Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Diamond Platnumz, Ababuu, Msami na Jaquar Walishatoka na Irene Uwoya..Mumewe Afichua Siri

$
0
0
Aliyekuwa mume wa muigizaji wa filamu nchini Irene Uwoya, mchezaji Hamad Ndikumana kutoka nchini Rwanda amefunguka mambo kibao ya moyoni kuhusu ndoa yake na mrembo huyo ambapo kwa sasa ameweka wazi dhamira yake ya kumpa talaka.

Ndikumana ametumia mtandao wa Instagram kueleza madudu yote yalikuwa katika ndoa yake huku akiwataja wasanii maarufu kuingilia ndoa yake.

Unasema sina aibu kuandika hayo mitandaoni, wewe uliona aibu kuwa kwenye mahusiano na msami mnyaka miwili ukiwa ndani ya ndoa ? mara ngapi nilikuuliza kuhusu huyo mtu ukalala chini eti uongo ? Mara ngapi nilikuuliza kuhusu kulala na Diamond ukaapa kufa ? ila mwisho wa siku mwenyewe kasema kwanini ilifanya vile. Mimi kama mjinga nilikutetea sana tena baada yako kuwaambia magazeti eti nimezimia kitu ambacho sijawahi kukanusha ila leo nakikanusa sijawahi kuzimia maishani mwangu…

Irene unakumbuka nilikuwa nilivyokuwa taabaaani karibu kufa huku upo mozambike unatanua na Ababuu hata ujali nataka kufa ? Na uliporudi hata ukutaka kuniona,but sikushaanga kwavile nilikuwa najua wewe ndo uliyofanya yote.ulikuja Rwanda kuniona baada ya kuondoka siku mbili yakaja ya JAGUAR ?…

Hayo ni machache kati ya mengi mno aliyoandika Ndikumana, wawili hao walifunga ndoa mwaka 2009 wakati mchezaji huyo akicheza soka hapa nchini, katika ndoa yao wamejaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume aitwae Krish.


Ruby Afunguka "Nilifanya Upumbavu na Usanii Kuhusu Ujauzito Wangu"

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Ruby ambaye hivi karibuni aliibua hali ya sintofahamu mitandaoni baada ya kupost picha akionyesha tumbo lake na wengi kuhisi ni mjamzito, amesema aliamua kufanya upumbavu kuhusu tukio hilo.

Akizungumza kwenye kipindi cha Friday Night Live kinachorushwa na East Africa Television na East Africa Radio, Ruby amesema hana ujauzito kabisa isipokuwa picha zilizoonekana akiwa na kitumbo alilitunisha tu.

"Actually hii itaonekana kama upumbavu sijui, ila niliamua tu kulitunisha tu tumbo langu, na si unajua Watanzania wanavyopenda ubuyu!! Ila sio mjamzito", alisema Ruby.

Ruby ambaye kwa sasa yupo kwenye mahusiano na kijana anayejulikana kwa jina la Genely Hb, kwa mara ya kwanza ameweka mahusiano yake wazi na kijana huyo, ambaye inasemekana alishawahi kugombana na wasichana wengine kwa ajili yake.

Kutana na Maalim Fadhal Rashid Kutoka Komoro ni Mtaalam wa Tiba za Asili

$
0
0
KUTANA NA MAALIM FADHIL RASHID KUTOKA KOMORO NI MTAALAM WA TIBA ZA ASILI

UNASHIDA NA MCHUMBA UNATATIZO PESA HAIKAI KURUDISHA MUME AU MKE KWA MUDA MFUPI MVUTO WA MAPENZI

MVUTO WA BIASHARA KUMSHIKA MUME AU MKE ASIKUSUMBUE

DAWA YA ( LIMBWATA )KUMTAWALA MPENZI WAKO KWA SABABU MAALUM KUSAFISHA NYOTA ILI UWE NA MUONEKANO

NA PIA ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA MASHARTI

NA KUMILIKI MALI DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZ UIPENDAYO

DAWA YA NGUVU ZA KIUME INAPATIKANA PIA ANAYO DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEP KUA NA UMBO BOMBA UMEIBIWA AU KUDHURUMIWA UTARUDISHIWA MALI YAKO NDANI YA MASAA 24 ANAFUNGA KESI NA KUPATA HAKI YAKO DAWA YA MVUTO WA BIASHARA KUUZA MALI YAKO KWA HARAKA KUZUIA CHUMA ULETE

NA KUONDOA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI ACHA KUTESEKA ACHA KUHANGAIKA MAALIM FADHIL RASHID

YUPO TANZANIA KWA AJIALI YAKO. CALL...
+255719362806/
+255763276239/

WhatsApp IMO +255785786436

Vimbwanga vya Uchaguzi Kenya...Kituo cha Kuhesabia Kura cha Upinzani Kenya (NASA) Chavamiwa

$
0
0
Ikiwa ni siku chache kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika nchini Kenya, Muungano wa Upinzani (NASA) umeishutumu serikali kuwa imevamia moja ya vituo vyake vya kuhesabia kura kilichopo eneo la Westlands jijini Nairobi.

Msemaji wa NASA ameeleza kuwa wanaume waliokuwa wamefunika nyuso zao walivamia ofisi hiyo wakafanya uharibifu na kubeba kompyuta, simu za mkononi na vitabu.

Kwa upande wake, serikali ya nchi hiyo imesisitiza kuwa hakuna uvamizi uliofanyika, . Mgombea wa upinzani Raila Odinga amesema kuwa atakubali tu kushindwa ikiwa uchaguzi utakuwa wa haki.

