Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live

BREAKING NEWS: Viongozi wa Nne wa CUF Wanaomuunga Mkono Lipumba Wamefariki kwa Ajari

$
0
0
BREAKING NEWS: Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam Linamshikiria Hashim Rungwe
Stori iliyonifikia asubuhi hii ya Jumatano September 6, 2017 ni kwamba Viongozi wanne wa Chama cha Wananchi CUF wanaomuunga mkono Profesa Ibrahim Lipumba wamefariki dunia baada ya msafara wao kupata ajali maeneo ya Ubenazomozi Mkoa wa Pwani.

Ajali hiyo imetokea jana usiku wakati Viongozi hao wakitokea Dodoma kwenye sherehe za kuapishwa kwa Wabunge wapya wa Chama hicho baada ya gari lao kugongana na Lori.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Habari wa CUF Abdallah Kambaya Viongozi waliofariki ni kutoka Wilaya ya Muheza, Tanga ambapo miongoni mwao ni Mgombea Udiwani wa Muheza Mjini, aliyefahmika kwa jina moja Uredi.

Aidha, idadi ya majeruhi haijajulikana ila ni hawazidi 10 na baadhi yao wapo Hospital ya Tumbi huku akisema chanzo cha ajali hiyo ni gari la wafuasi hao kugongana na lori.





SOMA Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Siku ya Leo

Kutana na Mtabibu wa Nyota Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH...AL_WATWAN MAFUSHO

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH...
 AL_WATWAN MAFUSHO

ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote

..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na AL_WATWAN MAFUSHO Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA).
Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?
Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
AL_WATWAN MAFUSHO Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.
Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA.
 Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.
Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,
HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp +255 759 084 996

Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote..

Siri Nzito Yaibuka Maputo Kwenye tumbo la Seth wa Escrow

$
0
0
Siri Nzito Yaibuka Mputo Kwenye tumbo la Seth wa Escrow
BAADA ya Wakili Joseph Makandege anayemtetea mtuhumiwa wa uhujumu uchumi, Harbinder Singh Seth kuiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa mteja wake huyo yupo hatarini kufa kutokana na maputo aliyowekewa tumboni, siri nzito imefichuka, UWAZI linakupasha.

Wakili Makandege alidai mahakamani hapo wiki iliyopita kuwa mahakama ilitoa amri mara mbili ili mteja wake apelekwe Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili akatibiwe lakini magereza hawajatekeleza amri hiyo. Gazeti hili lilimtafuta Dk. Godfrey Chale ambaye amewahi kuhudumu katika hospitali mbalimbali jijini ikiwemo ya Muhimbili na Temeke na kumuuliza maswali kadhaa kuhusiana na tatizo linalosababisha mtu kuwekewa maputo tumboni, faida yake na athari zake, na kwa nini yanawekwa?

Akitoboa siri hiyo Dk Chale alisema maputo hayo yanawekwa tumboni kama tiba na yanaweza kukaa humo kwa muda mrefu, akafafanua kuwa maputo hayo yaitwayo kitaalamu intra-gastric balloon, ni laini sana na yanaweza kupasuka kirahisi kama mgonjwa hatafuatilia utaratibu wa uchunguzi wa mara kwa mara kuona kama bado yapo sawa na yametengenezwa kwa kutumia madini ya Silicon.

“Maputo huwekwa ndani ya tumbo la chakula na ndani yake huwekwa maji safi ya chumvi yaitwayo sterile salt au saline solution. Puto linapowekwa tumboni, hujaza nusu ya tumbo na muda wote aliyewekewa huhisi tumbo lake limejaa.
Kazi ya maputo haya husaidia kudhibiti hamu ya kula na kujikuta unakula kiasi kidogo sana cha chakula hivyo inakusaidia kudhibiti tatizo la kuongezeka unene kwa kasi,” alisema. Ili kupata undani wa maputo yanayowekwa tumboni, fuatana nasi katika maswali na majibu na Dk. Chale:

KWA NINI MTU ANAWEKEWA PUTO TUMBONI?

