Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Niwaombe Wabunge wa CCM vaeni Uzalendo kwenye Hili la Nkamia

$
0
0
Tangu uhuru wabunge wanakaa miaka mitano mitano na mambo yana enda iweje sahizi ndio ionekane haitoshi?? Je hii ya kutaka miaka saba ni la JUMA NKAMIA peke yake?? Au kuna watu nyuma yake? Jamani mnatuongoza wananchi si miti , NKAMIA imekuwaje Tena? Miaka mitano kuwa michache imeanza leo tangu 1985?

Jamani msicheze nakatiba yetu mtuachie nchi ikiwa salama tunawaomba sana acheni ubinafsi na tamaa ya madaraka toshokeni kama walivyo tosheka walio waruhusu na ninyi mkaipata nafasi hiyo, maana kila walio waachia hizo nafasi nao wangekuwa na tamaaa wakaongeza mda kama matakavyo kufanya ninyi hakika hata ninyi msinge zipata nafasi hizo.

Ukimya huu wa watanzani na upole wao msitake kuwatumia vibaya msifikiri hawajui kitu, tafadhari sana msicheze na katiba ya nchi msutulazishe kutuongoza bila hiyari yetu miaka mitano haitoshi???  Wakati wengine wana tawala miaka minne wewe mitano haikutoshi ?

Kwa masikio yangu nilimsikia Mh. Rais akisema kwa kinywa chake kuwa katiba sio kipaombele chake na ndio maana hata kwenye kampeni hakuongelea katiba hivyo naamini kuwa Mh. Rais hatokuwa sehemu ya mpango huu maana alikiri mwenyewe kuto hangaika na katiba , sasa nitashangaa kama kayageuka maneno yake mwenyewe, ndio maana huenda haya ni matakwa na   NKAMIA na kundi lake kama hakuna aliye nyuma yake.

Jamii Forums

Kutana na Mtabibu wa Magonjwa Sharifu Seif Mohamed Kutoka Mombasa Kenya Sasa Yupo Tanza

$
0
0
KUTANA NA SHARIFU SEIF MOHAMED KUTOKA MOMBASA KENYA sasa yupo TANZANIA, pia atayatembelea maeneo mbali mbali ndani ya nchi popote pale atakapo hitajika,

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 72 TU)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, anatumia kitabu cha Qur'an, dawa za kiarabu, njiwa, juju za mombasa, na majini kwa kumtuliza mke, mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, Anazo dawa za napenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji, miguu kuwaka moto na kuvimba na n.k, Je? Umezunguka bila mafanikio na unahitaji Pete ya bahati iliyo ambatanishwa na jini mali? Kusafisha nyota , mafanikio ya maisha bila mashart, mvuto wa  biashara, zindiko la nyumba na mashamba, umaarufu, kupata kazi  kulingana na elimu yako, kupandishwa cheo kazini, na mengine mengi ya siri, Je  umehangaika kupata mtoto bila mafanikio? Wasiliana na mtaalam huyu  kwani yeye ufaulu pale wote  walipo shindwa, pia humaliza kazi  zilizo shindikana kumalizwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 24 tu, Pia anatibu kwa njia ya simu popote pale ndani au nje ya nchi, Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi:

Mobile + imo  +255 654-836970
Mobile + WhatsApp +255 756-033670

NB: kama unahitaji msaada ni  bora kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate  msaada kwa haraka.

Mwanamke Kalio Bwana, Kama Sura Hata Mbuzi Anayo

$
0
0
Nimekutana na hii Mahali:

"Mwanamke mwenye kalio halali na njaa hapa town hata awe na sura mbaya vipi
Hakuna mwanaume atakayegeuka nyuma kumuangalia mwanamke mwenye sura nzuri
Siku zote wanaume wanageuka nyuma kuangalia mwanamke mwenye kalio la kutosha.

Wanaohongwa magari na nyumba wengi ni wenye makalio makubwa, wenye makalio kama wamepigwa pasi wanaishia kuhongwa vocha tu.

Achana na Wezere Bana......KALIO KWANZA, Sura peleka kwa mzee wako"

Historia Fupi ya Mwanamapinduzi Che Guevara, Alivyokamatwa na Kuuawa Kikatili

$
0
0
Jina kamili : Ernesto Guevara

Kazi : Daktari, mwanamapinduzi wa kijamaa (marxist)

Uraia : Argentina

Kuzaliwa : June 14 1928

Kufariki : October 9, 1967 ,Bolivia milima ya La heguera

Chanzo cha kifo : kuuwawa kwa kupigwa risasi

Kama kijana msomi wa shahada ya udaktari, che Guevara alisafiri nchi nyingi sana huko bara la Amerika ya kusini na rafiki yake, akawa ni mtu mwenye uchungu mkubwa kuona maisha ya dhiki,njaa, magonjwa nchi za America ya kusini, akawa na mwamko mkubwa kubadili hali ile kwa kuwa aliamini ya kuwa mfumo wa ubepari ndio chanzo kikubwa kilichokuwa kinaitafuna Latin America.

