Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Maskini..Utajiri wa Bilione Dangote Waporomoka zaidi ya Nusu...

$
0
0
Aliko Dangote ana utajiri wa dola za Marekani bilioni 12.2 (trilioni 27), ambaye utajiri wake ni takriban asilimia 3 ya pato la Taifa la Naijeria, unamfanya awe mtu tajiri zaidi barani Afrika kwa urahisi — na ndio bilionea mweusi aliye juu zaidi kwenye orodha ya watu matajiri duniani.

Hii ni taarifa nzuri, lakini hii ni nusu tu ya utajiri aliokuwa nao Dangote mwaka 2014 ambapo hadi mwaka huo ulipoisha, Dangote alikuwa na utajiri wa dola za Marekani bilioni 25 (trilioni 56).

Sehemu kubwa ya utajiri wake (asilimia 90) inatoka kwenye viwanda vyake vya kutengeneza saruji (Dangote Cement), kampuni iliyoorodheshwa kwenye Soko la Hisa nchini Naijeria yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 11, sawa na trilioni 24.

Biashara za bilionea Dangote zimesambaa kwenye nchi kadhaa barani Afrika. Anamiliki viwanda vya kutengeneza saruji nchini Zambia, Senegal, Tanzania, na Afrika Kusini.

Dangote, ambaye amekuwa Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa kundi la kampuni za Dangote kwa zaidi ya miaka 35 sasa pia ni mtu anayetoa misaada ya kibinadamu. Akiwa ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Misaadaya ya Dangote, anasimamia misaada katika elimu, kilimo na afya ikiwamo msaada wa dola za Marekani 12,000 (takriban shilingi nilioni 27) kwa siku kwa watu wanaokosa huduma muhimu.

“Aliko ni tajiri namba moja barani Afrika, na biashara zake zinachangia kukuza uchumi wa bara zima. Hilo ni jambo zuri, lakini namtambua zaidi kama kiongozi ambaye yupo mstari wa mbele kupunguza tofauti kati ya biashara za watu binafsi na sekta ya afya ya jamii nzima,” aliandika bilionea namba moja duniani, Bill Gates. Bilionea huyo kwenye sekta ya teknolojia almemsifu Dangote kwa mafanikio makubwa aliyochangia kuitoa Naijeria kutoka kwenye orodha ya dunia ya nchi zenye magonjwa ya milipuko kwa juhudi zake za kupambana kutokomeza ugonjwa wa polio.

Mwezi Januari 2016, Dangote na Bill Gates walitoa ahadi ya kutoa dola milioni 100 ili kutokomeza utapiamlo nchini Naijeria, nchi yenye idadi kubwa zaidi ya watu barani Afrika.

Kimenuka...Aliyeisaliti CCM Kwenye Uchaguzi Kujadiliwa na Kamati ya Maadili

$
0
0

Kamati ya Maadili ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Musoma Mjini inatarajiwa kukutana na kujadili hatua ya Diwani wa Kata ya Sunguti, Denis Ekwabi kukisaliti chama hicho na kumpigia kura mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakati wa uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti uliofanyika katika Halmashauri ya Musoma Vijijini.

“Sisi baada ya uchaguzi kuisha tuliitana wanachama wote wa CCM ili kutaka kujua nani aliyetusaliti wakati kwenye vikao vyetu vya ndani ya chama tulikuwa tumeshampitisha mgombea wetu atakayegombea nafasi hiyo na tukakubaliana, lakini tulipokutana tu Diwani wa Kata ya Sunguti, Denis Ekwabi alikiri mwenyewe kuwa ndiye aliyepigia kura CHADEMA,” alieleza Bernard Ghati, Katibu wa CCM Wilaya ya Musoma Mjini

Katibu huyo alilaani kitendo cha Diwani huyo kukisaliti chama na kupigia kura chama kingine, akieleza kuwa ni utovu wa nidhamu na kutozingatia kanuni za chama hicho, hivyo watakapokutana na Kamati ya Maadili watatoa tamko juu ya tukio hilo.

