Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Amenisomesha, Kaninunulia Gari Lakini Sina Mapenzi Naye! Nifanyeje?

$
0
0
Amenisomesha, Kaninunulia Gari Lakini Sina Mapenzi Naye! Nifanyeje?
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 28 Naishi Tabata jijini Dar nimejitokeza kwenu kuomba ushauri, Mimi na mpenzi wangu ambae amenisomesha toka form one hadi sasa nipo chuo kwani wazazi wangu walifariki wakati mimi nikiwa mtoto mdogo sana.

Sasa huyu mpenzi wangu amenigharamia sana yani kuanzia nguo zote hadi chakula nacho kula vyote ni msaada wake yeye na amejitolea kuninunulia gari la kutembelea na kanambia nitafute kiwanja ili tujenge nyumba ya kupangisha.

Ila mimi kwa sasa naona kama huyu mwanaume hatuendani kwani yeye hana elimu ila anafanya kazi kutumia akili ya kuzaliwa, Jamani mimi nataka kuishi na msomi mwenzangu ila huyu kaka mimi naona kama freemasson kwani kanisaidia sana asije akanitoa kafala, Mimi kwa sasa nimepata mpenzi mpya ambae anaelimu ya chuo pia ni sharo sio mshamba kama huyu wa zamani.

Sasa please naombeni ushauri wenu jamani nimwambiaje kama sipo tayari kuishi na yeye huyu mpenzi wa zamani bila kuumiza moyo wake...?


Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Ufafanuzi: Kuhusu Polisi Kudaiwa Kumpiga Risasi Mke wa Mwenyekiti, Mwanza

$
0
0
Mapema jana August 9, 2017 kulikuwa na taarifa zilizosambaa mitandaoni zilizoeleza kuhusu tukio la Mke wa Mwenyekiti wa Mtaa wa Mabatini, Mwanza kupigwa risasi na Polisi.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mabatini, Mwanza Ntobi Boniphace ambaye mke wake alijeruhiwa kwa risasi usiku wa uliopita ameelezea tukio hilo akisema gari lililokua likiendeshwa na dereva mwanafunzi liligonga nyumba yao ambapo dereva huyo alikimbia.

Aidha, baada ya kuwasiliana na Polisi kuomba msaada walifika katika eneo la tukio wakiwa wamelewa na kuanza kufanya kuvuru huku wakimpiga ambapo mwanamke kuwalazimisha watoe bunduki waliyoificha kabla ya kumpiga risasi mama huyo.

Kwenye video hapa chini kuna kila kitu na unaweza kutazama kwa kuplay!!!

Kanisa Katoliki Lakataa Kumzika Bilionea wa Ngurudoto Arusha

$
0
0

KANISA Katoliki Jimbo Kuu la Arusha, limekataa kuendesha misa ya maziko ya mfanyabiashara bilionea Faustine Mrema kwa madai hakuwa na Sakramenti ya ndoa na mke wake wala kipaimara.

Paroko Msaidizi wa Parokia ya Mtakatifu Theresia, Mtoto Yesu, Jimbo Kuu la Arusha Padri Festus Mangwangi amekiri suala hilo na kuongeza kuwa marehemu enzi za uhai wake hakuweka heshima na kanisa.

“Marehemu ni mkatoliki wa kuzaliwa, lakini hakuwahi kuwa na sakramenti ya ndoa na mke aliyezaa naye watoto wala kupata Kipaimara. Kanisa haliwezi kumzika kabisa, kawaida mazishi ya Kanisa Katoliki ni heshima inayotolewa kwa mhusika kama anastahili.”

“Huyu hakuwahi kufunga ndoa kanisani, alijitenga na kanisa kwa hiyo kusema tumemtenga si kweli, yeye ndiyo alijikataa hakutaka kutafuta heshima yake na kanisa akiwa hai,” alisema Padri Mangwangi.

Kuhusu kutokwenda kwenye Misa za Jumuiya ambayo nayo ni moja ya taratibu muhimu inayowataka waumini wa kikatoliki kushiriki ibada za nyumba kwa nyumba Padri Mangwangi amesema, hata ibada hizo nazo pia marehemu alikuwa hashiriki.

“Jumuiya ni utaratibu wa kanisa unaowataka waumini wawe na ushirika wa karibu ikiwamo kufahamiana marehemu pia alikuwa hashiriki kabisa sasa unaanzaje kumzika mtu kwa heshima za Kanisa Katoliki?” amehoji Padri Mangwangi.

Wakati Kanisa hilo likijivua kushiriki Misa ya heshima ya maziko ya marehemu Mrema hiyo jana, Askofu Dk. Eliud Issangya wa Kanisa la Kimataifa la Kiinjili, alilazimika kuongoza Ibada hiyo ya maziko iliyofanyika Hoteli ya Ngurdoto, wilayani Arumeru.

Chanzo: MTANZANIA

Kichanga cha Faiza Ally Cha Anza Kutembezwa Kwenye Mitaa Wakati Hata Wiki Hakijafikisha

$
0
0
Naona sasa hivi utandawazi umekuwa kwa kasi sana kichanga hakija fikisha hata siku 7(wiki moja) kinaanza kutembezwa kwenye mitaa,hili nimeliona kwa mrembo Faiza Ally.



