Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104807 articles
Browse latest View live

Chukua Hii..Wataalam Watoa Toleo la Tv Inayoua na Kufukuza Mbu..!!!

$
0
0

Kampuni ya Korea Kusini ya LG Electronics Inc imekuja na toleo jipya la TV yenye kioo chembamba aina LED ambayo inaweza kufukuza mbu pale inapowashwa.

LG wametumia teknolojia kuondoa kero ya mdudu mbu kwa watazamaji wanaotumia kifaa hicho, ambayo itakuwa ikitoa mawimbi ya sauti (ultrasonic wave) kupitia spika zake na kama mtumiaji atachagua kufukuza mbu, spika hizo zitatoa mawimbi ya sauti (sio sauti kubwa ni mawimbi ya sauti yenye frequency kubwa) yatakayofukuza mbu.

Kwa lugha ya kitaalam, spika hizo zitatoa mawimbi kwenye frequency ya zaidi ya ukubwa wa 30kHz, mawimbi ambayo binadamu hawezi kuyasikia na yasiyo na madhara kwa binadamu.

Kumbuka kuwa binadamu anaweza kusikia sauti yenye mawimbi kati ya 20Hz hadi 20kHz. Hivyo mawimbi ya 30KHz yatakuwa kwa ajili ya kuwatimua mbu pekee.

Hivyo kutakuwa na njia nyingine ya spika itakayotoa mawimbi yenye usikivu kwa binadamu.

Toka Kwenye Vifungo Hivi,..Utengeneze Zaidi Mafanikio...!!!

$
0
0

Vipo vifungo vingi ambavyo vinaweza kukufunga na kukupotezea mafanikio yako. Vifungo vingine unavijua na vingine unaweza ukawa huvijui. Kwa mfano;-

Acha kujiweka kwenye vifungo vya kidini na kuamini utajiri mkubwa ni dhambi. Kumbuka, mafanikio hayana uhusiano moja kwa moja na kutenda mabaya.

Acha kuamini umaskini ndio ni kitu kizuri kwako. Hivyo ukashindwa kuweka juhudi zako zote kwa kisingizio cha kwamba ukiwa maskini ni sawa kwako.

Acha kuamini ukiwa na pesa nyingi ndio ushetani. Utajikwamisha sana wewe mwenyewe kufikia mafanikio yako bila kujijua ukiwa upo kwenye kifungo cha dini.

Acha kuamini kwamba Mungu atakusaidia kila kitu, hata kama umebweteka na wala hujitumi sana yaani huweki juhudi sana, ndio maana amekupa akili ufikirie na vingine.

Acha kutumia uvivu wako kutumia kama kisingizo ukiamini hio ndiyo imani sahihi.. Kama kuna kazi unayotakiwa kufanya, fanya kweli. acha kuendekeza uvivu unaomba kazi kwenye kampuni moja halafu unamlaumu Mungu. Ukiona uko hivyo ujue kabisa upo kwenye kifungo..

Toka kwenye kila aina ya vifungo ambavyo unaona vinakukwamisha kufanikiwa sana kwenye maisha yako, kuwa huru ili utengeneze mafanikio yako.

Yanga wa Kimataifa Wafanya Kweli na Kuiondoa Simba Kileleni

$
0
0

YANGA SC imerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Azam FC jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Sifa nyingi kwa mfungaji wa bao hilo, Mzambia Obrey Chirwa dakika ya 70 baada ya kumtoka beki wa Azam FC, Mghana Yakubu Mohamed kufuatia pasi ndefu ya kiungo Mnyarwanda, Haruna Niyonzima.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa wa kike mwenye beji ya FIFA, Deonesya Rukyaa wa Kagera, Yanga ilipata pigo dakika ya 30 baada ya kiungo wake Mzambia, Justin Zulu kuumia mguu wa kushoto na kushindwa kuendelea na mchezo nafasi yake kuchukuliwa na winga, Emmanuel Martin.

Zulu aliwekewa mguu na kiungo wa Azam FC, Himid Mao wakati anapiga shuti kuunga mpira uliorudi baada ya kuokolewa kufuatia krosi ya kiungo Haruna Niyonzima kutoka Rwanda.
Martin alikwenda kucheza wingi ya kulia na Niyonzima akahamia katikati kuchukua nafasi ya Zulu aliyekuwa akicheza kama kiungo mchezeshaji.

Mabadiliko hayo ambayo hayakuwa mipango ya mwalimu, yaligeuka msaada mkubwa kwa timu hiyo, kwani Niyozima alikwenda kucheza vizuri sehemu ya katikati ya Uwanja na Yanga ikaanza kushambulia.

Azam nao wakapata pigo dakika ya 43 baada ya mshambuliaji wake, Yahya Mohammed kuumia msuli baada ya kupiga shuti na kushindwa kuendelea nafasi yake ikichukuliwa na Mghana mwenzake, Samuel Afful.

Kipindi cha pili, timu zote zilirudi vizuri na zikaendelea kushambuliana kwa zamu, ingawa baada ya Yanga kupata bao dakika ya 70, wakaanza kucheza kwa kupoteza muda.

Ushindi huo unaifanya Yanga sasa ifikishe pointi 56 baada ya kucheza mechi 25 na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu ikiwaangushia nafasi ya pili mahasimu wao, Simba SC ambao kesho watacheza mechi ya 25 pia dhidi ya Kagera Sugar mjini Bukoba.

Kikosi cha Yanga kilikuwa; Deo Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Mwinyi Mngwali, Vincent Bossou, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Said Juma ‘Makapu’, Simon Msuva/Juma Mahadhi dk90+2, Justin Zulu/Emmanuel Martin dk30, Obrey Chirwa, Deus Kaseke/Geoffrey Mwashiuya dk54 na Haruna Niyonzima.

Azam; Aishi Manula, Erasto Nyoni, Gardiel Michael, Daniel Amoah, Yakubu Mohammed, Himid Mao, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Frank Domayo, Yahya Mohmmed/Samuel Afful dk44, Shaaban Iddi/Bruce Kangwa dk75 na Ramadhani Singano ‘Messi’/Joseph Mahundi dk69.

Hataree..Mzee Mwinyi Afunguka Mazito Kuhusu Tanzania ya Magufuli..!!!

$
0
0

RAIS mstaafu wa Awamu ya Pili, Ally Hassan Mwinyi amemuomba kiongozi wa dini ya Wahindu ya Swaminarayan Duniani, Mahant Swami Maharaji kuiombea Tanzania amani na umoja viweze kudumu na kusiwepo aina yoyote ya ubaguzi kwa sasa na hata vizazi vijavyo.

Mwinyi aliyasema hayo Dar es Salaam baada ya kualikwa katika hafla ya kumkaribisha kiongozi huyo hapa nchini na kukutana na waumini wa dini hiyo.

Pia ilikua ni maadhimisho ya miaka 40 tangu kujengwa misikiti miwili ya dini hiyo hapa nchini.

Alishukuru kwa kualikwa katika hafla hiyo ya kidini kwani sio jambo la kawaida kupokea ugeni wa kiongozi wa kidini nchini.

