Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

UKWELI Mchungu..Ulipumba Unadumaza Demokrasia Nchini...!!!!

$
0
0

KATIKA siasa za Tanzania kuna kupakaziana kwa kila aina, walio madarakani huwakazia wa upande ule wanaoitwa wapinzani. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kiliitwa chama cha Wachaga kwa sababu mwaasisi wake ni Eddwin Mtei.

Hawakusema lolote kwa aliyekuwa Makamu wake, Bob Makani (marehemu) ambaye ni Msukuma wa Shinyanga. Baadaye siku zilivyokuwa zinasogea na Chadema kushika moto Kanda ya Kaskazini, wa upande wa pili wakasema chama cha ukanda kupitia Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa, Mwenyekiti Freeman Mbowe.


Ujio wa waliokuwa mawaziri wakuu, Edward Lowassa na Frederick Sumaye, ukatafsiriwa, wakipewa nchi ni hatari na kwamba wataigawa nchi kikanda. Nadhani ni kutokana na mtazamo huo, Freeman Mbowe akamteua Dk. Mashinji Msukuma kutoka Kanda ya Ziwa, ili kuifuta ile dhana ya Chadema kuwa chama cha Ukanda wa Kaskazini.

Kwa upande wa Chama cha Wananchi (CUF), wa upande ule wakadai kuwa ni chama chenye udini; chama cha Waislamu, huku wakijua fika kwamba Sheria ya Vyama vya Siasa inakataza na katika katiba ya chama hicho, hakuna mahali unatajwa uislamu.

Kule Unguja wa upande ule wakasema CUF ni chama cha Wapemba. Ninavyojua mimi hakuna kabila hapa Tanzania linaloitwa Wapemba. Mbona hakuna Wambeya!

Kama hiyo haitoshi, wakaongeza sifa mbaya nyingine kwamba CUF kikipewa kushika madaraka Zanzibar, kitarudisha usultani eti CUF kina nasaba na uwarabu na ikasanifiwa kwamba Waarabu walioikimbia Zanzibar, ndio wanaotoa fedha za kuendesha chama hicho.

Mwaka 2015 kuelekea Uchaguzi Mkuu, vyama vya upinzani vilijiunga pamoja na kuazimia kumsimamisha mgombea mmoja kama mkakati wa kukiondoa madarakani Chama cha Mapinduzi (CCM), ikazaliwa Ukawa (Umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi), umoja ambao uliundwa kutokana na kupinga jinsi Bunge la Katiba lilivyokuwa likiendeshwa na Spika Samuel Sitta (marehemu), alikuwa anapendelea wajumbe wa chama tawala. Vyama vya upinzani vikaamua kususa Bunge na imeelezwa jina la Ukawa aliliibua Profesa Ibrahim Lipumba ambaye pia alikuwa mjumbe kwa tiketi ya CUF na alikuwa na kofia ya Mwenyekiti wa chama hicho.

Viongozi wakuu wa Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na National League for Democracy (NLD), wakaita mkutano mkubwa uliofanyika pale Jangwani, Dar es Salaam na wakatiliana saini ya kuungana kuipinga CCM. Prof Lipumba ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa wenyeviti na alishiriki kikamilifu katika mazungumzo ya kumkaribisha Lowassa Ukawa.

Ujio wa Lowassa na kuteuliwa kwake kuwa mgombea wa nafasi ya urais, kulizima ndoto ya Prof Lipumba ambaye tayari chama chake cha CUF kilikuwa kimemteua kugombea urais. Yako mengi yaliyosemwa kwamba Lipumba na Dk. Slaa walirubuniwa na kuahidiwa kula vinono kama watajiuzulu uongozi. Mkakati huu ulifanikiwa, lakini haukudhoofisha dhamira ya Ukawa. Lipumba na Slaa waliondoka nchini; mmoja akadai anaenda kufanya utafiti Rwanda, mwingine akaenda Marekani na baadaye Canada.

Prof Lipumba aliandika barua ya kujiuzulu nafasi yake ya Mwenyekiti na aliondokea hotelini alipofanyia mkutano na wanahabari kwenda kupanda ndege Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam. Ukawa wakapata pigo jingine kubwa kwa kuondokewa na Mwenyekiti wa NLD, Dk. Emmanuel Makaidi, lakini waliendelea kupigana na kukamilisha ‘vita’ vya Uchaguzi Mkuu Oktoba, mwaka 2015.

Miezi minane baadaye, Lipumba akarejea nchini. Akawashangaza wenzake aliposema hataunga mkono Ukawa, umoja alioshiriki kuunda. Kama hiyo haikutosha, akaenda Ikulu kumwona Rais John Magufuli na kumpongeza kwa ushindi, ingawaje CUF kama chama walikuwa wanapinga kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi Zanzibar. Walioelewa hili walielewa.

Miezi michache baadaye, Lipumba akaandika barua kwa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad, akieleza kwamba anafuta barua yake ya kujiuzulu na anataka kurejea kwenye nafasi yake ya uwenyekiti. Barua yake ya awali ilikuwa haijajibiwa kwa sababu chama kilikuwa kwenye harakati za uchaguzi, yeye akachukulia kwamba kwa vile hakujibiwa, basi ana haki ya kuendelea kuwa Mwenyekiti!

Walioelewa wameelewa baada ya Lipumba kuvamia mkutano mkuu na kujisimika uwenyekiti. Hapo ndipo mimi nasema sitaki ulipumba, unadumaza demokrasia na watu wote wenye uelewa hawapendi ulipumba, unavuruga chama ambacho umetoka nacho mbali, unashirikiana na polisi ambao kabla ya Uchaguzi Mkuu walikupiga virungu, wakakusweka ndani na kukufungulia kesi katika Mahakama ya Kisutu. Leo ndio maswahiba wako, wanakupa jeuri ya kuvamia ofisi za chama, kuwapiga na kuwajeruhi wale ambao hawakubaliani na ulipumba wako!

Hili liwe fundisho kwa viongozi wa vyama vingine kwamba visifanye ajizi ya kumwaminisha mtu mmoja kwamba bila yeye mambo hayaendi. Anzeni kupeana kijiti cha uongozi kama wanavyofanya wale wa chama cha dola. Chama ni cha wanachama, hata kama wewe ndiye uliyekianzisha na viongozi wasimilikishe uongozi. Kuna vyama vina viongozi wale wale toka vianzishwe na vimekwishapoteza uhalali wa kuitwa vyama vya siasa, lakini vinalelewa tu kwa sababu iko sababu ya kuviacha vidumae na kudumaza demokrasia.