Miaka ya 50 akiwa anasoma udaktari huko Mexico Che Guevara alikutana na Fidel Castro na Raul Castro ambapo watatu hao walipanga mapinduzi ya kumg’oa raisi wa Cuba wakati huo Fulgencio batista ambaye alikuwa na huhusiano wa kimaslahi na America, Che akapata nguvu na uaminifu mkubwa kutoka kwa Fedel Castro na kupandishwa kuwa kiongozi wa wanamgambo (guerilla insurgents)

Punde tu baada ya Fulgencio batista kukimbia CUBA,Che alihusika kama mtu muhimu katika serikali ya Cuba iliyoongozwa na Fidel Castro, akiwa kama Gavana wa benki kuu ya Cuba ambapo saini yake ilianza kutumika katika noti za CUBA , baadae kama waziri wa kilimo wa Cuba.

Mwaka 1964 akiwa kama mmoja ya msafara wa watu wa serikali ya Cuba umoja wa Mataifa New York MArekani, aliweza kupata “sifa” ya “mwanamapinduzi halisi wa kukumbukwa” pale alipotoa hotuba ndefu katika ukumbi wa UN akilaumu wazi ukimya wa Umoja huo juu ya kilichokuwa kinaendelea Afrika ya kusini (ubaguzi wa Rangi) alinukuliwa akisema

“wale wanaoua watoto wao na kuwabagua kila siku kwa sababu ya rangi ya ngozi zao, wazungu wanawaua watu weusi na hawakamatwi, serikali ya kikaburu inawalinda wauaji, na mbaya Zaidi inawaadhibu watu weusi kwa kuwa tu wanatataka haki zao na utu wao, vipi watu hawa (makaburu) wakaitwa watetezi na walinzi wa Amani?”

MGOGORO WA CONGO – DRC
Miezi michache baada ya kutoa hotuba UN, Che alitoweka katika maisha ya kawaida “public life” na hakuna aliyejua alikwenda wapi mpaka baadae ilipokuja gundulika Che alikuwa akipigana sambamba na Laurent Kabila huko Congo dhidi ya wabeligiji na baadhi ya wapiganaji wa ki cuba waliokuwa Afrika, vita ambayo ilishindikana na akakimbilia Tanzania na kukaa maeneo ya karibu na ziwa Tanganyika na baadae Dar es salaam huku akiishi kwa kujificha

Baadae mwaka 1966 alirejea Cuba kumuaga kwa Fudel castro na kusafiri kwenda Bolivia kuendeleza harakati zake za kuzikomboa nchi za America ya kusini kutoka kwenye makucha ya Ubepari…aliingia Bolivia akiwa kama mfanyabiashara hasiyejulikana baada ya kunyoa upara, kuweka mvi bandia na kuyoa ndevu zake zote, akaweka kambi na baadhi ya wapiganaji wenzake aliowakuta Bolivia maeneo ya milima ya montane dry fores

KUKAMTWA NA KUUWAWA
Mwaka 1967, makachero wa Bolivia wakisaidiwa na CIA amabye alikuwa akiwakilsha ndugu Felix Rodriguez waligundua maficho ya ache na kundi lake huko milimani Bolivia, asubuhi ya October 8 mwaka 1967 wanajeshi takribani 1,800 walizingira maeneo yoote ya milima walikokuwa wamejificha akina Che na ikapiganwa vita ya masaa kadhaa na Che akipigwa Risasi za miguu na kukamatwa na wenzake,

Yasemekana baada ya kuzidiwa katika mapigano yale alisema
“Usifyatue risasi, mi ni Che Guevara nina thamani kubwa kuwa hai kuliko kunikamata nimekufa”

Alifungwa kama na wenzake akakamatwa na kupelekwa kijiji cha La higuera ambapo baada ya raisi wa Bolivia ndugu kusikia amekamtwa alitoa amri auwawe haraka sana, wakati huo huo CIA walimtaka apelekwe Panama akahojiwe kwa kina na salama yake ili hasiuwawe alikuwa apelekwe America japo haikutokea.