Ghati alisema kuwa idadi ya Madiwani wa Halmashauri hiyo ni 26 na Madiwani wa CCM wapo 22 na wa CHADEMA wanne, lakini kura zilipopigwa zilionesha kuwa mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti kupitia CHADEMA alipata kura tano na wa CCM alipata kura 21, kitendo kilichowafanya wanaCCM kubaini kuwa kuna mmoja wao aliyewasaliti.

Mugabe Aishangaza Dunia...Atangaza Msamaha Kwa Raia wa Zimbabwe Waliowaua Wazungu

$
0
0

Mugabe Aishangaza Dunia...Atangaza Msamaha Kwa Raia wa Zimbabwe Waliowaua Wazungu
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ametangaza kuwa raia wote wa nchi hiyo waliokuwa wakituhumiwa kuwaua wazungu waliokuwa wakifanya biashara katika mashamba tangu kuanza kwa programu ya mabadiliko ya ardhi mwaka 2000, hawatoshtakiwa.

Akizungumza mbele ya umati wa watu katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa, Mugabe alisema wazungu hao waliuawa kwa sababu walipinga agizo lililokuwa limewekwa na serikali.

“Kuna waliouawa wakati walipoleta ubishi. Hatutokaa tuwashtaki wale wote walioawaua. Nauliza; Kwanini tuwakamate?” aliuliza Rais Mugabe wakati akihutubia wananchi.

Takribani wazungu 12 waliokuwa wakijihusisha na kilimo katika mashamba ya biashara waliuawa na wanaodaiwa kwamba ni wanaharakati wa Chama cha ZANU-PF na wapiganaji vita wastaafu wakati wakugombea mashamba, tukio lililotupiwa lawama na mataifa mbalimbali.

Tukio hilo lilisababisha pia mataifa ya magharibi kumuwekea vizuizi Rais Mugabe asiweze kusafiri kwenda katika nchi hizo wakimtuhumiwa kwa ukiukwaji wa haki za binadamu pamoja na umiliki mali.

Mugabe amewaambia wajumbe wa mkutano wa mwaka wa ZANU-PF kwamba, hakuna uamuzi wa mahakama utakaobatilisha namna walivyoamua kupata ardhi yao. Alisema kuwa, hata hivyo, ardhi ni yao kwa haki ya kuzaliwa, kama raia ni haki yao, na ni yao kwa kuipigania.

Rais Mugabe amewataka raia wa taifa hilo ambao wamepata ardhi kutokodisha kwa wakulima wakizungu.

“Wakati mwingine wakulima wa kizungu wanarudi kuja kukusanya matrekta yao au kutaka kushirikiana na wakulima wapya. Wakulima wapya wanalaghaiwa bila ya wao kujua.”

Mugabe alisema kwamba taifa hilo halikuwahi kutaka kuwafukuza raia wa kigeni (wazungu) nchini humo na kwamba walioondoka walifanya hivyo kwa maamuzi yao wenyewe.

Alieleza kwamba, takribani watu 100,000 ambao ni wazungu wapo nchini humo kati ya 250,000 waliokuwepo wakati nchi hiyo inapata uhuru.

Picha: Mwanajeshi Amvua Nguo Msichana Hadharani Baada ya Kumkuta Amevaa Nguo za Jeshi

$
0
0
Picha inasambaa mitandaoni ikionyesha msichana akivuliwa nguo baada ya msichana huyo kuvaa nguo zinazofanania na sare za jeshi, Haijajulikana ni nchi gani au jeshi gani tukio hili lilipotekea


Toa Maoni yako

Nani Atafaa Kuogombea Urais kwa Chadema 2020?

$
0
0

Kwanza niseme binafsi simwitaji EL kuwa mpeperusha bendera ya CHADEMA 2020, ila kama anataka astaafishwe siasa kwa lazima agombee tu.

Ila kwa ujumla naangalia tunavyojipanga na tunavyoenenda ndani ya chama chetu cha CHADEMA, hivi ni nani anaweza kupeperusha bendera yetu 2020?

Ukiangalia kwa macho ya nyama hupati hata mmoja labda itokee kama 2015. Kama Dr. Slaa ambaye tuliamini alikuwa na nguvu ya kuitoa CCM bila jasho kabisa, kwa sasa nani anafikia hata nusu ya Dr. Slaa pale kwetu?

