Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Huyu Ndiye Kidume Anayemfaidi Agnes Masogange

$
0
0
Kama mnavyojua dada yetu MASOGANGE kwa muda sasa yupo nchini SAUZI na amekuwa sio mchoyo wa PICHA zake, wakati wote amekuwa anashare nasi picha zake kupitia ukurasa wake wa INSTAGRAM

Sasa mimi sijajua SAUZI anafanya nini...(Kwa hapa huwa anajishughulisha na kazi ya u-VIDEO KWINI)
Kupitia kile anachoweka huko INSTAGRAM hatimaye imedhihilika wazi kwa jamaa hapo pichani anaitwa Louis Dolnard.... ndio mpango mzima kwa dada yetu...TEMBEA NAMI


kwanza ya huyu jamaa alipost miezi miwili iliyopita!!
Wambea tukapotezea!!! Dah

Wiki iliyopita alitupia tena picha ya huyu jamaa bila kuandika chochote ......washambenga tukahisi kuna....MAUMIVU NIACHE ....MAHABA NIKUMBATIE hapa....hahahahahaha!!!!


Na kweli toka jana usiku fujo ikaanza huko INSTAGRAM..Masogange aliweka picha hapo chini na kuandika"Mtoto si unanielewa, in Diamond Voice
 punde jamaa nae akaposti the same picha na kuandika "With my Everything


Daah kumbe nilikuwa nachelewa...jamaa kitambo alishawekawazi kupitia ukurasa wake wa INSTAGRAM.....

Alikuwa anawekapicha za Masogange na kufunguka ya moyoni......Jionee mwenyewe!!!

Mama Kanumba kumfuta mdogo wa marehemu Kanumba "Seth Bosco" kwenye kampuni ya Kanumba

$
0
0
MAMA-wa Marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa amemchimba mkwara mzito mdogo wa marehemu, Seth Bosco baada ya kuona amefanya kosa na kuamua kumtishia kuwa atamfuta kwenye Kampuni ya Kanumba The Great. 

Mama huyo pasipo kuweka wazi moja kwa moja tatizo, alisema kuwa kuna kosa kubwa Seth alilifanya na alishindwa kulivumilia hivyo kumuonya kuwa atamuondoa kwenye kampuni.“Ni juzi tu amefika nyumbani kwangu kuniomba msamaha nimemsamehe kama mtoto ingawa kwenye kampuni hatashiriki kwa sasa kwani ameanza kazi zake nyingine,” alisema.


Hivi Ndivyo Tanzania Tunavyosemwa na Wenzetu Kuhusu Ushirikiano Wetu East Africa

$
0
0
East Africa should let Tanzania go
Share this story: By Peter Wanyonyi
Tanzania is behaving badly. Something has spoilt the people of hela and dala dala. They are clearly growing horns and something needs to be done about it before they begin thinking they are the regional bullyboys. In the village, neighbours drop by unannounced for a cup of tea every now and then. Thus, a few months ago, President Museveni of Uganda dropped by the cattle boma of President Kagame of Rwanda. Over a cup of tea, they agreed to bury their past disagreements and forge new relations. Shortly afterwards, President Kagame paid a revenge Christmas visit to Uganda. Since then, matters have been smooth between those two countries. Makerere Down here, President Kibaki paid a visit to his alma mater, Makerere University, the other day. Apparently, he was so sharp a learner that he was invited back to teach at Makerere shortly after graduation. At any rate, he received an honorary doctorate thanking him for his service to the institution, had a chat with President Museveni and flew back home. Hardly a couple of weeks later, President Museveni dropped by Kisumu to preside over a harambee. Never mind that, in days past, he had taken to calling our Prime Minister’s people "hii wanjaruo" in that inimitable Nyankole-accented "chiswahili" that he speaks so well. Well, bygones are bygones, and President Museveni is now Ruoth — senior elder of the Luo Nation. Noisy stink Not so Tanzanian leaders. Tanzania is cold and haughty where East African matters are concerned. They attend East African Community (EAC) meetings only to throw spanners in the works. Double standards reign in that country. Evidence is everywhere. A few days ago, the Kenya- Tanzania border crossing had to be closed after Kenyans did what we do best: raise a noisy stink over double standards. You see, because of our good neighbourliness and some EAC protocols that we have signed, Tanzanians can drive into Kenya and conduct their business here with no problem. No charges, no permits, no questions asked. But the reverse is not true for Dar. Kenyans who want to drive into Tanzania for business must cough US$200 (Sh16,400) each time they cross the border. Tanzania’s GDP per person per month is a mere US$100 (Sh8,200), so every Kenyan vehicle that crosses into that country pays the equivalent of two Tanzanians’ monthly economic output. Even passenger vehicles are not spared the levies. And it doesn’t stop there. Whereas Tanzanians visiting Kenyan public facilities — like game parks — are charged the concessionary rates that Kenyans and other East Africans pay, Kenyans doing the same in Tanzania are charged exorbitant "tourist" levies. These guys are also hell bent on sport hunting, notwithstanding the fact that our elephants routinely stroll across the common border. Which explains why President Jakaya Kikwete hasn’t seen it fit to drop by Kenya, Uganda, Rwanda or even Burundi for a cup of chai. Why should he? Tanzania — with their South African sounding national anthem — after all, pays little more than lip service to the idea of East African cooperation, enraptured as it is by the glittering prospects offered up by South Africa. The time has come to bid kwaheri to Tanzania and move on with EAC integration.
standardmedia

Kashfa Nzito Sekta ya Afya..Maisha ya Baadhi ya Watu yapo Hatarini

$
0
0
Maisha ya baadhi ya watu wanaotumia dawa za kufubaza makali ya ugonjwa wa Ukimwi (ARVs), yapo hatarini, baada ya kupungua kwa dawa hizo nchini na hivyo kufanya wagonjwa kutumia dawa tofauti na zile wanazotumia siku zote.

Uchunguzi wa gazeti hili umegundua kuwa hali hiyo inatokana na urasimu wa baadhi ya taasisi za Serikali, ambazo zinachelewa kuagiza dawa za ARVs kwenye viwanda vya nje ya nchi.

Tayari Mfuko wa Kimataifa unaoshughulikia Ugonjwa wa Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria wa Global Fund, Shirika lisilo la Serikali linalojihusisha na masuala ya afya (Sikika) na watumiaji wa ARV nchini wamethibitisha kuwapo kwa upungufu huo na hatari zake kiafya kwa wagonjwa.

Global Fund katika ripoti yake ya robo ya mwaka huu (Januari- Machi), imekiri kuwapo kwa upungufu wa dawa za ARV nchini na athari ambazo wameanza kupata wagonjwa.

