Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Ahukumiwa Kifungo cha Maisha kwa Kumbaka Mjukuu Wake..!!!

$
0
0

Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilayani Nzega mkoani Tabora, imemhukumu kifungo cha maisha Hubasha Ngasa (62) mkazi wa Kijiji cha Ngonho baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumbaka mjukuu wake mwenye umri wa miaka minne.

Awali Mwendesha Mashtaka wa Jeshi la Polisi, Melito Ukongoji, aliieleza mahakama hiyo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa la kumbaka mtoto huyo Aprili 24 mwaka 2016 baada ya kuachwa na wazazi wake walipokwenda shambani kulima.

Ukongoji alisema, “Baada ya muda wazazi wa mtoto huyo wakiwa shambani walisikia kelele za mtoto na walipokwenda kuangalia nini kimetokea, walikuta tayari mshtakiwa amembaka na kumjeruhi sehemu zake za siri.”

Akisoma hukumu hiyo juzi, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Serafina Nsana, alisema adhabu hiyo imetolewa baada ya mahakama kuridhika na ushahidi uliowasilisishwa na upande wa mashtaka.

Man Fongo Anyang'anywa Gari na Aliyekuwa Meneja wake...Kisa Uchawi

$
0
0
Man Fongo anyang'anywa gari na aliyekuwa meneja wake baada ya kupigana chini, Bonyeza play kusikiliza kisa kizima:

Harmorapa , Harmonize Hajui kuimba Anabebwa na Media

$
0
0
Bwana mdogo anayekuja juu kwenye anga ya muziki anayetamba na ngoma yake ya usigawe pasi ambaye pia anafananishwa kimuonekano na sura kwa mbali na mwanamuziki kutoka WCB ,Harmonize ,amedai kuwa yeye ni mwanamuziki mzuri kuliko Harmonize sema tu alichelewa kutoka pia amedai kuwa hata wakiandaliwa live performance yeye na Harmonize basi atamkimbiza vibaya kama Harmonize haamini hivyo waandaliwe show aone kama anachosema ni kweli au lah

Harmorapa akaendelea kusema kuwa kinachomfanya Harmonize aonekane yupo vizuri ni media zinazo mbeba na WCB nzima yeye peke yake hajui kuimba.


Harmorapa pia alidai kuwa yeye ni team kiba damu na atafanya juu chini amshirikishe kiba kwenye ngoma zake zinazokuja .


Harmorapa pia ameendelea kung'ang'ania jina hilo na kudai kuwa halibadilishi kamwe kwa kuwa atapoteza mashabiki wake atachokifanya labda kuongeza AKA tu basi .


Harmorapa amesema kwa sasa anafanya mazoezi kwa ajili ya kuweka mwili wake uwe wa kuvutia zaidi(sexy body)uwe wa ki super star zaidi kwa kuwa yeye kwa sasa si underground tena bali ni super star hivyo basi lazima ajiweke kisupee star ili aendane na jina lake na ndio maana hata zile studio alizokuwa anaenda zamani kwa ajili ya kurecord ngoma zake haendi tena kwa kuwa si hadhi yake amewaachia underground yeye anaenda studio zenye hadhi yake

Tundu Lissu Apanga Kugoma Kula Mahabusu

$
0
0
“Nimekamatwa asubuhi na mapema. Hakuna sababu ya kutokunipeleka mahakamani leo. Kama hawatanipeleka mahakamani, nitaanza mgomo wa kula chakula, sitakula hadi nitakapopelekwa mahakamani,” amesema.

TUNDU Lissu, Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amekamatwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam leo ikiwa ni dakika chache baada ya kufutiwa mashtaka ya uchochezi yaliyokuwa yakimkabili,

Lissu amekamatwa akiwa ndani ya Mahakama ya Kisutu ambapo hii leo mahakama hiyo ilitoa uamuzi wa kufuta kesi ya uchochezi iliyokuwa ikimkabili baada ya serikali kuwasilisha taarifa kuwa haina nia ya kuendelea na kesi hiyo.