“Sina shaka kuwa sio nchi zote wenye kuwa na uwezo wa kumuona kiongozi mwenye nafasi kubwa kama hiyo katika nchi zote,” alisema na kuongeza kuwa kama Watanzania wengine amekuwa mwenye bahati.

Alimkaribisha kiongozi huyo nchini na kumtaka kuiombea sana Tanzania ili iendelee kudumisha amani na umoja na licha ya kutokuwepo kwa aina yoyote ya ubaguzi, aendelee kuomba ili hali hiyo isiwepo kamwe na wananchi waendelee kuishi kama ndugu.

Kwa upande wake, kiongozi huyo ambaye ni wa sita kwa nafasi hiyo, Maharaji alisema ataendelea kuiombea Tanzania na dunia nzima kwa ujumla ili wananchi wake waendelee kubarikiwa katika maisha yao pamoja na kukuza maendeleo yao.

Alisema mwanadamu siku zote hupenda raha lakini ni vyema wakafahamu kuwa hakuna raha kubwa kama kupata kutoka kwa Mungu kwa kuwa raha nyingine zote ni za muda, hazidumu.

“ Starehe ya mwanadamu ni ya muda mfupi na raha ya kuishi anayeitoa ni Mungu na ambayo haidumu, hivyo siku zote yapasa kuomba sana kwa Mungu kupata raha ya kudumu,” alisema na kusisitiza wajibu wa kila mwanadamu kuomba amani siku zote na kila wakati na kuishi kwa kanuni za Mungu.

Katuni 11 Bora Leo:SIASA, MICHEZONA ELIMU

$
0
0

Nimekuwekea Katuni 11 Bora kabisa week hii, Bonyeza HAPA kuzitazama

Mkanganyiko Baada ya Roho Kuachana na Mwili,Roho Huenda Wapi

$
0
0

Haya mambo bado yanachanganya wengi kwamba roho inaenda wapi baada ya kuachana na mwili
1.Je inaenda kuzimu?
2.Je inaenda peponi? 
3.Je inazaliwa upya?
4.Je inawayawaya na kutangatanga huku na kule?

Maswali yote hapo juu yana majibu yanayofanana, kuwa roho zipo na zinakuwa kote huko kulikotajwa kutegemeana na kwenye uhai wake kidunia zilibeba/ zilifanya nini? Hebu twende moja baada ya jingine.

Kwanza, dini zote zinahimiza matendo mema na maisha baada ya kifo; hata wapagani pia. Hivyo basi, japokuwa maelezo yanatofautiana, lakini msingi unabaki kuwa ule ule wa roho kuwa sehemu husika.

1.Je, roho inaenda kuzimu? Jibu ni ndio

Kwamba bila kujali unaamini nini lakini jehanam iko hapahapa duniani , roho iliyotenda mabaya duniani baada ya kutoka katika mwili uharibikao huingia kwenye mwili mwingine uliojaa mateso tabu na mahangaiko mengi! Kumbuka ili roho iweze kubeba hisia za mateso na maumivu lazima zipate jumba/ mwili!! Hiyo ni jehanam au kuzimu.

2.Je, roho huenda peponi? Jibu ni ndio

Pepo iko hapahapa duniani, roho iliyoishi kwa kutenda mema hubaki mahali kwenye dunia hii ikiwa iko live lakini domant ikiwa haihisi wala kufanya chochote na kama ikibidi kupata mwili huingia kwenye mwili ambao haujui shida za dunia hii kila kitu kwake ni mteremko tu mpaka mwili husika unapochoka na kuharibika/ kufa!! Hii ni peponi.

3.Je, roho inazaliwa upya? Jibu ni ndio japo kimsingi sio kuzaliwa upya bali ni kupata makao/ makazi mapya hapa ndio penye dhana nzima ya reincarnation, ambapo sasa hutegemea matendo ya nyuma Kwahiyo yaweza kuwa kwenye mwili mzuri au mbaya refer pepo na kuzimu.

4.Je, roho zinatangatanga? Jibu ni ndio
kwanza roho huwa hazifi bali kuna wakati hukosa makao mapya/mwili baada ya zamani kwisha na kuharibika 
Haijulikani hasa nini hutokea lakini hizi ni roho zenye matatizo makubwa na ndio hizi huwa mashetani majini vinyamkera na viumbe vya ajabu ajabu. Ni roho hizi hizi ambazo huweza kuingia kwenye familia kikundi au mkusanyiko wowote na kuleta mirafaruku mikubwa tu ambayo mingine huleta maafa makubwa. 

Kwahiyo roho zipo na zipo sana na kamwe hazifi wala hazipotei jehanam, na pepo zao zipo hapahapa duniani na kwenye kila nyanja ya maisha yetu 

Penzi la Mwanamuziki Vanessa Mdee na Jux Chali...

$
0
0

Habari zilizotufikia hivi punde ni kuwa Vanessa Mdee ameweka wazi kuwa mapenzi yake na Jux yameisha, sababu ya Vanessa kusema hayo ni kuwa Jux amekuwa na wanawake wengi,

Nini maoni yako?

Kumekucha...! Bifu la Watangazi wa Shilawadu na RC Makonda Lafikia Patamu na Limenoga Sasa..!!!

$
0
0

Wakiwa katika Kipindi chao ambacho kilikuwa mubashara kabisa Mtangazaji muongozaji wa Kipindi pendwa na Watanzania wengi hadi Mheshimiwa Rais wetu JPM aitwae Soud Brown amekuwa kila mara akifumba Fumbo huku akicheka mno na mwenzake Kwissa.

Ukiwaangalia zaidi utagundua kuwa kwa yale yaliyowatokea wiki mbili zilizopita utagundua kuwa Kipindi chao Kizima cha leo ni kama vile na wao wameamua kulipiza Kisasi kwa waliyofanyiwa na ' Mvamizi ' Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Paul Christian Makonda.

Mtangazaji Soud Brown amekuwa kila mara akifumba fumbo moja hilo hilo huku akilinogesha na Kiitikio na Mistari iliyopo katika Wimbo maarufu wa Ney wa Mitego wa WAPO huku kila mara akimuuliza mwenzie kuwa ' Je mlango wetu umefungwa? '.

Fumbo lenyewe la Mtangazaji Soud Brown ambalo si Siri kuwa amelielekeza ' makusudically ' kabisa kwa ' adui ' yao na ' mvamizi ' wao Makonda ni kama lifuatalo nalinukuu " Hata wanaovua Viatu na Soksi zao zinanuka Wapo........unasema Wapo.......hata wanaonuka Midomo pia Wapo......unasema Wapo.....Oya Kwissa umefunga mlango lakini?...... Jamani hata wanaonuka miguu wakivua Viatu vyao Wapo.......unasema Wapo......hata wanaonuka Midomo sana Wapo......unasema Wapo......Kaka angalia umefunga lakini mlango? Walinzi wapo gado?

Sasa Kazi imeanza na naomba mlio karibu na hawa Watangazi akina Soud Brown na Kwissa mtusaidie kutuulizia kutoka Kwao kuwa huyo anayenuka Soksi na Miguu akivua Viatu ni nani? Halafu na huyo anayenuka mdomo pia ni nani?

