Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Shamsa Ford Amuoneaa Wivu Odama

$
0
0
Malkia wa filamu Bongo, Shamsa Ford ameweka wazi kumuonea wivu mahusiano ya muigizaji mwenzake, Jenipher Kyaka 'Odama' kwa kuyafanya kuwa na usiri mkubwa huku akipongeza na kusema ndivyo inavyopaswa mtoto wa kike kufanya kwenye mapenzi.

Shamsa amefunguka hayo na kusema anapenda jinsi muigizaji huyo anavyoweza kuweka mahusiano yake ya mapenzi kuwa faragha yake peke yake na kuongeza kuwa anatamani kama siku zingerudi nyuma asingethubutu kumuonyesha mpenzi wake hadharani bali mume wake wa ndoa.

"Napenda unavyoweka mahusiano yako ya mapenzi 'private'. Sijawahi ona hata siku moja umempost sijui boyfriend na hicho ndo kitu kizuri kwa mtoto wa kike. Mimi kwa upande wangu ningerudisha siku nyuma kipindi kile nipo single nisingempost au kumuweka wazi mwanaume yoyote niliyekuwa naye kipindi kile kwenye mahusiano. Natamani mume wangu ndio angekuwa mwanaume wa kwanza kwa watanzania kumjua" - Shamsa Ford alifunguka.

Rose Mhando Akamatwa na Polisi Mkoani Singida

$
0
0

Jeshi  la Polisi Mkoa wa Singida linamshikilia mwanamuziki mashuhuri wa nyimbo za injili, Rose Muhando akituhumiwa kujipati fedha kwa njia ya udanganyifu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Debora Mgiligimba alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo alisema mwimbaji huyo alikamatwa juzi Wilaya ya Ikungi baada ya wadeni wake ambao ni Waumini wa Kanisa la AICT Singida kupata taarifa kuwa yupo wilayani humo.

Inadaiwa kuwa Novemba 3 mwaka jana, mwimbaji huyo alitumiwa fedha na Mwenyekiti wa Kwaya ya Kanisa la AICT Singida, Mashala Japhet Tsh 800,000 ambapo zilitumwa baada ya pande mbili kukubaliana kuwa angekwenda kwenye uzinduzi wa Album ya kwaya na kanisa hilo, hata hivyo hakutokea.

Kwa mujibu wa kamanda huyo, uzinduzi wa kwaya hiyo ulikuwa ufanyike Novemba 13 mwaka jana, saa 8 mchana katika uwanja wa Namfua Singida.

Novemba 8 mwaka jana, mwimbaji huyo aliomba kutumiwa tena 150,000 kwa ajili ya nauli ya kutoka Dodoma kwenda Singida yeye na wasaidizi wake, fedha ambayo ilitumwa na mawasiliano yakaendelea kufanyika ili kuakikisha kuwa siku ya tukio anakuwepo.

Chakushangaza, siku ya tukio msanii huyo hakujitokeza na walipata taarifa kuwa yupo Kahama anatoa huduma, walipofanya mahojiano walithibitisha kuwa ni kweli.

Alipofanyiwa mahojiano na Polisi, Rose Muhando alikiri kutenda kosa hilo kwa kutotoa taarifa kwamba hawezi kuja na alieleza si kweli kwamba alikuwa kahama, bali alikuwa na mgonjwa nyumbani hivyo hakuweza kutoka. Muhando amesema kuwa yupo tayari kurejesha fedha hizo alizotumiwa.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Magazetini

Askofu Gwajima Ageuza Kibao Kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo Kwa Kuleta Siasa Msibani

$
0
0
Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima akiwa msibani Moshi amemshukia Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa kuleta siasa msibani huko Arusha ambapo alimzuia mbunge wa jimbo hilo Godbless Lema kutoongea.

Aidha Gwajima amesema jambo lililofanywa na viongozi wa serikali kukataza Uwanja wa Mashujaa kutumika kuaga mwili wa Marehemu Ndesamburo siyo jambo la busara hata kidogo huku nakimlaumu mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa kile alichokisema ni tetesi alizosikia kuwa alitoa maelekezo uwanja huo usitumike na badala yake vitumike Viwanja vya Majengo.

Yeriko Nyerere Akana Tuhuma za Uchochezi Facebook

$
0
0
MFANYABIASHARA, Yeriko Nyerere amekana mahakamani kutoa taarifa za upotoshaji kupitia mtandao wa Facebook, baada ya kusomewa maelezo ya awali katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.

Nyerere alisomewa maelezo yake jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri.

Wakili wa Serikali, Elia Athanas, alidai Oktoba 25, 2015 katika eneo lisilojulikana Dar es Salaam, Nyerere alichapisha taarifa za upotoshaji kupitia mtandao wa Facebook kuwa ‘piga kura leo huku ukikumbuka kifo cha Mwangosi, mateso ya Ulimboka na Kibanda, mateso ya kijana wetu wa JKT, ukikumbuka hayo fanya uamuzi sahihi bila ushabiki’.

Upande wa Jamhuri uliendelea kudai kuwa Oktoba 24, 2015 katika eneo lisilojulikana  Dar es Salaam, Nyerere alichapisha taarifa za upotoshaji kupitia mtandao wa Facebook kuwa Taifa la Tanzania kuanzia siku hiyo halihitaji amani, linahitaji haki tu.