Ripoti hiyo inaonyesha upungufu huo wa dawa za ARV unatokana na uzembe wa baadhi ya taasisi za Serikali kuchelewa kuagiza dawa hizo pamoja na kuwapo kwa mabadiliko katika ununuaji na ucheleweshwaji wa kupatikana fedha za kununulia ambao umesababisha upungufu huo.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa waathirika wakuu katika upungufu huo wa dawa ni wanawake wajawazito wanaoishi na virusi vya Ukimwi, ambao wanatakiwa kutumia ARV aina ya TLE ili kuzuia maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto.

Upungufu huo, umesababisha wagonjwa kubadilishiwa dawa tofauti na zile wanazotumia hali ambayo imesababisha baadhi yao kinga ya mwili (CD4) kushuka.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika baadhi ya mikoa nchini unaonyesha tatizo hilo la kupungua kwa ARVs nchini, limewaumiza wagonjwa wengi na kwamba sasa wanapokwenda hospitali wanapewa dawa za kutumia wiki mbili au vidonge 10 badala ya dawa za mwezi mmoja au miwili.

Sikika

Shirika lisilo la Kiserikali (Sikika), linalojihusisha na masula ya afya, wamebaini kuwapo kwa upungufu wa dawa za ARV katika mikoa ya Kigoma, Kilimanjaro, Tabora, Shinyanga, Morogoro, na Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Sikika, Irenei Kiria alimwambia mwandishi wa gazeti hili kuwa taarifa walizozipata kutoka kwa watu wanaotumia ARV, upungufu mkubwa wa dawa hizo kwa Mkoa wa Dar es Salaam upo katika katika Hospitali za Mnazi Mmoja, Mwananyamala, Amana na Temeke.

Katika hospitali hizo wagonjwa wanabadilishiwa dawa za ARV na kupewa tofauti na zile ambazo wamezoea kuzitumia.
“Taarifa tulizopata Machi mwaka huu, ni kwamba tatizo hilo bado lipo na wagonjwa wanaendelea kupewa dawa pungufu, mfano badala ya kupewa za mwezi mara nyingine walikuwa wanapewa za wiki au kubadilishiwa dawa bila kupewa maelezo ya mabadiliko hayo,” anasema Kiria.

Kiria aliiomba Wizara ya Afya itoe tamko rasmi kuwaeleza wananchi hali halisi ya dawa za ARV, ili kuepusha hali ya wasiwasi na madhara ya kisaikolojia wanayoyapata wagonjwa hivi sasa.

“Ni haki ya kila mwananchi kupata taarifa sahihi ambazo zinahusu afya yake, ili naye aweze kutimiza wajibu wake wa kuilinda afya yake na za wenzake,” anasema Kiria.

Kiria anaishauri Serikali kutenga bajeti kwa ajili ya shughuli za dharura pale ambapo itatokea, huku akiitaka kupunguza utegemezi.

Anasema taarifa ya matumizi ya Serikali ya ugonjwa wa Ukimwi mwaka 2011 na Mkakati wa Tatu wa Kitaifa wa Kudhibiti Ukimwi (NMSF III) wa mwaka 2013/14 – 2017/18 unaonyesha kuwa bajeti hiyo imekuwa ikipungua na kwamba utegemezi wa wafadhili ni zaidi ya asilimia 97.

Naibu Waziri

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Kebwe Steven, anasema kuwa licha ya kutegemea ufadhili, lakini Serikali ina fedha kwa ajili ya kununua dawa ndani na nje ya nchi kama itatokea kutakuwa na dharura.

Anasema kuwa hafahamu kuhusu kuwapo kwa upungufu, anachofahamu ni kuchelewa kufika kwa dawa kutokana na taratibu za uagizaji, kwani Global Fund ambayo ndiyo inayoagiza dawa hizo husambaza kwa nchi nyingi.

Anasema kuwa anadhani hilo ndilo tatizo lililosababisha kupungua kwa dawa hizo nchini.

Naibu waziri huyo anasema pamoja na Global Fund kutoa dawa hizo nchini, lakini Serikali wamekuwa wakichangia kiasi katika kuziingiza dawa hizo.

“Siyo kwamba hatuchangii kabisa, kuna vitu ambavyo tunafanya ikiwamo gharama za kutoa dawa hizo bandarini, hatuwezi kumwachia jirani atujengee nyumba,” anasema Kebwe.

Mirathi ya George Tyson, Monalisa Acharuka

$
0
0

Oohoo nooo! Wakati aliyekuwa mumewe, George Otieno Okumu ‘Tyson’ (41) akipumzishwa kwenye nyumba ya milele huko Kisumu nchini Kenya, Yvone-Cherry Ngatikwa ‘Monalisa’ amewacharukia watu waliodai alikuwa akijipendekeza msibani ili kupata mirathi ya mwanaume huyo.

Awali, Mona ambaye ni staa mkubwa wa sinema za Kibongo alianza kutupia mitandaoni picha za kumbukumbu (mastaa wanaita Throw Back Thursday au TBT) akiwa na Tyson kuanzia siku ya send-off yake Agosti 14, 2001 na ile ya siku ya harusi yao Agosti 25, 2001.
Picha hizo ziliambata na maneno ikionesha ni kwa jinsi gani Tyson au baba Sonia (mtoto wao) alivyokuwa mtu muhimu maishani mwake.

Ishu hiyo ndiyo iliyosababisha tafrani kubwa huku akiambulia kushambuliwa kwa maneno makali kuwa anajipendekeza.

Habari za kiintelijensia zilidai kuwa kati ya wanawake wanne aliowaacha Tyson, pamoja na kutengana mwaka 2006 bila talaka, Mona ndiye amekuwa akipewa pole badala ya wanawake hao wengine akiwemo Beatrice, Angel na Lucy.

Kuna madai mazito yanayorushwa kwamba ishu ya mirathi ya Tyson inazidi kuzua tafrani kila mmoja akijiaminisha kuwa ndiye mrithi halali.Baada ya kuona maneno yanakuwa mengi ndipo Mona akacharuka na kuandika kwa kile anachokijua juu ya ishu hiyo.

Aliandika: “Let me clear the air. Ni hivi, pamoja na ujinga tulioufanya mimi na George katika maisha yetu, kwa macho ya kibinadamu utasema alikuwa na mke mwingine lakini kwa macho ya ki-Mungu, mimi ni mke halali wa George Otieno Okumu aliyelala.
Anayesema mke wa Tyson alijifungia ndani mimi nikawa nachukua pole zisizo zangu, dah! Kwanza wanawake walikuwa wawili ndani siyo mmoja na wote walijifungia ndani. Kwa nini? Ni Wakristo na wanaijua dini. Waombolezaji walikuwa wakinipa pole mimi. Ni kwa nini?

