Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live

WANACHAMA wa Simba Waamua Kuendesha Simba Kwa Mfumo wa Hisa...Hichi Ndio Walichoamua Leo

$
0
0
 Wanachama 1,216 wa klabu ya Simba, leo wamepitisha uamuzi wa klabu yao kuanza kuendeshwa kwa mfumo wa hisa.

Mwanachama mmoja pekee katika mkutano huo, ndiye alionyesha hisia zake kwa kupinga mfumo huo.

Wanachama bado wataendelea kubaki kuwa wamiliki wa klabu hiyo kwa asilimia 50 huku wawekezaji nao wakilimiliki kwa asilimia 50 pia.

Mbadiliko yaliyopitishwa na wanachama wa Simba yako hivi, wanachama watamiliki klabu yao kwa 50% huku 50% zikilikiwa na wawekezaji.

Wawekezaji au mmoja, wawili au watatu watatakiwa kutoa Sh bilioni 20 katika uwekezaji huo sawa na wanachama.

Kwa wanachama, kwa kuwa wanaonekana si wenye uwezo wa kutosha kifedha, wao watatakiwa kuchangia Sh bilioni 4 tu ambazo nia silimia 10 huku 40 ambayo ni bilioni 16 zitawekwa kando kwa kuangalia uwezo wao.

Suala la nani atakuwa mwekezaji itaundwa kamati baada ya watu kujitokeza, nayo itaandaa mkutano kuwaita wanachama kuwaeleza waliojitokeza katika uwekezaji ni akina nani.

Wawekezaji wanaweza kuwa wawili, watatu au vinginevyo na mgawanyo wa hisa kwa maana ya thamani na asilimia ndiyo utakaohusika.

SHILAWADU Watolewa Nduki na Mbwa Nyumbani kwa Alikiba.

$
0
0
Imebainika kuwa licha ya vijana hawa wa shilawadu kuwa na kipaji cha kunyapia umbea, wanakipaji kingine cha ziada cha kukimbia mbio fupi na hata zile ndefu kwa kasi kubwa zaidi hata kumshinda Usain Bolt.

Hayo yamebainika baada ya vijana hao kunyapia umbea nyumbani kwa Alikiba mda wa usiku na kukutana na bonge la mbwa jike aitwae rubi ambae hata hakuwabwekea lakini kutokana na uzoefu na kumbukumbu za hivi karibuni za kuingiliwa katika eneo lao la kazi na machine gun za kisasa waliamua kufunga turbo kwenye miguu yao na kukimbia mbio mithili ya mashindano ya olympic hali iliyopelekea kukosa umbea uliowapeleka kwa King Kiba, mzee wa Aje anayemiliki BMWX5 la kisasa kabisa...

Uhondo zaidi tazama video hii...

ODINGA Auawa, Mwili Wake Watupwa Sokoni inchini Kenya

$
0
0
JESHI la Polisi katika Kaunti ya Siaya linaendelea na upelelezi baada ya mwili wa mwalimu wa kike aliyetambulika kwa jina la Caroline Odinga ambaye alikuwa msimamizi msaidizi wa Tume ya Uchaguzi (IEBC) katika Uchaguzi Mkuu wa Kenya wa Agosti 8 mwaka huu.

Mwili wa mwalimu huyo wa Ugenya High School ulikutwa katika soko la Sega jana Jumamosi asubuhi na watu waliokuwa wakielekea katika mazishi ya Mkurugenzi wa TEHAMA wa IEBC, Chris Msando, Kijiji cha Lifunga.

Mkuu wa Polisi katika Kaunti ya Siaya, Sarah Duncan amesema uchunguzi unaendelea na upelelezi wa awali unaonyesha kuwa marehemu alibakwa na watu wengi na sehemu zake za siri pamoja na sikio moja kukatwa vibaya.