Hivi karibuni, Rais wa Uhuru Kenyatta alikaririwa akisema ataheshimu matokeo ya uchaguzi huo wa siku ya Jumanne licha ya kila mmoja kusisitiza kuwa ataibuka mshindi.

Uchaguzi wa Kenya mara nyingi umekua ukikumbwa na ghasia. Zaidi ya watu 1000 waliuawa wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007.

Vyombo vya Habari Vyautupilia Mbali Upatanisho wa RC Dar na Ruge....Vichwa vya Habari vya Magazeti ya Leo..

$
0
0


Naona vyombo vya habari jana vilivyo vingi mda wa habari hawajarusha tukio la upatanishi kati bwana ruge na bwana makonda ni kwamba hawajaridhi bado, 

Maana haiingii akilin kuvamia wavamie kimya kimya halafu eti wakapatishiane majukwaani
Huku mvamiaji akiendelea kuto kiri kosa lake , naona wana habari hawako tayari kugeuzwa mazwazwa.

Mr Nice Awatolea Povu Wanaomsema Vibaya Aanika Utajiri Wake Anaomiliki Instagram

$
0
0
Mr Nice Awatolea Povu Wanaomsema Vibaya Aanika Utajiri Wake Anaomiliki Instagram

Washukiwa wa Mauaji ya Mkurugenzi TEHAMA Kenya Wakamatwa Uganda.....

$
0
0

WASHUKIWA WA MAUAJI YA MKURUGENZI TEHAMA KENYA WAKAMATWA

Jeshi la Polisi nchini Uganda linawashikiliwa watuhumiwa 3 (Mkenya 1 na Waganda 2) wa mauaji ya Meneja wa TEHAMA wa Tume ya Uchaguzi nchini Kenya, Chris Msando.
Msando alitoweka nchini Kenya na kupatikana akiwa amefariki. Polisi wa Uganda wamesema watuhumiwa hao wamekamatwa wakiwa na gari aina ya Toyota Fortuner. Gari hilo lenye namba za usajiri za Uganda huku ikidaiwa lilikuwa na namba za Kenya wakati wa kuvuka mpaka wa Busia.

Mawasiliano ya mwisho kutoka mwa Musando aliyafanya siku ya Jumamosi majira ya saa 9 alfajiri kupitia ujumbe wa SMS kwa mmoja wa wafanyakazi wenzake.


Marekani na Uingereza zilikubali kutoa maofisa wao wawili wa ngazi za juu kutoka mashirika ya upelelezi ya FBI na Scotland Yard baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) Keriako Tobiko kutaka uchunguzi ufanywe kuhusu mauaji ya Msando. Aliitaka pia serikali kuhakikisha usalama wa maofisa wa IEBC ili uchaguzi ufanyike kwa usalama.

Polisi walisema mwili wa Msando uligunduliwa katika msitu wa Kikuyu na kumbukumbu za mochwari zinaonyesha kwamba ulipelekwa hapo Jumapili asubuhi pamoja na mwili wa mwanamke mmoja asiyefahamika uliopatikana sehemu hiyohiyo.

Jeneza lenye mwili wa Chris Msando.
Marehemu Msando ameelezewa na marafiki zake kuwa mwalidifu na mcheshi, ambapo wafanyakazi wenzake katika IEBC wakiwemo Andrew Limo, Tabitha Mutemi na Ronnel Onchagwa wakisema alikuwa na utaalam mkubwa wa teknolojia, mwadilifu na mcheshi. Kabla ya kupatikana kwake, gari lake lilikutwa likiwa halina mtu eneo la Roysambu, Nairobi.
Source: Daily Nation

Una Tatizo la Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo?

$
0
0

JE, UNA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUFIKA KILELENI HARAKA NA KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME?

Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA (MASTER BLASHION), HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k. Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa ☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni ☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa. Kwa kutumia mimea na matunda @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250000@250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @150000@150,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150000@150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130000@130,000/= BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA. KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :- @markson_beauty_pr @markson_beauty_pr @markson_beauty_pr

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa (+255) 0767447444 na 0714335378 

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Ruge na Paul Makonda Wanapataneje na vipi Nyasi zilizoumia?

$
0
0
Na Zawadi B Lupelo

Wanajamvi salamu mbele!
Nimeona katika mtandao wa YouTube kile kinachoitwa kupatanishwa kwa Makonda na Ruge na mpatanishaji akiwa ni Rais John Pombe Magufuli. Naomba niweke maoni yangu hapa Jf na maoni haya yasitafsiriwe kuwa ninapinga watu kupatana wala kuishi kwa amani zaidi kushirikiana.

Makonda na Ruge wamekuwa katika mtanziko na hali ya kutokuelewana kwa muda wa miezi kadhaa sasa chanzo kikubwa kikiwa ni kile kinachodaiwa kwamba Makonda alivamia kituo cha utangazaji cha clouds tv na kupora vifaa kadhaa vya ofisi. Makonda alikwisha kanusha kuvamia clouds media katika kipindi chake alichojiandalia StarTv na kudai kwamba yote aliyoyaongea Ruge ni uongo ametunga akaenda mbali zaidi kusema Ruge hajui kitu zaidi ya utunzi wa story za mapenzi (kifupi msanii).

