Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Ukweli Ndio Huu..Watumiaji wa Mitandao na Watanzania Tumelishwa Tango Pori Kuhusu Mtoaji Bastola kwa Nape Pale Protea..!!!

$
0
0

Najua wengi mtashtuka na wengine kunipinga hadi kunibishia ila kwa ushahidi wa jicho la Tatu na la msaada wa Wataalam wa Saikolojia na Wabobezi waliotukuka kwa Utambuaji wa Mtu / Watu yule Mtu tunayeambiwa kuwa ndiyo alimtolea Bastola Nape Nnauye pale Protea na ambaye picha zake zinasambazwa Mitandaoni siyo Mhusika halisi bali tumedanganywa.

Ili kuweza kuamini hili tafadhali hapo hapo ulipo itafute picha ile ya yule wa Protea kisha kwa umakini wako mkubwa kabisa huku ukiwa umetuliza akili zako zote ilinganishe na hizi picha zinazotembea Mitandaoni na utapata jibu.

Mbinu iliyotumika hapa ni ya Kijasusi zaidi na ya hali ya juu ambapo kuna Mtanzania mmoja anayeaminika yupo Ughaibuni na hupenda mno kukurupuka kuwalisha matango pori Watanzania na wapo wanaomuamini hivyo kilichofanyika kwakuwa anajulikana kuwa na ' kiherehere ' Watu wenye Kazi zao na waliobobea wakaamua kumtumia picha za Mtu anayeonekana katika Mitandao ili zisambae haraka lakini Mhusika Mkuu ( Mtoaji Bastola ) akiwa yupo mahala pengine na anaendelea na majukumu yake.

Nasisitiza tena kuwa tulieni na ziangalieni kwa umakini mkubwa hizo picha na mwishoni mtapata majibu kuwa tumelishwa matango pori na tumeshiba kabisa ila mchomoaji Bastola kwa Nape pale Protea kwa 100% siyo huyu mwenye picha tunazoziona Mitandaoni. Huyo Binti wenu wa Ughaibuni sasa hivi Watu wanampa taarifa za Uwongo ili kuweza kumuharibia na aonekane bure na nasikitika kwamba huu mtego hajaushtukia na kila mara anauvagaa tu.

Ijumaa Karim nyote.

Skendo Zampa Stress Davido, Alazwa Hospitali!

$
0
0

MKURUGENZI wa Lebo ya HKN, David Adeleke ‘Davido’ amekimbizwa hospitali na kulazwa huku chanzo kikidaiwa kuwa ni ‘stress’. Tukio hilo limejiri juzikati ambapo inaelezwa kuwa, Davido amekuwa akisumbuliwa na skendo inayozidi kuenea kwa kasi kuhusiana na kuzaa na mwanamke anayefahamika kama Ayomide Labinjo.

Haikuelezwa hasa hospitali ipi amelazwa lakini kupitia Mtandao wa Snaptchat, Davido liweka kipande cha video akiwa ametundukiwa dripu na kuwaambia mashabiki wake wamuombee.

Hivi karibuni, Ayomide alizungumza na Jarida la Punch na kuanika kila kitu kuwa, amezaa na Davido baada ya kulazimishwa wasitumie kinga.

“Kama Davido unanisikiliza ulijue hili kuwa uligoma kutumia kinga,” Ayomide aliliambia Punch. Tayari, Ayomide kwa kushirikiana na mama yake wameshafungua mashtaka yakumtaka Davido ashiriki katika malezi ya mtoto huyo.

Mahakama Kenya Imeizuia Serikali Kuajiri Madaktari Kutoka Tanzania

$
0
0

KENYA: Mahakama imeizuia Serikali kuajiri Madaktari kutoka Tanzania kwa sababu ndani ya nchi hiyo kuna Madaktari 1,400 wasioajiriwa.

Mpaka sasa takribani watanzania 400 wenye taaluma ya Utabibu wameomba kazi hiyo.

Rais Magufuli alikubali ombi la kupeleka Madaktari 500 ili kupunguza uhaba wa Madaktari nchini Kenya kutokana na mgomo unaoendelea nchini humo.

Erick Shigongo Aendelea Kuwapa Makavu Live Diamond na Uongozi Wake...Adai Wanajichimbia Shimo

$
0
0

Kama nilivyosema wakati naanza kwamba ninampenda sana Diamond kwa sababu amekuwa mtu wa kujituma, aliyeng’ang’ania kutoka kwenye umasikini mpaka kuwa na mafanikio aliyokuwa nayo.
Ieleweke kwamba sipo kwa ajili ya kumsema, kumponda, hapana, nipo kwa ajili ya kumshauri kama mdogo wangu, rafiki yangu kwa hiyo naomba nisieleweke vibaya.
Diamond Platnumz kwao ni Tanzania, ni mwanamuziki wa Kitanzania na hata wapenzi wake wengi wanaomsapoti kwa nguvu nyingi ni Watanzania ambao asilimia kubwa vipato vyao ni vya chini mno.
Wengi wanatamani kumuona akifanya shoo katika ardhi yake ya nyumbani, lakini badala yake wamekuwa wakimuona mara nyingi akifanya shoo Marekani, Ulaya, Nigeria, Afrika Kusini, kwenye Mashindano ya Afcon na sehemu nyingine nyingi ambazo ni nje ya Tanzania, mahali alipozaliwa na kuthaminiwa, mahali ambapo aliweza kujijazia mashabiki wengi.
Mashabiki zake wanahitaji shoo, kumsoma kwamba amejenga nyumba, amenunua au amepata watoto na Zari si kitu ambacho mashabiki wanakihitaji zaidi kutoka kwake, wanachohitaji ni kuona shoo zake kwa wingi kama kilivyokuwa kipindi cha Moyo Wangu, Kamwambie na nyimbo nyingine.
Ni kweli ana jina kubwa, ana mashabiki wengi, amepambana sana kufika alipokuwa lakini kwa upande mwingine anatakiwa kuangalia gharama za shoo zake hasa anapofanya nchini Tanzania, kwa watu ambao walimfanya leo kujulikana zaidi kama Diamond na si Naseeb Abdul.
Leo, Diamond anafanya shoo kwa dola 55,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 100. Hii inamaanisha kwamba kwa mtu kama mimi, nikimchukua Diamond kwa gharama hiyo inamaana kwamba nitataka niingize kiasi kikubwa kama faida, kwa hiyo badala ya kufanya shoo Dar Live, Diamond Jubilee au sehemu nyingine, nitaihamishia shoo yangu Mlimani City na kufanya kiingilio cha shilingi elfu hamsini.
Swali la kujiuliza, je, yule bodaboda anayepiga sana nyimbo za Diamond ataweza kuingia kwa kiingilio cha shilingi elfu hamsini? Yule kijana anayatafuta riziki kwa kuingiza nyimbo za Diamond kwenye simu za wateja ataweza kuingia kwa gharama hiyo? Je, yule kijana wa Tandale, Temeke, Mbagala mwenye fulana kubwa iliyoandikwa WCB ataweza kuingia kwa gharama hiyo?


Je, yule kijana wa Tandale, Temeke, Mbagala mwenye fulana kubwa iliyoandikwa WCB ataweza kuingia kwa gharama hiyo? Jibu rahisi ni kwamba hatoweza.
Ni lazima afikirie ajue kwamba gharama anazotoza sehemu nyingine ziwe tofauti na Tanzania, au azifanyie gharama hizo kampuni kubwa za mitandao ya simu na vinywaji lakini si mtu binafsi.
Mara nyingi amekuwa akisema huko nje analipwa zaidi ya milioni mia moja, je, ni halali hata kwa Watanzania wenzake waliomfanya kuwa hapo alipo kuwatoza kiasi hicho cha fedha huku huyo anayemchukua akitarajia shoo yake iingiwe na watu wa hali ya chini wenye kiu ya kumuona?
Labda Naseeb Abdul mwenyewe ndiye aliyelazimisha ada hii, kama si yeye bali ni mameneja wake (Salam na Tale) basi wanamshauri vibaya na matokeo yake kutofanya shoo nyumbani kwake (Tanzania) kutamfanya apoteze kupendwa na mashabiki sababu ya umbali alioutengeneza.
Ikumbukwe kwamba watu hununua bidhaa ya mtu wanayempenda, mtu akichukiwa na bidhaa zake hususiwa.
Diamond na WCB ni biashara ya Naseeb Abdul, hivyo basi Naseeb Abdul hatakiwi kuthamini sana fedha na kusahau mashabiki zake waliomfanya kuwa hapo alipo. Kifike kipindi awaeleze mameneja wake “HAPANA! TANZANIA NI NYUMBANI NA HAWA NI NDUGU ZANGU”
Basi kama waandaaji watashindwa kumudu gharama zake sababu Naseeb ni mfanyabiashara kama mimi, basi afanye shoo ya kujitolea (Charity show) kama tuliyofanya naye huko Tandale huko Mwanza, Kigoma, Mbeya, Arusha, Kilimanjaro kwenye viwanja kwa kiingilio cha shilingi 3000 na kisha fedha hizo azipeleke kusaidia watu wanaoishi kwenye mazingira magumu na hiyo itamfanya kupendwa na mashabiki na kumfanya kwenda juu kimuziki.
TOFAUTI NA HAPA, MBELE YAKE KUNA SHIMO, UKIMYA WAKE BILA SHOO NYUMBANI UTAMZAMISHA!! MWISHO.