Familia yake inaeleza kuwa mara ya mwisho alitoka nyumbani siku ya Ijumaa na kwenda kudai malipo yake kwa kazi aliyofanya ya usimamizi wa Uchaguzi Mkuu uliomalizika.

Mcheza Filamu Johari Atoa Mpya...Adai yeye na Mwigizaji Ray Hawawezi Kuachana.....

$
0
0
Msanii nguli wa filamu ambaye amekuwa kimya kwa muda mrefu Bi. Blandina Chagula, ameweka wazi mahusiano yake na muigizaji mwenzake Vicent Kigosi, ambaye wanamiliki kampuni moja ya filamu.

Akizungumza na mwandishi wetu Johari amesema hawezi kuvunja mahusiano yake na Ray ambaye kwa sasa yupo kwenye mahusiano ya kimapenzi na muigizaji mwengine Chuchu Hansa, kwani wana miliki kampuni kwa pamoja.

"Mimi na Ray tunafanya kazi, kwa hiyo kuachana nae ni vigumu, naacaha nae kivipi sasa wakati wote tunamiliki kampuni ya RJ? Yule ni mkurugenzo mwenzangu kwa hiyo sio rahisi kuvunja uhusiano wetu", alisema JOhari.

Pia Johari amewataka mashabiki wake kukaa mkao wa kula kwani anatarajia kuwapakulia kazi mpya, ambayo itakuwa inawaletea yule Johari waliyemzoea kwenye filamu zake zenye ubora wa hali ya juu.

"Unajua mi siwezi kuacha anaa kwa sababu sanaa ni maisha yangu, siku si nyingi ntatoa kazi mpya hii kazi haina kustaafu,m na sasa hivi wale wasanii wakongwe karibia wengi tunajipanga kurudi kwenye game, kwa hiyo watu wakae mkao wa kula", alisema Johari.

Hivi sasa Johari amekuwa kimya kwa muda mrefu kuonekana kwenye kamera, na badala yake amekuwa mtu ambaye anakaa nyuma ya kamera kwenye utengenezaji wa filamu nyingi zinazotengenezwa na kampuni ya RJ.

Godbless Lema Ashindwa Kunyamaza Kukamatwa Kwa Ester Bulaya, Adai ni Hatari Kwa Nchi

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Mh. God Bless Lema amelaani vikali kitendo cha Mbunge mwenzake Ester Bulaya wa Bunda kukamatwa na kuwekwa Rumande kwa amri ya Mkuu wa Wilaya kwa madai kuwa hakuna sheria Tanzania inayokubali vitendo hivyo.

Akizungumza ofisini kwake mapema leo asubuhi, Lema amesisitiza kuwa vitendo hivyo ni muendelezo wa  uvunjifu wa amani huku akihofia kwamba nchi inapoelekea ni kubaya hasa mbegu za chuki ambazo zinapandikizwa zinaweza kuleta mpasuko mbaya katika taifa.

Mh. Lema ambaye pia ni Waziri Kivuli wa mambo ya ndani amesema kuwa kosa lililomuweka ndani Mh. Bulaya la kushiriki mkutano wa hadhara uliofanyika Tarime halipo katika sheria ya Tanzania na hata ikifanyiwa marekebisho hakuna sheria inayomzuia mtu kuzungumza katika mipaka ya taifa lake.

"Kama mbunge niliyepitia madhila mengi yakiwepo ya kukamatwa na polisi mara kwa mara  hili jambo linasikitisha sana kwamba Mbunge amekamatwa kwa sababu ya kwenda kuhudhuria au kuhutubia jimbo lingine, Wakati Mbunge anaruhusiwa kuhutubia mahali popote ndani ya mipaka ya Tanzania ndiyo maana anaitwa mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hata wewe Mwandishi au mtu wa kawaida. Hii ni hatari kwa nchi"
Tunapoelekea wasukuma watasema hawawataki wachaga usukumani yaani tutaanza kukataana. Hii mbegu siyo kwamba tu inauua demokrasia, uhuru wa kutoa maoni na uhuru wa kutembea popote kama katiba inavyoainisha lakini kinatengeneza mpasuko mkubwa katika taifa. Mbegu hii ikiota italeta machafuko makubwa hapo mbeleni.

