa ghafla akiwa nyumbani kwake, Tangibovu kwa Komba.

Mtoto huyo wa Jihn Komba aliyekuwa mwanamuziki nguri wa utunzi na uimbaji wa nyimbo za kwaya, amesema, wimbo aliotoa nimarejeo ya wimbo ambao ulitungwa na nguri huyo, kukemea usambazaji na matumizi ya dawa za kulevya miaka zaidi ya kumi iliyopita, lakini baada ya kuurekodi haukuwahi kuimbwa na TOT wala kuchezwa kwenye vituo vya Radio au Televisheni.

Gerald ambaye amesomea Sheria katika Chuo Kikuu cha Saint Augustine kilichopo Mwanza,  Tanzania,  baada ya masomo ya shule ya Msingi katika shule ya Kawe “A” na shule yasekondari Mbezi Beach High school, anasema katika kuutoa wimbo huo, hakubabaisha kwa kuwa na yeye anacho kipaji cha kuimba japo amekuwa hakitumii sana. Zamani Shule ya Kawe A’ ilifahamika kwa jina la Tanganyika Packers, lakini baada ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi kubaini kuwa kiwanda cha kusindika nyama cha Tanganyika Packers kimeshakufa, akaamua shule hiyo kubadilishwa jina.

“Nimeanza kupenda sanaa ya muziki tangu nilipokuwa mtoto, kwa kuwa nilikuwa naenda na Baba (John Komba) kwenye maonesho yake na kundi la TOT,  na nilikuwa navutiwa sana na namna baba yangu alivyokuwa akitamba jukwaani wakati akiimba”, alisema Gerald.

“Tangu wakati huo, nilikuwa napenda kukariri nyimbo zote za Baba, na hakuna wimbo nisioujua kuanzia ala hadi mpangilio wa mashairi, lakini pia pia shuleni nilikuwa naimba kwenye kwaya ya shule, na siku za karibuni nimekuwa pia nikiimba kwaya kwenye Kanisa la Praise team, hapa jijini Dar es Salaam”, aliongeza.

Anasema, ameambua  kuurudia wimbo wa Marehemu Baba yake kwa sababu, kwanza yeye binafsi anachukia mamia ya vijana wanavyoharibika kwa matumizi ya dawa za kulevya kwa namna ambavyo wanatumiaji wengi wa dawa hizo hukatishwa ndoto zao mbalimbali za kuwa watu muhimu katika ujenzi wa taifa la Tanzania.

“Kwanza ukizingatia hakuna aliyezaliwa teja, wengi  wanaokuwa hivyo wanakutana na hili balaa wanapoingia kwenye jamii kwa hiyo nikaona nifanye kitu ili jamii iweze kutoa mchangu wangu katika kuelimisha jamisha jamii ili izinduke na kuelewa namna dawa hizi za kulevya zilivyo za hatari.

Pili niliamua kuurudia wimbo huu kwa sababu, watu wengine hasa Walimu na Wazazi wengi wao wanajisahau katika kusimamia malezi ya vijana. Wazazi wanamwachia Mwalimu jukumu la kutazama mwanafunzi akiwa shule bila kujua mtoto anaharibika katikati ya shule na nyumbani wakati wa kwenda na kurudi nyumbani, kwa hiyo Mwalimu na mzazi  ni Watu muhimu wa kuchunga mwanafunzi”, alisema Gerald.

Anasema, sababu yake ya tatu ya kuamua kuurudia na kuongeza vionjo kwenye wimbo huo ni kusisitiza kuwa mapambano hayo ni ya Watanzania wote ambapo anasema ameweka baadhi ya majina ya wakuu wa mikoa kwenye wimbo huo kwa kuwa vita hii ya mapambano dhi ya dawa za kulevya ni ya Watanzania wote na hao ndiyo wawakilishi wa Rais kwenye kila mkoa.

“Nimeongeza vionjo kwa kutaja hawa wakuu wa mikoa kwa kuwa najua hawa ndiyo waakilishi wa Rais, na Rais Dk. John Magufuli hawezi kukabiliana nayo peke yake hivyo unahitajika ushirikiano na wananchi kuanzia ngazi ya Kaya, Vijiji, Kata, wilaya hadi mkoa.

Na mwisho niliamua kuurudia kama Kumbukumbu ya miaka miwili ya kifo cha Marehemu Baba, ukiuusikiliza wimbo huu utangua kuwa sauti yangu na yake zimefanana kwa karibu sana katika uimbaji, hivyo itaweza kuashiria kuwa yale alyolenga kuyakemea kwenye nyimbo zake, hata baada ya kufariki dunia lakini bado kuna mtu mwingine ambaye ni mtoto wake atakayeendelea nyimbo hizo kufanya lengo lake la kuionya jamii ibaki pale pale”, alisema Gerald

“Mtindo nilioutumia kwenye wimbo huu ni uleule wa kwaya aliotumia Baba, na nimeuimba upya kwa kushirikiana na Mama yangu Mzazi, Jane Mkondwa ambaye ni mwimbaji wa miaka mingi katika Kundi la TOT, Nimeurekodi katika Studio za PM Records chini ya Mtayarishaji anayefahamika kwa jina la Testimony.

