Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Taarifa za Kuzushiwa Kifo zimemfikia King Majuto, Katuma Ujumbe ‘Sote tutakufa’

$
0
0
Siku chache zilizopita kulikuwa na taarifa za uzushi zilizokuwa zinaenea kumuhusu Mchekeshaji maarufu Bongo, Amri Athuman ‘King Majuto’ zikidai kuwa amefariki kutokana na kuumwa kwa muda.

Baada ya kusambaa kwa taarifa hizo zilimfikia mwigizaji na mchekeshaji Mboto Haji ambaye alisafiri hadi Tanga kujua kinachoendelea na kupost picha kwenye Instagram yake akiwa na Mzee Majuto nyumbani kwake na kutueleza hakuwa amekufa kama ilivyozushwa ingawa alikuwa mgonjwa lakini aliyekuwa na ahueni.

Sasa Ayo TV na millardayo.com zilifanya jitihada kumpata King Majuto ili kufahamu hali yake na kuhusu taarifa za kuzushiwa kifo kama zilimfikia na alivyozipokea:>>>”Mimi ni mzima niko nyumbani kwangu, nimeshatoka Hospitali. Nilipelekwa kwa maradhi ya henia, nimeshafanyiwa upasuaji na nyuzi zimeshatoka zote. Niko nyumbani nafanya mazoezi na kula kurudisha nguvu za mwili.

“Kitu ambacho kimeniudhi ni kwamba kuna Watanzania simu hawana kazi nazo. Wanapokuwa hawana kazi nazo wanaposti post vitu vya kipumbavu waache sio vizuri.” – Mzee Majuto.

Am Very Beautiful but Cant Keep a Man for Long

$
0
0
Hi Guys My Name is Cynthia. Iam a young beautiful woman and alot of men keep chasing me. But i have noticed a very worrying thing, i cant keep a man for more than 4 months. Every man who hooks up with me drops me after some time. Iam financially stable so i cant say iam a burden to them. Whenever i try to ask them what is the problem, none has told me the truth. They simply say, You are a very beautiful and sexy lady but you are not my Type. Iam now losing my self esteem. Is this Beauty of mine a curse?

yours Cynthia

Mwana FA na AY Kuikaba Koo TIGO....Kulipwa Sh Bil 2

$
0
0
Wasanii wakongwe wa Bongo Flava, Ambwene ‘AY’ Yesaya na Hamisi ‘Mwana FA’ Mwinjuma wameendelea kupeta mahakamani wakitarajiwa kulipwa kiasi cha shilingi bilioni 2.1 na kampuni ya Mic Tanzania Limited.

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali maombi ya Kampuni hiyo ya huduma za simu za mkononi iliyotaka kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa kupinga amri ya kutakiwa kuwalipa wasanii hao kiasi hicho cha fedha.

Hivi karibuni, Mahakama Kuu ilihalalisha uamuzi wa Mahakama ya Wilaya iliyoikuta na hatia ya kutumia bila kibali nyimbo za wasanii hao kama miito ya simu na kuitaka kuwalipa kiasi hicho cha fedha.

Wakili wa wasanii hao, Albert Msando aliweka pingamizi akiiomba Mahakama Kuu kuyakataa maombi yaliyowasilishwa na wanasheria wa kampuni ya Mic kwa madai kuwa ni batili kwani yalikuwa na makosa ya kisheria.

Jaji Isaya Arufani wa Mahakama Kuu alikubaliana na maelezo ya Wakili Msando na kuyatupilia mbali maombi ya wanasheria wa kampuni hiyo. Bado haijafahamika kama watafanya marekebisho na kurejesha maombi mapya au la.

AY na Mwana FA wanadai kuwa kampuni ya Mic Tanzania Limited ilitumia bila ruhusa yao nyimbo zao ‘Usije Mjini’ na ‘Dakika Moja’.

Nigeria Yaongoza Afrika Orodha ya nchi 10 duniani Ambazo Wanaume Huridhisha wake zao kitandani

$
0
0
Kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na misukosuko ya maisha, ukosefu wa chakula, magonjwa na kipato inaelezwa kuwa ndiyo sababu ya bara la Afrika kuwa la mwisho kwenye orodha ya nchi zenye wanaume ambao wanawaridhisha wake zao kwenye ndoa wakiwa faragha.

Kwa utafiti uliofanywa na mtaalamu wa masuala ya ya mahusiano an aliyebobea kwenye masuala ya ndoa, Bi Victoria Milan kupitia mtandao wake wa victoriamilan.com unaojihusisha na masuluhisho, ushauri na takwimu mbalimbali za mahusiano mtafiti huyo amesema nchi za Ulaya, ndiyo zinaongoza kwa wanaume kuwaridhisha wake zao kwenye ndoa ukilinganisha na mabara mengine kama Amerika, Asia na Afrika.

Bi Milan amesema kwenye utafiti huo alitumika idadi ya watu 9,165 walio kwenye ndoa kutoka nchi 80 za mabara ya Afrika, Ulaya, Asia na Amerika ya Kusini/Kaskazini ambapo kila nchi alihoji ndoa 80 hadi 82 kutokana na idadi ya watu wa nchi husika.

Kwenye takwimu hizo alipata wastani wa muda wa wapenzi wanaotumia wakiwa faragha kwa kila mzunguuko mmoja ambapo wastani wa nchi za Ulaya ulikuwa ni dakika 32.1 kwa kila mzunguumko mmoja wa tendo la ndoa ambapo nchi zilizoongoza ni Denmark, Finland na Sweden.

Bara lingine ambalo limefuatia ni Amerika ya Kaskazini/Kusini ambapo wastani wao ni dakika 23.4 wakiongozwa na nchi za Marekani na Canada.

Bara la tatu ni Asia na la mwisho kwenye utafiti huo ni Afrika ambapo wapenzi walio kwenye ndoa hutumia wastani wa dakika 5 kwa mzunguuko mmoja na nchi zinazoongoza kwa kukaa muda mrefu kwa mzunguuko mmoja ni Nigeria na Afrika Kusini.

Orodha ya nchi hizo ni kama ifuatavyo NB: Huu ni muda ambao wanaume hutumia kwa kila mzunguuko mmoja bila ya maandalizi.

