Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Mkuu wa Majeshi Tanzania, Jenerali Mabeyo Aguswa na Tukio la Tundu Lissu...Afunguka Makubwa

$
0
0
Mkuu wa majeshi nchini, Venance Mabeyo amewataka wananchi kutulia kwani vyombo vya ulinzi na usalama vimekuwa vikipapambana na matukio ya kihalifu wakati wote, akitolea mfano matukio yaliyotokea Kibiti lakini ameshangazwa na mshtuko uliotokea sasa, Mabeyo amesema asingependa kuingia huko lakini vyombo vya ulinzi na usalama vinapambana na matukio kadri yanavyojitokeza na anaamini hali itakuwa shwari.

Jenerali Mabeyo amesema kwa sasa vyombo vya usalama vinashughulika na hoja ya msingi ni kutaka kujiridhisha silaha zinapotoka na watu ni wa aina gani hivyo watu waviache vyombo vya ulinzi vifanye kazi yake na kuacha kutoa majibu haraka. Ameendelea kwa kusema tukio linapotokea lazima liangaliwe limetokeaje, chanzo nini na dhamira yake.

Swala la pili aliloongelea Jenerali Mabeyo ni uzoefu walionao, vijana wanaofanya uhalifu hawajapitia Jeshi la Kujenga Taifa hivyo wana imani vijana wao wote wanaopitia JKT wanakuwa na nidhamu. VIDEO:

Vijana ACT Wazalendo Wafunguka.."Bunge Limepoteza Imani yake Kwa Umma kwa Kiwango Kikubwa"

$
0
0
Katika taarifa ya Ngome ya Vijana iliyotolewa leo September 13, 2017 kupitia kwa Katibu wa Itikadi, Mawasilano na Uenezi, Karama Kaila imeridhia Zitto Kabwe kuitikia wito na kueleza hoja tano kuhusu Bunge na mwenendo wake.

1. Bunge limepoteza imani yake kwa umma kwa kiwango kikubwa Sana.

Jambo hili lisipochukuliwa hatua za haraka na makusudi na Bunge itafika wakati kujitambulisha Kama Mbunge itakuwa ni aibu mbele ya Jamii.

2. Bunge limepoteza nguvu mbele ya serikali ndiyo maana leo taarifa ya Kamati teule ya bunge kuhusu madini imeshindwa kujadiliwa ndani ya bunge na kuwa Na maazimio badala yake imepelekwa moja kwa moja serikalini.

Kwa Jambo hili Bunge linapaswa kurudi kusimamia kanuni zake ilizojiwekea ili mambo Kama haya yasifanyike tena.

3. Bunge limeshindwa kuwapa wabunge ulinzi wa kutosha hasa kipindi ambacho Bunge linaendelea na hata linapoahirishwa pamoja na wabunge kutoa taarifa ya kuwa usalama wao upo mashakani.

Ngome ya Vijana tunaitaka Kamati ya bunge ya ulinzi Na usalama ivunjwe Na kuundwa upya.

4. Muendelezo wa wabunge kuitwa Kwenye Kamati ya maadili kwa sababu zisizo na kichwa wala miguu hakiashirii mwisho mwema na kina lengo la kuwafanya wabunge washindwe kutimiza wajibu wao wa kuisimamia serikali

Ngome ya Vijana tumeridhia Kiongozi wetu wa Chama Ndugu Zitto Kabwe kuitikia wito wa Kamati ya maadili Ila Kamati itambue kuwa maamuzi yoyote itakayochukua dhidi yake yasiyostahili Vijana wa ACT-wazalendo nchi nzima tutayapinga kwa vitendo.

5. Mwisho Kitendo cha Bunge kuridhia kuzimwa kwa Bunge kurushwa moja kwa moja Ngome ya Vijana tunathubutu kusema hapa ndipo Bunge letu lilipoamua kujichimbia Kaburi.

Karama Kaila
Katibu Itikadi, Mawasilano Na Uenezi,
Ngome ya Vijana ya ACT-Wazalendo Taifa,
13/9/2017

Jirani Yangu Ananiomba Nimpige Picha Akiwa Uchi Mara Kwa Mara...

$
0
0
Sisi ni majirani tumetokea kuzoeana tu kidogo kwakuwa mwenzangu  yeye ni mwenyeji mimi nimemkuta tu hapo nilivyo hamia, lakini naona kama kuna mazoea fulani ya ajabu, hii ni mara ya tatu huyu dada ananiomba nimpige picha tena akiwa amevaa kiajabu ajabu, siku nyingine anadiriki hata kunigongea chumbani kwangu ili nitoke tu nimpige picha halafu aendelee na shughuli zake...leo Kaniomba nimpige akiwa na chupi tuu kitandani kwake sasa imekuwa kero Simuelewe kabisaaaa Wadau..

Naomba Ushauri

Ray


Vyakula 6 ambavyo wanaume hawatakiwi kula Kamwe

$
0
0
Katika post hii utajifunza vyakula mbalimbali ambavyo wanaume hawatakiwi kula ili kubaki na afya bora wakati wote. Kuna vingine unaweza kuwa unavitumia kila siku bila mwenyewe kujuwa.

1. Punguza kula vyakula feki kuzuia kupoteza nywele


Moja ya matatizo makubwa upande wa urembo kwa wanaume ni kupoteza nywele (upala). Lakini kama unatafuta kitu cha kukilaumu dhidi ya tatizo lako la kunyonyoka nywele basi ni hiyo sahani yako ya chipsi unayokula kila siku.  Vyakula feki (junk foods) ni hivyo vinapatikana kwenye fast foods na takeaway centers nyingi hasa mijini kadharika vyakula vile vyote vya kwenye maboksi.

Vyakula hivi feki vina kiasi kingi mno cha lehemu (cholesterol) na lehemu hii hupelekea kile huitwa kwa kitaalamu kama ‘pregnenolone’ na kupelekea kiasi kikubwa cha ‘dihydrotestosterone’ (DHT) na hatimaye kupotea kwa nywele kichwani a.k.a upara.

Kunyonyoka kwa nywele kunaweza kuwa ni jambo la kurithi (genetics) lakini vile vile aina ya chakula unachokula kinaweza kuwa kinahusika moja kwa moja.

