Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Jinsi ya Kujua Kama Umemfikisha Kweli au Anakuibia na Kukushika Masikio kwa Kelele za Kimahaba...!!!

$
0
0

Unahisi unaweza kutofautisha kama umemfikisha kweli au anapiga kelele za kimahaba za kukuzingua?, mwanamke ambaye zamani alikua anamzingua mpenzi wake kwa kelele za kimahaba anatuelezea kwanini ni vigumu kuliko unavyofikili kutambua na utatambuaje!.

Mimi sio mwigizaji, zaidi ya hapo nilikuwa mtu wa mwisho kwenye maigizo kipindi cha shule ya msingi, ila nina uwezo mkubwa wa kusema "Oooh, hapo hapo.. unanifikishaaa!", mpaka mwanaume akahisi kweli amenifikisha, hata hivyo siko peke yangu wanawake wengi tu wanaigiza wakati wapo wanafanya mapenzi.

Utafiti wa kitaifa wa ngono uliofanywa na chuo cha indiana, ulionyesha asilimia 85% ya wanaume wakisema mara ya mwisho kufanya ngono waliwafikisha kileleni wenza wao, hata hivyo asilimia 64% tu ya wanawake walisema walifika kileleni mara ya mwisho walipofanya ngono, hii inamaanisha ni hesabu ya ajabu hata mtoto wa darasa la pili anajua imekosewa, na inamaanisha asilimia 21% ya wanaume walidanganywa na milio ya kimahaba ya wenza wao na wakaamini kuwa waliwafikisha.
Iwapo tukichukulia na wewe utaki kuwa mmoja wa hao waliodanganywa na mbaya zaidi hawakua na ufahamu wowote kuwa wamedanganywa, waulize wanaume wamekuandalia dalili zinazoonyesha na zitakazokuwa zinakuonyesha iwapo unadanganywa.

#1; Unamwelewa

Tuweke hivi, "Ooooh, hapo hapo usiitoe... ooh, naisikia mpaka kichwani!", mwanamke huwa anasema hivi akiwa anakandwa miguu yake na maji ya moto baada ya safari ya miguu ya mwendo mrefu, "OH... USI...., JAMA... UNA.... NDIO...., HAPO HA...", hivi ndomwanamke anavyosema ukiwa unashughurika vizuri kitandani, akiweza kuunganisha sentensi nzima na ikaeleweka ujue anakuzuga, maana akifikia mshindo akili yote inakua kama haifanyi kazi vizuri na ikitokea akiwa analia kama kwenye video za ngono wanavyolia, ujue anakusubiri umalize mambo yako aanze kukuelezea shida zake alizonazo, wale wa kwenye video za ngono huwa wana igiza, mwanamke wa kihalisia wa kawaida huwa hawafiki kileleni iwapo mwanaume anatumia nguvu ovyo ovyo bila ya mpangilio na msuguano wowote unaohusisha kinembe.

#2; Anakubusu bila kuacha

Kwa mwanamke ili afike mshindo, inabidi awe na umakini mkubwa na kuweka hisia zake zote kwenye msuguano na msisimko anaoupata mwilini mwake ili afike mshindo, kubusu na kutekenya hawezi kuvifanya kwa wakati huo ambao anaweka mawazo yote mahala hapo, ukiona unataka kumpiga denda akageukia pembeni ujue mambo ndo yamemkolea vizuri na sio vinginevyo.

#3; Uso wake unakuwa mzuri

Ulishawahi kujiangalia kwenye kioo wakati uume wako unagombana na mikono yako, najua ulishawahi kujisugua, nani ambae hajawai..., hakuna!, na unaelekea yale mambo kumwagika, unajua usowako unakuwaje?, uso wako unakuwa kama vile unataka kutolewa maisha au kama unataka kulia vile, binadamu wote wako sawa upande wa kihisia, hata wanawake pia!, akiwa na sura nzuri wakati ndo anafika mshindo ujue hapo hakuna!, anatakiwa kuwa na sura ambayo haina mvuto kama anataka kulia na sio awe bado anapendeza kama ndo anaingia harusini.

#4; Unafanya mapenzi na mpenzi wako kwa staili ya kimbwa mbwa

Mwanamke kufika kileleni kwa stairi ya kutoka kwa nyuma ni sawa na wewe kufika mshindo huku mwanamke akiwa anakuchzea kwa mikono.
Sijasema haiwezekani, ila inahitaji ufundi mkubwa na dereva inabidi awe anaijua kwa umakini mkubwa njia yake anayopita, ili manbo hayo yaweze kutokea, kwa hio nitakua na wasiwasi kama mwanamke akisema kafika kileleni kwa kutumia hio stairi, mwanamke anauwezo mkubwa wa kufika kileleni iwapo anafanya mapenzi ila yeye ndo yuko juu ya mwanaume kashika msukani, au kwa stairi ya missionary inayoitwa Coital Alignment Technique kwa kifupi The Cat, najua huijui... i gugo(google) na utaiona.

#5; Ngozi yake inakuwa nyororo na kavu

Mwanamke akiwa amefika kileleni, moyo, presha ya damu na mdundo vyote vinakuja juu ambavyo inamaanisha lazima jasho limtoke kwa aina yeyote ile na mwili unakua na majimaji kwenye ngozi, hii ni moja ya dalili amekwea mlima na kufika kileleni kwa furaha

Experience Yangu Jinsi Ngono Zinavyotokea Wakati wa Kusafirisha Misiba..!!!

$
0
0

mimi ni mfanyabiashara,ambapo nilianza na biashara hizi juakali tangu miaka ya 2009 baada ya kustop chuo nilikokua nasomea bachelor of human resources kutokana na sababu za ujana zaidi. 