1- Denmark Dk 43

2-Marekani Dk 41

3- Finland Dk 39

4- Canada Dk 36

5- Norway Dk 34

6- Uingereza Dk 33

7- Ujerumani dk 31

8- Czech Republi Dk 29

9- Ireland Dk 27

10- Austria Dk 27

Kwenye orodha hiyo ya 10 bora duniani hakuna hata nchi moja kutoka Afrika ingawaje nchi ya Nigeria imeingia kwenye 20 bora kwa kushika nafasi ya 19 ikiwa nawastani wa dakika 20 ikifuatiwa na Afrika Kusini nafasi ya 20 ikiwa na Wastani wa dakika 18 pekee.

Sababu kubwa zilizotajwa kwa wanaume wengi kwenye ndoa kutumia muda mfupi kwenye tendo hilo ni uvivu, Mazoea, majukumu ya kila siku, msongo wa mawazo na aina ya vyakula .

“Wakati nafaya utafiti wanandoa wengi hususani wanawake walisema kabla ya ndoa wenza wao walikuwa wakitumia muda mwingi kuwaandaa na hata kwenye tendo lenyewe lakini baada ya kuishi nao walianza kupoteza uwezo wao kitandao”,amesema Bi Milan kwenye mdahalo wa kipindi cha Loose Women kinachorushwa na kituo cha itv cha Uingereza .

Hata hivyo kwenye utafiti huo amebaini kuwa Wanawake ambao wanaridhishwa na wenza wao bado wanaonekana ni vijana wenye afya na nyuso zenye furaha ukilinganisha na wale ambao hawaridhishwi kwenye tendo la ndoa.



Bongo5

CCM si wa Mchezo yaibomoa CHADEMA Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro

$
0
0
Pole pole akiwa Mkoani Kilimanjaro anasema yafuatayo.

Kuna viongozi kadhaa kutoka Upinzani wameikubali kazi na kasi ya Rais Magufuli. Lazima tuwapokee kwa heshima kubwa.

Watu hawa wametumia Uhuru na haki yao ya Kidemokrasia na kuamua kuondoka katika vyama vyao na kujiunga na CCM. Ni watu wazito.

Wafuatao ni Madiwani wamejiondoa CHADEMA na kumuunga mkono Rais Magufuli(Wamehamia CCM).

1- Diwani wa Kata ya Machame Magharibi. Ndugu, Goodluck Kimaro ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Wilaya ya Hai(CHADEMA). Hivyo nimeamua kumuunga mkono Rais Magufuli.

2- Diwani wa Kata ya Weruweru,

3- Diwani wa Kata ya Mnadani Wilaya ya Hai, Ndugu Everist Peter Kimati amesema kuwa japokuwa walipata ushindi mkubwa 2015 lakini ndani ya chama kulitokea mpasuko uliosababishwa na uhujuma ndani ya uchaguzi wa ndani ya chama.

Katibu wa Itikadi na Uendezi wa CCM, Ndugu Humphrey Polepole amesisitiza kuwa kuna lundo la viongozi wa Uponzani wanaotaka kujiunga na CCM.

Deni la ACACIA: Mdau Mmoja wa Kigeni Kanena Haya Mtandaoni....

$
0
0
Kaandika:

Doing business in Tanzania-Going to the moon is cheaper.

Akaongeza:

That US $190 billions is 10 times the budget for NASA.

Akamalizia:

May be the Goverment of Tanzania is planning space programme with Acacia billions.

Naona hata CNN nao wameripoti hii habari.

My take:

Hii inaweza kutuathiri sana katika uwekezaji.
Add caption

PENDEZA na Kessy Products, Kutoa Mvi, Kurefusha Nywele, Tengeneza Shepu na Mengine

$
0
0
PENDEZA NA KESSY PTODUCT:-MSIMU MPYA WA 2017_ BIDHA AINA ZOTE KWA UBORA MZURI%
PATA DAWA ZA ASILI ZISIZO NA MAD, HARA NA MATOKEO NI KWAHARAKA BAADA YA WEEK (2-/-4) 🍎🍌🍉☘
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _80,000/
2) KUREFUSH NYWELE KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA _80,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO FIGA UMBO (8) NA KUJAZA HIPC NA KALIO @ KUPAK _80,000/
@ KUNYWA AU VIDONGE _130,000/ 4) KUPUNGUZA NYAMA ZA MIKONO TUMBONI ZILIZOTEPWETA _80,000/
5) PUNGUZA KITAMBI KWA HARAKA KWA DAW HIZI ZA KUNYWA
@) KUNYWAA _100,000/
@) VIDONGE _100,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KGM 150 ADI 80 KIASI UNACHOTAK WEWE KWA DAW HIZI
@) DAW YAKUNYWA YA _100,000/
@) VIDONGE VYA HARAKA _100,000/
7) PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KWA MUDA WA WEEK MOJA _70,000/
8) ONGEZA MAZIWA NA SAIZ UNAYOTAKA WEWE _70,000/
9) ONGEZA MWILI MZIMA NA KUKUPA HAMU YAKULA KWA RIKA LOLOYE _80,000/
10) TOA MICHIRIZI SUGU PIA NA ILE YAKUJIFUNGUA MWILI MZIMA _70,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KATIKATI YA MAPAJA _70,000/
13) KUWA MWEUP NA SOFTI MWILI MZIMA NA KUTOA WEUS MACHON NA VIMISHIPA VIDOGO VIDOGO @ MAFUTA YA KUPAKA _80,000/(@) VIDONGE (WHITE SOLUTION) _120,000/
14) ONDOA NDEVU NA VINYWELEO MWILINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME NA KUIMARISHA MISHIPA ILIYO LEGEA KWA DAW HIZ
@) JEL KUPAKA (MEN GEL) _70,000/
@) VIDONGE (MAXMAN) _80,000/
16) ONGEZA MAUMBIL YA KIUME SAIZI UNAYOITAKA WEWE KWA:
@) (HANDSOME UP) MASHINE _170,000/
@) JELI YAKUPAKA INABORESHA ANZIA NCHI (4 ADI 6 )_100,000/ PIA NA VIDNGE VYAKE VIPO
17) RUDISHA HAMU YA TENDO LA NDOA KWA WALIOPOTEZA KUTOKANA NA NGIRI, KISUKARI NA MAGONJWA MENGINE KWA _80,000/
18) RUDISHA USICHAN(BIKRA)Na KUTO UCHAFU SEHEMU ZA SIRI _80,000/
19) FANYA USO WAKO KUWA MKAVU NAKUTOA VIJIPELE ILIYOSABABISHWA NA MAFUTS MAKALI _80,000/
20) ONDOA MAKUNYANZI USONI _70,000 (21) ENGEZA MGUU WAKO _70,000/ TUNAPATIKAN K/ KOO NA SINZ
MAPAMBAN, KWA MIKOAN DUNIAN KOTE UTAPATA