“Tiba ya kuwekewa puto inasaidia sana kudhibiti unene, ni njia ambayo siyo ya upasuaji, inapotumika pia husaidia kumuepusha mhusika kupata matatizo ya ini na figo. “Sababu za kuwekewa puto tumboni ni endapo mtu yupo katika hatari ya kupata magonjwa makubwa yanayohusiana na unene ambapo kitaalamu tunasema body mass index (BMI) yake inazidi 35 ambapo inaweza kumsababishia apate kisukari, ini kujaa mafuta, kupanda kwa shinikizo la damu, matatizo ya miguu na kwa mwanamke anapata vivimbe katika vifuko vya mayai au polycystic ovary syndrome.
“Mtu mwenye BMI zaidi ya 35 huwa ni mfupi na mnene sana. Mtu anaweza kuwekewa puto endapo tiba nyingine za kupunguza uzito au unene zimeshindikana, iwe kudhibiti ulaji au matumizi ya dawa za kupunguza unene kushindikana, na hawako tayari kupunguza unene kwa njia ya upasuaji.

PUTO LINAFANYAJE KAZI TUMBONI?

“Puto linapunguza nafasi tumboni hivyo inakusaidia ukila kidogo unahisi umeshiba. Mtu aliyewekewa puto anatakiwa ale chakula maalumu chenye kiwango kidogo cha nishati, awe mara kwa mara karibu na daktari wake, wauguzi na wataalamu wa lishe ili
kuhakikisha puto hilo linaendelea kuwepo bila tatizo.

NINI ATHARI YA KUWA NA PUTO TUMBONI?

“Mara nyingi watu wote waliowekewa puto huwa hawapati athari zozote na wanaendelea na maisha yao kama kawaida ila ni muhumu kuwa karibu na daktari wako kwa mawasiliano na endapo utahisi tatizo lolote basi toa taarifa kwa daktari wako, muuguzi wako au mtaalamu wa lishe.
“Hata hivyo, matatizo yanaweza kutokea mara chache sana inaweza kuumiza njia ya chakula kuanzia kinywani hasa wakati wa kuupitisha lakini ni jambo linalotibika wakati huohuo. Siku za mwanzo baada ya kuwekewa puto tumboni unaweza kujihisi vibaya tumboni, kichefuchefu na kutapika lakini haiendelei kwa muda mrefu.
“Kwa kuwa ni kitu kigeni tumboni, mwanzoni utahisi tumbo linakuwa zito, unacheua asidi mara kwa mara, maumivu ya mgongo na tumbo kujaa gesi lakini baadaye hali hiyo inapotea.

JE PUTO LIKIPASUKA TUMBONI INAKUWAJE?

“Athari mbaya inayoweza kutokea ni endapo puto hilo litanywea lote au kupasuka tumboni kwani husababisha puto hilo liende mbele na kuziba utumbo na tiba yake ni upasuaji wa dharura wa tumbo.
“Kama katika ufanyaji uchunguzi wa mara kwa mara itaonekana puto linaanza kunywea, au tunasema kitaalamu defleted, inamaanisha yale maji ya chumvi yanapungua taratibu, basi puto hilo itabidi litolewe kama lilivyowekwa.
“Kama umewekewa puto, basi hauruhusiwi kusafiri mbali na sehemu walipo wataalamu wako waliokuwekea na endapo itakulazimu usafiri, basi ni vizuri daktari wako akuruhusu na likitokea tatizo wasiliana naye mara moja ili afanye mawasiliano na daktari wa mahali ulipo.

JE PUTO LINAWEZA KUKAA TUMBONI KWA MUDA GANI?

“Muda wa puto kukaa tumboni na kuendelea kufanya kazi ni miezi sita hadi mwaka mmoja kutegemea na aina ya puto lililowekwa, maputo mengi hukaa kwa miezi sita halafu yananywea. “Endapo puto ni la miezi sita, basi lifuatiliwe na kutolewa kwa njia inayoitwa kitaalamu endoscopy. Njia ya kuyaweka huitwa Endoscopic Intragastric Balloon Insertion, na huwekwa tumboni puto moja hadi matatu na kama nilivyosema hukaa si chini ya miezi sita tumboni.

KUNA AINA NGAPI ZA MAPUTO HAYO YA TUMBONI?

“Aina za maputo haya ni nyingi kama vile Spatz, Orbera na Bio Enterics Intra-Gastric Balloon. NINI USHAURI WAKO? “Inashauriwa maputo haya yasikae tumboni kwa zaidi ya miezi sita ili kuepusha kunywea na kuleta madhara makubwa ikiwa ni pamoja na kupoteza maisha kama mgonjwa atachelewa tiba.”