Siku moja kabal ya kuuwawa alichukuliwa na baadhi ya wanajeshi na kupiga picha ya kumbukumbu na kesho yake akauliwa na askari mmoja aliyejitolea na kumpiga risasi sita za kifua na kufa palepale

Kabla hajapigwa risasi na muuaji wake haya ndio yalikuwa maneno yake ya mwisho

“Najua umekuja kuniua, shoot mtu mwoga wewe!!! na ufahamu utakua umeua mwanaume kamili”
Aliacha wake wawili na watoto watano

Watu 20 Wanaojihusisha na Mapenzi ya Jinsia Moja Wakamatwa Zanzibar

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi-Unguja linawashikilia watu 20, ambao ni wanawake(12) na wanaume(8) kwa tuhuma za kukutwa wakifundishana kufanya mapenzi ya jinsia moja.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi Mkoa wa Mjini Magharib, Hassan Nassir amesema watu hao wamekamatwa wakati wakipatiwa mafunzo ya namna ya kuzitambua haki zao yaliyokuwa yakitolewa na taasisi iliyotambulika kwa jina la Bridge Initiative.

“Ni kweli tuliweza kuwakamata kwa sababu walikuwa wakishiriki katika mapenzi ya jinsia moja kitu ambacho ni kinyume na sheria kisiwani zanzibar na ni ukiukaji wa sheria za Tanzania”, alisema Hassan pia akaongeza kuwa polisi wataongeza doria zao dhidi ya makundi kama hayo.

Mwezi michache iliopita Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed alitangaza vita kwa wanaojihushisha na biashara hiyo haramu na alipiga ‘stop’ taasisi zinazofadhiri watu hao.

Spika Ndugai Awashangaa Wabunge Zitto na Lema Kutumia Mitandao Kuzungumza Mambo Ambayo Hayana Mantiki

$
0
0
Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai, ameuchambua mkutano wa nane wa Bunge la 11, ikiwemo mivutano iliyojitokeza kati yake na baadhi ya wabunge wa upinzani na kazi za bunge zilizokuwa zikiendelea.

Akizungumza na Azam Tv, Spika Ndugai amesema kuwa yeye hana ugomvi na mbunge, Zitto Kabwe, Kubenea na Godbless Lema ambaye ni mbunge wa Arusha mjini.

“Bunge hili ni la wiki mbili ni la muda mfupi sana kwa kazi za bunge, wabunge wamefanya kazi vizuri wamelichambua kwenye level ya kamati, wamesikiliza maoni ya wadau na imefika hapa bungeni imejadiliwa kwa uwazi ikafanyiwa mabadiliko muhimu yaliyotakiwa kufanyika na baadae ikapitishwa, kwa ujumla wake tunawashukuru wabunge tunashukuru serikali kazi hii imefanywa vizuri kwa niaba ya Watanzania,” alisema Spika Ndugai.

Hata hivyo Spika Ndugai alipoulizwa kuhusu mivutano iliyotokea kati yake na Mbunge wa Kigoma, Zitto Kabwe, Said Kubenea, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema ni bora mwandishi akawauliza wahusika wenyewe, huku akisema kuwa yeye hana ugomvi na wabunge hao huku akisema walipokuwa wakifanya kazi za hapo bungeni wao hawakuwepo bungeni Dodoma walikuwa katika maeneo wanayoyajua wao, pia amekuwa akiwashangaa wabunge hao wakitumia mitandao na kujirokodi kuzungumza mambo mbalimbali ambao hayana mantiki.

Zitto Kabwe Asubiriwa na Polisi Kigoma

$
0
0
Jeshi la polisi mkoni Kigoma limesema wanamsubiri Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe awasili mkoani hapo, ili kuweza kutoa taarifa rasmi ya kuteketea kwa nyumba yake iliyopo Mwandiga mkoani Kigoma.

Akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi wa East Africa Television kamanda wa polisi mkoa wa Kigoma Ferdinand Mtui, amesema polisi inachelea kutoa ripoti hiyo kwa sababu mwenyewe mhusika (Zitto Kabwe) hayuko Kigoma, hivyo hawawezi kujua thamani ya mali ambazo zilikuwepo.

"Bado tunaendelea mpaka mwenyewe apatikane na yuko Dodoma, kwa sababu huwezi kujua gharama mpaka yeye mwenyewe awepo, na nyumba ambayo imeungua ni nyumba ndogo aliyokuwa anakaa mlinzi sio nyumba kubwa", amesema Kamanda Mtui.

Kwa upande wake Zitto Kabwe amewataka wananchi kuwa na subira juu ya ripoti ya tukio hilo, huku akiwashukuru wananchi waliosaidia kuzima moto huo.

"Nawashukuru Jeshi la Zimamoto, majirani zangu pamoja na wananchi wenzangu kwa ushirikiano walioutoa mpaka kuuzima moto, kwa sasa Jeshi la Polisi wanafanyia kazi kujua chanzo cha ajali, naomba wananchi wawe watulivu wakati polisi wanaendelea na uchunguzi husika", ameandika Zitto Kabwe.

Hapo jana moto uliteketeza nyumba ya Zitto Kabwe mkoani Kigoma ikiwa na  vitu ambavyo thamani yake bado haijawekwa wazi, lakini hakuna mtu aliyeathirika na ajali hiyo.