Baada ya Harmorapa..Sasa Kuna Wemarapa..Adai Wema Anajipendekeza Kwake Ila Hana Mpango Nae..!!!

$
0
0

Kuna imani kuwa duniani wawiliwawili! Hii inajidhihirisha kwa mwanadada Lisa Deedee `Tuerny’ ambaye amejipatia umaarufu mitandaoni kutokana na kufananishwa na staa wa sinema za Kibongo, Wema Sepetu.

Kupitia gazeti hili, mrembo huyo anafunguka mambo mbalimbali usiyoyajua kuhusu yeye; Ijumaa: Hivi Tuerny ulijuaje kuwa unafanana na Wema?

Tuerny: Nakumbuka mwaka 2012 niliweka picha mtandaoni, mama akanitumia sms kwamba ninafanana na Wema, nilishtuka lakini tangu hapo akawa kama amebariki hicho kitu. Nilishangaa kila sehemu niliyokwenda watu wananiambia nafanana na Wema.

Ijumaa: Ulijisikiaje kufananishwa naye na ni changamoto zipi unazokutana nazo?

Tuerny: Sikuona kama ni kero, nilichukulia kawaida tu, haikuwa chanzo cha mimi kufanya vitu vya kufanana naye, mimi siyo mtu wa shobo kama hao wengine na sijawahi kuwa shabiki wake, changamoto ni kwamba wengi wanajua Wema ni ndugu yangu wakati si kweli.

Ijumaa: Je, umeshawahi kuwa na ukaribu na Wema?

Tuerny: Sijawahi na sifikirii, ila kipindi watu wanaanza kunifananisha naye alifurahi akawa ana-comment kwenye picha zangu Instagram, akawa ananisifia na mimi ninamjibu, lakini kutokana na maneno ya watu akachukia na kunipotezea.

Ijumaa: Kwa nini hupendi awe rafiki yako?

Tuerny: Yeye ana marafiki wengi na kwenye maisha yangu sipendi kuwa na mtu mwenye marafiki wengi, kwani majungu yatakuwa mengi.

Ijumaa: Nilisikia kuna kipindi uliwahi kukutana na Wema lakini ukampotezea hata salamu hukumpa, kwa nini?

Tuerny: Ni kweli, mwaka 2015 nikiwa kwenye mishe zangu nilimuona pale Klabu Cafee, akatabasamu na mimi pia, tatizo mimi sijui kujipendekeza ndiyo maana sikumfuata.

Ijumaa: Vigogo wangapi ambao wamewahi kukuomba penzi, kwa kutaka kuonja ladha ya copy ya Wema?

Tuerny: Inawezekana watu wanaumiza kichwa kwa sababu hiyo, lakini wanashindwa kunifuata kutokana muonekano wangu, mimi ni kauzu zaidi ya dagaa.

Ijumaa: Uliwahi kukumbwa na kashfa ya kutoka kimapenzi na Romy Jones, ilikuwaje?

Tuerny: Sijawahi kuwa naye, watu walizusha kwa sababu zao binafsi.

Ijumaa: Mfano Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ sukari ya warembo, akikutokea utakubali?

Tuerny: Hahaa siwezi, kuwa na mwanaume mpaka nimpende siyo tu kwa sababu yeye ni f’lani.

Ijumaa: Ni mwanaume wa aina gani anakidhi vigezo kuingia naye kwenye uhusiano?

Tuerny: (anacheka) awe mrefu, mwenye bodi na anajielewa, yaani asiwe mtu wa kuongea sana, maana sipendi mtu muongo.

Ijumaa: Kuna mastaa ambao wameshawahi kukuomba penzi na ulishawahi kutoka na wangapi?

Tuerny: Wapo wengi wanaoshoboka, huwa nawapotezea na siwezi kuwataja kwa sababu sipendi kujikweza.

Ijumaa: Je, una ndoto ya kuwa msanii wa filamu au muziki au video queen?

Tuerny: Mmh, kuwa video queen hapana labda mtu anilipe si chini ya milioni saba, kuhusu filamu labda niwe dairekta, ila ndoto yangu kubwa ni kuwa mwanamuziki, naamini itatimia ‘soon’.

Ijumaa: Unajishughulisha na nini, kinachoweza kukukwamua kimaisha?

Tuerny: Nina saluni yangu inaitwa T flawless ipo Magomeni-Mikumi ninapoishi, yaani make up studio, napamba maharusi na watu wa kawaida.

Masikini Davido Weee..Skendo Zampa Stress, Alazwa Hospitali..!!!!

$
0
0

MKURUGENZI wa Lebo ya HKN, David Adeleke ‘Davido’ amekimbizwa hospitali na kulazwa huku chanzo kikidaiwa kuwa ni ‘stress’. Tukio hilo limejiri juzikati ambapo inaelezwa kuwa, Davido amekuwa akisumbuliwa na skendo inayozidi kuenea kwa kasi kuhusiana na kuzaa na mwanamke anayefahamika kama Ayomide Labinjo.

Haikuelezwa hasa hospitali ipi amelazwa lakini kupitia Mtandao wa Snaptchat, Davido liweka kipande cha video akiwa ametundukiwa dripu na kuwaambia mashabiki wake wamuombee.

Hivi karibuni, Ayomide alizungumza na Jarida la Punch na kuanika kila kitu kuwa, amezaa na Davido baada ya kulazimishwa wasitumie kinga.

“Kama Davido unanisikiliza ulijue hili kuwa uligoma kutumia kinga,” Ayomide aliliambia Punch. Tayari, Ayomide kwa kushirikiana na mama yake wameshafungua mashtaka yakumtaka Davido ashiriki katika malezi ya mtoto huyo.

Amini Usiamini..Makonda na Mchungaji Gwajima Kupatanishwa!..!!!

$
0
0

Kuna habari zilizoko chini ya viunga vya watawala zinasema watu wa ‘’kitengo’’ wameamua kulifanyia kazi suala la Mchungaji Gwajima, Clouds Media International na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa sababu halitoi afya njema kisiasa.

Kwa kifupi, ‘’kitengo’’ ni neno ambalo kwa kiingereza ni ‘’The ruling class/The Establishment’’. Hawa ni watu ambao moja ya kazi zao ni kutathmini kwa kina hali ya kisiasa, kiuchumi na kiulinzi nchini halafu baadaye hutoa mwelekeo kwa taasisi zinazohusika.

Kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa hatutaweza kumsikia tena Mchungaji Gwajima akimzodoa Makonda katika mahubiri yake kanisani.

Ieleweke kuwa baada ya Uchaguzi Mkuu 2015 kumalizika, watu wa ‘’kitengo’’ walifanya tathmini na kubainisha watu ambayo wataweza kufanikisha mikakati ya kisiasa kwa CCM na kiuchumi kwa serikali katika mikoa ambayo inaonekana ni muhimu sana kisiasa na kiuchumi. Mikoa hiyo muhimu sana ilipelekewa viongozi ambao watafanikisha mikakati hiyo na mojawapo ni Mkoa wa Dar es Salaam.