Pia, Oktoba 24, 2015 mshtakiwa anadaiwa kuchapisha taarifa za uongo kupitia Facebook kuwa siku hiyo mpaka siku ya kuapishwa Lowassa Taifa halihitaji amani bali linahitaji haki tu, amani ilishatoweka siku nyingi, kilichosalia ni uvumilivu tu.

Pia alidaiwa kuchapisha taarifa za uongo kuwa njia sahihi ya kulitibu taifa hili ni kwa dola dharimu kutenda haki hata kama itawauma.

Ilidaiwa Nyerere aliandika kwenye mtandao huo kuwa “Uchaguzi huu ni vita, anayedhani ni demokrasia apimwe akili. Kwamba “hii ni vita kati ya umma na dola, ni vita kati ya wema na ubaya, ni vita kati ya shibe na njaa, ni vita kati ya maskini na matajiri, CCM sio chama cha siasa kwa sasa, ni muungano wa kihalifu unaolindwa na baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola.”

Mshtakiwa huyo anadaiwa Agosti 24, mwaka 2015 alichapisha taarifa nyingine ya upotoshaji kupitia mtandao huo wa Facebook kwamba Kikwete yupo Ngurdoto Arusha na wakuu wote wa mikoa na wilaya Tanzania nzima pia wakuu wa vyombo vya dola na wanadhimu.

Kwamba wakuu wa mikoa wanaelezwa kwanza kuwa NEC kwa kushirikiana na CCM tayari wameshatengeneza kura bandia kwa kutumia mfumo wa kalamu za Kichina.

Pia, wanaamuliwa kuhakikisha wanahujumu kampeni za Ukawa kwa kutumia vyombo vya dola, wanaagizwa kuhakikisha kamatakamata ya vijana bodaboda wiki moja kabla ya uchaguzi na zaidi ni wakuu hao wa mikoa wanaagizwa  wakawaagize wakuu wa wilaya kote nchini kuhakikisha wanalinda maslahi ya CCM siku ya uchaguzi.”

Nyerere anadaiwa kuwa Septemba 3, 2015 katika eneo lisilojulikana alichapisha taarifa za upotoshaji kupitia mtandao wa Facebook  kuhusu uwapo wa akaunti ya benki ya kughushi inayomilikiwa na Mtanzania katika benki ya HSBC tawi la North London ikionyesha CCM imemwekea Dk. Slaa  pauni milioni 1.5 kupitia kwa mchumba wake Josephine Mshumbusi ikiwa ni rushwa ili kushinda uchaguzi 2015.

Mshtakiwa huyo andaiwa kuchapisha taarifa hizo za upotoshaji akiwa na lengo la kupotosha umma katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Hata hivyo, mshtakiwa alikiri kukamatwa kuhojiwa na polisi na kufikishwa mahakamani kwa mashtaka hayo pamoja na jina na anuani yake.

Mshtakiwa alikana maelezo yote kwamba hayatambui na kwamba hajatenda kosa hilo.

Hakimu Mashauri alisema kesi hiyo itaanza kusikilizwa ushahidi wa Jamhuri Julai 6, mwaka huu.

Lowassa,Mbowe na Sumaye Walilia Demokrasia Mbele ya Jeneza la Ndesamburo..!!!

$
0
0

Mawaziri wakuu wastaafu, Edward Lowassa na Frederick Sumaye jana walitema cheche katika shughuli ya kuaga mwili wa mbunge wa zamani wa Moshi Mjini (Chadema), Philemon Ndesamburo.

Mawaziri hao katika salamu zao za rambirambi walielezea masikitiko yao juu ya chuki kubwa inayopandikizwa nchini na pia jitihada zinazoendelea za kukandamiza demokrasia.

Hata hivyo, hakuna kiongozi yeyote wa Serikali aliyehudhuria shughuli hiyo hali ambayo ilionekana kuibua minong’ono kwa baadhi ya waombolezaji.

Mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), James Mbatia alienda mbali zaidi na kusema hakukuwa na uwakilishi wa CCM unaofanana na sifa ya Ndesamburo aliyependa amani.

Katika hafla hiyo ya kumuaga kitaifa iliyofanyika uwanja wa Majengo, wabunge wa CCM waliwakilishwa na mbunge wa viti maalumu, Ester Mmasi aliyedai kuiwakilisha pia CCM.

Hotuba ya Mbowe

Hotuba ambayo iligusa hisia za waombolezaji wengi ni ya mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliyesema hatua ya viongozi wa Serikali na CCM kutohudhuria si tukio la bahati mbaya.

“Leo tumejenga Taifa lenye hofu. Watu wamekuwa waoga kwa sababu viongozi wameingiza hofu katika Taifa letu. Watu wenye hatia wana hofu. Kukosekana kwa uwakilishi wa Serikali mahali hapa si ajabu,” alisema Mbowe na kuongeza:

“Ni hofu ya hatia. Kwa heshima sana dada yangu Mmasi (Ester) pole. Asante sana kwa kufika. Umekuja hapa na kujaribu sana unamwakilisha sijui Serikali, sijui Rais. Hakuna.”