Chokoza wote lakini kamwe usichokoze na kuanzisha vita na Waandishi wa Habari kwani wana mbinu nyingi za kukuchafua, kukumaliza na ikibidi hata kukudhalilisha. Pole sana ' mvamizi ' Mkuu wa Clouds nadhani sasa Vita baina yako na wao ndiyo imeanza na imefika patamu mno.

Kuna Watu wanajua mno kulipiza Visasi hasa kwa waliyofanyiwa au mateso ya kimanyanyaso waliyopata.


Fahamu Tabia za Wanawake Wanaopenda Sana Pesa

$
0
0

1. Huwa na tamaa ya mambo yasiyo ya lazima.
Wanawake wengi wapendao pesa huwa na tamaa ya mambo yasiyo ya lazima, mambo ambayo hayagusi maisha moja kwa moja. Hata nilipokuwa chuo wanawake wengi waliokuwa wanapenda pesa Sana walikuwa na tamaa za kusikitisha ambazo zilipofusha fahamu zao.

Unakuta mwanamke anaomba laki tano kwaajili tuu ya kununua Simu nyingine kubwa wakati akiwa bado na simu mpya.

Katika maisha ni bora uingie jehanam kuliko kukutana na mwanamke mpenda pesa kwani utateseka Sana kwa ajili yake na bado hata ona msaada wako.

Sio rahisi kujenga familia bora na mwanamke mpenda pesa.

2. Wengi hutoka familia masikini.
Wanawake wengi Kama sio wote ambao hupenda pesa kuliko utu wao hutoka familia kame Sana. Ukame wa kiuchumi mpaka kiakili. Wengi wao huweza kutoa hata rushwa ya ngono ili tuu wapate pesa wasijue miili yao inathamani zaidi ya zile karatasi.

Mtu ni masikini unandoto za kuwa na mwanaume mwenye pesa nani alikuambia wenye pesa wanataka masikini.

Umasikini wako usikufanye ujidharau au mtu akudharau. Lipo kundi dogo la wanawake wanaojitahidi kutetea thamani ya jinsia yao lakini wengi wao ni wakuonewa huruma tuu.

3. Wengi wao hawana elimu ya kutosha.
Mwanamke aliesoma akaelimika hawezi hangaika na pesa ya mtu. Ndio maana wanawake wachache huhangaika kwajili ya kujitegemea na sio kumtegemea mwanaume.

Wanawake wengi wenye elimu na vipato vizuri huwezi msikie akiongelea pesa Kama kigezo muhimu kwa mwanaume anayemuhitaji awe mume wake.

4. Ni wavivu na wasio na mawazo.
Wanawake wote wanaopenda pesa ni wavivu kupita kiasi. Uvivu wao umeanzia akilini kiasi kwamba hawana mawazo ya maendelo. Utakuta mwanamke anawaza mambo mepesi kabisa Kama urembo, nguo, mtoko, n.k.

Wanawake wapenda pesa ni hatari kwa ustawi wa familia.
Huwezi kuwa na familia kubwa ukiingia katika bahari ya viumbe hawa.

5. Hawana shukrani wala uvumilivu.
Wanawake wapenda pesa huwezi msikia akikushukuru zaidi ya kujichekesha tuu na kubinua makalio.

Kwa mfano amekuomba milioni moja then ukampa laki tano basi utamsikia akisema sasa hii nitafanyia nini, au niongezee tena mume wangu huku akikushika kifua au ndevu.

Wanawake wenye hekima hushukuru mpaka mwanaume anasikia aibu.

Suala la uvumilivu halipo kwa hawa wanawake. Shida ikitokea ukishindwa kuitatua kwa wakati huo basi hesabu umeliwa. Yaani kwao kukusaliti ni jambo lisilo na mashaka.

Kimenukaa Cuf..Maalim Seif Ampasua Prof Lipumba..Atoa Kauli Hii Nzito kwa Hasira ..!!!

$
0
0

VITA vya maneno vimezidi kushika kasi ndani ya Chama cha Wananchi (CUF) na sasa Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad, ameibuka na kumtaka aliyekuwa mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba, amwache kwa kuwa hana uwezo wa kumfukuza kazi.

Kadhalika, amesema kama kweli Profesa Lipumba anadhani yeye ni mwenyekiti halali, afike makao makuu ya CUF kisiwani Unguja ili kufanya kazi badala ya kukubali aendelee kutumika.

Hivi karibuni Profesa Lipumba alitangaza kumfukuza kazi, Maalim Seif na kumteua Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Tanzania bara, Magdalena Sakaya, kuwa kaimu Katibu Mkuu.

Akizungumza na wananchi na wanachama wa chama hicho katika kisiwa kidogo cha Tumbatu Mvuvini, Maalim Seif alisema anamshangaa Profesa Lipumba kwa madai kwamba yeye ameshindwa kazi kwa kuwa haendi kazini katika ofisi za chama zilikozo Buguruni, Dar es Salaam.

"Eti nimeshindwa kazi akidai kuwa siendi ofisi kuu ya CUF Buguruni. Mbona yeye haji makao makuu ya CUF Mtendeni. Lipumba hana mamlaka ya kuniondoa nafasi yangu ya ukatibu mkuu,” alisema.

Alisema tangu Agosti, 2015, Lipumba hajawahi kukanyaga makao makuu ya CUF Mtendeni na kwamba hata kama angekuwa Mwenyekiti halali wa chama, alipaswa kumwita na kumhoji kwa nini haendi ofisi kuu za chama Buguruni kuliko kuchukua madaraka ya kutangaza kuwa amemtimua.

Maalim Seif pia alikemea siasa za chuki na uhasama zilizotawala kisiwani humo kati ya CCM na CUF na kusema zimesababisha mapigano na hujuma ikiwamo kuchomeana nyumba kutokana na itikadi za vyama.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui, alisema Profesa Lipumba ametumika na amefanya kazi kubwa ya kukihujumu chama huku akiungwa mkono na baadhi ya wanachama.

Mazrui pia alimwomba Rais John Magufuli kumtimua Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, kwa madai kuwa ni miongoni mwa watendaji wabovu wa serikali.

Alisema utendaji mbovu wa Jaji Mutungi umesababisha mtafaruku mkubwa na mgogoro unaoendelea ndani ya CUF.

“Rais Magufuli anatumbua watendaji ambao si waadilifu, lakini Msajili amemwacha kwani anapaswa kutumbuliwa kwa sababu ameivuruga nchi,” alisema.

Alisema Msajili huyo amempa uhalali Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyekiti wa CUF, wakati alijiuzulu kabla ya uchaguzi mkuu na sasa amekuwa akikihujumu chama.