Wahenga wanasema mafahari wawili wagombanapo ziumiazo ni nyasi katika vita hii nyasi hazikukosekana. Mh Waziri Nape Mnauye ni mmojawapo katika juhudi za kutafuta ukweli na pengine suluhu la swala la Clouds media na Makonda yalimkuta ya kumkuta akaumia.
Kuna vyombo mbalimbali vya habari, watu binafsi na taasisi zingine ambazo kwa kweli zilisikitishwa na na kitendo cha Makonda kuvamia kituo cha Clouds media na wakatoa msaada wa kulaani na zaidi vilisusia kuandika habari za Makonda na mbali na vitisho vilivyotolewa na Rais ( refer "watch it")

Kubwa zaidi ni TEF (Jukwaa la Wahariri) lilisimama kidete katika hili kuhakikisha haki inatendeka kwa clouds media.

Jambo Kubwa la kunote wakati yote haya yanatokea mpatanishi (Rais Magufuli) aliamua kuegemea upande mmoja hii haijawahi kuwa sifa ya msuluhishi mahali popote pale duniani. Msuluhishi anatakiwa kuwa impartial asiyeegemea upande wowote.

Magufuli alikwishatamka hadharani kwamba kinachoendelea kwenye mitandao (tuhuma dhidi ya Makonda) ni udaku na yeye hasikilizi udaku. Hakuishia hapo alienda mbele zaidi na kutangaza interest kuwa hatamtumbua Makonda wala hata fanya lolote lile. Kauli kama hii inadhihirisha alikubaliana na alichokifanya Makonda na wala hakua akijali lolote na huku ni kuegemea upande mmoja.

Leo hii Mbele ya hadhara mlolongo huu wa matukio unamalizwa kwa kushikana mikono watu wawili yaani Ruge na Makonda? Kweli kabisa bila maelezo yoyote?

Mpaka naandika haya kuna mambo yameishughulisha akili yangu kama ifuatavyo.

Kwanza, Rais Magufuli katika mgogoro huu hakupaswa kuwa msuluhishi kwani alishaonesha upande hii inayofanywa ni danganya toto kwa Ruge.

Pili, swala hili lilipaswa sasa lisiwe mikononi mwa Clouds media na Ruge tena maana lilikwishafika kwenye chombo kinachohusika na vyombo vya habari TEF.

Tatu, Ni lazima umma uambiwe wanachopatana Ruge na Makonda ni nini ni ishu ya uvamizi au walikwaruzana mambo mengine barabarani? Na kama ni ishu ya uvamizi lazima tujue kwanza ukweli ni nani mkosaji ambaye anaomba radhi ili asamehewe? Je wanasameheana kwamba walikoseana Ruge alikosa nini na Makonda alikosa nini? Isijekuwa anayesamehewa ni Ruge kwa kumsingizia Makonda.

Je kuanzia sasa Clouds media wataanza kurusha habari za Makonda vipi kuhusu TEF na washirika wao?.
Vipi kuhusu Nape Mnauye? Na wengine walioumia kama nyasi remedy yao ni ipi?

Unless tupate maelezo kuwa kuna mazungumzo ya siri ya kuwapatanisha na mwenye makosa amefahamika na ameomba msamaha kilichofanyika ni kizungumkuti tu na kuuziana mbuzi kwenye gunia.

Zawadi B. Lupelo

Mwanaume Akamtwa Akiwa Amevaa vazi la Kike la Hijab

$
0
0

Jeshi la Polisi mkoani Pwani limemkamata kijana mmoja mkazi wa Mbagala jijini Dar es salaam akiwa amejibadilisha sura kwa kuvaa mavazi ya kike na kujifunika kwa hijabu.

Akizungumzi tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jonathan Shana amewaambia waandishi wa habari kwamba, kijana huyo amekamatwa eneo la picha ya Ndege barabara ya kwenda Magereza wilayani Kibaha baada kupata taarifa kutoka watu waliomuona na kumtilia shaka nyenendo zake.

Matukio ya wanaume wanaovalia mavazi ya kike na kufunika nyuso zao ili kutekeleza vitendo vya kihalifu yameanza kuongezaka ambapo siku za hivi karibuni Polisi waliwaua watu watatu ambao majina yao hayajatambulika kwa kuwapiga risasi karibu na daraja la Mto Mkapa, wilayani Ruji waakidhaniwa kuwa ni majambazi.

Kamanda wa Polisi alisema watu hao ambao wote ni wanaume walikuwa wameficha nyuso zao kwa hijabu na walikaidi agizo la
polisi kila walipotakiwa kusimama.

Mnyama Akichinjwa Hivi Nyama yake ni Hatari Kwa Kula......

$
0
0
Ulaji wa nyama una faida lukuki kwa afya ya binadamu ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa virutubisho vya aina ya protini ambayo ni rahisi kutumika mwilini, madini mbalimbali (Calcium, Magnesium, Phosphorus, Zinc na Chuma); vitamini aina ya folic asidi, E, B na B12 ambayo inapatikana katika nyama pekee.

Nyama pia inasaidia katika ukuaji na kuongeza afya ya mlaji kutokana na uwezo mkubwa wa kujenga mwili, kukarabati seli za mwili zilizokufa, kuzalisha chembe hai mpya, kurekebisha kinga ya mwili, kuongeza damu na kuimarisha mifupa.

Hata hivyo faida zote hizo zinapatikana tu, kwa walaji wa nyama iliyo bora na yenye kiwango. Hivyo ni vizuri wananchi wakazingatia kanuni za ulaji wa nyama yenye kiwango ili kujiepusha na athari zinazoletwa na nyama isiyo na kiwango.

Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania (TMB) Bi.Suzana Kiango amesema kuwa nyama yenye kiwango na bora huanzia kwenye utunzwaji wa mifugo wenye kuzingatia kanuni za uzalishaji bora, unenepeshaji wa mifugo yenye umri mdogo kwa kuwalisha chakula mchanganyiko kwa muda usiopungua siku 90 kabla ya kuchinja.

Bi.Kiango amesema kuwa hatua nyingine ni katika uchinjaji ambapo inashauriwa ufanyike kwenye machinjio bora ambayo yanakidhi viwango vya usafi. Hii ni pamoja na kuwa na sakafu na kuta zinazosafishika, maji ya kutosha na sehemu za kuning’iniza wakati wa kuchuna na kupasua.

“Kanuni za uchinjaji ni pamoja na kupumzisha mifugo ili kuipoteza fahamu na kumfanya mnyama asiogope na kuzalisha asidi nyingi inayosababisha nyama kuwa ngumu, pia iwe rahisi kutoa damu yote katika misuli. Uning’inizwaji wa chune mara baada ya kuchinjwa unasaidia kuondoa damu iliyo mwilini. Endapo damu haitatoka yote kwenye chune itasababisha nyama kuwa na rangi nyeusi na kuharibika mapema”, alisema Bi.Kiango.

Madhara ya ulaji wa nyama isiyo na viwango na bora ni pamoja na kupata magonjwa ya tumbo, kuharisha na kutapika endapo nyama itapata vimelea vya magonjwa hayo, kuugua magonjwa ya kuvimba miguu, kifua kikuu, shinikizo la damu, kisukari na kansa.

Hata hivyo, Bi. Kiango amesisitiza kuwa magonjwa haya yanaweza kuwatokea pia watu ambao hawatumii kabisa nyama kwa hivyo si nyama pekee ndio chanzo cha magonjwa haya japo inaweza kuwa sababu ya mtu kuugua.

“Bodi imeendelea kutoa elimu kwa watumiaji na wachinjaji wa nyama kupitia vyombo mbalimbali vya habari kama vile, redio, televisheni na magazeti. Pia katika maonesho mbalimbali kama Saba saba na Nane nane ambapo wataalamu wa bodi hutoa elimu kwa wananchi wanaotembelea mabanda ikiwa ni pamoja na kusambaza vipeperushi” amesema Bi.Kiango.

Namna nyingine ya kutoa elimu ni pamoja na kutumia matamasha ya nyama choma, wiki ya mayai na maonesho ya kuku, wiki ya chakula salama na siku ya chakula duniani. Wakati wa shughuli hizi wanashiriki hupatiwa elimu kuhusu faida na athari za kula nyama isiyo na viwango ili kunusuru afya zao.

Aidha walaji huelekezwa maeneo mbalimbali wanayoweza kupata nyama hiyo, na kwa upande wa wafanyabiashara wa nyama hupewa maelekezo ya kuboresha miundombinu ya kuzalisha, kuchinja na kuuza kwa kuzingatia viwango vya ubora na usalama.

Kutokana na baadhi ya wafanyabiashara ya nyama kuendelea kuwauzia walaji nyama isiyo na viwango kwa kujua au kutojua madhara ya nyama hizo, Bi.Kiango alisema kuwa Bodi inachukua hatua za kuhakikisha wafanyabiashara hao wanapata uelewa wa kutosha.

“Bodi imeanza kutoa mafunzo kwa watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa ambao watashiriki katika kutekeleza majukumu ya Bodi ikiwa ni pamoja na kusimamia uzalishaji wa nyama na kuelimisha wachinjaji ,walaji na wadau wengine wanaojishughulisha na uzalishaji wa nyama”alifafanua Bi.Kiango.

Aliendelea kusema mafunzo hayo yameshatolewa kwa vitendo kwa watumishi wanne kutoka katika kila Mamlaka za Serikali za Mitaa za mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Dodoma ambapo hadi sasa jumla ya wadau 490 katika maeneo tajwa wamekwisha patiwa elimu hiyo. Pia mafunzo yanatolewa na wadau wengine ambao ni Chuo cha nyama cha VETA, Dodoma na Kampuni ya nyama ya jijini Arusha.

Ishara Zinazoonyesha Kuwa Una Matatizo Ya Kiafya Mwilini Mwako

$
0
0
KWA kawaida mwili ukiwa umepungukiwa aina yoyote ya kirutubisho (ingredients), huonesha dalili kabla ya kujitokeza kwa ugonjwa. Bahati mbaya sana, watu wengi hawana uelewa wa dalili hizo. Katika makala haya, nakutajia dalili chache miongoni mwa dalili hizo.

MIDOMO KUKAUKA
Midomo huakisi afya ya mwili na hali ya maji katika mwili mzima. Kama una maji ya kutosha mwilini, basi hata midomo yako itakuwa laini na yenye unyevu. Unapokuwa na upungufu wa maji, ngozi huwa kavu. Kwa wale akina dada ambao hulazimika kulainisha midomo yao kila wakati kwa kutumia ‘lip sticks’, wajue kwamba wana upungufu wa maji mwilini.
Dalili nyingine…
Kuumwa kichwa, kukosa haja ndogo kwa muda mrefu, kukojoa mkojo wa njano-nyeusi au mkojo wenye harufu kali, ngozi kavu na unapoiminya ngozi ya nyuma ya kiganja inachelewa kunyooka, nazo ni dalili kwamba mwili una upungufu wa maji.