Nb:Wabobezi wa mambo ya Afya na dini hii imekaaje? Piteni mtutoe tongo tongo kwenye hili.

By Ndumilakuwili

Kimenuka..Emmanuel Mbasha Amvua Nguo Madam Flora Mbasha.....

$
0
0
BAADA ya mwanamuziki wa Nyimbo za Injili Bongo, Flora Mbasha kusambaza kitabu alichokipa jina la Siri za Flora Mbasha kilichoanika ‘mabaya’ ya aliyekuwa mumewe, Emmanuel Mbasha, mumewe huyo ameibuka na ‘kumchana’ vibaya mwimbaji huyo na kusema hafai kuwa mke.

Flora alikiachia kitabu hicho hivi karibuni ambapo pamoja na mambo mengine aliyopitia kwenye maisha yake na Mbasha, alieleza namna ambavyo mumewe huyo wa zamani alivyokuwa akimtesa na hata kumuingilia kwa nguvu akiwa kwenye siku zake.
Akizungumza na mwanahabari wetu katika ofisi za gazeti hili, Bamaga- Mwenge jijini Dar, Mbasha alianza kwa kueleza masikitiko yake juu ya kitabu hicho kwa kusema anashindwa kuelewa mume wa sasa wa Flora, Daud Kusekwa anajisikiaje pale Flora anapomzungumzia mara kwa mara.
“Yaani unajua watu wengine sijui wapoje bwana. Hivi kweli wewe hata huyo mwanaume wake anajisikiaje kuona mkewe ananiongelea kila wakati? Ni kukosa adabu, kwa nini wasifanye maisha yao?


“Kweli mwanamke aliyefunzwa, akafunzika anaanzaje kumuongelea mwanaume wake wa zamani? Yaani kwangu mimi mwanamke wa aina hiyo anapoteza sifa ya kuwa mke,” alisema Mbasha.
Mbasha akizidi kutema cheche mbele ya kinasa sauti cha Amani, alisema kuwa, aliamua kukaa kimya baada ya kupitia mambo mazito na mwanamuziki huyo ambayo kamwe hataki kuyasikia wala kurudi nyuma.
“Ametaka talaka mahakamani, tumeachana na mimi sikutaka tena hata kumzungumzia, lakini yeye kutwa amekuwa akinizungumzia. Halafu kwanza unamzungumziaje mtu ambaye mlishaachana? Mtu ambaye kwanza hana hata habari na wewe, anafanya maisha yake mengine, huu kama siyo ujinga ni nini?” Alihoji Mbasha.

Kama hiyo haitoshi, Mbasha alizidi kumwaga mboga kwa kusema kuwa, siku zote sikio la kufa huwa halisikii dawa kwani kitendo anachokifanya Flora cha kumzungumzia yeye kama zilipendwa wake, alishakifanya kwake kwa mwanaume mwingine.
“Kifupi ni kwamba tabia ni kama ngozi, huwezi kuibadili. Wewe unaona sasa hivi anavyoelezea mambo aliyokuwa akiyafanya na mimi na kuongeza uongo wake, alishanifanyia hata mimi wakati nimemuoa.

“Yaani yule mwanamke sijui bana, Mungu amsaidie. Yaani kwanza wakati mimi naanza kumfuatilia, huwezi kuamini, alikuwa na mwanaume mwingine. Akamuacha kwenye mataa wakati tayari walikuwa wanaelekea kwenye ndoa na vikao tayari walikuwa wameshaanza kufanya,” alisema Mbasha.
Mbasha ambaye kwa sasa hajaingia kwenye ndoa tangu aachane na Flora, alisema kuwa, anamshauri Flora aache kumzungumzia kwani kama ni ndoa ilishavunjika, aitazame zaidi ndoa yake mpya.

“Aachane na mimi. Namshauri atulie kwenye ndoa yake kuliko kila kukicha ni Mbasha… Mbasha…,” alisema Mbasha.
Mbasha na Flora walidumu kwenye ndoa kwa miaka 12 na kubarikiwa mtoto mmoja kabla ya kuachana mahakamani.
Kabla ya kuachana huko, Mbasha alituhumiwa kumbaka mdogo wa Flora na kesi kuunguruma muda mrefu na baadaye Mbasha alishinda hivyo kuachiwa huru.

 STORI: ERICK EVARIST | GAZETI LA AMANI

Magufuli Awafitini Wabunge wa Upinzani....Waonekana Kama ni CCM B

$
0
0
Magufuli Awafitini Wabunge wa Upinzani....Waonekana Kama ni CCM B

Rais John Magufuli amewaweka katika mtego wabunge watano wa vyama vya upinzani katika majimbo yao kutokana na kauli za mafumbo alizotumia katika ziara mbalimbali ambazo amekuwa akizifanya.

