Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live

JPM Ahaidi Kuwafukuza Wakurugenzi wa Halmashauri Nne kwa Ulevi

$
0
0
JPM Ahaidi Kuwafukuza Wakurugenzi wa Halmashauri Nne kwa Ulevi
Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameahidi kuwafukuza kazi Wakurugenzi wa halmashauri wanne kwa ulevi wa pombe pindi wawapo makazini.

Rais Magufuli
Rais Magufuli amesema hayo alipokuwa kwenye Mkutano wa 33 wa Jumuiya Ya Tawala za Mitaa (ALAT) ambao uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam na kusema amepata taarifa kuwa wapo Wakurugenzi kadhaa ambaio ni walevi na kudai wasipobadilika ndani ya muda mfupi atawafukuza kazi.

"Nimepata taarifa ya Wakurugenzi kama wawili watatu hivi ni walevi sana, nawaambia hao wataondoka kama upo hapa Mkurugenzi halafu ni mlevi ukajirekebishe haraka sana, kabla sijaja huko ili angalau uonekane umebadilika" alisema Rais Magufuli.

Mbali na hilo Rais Magufuli aliwataka viongozi hao kwenda kumaliza migogoro mbalimbali ndani ya halmashauri zao na mivutano isiyokuwa na msingi na kusema kuwa vyama vya siasa si adui bali adui wa kwanza wa serikali yake ni watu wanaokuja kuiba maliasili za Tanzania.

"Haipendezi kuwa na makundi muyamalize makundu hayo kwenye manispaa, tunajenga nyumba moja adui yetu siyo vyama tunachelewa sana, adui yetu ni wale wanaotuibia nasema mkamalize hayo makundi huko, najua tofauti lazima zitakuwepo lakini kwenye masuala ya kazi lazima tushikamane kwa maslahi ya Watanzania, mkawaimize Watanzania kufanya mambo ya maendeleo" alisisitiza Rais Magufuli

Chama cha CCK Chajiandaa Kufanya Mkutano Ikulu

$
0
0
Chama cha CCK Chajiandaa Kufanya Mkutano Ikulu
Chama cha Kijamii (CCK) kinajiandaa kufanya mkutano wake mkuu mapema mwakani katika ofisi ya Rais, Ikulu ya Dar es Salaam.

Mpango huo umetangazwa na mwenyekiti wa chama hicho, Constantine Akitanda ikiwa ni siku chache baada ya Rais John Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM kuvialika vyama vya upinzani kufanya mikutano yake Ikulu kama chama hicho kinavyofanya baadhi ya mikutano yake.

Kauli ya Rais Magufuli ilikuja huku kukiwa na malalamiko ya baadhi ya vyama vya siasa ikiwemo Chadema vikisema CCM imekiuka Sheria ya Vyama vya Siasa inayokataza vyama vya siasa kutumia rasilimali za Serikali kwa manufaa yake.

Akifungua mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) kilichofanyika katika ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Rais Magufuli alisema:

“Nawakaribisha sana hapa Ikulu hapa ni kwenu. Bila ninyi mimi nisingekuwa hapa. Kwahiyo sioni aibu kuwakaribisha wana CCM, lakini pia hapa ni kwa Watanzania wote, na ndio maana kuna wageni kutoka nje wamefika hapa Ikulu, wanamuziki niliwakaribisha Ikulu, wakati wa futari tulifanyia hapa hapa.

“Kwahiyo sioni ajabu ninyi kuwakaribisha hapa. Halafu kuona watu wajiulize kwanini mikutano wanafanyia Ikulu,” alisema Rais Magufuli.

Akizungumza kwa njia ya simu na gazeti hili leo Jumanne, Mwenyekiti wa CCK, Akitanda amesema wameipokea kauli hiyo ya Rais na wataitekeleza kwa kufanya mkutano wao mkuu mapema mwakani.

Amesema awali walipanga kufanyia kikao cha Kamati Kuu Ikulu, lakini wameona wasogeze mbele ili wafanye mkutano mkuu Februari mwakani.

“Tunataka kutumia ukumbi wa Ikulu kama alivyoelekeza Rais, maana ni ukumbi wa wananchi wote,” amesema Akitanda.

Aliongeza: “Tulitaka tuombe ukumbi wa Ikulu kwa ajili kikao cha Kamati Kuu wiki ijayo, lakini tukaona kikao hicho kitakuwa na wajumbe wachache tu yaani 30, sasa tunajipanga kufanya mkutano mkuu utakaokuwa na wajumbe 500 maana ule ukumbi ni mkubwa sana.”

Ameongeza pia sababu za kusogeza mbele mkutano wao ni barua waliyopokea kutoka kwa Msajili wa Vyama vya Siasa ikiwataka wauandae mkutano huo kwa miezi minne.