SULUHISHO
Kunywa maji ya kutosha kulingana na uzito wa kazi unazozifanya. Kiwango cha chini ni angalau lita moja ya maji safi na salama, hakikisha umekunywa maji hata kama husikii kiu. Vile vile ulaji wa matunda na unywaji wa juisi zitokanazo na matunda au mboga mboga, huweza kuondoa upungufu wa maji mwilini.

KUKOSA HAJA KUBWA
Kitendo cha kukaa zaidi ya siku moja bila kupata haja kubwa ni dalili ya wazi ya ukosefu wa kamba lishe (fibre) mwilini. Kwa kawaida binadamu anatakiwa kupata choo kikubwa kila siku kilicho laini na kingi. Iwapo hupati choo kila siku na ukipata unapata kigumu, tena kidogo, jua una matatizo!
Haja kubwa ni muhimu kwa sababu ndiyo inayosafisha tumbo, uchafu unapokaa tumboni kwa muda mrefu, sumu zilizomo kwenye haja kubwa hurejea mwilini na husababisha matatizo mengi ya kiafya, kuanzia magonjwa ya uvimbe, moyo na hata ubongo. Sumu huvuruga pia mtiririko wa homoni mwilini na hudhoofisha kinga ya mwili.

SULUHISHO
Kula kwa wingi matunda mbalimbali, mboga za majani na vyakula vitokanavyo na nafaka zisizokobolewa, kama vile ugali wa dona, mtama, ulezi, n.k. Ulaji wa vyakula hivyo bora, siyo tu kutaondoa tatizo la ukosefu wa haja kubwa, bali vitakulinda pia dhidi ya magonjwa ya kisukari, presha, ugonjwa wa moyo na mengine mengi.

VIDONDA PEMBENI MWA MDOMO
Utafiti umeonesha kwamba kupasuka kwa midomo na kutokea kwa vidonda pembeni ya midomo, huwa ni dalili moja wapo ya upungufu wa vitamini B mwilini na mara nyingi huwatokea watu wanaopenda kunywa kilevi kupita kiasi, kula vyakula vya kwenye makopo (processed foods) na kula sukari kwa wingi.

SULUHISHO
Suluhisho ni kula vyakula vyenye kuongeza vitamin B kwa wingi. Miongoni mwa vyakula vyenye kiwango kingi cha vitamin B ni pamoja na kiini cha mayai ya kienyeji, viazi vitamu, nyama ya ng’ombe na ya kuku, maini na vyakula vitokanavyo na nafaka isiyokobolewa.
Ingawa unaweza pia kula vidonge lishe vya vitamin B ili kuondoa upungufu huo, lakini tahadhari lazima ichukuliwe na ina shauriwa kula vyakula vya kuongeza vitamini hiyo zaidi kuliko vidonge.

Usain Bolt Amepoteza Shindano lake la Mwisho la mita 100

$
0
0

Usain Bolt amepoteza shindano lake la mwisho la mita 100 baada ya kusgindwa na Mmarekani Justin Gatlin katika mashindano ya dunia ya IAAF jijini London, Uingereza.

Katika mashindano hayo yaliyomalizika hive punde, Bolt ameambulia nafasi ya tatu na Gatlin aliyewahi kuingia kwenye kasha ya kutumia dawa za kuongeza nguvu akiibuka na ushindi.

Video: Witness Awachana Wanawake Wasionyonyesha Kuogopa Maziwa Kulala

$
0
0
Msanii Witness a.k.a Kibonge Mwepesi amewachana wanawake wasiopenda kunyonyesha pindi wanapojifungua kuhofia maziwa yao kulala.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake ‘Mzuka’, amesema suala hilo halina ukweli wowote na wanaponyonyesha wanajiepusha na mambo mengi.

“Kwenye maziwa kuna fat kwa maana ya mafuta wao wanaposema sinyonyeshi kwa sababu ziwa langu litalala ndipo wanapoharibu mfumo mzima wa shape zao lakini wanatakiwa wafahamu kuwa wanatakiwa kunyonyesha miezi sita,” Witness ameiambia Bongo5 na kuongeza.
“Faida zake utatengeneza mfumo mzuri kwa mtoto  na kujikinga na magonjwa, pia yeye mwenyewe inamsaidia kwa sababu mfumo wake wa mwili unarudi katika hali yake ya kawaida kwa sababu vile virutubisho vyote vilitengenezwa kwa ajili ya mtoto, sasa ukiviacha ndio unakuta matinginya mtu anakuwa na mwili mbaya lakini mwisho wa siku watu nyonyosheni,” amesema Witness.

Kwanini Ufie Hapo? Wacha Kumsingizia Mungu Kwa Kila Shida Unayopata....Pambana na Hali yako Utoke

$
0
0
KWA NINI UFIE HAPO?
Kama kuna watu ninaowahurumia ni wale ambao kila shida, jaribu, tatizo ama changamoto wanayopitia wanabaki kusema ni mapenzi ya Mungu, na wala hawachukui hatua yeyote ya kupambana kiimani ili kutoka hapo.
SIKILIZA..
Hakuna jaribu, shida, wala tatizo unalostahili kulipa heshima na hadhi ya "mapenzi ya Mungu" ikiwa lipo kinyume na Neno la Mungu. Vinginevyo, Shetani ataendelea kukuchezea for good na anaweza kuua furaha yako, kuua uchumi wako, na hata kuwaua wapendwa wako ama wewe mwenyewe kabla ya wakati wao.