Mbowe alisema ameona vituko vingi katika msiba wa Ndesamburo kiasi kwamba anajiuliza inakuwaje wakati alikuwa mtu mwema na walitamani hata kumsindikiza kwa bendi ya polisi. “Tukaenda Chuo cha Polisi kuomba bendi ambacho mzee (Ndesamburo) anawasaidia mambo mbalimbali. Brass band hii inakodishwa kwa Sh300,000, tulikuwa tayari kulipa gharama hiyo,” alisema Mbowe na kuongeza:

“Mkuu wa chuo anaogopa kutoa Brass band ananiambia mwenyekiti Mbowe ongea na IGP (mkuu wa Jeshi la Polisi). Yaani Mbowe nimpigie IGP simu kumuomba Brass band (bendi ya polisi), mimi?”

“Leo polisi wanaogopa kufanya kazi kwa sababu hawajui bwana mkubwa atafurahi ama atakasirika. Ni mambo ambayo si ya Kitanzania. Tukahitaji kiwanja cha kumuaga baba nacho tukanyimwa.”

“Si kwamba kiwanja hiki cha Majengo hakifai. Ila kwa historia ya Moshi, uwanja wa Mashujaa kama unavyoitwa unastahili kuwa uwanja wa kuagwa mzee wetu Ndesamburo. Polisi wakaweka mizengwe.”

Mbowe alisema alifanya juhudi kubwa ikiwamo kuwasiliana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye alimueleza kuwa anashughulikia, lakini hata hivyo ilikuwa ahadi hewa.

“Tulisema baba yetu ni kiongozi wa watu na sio wote wataweza kuja uwanjani. Tukaona ni haki tumpitishe (Ndesamburo) katikati ya mji lakini usiku tukaletewa barua ya zuio la polisi,” alisema.

“Kuna kiburi kinajengwa sana mikoa ya Kilimanjaro na Arusha. Naomba nimpelekee salamu mheshimiwa Rais, Watanzania wote sisi ni ndugu,” alisisitiza Mbowe ambaye ni mbunge wa Hai.

“Mwalimu (Nyerere) alitujenga tukawa tunapendana, lakini utawala huu wa awamu ya tano unafanya matendo yanayoonyesha ubaguzi na tunaona uonevu usiohimilika kwa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha”.

Mbowe alisema ingawa watu wengi wanaogopa kuyasema hayo, yeye atayasema ili Rais, Waziri Mkuu na Serikali nzima ielewe kuwa Kilimanjaro na Arusha ni sehemu ya Tanzania.

“Watu wengi wanaogopa kusema. Siku hizi hata unaogopa kusema wewe ni Mushi. Uongo? Siku hizi watu wanaogopa kujiita Masawe, kujiita Tarimo kwa sababu huna uhakika watawala watafanya nini.”

“Hatuhitaji kujenga Taifa lenye ubaguzi, tunahitaji kumheshimu na kumthamini kila Mtanzania bila kujali dini yake, kabila lake wala jinsia. Tumuenzi Ndesamburo kwa kupendana,” alisema Mbowe.

Mbowe alisema Ndesamburo katika uhai wake alifanya mambo mengi na alikuwa mfadhili mkubwa si kwa Chadema pekee, bali watu wengi na makundi mbalimbali.

“Wakati polisi wanakuja kutufukuza katika uwanja wa Mashujaa na mabomu. Tukawaambia gari mnaloendesha tairi amenunua Ndesamburo. Na ni ukweli, sio nasema maneno ya uongo.”

“Huyu baba amejenga Mawenzi (hospitali) nani asiyejua. Amesaidia taasisi mbalimbali za dini, Wakristo na Waislamu. Amesaidia mashule sio tu kwa mkoa wa Kilimanjaro hata mikoa mingine.”

Mbowe alisema pamoja na kujitoa kwake huko, wako watu wanashindwa kuona thamani yake kwa sababu ya itikadi za kisiasa na kusisitiza kuwa siasa ni mambo ya mpito, lakini jamii itabaki.

“Leo sisi tunazika huku, bungeni wanamsimamisha Halima Mdee na Ester Bulaya. Hatuwezi kujenga Bunge la vibogoyo. Hatuwezi kujenga Bunge la wabunge waoga,” alisisitiza kiongozi huyo wa upinzani.

“Hii nchi imefika hapa kwa sababu kuna watu waoga na wenye hofu. Ugomvi wa Ester Bulaya na Halima Mdee ulianza wakati wa bajeti ya Nishati na Madini.”

“Katika mjadala ule mheshimiwa Mnyika (John) kaamriwa kutoka nje na spika kwa uonevu ulio dhahiri. Wabunge wale akina mama wakasimama wakasema huyu mtu hatendewi haki. Wabunge msifungwe midomo na mkienda bungeni wabunge wote msimame imara na Watanzania bila kujali vyama vya siasa tuitake nchi hii ijifunze kuhoji viongozi wanapofanya makosa.”

Mbowe alitumia hadhara hiyo kutuma salamu kwa wale aliosema wanafikiri kuondoka kwa Ndesamburo ni kuterereka kwa Chadema akisema haitatokea na wataendelea kuijenga vyema Moshi.

Sumaye, Lowassa na Mbatia

Sumaye ambaye ndiye aliyeongea kwa kirefu alisema Afrika itaendelea kama Serikali zilizo madarakani zitaenzi demokrasia na kuachia madaraka kwa amani badala ya kung’ang’ania.