Jiulize kabla ya kuropoka halafu wewe ni mwanamke kuna siku yatakukuta.
Nilienda (msibani) kutimiza wajibu wangu kama mke, ningelia peke yangu kwetu mngenisema sana, nimekaa msibani naambiwa nachukua pole za bure.

Acha nikukumbushe maandiko... Alichokiunganisha Mungu?....(binadamu asikitenganishe). Kilichofungwa duniani?.....(kimefungwa na mbinguni) Nikupende, nikutunze hadi kifo?.....(kitakapotutenganisha).
Sasa kifo kimetutenganisha. Siku ya mwisho unadhani George ataitwa na nani? Pamoja na mambo yake yote acheni nimlilie, he was a good father kwa Sonia wangu especial miaka 5 ya mwisho wa uhai wake.
Acheni nimlilie, he was my best friend 1998-2014. Nime-share naye kitanda 2000-2006. Nitakuwa mtu wa aina gani nisiwe na uchungu?

Ukiona mwanamke mwenzio kaishindwa ndoa, usimcheke jua kuna sababu...na ni fundisho kwa wachukua waume za watu wote mjini.
Mume akiumwa huwa anarudi kwa mkewe na akifa? And for your info...msianze anajifanya mke sasa hivi ili apewe mali...

Sonia ni mali kubwa sana aliyoniachia, am so happy. Waache wao wanaolilia kupewa pole wapiganie. Mwenyewe aliyetafuta kafa kaziacha, sembuse tuliobaki?
“Niacheni nimlilie, waacheni fans wangu walie na mimi.”

Hata hivyo, baadhi ya mashabiki wake walimshauri kuwa angenyamaza na kuacha watu wazungumze kwani ni upepo tu unapita hivyo naye aliwasikiliza na kuamua kuondoa maneno hayo katika kurasa zake kwenye mitandao ya kijamii.

Tyson ambaye alikuwa bonge la mwongozaji wa vipindi vya runungani na sinema za Kibongo alifariki dunia kufuatia ajali mbaya ya gari aina ya Toyota Noah, iliyotokea eneo la Gairo mkoani Morogoro ambapo Jumamosi iliyopita alizikwa kijijini kwao huko Kisumu nchini Kenya.
GPL

Wema Sepetu na Kajala Beef Upya

$
0
0

Stori:  Shakoor Jongo na Musa Mateja

ZIKIWA zimepita wiki kadhaa tangu kuripotiwa kupatanishwa kwa mastaa wawili katika tasnia ya filamu Bongo, Wema Sepetu na Kajala Masanja, taarifa zisizo na shaka zilizotua kwenye meza ya Ijumaa Wikienda zinaeleza kwamba upatanisho huo haukusaidia chochote na sasa bifu jipya limeibuka kati yao.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha ndani kilichoomba hifadhi ya jina lake, zoezi la upatanishi kati ya mastaa hao lililofanyika kwenye msiba wa dairekta wa filamu za Kibongo, George Tyson, Mbezi Beach jijini Dar lilikuwa sawa na kazi bure.

“Hakuna yeyote kati yao aliyekuwa na nia ya dhati ya kumaliza tofauti zilizokuwepo, walikubali kupatana kwa sababu ya heshima ya waliokuwa wanawapatanisha lakini kiukweli ilikuwa ni sawa na danganya toto, bifu limelipuka upya,” kilisema chanzo hicho ambacho ni rafiki wa karibu wa mastaa hao wakubwa mjini.

TEAM WEMA, TEAM KAJALA WANOGESHA BIFU
Kwa mujibu wa sosi wetu, ukiachilia mbali kukosekana kwa utayari wa kupatanishwa kati ya wawili hao, pande mbili za mashabiki wao wenye ushawishi mkubwa kwenye mitandao ya kijamii waliojipachika majina ya Team Wema na Team Kajala, zimekuwa zikinogesha bifu hilo kwa kumwagia petroli kwenye moto, hali inayozidi kutibua mambo.

“Sikia nikwambie, kuna vitu vinafanyika katika mitandao ya kijamii hasa Instagram kuhusiana na hizi pande mbili halafu wahusika wakuu wanajifanya hawazijui, kuna Team Wema ambayo inamsapoti Wema na ile ya Kajala inayoitwa Team Kajala, wenyewe wanawajua fika ni akina nani wanaounda pande hizo ila ukiwauliza wanajifanya hawajui chochote.

“Wengine wananunuliwa mpaka simu za kisasa zenye uwezo wa kufungua mitandao ya kijamii ili wasambaze uzushi na uongo kuhusu upande pinzani, sasa timu hizo ziliposikia juu ya upatanisho huo, ziliwajia juu wahusika ambapo kila mmoja kwa upande wake alikanusha kupatana na mwenzake,” kilizidi kutiririka chanzo hicho.

KAJALA HATAKI KABISA SULUHU
Chanzo chetu kiliendelea kufunguka kuwa Kajala hataki kabisa kusikia kuhusu mambo ya suluhu kwa sababu Team Wema imemdhalilisha sana mtandaoni kiasi cha kumpa wakati mgumu kujieleza mbele ya mwanaye, Paula ambaye inadaiwa naye aliyashuhudia matusi hayo ya nguoni.

“Yaani Kajala anasema labda Wema mwenyewe ndiyo aende kumuomba radhi kwa kashfa zilizokuwa zinatolewa na timu yake anaweza kumfikiria mara mbilimbili kuhusu suluhu na siyo kusuluhishwa juujuu tu kama ilivyotokea,” alizidi kutiririka sosi wetu na kuongeza:

“We si unaona mara ngapi Wema na Kajala wanakutana sehemu na wewe mwenyewe kama mwandishi unashuhudia, umewahi kuwaona wakiwa pamoja au hata kusalimiana?”

MSIKIE KAJALA
Baada ya kusikia  kauli hizo kutoka kwa chanzo chetu, kama kawaida ya Ijumaa Wikienda liliingia mzigoni kutafuta mzani wa habari ambapo wa kwanza kutafutwa alikuwa ni Kajala ambaye hakutaka kabisa kulizungumzia kwa kina suala hilo. Hebu msikie:

“Kiukweli mi naona hili tatizo letu linachangiwa na hizi timu ambazo zipo kwa ajili ya kuongeza matatizo. Nasikia eti baada ya siku ile mimi na Wema kupatanishwa, watu wa timu yake walimpigia kumuuliza, akakataa kuwa hajakubali kupatanishwa na mimi ili kuwafurahisha watu wake, sasa unategemea mimi nitasema nini? Nafikiri siyo rahisi mimi kukaa karibu na Wema kama zamani,” alisema Kajala.