CANT YOU SEE?
Umechelewa kupata mtoto ama mimba zimekua zikiharibika, halafu unapigwa chenga kuamini kwamba ni mapenzi ya Mungu, ilhali unajua kabisa Neno linasema "Hakuna atakaekua tasa wala mwenye kuharibu mimba".(KUTOKA 23:26) Whaaaat!??? Huyo ni shetani, inuka upiganie haki yako.
Madeni yamekuzidia, bado unaenda kukopa zaidi ili uwalipe wale wanaosumbua, halafu unajisemea na kuamini kwamba ni mapenzi ya Mungu? Kivipi? Neno linasema, anaekopa ni mtumwa wa anaekopesha. (MITHALI 22:7). Mungu anaanzaje kukutia utumwani? Huyo ni shetani anacheza na mindset yako kuhusu mikopo na madeni!
Umeugua ama umeuguza muda mrefu halafu mtu anatokea from no where anakuambia vumilia tu kwa sababu ni mapenzi ya Mungu na wewe unaamini? How? Ina maana hujui kwamba Neno linasema unatakiwa uishi maisha marefu yenye amani, uzima na furaha? (MITHALI 3:2). Sometime shetani analeta magonjwa kwako wewe ama kwa wanaokutegemea, ili uwe bize mahospitalini na mambo mengine yaparaganyike. Stand up and fight in faith!

NIKWAMBIE KITU?
Shetani na Mungu huwa hawatendi lolote maishani mwako pasipo ruhusa yako. Shetani anasubiri uende kinyume na Neno (ukate tamaa) ili atekeleze yake. Mungu anasubiri usimame katika Neno ili atimize mpango wake. Be careful!

HOPE UNAKUMBUKA.....
Namna shetani alivyonijia ili kupata ruhusa yangu ili amuue mke wangu alipokua akijifungua hawa mapacha wa pili(Nathan na Nathanael). Kilichoniokoa ilikua ni kusimama katika Neno na kujibizana nae strongly. Mind you kwamba, kumshinda Shetani kunahitaji "ungangari" wako katika Neno na katika Imani, vinginevyo, you will always be a cheap prey of a devil!
Mke wangu akiwa kaingia theatre, shetani akaniambia "Albert umeshafeli kiimani! Kwa nini umeruhusu mke wako afanyiwe oparesheni ya uzazi? Oparesheni sio mpango wa Mungu na katika oparesheni wanawake wengi huwa wanakufa wao ama watoto wanaozaliwa". Shetani alitaka nikubaliane nae ili nisiendelee kuomba na nibaki nasubiri patapotea ya eidha mke kutoka mzima ama akiwa maiti. Nikamwambia, Shetani acha kunitisha, oparesheni ya uzazi sio jambo jipya kwa Mungu kwa sababu ipo katika, ISAYA 66:7. Shetani aliponisikia hivyo akanywea!
Lilipotokea tatizo la kuishiwa damu, Shetani akaniambia mke wangu atakufa kwa sababu ya kukosa damu. Nami chapchap nikamjibu na kumwambia, Yesu Kristo ana damu nyingi hadi aliimwaga chini, kwa hiyo haiwezekani Yesu awe ndani yangu na ndani ya mke wangu halafu damu iwe ni tatizo.
(MATHAYO 26:28).
Aliponiletea picha ya jeneza likiwa na mwili wa mke wangu, nikamwambia, shetani unapoteza muda kwa sababu Neno linasema nitamfurahia mke wa ujana wangu hata niwapo mzee, kwa hiyo siwezi kuzika mke katika ujana huu.(MITHALI 5:8, ZABURI 92:14). Kwa masaa karibu manne (saa saba usiku hadi saa 11 nilikua nikipambana na shetani, aliekua akitafuta ruhusa yangu amuondoe mke wangu. Alinisemesha na kunionesha mengi nami nilimjibu kwa Neno hatua kwa hatua. Hatimae nilimshinda na akaondoka akiwa ameaibika na kuacha Mungu akijitwalia utukufu (YAKOBO 4:7)

NAKUSHAURI USIFIE HAPO..!!
Kuanzia dakika hii, achana na habari ya kuvumilia shida, jaribu ama tatizo lako kwa kujifariji kuwa ni mapenzi ya Mungu. No! No! No! Hebu inuka, jikung'ute, acha kujikunyata, funga ngumi za kiimani, pigania haki yako iliyopo katika Neno inayohusiana na jaribu, shida ama tatizo linalokuliza na kukuhuzunisha kila siku. Maandiko yanasema Ufalme wa Mungu unatekwa kwa nguvu, tafadhali usiende kama kondoo bali simama na upambane kama simba tena kwa nguvu zote. (MATHAYO 11:12) #SmartMind

Mwanamuziki Rubby Acharuka na Kuwatolea Povu Wanaosema Amefunikwa...'Bongo Hakuna wa Kunifunika'

$
0
0
Msanii anayefanya vizuri na wimbo wake 'Na Yule' Ruby amesema hakuna wa kuziba nafasi yake katika 'industry' ya muziki huku akidai hawezi kumchukia Nandy kwa kuwa ameshafanya naye kazi nyingi na mafanikio yake ndiyo furaha kwake.

Ruby amefunguka hayo kupitia kipindi cha Friday Night Live (FNL) kinachorushwa na East Africa Television na East Africa Radio, baada ya kuwepo kwa tetesi zinazodai kuwa msanii huyo amepotezwa Nandy kwenye muziki.

"Ni maneno ya watu ambayo yapo kila kukicha na mimi siwezi kujifananisha naye kwa kuwa mimi ni Ruby na yeye ni Nandy. Nafasi yangu ipo pale pale", amesema Ruby.