“Kuna juhudi kubwa sana zinaendelea za watu kujidanganya kuwa wanaweza kukandamiza demokrasia. Hapa demokrasia ilipofikia huwezi tena kuikandamiza,” alisema Sumaye na kuongeza:

“Mpira una bladder (puto) ndani. Ukiikandamiza sana itapasuka na ikipasuka itakuwa na madhara makubwa. Tuache Watanzania wafurahie demokrasia katika nchi yao. Hili ni muhimu.”

“Tuache kupandikiza chuki. Mikutano ya siasa inazuiwa, njia za kupitisha maiti (ya Ndesamburo) zinazuiwa. Hatuwezi kuwaonea wananchi hawa kwa muda mrefu.”

Lowassa aliunga mkono maneno yaliyosemwa na Sumaye kuhusu jitihada kubwa zinazoendelea za kudidimiza demokrasia na kupandikiza chuki katika jamii.

“Jitihada za kudidimiza demokrasia inaendelea sana. Hawa waliozuia tusiagie Mashujaa tuwasamehe. Hupimi watu kwa uwanja, bali kwa roho zao,” alisema Lowassa aliyegombea urais mwaka 2015 kupitia Ukawa.

Awali, katika hotuba yake Mbatia alilaani tabia iliyoanza kujengeka ya kuwafarakanisha Watanzania na kumtaka Rais Magufuli ajue kuwa Tanzania ni ya Watanzania wote.

Mbatia ambaye pia ni mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi) alitoa mfano wa tukio la Aprili 30, wakati Rais alipofanya ziara mkoani Kilimanjaro ambapo meya na mbunge walitimuliwa Ikulu.

“Mbunge wa Moshi Mjini (Jaffar Michael) na meya wa Moshi (Raymond Mboya) wakaondolewa Ikulu na Rais akakaa kimya tu. Tanzania ni mali ya Watanzania na sio ya John Pombe Magufuli,” alisema.

“Tangu tumeanzisha mageuzi haya labda John Magufuli alikuwa shule, lakini hatuwezi kukubali Taifa letu likasambaratika kwa maslahi ya watu wachache,” aliongeza kusema na kusisitiza:

“Rais akija Moshi, mwenyeji wako ni meya na mbunge, watu wako wa usalama hawawezi kuwaondoa.

“Niwaombe CCM, Tanzania ni mali ya Watanzania wote, nitaongea nao. Kitendo walichofanya leo sio utamaduni wa Watanzania. Sioni uwakilishi wa CCM unaofanana na Ndesamburo.”

Makamu Mwenyekiti wa CUF, Severina Mwijage alisema wale wote waliozuia Ndesamburo asiagwe katika Uwanja wa Mashujaa Mungu atawalipa kwa kile walichokifanya.

“Huwezi kuwachonganisha wananchi namna hii. Chadema mna salamu inasema peoples power. Tungeamua kutumia nguvu ya umma msingeweza (polisi) kufanya lolote,” alisema.

Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe alipendekeza halmashauri ya manispaa ya Moshi inayoongozwa na Chadema kutafuta mtaa bora ndani ya mji na upewe jina la Ndesamburo.

Zitto alisema hiyo itakuwa ni njia bora ya kuenzi mchango mkubwa wa Ndesamburo katika jimbo hilo ili mtu yeyote akifika Moshi ajue jabali la siasa alikuwa anaishi mjini humo.

Katika shughuli hiyo ya kuaga mwili wa Ndesamburo, waziri wa zamani wa fedha na mbunge wa zamani wa Rombo (CCM), Basil Mramba alikuwa kivutio alipoingia uwanjani hapo.

Jokate Alia Baba Yake Kuteseka na Ugonjwa Kitandani..!!!

$
0
0

Mjasiriamali na mwanamitindo maarufu nchini Tanzania, Jokate Mwegelo amedai kitu ambacho kimemtoa machozi hivi karibuni ni jinsi mama yake anavyotumia nguvu kubwa kumuuguza baba yake ambaye anaumwa kwa muda mrefu.

Mrembo huyo ambaye ametajwa katika orodha la jarida la Forbes Africa la kuwa miongoni mwa vijana walio na umri chini ya miaka 30 wenye mafanikio mbalimbali kwa mwaka 2017, alisema hayo baada ya kuulizwa ni kitu gani hivi karibuni kimemtoa machozi.

“Kusema kweli hivi karibuni nimelia sana, baba yangu anaumwa sasa mama yangu anatumia nguvu kubwa kumuudumia kwa sababu baba anahitaji uangalizi wa karibu sana,” Jokate aliimbia MCL.

Pia mwanamitindo huyo amedai kwa sasa anatamani kuwa na familia lakini bado hajajua ni lini.

Ndesamburo Aaacha Historia Moshi..Mji Wazizima Tukio la Kuagwa Kwake..!!!

$
0
0

Mwili wa mbunge wa zamani wa Moshi Mjini kupitia Chadema (2000-2015), Philemon Ndesamburo jana uliweka rekodi ya aina yake mkoani Kilimanjaro kwa kuagwa na kuhudhuriwa na maelfu ya waombolezaji.