Mtego unaowakabili ni ama wachague kuhamia CCM au wabakie upinzani lakini wananchi wasiwakubali tena katika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2020.

Rais Magufuli ambaye alifanya kazi hiyo ya kichama kupitia ziara za uzinduzi wa miradi mbalimbali ya kiserikali mikoani, alitumia kauli kama “Huyu ingawa ni upinzani lakini damu yake ni CCM.”

Mbali ya kauli hiyo ambayo imewafanya baadhi yao kuonekana kama ni ‘CCM B’, akiwa katika majimbo yanayoshikiliwa na upinzani, kila alipopokea kero kutoka kwa wananchi, Rais Magufuli alichomekea kauli za kuwabeza au kuwataka wananchi wasifanye tena makosa.

Lakini pamoja na kuchomekea maneno hayo, katika ziara zake Rais Magufuli amekuwa akisisitiza  kuwa yeye ni Rais wa Watanzania wote bila kubagua vyama, dini au makabila yao, akisema maendeleo hayana vyama.

Wabunge walioingizwa mtegoni katika majimbo yao ni; Magdalena Sakaya (Kaliua - CUF), Kasuku Bilago (Buyungu - Chadema), Mussa Mbarouk (Tanga Mjini - CUF) Vedasto Ngombale (Kilwa Kaskazini - CUF) na Saed Kubenea Ubungo - Chadema).

Alivyowatega

Julai 23, Rais Magufuli alimpongeza Sakaya kwa ushirikiano wake katika shughuli za maendeleo huku akisema ingawa kimwili mbunge huyo ni CUF, lakini damu yake na roho yake ni vya CCM.

Rais Magufuli ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM, alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kaliua, Tabora wakati wa ufunguzi wa Barabara ya Kaliua – Kazilambwa, kwenye Uwanja wa Kasungu.

Dk Magufuli alisema Sakaya amekuwa akifanya kazi nzuri za maendeleo katika kutekeleza ilani ya CCM, bila kuwabagua kwa itikadi ya vyama vyao na akawataka wanaCCM kushirikiana naye.

“Mheshimiwa Sakaya ukimwangalia mwili wake ni mwana-CUF, lakini damu yake na roho yake ni mwana CCM. Inawezekana siku moja akahamia CCM. Ni bora kuwa na mwanaCUF, au mwana Chadema, au mwana-ACT anayefanya kazi za CCM kuliko kuwa na mwana CCM anayefanya kazi za chama kingine. Si mmenielewa? Mimi najua maana hata wakati wa kampeni niliyaona.”

Mbali na Sakaya ambaye pia ni naibu katibu mkuu wa CUF upande wa mwenyekiti wa chama hicho anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba, Rais Magufuli, Julai 22, mwaka huu alimshtaki Bilago kwa wapigakura wake kwamba, wananchi wa eneo hilo wanateseka kutokana na makosa ambayo waliyafanya wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Akiwa katika Jimbo la Buyungu, Rais Magufuli aliwapiga vijembe wapigakura akisema  mbunge wa hapo (Bilago), aliwaahidi wananchi kwamba angemaliza suala la maji na kuwahoji, “Leo amelimaliza?” akajibiwa badooo... kisha akasema ndiyo mjifunze sasa.

Kutoka na kauli hiyo ya Rais, Bilago aliliambia gazeti hili jana kwamba ilimlazimu kufanya ziara katika kata zote 13 za jimbo lake ili kujitetea mbele ya wapigakura wake. Alisema Rais Magufuli alikosea kuwaambia wananchi wasimchague tena katika uchaguzi ujao kwa kigezo cha kero ya maji kwani kazi ya mbunge siyo kupeleka maji, umeme wala kujenga barabara.

“Wapo walionipigia simu wakihoji juu ya kauli hiyo ya Rais, nikawaelewesha, wengine walielewa palepale na wengine ilibidi niwazungukie kwenye kata zangu kuwaelewesha, wananchi wanatakiwa kujua mbunge hawezi kuleta maji, mbona mbunge wa CCM hakuwaletea maji? Hili ni tatizo la utawala uliopo,” alisema.

Mbali na Bilago, siku tatu zilizopita akiwa Tanga mjini, Rais Magufuli alimpongeza Mbarouk kwa kutumia udhaifu wa CCM kushinda ‘ili baadaye aweze kuhamia CCM.’

Kabla ya kauli hiyo, Mbarouk alimwambia Rais kuwa milango ya kuingilia kwenye nyumba ya kuwatumikia wananchi iko mingi kwa hiyo maendeleo ya wananchi yasihusishwe na tofauti za vyama vyao kwa sasa.

Hata hivyo, Rais Magufuli alifafanua kauli hiyo kwa kumkaribisha ndani ya CCM kupitia mlango wake mkubwa.

“Mimi nakubaliana na mbunge wenu, kwamba milango ya kuingia kwenye nyumba iko mingi, nikajua linyumba ni li-CCM kwa hiyo anatafuta (Mbarouk) njia ya kuingia kwenye linyumba la CCM ambalo ni likubwa, nyumba ya wengi,” alisema.