Lema ameongeza kuwa tabia zinazofanywa na viongozi wa serikali zinawapa nafasi wananchi kutenga watu kwa kabila zao, ukanda wao.

"Kitakuja kizazi ambacho hakitataka kuzungumza kupitia vipaza sauti au mitandao ya kijamii au kwenda kulilia kwenye mataifa mengine na badala yake vitafuata usemi wa jino kwa jino. Nazungumza hivi kwa sababu naipenda nchi yangu" Lema

Qatar yafanya Kufuru ya Kujenga Uwanja wa Kibaragashia

$
0
0
Unaweza kusema Qatar hawataki mchezo kuhusiana na Kombe la Dunia mwaka 2022.

Maana wametangaza ujenzi wa uwanja mpya utakaojulikana kwa la Al Thumama, yaani kibaragashia.

Mwonekano wa uwanja huo ni kama kibaragashia na utakuwa na uwezo wa kuchukua watu 40,000 lakini thamani yake ni pauni bilioni 5, hivyo kuufanya kuwa mmoja wa viwanja ghali duniani.

Umbo lake la 'gahfiya' yaani kofia aina ya kibaragashia ndiyo inaufanya kuwa kivutio zaidi.

Imeelezwa kama ilivyo viwanja linguine vilivyojengwa kwa ajili ya Kombe la Dunia, kutakuwa na mfumo wa kisasa wa AC ndani yake ili watu kupata hewa safi kwa kuwa kipindi hicho kutakuwa na joto kali nchini humo wakati wa Kombe la Dunia.

Ukiachana na Uwanja wa Al Thumama, kuna viwanja linguine saba vinaendelea kujengwa ukiachana na ule wa Khalifa International uliozinduliwa Mei, mwaka huu.

Mke wa Rais Mugabe Awakimbia Polisi Afrika Kusini

$
0
0
Vyombo vya habari nchini Zimbabwe vimeripoti kuwa mke wa  Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, Bi Grace Mugabe amerejea nchini humo kutoka Afrika Kusini licha ya kutafutwa na jeshi la polisi kujibu mashtaka ya kumshambulia Mwanamitindo Gabriella Engels katika hoteli moja jijini Johannesburg.


Bado haijajulikani kama serikali ya Afrika Kusini imempa Bi Grace Mugabe kinga ya kidiplomasia kwani awali ilielezwa kuwa alizuiliwa na mahakama nchini humo.

Mwamitindo Gabriella Engels 20, alimshutumu Bi Mugabe kwa kumpiga baada ya kumkuta akiwa na watoto wake wawili wakiume lwenye chumba kimoja cha hoteli nchini Afrika Kusini mtaa mmoja wa kifahari wa Sandton, kaskazini mwa mji wa Johannesburg.

Mawakili wa Gabriella Engels mwanamke ambaye anamshtaki Bi Mugabe kwa kumjeruhi, wanasema kuwa mteja wao alipewa pesa kuachana na kesi hiyo lakini akakataa.

Bi Engels, alionekana kwenye mkutano wa waandishi waahabari siku ya Alhamisi akiwa na bendeji kubwa kwenye uso wake huku Bi Grace Mugabe akikataa kufika mahakamani baada ya kushtakiwa wiki jana, akidai kuwa na kinga ya kidiplomasia.

Hata hivyo Mamalaka za Afrika kusini zimekanusha madai hayo kwamba Bi Grace Mugabe ana kinga ya kidiplomasia.

Tundu Lissu Apewa Siku Saba na Serikali Kuomba Radhi na Kufuta Maneno yake

$
0
0

Tundu Lissu Apewa Siku Saba na Serikali Kuomba Radhi na Kufuta Maneno yake, Soma kwa urefu hapa chini:


Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE..