“Nimekamatiwa Mahakamani Kisutu. Sikutoka hata nje ya mahakama nikakamatwa tena. Wamenipeleka Central kwa mahojiano, polisi walionikamata wamekataa kuniambia wananikamata kwa kosa gani,” amesema Lissu katika taarifa aliyoandika na kusambaza akiwa mikononi mwa polisi.

Lissu amedai kuwa, anaamini kukamatwa kwake kuna uhusiano wa moja kwa moja uchaguzi ujao wa Chama cha Mawakili hapa nchini (TLS), unaotarajia kufanyika wiki mbili zijazo.

“Serikali hii, kwa kutumia mawakili wao vibaraka, imekuwa na mkakati mkubwa wa kunizuia kugombea urais wa TLS. Walipanga kwenda kupinga kugombea kwangu mahakamani. Tumewasema hadharani na kuzianika njama zao. Sasa wameamua kutumia rungu lao la siku zote.

“Hofu yao ni kubwa sana. Natabiri watataka kuniweka ndani hadi baada ya uchaguzi huo. Mawakili vibaraka wao wataleta hoja kwenye TLS kwamba mgombea asiyekuwapo ukumbini wakati wa Uchaguzi aondolewe kwenye kinyang’anyiro hicho,” ameandika.

Lissu ameeleza kuwa hakuna makatazo yoyote katika kanuni za uchaguzi yanayozuia mgombea kuondolewa kwenye uchaguzi kwasababu tu hayupo ukumbini na amewataka mawakili washikilie msimamo kwamba wote walioteuliwa kugombea wapigiwe kura.

Kauli ya Wakili Lawrence Masha Baada ya Kukamatwa Kwa Tundu Lissu

$
0
0
Kukamatwa kwa Mhe. Tundu Antiphas Mughwai Lissu (MB) leo tarehe 6 Machi, 2017

Nimepokea taarifa muda mfupi uliyopita kuhusu kukamatwa kwa Mhe. Tundu Lissu (Mb) na Jeshi la Polisi leo asubuhi tarehe 6 Machi, 2017. Hii taarifa nimeithibitisha baada ya kuongea naye Mhe. Lissu kwa njia ya simu akiwa Central Polisi, Dar es Salaam.

Mhe. Lissu ambaye ni wakili mwenzangu, amekamatwa baada ya kesi dhidi yake, iliofungiliwa na Serekali baada ya kukamatwa kwake Bungeni mwezi uliyopita, kufutwa katika Mahakama ya Kisutu kwa maombi ya waendesha mashtaka. Alipokamatwa Mhe. Lissu alikua akilelekea kwenye kesi nyingine akiwa kama wakili mtetezi katika shauri hilo.

Tabia ya polisi ya kukamata watu baada ya kuachiwa na mahakama au kufutiwa kesi na waendesha mashtaka imeanza kuwa mazoea. Hii siyo mara ya kwanza imefanyika. Natoa rai kwa watumishi wa vyombo vya dola kwamba waheshimu haki za binadamu na waheshimu misingi ya sheria zetu. Kupindisha sheria ili kutimiza malengo ya watu fulani bila kuzingatia misingi ya haki itatupeleka pabaya kama nchi.

Kuna tetesi kwamba kukamatwa kwa Mhe. Lissu inahusiana na njama zinazofanyika na watu wasiojulikana kumzuwia kushiriki katika uchaguzi wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) ambayo inatarajiwa kufanyika tarehe 18 mwezi huu. Kama hizi tetesi zina ukweli wowote napenda kuweka wazi msimamo wangu kwamba uchaguzi wa TLS usiingiliwe na chombo chochote cha dola. Wanasheria waruhusiwe kuchaguwa Rais wanaomtaka.

Uchaguzi huu wa TLS umekuwa na msisimko wa kipekee kwasababu Wanasheria walio wengi wamechoka kuona haki za watanzania zikiminywa kwa matumizi mabaya ya vyombo vya dola. Watanzania wanataka Nchi inayoheshimu utawala bora na utawala wa kisheria, na wanataka chama cha wanasheria ambalo lina nguvu ya kukemea pale ambapo haki haitendeki.