Na hivi ndivyo ilivyo kwamba  chama tawala kinafurahia wapinzani wakivurugana. Kuna chama hakina hata mwakilishi ngazi ya kijiji/kitongoji. Chama kiko mfukoni hakina hata ofisi na kimeshindwa kupata hata diwani mmoja, lakini vinatoa matamko ya kuvipinga vyama vyenye uwakilishi bungeni!

TRUMP Akubali Kuiuzia Silaha Saudi Arabia ..Asaini Mkataba wa Dola Bilioni 110 ..!!!

$
0
0

Makubaliano ya ununuzi wa silaha za thamani ya dola za Kimarekani bilioni 110 ambayo yamesainiwa na Marekani na Saudi Arabia Jumamosi yanakusudia kutokomeza uchochezi hatarishi wa Iran.

Hayo yamesemwa Jumamosi na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Rex Tillerson wakati wa mkutano wake na Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia.

Akizungumza katika mkutano wa pamoja Riyadh na Waziri wa Mambo ya Nje Adel al-Jubeir, Tillerson amesema mkataba huo wa ulinzi umekusudia kusaidia “mkakati wa ulinzi wa muda mrefu wa Saudi Arabia na eneo lote la Ghuba ya Uajemi.”

Mkataba huo tayari umekwisha pitishwa, Tillerson amesema, “katika hali ya hivi sasa ya kupambana na kampeni hatarishi ya Iran na vitisho vyake, ambavyo vipo katika maeneo yote ya mipaka ya Saudi Arabia.”

Mkataba huo wa ulinzi ambao unaanza mara moja, ni moja kati ya mtiririko wa mikataba iliyosainiwa Jumamosi na Mfalme wa Saudi Arabia Salman na Rais Donald Trump.

Imelenga katika kuimarisha ushirikiano wa kijeshi na kibiashara kati ya nchi hizo mbili na unajumuisha mkataba wa pili wa ulinzi ambao unahiari mbalimbali zenye thamani ya mpaka dola billioni 350 kwa kipindi cha miaka 10 ijayo.

Tillerson amesema lengo la Trump kufanya ziara Saudi Arabia ilikuwa kukabiliana na aina yoyote ya vitisho vinavyofanywa na Iran. Amesema mlolongo wa mikutano ya hadhara na ya ndani ambayo Trump amekuwa akiifanya inalengo la “kupeleka ujumbe mzito kwa maadui zetu wanaofanana.”

Tillerson amemtaka rais aliyechaguliwa tena Iran Hassan Rouhani kutumia kipindi chake cha pili madarakani kusitisha programu ya kombora la balistiki nchini humo na tabia ya nchi yake kusaidia magaidi

Kutokana na hofu ya wauaji maisha yasimama Rufiji

$
0
0

Rufiji. Kuongezeka kwa mauaji ya viongozi wa serikali za mtaa na polisi kumeathiri kwa kiasi kikubwa shughuli za kiuchumi, kisiasa na kijamii katika maeneo kadhaa wilayani Rufiji na Kibiti mkoani Pwani.

Awali, hali haikuwa mbaya lakini baada ya mauaji ya askari wanane Aprili, shunguli nyingi za kiuchumi na kijamii zilianza kuathirika baada ya vyombo vya ulinzi na usalama kuamua kutumia nguvu kubwa.

Hali hiyo imejenga hofu na sintofahamu miongoni mwa wakazi wa maeneo hayo.Biashara nyingi zimefungwa na wananchi wengi hawaendi mashambani wakihofia, ama kukutana na wauaji au polisi wanaokuwa katika doria, ambao hawana ‘msalie mtume’ wanapomshuku mtu yeyote.

Na katazo la wananchi kutembea baada ya saa 12:00 jioni limezidisha hofu na limeondoa nafasi za vijana na kina mama wengi kufanya shughuli za kujiongezea kipato.

Hadi sasa zaidi ya viongozi 15. polisi 10, wafanyakazi wawili wa Idara ya Maliasili, mwananchi mmoja na watu wengine watatu waliokuwa wamevalia nguo za kike, wameshauawa tangu Mei mwaka jana. Na tangu mapema 2015, zaidi ya viongozi 21 wameshauawa.

Shughuli za serikali za vijiji zasimama

Pamoja na polisi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kuweka kambi maeneo hayo, sehemu kubwa ya wilaya hizo ni kama hazina uongozi.

Viongozi wengi kama si wote wa serikali za mitaa hasa watendaji wa kata, wenyeviti wa vijiji na vitongoji ambao wameonekana kulengwa zaidi na wauaji, wamefunga ofisi na sasa wanaishi mafichoni.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Jaribu Mpakani wilayani Kibiti, Ramadhani Msanga aliyekimbilia mafichoni tangu Februari 4 baada ya nyumba yake kuchomwa na watu wenye silaha, ni kielelezo cha maisha ya hofu.

Dada wa mwenyekiti huyo, Shela Msanga anasema awali, kaka yake alikuwa akipata vitisho vya maneno na maandishi, lakini Februari 4 wauaji waliamfuata nyumbani kwake saa moja jioni wakiwa na bunduki.

“Kwa bahati kaka hakuwepo nyumbani,” anasema dada huyo.

Baada ya kumkosa, wauaji hao waliwaamuru wapangaji watoke ndani na baada ya kufanya hivyo, waliichoma nyumba hiyo moto.

Diwani wa Mjawa, Ramadhani Chepa anasema wenyeviti wa vijiji vyote saba wametorokea mafichoni na shughuli za Serikali zimesimama.

“Huduma zote za Serikali za mitaa zimesimama kwa sababu vikao vya maendeleo ya kata havifanyiki,” anasema Chepa.

Diwani huyo anasema ofisi ya Serikali ya kijiji hicho haijafunguliwa kwa miezi mitatu.

Ofisa mtendaji wa Kata ya Umwe wilayani Rufiji, Adam Mkumbaamani, pia amekimbia makazi baada ya kupata vitisho vya kuuawa mara mbili.

“Tishio la kwanza lilikuwa Aprili 2, 2017. Walikuja watu wawili kati ya saa tano na saa saba mchana. Walimkuta mke wangu mkubwa akawaambia sipo. Nilikuwa kwa mke mdogo, nikajiuliza kama ni watu wema kwa nini wasije ofisini,” alisema Mkumbaamani aliyezungumza na Mwananchi akiwa mafichoni.

“Aprili 15, 2017 walikuja tena usiku tukiwa tumelala, wakagonga mlango nusura ya kuuvunja. Kumbe wanafuatilia sana, maana gari yangu niliilaza kwingine tofauti na nilipolala, lakini wakajua. Nilitoa taarifa kitengo maalumu cha polisi.”

Mahudhurio shuleni yashuka

Hofu hiyo haijaathiri ofisi za Serikali za mitaa pekee. Shule nazo zimepata pigo.

Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) wilayani Kibiti, Hamza Malwile anasema wanafunzi wa shule za msingi za Jaribu na Uponda zilizopo katika Kata ya Mjawa, wamekimbia pamoja na wazazi wao.

Anasema hali hiyo imesababisha mahudhurio mabovu katika shule hizo ambazo zipo katika eneo ambalo askari tisa waliuawa baada ya kushambuliwa, akiwamo aliyekuwa ofisa upelelezi wa Wilaya ya Kibiti, Peter Kubezya.

Anasema baada ya kumalizika kwa likizo fupi, ni wanafunzi 46 tu kati ya 2,487 wa Shule ya Jaribu walioripoti shuleni, wakati Uponda yenye wanafunzi zaidi ya 1,000, ilipata wanafunzi wasiozidi 150 siku hiyo.

Lakini hali hiyo pia imewakumba walimu ambao wametoweka kutokana na kile wanachodai kuwa ni polisi kunyanyasa wananchi na watumishi wa umma.

“Serikali iangalie namna ya kuondoa changamoto hiyo kwa kukaa pamoja na wananchi wa maeneo haya ili warejee,” alisema Malwile.

Hali hiyo inathibitishwa na Mratibu wa Elimu wa Kata ya Mjawa, Sylvester Mbata.

“Baada ya kuuawa wale askari, hali haikuwa mbaya sana kwa walimu na wanafunzi kwa kuwa waliendelea kuhudhuria na kufundisha. Lakini ujumbe ulioachwa na wauaji baada ya jaribio la kuchoma kigango cha Kanisa Katoliki, umeongeza hofu kwa watumishi,” anasema Mbata.

Wahalifu hao waliacha ujumbe unaosomeka: “Tunatoa tahadhari, mmewaua ndugu zetu wawili siku ya Jumamosi na sisi leo tunaanza kazi kuanzia ngazi ya vijiji, kata na hata wilaya. Walimu madaktari, manesi watendaji wa vijiji na kata na taasisi zote.”

Malwile alisema walimu wamekuwa wakitaka ushauri wafanye nini kuchukua tahadhari.

Afya

Hofu hiyo pia imeathiri huduma za afya. “Huduma ya zahanaji inapatikana, lakini mganga mfawidhi ameshaomba kuhama kwa sababu ametishiwa kuuawa,” anasema Chepa, ambaye ni Diwani wa Mjawa.

“Zamani alikuwa anaishi hapa kijijini lakini sasa ameondoka kwa hiyo huduma ya saa 24 hazipatikani tena.”

Alipotafutwa katika zahanati hiyo, daktari huyo, Abdallah Mbonde alikataa kuzungumzia vitisho hivyo akisema taarifa zake ameshazipeleka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kibiti na katibu wa Idara ya Afya wa wilaya.

Diwani Chepa alisema kwa sasa wanategemea ulinzi wa Jeshi la Polisi na kikosi maalumu cha ulinzi kilichoweka kambi Kijiji cha Bungu.

Lakini Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Rufiji, Rashidi Salum alisema kazi zinaendelea kama kawaida.

“Unajua hili ni suala tete sana, lakini sisi kama Serikali hatuwezi kusema tumeshindwa. Watumishi na wananchi kwa ujumla wanaishi kwa wasiwasi kwa usalama wao. Kwa kiasi fulani kuna athari ya ufanyaji kazi hasa maeneo ya vijijini, wananchi wanahofia kufanya shughuli zao, wafanyabiashara wana hofu, lakini wanaendelea hivyohivyo,” alisema Salum.

Lakini akasema Serikali imeongeza ulinzi katika ofisi za Serikali.

“Ungegeuka tu ukaona hata hii ofisi yangu inavyolindwa utakubali. Kwa hiyo shughuli hazijasimama, zinafanyika kwa tahadhari.

Kauli yake inalingana na ya Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Sekondari ya Ikwiriri, Said Omar aliyesema mahudhurio hayajaathirika.

Biashara zaaathirika

Sekta ya biashara nayo imeathiriwa na hofu hiyo. Moja ya makundi yaliyoathirika, ni ya wafanyabiashara wadogo waliokuwa wakifanya shughuli zao usiku au kukesha.

Kabla ha hali kubadilika, Amina Salum, mama lishe wa Ikwiriri, aliuza hadi kilo tatu za mchele.

“Biashara yetu ilikuwa inaanza saa 12:00 jioni, lakini hatuwezi tena,” alisema Amina aliyekuwa akitegemea madereva wa malori yanayotoka Kiwanda cha Saruji cha Dangote.

Hata shughuli za shamba sasa hazifanyiki.

“Utakwendaje shamba wakati kuna vitisho vya kuuawa? Tunasikia wanafanyia mazoezi porini, kwa hiyo unaweza kukutana nao,” anasema Juma Msati, mkulima anayeishi Kijiji cha Mpalage.

Mtoto auawa kinyama, ang'olewa Sehemu za Siri na Macho

$
0
0

Katika hali isiyokuwa ya kawaida mtoto wa miaka 12, Dorcas Meshak mkazi wa kitongoji cha Mbughantigha kijiji cha Matongo tarafa ya Ikungi, ameuawa na watu wasiojulikana na kunyofolewa baadhi ya viungo vyake.

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Kaimu Kamanda Jeshi la Polisi mkoani hapa, SSP Isay Mbugh alisema Mei, 18 mwaka huu saa sita mchana wakati ambao Dorcas alipoondoka nyumbani kwao kwa lengo la kwenda shambani kuchuma mahindi, umbali wa kilometa 70.

Alisema mtoto huyo amenyofolewa macho yote mawili, kukatwa matiti yote na kuondolewa sehemu zake za siri.

“Mtoto Dorcas hakuweza kurudi nyumbani kitendo kilichosababisha ipigwe yowe ili watu wakusanyike kwa ajili ya kumtafuta. Haikuchukua muda mrefu, mwili wa Dorcas ulikutwa ukiwa umenyongwa hadi kufa kwa kamba ya ngozi,” alisema.

Alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa mauaji hayo yanahusishwa na imani za ushirikina na hadi sasa hakuna watu waliokamatwa kuhusiana na mauaji hayo.

Katika tukio la pili, Kaimu Kamanda Mbugh, alisema watu wawili wamepoteza maisha kufuatia kutokea ajali ya gari anina ya Noah, tukio ambalo lilitokea Mei, 20 mwaka huu saa 6.45 mchana huko katika kijiji cha Mwaja tarafa ya Unyankumi Manispaa ya Singida.