Ni mawazo tu haya.

Hebu tuchangie kwa utulivu.

By Ufipa-Kinondoni

Imefichuka... Ruby Afunguka Kutoka Kimepenzi na Soudy wa 'Shilawadu' -Audio

$
0
0

Hatimaye Ruby Atoa ya Moyoni Afunguka Uhusiano Wake na Soudy wa 'Shilawadu'
Msanii wa muziki Ruby amefunguka kwa kudai kuwa alitoka kimapenzi na mtangazaji wa kipindi cha Shilawadu cha Clouds FM, Soudy Brown kwa miaka miwili lakini baadaye alikuja kuachana naye baada ya kuona hana msimamo.


Ruby amedai Soudy Brown ndiye mwanaume pekee aliyetoka naye kimapenzi kutoka kwenye industry ya muziki.

“Nikisema nitoke na mastaa wenzangu sio kwamba hawanisumbui wananisumbua sana lakini nawajua tayari the way walivyo,” Ruby aliuambia mtandao wa Spin Tanzania. “Lakini vitu vingi ambavyo naona wanafanyiwa wasanii wenzangu na mimi kweli nikawe na msanii? Hapana siwasemi kwa sifa mbaya wasanii lakini mimi siwezi kuisha nao kutokana na tabia zao kwa sababu mimi ni mwepesi sana kuumia,”

Aliongeza,”Mimi mwanaume ambaye nimetoka naye kwenye mapenzi na yupo kwenye industry yetu only ni Soudy Brown, na nimeishi naye kwa mwaka mmoja na miezi sita,”

Pia muimbaji huyo wa ‘Na Yule’ alikanusha tetesi kwamba alibeba mimba na kuitoa ya mtangazaji huyo ambaye anaendesha kipindi cha Shilawadu cha Clouds FM. VIDEO:

Mamia Wazikwa Sierra Leone Kutokana na Mafuriko.....

$
0
0
Mamia Wazikwa Sierra Leone
Wiizara ya afya nchini Sierra Leone imesema takriban nusu ya maiti 400 zitokanazo na maporomoko ya udongo na mafuriko nje ya mji wa Freetown tayari zimezikwa.
Serikali ilisema mazishi ya pamoja yangeahirishwa hadi leo ili kutoa fursa kwa ndugu na jamaa kutambua miili ya maiti ya waathirika.

Lakini mkuu wa wataalamu wa magonjwa kutoka mjini Freetown ameiambia BBC kwamba baadhi ya mazishi yalikuwa yamefanyika.
Imefahamika kuwa mazishi hayo yamehusisha miili ambayo tayari ilitambuliwa au ilikuwa imeharibika kabisa.

Nathaniel Williams ni daktari katika hospitali kuu ya Connaught, iliyopo Freetown, anasema hivi sasa kuna tahadhari kubwa ya kutokea magonjwa ya milipuko kama vile kipindupindu.
Ameongeza kusema kuwa hivi sasa kunahitajika madawa na vyakula, kwa wale walioathirika.
Hata hivyo, Umoja wa Mataifa nchini humo umesema tayari umeweka mikakati ya kuweza kukabiliana na magonjwa ya milipuko iwapo yatatokea.

Mke wa Roma Awapa Makavu Wale Wanaosema Safari ya Zimbambwe ya Mke wa Mume ni Kiki

$
0
0


Mke wa Roma Awapa Makavu Wale Wanaosema Safari ya Zimbambwe ya Mke wa Mume ni Kiki
Mke wa rapa Roma Mkatoliki, bibie Nancy Mshana amedai watu wanaodhani mume wake katumia kiki ya kwenda Zimbabwe ili wimbo wake mpya uwe gumzo wapo sahihi na hafikirii kumlaumu mtu yeyote kwani ni uhuru wa kujieleza

 Nancy amesema kuwa hafahamu kama mumewe anaweza  kumtumia  kama kupata kiki na iwapo kama ni kweli  mume wake kafanya hivyo  basi kafanikiwa kwa kiasi kikubwa  atakuwa ametisha
"Watu kama wanadai hii ni kiki ni idea nzuri sana kwani katumia njia sahihi. Pia mimi naona ni jambo zuri kama amenichagua mimi na ameona hii ndiyo njia sahihi ya ya kukuza muziki wake mimi ninamsapoti kwani siku zote nimekuwa nikimsapoti katika kazi zake ambazo zinatufanya chakula kifike mezani.