“Baadhi ya maneno yaliyomo kwenye wimbo huu ni maneno ambayo ambayo hutumiwa zaidi na mateja na nimefanya hivyo kwa kuwa ni miongoni mwa walegwa katika vita hii. Hivyo, nikaona nitumie maneno wanayoweza kuyaelewa haraka kama;  ‘nywele misumari’, ‘twende kilioni’, ‘Macho kufutuka’, ‘akili inayeya’ ambapo neno kama akili inayeya kwa teja humaanisha anavyokuwa baada ya kulewa dawa za kulevya yaani ufahamu katika akili zake unapotea.

“Maneno mengine ni Gheto na Washkaji (nyumba wanapoishi vijana wa kiume au wa kike, lakini neno mshkaji au washkaji unategemea na umri, wale wa miaka ya 1960 walimaanisha wanawake wao lakini wa sasa wanamaanisha marafiki wao ingawa maana zote mbili zina maana sawa”, anafafanua Gerald.

Anasema, kwa sasa wimbo huo bado upo katika sauti tu (Audi), kwa kuwa hajapata uwezo wa kuurekodi katika video, ingawa yupo katika jitihada za kutafuta uwezo ili kuhakikisha anaurekodi katika video ili ujumbe uweze kufika kwa urahisikwa walengwa wote.

Gerald anatoa mwito kwa Watanzania kuungana ili tulitokomeza usambazaji na matumizi ya dawa za kulevya bila kujali itikadi za vyama, kabila, jinsia kwa kuwa ni janga linaloweza kuingia katika familia, Taasisi, Chama cha siasa, kabila au jinsia yoyote.

“Watanzania wenzangu naomba kila atakayepata fursa ausikilize kwa makini wimbo wangu huu,  ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono Rais Dk. John Magufuli katika mapambano haya mapaya dhidi ya usambazaji na matumizi ya dawa za kulevya katika nchi yetu ya Tanzania”, anasema Geral

Elimu ya Makonda Kaa la Moto,Mawaziri Waogopa Kuzungumzia..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 3/3/2017..!!!

Kigogo ALAT Atumbuliwa Hadharani kwa 'Kupiga' Mil 90...!!!

$
0
0

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa nchini ALAT Bwana Gulam Mukadam amemsimamisha kazi Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo Bw Abraham Shemoboyo kupisha uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu wa shilingi milioni 150 za ufadhili wa jumuiya hiyo mwaka 2015.

Akiongea  katika ofisi za jumuiya hiyo Jijini Dar es salaam, Gulam ambaye pia ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga amesema, benki ya NMB ilitoa kiasi hicho cha pesa kwa jumuiya hiyo kwaajili ya ufadhili wa Tuzo ya Meya (Mayor Awards) na kwamba Katibu huyo huyo hakuwasilisha kiasi chote na badala yake aliwasilisha shilingi milioni 60 huku kiasi cha shilingi milioni 90 kikiwa hakijulikani kilipo.

Mukadam amesema, uamuzi wa kumsimamisha uliamuliwa na kamati tendaji ya ALAT Taifa na mkutano mkuu wa ALAT taifa, ambapo iliundwa tume ndogo kuchunguza upotevu wa kiasi hicho cha pesa na kuamuliwa kuwa apishe uchunguzi dhidi yake kwa upotevu wa pesa hizo.

Aidha Mstahiki Mukadam amesema, uchunguzi dhidi yake utafanywa na CAG na kwamba pesa hizo hazikuwekwa kwenye akaunt ya ALAT na badala yake zilihifadhiwa kwenye akaunti binafsi ijulikanayo kama 'Vision Investment'.

Sirro - Nasumbuliwa Sana na Wanawake Usiku,Wananipigia Simu na Kunitongoza ...!!!!

$
0
0

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna Simon Sirro, amesema miongoni mwa changamoto anazokutana nazo ni pamoja kupigiwa simu za vishawishi na wanawake hasa usiku wa manane, wakidhani anapata pesa nyingi kwenye kazi yake.

Kamishna Sirro afichua siri hiyo hivi karibuni akiwa kwenye kipindi cha East Africa Breakfast, ambapo amesema pamoja na changamoto hizo, anajitahidi kukabiliana nazo kwa kuwa tayari amekwishawazoea.
Amesema kuna wanawake wengine wakiona amependeza kwenye tukio fulani, wanajua lazima atakuwa na pesa za kuwasaidia katika maisha yao hivyo wakati mwingine humpigia usiku, na yeye akidhani kuwa ni taarifa za uhalifu, lakini hukutana na vishawishi vikiambatana na sifa kedekede.