Basi baada ya kufanya biashara hizi za juakali huku nikijihusisha na shughuli zingine za hapa napale njee ya Tanzania katika kitongoji kidogo kinachoitwa falcon hatimaye nikapata mtaji kidogo
ulionirudisha bongo kufungua biashara 

basi nilipofika bongo nikaona ngoja nichukue coaster moja niifanye kwa shughuli za kukodisha. 
Basi moja kwa moja niende kwenye mada sasa mana sipo kutoa historia mwisho mniokote mabwe pande. 
Nikaanza rasmi kazi hii ya kukodiasha gari yangu aina ya coaster wakati huo ninayo moja nasafari yangu ya kwanza ilikuwa kwenda marangu. 
Hapa sasa ndio penye mambo safari inaanza pale upanga ndugu wameaga wamemaliza huku mimi na kijana wangu tukiwa tumekaa kwenye gari tukiwaacha wamalize taratibu zao tupakize mwili (kiroba) tuanze safari kuelekea kilimanjaro. Basi wakati tumejilalia kwenye gari wakaanza kuingia wadada wazuri wasafi wanaonekana wana pesa wakaingia kuwahi siti na wengine wanabadilisha nguo na sisi tukiwa humo. zikaingizwa katoni za bia na na pombe kali nyingi. mara kiroba kilikuwa tayari kuingizwa kwenyw gari tukasaidiana na wafiwa kuingiza mwili ndani ya gari. baadae waendaji wakaingia kwenye gari mlango ukafungwa ac ikawashwa na gafla story zikabadilika kwenye gari huku wale wa nje wakitupungia mkono kama ishara ya kututakia safari njema. Story zilizokuwa zinapigwa ndani ndizo zilizonishangaza kwani ni sikuwa na uzoefu na ni siku chache tangu ninunue hii gari,basi wakaanza kuuliza Jack Daniel yangu iko wapi mwingine anaeuliza konyagi yaani ilikuwa kila mtu na kiburudisho chake huku gospel zikiendela kwenye tv tatu za ndani ya gari. 

Hatimaye bagamoyo wakaomba kuchimba dawa sheli huku wengine wakiwa tayari wamelewa basi tukashuka wote hapo nje full kukumbatiwa mnapewa sifa sijui za uongo na kweli, mwingine anakuganda mpige story na yeye tu huku akikuona unaongea na mwingine anakununia flani hv. 
Safari inaendelea hadi tunafika hotelin sasa pale ndio pombe ndio zinanyweka in large scale na watu kulewa hoi.hapa sasa ndio kuna vioja mwingine anapete mkononi anakuja anakukumbatia kimahaba na busu juu huku anakuuliza unakunywa nini nikununulie(wadada mkisafirishaga misiba sijui mnapataga wapi rundo la hela namna ile) basi ikifika saa tano usiku tunaendelea na safari kuelekea njia panda himo ambapo ndio kituo kikuu cha kupumzika. basi baada ya kutoka hotelin unajikuta tayari ushadendeka na wawili bila hata kujijua na mbaya zaidi wengi wanaofanya hivi ni wananafasi nzuri kimaisha, wengine ni maafisa wa jeshi wengine unaona kabisa msibani aliletwa na shangingi la kifahari. basi pale tumiendelea na safari taa za ndani zinazimwa na hakuna anaekumbuka kama ndani kuna maiti tena maana utakuta wale wamelaliana hawa wanadendeka mimi mwenyewe naongeleshwa na jinsia za kike tatu tofauti. hadi tukafika njia panda tukapumzika baadae saa moja asubuhi tukaanza safari ya kupanda marangu,maajabu tulipofika pale msibaa ukaanza tena vilio kwenye gari hatari.basi mnashusha maiti mnatulia pale kama robo saa hapa sasa ndio kila mtu anachukua namba zenu eti wakimaliza kuzika mje kuwafuata wakalale sehem nzuri. Wakimaliza kuchukua namba sisi tunashuka njia panda himo kutafuta vyumba vya kulala pale double M lodge.

Basi tukifika double M tunachukua vyumba huku tukiwawekea booking baadhi ya wafiwa waliotuambia tuwaweke vyumba

Naama saa tisa imefika wafiwa wanaanza kupiga simu tuwafuate baadhi waje kulala kwenyw lodge, hapa sasa ndio patamu, tunawafuata kisha tunarudi nao njia panda himo bia zinanyweka kupoteza mawazo ya kufiwa huku wengine wakiwaponda waume zao waliowaacha dar kuwa hawawatoshelezi kimapenzi, nadhan mnaeza kuvuta picha wadada wakikutana pamoja huku wakiwa tayari wameshalewa hapa nakwambia mnakuwa na wadada wengine wenye majina makubwa mjini lakini hapa hutaamini kama ni yeye ndio yanayomtoka maneno hayo mdomoni. basi sikukaa mda mrefu mwenzangu akaambiwa amsindikize mfiwa mmoja kubeba katoni za vinywaji kumbe wameenda kumalizana hukohuko, basi sasa hapa nimebakiwa peke yangu na sijui niongee na yupi nimuache yupi maana unakuta wengi wako kwenye ndoa na tayari wote wameingia kingi. 


nadhani leo niishie hapa
ila visa ni vingi kuna siku mwenzangu alienda kulala na mtoto wa marehem masaa mawili baada ya kumzika baba yake kule mafinga. 

pia hii tabia ya ngono wakati wa kusagirisha misiba iko kwa mikoa yote ya Tanzania ukienda mbeya musoma bukoba... na hakuna msiba nilioshuhudia warembo wengi kama msiba wa yule dada aliyeungua gorofani na mpenzi wake kwenye apartment yake mikocheni tukamsafirisha kibosho. 

Pia nilichojifunza mabint wengi wa mikoani hawajawahi kufika dar hivyo wakijua mmetoka dar ni kama wanakuwa na kichaa fulani kuhakikisha mnalala wote

karibuni tusikilize bambi bambi ya jidena

Chanzo JF

Fahamu jinsi Damu ya Hedhi ya Mwanamke Ilivyo na Nguvu Katika Imani za Kishirikina..!!!

$
0
0

Nitangulie kuomba radhi kwa wale watakaokereka na hii mada..Nina heshima kubwa kwa akina mama wote na privacy yao..naomba tuichukulie hii kwa muktadha wa maarifa, elimu na ufunuo wa dunia ya upande wa imani

Makuzi yetu yametulea kutufundisha kwamba damu husika ni uchafu na jambo la Siri sana... Wahusika kwenye hili hufanya ni jambo la siri huku wengine wakijichukia kabisa

Kwa dhima ya udugu wa kishetani damu ya hedhi ni kitu cha thamani kubwa kwakuwa imebeba uhai nguvu na kiwakilishi cha maisha marefu, ikijulikana kama nyota ya moto kiashiria cha mungu mwezi...kwenye ibada za kishetani alama nyekundu ni kiwakilishi cha hiyo damu na hata wale ANNUNAKI(malaika walioanguka) wanaichukulia kama dhahabu ya miungu kwa imani yao
Hedhi mzunguko wake unatawaliwa na mizunguko ya mwezi na kuna mahusiano ya moja kwa moja kati ya damu ya hedhi mzunguko wa mwezi na mwanamke!

