Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Zijue Dalili, Athari na Tiba ya Upungufu wa Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo....

$
0
0
ZIJUE DALILI, ATHARI NA TIBA YA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO NA KUONGEZA UUME.
       Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA  (MASTER BLASHION), UNYWAJI WA POMBE, HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k.
     Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

      BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo.
     Kwa kutumia mimea na matunda @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-

1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 hadi 7 @150,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari na kuweza kurudia tendo @150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130,000/=
      BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA.
    KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE KAMA
>Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
>Kuondoa mvi milele zisiludi @150,000/=
>Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) 200,000/=
>Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @130,000/=  
           
   Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa (+255)
           0767447444 na
              0714335378
    NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Chakula Cha Kuzuia Kuzeeka Haraka......

$
0
0
Maisha ya sasa hivi yamegubikwa na matumizi ya vipodozi vya kuzuia uzee hadi kufikia kiwango cha kuonekana kama ni chakula kuliko vitu vya urembo. Vipodozi hivyo huja kama creams, visafisha ngozi au serums. Lakini ieleweke kuwa kutumia vipodozi vya kuondoa uzee juu ya ngozi hakuwezi kuwa mbadala wa chakula ambacho kinaboresha mwonekano na kutunza ngozi yako kuanzia ndani. Chakula cha kuzuia kuzeeka haraka ndiyo kitu muhimu katika kuufanya mwili wako usizeeke haraka na katika kuulinda mwili wako kutokana na mionzi ya UV (ultra violet) ambayo ndio chanzo kikuu cha mistari na mikunyanzi juu ya ngozi yako. Ungana nami leo kuona ni chakula gani kinasaidia kutunza mwonekano wako wa ujana.  Lakini kwanza tuvichambue vitu muhimu katika  chakula vyenye uwezo wa kulinda mwili wako usizeeke haraka.

 Vitu Muhimu Katika Chakula Vya Kuzuia Kuzeeka Haraka

 Katika mada yetu ya Ondoa Uzee tuliona kwamba mahitaji ya mwili hubadilika kadri umri unavyosonga mbele na kwamba ili kudumisha muonekano wa ujana kwa mwili wako unahitaji kuupa mwili wako mahitaji yake yaliyobadilika. Tuliona kwamba kuzuia kuzeeka haraka unahitaji chakula chenye calcium ya kutosha kuipa mifupa yako nguvu na kupata chakula chenye collagen kwa wingi ili kuifanya ngozi yako isiwe na mikunyanzi (wrinkles).

Katika miaka ya 1950 mwanasayansi Denham Harman aligundua kuwepo uhusiano mkubwa kati ya mwili kuzeeka na uwepo wa “free radicals” katika mwili wa mtu. Free radicals ni kemikali ambazo hutengenezwa na mwili katika ufanyaji wake kazi wa kawaida. Mwili una uwezo wa kudhibiti madhara yanayotokana na uwepo wa free radicals kwa kiasi fulani, lakini idadi ikizidi mwili huzidiwa na madhara mengi hutokea, yakiwepo kuzeeka kwa mwili na magonjwa mengi kama kansa, magonjwa ya moyo, arthritis, atherosclerosis, Alzheimer’s, ugonjwa wa Parkinson’s na kisukari.

Free radicals katika mwili huweza kuongezeka kwa kutumia vitu kutoka nje ya mwili. Sumu kutoka nje zinazozalisha free radicals katika mwili ni pamoja na hewa chafu hasa inayotoka kwenye viwanda, moshi wa sigara, maji na chakula chenye dawa za kuulia wadudu na utumiaji wa pombe kwa kiwango cha kuzidi kiwango.

Kiwango kidogo cha free radicals kinachozalishwa na mwili wenyewe kinaweza kikadhibitiwa vizuri na kemikali nyingine zinazoitwa antioxidants ambazo nazo pia huzalishwa na mwili. Free radicals za ziada zinazozalishwa na vitu kutoka nje ya mwili zisipodhibitiwa kikamilifu husababisha madhara mengi pamoja na magonjwa yaliyotajwa hapo juu.

Hivyo basi tunahitaji kupata chakula chenye antioxidants kwa wingi ili kuisaidia miili yetu kupambana na free radicals hizi za ziada. Kuna aina nyingi za antioxidants zilikwemo vitamini C, vitamini E, Flavonoids na Polyphenols kwa kutaja tu bila kuingia kwa undani zaidi.

Baada ya maelezo haya kidogo ya utangulizi, nafikiri sasa ni wakati mwafaka wa kupitia chakula ambacho kikitumiwa kitakupa vitu tulivyovitaja hapo juu na kuufanya mwili wako kuwa na mwonekano wa ujana daima.

 Chakula Chenye Vitamini C 

 Utafiti uliofanywa kwenye kikundi cha wanawake wenye umri wa miaka zaidi ya 40 ulionyesha kwamba wanawake wanaotumia chakula chenye vitamini C zaidi walikuwa na mikunyanzi (wrinkles) kidogo zaidi na ngozi zao hazikuwa kavu ukilinganisha na wale ambao walitumia vitamini hiyo kidogo. Hii ni kwa sababu vitamini C ni antioxidant yenye nguvu inayozuia uharibifu wa seli na DNA za seli hivyo kulinda uzalishaji wa collagen ambayo ndiyo nguzo muhimu ya kulinda ngozi yako.

 Unashauriwa basi upate angalau mg 75 za vitamini hii kwa siku. Kwa mfano unaweza kupata chungwa moja wakati wa kifungua kinywa na piliplili tano za njano ndani ya saladi kwenye mlo wako wa mchana. Chakula chenye vitamini C kwa wingi ni broccoli, strawberries, pilipili nyekundu, nyanya, tikitimaji, pomegranate n.k.

 Chakula Chenye Protini

 Tafiti zilionyesha kuwa wanawake waliotumia proteni zaidi walikuwa na wrinkles chache zaidi kwenye ngozi zao kuliko wale ambao walitumia proteni kidogo, hii kwa sababu proteni hutoa viungo muhimu katika ujenzi wa collagen.