Kwa wale wanadhani Makonda ataondolewa hivi karibuni katika Mkoa wa Dar es Salaam, nadhani wataendelea kusubiri sana mpaka pale watu wa ‘’kitengo’’ watakapo jiridhisha kuwa kazi waliyomtuma ameshindwa kuifanya au makosa anayofanya ni makubwa kiasi kwamba yanaondoa hata madhumuni makuu ya uwepo wake kama Mkuu wa Mkoa.

Nimalizie kwa kusema, Mkuu wa taasisi ya watu wenye ‘’suti nyeusi’’ ametoa onyo kali kwa vijana wake kwa yaliyotokea Clouds Media International na kwa Nape Nnauye kwa sababu kazi waliyopewa ni kumlinda Mkuu wa Mkoa na sio yeye Mkuu wa Mkoa awape kazi za kufanya nje ya misingi yao ya kazi. Ieleweke kuwa baada ya kufanyika uchunguzi wa kina kiulinzi ilibainika Makonda anatakiwa kuboreshewa ulinzi.

Msishangae sana kwa nini Nape Nnauye ameamua kuwa kimya kuhusiana na kadhia ya kutishiwa bastola. Ameelezwa ukweli wa hali halisi iliyopelekea kitendo hicho kutokea.

Mjumbe hauwawi! Naiwakilisha jinsi ilivyo!

Bombardier Zaingiza Faida ya Bilioni 9 kwa Miezi Minne Toka Zianze Kufanya Kazi Rasmi..!!!

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la ATCL, Lasislaus Matindi amesema wamefanikiwa kukusanya shilingi Bilioni 9 kwa miezi minne tu kwa kutumia ndege hmbili zilizonunuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Kipindi ndege hizo zinanunuliwa baadhi ya watu walikosoa kuwa hazikuwa na tija kwa Taifa.

Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) ilianzishwa mwezi Novemba 2002 baada ya Serikali kubinafsisha lililokuwa Shirika la Ndege la Tanzania (Air Tanzania Corporation, ATC). katika Shirika hilo, Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) lilinunua hisa asilimia 49 ndani ya ATC.

Hata hivyo ubia kati ya ATCL na SAA ulikabiliwa na matatizo ya kiuendeshaji na kulazimika kusitishwa mwezi Agosti 2006 na ATCL kurejeshwa tena serikalini kwa asilimia 100.

Dr Slaa Ajitathimni Kurud Nchini.......Adai Upinzani Usipojipanga Unaweza Kufutika 2020

$
0
0

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye kwa sasa anaishi nje ya nchi, Willbrod Slaa amesema anajitathmini kwa kile kilichomfanya aondoke hapa nchini na familia yake kama hakipo aweze kurejea nyumbani.

Dkt. Slaa aliamua kuweka pembeni masuala ya siasa baada ya kutofautiana na chama chake juu ya masharti ya kumpokea aliyekuwa mgombea wa Urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa.

Amesema kuwa kwa sasa amemaliza masomo yake na baada ya kutafakari na kujitathmini atarejea nyumbani muda wowote.

“Ni kweli nimemaliza masomo yangu, bado napima mazingira yaliyonifanya niondoke na familia yangu, baada ya hapo nitaangalia uwezekano wa kurejea nyumbani,”amesema Dkt. Slaa.

Aidha, kuhusu mwenendo mzima wa Serikali ya awamu ya Tano, amesema kuwa hakuna nchi hata moja ulimwenguni ambayo Rais wake atakubarika kwa asilimia mia moja, hivyo Rais Magufuli ameonyesha msimamo wa kusimamia kile anachokiamini

Hata hivyo, ameongeza kuwa kama wapinzani hawatakuja na ajenda makini na mkakati unaoweza kuwasaidia wananchi hapo walipo, basi upinzani unaweza kufutika mwaka 2020.

“Kama nilivyorejea mara kadhaa, upinzani makini utaingia Ikulu kwa ajenda mbadala. Ajenda makini yenye kuwalenga wananchi moja kwa moja katika kuwatoa kwenye kero zao mbalimbali. 

“Hadi sasa ninachoona ni ‘kurukia’ kauli za JPM, lakini kauli si ajenda na hatupeani maksi kwa kuzungumzia usahihi wa lugha. Wako wanaotazama usahihi wa lugha na mahali pa kutazama usahihi huo. Kimsingi hayo ni masuala ya darasani au kwenye uandishi wa vitabu.

“Aidha kumtuhumu JPM kukiuka Katiba na sheria nayo haina tija. Wote wanaomtuhumu wanajua kuwa wakiambiwa waonyeshe kifungu mahususi alichokiuka yeye mwenyewe katika utendaji wake hawana majibu ya kuridhisha.

“Hivyo mimi sijaona mwenendo wa JPM unaosaidia kuingiza upinzani Ikulu. Isitoshe kama hawatakuja na ajenda makini na mkakati ulioandaliwa unaowatoa wananchi hapa walipo kwenda kwenye raha, upinzani unaweza kufutika kabla ya 2020,”alisema Dk. Slaa.

Lissu Adai Mazingira ya Sasa Yanamfanya MTU wa Kawaida Kujua Siasa

$
0
0

Dar es Salaam. Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu amesema anashukuru mazingira ya sasa yameuamsha umma kujua haki zao.

Lissu pia amesema mazingira magumu kisiasa yaliyowekwa na utawala, yamewafanya wapinzani kupata fursa za kujiimarisha.

Mbunge huyo wa Singida Mashariki alikuwa akizungumza na waandishi wa gazeti hili alipofanya ziara juzi katika ofisi za Mwananchi Communications Limited (MCL) inayozalisha magazeti ya Mwananchi, Mwanaspoti na The Citizen.

“Ni kama tuko njiapanda kwa sababu mahali tulipofika ni ama tusimame kama taifa au mwananchi mmojammoja tupinge hali hii,” alisema Lissu.

Alidai kuwa nchi imekuwa ikiendeshwa kibabe na kutofuata demokrasia, hali aliyosema inawafanya wananchi wasipate haki zao, uhuru wao wa kuzungumza, uhuru wa habari na haki za msingi.

“Si makundi ya kijamii, vyama vya siasa, vya wafanyakazi, vya kijamii, wasanii na hata nyinyi media tusimame kutengeneza harakati za kupambana na giza nene,” alisema Lissu.

Alisema nchi haiwezi kusonga mbele kama hakuna vyombo huru vya habari, kama wanasheria watajificha na kama makundi mengine ya kitaaluma yatakaa kimya.

Lissu alisema kwa sasa vyama vya siasa vimezuiwa kufanya mikutano ya hadhara, lakini hilo halijawafanya wakate tamaa wala kukubaliana na hilo.

“Katika historia ya mapambano, vyama vya siasa, taasisi za dini, vyombo vya habari, vyama vya kiraia. Wasanii kihistoria na si akina Ney wa Mitego wamechangia sana tangu miaka ya 1950 wamechangia kupatikana uhuru.”

“Nyie waandishi wa habari na vyombo vyenu vina nafasi kubwa kama wanasheria tu. Kusipokuwa na independent press (uhuru wa vyombo vya habari) mapambano yanakuwa magumu. Kama wanasheria wanajifungia kwenye chemba zao mapambano yanakuwa magumu hasa kwa wanaoteswa lakini ili iwezekane tunahitaji nguvu ya kila mtu,” alisema mbunge huyo ambaye mara kwa mara amekuwa akikamatwa na jeshi la polisi akidaiwa kutoa kauli za uchochezi.

“Si sahihi kusema kuwa tumekubaliana na hali hii,” alisema Lissu alipoulizwa kama wamekubaliana na uamuzi wa Serikali kupiga marufuku mikutano ya hadhara ya kisiasa.

“Hatujapotea, kama unaona adui amejipanga una-retreat (unarudi nyuma kujipanga). Kwenye vita kuna tactical retreat (kurudi nyuma kimkakati) ili kujipanga upya.

“Tunakabiliana na hali ambayo hatujawahi kukabiliana nayo tangu mwaka 1992. Awali, wapinzani tulidharaulika. Walisema hawana uwezo wa kufanya mikutano, lakini sasa mikutano ya hadhara ni hatari kwa walioko madarakani.”