“Chama kimepokea barua kutoka kwa Msajili wa Vyama vya Siasa ambayo inatuelekeza kufanya maandalizi ya Mkutano Mkuu ndani ya miezi minne, nadhani kuanzia mwezi huu itakuwa Februari mwakani,” amesema Akitanda.

“Katiba yetu inasema Mkutano Mkuu utakuwa na wajumbe 500, lakini hata wakiwepo nusu yake wanaweza kufanya uamuzi. Tunaamini kabisa Rais atatukubalia kufanyia mkutano Ikulu, akikataa basi tutajua kwamba hatufai, lakini hatutarajii kukataliwa,” ameongeza.

Amesema kabla ya mkutano huo, kutakuwa na vikao vya utangulizi vitatu ambavyo ni pamoja na kamati ya utendaji, sekretarieti na mwisho Kamati Kuu ambayo itapendekeza tarehe ya Mkutano Mkuu.

Tume ya Uchaguzi Kenya Yaitisha Mkutano na Wagombea wa Urais

$
0
0
Tume ya Uchaguzi Kenya Yaitisha Mkutano na Wagombea wa Urais
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amefika kwenye mkutano ulioitishwa na tume ya uchaguzi na mipaka nchini Kenya IEBC katika ukumbi wa Bomas of Kenya mjini Nairobi.
Rais Uhuru Kenyatta naye amealikwa kwenye mkutano huo na IEBC inatarajia kuwa atafika.

Tume ya IEBC ilitisha mkutano na wagombea hao wakuu wa urais kabla ya uchaguzi wa tarehe 26 mwezi huu, kujadiliana kuhusu maandalizi ya uchaguzi huo.
IEBC imewaalika rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga, siku moja baada kufanya mazungumzo na wajumbe 12 kutoka nchi za kigeni wakiongzowa na balozi wa Marekania nchini Kenya Robert Godec na naibu balozi wa Uingerzea nchi Kenya,Susie Kitchens, ambao wamewataka wanasiasa kuheshimu uhuru wa tume ya uchaguzi.

Kufuatia kuporomoka kwa mazungumzo kati ya waakilshi wa chama cha Jubilee, chama cha National Super Alliance (NASA) na tunme ya IEBC siku ya Alhamisi, mwenyekiti wa tume ya IEBC Wafula Chebukati, alisema kuwa alitaka kukutana ana kwa ana na wagombea wakuu akiwalaumu waakilishi wao kwa misimamo mikali.
Wakiongea na waandishi wa habari siku ya Jumatatu wanadiplomasia hao waliitaka Jubilee na NASA kuacha kutumia maneno makali na kutochukua misimamo ambayo inahujuma shughuli ya upigaji kura.

Janga la Lissu , Lema Lilimkosa Kosa Ester Bulaya Asimulia Alivyofuatiliwa na Gari

$
0
0
Janga la Lissu , Lema Lilimkosa Kosa Ester Bulaya Asimulia Alivyofuatiliwa na Gar
Mbunge wa Bunda Mjini Ester Amos Bulaya, amesema matukio hatarishi ya kiusalama yanayowatokea baadhi ya wabunge wa CHADEMA likiwemo la Lissu na Lema, ililikuwa limkute na yeye ispokuwa aliwahi kujisalimisha polisi.

Akizungumza na mwandishi wa habari wa East Africa Television, Ester Bulaya amesema aliwahi kufuatiliwa na gari ambao alikuwa na mashaka nalo akielekea mkoani Arusha, hali ambayo iliibua hofu kwake na dereva wake, na kwenda kujisalimisha katika kituo cha polisi cha Usa River.

Ester Bulaya amesema siku hiyo wakiwa njiani kuelekea Arusha, dereva wake akamwambia anaona kuna gari inawafuatilia, na walipowakaribia walishusha kioo upande aliokaa Ester Bulaya, na ndipo akaongeza spidi zaidi kuweza kuwatoka na kwenda kuingia polisi kutoa taarifa, na kuwapa ulinzi.

Nawal Anatafuta Kiki Tena Ananitafuta Undani- Nuh Mziwanda

$
0
0
Nawal Anatafuta Kiki Tena Ananitafuta Undani- Nuh Mziwanda
KUFUATIA povu alilolitoa aliyewahi kuwa mke wa mwanamuziki Nuh Mziwanda, bidada Nawali kwenye kituo kimoja cha televisheni kwamba baba wa mtoto wake huyo hamuhudumii mtoto wao, Nuh amefunguka kuwa mwanamke huyo anatafuta kiki na si bure.

Akichonga na Uwazi Showbiz, Nuh alisema kuwa mara kwa mara amekuwa akiwasiliana na mwanamke huyo kumjulia hali mwanaye ikiwa ni pamoja na kumhudumia lakini anashangazwa na yeye kuibuka kwenye media na kudai hamhudumii.