WEMA NAYE
Kwa upande wa Wema yeye alishangaa habari hizo na kutoa dukuduku lake kwa kusema anachojua ni kwamba hana bifu na mtu yeyote, siyo Kajala tu bali mtu yeyote ambaye walikuwa na tofauti huko nyuma yeye hana bifu naye tena.

“Mi nadhani watu wanahitaji kuona picha ambayo tumepiga pamoja na Kajala ndiyo waamini kuwa tumemaliza bifu letu, unajua huu unaokuja ni Mwezi Mtukufu wa Ramadhan na mimi ni mtoto wa Kiislam sasa nitafungaje Ramadhan huku nikiwa na bifu na mtu?” alisema Wema.
Kukinzana kwa maelezo ya wawili hao kunatosha kuonesha jinsi ambavyo suluhu ya awali haikuweza kumaliza bifu kati yao.

KUTOKA KWA MHARIRI
Wema na Kajala nyie ni wasanii wakubwa ambao jamii inawatazama kama kioo chao. Haipendezi kuendeleza malumbano yasiyo na msingi, huu si wakati wa kuwekeana visasi bali sameheaneni kutoka ndani ya mioyo yenu na mshirikiane kuisimamisha sanaa ya filamu za Kibongo.
GPL

Audio: Baada ya Wababa kuwatuhumu Diamond na Nay wa Mitego kwa Wizi, Nay ajibu tuhuma

$
0
0
Mshiriki wa Bongo Star Search, Wababa aliwatuhumu Diamond Platinumz na Nay wa Mitego kwa wizi wa kazi zake za muziki kwa wakati tofauti.

Akiongea na Bongo Dot Home ya 100.5 Times Fm,inayoongozwa na Jabir Saleh Wababa alidai kuwa Diamond Platinumz alimuibia wimbo wake wa Kitorondo kwa kuurudia bila kumwambia, wimbo ambao anadai aliuimba miaka minne iyopita akiwa na Dogo Aslay wakati huo yeye anatumia jina la Nurdi.

Alidai baada ya wimbo wa Diamond kuvuja ukiwa na jina la Kitorondo yeye alipigiwa simu na watu wakamwambia na akausikiliza akaona ni kweli amefanya kile alichofanya yeye miaka mingi iliyopita. Hata hivyo anadai wimbo huo Diamond ameubadilisha baadae na kuuita Kidogo Kidogo huku akibadilisha ujumbe(Wimbo mpya wa Diamond).

“Mimi nilikuwa naongelea msichana mdogo, lakini yeye ameongelea mapenzi lakini melodies, mtiririko ni ule ule bado.” Alisema Wababa.

Hata hivyo Wababa alidai kuwa hana cha kufanya kwa upande huo na kwamba anaona kama Diamond anarudi nyuma kwa kuwa yeye anamchukulia kama mfano wa kuigwa kwa hatua alizopiga, lakini kurudi kuchukua wimbo wa msanii mchanga aliofanya miaka minne iliyopita ni kujirudisha nyuma.

Katika hatua nyingine, Wababa alimrushia lawama Nay wa Mitego ambaye anadai amemshirikisha kwenye wimbo wake alioufanya Mazoo Records lakini Nay alimzunguka na kurudi kwa producer Mazoo akidai anataka aununue wimbo huo na ataulipia shilingi milioni moja.

“Watu wa pale ndio walinishtua kuwa aisee njoo kwa sababu kuna kitu kinaendelea hapa Nay anataka kuchukua wimbo wako aulipie milioni moja.” Ameeleza Wababa.

Anasema alimpigia simu Mazoo lakini muda huo alikuwa na Nay wa Mitego hivyo hakupokea na yeye hakuweza kwenda. Lakini tangu kipindi hicho akimpigia simu Nay wa Mitego hapokei na akipokea anamwambia yuko busy amtafute baadae.

“Mimi nataka tu Watanzania wafahamu kwa sababu akija kutoa wimbo halafu mimi nikalalamika, ndio yataibuka yale yaliozoleka pale msanii anapoibiwa na kudai haki yake anaambiwa anatafuta kick….”

Bongo Dot Home ilimtafuta Nay wa Mitego ambaye alieleza kwa upande wake nini kilitokea na mpango uko vipi kuhusu tuhuma hizo.

“Sijui niongee nini kuhusu hii issue…mimi nimeisikia. Lakini mimi napenda beat nzuri, mimi sijataka ile beat. Lakini kilichofanyika ni kwamba producer ametaka kunipa mdundo wa design ile lakini sielewi ni kwa nini tena maneno yamekuja kwamba mimi nimetaka kuilipia ile beat. No, mimi nilisema napenda ule mdundo wa design ile kwa gharama yeyote naweza nikaulipia lakini sio kama nimetaka mdundo wa dogo..no.

“Ngoma ya dogo nzuri, mimi mwenyewe nimependa the way nilivyoimba lakini sio kama nitake ngoma yake au beat yake hapana ntakuwa nakosea, nitakuwa nakosea sana. Lakini mimi nilichoongea ni tofauti na hicho labda wale wameninukuu vibaya. Mwisho wa siku naweza kusema mimi siwezi…kwanza muziki wangu watu wanaujua uko tofauti sana. Hiyo ngoma yenyewe ukiisikia iko tofauti sana, na mimi nimetaka changes kwenye muziki wangu.. nilimwambia producer nataka beat ya design hii ambayo inaweza kuwa kali zaidi ya hii na mimi nikailipia hela yoyote unayoitaka. Kwa hiyo mwisho wa siku sijui nini kiliendelea hapo katikati.

“Si kweli…ni nyimbo nzuri kweli mimi niliipenda niliisifia na ndio maana nilikuwa na nguvu ya kuweza kuifanya naweza kusema kwa asilimia mia moja. Mimi sijafanya featuring tangu mwaka jana. Kwa mwaka huu nilifanya featuring mbili tu,  nilifanya ya kwanza ya Kala Jeremiah na hii ni ya pili tena baada ya kutumiwa demo nikaoni ni nzuri sana. Niliifanya kwa nguvu kwa sababu niliona ni nyimbo nzuri ambayo hata mimi mwenyewe watu wanaweza kuendelea kusema ‘okay mwana amefanya collabo nzuri’. Siwezi kuchukua nyimbo yake yeye, nyimbo yake yeye.