Alisema kuonyesha kuwa mikutano ya wapinzani sasa inawatisha watawala, mwaka jana jeshi polisi lilifanya mazoezi hadharani likionyesha magari ya deraya na silaha, tofauti na hali ilivyokuwa zamani kuwa kazi ya chombo hicho kubakia kuwa ni kupambania nchi.

Alisema ndio maana waliamua kutotekeleza azma yao ya Ukuta ya kuandamana na kuendesha mikutano nchi nzima.

“Kwa hiyo ilikuwa ni kuamua; twende tukauawe au turudi tukafikirie upya. Ilikuwa ni uamuzi sahihi (wa kutofanya mikutano),” alisema Lissu.

Lissu alisema kuwa walidokezwa na kiongozi mmoja kuwa hali ingekuwa mbaya kama wangetekeleza azma yao ya kuandamana.

Chadema ilitangaza kuwa ingeanzisha maandamano na mikutano ya hadhara nchi nzima kuanzia Agosti 31 mwaka jana kuendesha operesheni waliyoiita Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta).

Tangazo la kampeni hiyo lilifuatiwa na Jeshi la Polisi kuonya dhidi ya mpango huo na baadaye askari wake kuanza mazoezi ya mitaani, wakionyesha silaha mbalimbali za kukabiliana na waandamanaji.

Baadaye Chadema ilisitisha mpango huo ikisema imetoa nafasi kwa viongozi wa dini kuzungumza na Serikali.

“Ukuta haukuishia palepale. Ukitaka kujua tulikuwa sahihi kutofanya maandamano mwaka jana Septemba na ukitaka kujua ni jinsi wapinzani wa (Rais John) Magufuli walivyoongezeka. wameongezeka kwelikweli,” alisema Lissu.

“Leo upinzani umetapakaa kila mahali. Vile vigelegele vimepotea. Hakuna makundi yanayojitokeza na kuunga mkono yanayofanywa na Serikali. Kwa sisi, kutochukua uamuzi mwaka jana leo kila mtu anajua.

“Sasa kuna upinzani ndani ya chama tawala na ndani ya Bunge ni mkubwa zaidi. Pamoja na giza nene tunalokabiliana nalo, lakini kuna weupe mwingi. Upinzani umekuwa more generalized (wa sehemu tofauti). Upinzani unakwenda nje ya vyama vya siasa. Marufuku ya mikutano sasa haina maana tena.”

Aliongeza kuwa hata uamuzi wa kutorusha matangazo ya moja kwa moja ya baadhi ya shughuli za Bunge, haujafanikiwa kuzima upinzani.

“Nilisema mwaka juzi vigelegele havitadumu, ukiangalia kwenye vyombo vya habari hilo linajidhihirisha,” alisema.

Kubadili mbinu

Lissu alisema kuzuiwa kwa mikutano kumekuwa fursa nyingine ya kujiimarisha ambayo hawakuijua awali.

“Chadema ilikuwa chama cha mikutano ya hadhara kwa hiyo vikao vya ndani havikuwa muhimu na hivyo internal structures hazikuwa nzuri,” alisema Lissu.

“Tumebadilisha mapambano na sasa tunafanya mikutano ya ndani. Mikutano ya ndani imekuwa na mahudhurio makubwa. Imetusaidia kuimarisha internal structures.”

Tangu mwaka jana, viongozi wa juu wa Chadema pamoja na wajumbe wa Kamati Kuu wamekuwa wakizunguka kwenye kanda za chama hicho, kufanya mikutano ya ndani na baadaye kusimika viongozi.

Alisema marufuku hiyo ya mikutano ya hadhara haitadumu kwa sababu ya shughuli za kisiasa zinazokuja, kama uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa.

Nguvu ya Lowassa

Lissu pia alizungumzia ujio wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Edward Lowassa akisema uliongeza nguvu muungano wa upinzani katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

“Ukizungumzia uchaguzi tu; umpende au umchukie, umtukane au umshangilie, huyu mtu anapendwa. Kura milioni 6.07?” alisema.

“Ukichanganya kura walizopata wagombea wa upinzani tangu uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi 1995, Lowassa amepata kura nyingi kuliko wote. Ni kiongozi wa kihistoria. Pamoja na uzee wake, Watanzania hawa na matusi yote waliyomtukana bado ana nguvu kiasi hicho. Hali yake si nzuri sana, lakini ana nguvu kiasi hicho.”

Lowassa alikuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Nne, lakini alijiuzulu mwaka 2008 kutokana na kashfa ya mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura na kampuni ya Richmond Development ya Marekani iliyoonekana kutokuwa na uwezo huo.

Akijibu swali kuhusu msimamo wa Chadema wakati wa kashfa hiyo na baada ya Lowassa kuihama CCM, Lissu alisema mbunge huyo wa zamani wa Monduli amebebeshwa mzigo mzito peke yake.

“Mimi ndiye niliyeandika orodha ya mafisadi na tuliisoma kwa kupokezana na (katibu mkuu wa zamani wa Chadema, Dk Willibrod) Slaa pale Mwembeyanga,” alisema.

“Kile tulichokisema kilithibitishwa na kamati ya (Mbunge wa Kyela, Dk Harrison) Mwakyembe. Je, tuliyosema mwaka 2007 ni uongo? Ukisema uongo, maana yake Richmond haikuwepo. Ukisema kweli maana yake Lowassa alishiriki.

“Kamati ya Mwakyembe ilithibitisha kwamba alishiriki. Sasa amebebeshwa mzigo peke yake. Uamuzi ule ulikuwa wa cabinet (wa Baraza la Mawaziri). Cabinet inaongozwa na Rais. Lowassa aliwajibishwa kwa sababu hakuwasimamia wa chini yake.

“Kuna watu kumi na moja walitajwa na Kamati ya Mwakyembe. Walitakiwa wafukuzwe kazi na washtakiwe. Hadi leo hakuna hatua zilizochukuliwa. Kwa hiyo uwajibikaji wa Lowassa ulikuwa wa kisiasa kwa kuwa alikuwa mtendaji mkuu wa Serikali.”

Lissu alisema hata kamati teule ya Bunge iliyochunguza mkataba huo haikumtaja Lowassa kama mhusika wa moja kwa moja katika kufanikisha kusainiwa mkataba wa Richmond.

“Kitu gani kilitokea kwa (Jakaya) Kikwete aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la mawaziri?” alihoji Lissu

Azungumzia fursa ya upinzani

Akizungumzia nafasi ya upinzani katika uchaguzi wa Serikali za mitaa wa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa 2020, Lissu alisema vitendo vinavyofanywa na Serikali vinaimarisha upinzani kila uchao.

“Serikali hii ni fursa kubwa kwa upinzania mwaka 2019 na 2020. Fikiria alivyokuwa fursa kubwa Arusha katika uchaguzi wa TLS. Wanasheria walilala kabisa kwa miaka kumi,” alisema Lissu.

“Si wanasheria walioanzisha harakati za vyama vingi? Si kina (Dk Masumbuko) Lamwai, sio kina Mabere Marando walioanzisha NCCR-Mageuzi? Tulipopata vyama vingi wanasheria walienda kulala, utawala wa sasa umewaamsha .”

Katika uchaguzi wa viongozi wa TLS, Lissu alipata ushindi wa asilimia 84 ya kura na kuwabwaga wapinzani wake watatu.

Alisema utawala wa sasa umesaidia kila mmoja kujua umuhimu wa utawala bora, utawala wa sheria, uhuru wa habari na hata umuhimu wa matangazo ya moja kwa moja ya shughuli za Bunge.

Alisema hata wasanii nao wameanza kujitokeza, akisema baadhi wana lugha inayofanana na Chadema ingawa alisema hawafahamu.

Chadema ni chama cha vijana

Kumekuwepo na madai kuwa CCM imekuwa ikiandaa vijana kuwa viongozi wa baadaye, wakati Chadema iking’ang’ania wazee, lakini Lissu anapingana na dhana hiyo.

“Hilo ni tatizo la CCM inayokumbatia vijana waliozima Bunge (waliosababisha Bunge lisirushwe na vituo vya televisheni), waliowasilisha muswada wa habari. Hayo ndiyo malezi?

Alisema inawezekana asilimia 90 ya waliompigia kura Lowassa katika uchaguzi uliopita ni vijana.  