Pendeza Kwa Kutumia Products za Marks on Beauty Products

$
0
0

MARKSON BEAUTY PRODUCTS ni kampuni inayotoa bidhaa ORIGINAL zenye matokeo mazuri bila kemikali wala madhara yoyote na Zimethibitishwa kiafya.
Pata punguzo la bei kwa bidhaa hizi msimu huu wa sikukuu.
1.HANDSOME UP ni kifaa kinachoongeza maumbile ya kiume kwa 99% kwa size uipendayo wewe na kuimarisha misuli ya uume kwa @190,000/= tuu.
2.MEN GELY ya kupaka. Hii inaongeza kwa wastani wa inch 6.5 na inapatikana kwa @120,000/=.
3. MAX MAN 2. Ni vidonge kwa ajili ya nguvu ambavyo vinasaidia sana hata kwa watu wenye kisukari na waliokua wakifanya sana master blashion. Pia huongeza hamu ya tendo la ndoa kwa @120,000/=tu. PIA tuna dawa ya kuongeza nguvu za kiume ya kunywa (syrup) kwa @140,000/=
4 .BOTCHO MULT-PLUS 10× ni dawa mpya ya kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) bila madhara. Inapatikana kwa @190,000/=
5.MARK BEAUTY CREAM ni mafuta ya kukufanya kuwa mweupe na soft mwili mzima. Huondoa sugu, madoa na makovu. Yanapatikana kwa @120,000/=.
6.GREY HAIR STIMULATOR huondoa mvi milele zisirudi na kuzuia nywele kukatika ovyo (kipara). Inapatikana kwa @120,000/= tu.
Tupo DAR ES SALAAM kariakoo na posta mpya.
Popote ulipo duniani utapata huduma zetu.

Wasiliana nasi kwa (+255)
0767447444 au
0714335378
Follow us
@Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr

Tundu Lissu Afunguka Historia ya Maisha Yake,,Asimulia Jinsi Alivyopigwa na Wasira..Adai Anapenda Kulewa na Tusker ya Bariidii..!!!

$
0
0

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lisu alinusurika kushambuliwa na mbunge wa zamani wa Bunda, Steven Wasira katika moja ya vikao vya Bunge mjini Dodoma.

Lissu alisema hayo wakati akisimulia sehemu ya maisha yake binafsi na mambo aliyowahi kukutana nayo maishani katika mahojiano maalumu na Mwananchi yaliyofanyika Jumatano.

Katika simulizi hiyo, Lissu, ambaye kwa sasa ni rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), alizungumzia pia kesi zinazomkabili, maisha ya mahabusu, familia, kazi zake, burudani anazopenda na mahusiano yake na watu wa aina tofauti.

Akizungumzia mkasa uliosababisha anusurike kupata kipigo hicho, Lissu alisema Wasira alikuwa amechukizwa na maneno yake makali bungeni.

“Nilikuwa nimemuudhi kwa kumtolea maneno makali wakati nikichangia,” alisema Lissu akijaribu kukumbuka alichosema.

Pamoja na kutokumbuka alichokisema, wakati huo Lissu alimponda Wasira kuwa alijiunga upinzani kwa kuwa alidhani kuna fedha na alipogundua hakuna ndipo akakimbia kurudi CCM.


“Alichukia sana. Sasa nimetoka pale naenda chooni, nikamkuta akiwa na wabunge wengine wa CCM. Aliponiona akaanza kunifuata akiniambia kuwa atanipiga,” alikumbuka Lissu.

“Akichukia anakuwa mkubwa kweli, na mimi mdogo. Anakuwa tofauti na niliona anaelekeza kwenye kona ili anipate vizuri. Nikiangalia kama wale wabunge wengine wa CCM wataingilia kuamulia, naona hakuna anayetaka kumzuia.

“Nilikuwa natamani mtu aje aingilie, nichomoke, lakini hawakujishughulisha nasi. Akarusha ngumi ya kwanza, nikakwepa. Akanisogelea tena, akarusha ngumi nyingine ikanikosa. Hapo sasa nikawa napiga hesabu. Nikasema akisogea tena, nampiga teke, na akiinama tu kuugulia, mimi nachomoka.”

Hata hivyo, Lissu alisema, Wasira hakuendelea na badala yake akageuka na kuanza kuondoka.

“Hapo ilikuwa pona yangu. Yule anatisha akichukia,” alisema.

Hata hivyo, Wasira amedai Lissu hasemi ukweli.

Lissu analichukulia tukio hilo kuwa la kawaida katika maisha yake ya mapambano ya kutetea mazingira, haki za wanyonge na kupigania demokrasia na utawala bora.

Akijibu swali kuhusu hali ya usalama wake katika maisha anayoendesha ya mapambano, Lissu alisema hajawahi kutishiwa maisha yake kwenye siasa na anakumbuka ni mara moja tu alitishiwa maisha wakati akipigania mazingira.

“Kuna watu wana hasira na mimi kwelikweli, lakini hawajawahi kunitishia,” alisema.

“Nakumbuka zamani kabla sijawa mbaya namna hii, twenty years ago, wakati nikiongoza Chama cha Wanasheria Watetezi wa Mazingira (LEAT) niliwahi kupata vitisho,” alisema Lissu.

Alisema wakati huo Serikali ya Awamu ya Tatu ilimpa raia wa Ireland, Reginald Nolan eneo kwenye delta ya Rufiji ili aendeshe mradi wa kuvuna kamba.

Alisema Serikali ilimpa hekta 20,000 ili atengeneze mabwawa ya kufuga kamba kwenye delta ya Rufiji, maeneo ambayo yana vijiji vinane, shughuli za kilimo na makazi na msitu ya mikoko.

“Niliongoza kampeni ya kimataifa kwa kila njia, ikiwamo mitandao ya kimataifa ya wanaharakati kuupinga mradi huo. Hatimaye, Benki ya Vitega Uchumi ya Ulaya (European Investment Bank) iliyokuwa itoe mkopo kwa Nolan ambao ungedhaminiwa na Serikali ya Tanzania, wakasema hawatatoa mkopo na kwa hiyo, mradi mzima ukasambaratika,” alisema.

“Wakati huo ndipo tukaletewa barua ya vitisho iliyopitishwa chini ya mlango. Asubuhi ndipo tukaikuta. Lakini zaidi ya hapo sijawahi kupata vitisho.

“Kwanza watanitishia nini? Wataniambia nyamaza tutakuua?”

Hata hivyo alisema anajua hayuko salama kutokana na aina ya siasa anazoendesha.

“Huwezi ukawa unaendesha siasa za aina hii halafu ukawa salama. Lazima utegemee kusumbuliwa. Usipotegemea kusumbuliwa, utapata shock,” alisema.

Lissu alisema hata matukio ya kukamatwakamatwa na askari wa Jeshi la Polisi hayajawahi kumshangaza kwa kuwa amekuwa akiendesha siasa za mapambano.

“Na wala sikosi usingizi. Nilale central (kituo kikuu cha poli) au nilale nyumbani, napata usingizi wangu mzuri kabisa,” alisema Lissu.

“Ili mradi nipate chupa zangu tatu kubwa za maji ya Kilimanjaro. Hizi chupa huwa nazitumia kama mto. Nikizipata tu, naweka kichwani na nalala usingizi mzuri kabisa. Tena mimi huwa nakoroma. Ndio maana nikitoka mahabusu huwa mnaniona nimebeba chupa ya maji ya Kilimanjaro.”