“Kwa hiyo nyumba ipo na unakaribishwa kuingia kwenye nyumba hii ya CCM,” Rais Magufuli alimkaribisha huku mbunge huyo akisimama alipokaa na kutoa heshima kwa Rais.

Lakini jana, Mbarouk alisema yeye bado ni CUF na hafikirii kuingia nyumba ya CCM kutokana na imani iliyojengwa na wananchi wa jimbo lake kupitia tiketi ya CUF.

“Najua Rais ananihitaji sana CCM na baada ya kauli yake yaliibuka makundi mawili; kundi lililoamini ni utani na lingine ndani ya chama wakihofia usaliti. Maneno ya kunituhumu kwa wapinzani ndani ya chama yalianza kutolewa lakini nikawatoa hofu kwamba kimwili na kimoyo ni CUF,” alisema Mbarouk.

Machi 3, mwaka huu, Rais Magufuli alimuweka katika wakati mgumu Ngombale wa Kilwa Kaskazini mbele ya wapigakura wake baada ya kumtaka achangie angalau Sh15 milioni kutoka mfuko wa jimbo kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya, lakini mbunge huyo akasema hawezi kutoa ahadi ambayo hataitekeleza.

Tukio hilo lilitokea eneo la Somanga Wilaya ya Kilwa wakati Rais aliposimama kuwasalimia wananchi ikiwa ni sehemu ya ziara yake katika mikoa ya Kusini.

Katika tukio hilo, Rais Magufuli alikuwa akimuuliza maswali ya mtego mbele ya wapigakura, huku akisisitiza umuhimu wake kama mbunge kuchangia ujenzi huo. Rais aliahidi kuchangia Sh20milioni.

“Jamani si mnataka na mimi nichangie? Sasa na mbunge achangie. Aseme anazipeleka wapi hizo (fedha za mfuko wa jimbo)? Sasa wewe umetoka Dar es Salaam unapitia hapa Somanga, unaenda unazitoa tu huko na hapa wana shida ya hospitali. Huoni kama unawaonea? Sasa mimi ngoja nijitolee mwenyewe, ila wananchi wanajua,” alisema Dk Magufuli huku akishangiliwa.

Jana, mbunge huyo alisema kauli hiyo ya Rais ilimlazimu kufanya mikutano katika kata za Kinjumbi na Namayuni kuwaweka sawa wapigakura wake.

“Wapo wananchi ambao hawakuelewa pale na ndiyo maana niliamua kufanya mikutano, maana ilionekana Rais ndiye mwenye msaada na mimi sina umuhimu, niliwaeleza kuwa fedha za mfuko siyo za mbunge na zina utaratibu wa kutolewa, nina kata 13, vijiji 54, haikuwezekana kutoa Sh15milioni kati ya Sh36 milioni zilizokuwa zimebakia,” alisema.

Ngombale alisema Rais aliamua kutumia mbinu hiyo kuzunguka katika majimbo mbalimbali ya wabunge wa upinzani ili kuwadhoofisha kwa wapigakura wao, jambo ambalo halitafanikiwa.

Pia, katika hafla ya uzinduzi wa majengo ya mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Aprili 15, Rais Magufuli alitumia staili nyingine ya kumshtaki kwa wananchi Kubenea wa Ubungo.

Kwa kuwa chuo hicho kipo katika jimbo hilo linaloongozwa na mbunge huyo wa Chadema alitarajiwa kwamba angehudhuria sherehe hizo za ufunguzi, lakini Rais Magufuli alipomuulizia ili azungumze chochote kwa niaba ya wananchi wake, hakuwapo.

Mwananchi

Mwanafunzi Ashinda Ubunge Kenya..Alikuwa Akifanya Kampeni Kwa Baiskeli na Boda Boda

$
0
0
 Aliyekuwa mgombea wa Ubunge Igembe Kusini nchini Kenya, John Mwirigi (24) ameshinda nafasi hiyo baada ya matokeo kutangazwa na Tume huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).

Mwirigi ambaye anatajwa kuwa Mbunge mwenye umri mdogo kuwahi kutokea aliwashangaza wengi katika kampeni zake ambapo alikuwa akitumia baiskeli na bodaboda.

Mwirigi ambaye ni mwanafunzi wa Shahada ya elimu katika chuo cha Mount Kenya alikuwa mgombea binafsi hakuwahi kuwa na matangazo kwa kile kilichodaiwa kukosa pesa za kufanya kazi hiyo.

Katika matokeo hayo, Mwirigi alipata kura 18,867 huku mgombea wa Jubilee, Rufus Miriti akipata kura 15,411.