Kwa wenzetu wahindi hii wanaita SOMA na Greece ikijulikana kama AMBROSIA...Tafsiri kwa muktadha wao ikiwa asali ya miungu. ...

Mwezi ni alama ya makazi ya mungu na malaika wa kike. Hivyo basi ibada yoyote inayouhusika na kunywa damu ya hedhi, hiyo ni ibada ya kuabudu mwezi kwa maana ya kumuabudu mwanamke
Hapa kuna mifakarano kwa baadhi ya wayahudi kwakuwa baadhi yao hupenda kufuata kalenda ya mwezi na hata miungu yao mingi ikiwa ni masanamu ya kike lakini wale wanaojiita Israeties wakipinga hilo kwakuwa wanaamini anayepaswa kuabudiwa ni mungu jua hivyo kuabudu mwezi ni kuruhusu kutawaliwa na mwanamke....

Tukiachana na hao hapa kwetu damu ya hedhi hutumika kutengeneza dawa za mvuto wa kimapenzi na ishu za kishirikina kufarakanisha ama hata kupatanisha...!

Vyovyote iwavyo hiki tunachodhani ni uchafu kina siri yenye nguvu kubwa kwenye ulimwengu wa roho

Mauaji Yanayoendelea Kibiti Mkoani Pwani Yamfanya IGP Sirro Kuibuka na Kauli Hii Mpya..!!!

$
0
0

Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro amewataka Watanzania wawe wavumilivu kwa kuwa Polisi wanafanya uchunguzi wa kina kuhusu mauaji yanayoendelea mkoani Pwani.

Sirro ameyasema hayo jana (Jumamosi) katika ziara yake ya kwanza mkoani Morogoro tangu ateuliwe kuwa IGP na kusisitiza kuwa polisi wanafanya kazi usiku kucha kudumisha hali ya usalama.

“Hatulali, tunafanya kazi kwa juhudi kubwa, lakini ni lazima wananchi watupe ushirikiano na nyinyi waandishi wa habari pia mnatakiwa mwandike kwa hekima bila uchochezi,” amesema.

Sirro amesema amefanya ziara hiyo Morogoro na katika maeneo mengine nchini ili kuzungumza na polisi namna ya  kusimamia ulinzi na usalama katika maeneo yao. 

Bajeti Mpya ya Serikali Kuibana Zaidi Sekta ya Madini,,Kodi Iliyoongezwa Itaacha Nchini Zaidi ya Bilioni 46..!!

$
0
0

Kodi mpya ya asilimia moja iliyoongezwa katika madini yatakayokuwa yanasafirishwa nje, itaipatia Tanzania zaidi ya nusu ya mapato ambayo nchi ilikuwa inapata katika mirabaha inayolipwa na kampuni za uchimbaji.

Kodi hiyo imo kwenye mapendekezo ya mabadiliko ya sheria yaliyosomwa juzi bungeni na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango katika bajeti ya Serikali ya mwaka 2017/18.

Hadi sasa, kampuni hizo zinalipa mirabaha ya hadi asilimia 4 ya madini yanayouzwa nje, lakini mabadiliko hayo yatazikamua zaidi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA) ya mwaka 2016, mauzo ya dhahabu nje yalikuwa dola 1.8 bilioni za Kimarekani (sawa na Sh3.96 trilioni)

Kwa maana hiyo, iwapo kodi hiyo ingetozwa kwa mwaka huo, Serikali ingepata ziada ya Sh39.6 bilioni kwa mwaka huo.

Pia mauzo ya almasi nje yalikuwa dola 82.18 milioni za Kimarekani (sawa na Sh180.79 bilioni) na kama Serikali ingekata asilimia moja ya fedha hizo, ingepata Sh1.807 bilioni, huku wachimbaji wadogo waliouza dhahabu ya Sh106.7 bilioni, wangeipa Serikali Sh5.3 bilioni za ziada kwa kuongezewa kodi hiyo.

Kwa mujibu wa takwimu hizo, Serikali ingelipwa jumla ya Sh46.707 bilioni za kodi hiyo mpya kwa mauzo ya madini yote kwa mwaka 2016.

Kiwango hicho ni zaidi ya nusu ya mapato yote ya mrabaha ambao Serikali hupata kwa mwaka. Serikali ililipwa mrabaha wa Sh76.1 bilioni.

Kumekuwepo na mjadala wa muda mrefu kuhusu mikataba ya madini, ambayo wengi wanatuhumu kuwa inainyonya nchi.

Mwezi Machi, Rais John Magufuli alisimamisha usafirishaji nje wa mchanga wa dhahabu na shaba na baadaye kuunda kamati mbili za kuchunguza kiwango cha madini kilichokuwa katika makontena yaliyozuiwa bandarini na nyingine kutathmini athari zinazotokana na kusafirisha mchanga huo nje na kuangalia mikataba.

Tayari kamati ya kwanza imeshakabidhi ripoti inayoonyesha kuwa Acacia ilidanganya.

Wema Sepetu - "Imetosha Jamani ,Mimi Kuwa Staa Isiwe Tabu "..!!!

$
0
0

“NAHITAJI kupumzika sasa, nimechoka kuhusishwa na mambo yasiyo na mashiko. Kwakweli nimechoshwa na ninaumizwa sana na hii hali,” ndivyo anavyosema msanii wa filamu za Kibongo, Wema Sepetu.

Wema ambaye ni Miss Tanzania mwaka 2006, amezua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii baada ya clip inayosikika sauti inayodaiwa ni yake akizungumza kimahaba na mtu anayedaiwa kuwa ni Freeman Mbowe, Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chadema, taifa.


Katika clip hiyo iliyoanza kusambaa kwa kasi tangu wikiendi iliyopita, sauti inayodaiwa kuwa ni ya Wema na ile inayoelezwa ni ya Mbowe, wanazungumza katika hali ya mahaba huku wakionekana kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi.

Mwanamume kwenye clip hiyo (anayedaiwa kuwa ni Mbowe), anajaribu kumuomba msamaha mwanamke (anayedhaniwa kuwa ni Wema) na kumtaka aende Kilimanjaro kwa mazungumzo zaidi katika siku za mwisho wa wiki.

Tayari Mbowe ameshakanusha vikali kuwa sauti ile siyo yake, bila kufafanua zaidi, akitaka muda uachwe uzungumze kwa vile suala hilo linafanyiwa kazi kwa upande wao.