Hata hivyo, Lissu alisema hafurahii maisha ya mahabusu kwa kuwa si sehemu nzuri.

“Kusema sikosi usingizi, hakumaanishi kuwa nafurahia kulala mahabusu, hasa unapokuwa huna kosa,” alisema.

“Huko kuna watu wengi wanakamatwa na kuwekwa mahabusu bila ya makosa. Si kitu kizuri.”

Alisema hadi sasa ameshakaa mahabusu kwa kesi nne, ambazo zote ni za uchochezi. Akizungumzia jinsi anavyoweza kumudu maisha ya kifamilia, uwakili, ubunge, uongozi wa Chadema na urais wa TLS, Lissu alisema hayo yote yanawezekana kama unajipanga.

“I’m a very busy man (ni mtu niliye na kazi nyingi), lakini nimejifunza kitu. Fikiria tunatumia muda kiasi gani kwenye kinywaji. Kwa hiyo there’s plenty of time (kuna muda mwingi),” alisema Lissu.

“Napata muda wa TLS, tuna vikao viwili, muda wa kukaa na mama, wa Chadema, na napata muda wa mahakamani, Napata muda wa kinywaji. Mimi nakunywa Tusker ya baridi.

“Ukipanga muda wako sawasawa, there’s plenty of time.”

Lakini alisema kutokana na harakati ambazo zimekuwa zinamkabili, mwaka jana hakupata muda wa kutosha wa kuwa karibu na wapigakura wake wa Jimbo la Singida Mashariki.

“Najua hilo lina gharama zake, lakini ni lazima nifanye kazi zote,” alisema.

Lissu alisema kati ya mambo hayo, hupata muda wa kutosha wa kusoma kwa kuwa hicho ndicho kitu anachokipenda sana maishani mwake.

“Nikisafiri, iwe kwa ndege au kwa gari, ni lazima niwe na vitabu, magazeti. Hata nikiwa gerezani huwa naenda na magazeti,” alisema Lissu.

“Kwa kweli, ikitokea kwamba ninahukumiwa kufungwa, kitu ambacho kitanisumbua sana ni kukosa freedom ya kusoma.”

Lissu amekuwa akihusika katika kesi lukuki, kuanzia zile za kawaida za ofisi yake, za kisiasa zinazohusu wanachama wa Chadema, za wananchi na zinazomkabili, lakini anasema mashauri hayo hayajamfanya awe tajiri.

“Mimi si tajiri, ni mtu wa kawaida. Kazi yangu kubwa ni kutoa msaada wa kisheria,” alisema.

“Nimeoa Tarime, mke wangu ni mwanasheria na anatoka Tarime. Huko mimi ni maarufu sana, lakini si kwa sababu ya mke wangu.

“Huko nilitoa watu 466 gerezani ambao walikuwa wamefungwa kutokana na kupinga kunyang’anywa ardhi.”

Alisema hiyo ilikuwa wakati wawekezaji walipokuwa wakipewa ardhi kwa ajili ya kuchimba madini.

Alisema wateja wake wengine wakubwa kwa sasa ni vijana wanaoshtakiwa kwa makosa ya mtandaoni.

“Sheria mbili za makosa ya mtandaoni zimesababisha watu wengi kukamatwa. Wote wamekuwa wateja wangu,” alisema.

“Usipowatetea hawa wadogo wasio na kitu na wasioweza kusema, siku mkianza kushughulikiwa hakuna atakayewatetea.”

Alisema shughuli hizo huzifanya kwa kutoa msaada na anamudu kufanya hivyo kwa kuwa ni mbunge.

“Mshahara wa ubunge unaniwezesha kutetea Watanzania mahakamani. Fedha kidogo ninayopata ndiyo ninayoitumia kusafiri na gharama nyingine. Si tajiri, lakini naishi confortably,” alisema.

Alisema tofauti na mawakili wengine, kazi yake haina gharama kubwa za uendeshaji kwa kuwa ameziepuka.

“Kwanza ofisi yangu iko nyumbani. Pale ndipo nafanya kila kitu, kwa hiyo hakuna cha kumlipa msichana wa usafi,” alisema mbunge huyo wa Singida Mashariki.

Kuhusu mjadala uliotuama mitandaoni ikimtaja Nape Nnauye kuwa shujaa baada ya kupinga uvamizi wa kituo cha televisheni cha Clouds Media uliofanywa na kiongozi wa Serikali aliyeambatana na askari wenye silaha za moto, Lissu alisema mbunge huyo wa Mtama si shujaa na kumfananisha na waziri wa zamani wa mambo ya ndani wa Ghana, Tawia Adamafyo.

“Huyu mtu amezima Bunge na kulivuruga kwelikweli. Amefungia magazeti. Akiwa waziri amepitisha sheria ya mbovu ya Huduma ya Vyombo vya Habari, sioni ushujaa wowote bali amevuna matunda ya kazi yake na siasa za ndani ya CCM,”alifafanua

Tawia aliwasilisha muswada wa kuwaweka ndani watu enzi za Kwame Nkrumah, sheria ambayo ilipigiwa kelele na wabunge.

“Huyo Tawio hakujua sheria anayotunga inatengeneza rat trap (mtego). Kilichotokea ni yeye kuwa wa kwanza kuwekwa kizuizini kwa kutumia sheria hiyo maofisa usalama kutegesha bomu karibu na eneo alilokuwa akihutbia Rais Nkurumah na hivyo waziri huyo kuonekana alihusika.

“Hawa viongozi wanatunga sheria wanazodhani zitawabana na kuwashughulikia wapinzani, yakiwakuta wao wanapiga kelele. Kwahiyo mimi sioni ushujaa wowote wa Nape,”alieleza Lissu ambaye pia ni mwanasheria mkuu wa Chadema.

Nape alivuliwa uwaziri wa habari Machi 23 baada ya kuachwa kwenye mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri.

Habari zaidi na Fredrick Nwaka

Noma Sana ..Rais Magufuli Akomalia Sakata la Mchanga....Hii Ndiyo Amri Mpya Aliyoitoa..!!!

$
0
0

RAIS John Magufuli amekazia msimamo wake wa kutaka kujua kila kilichomo kwenye makontena ya mchanga wa dhahabu baada ya kuwataka wajumbe wa kamati maalumu aliyounda kutumia utaalamu wao wote katika kupata ukweli bila kuyumbishwa na mtu.

Rais Magufuli (JPM) alitoa maelekezo hayo Ikulu jijini Dar es Salaam, jana, wakati akiwaapisha wajumbe hao wa kamati maalumu aliyounda kuchunguza kiwango na aina ya madini yaliyomo kwenye mchanga wenye madini ulio ndani ya makontena yaliyoko katika maeneo mbalimbali nchini.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, ilieleza kuwa hafla ya kiapo kwa wajumbe wa kamati hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju;

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi; Kamishna wa Maadili, Jaji Harold Nsekela na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Taarifa ya Ikulu ilieleza kuwa Rais alitoa maelekezo hayo baada ya kuwaapisha, akisema kuwa ameamua kuunda kamati hiyo yenye wasomi waliobobea katika masuala ya jiolojia, kemikali na uchambuzi wa kisayansi ili wawawakilishe Watanzania zaidi ya Milioni 50 ambao wanataka kujua ukweli kuhusu rasilimali yao ya madini.