Kwa upande mwingine, Ruby ameweza kuyaweka mahusiano yake wazo kwa mara ya kwanza ndani ya FNL ambapo amelimtambulisha kijana mwenye jina la Genely Hb kuwa ndiye mpenzi wake wa sasa.

Serikali Kupitia Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) Imekana Kuwa na Taarifa ya Ndege ya Gwajima

$
0
0
Serikali kupitia Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) imekana kuwa na taarifa ya ndege iliyonunuliwa na Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima nchini Marekani.

Juzi, Askofu Gwajima alithibitisha kununua ndege hiyo aina ya Gulfstream N60983 yenye thamani ya Sh2.64 bilioni kwa ajili ya kuitumia kusambaza injili.

Ili kuonyesha msisitizo, Askofu Gwajima aliweka picha kwenye mitandao ya kijamii iliyomwonyesha akiwa mbele ya ndege hiyo.

Kiongozi huyo wa dini alisema ameijaribisha ndege hiyo kwa kusafiri viwanja tofauti nchini Marekani na kuridhika nayo.

Hata hivyo, akieleza utaratibu wa kuiingiza nchini, Ofisa Habari wa TCAA, Ali Changwila alisema mamlaka hiyo haina taarifa ya ununuzi wa ndege hiyo.

Alisema Mtanzania yeyote anayenunua ndege nje ya nchi kuiingiza nchini anatakiwa kwanza kuitaarifu mamlaka hiyo ili ifahamu na kuwa na taarifa nayo.

“Nimejiridhisha kwa wataalamu wetu, hakuna taarifa yoyote ya ununuzi wa ndege hiyo hapa ofisini,” alisema Changwila na kuongeza: “Kwa kawaida mtu anapotaka kununua ndege na kuileta Tanzania, kwanza lazima aje TCAA atuambie ni ndege ya aina gani ili tujue kama watalaamu wetu wanaifahamu. Kama hawaifahamu itabidi awape mafunzo ili waweze kuikagua hiyo ndege ikiwa nje ya nchi.”

Hata hivyo, alisema TCAA ina wataalamu waliobebea katika urubani na uhandisi wa ndege walio tayari kufanya ukaguzi wa ndege mbalimbali zinazoingizwa nchini.

Alisema hatua ya kwanza ni watalaamu hao kwenda ilikonunuliwa ndege husika na kuikagua kama inakidhi vigezo vya Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO).

“Je, imekidhi vigezo vya ICAO? Inacho cheti cha kusajiliwa? Historia yake ikoje? Imekwisha muda wake? Imeshakatazwa kusafiri? Maana kuna ndege zimeshapitisha muda wa kutumika halafu zinauzwa,” alisema Changwila.

Ofisa huyo aliongeza kuwa baada ya wataalamu wao kujiridhisha, mwenye ndege atatakiwa kujaza fomu ya TCAA ili kufuata sheria za ndani na pia ataeleza ndege hiyo itaendeshwa na rubani gani na itatumika katika viwanja gani.

“Ni kama tu unataka leseni ya biashara, lazima ukidhi vigezo,” alisisitiza Changwila.

“Wapo Watanzania walionunua ndege na wamefuata masharti hayo, kwa mfano Precision Air inamilikiwa na Watanzania, Coastal Aviation, hata marehemu Philemon Ndesamburo alikuwa akimiliki helkopta kwa kufuata masharti hayo.”

Aprili 23, Askofu Gwajima aliwatangazia waumini wake kanisani kwake kuwa anapanga kununua treni ya abiria ya kisasa (standard gauge) baada ya Serikali kupanga kununua treni ya aina hiyo. Kauli hiyo ya Gwajima ilifuatiwa na kukunwa na utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano ambayo aliisifu kwa kuwa na mipango mizuri.

Alisema kaulimbiu ya Serikali ya ‘Tanzania ya Viwanda’ haitakuwa na mafanikio makubwa kama hakutakuwa na usafiri wa uhakika wa kutoka sehemu moja hadi nyingine.

Pia, Gwajima alisema kuwa tayari amefanikiwa katika mpango wake wa kujenga chuo cha mafunzo ya kurusha ndege na anachosubiri ni ruhusa ya Rais Magufuli ili kianze kutoa mafunzo.

“Naomba Serikali isiingize masuala ya siasa katika hili kwani lina manufaa kwa Watanzania wote, nimeamua kuwekeza ili kuwakomboa (Watanzania) na kuzalisha ajira,” alisema.

Mwananchi:

Simon Msuva Azidi Kung'ara Morocco..Atupia Tena Goli

$
0
0
WINGA wa kimataifa wa Tanzania, Simon Msuva amekuwa miongoni mwa wachezaji wa Difaa Hassan El- Jadida waliotumika kutambulisha jezi za msimu mpya za timu hiyo kabla ya baadaye kuingia uwanjani kuiongoza timu hiyo kushinda 2-1 dhidi ya ASO  Daraja la Kwanza.

Msuva amesema kwamba katika mchezo huo uliofanyika wa El Abdi mjini Jadida, yeye amefunga bao moja ambalo lilikuwa la kusawazisha na kuseti la ushindi.

“Tumeshinda mabao 2-1, maana huku kila siku tunacheza mechi, kweli wenzetu wapo tofauti sana,”amesema Msuva na kuongeza; “Leo mimi nimefunga la kusawazisha na kutengeneza la ushindi,”.

Msuva amesema mechi zote wanazocheza za kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Morocco, maarufu kama Botola dhidi ya timu tofauti, zikiwemo za Daraja la Kwanza ni ngumu.