Madhara ya Kujichora Michoro Mwilini (Tattoo)

$
0
0
Wanasayansi wa afya ya jamii wanaonya kuwa michoro iliyotokana na rangi za madukani pamoja na vichoreo vyake, vinaweza kusababisha madhara ya kiafya kwa wahusika.

Watu wengi, wanaume kwa wanawake hupenda kuweka michoro mwilini kama mapambo yaani tattoo au namna fulani ya kiimani.

Baadhi ya rangi zinazotumika kuchora mapambo mwilini zinaweza kusababisha mzio wa ngozi katika eneo la mwili mahali palipo na tattoo. Mzio huu unaweza kutokea kipindi kirefu baada ya kuchora tattoo.

Tafiti nyingi za kitabibu pia zinaonesha kwamba, wino au rangi za tattoo zinaweza kusababisha uambukizo wa bakteria aina ya Mycobacterium cholonae.

Bakteria hawa wanaweza kusababisha magonjwa ya ngozi na nyama za mwili, matatizo ya njia ya mkojo, mfumo wa kupumua, magonjwa ya uambukizo kwenye mifupa na nyama za moyo.

Michoro hiyo pia huweza kusababisha homa ya uti wa mgongo na tatizo la macho.

Vilevile, vifaa vinavyotumiwa kuchora mapambo hayo hutumika kwa watu mbalimbali kwa wakati mmoja bila utaalamu sahihi wa kuvisafisha.

Hali hiyo huweza kusababisha vibebe vimelea vya magonjwa mbalimbali na kuyahamishia kwa wengine.

Hali hii inaweza kusababisha uambukizo wa magonjwa yatokanayo na virusi hatari kama vile virusi vya Ukimwi, virusi ninavyosababisha homa ya ini (Hepatitis B na C) au virusi vya malengelenge (herpes simplex virus).

Kumbuka, wakati wa kuchora tattoo, ngozi hutobolewa kwa mashine au sindano hadi kuifikia sehemu ya ndani kabisa. Hii ni hatari kwa afya yako.


List ya Wachungaji Matajiri zaidi Duniani 2017 hii hapa

$
0
0
Zipo list kibao za viongozi wa dini ambazo huonesha namna gani wanakuwa na ushawishi wa kuponya watu kiroho lakini fahamu pia kuwa zipo list za viongozi hao hao wa dini ambao wanatajwa kuwa na fedha nyingi zaidi duniani…na kwa mwaka huu wa 2017 tayari ninayo list ya wachungaji 10 wanaotajwa kuwa na fedha nyingi zaidi duniani.


10. Joseph Prince.
Dola Milioni 5 Ni Mchungaji kutoka Singapore ambaye anatajwa kuwa na utajiri wa Dola za Kimarekani Milioni 5. Mchungaji Joseph hufanya ibada ambazo pia hurushwa LIVE kwenye mtandao wa youtube hivyo kupata umaarufu mkubwa sana barani Asia na duniani.


9. T.B Joshua
Dola Milioni 10 Ni mzaliwa wa Nigeria na anatajwa kuwa na utajiri wa Dola za Kimarekani Milioni 10. Kwa Nigeria, mchungaji huyu ni maarufu kama Nabii na ana watu wanaomfuatilia kwenye mtandao wa Facebook zaidi ya Milioni 1.5.


8. Billy Graham
Dola Milioni 25 Huyu ni mchungaji wa Marekani na moja kati ya wachungaji wenye umri mkubwa. Alizaliwa mwaka 1918 na kusomea masomo Anthropolojia na Biblia. Anaripotiwa kuwa na waumini wanaomfuatilia zaidi ya Bilioni 2.2 na utajiri wa Dola za Kimarekani Milioni 25.


7. Kenneth Copeland
Dola Milioni 25 Anafahamika sana kwa ujumbe mkubwa wa mahubiri yake ambayo ni mafanikio na utoshelevu. Kabla ya kuwa Mkristo alikua mwanamuziki kazi iliyompa mafanikio makubwa. Moja ya nyimbo zake ni pamoja na “Pledge of Love” alioufanya mwaka 1957 na kuingia kwenye chat bora za Billboard kwa kushika namba 17. Yeye na familia yake wanaishi katika nyumba yenye gharama ya Dola Milioni 6.3


6. Creflo Dollar
Dola Milioni 27 Ni Mchungaji wa Marekani, na kama jina lake lilivyo, Mchungai huyu anamiliki gari ya thamani aina ya Rolls Royce, na nyumba tatu za gharama ya Dola Milioni 2.5. Mwaka 2013 alishitakiwa kwa kosa la kumshambulia mwanaye wa kike lakini baadaye kesi hiyo kuachwa kwa madai ya kutatua kifamilia.