YAPO MADAI KUWA KUNA UVIMBE MWINGINE TUMBONI KAMA PUTO, JE NI KWELI?

“Ni kweli tatizo hilo kitaalamu huitwa spasmodic pains, ni aina ya maumivu makali yanayohusisha mishipa ya fahamu na misuli. Maumivu haya yana tabia ya kuja kwa ukali na kupotea , ni maumivu ya kukata, yakitokea sehemu yeyote ya mwili lazima ukae na ushike sehemu hiyo.
“Spasmodic pains hutokea kwenye misuli ya miguu, ini, moyo, bandama, kongosho na tumbo. Ni maumivu yanayowatokea watoto na watu wazima. Zaidi maumivu haya hutokea tumboni sehemu yoyote lakini wengi hutokea upande wa juu wa tumbo na wanawake hutokea upande wa juu na hata upande wa chini kwenye kizazi hasa pale mwanamke anapokuwa kwenye siku zake, mimba kutishia kutoka na wakati mwingine anapokuwa katika kipindi cha upevushaji mayai au ovulation.

NINI TIBA YA TATIZO HILO?

“Tatizo la maumivu haya huchunguzwa hospitali kutegemea na sehemu yanapojitokeza. Pamoja na kutibu chanzo dawa za kutuliza maumivu haya zinaitwa Antispasmodic, pia zipo dawa za kupaka, kunywa na sindano,” alisema Dk Chale. Seth na James Rugemalira wanakabiliwa na mashitaka 12 ya uhujumu uchumi kwa kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kughushi nyaraka, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kutakatisha fedha na kuisababishia serikali hasara ya dola za Marekani 22,198, 544. 60 na Sh. 309, 461,300, 158.27. Wote wapo rumande Gereza la Segerea.

Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam Linamshikiria Hashim Rungwe

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam Linamshikiria Hashim Rungwe
ALIYEKUWA mgombea Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Hashim Rungwe Spunda anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa siku nne sasa.

Rungwe ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Umma (Chaumma) anashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam akituhumiwa kughushi nyaraka.

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema leo Septemba 5 kuwa, Rungwe anashikiliwa kituoni hapo kwa siku nne.
Hata hivyo, Kamanda Mambosasa hakutaka kuingia kwa undani kuhusu suala hilo akisema hana taarifa za kutosha.




Hiki ndicho Madee Alichomjibu Chid Benz Baada ya Kuitwa Mnafki

$
0
0
Hiki ndicho Madee Alichomjibu Chid Benz Baada ya Kuitwa Mnafki
Msanii wa muziki Bongo kutoka Tip Top Connection, Madee amechukulia poa kauli ya Chidi Benzi aliyedai kuwa msanii huyo ni mnafiki.

Madee ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake ‘Sikila’ aliyofanya na Tekno ameiambia Planet Bongo ya EA Radio kuwa hicho ni kitu kisichoweza kumuumiza kwa sababu siyo tusi.

“Chidi namuheshimu kama mdogo wangu kama rafiki yangu hatujawahi kutaniana. Ni kawaida sio tusi ambalo lingeweza kunifanya nichukie,” amesema Madee.

Kuhusu ujumbe aliandika katika mtandao wake wa twitter; ndio maana huwa sivuti sigara. Madee amekanusha ujumbe huo kumlenga Chidi Benz.

“Hilo ndio tatizo ambalo watu wengi wanashindwa kutafsiri ndio maana huwa napenda kujiita wino mweusi naandika kitu halafu kinakuweka wewe kwenye giza haujui, mpaka unitafute mimi nikueleweshe,” ameongeza.

Suala hilo lilifikia hapo baada ya Chidi Benz kudai kuwa amefanya kolabo na Tupac ambaye kwa sasa ni marehemu kitu kilicholeta mshangao.


Tunda Awapa Makavu Mamodo Wanaoibukia Kwa Staili ya Picha za Utupu

$
0
0

Tunda Awapa Makavu Mamodo Wanaoibukia Kwa Staili ya Picha za Utupu
MUUZA nyago machachari Bongo, Tunda Sebastian amewapa makavu mamodo wanaoibuka kwa staili ya kupiga picha za utupu akisema fasheni hiyo hivi sasa imefeli, hivyo ni bora wakitafuta namna nyingine ya kutoka.