Akizungumzia maisha ya umaarufu Nancy anasema bado hajaona kama yana ugumu kwani yeye hajawa mtu wa kujichanganya sana katika makundi ya watu, kitu ambacho anamuomba Mungu kisije kikabadilika na kumbadilishia mfumo mzima wa maisha yakle.
Hata hivyo mwana mama huyo alikataa kuweka wazi ni kitu gani kilichompeleka Zimbabwe mume wake

"Safari yake ilikuwa ya ghafla sana na hajakwenda kufanya show. Lakini mimi sipendi kuweka wazi kwani nitaharibu 'suprise' iliyoandaliwa lakini yeye akirudi atawaambia kila kitu, sitaki kuharibu suprise mapema.

Pamoja na hayo Msanii Roma amewashawasili nchini usiku wa kuamkia jana kutoka Zimbabwe ili kuanza 'Media tour' ya wimbo wake mpya 'Zimbabwe' uliokuwa gumzo kila kona ya mji kutokana na mashairi yake.

Mapacha Walioungana Wafariki Dunia

$
0
0

Mapacha Walioungana  Wafariki Dunia
Mapacha walioungana kuanzia kifuani hadi tumboni wamefariki dunia jana katika hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam walipokuwa wakipatiwa matibabu baada ya kuzaliwa katika hospitali ya Berege wilayani Kilosa mkoani Morogoro.

Afisa uhusiano wa hospitali ya Taifa Muhimbili, Neema Mwangomo amethibitisha kufariki kwa watoto hao ambao walikuwa wakisubiri kufanyiwa upasuaji, huku akisema kuwa uchunguzi unafanyika kubaini chanzo cha kifo cha watoto hao.

Watoto hao waliozaliwa wakiwa na uzito wa kilo nne walipewa rufaa ya kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kupatiwa uangalizi zaidi na waliwasili katika hospitali hiyo Juni 24 na kuwekwa katika chumba cha uangalizi maalum.

Daktari bingwa wa upasuaji wa watoto, Dkt. Zaituni Buhari Agosti 2 mwaka huu alieleza wanahabari kuwa  watoto hao walikuwa wanachangia ini na sehemu ndogo ya moyo lakini wangeweza kufanyiwa upasuaji.

Hata hivyo baadhi ya mapacha wa aina hiyo ambao hawajawahi kufanyiwa upasuaji na kufanikiwa kuishi na kuwa watu wazima ni pamoja wale wanaoishi wilayani Kilolo mkoani Iringa na wamehitimu kidato cha sita mwaka huu na kupata ufaulu mzuri wa kuendelea na elimu ya juu..


Watu DR Congo 40 Wametekwa na Waasi wa LRA

$
0
0
Watu DR Congo 40 Wametekwa na Waasi wa LRA
Waasi wa kundi la LRA wamewateka takriban watu 10 na hadi 40 kutoka kijiji cha Kunu katika jimbo la kaskazini mashariki mwa DR Congo kulingana na kitengo cha habari cha AFP .
Kitengo hicho kilimnukuu afisa Dungu Christophe Ikando akisema walijitambulisha kuwa wale wa LRA.

''Tunashutumu utekaji wa watu 10 kutoka kijiji cha Kunu na watu waliojihami kwa bunduki ambao walijitambulisha kuwa waasi wa LRA''
Idhaa ya redio ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa takriban watu 40 walitekwa ikiwemo maafisa wawili wa tume ya uchaguzi nchini humo.

Ettiene Akangiambe ambaye ni afisa mkuu wa tume hiyo ya CENI alitibitisha habari hizo.
''Maajenti wetu wawili ambao walikuwa wakirudi kutoka katika kituo cha kusajili wapiga kura walivamiwa na watu hao waliojihami''.