5. Enock Adeboye
Dola Milioni 39 Mchungaji huyu yuko Nigeria. Kanisa lake la Redeemed Christian Church of God lina matawi 14, 000 ndani ya Nigeria pekee na katika nchi nyingine zaidi ya 100 nje ya nchi hiyo. Image result for Enoch Adeboye.



4. Benny Hinn
 Dola Milioni 42 Mchungaji huyu pia ni Mmarekani. Mafundisho yake ni kuhusu imani na uponyaji. Anaripotiwa kuwahi kuchunguzwa na Serikali ya nchi hiyo kwa kashfa za kutolipa kodi.


3. Chris Oyakhilome.
Dola Milioni 50 Mchungaji Chris ni miongoni mwa wahungaji matajiri kutoka Afrika ambaye anatokea Afrika Kusini. Tofauti na kuwa na waumini wengi kwenye matawi ya Kanisa lake mchungaji huyu pia anamiliki matawi ya kazi za misaada na elimu. Anamiliki vituo vitatu vya Televisheni ambavyo vinapata waangaliaji hadi Milioni 2.5 kila siku.


2. Bishop T.D. Jakes.
Dola Milioni 147 Askofu huyu anatokea Marekani na anaongoza Kanisa la Potter’s House. Amewahi kuonekana na Maraisi wa Marekani George Bush na Barack Obama ambao kwa nyakati tofauti wamemsifia mchungaji huyo kwa kuwa mwaminifu.


1. Bishop David Oyedepo
Dola Milioni 150 Huyu ndiye Mchungaji tajiri kuliko wote duniani ambaye anamiliki Kanisa lijulikanalo kama Winners Chapel. Kanisa lake lina matawi katika nchi 45 barani Afrika ikiwa ni pamoja na mengine nchini Dubai, Uingereza na Marekani.

Balozi Aomba Kumpeleka Rais Magufuli Marekani Wiki Tano

$
0
0
Kaimu balozi wa Marekani nchini Tanzania Dkt Inmi Patterson amesema kuwa angependa kumpeleka rais John Pombe Magufuli nchini Marekani kwa ziara ya wiki tano.

Kulingana na gazeti la The Citizen nchini Tanzania, alitoa matamshi hayo mjini Dar es Salaam hivi majuzi wakati wa sherehe fupi ya kumkaribisha afisa wa maswala ya umma katika ubalozi huo Bi Bribille Ellis.

''Mwalimu Nyerere alitembelea Marekani miaka 1960 kwa ziara ya wiki tano.
Wiki tano ni wakati mrefu na aliweza kutembelea miji kadhaa...Ningependa kumpeleka rais Magufuli kwa ziara ya wiki tano nchini Marekani'', alisema na kuvutia kicheko kutoka kwa umma uliokuwepo.
Gazeti hilo lilimnukuu bi Patterson akisema kuwa katika uzoefu wa uongozi na programu za kubadilishana kama zile zilizotekelezwa na Mwalimu Nyerere 1960 zimefuatiliwa kwa sababu zilikuwa muhimu katika kuimarisha uhusiano kati ya Marekani na Tanzania.

Akimnukuu mtangazaji maarufu wa redio nchini Marekani, Edward Murrow, Bi Patterson alisema kuwa kwa uhusiano wa taasisi na mataifa kuimarika , lazima uanze katika kiwango cha kibinafsi.
Rais Magufuli hajawahi kutembelea taifa lolote nje ya Afrika tangu alipochaguliwa kuwa rais mnamo mwezi Oktoba 25.

Amekuwa akisisitiza kwamba ana kazi nyingi za kufanya nchini na kwamba kile ambacho kinaweza kufanywa kimataifa kinaweza kufanywa na mabalozi wa Tanzania waliopo mataifa hayo.

KRC Genk yapigwa 2-1, Samatta atokea benchi dakika za mwishoni

$
0
0
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ametokea benchi usiku wa Jumamosi timu yake, KRC Genk ikifungwa 2-1 na mahasimu, Sint-Truiden katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A Ubelgiji uliofanyika Uwanja wa Stayen mjini Sint-Truiden, St.-Trond.

Samatta aliingia dakika ya 73 kuchukua nafasi ya mshambuliaji kinda wa umri wa miaka 21, Mdenmark, Marcus Ingvartsen dakika ya 73 wakati huo timu hazijafungana.

Lakini baada ya Nahodha wa Tanzania kuingia, Genk ikafungwa mabao mawili ya haraka haraka ndani ya dakika tano, kwanza Roman Bezus dakika ya 78 na baadaye Damien Dussaut dakika ya 83, kabla ya  Siebe Writers kuifungia bao la iufutia machoi dakika ya 88.

Huo unakuwa mchezo wa 62 kwa Samatta katika mashindano tangu Januari mwaka jana alipojiunga na Genk, kati ya hiyo mechi 36 alianza na mechi 23 ametokea benchi.