Pendeza na Kessy Products, Kutoa Mvi, Kurefusha Nywele, Tengeneza Shepu na Mengine

$
0
0
PENDEZA NA KESSY PTODUCT:-MSIMU MPYA WA 2017_ BIDHA AINA ZOTE KWA UBORA MZURI%
PATA DAWA ZA ASILI ZISIZO NA MAD, HARA NA MATOKEO NI KWAHARAKA BAADA YA WEEK

1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _80,000/
2) KUREFUSH NYWELE KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA _80,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO FIGA UMBO (8) NA KUJAZA HIPC NA KALIO @ KUPAK _80,000/
@ KUNYWA AU VIDONGE _130,000/ 4) KUPUNGUZA NYAMA ZA MIKONO TUMBONI ZILIZOTEPWETA _80,000/
5) PUNGUZA KITAMBI KWA HARAKA KWA DAW HIZI ZA KUNYWA
@) KUNYWAA _100,000/
@) VIDONGE _100,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KGM 150 ADI 80 KIASI UNACHOTAK WEWE KWA DAW HIZI
@) DAW YAKUNYWA YA _100,000/
@) VIDONGE VYA HARAKA _100,000/
7) PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KWA MUDA WA WEEK MOJA _70,000/
8) ONGEZA MAZIWA NA SAIZ UNAYOTAKA WEWE _70,000/
9) ONGEZA MWILI MZIMA NA KUKUPA HAMU YAKULA KWA RIKA LOLOYE _80,000/
10) TOA MICHIRIZI SUGU PIA NA ILE YAKUJIFUNGUA MWILI MZIMA _70,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KATIKATI YA MAPAJA _70,000/
13) KUWA MWEUP NA SOFTI MWILI MZIMA NA KUTOA WEUS MACHON NA VIMISHIPA VIDOGO VIDOGO @ MAFUTA YA KUPAKA _80,000/(@) VIDONGE (WHITE SOLUTION) _120,000/
14) ONDOA NDEVU NA VINYWELEO MWILINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME NA KUIMARISHA MISHIPA ILIYO LEGEA KWA DAW HIZ
@) JEL KUPAKA (MEN GEL) _70,000/
@) VIDONGE (MAXMAN) _80,000/
16) ONGEZA MAUMBIL YA KIUME SAIZI UNAYOITAKA WEWE KWA:
@) (HANDSOME UP) MASHINE _170,000/
@) JELI YAKUPAKA INABORESHA ANZIA NCHI (4 ADI 6 )_100,000/ PIA NA VIDNGE VYAKE VIPO
17) RUDISHA HAMU YA TENDO LA NDOA KWA WALIOPOTEZA KUTOKANA NA NGIRI, KISUKARI NA MAGONJWA MENGINE KWA _80,000/
18) RUDISHA USICHAN(BIKRA)Na KUTO UCHAFU SEHEMU ZA SIRI _80,000/
19) FANYA USO WAKO KUWA MKAVU NAKUTOA VIJIPELE ILIYOSABABISHWA NA MAFUTS MAKALI _80,000/
20) ONDOA MAKUNYANZI USONI _70,000 (21) ENGEZA MGUU WAKO _70,000/ TUNAPATIKAN K/ KOO NA SINZ
MAPAMBAN, KWA MIKOAN DUNIAN KOTE UTAPATA

(+255) 0719955528
0756259180
0785371237

@dr_kessy_product
Delivery POPOTE ULIPO,

Freeman Mbowe Ataka Rais Aombewe Kupunguza Ukali wa Maneno

$
0
0
Freeman Mbowe Ataka Rais Aombewe Kupunguza Ukali wa Maneno
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amewaomba Watanzania wamuombee Rais John Magufuli kwa Mungu ili apunguze ukali wa maneno yake kwani analigawa na kulitia hofu Taifa.

Mbowe, ambaye pia ni Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni alitoa kauli hiyo juzi na kuirudia jana wakati akihutubia mikutano ya hadhara maeneo ya Masama, Mailisita na Bomang’ombe.

“Nimeongea Bomang’ombe nikampelekea Rais salamu na wasaidizi wake wakanipigia wakaniambia tunakusikia Mbowe... Tumia ulimi laini. Acha ulimi wa maneno makali makali tu kila siku,” alisema. “Mwanadamu saa nyingine wanahitaji wapewe mapenzi ya viongozi. Sio kila siku kiongozi umekaza tu misuli. Kuna mahali unatakiwa uwaambie maneno ya kuwatia faraja.

“Unajenga Taifa lenye upendo sio kujenga Taifa la kutishana tu kila saa. Namuomba Rais aelewe unapokuwa Rais, unakuwa mfariji mkuu. Kauli zako zinaweza kulijenga Taifa au kuliogofya Taifa.

“Rais wetu tumuombee Mungu ampe uungwana wa kujua kuwa anaowaongoza ni binadamu wenye damu wenye nyama, walio maskini na tajiri. Kauli za mkuu wetu wa nchi zinatukwaza.

“Yapo mambo mazuri anayofanya lakini yapo mambo mengine anayofanya na kauli ambazo haziashirii kuwa kiongozi mkuu wa Taifa ni mfariji. Wewe Rais wa nchi, sawa lakini ruhusu tukukosoe.

“Sisi tunaamini huwezi kwenda kwenye wahanga (waathirika)  wa tetemeko la ardhi Bukoba, ukawasimanga badala ya kuwapelekea chakula. Huwezi kutoa kauli kuwa wasio na chakula Serikali haigawi chakula wafe.”