Kwasababu Jeshi la polisi hawajatangaza sababu ya kukamatwa kwa Mhe. Lissu ni vigumu kwa wakati huu kuongelea kilichosababisha akamtwe. Ni vema lakini kwamba Jeshi la Polisi litoe tamko mapema ili watanzania wafahamu ni kosa gani ambalo Mhe. Lissu ametuhumiwa kufanya. Kukaa kimya kwa Jeshi la Polisi itaendelea kujenga hisia kwamba kuna ukweli kwamba kuna njama ya kumzuwia Mhe. Lissu kushiriki katika uchaguzi wa TLS, jambo ambalo ni haki yake kama mwanachama aliyechujwa na kupitishwa kuwa mgombea wa nafasi ya urais wa TLS.

Lawrence Masha
Machi 6, 2017

Mbunge Peter Msigwa Amrushia Dongo Paul Makonda Kupitia Facebook

$
0
0

Mbunge Peter Msigwa Ameweka Picha hiyo hapo juu katika ukurasa wake wa Facebook na Kuandika Haya Hapa chini:


"Hakuna vita yoyote ya kiroho wal kimwili ALIYOFANYA (BASHITE)Makonda BALI, ni Upuuzi wa kiwango cha juu in the real sense, ANAJARIBU KUFANYA MAMBO YA TEMBO , KUMBE ANA ROHO YA SUNGURA, kulia haitasaidia , atubu kwa kuwasingizia watu UONGO!! Bashite you are still young , go get some leadership skills!, TITTLE , AUTHORITY AND POWER is dangerous without leadership skills" Peter Msigwa


Una maoni Gani?

Sakata la Vyeti Feki: Daudi Bashite Vs Paulo Makonda..!!

$
0
0

Kuna vitu huwa sielewi hapa. Mwaka fulani ilitajwa orodha ya mafisadi wa elimu waliokuwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Spika wa Bunge alikuwa Marehemu Mzee Samwel Sita (Mwenyezi Mungu ailaze Roho yake mahala pema peponi, Amina), Spika akaingilia kati kusema PhD ya Dr. Mathayo David ilikuwa halali hivyo katajwa kimakosa, ila wengine wote waliobaki hakuwasemea mf, akina Dialo (Dr.), Merry Nagu (Dr.) nk. Lakini nakumbuka baada ya Mzee Sita kusema hivyo, TCU immediately walitoa tamko, ya kwamba wao ndio wenye mamlaka ya kusema kama Degree ya mtu fulani ni feki ama vinginevyo na baada ya hapo hata vile vijarida na yule bwana aliyekuwa kinara wa ile scandal sijui walipotelea wapi.

Nirejee kwenye hii scandal maarufu ya Daudi Bashite Vs Paulo Makonda, tunazo taasisi zetu nyingi kuanzia hizo za kitaaluma alikopita huyo Ndg, anza secondary school both O level and Advanced Level, kuna walimu waliomfundisha, na baraza la Mtihani NECTA nk. Twende kwenye Chuo alichosoma tena hivi majuzi tu kote huko vyombo vya kiuchunguzi vinapajua na panafikika na sio wala nje ya nchi na hakuna gharama kihivyo.

Binafsi naamini kama hiyo ni kweli ni swala la muda tu, let us wait and see, lakini kama ni longo longo kwa nini tunapoteza muda wetu.
Kuna mkubwa mmoja katika taasisi moja hapa nchini, yeye alisema ana PhD, Chuo alichopata hiyo Degree yake SA, watu wakaanza kusema sema alikimbia mwenyewe ofisi, ingawa kiutendaji alikuwa mzuri kabisa na ni kweli aliwahi kufanya hiyo Degree yake huko SA ingawa haiku- materialize. 
Kumbe basi ni swala la muda tu, maana tumeshudia watu wengi wakifutika humu makazini kama upepo na wengine wakistafu gafla, ukiuliza unaambiwa vyeti vina utata, hivyo basi kama jamaa naye kuna hila ipo siku ataondoka tu. Binafsi naamini kwa hizi kelele ambazo zimepigwa kuhusu Bashite vyombo vya uchunguzi vilikwisha maliza kukusanya taarifa kuanzia kijijini Kolomije, shuleni msingi na sekondari na hadi chuo. 