Waasi wa LRA wanekuwa wakifanya operesheni zao nchini Uganda, DR Congo na Jamhuri ya Afrika ya kati CAR na Sudan kwa miongo kadhaa lakini uwepo wao umepungua kufuatia operesheni za kieneo na zila za majeshi ya kimataifa.
Umoja wa mataifa unakadiria kwamba LRA limewaua takriban watu 100,000 na kuwateka watoto 60,000 tangu lianzishwe na Joseph Kony 1987.

Mnamo mwezi Mei , wanajeshi wa Uganda na wenzao wa Marekani walitangaza kwamba wanasitisha operesheni yao ya kumsaka Kony ambaye alipatikana na hatia ya uhalifu wa kivita 2005 na uhalifu dhidi ya binaadamu na mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC mjini The Hague.

Wasiwasi wa kisiasa umekuwa ukiongezeka DR Congo huku shinikizo za kumtaka rais Kabila kuandaa uchaguzi mkuu zikiendelea.
Muda wake wa kutawala ulikamilika mwezi Disemba mwaka uliopita na makubaliano ya kuandaa uchaguzi mwengine mwishoni mwa 2017 yaliafikiwa.

Madee Yamemfika Hapa Aamua Kumuangukia Wolper

$
0
0

Madee Yamemfika Hapa Aamua Kumuangukia Wolper
Rais wa Manzese, Madee amefunguka kwa kumuomba radhi msanii wa bongo movie Jacqueline Wolper kwa kitendo cha kumfanya katuni mrembo huyo katika video yake mpya ya wimbo 'Sikila' bila ya ridhaa yake mwenyewe.

Madee ameomba msamaha huo mbele ya kamera za eNewz kutokea EATV baada ya Wolper kudai anateenda kumshtaki kwa kitendo cha kumtumia katika kazi zake bila ya kuwa na makubaliano baina yao kwa kuwa ni kinyume na taratibu zake.

"Niliamua kumtumia Jacqueline Wolper baada ya 'director' kuniambia nitafugte picha ya msanii yeyote maarufu ndipo nikaamua kumpatia picha ya ya Wolper na kabla ya kumtumia nilimpigia simu, nikampa taarifa ili aelewe kinachoendelea", alisema Madee.
Pamoja na hayo, Madee amedai haamini kama ni kweli mrembo huyo anataka kumfungulia kesi juu ya jambo hilo.

Real Madrid Watwaa Ubingwa wa Super Cup kwa Kuichakaza Barcelona 2-1

$
0
0




Real Madrid  Watwaa Ubingwa wa Super Cup kwa Kuichakaza Barcelona 2-1
Klabu ya Real Madrid imetwaa ubingwa wa Super Cup wa nchini Hispania baada ya kuwagaragaza mahasimu wao, Barcelona kwa goli 2-0 kwenye mchezo wa mkondo wa pili uliopigwa kwenye dimba la Santiago Bernabeu usiku wa kuamkia leo.




Real Madrid bila ya Cristiano Ronaldo aliyefungiwa mechi tano kwa kosa la kumsukuma mwamuzi kwenye mchezo wa awali, walianza kupata bao la kwanza lililowekwa kimiani na kinda wa mabingwa hao wa Ulaya, Marco Asensio kunako dakika ya 4 kabla ya Karim Benzema kutupia goli la pili la ushindi kunako dakika ya 39 kipindi cha kwanza na mpaka filimbi ya mwisho, Madrid 2 Barcelona 0.

Kwenye mchezo wa raundi ya kwanza, Real Madrid waliibuka na ushindi wa mabao 3-1 ugenini kwenye dimba la Camp Nou mwishoni mwa wiki kwa goli la kujifunga la Gerald Pique, Cristiano Ronaldo na Marco Asensio huku bao la kufutia machozi kwa upande wa Barcelona likifungwa na Lionel Messi kwa mkwaju wa penati.

Real Madrid wametwaa ubingwa huo kwa jumla ya goli 5-1 dhidi ya Barcelona na kumfanya kocha Zinedine Zidane kuongeza idadi ya vikombe na kuweka rekodi ya kuwa kocha mwenye mataji mengi (7) kwa muda mfupi klabuni hapo .