“Mambo mengine unaweza kusema hata mtu anatafuta kiki au anakutafuta la undani. Kiukweli sitaki kulizungumzia suala hili sana lakini ukweli ni kwamba siwezi kuacha kumhudumia mwanangu!

Ustaazi Ahukumiwa Miaka 30 Jela kwa Kulawiti

$
0
0

Ustaazi Ahukumiwa Miaka 30 Jela kwa Kulawiti
Mwalimu wa madrasa, Abdillah Sharifu, amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela baada ya kutiwa hatiani kwa kumlawiti mtoto wa kiume wa miaka 11.

Sharifu (30), mkazi wa Gongo la Mboto eneo la Moshi Baa amehukumiwa kifungo leo Jumanne katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala.

Mshtakiwa anadaiwa kumlawiti mtoto huyo na pia kumtishia kuwa angemroga endapo angetoa taarifa kwa wazazi wake kuwa anamfanyia kitendo hicho.

Akisoma hukumu, Hakimu Mkazi Mwandamizi, Juma Hassan amesema ameridhishwa na ushahidi wa mashahidi wanne akiwemo daktari.

"Mshtakiwa nimekutia hatiani kama ulivyoshtakiwa, ninakuhukumu kifungo cha miaka 30 jela ili iwe fundisho kwako na watu wengine wenye tabia mbaya kama hii," amesema.

Hakimu Hassan amesema kitendo kilichofanywa na mshtakiwa ambaye ni mwalimu wa dini ni cha kikatili.

Akipitia ushahidi wa upande wa mashtaka, hakimu Hassan amesema shahidi wa kwanza ambaye ni mtoto huyo aliieleza Mahakama kuwa mshtakiwa Februari 25 alimtaka kwenda nyumbani kwake.

Baada ya kufika nyumbani kwa mshtakiwa ambaye mke wake ana tatizo la kutoona, shahidi huyo alieleza alitakiwa kuvua nguo kitendo ambacho pia kilifanywa na Sharifu.

Shahidi huyo aliieleza Mahakama kuwa mshtakiwa alimfanyia ukatili huo, huku akimtishia kuwa iwapo angethubutu kutoa siri hiyo angemroga.

“Mara kwa mara alikuwa akinifanyia mchezo huu hadi nilipomwambia mama na kisha kwenda kufungua kesi katika kituo cha polisi Mazizini,” alisema mtoto huyo katika ushahidi alioutoa mahakamani.

Katika ushahidi wa mama mzazi wa mtoto huyo, alidai baada ya kuripoti polisi walikwenda hospitali ambako kwa mujibu wa vipimo vya daktari licha ya kutokuwa na michubuko ilionekana aliingiliwa.

Mshtakiwa alidai ana mke kipofu na kwamba, hafanyi vitendo hivyo isipokuwa alikuwa na ugomvi na mama wa mtoto huyo na ndiyo sababu ya kumfungulia kesi.

Hata hivyo, mshtakiwa alishindwa kuifafanulia Mahakama chanzo cha ugomvi hivyo ilitupilia mbali utetezi wake na kumtia hatiani.

Awali, Wakili wa Serikali, Grace Mwanga aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali kwa mshtakiwa ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia za kulawiti watoto na wanaotumia kimvuli cha nyumba za ibada kufanya ukatili.

Mshtakiwa alitenda kosa hilo, Februari 25 katika eneo la Moshi Baa, Gongo la Mboto.

Pendeza na Products za Kessy...Kutengeneza Shape, Kutoa Mvi na Mengine

$
0
0

PENDEZA NA KESSY PTODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA  MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA🌺🍌🍍
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK (B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _90,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _80,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_90,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MILINI _90,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI_80,000/(B)VIDONGE MAX MAN_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_120,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_90,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA     MGUU_80,000/🍍🍉🍊                                                                                     TUNAPATIKAN DAR W SALAAM: NAKWA MIKOAN KOTE UTAPATA PIGA CM                                         (+255) 0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product
Delivery  POPOTE ULIPO,

Yanga Kumkosa Ngoma kwa Muda Usiojulikana

$
0
0
Yanga Kumkosa Ngoma kwa Muda Usiojulikana
Mshambuliaji wa klabu ya soka ya Yanga Donald Ngoma ataendelea kuwa nje ya uwanja kwa muda usiojulikana baada ya kuumia kwenye mechi ya ligi kuu dhidi ya Mtibwa Sugar  na jana asubuhi Oktoba 2 akashindwa kuendelea na mazoezi.

Msemaji wa Yanga Dismas Ten amesema kuwa bado wanasubiri ripoti ya daktari wa timu Dr. Edward Bavu ili kujua ni muda gani Ngoma atakaa nje.