Akipiga stori na Risasi Vibes, Tunda alisema wasichana wanaokuja na kudhani kuwa kupiga picha za utupu na kuzisambaza mitandaoni kutawafanya wawe maarufu, wamechemsha kwa sababu wanachokifanya ni ujinga uliopitiliza.

“Ninachokiona hapo ni upumbavu tu na tamaa ya umaarufu bila kutafakari madhara yake, kifupi watafute plan B maana A imefeli na kuwadhalilisha,”alisema.

Mama Samia: Licha ya Wadhifa Nilionao Nikifika Nyumbani Nampigia Goti Mume Wangu kwa Unyenyekevu Kuimarisha Mapenzi

$
0
0
Mama Samia: Licha ya Wadhifa Nilionao Nikifika Nyumbani Nampigia Goti Mume Wangu kwa Unyenyekevu Kuimarisha Mapenzi
 Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema licha ya wadhifa alionao, akifika kwa mumewe hupiga goti kwa unyenyekevu ili kuimarisha mapenzi na familia.

Samia alisema hayo jana akiwakumbusha wanawake wajibu wao kwenye jamii  wakati wa ufunguzi wa tamasha la jinsia linaloendelea kwenye viwanja vya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), jijini Dar es Salaam.

“Nasema haya kwa sababu mwingine anaweza kutoka hapa akasema Makamu wa Rais kasema tupo sawa nyanja zote za jamii, uongo! Hatupo hivyo kwenye nyanja zote,” alisema Samia na kuongeza;

“Pamoja na umakamu wangu wa Rais mbele ya mume wangu nitapiga goti. Sipigi goti kwamba ni inferior (kujishusha) hapana! bali ni huba na mapenzi.”

Pia alizungumzia Benki ya Wanawake na kusema Serikali ina mpango wa kuifufua na kuipa nguvu zaidi baada ya kudorora. Alisema wakati inaanzishwa walitegemea isaidie kukwamua wanawake wengi zaidi kiuchumi.

Katika tamasha hilo, wanawake mbalimbali akiwamo Makamu wa Rais, Spika wa Bunge mstaafu, Anne Makinda, Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya na Balozi Getrude Mongella, walikabidhiwa Tuzo ya Heshima inayolenga kutambua mchango wao kijinsia katika kukuza maendeleo ya Taifa.

Samia alisema mwanamke ana haki sawa na mwanamume kwenye nyanja zote za kijamii na kiuchumi, lakini  kuna mila na desturi nzuri ambazo hapaswi kuziacha ili kuimarisha familia yake. “Tuache zile mila potofu na tubebe zile nzuri zinazotufanya tuseme, tusikike na tuonekane. Tushirikiane bila kuacha mila zetu, sifa na desturi nzuri,” alisisitiza.

Mkurugenzi wa TGNP, Lilian Liundi alisema tamasha hilo linafanyika ili kutafakari na kusherehekea mafanikio, kujadili changamoto  na kuweka mikakati ya pamoja ili kuzitatua.




Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kenya Yatoa Taarifa Mpya ya Mabadiriko ya Uchaguzi wa Marudio

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kenya Yatoa Taarifa Mpya ya Mabadiriko ya Uchaguzi wa Marudio
Saa kadhaa baada ya kiongozi wa upinzani Kenya Raila Odinga kutangaza kutoshiriki katika marudio ya Uchaguzi Mkuu mpaka Tume ya Uchaguzi ifanyiwe mabadiliko, sasa taarifa inasema Tume hiyo imetangaza kundi la watu sita ambalo litasimamia uchaguzi huo.

Walioteuliwa ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo Ezra Chiloba, Naibu wake Betty Nyabuto, Mkurugenzi wa Usajili wa wapiga kura pamoja na Mkuu wa Operesheni za Uchaguzi Immaculate Kasait, Naibu wake Mwaura Kamwati, Mkuu wa Operesheni za Tume na Mkuu wa Teknolojia James Muhati.

Uchaguzi wa marudio Kenya umepangwa kufanyika October 17, 2017 kutokana na ruhusa ya Mahakama ya Juu nchini humo kufuatia kesi ya kupinga matokeo iliyofunguliwa na Odinga.