Ili upate proteni unashauriwa kula nyama ya kuku isiyo na ngozi, sehemu nyeupe ya mayai na samaki. Unapochagua kula nyama ya ng’ombe au nguruwe, pendelea kutumia ile isiyo na mafuta sana. Matumizi ya soya yameonyesha kusaidia kuondoa ile mistari myembamba kweye macho.

 Samaki Wenye Mafuta

Samaki wa baharini wenye mafuta wamebainika kuwa na kiwango kikubwa cha “omega-3 fatty acids”, kitu ambacho husaidia kuilinda ngozi yako kutokana na mionzi mibaya ya jua ambayo hudhoofisha collagen.


Nafaka Nzima

 Utumiaji wa nafaka nzima badala ya wali mweupe, mikate inayotokana na ngano nyeupe na nafaka nyingine zilizokobolewa una faida nyingi. Moja ni kuzuia mwongezeko wa insulin katika mwili ambayo ina madhara ya kuharibu ngozi. Pia nafaka nzima ni chanzo cha madini ya selenium ambayo husaidia kuikinga ngozi yako kutokana na mionzi ya jua (UV rays).


Unashauriwa kutumia brown rice, shayiri na ngano nzima ili uweze kupata madini haya yatakayokusaidia kulinda ngozi yako.


Green Tea

Green tea ni kinywaji chenye antioxidants nyingi. Unywaji wa vikombe viwili au vitatu kwa siku wa chai hii utaifanya ngozi yako kuwa nyororo. Chai hii pia huzuia mikunyanzi isitokee kwenye ngozi yako.

Hatuwezi kuorodhesha chakula chote ambacho kinafaa katika kuzuia kuzeeka haraka katika ukurasa mmoja, hivyo makala yetu inatoa mwongozo tu wa namna ambavyo unaweza kupanga mlo wako. Usisite kutoa maoni yako kuhusu mada hii, tutafurahi mno kusikia kutoka kwako msomaji.

Je Kunyonyesha Kuna Sababisha Maziwa ya Mwanamke Kudondoka? Huu Hapa Ukweli na Uongo Kuhusu Konyonyesha

$
0
0
Na Mary Mathenge

Maziwa ya mama yana virutubisho vyote kwa uwiano unaotakiwa kwa ajili ya ukuaji wa mtoto. Karibu wanawake wote wana uwezo wa kunyonyesha. Ni jambo ambalo mwanamke inabidi ajifunze na kujizoesha kabla halijawa jepesi kwake.

Uzushi mwingi unaosambaa kuhusu kunyonyesha umekuwa ukisambazwa kupitia kwa wanafamilia na marafiki lakini taarifa nyingine za aina hiyo hazina ukweli wowote au zimepitwa na wakati. Mary Mathenge ni Meneja wa Unyonyeshaji katika Chuo Kikuu cha Tiba Aga Khan jijini Nairobi anaelezea baadhi ya imani hizi za kizushi pamoja na kueleza usahihi wa jambo hilo.

UONGO KUHUSU KUNYONYESHA

Kunyonyesha kutasababisha matiti yadondoke

Kunyonyesha mtoto hakusababishi maziwa ya mama kuanguka. Kinachosababisha maziwa kuanguka ni kuongezeka kwa umri wa mwanamke, kupungua au kuongezeka kwa uzito wa mwili. Lakini pia, ni muhimu kwa mwanamke kuvaa sidiria sahihi ili kuyapunguzia uzito matiti ya mama anayenyonyesha kutokana na kuongezeka kwa maziwa yanayotakiwa kunyonywa na mtoto (uzito wa matiti huongezeka wakati wa kunyonyesha).

Maziwa ya kopo yana virutubisho sawa na vilivyomo kwenye maziwa ya mama

Virutubisho vinavyowekwa kwenye maziwa ya kopo havalingani na vilivyomo kwenye maziwa ya mama. Maziwa ya kopo hayatokani na kiumbe hai, kwahiyo hayana vimelea vya kuulinda mwili, seli hai, enzaimu au homoni ambazo zinamlinda mtoto wako asipate maambukizi na magonjwa mara kwa mara katika ukuaji wake.

Maziwa ya kopo yanatengenezwa kwa protini mbalimbali ikiwamo protini inayopatikana kwenye maziwa ya wanyama, soya na mafuta ya mimea. Na ingawa yameboreshwa ili kufananishwa na maziwa ya mama, bado maziwa haya ya makopo hayana uwezo wa kufananishwa kwakuwa hayatoki kwenye kiumbe hai kwenda moja kwa moja kwa mtoto.

Watoto wanaonyonya maziwa ya kopo wanakuwa na afya bora zaidi ya wale wanaonyonya maziwa ya mama

Watoto wanaonyonya maziwa ya mama zao wanaongezeka uzito kidogo baada ya mwaka mmoja ikilinganishwa na uzito mkubwa ambao huongezeka kwa watoto wanaonyonya maziwa ya kopo. Tafiti zinaonesha kwamba watoto walionyonyeshwa na mama zao si rahisi kuzidi uzito utotoni mwao au wanapokuwa watu wazima ikilinganishwa na watoto waliopewa maziwa ya kopo – pia huwa wanapata matatizo kidogo kiafya.

Watoto walionyonya maziwa ya kopo wanaweza kuwa na tatizo la kushindwa maziwa ya mama au ya mnyama ambayo yana protini kwa wingi, wana hatari kubwa zaidi ya kupata magonjwa ya kuharisha, matatizo ya tumbo, upele na magonjwa mengine kutokana na kunyweshwa maziwa yenye aina tofauti za protini.