"Mwigine anaweza kukupigia simu tu usiku, kama unavyojua hawa wadada wa mjini, wakiniona wanajua niko vizuri, mwingine anakupigia anakuambia mzee tulikuona umevaa kofia vizuri, mjini kuna namna nyingi ya kuishi". Amesema Kamanda Sirro

Sirro ametaja changamoto nyingine ambazo hukutana nazo kuwa ni pamoja na suala la askari wake kulalamikiwa jambo linaloonesha dhahiri kama kiongozi ameshindwa kuwasimamia vijana anaowaongoza  na mara nyingi huwa anachukua hatua.

Lingine ni uhalifu kuzidi katika eneo fulani na hufanya wananchi kuwa na uoga, na kupoteza imani kwa jeshi la polisi jambo ambalo linamfanya yeye ajisikie vibaya zaidi kuliko hata wananchi, huku nyingine ikiwa ni viongozi wa mitaa kutowajibika katika kudhibiti uhalifu pamoja na kuletewa taarifa za uongo.

Ali Kiba Apika Bomu la Kumlipua Diamond...!!!

$
0
0

Msanii Alikiba ameingia katika orodha ya miongoni mwa wasanii wanaotarajia kufanya mapinduzi ya muziki kwa mashabiki zao kwa kutoa albam.

Baada ya kutua katika Jiji la Dar es Salaam akitokea nchini Afrika Kusini siku ya jana, 'King' Kiba aliwashukuru mashabiki zake kwa upendo walioonesha kwake kwa kumsubiria muda mrefu bila ya kukata tamaa na kusema endapo mambo yakienda vizuri na yaye anatarajia kuachia albam ambayo atafanya na wasanii wa kimataifa bila ya kuwasahau hapa bongo.

“Chochote kinaweza kutokea ila kwa sasa hivi niko 'busy' namalizia albam yangu mpya itakuwa na vichwa 'international' na 'local' itakuwa 'full' nadhani itatoka mwaka huu kama mambo yakiwa fresh Inshaallah Mungu asaidie”. Alisema Kiba

Vilevile msanii huyo amesema amefurahi na ameipenda sana zawadi aliyopatiwa na rapa chipukizi Harmorapa wakati amekwenda kumpokea katika uwanja wa ndege wa Dar es Salaam. 

Seven Mosha: Kuna wakati mashabiki wa Alikiba wanatunyima usingizi

$
0
0

Meneja wa Alikiba, Seven Mosha amekiri kuwa pressure wanayoipata kutoka kwa mashabiki wa staa huyo ni kubwa na wakati mwingine huwakosesha usingizi.

Seven ameiambia Bongo5 kuwa pindi kazi za Ali zinapochelewa kidogo kutoka, hukuiona cha mtema kuni kutokana na shinikizo toka kwa mashabiki wake.

“Ukiwa na kipaji kama hicho, na potential hivyo, sio rahisi watu waelewe vitu kibiashara,” amesema. “Na saa zingine vile vile unaweza kuvuka kibiashara ukaspeed up issue zaidi. Kwahiyo Alikiba amekuwa msanii ambaye amekuwa highlighted na upande wa Sony kwamba speed up the situation,” ameongeza.

Seven anasema pressure kubwa huipata pindi mashabiki wa Alikiba wakikasirika. “When they are not happy, we all are not happy,” anasema.

Nilipomuuliza kama mashabiki wanawanyima usingizi, Seven amesema, ” Oh Yeah, kabisa, na politics ukichanganya huko ndani basi vurugu.”

Meneja huyo amekiri kuwa wakati mwingine licha ya kupost vitu Instagram huacha kusoma comments sababu zinaweza kumtoa kwenye reli.