Tofauti Kati ya Wenye Vibamia na Wenye Mihogo ya Muheza...!!!

$
0
0

Siku hizi miongoni mwa mada zinazotrend kwenye sosho network ni pamoja na ukubwa ya maumbile ya mbo*. Imefikia hatua jambo hili limekuwa biashara kubwa Sana inayowaingizia watu kipato na kuwafanya waendeshe maisha yao.

Zifuatazo ni tofauti Kati ya wenye Vibamia na wenye mihogo ya Muheza;-

1. Play boy
Mapleya boi wengi ni Wenye vibamia ukubali au ukatae. Wenye Vibamia ndio wanaoshika nafasi ya kwanza kwa kuwa na wanawake wengi. Hii ni kutokana na sababu kwamba maumbile yao huwaruhusu kufanya na mwanamke yeyote yule bila kujali umri. Hii ni tofauti na wenye mitambo ambao huambulia wanawake wachache wenye uwezo wa kumiliki na kuvumilia mihogo yao.

Hivyo mwanamke akiwa na mwanaume mwenye hogo la maana ni rahisi kwake kuwa pekee yake tofauti na yule mwenye mshikaji mwenye kibamia ambaye anaweza kutoka hata na mtoto wa miaka kumi.

2. Ulaji wa tigo.
Wenye vibamia ndio wanaoongoza kwa kula tigo. Hii ni kutokana na sababu ile ile ya maumbile yao kuwaruhusu kupenya kwa urahisi bila mshike mshike. Wanawake wengi huzingatia ukubwa wa Mashine kwenye sex. Ukikaa hata na malaya wale wanaojiuza ukiwauliza watakuambia kuwa wenye vibamia ni bora kuliko.

3. Mahanithi na wanaopiga kibao kimoja chali.
Wanaume wenye mihogo wengi wao ni mahanithi. Mashine zao hulegee mapema kutokana na ukubwa hivyo kushindwa kusimama. Kulegea huku husababishwa na sababu nyingi moja wapo ikiwa ukosefu wa nguvu za kiume.
Wenye mihogo pia huweza kumwaga bao moja na hogo kulala moja kwa moja. Hii hutokea kwa wanaume wasiokula chakula kizuri na wasiofanya mazoezi.
Vibamia wao hili tatizo sio Sana.
Tatizo la wanaume wenye mihogo mikubwa huwa serious miaka ya 30+.

4. Kugongewa.
Pamoja na kuwa wanaume wanapenda wawe na maumbile makubwa lakini hii ni tofauti kwa akina dada. Wanawake wengi hupenda maumbile ya Wastani au vinamia kabisa. Wanawake wachache ndio hupenda mihogo.
Wanaume wenye mihogo hugongewa Sana mademu zao na hii ni sababu ya wao kutokuwa na nguvu za kuyafanya maumbile yao kufunction vizuri.

Wanaume wenye vibamia hawana hili tatizo sana. Japo kuna propaganda ya kibiashara ili kuwatisha vibamia.

5. Hofu.
Wanaume wenye vibamia huwa na hofu kipindi cha mwanzoni tuu wakiwa ndio wanaanza mapenzi. Huogopa kuonekana na vichululu vidogo lakini kwa kadiri anavyofanya na wanawake tofauti tofauti ndivyo hofu inavyoisha. Hii ni tofauti na wale wenye mandingo makubwa. Hawa huwa na hofu siku zote ndio maana sio mapleya boy kwani huogopa kukataliwa chumbani.

6. Wanaokimbiwa chumbani.
Wanaume wenye mahogo makubwa ndio huongoza kwa kukimbiwa chumbani. Iwe guest au Ghetto. Hii ni tofauti na wenye vibamia ambao hujilia kwa urahisi hata Kama demu hatarudi huenda kwa kutoridhika lakini ndio keshaliwa hivyo.

7. Kutoa bikra.
Wanaume wenye vibamia ndio wanaoongoza kwa kukata utepe tofauti na wenye Mandingo bikra nyingi hutolewa kwenye early teenage hivyo wenye mandingo hujikuta wakila makombo ya vibamia.

8. Kutoka na majimama.
Majimama wengi au masugar mummy wengi hupenda mandingo makubwa kulingana na maumbile yao. Wenye vibamia hapa hutukanwa kwa hakika na hii ni fursa pekee kwa wenye mihogo ya kutisha.

Ikumbukwe kuwa kibamia hapa kinaanzia nchi 5 kurudi chini na hogo linaanzia 7+.

Hizo ndizo tofauti Kati ya wenye vibamia na wenye mahogo makubwa.

Bado Mienendo Yake Huielewi..Fanya Hivi Itakusaidia..!!!

$
0
0

WAKATI mwingine unaweza kujikuta njiapanda muda wa kutaka kuchukua maamuzi. Kila unachotaka kufanya unahisi kama unahitajika muda zaidi au uvumilivu zaidi. Katika maisha vitu vya namna hiyo huwa vinatokea!
Umeshawahi kuwa na mtu na kujikuta kama humuelewi hivi, halafu ukashindwa kujua ni uamuzi wa aina gani unafaa kuuchukua? Mtu ambaye unajitahidi kwa kila hali kumuonesha namna unavyompenda ila wapi! Anakuchukulia kawaida tu.

Wala haoneshi kuthamini wala kuheshimu upendo na mapenzi unayomuonesha. Ulishawahi kuwa naye? Au ndiyo huyo uliye naye? Hapa suala ni moja tu. Mueleze namna unavyojisikia kwa tabia yake.

Katika kumweleza huku unapaswa kutafuta siku ambayo ni tulivu, kwa maana kila mmoja asiwe na kazi kwa muda huo ili maongezi yenu yapate heshima inayostahili.

Tumia nafasi hiyo kuwasilisha yote ya moyoni unayojihisi juu ya tabia yake. Mwambie katika hali isiyokuwa ya kulaumu wala jazba. Eleza namna yote unavyoteswa na tabia yake isiyoonesha kukupenda wala kuuthamini upendo wako.

Baada ya kuhakikisha tayari anajua namna unavyojisikia, sikiliza atakachokisema. Kuwa makini kupima kauli zake na jinsi sura yake inavyomaanisha. Wengine wanaweza kukupa majibu mazuri huku sura yake ikiwa inaonesha dharau na kejeli. Haina maana!

Pima uzito wa maneno uliyomwambia na majibu atakayokupa. Ukiona vina uwiano na ni majibu mazuri, mpe nafasi nyingine hata kama hiyo ni mara ya pili anakukosea. Kuwa mvumilivu – bila uvumilivu hakuna mapenzi ya kweli. Uvumilivu ni mama wa mafanikio.

Baada ya kuwa tayari umemweleza jaribu kusahau makosa yake na ufungue ukurasa mwingine katika maisha yenu. Hapo haitakiwi tena kukumbushia makosa yaliyopita.

Hiyo itamnyima uhuru wa kufurahi kikamilifu na wewe pia kuna uwezekano mkubwa wa kuchochea migogoro isiyo ya lazima katika mapenzi yenu.

Maana unaweza kumkumbusha hili na yeye akakukumbusha lile. Na kila mmoja hapo akataka kumuona mwenzake ndiyo mkosaji zaidi. Mapenzi hayawezi kuwa mazuri kwa staili hiyo.

Baada ya kuwa mmemaliza tofauti zenu anza kuangalia mabadiliko chanya katika matendo yake. Ni kweli kabadilika? Au kilichobadilika ni staili tu ya kukunyima furaha ila balaa ni lile lile?

Kama alikuwa na skendo za vimada sasa huzisikii ila kila siku safari zisizokuwa na sababu na ukijaribu kuuliza anakwambia “kuna mambo naweka sawa”. Mambo gani? Hakwambii! Akirudi ‘break’ ya kwanza bafuni akaoge kwanza ndiyo arudi muongee.

Ikiwa unamfanyia mpenzi wako kila lililojema katika mahusiano na bado haoneshi kubadilika zaidi ya kukusema “we msemaji sana” au anatoa ahadi tu zisizotekelezeka, kuna jambo la kufanya.

Kaa naye kisha mueleze kwa mara ya mwisho juu ya tabia yake na umueleze hatua unayokwenda kuchukua kama asipobadilika. Mapenzi ni raha na amani. Kama mtu hakupi hayo basi hakufai.