Katika mechi hizo, mshambuliaji huyo wa zamani wa African Lyon, zamani Mbagala Market na Simba zote za Dar e Salaam, amefunga jumla ya mabao 21.

Kikosi cha STVV kilikuwa: Lucas Pirard, Stelios Kitsiou, Jorge Teixeira, Sascha Kotysch, Casper de Norre/Dussaut dk80, Igor Vetokele/Jordan Botaka dk67, Charilaos Charisis, Steven De Petter, Jonathan Legear/Roman Bezus dk67, Yohan Boli na Alexis De Sart.

KRC Genk: Danny Vukovic, Joakim Mæhle, Omar Colley, Jakub Brabec, Jere Uronen, Ruslan Malinovskiy/Bryan Heynen dk88, Sander Berge, Alejandro Pozuelo, Thomas Buffel/Edon Zhegrova dk73, Marcus Ingvartsen/Mbwana Samatta dk73 na Siebe Writers.

KIMENUKA...Watu Watatu Wakamatwa na Polisi Kwa Kumuombea Tundu Lissu

$
0
0
Jeshi la Polisi jijini Dar es salaam, linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za kuratibu shughuli za maombezi maalum kwa ajili ya mbunge Tundu Lissu, katika viwanja vya TIP Sinza.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni Murilo Jumanne aliyekuwa eneo la tukio, amesema wameamua kuwakamata watu hao kwa kuwa wanatishia amani na utulivu wa nchi.

"Wale wenye nia mbaya ambao bila shaka wana ajenda binafsi ajenda ambazo kimsingi zina uelekeo wa kutishia masuala ya amani, mimi kama Kamnda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, siwezi kukubali hali hiyo itokee kwenye eneo langu, watu wanaendelea na shughuli zao na wachache wakiwa wamevaa nguo za kawaida lakini wameficha tishirt ndani, wanafika sehemu wanaanza kuzitoa", amesema Kamanda Jumanne.

Kamanda Jumanne ameendelea kwa kuwataka wananchi kuacha kufanya mikusanyiko ya aina hiyo, na iwapo wanahitaji kufanya ibada waende kwenye sehemu za ibada.
Wiki iliyopita Jeshi la polisi Kanda maalum lilitoa taarifa ya kupiga marufuku kusanyiko lolote lisilo halali kumuombea Mbunge Tundu Lissu ambaye yuko Nairobi kwa matibabu, na kusema ni kuhatarisha hali ya amani.

Baraza la Vijana wa CHADEMA Wafichua Siri ya Albadiri Tanga...Hichi Ndio Kilichotokea

$
0
0
Baraza la Vijana wa CHADEMA wilayani Muheza mkoani Tanga wamekanusha kusoma albadili ambayo walidhamiria kuifanya siku chache zilizopita, wakisema bado wanalipa muda huku mtaani kukiwa na tetesi kuwa ilishasomwa.

Akizungumza na mwandishi wa habari wa East Africa Television mwenyekiti wa BAVICHA Muheza, Joseph Saja, amesema sababu ya zoezi hilo kutofanyika ni kwamba siku walizotangaza kuwataka waliofanya tukio hilo kujisalimisha zilikuwa hazijaisha, hivyo wataendelea na zoezi hilo mapema wiki ijayo.

"Siku ambazo tuliwapa wale watu kujitokeza ilikuwa mwisho Ijumaa, na mpaka leo bado hawajajitokeza sasa ndio tutatekeleza majukumu yetu ya kuanza kwenda huko tunakoenda kuisoma, inawezakana katika juma tatu au jumanne ndio tutatoka kwenda", amesema Joseph Saja.

Wiki iliyopita BAVICHA wilayani Muheza mkoani Tanga walitangaza kusoma albadili ili kuwajua watu waliomshambulia kwa risasi Tundu Lissu, na kuisaidia serikali ambayo mpaka sasa haijafahamu waliohusika.

Watoto Watatu Walipukiwa na Bomu Baada ya Kulichezea Kama Mpira

$
0
0

Watoto watatu waliokuwa wakichunga ng'ombe katika Kijiji cha Nafco  kilichopo Kata ya Loksale wilayani Monduli mkoani Arusha wamefariki dunia baada ya kulipukiwa na bomu walilolichezea wakidhani ni mpira.

Tukio hilo linadaiwa kutokea  Ijumaa jioni ambapo Mwenyekiti wa kijiji hicho, Julius Mhale amesema watoto hao wanatarajiwa kuzikwa Jumatatu Septemba 18
Mwenyekiti huyo amesema kuwa eneo ambalo bomu lililipuka hutumiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa mazoezi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha tukio hilo na kuahidi kutoa taarifa rasmi hapo baadae.

SHINDA GARI LA BUREEEE!!! , Shindano hili ni la Bure Usipuuzie tu.