Kunyonyesha ni rahisi kwa baadhi ya wanawake, lakini wengine hawatoi maziwa ya kutosha

Karibu wanawake wote kimaumbile wana uwezo wa kunyonyesha. Ni ujuzi ambao kila mwanamke anatakiwa kujifunza na kuufanyia mazoezi kabla hajazoea. Baadhi ya wanawake wanajifunza haraka na wengine huchelewa, lakini karibu wanawake wote wana uwezo wa kutengeneza maziwa ya kuwatosha watoto wao. Chakula anachokula mama anayenyonyesha huchukua nafasi kubwa sana katika utengenezwaji wa maziwa.

Wanawake wenye matiti madogo, hayatoi maziwa mengi

Umbo na ukubwa wa matiti na chuchu za mzazi unatokana na kiwango cha mafuta tishu zilizopo kwenye maziwa, hivyo, mwanamke awe na matiti makubwa au madogo, bado wana uwezo wa kuwa na maziwa mengi ya kutosha.

Mwenye chuchu ndogo au zilizoelekea juu hawezi kunyonyesha

Baada ya kujifungua, wanawake wengi wenye chuchu ndogo au zilizoelekea juu wataona mabadiliko ambapo chuchu zake zitajirekebisha mara baada ya kuanza kunyonyesha – hakuna matayarisho yoyote yanayotakiwa kufanywa wakati wa ujauzito. Mazoezi yanayofanywa na wengi ya kuvuta na kuzungusha chuchu za matiti hayasaidii chochote.

Wanaonyonyesha wanapunguza uwezekano wa kubeba mimba tena

Kumnyonyesha mtoto mchanga kunamsaidia mwanamke. Kunyonyesha ni njia ya asili ya kupanga uzazi inayosaidia sana mtoto anapokuwa chini ya miezi sita kwakuwa anakuwa mzazi anakuwa anatumia muda mrefu kumnyonyesha mtoto na bado mzunguko wa hedhi unakuwa haujaanza rasmi. Kunyonyesha kunasaidia kuchelewa kurutubishwa kwa mayai, lakini ufanisi wa njia hii ya kupanga uzazi huondoka mtoto kunyonya kidogo na kulala zaidi. Kwahiyo, kama mzazi hataki kupata mimba anatakiwa kutumia njia nyingine salama zaidi ya uzazi wa mpango mapema anapoanza tena kujamiiana baada ya kujifungua.

Mama anayenyonyesha hawezi kufanya mapenzi kwa njia salama

Baada ya kujifungua, utaamua mwenyewe uanze lini uanze tena kujamiiana na mwenza wako. Aina ya homoni inayosaidia kuruhusu maziwa kutoka ili yanyonywe na mtoto (xytocin) hutengenezwa pia wakati wa kujamiiana. Hivyo wakati wa kujamiiana, mwanamke anaweza kutokwa na maziwa kidogo – hili ni jambo la kawaida, usishangazwe nalo.

Watu hawapendi kuona mwanamke akinyonyesha hadharani

Tafiti zinaonesha kwamba watu wengi hawashangazwi na hawakerwi kuona mwanamke anamnyonyesha mwanaye hadharani. Sanasana watu watamkasirikia na kumkaripia mzazi ambaye anamwacha mtoto alie muda mrefu kwa njaa akihofu kuonekana. Watoto wanatakiwa kunyonya kila mara, na hii inamaanisha mama anakosa sehemu ya faragha ya kumnyonyesha mtoto.

Mzazi anatakiwa kuvaa nguo zinazoweza kumfanya anyonyeshwe kirahisi, kama sidiria maalum za kunyonyeshea au nguo inayoweza kupanda juu kwa urahisi kutokea kiunoni au inayoshuka kirahisi kutokea juu. Pia ni vizuri kuwa na kitambaa chepesi au mtandio kwa kujifunika kuzunguka mabega ili kujisitiri.

UKWELI KUHUSU KUNYONYESHA

Watoto wanaweza kuishi kwa kunyonya maziwa ya mama tu kwa miezi sita ya mwanzo

Inashauriwa kwamba watoto wapewe maziwa ya mama tu katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo toka kuzaliwa. Maziwa ya mama yana virutubisho sahihi katika uwiano unaotakiwa kwa ajili ya ukuaji wa kawaida wa mtoto mpaka atakapofikisha umri wa miezi sita. Maziwa ya mama ni rahisi kumeng’enywa, yanatumiwa kwa kiasi kikubwa mwilini, masafa, yana joto linalotakiwa na binadamu na si rahisi kupata maambukizi kabla mtoto hajayanyonya na pia yanaondoa uwezekano wa mtoto kuwa na uzito mkubwa sana utotoni mwake.

Kunyonyesha kunamsaidia mama kupunguza uzito ulioongezeka wakati wa ujauzito

Sio tu kwamba kunyonyesha kunamsaidia mwanamke kupunguza uzito wa ziada (ulioongezeka wakati wa ujauzito), pia inasaidia kufanya mji wa uzazi kurudi katika hali yake ya kawaida na kupunguza kiasi cha damu inayotoka katika wiki sita za kwanza toka kujifungua (kipindi ambacho maumbile ya mzazi yanarudi kwenye hali yake ya kawaida yalivyokuwa kabla ya ujauzito).

Mtoto anatakiwa kunyonyeshwa haraka iwezekanavyo baada ya kuzaliwa

Haraka sana baada ya kuzaliwa (ikiwezekana kabla ya kitovu kukatwa), mtoto anatakiwa anyonyeshwe na kisha anyonye mara kwa mara anapopata njaa. Mara nyingi mtoto ananyonya maziwa mengi katika saa mbili za kwanza tangu azaliwe. Kwa wale waliojifungua kwa upasuaji, mama anatakiwa apewe mwanaye mara moja baada ya kutoka kwenye chumba cha upasuaji (hasa katika upasuaji ambao mama anakuwa hajapewa dawa za usingizi au kupoteza fahamu) ili aweze kumnyonyesha mtoto.