Kwa nini kila siku mahusiano yako yawe ya masimango na majuto yasiyokwisha? Kila siku machozi yatoke kwako tu. Kwani wengine hawana wapenzi? Mbona hawalalami wala kuumizwa?

Unapaswa kujua kitu – anayekupenda atakujali na kukuthamini. Hata siku moja hatapenda kuona unahangaika na kulia kwa sababu yake. Ukiona mtu anaona unaumia na kuteseka kwa ajili yake halafu hana habari na wewe jua kuna namna. Siyo bure.

Kama hakuna ulichomkosea wala kumkera basi jua hana mapenzi na wewe. Iweje akupende halafu asijali chozi lako? Kivipi aseme anakuthamini wakati hajali maumivu yako? Kuwa makini. Kuwa makini zaidi!

Hizi ndizo Sifa za Mwanaume Rijali, Soma Ili Ujue Upo Kundi Gani..!!!

$
0
0

Kila mwanaume anapenda kujiita yeye ni rijali hata kama hana sifa hizo na kama anazo habainishi urijali wake ni wa daraja gani. Kimsingi maelezo yafuatayo yanabainisha aina za marijali na madaraja yao. 

1: Rijali kamili kamili, huyu anauwezo wa kukaa juu ya kifua cha mwanamke na kupampu mfululizo kwa takribani dakika 45 hadi saa moja dakika hizo ni za kusugua K na si vinginevyo, kimsingi hawa ndio wanaofaidi mapenzi.

2: Rijali kamili, mwanaume aliye kwenye kundi hili anakuwa na uwezo kukaa juu ya kifua cha mdada na kusugua K kwa takribani kati ya dakika 21 hadi 44. Huo muda ni wa kazi bila ya kuhesabia muda wa romance .

3: Rijali nusu, huyu anauwezo wa kukaa juu ya kifua cha mdada na kusugua K kwa takribani kati ya dakika 10 hadi 20 ,kimsingi wanaume wengi wapokatika kundi hili.

4: Rijali dhaifu ; huyu ana uwezo wa kukaa juu ya kifua cha mwanamke na kusugua K kwa takribani kuanzia dk 5 hadi 9 na hana uwezo wa kupita muda huo kwani huwai kukojoa .

5: Rijali koko ; hawa mara nyingi wanawai sana kukojoa huweza kukaa juuya kifua na kusugua K kwa takribani kati ya dakika 2 hadi 4 na wanakuwa wameshafika kileleni . Kundi hili ndilo lenye shida zaidi kwani wapenzi 
wao huishi nao kwa kuwavumilia tu.

Kimsingi mwanaume unatakiwa kuhesabu dakika mara tu unapoanza kupampu hii itakusaidia kujua upo kundi gani. Wanaume wengi waliopo kundi la tano, nne na la tatu wanaweza kusaidiwa na wapenzi wao ili kuingia katika kundi super la kwanza na la pili kwa kufanya yafuatayo. 

Moja mwanamke anatakiwa kupiga kelele sana na kwa sauti pale anapoona mwanaume anakaribia kufika kileleni, kelele hizo zitamfanya kidume koko hicho kushtuka hivyo mshtuko huo utamfanya aanze tena upya kusugua vargina.

Lakini njia ya pili ambayo inatumiwa na wengi ni ile ya mwanamke kupanua makalio ya mwanaume pindi anapoona mwanaume anataka kufika kileleni.Kitendo hicho kinasaidia kuruhusu hewa kuingia katikati ya makalio hadi tumboni hivyo kusababisha baridi kwenda kupooza sehemu za ndani hivyo kuzuia mbegu kughairi kutoka, mdada anatakiwa ashike makalio ya mkaka vizuri na kuyapanua kwa nguvu ili hewa iingie kwa wingi. 

Lakini njia ya tatu ni mwanamke kuamua kuruka na kumsukuma mwanaume kwa ghafla kana kwamba ameona kitu cha hatari hivyo mwanaume hatafika kileleni kwa wakati ule. 

Njia ya nne ni mwanamke kuamua kuchomoa uume na kuupekecha pekecha pindi mwanaume anapotaka kufika kileleni, hii njia ni nzuri kwa sababu mwanamke anatakiwa ashike uume kwa mikono.yote miwili na kuupekecha pekecha kwa muda kadhaa na kuuingiza tena hii njia inaweza kumfanya mtu akatoka kutoka kundi la mwisho hadi la pili lakini hawezi kuingia kundi la kwanza. 

Wewe mwenyewe unaweza kujitathmini upo kundi gani na kama wewe ni mdada unaweza kujua mpenzi yupo kundi gani na ungehitaji kumsaidia hadi afike kundi gani kwa kadiri ya uhitaji wako. Je wewe upo kundi gani na unahitaji mpenzi wako atumie mbinu gani ili akubuust na kama ni mwanamke mpenzi wako yupo kundi gani na mbinu unaona inafaa ya kumboost 

Usafi kwa Wanaume: Namna Nzuri ya Kutunza Uume...!!!

$
0
0

Mgegedo ni tafsida nimeitumia kama kiwakilishi cha maumbile ya mwanaume yaani uume. Mgegedo ni eneo muhimu sana kwawanaume ambalo wanalitukuza kuliko kitu chochote hapa duniani, hivyo leo hiinimeona ni vyema kutoa darasa kwa wanaume ili wajue namna nzuri ya kutunza migegedoyao ili iwe misafi na yenye afya kwa ustawa wa mahusiano yao na wenzi wao.

Ni vyema wanaume wakajengautaratibu wa kuweka migegedo yao katika hali ya usafi unaostahili kwa ajili yakujenga mahusiano mazuri na wenzi wao inashauriwa kuosha mgegedo kwamakini kwa kutumia maji ya uvuguvugu kila siku mwanaume anapooga, kama mwanaumeatakuwa hajatahiriwa, basi anatakiwa kuigeuza ile ngozi inayofunika sehemu yambele ya mgegedo wake na kuisafisha kwa makini ili kuondoa ukando kando unaokuwaumeganda ndani unaofanana na jibini ambapo ukando kando huo hufahamikakitaalamu kama smegma.

Huu ukando kando unaopatikanandani ya migegedo ya wanaume wasiotahiriwa ni kilainishi maalum kinachoufanyamgegedo usiwe mkavu,kilainishi hiki ni cha kimaumbile.

Kama kilainishi hiki kikiachwabila kusafishwa kwa muda mrefu kitaanza kutoa harufu mbaya na baadayekitazalisha vijidudu (bacteria) ambavyo vitasababisha mgegedo kuvimba na kuwamwekundu sehemu ya mbele ambapo tatizo hilo hufahamika kitaamu kama balanitis.

Mwanaume asiyetahiriwa asiyesafishamgegedo wake vizuri licha ya kupatamatatizo niliyoyaeleza hapo juu lakini pia huweza kuharibu mahusiano yake namwenzi wake. Hakuna mwanamke ambaye atapenda kujinafasi kwa kulamba koni yamgegedo usio msafi, kwani ni kujitafutia fangasi za kinywa.

Hata hivyo ningependa kuwaonya kina mama kamwe wasijaribu kuigeuza ngozi ya migegedo ya watoto wao wadogo ambao hawajatahiriwa, kwani hiyo inaweza kuwaumiza na kuwasababishia maumivu makali. Kwa kawaida ngozi ya mbele ya migegegdo ya watoto wadogo inakuwaimeshikana na kichwa cha mgegedo hivyo haiwezi kuvutika yote na ukilazimisha unaweza kumjeruhi. Kwa watoto wadogo katika makuzi yao hawahitaji kusafishwa migegedo yao kwa namna hiyo. 

Lakini pia pamoja nakwamba usafi ni muhimu lakini haishauriwi kusafisha migegedo kwa kiwangokilichopitiliza kwa kutumia sabuni ya kipande au ya maji kunaweza kusababisha muwasho na uvimbe kwenye mgegedo hususani kwa wanaume wasiotahiriwa.Kwa kusafisha mgegedo mara mojakwa siku kwa maji ya uvuguvugu inasaidia kuiweka migegedo katika hali ya usafi kiafya. Na kama unataka kutumia sabuni, ni nyema kutumia sabuni zisizo za manukato yaani wengine huita sabuni mbuni au sabuni ya kipande. Kwa kutumia sabuni za manukato unaweza kusababisha muwasho na uvimbe wa ngozi wa mgegedo wako.