“Ajali hiyo imehusisha noah T.402 DFH iliyokuwa ikiendeshwa na Said Shaban (33), na chanzo cha ajali ni mwendo kasi kitendo kilichosababisha ashindwe kulimudu. Waliofariki kwenye ajali hiyo,ni Elia Daniel (34) mkulima kijiji cha Mwankoko na mwanamke mmoja ambaye jina wala makazi yake,hayajafahamika,” alisema.

Aidha, aliwataja majeruhi wa ajali hiyo kuwa ni Mratibu Elimu kata ya Mtamaa, Nicodem Elias (45), Juma Ramadhan, mwalimu Chuo cha Maendeleo ya Wananchi, Elia Bilau mkulima na mkazi wa Magungumka Kapela Donad (28).

Kaimu kamanda huyo, alisema dereva wa Noah hiyo Said Shaban anashikiliwa na Jeshi la Polisi na upepelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Msichana amkata uume mtuhumiwa aliyembaka

$
0
0

Mwanamke mmoja nchini India amezikata sehemu ‘nyeti’ za mwalimu wa dini katika jimbo la kusini la Keral kwa kudai kuwa alimbaka kwa miaka mingi.


Polisi wamesema kuwa mtuhumiwa anayejulikana kama Gangeshananda Theerthapada alikuwa akizuru katika nyumba ya mwanamke huyo ili kumfanyia matambiko ya ibada baba ya mwanamke huyo aliyekuwa mgonjwa.


Mama yake alikuwa na matumaini kuwa mtuhumiwa huyo aliyejidai kuwa mtakatifu ataiondolea familia hiyo matatizo. Badala yake alikuwa akimbaka msichana huyo mwenye miaka 23 kila anapotembea nyumba hiyo.


Ijumaa iliyopita alichukua kisu na kumshambulia alipojaribu kumbaka na baadaye akaita maofisa wa polisi. Mbakaji huyo alikimbizwa hospitalini ili kufanyiwa upasuaji wa dharura

JE Dada Unapenda Kuwa Mrembo? Na Kaka Unapenda Kuwa Mtanashati na Kurudisha Heshima ya Ndoa?

$
0
0

JE, DADA UNAPENDA KUWA MREMBO? NA KAKA UNAPENDA KUWA MTANASHATI NA KURUDISHA HESHIMA YA NDOA? Tumia Bidhaa halisi za MARKSON kwa mafanikio ya uhakika na bila madhara.
Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kuthibitishwa kiafya.
🍉🌿🍓🍒🎄🍍🍀🍓🍉
Pata hizi 👇👇👇👇👇👇

1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @120,000/=
2. Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa (a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge @180,000/=
3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @120,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa :-
(a) Gely ya kupaka @130,000/=
(b) Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @130,000/= (c)Handsome up (mashine) original @200,000/=
6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @120,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @120,000/=
8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/=
(b)Mkanda wa kawaida @100,000/=
(c)Mkanda wa umeme @200,000/=
9 .Kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120,000/=
10.Kushepu miguu na kuwa minene na kuondoa migimbi @120,000/=
11.Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @100,000/=
12.Kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @120,000/=

NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Wasiliana nasi :-
(+255) 0767447444 na
0714335378
👉🏻Ili kuona bidhaa zetu na baadhi ya shuhuda za waliotumia bidhaa zetu
Follow us on instagram
👇👇👇👇👇👇👇👇👇
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

Ruge Ajibu Baada ya Kuambiwa na Makonda Kuwa na Mtunga Nyimbo za Mapenzi na Ngonjera

$
0
0

Mkurugenzi na mzalishaji wa vipindi waClouds Media Group, Ruge Mutahaba, ameijibu kauli iliyotolewa na Mkuu wa mkoa wa Dar Dar es salaam, Paul Makonda ya kuwa yeye ni muongo, na anafaa tu kuwa muandishi wa mashairi na nyimbo za mapenzi na ngonjera.


Ruge ametoa kauli hiyo leo katika kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na kituo hicho, ambapo walikuwa na kipindi cha ‘SHUKRANI’ kwa wasikilizaji wao na watu waliowahi kuwasaidia kupata misaada.


“Kila mtu ana mtazamo wake, na huwezi kulazimisha mtazamo wa mtu ubadilike. Inasikitisha sana kuona mtu anayesambaza haya mambo ni bosi wangu, Bosi wa mkoa wetu. Yeye akipiga mhuri kitu ndio imekaa hiyo, Yeye ana nguvu zote,” amesema Ruge.


“Sasa akisema hivyo mimi ni tapeli anataka kila mtu Dar es Salaam anione hivyo. Mimi sina nguvu kwa hiyo nachagua kubaki kwenye ninacho kiamini. Tangu mwanzo nilisema mimi nataka haya mambo yaishe, cha kusikitisha huyu mtu ni kiongozi lakini anashindwa kumaliza jambo hili kwa busara na anataka kuliendeleza.


“Kuna mambo hapa yanajaribu kutengenezwa. Watu wanajaribu kutusukuma turudi kwenye mjadala ambao tulishaumaliza. Mimi ni mtu mzima , na busara inaniambia watu wazima hatuna haja ya kurudi kwenye majibizano ambayo kwangu yaliisha siku nyingi “alieleza Ruge.

SAKATA la Vyeti Feki Lasababisha Uhaba wa Wauguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili...!!!

$
0
0

HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili inakabiliwa na upungufu mkubwa wa wauguzi uliosababishwa na kuondolewa kwa wauguzi 60 waliokutwa na vyeti bandia vya elimu ya sekondari.

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru alisema jana kuwa hali hiyo imeathiri zaidi vyumba vya wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU), ambavyo vinahitaji zaidi wauguzi kwa ajili ya kutoa huduma kwa wagonjwa hao.

Alisema hayo jana wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani, na kutaja sakata hilo kuwa miongoni mwa changamoto zinazoikabili hospitali hiyo.

“Hospitali yetu imepungukiwa na baadhi ya wauguzi walioondoka wenyewe kwa kuwa na vyeti bandia,” alisema.

Pamoja na upungufu huo, aliwataka wauguzi wafanye kazi kwa kufuata maadili ya taaluma, kuwa na nidhamu na tabia njema na kuwaonya  wachache wanaochafua taswira ya uuguzi.

Aliagiza kila muuguzi awe na kitambulisho cha kazi kwa ajili ya kutoa huduma na kuwataka waheshimu taaluma yao.

“Mnapaswa kutumia lugha nzuri kwa wateja wetu ambao ni wagonjwa, mtoe maneno yanayostahili ili kutowakwaza maana yanasemwa kuwa baadhi ya wafanyakazi hawana lugha nzuri,” alisema Profesa Museru.