Haijapata kutokea tangu Uhuru wa nchi hii kwa kiongozi kuagwa uwanjani na watu wengi kwani kumbukumbu zinaonyesha wote waliomtangulia ama waliagwa nyumbani kwao au katika makanisa waliyokuwa wakisali.

Awali, Ndesamburo alikuwa aagwe katika Uwanja vya Mashujaa ili kuakisi ushujaa wake wa kuwaletea maendeleo wananchi wa Moshi, lakini Serikali ilizuia.

Hata hivyo, pamoja na kuzuia shughuli ya kufanya kumbukizi na kutoa heshima za mwisho katika uwanja huo na kuhamishia shughuli hiyo katika Uwanja wa Majengo, bado tukio hilo liliutikisa mji wa Moshi.

Mapema jeneza lililobeba mwili wake lilipangiwa kutembezwa katika mitaa na barabara mbalimbali za mji huo, lakini polisi ikazuia ikisema hayo yangekuwa ni sawa na maandamano. Hata jeshi hilo lilipoelekeza msafara huo utoke hospitali ya rufaa ya KCMC hadi Uwanja wa Majengo, bado barabarani watu walikusanyika kuuaga mwili huo hali iliyowapa wakati mgumu polisi.

Kuanzia saa 4:20 asubuhi, polisi wa kutuliza ghasia wakishirikiana na askari wa usalama barabarani, walianza kujipanga katika mzunguko wa magari wa YMCA ili msafara usiingie katikati ya mji.

Polisi hao wakiwa na magari matatu na silaha walijipanga na kuelekezana namna watakavyohakikisha msafara huo hauingii mjini kama jeshi hilo lilivyokuwa limetoa maelekezo.

Msafara ulipokaribia shule ya msingi J.K Nyerere (zamani Kibo) polisi walitumia mbinu ya kukamata magari ya kiraia na kuyatumia kuziba barabara inayoelekea mjini ili kuhakikisha hakuna gari linapita.

Kutokana na ukubwa wa msafara wa magari likiwamo lililobeba mwili wa Ndesamburo, barabara zote zinazoingia na kutoka katika mzunguko huo wa YMCA zilifungwa isipokuwa ya kuelekea Majengo.

Baadhi ya madereva waliokuwa wakienda barabara kuu ya Moshi-Dar es Salaam walilazimika kutumia barabara mbadala, ingawa hata huko mbele walikutana na vizuizi vya polisi wakiwamo wa usalama barabarani.

Msafara huo ulitanguliwa na waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda na kisha watembea kwa miguu ambao walitembea kuanzia maeneo ya madukani hadi Uwanja wa Majengo.

Mbali na pikipiki na watembea kwa miguu, msafara huo ulikuwa na magari zaidi ya 50 yaliyowabeba baadhi ya viongozi wa kitaifa ambao walilazimika kwenda mwendo sawa na wa watembea kwa miguu.

Mamia ya wananchi walijipanga katika barabara nzima kuanzia KCMC hadi Uwanja wa Majengo huku baadhi ya wananchi wakitumia simu zao za mikononi kupiga picha za kumbukumbu.

Msafara ulipofika uwanjani, ulipokewa na wabunge, madiwani na watu waliopata shahada ya udaktari wa heshima (PhD) pamoja na marehemu ambao walipata fursa ya kubeba jeneza lake.

Pia, washirika hao waliopata heshima hiyo pamoja na Ndesamburo walifanya tendo la kuweka joho na kofia ya Ndesamburo aliyotunukiwa juu ya jeneza lake.

Credit - Mwananchi

Kimenukaa..Kenya Wamshutumu Rais Magufuli Kuingilia Uchaguzi Wao Mkuu..!!!

$
0
0



Dar es Salaam. The fear that President John Magufuli could interfere in the Kenyan presidential election slated for August this year in favour of the opposition candidate Raila Odinga seems to be real in President Uhuru Kenyatta’s camp.

Whether the fear is founded or unfounded it remains to be seen but the Jubilee party has, clear, demonstrated some signs of panic over the purpoted “conspiracy” from the southern neighbor.

In fact the issue was so serious that JPM’s plans for “evil machinations” warranted being mentioned in the Jubilee’s National Delegates Conference on Saturday May 6, 2017 in front of President Kenyatta who was crowned the same day as Jubilee’s flag-bearer.

It was Aden Duale, the Majority Leader of the National Assembly of Kenya and a close political confidant of President Kenyatta, who had the task of warning Raila (as they refer to him in Kenya) against using Tanzania as the base for hacking the elections.

Mr Duale said; “We are aware they are setting up a tallying centre in Tanzania. We are also aware the tallying centre is for hacking the IEBC [Independent Electoral and Boundaries Commission] system. And they want to use fake results and imaginary voters to claim victory. But we the Jubilee leaders will form teams that will guide our votes.”

Mr Duale did not mention Dr Magufuli’s name. But the implications were clear. A foreign political party cannot form a tallying centre in Tanzania without a nod from the top leadership.

In the past, reports of “plans” Dr Magufuli’s interference in the Kenyan elections were treated only as rumours, propagated in the social media and in the yellow press in Kenya.