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo Alhamisi

Huu ni Uamuzi wa Mahakama kwa Chidy Benzi Baada ya Kukamatwa na Madawa ya Kulevya

$
0
0




Huu ni Uamuzi wa Mahakama kwa Chidy Benzi Baada ya Kukamatwa na Madawa ya Kulevya
Mahakama ya Wilaya ya Ilala imewaweka chini ya uangalizi kwa kipindi cha miaka miwili Msanii wa Bongofleva Rashid Abdalah maarufu Chidbenzi na wenzake watano baada ya upande wa mashtaka kuwasilisha hati ya kiapo dhidi ya maombi hayo.


Aidha, upande wa mashtaka uliwasilisha kiapo hicho kwamba mahakama iwaweke chini ya uangalizi baada ya kubainikia kujihusha na matumizi ya dawa za kulevya.

Maombi hayo yalisikilizwa na kutolewa uamuzi jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi,Mfawidhi Ritha Tarimo. Mbali na Chidi Benz, wengine watakaokuwa chini ya ungalizi ni, Hadia Abeid, Said Ally, Athuman Elias na Hassan Mohamed.

Wakili wa Serikali Glory Mwenda, alidai kuwa upande wa Jamhuri unawasilisha hati ya kiapo kutoka kituo cha polisi Msimbazi kwamba watuhumiwa hao wamekuwa wakijihusisha na matumizi ya dawa za kulevya hivyo mahakama itoe dhamana kwani wamekuwa na tabia mbaya katika jamii.

Glory alidai kuwa wanaiomba mahakama itoe amri ya kuwaweka wajibu maombi chini ya uangalizi wa polisi na mahakama kwa kipindi kisichozidi miaka mitatu na kusaidi dhamana ambayo itahakikisha wanakuwa na tabia njema na kutojihusisha vitendo vya dawa za kulevya.

Akitoa uamuzi hakimu alisema wajibu maombi watakuwa chini ya uangalizi wa polisi miaka miwili na kudhaminiwa na wadhamini wawili watakaotia saini ya dhamana ya Sh.milioni mbili kila mmoja na kuripoti kituo cha polisi Msimbazi kwa mwezi mara moja.

Roma Mkatoliki: Sina Deni Ninalodaiwa na Mashabiki Zake

$
0
0


Roma Mkatoliki: Sina Deni Ninalodaiwa na Mashabiki Zake
Rapa Roma Mkatoliki amefunguka na kudai hana deni analodaiwa na mashabiki zake mpaka sasa ila anachojua yeye kuwa ndiyo alikuwa anawadai na ameshalipwa baada ya wao kupiga kelele za 'free Roma' kipindi alipotoweka.

Roma amebainisha hayo siku za hivi karibuni baada ya watu wengi kudai msanii huyo anadeni la kulilipa kwa wananchi kwa kuwa hajazungumza jambo lolote lililomsababisha yeye mpaka kutekwa na watu wasiyojulikana.

"Mimi ndiyo naweza kusema niliwakopesha washkaji deni maana ndani ya miaka 10 nimeimba nyimbo za kiharakati, changamoto pamoja kero za jamii vyote nawaimbia watu bila ya kulipwa chochote. Leo limenikuta la kunitokea wananchi basi wameungana kutokana na ngoma zangu wamepaza sauti zao, ukiniambia mimi nina deni ni kama wao wamenilipa kwa sababu mimi niliwakopesha kupitia ngoma zangu", alisema Roma.

Pamoja na hayo, Roma amesema hadhani kama chochote atakachokieleza kwa umma wataweza kuridhika kutokana na tukio lake jinsi lilivyokuwa.

"Sidhani kama kuna majibu sahihi ukamwambia mtu akaridhika kuhusiana uhalisia wa tukio lililonitokea mimi, sina cha kufanya zaidi kusema asante kwa kupaza sauti zenu mpaka kupatikana kwangu, maisha yaendelee, nipo poa, nipo strong, niombeeni tuendelee", alisisitiza Roma.
Video mpya ya Roma Mkatoliki 'Zimbabwe' aliyoiachia Agosti 10 mpaka sasa imeweza kuendelea kushikilia nafasi ya kwanza kuwa 'trending' za video katika mtandao wa Youtube.