“Hivi sasa duniani kuna vita nyingi na vita mojawapo ni vita ya uchumi, kwa hiyo tunawatuma nyinyi mwende mkapigane vita hii katika sekta hii ya madini, mkawawakilishe Watanzania zaidi ya Milioni 50, mkapate ukweli wote na wala msikubali kuyumbishwa na mtu yeyote,” alisema Rais Magufuli na kuongeza:

“Tumieni utaalamu wenu, busara zenu, uzalendo wenu kwa Taifa na upendo wenu kwa Watanzania hasa masikini wenye shida nyingi.”

Kamati hiyo ya wanasayansi wanane iliteuliwa na Rais Magufuli Machi 29 na inaongozwa na Mwenyekiti wake Prof. Abdulkarim Hamis Mruma. Itafanya kazi ya uchunguzi kwa siku 20 kabla kuwasilisha ripoti yake kwa Rais.

Aidha, Rais Magufuli aliwahakikishia wajumbe wa kamati hiyo kuwa Serikali itatoa kila aina ya ushirikiano kwao ili kufanikisha kazi hiyo na ametaka wawe huru kutumia vitendea kazi vyovyote vinavyohitajika, ikiwamo maabara mbalimbali za taasisi za Serikali na nyinginezo.

“Nendeni popote mnapohitaji kufanya kazi tutawapa ushirikiano, fungueni makontena popote yalipo, chukueni sampuli na mkazipime mjue kilichomo na naviagiza vyombo vya dola vihakikishe hakuna mtu atakayewakwamisha,” alisema Rais Magufuli.

WACHUMI, WANASHERIA PIA KUCHUNGUZA

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli alisema baada ya kuunda kamati hiyo ya wanasayansi, ataunda kamati nyingine ya wachumi na wanasheria kwa ajili ya kufanya tathmini na kuiangalia sera na sheria ya madini kwa lengo la kupata taarifa zaidi juu ya biashara ya madini hapa nchini.

Hivi karibuni, Rais Magufuli alifanya ziara ya kushtukiza katika bandari ya Dar es Salaam na kukuta makontena 20 ya mchanga wa dhahabu yaliyokuwa tayari kusafirishwa kwenda nje ya nchi.

Siku chache baadaye, yalibainika makontena mengine 262 yenye mchanga wa dhahabu yakiwa yamehifadhiwa baada ya kufuata taratibu zote za kuyasafirisha kwenda nje.

Uongozi wa Mgodi wa Acacia wenye sehemu kubwa ya makontena hayo yaliyoko bandarini Dar es Salaam ulitoa ufafanuzi kuwa makontena hayo yalifikishwa baada ya mchakato wake kufanyika kabla ya agizo la Rais kuzuia usafirishaji wa mchanga aina hiyo kwenda nje ya nchi.

KIONGOZI WA KIHINDU

Wakati huo huo, Rais Magufuli alikutana na kufanya mazungumzo na Kiongozi Mkuu wa Jumuiya ya Kihindu ya BAPS Swaminarayan Sanstha Duniani, Mtukufu Mahant Swami Maharaj ambaye yupo nchini kwa ziara ya siku 7.

Pamoja na kumshukuru kwa ujio wake nchini, Rais Magufuli alimhakikishia kuwa Serikali ya Tanzania itaendeleza na kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano wake na Jumuiya hiyo na amewaalika wafanyabiashara walio chini ya Jumuiya hiyo kuja nchini Tanzania kuwekeza katika viwanda, kilimo na shughuli nyingine za biashara na uwekezaji.

Mbwana Samatta Hashikiki Atupia Tena, Genk ikiua 4 - 0

$
0
0

Mbwana Samatta akifunga bao hilo jana, ambalo lilikuwa la pili kwenye mchezo

NAHODHA wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta jana amefunga bao moja timu yake, KRC Genk ikishinda 4-0 Uwanja wa Luminus Arena mjini Genk dhidi ya Lokeren katika mchezo wa mchujo wa kuwania kucheza UEFA Europa League msimu ujao.

Samatta alifunga bao lake dakika ya 72, likiwa la pili katika mchezo huo baada ya Alejandro Pozuelo kutangulia kuifungia Genk la kwanza dakika ya 45 na ushei, kabla ya Jean-Paul Boetius kufunga la tatu dakika ya 77 na Jose Naranjo kumalizia la nne dakika ya 90.

Bao hilo linamfanya Samatta aliyecheza mechi hiyo akitoka nyumbani kuichezea timu yake ya taifa, Taifa Stars na kuufunga mabao yote katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Botswana Jumamosi iliyopita, afikishe mabao 18 katika mechi 49 alizoichezea Genk tangu asajiliwe Januari mwaka jana akitokea TP Mazembe ya DRC.

Kati ya mechi hizo 49, michezo 18 Samatta alicheza msimu uliopita na 31 msimu huu na kati ya hiyo, ni michezo 30 tu ndiyo alianza, 10 msimu uliopita na 20 msimu huu.

Mechi 19 kati ya hizo alitokea benchi, nane msimu uliopita na 11 msimu huu, wakati 11 hakumaliza baada ya kutolewa, tano msimu uliopita na sita msimu huu na katika mabao hayo 18, 11 amefunga msimu huu na sita msimu uliopita.

Kikosi cha KRC Genk kilikuwa: Ryan, Castagne, Brabec, Colley, Uronen, Berge, Pozuelo, Malinovskyi/Heynen dk68, Trossard, Boetius/Buffalo dk83 na Samatta/Naranjo dk79.

Lokeren: Verhulst, Maric, Skulason, Person, De Sutter, Galitsios, Ofkir, Hupperts/Stra Sunsetman dk61, Ticinovic/De Prycker dk77, na De Ridder Bolbat/Martin dk58.

Rafiki wa Alikiba Apata Shavu la Uwaziri wa Fedha Afrika Kusini..!!!

$
0
0

Kumbe Alikiba na waziri mpya wa fedha wa Afrika Kusini, Malusi Gigaba ni watu wa karibu! Hitmaker huyo wa Aje amempongeza waziri huyo kupitia mtandao wa Instagram kwa kuchaguliwa na Rais Jacob Zuma kukalia kiti hicho.

Kupitia mtandao huo, Alikiba ameandika:

Honorable minister Gigaba @malusi_gigaba, it’s such an honour to be an Ambassador under one of the campaigns you started for Africa as Minister of Home Affairs: Stop child Trafficking. I want to thank you for the opportunity and congratulate you in your new role as the Minister of Finance For South Africa, Stay blessed

Kimenukaa CCM..Vigogo wengine Kibao Kumfuata Sophia Simba..!!!