Maoni ya Zitto Kabwe Kuhusu Uteuzi wa Mama Salma Kikwete na Kuhusu Baa la Njaa

$
0
0
Serikali Ina Kauli Mbili Zinazokingana Juu ya Hali ya Chakula Nchini

Siku nzima ya jaa nilikuwa natakiwa na waandishi wa Habari kutoa maoni yangu kuhusu uteuzi wa Mtanzania mwenzetu, na mke wa Rais aliyepita, Mama Salma Kikwete kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.
Niliwaambia sina maoni yeyote. Leo baada ya magazeti kuandika maoni ya watu mbali mbali nimeulizwa tena. Jibu langu, ambalo ninaliweka hapa kwa umma, ni kwamba Mama Salma Kikwete ana haki zote kama Mtanzania mwengine yeyote kuteuliwa ama kuchaguliwa Kwa mujibu wa Katiba yetu. Hivyo uteuzi wake kwa maoni yangu ni kama teuzi nyengine zozote zile.
Kuolewa kwake na aliyekuwa Rais hakumwondolei yeye haki zake za kikatiba. Kama mwenyewe ataridhia ninamtakia kila la kheri katika kazi yake mpya. Sababu za kuteuliwa kwake anajizuia aliyemteua na baadhi ya wasomi wabobezi Kama Prof. Kitila Mkumbo wamenukuliwa wakifanya uchambuzi mzuri Kabisa kwenye gazeti la The Citizen la Leo.
Kwangu Mimi, kwa maoni yangu, nchi yetu inakabiliwa na mambo makubwa zaidi ya kujadili na kutolea maoni ikiwemo suala la njaa. Serikali kwenye suala hili la njaa imeyumba sana na kwa kiasi flani imewayumbisha pia wananchi wanyonge wanaokabiliwa na tatizo hili, na kwa maoni yangu naamini kabisa Serikali haijatekeleza wajibu inavyostahili. Kama mzalendo kwa taifa langu nachukua wajibu wangu kuonyesha mapungufu hayo ya Serikali pamoja na kutoa njia mbadala.

Jana, Serikali kupitia Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kusisitiza kuwa haitatoa chakula cha msaada kwa Watanzania watakaokabiliwa na njaa. Rais alisema "tumezoea kuambiwa maneno matamu matamu kwamba hakuna mtu atakeyekufa kwa njaa. Mimi nawaambia usipolima utakufa na njaa". Serikali kwa kauli za namna hii inawachanganya watanzania, kwanza ni muhimu sana kujua (na naamini Serikali inajua) kuwa wananchi hawa wamelima, suala la hali ya njaa si kwa sababu ya kutokulima kwao, bali ni kwa sababu kadhaa zilizo nje ya uwezo wao, ikiwemo hali ya hewa yenye mvua chache.
Mfano mikoa ya Singida, Shinyanga

Beki wa Yanga Amchana Haji Manara wa Simba,Amfananisha na Ibilisi....!!!

$
0
0

BEKI wa pembeni wa Yanga, Juma Abdul amesema hataki kubishana na Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliani wa Simba, Haji Manara na badala yake yeye atamuonyeshea kwa vitendo ndani ya uwanja.

Kessy aliitoa kauli hiyo mara baada ya mechi ya Ligi Kuu Bara iliyochezwa juzi Jumatano na Yanga kufanikiwa kuibuka kwa ushindi wa mabao 2-0 huku beki huyo akianza kwenye kikosi cha kwanza cha Mzambia, George Lwandamina.

Beki huyo, tangu atue kuichezea Yanga hakuwa na nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo na mara kadhaa amekuwa akitokea benchi katika timu hiyo. Akizungumza na Championi Ijumaa, Kessy alisema aliiona na kuisoma ‘post’ ya Manara kwenye ukurasa wake wa Instagram ambayo ilikuwa ikimdhihaki kutokana na kukaa benchi.

Kessy alisema baada ya kuisoma hakutaka kumjibu na badala yake alikaa kimya kuhofia majibizano yasiyokuwa na maana na badala yake akili zake alizielekeza kwenye kucheza soka pekee. “Hivi vitu vinavyotokea hivi sasa kutoka kwa viongozi wa Simba akiwemo huyo Manara nilivitarajia tangu natoka Simba ninakuja kuichezea Yanga.

“Nakumbuka mwanzoni wakati nasaini kuichezea Yanga nilikuwa najibizana nao kwenye vyombo vya habari, lakini baada ya kugundua kuwa ninatoka mchezoni ninapojibizana nao, nikaamua kukaa kimya.

“Hivyo, sitaki kumkaribisha ibilisi hivi sasa na badala yake nitakaa kimya nikifanya kazi yangu ndani ya uwanja kwa kuwajibu kuonyesha kiwango kikubwa kwa lengo la kuipa ubingwa timu yangu ya Yanga,” alisema Kessy.

Noma Sana..Ridhiwani Atema Cheche kwa Wanaopinga Mama Yake Kuteuliwa Kuwa Mbunge...!!!

$
0
0

SIKU moja baada ya Rais John Magufuli kumteua Salma Kikwete ambaye ni mke wa Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete kuwa mbunge, mtoto wake Ridhiwani Kikwete, amepongeza na pia kujibu mapigo ya wale wanaohoji uteuzi huo.


Juzi, taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu ilitoa taarifa juu ya uamuzi wa Rais Magufuli kumteua Mama Salma kuwa mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa ni sehemu ya nafasi 10 za Rais. Mama Salma ni mbunge wa tisa kuteuliwa ubunge na Rais.