“Mimi anitafute, siku mbili tatu hizi nilikuwa busy na mambo yangu. Nilikuwa namalizia nyumbani kwangu huku na kule vitu vingi shows na vitu vingine. Anitafute tutaongea. Mimi naweza kusema hivi ni mdogo wangu, hakuna ambacho kitaharibika lakini sidhani kama itaweza kufikia hatua tukagombana mimi nay eye. Labda yeye alininukuu vibaya."

Msikilize hapa:

Kikwete Aagiza Waliolipua Bomu Wasakwe

$
0
0
RAIS Jakaya Kikwete amelitaka Jeshi la Polisi kuwasaka na kuwafikisha mbele ya vyombo vya haki watu wote waliohusika katika ulipuaji bomu lililosababisha kifo na kujeruhi watu saba mjini Unguja, Zanzibar.

Kikwete ambaye amesema kitendo hicho ni cha kulaaniwa kwa nguvu zote na watu wote wapenda amani Bara na Visiwani, amekitaja kuwa ni cha woga kisicho na ustaarabu, kisichokubalika katika dunia ya sasa.

Alisema hayo katika salamu za rambirambi alizotuma jana kwa Rais Ali Mohamed Shein wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Bomu hilo lilirushwa katika shughuli ya kidini iliyokuwa ikifanyika katika eneo la Darajani , mjini Unguja. Miongoni mwa majeruhi, yumo mhubiri wa amani ajulikanaye kama Sheikh Ahmed Haidari Jabir wa Zanzibar.

“Hicho ni kitendo cha kulaaniwa kwa nguvu zote na watu wote wapenda amani Bara na Visiwani, ni kitendo cha woga na kisicho na ustaarabu na wala hakikubaliki katika dunia ya sasa,” alisema. Rais Kikwete aliongeza,

“Hiki ni kitendo kilichofanywa na watu waoga, wasio na ustaarabu wa aina yeyote ile.”

Alikemea wanaofanya vitendo hivyo na akahimiza watu kuwa wastaarabu, wavumilivu na kuheshimu imani na mitizamo ya watu wengine hata kama hawakubaliani nao.

Akiendelea kulaani, alisema amesikitishwa zaidi na watu hao wasio na ustaarabu ambao wamefanya kitendo hicho cha kihalifu kwenye shughuli ya kidini ambapo ndipo mahali panapostahili amani, uvumilivu na unyenyekevu zaidi kwa kuwa ni wakati ambapo binadamu anapofanya mawasiliano na muumba wake.

Alihimiza polisi kuwasaka na kuwafikisha mbele ya vyombo vya haki wahusika wa tukio hilo. Kwa mujibu wa Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai wa Zanzibar, Yussfu Ilembo, aliyekufa papo hapo ni Muhammad Mkombalaguha (26), mkazi wa Tanga.

Kutokana na tukio hilo, polisi visiwani humo ilitangazia hali ya hatari watu waliohusika na shambulio hilo. Ilielezwa kwamba uchunguzi umeanzia kwenye mabaki ya vitu vilivyokutwa katika eneo la tukio.

Miongoni mwa vielelezo vilivyokusanywa ni pamoja na vipande vya mabaki ya gundi ya karatasi na vitu vingine ambavyo vinasadikikwa vimetumika kutengeneza bomu hilo.

Mtu aliyekufa pamoja na majeruhi, walikutwa na mkasa huo wakati wakitoa Msikiti wa Darajani baada ya Ibada ya Swala ya Isha inayoswaliwa kuanzia saa 1:45 usiku na kuendelea.

Baada ya kumalizika ibada hiyo, walitoka msikitini na kufika eneo la Darajani wakisubiri gari na ndipo mlipuko mkubwa uliposikika ambao unasadikiwa kuwa ni bomu.

Amani, uzalendo Katika hatua nyingine, akiwa mkoani Dodoma juzi, Rais Kikwete aliwataka Watanzania kuendelea kulinda na kupigania amani iliyopo kwa ustawi na usalama wa nchi .

Rais Kikwete alisema hayo juzi kwenye uzinduzi wa tamasha la uzalendo lililoasisiwa na wasanii wa muziki na filamu nchini ikiwa ni pamoja na uzinduzi wa video ya wimbo maalumu wa Muungano wa Tanzania na Zanzibar.

Alisema uzalendo kwa Watanzania ndiyo njia pekee ya kufanya taifa liendelee kutunukiwa hadhi ya kisiwa cha amani duniani.

Katika tamasha hilo lililofanyika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, Rais Kikwete alisema ili kuwaenzi waasisi wa taifa, ni lazima kudumisha misingi ya amani na kujitolea kizalendo kulilinda na kulitetea taifa kama walivyofanya waasisi Mwalimu Julius Nyerere na Shehe Abeid Amani Karume.

Pia aliwataka wasanii kutumia vizuri talanta walizojaliwa kufikisha ujumbe wenye uzalendo kwa Tanzania.

Instagramers Wamshambulia Diva na Kusema Ameedit Picha zake ili Aonekana na Makalio Makubwa

$
0
0
Katika Hali Isiyo ya kawaida kuna baadhi ya watu ama Vikundi Instagram wameanza kumchimba Diva Loveness Baada ya Kujitoa Team Wema, Sasa leo wamekuja na Mpya na Kusema kuwa Diva anajiongezea makalio kwenye picha zake kwa kutumia Photoshop, na Wameenda mbali zaidi na kutoa ushahidi wa baadhi ya Picha jionee mwenyewe hapo chini na Ujudge mwenyewe kama ni kweli ama la kwa kuziangalia hizo Picha:




Angalia hiyo Kabati ya Viatu Ilivyopinda pinda

Angalia Ukuta na Frame ya Mlango ilivyopata Dhahama

Angalia Kiti hapo nyuma na Juu ukuta kwenye rangi ya blue ukuta umeyumba na tako
Wataalamu Kazi Kwenu kutuambia kama ni kweli ama wanamsingizia ..
Khaa Ustaa Kazi Kweli Kweli

Maskini Watu Wengine 30 Wauwawa Kenya kwa Shambulio la Kigaidi

$
0
0
WATU zaidi ya 30 wameuawa, hoteli mbili, kituo cha polisi na kituo cha mafuta kuchomwa moto baada ya shambulio lililotokea eneo la Mpeketoni, Lamu nchini Kenya jana usiku.

Kituo cha Polisi cha Mpeketoni, hoteli ya Breeze View na Taweel ndivyo vilivyochomwa moto na moshi ulikuwa bado unafuka asubuhi hii.