Mtoto anapokataa kunyonya

Kama mtoto atakataa kunyonya, basi yawezekana ni kwa sababu ana vidonda mdomoni ambavyo anaweza kuvipata wakati mama anajifungua. Pia, mtoto anaweza kuwa amezaliwa akiwa anaumwa lakini jambo kama hili linapotokea inatakiwa lichunguzwe na kupatiwa matibabu. Muda mwingine sababu yawezekana mzazi anakuwa na maziwa mengi sana na yanayotoka kwa kasi hadi kumpalia mtoto wakati ananyonya. Ikiwa ni hivi, ni vyema mama akakamua na kuhifadhi maziwa haya kwenye chombo safi na kuyaweka kwenye friza ili yatumike baadaye.

Chuchu za mama zinapouma, ni ngumu kunyonyesha

Maumivu kwenye chuchu yanatokea iwapo mtoto atawekwa vibaya kwenye titi la mama. Mtoto anatakiwa kuingiza mdomoni sehemu ya titi la mama, sio chuchu peke yake. Kama ikifanyika hivi, chuchu za mama hazitakiwi kuuma, hata kwa siku za mwanzo za kunyonyesha. Mafuta-salama yanayomsaidia mzazi aendelee kumnyonyesha mtoto hata kama chuchu zinauma.

Mzazi anayefanyakazi pia anaweza kumpa mwanae maziwa tu kwa miezi sita ya mwanzo

Mzazi anaweza kuendelea kumpa mwanaye maziwa tu kwa miezi sita ya mwanzo au zaidi akiwa ameajiriwa. Anaweza kumnyonyesha moja kwa moja nyakati anazokuwa nyumbani baada ya muda wa kazi na kukamua maziwa na kuyahifadhi ili anyweshwe wakati anapokuwa kazini. Maziwa haya yanaweza kuhifadhiwa na mtoto kuyanywa siku inayofata.

Maziwa haya yaliyokamuliwa kutoka kwenye matiti ya mzazi yanabaki kuwa salama kwa mtoto yakihifadhiwa kwa muda wa saa nane kwenye joto la kawaida la nyumbani. Pia yanaweza kuhifadhiwa kwa kugandishwa kwenye friza kwa miezi sita na kuwa salama kwa mtoto. Chombo kilichogandisha maziwa hayo kinatakiwa kiwekwe kwenye maji ya moto ili maziwa yaweze kuyeyuka taratibu.

Namna ya Kupunguza Tumbo Kubwa Au Kitambi.....

$
0
0
Katika jamii yetu wanawake ndio wanaohangaika zaid kutoa matumbo yao makubwa, utawasikia mara nyingi wakiulizia kuhusu dawa ya kupunguza tumbo kwa wanawake, lakini si kwa ajili ya kukwepa madhara ya kiafya, bali kwa ajili ya kuboresha mwonekano wao kiurembo-kwao ni suala la urembo tu na si suala la afya. Kwa upande mwingine akina baba huona fahari kuwa na vitambi, kwao kitambi ni dalili ya kunyookewa na maisha.

Katika mada ya leo tutazungumzia hayo matumbo makubwa na vitambi ambapo tutaona matumbo hayo au vitambi hivyo ni nini, tutaeleza madhara ya kuwa na matumbo hayo makubwa na mwisho kutoa ushauri wa jinsi ya kuyapunguza matumbo hayo.



Nini Maana Ya Tumbo Kubwa Au Kitambi

Leo utasikia neno la ajabu kuwa “kila mtu ana kitambi, hata yule ambaye tumbo lake kwa nje linaonekana kuwa flat kabisa na kuwa kitambi kina madhara makubwa kwa afya yako kuliko aina nyingine yo yote ya mafuta yaliyo ndani ya mwili wako.”

Hii ina maana gani?

Kitambi ni mafuta na mafuta haya yanaweza kuwa chini ya ngozi yako au ndani kabisa kuzunguka moyo, mapafu, maini na viungo vingine. Ni mafuta haya ya ndani (visceral fat) ambayo yanaweza kuwa tatizo kubwa kwa afya yako hata kama mwili wako ni mwembamba kiasi gani. Mwili huhitaji mafuta haya ya ndani kwa ajili ya kutenganisha viungo vya ndani ya mwili visigusane na kusuguana, lakini yakizidi huleta matatizo ya kiafya. Ukiwa na mafuta mengi mno utakuwa kwenye hatari ya kukumbwa na magonjwa kama ya high blood pressure, kisukari (Type 2 Diabetes), magonjwa ya moyo, kansa (kansa ya maziwa na kansa ya utumbo) na mengine. Kuongeza uzito au kunenepa kunasababisha mwili ushindwe kupata sehemu ya kutosha ya kuhifadhi mafuta na hivyo kuanza kuyatunza mafuta hayo kwenye sehemu za ndani ya mwili, kuuzunguka moyo, na ndipo matatizo yanapoanza.

 Utapimaje Tumbo Lako?

 Kuna njia za kitaalamu za kupima kiasi cha mafuta ya ndani uliyo nayo ambazo ni CT Scan au MRI lakini pia unaweza kujipima mwenyewe ukapata picha nzuri tu ya hali yako. Chukua kipimo cha utepe, kile kinachotumiwa na mafundi cherehani (measuring tape), jipime eneo la kitovuni ukiwa umesimama huku ukihakikisha kuwa utepe ni mnyoofu. Kwa afya nzuri, kipimo kisizidi nchi 35 kwa mwanamke na kisidi nchi 40 kwa mwanamme.

Kuwa na mwili wenye umbo la pears “pear shape”, hips na mapaja makubwa, kunafikiriwa kuwa ni bora zaidi ya umbo la apple ambalo linamaanisha kiuno kipana zaidi. Kuwa na kiuno kipana kuna uwiano na kiasi cha mafuta ya ndani (visceral fat) uliyo nayo.