 (+255) 0719955528
0756259180
0785371237

@dr_kessy_product
Delivery POPOTE ULIPO,

Shilole ‘Ampuuzia’ Gigy Money

$
0
0
Baada ya choko choko za kila mara kutoka kwa Gigy Money kwenda kwa msanii Shilole, hatimaye msanii huyo ameonyesha kuchukulia poa choko choko za video vixen huyo.

Siku zilizopita Gigy Money alidai hawezi kufanya muziki na Shilole kwa sababu hamshabikii na hajawahi kupenda muziki wake, pia hivi karibuni alidai Shilole hajui kuongea kingereza vizuri.

Kupitia 5 Selekt ya EATV Shilole amesema ni kweli hajui kingereza vizuri, na anamchukulia Gigy Money kama mdogo wake.

“Ni mdogo wangu kwa hiyo lazima apite kwa dada yake, kwa hiyo watu kama hao wadogo zangu ninawachukulia poa tu, hamna tatizo,” amesema Shilole na kuongeza kuwa.

“Kingereza is not my language, kwa hiyo nikisema bado hainilazimishi kukijua sana lakini najifunza kuongea, na pale panapobidi nitaongea. Hiyo ni kweli hamna shida kama sijaenda (shule) ni sawa, kwani watu wangapi hawajaenda shule, ukiwa umeenda shule na hela uwenayo,” amesistiza.

Makala: Alikiba Ukishindwa Kujifunza kwa Davido Jifunze Hata kwa Aslay

$
0
0
Katika maisha kuna muda hata kama ungejiita mjuaji wa kila kitu lakini kuna muda itakupasa kusikiliza maoni ya wengi hususani yale ambayo unaona yanaelekea kwenye ukweli kwani hata waliosema’ waliowengi wape’ walikuwa na maana hiyo bila shaka.



Msemo huu unanifanya nimfikirie kwa kina Mfalme wa Bongo Fleva, Alikiba kama mwenyewe anavyojiita King Kiba, kuwa ni kweli hasikii wala kusoma maoni ya mashabiki wake?, mashabiki ambao kila uchao wanaolia atoe wimbo mpya huku yeye akiendelea kupuuzia kilio chao na kuwaacha mashavu yao yakilowa machozi.

Bila shaka yoyote AliKiba kama utaendelea na mwendo wako wa kutoa ngoma moja kila mwaka kwa soko la muziki jinsi lilivyo hapa barani Afrika utasahaulika kwa kizazi hiki ambacho hakishabikii msanii bali kinashabikia kazi unazotoa.

Anyway inawezekana ukawa bado una mtazamo wako wa kutopangiwa na mtu kama ulivyosema siku moja kwenye mahojiano yako na kituo cha Radio cha Kiss FM cha nchini Kenya, nanukuu “sitaki kuwasikiliza hao  kwa sababu nina Target yangu ninavitu vya kufuatilia  sitaki  hata mtu yeyote aniingilie kwenye Target yangu kwahiyo kama utawafuatilia utapotea sifanyi muziki kwa kushindana kama hao watafanya muziki kwa kushindana nitawaacha washindane “



Hapo nilianza kupata mashaka baada ya kusikiliza mahojiano yako kuwa hutaki kuwasikiliza mashabiki wako na hufanyi muziki wa kushindana, Je muziki unaoufanya ni muziki wa aina gani na nini? na kwanini uhangaike kila siku kwenda kushoot video nje ya nchi ile hali muziki wako sio wa ushindani?

Mosi kauli ya kusema unafanya muziki bila ushindani naifananisha na ile inayosema nafanya muziki for fun ambayo mpaka sasa sijaisikia tena kwani hata waimbaji wa muziki wa kisingeli nao wenyewe wanaushindani hii yote ili kuleta ladha ya muziki.

Pili kama utakuwa unafanya muziki usiokuwa na ushindani basi tukubaliane na wewe kuwa muziki wako pia sio biashara unafanya kwa kujifurahisha kitu ambacho kiuhalisia kina kinzana na kauli yako.

 Kilio cha mashabiki wako 

Ni mwaka sasa umepita AliKiba hajatoa ngoma kitu ambacho kwa muziki wetu wa kiafrika ni rahisi sana kusahaulika kwenye soko kwani mashabiki wengi wa muziki hawaangalii Msanii anafanya biashara gani nje ya muziki bali huangalia ana nyimbo gani katoa na kuanza kumsikiliza hii ni tofauti na mashabiki wa Ulaya au Marekani.

Kitu ambacho Alikiba ameshindwa kuendana nacho ni kukaa muda mrefu bila kutoa nyimbo kitu ambacho mashabiki wake hufikia muda na kuanza kumsahau huku akiwaahidi kuendelea kusubiri na ahadi ya kuku kwa vifaranga wake kuwa “ipo siku nitawapa maziwa”.

