Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all articles
Browse latest Browse all 109637

Hatimaye John Shibuda Ajifukuzisha Chadema Mwenye, Atoa Shutuma Kali Dhidi ya Chadema

$
0
0
WAKATI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kikijipanga wakuchukulia hatua wabunge wake waliosaliti msimamo wa Kamati Kuu na kuhudhuria vikao vya Bunge la Katiba, Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda ametangaza kutogombea ubunge tena kupita chama hicho.

Shibuda, Said Arfi (Mpanda Mjini) na Leticia Nyerere (Viti Maalum) wamewasili mjini Dodoma na kujisajili kwa lengo la kushiriki vikao hivyo, licha ya kuzuiliwa na chama chao ambacho kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kimesusia Bunge hilo.

Shibuda alitangaza uamuzi huo kwa nyakati tofauti jana, wakati akizungumza na wazee wa mji wa Maswa na Malampaka wilayani humo, walipotaka kujua hatima yake ya kisiasa ndani ya CHADEMA.

Alidai kauli za vitisho na kejeli dhidi yake zinazofanywa na baadhi ya viongozi wa CHADEMA, ndizo zimemfanya achukue hatua hiyo.

“Mimi niliingia CHADEMA kwa hiari yangu baada ya kuona dhuluma zilizokuwa ndani ya CCM, chama ambacho kimenilea kisiasa, nikaona heri niende CHADEMA ambako nilidhani kuna demokrasia na ukombozi wa kweli.

“Lakini nilichokikuta humo ni tofauti, kwani kila siku wazee wangu mnasikia napata misukosuko isiyo na maana,” alisema.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 109637

Trending Articles