Tatizo la Nguvu za Kiume Laibua Maswali Mengi Bungeni

$
0
0
Tatizo la Nguvu za Kiume Laibua Maswali Mengi Bungeni
Swali la mbunge wa Konde (CUF), Khatib Said Haji kuhusu nguvu za kiume limewaibua wabunge wengine wakitaka kuuliza maswali ya nyongeza, ingawa Naibu Spika, Dk Tulia Ackson hakuwapa nafasi.

Mbunge huyo ametaka kujua kuhusu ongezeko la wanaume wanaopungukiwa nguvu za kiume, hivyo kuhoji iwapo Serikali inalijua tatizo hilo.

"Kama jibu ni ndiyo, je, Serikali inachukua hatua gani kukabiliana na tatizo hilo ambalo linaondoa amani ndani ya nyumba na kwa nini Tanzania imekuwa ya 10 duniani miongoni mwa nchi zilizopoteza furaha," alihoji Haji.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Afya, Dk Hamisi Kigwangalla amesema Serikali inalitambua tatizo hilo ijapokuwa hakuna jibu la moja kwa moja kwa kuwa tendo la ndoa ni siri ya wanandoa.

Dk Kigwangalla ametaja baadhi ya sababu za kupungua nguvu za kiume ni umri wa zaidi ya miaka 60, maradhi sugu, kifua kikuu, kisukari, kansa, ukimwi na wanaotumia dawa muda mrefu.

Kuhusu wauza dawa zinazoelezwa kuwa zinaongeza nguvu za kiume, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ameagiza waganga wakuu wa mikoa kuwakamata wote ambao wanafanya hivyo na hawana vibali kutoka mamlaka husika.



Wazazi Waja Juu Wataka Uchunguzi Miili Iliyookolewa Katika Shimo la Choo

$
0
0
Wazazi Waja Juu Wataka Uchunguzi Miili Iliyookolewa Katika Shimo la Choo
Miili ya watoto hao iliopolewa jana jioni kwenye nyumba ambayo ujenzi wake haujakamilika ikiwa  Wazazi wa watoto Moureen David (6) na Ikram Salim (3), wakazi wa Kata ya Olasiti, Arusha waliotekwa katika siku tofauti na kubainika kuwa wamekufa wameelekeza polisi kujua utaratibu wa uchunguzi wa miili.

David Njau, baba wa Moureen aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Lucky Vincent na Salum Kassim, baba wa Ikram wanafuatilia uchunguzi wa miili ya watoto wao iliyoopolewa kwenye shimo la choo jana Septemba 5 usiku katika eneo la Mji Mpya, Mtaa wa Olkerian.

Wakati Moureen alitekwa Agosti 21 saa kumi na moja jioni, Ikram alitekwa Agosti 26, saa 12 jioni.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Olkerian, David Safari ambaye yupo pamoja na familia hizo, amesema wanakwenda kuwaomba polisi wawapatie miili kwa ajili ya maziko.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo anatarajiwa kutoa tamko baadaye kuhusu tukio hilo.

Okwi Apewa Majukumu Mazito Mechi Dhidi ya Azam

$
0
0
Okwi Apewa Majukumu Mazito Mechi Dhidi ya Azam
BENCHI la ufundi la Simba likiongozwa na kocha wake mkuu, Joseph Omog raia wa Cameroon limempa kazi nyota wao, Emmanuel Okwi kuhakikisha anaibeba timu hiyo katika mchezo wake wa wikiendi hii dhidi ya Azam FC.

Simba na Azam zinatarajiwa kukutana wikiendi hii kwenye pambano la Ligi Kuu Bara ambalo limepangwa kupigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Da

Awali mchezo baina ya vikosi hivi viwili ulipangwa kupigwa Agosti 2, mwaka huu kabla ya kupanguliwa kutokana na kuingiliana kwa ratiba ya TFF na Kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).

Kikizungumza na Championi Jumatano, chanzo makini toka ndani ya Simba kimesema kuwa benchi hilo limefikia maamuzi hayo kutokana na muendelezo mzuri wa Okwi katika kufunga mabao ambao ni mzuri kulinganisha na washambuliaji wengine wa timu hiyo.
“Benchi letu limekaa na kuona kwamba ni Okwi pekee ambaye anaweza kutubeba kwenye mchezo huu na Azam kwa kuzipata pointi za wapinzani wetu hao, hivyo kila kitu ameachiwa yeye na atakaporudi nchini toka Uganda, basi atapewa ujumbe huo na mtu maalum wa kumpa wameshaandaliwa.