2. Punguza kunywa pombe au acha kabisa kuzuia kuota matiti

Wanaume wengi wanaokunywa bia kupita kiasi huwa na uwezekano mkubwa wa kupatwa na tatizo la kuota matiti kama wamama tatizo lijulikanalo kwa kitaalamu kama ‘gynecomastia’.

Kwenye bia au pombe mara nyingi hakuna lishe ya moja kwa moja na hivyo hukufanya ujisikie njaa au hata kuongzeka kwa njaa zaidi na ndiyo sababu unaambiwa kama huna uhakika utakula wapi ni bora usinywe pombe ili kulinda afya yako.

Kwenye bia kuna kitu kama homoni ya oestrogen ya kupandikizwa na hivyo unywaji pombe kupita kiasi kuna uhusiano wa moja kwa moja na matokeo ya wanaume kuwa na matiti kama wanawake.

3. Acha kutumia mafuta ya mboga mboga kuepuka saratani ya tezi dume

Mafuta yatokanayo na mboga mboga au mimea yamekuwa yakipigiwa debe kwa miaka mingi na watu wanaojihusisha na lishe na wale wenye hasira sana na mafuta yatokanayo na wanyama. Hata hivyo leo nakujulisha mafuta hayo si salama sana kutumika na mwanaume kila siku. Hili limekuja hasa kutokana na kuongezeka kwa magonjwa ya moyo na lehemu na watu wakahimizwa kutumia mafuta ya namna hiyo.

Lakini mafuta haya ya mboga mboga ndiyo kitu kibovu kabisa unatakiwa kukiepuka ili usipatwe na saratani ya tezi dume.  Linapokuja suala la kujilinda saratani ya tezi dume basi mafuta yenye omega 3 ndiyo suluhisho la kudumu na siyo omega 6 kama ilivyo kwenye vyakula vingi vya kwenye makopo, mafuta ya alizeti, maharage ya soya, mafuta ya  canola na mafuta ya corn na mengine yote yenye omega 6.

4. Popcorn

Popcorn au bisi ni chakula kingine mwanaume hatakiwi kula, hupikwa kwa kutumia mafuta yasiyo na afya, sodiamu nyingi na ni chanzo cha baadhi ya kansa. Kuna kitu kinaitwa ‘Diacetyl’ kinachopatikana kwenye popcorn ambacho kinahusika na kusababisha kansa na kuna kingine kiitwacho ‘Perfluorochemicals’ ambacho huathiri tezi ya thyroid na ugonjwa wakati huo huo husababisha ugonjwa wa kupungukiwa umakini ujulikanao kwa kiingereza kama ‘Attention-deficit/hyperactivity disorder (ADHD)‘.

Ni vizuri kuacha kula popcorn

5. Mkate mweupe


Mkate mweupe una wanga mwingi zaidi usio na faida. Kwenye hatua za kutengeneza mkate mweupe vitamini zote za kundi B hupotea, hupotea pia nyuzinyuzi (fiber). Siyo hivyo tu mkate mweupe umesemekana kuwa ni sababu ya ugonjwa wa kisukari na kuongeza uzito zaidi mwilini wakati huo huo ukisababisha tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu sana.

Vingine vinavyofanana na na hilo ni ugali wa sembe, tambi nyeupe, chai ya rangi na kahawa.

Kula mkate ambao ngano yake haikukobolewa (brown bread), kula ugali wa dona na chai unaweza kutumia tangawizi au mdalasini badala ya majani ya chai.

6. Chumvi ya mezani

Chumvi ya mezani ile ya unga nyeupe haifai kwa mwanaume. Kila mmoja amesikia chumvi hii husababisha shinikizo la juu la damu na pamoja na hayo bado sehemu kubwa ya watu wanatumia chumvi hii.

Chumvi ya mezani husafishwa kwa kuondoa madini madini na hupitishwa katika joto la nyuzi joto 1093. Kwa hiyo uliyonayo sasa ni asilimia 40 ya sodiamu na asilimia 60 ya kloridi, na kisha kemikali kama vile ‘aluminium silicate’ huongezwa ili kuifanya isishikane na hivyo kubaki katika hali ya unga. Aluminium silicate ni sumu kali inayoharibu mfumo wetu wa fahamu. Inatajwa kuwa ni miongoni mwa sababu zinazosababisha ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu (Alzheimer).

Chumvi ya mawe ya baharini ile ambayo haijapita kiwandani (unrefined sea salt) ndiyo nzuri zaidi kwa afya ya mwanaume.



Kama una swali uliza hapo kwenye comment Dr Fadhili Paulo Atakujibu


Dawa za Asili zinazoondoa Maumivu Wakati wa Hedhi Kwa Mwanamke

$
0
0
Wanawake wote hutokewa na kupata na hedhi mara moja kila mwezi na ni jambo la kawaida kwao kama wanawake. Hata hivyo wengi wao hupatwa na matatizo siku chache kabla au wakati wa siku zao, matatizo haya hutofautiana toka mwanamke mmoja hadi mwingine kutegemeana na afya ya muhusika.

DALILI ZA TATIZO HILI NI KAMA ZIFUATAZO:

Siku chache kabla ya hedhi, mhusika hupatwa na:

1. Kichwa kuuma
2. Msongo wa mawazo (stress)
3. Hofu na hasira za hapa na hapa
4. kuvimba sehemu za siri
5. Kukosa usingizi na
6. Matiti kujaa

Hali hii hutokea kwa sehemu kubwa kama matokeo ya homoni kutokuwa kuwa sawa (Homone imbalance) na hali hii inaweza kukoma ndani ya siku 1 baada ya kuanza hedhi.

Wengine hupatwa na maumivu makali sana wakati wa hedhi. Maumivu hayo huwapata akina mama ama siku mbili ama tatu kabla au mara tu waanzapo siku zao. Hali hii pia inasababishwa na kutokuwepo kwa uwiano wa homoni mwilini, ambako kumesababishwa na ukosefu wa virutubisho fulani.