Wema ameibuka na kueleza masikito yake kwa kuhusishwa katika clip hiyo akidai kuwa anaumizwa na namna watu wanavyomfuatafuata na kumchafulia jina lake.

Wema ameliambia Swaggaz kuwa, amekuwa akijitahidi sana kukaa mbali na vyombo vya habari ili asiripotiwe vibaya lakini anaona haisaidii.

“Nimeamua nikae mbali na mitandao, nitulie nifanye mambo yangu lakini naona haisadiii. Siyo siri nimechoshwa na hii hali, natamani atokee staa mwingine abebe huu mzigo nami nipumzike ili niweze kufanya majukumu yangu niliyonayo.

“Nafahamu Watanzania wana shida nyingi, nami nimejipanga kuwa mtetezi wao hasa wanawake na wasichana kwa ujumla.

“Nimejitahidi kukaa kimya kwa muda mrefu na kupotea  kwenye mitandao ni  na sehemu za starehe kwa kujichimbia nikifanya mambo yangu na kutafakari namna ambayo nitakitumikia chama changu (Chadema) lakini binadamu bado wameendelea kuniandama ili wapate cha kuniongelea,” anasema Wema na kuongeza:

“Kweli kabisa… huu ustaa sasa naona ni mzigo kwangu. Natamani atokee msichana mwingine awe staa kunizidi ili na yeye aandikwe sasa. Kila siku Wema, why? Nakwazika sana kwa kweli.”



KINACHOMKERA ZAIDI

Wema anasema anachukizwa sana na tabia ya kuzushiwa mambo, kwani anaweza kuwa karibu hata na ndugu yake, akazushiwa ni mpenzi wake.

“Nakerwa mno ninapokuwa na mwanamume karibu hata kikazi nasingiziwa kuwa ni mpenzi wangu, hii ni kero. Naomba nisionekane mwanamke wa kila mtu, sasa niheshimiwe kama wengine wanavyoheshimiwa.

“Ninapokuwa karibu na mtu wa jinsia nyingine nisifikiriwe kutoka naye kimapenzi, kwa kuwa kuna watu ninawaheshimu kama Mwenyekiti…

“Hii imeniumiza hadi nilitamani kuachana na siasa ila mama yangu, ndugu zangu na Mwenyekiti mwenyewe wamenipa moyo na hapo ndipo nimepata nguvu za kufanya kazi kwa nguvu kuliko hapo awali,” anasema Wema.



AFAFANUA KUHUSU CLIP

“Sina uhakika kama ni sauti yangu kwa kuwa sikumbuki siku wala saa niliyoongea maneno hayo, hivyo kazi hiyo naiacha chini ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ‘TCRA’ ili kubaini ukweli wa jambo hili.

“Kwa sasa sihitaji kuhusika wala kuliongelea kwa kina, nina uhakika ukweli utajulikana na sheria itachukua mkondo wake,” anasema Wema.



MIKAKATI YAKE

“Kwa sasa mikakati yangu ni kukitumikia chama changu kwa kuleta wanachama wengi zaidi kuhakikisha uchaguzi ujao kinafanya vizuri na kushinda ushindi wa kishindo.

“Hilo wapinzani wangu wanalijua na ndiyo maana wanatafuta skendo zisizo na maana ili kunirudisha nyuma ila ndiyo wamenipa nguvu ya kufanya kazi kwa kasi na kuniweka katika nafasi ya kujua siasa ni mchezo wa aina gani,” anasema.



MALENGO YAKE

“Malengo yangu ni kuwa kiongozi na hilo linajulikana kwa sababu uwezo ninao, nia ninayo na nguvu za kuwatumikia wananchi ninazo hivyo siasa zao za majitaka kwangu hazitakuwa na nafasi.

“Kama walikuwa wanajua Wema ni yule wa zamani, wa kukwazwa na vitu visivyo na msingi hilo wamenoa. Wema huyu ni kamanda ambaye anajiamini na kujitambua na nitasimama kutetea haki za wanyonge kama ilivyo sera ya chama changu,” anasema.

Morata Kutua Old Trafford Kesho Jumatatu kwa Ajili ya Kupimwa Afya..!!!

$
0
0

Manchester United imekubali kulipa ada ya uhamisho wa pauni 64milioni  kwa ajili ya Alvaro Morata.

Morata atawasili England kwa ajili ya vipimo Jumatatu kwa mujibu wa magazeti ya Hispania. 

Mshambuliaji huyo wa Real Madrid uhamisho wake kwenda Old Trafford umechochewa na kukwama kwa usajili wa Antoine Griezmann kufuatia Fifa kuifungia Atletico Madrid kusajili.

Uhamisho huo umekuwa rahisi baada ya Man United kuthibisha kuachana na Zlatan Ibrahimovic msimu huu.

Morata alianza maisha yake ya soka la kulipwa akiwa chini ya kocha wa sasa Man United, Jose Mourinho, alipokuwa kifundisha Real Madrid mwezi Desemba 2010 alipocheza dhidi ya Real Zaragoza.

Imefichuka..Hii Hapa Sababu ya Nyuma ya Pazia ya Uteuzi wa Mhe Mghwira Kuwa RC Kilimanjaro..!!!

$
0
0

MWENYEKITI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mgwira, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kwa kile kilichoelezwa kuwa ni “mkosoaji mwenye faida” na kwamba Rais John Magufuli bado ana nafasi kwa wote wanaomkosoa kwa hoja na si vinginevyo.

Hatua hiyo inatajwa kumweka Magufuli katika taswira ya kukanganya zaidi kwa kuwa tayari amepata kutoa kauli zinazokandamiza siasa za upinzani nchini, ikizingatia kuwa Juni, mwaka jana, alitangaza kusitisha mikutano ya kisiasa akitoa ruksa kwa wabunge pekee hali iliyozua malumbano kati yake na viongozi wa vyama vya upinzani.

Vile vile akiwa Zanzibar, katika mikutano ya hadhara, mwaka jana, alimshangaa Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na wapinzani ambao anaamini hawakustahili kuwamo kwenye serikali hiyo.

Lakini kwa sasa Raia Mwema limeambiwa na mmoja wa wandani ya Ikulu ya Magogoni jijini Dar es Salaam kwamba uteuzi huo si wa mwisho na kwamba Rais Magufuli haamini kwamba kuna watu wameumbwa kuwa wapinzani maisha yao wote.