Pitia maoni ya baadhi ya mashabiki wake jinsi wanavyoumizwa na ahadi zake za ngoja ngoja kwenye mitandao ya kijamii.

andesyzabron360Yani alikiba tumekuchoka xana yani wewe msanii gani unashindwa na wasanii wachanga hebu angalia hata Asley anakushinda kila Siku anatoa ngoma juu ya ngoma wewe unabakikucheza na TEMBO tumekuchoka xaxa tunahamia WASAFI kupiga selfu na TIFA wewe cheza na tembo TU
___aysher___the___modestyYaani ALIKIBA yupo SLOW sana na mashabiki ndo wanampa kiburi kumsifia ujinga Hivi msanii gani ukae mwaka mzima nyimbo mpya huna kiki huna Ukiulizwa eti mziki ni business biashara gani Hyo huleti bidhaa mpya kwa wateja wako endelea kukaa kimya me saivi TEAM MZIKI MZURI No matter nani ameimba Bora univutie tu!
chugaellynaandika sms hii huku moyo wangu ukisononeka nimepitia sms za mashabiki wezangu nikagundua tulioumia kisa ali kiba kuto achia ngoma ni wengi na nina apaa itakuwa nimwazo namwisho kuku fatilia tena mpaka pale utapotoa sababu yenye kueleweka nn chazo chakuchelewesha ngoma
Haya ni baadhi ya maoni ya mashabiki wako ambao mamilioni ya mashabiki wanasononeka, sitaki kuamini kama Alikiba husikii kilio cha mashabiki hawa ambao asilimia kubwa uvumilivu umewashinda kwa ngoja ngoja zako.

Kwanini Davido au Aslay?

Davido mwanzoni mwa mwaka 2016 alivyosainiwa na Sony alikaa karibia mwaka bila kuachia ngoma, kitendo ambacho mashabiki wake walianza kumuandama mitandaoni wakimshinikiza kutemana na Sony kama wanambana asiachie ngoma kitu ambacho hata Davido mwenyewe alianza kuona kinampoteza na alijaribu kuonesha hisia zake kuwa hakufurahia hali ile kwani alianza kupoteza mashabiki.



Baada ya malalamiko hayo Davido akaanza kurejea kwenye maisha yake ya kawaida na kuanza kuachia ngoma juu ngoma ambapo kuanzia Novemba mwaka jana hadi Julai mwaka huu, tayari kaachia nyimbo nne ambazo zimemfanya mwaka huu kupokelewa vizuri zaidi tofauti na mwaka jana ambapo hata yeye mwenyewe alikiri muziki wake uliyumba kutokana na kukaa kimya kwa muda mrefu bila kutoa ngoma kitu ambacho kilimfanya hadi kukosa nominations kwenye tuzo kubwa duniani.



Kwa hiyo Alikiba ni vema ukatumia kilio cha mashabiki wako kiwe kama chachu ya kudondosha ngoma kali kwa muda kwani ni Wasanii wachache sana wanaolazimishwa na mashabiki wao kuachia ngoma na ni bahati kwako kwani wapo wasanii wengi hawatoi ngoma na bado hawaulizwi na mashabiki wao.

Kama kwa Davido ni mbali basi jifunze kwa Aslay ambaye baada ya kundi la Yamoto Band kuyumba kwa mwaka mmoja huku watu wengi wakiamini kuwa kundi hilo limekufa pamoja na wasanii wake ambao walikuwa wakitoa ngoma kila mwezi kipindi cha nyuma. Nakumbuka wakati anatangaza kuwa ataanza kuachia ngoma zake kama Solo Artist wengi walimbeza kuwa hawezi kurudi kama miaka ya nyuma alivyokuwa akifanya muziki peke yake kabla ya Yamoto Band.

“Nawahakikishia mashabiki wangu nitarudi kama zamani kwani hapa katikati tulisimama kidogo ila kwa sasa nitatoa ngoma kama Solo Artist”,alisema Aslay kwenye mahojiano yake na kituo cha redio cha  Clouds Fm.

Baada ya hapo Aslay akaanza kuwarudisha mashabiki wake kwa kuachia ngoma juu ya ngoma yaani kuanzia Januari mpaka Julai mwaka huu tayari ameachia ngoma kubwa tano kitu ambacho kwa sasa ukipita kila mitaani, ukisikiliza Radio au kutazama TV hauwezi kukwepa kukutana na ngoma zake hicho ndio kitu mashabiki wanataka, na sio ahadi nyingi.

Ushauri wangu kwa Alikiba

Mosi, Alikiba jifunze kuchukua na kuyafanyia kazi maoni ya mashabiki wako kwani hao ndiyo wamekufanya ufike hapo ulipo usipuuze kwani mtaji wa msanii yeyote duniani ni mashabiki wake.

Pili, kwa aina ya mashabiki wa muziki wa Afrika hususani Tanzania hawaangalii unafanya nini nje ya muziki wako, wanachoangalia ni ngoma tu ndio maana hata Davido alivyokuwa kimya mashabiki walimuandama mitandaoni wakidai atoe ngoma haimaanishi alikuwa hafanyi show au hakuwa na biashara nyingine ila mashabiki wake walitaka kusikia ngoma kutoka kwake.

Tatu, sitaki kuamini kuwa una Menejimenti mbovu kiasi hicho, mimi ninachoamini ni kwamba una Menejimenti nzuri ambayo inauwezo wa kila kitu hivyo ni bora ukawapa taarifa kama Davido alivyowachana ili wakupe muda wa kutoa ngoma kwa wakati, Alikiba wewe sio Msanii wa kukaa mwaka mmoja na wimbo mmoja wa AJE bila kutoa ngoma nyingine mpya ni maumivu kwa sisi mashabiki wako ambao tunataka kazi tuu na sio ahadi.

Naamini baada ya makala haya Alikiba na Menejimenti yako mtawapoza maumivu mashabiki wenu kwa kuachia ngoma mpya kwani wanaumia na nyie hamsikilizi vilio vyao mnaacha machozi yao yanafutwa na wasanii wengine ambao ni washindani wenu wakubwa.

Breaking News: Bunge Limeridhia kuvuliwa Uanachama Wabunge 8 wa CUF

$
0
0
Siku moja baada ya Spika wa Bunge Job Ndugai kupokea barua kutoka kwa Mwenyekiti wa CUF Taifa anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili, Prof. Ibrahim Lipumba inayoeleza kuwafukuza uanachama Wabunge wanane wa Viti Maalum na Madiwani wawili, Bunge limeridhia.

Leo July 26, 2017 taarifa kutoka ofisi ya Bunge imeeleza kuwa Spika Job Ndugai ameridhia kufutwa uanachama kwa Wabunge hao na hivyo nafasi zao ziko wazi.

Prof. Lipumba alitangaza kuwafuta uanachama Wabunge wanane na Madiwani wawili kwa makosa mbalimbali yakiwemo ya kinidhamu, kukihujumu chama, Kumkashifu na kumdhalilisha Mwenyekiti.