Wengine hutokwa na damu nyingi kuliko kawaida au kukaa katika siku za hedhi kwa kipindi kirefu kuliko kawaida. Kuna sababu nyingi zinazoweza kuchangia hali hii, ikiwemo kuugua kwa muda mrefu, kupatwa na hofu, huzuni, mshtuko na sababu nyingine za kitabibu.

Dawa zinazoondoa maumivu wakati wa hedhi

1. JUISI YA MBOGA ZIFUATAZO

Tumia juisi ya mchanganyiko huu: Kotimiri (Parsley), viazi pori (Beet Root), karoti au matango. Tumia asali mbichi ukitengeneza juisi hii. Hii kotimiri inapatikana kirahisi Dar na Zanzibar ni mboga mboga inayotumika zaidi kwenye mahoteli ya kitalii. Mboga hii inacho kitu mhimu sana kijulikanacho kama ‘Apiol’ amabcho kazi yake kuu ni kurekebisha na kuweka sawa homoni za kike.

Changanya kwa ujazo sawa yaani kama juisi ya kotimiri ni kikombe kimoja basi ya kiazi pori nayo kikombe kimoja kadharika kwa matango. Juisi hii ni dawa tosha ya maumivu wakati wa siku za hedhi na imethibitika kuwa bora kuliko dawa nyingi za kizungu.

Kunywa glasi moja kutwa mara 2.

2. TANGAWIZI

Tangawizi ni moja ya dawa nzuri sana ya asili linapokuja suala la kutibu na kutuliza maumivu wakati wa hedhi. Tengeneza chai ya tangawizi na unywe kikombe kimoja (robo lita/ml 250) kutwa mara mbili mara baada ya chakula cha mchana na baada ya chakula cha usiku. Unaweza kuweka mazoea ya kunywa dawa hii kila siku 3 kabla ya kuanza siku zako na ukaendelea hivyo wakati wote unapokuwa kwenye siku, na unashauriwa kuishi hivi kila mara ili kujijengea kinga mwili wako dhidi ya tatizo hili.

3. UFUTA

Dawa nyingine inayotibu tatizo hili ya asili isiyo na madhara yoyote kwa mtumiaji ni UFUTA. Dawa hii pia ni nzuri kwa wale wenye tatizo hedhi kidogo.

Hata hivyo kwenye majaribio kadhaa ufuta umeonekana kufanya kazi vizuri zaidi kwa wasichana wadogo kuliko kwa wamama watu wazima.

Namna ya kutumia: Saga ufuta kiasi upendacho na utumie kijiko kikubwa kimoja cha chakula ndani ya kikombe kimoja (robo lita au ml 250) kutwa mara 2.

Ufuta pia unaweza kupondwapondwa kiasi cha kiganja cha mkono wako na kuchanganywa katika maji yako ya kuoga ya uvuguvugu na utapata nafuu kubwa pia dhidi ya maumivu haya hasa ukianza kutumia siku 3 kabla ya kuanza siku.

4. PAPAI

Tuna kila sababu ya kusema ahsante kwa Mungu kwa kutukirimia mimea na miti mingi ambayo ni dawa kwa maradhi mengi yanayotusumbuwa.

Papai ni moja ya dawa za asili zinazoondoa maumivu wakati wa hedhi na linatajwa na watafiti mbalimbali kuwa ni msaada mkubwa kwa wasichana wanaopatwa na tatizo la kutokuona kabisa siku zao kama matokeo ya stress au mifadhaiko mingi ya kimaisha.

Ili liwe dawa unashauriwa kula kila mara tunda hili hasa lile ambalo halijaiva sana lakini tayari limekoaa na hata ile rangi ya ukijani iwe haijaondoka yote. Hii iwe ni tabia yako kusishi hivi kama una tatizo hili la maumivu wakati wa siku zako au hupati kabisa kuona siku.

Papai huweza haya yote kutokana na sifa yake kuu ya kuweza kulainisha misuli katika njia ya uzazi na hatimaye kuwezesha utokaji wa hedhi kuwa mrahisi bila maumivu yoyote. Jaribu hili na uniletee majibu.

5. MSHUBIRI (Aloe vera)

Hii ni dawa nyingine ya maajbu ya asili ambayo inatibu maradhi mengi mengi sana mwilini bila idadi ikiwemo hili la kupunguza au kuondoa kabisa maumivu wakati wa hedhi.

Matumizi: Changanya jeli ya Aloe vera (maji maji ya mshubiri) na pilipili manga nyeusi ya unga kidooogo, meza kijiko cha chakula kimoja mara tatu kwa siku kila siku hadi maumivu yatakapoacha.

6. NDIZI

Utashangaa sana kuona kumbe hata ndizi ni dawa na ingekuondolea maumivu hayo bila gharama yoyote. Wataalamu wamethibitisha pasipo na shaka kuwa ndizi mbivu zinao uwezo wa kutibu tatizo hili.

Nguvu ya ndizi kutibu hili zinatokana na ukweli kwamba ndizi ina B6 na madini ya chuma vitu viwili vinavyoweza kusaidia kurekebisha kiwango cha sukari, kuondoa au kupunguza uwezekano wa kupata maradhi ya kupooza, kuweka sawa shinikizo la damu na kudhibiti tatizo la upungufu wa damu kama matokeo ya siku zako.

Matumizi: Kula ndizi mbivu mbili mpaka tatu siku 4 kabla ya kuanza siku zako na wakati wote unapoendelea na siku zako. Kwa kifupi jizoeshe kuongeza tunda hili kwenye kila mlo ikiwa wewe ni mhanga wa tatizo hili la maumivu wakati wa hedhi na hutachelewa kuanza kuona tofauti. Kumbuka pia kutumia chumvi ya kutosha (hasa ya mawe kwenye vyakula vyako) kama unakula ndizi mara kwa mara ili kuiweka sawa potasiamu iliyomo kwenye ndizi ambayo nayo ikizidi huleta tatizo la kukakamaa kwa mishipa mwilini.