Dismas ameongeza kuwa daktari Bavu amethibitisha kuwa ripoti hiyo inaweza kutoka ndani ya saa 48 zijazo baada ya kumfanyia uchunguzi wa kina nyota huyo raia wa Zimbabwe.
Donald Ngoma alishindwa kufanya Mazoezi asubuhi ya jana kufuatia maumivu misuli ya paja aliyoyapata kwenye mchezo uliopigwa Jumamosi dhidi ya Mtibwa Sugar ambapo timu hizo zilitoka sare. Mchezo wa Yanga unaofuata utakuwa dhidi ya Kagera Sugar tarehe 14/10/2017 Kwenye uwanja wa Kaitaba.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Akerwa na Uchafu wa Mazingira

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Akerwa na Uchafu wa Mazingira
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amesema haridhishwi na hali ya usafi wa mazingira wilayani humo, hivyo amewataka viongozi kuwajibika ipasavyo.

Amewataka watendaji wa kata kuongeza jitihada za kusimamia usafi ili kuepusha hatari ya kuibuka maradhi ya mlipuko kikiwemo kipindupindu.

Hapi akizungumza leo Jumanne wakati wa mkutano na viongozi, wakiwemo maofisa afya, watendaji kata na wenyeviti wa mitaa amesema baadhi ya maeneo yamekithiri kwa uchafu ukiwemo utiririshaji maji taka, huku baadhi ya mitaro ikiwa michafu kwa muda mrefu.

"Kila baada ya msimu wa mvua kinachofuata ni kipindupindu. Ni aibu kuwa na kipindupindu Kinondoni," amesema.

Amesema kuna umuhimu wa kuchukua tahadhari kwa kuwa hali ya usafi wa mazingira ni mbaya.

Amewataka kusimamia sheria bila woga kwa kuwachukulia hatua watu wanachafua mazingira ikiwemo kutiririsha maji taka hovyo.

"Ni gharama kutibu watu wenye kipindupindu. Mwaka juzi tulikuwa na kambi pale Mburahati na Serikali iliingia gharama kutoa huduma," amesema.

Baadhi ya viongozi wa Serikali za Mitaa wamesema tatizo la mlundikano wa taka linatokana na uhaba wa magari ya taka na madampo.

Katika hatua nyingine, mkuu wa wilaya amewataka kusimamia haki hasa katika suala la ardhi kwa kuwasaidia wanyonge ambao wamedhulumiwa viwanja.

Tanzia; Mgonjwa wa Nyarandu Amefariki Dunia Leo

$
0
0
Mgonjwa wa Nyarandu Afariki Dunia Leo
Mbunge wa Singida Kaskazini  Lazaro Nyalandu jana alikuwa jijini Nairobi nchini Kenya ambapo alikwenda kuchukua dawa kwa ajili ya mgonjwa Samson Mwanga ambaye alipasuka mshipa wa kichwa ametangaza kuwa mgonjwa huyo amepoteza maisha alfajiri ya leo.

Nyarandu amesema kuwa mgonjwa huyo Samson Mwanga amefariki dunia alfajiri ya leo akiwa katika Hospitali ya rufaa ya KCMC iliyopo Moshi mkoani Kilimanjaro
"Nilikuwa hospitali ya KCMC, Moshi saa 7:00 usiku kuamkia leo kupeleka dawa (Intravenous Immunoglobulin) nilizozitoa Nairobi Hospital na kuzisafirisha usiku kwa ajili ya kuendelea kumtibu mgonjwa Samson Mwanga tuliyemrusha kwa ndege toka Hydom Hospital Jumanne iliyopita. Kwa bahati mbaya sana, tumempoteza Samson alfajiri majira ya 11:00 asubuhi" alisema Nyalandu
Aidha Mbunge huyo wa Singida Kaskazini ametoa shukrani zake kwa madaktari wa KCMC kwa kila walichoweza kufanya ili kuweza kuokoa maisha ya Samson mbaka pale umauti ulipomkuta alfajiri ya leo.

Septemba 26, 2017 Lazaro Nyalandu aliweza kufanikisha safari ya Samson kutoka katika hospitali ya Hyadom na kumpeleka Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Kilimanjaro kwa dharura kutokana na mgonjwa huyo kupasuka mshipa wa kichwa hivyo alipelekwa KCMC kwa matibabu zaidi lakini leo amepoteza maisha akiwa bado anapatiwa matibabu.
Bwana ametoa, na Bwana ametwaa, jina la bwana lihimidiwe

Aliyesambaza Habari za Uongo Kuhusu Mazungumzo ya Serikali Wawakilishi wa Kampuni ya Acacia Apandishwa Kizimbani

$
0
0
Aliyesambaza Habari za Uongo Kuhusu Mazungumzo ya Serikali Wawakilishi wa Kampuni ya Acacia Apandishwa Kizimbani
Mkazi wa Chato mkoani Geita, Obadia Kiko (41), amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shtaka la kusambaza taarifa za uongo kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook kuhusu mazungumzo kati ya Serikali na wawakilishi wa kampuni ya Acacia.