Nikimwaangalia Makonda bado ni kijana kuliko mimi, lakini mimi nikienda shuleni kwangu msingi bado wapo walimu walionifundisha primary pale kituoni zaidi ya 20 yrs ago, ingawa wengine wamehama na wengine kustaafu, lakini hata wasipokuwepo taarifa zinapatikana tu. Sasa sembuse huyo, Jamani Sefue Ombeni aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi aliandikwa na Gazeti moja tu, akatoka akakanusha kwa nguvu zote juu ya ile taarifa na vitisho vya kwenda mahakamani na kudai fidia, mbona baada ya muda mfupi aliondoka. Ingawa sijui kama kuondoka kwake kulitokana na ile habari iliyooandikwa na lile gazeti, lakini walau ndio taarifa pekee ya mwisho iliyokuwa na ukakasi kumuhusu yeye binafsi na sio taasisi.

Mamlaka ya uteuzi wa Mkuu wa Mkoa (RC) ambayo ni Rais, ina mikono mirefu na mipana, ina macho mengi na yenye nguvu ya kuona kila sehemu, tuipe ushirikiano chanya katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku likiwemo hili la Daudi Bashite nadhani itatoa majibu nasi tutayaona hata pasipokuambiwa. Hizi kelele nyingi kupita kiasi zinaweza hata kuwapoteza na kuipuuzia hii taarifa kwa kuzani ni kelele za watu walioguswa na utendaji wa Ndg Makonda hasa kwenye dawa za kulevya.

Katika utendaji kazi wake hasa kwa siku za hivi karibuni kama Mkuu wa Mkoa Ndg Makonda sote tunajua amegusa eneo la watu wenye nguvu ya pesa chafu, majuzi nimeona comment ya Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif, juu ya hii vita, kila mtu anajua nguvu ya hao watu, wanaweza fanya jambo lolote hasa kwa watu wa kawaida kama akina RCs nk, maana kuna nchi tunaambiwa hata President anaweza kupinduliwa na drug dealers, hivyo mimi kwa kutambua uwezo mkubwa wa watu walioguswa na RC Makonda hivi karibuni, nitakuwa wa mwisho kuamini kila baya linalozungumzwa kuhusu Makonda kwenye social media na kwingineko mpaka vyombo husika vitakapo toa taarifa aidha in public ama tukaona vitendo kama enzi ya kina Sefue nk. Mwanzoni kuanzia kule Bungeni tuliambiwa ana majumba ya Gorofa ndani mwaka mmoja nk, leo havisemwi tena.

Mwisho kabisa, natamani kuona vyombo vyetu (Responsible Institution) zikifanya kazi yake kwa umakini na kutoa taarifa sehemu husika kwa utekelezaji na sio vinginevyo. Ahsante

Hizi Ndio Akili za Watanzania...Ndio Maana Hatuendelei...!!!

$
0
0

Watu wameambiwa waandike panua na picha itabadilika na miguu itapanuka, na watu wanaamini kweli,yaani vichwa ngono na vilaza hadi basi




Vurugu za machinga zajeruhi watu 9 Jijini Mwanza Wakiwemo Mgambo wa jiji

$
0
0

Watu tisa (9) wamejeruhiwa katika vurugu wakati wa kuwaondoa wafanyabiashara wadogowadogo sehemu zisizo ruhusiwa wilayani Nyamagana, mkoani Mwanza


Taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa w Mwanza DCP Ahmed Msangi imesema kwamba tukio hilo limetokea mnamo tarehe 05.03.2017 majira ya saa15:45hrs katika mtaa wa Buhongwa Center ambapo watu tisa wakiwemo askari mgambo wa jiji la mwanza saba (07), afisa mazingira mmoja (01) na dereva wa jiji mmoja (01) walijeruhiwa.


Amesema watu hao walijeruhiwa kwa kupigwa na mawe sehemu mbalimbali ya miili yao na wafanyabiashara wadogowadogo waliokuwa wakifanya biashara pembeni ya barabara wakishirikiana na watu wengine waliokua wakishabikia wakati wakiendelea na zoezi la kuwaondoa wafanya biashara wadogowadogo katika maeneo yasiyo ruhusiwa haswa kwenye hifadhi ya barabara ya mwanza kwenda shinyanga.