7. MAJI YA KUNYWA

Hii ndiyo dawa namba 1 na mhimu zaidi kuliko zote na ni ya lazima itumike na yeyote. Sababu kuu ya maumivu haya kama nilivyoyapeleza mimi ni mwili kutokuwa na maji ya kutosha na hii ni matokeo ya watu kusubiri ndipo wanywe maji jambo ambalo ni kosa kubwa tunalifanya dhidi ya miili yetu bila kujuwa. Kila siku iendayo kwa Mungu kunywa maji lita 2 mpaka lita 3, kunywa kidogo kidogo kutwa nzima, maji ya kawaida siyo ya kwenye friji na hutakaa uone maumivu katika siku zako. Mke wangu hajawahi kusikia maumivu haya sababu nyumbani kwangu suala la kunywa maji linajulikana tangu siku ya kwanza.

8. MDALASINI

Tengeneza chai ukitumia unga wa mdalasini, kunywa kikombe kimoja kutwa mara 2 wakati wote wa siku zako au anza siku 2 kabla pia unaweza kuweka mazoea ya kuwa hiyo ndiyo chai yako kila mara ili iwe kama kinga. Kumbuka kutumia asali badala ya sukari kwenye hii chai

9. JUISI YA KAROTI

Kunywa juisi ya karoti fresh glasi 1 kutwa mara 2 wakati wote wa siku zako, unaweza pia kujenga mazoea ya kula karoti tu moja hadi mbili kila siku kujenga kinga dhidi ya ugonjwa huu. Juisi itakuwa rahisi kwa wale wa mjini na ambao wana blenda pia, kijijini kula karoti fresh kila siku.

10. MCHAICHAI

Kama unasumbuliwa na tatizo hili kila mara basi hamia kunywa chai ya mchaichai kikombe kimoja kutwa mara 2 kila siku huku ukitumia asali badala ya sukari. Kama unaweza tengeneza juisi ya mchaichai na unywe kikombe kimoja kutwa mara 2 pia wakati wote wa siku zako.

Dawa ni hizo na hakuna sababu ya kuendelea kuteseka na maumivu haya bila sababu. Utaniuliza nitumie kwa muda gani? hivyo ni vyakula tu unaweza kutumia mpaka utakapopona na unaweza kuendelea kuzitumia hata kama huumwi chochote. Unaweza kutumia moja tu au ukachagua mbili hadi 3 ukatumia kwa pamoja ila kumbuka dawa namba 7 ni lazima.

MAMBO YA MHIMU KUZINGATIA KILA SIKU:

1. Kula matunda na mboga majani kwa wingi kila siku, matango, matikiti maji nk

2. Jishughulishe na mazoezi madogo madogo ya viungo

3. Oga maji ya moto (kama unasumbuliwa na hili tatizo kila mara)

4. Tumia mafuta ya samaki kila mara kwenye vyakula vyako au unaweza kunywa tu yenyewe kijiko kidogo kimoja cha chai kutwa mara 1 kila siku

5. Pata muda wa kutosha wa kulala usingizi masaa 7 mpaka 8 kila siku

6. Acha kula nyama nyekundu, sukari (tumia asali badala yake), usitumie unga wa ngano mweupe (uliokobolewa), usitumie sembe (kula dona).

7. Achana na msongo wa mawazo (stress)

8. Usivae nguo za kubana sana wakati wa siku zako

9. Acha chai ya rangi, kahawa, vilevi vyote, soda na vinywaji baridi vingine vyote (hii ni kwa mgonjwa usinielewe vibaya, kama huumwi chochote vitumie isipokuwa vilevi havifai kwa yoyote uwe unaumwa au huumwi).

Source:FadhiliPaulo

Kutana na Mtabibu wa Magonjwa Sharifu Seif Mohamed Kutoka Mombasa Kenya Sasa Yupo Tanza

$
0
0
KUTANA NA SHARIFU SEIF MOHAMED KUTOKA MOMBASA KENYA sasa yupo TANZANIA, pia atayatembelea maeneo mbali mbali ndani ya nchi popote pale atakapo hitajika,

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 72 TU)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, anatumia kitabu cha Qur'an, dawa za kiarabu, njiwa, juju za mombasa, na majini kwa kumtuliza mke, mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, Anazo dawa za napenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji, miguu kuwaka moto na kuvimba na n.k, Je? Umezunguka bila mafanikio na unahitaji Pete ya bahati iliyo ambatanishwa na jini mali? Kusafisha nyota , mafanikio ya maisha bila mashart, mvuto wa  biashara, zindiko la nyumba na mashamba, umaarufu, kupata kazi  kulingana na elimu yako, kupandishwa cheo kazini, na mengine mengi ya siri, Je  umehangaika kupata mtoto bila mafanikio? Wasiliana na mtaalam huyu  kwani yeye ufaulu pale wote  walipo shindwa, pia humaliza kazi  zilizo shindikana kumalizwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 24 tu, Pia anatibu kwa njia ya simu popote pale ndani au nje ya nchi, Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi:

Mobile + imo  +255 654-836970
Mobile + WhatsApp +255 756-033670

NB: kama unahitaji msaada ni  bora kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate  msaada kwa haraka.

Hivi Ndivyo Korea Kaskazini Ilivyoiweka Matatizoni Tanzania

$
0
0

Umoja wa Mataifa unaichunguza Tanzania kwa tuhuma za kikuikwa vikwazo vua kisilaha ilivyoiwekea Korea Kaskazini ambapo inadaiwa kuwa licha ya vikwazo vilivyowekwa, Tanzania imeendeleza biashara ya silaha na nchi hiyo.

Katika ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa Septemba 5 mwaka huu imeeleza inachunguza madai ya kampuni ya Korea Kaskazini, Haegeumgang Trading Corporation kuwa inafanyakazi ya kuboresha eneo la kurushia makombora la Tanzania.

Mbali na hiyo, Umoja wa Mataifa umedai kuwa kampuni hiyo inafanyia maboresho rada za ulinzi za Tanzania.

UN imeeleza kuwa, thamani ya mkataba huo wa kijeshi kati ya Tanzania na Korea Kaskazini ambao sio halali ni €10.49 million (Tsh bilioni 28).

Katika ripoti hiyo, UN wameeleza kwamba Tanzania bado haijatoa ufafanuzi kuhusu madai hayo.