 Namna Ya kuondoa Matumbo

Tumeona hapo juu kuwa hata watu wembamba wana mafuta ya ndani ambayo yanaweza kuwasababishia matatizo ya kiafya. Uwingi wa mafuta unakuwa ni wa kiurithi, utalingana na style ya maisha unayoishi na jinsi gani mwili wako unafanya mazoezi – mafuta haya hupenda mtu asiyejishugulisha yaani yule ambaye anaufanya mwili wake kubweteka.

Maandiko mengi sana yameandikwa kuhusu namna ya kupunguza unene wa mwili na makampuni mengi yamekuja na dawa za kudai kupunguza unene wa mtu. Kimsingi ili mwili upungue unene, unahitaji kutumia kalori nyingi kuliko unazozipokea. Hili ni la kweli vilevile kwa mada yetu ya leo ya kupunguza tumbo kwani si rahisi kupunguza tumbo peke yake bila kupunguza sehemu nyingine za mwili. Ili kufanikisha azma ya kutumia kalori nyingi zaidi ya zile unazozipokea, hapa nashauri njia 4 za kuzitumia:



1. Mazoezi Ya Viungo Ya Kupunguza Tumbo

Unaweza kufanya mazoezi ya aina nyingi ili kupunguza tumbo. Mazoezi yo yote ya nguvu yatapunguza mafuta ya mwili wako pamoja na mafuta ya ndani (visceral fat).

Mazoezi ya kadri ya dakika 30 mara tano kwa wiki yanafaa, kama vile kutembea, ili mradi unatoa jasho, yatakufanya uheme kwa haraka na kuongeza mapigo ya moyo wako.

Unaweza kupunguza muda kwa kufanya mazoezi ya nguvu zaidi kama jogging kwa dakika 20 mara nne kwa wiki.
 Unaweza kupata matokeo mazuri vile vile kwa kufanya mazoezi ya ndani ukiwa nyumbani mwako. Nitaonyesha video mbili katika ukurasa huu ili uweze kuchagua ile utayoiona kuwa inakufaa zaidi. Video hizi zinaonyesha mazoezi ambayo wengi wameyajaribu na kuona kuwa yaliwapunguzia matumbo yao katika muda mfupi. Cha msing ni kuanza na mazoezi mepesi na taratibu, kuongeza ugumu wake hadi kufikia mazoezi ya nguvu.

  
2. Chakula

Kuna maandishi mengi mno kuhusu somo hili la kupunguza mafuta ya mwili kwa kuwa na mpango mzuri wa ulaji chakula. Unaweza pia kusoma ukurasa wetu wa “Punguza Unene“. Kwa kifupi unahitaji kuzingatia yafuatayo:


  • Kula mboga za majani kwa wingi sana kulijaza tumbo lako
  • Kunywa maji mengi sana
  • Weka chakula cha kukutia hamu mbali na nyumba yako
  • Tafuta shughuli za kukufanya uwe busy kila wakati
  • Kula kutoka kwenye sahani tu ukiwa umeketi mezani
  • Kula milo yote, acha tabia ya kuruka milo



3. Kupata Usingizi Wa Kutosha

Kupata usingizi kwa muda mzuri kumeonyesha kuwa na mchango katika kudhibiti kiwango cha mafuta katika mwili wa binadamu. Katika utafiti mmoja, watu waliopata usingizi kwa saa 5 hadi 6 kwa siku katika kipindi cha miaka 5, walionyesha kuwa na mafuta mwilini kidogo zaidi ukilinganisha na wale waliopata usingizi kwa pungufu ya saa 5 kwa siku au wale waliolala kwa saa 8 au zaidi kwa siku.

4. Kuepusha Msongo Wa Mawazo

Kila mmoja wetu hapatwa na mawazo. Jinsi unavyoyachukulia mawazo hayo huwa na mchango mkubwa katika kujaza mafuta mwilini. Jaribu kushiriki katika mazungumzo na ndugu katika familia na marafiki zako. Mazoezi ndiyo ndiyo bora kabisa kwani hukutoa kwenye msongo wa mawazo wakati huo huo yakikupunguzia unene. Ukipungukiwa na mawazo utaweza kufanya maamuzi mazuri zaidi kuhusu maisha yako.

5. Kutumia Virutubishi

Kuna virutubishi ambavyo vimethibitika kusaidia kupunguza uzito wa mwili. Virutubishi vinafanya kazi vizuri ikiwa mwili utakuwa na kiwango kizuri cha madini ya calcium katika damu. Tafiti zimeonyesha kuwa asilimia moja ya madini ya calcium ndani ya mwili huwa katika mzunguko wa damu. Kiwango hiki cha calcium kikipungua, homoni ya parathyroid huzuia uvunjwaji wa mafuta katika mwili. Hivyo basi, kama kiwango cha calcium katika damu kitakuwa kimepungua, zoezi la kupunguza mafuta mwilini halitafanikiwa.

Baadhi ya virutubishi vya kupunguza mafuta mwilini ni kama:

1. Slimming Capsules



2. Pro Slim Tea


 i.

Breaking News: Huyu Hapa Atangazwa Kuwa Rais Mpya wa TFF....

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya uchaguzi mkuu wa TFF Revocatus Kuuli amemtangaza Wallace Karia kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kufuatia uchaguzi wa shirikisho hilo uliofanyika leo Makao Makuu ya Tanzania Dodoma.