$
0
0

Baada ya kubadilisha katiba, CCM inaonekana kuendelea kujipanga kukabiliana na ongezeko la upinzani nchini baada ya kuteua makatibu wa mikoa na wilaya, wanaoelezewa kuwa “majemedari” waliopewa jukumu la kukipitisha chama katika mtihani wa kwanza wa uchaguzi wa ndani.

CCM inatarajia kuanza chaguzi za ngazi za chini za ndani wakati wowote kuanzia sasa na kukamilisha baadaye mwka huu itakapochagua wajumbe wa vyombo vya juu vya maamuzi.

Mtihani wa pili utakuwa uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa mwaka 2019 kabla ya kumalizia na Uchaguzi Mkuu 2020.

Ikiwa imetingishwa na Uchaguzi Mkuu uliopita, tayari CCM imeshapunguza idadi ya wajumbe wa Kamati Kuu kutoka 34 hadi 24, na wa Halmashauri Kuu kutoka 388 hadi 160.

Imeondoa nafasi zisizo za kikatiba katika wilaya na jumuiya zake na kufanya mabadiliko ya sekretarieti. Na sasa imetangaza makatibu wa mikoa na wilaya.

“Hao ndio majemedari waliopewa jukumu la kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa mafanikio,” alisema kada mmoja ambaye hakupenda kutajwa jina lake.


Katika Uchaguzi Mkuu uliopita, CCM ilipoteza mawaziri wakuu wawili wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye ambao walifuatwa na makada wengine kadhaa wakiwemo wenyeviti wa mikoa, wilaya, wabunge na madiwani.

Pia CCM iliruhusu vyama vya upinzani, hasa vilivyokuwa chini ya mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kupata zaidi ya viti 100 vya ubunge, viti zaidi vya udiwani na halmashauri 19.

Baadhi ya watendaji wa chama hicho hasa makatibu wa mkoa na wilaya, ndio wanaodaiwa kusababisha CCM kupata ushindi mdogo katika Uchaguzi Mkuu uliopita ambao ulikuwa na msisimko mkubwa.

Mwenyekiti John Magufuli alisema waziwazi kuwa makatibu hawakusaidia wakati wajumbe wa Halmashauri Kuu walipoimba wimbo wa kuwa na imani na Lowassa baada ya jina lake kukatwa na Kamati Kuu.

Hivyo, haikuwa ajabu kwa CCM kupanga upya safu ya uongozi kuondokana na masalia ya wasaliti, hasa wanaomuunga mkono Lowassa na wenzake.

Mapema wiki hii, katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Humphrey Polepole alitangaza majina mapya ya makatibu wa mikoa na wilaya. Kati yao wamo 31 wa mikoa na 155 wa wilaya. Hata hivyo majina yaliyotangazwa ni ya upande wa Bara pekee.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Polepole alisema uteuzi uliofanywa umezingatia weledi, jinsia na mpango wa kuachiana vijiti kwa kuzingatia rika.

Alisema kati ya makatibu hao walioteuliwa wa mikoa. kumi na moja ni wale waliopandishwa hadhi kutokana na utendaji wao, na 20 ni wapya kabisa.

Uteuzi huo umefanyika baada ya chama hicho kupitia ripoti ya tathmini ya uchaguzi uliopita na kubaini baadhi yao walikisaliti chama wakati wa Uchaguzi Mkuu na kusababisha kupoteza viti vingi vya ubunge, udiwani na baadhi ya halmashauri.

Uteuzi huo ni mwendelezo wa CCM kuweka majemedari wapya. Mwenyekiti alianza kupanga safu ya uongozi kwa kuwaondoa Rajab Luhwavi, aliyekuwa naibu katibu mkuu bara na nafasi yake kuchukuliwa na Rodrick Mpogolo, na Nape Nnauye, aliyekuwa katibu wa itikadi na Christopher Ole Sendeka akapewa usemaji wa chama.

Wengine walioondolewa ni Pindi Chana, aliyekuwa katibu wa NEC wa siasa na uhusiano wa kimataifa na nafasi yake kuchukuliwa na Kanali Ngemela Lubinga. Pia Vuai Ali Vuai, aliyekuwa naibu katibu mkuu Zanzibar, Dk Muhammad Seif Khatib na Zakhia Meghji. Nafasi ya kiutendaji ambayo haijaguswa ni ya katibu mkuu.

Makatibu hao kwa mujibu wa katiba ya CCM wana jukumu la kujua takwimu zote za chama katika maeneo yao ya kazi, ikiwamo idadi ya wanachama, matawi, mali za chama, kuandaa uchaguzi wa ndani na kufanya tathmini ya mgombea anayekubalika kwenye eneo lake.

Vigogo 12 wa chama hicho walifukuzwa uanachama kwa usaliti, akiwemo aliyekuwa mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT), Sophia Simba na wenyeviti wanne wa mikoa ya Dar es Salaam, Iringa, Shinyanga na Mara.

Shilole 'Mwanaume kuwa Mario ni kumtia aibu mama yako mzazi na dada yako'

$
0
0

"Mwanaume kuwa Mario ni kumtia aibu mama yako mzazi, na dada yako. Nawashauri vijana marioo mkafanye kazi mpate pesa, hata kushona viatu ni kazi mkafanye kazi siyo kutegemea wanawake tu" Shilole

Kwa uonavyo wewe, kijana kulelewa na mwanamke ni sawa au si sawa?

Shilole Ajivisha Pete ya Uchumba mwenyewe

$
0
0

STAA wa Filamu za Kibongo, Zuwena Mohammed ameamua kujivisha pete ya uchumba mwenyewe, kitendo ambacho kimezua minong’ono kwa watu wengi wakidai kuwa amevishwa na mtu ambaye hajamuweka wazi.

Akizungumza na Ijumaa, Shilole alisema kuwa aliwahi kuvishwa pete na aliyekuwa mpenzi wake, Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’, ikapotea kitatanishi kisha Nuh akaoa mwanamke mwingine hivyo akaona kuliko kidole hicho kibaki tupu, akisitiri.

“Pete ile ya Nuh ilipotea, sijui huwa ni za mashetani? Nimeona ninunue nyingine niivae, hakuna cha mwanaume wala nini, mimi sijaona tatizo kuivaa na huenda ndiyo naiita ndoa,” alisema Shilole.

Harmorapa Amganda Mzungu wa Kampuni ya Swala Escape One

$
0
0

MSANII wa Bongo Fleva anayetrendi katika mitandao ya kijamii Bongo, Athuman Omary ‘Hamorapa’, jana jumamosi katika viwanja vya Escape One Kinondoni Jijini Dar es Salaam, alionekana kumganda mzungu wa kampuni ya kinywaji cha Swala baada ya kusambaa kwa taarifa za kupewa dili nono na kampuni inayozalisha kinywaji cha Swala.

Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Hamorapa, imeweka Ujumbe akijinadi kwa mashabiki wake kuwa yupo na mzungu wake bosi wa kijanywaji hicho.

Aidha kwa sasa mashabiki wanamshauri Hamorapa kufanya kazi nzuri za sanaa na kuachana na kiki zisizo na kichwa wala miguu.