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje, Dr. Suzan Kolimba alisema kuwa hawajapokea taarifa yoyote kutoka UN na hivyo kwa sasa hawawezi kuzungumza kuhusu madai hayo yaliyotolewa.

Mbali na Tanzania, mataifa mengine yanayochunguzwa na UN ni kwa kuendeleza biashara na Korea Kaskazini ni Angola, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Eritrea, Msumbiji, Namibia, Syria na Uganda.

Korea Kaskazini imekuwa ikiwekewa vikwazo mbalimbali siku za karibuni kutokana na kuendelea na majaribio ya silaha za nyuklia kinyume na makubaliano ya UN.

Kiongozi wa nchi huyo, amewahi kunukuliwa akisema kuwa nchi hiyo kwa sasa ina makombora makubwa yanayoweza kulenga sehemu yoyote ya dunia. Moja ya kombora ambalo inadaiwa Korea Kaskazini wanalo, lina uwezo kuliko makombora mawili ya Hiroshima na Nagasaki yakiwekwa pamoja.

Nchi mbalimbali ikiwwamo Marekani na China zimekata au kupunguza biashara na Korea Kaskazini ikiwa ni lengo la kuishinikiza nchi hiyo kusitisha majaribio ya silaha za nyuklia.

Zitto Kabwe Kupigwa Marufuku Kuzungumza Bungeni.......

$
0
0
Kwa mara nyingine tena Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai (Mb) amemuagiza Zitto Kabwe kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya Bunge kuhojiwa kutokana na kuendelea kuudhalilisha mhimili wa Bunge.

Spika Ndugai ametoa agizo hilo leo katika kikao cha Bunge vinavyoendelea mjini Dodoma ambapo amesema, Zitto Kabwe ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini ameendelea kudhalilisha mhimili huo licha ya kuwa ameonywa na kutakiwa kufika mbele ya kamati kujieleza sababu za kufanya hivyo.

Akizungumza baada ya kipindi cha maswali na majibu, Ndugai amesema kuwa anaweza kumzuia Zitto asiongee bungeni katika kipindi chote cha ubunge na kwamba hatakuwa na kitu cha kumfanya.

“Zitto utapambana na spika kweli! Naweza kukupiga marufuku kuongea humu mpaka miaka yako yote ikaisha na hakuna pakwenda. Hakuna cha swali, hakuna cha nyongeza, hakuna cha kuongea chochote humu ndani ya Bunge. Utanifanya nini?”

Aidha Spika Ndugai amemtaka Mbunge Zitto Kabwe kupambana na kitu kingine lakini sio yeye.

Awali jana Zitto alitakiwa kufika mbele ya kamati kuhojiwa baada ya kusema kuwa mhimili wa bunge umewekwa mfukoni na mhimili fulani wa serikali.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter jana, Zitto aliendelea kuandika habari zilizokosoa namna Spika Ndugai anavyouongoza mhimili huo huku akisema kwamba hajafika hata asilimia 10 ya Annie Makinda.

Mlinzi wa Meja Jenerali Aliyejeruhiwa Kwa Risasi Dar Akamatwa

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linawashikilia watu wawili akiwemo mlinzi wa Suma JKT na mhudumu wa benki ya NBC tawi la Tangibovu ambao wanatuhumiwa katika tukio la kujeruhiwa kwa risasi Meja Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ), Vincent  Mritaba.

Kamanda wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa amesema leo Jumatano kuwa Septemba 11 mwaka huu saa 11 jioni maeneo ya Tegeta Masaiti jeshi hilo lilipata taarifa ya Mritaba kuvamiwa na watu wawili wasiojulikana ambao walimjeruhi na kumpiga risasi ya begani, tumnoni na kwenye paja la mkono wa kulia huku wakimpora kiasi cha Sh5 milioni.

Amesema tukio hilo lilitokea baada ya mstaafu huyo kutoka kuchukua fedha hizo katika benki ya NBC tawi la Tangibovu akiwa kwenye gari lake ya Volkswagen Amarok.

Mambosasa amesema alipofika nyumbani kwake alipiga honi na kufunguliwa geti na mlinzi wake Godfrey Gasper.

Amesema geti lilipofunguliwa pikipiki ilisimama hapo getini na watu wawili waliokuwa wamevaa helment walishuka na kulifuata gari huku wakiwa na silaha aina ya bastola ndipo walishambulia upande wa kulia wa dereva na katika kioo cha mbele.

"Huku wakimwamuru ashuke ambapo risasi zilimjeruhi maeneo ya begani, tumboni na kwenye paja la mkono wa kulia na kutokomea kusikojulikana kwa kutumia pikipiki waliokuja nayo," amesema Mambosasa.

Mambosasa amesema cha kushangaza wakati mlinzi huyo anaenda kufungua geti silaha yake aina ya shotgun yenye namba TZCAR9644 aliiacha kwenye kibanda cha ulinzi huku ikiwa chini ya kitanda.

Amesema baadaye watuhumiwa walimwambia akimbie katika eneo hilo na yeye alitii amri hiyo na kwenda mbali na tukio hilo jambo ambalo linatia shaka.

"Ninavyojua askari wa Suma JKT anapewa mafunzo ya ukakamavu haiwezekani uache silaha chini ya kitanda unakwenda kufungua geti kitu ambacho sikubaliani nacho,"amesema

Amesema walipofuatilia mawasiliano ya mmoja wa wahudumu wa benki hiyo walibaini kuwa alikuwa anapanga mipango na watu mbalimbali wanaokwenda katika benki hiyo. Hivyo msako mkali unaendelea ili kuwabaini watuhumiwa waliohusika katika tukio la kujeruhi kwa risasi afande huyo.

Pia alizungumzia kuvunjwa kwa ofisi ya wakili ya Prime Attoneys akieleza kuwa wanaendelea na msako mkali ili kuwabaini waliohusika katika tukio hilo na watakapokamatwa watachukuliwa hatua za kisheria.

Polisi yasikitishwa dereva wa Tundu Lissu Kutojisalimisha Polisi

$
0
0
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto ameeleza kusikitishwa kwao na kitendo cha dereva wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kutokufika polisi na kutoa maelezo yake.

Kamanda Muroto amesema hayo leo  Jumatano wakati akijibu swali la upelelezi unaendeleaje kuhusu tukio hilo.