“Hivyo wauguzi mshiriki kuongeza mapato ya ndani ambayo yatakayosaidia kulipa baadhi ya madai na kuhusu suala la sare tunalifanyia kazi ili kila muuguzi apewe,” alisema Museru.

Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga wa Hospitali hiyo, Agnes Mtawa alisisitiza kuwa wauguzi wote wanatakiwa kuwa na leseni ya kazi.

Alisema kitambulisho hicho ndicho kitakachowawezesha kutoa huduma  kwa wagonjwa na atakayekiuka, atakuwa hatarini kukabiliwa na kifungo cha miaka mitano jela au faini ya Sh milioni tano.

Agnes alisema wauguzi wengi hufanya kazi bila leseni hali ambayo ni kinyume na sheria ya utoaji huduma kwa wagonjwa.

“Hivyo sheria hii itachukua mkondo wake kwa kila muuguzi atakayekwenda kinyume, kwa kutokuwa na leseni ya utoaji huduma kwa wagonjwa,” alisisitiza Agnes.

POLISI: Mauaji ya Kibiti, Rufiji Hayajapoteza Amani..!!!!

$
0
0

KAMISHNA wa Mafunzo na Operesheni wa Jeshi la Polisi Tanzania, Nsato Mssanzya, amesema matukio ya uhalifu yanayoendelea maeneo mbalimbali nchini, hasa Kibiti na Rufiji yasitafsiriwe kuwa Taifa limepoteza amani.

Aidha, amesema watu wanaouawa wasihusishwe na vyama vya siasa, kwani hakuna taarifa zinazoonesha kuuawa kutokana na vyama vyao, kwani matukio ya uhalifu yako duniani kote.

Mssanzya  alisema Jeshi la Polisi limejipanga kila kona kuhakikisha amani inadumu nchini, akieleza kwamba matukio yanayotokea si taswira sahihi ya kusema Taifa halina amani.

“Kila siku inayopita ni vigumu kutopata taarifa ya matukio ya uhalifu, hivyo hali hiyo isihusishwe na kukosekana kwa amani nchini, lakini pia si vema kuhusisha matukio hayo na siasa,” alisema.

Kamishna alisema hali ya usalama ni nzuri na hakuna mwananchi anayekosa amani.

Alisema wananchi katika maeneo yanayotajwa kuwa na uhalifu wananchi wanajihusisha na shughuli za uzalishaji hali aliyosema inatoa tafsiri ya uwepo wa amani.

Hata hivyo, alisema Jeshi hilo limejipanga kupambana na uhalifu bila kuangalia siasa au vyama, kwani wanaopoteza maisha ni raia wa Tanzania.

Alisema yanayotokea Kibiti na Rufiji ni matukio kama mengine na kinachotakiwa ni wananchi kutoa taarifa za viashiria vya uhalifu na matukio hayo kwa Jeshi hilo, ili liweze kuyafanyia kazi haraka.

Kamishna alisema matukio mengi yanayotokea Kibiti na Rufiji yamekuwa yakitokea vijijini, ambako hakuna polisi tofauti na ilivyo mijini na kwamba kinachohitajika ni taarifa za haraka.

Kamishna aliwataka wananchi kushirikiana na Jeshi hilo kufanikisha kukamata wahusika, ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

IMEFICHUKAA..Hiki Hapa Ndio Chanzo cha Wazazi Waliofiwa na Watoto Wao Ajalini Arusha Kujitoa Kwenye Kamati ya Gambo..!!!

$
0
0

Wazazi waliokuwepo kwenye kamati ya rambirambi ya msiba huo iliyoundwa na Mkuu wa mkoa wa Arusha wamejitoa rasmi katika kamati hiyo.

Kwa mujibu wa mzazi huyo ambaye hakutaka jina lake linukuliwe ameeleza Sababu kubwa ya wao kujitoa kwamba ni kitendo cha kutumika nguvu ya dola hasa wakati ambapo kulikuwa na ibada ya kupewa pole na rambirambi , ibada ambayo haikufanyika kutokana na kuvamiwa na Jeshi la Polisi na kukamatwa Meya wa jiji la Arusha mh. Kalisti Lazaro ,Katibu wa TAMONGSCO kanda ya Kaskazini Mh. Leonard Mao , Waandishi wa Habari 10 , pamoja na wamiliki wa shule binafsi waliokuwepo katika hafla hiyo.

TUMEKWISHA..! Waziri wa Viwanda, Charles Mwijage Asema Ukiwa na Vyerehani Vinne Hicho ni Kiwanda..!!!

$
0
0

Waziri wa viwanda na  biashara Mhe Charles Mwijage Amesema Kuwa dhana ya viwanda ni pamoja na mtu mwenye kuwa na uwezo wa kumiliki hata cherehani nne na akajisajili basi huyo atafahamika kuwa anamiliki kiwanda.

Je wewe unamtazamo gani juu ya hili...!!!?

UBUYU wa Motomoto...Huyu Ndiye Waziri wa Magufuli Anaye Banjuka na Msanii Batuli..!!!

$
0
0

UBUYU ulionyooka kabisa umetua kwenye meza ya gazeti hili ukidai kuwa, waziri kijana katika serikali ya Rais Dk.John Magufuli ‘JPM’, amedata kinomanoma na penzi la msanii wa filamu Bongo mwenye shepu bomba, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’, Ijumaa lina full stori.

Awali zilivuja taarifa kuwa, waziri huyo wa wizara nyeti ambaye ni mume wa mtu (jina lake linahifadhiwa kwa sasa) kafa, kaoza kwa mrembo huyo ambaye ni kada wa CCM na hivyo ameamua kumng’arishia maisha yake ili aweze kumfaidi vizuri.

KISIKIE CHANZO

“Kama ni kuyapatia maisha, Batuli sasa hivi kayapitia maana mheshimiwa….(anamtaja jina) ndiyo kajiweka kwake sasa hivi, anamhudumia kwa kila kitu, ndiyo maana unamuona mambo yake sasa hivi supa kuliko hata mastaa wengine,” alimwaga ubuyu mtoa habari huyo kisha akaongeza: “Kampangishia mjengo kule Kunduchi na ndinga pia kamnunulia, nyie fuatilieni mtajua ukweli wa ubuyu huu ninaowapa.”

IJUMAA KAZINI

Baada siri hiyo kuvuja, mmoja wa waandishi wetu alimpigia simu Batuli na kumuuliza juu ya madai hayo ambapo alifunguka kuwa na uhusiano na mheshimiwa huyo ila akasema, hayo si mambo ya kuandikwa gazetini kwani ni maisha yake binafsi li kujiridhisha na habari hiyo, siku nyingine mwandishi mwingine alimpigia simu na kutaka kuonana naye kwa ajili ya mahojiano maalum ambapo, siku hiyo alimtaka paparazi huyo wakutane Bahari Beach, eneo la Bakery, Kunduchi jijini Dar.