Hii ni mara ya kwanza kwa mmoja wa wandani wa Rais Magufuli kueleza kinagaubaga kuhusu uteuzi huo wa Mghwira ambaye alikuwa mshindani wa mgombea huyo wa urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

“Nenda kawaambie Watanzania kwamba Mghwira amechaguliwa kwa sababu ya constructive criticism (ukosoaji wenye hoja) yake. Rais hana shida na wakosoaji wa namna hiyo na siku zote wana nafasi kwa serikali yake.

“Hata Profesa Kitila Mkumbo naye alikuwa anamkosoa Rais Magufuli mara kwa mara lakini bado alimteua kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji. Hii ni kwa sababu siku zote Kitila alikuwa akimkosoa kwa haki na kwa hoja.

“Sasa kuna wakosoaji wengine kila siku wanakosoa tu na wakati mwingine wanaweka matusi na kashfa humohumo. Watu kama hawa Rais Magufuli hawezi kufanya nao kazi.

“Na naomba wewe mwenyewe nikupe home work ya kujiuliza nini maana ya mwanasiasa wa upinzani. Je, maana yake ni kupinga kila kinachofanywa na serikali iliyo madarakani?

“Kwa tafsiri ya Rais Magufuli, hakuna mpinzani wa kudumu. Yeye anaamini vyama visivyo madarakani ni vyama mbadala tu kwa CCM na haimaanishi kazi yao ni kupinga tu bila hoja. Ujumbe kwa wanasiasa wote ni kwamba yeye hana ubaguzi na yuko tayari kufanya kazi na wote wenye hoja, Raia Mwema limeambiwa na chanzo chake hicho cha uhakika kutoka Ikulu.

Polepole azungumza

Kwa upande wake, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole alisisitiza kwamba rais amefanya uteuzi huo kwa kuzingatia kigezi kikuu cha Utanzania wa mteuliwa.

“Ni rais wa Watanzania wote anapofanya uamuzi huzingatia katiba na sheria za nchi. Amepewa mamlaka kikatiba kuteua wasaidizi wake wakiwamo wakuu wa mikoa na wilaya, msingi wa kwanza katika uteuzi ni Utanzania wa watu hao anaowateua na mengine kama uadilifu.

Hizi ni zama za CCM mpya tunatazama uadilifu na kuzingatia watu wenye fikra na mwelekeo sawa na ule wa rais wetu, kuendeleza mapambano ya kuelekea uchumi wa kati ambao kimsingi ndio uchumi wa viwanda.

Rais anapofanya uamuzi hafungwi, kuna maeneo anaelekezwa na kuna maeneo anaachwa afanye kutokana na imani ya wananchi juu yake. Rais anapoteua Watanzania wanaweza kutoka popote kwenye vyama vya siasa au hata vyombo vya ulinzi, kuna askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania amewateua kuwa wakuu wa wilaya kwenye wilaya za pembezoni mwa nchi, hawa bado ni askari walioko kwenye utumishi wa jeshi,” alisema Polepole.

Credit - Raia Mwema

Ripoti ya Pili ya Mchanga wa Dhahabu ..Baada ya Muhongo Kuondoka Hii ni Zamu ya Kikwete na Mkapa..Habari Vichwa vya Magazeti ya leo 11/6/2017..!!!

Mayai Yasipoiva Ni Hatari

$
0
0

Mayai ni moja ya vyakula vyenye viini lishe muhimu kwa ajili ya afya ya mwili wa binadamu. Kwa kawaida mayai kabla ya kuliwa, huandaliwa kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuchemshwa, kukaangwa au kuchanganywa na vyakula vingine kama vipande vya viazi mviringo ambavyo ni maarufu kwa jina la chips.

Pia, kuna baadhi ya watu wanaopendelea kula mayai mabichi kama dawa ya tiba mbadala, kwa ajili ya kulainisha sauti na wengine hupendelea kula mayai ya kukaanga ambayo hayakukaushwa vizuri.
Ukitembelea migahawa mingi utabaini kuwa watu wanakuwa na mitazamo tofauti na wanavyopenda kula mayai.

Mfano kuna wanaoagiza watengenezewe mayai kwa mtindo unaojulikana kama ‘macho ya ng’ombe.’ Ukiagiza namna hiyo, mpishi atataka kuuliza kama ni ‘macho ya ng’ombe’ ya kugeuza.

Ina maana kuwa ‘macho ya ngombe’ ya kugeuzwa ni yale yanayoivishwa pande zote lakini yale ambayo siyo ya kugeuza, huwa linaiva nusu. Upande mmoja unabaki ukiwa mbichi, na ndiyo raha ya baadhi ya watu.

Hata ukienda kwa wakaanga chipsi, utakuta wanawauliza wateja wao kama wanapokaanga na mayai wakaushe au wasikaushe. Hii inaashiria kuna watu wanataka wale chipsi zikiwa na mayai ambayo halijaiva sawasawa.

Kuna watu wengine wanaamini kwamba kula mayai mabichi kunafanya sauti inakuwa nyororo, hivyo wale waimbaji huwalazimu kufanya hivyo ili kufanya nyimbo zao zivutie.

Si hivyo tu, kuna baadhi ya watu huamini pia dawa ya kikohozi ni kunywa yai bichi lililochanganywa na asali. Hizi ni imani ambazo zimejengeka kwenye jamii na watu hufanya hivyo ili kufikia malengo waliyokusudia.

Katika siku za karibuni, imevuma kuwa mayai ya kwale yanatibu magonjwa sugu kama vile kisukari, shinikizo la damu, saratani na kifua.

Katika mpango huo, wanapendekeza wahusika kula mayai mabichi ya kwale tena kwa kutafuna hadi kaka lake, yaani ganda la nje.

Hali hii imesababisha biashara ya mayai ya kwale kuwa kubwa na hata wafugaji wameongezeka mara dufu.

Mkude: Kwa dau hili nipo tayari kujiunga na Yanga

$
0
0

UNAWEZA ukashituka kidogo ila habari ndiyo hivyo anaweza kusaini Yanga kwa milioni 70 tu, Mkude ambaye mara kadhaa amewahi kuhusishwa kuwaniwa na Yanga ameamua kuweka wazi kuwa atatua ndani ya kikosi cha Yanga kwa ajili ya kukitumikia msimu ujao kwa kutoa sharti moja kubwa ambalo ni klabu hiyo kumpatia shilingi milioni 70.