Mwenyekiti wa Mtaa Mikononi Mwa Polisi kwa Kuhamasisha Vurugu

$
0
0

 Mwenyekiti wa Mtaa Mikononi Mwa Polisi kwa Kuhamasisha Vurugu
Wananchi wa mtaa wa Magadula kata ya Ngokolo manispaa ya Shinyanga wameifunga kwa mawe barabara inayoendelea kujengwa na kampuni ya ukandarasi  ya Jasco Investment, kwa madai ya kuchoshwa na vumbi.

Pia Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga Kadama Malunde na mwenyekiti wa mtaa huo Diana Ezekiel wakishikiliwa na jeshi la polisi.

Wananchi hao walifanya tukio hilo jana saa tano asubuhi katika eneo hilo huku wakiongozwa na mwenyekiti wa mtaa huo, wakidai kuchoshwa na  vumbi kali linatokana na mchanga na saruji baada ya magari kupita eneo hilo.

Wakati Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari akishikiliwa kwa muda wa saa mbili na kuachiwa kwa madai ya kupiga picha tukio hilo, mwenyekiti wa mtaa anashikiliwa kwa madai ya kuhamasisha wananchi kufunga barabara.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga Simon Haule alisema walikamatwa watu wawili akiwemo mwenyekiti wa mtaa huo na mwanamume mmoja akipiga picha.

“Huyo mwananume mwingine alipofikishwa kituoni akahojiwa alijitambulisha kama mwandishi wa habari hivyo akaachiwa bila masharti lakini mwenyekiti wa mtaa huyo bado tunamshikilia,” alisema Kamanda




Jini Mkatakamba Atua kwa Jenifer wa Kanumba Achafua Hali ya Hewa Mitandaoni

$
0
0




Jini Mkatakamba Atua kwa Jenifer wa Kanumba Achafua Hali ya Hewa Mitandaoni
MTOTO ‘mtukutu’ aliyejizolea umaarufu mkubwa kupitia filamu za marehemu Kanumba, Hanifa Daudi amekumbwa na kashfa ya kitapeli, kufuatia watu wasiojulikana kufungua akaunti feki ya jina lake kwenye Mtandao wa Facebook na Instagram na kuanza kuomba pesa kwa watu mbalimbali.

Kwa mujibu wa chanzo makini, baadhi ya watu wamekuwa wakimlalamikia  kwa tabia ya kuomba pesa kupitia mitandao ya kijamii, jambo ambalo liliwashangaza wengi. “Kuna watu wanatumia jina la Jennifer kwenye mitandao kutapeli hivyo wameondoa lawama kwa muigizaji huyo na badala yake wameanza kumkingia kifua, tofauti na zamani ambapo walidhani ni yeye kweli anayefanya utapeli huo, mwenyewe maskini amekuwa ni mtu wa kulia na kuumia kwa kashfa hiyo,” alisema mtoa habari wetu.

Mwandishi wetu alizungumza na Jennifer na kusema: “Naumia sana jamani, hebu nisaidieni, mimi sina akaunti kwenye Facebook, ni juzi tu mama yangu alinishauri nifungue akaunti ya Instagram ili kujitofautisha na hao matapeli, lakini sina simu na hiyo akaunti siitumii niko huku Tanga masomoni, wanatumia jina langu kutapeli, eti wanajiita Hanifa Jennifer Kanumba na wanaposti picha zangu, kweli sijui wanazitoa wapi, naumia jamani aah.”

Rugemalila, Singasinga Bado Hakijaeleweka Mahakamani

$
0
0


Rugemalila, Singasinga Bado Hakijaeleweka Mahakamani
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Alhamisi, Agosti 17, 2017 imeahirisha kesi inayowakabili mmiliki wa kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder  Singh Sethi maarufu kama ‘Singasinga’ na  mfanyabiashara James Rugemalira wanaokabiliwa na mashtaka 12, yakiwemo ya kutakatisha fedha na kuisababishia serikali hasara.