$
0
0
Jee!! Katika Maisha yako umewahi kuwa na ndoto ya kumiliki Gari lako?  Kama jibu ni Ndio Basi Kampuni ya Kijapan inakupa Fasi ya kushinda Gari Buree yani Buree bila kulipa chochote..

Chakufanya ni kubofiya neno SHINDA GARI hapo chini na kisha Bonyeza Neno APPLY NOW kwa kujisajili...

Kumbuka huduma hii ni ya Bure kabisaaaaa...


>> SHINDA GARI <<



Okwi Noma Sana Akataa Kiatu cha Dhahabu Adai yeye Anataka Simba Ichukue tu Kombe

$
0
0
Mshambuliaji mwenye asili ya Kiganda, Emmanuel Okwi amefunguka na kudai kwa sasa hatazamii kucheza ili kupata kiatu cha dhahabu baada ya ligi kuisha bali malengo yake ni kuisaidia timu yake yake ya Simba SC kupata ushindi.

Okwi amefunguka hayo baada ya kutoka kwenye mchezo wa uliomalizika leo jioni kwenye uwanja wa Uhuru Dar es salaam kwa klabu yake kuichapa Mwadui FC ya Shinyanga mabao 3 -0 na kupata nafasi ya kurejea nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kuu bara.

"Nawashukuru wacheaji wenzangu kwa ushirikiano na hivi sasa siangalii kupata kiatu cha dhahabu bali kuisaidi timu yangu kupata ushindi, lakini ikitokea kuwa nimepata nitashukuru".

Mabao ya Emmanuel Okwi dakika ya 7 na 67 yaliipa Simba uongozi kabla ya John Bocco kuhitimisha ushindi huo wa pili kwa Simba msimu huu kwa bao safi dakika ya 72.

Simba sasa imefikisha alama 7 ikiwa katika nafasi ya pili nyuma ya Mtibwa Sugar yenye alama 9. Mshambuliaji Emamanuel Okwi amefikisha mabao 8 katika michezo yake miwiwli aliyocheza huku John Bocco naye akifungua akaunti ya mabao ndani ya Simba.

Katika mchezo mwingine jioni ya leo Mbeya City wakiwa nyumbani Sokoine Mbeya wameifunga Njombe Mji bao 1-0.

Polisi wa Dar es Salaam Anayejiita 'Faru John' Atakiwa Kuhojiwa Kwa Rushwa

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amemuagiza Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Temeke kuhakikisha askari anayejiita Faru John anafikishwa ofisi kwake kuhojiwa akituhumiwa kwa rushwa.

Agizo hilo amelitoa leo Jumapili baada ya wakazi wa Mbagala kumlalamikia wakidai askari huyo amekuwa akiwakamata wafanyabiashara na kudai kwa nguvu rushwa ya Sh20,000.

Wananchi  hao wamelalamika kuwa, mfanyabiashara ambaye hatoi fedha hizo hufungwa pingu na kuzungushwa usiku kucha akiwa kwenye gari la polisi.

Kamanda Mambosasa aliyekuwa akisikiliza kero za wananchi wa Mbagala Zakhem amesema Jeshi la Polisi haliwezi kuwa na askari anayejipa jina la mzaha, huku akiwakandamiza wananchi.

Amesema huo ni mmomonyoko wa maadili kwa askari ambao kazi yao ni kulinda raia na mali zao, hivyo atawachukulia hatua wote watakaobainika kuomba na kupokea rushwa.

"Ninawaomba askari kuwalinda wafanyabiashara wenye mitaji midogo kama vile wakaanga chipsi. Kuwadai Sh20,000 eti kwa sababu wamechelewa kufunga biashara hilo sikubaliani nalo hata kidogo, lazima niwachukulie hatua," amesema Kamanda Mambosasa.

Pia, amekemea askari wanaodai rushwa kwenye vituo vya polisi ambavyo amesema vipo kwa ajili ya kutoa huduma.

Amewaagiza wakuu wa vituo kuhakikisha watu hawakai muda mrefu vituoni kwa kuwa kufanya hivyo ni kutengeneza mazingira ya kupokea rushwa.

Mkazi wa Mbagala, Thabiti Mohamed alisema kuna askari anayejulikana kwa jina la Faru John amekuwa akiwakamata wafanyabiashara, wakiwemo wauza chipsi ambao huchelewa kufunga maduka hadi saa tano usiku na huzunguka nao usiku kucha wakiwa wamewafunga pingu.

Mohamed alisema askari hao huomba kwanza Sh20,000 ili kuwaachia na wasipozitoa ndipo hufungwa pingu na kupakiwa kwenye gari.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Kibangulile, Mashaka Selemani amemuomba Kamanda Mambosasa kuwahamisha askari wa Kituo cha Polisi Maturubai akisema hawakamati wahalifu bali wapo kwa ajili ya kupokea rushwa.