Kwa mujibu wa  taarifa hiyo, Spika Ndugai amejiridhisha kuwa Wabunge hao wamefutiwa uanachama kulingana na taratibu za chama hicho na hivyo hawana sifa za kuendelea na Ubunge


Shaffih Dauda, Mwenyekiti DRFA Wakamatwa na Takukuru

$
0
0
Wadau mbalimbali wa soka wakiwemo wagombea wa uchaguzi katika nafasi mbalimbali za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wamekamatwa jijini Mwanza.

Baadhi ya waliokamatwa ni pamoja na Mtangazaji wa Clouds FM, Shaffih Dauda, Mwenyekiti wa Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA), Almas Kasongo.

Imeelezwa walikamatwa jana saa tatu usiku jijini humo wakituhumiwa kujihusisha na vitendo vya rushwa ikiwa ni kuelekea uchaguzi huo utakaofanyika Agosti 12 mjini Dodoma.


Wengine waliokamatwa ni pamoja na Elias Mwanjale,  Leonald Malongo, Effam Majinge, Osuri Kasuli, Richard Kayenzi, Lazack Juma na Kelvin Shevi.

Msemaji wa Takukuru jijini hapa, Ernest Makale amethibitisha kukamatwa kwao na kusema wamehojiwa.

“Tumewahoji na kuwaachia kwa dhamana, sasa uchunguzi unaendelea,” alisema.

Imeelezwa watuhumiwa walisema kwamba walifika jijini Mwanza kwa ajili ya uzinduzi wa michuano ya Ndondo Cup jijini humo

Hatimaye Maradona Akiri Bao Lake la ''Hand of God'' Halikufaa Kukubalika

$
0
0
Diego Maradona ameunga mkono utumiaji wa kanda za video licha ya kukiri kwamba bao lake la ''Hand of God'' dhidi ya Uingereza 1986 halikufaa kukubalika.

Maradona alitumia mkono wake kufunga bao ambalo liliisaidia Argentina kuishinda Uingereza 2-1 katika robo fainali ya kombe la dunia miaka 31 iliopita.

''Kwa kweli mimi hukumbuka bao hilo kila mara ninapounga mkono utumizi wa teknolojia'' ,Maradona aliambia Fifa.com.

''Nilifikiria kuhusu bao hilo na kwa kweli bao hilo halikufaa kuidhinihswa''.

Maradona anasema kuwa alifaidika kutokana na ukosefu wa teknolojia katika kombe la dunia na haikuwa mara moja bali mara mbili.

''Nitakwambia kitu chengine -katika kombe la dunia la 1990 nilitumia mkono wangu kuondoa mpira uliokuwa karibu kuingia katika goli letu dhidi ya taifa la Usovieti.

''Tulikuwa na bahati kwa sababu refa hakuona.Hakukuwepo na teknolojia wakati huo lakini sasa ni mambo mengine''.

Faida Za Pilipili Kichaa Kiafya Na Kitiba

$
0
0
Pilipili kichaa inaweza kustawi sehemu mbalimbali na inahitaji siku 100 za ukuwaji.

Hustawi zaidi kwenye mazingira ya joto na unyevunyevu.Mmea huu hukua kufikia urefu wa futi mbili hadi nne.

Ina wingi wa

vitamini A
pia ina vitamini B,
vitamini E,
vitamini C,
Riboflavin,
Potassium,
Manganese.


- Jamii nyingi hususa Marekani na bara la Asia wana historia ya kutumia pilipili kichaa kama tiba.

Ni dawa yenye nguvu sana na matumizi mengi,

hutumika sana kwa kusafisha damu na
kutoa sumu mwilini,
pia hutumika kusisimua mzunguko wa damu na
kuweka sawa uwiano wa tindikali(acid)mwilini.


Pilipili kichaa imetumika kwa maradhi tofauti tofauti ikiwemo moyo,

gauts,
kupooza
homa,
kikohozi,
tonsilatis,
kichefuchefu
hemorhoids

kwa miaka mingi huko Asia na mashariki ya mbali.


MAAJABU YA PILIPILI KICHAA;
1.Kutibu kidonda-Hii inaweza kuwa ni ajabu kwa walio wengi lakini ni tiba liyothibitishwa na imekuwa ikitumika miaka kadhaa iliyopita katika nchi mbalimbali.Sio tu kuzuia kutokwa na damu katika kidonda cha kujikata kama ilivyozoea kutumiwa na wengi huko majumbani kwa miaka mingi bali pia huzuia fangasi na bakteria kuingia katika uwazi wa kidonda hicho hutumika pia kuondoa sumu mwilini

2.Hufanya mwili kuweza kutumia vyema virutubisho vipatikanavyo kutokana na chakula

3.Husaidia uyeyushaji wa mafuta mwilini/Kuchoma mafuta

4.Pilipili ina antioxidants muhimu kama beta carotene,ina wingi wa vitamini A,C na K hebu tuziangalie vitamini hizo: a.Vitamini A husaidia kuweka sawa kinga ya mwili pia hutukinga na kansa na magonjwa ya moyob.Kazi ya vitamini C-ni kuzuia strock,magonjwa ya moyo,macho na kansa mbalimbali.Miili ya binadamu haiwezi kujitengenezea vitamini C,hivyo basi tunaweza kupata vitamini C kupitia chakula.c.Vitamini K-Husaidia katika ukuwaji wa mifupa,pia ni muhimu katika mzunguko wa damu.Pilipili zote huwa na Capsaicin ambayo kazi yake ni kupunguza maumivu,kuzuia kansa na magonjwa ya moyo.

5.Inasaidia sana kusawazisha sukari kwenye damu

6.Huwasaidia watu wanene(over weight) au wanaougua ugonjwa wa kisukari.Hii ni kwa mujibu wa watafiti katika chuo kikuu cha Tasmania uliochapishwa katika American Joarnal of Clinical Neutition mwezi julai 2006.

7.Inasaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti kwa kiasi kikubwa INSULIN kwa 60% baada ya kula chakula

8.Husaidia kupunguza maumivu na uvimbe kwenye tezi na vilevile huwasaidia wagonjwa wa RHEMATOID na ARTHRITIS kupata nafuu

9.Husaidia kuondoa mkusanyiko wa damu sehemu moja mwilini

10.Husaidia kufungua kwa haraka na kwa ufanisi pua zilizoziba kwa mafua na kukufanya upumue kwa urahisi.