Imeelezwa kuwa washambuliaji walitokomea na silaha na magari ya polisi kutoka kutuo hicho cha polisi baada ya kushambulia.

Awali washambuliaji hao waliteka daladala mbili 'matatu' eneo la Witu kabla ya kufanya shambulio hilo.

Wananchi walikimbilia katika nyumba zao wakati polisi wakijibizana risasi na magaidi hao ambapo mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo anadai kusikia washambuliaji hao wakisema "ambieni baba yenu atoe jeshi Somalia” wakimaanisha wamwambie Rais Kenyatta aondoe jeshi nchini Somalia.

Makundi ya Al Shabaab na MRC militia yanadaiwa kuhusika na shambulio hilo

Maimatha Akwaa Skendo ya Utapeli..Ni Kuhusu Dawa za Kukuza Makalio

$
0
0
Stori: Gladness Mallya

SKANDALI! Prizenta maarufu Bongo, Maimatha Jesse amejikuta katika wakati mgumu baada ya kukwaa skendo ya utapeli kutokana na dawa za kukuza maungo anazoziuza kuwa hazifanyi kazi.
Sosi ameibua utapeli huo wa Maimatha kwa kusema:

“Maimatha anatapeli watu na dawa zake, yaani tumepaka mabinti wengi hazitusaidii chochote, ni wizi mtupu, laki mbili bila chochote kweli roho inauma.”

Baada ya kunyaka madai hayo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Maimatha akakanusha:
“Hao wamejisikia tu kuongea hata siwafahamu na wala sijawahi kupata kesi kama hizo, mbona nilishawauzia wengi? Mimi mwenyewe zimenisaidia, wazushi tu,” alisema Maimatha.
GPL

Msiwalaumu Wadada wa Mjini Kutembea na Wazee

$
0
0
Nimepanda lift kwenye moja ya jengo maarufu na refu hapa mjinikati karibu na Ohio st. Niko ndani ya lift mzee mmoja smart anongea na simu kwa sauti ya maringo , upole na yenye kujiamini, kulikua kimya hivyo unasikia kabisa upande wa pili ni sauti ya kasichana mazungumzo yalikua hivi.

Mzee - What do you mean..I've told you before not to worry it is within my capability usichukue gari ya chini, chagua landcruiser au yoyote ya juu.

Mdada.- '............. .... ....... ..... ........ ........ .... ............

Mzee. - Ok no problem, njoo sasa hivi uchukue cheque kwa ajili ya kuwalipa NSSF niliongea na mkurugenzi wake akanipromse a nice location for your appartment.

Anyway we njoo ukifika go to reception I have already reserve a place, just wait me in the room nina kikao na waziri nikimaliza nakuja. 

Niliwai kufika nikatoka liftini nikamuacha bado anaongea.

Kwa kweli niliona hamna sababu ya kuwasema wadada wanaotembea na wazee this dudes knows how to care jamani......

Vijana Siku hizi Hawajui Kuhonga zaidi ya Kuchafuana tu hata hela ya kununua sababu ni kujisafishia hupati

Polisi wafanikiwa kumkamata Mwanamke aliyekuwa akimtesa binti yake wa kazi kwa kumjeruhi kichwani

$
0
0
Polisi wamefanikiwa kumnasa mwanamke anayedaiwa kumtesa kwa kipigo na kumng’ata mtoto Merina Mathayo (15), kumsababishia majeraha makubwa kichwani.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Camillius Wambura akizungumza na Mwananchi jana alisema walifanikiwa kumnasa juzi, mwanamke huyo akiwa mafichoni Mbagala wilayani Temeke.
“Tumefanikiwa kumnasa juzi usiku akiwa mafichoni kwa jamaa zake, ni mwanasheria wa kujitegemea ana umri wa miaka 44, lakini inashangaza kwa hayo aliyoyatenda, anaendelea kuhojiwa wiki ijayo tunatarajia kumpandisha kizimbani,” alisema Wambura.

Mtuhumiwa huyo ambaye ni mkazi wa Boko, anadaiwa kumtesa mtoto huyo ambaye ni mtumishi wake wa kazi za nyumbani, ambaye sasa amelazwa katika wodi ya dharura ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa(MOI) Muhimbili Dar es Salaam.
Wakati huo huo, Uongozi wa MOI umejizatiti kulinda usalama wa mtoto huyo, kwa kuzuia vyakula kutoka nje ya taasisi hiyo, ikiwa ni pamoja na kudhibiti watu kumtembelea na kuzungumza naye.
Mmoja wa wauguzi katika wodi aliyolazwa alieleza mtoto huyo kwa sasa anahudumiwa kila kitu na taasisi hiyo.
Ofisa Uhusiano wa MOI, Patric Mvungi , alieleza kwamba majibu ya kipimo kikubwa cha CT Scan alichofanyiwa yametoka, ambapo yameonyesha hakuna mfupa uliovunjika kichwani.
Mtoto Merina amelazwa Moi baada ya kupewa rufaa na Hospitali ya Mwananyamala alipokuwa amelazwa awali, kutokana na majeraha hayo ya kung’atwa meno na kupigwa na vitu mbalimbali.

Flora Mbasha na Mumewe kumbe wana Laana ya Askofu Kulola

$
0
0
SAKATA  la  tuhuma  za  ubakaji  zinazomkabili  mume  wa  Flora  Mbasha  sasa  limechukua  sura  mpya  baada  ya  maovu  yao  mengine  kuanikwa  hadharani  na  ndugu  wa  Flora…..

Msichana  mmoja  aliyejitambulisha kwa  jina  la Cathy  ambaye  ni  dada  binamu  wa  Flora  amedai  kuwa  kinachowatafuna  wawili  hao  ni  laana  waliyoipata  kutoka  kwa  babu  wa  Flora, marehemu  baba  Askofu  Moses  Kulola…..

Ndugu  huyo  wa  Flora  amesema  kuwa  wawili  hao  waliwahi  kufikia  nyumbani  kwa  askofu  Kulola  huko  Mwanza,siku  chache  kabla  ya  Kulola  kuaga  dunia  na  kufanya  madudu  mengi  ikiwemo  kuingiza  askari  polisi  kwenye  chumba  cha  Kulola.

Ndugu  huyo  alidai  kuwa  wawili  hao  walifikia  hatua  ya  kuingiza  askari  kwenye  chumba  cha  askofu  Kulola  kwa  madai  ya  kuibiwa   sh.  300,000 ( Laki  tatu )    za  Emmanuel  Mbasha, mume  wa  Flora  huku  wakimwaga  matusi  mazito  kwa  wajukuu  wa  Kulola….