Amesema upepelezi unaendelea kuhusu tukio la Lissu kupigwa risasi na watu mbalimbali wanaendelea kuhojiwa wakiwemo wamiliki nane wa gari aina ya Nissan ambazo zilikamatwa kuhusiana na shambulizi hilo.

“Wamiliki wa gari tumewahoji na tunapogundua hakuna muunganiko wowote basi tunaachana nao maana hakuna haja ya kuendelea kuwashikilia au kushikilia gari hizo,” amesema.

Hata hivyo Kamanda Muroto amesema anasikitishwa na kitendo cha aliyekuwa dereva wa mbunge huyo wakati wa tukio kutoonyesha ushirikiano kwa jeshi la polisi.

“Tunasikia yupo nje ya nchi na hadi leo hajaitikia wito wa kufika polisi kupata maelezo yake ambayo yangesaidia katika upepelezi wa tukio hilo.”

Lissu Hali Tete, Afya yake Hubadilika Kila Wakati...Waliomshambulia Kusomewa Albadiri...Magazeti ya Leo

$
0
0

Lissu Hali Tete, Afya yake Hubadilika Kila Wakati...Waliomshambulia Kusomewa Albadiri...Magazeti ya Leo

Breaking News: Magari ya Mwendo Kasi yagongana Maeneo ya Shekilango

$
0
0
Breaking News: Magari ya Mwendo Kasi yagongana Maeneo ya Shekilango
Mabasi ya mwendokasi yamegongana yenyewe kwa yenyewe hapa maeneo ya Shekilango. Huduma imesimama kwa muda sababu barabara ya Mwendo kasi ni nyembamba.

Ajali hii imetokea leo Asubuhi:




Kwa nini Alikiba Hapati offer za Matangazo ya Makampuni Makubwa Kama Diamond platnumz?

$
0
0
dIAMOND PLATNUMZ
Nnje ya mziki biashara ya matangazo kwa makampuni makubwa imekuwa inalipa wasanii wengi na hivi majuzi Diamond amevuta mkwanja wa Billioni 1 kukitangaza kinywaji cha ufaransa cha Bllaire

Lakini Kng Kba hapati offer za matangazo makubwa kwa nini?

Hana mvuto au hana Mnagement nzuri inayomuunganisha na makampuni?

Na kama hataki pesa ndogo kutoka kwa makampuni kwa nini bado anapiga show za bei raisi za fiesta na zile za vichochoroni za Cub za Uaya?

Bi Cheka Afunguka Anavyompenda Ali Kiba

$
0
0
Bi Cheka Afunguka Anavyompenda Ali Kiba
KWENYE ulimwengu wa muziki jina la Cheka Hija ‘Bi. Cheka’ siyo geni. Ni miongoni mwa wasanii waliojizolea umaarufu mkubwa kwa mashabiki kupitia Lebo ya Mkubwa na Wanawe iliyo chini ya Mkubwa Fella, huku swali la wengi likiwa ni ukimya wake kwa sasa kama ameacha muziki au laa.

Kwe-nye maho-jiano haya maal-umu ambayo mwa-ndishi wetu ame-fanya naye uso kwa uso nyumbani kwake, Bunju jijini Dar, utapata majibu ya maswali yako, songa nayo;
Swali: Habari yako Bi. Cheka, naona upo kimya vipi muziki umeacha?
Bi. Cheka: Naanzaje kuiacha fani yangu? Muziki upo kwenye damu, bado ninafanya ila tu watu hawajui.
Swali: Nakumbuka kuna kipindi ulikuwa na mgogoro na Fella, alikuahidi kukujengea, akakutelekeza, mliishia vipi?

Bi. Cheka: Sina tatizo naye, alinipa matofali kadhaa ya kujengea hii nyumba, mengine nikaongeza mwenyewe. Sitaki kumuongelea sana kwa sababu sipo kwake, nilivunja mkataba, ulikuwa wa miaka mitano, nikafanya minne.
Swali: Baada ya hapo hakukwambia kama anataka aendelee ‘kukumeneji’ na ikitokea akakwambia hivyo, je, utakubali?
Bi. Cheka: Ni kweli ninahitaji meneja wa kusimamia kazi zangu, lakini sipo tayari kurudi kwake kwa sababu tulishindwana.
Swali: Ni changamoto gani unakutana nazo katika kipindi hiki ambacho huna meneja?
Bi. Cheka: Kuna ugumu, ila ninashukuru Mungu kuna kijana anaitwa Jophrey aliniafanyia bure video ya ngoma yangu ya Cheka Bella Pansupansupa ambayo itatoka hivi karibuni.
Showbiz Extra: Kuna tofauti gani kwenye maslahi unavyofanya shoo sasa na ilivyokuwa kipindi cha nyuma wakati upo kwa Fella?
Bi. Cheka: Tofauti ipo japo siyo kubwa sana, kwa kuwa pesa ninayolipwa sasa sigawani na mtu.
Showbiz Extra: Unawezaje kujikimu kimaisha, kuna kitu unafanya mbali na muziki?
Bi. Cheka: Sina biashara yoyote, kinachopatikana siku zinaenda japo ninasumbuliwa na miguu, muda mwingine inavimba, ndo’ inanitesa kwenye matibabu, lakini hainizuii kufanya shoo.
Swali: Kuna baadhi ya wanaume wanaona fahari kutembea na watu maarufu, hakuna mtu alitejito-keza kukuoa?
Bi. Cheka: (Kicheko) wapo hao, kuna mmoja nd’o aliniacha hoi, alitaka anioe mke wa tatu na kuniahidi mambo kibao ikiwemo kunijengea na kunipa gari, nikakataa hivyo ninaishi mwenyewe na wajukuu wangu
Swali; Unazungumziaje soko la muziki kwa sasa?
Bi. Cheka: Hivyohivyo tu, naona wasanii wengi siku hizi muziki wao wanawaza kupondana tu kuliko kujali ubora wa kazi.
Swali: Ni mwanamuziki gani unamkubali kwa sasa?
Bi. Cheka: Nampenda sana Ali Kiba, kwa sababu muziki wake anaofanya ni wa kipekee, siyo wa kumuiga mtu, kama mimi ninavyofanya muziki wa peke yangu, pia ni kijana mstaarabu, hana mashauzi kama wengine, ananijua vizuri na hajawahi kuniringia, hiyo ndiyo sifa ya msanii.
Swali: Unazungumziaje kitendo cha wasanii kuvaa utupu jukwaani, inasaidia kufanya shoo kwa uhuru au ndo’ mambo ya kizungu?
Bi. Cheka: Ushamba tu unawasumbua, siyo lazima ukae uchi jukwaani ndo’ uonekane mjanja, siku hizi wamezidisha, wabadilike.
Swali: Mashabiki watarajie nini kutoka kwako?
Bi. Cheka: Watarajie kazi nzuri kutoka kwangu, sijafa, nikifa watasikia, wanipende na kunisapoti.
Swali: Ahsante kwa ushirikiano.
Bi. Cheka: Karibu tena.