Wakili wa Serikali, Leonard Challo amedai mahakamani kuwa Agosti 3, 2017 huko Chato Geita mshtakiwa huyo alifanya kosa hilo kupitia mtandao huo wa kijamii wa Facebook.

Challo ametoa madai hayo leo Jumanne mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri. Mshtakiwa huyo anadaiwa kusambaza maneno kuwa "Taarifa kutoka  kikao cha mazungumzo kati ya Serikali na wawakilishi wa kampuni ya Acacia kuwa wanasheria wa upande wetu wanashindwa kutafsiri baadhi ya vifungu vya sheria hadi kufikia kuomba msaada kwa wanasheria wa Acacia sasa huoni hivi ni vituko mwizi anakusaidia sheria haahaa haha."



Inadaiwa aliendelea kusambaza maneno kuwa, "mazungumzo bado yanaendelea lakini wanasheria wetu wamebanwa sana ukizingatia wale jamaa wana vielelezo vyote vya mikataba kiukweli tumuombe Mungu maana Serikali ikitaka kuvunja mkataba na Acacia gharama kubwa zitatuusu."

"Lakini pia kuendeleza uvyama utatugharimu saana, baada ya mh. Rais Magufuli angewashirikisha mawakili wasomi waliokwishaiva wakili Lissu, wakili Kibatara na Fatma Karume kwenye mambo ya umuhimu kama haya yeye kaleta uchama sasa itatugharimu .// Dicteta Magufuli mist go" . Maneno hayo yanadaiwa kusambazwa na mshtakiwa huyo kupitia mtandao huo wa kijamii wa Facebook.

Wakili Challo amedai kuwa maneno hayo yalikuwa na lengo la kupotosha umma.

Baada ya kusomewa shtaka hilo, mshtakiwa huyo alikana na upande wa mashtaka ukadai kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Kwa upande wa Wakili Peter Kibatala anayemtetea mshtakiwa huyo aliomba mteja wake apatiwe dhamana na kwa masharti nafuu.

Wakili Challo alieleza kuwa hana pingamizi la dhamana.

Hakimu Mashauri alimtaka mshtakiwa huyo kuwa na wadhamini wawili wanaoamika ambao kila mmoja atasaini bondi ya Sh 5 milioni.

Kesi imeahirishwa hadi Oktoba 16, 2017. Hata hivyo mshtakiwa huyo hakuwa na wadhamini.

Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ????

$
0
0

Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha vidonda vya tumbo,korodani kuvimba,na anatoa dagu za utajiri kwa wanaohitaji bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM, NAUTALETEWA POPOTE ULIPO TIBA HII

SIMU; NO 0767145357/0629034550.
WHATS APP 0759030343

Rais Magufuli Amwagia Sifa Makonda..Adai Hata Kama Hajui Kusoma Lakini Kama Anashika Madawa ya Kulevya Kwake ni Msomi Mzuri

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amemsifia Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda kwa kupambana vita dhidi ya dawa za kulevya aliyoianzisha huku akitaka viongozi wengine kuiga mfano wa kiongozi huyo .

Rais Magufuli amesema hayo kwenye Mkutano wa 33 wa Jumuiya Ya Tawala za Mitaa (ALAT) ambao umefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam ambapo amemtaka Waziri mkuu, Kassim Majaliwa kuwaambie wakuu wa Mikoa wengine kujifunza kwa Makonda.

“RC wa Dar es salaam alipojaribu kusema kuhusu dawa za kulevya kelele zikawa nyingi kweli, mara ooh hajasoma. Mimi hata kama hajui ‘a’ lakini kama anashika madawa ya kulevya huyo ni msomi mzuri,” alisema Rais Magufuli.

Hata hivyo Rais Magufuli amesema kuwa wakati anaanza Urais alitoa milioni mbili kwaajili ya ujenzi wa darasa mkoa wa Dar es salaam, hivyo amemtaka Mkuu wa mkoa huyo kujiandaa maana ataenda kukagua.

Chama Cha CCK Chatoa Mpya..Chapanga Kufanya Mkutano Mkuu Ikulu Kama CCM

$
0
0
Chama cha Kijamii (CCK) kimepanga kufanya mkutano wake mkuu katika ukumbi ulioko ndani ya Ikulu iliyoko Magogoni jijini Dar es Salaam, Februari Mwakani.
Mwenyekiti wa chama hicho, Constantine Akitanda amesema kuwa mpango huo ni sehemu ya kuitikia mwaliko wa Rais John Magufuli kwa vyama vingine vya siasa na Watanzania wote kutumia kumbi zilizoko Ikulu.

Akitanda amesema kuwa chama chake kilikuwa na mpango wa kufanya mkutano wake wa kawaida ndani ya Ikulu hivi karibuni lakini wameamua kuahirisha na kufanya mkutano mkuu utakaochukua watu takribani 500.