Taarifa ya uteuzi huo iliibua mijadala mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii, baadhi wakiunga mkono na wengine wakihoji usahihi wake, huku hoja kuu ikiwa ni upekee wa uteuzi huo ambao ni wa kwanza kumhusisha mke wa Rais mstaafu.

Katika maelezo yake kwa Nipashe jana, Ridhiwani ambaye pia ni Mbunge wa Chalinze (CCM), alisifu uteuzi huo na kueleza kuwa kadri anavyofahamu, kuteuliwa kwa mama yake kumetokana na jitihada anazozionyesha kila uchao katika kutetea haki za wanawake na usawa wa kijinsia.

Ridhiwani alisema mama yake (Salma) amekuwa akiwawezesha wasichana wengi kupata elimu na pia kusaidia maendeleo ya jamii kwa nguvu kubwa.

Alisema wale wanaohoji uteuzi huo ni haki yao, lakini ukweli unabaki kuwa ni uteuzi sahihi.

“Waliohoji wana haki yao kimtazamo. Lakini la msingi ni kuelewa kuwa Rais amemchagua kutokana na mahitaji ambayo yeye anadhani kuwa Mama Salma anakwenda kusaidia nchi,” alisema Ridhiwani kupitia ufafanuzi wake huo kwa Nipashe na kuongeza:

“Kwangu mimi, nikitaja kazi alizowahi kuzifanya na mafanikio aliyoyapata katika kuhudumia nchi na Watanzania, ninaamini ndiyo sababu za msingi zilizomsukuma Rais kufanya maamuzi (hayo) muhimu na mazuri kipindi hiki.”

Ridhiwani alisisitiza kuwa yeye ni miongoni mwa Watanzania waliofurahishwa na uteuzi huo na kuupokea kwa mikono miwili.

“Nimefurahi kwa uteuzi wake na nimeupokea vizuri. Amekuwa mtetezi wa hazi za wanawake na usawa wa kijinsia … amewawezesha wanawake wengi kupata elimu,” alisema Ridhiwani.

Akieleza zaidi mama yake, Ridhiwani alisema kuteuliwa kwake kutakuwa kumempatia nafasi nzuri ya kupambana ili kurekebisha au kubadilisha changamoto kuwa fursa.

"Wewe ni mwanamke wa Shoka. Hongera sana kwa uteuzi. Imani sasa umepata sehemu ya kuwezesha mapambano kuwa sheria. Mungu akutangulie Mama yangu, Mheshimiwa Mbunge," alisema Ridhiwani kupitia ufafanuzi wake huo.

Mbali ya kuteuliwa kuwa mbunge, Mama Salma pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) ambayo hushughulikia zaidi masuala ya wanawake na usawa wa kijinsia.

Hatma ya Lema Kutoka Gerezani kwa Njia ya Dhamana Kujulikana Leo...!!!!

$
0
0

MAHAKAMA Kuu leo inataraji kutoa uamuzi wa maombi ya dhamana ya Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema (Chadema), baada ya pingamizi la Jamhuri kuondolewa Mahakama ya Rufani Jumatatu.

Wakati Mahakama ya Rufani ikiridhia kurudishwa kwa shauri hilo Mahakama Kuu, mwenyekiti wa kopo la majaji watatu, Jaji Benard Luanda alisema walishangazwa na Mbunge huyo kushikiliwa kwa miezi minne bila sababu za msingi.

Lema anashikiliwa tangu Novemba 2, mwaka jana.

Jaji Luanda pia alihoji kama ofisi ya DPP ina wanasheria. Mbali na Luanda, jopo hilo linakamilishwa na Jaji Stella Mugasha na Jaji Kipenka Mussa.

Wakili wa Serikali, Faraja Nchimbi ndiye aliomba mahakama kuiondoa rufani hiyo kwa vile hawakuwa wamepeleka kusudio la kukata rufani kwa Msajili wa Mahakama ya Rufani, kosa ambalo waliligundua Ijumaa iliyopita baada ya saa za kazi za mahakama.

Rufani iliyoondolewa iliombwa na Njau, aliyepinga Jaji Dk. Modesta Opiyo wa Mahakama Kuu kumwongezea Lema muda wa siku 10 ili akate rufani ya kunyimwa dhamana nje ya muda.

Jaji Luanda aliwaagiza mawakili wa Lema kurudi Mahakama Kuu kuendelea na masuala ya dhamana.

DHAMIRA MBAYA
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliwaambia waandishi wa habari nje ya Mahakama ya Rufani Jumatatu kuwa Jamhuri ilikuwa ikifanya ucheleweshaji kwa dhamira mbaya dhidi ya Lema.

Alisema chama hicho kimesikitishwa kwani Lema yuko gerezani bila sababu za msingi, kitendo kilichowafanya waichukie mahakama kuona inapewa maelekezo na serikali, lakini kumbe ni "mchezo wa ofisi ya DPP."