“Wameamua hivyo kwa sababu yeye ndiye mwenye rekodi nzuri ya kufunga mabao kulinganisha na washambuliaji wengine waliopo hapa, na imani yetu ni kwamba atalitimiza suala hilo kikamilifu kwa sababu ameshazoea kuamua matokeo kwenye michezo mikubwa kama alivyofanya hivi karibuni wakati akiichezea timu yake ya Uganda dhidi ya Misri,” kilisema chanzo hicho.

Championi Jumatano, lilimtafuta kocha msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja, ambapo alisema: “Okwi ni mshambuliaji mzuri linapokuja suala la kufunga mabao, tunamuamini kwamba atatubeba tu siyo kwenye mchezo huo bali kwenye kila mechi yetu ya ligi kuu.”  

Picha za Utupu za Witness Zampa Kigugumizi Ochu

$
0
0
Picha za Utupu za Witness Zampa Kigugumizi Ochu
Baada ya msanii wa Bongo Flava, Witness ‘Kibonge Mwepesi’ kuachia picha zenye utata/utupu katika mitandao ya kijamii mpenzi Ochu Shaggy ameshindwa kunyoosha maelezo kuhusu picha hizo kwa kudai hajawahi kuziona.

Muimbaji huyo amesema kuwa huwa hapendi kufuatilia anachoweka mpenzi wake katika mitandao na ndio sababu ya kutojua hilo ingawa wapo pamoja.

“Nimeziona kwa bahati mbaya, sipendi kuingia kwenye akaunti yake kuangalia ameposti nini, natamani ningeweza kuwaambia watu msiwe mnanitag na bahati nzuri wakati anaposti hizo picha sikuwa online karibu siku tatu na sikujua hata wakati anapiga hizo picha na anaposti,” amesema.

“Huwezi kuamini, kwanza sioni cha ajabu sana sijui kwa sababu namjua. Nikiingia Instagrama nashughulika na michogo yangu ya biashara ama stori zangu zinazohusiana na muziki,” ameongeza.

Mwaka jana Witness  pamoja na Ochu Shaggy waliachia wimbo ‘Sharifa’ ukiwa ni maalum kwa ajili ya kupinga mimba za utotoni.

Kampeni ya Upimaji Afya Bure Iliyoanzishwa na RC Makonda Yaanza Leo

$
0
0
Kampeni ya Upimaji Afya Bure Iliyoanzishwa na RC Makonda Yaanza Leo
Zoezi la Upimaji wa Afya Bure kwa muda wa siku tano limeanza Jumatano hii kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam ambapo baadhi ya wananchi wamewahi kwenye viwanja hivyo tokea saa 10 Usiku.

Mwamko huu ni baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kutangaza zoezi la Upimaji bila Malipo.

Madaktari bingwa na Wauguzi kutoka Hospital za Umma,Jeshi na zile za Watu Binafsi wanaendelea na zoezi la Upimaji kwa Wananchi.

Katika Upimaji huo Mwananchi atakaepimwa na kubainika kuwa na matatizo ya kiafya atapelekwa Hospital na kupatiwa Matibabu Bure. Picha za watu waliojitokeza.


Nissan Yaja na Ujio Mpya wa Magari Yanayotumia Umeme

$
0
0
Nissan Yaja na Ujio Mpya wa Magari Yanayotumia Umeme
Kampuni ya magari ya Nissan imezindua magari mapya ya umeme, wakati inakabiliana na ushindani unaozidi kukua wa magari ya umeme
Aina hiyo mpya ya magari yanaweza kusafiri mwendo wa asilimia 50 zaidi baada ya kupata chaji, kwa mujibu wa kampuni hiyo.

Hata hivyo bado magari hayo hayajafikia mwendo wa magari wa Tesla na GM.
Magari hayo yanayofahamika kama 'Leaf' yanakabiliwa na ushindani mkali wakati sekta ya magari yanayotumia umeme inazidi kukua.
Magari mapya ya Leaf yameuzwa nchini Japan kuanzia Oktoba na yataanza kuuzwa sehemu zingine mwaka ujao.

Kati ya mabadiliko yaliyofanyiwa hayo magari hayo ni mfumo wa kujindesha unaofahamika kama ProPilot Park, ambao huyawezesha kepenya maeneoimagumu hususan wakati wa kuegeshwa.
Pia yana teknolojia ya kujiendesha yenyewe hasa kwenye babara ambayo inaelekea upande mmoja tu.
Bei ya magari hayo itaanzia yen 3,150,360 au pauni 22,220.