“Walifikia  pale  kwa  babu, yule  Mbasha  akawa  na  pesa  kama  laki  tatu  hivi, akazihifadhi  kwenye   nyumba  ndogo  ya  chini  waliyofikia,nyuma  ya  nyumba  ya  babu, akawa  amesahau  alikoziweka  zile  pesa  basi  wakaanza  kuwatukana  matusi  ya  nguoni  wajukuu  wa  babu  pale  kama  hawana  akili  nzuri, yeye  Mbasha  na  Flora,” alisema  ndugu  huyon wa  Flora.

Akaendelea  kudai  kuwa  walipoona  hakuna  ushirikiano  kwa  wajukuu  wa  babu  wakaamua  kuita  polisi  waliofika  pale  nyumbani  na  kuanza  kufanya  upekuzi  wa  nguvu  kwenye  kila  kona  ya  nyumba    ya  baba  Askofu….

“Walipoona hawajafanikiwa kuzipata  akaamua  kuwaingiza  polisi  mpaka  chumbani  kwa  babu,  na  babu  alikuwa  hayupo  nyumbani, alikuwa  kanisani, sasa  aliporudi  ndipo  alikuta  askari  chumbani  kwake  wakifanya  upekuzi. Babu  alikasirika  sana  na  kujikuta  akimwaga  machozi,” alisema  Cathy

Akaendelea  kudai  kuwa  babu  alishangaa  sana  kufikia  hatua  ya  wawili  hao( Flora  na  mumewe)   kutomwamini  hata  yeye  mpaka  kuingiza  askari  ndani  ya  chumba  anacholala  lakini  wawili  hao  walimpuzaa  hata  baba  Askofu  huyo….

“Babu  aliwalaani  wale  na  aliwaambia  kuwa  siku  si  nyingi  maovu   na  uchafu  wao  utajulikana  kwenye  jamii  huko  Dar  wanakowaibia  watu  kwa  kujifanya  wameokoka  wakati  siyo  kweli  na  wanatapeli  watu  kila  siku,akasema  wataishia  pabaya  muda  si  mrefu,” alisema  Cathy.

Akaendelea  kudai  kuwa  Flora  na  mumewe  hawakuwahi  kuomba  radhi  kwa  babu  yao  Askofu  Kulola  mpaka  alipofariki, na  mpaka  leo  hii  laana  yake  bado  inaawatafuna  sana  na  haya  yanayoendelea  ni  matokeo  ya  laana  hiyo.

Tuwe Makini Yanayotokea Kenya Hata Tanzania Yanawezekana.

$
0
0
Jamani naombeni niwe mkweli hata kama nikionekana kuwa mimi ni mubaguzi, kwa kweli wasomali mimi huwa sina imani nao popote pale walipo, kwa sababu mashambulio ya kigaidi yanayotokea kenya, magaidi huhifadhiwa na wasomali waliopewa hifadhi ya ukimbizi kenya, angalizo kwa Tanzania juzi juzi tanzania imewapa uraia, raia wa somalia jambo ambalo mm naliona ni hatari..kwani hao ndio sasa wanaisumbua Kenya...jamani Watanzia hii nchi ni ya kwetu na siyo ya viongozi leo hii usalama ukivurugika viongozi wao watapaa kwenda nje wakati ss tunabaki Tunahangaika.
JF

Chadema Wahaha Kusaka Mgombea Urais 2015

$
0
0
Wadau, ni dhahiri kuwa CHADEMA sasa hakijiwezi tena na kimechoka hadi huruma.

Kwa ujumla ni kwamba, CHADEMA hawana mtu mwenye sifa, uwezo wala hadhi kuweza kukiwezesha chama kupata angalau asilimia 10 ya kura za Rais. Tegemeo lao hapo awali lilikuwa kwa Dr Slaa. Hata hivyo, imedhihirika kuwa kwa sasa Dr Slaa hana mvuto tena na kama chadema wataamua kiubishi ubishi kumsimamisha kugombea, hakika wataangukia pua kabisa. Hadhi ya Dr Slaa kwa sasa imeshuka sana na wataalam wa masuala ya kisiasa wanasema kuwa asipojiangalia mwisho wake utakuwa mbaya zaidi. Kushuka kwa hadhi kwa Dr Slaa pamoja na mambo mengine kumeelezwa kuwa kumetokana na kitendo chake cha kupanga, kuratibu na kusimamia mpango wa kumng'oa Zitto Kabwe kwenye chama hicho. Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema kuwa uwepo wa wanasiasa nguli kama Zitto Kabwe na wasomi mahiri kama Dr Kitila Mkumbo na wapanga mikakati kama Samson Mwigamba kulikiwezesha chama hicho kuaminiwa na wananchi wengi. hata hivyo, baada ya maamuzi ya kuwafukuza akina Zitto, imeelezwa kuwa wafuasi wengi wa chama hicho wameamua kurejea CCM huku wengine wakijiunga chama kipya cha ACT Tanzania. Freeman Mbowe anayo tamaa ya kugombea urais. Hata hivyo tatizo kwake ni Elimu. Mbowe hana elimu ya Shahada inayohitajika kwa mtu kuteuliwa kuwa mgombea Urais. 

Blan B ya CHADEMA katika kupata mgombea mwenye sifa ni kuangalia ndani ya mahasimu wao wakubwa kisiasa, Chama cha Mapinduzi ambacho kimesheheni wanasiasa nguli vijana kwa wazee ambao ni Presidential Materials. Target yao kubwa ni wanasiasa wanaotoka mikoa ya Kaskazini na kanda ya Ziwa. Hapa CHADEMA wamekuwa kama fisi ambaye anangojea mkono wa binadau udondoke ili auokote. Lakini wapiiii! CHADEMA nao wanafuata matendo ya fisi. Wanasubiri CCM wateleze hasa katika mchakato wao wa kumpata mgombea urais. Inadaiwa kuwa CHADEMA wanamuangalia sana Edward Lowasa. Kwao wanamuona kuwa Lowasa ni mtu ambaye atakisaidia chama chao kushinda urais wa 2015. Wao wanaamini kuwa LOWASA atatemwa na chama chake kwenye kinyang'anyiro cha urais kitendo ambacho kitasababisha EL ahame chama chake na kujiunga na CDM. Inadaiwa kuwa tayari CHADEMA wamewasilisha mpango wao kwa EL. Hata hivyo, taarifa za ndani zinasema kuwa Lowasa amewaambia live kwamba ikiwa ataamua kugombea urais, basi itakuwa ni kwa tiketi ya CCM kauli ambayo imewakatisha tamaa sana. Baada ya kugonga mwamba kwa Lowasa, inaelezwa kuwa Sumaye na Mama Anna Kajumulo Tibaijuka ni miongoni mwa wanaopendekezwa na Mzee wa Tengeru katika nafasi ya Urais.