“Leo Mahakama imetufariji sana na kuturudishia imani yetu kwao kuwa ni chombo kilichosimama kwa miguu yake kama mhimili wake na haipokei maagizo ya serikali."

Lema alianza kukaa mahabusu Novemba 2, mwaka jana, baada ya kukamatwa katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma na kusafirishwa kuletwa Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Arusha.

Novemba 8 alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, mbele ya Hakimu Desderi Kamugisha ambapo alisomewa shitaka la uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli.

Hakimu Kamugisha alikubali kutoa dhamana kwa Lema kwa madai kuwa sheria haizuii kutoa haki hiyo kwa mshtakiwa wa kesi ya uchochezi, lakini kabla ya kutamka masharti ya dhamana, Mawakili wa Serikali, Paul Kadushi na Materius Marandu walidai wana nia kukata rufani dhidi ya msimamo huo.

Kutokana na mawakili hao kusema hivyo, Hakimu aliamua kesi hiyo ibaki kama ilivyo, huku mtuhumiwa akisubiri maamuzi ya rufani ya Jamhuri katika Mahakama Kuu.

Jaji Dk. Opiyo alipotupa rufani ya Jamhuri na kumpa Lema siku 10 zaidi ili akate rufani ya kupinga kupewa dhamana bila masharti ya dhamana kwa kuwa hoja hizo hazikuwa na mashiko, mawakili wa serikali wakakata rufani Mahakama ya Rufani.

Tangu wakati huo Lema ameendelea kukaa mahabusu katika Gereza la Kisongo.

Sanchoka Akubali Kumpa Penzi Idris kwa Masharti Haya...!!!

$
0
0

MODO mwenye fi ga bomba, Jane Ramoy ‘Sanchi’ ameweka wazi kuwa, sasa amekubali rasmi kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na mchekeshaji ambaye pia ni Mtangazaji wa Redio Choice FM ya jijini Dar, Idris Sultan lakini kwa masharti.Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Sanchi alisema:

“Ni kweli nilikutana na Idris kipindi f’lani kule Sauzi, akaonesha kunipenda na mimi nikavutiwa naye hivyo tukaanzisha uhusiano. “Niliporudi Bongo nikapata taarifa kuwa bado Idris anatoka na Wema, hapo ndipo nilipoamua kumpotezea. Alikuwa akinibembeleza kuwa, hayuko naye lakini nilibaini bado wapo pamoja, nikakaa kando

“Sasa hivi nimeamini kweli wameachana hivyo sioni shida kuwa hivyo sioni shida kuwa naye kwa kuwa ni mwanaume wa aina yangu lakini masharti ni kwamba, asiwe na michepuko na pia aoneshe kunipenda kweli, nikibaini tofauti sidhani kama nitakuwa na amani,”alisema Sanchi.

Idris aliwahi kutangaza kuwa ndiye anayemmiliki mdada huyo huku akimsifia kuwa ni kifaa kuliko aliyekuwa mpenzi wake, Wema Sepetu.

Ubunge wa mama Salma Kikwete wazua gumzo

$
0
0

SIKU moja baada ya Rais Dk. John Magufuli kumteua mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Salma Kikwete kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mjadala mkali umeibuka kutokana na uteuzi wake.

Watu wa kada mbalimbali wakiwemo wasomi na wachambuzi wa masuala ya kisiasa, wameuchambua uteuzi huo kwa kuupinga na wengine kuupongeza.

Salma ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, akitokea Wilaya ya Lindi Mjini, amekuwa akitajwa kujitosa katika kinyang’anyiro cha ubunge Jimbo la Lindi Mjini, katika uchaguzi ujao.

Baadhi ya wachambuzi wanautazama uteuzi huo kama ni hatua ya kuimarisha uhusiano kati ya utawala wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na utawala wake.

PROFESA MPANGALA

Akizungumzia uteuzi huo, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCO), Profesa Gaudence Mpangala, alisema ni kawaida katika mfumo wa kiutawala kwani kuna kulindana na kuendelezana.

“Mfumo wa kiutawala unajiendesha, watawala ni wale wale kama Magufuli, Kikwete na Mkapa bado wapo kwa hiyo kuna kulindana na kuendelezana,” alisema Profesa Mpangala.

Pia alisema azma ya Mama Salma kutaka ubunge ilianza siku nyingi tangu mumewe akiwa Rais, kwani alikuwa ananyemelea ubunge Lindi na wakati huo mtoto wake Ridhiwani akinyemelea Jimbo la Chalinze.