Mwandishi alipofika eneo hilo, aliona gari la kifahari, Range Rover Discovery lenye rangi nyekundu na kulifuata, ambapo Batuli alimfungulia mlango na kuondoka eneo hilo huku wakiendelea na mazungumzo.

Licha ya kuzungumza mambo mengi siku hiyo, huku mwandishi wetu wakati mwingine akimrekodi, staa huyo alimtaja mheshimiwa huyo kuonesha kuwa ndiye
anayemuweka mjini.

SIKU ILIYOFUATA

Siku iliyofuata, mwandishi wetu alipotaka kuandika habari hii alisikiliza rekodi katika maelezo ya Batuli na akaamua kumpigia simu tena ili kujiridhisha pale alipomtaja mheshimiwa huyo kuwa ndiye anayemuweka mjini ambapo hakutaka kulizungumzia tena. Hata hivyo, mwandishi wetu alimtumia ujumbe mfupi wa maandishi uliosomeka hivi; “Batuli, wakati tunazungumza kabla ya ishu nzima, ulitamka mtu uliyenaye ni (jina la waziri)…” Batuli alivyojibu “Hilo siyo geni hapo kwenu (Global) kwa msaada muulize (akimtaja mmoja wa waandishi wetu aliyewahi kuongea naye)…”

IJUMAA KWENYE MJENGO ANAOISHI BATULI

Katika kuendelea kuchimba, hivi karibuni mapaparazi wetu walifika kwenye nyumba anayoishi Batuli iliyopo Kunduchi (Uzunguni) lakini baada ya kugonga geti alitokea mlinzi na kueleza kuwa, ni kweli staa huyo anaishi hapo ila hawezi kupatikana hadi mtu anayemhitaji awe na miadi (appointment) naye.

IJUMAA LAMSAKA WAZIRI

Katika kubalansi habari hii, waandishi wetu walitumia kila njia kumpata mheshimiwa huyo lakini hakuweza kupatikana hivyo linaendelea kumsaka ikiwa ni pamoja na kuhakikisha linamnasa akiingia kwenye mjengo anaoishi Batuli kisha tutawamwagia kila kitu hapahapa.

From GlobalPublisher

Sirro: Naomba Uongozi wa Clouds Media Utoe Ushirikiano Uvamizi

$
0
0

Dar Es Salaam. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam, Simon Sirro amewataka uongozi wa Clouds Media Group kushirikiana na jeshi la polisi katika upelelezi wa tukio la uvamizi wa kituo chao cha matangazo.
Akiongea na waandishi wa habari leo Sirro amesema kesi yoyote inahitaji ushahidi na uvamizi wa Clouds bado upelelezi wake unaendelea ukikamilika utapelekwa kwa wakili wa Serikali ili aone kama anaipeleka kesi hiyo mahakamani au kutoipeleka. "Ndugu zetu wa Clouds watoe ushirikiano kwa mpelelezi wa kesi yao, wao wanataarifa za kutusaidia kukamilika kwa upelelezi ila nasi tuweze kuipeleka katika hatua inayofuata. Na sio kwamba tukio limesahaurika bali upelezi wake unaendelea," amesema Sirro.
.
TOA MAONI YAKO HAPA

NOMA Sana..Wakati Watu Wakipiga Kelele..Serikali ya JPM Yashusha Bongo Kivuko Hiki Kipya Kimya Kimya..!!!

$
0
0

 Kivuko cha Mv Kazi  kimefanyiwa majaribio ya kubeba abiria na magari kwa mara ya kwanza leo (Jumatatu) baada ya matengenezo kukamilika.

Majaribio hayo yamefanyika kulingana na sheria na utaratibu wa vyombo vya majini ambayo inavitaka kufanyiwa majaribio kabla ya kuanza kazi ili viweze kupatiwa cheti cha ubora.

Awali, wataalamu kutoka Chuo cha Ubaharia Dar es Salaam (DMI) walipima ubora na uimara wa kivuko hicho kwa kutumia utaratibu wa kuweka mawe yenye kilo zinazolingana na uwezo wa kivuko na magunia ya mchanga ili kupima uwezo wa kivuko kulingana na mahitaji yaliyoainishwa kabla hakijabeba abiria na mizigo.

Taarifa ya Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa) imesema kazi hiyo ilifanyika kwa kipimo cha kuhakikisha kuwa kivuko hakilali upande mmoja na kilionyesha kivuko kiko sawa. Taarifa ya kazi hiyo itakuwa sehemu ya vitu vya makabidhiano wakati wa upokeaji wa kivuko.

Miongoni mwa waliokuwapo kushuhudia majaribio hayo alikuwa mkuu wa vivuko Magogoni/Kigamboni, Mhandisi Lukombe King’ombe ambaye alisifu uwezo wa kivuko hicho na kuwataka wakazi wa maeneo hayo kuhakikisha wanakitunza kivuko hicho kwa kuwa kitawasaidia kupunguza msongamano wa abiria na magari hasa asubuhi na jioni.

Kivuko hicho kitaongeza idadi ya vivuko kufikia vitatu vitakavyotoa huduma ya kuvusha abiria na magari katika eneo la Magogoni/Kigamboni.

Ujenzi wa kivuko cha Mv Kazi umegharimu Sh7.3 bilioni na kina uwezo wa kubeba abiria 800 na magari 22 sawa na jumla ya tani 170. Kivuko hicho kitakabidhiwa rasmi hivi karibuni kwa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa) kwa ajili ya kuanza kutoa huduma.

BILA Unafiki; Makonda Leo Sikutegemea Haya Ungeyafanya Wewe Ukiwa Live Star Tv..!!!!!

$
0
0

Nirudie bila ya Unafiki kiukweli leo nilikerwa na kushindwa kuendelea Kutazama kipindi cha Tuongee Asubuhi mwanzo mwisho.
Nilipatwa na Hasira kupelekea kuzima Tv na kuingia mtaani kutokana na Kile nilicho kishuhudia machoni mwangu japo ni kutoka Luningani!!

Hivi ilikuwaje Makonda ukubari kwenda /Kualika Tv kukuhoji ikiwa haukuwa Tayari!!?

Makonda Hivi Unajiamini vipi kucheka hovyo Ukiwa live tena kwamadharau Wakati ukitambua Unayo hojiwa ni mambo makubwa na si Masihala kabisa!!

Makonda unatambua wewe unapelekea kutukanwa kwa Rais wetu kipenzi na mtetezi wetu
unapata nafasi ya walau kututoa kimasomaso lakini bado unaweka petrol kwenye moto ulio kolea kweli!!