Aidha, Msangi amesema katika harakati za kudhibiti vurugu hizo askari walifanikiwa kuwakamata watu tisa ambao inadaiwa kuwa walikuwa wakihusika katika vurugu hizo kwa ajili ya mahojiano na uchunguzi utakapokamilika, watafikishwa mahakamani.


Majeruhi wote wapo hospitali ya mkoa ya Sekou Toure wakiendelea kupatiwa matibabu na hali zao inaendelea vizuri.

Kwanini Wanaume Wengi Hufeli Swali Hili Wakitongoza?

$
0
0
Wanaume wamekuwa wakijifanya ni mabingwa kama siyo majabali wa kutongoza lakini mara baada tu ya ujio wa simu za mkononi hakika zimekuwa ni kama ni mateso makubwa kwao.

Nalisema hili kutokana na kwamba unaweza kumkuta mwanaume anapambana au anahangaika kuipata namba ya mwanamke fulani ambaye hajuani nae au labda namba yake kaipata tu kwa mtu ili aanze kumtongoza kwa simu ama kwa kumpigia au kumtumia meseji lakini imekuja kujulikana kuwa hakuna mtihani mgumu au swali gumu ambalo wanaume wengi hukumbana nalo na ambalo wengi wao hushindwa kulijibu na hatimaye kujikuta wanajichanganya na wanamkosa huyo mwanamke.

Utakuta mwanaume anaanza kujitutumua kwa kuwasiliana na huyo mwanamke lakini akiulizwa tu swali hili " je namba yangu umeitoa wapi au kakupa nani? " wengi wao hukata tamaa kabisa na hata kuishiwa tena nguvu za kuendelea kuwasiliana na yule binti au mwanamke kwani hakuna swali ambalo wanaume wengi hawalipendi na hawaliwezi kulijibu kama hilo.

Labda leo tupate uzoefu kutoka kwa wanaume ambao naamini humu mpo wengi ni kwanini wengi wenu pamoja na jeuri zenu zote mkiulizwa tu hilo swali tajwa hapo juu huwa mnajiumauma na hatimaye kusepa na kuishia kulalamika tu?

Na je unadhani majibu sahihi ya kumjibu mwanamke ambaye hujuani nae halafu umepata tu namba yake kwa mtu na unataka kumtongoza endapo atakuuliza hilo swali kuwa " namba yangu umeitoa wapi au namba yangu kakupa nani? " ni yapi au ni lipi?

Hatarii..Mchungaji Msigwa Naye Amrushia Makonda Kombora Zito,Adai Anayoyafanya ni Upuuzi wa Kiwango cha Juu..!!!

$
0
0

Hakuna vita yoyote ya kiroho wala kimwili ALIYOFANYA (BASHITE)Makonda BALI, ni Upuuzi wa kiwango cha juu in the real sense,

ANAJARIBU KUFANYA MAMBO YA TEMBO , KUMBE ANA ROHO YA SUNGURA, kulia haitasaidia , atubu kwa kuwasingizia watu UONGO!! Bashite you are still young , go get some leadership skills!,

TITTLE , AUTHORITY AND POWER is dangerous without leadership skills.

By Peter Msigwa

Baada ya TID Kumfananisha na Panya..Steve Nyerere Ampa Jibu Hili ...!!!

$
0
0

Msanii mchekeshaji Steven Nyerere ameendelea kum diss TID kwa kusema ni mtu ambaye wakati wake umepita na pia hajielewi na hawezi kujifananisha naye
Amedai msanii huyo anaishi kwao na amekuwa akimpiga vizinga vya 10,000 na 5,000 kila akiona gari lake huku yeye akiwa ana nyumba na anatunza familia na kununua mafuta ya magari kadhaa

Rais Magufuli Amsifia Mbunge wa Cuf,Amtaka Ahamie CCM Haraka..!!!

$
0
0

Rais Magufuli amempongeza Mbunge wa Mtwara Mjini kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Maftaha Nachuma kwa utendaji kazi wake.