“Hizi ni siasa za kifamilia na zilijitokeza sana katika awamu ya nne. Ingawa Rais Dk. Magufuli aliliona hilo lakini amebanwa na Katiba kwa sababu alimwondoa Possi (Dk. Abdallah) kubalance  jinsia,” alisema Prof. Mpangala.

BUTIKU

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku alisema alichokifanya Rais Dk. John Magufuli ni jambo jema na kwamba watu wasiunganishe uteuzi huo na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete.

“Ni jambo jema, Rais  (Magufuli) amefanya vizuri na watu wasimuunganishe na mumewe. Salma ana sifa zake binafsi na wala haihusiani na mume wake,” alisema Butiku.

BISIMBA

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk. Hellen Kijo Bisimba alisema uteuzi huo umemshusha daraja Salma Kikwete.

“Naona kama wamemshusha daraja huyu mama. Hiyo nafasi angepewa mwanamke mpya mwenye mawazo mapya na si kumpa mtu anayepaswa kupumzika.

“Kuchaguliwa kuwa mbunge ni kupoteza sifa, angepewa fursa ya kupumzika baada ya kazi kubwa aliyoifanya akiwa mke wa Rais,”alisema Dk. Bisimba.

RIDHIWANI

Mbunge wa Chalinze, Ridhiwan Kikwete aliweka katika ukurasa wake wa istagram na Facebook akisema mama yake (Salma) ni mwanamke wa shoka, kwani amewawezesha wasichana wengi kupata elimu.

Ridhiwani ambaye ni mtoto wa kwanza wa kiume wa Rais Mstaafu Kikwete, alisema mama yake amekuwa mtetezi wa haki za wanawake, hivyo anaamini atakwenda bungeni kuwezesha mapambano kuwa sheria rasmi.

 “Umekuwa mtetezi wa haki za wanawake na usawa wa kijinsia, umewezesha wasichana kupata elimu. Wewe ni mwanamke wa shoka. Hongera sana kwa uteuzi. Imani sasa umepata sehemu ya kuwezesha mapambano kuwa sheria. Mungu akutangulie mama yangu. Hongera tena,” aliandika Ridhiwani.

KIBAMBA

Akizungumza na MTANZANIA jana, mchambuzi wa masuala ya siasa, Deus Kibamba alisema uteuzi huo unadhihirisha wazi kwamba ni kuweka mahusiano baina ya awamu iliyopita na ya sasa.

“Nadhani ungewauliza wananchi wa kawaida wao ndio watazungumzia vizuri. Lakini kwa kifupi nadhani ni kuweka vizuri mahusiano ya awamu iliyopita na sasa lakini ni sahihi kikatiba.

“Kwa kifupi mama Salma ni mchapakazi, tulimwona akiwa pale WAMA aliendeleza harakati za wanawake vizuri,”alisema Kibamba.

DK. BANA

Naye Mhadhiri wa Siasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Benson Bana, alisema haoni kama kuna ukakasi katika uteuzi huo kwa sababu hata katika nchi za nje wako wake wa marais walishawahi kuteuliwa kuwa mawaziri.

“Kila zama zina historia mimi sioni kama kuna tatizo na kuna mifano hai Rais Yoweri Museveni wa Uganda aliwahi kumteua mkewe Janeth kuwa waziri. Cha msingi aonyeshe uwezo katika kutumikia nafasi aliyoteuliwa,” alisema Dk. Bana.

Pia alisema Rais Dk. Magufuli ametumia vigezo stahiki kumteua kwa sababu amekuwa na harakati za kuwasaidia watoto wa kike nchini.

“Mama Salma akiwa Ikulu alianzisha taasisi ya WAMA (Wanawake na Maendeleo) ambayo ilijikita katika maendeleo ya watoto wa kike, ni jambo jema kwa nchi. Hivi karibuni pia alitunukiwa kuwa balozi mwema wa lugha ya Kiswahili na tusisahau ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa akiwakilisha Mkoa wa Lindi.

“Sidhani kama katika marais wengine waliopita kuna mke ambaye amewahi hata kuwa mjumbe wa NEC. Yeye ni raia wa Tanzania anayo haki ya kutumikia nafasi yoyote iwe ya kuchaguliwa au kuteuliwa,” alisema.

Hata hivyo mkazi wa Dar es Salaam, Nayera Bakalemwa, alishangazwa na uteuzi huo kwa madai kwamba haukutarajiwa na wengi katika karne hii kwa siasa za Tanzania.

“Zipo taarifa kwamba Regina Lowassa ambaye ni mke wa aliyekuwa mgombea urais wa Ukawa mwaka juzi, Edward Lowassa, alitaka kupewa ubunge wa viti maalumu lakini kwa busara na weledi alikataa uteuzi huo.