And the fear that Dr Magufuli could play a hand in Kenyan presidential election seem to have originated from his close personal friendship with Raila. Their friendship started when they were both Works ministers in their respective countries in the early 2000s. The two have since exchanged visits in personal capacity for political and family events.

Dr Magufuli attended the Orange Democratic Movement (ODM)’s conference in December 2012 that endorsed Raila as the flag-bearer in the 2013 presidential election. When given a chance to address the conference he urged Kenyans to vote for Raila because he was the transformative candidate.

This prompted a strong reaction from Tanzania’s main opposition party Chadema who wanted the government to state clarify on Dr Magufuli’s support of Raila.

“The government must come out and say if it condones Dr Magufuli’s statements and his presence in the ODM meeting in Kenya last week. If not, it should take action against its minister for getting involved in the campaign politics of a neighbouring country,” Chadema’s Foreign Affairs Director Ezekia Wenje had said.

Given the fact that Kenya’s politics are driven along ethnic lines and its history of post-election violence, Mr Wenje had added, Dr Magufuli’s statements were a diplomatic disaster.

As things turned out, no diplomatic disaster ensued. Either way ODM’s opponents, the National Alliance (TNA) that had fronted Kenyatta and Ruto as the flagbearer and running mate, respectively, did not make much noise about it.

But visits between the two continued. Dr Magufuli, again, attended the burial ceremony of Raila’s son Fidel in January 2015.

Raila visited Dr Magufuli only a couple of days after the latter was nominated CCM’s presidential candidate. Again Raila led an ODM delegation to attended Dr Magufuli’s swearing in ceremony at the National Stadium in November 2015. Mr Kenyatta also attended the event in his capacity as the President of Kenya.

In April 2016, about five months after Dr Magufuli’s swearing in Raila and his wife Idda joined the Tanzanian President’s family in their ancestral home of Chato for the Easter Holidays.

It was soon after this visit that reports of Dr Magufuli’s “plotting” with Raila for Kenya’s presidential elections started receiving much attention.

In May 2016 a Kenyan MP, Maina Kamanda alleged that Dr Magufuli and South Sudan’s President Salvar Kiir and some other foreign powers were funding Raila to destabilise Kenya.

Kamanda’s remarks at a press conference in Nairobi echoed a Kenyan government’s spokesperson statement claiming that some individuals were working with foreign government, including some Kenya’s neighbours, to destabilise the country. Mr Eric Kiraithe did not mention the countries but warned Kenyans found to be working with foreigners will face treason charges.

Again in December 12, 2016 President Kenyatta, addressing an Independence Day rally in Nairobi, claimed that some external powers wanted to influence Kenya’s August 2017 polls. He did not mention those powers but a section of the Kenyan media went ahead and said Tanzania was one of those “powers” working to influence polls.

The Tanzania State House has not commented on Mr Duale’s remarks at the Jubilee conference on Saturday, but it remains to be seen how watertight these allegations of Tanzania’s influence in the Kenyan elections are and how they would weigh in in diplomatic relations between the two friendly nations.

Ironically Mr Kenyatta also faced similar allegations, from some ODM supporters in Kenya, of seeking to interfere with the outcome of Tanzania’s 2015 presidential election. These allegations were heightened by the inclusion of a Kenyan, Julius Mwonga Matei, reportedly a Kenyan intelligence agent, among the seven people arrested on October 25, 2015 on allegations of trying to hack the Tanzanian presidential election tallying.

The seven were apprehended in an “illegal” tallying centre set by Chadema in Dar es Salaam along two other foreign nationals, an Angolan and a South Korean and four locals.

They were charged in court in October 28, 2015 but were released in December 2016 after the Director of Public Prosecution dropped charges.

Could the panick in Uhuru’s camp over “Tanzania’s plans for a conspiracy against Kenyan presidential election” been driven by fears of reprisals from Dr Magufuli?

Ukweli Lazima Usemwe..Maamuzi ya Bunge Kuwafungia Wabunge Kuhudhuria Vikao ni Ukiukwaji wa KATIBA..!!!

$
0
0

Haki ya wabunge kuhudhuria vikao na kuwawakilisha wananchi wa majimbo yao ni ya kikatiba na kanuni feki za Bunge zinazolipa Bunge mamlaka ya kuwasimamisha wabunge kutekeleza majukumu yao ya kikatiba zinakiuka katiba ambayo wabunge hawa waliapa kuilinda na kuitetea Katiba husika!

Bunge halipo juu ya katiba na ndiyo maana wabunge wote huapa kabla ya kuanza shughuli za Bunge ya kuwa wataitii katiba ambayo hakuna mahali ndani ya katiba hiyo wamepewa mamlaka ya kuwasimamisha wabunge na kuwapora wananchi wanaowawakilisha haki yao ya kikatiba ya uwakilishi.

Tusipokuwa waangalifu itafikia wakati Bunge linamsimamisha Mbunge kwa miaka mitano na kuwapora wananchi wa jimbo husika haki yao ya kikatiba ya kuwakilishwa kwa kipindi chote cha uwakilishi.

Adhabu za kikanuni za Bunge hazina mamlaka ya kupora wananchi haki zao za kikatiba kama kuwakilishwa.

Kama Mbunge kavunja kanuni Bunge linaweza kumpa faini ili aathirike Mbunge mwenyewe bila kuathiri haki ya kuwakilishwa ya wananchi wa jimbo lake.