Kampuni Zote za Madini na Gesi Nchini Zatakiwa Kufungasha Virago

$
0
0

Kampuni Zote za Madini na Gesi Nchini Zatakiwa Kufungasha Virago
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani amezitaka kampuni zote za madini na gesi nchini kulipa kodi stahiki na kwamba ambazo hazijaanza kupata faida mpaka sasa zifungashe virago.

Dk Kalemali alibainisha hayo juzi wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya gesi na mafuta nchini, ambao ulikuwa ukizungumzia ushirikiano wa Serikali na viwanda katika sekta ya mafuta na gesi.

Kauli hiyo inakuja wakati Serikali ikiwa katika mchakato endelevu wa kubaini upungufu uliopo katika Sekta ya madini, mpaka sasa tayari kamati nne zimefanya uchunguzi na kuwasilisha mapendekezo ambayo yanaonyesha uwapo wa udanganyifu katika uwekezaji huo.

Alisema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Fedha, watafanya ukaguzi katika kampuni mbalimbali ili kujiridhisha kama kweli hazipati faida.

Dk Kalemani alisema suala la kujua faida anayoipata mwekezaji ni mpaka kukaa naye na kupiga hesabu, suala ambalo TRA inatakiwa kufanya ili Watanzania waweze kunufaika na rasilimali zao.

“Kodi inayokwepwa zaidi katika sekta hizi ni baada ya kupata faida (Cooperate tax), hii inahitaji hesabu hivyo TRA na mamlaka nyingine zinazohusika zitafanya hivyo,” alisema Dk Kalemani.

Hata hivyo, wajumbe waliohudhuria mkutano huo walitoa mapendekezo namna Serikali na wazawa wanavyoweza kunufaika, kutokana na miradi inayofanyika.

Mwenyekiti wa Kampuni PanAfrican Energy Tanzania, Patrick Rutabanzibwa alisema Serikali inapaswa kuendeleza utaratibu wa kuwasomesha watu wake ili kupata ujuzi zaidi, namna shughuli hizo zinavyofanyika duniani.

“Nikiwa kijana mdogo nilikuwa nafanya kazi Wizara ya Nishati na Madini, nilipelekwa Uingereza kusoma ili miradi kama hii ikianza Serikali iwe na wataalamu wa ndani lakini kwa bahati mbaya ilichelewa mpaka nimestaafu ndiyo inakuja hii ya ujenzi wa bomba la mafuta,” alisema Rutabanzibwa.

Naye Mwenyekiti wa Kampuni ya Alliend Petroleum Service limited Tanzania, Moses Asanga alisema Tanzania na nchi nyingine zenye kiu ya kuona manufaa ya mafuta na gesi, zinatakiwa kuandaa kanzi data ya kampuni za ndani ambazo mwekezaji anapaswa kuzitumia wakati wa utekelezaji mradi.



Wanawake Hupoteza Hamu ya Tendo la Ndoa Ikilinganishwa na Wanaume

$
0
0
Wanawake Hupoteza Hamu ya Tendo la Ndoa Ikilinganishwa na Wanaume
Wanawake wana uwezo mkubwa wa kupoteza hamu ya kufanya tendo la ngono katika ndoa kulingana na utafiti wa tabia za ngono uliofanywa nchini Uingereza.
Utafiti huo umebaini kwamba huku wanawake na wanaume wakionekana kupoteza hamu ya tendo la ngono kutokana na umri wao, wanawake wengi hupoteza hamu hiyo wanapoishi na wapenzi wao kwa muda mrefu.
Kwa jumla hali mbaya ya afya mbali na ukosefu wa uhusiano wa kihisia unaathiri hamu ya jinsia zote mbili ya kufanya tendo la ngono.
Matokeo hayo yanatokana na mahojiano ya wanaume 5000 na wanawake 6,700 yaliochapishwa na shirika la BMJ Open.
Watafiti hao wa Uingereza wamesema kuwa matatizo ya hamu ya ngono yanafaa kutibiwa kwa kumchunguza mtu badala ya kutumia dawa.
Machungu
Mtaalam wa maswala ya ngono Ammanda Major amesema kuwa kwa binadamu kukosa hamu ya tendo la ngono sio swala lilisilokuwa la kawaida na kuna sababu nyingi tofauti ambazo wanaume na wanawake wanahitaji mabadiliko.
''Kwa wengine ni kawaida lakini wengine husababisha machungu mengi'' ,alisema.
Kwa jumla asilimia 15 ya wanaume na asilimia 34 ya wanawake waliofanyiwa utafiti huo walisema kuwa walipoteza hamu ya tendo la ngono kwa muda wa miezi mitatu ama hata zaidi katika mwaka uliopita.
Kwa wanaume, ukosefu huo wa hamu ya ngono ulikuwa juu miongoni mwa wanaume wa kati ya umri wa miaka 35-44 huku kwa wanawake ukionekana kati ya umri wa miaka 55 na 64.