“Tulitaka kuomba ukumbi wa Ikulu kwa ajili ya ya Kikao cha Kamati Kuu wiki ijayo, lakini tukaona kikao hicho kitakuwa na wajumbe wachache tu yaani 30. Sasa tunajipanga kufanya mkutano huo mkuu utakaokuwa na watu 500,” Akitanda anakaririwa na Mwananchi.

Aliongeza kuwa kikao hicho kitatanguliwa na vikao vya Sekretarieti na Kamati ya Utendaji.



Hivi karibuni, Rais Magufuli alijibu malalamiko ya baadhi ya vyama vya siasa kuhusu kufanyika kwa mkutano wa CCM ikulu ambapo aliwaalika Watanzania wote akieleza kuwa Ikulu ni mahali pa Watanzania wote.

“Nawakaribisha sana hapa Ikulu ni kwenu. Kwahiyo sioni aibu kuwakaribisha wana CCM, lakini pia kwa Watanzania wote na ndio maana nina wageni kutoka nje wamefika hapa Ikulu, wanamuziki niliwakaribisha hapahapa na wakati wa futari tulifanyia hapa hapa,” alisema Rais Magufuli.
Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM (NEC) ulifanyika katika ukumbi wa Ikulu wiki iliyopita.

Siku, Dakika za Mwisho Kabla ya Ben Saanane Kutoweka

$
0
0

Siku chache kabla ya kupotea katika mazingira yasiyoelezeka, kada wa Chadema, Ben Saanane alifanya mambo mengi kama mawasiliano yake binafsi na pia ya chama chake.

Hata hivyo, kati ya mawasiliano hakuna kilichosaidia kung’amua ni katika mazingira gani mwanasiasa huyo kijana alipotea na yuko wapi hivi sasa; hai au amekufa.

Novemba 14 mwaka jana ndiyo ilikuwa siku ya mwisho kwa Ben kuonekaka ofisi za makao makuu ya Chadema yaliyopo Mtaa wa Ufipa wilayani Kinondoni ambako alitumia muda wake mwingi.

Siku hiyo alisaini kitabu cha mahudhurio ya watumishi wa ofisi hiyo na kufanya shughuli zake za kichama. Hiyo ikawa siku ya mwisho kwa Wanachadema kumuona.

Ben alikuwa msaidizi wa karibu wa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, akimsaidia kufanya tafiti na uchambuzi katika masuala ya siasa na uchumi.

Siku alipotoweka, vikao vya Bunge vilikuwa vikiendelea mjini Dodoma, na ni katika kipindi hicho hicho Taifa lilitangaziwa kifo cha aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta.

Wakati hayo yakitokea, Ben hakuwa Dodoma na bosi wake lakini aliwasiliana na Mbowe kwa kumtumia ujumbe mfupi wa simu kumpa pole kwa msiba mkubwa wa kitaifa. Hii ikawa mara yake ya mwisho kuwasiliana na Mbowe.

Ingawa kwa wanachadema, Novemba 14 ilikuwa siku ya mwisho kuonana naye, kwa majirani zake na watu wengine walikuwa na siku moja zaidi. Siku iliyofuata, yaani Novemba 15, Ben aliamkia nyumbani kwake Mabibo jijini Dar es Salaam.

Taarifa ya ufuatiliaji wa mawasiliano yake ya simu inaonesha kuwa Ben alitoka Mabibo asubuhi na kwenda au kupelekwa maeneo ya mikocheni ambako alitumia muda mrefu sana huko.

Mawasiliano yanaonyesha baada ya kutumia masaa kadhaa eneo la Mikocheni, alirudi ama kurudishwa eneo la Mabibo jioni. Alikuwa na nani na akifanya nini ni swali ambalo si ndugu zake wala vyombo vya usalama wameweza kulijibu.

Ufuatiliaji wa mawasiliano yake unaonyesha pia kuwa siku hiyo hiyo jioni simu yake ilitumika kutoa Sh50, 000 kwa wakala wa M-Pesa aliye eneo la Mburahati. Hiki kilikuwa kitendo cha mwisho kufanywa na Ben kupitia simu yake ya mkononi. Tangu hapo utambuzi wa simu yake ukapotea kabisa katika mtandao.

“Tumejaribu kufuatilia inaonekana wamei-block (wameizuia) ile simu,” alisema John Mrema, ambaye ni mkurugenzi wa uenezi, mawasiliano na mambo ya nje wa Chadema.

“Mtu anayeweza kufanya hivyo si mtu wa kawaida. Tulikuwa tunatumia njia mbalimbali kutafuta taarifa za Ben, sasa huwezi tena kum-trace (kumpata).

“To be frank (kusema kweli) ukitafuta namba ya Bern Saanane, ukiingiza kwenye system (mfumo) yao, unatakiwa uwe na password (nywila). Na ni simu hiyo tu sio simu zote zina password. So inaonekana ni mtu mmoja tu ndio anaweza kuaccess details (kuziona taarifa) za simu ya Ben.