Plan C ya CHADEMA ni kuanzisha muungano fake na vyama vingine vya siasa. Kwa kuanzia wameunda umoja ujulikanao kama UKAWA. Ingawa umoja huo lengo kuu ni kupigania Rasimu ya Katiba ya Jaji Warioba, inaelezwa kuwa lengo kuu ni kuwahadaa wanasiasa mahiri wa vyama vingine kama akina Prof Ibrahim Lipumba na James Mbatia. Hapa CHADEMA wanajifanya sitaki nataka. Kwamba, CHADEMA wametoa matamko kuwa UKAWA itasimamisha mgombea mmoja tu katika ngazi ya Rais. Mapendekezo ya awali ni kumsimamisha Mchungaji Christopher Mtikila. Hata hivyo, inadaiwa kuwa James Mbatia, Ibrahim Lipumba na wahafidhina wa CHADEMA wamekataa mapendekezo hayo. Lipumba anadai kuwa ndani ya UKAWA, yeye ndiye Msomi na mkongwe kwenye siasa kuliko wote. Hivyo amewapa masharti kwamba ikiwa UKAWA wataamua kusimamisha Mgombea Urais mmoja, basi wamteue yeye kuwa mgombea. Hata hivyo mzee wa Tengeru amekataa pendekezo hilo la Lipumba kwa sababu zinazojulikana. 

Kwa hali hiyo, mipango yote ya CHADEMA Yaani Plan A, B na C imekwama. Wamebaki kutapatapa tu na washauri wao akina Saed Kubenea wanaonekana kukosa kabisa mbinu za kukinusuru chama.

Nawasilisha.
By Lizaboni Via JF

WEMA Akana Kuwa Mjamzito

$
0
0
Staa wa movie Tanzania a.k.a Mrs. Diamond Platnumz ameamua kuandika ukweli kuhusu stori ulizosikia kwamba kwa sasa ni mjamzito… Kupitia page yake ya instagram Wema ameandika ‘Jamani hizi habari za mimi kuwa pregnant…. sijui watu wanatolea wapi… Im NAT… Dah… I wish I was… But im nat wapenzi wangu’

Kundi la Al Shabaab Lakiri Kushambulia Kenya na Kuuwa Watu 49

$
0
0
Watu zaidi ta arobaini na tano wameuawa katika mashambulizi ya Mpeketoni
Kundi la wapiganaji wa Al Shabaab nchini Somalia, limekiri kufanya mashambulizi katika eneo la Mpeketoni karibu na Lamu, Pwani ya Kenya.
Mashambulizi hayo yalisababisha vifo vya watu 49.

Taarifa ya kundi hilo ilisema kuwa shambulizi hilo lilikuwa la kulipiza kisasi dhidi ya serikali ya Kenya kwa kufanya msako dhidi ya waisilamu kwa njia ya kuwafunga kiholela na kuwaua wahubiri wa kiisilamu.
Baadhi ya walioshuhudia mashambulizi hayo wamearifu BBC kuwa wameona maiti kadhaa na majeruhi wengi japo Polisi hawajathibitisha ni watu wangapi wameuawa.

Mji wa Mpeketoni uko umbali wa kilomita miamoja kutoka eneo la mpakani na Somalia
Kenya imekumbwa na mashambulio kadhaa kutoka kwa wapiganaji wa kisomali wa Al Shabaab tangu ipeleke wanajeshi wake Somalia mwaka wa 2011.

Duru kutoka kisiwa cha Lamu zimearifu kuwa wapiganaji hao walifika katika malori mawili na kurusha kifaa kama bomu ndani ya kituo cha polisi kisha wakakivamia na kuiba silaha.
Pia waliteketeza hoteli na vijiji huku wakiwapiga watu risasi kiholela

Serikali Itoe Tamko Kuhusu Vodacoma M-pesa

$
0
0
Kwa muda wa siku mbili sasa huduma ya Mpesa kupitia mtandao wa Vodacom imekuwa haipatikani na hakuna kauli rasmi kutoka mamlaka zinazohusika kuhusu nini hatima ya pesa za watu au nini kifanyike katika tatizo lililopo.
Serikali ndio iliyoruhusu matumizi ya Mpesa na hata yenyewe inakubali kufanya shughuli zake kwa malipo ya kupitia mitandao hiyo, hivyo ni suala ambalo wao wenyewe wanalitambua na kulikubali.
Sasa kwa nini kama kwa siku mbili hakuna hii huduma na watu wanapesa zao huko TCRA au wizara mbona wako kimya?

Hili la miaka nane ya uchakavu magari ni kuwakomoa wananchi na kulinda barabara zisizo na Viwango

$
0
0
Nimejaribu siku hadi siku kuangalia hili swala la serikali kudai inalinda nchi na magari chakavu na sasa imepunguza miaka ya uchakavu kutoka kumi hadi nane. Hivi serikali hii imeangalia uwezo wa wananchi kununua magari yasiyo chakavu? Mbona hayo ya miaka nane yapo mengi yana zaidi ya milage 200,000? hapo siyo uchakavu?

Je wametathmini gharama za hayo magari yenye miaka nane kama mtanzania wa kawaida anaweza kuyanunua au lengo ni kupunguza uwezo wa wananchi kununua magari? Au hii ni mbinu mbadala ya kuongezea wananchi mzigo na wao kuvuna kodi? Wabunge nao watakaa kimya? Mbona hayo ya miaka kumi yapo mengi yenye milage chache na hayo ndo siyo chakavu ukilinganisha na haya ya miaka nane yenye mileage hadi laki 3? 

Ni imani yangu kuwa kutokana na mipango mibovu ya miundombinu ya barabara hii ni mbinu ya kupunguza watanzania wenye uwezo wa kumiliki gari. Waziri asisingizie kupunguza ajaili kwanza hana justification yeyote kuwa hayo magari analeta ajali ukiachilia ambayo tayari yapo. Asilimia 90 ya magari yaliyopo tz yakiwemo magari ya waziri mwenyewe ni mabovu zaidi na ungeyapeleka japani yasingeruhusiwa kuuzwa tena kwani ni mabovu mara mia ya yanayokuja yakiwemo yaliyotengenezwa miaka ya 90. 

Serikali iache ubabaishaji na badala yake wajenge barabara zenye uwezo na kuwapa nafasi wananchi kumiliki magari.
By nginda JF
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images