Rais Magufuli amesema, ''Pamoja na kwamba CCM tuliteleza kidogo lakini Mbunge huyu ni mchapakazi kweli''.

Aliendelea kusema, ''Tunahitaji Wabunge wa aina hii, tumezunguka naye katika ziara yangu na kujionea kazi zake anazozifanya, Yeye anataka maendeleo ya wananchi wake''.

Alimalizia kwa kusema, ''Kwa kweli ninakupongeza, hongera sana. Una moyo mzuri hata sura nzuri''.

''Inawezekana sura ikawa CUF CUF lakini moyo wake ni CCM, Ningetamani siku moja ukahamia CCM, ningefurahi sana'' alisema Rais.

Mbunge Maftaha alimshukuru Rais kwa kumpa ushirikiano wa karibu katika kazi zake za kuwatumikia wananchi wa Mtwara Mjini.

Kimenuka..Vigogo wa ‘unga’ wahojiwa,,!!!

$
0
0

Kazi ya kuchunguza majina 97 yaliyokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa Kamishna wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, imeanza kufanyiwa kazi kwa vigogo watano waliotajwa kuhojiwa.

Februari 13, Makonda alimkabidhi Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo, Rogers Sianga orodha ya majina 97 ikiwa ni awamu ya tatu ya watuhumiwa wa biashara ya dawa za kulevya.

Kamishna wa Intelijensia wa Mamlaka hiyo, Fredrick Kibula alisema jana kuwa wanawahoji na wanafanya uchunguzi dhidi ya watuhumiwa hao kabla ya kuwafikisha mahakamani.

“Tuna watu muhimu watano wanaotoka katika orodha ile ya mkuu wa mkoa. Tunao kwa ajili ya uchunguzi zaidi na muda ukifika tutawatajia mtawafahamu,” alisema Kamishna Kibula na kuongeza:

 “Hatukamati ovyoovyo ni lazima tujiridhishe bila shaka kwamba wahusika wana sifa ya kukamatwa. Pia hatutangazi ingawa tunafanya operesheni za kiuchunguzi ambazo zinafanyika mara kwa mara.”

Rais Magufuli Atengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha Dkt. Crispin Mpemba ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma za kiutendaji zinazomkabili ikiwemo uendeshaji wa shirika hilo

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI George Simbachawene amesema moja ya tuhuma zinazomkabili ni pamoja na kuingia mikataba kiholela.

Shirika la Elimu Kibaha ni Shirika la umma linalotoa huduma mbalimbali likiwa na ofisi zake Mkoa wa Pwani kilomita 40 Magharibi mwa Mji wa Dar es salaam.


Mrisho Mpoto Awataka Wananchi Kuangalia Utendaji kazi wa RC Makonda Siyo vyeti

$
0
0
Msanii wa muziki wa asili nchini Mrisho Mpoto ameamua kumkingia kifua RC Makonda ambaye kwa siku za karibuni amekuwa aki-trend kwenye mitandao ya kijamii akituhumiwa kufoji vyeti.


Mpoto amedai anashangaa kuona hata wale ambao walikuwa wanamsupport na kumsifia mkuu huyo wameshinndwa kufungua midomo yao.

“Hii nchi ya ajabu sana ukifanya vizuri lazima upate maadui mpaka wakushushe, ndiyo waanze kumpansisha mwingine. Wako wapi waliosema Makonda songa mbele usirudi nyuma? mko wapi mliomuita Makonda shujaa mkombozi wa Wa watoto wetu, leo kila mtu anamruka na kuona hakuna alichofanya This is not Fair at all,” alianidika Mpoto Instagram.

“Angalieni utendaji wake Wa kazi na siyo vyeti vyake guys!! Songa Songa Songa Makonda kama ulivyosema hii vita siyo ndogo na ina wanafiki wengi. @paulmakonda @paulmakonda unawaona waleeeeeee ndiyo siyo watu wazuri kabisa!!,” aliongeza Mpoto.

Mkuu huyo hivi karibuni alidai hayo yote yamezalishwa kutokana na vita yake dhidi ya madawa ya kulevya ambayo umezaa matunda kwa kiasi kikubwa.