11.Husaidia kupunguza uwezekano wa kupatwa na saratani ya utumbo.

12.Husaidia kuongezeka kiwango cha METABOLIC ambayo husaidia kuchoma mafuta

13.Husaidia kuongezeka kwa kiwango cha METABOLIC kwa 23% ndani ya masaa matatu.

14.Husaidia kupunguza cholestro na kupunguza kiasi cha fibrin katika damu.

Utofauti kati Ya Mwanamke na Mwanaume Katika Hisia Za Kimapenzi

$
0
0
Katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia inasadikika hakuna kitu ambacho kina nguvu sana kama mahusiano ya mapenzi, hata hivyo kutokana na nguvu hiyo ya mahusino, watu wengi husaani mwanaume ndio ambao wanaathiriwa kwa kiwango kiubwa na nguvu hiyo.

Watafiti wa masuala ya mahusiano wanazidi kusema ya kwamba, mwanaume kila baada ya dakika tano ni lazima awaze masuala ya kimapenzi, hii ni kutokana wanaume wengi hupenda zaidi jinsia ya kike kwa kuona kwa macho. Ndo maana ukichunguza kwa makini wanaume huwa wanakuwa wanazingatia zaidi katika kutazama jinsia hii ya kike mahali popote walipo.

Hivi hujawahi ona wanaume wamekaa mahali wanapiga stori ghafla akapite mwanamke mzuri mbele ya macho yao ghafla stori zile zikasimama kwa muda? Bila shaka umewahi kuona. Utawasikia wakisema kwa minong'ono aaah angalia kifaa hicho, wapo wengine utawasikia wakisema mcheki chura huyo. Hii ina maana ya kwamba macho ya mwanaume ndio chanzo kikubwa cha kuingia katika mahusiano kabla ya kumjua tabia aliyonayo mtu huyo.

Lakini ukweli ambao upo nyuma ya pazia ni kwamba wanaume wengi  huingia katika matamanio ya kimahusiono kwa kuona kwa macho zaidi tofauti na mwanamke. Hata hivyo mahusiano ya kimapenzi aliyonayo mwanaume ni matokeo ya macho yako. Kwa maneno mengine tunaweza kusema matamanio ya hisia za mwanamke yapo katika kuona zaidi kuliko kitu chichote.

Lakini ukienda upande wa pili wa shilingi, mwanamke huwa yupo tofauti sana ukilinganisha na mwanaume katika suala zima la kuingia katika mahusiano. Hisia za mwanamke huwa zipo zaidi katika maneno na mguso katoka kwa mwanaume. Hisia za mwanamke huwa hazipo katika kuona kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na mwanaume.

Mwanamke huamini sana katika maneno ambayo ataambiwa na mwanaume,  kwa mfano mwanamke akiambiwa anapendwa zaidi ya kitu chochote katika dunia hii mwanamke huamini hivyo,hivyo maneno ya mwanaume yana nafasi kubwa katika kuziteka hisia za mwabamke.

Lakini pia kama hiyo haitoshi mwanamke hupata hisia zaidi pale anapoguswa na mwanaume, hivyo ndo maana kama utakutana na msichana kwa mara ya kwanza atakaa usimguse katika mwili wake, hii ina maana mguso wa mwanaume una nguvu sana katika kuamsha hisia mwili wa mwanamke.

Hivyo kama ndivyo hivyo basi hii ni uofauti mkubwa ulipo kati ya mwanaume na mwanamke katika kuamsha hisia za kimapenzi. Na kitu kikubwa ambacho huongoza hamasa na kudumu katika mahusiona ya kimapenzi ni "mawasiliano" , mawasiliano ndiyo chachu kubwa katika mahusiano yenu. Hivyo kila wakati ili muweze kudumu katika mahusiano yenu hakikiasha unakuwa na mawasilino bora kati yako na mwenzi wako.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA..Anatibu Magonjwa Mbali Mbali, Kusoma Nyota na Mengine

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote


..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14.

Na Mengi zaidiWhatsapp/Calls +255 710 279 458
+255 710 279 458

Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Wivu wa Mapenzi Mbaya...Mama na Watoto Wake Wamwagiwa Tindikali

$
0
0
 VUMILIA Shengema (31) na watoto wake wawili wamemwagiwa tindikali wakati wakitokea dukani kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa mapenzi.

Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, linamsaka mtuhumiwa huyo, Emmy Kyando (40, mkazi wa Sai jijini Mbeya ambaye aliwafanyia kitendo hicho cha kinyama watu hao.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohamed Mpinga, aliwataja wengine waliomwagiwa tindikali kuwa ni Loveness John (11), mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Sinde na  Nancy Peter (5), wakazi wa Mtaa wa Mwanshinga, Kata ya Manga jijini Mbeya.

Walimwagiwa na kujeruhiwa na tindikali hiyo usoni, kifuani na mikononi Julai 19, mwaka huu saa tatu usiku.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mpinga alisema Emmy anadaiwa  kufanya kitendo hicho kutokana na wivu wa kimapenzi kwa kuwa ni mke mwenza  wa mwathirika.

Mpinga alifafanua kuwa baada ya mtuhumiwa kufanya kitendo hicho alikimbia  kusikojulikana na wasamaria wema waliwakuta waathirika wakiwa katika hali mbaya na kuwapeleka katika Hospitali ya Rufani ya Mbeya kwa ajili ya kupata matibabu.

Kamanda Mpinga alieleza kuwa juhudi za kumtafuta mtuhumiwa  kwa kushirikiana na mume wa muathirika huyo  aliyefahamika kwa jina la Lausi Kidagile ambaye naye ni mkazi wa Sae zinaendelea.

 “Jeshi la Polisi linalaani vikali kitendo hicho na tunaomba mwananchi yeyote mwenye taarifa zitakazofanikisha  kumkamata mtuhumiwa atupatie ili hatua za kisheria zichukuliwe,” alisema Kamanda Mpinga.

Akizungumza na Nipashe kwa taabu akiwa wadi namba mbili katika Hospitali ya Rufani Kanda ya Mbeya, muathirika wa tukio hilo, Vumilia Shangema, alisema mtuhumiwa alikuwa akimtolea lugha za vitisho mara kwa mara na aliahidi kuwa kuna siku atamjeruhi.