Spika Job Ndugai kuwaadhibu askari walioheshimu haki za binadamu pia linatia aibu si kwake tu bali kwa Bunge zima na taifa kwa ujumla.

Chanzo JF

H. Polepole: Anna Mghwira Amekubali Sharti la Kuwa RC na Kusimamia Ilani ya CCM..!!!

$
0
0

Hamphrey Polepole, amesema Anna Mghwira amekubaliana na sharti moja la kuwa RC na kusimamia ilani ya CCM na kufanya kazi bila kujali itikadi.

Rais Magufuli Afunguka Sababu ya Kumteua Mweyekiti wa ACT Wazalendo Kuwa Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro..!!

$
0
0

Rais John Magufuli ameeleza sababu ya kumteua Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro huku akimhimiza akachape kazi.

Rais Magufuli ametaja sababu hiyo wakati wa hafla ya kumwapisha Mghwira iliyofanyika leo, Jumanne jijini hapa na kuhudhuriwa na  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

“Mimi huwa siteui watu hivi hivi, huwa naangalia uwezo wa mtu na wewe nimekuchunguza na nimejiridhisha kuwa una uwezo wa kuwatumikia wananchi, nenda kachape kazi, kawaondolee kero wananchi wa Kilimanjaro,”amesema Rais Magufuli na kuongeza;

“Wapo watu watakaokusema na wengine watakuonea wivu, wewe kachape kazi.”

Rais Magufuli amemhakikishia kuwa atapata ushirikiano wa kutosha wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yake na asikubali kuyumbishwa na mtu yeyote katika majukumu yake.

Mghwira amejaza nafasi iliyoachwa wazi na Saidi Meck Sadiki aliyekuwa mkuu wa mkoa huo.

Kwa upande, Mghwira amemshukuru Rais Magufuli kwa kumuamini na kumteua kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na amemuahidi kuwa yupo tayari kwenda kufanya kazi ya kuwatumikia wananchi na kujenga Taifa.

“Ninasema hii ni heshima kwa Taifa letu, ni heshima kwa umoja wa nchi yetu, ni heshima kwa siasa za umoja wa nchi yetu, kumekuwa na minong’ono mingi sana kuwa Rais analeta nini, kuteua watu wanaitwa wapinzani, mimi sio mpinzani wa maendeleo,” amesema Mghwira. 

Rais Magufuli: Msimamo Wangu wa Kutoteua Upinzani Bado Upo Palepale..!!!

$
0
0

Rais Magufuli akiongea baada ya kumuapisha Anna Mghwira kuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro alisema kuna watu wanahoji alikuwa amezungumza hatoteua wapinzani amesema watu wanatakiwa waelewe alikuwa anazungumza katika maeneo gani, 

Amesema alizungumza akiwa Zanzibar na msimamo wa kutoteua mbunge wa upinzani kutoka nafasi 10 za ubunge upo pale pale na ameshateua 9 bado nafasi moja

Amesema wapo watakaomuonea wivu kutoka CCM, Chadema kwa sababu hakuchagua huko japo wengi wanamuomba omba ila anataka upinzani uwepo

Ukweli Usiosemwa..Hali ya Mapato ya Serikali Yashuka, Serikali Haina Pesa Wananchi Tujifunge Mikanda..!!!

$
0
0

Nimepata fursa ya kuongea na kiongozi mmoja toka BOT nilikokuwa nafatilia mambo yangu ya kifedha.

Ni ukweli unafichwa kwa gharama kubwa sana kuwa hari ya kiuchumi wa nchi nimbaya sana.

Mapato ya kodi yameshuka kwa kasi sana na serikali inashindwa kujiendesha vizuri na kuna baadhi ya malipo yamesitishwa hasa kwa wazabuni.

Na njia walio itumia ya kuhamishia makato BOT badala ya hazina ni kuwa kuna baadhi ya taasisi hazitapata fedha kwa wakati hasa makusanyo mbalimbali kama makato ya mishahara na michango mbalimbali kama ile ya mifuko ya hifadhi za jamii, na makato ya hiyari ya taasisi mbalimbali kama vile mikopo nk.

Lengo ni kuzitumia wakati wakikusanya mapato.

Sababu kubwa ya kudorora kwa uchumi inadaiwa ni sera zilizoanzishwa na kupelekea biashara nyingi kufungwa na kuhamisha fedha yoka benki za biashara na kupeleka BOT.

Sasa huko BOT ni vimemo vya maagizo fedha ziende wapi lakni hawafati bajeti pangwa na kujikuta kuwekeza sehemu zisizo na return ya mda mfupi na kuzima mzunguko wa fedha.

Hivyo jamaa kashauri kila pesa unayoipata itunze maana ya kesho haijulikani itakuwaje

Chanzo JF

Baada ya Kudaiwa Kuigiza Sauti ya Mbowe Akiongea Kimahaba na Wema Sepete..Steven Nyerere Afunguka Haya Mazito..!!!

$
0
0

Msanii na mchekeshaji mwenye vipaji vya kuigiza sauti mbalimbali za viongozi mbalimbali wa serikalini na watu mbalimbali Tanzania, akiongea na baadhi ya waandishi wa habari amesema kwamba hawezi kufanya ujinga huo wa kuigiza sauti za watu na kwamba Mh Freeman Mbowe ni kiongozi mkubwa sana na hawezi kufanya hivyo na kusisitiza kwamba wale wanaoelewa watakuwa wamesikia hiyo audio note na kujua kwamba sio mimi.