Usafi wa eneo la korodani za mgegedo

Kuzungumzia usafi wa mgegedo sikwamba nimesahau kuzungumzia usafi wasehemu ya chini ya mgegedo yaani korodani. Eneo la korodani lisipofanyiwa usafi makini lile jasho na nywele za chini husababisha harufu Fulani yenye kukera. Eeneo la korodani linatakiwa kufanyiwa usafi makini hasa kwa wale wanaovaa nguo za ndani muda wote kwa siku nzima. Ni vyema kuhakikisha eneo lachini la korodani karibu na sehemu ya kutolea haja kubwa inakuwa safi wakatiwote ili isiwe na harufu isiyovutia.

Fahamu Mambo 10 Muhimu Ya Kuufanya Uume Kuwa Na Afya

$
0
0

Uume (Penis) ni kiungo chenye hisia na muhimu katika jinsi ya kiume kutokana na nafasi yake katika mwili.
Wanaume wengi wamekuwa wakitumia kiungo hicho pasipo kuzingatia utunzaji wake nakuifanya sehemu hiyo nyeti kuwa chafu na hata pengine kutoa harufu mbaya kwa kutoifanyia usafi sawasawa hasa baada ya kushiriki tendo la ndoa na kusisahidia haja ndogo.

Leo kati safu hii ya afya nikakufahamisha jinsi 10 muhimu za kutunza uume wako:

Usafi kwa asiyefanyiwa Tohara

Watu wengi usahau hata kushindwa kusafisha ngozi ya juu ya Uume wakati wa kuoga na baada ya tendo la ndoa na hasa wale ambao bado wana Ngozi ya juu ya uume (govi) na kusahau kusafisha eneo la chini yake. Kama una ngozi ya mbele katika uume (govi), unapaswa kuvuta kwa chini kwa upole ngozi hiyo na kufua eneo la chini yake na maji moto. Kama utashindwa kufanya hivyo utasababisha eneo hilo kuwa na harufu mbaya na kusababisha kuzaliana kwa bakteria.

Kunawa mikono

Ni lazima kuwa na tabia ya kusafisha uume wako si tu baada ya kutoka chooni lakini pia kabla. Osha mikono yako wakati wowote kabla ya kugusa uume wako. Hii ni kutokana kushika vitu vingi ambapo kunakuwa na uwezekano mkubwa wa kutunza kemikali. Pia ni muhimu kama umekuwa katika kuwasiliana na watu hivyo uweza kubaki na chembechembe ambazo zinaweza kusababisha muwasho kwa kushika pilipili hivyo utajikuna na kusababisha michubuko katika uume.

Uchunguzi wa Mara kwa Mara

Si tu kama wanawake wenyewe ndio wanashauriwa kujitegemea kwa kufanyiwa uchunguzi wa saratani ya matiti na kizazi, Lakini pia wanaume wanapaswa kuwa na utaratibu wa kuangalia sehemu zao za siri kama wana uvimbe wowote na pia kwa ishara ya magonjwa ya zinaa. Kuchunguza pia shahawa yako kutambua mabadiliko yoyote katika muonekano au uwepo wa damu katika uume.

Epuka Majeraha

Uume wako unahitaji ulinzi, upendo na huduma kutoka kwako sambamba na kuepuka hali ambazo zinaweza kusababisha majeraha katika uume. Hii inaweza kutokea kwenye ngono isiyo salama au punyeto bila kurainisha ngozi. Pia kuhakikisha unaepuka kuvaa nguo ya ndani (chupi) ambayo haibani sana. Ni vyema ukapata muda wa kukaa bila nguo ya ndani (chupi) ili kuweka wazi uume na kuepusha msuguano utakaoweza kuleta madhara.

Kuwa na mwanamke mmoja

Kuwa na mpenzi zaidi ya mmoja uua uwezo wako kingono lakini pia kuwa na mwanamke mmoja kutakusaidia kuwa mwenye tabia njema na kuwa na nguvu na uwezo mzuri wakati wa kufanya tendo la ndoa na hasa kabisa kujikinga na magonjwa ya zinaa.

Kupata muda wa Mapumziko

Hii ni nzuri kwa afya yako kwa ujumla lakini nzuri hasa kwa uume wako kuwa na afya. Kila wakati kila unapokuwa umepumzika kwa usingizi mzito, uume wako utakuwa na uimara kutokana na kuupumzisha. Hii ni muhimu kwa sababu husaidia kurejesha sura yake na pia kuongeza muda wa utendaji kazi wa damu yenye oksijeni.

Kunywa maji

Kuwa na tabia ya kunywa angalau glasi nane za maji safi. Maji huvuta sumu nje ya mwili wako na kuruhusu damu kufanya kazi na kuongeza kukusisimua wakati wa tendo la ndoa.
Uchaguzi wa sabuni ya Kuogea na mafuta

Ni vizuri na muhimu kufanya usafi wa sehemu za uzazi. Na hata hivyo haipaswi kwenda kuosha na kuskrabu sehemu za siri kwani ngozi ya uume ni raini na nyeti. Matumizi ya sabuni ambazo uondoa vidonda si nzuri kwa kutumia katika uume na kwa kutumia kama njia ya kurainisha uume wakati wa tendo la ndoa lakini pia ni kivutio cha maambukizi. Vizuri kuosha mara mbili kwa siku na maji ya joto kwa kutumia sabuni za kawaida.

Kwa nini unapaswa kunyoa

Mwanaume unaweza kutoona umuhimu wa kunyoa kama ilivyo kwa mwanamke lakini ukweli ni kwamba hata wewe unapaswa kunyoa na kutumia nyia nyepesi za kunyoa ili kuweka eneo lako la uzazi laini na safi. hivyo kama kunyoa mwenyewe kutakuwa na kisingizio mnaweza kufanya hivyo pamoja kama wanandoa hivyo mwenza wako akakuweka katika hali ya usafi.

Tanzania na Ethiopia zasaini mikataba 3.

$
0
0

IKULU, DAR: Tanzania na Ethiopia zasaini mikataba 3. Rais Magufuli na Waziri Mkuu wa taifa hilo wakubaliana kushirikiana katika Ulinzi, Riadha, Mafunzo ya Kiswahili na Bandari.

Kiongozi huyo wa Ethipia ameahidi na kufungua Ubalozi wa Ethiopia hapa Tanzania.
Aidha rais Magufuli ameahidi kutoa eneo la bure kwaajili ya kujengwa kwa ofisi za ubalozi huo.

Kimenuka: Babu Tale Amchana Erick Shigongo..Adai Magazeti yake Yamefulia na Sasa Anataka Kumwaribia Diamond

$
0
0

Baada ya Eric Shigongo kuandika barua ndefu ya kumuonya Diamond kuhusiana na jinsi anavyowawekea ngumu waandaji wa show za ndani kwa kuwatoza bei zile zile kama anavyowatoza wa nje ya nchi na kuhusisha uongozi wa WCB kuwa ni sehemu ya tatizo hilo, Babutale amejibu.


Tale amefunguka mengi huku akimshutumu Shigongo kuwa na hila ya kuharibu biashara zake kupitia magazeti ya Global Publishers.