"Askari hawa kazi yao wanapomkamata mtuhumiwa wanampeleka ofisi ya Serikali ya Mtaa Mikwambe, wanapofika kazi yao wanataka fedha kwa nguvu. Wasipopata wanawapiga na kuwabambikia kesi. Tumefuatilia wanakusanya hadi Sh1 milioni kwa siku, hivyo wameshazoeleka tunataka waondolewe Mbagala," alisema Selemani.

Chanzo: Mwananchi

Uhuru Kenyatta Noma Sana..Akataa Kukopa hela Kwa Ajili ya Uchaguzi wa Marudio...Aamua Kufanya Magufuli Way

$
0
0
Serikali ya Kenya imetangaza kupunguza matumizi katika baadhi ya taasisi za serikali ili kupata fedha kwa ajili ya kugharamia uchaguzi wa marudio wa Urais unaotarajiwa kufanyika Oktoba 17.

Waziri wa Fedha wa nchi hiyo, Henry Rotich, amesema, tume mbalimbali pamoja na County zote 47 zitaathirika na uamuzi huo wa kubana matumizi.

Bw. Rotich amesema tayari wametangaza kupiga marufuku safari za nje kwa maafisa wa serikali bila ya kibali maalum kutoka kwa Rais Uhuru Kenyatta.

Uchaguzi huo wa marudio unatarajia kuligharimu taifa hilo la Afrika Mashariki Dola za Kimarekani milioni 150, na kwamba serikali haitarajii kukopa fedha nje kwa ajili ya kufanikisha uchaguzi huo.

Emmanuel Mbasha Atuhumiwa Kuzaa na Wanawake Tofauti na Kuwatelekeza

$
0
0
Msanii wa muziki wa Injili bongo Emmanuel Mbasha, ameamua kuvunja ukimya juu ya tuhuma alizopewa za kutelekeza watoto aliozaa na wanawake wotauti tofauti, na kusema habari hizo hazina ukweli wowote.

Akizungumza na mwandishi wa East Africa Television, Emmanuel Mbasha amesema tuhuma hizo ni uongo na anachukia watu wanaotengeneza habari hizo, kwani yeye haitaji habari za kutunga kupata kiki kwa kuwa yeye sio mwanamuziki wa bongo fleva.

"Sio kweli hivyo vitu ni vya uongo, nakanusha kabisa, hivi kwa nini vitu vingi vinaongelewa vya uongo! alafu mimi sipendi, huu uongo uongo ni vitu vya bongo fleva, mimi sipo kwenye kutafuta kiki wala kuongelea vitu ambavyo havina faida", amesema Emmanuel Mbasha.

Hivi karibuni kumekuwa na tetesi kwamba Emmanuel Mbasha amewazalisha wanawake wawili tofauti na kuwatelekeza, kisha kukimbilia kwa mwanamke mmoja mwenye uwezo mzuri kipesa hapa mjini na kuweka kambi.

Maombi ya Tundu Lissu Yalivyoota Mbawa leo D'Salaam Kama Kampeni ya Ukuta

$
0
0
Mkutano wa kumuombea Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ulioandaliwa na Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha), leo umeota mbawa baada ya polisi kuuzingira uwanja uliopangwa kufanyika maombezi hayo.

Maombi hayo, yalikuwa yafanyike katika Uwanja wa TP, Sinza Darajani jijini Dar es Salaam, yameshindwa kufanyika baada ya polisi kuimarisha ulinzi uwanjani hapo na maeneo jirani ambapo magari zaidi ya 10 mengine binafsi na askari zaidi ya 50, walitapakaa uwanjani hapo na katika Kanisa la Waadventista Wasababto (SDA), lililoko mkabala na uwanja huo.

Wakati jeshi hilo likifanikiwa kuimarisha ulinzi lilijikuta likizidiwa kete na wafuasi hao wa Chadema ambao walifika katika viwanja hivyo saa nne asubuhi kisha kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya maombi hayo.

Wakati Mwenyekiti wa Bavicha, Patrobas Katambi na wafuasi zaidi ya 15 wakiendelea kuelezea shughuli hiyo wakiwa wamevalia fulana zilizoandikwa ‘Pray For Lissu’ ghafla polisi waliibuka na kuwafukuza.

Katika sakata hilo wafuasi watano walitiwa mbaroni huku polisi wakiendelea kuwasaka watakaokaidi agizo la kutokufanyika kwa maombi hayo.

Hata hivyo, Katambi amesema katika maombi hayo walipanga kumuombea Lissu na Meja Jenerali Mstaafu, Vincent Mritaba ambaye naye alijeruhiwa kwa risasi na watu wasiojulikana na kumpora Sh milioni tano.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Jumanne Muliro amesema wanaendelea kuwahoji watuhumiwa hao ili waeleze wametumwa na nani na kwa dhamira gani.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images