Hakuna Msalia Mtume...Wanafunzi 22 Milambo Wafikishwa Mahakamani..Washtakiwa Kwa Makosa Haya

$
0
0
Wanafunzi  22 wa Shule ya Sekondari ya Milambo ya mkoani Tabora wamepandishwa kizimbani wakikabiliwa na mashitaka 12 matano yakiwa ya kujeruhi na saba ya kuharibu mali, ambapo mmoja amesomewa tuhuma zake akiwa amelazwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete.

Upande wa serikali ukiongozwa na wakili Iddy Mgeni ulidai mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Tabora, Emanuel Ngingwana kuwa washitakiwa walitenda makosa hayo 12 Agosti 14 mwaka huu majira ya usiku.

Wakili Mgeni alidai katika mashitaka ya kwanza hadi ya tano kuwa siku hiyo, watuhumiwa kwa pamoja waliwashambulia na kuwajeruhi wakazi watano wa kata ya Chemchem kinyume na kifungu namba 241 sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Aliwataja walioshambuliwa na kujeruhiwa kuwa ni Juma Farahani, Iman Elias, Salehe Ally na Ahmed Haruna wakazi wa mtaa wa Uhuru na Hamza Jafary mkazi wa mtaa wa Dawa.

Katika mashitaka ya sita na saba, walidaiwa siku hiyo watuhumiwa kwa pamoja waliharibu mali ya Shaban Farahani chini ya kifungu namba 326 (1) cha sheria ya makosa ya jinai huku wakijua kwamba ni kosa.

Upande wa mashitaka ulidai katika mashitaka ya nane kuwa watuhumiwa waliharibu vitu mbalimbali vyenye thamani ya Sh 440,000 zikiwemo spika mbili, dirisha moja na simu mbili mali ya Hemed Rajab.

Wanafunzi wa sekondari ya Milambo wanatuhumiwa kuvamia nyumba ya kulala wageni iitwayo Nyakitonto na kuharibu taa tano na bango vyote vikiwa na thamani ya Sh 750,000 mali ya Asia Maulid wakati katika shitaka la 10 ilidaiwa kuwa watuhumiwa hao waliharibu turubai mbili, milango miwili, sahani na vikombe, dirisha mbili, juzuu boksi tatu zinazotumiwa na waumini wa dini ya kiislam mali ya Ally Juma, yote ikiwa na thamani ya Sh 4,278,000.

Watuhumiwa wote walikana na mahakama ilisema dhamana ipo wazi na walitakiwa wadhamini wawili kwa kila mtuhumiwa mmoja ambao watasaini mkataba wa ahadi ya Sh milioni mbili kila mmoja na shauri hilo limeahirishwa hadi Agosti 31, 2017.

Mahakama Yazuia Bomoabomoa Kwa Nyumba 286 Dar

$
0
0
Wakati operesheni ya ubomoaji wa nyumba zilizoko ndani ya umbali wa mita 121.5 kutoka katikati ya Barabara ya Morogoro ikiendelea maeneo ya Kimara mpaka Kiluvya jijini Dar es Salaam, Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi imeziwekea kinga ya muda nyumba 286 zinazohusika.

Uamuzi huo wa Mahakama ulitolewa juzi na Jaji Leila Mgonya kutokana na maombi ya zuio yaliyowasilishwa mahakamani hapo na wakazi hao 286 wa maeneo ya Ubungo- Maji hadi Kiluvya wakiomba itoe zuio la muda hadi kesi yao ya msingi itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.

Maombi hayo ya zuio la muda kusubiri uamuzi wa kesi ya msingi yamepangwa kusikilizwa Agosti 30 baada ya upande wa wajibu maombi (Serikali) kuwasilisha hati ya kiapo kinzani.