Alichokifanya Rais Wakati wa Kumsindikiza PM wa Ethiopia ni "Aibu" Kiitifaki,Wahusika Msaidieni..!!!

$
0
0

Kwanza tunapaswa kujua vile vikundi vya ngoma na utamaduni wakati wa kupokea ugeni wa nchi au kusindikiza/kuaga huwa wanalipwa,na kazi ya kuvikusanya na kuvipeleka Airport ipo chini ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dsm.

Wale Wamama unaowaona wanapepea bendera za nchi mwenyeji na nchi mgeni huwa ni Walimu wanaochukuliwa katika shule za mkoa wa Dsm.Wengi ni walimu wa Shule ya Msingi.

Awali malipo yao ilikuwa ni shilingi 20,000 ila kwa sasa wamepandishiwa mpaka shilingi 50,000 kwa siku.Hivyo bajeti yao huwa ipo.Na vile vikundi vya ngoma huwa ni kutoka JKT au JWTZ.Wale wote wana posho yao.

Jana kama mlivyomsikia Rais,anasema ameamua kuwapa hiyo zawadi ya milioni 20 sbb wameonyesha uzalendo na ukarimu kwa wageni na kuiletea nchi sifa,lakini Rais akasema anajua huko nje wanasemwa sana na kuchekwa kuwa wanapoteza muda,hivyo kuwatia motisha akatoa milioni 15 na Waziri Mkuu Milioni 5.

Jambo la Kujifunza::

1)Kwanza nafikiri huu utaratibu wa Rais kumwaga mwaga pesa si jambo la ajabu sana,lkn linapaswa kuratibiwa vizuri,yaani washauri wake wampe kamuongozo tu ka namna ya kuzifikisha na kuwatia moyo anaokusudia kuwapa motisha.Hizi hela za hivi kwa JK zimeliwa sana,lkn hazikuwa na "Promo" kama hii.Nafikiri Rais anatumia utaratibu wa kutangaza na watu kugawiwa papo kwa papo sbb enzi za JK ikitolewa milion20 wale wamama wanakutana na milion10.Hizi kumi zinapotelea hapa katikati kutoka benk mpaka kwa kina Mama "upepo" unaziyeyusha hizo 10

2)Haka ka utaratibu ka kumstukiza mtu achangie papo kwa papo sio kazuri,maana ukiangalia hiyo ya Airport,Rais kachukua kipaza kaahidi milioni 15 hapo hapo akampasia Majaliwa naye aahidi,mpaka Majaliwa akapata kigugumizi akasema "Nilidhani protocol hazikubali,lakini kama mkubwa kasema,basi mi sitatoa nyingi kumzidi,mi ntawapa milioni 5".Hii ilitokea hata kule Nangurukuru,Rais anatoa milioni 20 ya Zahanati halafu anampa DED atoe milioni 10 na Mbunge anaambiwa atoe,aliposema hana akamnanga.

3)Jana Rais amevunja Protocol,kwenye itifaki ya "Arrival and Departure Protocol of State Visit at Airport" kuna mambo ya kuzingatiwa.

Wakati wa "Arrival",ni kawaida uwanja kufungwa nusu saa kabla ya mgeni kutua na kusubiri ametua na kupokelewa.Then Chief of Protocol akiwa na balozi wa nchi ya mgeni wanapanda kwenye ngazi kwenda kumpokea mgeni,anashuka,anapewa maua na mtoto aliyeandaliwa na baadae anasalimiana na mwenyeji,huku akimtambulisha kwa viongozi kwa itifaki. ile "Guard of Honour" inaweza kuwa "Silent" au ile ya mizinga 21.

Wakati wa "Departure" kadhalika uwanja hufungwa,hivyo ndege nyingine huendelea kuzunguka juu mpaka shughuli za kumuaga na ndege kunyanyuka zikamilike,na zile zilizo chini,husubiri mpaka ndege ya mgeni mashahuri iondoke.

Wakati wa kuondoka kwanza hupigwa nyimbo za nchi zote,then anasindikizwa mpaka kwenye mlango wa ndege...anaagana na na wenyeji na baadae anapanda peke yake hadi katika ngazi ya mwisho,anageuka na kupunga mkono na kuingia ndani.Na ujumbe uliombatana nae hufuata kuelekea ktk ndege kwa haraka tyari kwa safari.

Rais au msindikizaji (anaweza kuwa Waziri wa Mashauriano ya kigeni au yoyote) huendelea kusimama pembeni mpaka pale mgeni wake ktk ndege itakaponyanyuka "take off" kutoka kwenye runway,na ndipo bendera ya rais mgeni inashushwa kuashiria kuwa hayupo tena katika eneo lile kama mgeni.Hii ni heshima kwa mgeni na wawakilishi wake kama balozi waliobaki nchini na kwa nchi ya Rais mgeni.

Lakini jana sijui watu wa Protocol ilikuwaje,walipaswa kumwambia mkuu asubiri ile ndege ya Waziri Mkuu inyanyuke kutoka katika ardhi ya nchi yake na bendera ya Rais wa Ethiopia kushushwa ndio aende kwenye wale wanavikundi wa ngoma na utamaduni.Sasa kwenda wakati ndio kwanza ndege inaelekea eneo la kurukia ni "mapungufu madogo ya itifaki" ambayo yanapunguza "uweledi" wa wanadiplomasia wetu katika medani za kimataifa.Ni kukosa "heshima" za kiitifaki kwa mgeni na ujumbe wake,ni kuleta picha mbaya kwa balozi wa Ethiopia Tanzania aliyekuwa uwanjani kuambatana na Rais kumsindikiza Waziri Mkuu wake.

Hii si picha nzuri,siku zijazo viongozi wetu wanaweza tumika kama "rejea" (references) ya mfano wa viongozi wanaoongoza kuvunja taratibu za kiitifaki na tukabaki katika kumbukumbu zisizo nzuri katika medani ya kimataifa.Haya yalitokea kwa Amini miaka ile ya utawala wake.Kumbe si ajabu nchi nyingi duniani huwaandaa viongozi wakuu wa nchi na serikali kwa kuwaweka katika wizara ya mashauriano ya kigeni kwa muda kabla kama njia ya kuwaandaa kuwa viongozi wakuu.

Ndio maana wakati PM Majaliwa kapewa kipaza atoe ahadi kwa wale kina Mama alisema "Mimi mwenyewe nilivutiwa na jinsi mlivyocheza na kuimba,lakini nilidhani mambo ya protocol hayaruhusu kuja hapa,siwezi kuahidi kiasi kikubwa zaidi ya mkubwa wangu,mimi nitatoa milioni 5"

Tutaendelea kumkumbusha Rais wetu sababu bado tunampenda.Sisi tuliompigia kampeni na kumpa kura tutaendelea kusema ili kumfanya awe bora zaidi na zaidi.Ukosoaji wetu usichukuliwa kama nia mbaya kwa Raisi,bali upendo wa kweli wa kumfanya awe bora zaidi na zaidi.Maana siyekupenda hakuthamini.
Viewing all 104807 articles
Browse latest View live




Latest Images