Mkude kwa sasa yuko huru kujiunga na timu yoyote baada ya mkataba wake na Simba kudaiwa kumalizika hivi karibuni, ikiwa ni mwisho wa mkataba wake wa shilingi milioni 60 aliosaini kuitumikia Simba miaka miwili iliyopita.

Akizungumza kiungo huyo, amesema atakuwa tayari kusaini mkataba na klabu ya Yanga kwa dau la kuanzia milioni 70 kwenda juu kutokana na kiwango alichonacho kwa sasa. Simba wamempa ofa ya milioni 40-50 ila yeye amekataa kwa kigezo kwamba mkataba unaoisha walimpa milioni 60 kwa sasa lazima dau lipande.

“Kwa upande wangu nipo tayari kutua Yanga kwa dau la kuanzia milioni 70 na kuendelea hadi shilingi milioni 150 na siwezi kusaini chini ya hapo, nipo tayari kutua katika timu yoyote kwa kiasi ambacho tutakubaliana kwa kuwa kiwango changu kipo vizuri.

Nahodha huyo wa Simba amesema lolote linaweza kutokea kuanzia sasa: “Tusubiri kila kitu kitakuwa wazi muda si mrefu na wadau watajua nitasaini wapi kwa ajili ya msimu ujao, wasiwe na hofu.”

Bungeni: Waziri Mpango Asema Serikali Imetenga Bajeti 2017/18 Kufufua Kiwanda cha General Tyre..!!!

$
0
0

=> Kiwango cha ukuaji uchumi 2016/2017kimeendelea kukua kwa wastani wa asilimia saba ikiwa ni pungufu kidogo ya kile kilichotarajiwa awali. Makadirio ya awali yalionyesha kuwa uchumi huo ungekua kwa wastani wa asilimia 7.2.

=> Hali ya ukuaji uchumi imeendelea kushuhudiwa katika kiwango kilekile cha awali cha asilimia saba na hii imechangiwa na mambo mengi ikiwamo baadhi ya sekta kutofanya vizuri. Sababu hizo ni pamoja na kushuka wa sekta ya kilimo iliyotarajiwa kukua kwa asilimia 2.9, lakini malengo hayo hayakufikiwa na badala yake yalikuwa kwa asilimia 2.1.

=> Sekta ya biashara ilikuwa 6.7% hali ambayo ni tofauti na makadirio yaliyowekwa awali yaliyokuwa 7.8%

=> Eneo la chakula limechangia kufikia kwa malengo ya ukuaji uchumi. Makadirio yetu yalikuwa kwamba sekta ya chakula ingekua kwa 8%, lakini bahati mbaya ilishuka na kuwa 3.7%.

=> Kuna sekta zimefanya vizuri na kusaidia uchumi wa Taifa, sekta hizo ni pamoja na habari na mawasiliano, madini na kiashirio cha kuendelea kukua kwa sekta ya viwanda.

=> Kwa mwaka 2016/2017 Serikali ilipanga kutumia Shilingi Bilioni 11,820.5 kwa ajili ya bajeti ya mandeleo. Hadi April 2017 fedha zilizokuwa zimetolewa ni Shilingi Bilioni 4516.7 sawa na Asilimia "38" ya Bajeti nzima.

2017/2018

=> Serikali imetenga bajeti kwa mwaka wa fedha wa 2017/18 kwa ajili ya kufufua kiwanda cha matairi yaani General tyre.

=> Serikali inafanya utaratibu katika kuboresha maisha ya wananchi na watumishi wa umma kwa kuweka malengo na bajeti katika kutekeleza hayo.

Ukweli Mchungu...Achaneni na Lowassa Magufuli Ndiye Rais..!!!

$
0
0

Vyovyote ilivyokuwa na ndivyo ilivyo, John Pombe Magufuli ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania. Wale wote ambao kila siku wanataka kuwaonesha watanzania kwamba Edward Lowassa kugombea Urais kupitia CHADEMA lilikuwa ni kosa la Karne, wanaturudisha nyuma ya wakati hali ambayo haitusaidii kwa lolote.

Hoja kwamba kama angekuwa Wilbroad Slaa ndiye mgombea Urais basi CHADEMA ingeshinda, ni ya uongo kabisa. Slaa aligombea Urais mwaka 2010 na hakushinda. Na hakushinda si kwa kuwa hakushinda, bali hakushinda kwa kuwa hakutakiwa kushinda. Hao wasiotaka vyama vingine zaidi ya CCM kushinda ni kitu gani kingewafanya wakubali Slaa ashinde mwaka 2015?

Kumshupalia Lowassa na kushupalia "kosa" la CHADEMA kumsimamisha kuwa mgombea wao wa Urais ni kupoteza wakati. Kama kuna Mkuu wa Mkoa kaghushi vyeti na inajulikana na hafukuzwi kazi wakati kazi yake sifa kuu ni kujua kusoma na kuandika tu, hapo tatizo si Lowassa kugombea Urais mwaka 2015 bali kosa ni mtizamo wa mamlaka ya uteuzi.

Kama watumishi wa umma hawaongezwi mshahara, hawapandishwi madaraja, fao la kujitoa linafutwa, fedha zao zilizoko kwenye mifuko ya Hifadhi ya Jamii zinatumiwa na serikali bila ya wao kushirikishwa wakati wao wanacheleweshewa Pensheni zao, wanazuiwa kubadili kazi, wanadhalilishwa na hata kufukuzwa kazi bila ya kufuata sheria na taratibu zilizopo, hapo chanzo si Lowassa kugombea Urais Mwaka 2015.

Kama kuna watu wanaona mambo hayaendi kwenye nchi yetu, wajue nchi hii ina serikali na serikali hiyo haiongozwi na Lowassa bali Magufuli. Kama kuna mtu anaona serikali haitendi kile kinachotarajiwa, basi wasikimbilie kusema kwamba kosa ni CHADEMA kumsimamisha Lowassa kuwa Mgombea Urais mwaka 2015.

Kama mnashindwa kumkosoa Magufuli hasira zenu msizihamishie kwa Lowassa.

Mtatiro - Mwenyekiti wa Cuf Amepigwa Risasi na Polisi Kibiti..Siyo Majmbazi Waliohusika..!!!

$
0
0

Jana usiku Katika Oparesheni ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama, wamempiga Risasi Mwenyekiti wa Kitongoji wa CUF pamoja na raia mwingine, huko Nyamisati, Kibiti.