Picha za Nusu Utupu Zawapeleka Polisi Gigy Money, Sanchoka na Amber Lulu

$
0
0
Sekeseke la picha na video za utupu zinazopachikwa na baadhi ya warembo kwenye mitandao ya kijamii hasa Instagram kwa lengo la kujipatia wanaume yaani kujiuza mitandaoni (Cyber Prostitution), linadaiwa kusababisha baadhi yao kuitwa kwenye Kituo Kikuu cha Polisi ‘Sentro’ jijini Dar es Salaam.

TUJIUNGE NA CHANZO CHA NDANI
Kwa mujibu wa chanzo makini cha ndani ya jeshi hilo, warembo hao wanahitajika kwenye Kitengo cha Kupambana na Uhalifu wa Mtandaoni (Cyber Crimes) kilicho chini ya Jeshi la Polisi Tanzania kufuatia video na picha zao za utupu kuendelea ‘kutrendi’ mitandaoni na kumomonyoa maadili ya watoto wa Kitanzania. “Wapo wengi, ni kama ilivyokuwa kwa wale mastaa wa madawa ya kulevya.
Wengi ni hawa warembo, sijui wanawaita video queen. Hawa muda mwingi wapo mitandaoni wanatupia video na picha za utupu. “Polisi wanasema kabla ya sheria kuchukua mkondo wake itabidi wawabane ili kueleza lengo lao ni nini? Kama itabainika wanajua lakini wanafanya makusudi, sheria itachukua mkondo wake na adhabu kali itawahusu.

“Wanaoitwa Sentro wapo wengi lakini kuna huyu Sanchoka (Jane Ramoy), Gigy Money (Gift Stanford) na Amber Lulu (Lulu Auggen). Hawa watoto ni shida hivyo inabidi kuwapunguza spidi na wawe mfano kwa wengine.

YUMO PIA MTANGAZAJI WA REDIO
“Kimsingi hawa ndiyo ambao wamekuwa wakilalamikiwa zaidi. Lakini pia yumo mtangazaji wa redio moja ambaye siku hizi naye anachefua watu na kusababisha watu kuhoji utendani wa kitengo hiki cha polisi.


 Ambacho watu hawakijui ni kwamba polisi hawawezi kumkamata bila kupokea malalamiko kuwa anafanya hiki na hiki mtandaoni na kisheria siyo sahihi. “Lakini kwa hawa malalamiko yapo kila kukicha,” kilinyetisha chanzo chetu.

KWA NINI TCRA HAWACHUKUI HATUA?
Akizungumza na Wikienda juu ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) juu ya watu kama hao, Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy anafafanua kuwa, mamlaka hiyo haina mamlaka ya kumkamata mtu isipokuwa malalamiko yanapaswa kupelekwa polisi.

“Jeshi la Polisi likishapata malalamiko, wenyewe ndiyo wanajua namna ya kukamata wahusika,” alisema Mungy. Baada ya kuwasikia TCRA, Wikienda lilifika Sentro kwenye kitengo hicho cha uhalifu wa mitandaoni na kuonana na Kamanda wa Kitengo cha Uhalifu wa Mitandaoni (Cyber crimes Unity), Kamanda Mwangasa Joshua ambaye alizungumzia juu ya ishu hiyo.


Kamanda Mwangasa aliliambia Wikienda kuwa, baada ya kupokea malalamiko hayo, jopo lake la wachunguzi limekuwa likizipitia ‘accounts’ zote za warembo hao ili kuwachukulia hatua stahiki haraka iwezekanavyo.

“Sisi kama mamlaka yenye dhamana hatuwezi kuvumilia ukiukwaji wa sheria wa kiwango hicho. Tukishawahoji, tukijiridhisha, tutawafikisha mahakamani mara moja.

“Lakini niwatahadharishe tu kwamba uchunguzi ni muhimu kwa sababu mtu anaweza akatengeneza account kwa jina la mtu mwingine, lakini la kujiuliza hapo mtu huyo anapataje picha zako za utupu kila siku na kuzituma?

“Yote hayo tutayajua tukichunguza. Siwezi kupuuza taarifa tunazozipokea za warembo hao.