Hata hivyo, wakati wakisubiri usikilizwaji wa maombi ya zuio la muda, wananchi hao kupitia kwa wakili wao, Benito Mandele waliwasilisha maombi ya dharura wakioomba mahakama hiyo iamuru hali iendelee kuwa kama ilivyo kwa sasa hadi maombi hayo yatakaposikilizwa.

Jaji Mgonya anayesikiliza shauri hilo alikubaliana na maombi hayo na kuamuru hali iendelee kuwa kama ilivyo kwa sasa hadi tarehe hiyo ya maombi hayo yatakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.

Kwa uamuzi huo, Tanroads ambayo ndiyo mtekelezaji wa operesheni hiyo haitaweza kuzigusa nyumba hizo hadi hapo mahakama itakavyoelekeza vinginevyo baada ya usikilizwaji wa maombi hayo ya zuio la muda kusubiri kesi ya msingi kumalizika.

Wakili Mandele alisema kuwa watakachofanya baada ya kupata hati ya amri hiyo ya mahakama wataitoa nakala nyingine na kuwagawia kila mdaiwa kwa ajili ya kuiweka kwenye nyumba yake.

Katika kesi ya msingi namba 284 ya mwaka 2017, wananchi hao wanaiomba mahakama itamke kuwa wao ni wamiliki halali wa maeneo hayo yenye mgogoro na kwamba hawapo katika hifadhi ya barabara.

Pia, wanaiomba mahakama hiyo iamuru kuwa kama Serikali inata kuwahamisha na kuyachukua maeneo yao, basi iwalipe fidia stahiki kwa mujibu wa sheria.

Tanroads imetoa notisi kwa wakazi wote walipo katika umbali wa mita 121.5 kutoka katikati ya barabara ya Morogoro kila upande, kuanzia Ubungo - Maji hadi mpakani mwa Dar es Salaam na Pwani kuvunja nyumba zao kwa madai kuwa wapo kwenye hifadhi ya barabara.

Hivyo, Tanroads waliwataka wananchi hao kuondoka katika maeneo hayo ili kupisha upanuzi wa barabara hiyo.

Wananchi hao wanapinga amri hiyo wakidai kuwa wanaishi katika maeneo hayo kihalali kwa kuwa wana hatimiliki halali na hawapo kwenye hifadhi ya barabara, huku wakihoji sheria iliyotumika kuidhinisha umbali huo wa mita 121.5.

Kutokana na hali hiyo, wananchi hao wameamua kwenda mahakamani katika makundi tofauti na kufungua kesi tofautitofauti kupinga operesheni hiyo wakidai kulipwa fidia kama Serikali itawahamisha.

Mbali na kesi hiyo iliyotolewa amri hiyo, pia kuna kesi nyingine mbalimbali ambazo ziko katika hatua mbalimbali.

Kesi hizo nyingine ni ile iliyofunguliwa na Abdallah Maliki kwa niaba ya wenzake 570 ambao ni wakazi wa maeneo ya Kimara, Mbezi na Kiluvya dhidi ya Tanroads na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kwa upande mwingine.

Shauri jingine ni maombi ya kibali cha kufungua kesi ya uwakilishi kupinga operesheni hiyo lililofunguliwa na Ephrahim Kavishe na wenzake wanne ili wawe wawakilishi wa wenzao zaidi ya 198 ambao ni wakazi wa Kimara Stop Over na Mbezi.

Hata hivyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni mmoja wa wajibu maombi hayo amewawekea pingamizi akiiomba mahakama hiyo iyatupile mbali maombi hayo huku akiainisha kasoro mbalimbali za kisheria.

Maombi hayo yanasikilizwa na Jaji Crencecia Makuru na amepanga kutoa uamuzi kuhusu pingamizi hilo Agosti 30, uamuzi ambao ndio utakaotoa hatima ya maombi hayo kama yataendelea kusikilizwa au yatatupiliwa mbali.

Kwanini Roma Mkatoliki Anakataa Kabisa Kusema Alihojiwa nini na Watekaji?