“Hizo sio kauli. Tumuombe Mungu amjaze neema amlegeze ulimi. Ulimi unakaza sana nafikiri mnanielewa.”

Mbowe ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa muungano wa vyama vinne vya upinzani chini ya mwavuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) alisema yako mambo mabaya yanayofanyika katika nchi ambayo alisema wataendelea kuyasema bila ya kuogopa.

“Kwenye nchi zilizoendelea na zinazoheshimu demokrasia, wanaona upinzani kama nyenzo muhimu ya kujenga mshikamano na nguvu ya pamoja ya Taifa. Kwa Serikali yetu ya CCM wapinzani ni maadui.

“Kwa mataifa makubwa yaliyoendelea kama Marekani, Uingereza na Ujerumani, wana vyama vingi vya siasa. Ukienda Marekani wana mtu anaitwa (Donald) Trump na Democrat wana (Hilary) Clinton.

“Wamepambana kwenye uchaguzi na uchaguzi umemalizika hakuna anayempiga mwenzie ngumi. Hapa uchaguzi umeisha miaka miwili lakini bado ni visasi tu. Kamata viongozi, wabunge weka ndani.”

Tangu Rais Magufuli apige marufuku mikutano ya vyama vya siasa na maandamano hadi mwaka 2020, viongozi wa upinzani wakiwamo wabunge, wamejikuta katika msuguano na Jeshi la Polisi.

Ingawa Rais aliruhusu wabunge na madiwani kufanya mikutano katika maeneo yao ya uchaguzi, lakini bado baadhi ya viongozi hao wamejikuta matatani wanapofanya mikutano baadhi wakidaiwa kutoa maneno ya uchochezi au kutopata kibali.

Mbowe yupo katika ziara ya siku nane jimboni mwake, ambako pamoja na mambo mengine, atatembelea miradi ya maendeleo na kusikiliza kero mbalimbali kutoka kwa wananchi.

Akizungumza jana katika moja ya mikutano hiyo, Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Grace Kiwelu alisema Mbowe ameandaa mpango kabambe wa kuwakomboa wananchi wa jimbo hilo kiuchumi.

Kiwelu ambaye pia ni mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) Mkoa wa Kilimanjaro aliwaomba wanawake wa jimbo hilo kujiunga katika vikundi ili waweze kunufaika na mpango huo wa Mbowe.

Ingawa hakufafanua mpango huo utakuwaje, lakini Kiwelu alisema wanawake katika vikundi hivyo watapatiwa fedha za kuanzisha shughuli za kiuchumi ili kujikomboa dhidi ya umaskini.

Mwananchi

Mbunge Nape Nhauye Arusha Dongo Kizani...Je Unadhani Linamlenga Nani?

$
0
0
"Ukweli unatabia moja nzuri sana, haujali mkubwa wala mdogo, haujali adui wala rafiki. Kwake watu wote ni sawa." Mwl. Nyerere, Hayo ni maneno ya Nape Nnauye kupitia ukurasa wake wa Twitter jana Agosti 9, 2017


Wahariri Wapuuza Agizo la Viongozi wa TEF la Kusitisha Zuio la Kuandika Habari za Paul Makonda...

$
0
0
Ni wahariri wa magazeti ambao wameipuuzia kabisa habari ya Press Conference ya jana kati ya Makonda na wanahabari.

Gazeti pekee lilioripoti habari ya viongozi wa TEF kutangaza kusitisha zuio la kuandika habari za Makonda ni gazeti la Uhuru tu ila magazeti mengine yote yameipata kisogo habari hiyo na picha zake.

Viongozi wa TEF mjitafakari kama mnafaa kuendelea na nyazifa zenu ndani ya Taasisi hiyo maana ni wazi hata wahariri wenzenu wanawapinga katika hili jambo.

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa leo.......

$
0
0

Natukanwa Sana, Nashambuliwa Kisa Mke wangu – Roma Mkatoliki

$
0
0
Msanii wa muziki wa Hip Hop, Roma Mkatoliki amefunguka kwa kudai kuwa baada ya mama watoto wake kumpambania katika matatizo ya kutekwa miezi miwili iliyopita, mashabiki hawataki kuona rapa huyo akifanyia tendo lolote baya mwanamke huyo.

 Rapa huyo amedai akionekana anapiga picha na mwanamke yeyote tofauti na mke wake huyo anaoga matusi kupitia mitandao ya kijamii kitu ambacho kinamfanya aishi kwa taadhari.

“Natukanwa, nashambuliwa sana tena nikionekana nipo na mwanamke tunatembea maeneo fulani natukanwa sana, wanasema wewe mwanamke wako alivyokupambania halafu unafanya ushenzi,” Roma aliimbia Bongo5. “Kwa hiyo inaonekana ni mwanamke fulani aliyebarikiwa na hatakiwi kukosewa kabisa,”

Katika hatua nyingine rapa huyo amedai bado kidole chake kimoja hakijakaa sawa mpaka sasa baada ya kuteguka miezi miwili iliyopita baada ya kutekwa na watu wasiojulikana.