Mwenyekiti huyo ni Moshi Sefu Machela na ni mwanachama. Na baada ya kumpiga risasi vyombo hivyo vya ulinzi vilimkokota na kuelekea naye kusikojulikana na hali yake haijulikani.

Kinachotokea Rufiji/Mkuranga/Kibiti hivi sasa ni Dola kwenda kulipiza kisasi kwa raia wasio na hatia ( hususani Viongozi wa CUF) ili kufuraisha na kutuliza nafsi za ndugu jamaa na marafiki wa raia waliouawa ambao wengi wao walikuwa viongozi wa CCM.

Hadi sasa viongozi zaidi ya (20) wa CUF wameshakamatwa bila sababu, wanateswa na kisha kiachiwa bila kufunguliwa mashtaka. This is very bad and shameful indeed.

Unapotaka kuwafutalia JANJAWEED wanaowaua viongozi wa CCM kwa kuwatesa viongozi wa CUF unajenga visasi huko mkoani Pwani. Sijui nani anavifundisha vyombo vyetu kuwa mbinu yao hii ya kikatili na ya kuumiza watu wasio na hatia itakuwa na tija. 

I am so worried kuwa taifa letu linaelekea mahali kusiko salama.
Julius S. Mtatiro
09/06/2017

Fahamu Chanzo cha Wasomi Wengi Kutokufanikiwa Kimaisha na Kiutendaji...!!!

$
0
0

Mara nyingi wasomi wengi hasa hasa wale waliokuwa wakifanya vizuri darasani kuliko wengine, wengi wao wanamaisha ya kawaida licha ya kuwa na mshahara mnono pamoja na marupu rupu ya kutosha,

Si hapo tu,

Bali hata katika utendaji ufanisi wao ni wa kawaida sana ukilinganisha na wale walio kua medium au moderate performers mashuleni au vyuoni,

Mifano ipo mingi sana but nitaweka michache tu,

Mzee BAKHRESA anautajiri mkubwa sana na kila kukicha anazidi kupanua wigo wake wa kibiashara kwa kuongeza biashara zingine . Alianzia kuuza unga wa ngano kisha kapanua wigo mpaka kwenye biashara ya vinywaji n.k,

Pale UDSM ambapo tunaaminishwa kuwa ndio chuo bora kabisa nchini kuna maprofesor waliobobea kwenye masuala ya biashara na masoko lakini bado wanamaisha ya kawaida wana pesa ya mboga tu, na wanategemea teuzi kutoka kwa viongozi wa serikali ambao miaka kadhaa iliyopita walikuwa ni moderate students,

Tizama taasisi zinazo simamiwa na watu waliokuwa vipanga mashuleni zina hali gani mpaka sasa,
(Utapata jibu sahihi tumia mifano hai),

Sababu ni hii hapa

Unatakiwa uelewe concept mbili ambazo ni MEMORY na THINKING
Memory ni kumbu kumbu na Thinking ni kufikiri/ kutafakari
Ili ufauru mtihani unahitaji MEMORY (kukumbuka kile ulichokisoma), vipanga hufaulu kwa kuwa na uwezo mzuri wa KUKUMBUKA kile walicho kisoma, 
Pengine walikuwa vipanga kwa sababu walirudia rudia mara nyingi kusoma kile walichofundishwa,
THINKING (Kufikiri) ndiyo chanzo cha tatizo na ndio sababu inayofanya wasomi wengi kuwa na maisha ya kawaida na kipato cha chini ,

Matajiri wengi ni watu wenye elimu ndogo wanao umiza vichwa usiku na mchana kufikiria na kubuni mbinu za kuwaongezea kipato na kuboresha utendaji ,

Chukua muda kutafakari kwa nini watu wengi wenye GPA nzuri sana lakini hupigwa chini na watu wenye GPA ndogo ktk interview ,
Jibu ni kuwa kinacho angaliwa ni uwezo wa kufikiri na sio kumbu kumbu.

Tujijengee mazoea ya kufikiria na kutafakari.

HUU NDIO UGONJWA UNAO WASUMBUA WAHITIMU WA UDSM,

Karibuni tupigane kwa hoja.

Je Wajua ..Simba Hujitibu Maradhi Mbalimbali Yanayomsumbua kwa Kula Majani...!!!!?

$
0
0

SIMBA ni miongoni mwa wanyama ambao ni jamii ya paka, ukiondolea mbali kwamba ndiye mnyama mkubwa anayewinda katika jamii yao hiyo, lakini pia ni wanyama ambao hupenda kuishi kwa makundi makundi. Kwa lugha nyingine naweza kusema wanaishi kifamilia kama ilivyo kwa binadamu na familia zao huweza kuwa na simba takribani kumi na watano.



Njia rahisi ya kuwatambua kwa jinsia zao ni muonekano pamoja na majukumu, wakati simba dume shingoni likiwa limejaa manyoya mengi, simba jike huwa na manyoya sawa mwili mzima, hapo ni kwa mtazamo wa namna wanavyoonekana.

Katika majukumu, simba hugawana kazi ya kuhakikisha chakula cha kutosha kinapatikana katika familia, hilo ni jukumu la simba jike na simba jike aendapo mawindoni jukumu la simba dume ni kulinda mipaka tu. Uzito wa mnyama huyu huwa kati ya kilo 120 mpaka 240 inategemea na umri pamoja na afya.


Uhai wa simba kuishi ni kati ya miaka 10 mpaka 14 lakini kwa simba wa Afrika hufika hadi miaka 17 na zaidi. Simba huanza kufundisha mbinu za uwindaji watoto wake tangu wakiwa wadogo kabisa, ambapo huwatanguliza mbele na kuanza kuwabughuzi kwa kuwapiga piga ngwala, jambo ambalo hufanya watoto wake kuwa wenye hasira na wakali sana na mbinu hizo ndio hutumia akiwa anawinda ukubwani.

 Simba mara zote hupendelea kukaa sehemu ambazo kuna miamba mizuri, pamoja na nyasi kavu kavu ambazo hufanana kwa mbali na rangi yake, kwakuwa huishi kifamilia dume ndio huanzisha makazi mapya, ambapo likiunguruma kwa sauti yake, sauti hiyo husafiri umbali mrefu na sehemu inayoishia ndio huwa mpaka wa makazi yao na kama katikati ya sauti hiyo itakumbana na makazi ya simba wengine, basi dume jingine litaitikia, hapo kinachofuata ni simba hao kuhama lakini kama hawatakubaliana kutoka basi madume ya pande hizo mbili yatakutana kuoneshana ubabe na litakalokubali kushindwa litaondoka na familia yake.