Asema nina mke na watoto leo hii nimtukane Mh Freeman mbowe mwenye wanachama zaidi ya Milioni 30 najitakia nini mimi (steven), siwezi kufanya hivyo

Uteuzi wa Anna: Zitto Aandamwa Mitandaoni, Aweweseka..!!!

$
0
0

Kutokana na uteuzi wa Mama Anna Mgwira aliyekuwa mwenyekiti wa ACT Wazalendo kuwa RC Kilimanjaro na mjumbe wa vikao vya CCM mkoa, Mh.Zitto Kabwe amekuwa akiandamwa mitandaoni na mashabiki wake.

Zitto amekuwa akilazimishwa kutoa tamko ikiwa pamoja na kukejeliwa kwamba ACT ni ''Amri ya Chama Tawala''. Lakini toka uteuzi huo Zitto Kabwe amekuwa aki-post nukuu za Quran jambo linaloonyesha kuweweseka kwake.

Rasmi..Anna Mghwira Aikacha ACT Wazalendo na Kujiunga na CCM..Akabidhiwa Ilani kwa Amri ya JPM ..!!!

$
0
0

Tukio la Mkuu mpya a Mkoa wa Kilimanjaro Mhe Anna Mghwira Kukabidhiwa Ilani ya CCM Leo Ikulu inadhihirisha Wazi kuwa amekubali kwa moyo mmoja kujiunga na chama hiko ambacho kinaongoa Serikali.

Leo Hii mara baada ya kuapishwa Ikulu ,Mhe Anna alikabidhiwa Ilani ya CCM na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara ,mbele ya Rais Magufuli na Viongozi Wengine waandamizi  wa Serikali.

Ben Pal Akubali Ombo la Mchekeshaji Ebitoke la Kutaka Kumuoa ,Amtaka Waonane Ili "Wajuane Zaidi"..!!!

$
0
0

Baada ya ombi la mchekeshaji anaekuja kwa kasi kutoka Timamu African Media, Ebitoke la kuweka wazi hisia zake za kimapenzi kwa msanii wa Bongo Fleva, Ben Pol huku akimtaka amuoe ikibidi, hatimae mkali huyo wa RnB amemjibu kwa kusema atafurahi wakionana uso kwa uso.

Ben Pol amesema maombi hayo ya mrembo ‘Ebitoke’ aliyaona mitandaoni tangia jana ila hakuamini kwani alijua ni stori tuu za mitandaoni mpaka leo baada ya kuona video ikisambaa Instagram ikimuonesha mrembo huyo akibubujikwa na machozi huku akimtaka amuoe.

“Kweli nimeziona habari mitandaoni tuu tangia jana watu wakiposti lakini sikuamini siunajua habari za mitandao bro! ila leo pia nimeona video yake akisisitiza ombi lake lakini bado siamini na nitaamini na nitafurahi kama tukionana uso kwa uso.”amesema Ben Pol kwenye mahojiano yake na Bongo5.

Hata hivyo Ben Pol amesema anaheshimu sana hisia za kila mtu na kitendo cha Ebitoke kutamka hadharani kuwa anavutiwa nae amekiheshimu na kukichukulia kwa uzito.

“Kwanza niseme tuu naheshimu hisia za kila mtu yeye ni binadamu na ameonesha hisia zake soo naziheshimu sana.“amesema Ben Pol.

Ben Pol ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Tatu’ aliyomshirikisha Darassa, wiki tatu zilizopita alikuwa ni gumzo mitandaoni baada ya kuposti picha iliyoleta utata mitandaoni.

Magufuli 'Amrushia Madongo' (Lissu) Aliyesema Atashtakiwa Sakata la Mchanga wa Madini..!!!

$
0
0

Magufuli amesema kuna wapinzani wanapinga tu na wanapopinga wana information zao nyingi ila anawahifadhi tu.

Amesema wapo wanaotafuta data wanahangaika weee na kutuma meseji kwa wale anaowatafuta data na kusema eti atashtakiwa, mtu akiwa mwanasheria ataogopa kushtakiwa? Kisha akacheka kwa dharau na kusema subiri siku atakayopokea ripoti ya pili.

Prof. Tibaijuka Atoa Onyo kwa Wanaopotosha Kauli Yake ya 'Unavyopanua Zaidi Watu Wanazidi Kutamani'...!!!!

$
0
0

Mbunge wa Muleba Anna Tibaijuka ametoa onyo kwa watu wanaopotosha kauli yake na kukata vipande vifupi vya video na kuharibu maana ya aliyokuwa anamaanisha kwa mchango wake bungeni

Amesema kufanya hivyo ni kosa kisheria na watu wanafanya hivyo makusudi ili ujumbe aliokuwa amedhamiria kuufikisha usifike na kuwatupia lawama wapinzani ndio walifanya hivyo na kuwataka watu watafute hotuba yake yote

Amerudia tena anataka umeme upanuliwe na kama neno panua halitumiki tena basi msamiati mwingine utafutwe

Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images