Unaambiwa Maisha ya Jack Wolper yanategemea Pombe

$
0
0
IMEBAINIKA! Msanii wa Bongo Movie, Jacqueline Wolper akiwa hajapiga ‘tungi’ anakuwa na aibu kiasi cha kushindwa kuzungumza jambo mbele za watu.

Wolper alivujisha siri hiyo juzikati baada ya kufanya ‘interview’ akiwa hajaonja kilevi na kutoboa ukweli kuwa hakuwa na ‘konfidesi’ kwa sababu hakuwa ameshtua.

“Unajua nikiwa sijanywa mimi huwa nina aibu kweli lakini nikipiga mambo yetu utanikataa, jicho linakuwa kavu wala sibabaiki,” alisema Wolper.

Muigizaji Aliyejitokeza na Kudai Mtoto wa Mobetto ni wake Ashambuliwa

$
0
0
Mshindi wa milioni 50 za Tanzania Movie Talent, Dennis Louis amesema mtoto wa Hamisa ni wake sio wa Diamond kama watu wanavyodai kauli ambayo imewafanya madau wengi katika mitandao ya kijamii kupingana na kauli hiyo huku wengine wakienda mbali zaidi kwa kudai kwamba ametumwa.


Muigizaji huyo amekuwa akipost vitu mbalimbali kupitia mtandao wake wa Instagram kujaribu kuthitisha kwamba mtoto huyo ni wake.


“Mengi yamesemwa nimevumilia vya kutosha mwenye mzigo nadhani mshanijua!! Kabla hamjaandika mambo zenu muwe na evidence za kutosha!!. Basi wenye wivu watasema Photoshop shubaaamit!!! #babajunior #comingsoon” amepost picha akiwa na Hamisa,” aliandika muigizaji huyo Instagram.


Katika post nyingine yenye picha yake na Hamisa Mobetto ameandika, “Siku tuliyomtengeneza junior wetu mimi na mama Dee pale magomeni usalama. Hotel siitaji..kila mtu apambane na huba lake…kuna mwenye tatizo huko!? Kama yupo kufwaaaz you know!!,”

Hata hivyo imebainika kuwa picha zote alizoweka Dennis akiwa na Hamisa sio halisi bali zinadaiwa kutengenezwa.

Mobetto hajaweka wazi mtoto wake huyo ni wa nani huku wadai wa mambo wakidai mtoto huyo ni wa Diamond.

Haya ni maoni ya mashabiki hao.

real_monie
Anatafuta kiki kwa pikipiki @angel_zadamz tumegomaaaa!!babake twamjua!

aronmwenga
Ila mbona mtoto anamdomo km wa yule jamaa..mnyama.?au karithi kwa babuyako?

Mdeecaroline
Mhhh…. We umejiedit kabisa na hyo suti yako nyeusi… Loooh.

stelambithe
Kumbe we do mwenye mimba..😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨

naslike_
😂😂😂👌 asanteee dadiii kwakuniletea mama mremboooo🙈🙈 tho ulificha ila asante 😂😂😂😂😂 @charles_willson


Bongo5

Mange Amshukia Tena Wolper Baada ya Kuwaponda Wanaokatazwa Kupost Picha za Mabwana zao Mtandaoni..

$
0
0
Mange Kimambi amefunguka haya kupitia Instagram yake:

#Regrann from #mangekimambi_ .
"Wolper haki ya Mungu una akili ka za teenager vile...... Sasa unajiona mjanja sababu eti unaruhusa ya kumposti Huyo mtoto?? Unajua Wolper haupo serious. Sasa hiko kitoto kinalala kwako kinakula kwako kinaanzia wapi kukataaa usikiposti??

Simple fact is wanaume wengi wa kitanzania wenye maisha mazuri Na kazi nzuri hawapendi kupostiwa hovyo especially na nyinyi mastaaaa ni hao wanaotomba bure ndo wanaokubaligi kupostiwa wakifanya uupuuzi.

Yule Mcongo tu mbona ulikuwa humposti mkifanya upuuzi.Ulikuwa unamposti mara moja moja tena picha za heshma, si ni sababu yule angalau alikuwa anapesa flani angalau anakusaidia.Hawa wanaume wooote ulioanza kujirusha nao akili mitandaoni ni vitoto ambavyo havikulishi havikuvishi sana sana vinalala kwako vinaamkia kwako hata ukitaka kuposti mkiwa uchi havitokataaa sababu vinakutegemea...

Nakupa challenge Wolper embu pata boyfriend mwenye pesa zake za maana Na maisha ya maana Alafu jaribu kumrusha mitandaoni mkilambana lambana, utawarushaga hao hao wanaoishi kwako
Tena usiwadanganye wenzio wenye mabwana wa maana Wawarushe mitandaoni. Hivi bado hamjajifunza kwa Zari, Diamond na Hamisa kuwa kupostiwa sio issue. Unaweza kupostiwa mitandaoni huku nyuma watu ndo kwanza wanazaaa watoto.