$
0
0
Nimemsikiliza Roma Mkatoliki akihojiwa na Millard Ago kwa takribani dakika 35 lakini amekataa kata kata kueleza alikuwa anahojiwa nini!

Ameeleza tukio zima la yeye na Monie,Bin laden na Imma kuchukuliwa studio mpaka huko wasikokujua.

Ameeleza mateso aliyoyapata mpaka kuvunjwa kidole cha mwisho mkono wa kushoto na kuvunjwa jino la juu kwa kupigwa na mijeledi,virungu huku wakiwa wamefungwa USO na mikono na mateke huku mdomo Umefungwa sole tap usije ukatoa sauti

Roma alikuwa room ya peke yake,Imma room ya peke yake na Monie na Bin laden walikuwa room ya peke yao.

Na aliambiwa atatoka mwaka 2030 kama wimbo wake alioimba Roma.

Swali langu kwanini Roma anakataa kabisa na hata Katika hayo mahojiano kueleza alihojiwa nini?!

Ila anachosisitiza hayo yote aliyoulizwa yeye hayafanyi na anamwachia Mungu.

Rais Magufuli Kuingilia Ugomvi wa Kanisa?

$
0
0
Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Temeke limemuomba Rais Dkt John Pombe Magufuli kuingilia kumaliza mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 30 unaohusu umiliki wa kiwanja kilichopo Kitalu D Mtaa wa Everest jirani na Hospitali ya wilaya ya Temeke.

Mdhamini wa Kanisa la EAGT nchini Mchungaji Christom Isack Ngowi ametoa kauli hiyo kufuatia notisi inayowataka kuhamisha mali zote za kanisa kabla ya kesho Agosti 21, siku ambayo Manispaa ya Temeke imepanga kubomoa eneo hilo, kitendo ambacho waumini na viongozi wa kanisa hilo wamesema kingesubiri maamuzi ya barua waliyomuandikia Rais Magufuli kuhusu mgogoro huo.
Katika maelezo yao, viongozi na waumini wa kanisa hilo wameshangazwa na kile walichoeleza kuwa ni kutotekelezwa kwa maagizo ya mawaziri wa zamani wa ardhi akiwemo marehemu Mustafa Nyang'anyi na mwenzake Marcel Bujiku Komanya, ambao katika nyakati tofauti walizitaka mamlaka kulipatia kanisa la EAGT Temeke umiliki wa eneo hilo.

Kiwanja hicho kinagombewa kati yao na mfanyabiashara mmoja wa eneo hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Hai, Amweka Mwalimu Rumande kwa Kushindwa Kujibu Swali

$
0
0
Katika ziara ya kutembelea shule za sekondari, Mkuu wa wilaya ya Hai, Mh.Gelasius Byakanwa alifika shule moja iliyopo ukanda wa chini mwa wilaya ya hiyo akiambatana na afisa elimu msaidizi ndugu Jafari na mwandishi wa habari wa Redio Boma-Hai FM ndugu Davis Minja.

Dc alifanya kikao na walim hao,alianza kwa kuwauliza wangapi wanamfahamu kwa majina, Walim walikaa kimya, DC akawaamuru waandike majina yake kwny karatasi aliyowapa. Baadhi ya walim walishindwa na kuwaita WANAFIKI. Kosa ni kushindwa kuandika majina yake.

Baada ya mda akawataka waalimu waandike nafasi ya shule mwaka 2015 katika mtihani wa NECTA, mwalimu mmoja alishindwa kuandika na alipomfata akimwamuru aandike, mwalimu alimjibu hawezi kuandika uongo kwani hakumbiki. Jibu hilo lilimfanya DC apige simu Polisi na kuagiza polisi waje.