Simba dume huchukia sana jike akizaa dume, hasira yake huja pindi anapoyafikiria madaraka, kwani hutambua jamaa hao ndio watakao kuja kumpindua ili wao ndio wawe watawala, hivyo chuki yake hukuwa kila watoto hao wanapozidi kuongezeka kimo. Jukumu kubwa la kuyalinda madume hayo huwa chini ya mama yao, siku akizembea tu simba dume huvinyonga kikatili, mtifuano huo huwa hauishii kwa watoto tu. Hata simba dume linapozeeka na kushindwa kutimiza majukumu yake kwa ustadi hufukuzwa kabisa na wanafamilia wenza na nafasi yake itachukuliwa na simba dume ambaye anachipukia kwa wakati huo.

Kwa jina la kisayansi simba huitwa Pantela Leo, kuna msemo usemao akikosa nyama basi hula majani, msemo huu si sahihi inapotokea simba anakula majani si sababu ya njaa, bali hutumia baadhi ya mimea hasa majani, kama tiba pindi anaposumbuliwa na ugonjwa hususani tumbo.

Pamoja na kutumia tiba hiyo, lakini pia wana tabia ya kunyanyapaa simba mwenzao hasa anapopata ugonjwa ambao huonekana ni hatarishi katika jamii yao, badala ya msaada wenzie huamua kumtenga na kumfukuza ili kuepuka ugonjwa huo kusambaa zaidi.


Majambazi wajeruhi na kupora fedha na dhahabu katika mgodi

$
0
0

Kundi la watu wanaosadikiwa kuwa majambazi wamevamia mgodi wa dhahabu wa wachimbaji wadogo katika kijiji cha Nyakavangala kilichopo katika tarafa ya Isimani wilayani Iringa na kupora fedha tasilimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 80 na gramu 400 za dhahabu huku wakiwajeruhi watu tisa.

Majeruhi wa tukio hilo la uporaji ambao baadhi yao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa wamesimulia tukio hilo lililotokea siku ya tarehe 9 mwezi huu majira ya saa moja jioni ambapo kundi hilo la watu walivamia mgodini hapo na kuanza kuwasaka watu waliowataja kwa majina na kuwalazimisha baadhi ya wachimbaji kuwaonesha walipo watu hao.

Baadhi ya majeruhi hao wameiomba serikali kujenga kituo cha polisi katika eneo hilo la mgodi ili kuimarisha usalama wakisema kuwa uporaji huo ulifanyika kwa muda mrefu huku kukiwa hakuna msaada wowote kutokana na eneo hilo kutokuwa na kituo cha polisi wala huduma ya mtandao wa simu hali iliyowafanya majambazi hao kufanya tukio hilo kwa muda wa zaidi ya saa kwakuwa walijua hawatabughudhiwa wala kufurushwa na vyombo vya usalama.

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amesema Jeshi la Polisi linaendelea kuwasaka waporaji hao tangu walipopata taarifa hizo hapo jana na kuongeza kuwa serikali inashirikiana na wachimbaji katika eneo hilo la Nyakavangala kuratibu ujenzi wa kituo cha polisi ili kudhibiti usalama wa eneo hilo huku muhudumu wa afya wa Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa Bi Gloria Mnyonge akielezea hali za majeruhi hao.

Washauri wakuu wa waziri mkuu wa Uingereza wajiuzulu

$
0
0

Washauri wawili muhimu wa waziri mkuu wa Uingereza, Theresa May wamejiuzulu.
Pia kuna ripoti kwamba wanachama wakuu wa chama tawala cha Uingereza, cha Conservative, wametishia kuanza kutafuta kiongozi mpya, endapo washauri hao hawatotolewa kazini.

Mpambe wake, Nick Timothy, alisema anabeba dhamana kwa mchango wake katika kampeni ya chama, lakini alisema bado anaamini manifesto ilikuwa sawa, manifesto ambayo mwanachama mmoja maarufu alisema ni mbaya kabisa katika historia.

Msemaji wa chama amesema, mwenzake Bwana Timothy, Fiona Hill, piya amejiuzulu.
Bibi May anajaribu kuunda serikali ambayo haina wingi wa viti bungeni, kwa kutegemea chama kimoja cha Ireland Kaskazini.

Wanahabari toka Ubelgiji wapo nchini kumfuatilia Samatta

$
0
0

Waandishi wawili wa habari wamesafiri kutoka Ubelgiji kuja nchini kwa ajaili ya kumfuatilia mshambuliaji wa kimataifa Mbwana Samatta anaecheza kwenye klabu ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji.

Gauyentie Bogouet pamoja na Marc Cornelissen ambao wanaandikia gazeti la Het Belang van Limburg na website ya www.HBVL.BE wana siku tatu tangu wafike Tanzania na leo watatembelea familia ya Mbwana Samatta.

Lengo kuu la safari yao ni kutaka kujua kwa undani alipotoka Samatta njia alizopita kabla ya kutua Genk maisha na tamaduni za taifa anakotokea.

“Tupo hapa kwa siku mbili sasa (jana) tumekuja kwa ajili ya kutaka kujua zaidi kuhusu Samatta alipotoka alikopita na namna alivyofanikiwa kufika Genk. Kesho (leo) tutatembelea nyumbani kwao kwa ajili ya kukutana na familia yake,” alisema Cornelissen mara baada ya kumalizika kwa mechi ya Tanzania vs Lesotho.

Waandishi hao walikuwepo kwenye mechi kati ya Stars dhidi ya Lesotho na walishuhudia Mbwana Samatta akifunga goli katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya kufungana bao 1-1.

Huenda ziara yao ikawa na faida kwa wachezaji wa Tanzania kwa sababu wamepata fursa ya kushuhudia mechi na kuwaona baadhi ya wachezaji wakiwa katika kiwango bora katika mchezo huo hivyo huenda katika ripoti yao wakashauri vilabu vya Ubelgiji kuja Tanzania kusaka vipaji.

Mkurugenzi mkuu Ewura asimamishwa kazi

$
0
0

Mkurugenzi mkuu Ewura asimamishwa kazi soma zaidi hapa chini:
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images