Hii Hapa Sababu Iliyompeleka Ommy Dimpozi Polisi na Kuhojiwa kwa Masaa Matano

$
0
0
Hii Hapa Sababu Iliyompeleka Ommy Dimpozi Polisi na Kuhojiwa kwa Masaa Matano
September 13, 2017 Mwimbaji wa Bongofleva Ommy Dimpoz alionekana kwenye kituo kikuu cha Polisi Kati Dar Es Salaam akiwa amesindikizwa na watu wengine wawili wakiingia kituoni hapo majira ya Asubuhi, Ommy Dimpoz alionekana akiingia kituoni hapo mida ya saa tano wakati waandishi wa habari walipokwenda kwenye press Conference ya kamanda wa Polisi Mambosasa.

Hata hivyo Kamanda MamboSasa kwenye taarifa yake ya mchana kwa waandishi wa habari hakuzungumzia ishu yoyote ya Ommy Dimpoz kuhojiwa lakini taarifa za chinichini ambazo hazijathibitishwa inasemekana Ommy aliitwa kuhojiwa na polisi ni kwa sababu ya ile picha aliyopost akiwa amepiga na mama mzazi wa Diamond.

Trump Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Demokrat

$
0
0
Trump Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Demokrat
Rais wa Marekani Donald Trump amekutana na wanasiasa wawili waandamizi kutoka chama cha Demokrat katika bunge la Congress kujadili maswala tata, huku pande zote mbili zikisema mazungumzo hayo wakati wa chakula cha jioni ikulu ya white house yalikuwa yenye manufaa.
Katika taarifa, Chuck Schumer na Nancy Pelosi wamesema wamekubaliana kuunda mpango wa pamoja kuhusu usalama wa mipakani na Donald Trump.
Wanasema mpango huo unajumuisha kuwalinda wahamiaji wenye umri mdogo lakini haukujumuisha ujenzi wa ukuta kwenye mpaka na taifa la Mexico.

Nitapeleka Hoja Binafsi Bungeni Uchaguzi Mkuu Nchini Ufanyike Baada ya Miaka Saba- Nkamia

$
0
0
Nitapeleka Hoja Binafsi Bungeni Uchaguzi Mkuu Nchini Ufanyike Baada ya Miaka Saba- Nkamia
Mbunge wa jimbo la Chemba, Juma Nkamia (CCM) amethibitisha kuwa leo atapeleka hoja binafsi kwa spika wa bunge kuhusu uchaguzi mkuu nchini ufanyike kila baada ya miaka saba na isiwe mitano kama sasa ili kuepuka gharama kubwa ambazo huwa zinatumika.

Akifanya mahojiano kwa njia ya simu na mtangazaji wa EATV, Mh. Nkamia amesema kuwa yeye ameamua kupeleka muswada huo binafsi kwa spika wa bunge kutokana na serikali kutumia gharama kubwa za kufanya uchaguzi kwa wakati mmoja yaani ule wa serikali za mitaa pamoja na ule mkuu.
"Napeleka hoja au muswada binafsi kwa Spika wa bunge tulijadili hili kama linaweza kufanywa sheria lifanyike.  Ndani ya bunge kuna viongozi wetu wa chama kwa hiyo lazima nipeleke kwao ili kujadili na wao waweze kupitisha kama watakubaliana na mimi na kama ikifanikiwa kufika kwa rais basi iwe sheria ambayo itatuoongoza," amesema Nkamia.

"Nikipeleka hoja yangu kwa Spika nitachanganua gharama zinazotumika kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa pamoja uchaguzi mkuu. Tunaweza kufanya uchaguzi wote kwa pamoja kama wenzetu mfano Kenya wanakuwa na maboksi mengi sana wakati wa kura, hata sisi tunaweza kufanya kama wenzetu badala ya kutumia gharama mbili kwa kipindi kimoja" aliongeza Nkamia.
Aidha, Mh. Nkamia amefafanua kuwa aeleweke kuwa hajamlenga rais aliyoko madarakani ndiye aanze kwenda miaka saba bali ni kwa viongozi wote na kama wazo lake likitimia wakati Rais Magufuli akiwa madarakani nayo si vibaya.

"Muswada una 'process' zake kwani lazima upitie sehemu nyingi na kama ukishafika kwa wabunge ukajadiliwa na ikakubalika sheria ifanyiwe mabadiliko ndani ya sheria na rais akatia saini ndiyo itakuwa sheria kamili. Na ukifanikiwa kupita wakati Rais Magufuli akiwa madarakani ni vema tu kwani kuna matatizo gani?:", amehoji Nkamia.
Pamoja na hayo Mh. Nkamia amesema kuwa watu wengi na waoga wa kutoa hoja zao kwa kufikiria wananchi watamfikiriaje hivyo kwa upande wake huwa hana woga wowote linapokuja suala la kusimamia hoja.

Mabingwa Watetezi Real Madrid Waanza Vizuri Kwa Ushindi wa Mabao 3-0

$
0
0
Mabingwa Watetezi Real Madrid Waanza Vizuri Kwa Ushindi wa Mabao 3-0
Usiku wa Ulaya umeendelea usiku wa kuamkia leo kwa kukamilisha mechi 16 za ufunguzi wa hatua ya makundi.

Mabingwa watetezi Real Madrid wakiwa nyumbani Santiago Bernabeu wameibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Apoel. Mabao mawili kati ya hayo yakifungwa na Cristiano Ronaldo na kumfanya kuwa mchezaji mwenye mabao mengi zaidi katika UEFA pekee akiwa na mabao 107.

Liverpool wakiwa nyumbani wamelazimishwa sare ya 2-2 na wababe wao wa fainali ya EUROPA 2016 Sevilla. Huku Manchester City chini ya kocha mshindi wa UEFA mara mbili Pep Guardiola wakiiadhibu Fayenood ya Uholanzi mabao 4-0.
John Stone mlinzi wa kati wa Manchester City amejiwekea rekodi ya kuwa mlinzi wa kwanza kufunga mabao mawili sawa na Lionel Messi na Ronaldo katika hatua ya makundi Tottenham wakiwa Wembley wamelipiza kisasi kwa Borrusia Dortmund baada ya kuwachapa 3-1 Wajerumani hao.

Gabriel Jesus wa Man City ameungana na Romelo Lukaku kwenye orodha ya wachezaji waliofunga katika mchezo wao wa kwanza wa UEFA.



Viewing all 104809 articles
Browse latest View live


Latest Images