Wallace Karia ameibuka mshindi wa nafasi ya Urais wa shirikisho hilo huku nafasi ya Makamu ya Rais ikichukuliwa na Michael Wambura, kwa matokeo hayo Wallice Karia anakuwa mrithi wa aliyekuwa Rais wa shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Jamal Malinzi
Baada ya kutangazwa washindi viongozi hao waliweza kula kiapo mbele ya wajumbe wa Kamati ya Uchaguzi, naa baada ya hapo Rais mpya wa shirikisho la mpira wa miguu (TFF) Wallace Karia aliwashukuru wajumbe na watanzania kujumla na kusema kuwa furaha aliyonayo iende kuwa furaha ya kazi kwa kufanya kazi kwa ajili ya maendeleo ya soka la Tanzania.
Hata hivyo Wallace amesema katika uongozi wake uwazi na uwajibikaji ndiyo nguzo kuu na kusema hivi sasa ubabaishaji katika mpira wa miguu sasa umekwisha, ubabaishaji wa soka sasa ni mwisho.
Katika uchaguzi huo wajumbe wa Kamati Kuu ya Uchaguzi waliweza kuchagua pia Kamati ya Utendaji wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania (TFF) katika kanda mbalimbali mbao ni
Lameki Nyangaya (DSM)
Khalid Mohamed (Kilimanjaro na Tanga)
Francis Ndulane (Pwani na Morogoro)
Mohamed Adeo (Dodoma na Singida
Dustan Ditopile (Lindi na Mtwara)
James Mhagama (Njombe na Ruvuma)
Elias Mwanjala (Mbeya na Iringa)
Kenneth Pesambili (Rukwa na Katavi)
Issa Mrisho (Kigoma na Tabora)
Mbasha Matutu (Shinyanga & Simiyu)
Vedastus Lufano (Mara na Mwanza)
Salum Chama (Kagera na Geita)

Breaking News: Wambura Arudi Tena TFF....Ashinda Nafasi ya Makamu wa rais wa TFF, Aapishwa Tayari

$
0
0
Waswahili wanasema, “zege halilali” na ndiyo mambo yalivyokuwa Dodoma maana Michael Wambura ameshinda nafasi ya makamu rais wa TFF na baada ya hapo, tayari ameapishwa rasmi.

Maskini Nuh Mziwanda Adai 'Nawal Ameolewa na Mtu Mwingine Akiwa Bado ni Mke Wangu Halali'

$
0
0
Msanii wa muziki, Nuh Mziwanda amedai Baby Mama wake, Nawal alishinikizwa kuolewa na wazazi wake kabla hata ajampatia talaka.

Muimbaji huyo amedai ingawa tayari aliyekuwa mke wake huyo ameshaolewa mtu mwingine lakini bado hajampatia talaka ya kusema kwamba wameachana.

“Mimi sijaachana na Nawal, mpaka sasa mimi sijatoa talaka kusema mimi wewe sikutaki endelea na maisha yako.,” Nuh aliimbia Times Fm. “Lakini kulikuwa na msuguano wa hapa na pale ambao naamini haukuwa unatokana na mimi na yeye, ulitokana na familia yake. Kwahiyo haikuwa kwamba mimi simtaki Nawal yeye hanitaki mimi ila familia yake ndio iliyosimamia huu mchongo,”

Nuh alisema ingawa hajamuacha Nawal lakini sio mke wake tena kwa sababu tayari ameshaolewa na mwanaume mwingine.

Wawili hao walifanikiwa kupata mtoto mmoja wa kike aitwaye, ‘Anyaghile’.

Gigy Money Atumbua Jibu...Adai Wanawake Wote Wanapenda Pesa Hakuna Mapenzi - Video

$
0
0
Msanii wa muziki wa bongo fleva Giggy Money amefunguka na kusema kuwa hakuna mwanamke anapenda mwanaume bali wanawake wanapenda pesa tu hivyo amedai yeye sasa hajali kumfurahisha mwanaume kwa umbo lake ila anachoangalia yeye anapiga pesa.

Mbali na hilo Giggy Money anadai kuwa ndoto zake za kuja kutoka kimapenzi na msanii Wizkid kutoka Nigeria bado ziko pale pale na kusema siku zikitimia atawathibitishia watu kuwa jambo hilo limetimia.

Mtazame hapa Giggy hapa akifunguka mengi zaidi

Shilole Akana Kukwapua Mume wa Mtu.....

$
0
0
Msanii wa mziki Bongo, Shilole amekatana kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na mume wa mtu.

Hayo yamebuika mara baada ya muimbaji huyo kutangaza kuolewa ndani ya mwaka huu na mipango yote ya ndoa kukamilika kama kutolewa mahari.

“Siyo kweli sijanyangamya mume wa mtu, huyo bwana alikuwa naye lakini waliachana, before hata yangu, kwa hiyo haya mambo yanatokea kwa sisi haswa watu wa mashughuli mjini, huyo dada kusikia nipo na huyu kaka leo itakuwa inamchoma, hapo ndipo panaanzia utata,” Shilole amekiambia kipindi cha Mitikisiko ya Pwani cha Times Fm.

Hata hivyo amesema kuwa suala hilo halimuumizi kwa sababu ukweli anaujua, huku akiongeza mume wake mtarajiwa amekubali kazi yake anayofanya (muziki).

“Ndiyo amekubali kwa sababu amenikuta kwenye muziki na ndio kazi yangu na ameanza kunijua kupitia muziki wangu, kwa hiyo lazima anisapoti na anapenda kazi yangu,” amesisitiza.

VIDEO:Mfanyie Mkeo Style Hizi Hatokusahau Milele

$
0
0
Mfanyie Mkeo Style Hizi hatokusahau milele, Tazama Hii Video Hapa Chini Ujionee Mwenyewe

Mke wa Roma Alivyoongelea Usaliti wa Roma Wakati Akitambulisha Wimbo wa Zimbabwe Clouds FM...Afunguka Kwa Mara ya Kwanza

$
0
0
Mke wa Roma Alivyoongelea Usaliti wa Roma Wakati Akitambulisha Wimbo wa Zimbabwe Clouds FM...Afunguka Kwa Mara ya Kwanza, Tazama Hapa Chini Video Akifunguka yote:

Magufuli AVURUGA MCHORO wa Lowassa na Chadema!

$
0
0
Katika kampeni za kugombea urais nchini Kenya.LOWASSA na CHADEMA
walitaka kutumia tetesi zilizokuwepo kuwa Magufuli anamuunga mkono Raila Odinga.

Hivyo nao katika kulipiza uchungu wa kushindwa uchaguzi wakasema WATAAMUUNGA mkono Uhuru Kenyatta ili Magufuli asikie naye uchungu.