“Ni mechi ngumu, timu za huku wachezaji wake wapo fiti sana na wana nguvu na kasi sana, kwa kweli huku wenzetu wapo tofauti sana,”alisema.

Awali ya hapo, Msuva alishiriki zoezi la kutambulisha jezi mpya za Jadida za msimu ujao pamoja na wachezaji wenzake wengine watatu walioteuliwa.

Zoezi jilo lilifanyika katika mkutano na Waandishi wa Habari mabao makuu ya klabu. Ikumbukwe ni wiki iliyopita tu Msuva amesaini mkataba wa miaka mitatu kujiunga na DHJ kutoka Yanga ya Tanzania.

Rais Magufuli Amgomea Mwekezaji Kusamehe Kodi

$
0
0

Rais John Magufuli amekataa ombi la kusamehe kodi kwa muda wa miaka 10 katika kiwanda cha saruji cha Kilimanjaro kilichopo jijini Tanga kwa kueleza kuwa kufanya hivyo ni kinyume na sheria.

Rais Magufuli ametoa msimamo huo wakati akitoa hotuba  katika hafla ya uzinduzi na  kujibu maombi yaliyokuwa katika risala ya kiwanda hicho, ambacho kilitaka kisamehewe kodi kwa muda wa miaka 10 kutokana na deni kubwa ambalo kinadaiwa katika taasisi za kifedha, zilizokopwa kama mtaji wa kukianzisha.

Sababu nyingine za kutaka kiwanda hicho kusamehewe kodi ni kutokana na mchango wake katika shughuli za kijamii ikiwemo kuchangia madawati na vyumba vya madarasa katika shule za jiji hilo pamoja na kusaidia huduma za maji.

Rais Magufuli amesisitiza kuwa serikali yake inahimiza viwanda ili iweze kupata mapato kupitia kodi, kwahiyo haiwezi kufanya uamuzi wa kusamehe kodi na kujikosesha mapato.

"Nianze kumshukuru rmwenye kiwanda kwa kutoa misaada kwa jamii, na kwa vile mifuko ya saruji 1300 aliyoitoa nilikuwa hapa nikija nitataka mnipeleke sehemu zilipotumika. Lakini uliniomba kusamehe kodi hilo ni ombi gumu. Kwa sababu wito wa serikali kuhimiza kujenga viwanda maana yake ni kwamba serikali ipate pesa tuweze kusomesha watoto bure, kuongeza madawa hospital nk. Ninachokuomba ni wewe tu ujipange ndiyo ushindani wenyewe.

Katika hatua nyingine, rais Magufuli ameupongeza uongozi wa kiwanda hicho kinachomilikiwa na wazawa kwa hatua hiyo ya kufanya uzalishaji na kutoa ajira kwa watanzania zaidi ya 100

Lulu Michael Afunguka Ukweli Mchungu Kuhusu Bongo Movies Kutojielewa....

$
0
0

Msanii wa maigizo aliyefanya vizuri na filamu ya 'Mapenzi ya Mungu', Elizabeth Michael ' Lulu' amefunguka na kusema wasanii wa maigizo bongo wanafeli kutokana na kutojielewa ni kitu gani ambacho wanakitaka kwenye sanaa, badala yake wanafuata mikumbo.

Lulu amefunguka hayo hivi karibuni akizungumza na wanahabari na kusema kuwa wasanii wengi wa Tanzania hawapendi kujishughulisha kutafuta kitu kizuri kwa kuwa wengi wao walifuata mkumbo kwenye kuigiza  na wengine walichukulia kama sehemu ya kujipatia umaarufu ili maisha yaendelee au sehemu ya kupotezea muda.

"Ukweli upo kwenye uigizaji kuna watu tunachukulia hii ni kazi, wapo wanaofanya kama sehemu ya kipaji chake lakini pia wapo ambao wanachukulia kama sehemu ya kujipatia umaarufu au ku-refresh kwani wanakua na kazi zao zingine,  na hao ndio wanaosababisha tuonekane waigizaji wa muvi tumefeli".

Pamoja na hayo Lulu ameongeza, "Unajua pia kufuata mkumbo ni kitu kilichoturudisha nyuma. Watu wengi walikuwa wanaangalia mafanikio ya mtu mmoja na wote tukawa tunapita njia zilezile ili tufanikiwe badala ya kutafuta za kwetu ndiyo kama mnavyoona sasa hivi tunalalamika lakini mashabiki zetu wanatusapoti hivyo japo tunawakwaza".

Akizungumzia kuhusu wasanii wa Nigeria walivyoweza kufanikiwa katika filamu zao, Lulu amesema ni pamoja na upendo na ushirikiano wanaoonyeshana katika kazi zao na kuongeza kwamba pamoja na kufanya kazi zenye ubora wa kimataifa watu hao hawajasahau utamaduni wao.

Kuhusu sababu za wasanii wa filamu kutokaa 'Location' kwa muda mfupi kutengeneza filamu zao kwa usahii muingizaji Lulu amefunguka na kusema changamoto kubwa huwa ni bajeti kwa wasanii hao.

"Bajeti zetu ni tatizo. Bado hatujawa na uwezo wa kuweka bajeti kubwa kwenye filamu ndiyo maana tunaomba tuwezeshwe ili tufanye kazi zenye ubora. Kuna vitu ambavyo sisi pia tunavifanya kwa mapungufu kwa sababu hatuna uwezo wa kumpatia pesa mtu sahihi wa kufanya kazi husika ndiyo maana unakuta tunafanya kazi kwa uwezo wetu tu.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images