Jini Mkata Kamba Azidi Kumvaa Manji Leo Avuliwa Udiwani Rasmi

$
0
0
Jini Mkata Kamba Azidi Kumvaa Manji Avuliwa Udiwani Rasmi
Mfanyabiashara Yusuf Manji amepoteza sifa ya kuwa Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu kutokana na kutohudhuria vikao zaidi ya sita na vikao vya kamati vya maendeleo ya halmashauri ya Temeke zaidi ya vitatu.

Meya wa Manispaa ya Temeke, Abdallah Chaurembo amesema hayo leo Jumatano katika mkutano na waandishi wa habari.

Kutokana na hilo wamemuondoa Manji kwenye nafasi hiyo kutokana na kukosa sifa.

Chaurembo amesema amemwandikia Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene kuhusu suala hilo ili aweze kupanga uchaguzi mwingine.

Harmorapa Ataki Kupitwa Aamua Kujinoa kwenye Lugha ya Kingereza

$
0
0
Harmorapa Ataki Kupitwa Aamua Kujinoa kwenye Lugha ya Kingereza
BWA’MDOGO asiyekaukiwa matukio, Harmorapa anatarajia kuanza kujinoa katika suala zima la Lugha ya Kingereza kwa mtaalam wa kufundisha lugha hiyo, James Mramba ‘Mr. English’.

Hatua hiyo imekuja baada ya msanii huyo kuona kuna fursa anaikosa katika suala zima la kuwasiliana na wafanyabiashara mbalimbali hususan atakapokwenda kupiga shoo nje ya nchi.

“Nimeamua kujifunza Kingereza na sehemu sahihi kwangu ni kwa Mr. English kwa sababu anatoa huduma za mobile.

Atanifuata nyumbani, najifunza private,” alisema Harmorapa. Mr. English anatoa huduma hiyo katika ofisi yake iliyopo Sinza-Mapambano na unaweza kuwasiliana naye kwa namba 0713 369805 au 0767 369805 ili aweze kukuhudumia popote ulipo.

Wanne Wauawa na Washukiwa wa al-Shabab Lamu, Kenya

$
0
0
Watu Wanne Wauawa na ashukiwa wa al-Shabab Lamu, Kenya
Watu wanne wameuawa na watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa al-Shabab katika eneo la Hindi katika kaunti ya Lamu katika eneo la pwani nchini Kenya.
Kamishna wa kaunti hiyo Gilbert Kitiyo ameambia BBC kwamba maafisa wakuu wa usalama katika kaunti hiyo wanakutana na watatoa maelezo zaidi baada ya mkutano huo.

Gazeti la kibinafsi la Standard linasema wakazi wamejitokeza barabarani katika mji huo kuandama kulalamikia 'kukawia' kwa maafisa wa usalama kufika eneo la shambulio.
Kenya yaanza kuangusha mabomu ‘msitu wa al-Shabab’

Kisa hicho kimetokea siku chache baada ya watu watatu kuuawa wanamgambo wanaoshukiwa kuwa wanachama wa kundi la al-Shabab waliposhambulia basin a gari eneo la Nyongoro, Witu katika kaunti hiyo ya Lamu.

Gazeti la Standard linasema visa vya mashambulio vimeongezeka eneo hilo wiki za hivi karibuni.
Kamishna wa kanda ya Pwani Nelson Marwa majuzi alitangaza kwamba maafisa wa usalama wangeanza kuangusha mabomu katika msitu wa Boni ambapo wanamgambo wa kundi hilo la Kiislamu wanadaiwa kujificha.
Wakazi waliokuwa wakiishi msituni na karibu na msitu huo walitakiwa kuhama

Yaliyojiri Uwasilishaji wa Ripoti ya Makinikia ya Almasi na Biashara ya Tanzanite. Mruma, Maswi na Muhongo washutumiwa

$
0
0

Aliyewasirisha Ripoti hiyo ni mbunge wa Ilala, Musa Azan Zungu na anaongelea kamati iliyoyabaini ikiwemo kutowajika kwa mamlaka zinazohusika na almasi na Tanzanite ikiwemo NEMC na wizara ya nishati na madini.

