Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Maskini:Mwanafunzi wa Chuo Anusurika Kifo Baada ya Kuchomwa Moto Akidhaniwa ni Mwizi

$
0
0
Imagine guys kuna this guy mtanashati anasoma chuo cha ruaha a.k.a ruco huku iringa. Alikuwa sheria mwaka wa nne. Ameitiwa mwizi kumbe sio akachomwa moto. Ameungua ila hajafa, hivi ndivyo alivyo..

Unahisi ni Mzima Kweli ? Kaweka Pozi na Kutupia Picha Instagram

$
0
0
Unahisi ana akilli sawa huyu!!!!!!???? Hebu cheki alivyokaaa...Haya mie simo ...

Uwezi Amini Mbwa Ambaka Mwanafunzi na Kumtoa Bikira

$
0
0
Chanzo cha udaku huu kinasema kuwa mwanadada huyo alizoea sana kucheza na mbwa wa nyumbani kwao, asijue kuwa mbwa anammezea mate kila kukicha!

Siku ilipowadia, mwanadada huyo alitoka shuleni na kuvua sare ya shule na kutupia za nyumbani. Akiwa kainama kufunga kamba ya kiatu cha mguu wake wa kushoto, mbwa akaja kwa kasi sana, pengine akiwa anadhani kuwa kategeshewa goma, na kumrukia msichana huyo!
Alirarua suruali yake huku akilisaka shimo la mrembo huyo, na ndipo alipolikuta na kumsokemeza mtoto wa watu mashine yote na hivyo kujiridhisha nafsi yake.
Chanzo cha udaku huu kinaongezea kuwa mwanadada huyo alikuwa hajawahi kabisa kuliwa, na kuna mvulana, tena mwanafunzi mwenzake alikuwa akimsumbua sana kwa muda mrefu, kwani, malikia huyo alikuwa anasita kumvulia chu** mwanakaka huyo. Siku ilipowadia, mbwa akaamua kulianzisha goma mwenyewe!!!!

Kwa Wanaume tu: Wanawake wa Aina Hii ni Shida Usiwaguse Kabisa

$
0
0
Hakikisha unawakwepa aina hii ya wanawake ili usijiingize kwenye matatizo. Nitakwambia ni kwa nini…..

1.Demu wako wa zamani
Ni vizuri kutorudia mahusiano ya zamani na zaidi kama kwenye mahusiano yenu ya mwanzo mambo hayakuishia kwa uzuri. Sababu kuu ya msingi, kiukweli ni kwamba hakika mwanzoni mlikuwa hamuendani na ndio sababu ya iliyopelekea kuvunjika kwa mahusiano yenu, ndani ya hizo sababu kuna vitu vilivyopolekea kutokea kwa hayo, ukichunguza na kuziangalia kwa makini utagundua ni za asili na ambazo si rahisi kwa mmoja wenu kuzibadilisha sababu ni vitu au mambo ambayo yatakuwa ni ya damuni.

2.Dada wa rafiki yako kipenzi
Epukana na kujiingiza kwenye mahusiano na dada wa rafiki yako. Si tu kwamba utaweza kujiingiza kwenye uhasama na chuki kama mambo hayatakwenda sawa, ila pia utaweza kujiweka kwenye mazingira ya kujikuta siku moja unapigwa hata ngumi za uso sababu tu ulimuumiza dada yake. Pia, utaweza kumkosa mtu ambaye ndie alikuwa ni kimbilio lako kwa mambo mbalimbali pale ambapo itatokea wewe na dada yake mambo kutokwenda sawa, sababu hapo patakuwa na mgongano wa kimaslahi kwa huyo rafiki yako.

3.Wanawake wenye mambo mengi
Kiukweli, kutoka na watu kama hawa kinaweza kuwa ni kitu cha kufurahisha, ila mwisho wa siku itakuingiza kwenye matatizo. Mara zote kumbuka ni vyema kuwa salama kuliko kujuta. Usijiingize kwenye majaribu ambayo utakuja kuyajutia kwa maisha yako yote.