Nilipo sikia na kuona matangazo kupewa nafasi ya kueleza mbivu na Mbichi kuhusu Tuhuma zote ulizo elekezwa kwako
Nilipata nguvu kujua Sasa Star Tv wana jaribu kufuata utaratibu murua kumhoji mtu kabla ya kumtuhumu na kumuadhibu
lakini kiukweli niheri ungeendelea kukaa kimya kabisa!

Yaliyo tokea leo Yamekurudisha Nya 40% kuliko ulivyo kuwa Hapo jana na kuendelea nyuma.

Makonda kumbuka,Katika hii Dunia Mazuri 100 hupotezwa na baya moja(1) pekee
Tunafahamu unamengi Mazuri lakini Jichunge sana na Baya moja litakalo haribu mema yote.

Nini kilinikera leo!
1. Makonda hakuheshimu Mwenyekiti wa Mjadala ule,
Kweli yeye ni Mkuu wa mkoa
lakini pale alikuwa akihojiwa kama Makonda binafsi na Mkuu wa mkoa kama Wadhfa wake kama Tuhuma zilivyo elekezwa kwake,
kitendo cha Kumdharau Muongoza mjadala ni Upuuzi na Haliwezi kukubalika.

2. Kuchagua lipi uulizwe na lipi usiulizwe!!
Unaulizwa swali unatoa maelezo Yasiyo Endana na swali husika
Yasiyo endana na Kile tulicho Ambiwa au kuelezwa hapo awali kama lengo kuu la mjadala huo,
Nacho kifahamu ilikuwa utaulizwa maswali yoote na utayatolea ufafanuzi kulingana na tuhuma zako.

3. Makonda unacheka kwa dharau,kwa kejeli wakati wafahamu mahojiano hayo yapo live
kuna maelfu ya Watanzania wakitaka kujua je unaonewa au la!

4. Ulishindwa kujizuia na kutambua kuwa pale upo kama Makonda 90% sio kama Mkuu wa mkoa
mahojiano yale yalikuwa kujibu tuhuma kwa 80% sio kuelezea Nini kinaendelea mkoani kwako
kiasi kwamba Unakuwa mkali mpaka kuita watu Wanafiki!!
Kama hukuhitaji Mahojiano yale kwanini ukubari kuhojiwa!!?

5.Tunajua Aliye kuteua ni Kikwete
Ulipewa tuhumu ya kumpiga Warioba
lakini Jk aliona sio kweli na hata kama kweli ulikuwa sahihi hilo silihoji
ila Jk Akakuteua Kuwa mjumbe wa bunge la Katiba,
Haikutosha Jk akakuteua kuwa mkuu wa Wilaya,
Rais wetu akakuteua kuwa mkuu wa mkoa,
Hili halikufanyi Uchague swali lipi uuluzwe na mengine watu waende Kwa mamlaka zilizo Kuteua.
6. Unaonyeshwa picha ya Jumba na Gari
unakubari Vyako
lakini hutoi maelezo yeyote umevipataje!!
Kwa umli wako huo wa utumishi!!
Zaidi unakimbilia kutoa Kejeli,Dharau Kujiona!!

Bila kumung'unya maneno
Leo Makonda umenikera sana sana
nibora Ungegoma tu kuliko upuuzi huu ulio ufanya.

Star tv hawana lawama yeyote
wamefanya kile kinacho takiwa kufanywa,
Tuwape hongera kwa hilo.

NB
Haya ni maoni yangu binafsi
Tuache unafiki leo Jamaa Katia Doa Mahojiano yale

Credit Jamii Forum

PAMOJA na Kukosa Ubingwa ..Haji Manara Aendelea Kuikejeli Yanga..!!!

$
0
0

Msemaji wa Klabu ya Simba aliyefungiwa na TFF, Haji Manara amefunguka mengine mapya kwa kudai bado hajakubaliana na ubingwa wa ligi kuu Tanzania walioutwaa Yanga SC na kudai kuwa wao (Simba SC) ndiyo mabingwa wa ligi hiyo msimu huu.

Manara amebainisha hayo kupitia mitandao ya kijamii kwa kurusha vijembe kwa wapinzani wao wa jadi na kudai kwamba kama Serengeti Boys waliweza kushinda rufaa yao na kuweza kushiriki michuano ya vijana huko nchini Gabon basi nao watashinda bila shika.

"Wabongo bana kwa 'double standard' hawajambo, Serengeti Boys walikuwa Gabon kwa kushinda rufaa ila Simba hawastahili....Mjiandae kiakili Gongowazi, Simba ndiyo 'champion' msimu huu". Ameandika Manara

Tayari Simba imewasilisha malalamiko yao kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) wakipinga kupokwa pointi 3 na TFF baada ya kupewa na bodi ya ligi kutokana na Kagera Sugar kumtumia mchezaji asiyestahili katika mechi dhidi yao, ambapo Kagera Sugar ilipata ushindi wa mabao 2-1.

HUYU Ndiye Ruge Ninayemfahamu...!!!!

$
0
0

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni! Hata kama kwa ubinadamu wetu tutatashindwa kusimama na huyu ndugu hususan kwa kipindi hiki yupo Mungu aliye hai atamtetea. 

Ndio, Hakuna binadamu asiye na mapungufu, Ruge kama binadamu inawezekana ana mapungufu yake lakini katika hili suala la Clouds Vs "Yule Bwana" kwa binadamu mwenye akili za kawaida tu utakubaliana nami kwamba Ruge ameonyesha hekima na busara ya kiasi cha juu sana.

Alichoamua Kukisimamia Ruge ni kusema UKWELI, Ukweli kwamba "Yule Bwana" alikosea, pamoja na kwamba walikuwa marafiki lakini Ruge aliamua kusimama katika misingi ya ukweli, misingi ya kikazi, Kwamba "Yule bwana" alikosea. Kuna vitu wala havihitaji degree kuvielewa, yaani kule tu kwenda pale tena usiku tena na silaha bila mhusika kujua, na bila warrant ni kosa kisheria.

Leo baada ya kumsikia Ruge akijibu shutuma za "Yule Bwana" nimejisikia amani sana, Maana badalaa ya kujibu kwa jaziba, kwa matusi, kwa mhemko, Ruge kajishusha kaongea kwa ustaarabu kama binadamu, Pamoja na kuambiwa hana akili, anaimba ngonjera, na maneno mengine mengi ya kuudhi lakini jamaa kajibu ki proffesional na kwa unyenyekevu. U have my respect brother.