 “Nikiwa njiani  na wanangu ghafla nikaona mwanamke mmoja niliyemfahamu kwa jina la Emmy akinimwagia kitu usoni na sikuweza kuona tena, lakini nikakumbuka kuwa Emmy  aliwahi kuniambia kuwa atanifanyizia huku akinitolea vitisho vikali vilivyotishia usalama wa maisha yangu,” alisema  Shangema.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufani Kanda ya Mbeya, Goodlove Mbwanji, alithibitisha kuwapokea wagonjwa katika hali mbaya hususani mama wa watoto Shangema, akiwa ameharibika usoni na macho kutokuona kabisa huku mtoto Loveness akiendelea kupata matibabu na afya yake kuimarika pamoja na Nancy ambaye alitibiwa na kuruhusiwa.

Mbwanji alisema wanaendelea na matibabu kwa mama huyo na kwamba idara ya upasuaji pamoja na madaktari wengine bingwa wamemuwekea uangalizi mzuri ili apate matibabu stahiki.

Mrisho Gambo na Lema Watunishiana Vifua....Gambo Adai Atamchukulia Sheria Iwapo Atamtukana Rais na Serikali

$
0
0
Arusha. Wakati Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema akisema haogopi kusema ukweli, Mkuu wa mkoa huo, Mrisho Gambo amemtahadharisha kuwa hataacha kumchukulia hatua iwapo atamtukana Rais John Magufuli na Serikali yake.

Lema ambaye ameanza kufanya mikutano ya hadhara katika jimbo lake jana kwenye Soko Kuu la Arusha mjini alisema haogopi kusema ukweli hata kama akipingwa na baba yake mzazi.

“Taifa lipo kwenye mgawanyiko mkubwa, wakuu wa wilaya na mikoa wanafanya maamuzi kwa maelekezo kutoka ngazi za juu,” alisema.

Aliongeza kuwa hali ya demokrasia nchini ni mbaya kwa kuwa hakuna usawa na kuwataka viongozi kuomba hekima wanapopata mamlaka ya uongozi.

Kadhalika amezungumzia hatua ya kujiuzulu kwa Diwani wa Muriet, Credo Kifukwe akisema kuwa Chadema haihitaji jeshi la watu wengi bali la wachache wenye umoja. “Nimeteswa sana katika mji wa Arusha, lakini nawataka wafuasi wa Chadema msilipize kisasi kwa wanaohama chama. Leo wapinzani hawaruhusiwi kufanya siasa, lakini Rais anazunguka nchi nzima,” alisema.

Mbunge huyo alisema Tanzania inahitaji demokrasia ya kweli na amani ya nchi haiwezi kutunzwa na polisi isipokuwa kwa upendo wa Watanzania.

Pia, alimtaka Gambo kujipanga wakati wa uchaguzi mdogo wa madiwani kwa kuwa Chadema imejipanga kikamilifu. Katika mkutano huo, Lema aliwapandisha jukwaani madiwani wawili wa Chadema jijini Arusha, Obeid Meng’roriki wa Kata ya Terat na Ruben Ngowi wa Kimandolu huku akisema amesikia wanataka kujiuzulu nyadhifa zao.

Hata hivyo, madiwani hao waliposimama walisema wao hawana bei ya kuweza kununuliwa na mtu yeyote.

Wakati Lema akiyasema hayo, Gambo alisema Serikali ya Awamu ya Tano imejipambanua katika utendaji wake, hivyo mwanasiasa yeyote hataruhusiwa kutoa matamshi yenye kumdhihaki Rais na Serikali.

Akizungumza katika mkutano na viongozi wa madhehebu ya dini uliofanyika jana kwenye ukumbi wa mikutano wa AICC alisema: “Tumempa mbunge wa jimbo hili (Arusha Mjini) kibali cha kufanya mikutano na wananchi wake kwa sababu ni kiongozi aliyechaguliwa na wananchi, hatuna sababu ya kumzuia, ila hatutakubali kusikia kwenye mikutano yake akimtukana Rais wetu na Serikali yake. Akifanya hivyo tutamshughulikia.”

“Mtu yeyote anayetaka kuichezea Serikali na kutaka kukwamisha ajenda zake tutawang’oa iwe kwa greda au kwa namna nyingine yoyote, Rais Magufuli alipita nchi nzima akitoa ahadi zake na wamemchagua sasa wamwache atekeleze alichowaahidi wananchi.”

Gambo alitumia mkutano huo kuzungumzia kadhia ya rambirambi zilizotolewa kufuatia ajali ya wanafunzi wa Lucky Vincent iliyopoteza maisha ya watoto na wafanyakazi wapatao 35 na baadaye Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro na Lema kutilia shaka matumizi yake.

Breaking News...Tundu Lissu Aachiwa.......

$
0
0
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemwachia kwa dhamana Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema) na Rais wa Chama cha Wanasheria nchini, Tundu Lissu mapema leo asubuhi.
Lissu ametakiwa kudhaminiwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja ataweka bondi ya dhamana ya shilingi milioni 10 huku akiwekewa zuio la kutoka nje ya Mkoa wa Dar es Salaam bila kibali maalum cha mahakama.

Aidha kesi yake imepangwa kusikilizwa Agosti 24 mwaka huu baada ya wadhamini wake kukamilisha taratibu zote za kumdhamini.



Tundu  Lissu ambaye alikamatwa Alhamisi, Julai 20 mwaka huu, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) wakati akijiandaa kuelekea Kigali, Rwanda kwenye kikao cha Chama cha Wanasheria cha Afrika Mashariki (EALS), alifikishwa Mahakamani hapo Jumatatu Julai 24 na kusomewa mashtaka  ya kutoa lugha ya uchochezi dhidi ya Serikali, kosa ambalo anadaiwa kulitenda Julai 17.

Inadaiwa kuwa maneno hayo yalikuwa na lengo ya kuleta chuki dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alipotakiwa kukubali ama kukataa  makosa hayo na Hakimu Mashauri, Lissu alisema kusema kweli haijawahi kuwa kosa la jinai. Mahakama ya Kisutu ilimnyima dhamana Tundu Lissu, kesi iliahirishwa hadi leo Julai 27, 2017 ambapo amepewa dhamana.