Kesi hiyo iliyokuwa isikilizwe na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambaye hakuwepo ilipangiwa Hakimu mwingine Cyprian Mkeha aliyeiahirisha hadi Agosti 31 mwaka huu, baada ya wakili wa serikali, kueleza kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika

Mke wa Mugabe Aombewa Kinga ya Kidemokrasia na Serikali ya Zimbabwe

$
0
0


 Mke wa Mugabe Aombewa Kinga ya  Kidemokrasia na Serikali ya Zimbabwe
Serikali ya Zimbabwe imemuombea mke wa Rais Mugabe kinga ya kidiplomasia dhidi ya kesi ya ushambuliaji inayomkabili nchini Afrika kusini.

Taarifa hizo zimetolewa na maofisa wa  polisi wa taifa hilo leo asubuhi zikidai hayo yamefanyika kwa mujibu wa sheria.

''Grace Mugabe alikuwa bado yupo Afrika Kusini'' iliongezea wakipinga ripoti za awali kwamba alikuwa amerudi nchini Zimbabwe.

Taarifa ya mtandao wa BBC Swahili,imesema  kuwa,mwanamitindo mwenye umri wa miaka 20 amemtuhumu  Grace Mugabe kwa kumshambulia katika hoteli moja mjini Johannesburg.

Polisi walitarajia kwamba  mke huyo wa  Mugabe angejisalimisha  kwao mwenyewe siku ya Jumanne lakini hakufanya hivyo.

Hata hivyo Afrika Kusini bado ilikuwa inataka kuhakikisha kuwa kinga hiyo amepatiwa kulingana na sheria, ilisema taarifa hiyo.

Mazungumzo yalikuwa yanaendelea na mawawikili wa Mugabe na ubalozi wa Zimbabwe kuhusu swala hilo, ilisema taarifa.

Akizungumza mbele ya kamati ya bunge mapema, Kaimu Mkuu wa Polisi Lesetja Mothiba alisema kuwa Grace  Mugabe anatakiwa  aende mahakamni.

Hatahivyo,hajatoa tamko lolote tangu maaoisa wa polisi waanze kumchunguza kuhusu madai hayo ya unyanyasaji.

Wakazi Ashangazwa na Majigambo ya Malaika

$
0
0




Wakazi Ashangazwa na Majigambo ya Malaika
Baada ya msanii Malaika kudai yeye ndiye msanii aliyefanya show nyingi zaidi Marekani kutoka Bongo, Rapper Wakazi amesema hilo halina ukweli wowote kwani yeye toka mwaka 2009 anafanya show katika nchi hiyo.



Wakazi ameeleza kuwa muimbaji huyo hawezi kuwa amemfikia kwani yeye amefanya show nyingi zisizo na idadi hadi Marekani ikafika kipindi akaweza kuendesha maisha yake kupitia show pekee.

“Hawezi kuwa amenifikia kufanya show kwa kule kwa sababu nakumbuka mimi mwaka 2009 ndio nilianza kutoa free style za kwanza kwanza, 2010 nikatoa mixtape ya kwanza nikaanza kuwa maarufu kule. Hizo show ambazo anazifanya mimi ndio nakawa booked na kila mwaka nikawa booked, nikawa sikai ikibidi niache kazi ili niwe nafanya show tu, kuna kipindi ilifikia hivyo, so hawezi kuwa amefikia level yangu,” ameiambia The Playlist ya Times Fm na kuongeza.

“Nadhani hata Diamond, Kiba sidhani hata wao amewafikia kwa sababu hata wao wamefanya show nyingi sana ila mimi nimefanya show nyingi sana akija Fid Q Marekani show yake nitakuwepo, akija Professor Jay nitakuwepo, Chameleon show yake nitakuwepo na Mr Nice,” amesema Wakazi.

Wakazi kwa sasa anafanya vizuri na ngoma zake mbili ‘Hapa Wakazi Tu, Bakora’ na ngoma aliyoshirikishwa na Grace Matata ‘Dakika Moja’.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images