Kabla gari la polisi kuja, DC alimwita mwl pembeni na kumwambia achague kati ya kwenda rumande au kupiga push-up 20, lakini mwl alimjibu hawez kupiga push-up kwani anamatatizo ya kiafya. Basi gari lilipokuja mwalimu alipandishwa na kupelekwa kituo cha polisi Bomang'ombe.

DC aliwaambia walimu wakitaka wakashitaki kokote na hata kwny chama chao cha CWT.
Kisha aliwaamuru kupiga picha ya pamoja kama kumbukumbu...

Baada ya Kikao hicho DC amekuwa aliwapigia sim walim hao na kutaka kujua kinachoendelea.

Taarifa ilifikishwa chama cha waalim CWT-wilaya na kisha kuja kufanya kikao na waalimu ilikupata uhalisia wa tukio, ndio mwalim mmoja wa kike kuongeza kuwa baada ya kikao kwisha DC alimpigia simu saa zisizo za kazi ikiwa ni pamoja na usiku akimtala waonane.Mwalim alitoa vielelezo vya sms na muda aliopigiwa (screen shoot) zake na kumkabidhi katibu wa cwt mkoa wa kilimanjaro...

Swali: Je huu ndio uwajibikaji na utawala bora?

By Kimetah/Jamii Forums

Je Una Upungufu wa Nguvu za Kiume, Kukosa Hamu ya Tendo, Kufika Kileleni Haraka na Kushindwa Kurudia Tendo au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0
JE, UNA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUFIKA KILELENI HARAKA NA KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA (MASTER BLASHION), HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k. Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

 BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa ☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni ☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa. Kwa kutumia mimea na matunda @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250000@250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6 hadi 7 @150000@150,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150000@150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130000@130,000/= BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA. KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :- @markson_beauty_pr @markson_beauty_pr @markson_beauty_pr

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa (+255) 0767447444 na 0714335378 

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Serikali Yabanwa Sakata la Bombardier Kuzuiwa Canada...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya August 21

$
0
0

Serikali Yabanwa Sakata la Bombardier Kuzuiwa Canada...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya August 21

Rais Kenyatta Anyoosha Mikono Kwa Al Shabaab...Akiri Kuwa Wanamnyima Raha...

$
0
0
RAIS Uhuru Kenyatta amekiri kuwa, kama kuna kitu kilichomkosesha raha katika awamu ya kwanza ya utawala wake, basi ni matukio ya kigaidi yaliyofanywa mara kwa mara ya kundi la wanamgambo wa Kiislamu la Al Shabaab.

Ukiondoa jambo hilo, amesema kitu kilichomfurahisha sana katika utawala wake ni kukamilika na kuzinduliwa kwa mradi wa reli ya kisasa kati ya Mombasa na Jiji la Nairobi. Aliyasema hayo siku chache kabla ya Uchaguzi Mkuu wa Kenya, alipokuwa akijibu maswali ya Wakenya kupitia mtandao wake wa kijamii wa Facebook.

Akizungumzia jambo lililomfurahisha zaidi, hakusita kusema kuwa ni kukamilika na kuzindua reli ya kisasa `Standard Gauge Railway (SGR)’ naye kusafiri kwa treni kutoka Mombasa hadi Nairobi. Reli hiyo ya kisasa ilizinduliwa Mei mwaka huu na hivyo kuashiria ukuaji wa sekta ya usafirishaji nchini Kenya. Aidha, reli hiyo imesaidia kuimarisha usafiri wa kwenda na kutoka Mombasa.

Mbali ya kuwa ni usafiri wa uhakika, nauli ya treni pia ni nafuu huku ikisafiri kwa saa nne tu kati ya Nairobi na Mombasa, umbali wa kilometa 441, sawa na maili 271. Kuhusu kilichomsononesha akiwa madarakani, alisema ni mashambulizi ya kigaidi ya kundi la Al Shabaab.