“Kwa hiyo, inaonekana kuna mtu ambaye anacontroll (anadhibiti) hiyo system.”

Wakati ndugu wa karibu na viongozi wa Chadema wakitumia kila mbinu kujua aliko Ben, Desemba 24, siku moja kabla ya sikukuu ya Krismas mwaka jana, mtu asiyejulikana aliingia katika akaunti yake ya Facebook na kufuta baadhi ya maandishi yake yaliyokosoa viongozi wa juu serikalini.

“Huyu mtu aliingia kwenye akaunti ya Facebook ya Ben jioni na kufuta baadhi ya maandiko yake yoliyokuwa yanakosoa viongozi wa nchi.

“Sasa huyo aliyeweza kuwa na access (ruhusa ya kuingia), maana yake ni mtu aliyekuwa na password (nywila). Ni nani (huyo)?” anauliza Mrema.

“Ama alikuwa ni Ben mwenyewe na wakahakikisha anawapa password. Mashaka yetu yako hivyo.”

Kwa muda mrefu kabla ya kutoweka, Ben aliandika sana mawazo yake katika ukurasa wake wa Facebook, akichangia mijadala mingi ya kitaifa. Wakati mwingine aliwakosoa viongozi wakuu serikalini na wanasiasa.

“Ilifika mahali alipokea sms za vitisho zikimuonya kwa maneno kama ‘wewe endelea kuandika, kuna siku utajikuta uko mbele ya mamba peke yako’. Siku alipotushirikisha tulimwambia akaripoti polisi, na kweli alienda kuripoti. Sasa katikati ya sakata hilo ndio akapotea,” alisema Mrema.

“Sisi tuna shaka kwamba Ben alitekwa na watu wa usalama. Na tunasema hivyo kwa sababu moja kubwa, familia yake na sisi tumeomba polisi watuletee mawasiliano yake ya mwisho ya simu, wamekataa. Kwa sababu ingekuwa rahisi sana kujua aliwasiliana na nani mara ya mwisho na kuanza uchunguzi kuanzia hapo,” anasema Mrema.

Safari ya Afrika Kusini

Siku aliporipoti ofisi za makao makuu ya Chadema (Novemba 14, Ben aliaga baadhi ya watumishi wenzake kwamba alikuwa akijiandaa na safari ya Afrika Kusini kutetea tasnifu (thesis) yake ya Shahada ya Uzamivu (PHD) aliyokuwa akisoma.

Kwa zaidi ya miaka miwili kabla ya kutoweka, mwanaharakati huyo alikwenda Uholanzi mara kwa mara kwa ajili ya masomo yake hayo ya PHD. Mara tu baada ya tetesi za kutoweka kwake kuanza kusambaa, walioufahamu mpango wake huo hawakuwa na shaka kwani waliamini tayati angekuwa ameshaondoka kwenda Afrika Kusini.

Ilipofika Novemba 18, siku nne baada ya kuonekana makao makuu ya chadema, viongozi wa chama chake na ndugu zake walistuka baada ya familia yake kuanza kulalamika Ben haonekani nyumbani.

“Na sisi tukastuka, tukafanya jitihada za kuitafuta familia, tukakutana na dada yake, tukakutana na mdogo wake wakatuambia hajasafiri. Tukasema hapana, tukatumia network (mtandao) yetu kwenda uhamiaji lakini system za uhamiaji hazionyeshi kama amekwenda nje ya nchi. Kwa hiyo, tukajiridhisha kwamba hajaondoka nchini,” alisema Mrema.

“Tuliendelea kuwa na shaka tukasema ngoja twende Johannesburg, Afrika Kusini kujiridhisha endapo hajafika huko. Tulijiridhisha hajafika huko. Alikuwa ndani ya mipaka ya nchi na system ya uhamiaji imetuthibitishia.”

Habari hii ya kupotea kwa Ben Saanane itaendelea kesho.


Mwananchi

Rais Magufuli: Sitaongeza Mishahara kwa Watumishi wa Umma Mpaka Uzalishaji Uongezeke

$
0
0
Mheshimiwa Rais ameyaongea hayo katika mkutano mkuu was 33 wa ALAT jijini Dar es Salaam.

Kwa hiyo wafanyakazi jipeni moyo, msubiri mpaka uchumi utakapokua japo haijulikani ni lini uchumi utakua.