Mi nafikiri kama taifa kama tunakuwa na viongozi wa namna hii, ambao wanashindwa kuwa na akiba ya maneno na kuongea tu kama vijana wa mtaani bila kuangalia kuwa kuna watu wengi sana tunawaangalia ili kujifunza kwao, tutakuwa tunaelekea pabaya sana.

ARUSHA: Millioni 18 za Rambirambi za watoto wa Lucky Vicent bado zinashikiliwa na Polisi...!!!

$
0
0

Mapema leo Saa 9:30 Am waliripoti kituo kikuu cha polisi (Central Police) Arusha Meya wa jiji la Arusha Mh. Kalisti Lazaro , Katibu wa TAMONGSCO Kanda ya kaskazini Mh. Leonard Mao, mkuu wa shule ya Lucky Vincent ,na viongozi wengine kwa lengo la Kukabidhiwa fedha kiasi cha 18 Millioni ambayo ilikuwa rambi rambi kwa ajili ya ajali ya Lucky Vincent au kutajwa kesi inayowakabili viongozi hao na kufikishwa mahakamani viongozi hao endapo wangebainika na kosa.

Sawia na hilo nikamtafuta Meya Kalisti Lazaro kwa njia ya Simu ambapo alisema "Nimewasili central nikaambiwa turipoti ijumaa" Kalisti Lazaro

Kuhusu Fedha za rambi rambi
"Fedha zipo kwa OCD pamoja na simu yangu" Bw. Mao

Akizungumza kuhusu fedha hizo pamoja na tukio nzima la kukamatwa viongozi hao pamoja na Waandishi wa habri Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha RPC Mkumbo alisema "Bado sijui chochote kuhusu hizo fedha pamoja hatua zinazoendelea dhidi ya viongozi hao akiwemo Meya

Nay wa Mitego amjibu Mwakyembe

$
0
0

Rapa Nay wa Mitego amefunguka na kumtaka Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe kutoa ufafanuzi juu ya kauli yake aliyotoa kuwa wasanii wasijihusishe na masuala ya siasa.

Nay wa Mitego akiongea kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio, amesema kuwa yeye anaamini muziki ni siasa na siasa ni muziki hivyo ni ngumu kutofautisha vitu hivyo viwili, hivyo amemuomba Waziri mwenye dhamana kutoa ufafanuzi juu ya kauli hiyo na kudai yeye hajawahi kuimba wimbo wa siasa bali anaimba mambo yaliyopo kwenye jamii.

"Nachoamini mimi muziki ni siasa na siasa ni kama muziki, siasa ni maisha ya watu ambayo wanaishi kila siku na muziki pia ni maisha ya watu ambayo wanaishi kila siku kwa hiyo anahitaji kutoa ufafanuzi wa kutosha juu ya hili. Siasa ni maisha ya watu na muziki ni maisha ya watu, mimi binafsi naamini sijawahi kuimba wimbo wa siasa hata siku moja bali ninaimba maisha ya watu ambayo yanaendelea kila siku na ndiyo maana wengi wanathubutu kusimama upande wangu endapo linatokea tatizo lolote" alisema Nay wa Mitego.

Mbali na hilo Nay aliendelea kusisitiza kuwa kuna haja Waziri kutoa ufafanuzi wa jambo hilo
"Mh. Waziri anatakiwa kutoa ufafanuzi juu ya jambo hili ili watu wajue kipi hawatakiwi kuimba na kipi wanatakiwa kuimba sababu siasa ni maisha ya watu ya kila siku na muziki wa Hip hop ni maisha ya watu ya kila siku, kwangu mimi muziki wangu hauwezi kubadilika zaidi nitazidi kuongeza vitu ili nisiwaudhi watu na nizidi kuongeza idadi ya mashabiki" alisisitiza Nay wa Mitego

Zijue Tabia 7 Za Wanawake Wanao-Cheat Kwenye Mahusiano

$
0
0

Kama mke wako, demu wako au side chick wako ana tabia zifuatazo, amesha-cheat kwako au ipo siku ataku-cheat.

1) Ana boreka haraka – Wanawake wanaoboreka haraka nirahisi kutafuta mwanaume mwingine wa kum-entertain, muda sio mrefu huyo mwanaume atachoka kum-entatain rafiki asiye na faida na ndio hapo atakapo anza kudai faida zake na wanaishia kuwa friends with benefits.

2) Marafiki wengi wa kiume – Mwanamke mwenye marafiki wengi wa kiume ni rahisi ku-cheat kwasababu anapata muda mwingi wa kuongea na wanaume wengine, watamsifia anavyopendeza, kama wewe unamwambia amependeza mara moja kwa wiki basi wenzako watamwambia anapendeza kila wanapoonana. Wataabza kumtoa out na mwisho wake ataona hao wanaume wamanjali kuliko wewe na kulala nao.

3) Anapenda attention – Wanawake wanaopenda attention ni rahisi kudanganyika. Wanaume wengi hasa ambao hawataki kuwa committed kwenye mahusiano yoyote wanatoa sana attention kwa wanawake. Mwanamke anayependa sana attention hawezi ridhishwa na attention ya mwanaume mmoja.

4) Anapenda vitu “material things”-Wanawake wengi wanaopenda material things wanashindwa kupata kila kitu kutoka kwa waume zao au maboyfriend zao na kuishia kutafuta mwanaume mwingine ambaye ana uwezo wa kumnunulia vitu anavyotaka ili awatese wenzake kwenye instagram.

5) Ana marafiki ambao ni michepuko –Umeshasikia usemi kuwa ndege wanaofanana huruka pamoja, hata kama demu wako hana tabia ya ku-cheat, akiwa anakaa sana na marafiki ambao wana-cheat na yeye atashawishika kujaribu. Kama mke wako au demu wako ana kupigia story za marafiki zake wanao-cheat mwambie aachane nao haraka sana.

6) Anapenda kufanya ngono kuliko wewe – kila mkimaliza kufanya tendo la ndoa mwenzako anakwambia anataka tena, na wewe humtimizii basi lazima tatafuta serengeti boy ambaye anamsikiliza na kumpa anachotaka.



7) Anaujuzi kitandani kuliko wewe – Wewe kama umeshawahi kuingia kwenye dancing floor na kucheza na mtu ambaye anajua kucheza kuliko wewe, unasubiria tu wimbo ukiisha ukakae chini kabla hujaaibishwa, au kama wewe ndio unayejua kucheza vizuri utatafuta mtu mwingine anayejua kucheza kama wewe. Kwenye tendo la ndoa ni hivyo hivyo kama mwenzako ana ujuzi kuliko wewe, inabidi ufanye mazoezi ufikie kwenye ujuzi wake la sivo muda sio mrefu atasubiri wimbo ukiisha akakae chini au atafute mtu mwingine anayejua kucheza kama yeye.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images