FLORA Mbasha na Emmanuel Mbasha Watakiwa Kuacha Utoto...Kisa Kizima Hichi Hapa

$
0
0
Hakuna kazi ngumu kama kutoa ushauri kwa watu wenye mgogoro unaohusisha uhusiano wa kimapenzi, kwa sababu ni lazima upande mmoja utachukia, kwani ili kitu kiwe kizuri, ni lazima uwe mkweli kwa asilimia mia moja.

Ni lazima mmoja atachukia kwa sababu siku zote katika uhusiano wa kimapenzi, upande mmoja unakosea.

Barua yangu ya leo inawaelekea kaka na dada yangu, Emmanuel Mbasha na aliyekuwa mkewe, Flora, siku hizi akifahamika kama Madam Flora.

Dada yangu Flora, ninamkubali tangu alipoanza kufanya vyema na Wimbo wa Jipe Moyo, Majaribu na nyinginezo.

Dada Flora, wewe ni mtumishi wa Mungu, kama unaamini kuwa majaribu ni kipimo kwa mtu aliyeokoka, kwa nini unashindwa kumaliza bifu lenu kimya kimya ukizingatia kila mtu kwa sasa ana maisha yake mapya?

Hii ni kwa sababu ya ule unaodaiwa kuwa ujumbe wako kusambaa ambao ulimsema vibaya mumeo wa zamani, kwamba alikuwa chanzo cha kuachana kwenu.

Pengine maisha ya kistaa yamewaathiri au labda huenda bado mnapendana, lakini mbona mnafanya kama hili jambo la kutengana mmelianzisha nyinyi? Nasema hivi kwa sababu migogoro katika ndoa haijaanza leo na wala haitakwisha kesho, ni vitu vya kawaida ambavyo binadamu hupitia.
Sasa kama ilitokea kama ilivyotokea, kuna haja gani ya kupeana vijembe kila kukicha kana kwamba mnashindana kupata tuzo?

Maana kama mmeshindwana na kila mtu ana maisha yake, ya nini kuanza kufukunyua mambo ya faragha kwa watu ambao hawakuwepo huko?

Huko ni kujishushia heshima kwa wote, kwani wewe na mwenzio, mnatambulika kama Watumishi wa Mungu, wapo kondoo wengi ambao walikuwa wanapenda kuiga mfano wenu kama waimbaji na hata wanandoa.

Mmeachana basi, udhaifu na changamoto mlizopitia kwenye ndoa yenu zibaki mioyoni mwenu.
Ndoa yenu imefika mwisho, walimwengu wote wanajua hilo lakini mnapoanza kuchafuana mitandaoni, sidhani kama ni sahihi. Najaribu kuitafuta hekima ya Mungu kati yenu, siioni! Najaribu kujiuliza, mnachafuana kwa sababu ya uwepo wa mitandao ya kijamii au hata kama isingekuwepo mngefanya hivyo?

Kama ni ndoa kuvunjika yenu si ya kwanza, kama ni wanandoa kutibuana na kulumbana, nyinyi si wa kwanza, kama ni migogoro ya kwenye ndoa hata wazazi wetu wameipitia, lakini mbona sababu za mizozo yao hatuijui?

Kinachosikitisha ni kuona kaka Emma naye kaja kujibu mashambulizi kwa maneno makali na yenye vijembe ndani yake. Ingawa hakumtaja mwenzake moja kwa moja, lakini wanaojua fukuto hilo wanajua ndiyo maana vyombo vya habari vimeripoti.

Kaka Emma, mbona ndoa nyingi zina mifarakano mingi sana, mbona wanandoa wengi wameachana lakini wamebaki na vidonda vyao moyoni, si kila jambo la kujibu.

Wakati mwingine ili uonekane una hekima ni vyema ukapotezea tu kuliko kuanza kuandika maneno yanayoondoa hekima, uvumilivu, burasa na utashi wa Kimungu ndani yenu.

Wapo watu wengi ambao wamevunja ndoa zao na kila mtu akawa na maisha yake na wanasalimiana na kupendana kama watu wa kawaida, lakini kwa hiki ninachokiona kwenu si jambo jema, hakuna sababu ya kujengeana uhasama wakati mlioana ili mfurahie maisha lakini kwa kile kilichotokea basi kila mtu afanye yake kwa moyo mweupe.

Vinginevyo ni kama mnatafuta promo ili watu wajue uwepo wenu. Kuna njia nyingi nzuri na zenye mbolea zinazoweza kuwafanya muonekane mbele za watu, kama kufanya kazi yetu na kumtukuza Mungu kupitia nyimbo za Injili au hata kuwapa chochote watoto yatima au watu wenye uhitaji.
Haya mambo mnayofanya waachieni watoto wadogo wa Bongo Fleva wanaoamini kiki ndizo zitawapandisha badala ya kufanya kazi kwa bidii.

GABRIEL NG’OSHA | BARUA NZITO
Maoni & Ushauri:
+255 620 744 592
GPL

JE ni Kweli Mwanamuziki Dogo Janja Anatoka na Mrembo IRENE Uwoya....Jibu Hili Hapa

$
0
0
Mtangazaji Soudy Brown ametuletea U heard kwenye XXL ya Clouds FM ambayo inamuhusu staa wa Bongofleva Dogo Janja kudaiwa kuwa mapenzini na mwigizaji staa wa Bongomovie Irene Uwoya baada ya kudaiwa kuambatana pamoja kwenye safari ya Mwanza kuhudhuria Miss Ilemela.

Soudy Brown alimtafuta Dogo Janja lakini hakumpata hivyo akapiga stori na Madee ili aeleze chochote kuhusu issue hiyo ambapo alisema:
“Sina hizo taarifa za Uwoya labda wewe ndio unanipa taarifa hizo. Dogo Janja hajaniaga na sijui chochote kuhusu yeye na Irene. Ninavyojua mimi ni rafiki yake kama rafiki wengine. Sijawahi kuwaona pamoja, nasikia kama unavyosikia wewe. Nitazifuatilia.” – Madee.

Iko hapa FULL…bonyeza PLAY kusikiliza!!!
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images