Kupitia Instagram, Tale ameandika:


Umejitahidi kujaribu kubomoa biashara yangu kenye magazeti yako kwa kila aina ya uchafu kuwazushia na kuwaandika wasanii wangu tumekaa kimya…baada kufeli kuwabomoa wasanii wangu na kuona magazeti yako sasa hayauzi, watu wapo instagram Naona unajitahidi kujaribu kubomoa biashara yangu kupitia instagram yako… siku zote nimekuheshimu na Sijawai kuku vunjia heshima hata kwa kuteleza, ila unapoelekea Sina budi ya kukupa unacholazimisha kukipata…ili kesho ukawaambie vizuri waandishi wa magazeti yako wanitungie kashfa, uongo na kunitukana kama mnavyofanya kwa wasanii wangu, wasanii wwengine na watu mbalimbali…. tafadhali heshimu biashara yangu kama inavyokuheshimu…


Umekazana wiki nzima kuandika vitu vya uongo juu ya Diamond… ila sie tume kaa kimya… na kujifanya unazunga eti unatushauri… kweli mtu unasema unampenda unamshauria instagram, ama unamwita ofisi au nyumbani kumshauri?….. Mbona sie hatujawai kuingilia biashara yako wala kukupangia bei juu ya kuuza bidhaa yako yoyote labda kusema gazeti uuze kwa shilingi mia au hamsini? …na kuonesha hatukuwa na tatizo kabisa na wewe, juzi tu tumetoka kuongea na wewe kufanya show ya @Harmonize_tz DARLIVE na tukakubaliana asilimia, na hadi kupost tumepost… ila baada ya kuona watu wameipokea kwa ukubwa teaser ya show umetubadilikia na kutaka asilimia kuuuubwa wewe, eti sisi tuchukue asilimia ndogo kabisa….tukaona tukae tu kimya, na hatujakulalamikia wala kukuandika popote kiubaya juu ya kutaka asilimia kubwa…hivi kweli hata kama kuweka wasanii karibu na amshabiki zao hii ndio kuwaeka karibu wasanii na mashabiki zao kama usemavyo ama kuwaibia wananchi wanaodunduliza kuwasapoti wasanii wao na wewe kujifaidisha kwa kuendelea kuwanyonya wasanii na kutajirika wewe….mwisho wa siku wasanii waishie kuambulia jina, na kula Madawa….yote kutafuta sababu Msanii akikataa ama kudai aongezewe mapato Ukawaamuru watu wako wakamtungie kashfa na skendo za uongo na kweli ili kum’bomoa msanii kupitia magazeti yako…..tafadhali heshimu heshima yetu kwako👍…… “Mh Magufuli tafadhali Ulipo Kaza legeza, ona Wakubwa wanaanza kutaka kupora hadi watoto vidogo vyao…..😓”

Mbunge Lijualikali: Niliteswa na kupigwa sana na askari Magereza

$
0
0

PETER Lijualikali, Mbunge wa Kilombero, (Chadema) amesema akiwa mfugwa kwa yake kwa siku 79 katika gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam, aliteswa na kunyimwa haki zake, anaandika Pendo Omary.


Baada ya kutoka gereza la Ukonga amesema “kuishi gerezani unapaswa kuwa mvumilivu na mwenye busara. Kuna mateso ya kikatili ambayo ambayo wafugwa wanafanyiwa. Kuna wakati niliumwa maralia, daktari akashauri nipumzike. Lakini nilifanyishwa kazi ngumu na kuhatarisha afya yangu.”


“Askari Magereza saikolojia yao bado ipo kikoloni. Nimeshuhudia mtu anapigwa hadi anatambaa. Kuna harassment ambazo nilikuwa nafanyiwa. Nilipigwa sana.


“Gerazani kuna madaraja matatu, daraja la kwanza, la kati na la tatu. Kwa nafasi yangu ya ubunge nilipaswa kuwekwa daraja la kwanza. Ningekufa taifa lingepata hasara kubwa. Lingepoteza zaidi ya bilioni tano kurudia uchaguzi.


“Wakati haya yanafanywa kwa wafugwa wa kawaida, wezi wa meno ya tembo wakiwemo raia wa China wenyewe wanapewa huduma maalum ambazo ni nzuri, tena daraja la kwanza,” amesema Lijualikali.


Lijualikali amesema: “Uhusiano wangu na jeshi kama taasisi ulikuwa mbovu. Lakini uhusiano wangu na askari (mtu mmoja mmoja) haukuwa mbaya sana. Wengine walikuwa wananiambia walitumwa kunifanyia mateso na viongozi wao.”

Kenya: Mgombea Aahidi Kuboresha Biashara ya Ukahaba Akishinda..!!!

$
0
0

Mgombea Ugavana wa Jimbo la Kisumu amewaahidi wapiga kuwa kuwa ataweka mazingira rafiki kwa wanaofanya biashara ya kuuza miili yao (makahaba) na kuhakikisha wanapata faida endapo watamchagua katika uchaguzi mkuu ujao.

Dkt. Hezron Mc’Obewa, ambaye anarusha karata yake ya ugavana katika jimbo hilo kumng’oa kiongozi aliyepo sasa, Jack Ranguma aliyasema hayo siku ya Jumanne alipokuatana na makahaba zaidi 300 katika Taasisi ya Goan.

Dkt. Mc’Obewa alisema kuwa atashinikiza mikutano ya kimataifa iwe inafanyikia pia Kisumu ili makahaba hao waweze kupata soko.

“Watu hawa hulipa vizuri wanapokwenda nchi za ugenini, na wafanyabiashara hao hupata hadi Ksh 200,000 kwa usiku mmoja” alisema mgombea huyo. “Mikutano hii mikubwa ndiyo huleta wateja watakaowalipa ninyi kwa viwango vywa kimataifa” aliongeza.

Mbali na ahadi hiyo iliyozua gumzo maeneo mengi, mgombea huyo amewaahidi kuwa atahakikisha kunakuwapo ajira za kutosha ili watu wawe na fedha kwenye mifuko yako.

“Biashara yenu ninyi itakuwa na faida kama wanaume watakuwa na fedha mfukoni, na hii ndio sababu lazima tuhakikishe tunamaliza ukosefu wa ajira” alisema Dkt. Mc’Obewa.

Mgombea huyo alisema kiongozi wa sasa wa jimbo hilo hawajali kabisa makahaba hao ambao chini ya mwamvuli wa Kisumu Sex Workers Sacco. Hivyo amewasihi kumchagua yeye ili waweze kufurahia biashara yao na atahakikisha anaimarisha ulinzi dhidi yao.

“Wakati mwingine unapata mteja ambaye anakupakiza kwenye gari lake, lakini usalama wako unakuwa ni mdogo, au unafayia kazi katika mazingira machafu ambayo yanahatarisha afya yako. Haya yote ndiyo tunataka yabadilike”, alisema.

Aidha, mgombea huyo aliwataka makahaba hao kujisajili katika Shirika la Taifa la Bima ya Afya (NHIF) ili kuweza kupata huduma za kitabibu.

Kudadeki..Waakenya Nao Waanza Kuisoma Namba,Serikali ya Uhuru Kenyatta Yasitisha Ajira na Kubana Matumizi..!!!

$
0
0

Bajeti ya Kenya ya mwaka 2017/2018, imesomwa jana kinyume na inavyosomwa kawaida mwezi Juni, kutokana na uchaguzi mkuu utakaofanyika Agosti mwaka huu, huku ikitangaza kusimamisha ajira katika sekta ya umma.

Katika bajeti hiyo ya shilingi za Kenya trilioni 2.6 (Takriban shilingi trilioni 52 za Tanzania) Waziri wa Fedha, wa nchi hiyo, Henry Rotich ameondoa kodi kwenye mahindi yanayoagizwa kutoka nje kwa kipindi cha miezi minne ijayo,

Aidha kodi imeondolewa kwenye dawa za kuulia wadudu za nchini humo pamoja na magari ya utalii yanayoundwa nchini Kenya.

Katika bajeti hiyo ambayo ni ya mwisho kwa serikali ya Jubilee katika muhula wake wa kwanza, serikali imeongeza kodi kwenye kamari hadi 50% kutoka 7.5% ya awali kama njia ya kukomesha uchezaji kamari.

Serikali pia imetangaza kusimamisha ajira katika sekta za umma isipokuwa sekta ya elimu kama njia ya kupunguza matumizi.

Jumla ya Shilingi bilioni 524.6 za kenya katika bajeti hiyo zitatokana na mikopo kutoka nje na ndani ya nchi.

Shilingi bilioni 2 za Kenya  zimetengwa kuwaajiri walimu, na zingine bilioni 4 kuwalipia mtihani wanafunzi wa darasa la nane na kidato cha nnemwaka 2017 na 2018 huku serikali za kaunti zikipata jumla la shilingi bilioni 329.

Ili kuhakikisha kuwa vijana wana ajira, serikali imetenga shilingi milioni 450 Ksh kwa kuboresha kiwanda cha Rivatex, na zingine milioni 250 kuboresha kiwanda cha maziwa cha New KCC.

Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images