Lakini cha kushangaza ni kuwa Rais Magufuli AMETUMA haraka salamu za PONGEZI kwa rais Kenyatta kwa KUCHAGULIWA tena kwa MUHULA wa pili wa utawala wake. Mara tu zilipotangazwa.

Na hivyo KUSAMARATISHA KABISA mbinu za KUNGONISHA kati ya Serikali ya Tanzania na Kenya. Huku akiwaacha Chadema na Lowassa WAKISHANGAA wasijue nini cha kufanya.

Ikikumbukwa Lowassa alitoa waziwazi kauli yake na chama chake kuwa kinamuunga mkono Kenyatta(.....) NIA kubwa ilikuwa ni kwamba Rais Magufuli aonekane kuwa HAMPENDI Uhuru Kenyatta. Na pia aonekane kama ni Kiongozi asiyejua mambo ya
Utawala,
Prokali na
Diplomasia.

Lakini kwa HEKIMA na USHAURI aliopata akaamua kumpongeza Uhuru kenyatta HARAKA sana na kuwaacha CHADEMA na Lowassa wakishangaa tu wasijue nini cha kufanya.

Maana walikuwa wakifikiri Rais Magufuli ANGEJIKOKOTA kwa muda mrefu KUMPONGEZA Kenyatta katika ushindi wake.

Rais Magufuli aliangalia picha kubwa kati ya URAFIKI na MASLAHI ya NCHI. Na akachagua MASLAHI ya nchi/National Interests badala ya URAFIKI.
kwa Hilo tunampongeza sana.

ITABIDI basi Lowassa and Co. KURUDI kwenye drawing table/ Meza ya KUCHOREA maana MCHORO wao Magufuli AMEUVURUGA na sasa ni HISTORIA.
Hongera Magufuli kwa Hehima hiyo.

Je, Wajua Majina ya Pombe na Magufuli yalipotoka?

$
0
0
Majina mawili ya Dk. John Pombe Joseph Magufuli yana historia yake ya jinsi yalivyopatikana.

Majina hayo mawili ‘Pombe’ na ‘Magufuli’ yalitokana na bibi na babu wazaa baba yake Magufuli.

Jina la ‘Pombe’ alipewa na bibi yake kwani wakati anazaliwa bibi yake alikuwa amepika pombe siku
hiyo.

Jina la ‘Magufuli’ lilitokana na babu yake ambaye alikuwa shujaa wa kucheza ngoma za asili aliyepewa jina Magufuli kwani kila alipokuwa akicheza ngoma alikuwa anawashinda wengine hivyo kitendo hicho kilifananishwa na kufuli linavyofungwa mlangoni.

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE..

Mbowe Afunguka Mazito Sakata la Madiwani wa CHADEMA Kuhamia CCM

$
0
0
Mwenyekiti wa (CHADEMA) na Mbunge wa Hai Freeman Mbowe amefunguka na kusema ni upambavu mkubwa kutumia zaidi ya milioni mia saba kwa ajili ya kufanya marudio ya uchaguzi wa udiwani wa kata tatu baada ya madiwani wa CHADEMA kudaiwa kununuliwa na CCM.

Mbowe amesema hayo juzi alipokuwa akiongea na wakazi wa Machame Uroki akiwa kwenye ziara yake jimboni Hai na kusema fedha ambazo zinakwenda kwa ajili ya uchaguzi wa marudio zingeweza kufanya mambo mengine ya msingi.

"Gharama ya kurudia uchaguzi wa diwani mmoja ni shilingi milioni mia mbili hamsini, madiwani watatu waliopewa fedha wakaikimbia CHADEMA wakawaacha wananchi huo ni usaliti gharama ya kurudia uchaguzi kwenye kata tatu ni milioni mia saba na hamsini. 

"Hizi ni pesa zenu, hizi ni pesa za Watanzania pesa hizi zingetumia kujenga shule ya msingi kwa Kasagile, hizi ni pesa zingetumika kujenga barabara, tunaacha kujenga hospitali tunakwenda kuzitumia fedha hizi kwenye uchaguzi milioni mia saba na hamsini ni upumbavu mkubwa" alisema Mbowe

Hata hivyo Mbowe amesema kuwa licha ya madiwani hao kununuliwa hata uchaguzi ukifanyika kesho anaamini kuwa chama chake kitaibuka na ushindi kwa kata zote tatu

"Niwaambie tu CCM haki ya Mungu hizo Kata tatu haiondoki hata moja labda watu wa Uroki mniambie mko tayari tuwaachie hizo Kata, tutakesha usiku tutakesha mchana haipotei Kata hata moja waite uchaguzi hata kesho, kuna watu wanafika bei tuachane nao tuna mambo ya kupigana katika maisha yetu" alisisitiza Mbowe

Madiwani wa tatu wa jimbo la Hai walijiuzulu nafasi zao na kusema wanamuunga mkono Rais Magufuli na serikali ya awamu ya tano kutokana na utendaji wake madiwani hao ni pamoja na Diwani wa Kata ya Machame Magharibi, Goodluck Kimaro, Diwani wa Kata ya Weruweru, na  Diwani wa Kata ya Mnadani, Everist Peter Kimati ambao wote wamejiunga na CCM.


Huto Amini Hii Ndio Idadi Kamili ya Watu Waliouawa Kutokana na Vurugu za Uchaguzi Kenya....

$
0
0

Tume ya Haki za Binadamu nchini Kenya (KNCHR) imesema kuwa watu 24 wameuawa tangu kuanza kwa kipindi cha uchaguzi tangu Agosti 8.

Katika taarifa iliyotolewa na tume hiyo imeeleza kuwa watu 17 wameuawa katika mji wa Nairobi City, Homabay wameuawa 2, Kisumu ameuawa 1, Migori 2 na Siaya wameuawa watu 2.