VIDEO:

Naomba Ushauri: Mama Mkwe Amemtafutia Mke Wangu Mchepuko

$
0
0
Nina jamaa yangu mpaka hivi sasa dunia anaiona chungu na hajui achukue uamuzi gani dhidi ya mkewe na mkwewe

Jamaa ameoa mwanamke ambae tayari alishaolewa na kuzaa mtoto mmoja ila kutokana na maisha kuwa ya tabu mume aliondoka kuelekea mozambiq kuchimba madini na hakurudi tena mpaka jamaa yangu alipojitwisha majukumu ya kuoa

Tatizo linalomsumbua jamaa yangu ni pindi alipooa aliamua kwenda kuishi na mke wake nyumbani kwao lakini pale kwao ikatokea sintofahamu na dada wa jamaa yangu ikabidi waende wakapange chumba,kule mama mkwe ikawa kila asubuhi lazima aje ashinde pale home kwa gia ya kujifanya anacheza na wajukuu na jioni anabeba chakula

Kupita kama miezi sita tangu ule mchezo uanze mama mkwe akatoa ushauri kwanini wasihamie kule nyumbani yaani ukweni sababu nyumba ipo na nafasi na yeye mama mkwe atapunguza msafara wa kuja pale daily,jamaa yangu akashauriwa akakubali wakahamia ukweni sasa baada ya kuingia pale jamaa yangu ndio ameanziwa visa vya kuweza kuua mtu

Jamaa yangu yeye ni dereva wa daladala sasa siku moja alipata udhuru akarudi nyumbani akakuta mlango wa chumba chake umefungwa na mama mkwe yupo pale barazani anafanya shughuli zake jamaa kuuliza akaambiwa mke ametoka akapiga simu haikupokelewa jamaa akaondoka siku nyingine akarudi tena hali ni ile ile jamaa akamuuliza mama mkwe kwani mama zuberi akiondoka haachi funguo

Akajibiwa haachi basi jamaa jioni ikabidi angushe mtiti, kumbe pale kuna jirani anauona mchezo mzima ikabidi amg'ate sikio jamaa yangu ya kwamba kuna jamaa huwa anaingia pale na mama mkwe anawafungia kufuli kwa nje mpaka wanapomaliza shughuli zao na hawakuanza leo

inavyoonekana mkwe anampenda mwizi zaidi kuliko mkwe halali

Sasa mpaka muda huu jamaa amechanganyikiwa na mama mkwe amesema jamaa akitaka ahame yeye mwanawe abaki pale na mke ana mpenda na anafikiria watoto wake

Naomba tumsaidie ushauri maana ameathirika kisaikolojia

By Madala

Nassari: Maisha Yangu Yapo Hatarini..Aliowaanika Mchana Kweupe Wanamtafuta

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki (CHADEMA) Joshua Nassari amefunguka na kusema maisha yake yapo hatarini na kudai kuwa watu ambao amewaanika kwenye sakata la ununuzi wa madiwani wanamtafuta.

Nassari amesema hayo ikiwa imepita siku moja toka alipokwenda kwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kupeleka ushahidi wake juu ya madiwani wa CHADEMA waliohama chama kwa kuhongwa rushwa na wateule wa Rais John Pombe Magufuli.

"Maisha yangu yapo kwenye bonde la uvuli wa mauti, Maisha yangu yapo hatarini kwani Watesi wetu wananitafuta" aliandika Nassari kupitia ukurasa wake wa facebook

Mbali na hilo wachangiaji mbalimbali kwenye ukurasa wa Mbunge huyo walimtaka azidi kumuomba Mungu huku wakimshauri kuongeza ulinzi zaidi katika maisha yake ya kila siku kutokana na jambo ambalo ameliibua na kumtaka aendelee kupambana, baadhi ya wachangiaji wengine wamedai kuwa anachofanya ni njia ya kujitafutia umaarufu kisiasa.

Juzi  Mbunge Joshua Nassari, Godbless Lema pamoja na Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa walikwenda kwenye Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na kupeleka ushahidi wao juu ya sakata la kununuliwa kwa madiwani wa CHADEMA na kuhongwa fedha na ahadi mbalimbali kutoka kwa wateule wa Rais mkoani Arusha.

Je, nia ya Kumpa Support Kiba ni Kumshusha Diamond Platnumz

$
0
0

Hivi kuna uwezekano wanaompa support Ali Kiba wanataka kumshusha Diamond?, Kwenye hizi team nimeona sana team kiba wanafatilia sana habari na maisha ya Diamond, Kuna uwezekano mkubwa sana labda hawa baadhi ya team kiba walikuwa wanamkubali sana Diamond ila alivyoanza kupata mafanikio makubwa walichukia sana na hivyo wakaona watumie karata ya Ali Kiba ili wajaribu kumshusha Diamond,

JE KUNA UWEZEKANO WA KUWEPO HILI JAMBO

Je Wajua Hemed PhD ndiye Msanii Mwenye Watoto Wengi Tanzania?

$
0
0
Akihojiwa katika kipindi cha E News cha EATV Msanii wa bongo movie na bongo fleva Hemed amesema anawatoto zaidi ya sita lakini amekuwa akimpost mmoja kwenye mitandao ya kijamii

VIDEO:

Viewing all 104808 articles
Browse latest View live




Latest Images