“Wananchi wanapaswa waelewe kuwa sheria haikukatazi wewe kupiga picha ya utupu, lakini inakuzuia kutumia picha hiyo vibaya kwa kuituma kwenye mitandao kisha kila mtu akaiona. Hilo ni kosa kisheria, kwa hiyo sisi tutaanza na hao ambao tayari majina yao tunayo.

“Niwashukuru wanahabari kwa kuendelea kutuonyesha uozo unaofanywa na watu mbalimbali ambao wakati mwingine sisi tunakuwa hatuna taarifa zao, sheria ya mtandao haijambagua mtu, sheria hii ipo kwa ajili ya watu wote, haijalishi kama wewe ni mtu maarufu au siyo maarufu, ukifanya kosa utawajibishwa tu,” alisema Kamanda Mwangasa.

GIGY, AMBER WAJITETEA Wikienda liliwatafuta mamodo hao kwa nyakati tofuati ambapo Sanchoka hakuweza kupatikana huku Gigy na Amber Lulu wakijitetea kuwa watajieleza kwamba huwa wanafanya kwa ajili ya matangazo ya nguo.

Makonda Ajiuzulu?Ashindwa Kumpokea JPM,Akimbilia Afrika Kusini..Habari Katika Vichwa vya Magazeti ya Leo..!!!

Noma Sanaa..Filamu ya Lissu yanoga

$
0
0

 Mambo yanayomtokea kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) ni kama mchezo wa kuigiza.

Jana, Lissu alianza siku kwa furaha baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu kumuona hana kesi ya kujibu, lakini dakika chache baadaye polisi walimkamata tena, kumhoji na kumuachia kwa dhamana.

Licha ya kashikashi hizo mahakamani na kituo cha polisi, Lissu ameonyesha kuwa na sakata jingine katika uchaguzi wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) baada ya kudai kuwa kuna mkakati unasukwa na baadhi ya mawakili wenzake kutaka kumkwamisha asigombee urais wa chama hicho.

 Baada ya kuachiwa huru, Lissu alikamatwa na polisi akiwa Mahakama ya Kisutu na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi, lakini haikueleweka sababu za kukamatwa kwake.

Lissu alikutana na polisi hao saa 4:00  asubuhi na akaambiwa kuwa anahitajika kituoni, mbunge huyo aliomba aendeshe gari lake mwenyewe ambalo alikuwa nalo Kisutu.

Wakili wake, Fredrick Kihwelo alisema: “Polisi walikubaliana naye na kuingia kwenye gari lake na kuelekea kituoni hapo na walipofika walikaa muda kisha wakaelezwa kuwa, anadaiwa kutoa 
matamshi yanayoweza kusababisha matatizo ya kidini.”

Alisema Lissu alidaiwa kutoa matamshi hayo akiwa mkoani Dodoma, hivyo baada ya mahojiano aliachiwa kwa dhamana na kutakiwa kuripoti kituoni hapo Machi 13.

CUF Washtuka, Wadai Kuna Mpango wa Kumhujumu Maalim Seif..!!!

$
0
0

Chama cha Wananchi (CUF) kimedai kuna mipango inayofanyika ya kumvua ukatibu mkuu Maalim Seif Sharif Hamad kwa sababu anaonekana kama kikwazo cha utulivu Zanzibar.

Katika taarifa iliyotolewa na chama hicho jana, ilidai kuna kikao cha chini chini ambacho kimeandaliwa na baadhi ya wajumbe wa upande mmoja wa CUF, kikiwa na lengo hilo huku upande wa pili ikipinga kikao hicho ambacho hakitambuliki kikatiba.

“Kwa mujibu wa katiba ya CUF Ibara ya 84 (1) ikisomwa pamoja na ibara ya 93 (1)(d) inaeleza kuwa; ...kutakuwa na Kamati ya Utendaji ya Taifa ambayo itakutana mara moja kwa kila miezi miwili,” ilisema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo ilitolewa jana na Katibu Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano ya Umma, Mbarara Maharagande ilieleza mara ya mwisho kikao cha kawaida cha Kamati ya Utendaji ya Taifa kilifanyika Februari 2, 2017 katika ofisi ndogo ya chama Vuga, Mjini Unguja.

Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images