Wakielezea chanzo cha mauaji hayo, tume hiyo ilisema wengi wameuawa kwa kufyatuliwa risasi wakati wakiandamana katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Taarifa hiyo imekuja wakati chama cha upinzani kimesema kuwa zaidi ya watu 100 wameuawa lakini hawakutoa uthibitisho wowote wa madai hayo.

Serikali Yanyakua Ardhi Nyingine ya Aliyewahi Kuwa Waziri Mkuu, Frederick Sumaye

$
0
0
kwenye kampeni kwamba waliohodhi mashamba makubwa na kushindwa kuyaendeleza ,Rais Magufuli amefuta hati ya Shamba jingine la Waziri Mkuu mstaafu Sumaye.


Ikumbukwe pia kuwa utaratibu huu wa kuhodhi hadhi bila kuziendeleza imekuwa ni mojawapo ya chanzo cha migogoro ya ardhi nchini ikiwa ni pamoja na mauaji au mapigano kati ya wakulima na wafugaji.

Uchafu Vyoo Taasisi za Serilikali Wamkera Waziri wa Afya

$
0
0
Uchafu Vyoo Taasisi za Serilikali Wamkera Waziri wa Afya
Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii, Ummy Mwalimu ameonyesha kukerwa na uchafu wa vyoo katika ofisi na taasisi za Serikali na kutaka suala hilo liangaliwe kwa umakini ili kuepusha mlipuko wa maradhi yatokanayo na uchafu.

Mwalimu aliyasema hayo jana wakati akitangaza washindi wa shindalo la kitaifa la usafi wa mazingira ambalo lilihusisha vipengele kadhaa kikiwemo cha matumizi ya vyoo bora.

Alisema licha ya kuwa watendaji wa Serikali ndiyo wanapaswa kuwa wahamasishaji wa usafi kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakitumia vyoo vichafu.

Kutokana na hali hiyo Mwalimu alisema ipo haja ya kuanza kushindanisha taasisi na ofisi za Serikali katika usafi wa mazingira hasa wa vyoo.

Pia, Mwalimu aliagiza shule za msingi na sekondari nazo zishindanishwe kupata choo bora na safi.

“Kuna ofisi za umma ukienda chooni unaweza kutamani ukajisaidie barabarani kutokana na uchafu, tatizo kubwa ninaloliona Watanzania hatuzingatii mazingira na usafi wa vyoo,” alisema.

Katika shindano hilo kwa mara nyingine tena Halmashauri ya Mji wa Njombe iliibuka kidedea kati ya halmashari 73 za wilaya, miji, manispaa na majiji.

Ushindi huo ulipatikana baada ya kufanikiwa katika udhibiti wa taka ngumu, usimamizi wa sheria, udhibiti wa majitaka, uwepo wa majisafi na salama pamoja na ushirikishwaji wa sekta binafi katika usafi wa mazingira.

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ilishika nafasi ya pili katika kipengele cha utekelezaji wa kampeni ya Taifa ya usafi wa mazingira katika ujenzi na matumizi ya vyoo bora.

Njombe pia iliibuka mshindi katika kipengele cha kijiji bora chenye kaya ambazo zimefanikiwa kujenga na kutumia vyoo bora pamoja na sehemu za kunawia mikono kwa maji na sabuni nafasi iliyoshikwa na Kijiji cha Kanikele.


Rais wa FIFA Atoa Pongezi kwa Wallace Karia Muda Mchache Baada ya Kuchaguliwa Kuwa Rais Mpya wa TFF

$
0
0





Rais wa FIFA Atoa Pongezi kwa Wallace Karia Muda Mchache Baada ya Kuchaguliwa Kuwa Rais  Mpya wa TFF
Muda mfupi baada ya Kamati ya Uchauzi Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania kumtangaza, Wallace Karia kuwa ndiye rais mpya wa TFF,  rais Shirikisho la soka duniani( FIFA),  Gianni Infantino ametuma salamu zake za pongezi.



Hayo yameelezwa na rais wa TFF, Wallace Karia wakati alipopewa nafasi ya kuzungumza kwa mara ya kwanza mara baada ya kukalia kiti hicho kilikuwa kimeachwa wazi na Jamal Malinzi.

“Kwanza nipende kumshukuru Mwenyezi mungu kwa kufanikisha yote na washukuru wajumbe wa Mkutano Mkuu kwa imani mliyo hionyesha kwangu nideni kubwa sana nawaahidi sitawaangusha”, amesema Karia rais wa TFF.

Wallace Karia ameongeza kuwa “Muheshimiwa Waziri na wasaidizi wako nawashukuru kwa kutusaidia katika kipindi hiki kigumu tulichopitia, kutoka FIFA na Caf tunawashukuru kwa uwakilishi wenu na mmesimama na kuangalia zoezi letu hadi kufikia hapa nadhani mtakuwa ni mabalozi wazuri kwa utaratibu ambao tumeufanya na demokrasia ambayo imefanyika hapa kuwa na kupeleka salamu hizi”.

“Lakini pia nipende kuwaambia wajumbe wa Mkutano Mkuu muda mfupi nimeongea na rais wa FIFA,  Infantino na ametupongeza kwa maamuzi haya amesema yupo tayari na atashirikiana na sisi kwa maswala yote ya maendeleo katika kuhakikisha tunaendeleza soka letu”.

“Wakati huo huo rais wa Caf, Ahmad Ahmad amepiga simu naye yeye ameeleza hayo hayo na amefurahi sana anamategemeo makubwa katika kuendeleza soka letu sina mengi ya kuongea zaidi ya kuwashukuru lakini nipende kuwaambia tu hii furaha iyende kuwa furaha ya kazi”

Walichozungumza Rais Mpya wa TFF na Makamu Wake Baada ya Kushinda

$
0
0
Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya shirikisho la soka Tanzania TFF Revocatus Kuuli amemtangaza Wallace Karia kuwa Rais mpya wa TFF na amemtangaza Michael Richard Wambura kuwa makamu wa Rais wa TFF.

VIDEO:

Source:Millard
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images