“Alikataa mamilioni ya mshahara wanayolipwa wabunge, alizikataa posho za vikao wanazolipwa wabunge, aliyakataa mamilioni ya fedha wanayopewa wabunge kama kiinua mgongo.
“Ni Watanzania wangapi hawana ajira na wana uwezo wa kumudu nafasi hii?  Je, kwa cheo alichokuwa nacho kama ‘First lady’ hakikumtosha kiasi kwamba apewe nafasi nyingine?,” alihoji Bakalemwa.

JANET MUSEVEN

Juni mwaka jana Rais Yoweri Museveni wa Uganda,  alimteua mkewe Janet kuwa Waziri wa Elimu na Michezo katika orodha mpya ya baraza la mawaziri alilotangaza.

Uteuzi huo uliwashangaza wachambuzi wa siasa ambao walisema Museveni ana ajenda ya kuweka familia yake katika siasa kwani tayari alimpandisha cheo mwanawe Muhoozi Kainerugaba na kuwa mkuu wa vikosi maalumu.

GRACA MACHEL

Mjane wa Rais wa Kwanza wa Msumbiji, Hayati Samora Machel (Graca), aliwahi kuwa mbunge na Waziri wa Elimu na Utamaduni akiwa mwanamke pekee wa kwanza kushika nafasi hiyo kubwa baada ya Msumbiji kupata uhuru wake mwaka 1975.

Licha ya hofu aliyokuwa nayo baada ya kuteuliwa, lakini kwa mafanikio makubwa alibadilisha hali ya elimu Msumbiji na kiwango cha watoto kwenda shule kiliongezeka mara dufu kutoka watoto 400,000 hadi 1,500,000.

Hata hivyo kifo cha mumewe kilikuwa ni pigo kubwa kwake na ilipofika mwaka 1989 alistaafu wadhifa wake wa uwaziri na kujishughulisha na shughuli za maendeleo ya jamii hasa watoto.

HILLARY CLINTON

Baada ya mumewe Bill Clinton kustaafu urais wa Marekani, Hillary alichaguliwa kuwa Seneta ambaye pia alikuwa  Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani  ambapo mwaka jana alikuwa mwanamke wa kwanza kugombea urais nchini humo.

Seneta huyo wa zamani aliweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kuteuliwa na chama kikubwa nchini humo cha Democrat kugombea urais ambapo alipambana na Rais wa sasa, Donald Trump wa Republican.

Uteuzi huo wa Salma ni wa kwanza katika historia ya Tanzania kwa kuwa mke wa kwanza wa Rais mstaafu kuteuliwa ubunge.

Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, alitajwa kuwa ni mmoja ya wana CCM watakaowania ubunge Jimbo la Lindi Mjini, lakini hakuweza kufanya hivyo licha ya kutakiwa na wana CCM wenzake.

Hata hivyo, mke huyo wa Rais mstaafu Kikwete anatajwa kuwa huenda akawania Jimbo la Lindi Mjini mwaka 2020.

Salma Kikwete anakuwa ni mbunge wa tisa wa kuteuliwa na Rais Magufuli katika nafasi zake 10 kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

Hadi sasa wabunge walioteuliwa na Rais Magufuli ni Alhaji Abdallah Bulembo, Profesa Palamagamba Kabudi, Anne Malecela, Naibu Spika, Dk. Ackson Tulia, Waziri wa Mambo ya Nje, Dk. Augustino Mahiga, Profesa Makame Mbarawa (Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano), Profesa Joyce Ndalichako (Elimu)na Dk. Philip Mpango (Fedha na Mipango).

Jike Shupa Aununua Ugomvi wa Batuli, Wema

$
0
0

VIDEO Queen Zena Abdallah ‘Jike Shupa’ ameibuka na kudai kuwa, hawezi kumuacha shoga yake Wema Sepetu ashambuliwe halafu yeye abaki kimya kwani anaamini anayoyafanya yuko sahihi hivyo anatangaza kuununua ugomvi.

Jike Shupa aliyasema hayo juzikati baada ya kuibuka kundi la wasanii wa Bongo Muvi na kumshambulia Wema baada ya kujiunga Chadema ambapo inadaiwa sasa hivi kuna bifu kubwa kati ya Yobnesh Yusuf ‘Batuli na Wema.

“Kwanza kwa wasiojua na mimi nipo Chadema, sasa hao akina Batuli wanaoibuka na kumchamba Wema, nitakula nao sahani moja.

Ninachoamini yeye alikuwa na uhuru wa kufanya na kuongea kile alichojisikia na hao wanaompaka matope wajue nimenunua huu ugomvi kwa buku kumi tu,” alisema Jike Shupa. Jike Shupa katika siku za hivi karibuni ameonekana kuwa na ushosti na Wema lakini wafuatiliaji wa maisha ya mastaa wamemtahadharisha kuwa makini kwani staa huyo si mtu wa kudumu na marafiki.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images