Jamani msiwaige kina AmberRose wale ni professional goldiggers hawatembei na wanaume maskini. Msimuone na hiko kitoto chenye rasta mkadhani kile kitoto kimechacha au kinaishi kwa AmberRose Kama hao Kina BFF wenu.21 Savage had a song at #23 on the billboard chart.His album ISSA debuted at #2 kwenye billboard 200 chart. He is going places.

Ila Wolper unajua kupenda aiseee, Mimi na upare huu Eti mwanaume wa kuja kulala kwangu, kuendesha gari yangu , Uwiiiiiiiiiii hata nyege hazipandiiiiiiiii ..Yani bora nife mwenyewe nije kulea watoto wa kina Kenzo kuliko niwe na mwanaume hana hela ana kazi ya kunitia tu na kuniambia I love you🤣. Yani hata akihema ntakuwa napata hasira....Haki nna allergy na wanaume wasio na hela. Siweziiiiii" Mange Kimambi

Breaking News: Majambazi 13 Wauawa Kibiti, Wakutwa na Bunduki 8 Pamoja na Pikipiki Mbili...

$
0
0

Watu 13 wanaodaiwa kuwa ahalifu wameuawa na Askari wa Jeshi la Polisi. Watu hao wamekutwa na Bunduki nane, Pikipiki mbili pamoja na Begi moja la nguo.

Tukio hilo limetokea katika maeneo ya Tangibovu Kijiji cha Milaweni, huko Kibiti Mkoani Pwani.

Chanzo: Jeshi la Polisi Tanzania(Ukurasa wa Twitter)

Kutana Mtaalam wa Tiba Asili Mwenye Uwezo Mkubwa wa Kutatua Matatizo Kwa Nyota na Dua

$
0
0
Kutana Mtaalam wa Tiba Asili Mwenye Uwezo Mkubwa wa Kutatua Matatizo Kwa Nyota na Dua
KUTANA NA TABIBU MWENYE KUBRI KUTOKA KWA ALAH MAALIM ISSA NAJIMU. NI SHARIFU
MWENYE UWEZO WA KUBAINI TATIZO LAKO PUNDE TU UNAPO MFANYIA MAWASILIANO KUPITIA
WASAA NA SIKU KWA MAWASILIANO:-
MAALIM ISSA NAJIMU KUTOKA MKOA WA TANGA MWAMBONI MAGOFU KATA YA NGUVU MALI
NCHINI TANZANIA, NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA
QUR-AN, DAWA ZA ASILI PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.
ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE / MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-

 ULIJALI (NGUVU ZA KIUME)
 MIGUU KUWAKA MOTO
 KUTAFSIRI NDOTO
 MFARAKANO WA WANANDOA
 MFARAKANO KAZINI
 KUPANDSHWA CHEO
 KUTOA PETE YA BAHATI
 ANAO UWEZO WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUBASHIRI
 KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA
 KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU /MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA.
 ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA
KUMUOA AU KUWA NAYE.
 ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA KWA NJIA YA MSUKULE
 ANAO UWEZO WA KUUAq KESI SUGU NA PYA NDANI SIKU 7 TU.

 MENGINEYO MENGI ZAIDI YALIYO KUWA SUGU PIGA-
 Mobile; 0717 70 32 41.
 WhatsApp 06226 535419.

RC Paul Makonda Ametangaza Walemavu DSM Kupewa Miguu ya Bandia Bure

$
0
0

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amefanikiwa kupata miguu ya bandia itakayoweza kuwasaidia wananchi wenye mahitaji.

Miguu hiyo yenye thamani ya Shilingi Milion 800 itatolewa bila malipo kwa wananchi waliopata ajali na kushimdwa kupata miguu hiyo kutokana na kushindwa kumudu gharama za kununua miguu hiyo ambapo mguu mmoja unagharimu Milion tatu.

Kwa mantiki hiyo amewatangazia wananchi wote wenye mahitaji ya miguu ya bandia na hawana uwezo wa kumudu gharama kufika ofisini ya mkuu wa mkoa siku ya Jumatatu na Jumanne kwaajili kukutana na wataalamu wa miguu watakaochukua vipimo kwaajili ya kutengenezewa miguu kulingana na maumbile yao.

Amesema miguu hiyo ya watu 200 itatolewa kwa awamu hii ya kwanza ambapo kama mahitaji yatakuwa makubwa na wafadhili wakaongezeka itatolewa tena kwa awamu nyingine lengo likiwa ni kuwasaidia wananchi kutotumia magongo.

"Nimepewa kazi ya mkoa kuhudumia makundi yote, nafahamu kwenye mkoa wangu wapo waliopata ajali na wengine wakavunjika miguu lakini pesa ya kupata miguu ya bandia ili waachane na magongo kwao imekuwa ni moja ya changamoto, kutokana na sababu hiyo nimeona vyema nifikiri namna ya kuwasaidia wananchi ambao hawana uwezo ili waweze kupata, nimefanikiwa kupata wadau watakaonipatia miguu ya kuhudumia wananchi 200" Alisema Makonda.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images