Kundi hilo, kwa nyakati tofauti limefanya mashambulizi huko Lamu na Kaskazini Mashariki mwa Kenya na kuua watu kadhaa. Na tukio la hivi karibuni huko eneo la Milihoi liliua watu watatu, huku Karibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Maryam El Maawy akipigwa risasi begani. Rais Kenyatta anatarajiwa kuapishwa wakati wowote baada ya kuwa ameshinda kwa mara nyingine uchaguzi mkuu, akimbwaga mshindani wake wa karibu, Raila Odinga.

Mali za Lugumi zilizopo Mbweni na Upanga Kupigwa Mnada na TRA

$
0
0

Mali za Lugumi zilizopo Mbweni na Upanga Kupigwa Mnada na TRA

Mbunge wa Bunda Ester Bulaya Hali Mbaya Azidiwa Ghafla Rumande

$
0
0
Mbunge wa Bunda Ester Bulaya Hali Mbaya Azidiwa Ghafla Rumande
MBUNGE wa Bunda Mjini, Ester Amos Bulaya (Chadema) amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime mkoani Mara usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua ghafla akiwa rumande ambako alikuwa ameshikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda ya Tarime Rorya baada ya kumkamata akiwa hotelini kwa madai ya kutaka kufanya mkusanyiko usio halali.

Taarifa za kulazwa kwa Bulaya zimethibitishwa na Katibu wa Mbunge Tarime Vijijini, John Heche (Chadema), Mrimi Zabron ambaye ameeleza kuwa Bulaya anasumbuliwa na kifua ambacho kimesababisha ashindwe kuzungumza lakini hata hivyo madaktari wanaendelea kumtibu.
Aidha imeelezwa kuwa, Bulaya alianguka na kupoteza fahamu akiwa rumande hivyo kukimbizwa hospitali kwa matibabu.

Hatimaye Balozi Mwapachu Ampata Mbwa Wake

$
0
0

Hatimaye Balozi Mwapachu Ampata Mbwa Wake
Mwanadiplomasia wa siku nyingi nchini, Juma Mwapachu sasa atakuwa amejaa tabasamu baada ya mbwa wake aliyekuwa amepotea, kupatikana.

Mwapachu alitoa tangazo la aina yake katika gazeti hili Agosti 15, akieleza kuwa mbwa wake amepotea na kuomba msaada kwa atakayemuona.

Akizungumza na gazeti hili, Mwapachu alisema kuna mtu ambaye alisoma tangazo hilo na kwenda nyumbani kwake na kueleza nia yake ya kumsaidia kumtafuta.

Mwapachu alisema mtu huyo alianza kumsaka mbwa huyo kwenye nyumba za jirani, maeneo ya Mikocheni hadi alipofanikiwa kumkuta Mbezi Beach jijini hapa.

“Alimkuta kwa mtu ambaye alidai ameuziwa na baada ya kumrudisha hapa tulimpa zawadi ya Sh200,000 kama tulivyoahidi kuwa zawadi nono itatolewa,” alisema Mwapachu.

Mwapachu alisema kuna uwezekano mbwa huyo alitoroka nyumbani kupitia matundu yaliyopo katika geti la nyumba yake.

Alisema mbwa huyo alipewa na rafiki yake wa karibu kutoka familia ya marehemu Sir George Kahama, miezi sita iliyopita.

Mwapachu alisema tangu atoe taarifa ya kupotelewa na mbwa huyo, amepokea simu za watu mbalimbali wakionyesha nia ya kumsaidia kumtafuta.

“Rafiki yangu Anna Kahama aliniletea mbwa huyo na alinipa kama zawadi tu. Aliletwa hapa akiwa na miezi mitatu na picha kwenye gazeti ilipigwa akiwa mdogo. Sasa amekua,” alisema Mwapachu.

Tangu kuanza zoezi la kumtafuta mbwa huyo hakikuwekwa wazi kiasi ambacho kingetolewa kwa mtu ambaye angefanikisha kumpata mbwa huyo.    


Viewing all 104793 articles
Browse latest View live




Latest Images