Kamati ilibaini kutolipwa kwa income tax ikiwa kinyume na kifungu cha kodi kinacholazimisha kampuni za madini kulipa kodi. Kampuni ya Williamson haijalipa income tax kutoka 2007 mpaka 2017 kwa kisingizio cha kupata hasara.

Mapato stahiki nchi inatakiwa kupata ni kodi kwani mrahaba ni kiasi kidogo ambacho huwa ni fidia. Kuna mkanganyiko wa takwimu kwenye mauzo ya almasi. Kuna takwimu zinazokinzana ambapo nishati na madini na wakala wa madini(TIMA) umebaini kutofautiana kwa takwimu kutoka taasisi hizo mbili za serikali.




  • Kamati imebaini kwenye vyumba ambavyo Almasi huwa inahifadhiwa, kuna milango ya dharura ambayo hutumiwa vibaya.
  • Serikali inapata hasara kubwa kutokana na usafishaji wa Almasi nje ya nchi ambao hudaiwa kuwa inapungua thamani.
  • Kamati imeona kuna haja usafishaji wa mwisho wa madini ya Almasi ufanyike hapa nchini kwani haihitaji uwekezaji mkubwa.
  • Kutokana na kukosa mapato stahiki, kuna haja ya Serikali kupitia misamaha yote ya kodi ya madini ya Almasi hapa nchini.

Thamani ya Madini ya Almasi yanayouzwa nje ya nchi ni kubwa zaidi ukilinganisha na kodi inayolipwa hapa nchini.

  • Kwa maoni ya kamati kwa uamuzi wa serikali kutoinunua Petra kwa dola milioni 10 umesababisha hasara kwa sababu kwa sababu mgodi umezalisha almasi zenye thamani ya dola milioni 343. De Beers waliuza hisa bila kufata utaratibu, kamati ikiongozwa na waziri wa wakati huo, Ngonyani walitoa ushauri usinunuliwe.
  • Viongozi wa serikali waliopendekeza mgodi usinunuliwe ndio waliopendekezwa kuwa wajumbe wa bodi.
  • Kamati ilipowahoji wajumbe wa bodi, Professa Jairo na Prof Mruma chini ya kiapo, Prof Mruma aliiambia kamati alishindwa kufuatilia madeni(Akiwa mwenyekiti wa audit commitee ya mgodi) kwa sababu hakuwa na muda wa kusoma na aliawaamini waliompelekea taarifa hizo baada ya kamati kumuhoji madeni yaliyobambikwa kwa serikali yamekuwa ni mengi mno.



  • Kamati ilimuhoji mheshimiwa Maswi ambae alikuwa katibu mkuu na ni mmoja alietia saini mkataba ambao kamati inaona una utata, alijibu hata yeye aliona kilichofanyika ni upuuzi mtupu na alienda mara moja Tanzanite one na alichukia na kutorudi tena ilhali akiwa ndie msimamizi wa wizara.



  • Kamati imebaini kuna zawadi ilitolewa kwa kiongozi mmoja mkubwa, zawadi hio ya almasi kwa sasa inakadiriwa kuwa na thamani ya dola milioni 200.
  • Makinikia yaliyobakiwa yanakadiriwa kuwa na thamani inayokadiriwa kuwa trilioni 2.3. Kamati inahoji mbona taarifa haikutolewa na yalichimbwa na marehemu Wilamson miaka ya 50? Wataalam wahakikishe gharama za makinikia hayo hazijumuishwi kwenye gharama za mgodi.

Inasikitisha kuona watumishi wa serikali hawajui kinachoendelea kwenye makampuni ambayo walipaswa kuyasimamia.

Zungu amempongeza Rais Magufuli kwa kuliamsha dude na wao wanaendelea nalo.

Pendeza na Kessy Products: Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Wako Sawa Bila Madhara yoyote

$
0
0
PENDEZA NA KESSY PRODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA


1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _80,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK (B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _90,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _80,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_90,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MILINI _90,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI_80,000/(B)VIDONGE MAX MAN_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_120,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_90,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_70,000/
(21) ENGEZA  MGUU_80,000/  

 TUNAPATIKAN DAR W SALAAM: NAKWA MIKOAN KOTE UTAPATA PIGA CM                      (+255) 0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product
Delivery  POPOTE ULIPO
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live




Latest Images