4.Wanawake wanaopenda hela kupitiliza (Wachunaji)
Kuwa mbali nao, labda kama unataka salio lako limalizike pasipo wewe kujifahamu. Naamini hili kila mmoja analifahamu na halihitaji darasa zaidi. 5.Demu wa zamani wa rafiki yako
Kama unathamini urafiki wako na mshikaji wako achana na habari ya kutoka na aliyekuwa demu wake. Mambo yanaweza kubadilika na kuwa kama au zaidi ya yaliyotokea kwa rafiki yako na ikaja kula kwako zaidi. Wakati mwengine inaweza tengeneza chuki kati yako na rafiki yako, huku akiamini kwamba ulikuwa unatoka au kumnyemelea demu wake toka zamani.

Wadau mademu wapo wengi sana, fanya kutafuta wengine nje ya hawa….. ni ushauri tu..

Nataka Kupenda Kama Mjinga, Nizame Nipotee! Kama limbwata ni Kweli Lipo Basi Nilishwe Hata Hilo

$
0
0
It may sound strange but this has been my major wish for a while,

Nataka kupenda kama mjinga, yaani niwe zombiee, nizame mapenzini nipotelee huko. Kila nachoambiwa nione sawa niwe mjinga mjinga no reasoning.

Yale mapenzi usipowasiliana ama kumwona mtu wako for a day unajisikia mgonjwa, mapenzi ambayo unaongea na mtu wako for two or three hrs and you feel like its just 5 minutes na haujui mlikuwa mnaongea nini. 

Yaani mapenzi ambapo nikiachwa au nililazimika kuacha basi nichanganyikiwe, nishindwe kula, nikose usingizi, nipungue uzito, nione kama dunia imekwisha shughuli zangu nishindwe kufanya, kichwa kigome kufukiri

Kama limbwata ni kweli lipo basi nilishwe hata hilo, haya mapenzi ya kupenda robo robo with a lot of reasoning sio nayotaka.

Natamani kupenda with all my heart, soul, mind, body and my everything, nataka kupenda kamili kamili, kwa kila kitu, mpenzi wangu awe kila kitu, awe ndio dunia na maisha yangu.

Trust me I want to love like nothing else,

Hivi ni mimi tu?

Ridhiwani Kikwete Akanusha Taarifa Zilizo Sambaa Kuhusu Kifo cha Mheshimiwa Kawambwa

$
0
0
TAARIFA TOKA BAGAMOYO
Ndg Watanzania,WanaBagamoyo na wapenda maendeleo, kwa niaba ya CCM-Bagamoyo na Ofisi ya Mbunge-Jimbo la Bagamoyo napenda kuleta kwenu Masikitiko yetu kwa niaba ya Chama na Familia ya Mheshimiwa Mbunge Shukuru Jumanne Kawambwa kutokana na Usumbufu ambao umesababishwa na habari zinazoenezwa Mitandaoni kwamba Mheshimiwa Kawambwa amekumbwa na Umauti akiwa njiani anaelekea Mwanza.
UKWELI
Mheshimiwa Shukuru Jumanne Kawambwa yupo Nchini Canada Akitimiza majukumu yake. Hivyo Watanzania na wana Bagamoyo mnaombwa radhi kwa usumbufu uliotokea na kwamba Mheshimiwa Mbunge yuko na Afya njema na utekelezaji wa Majukumu unaendelea kama kawaida.
Ndg.Ridhiwani Kikwete (Mnec)
Mbunge -Chalinze

Taarifa mpya ya Luis Suarez, hii ndio adhabu atakayopata akikutwa na hatia ya kumn’gata mchezaji mwenzake.

$
0
0
Mchezaji wa Uruguay Luis Suarez atakabiliwa na adhabu ya kufungiwa kwa muda mrefu kucheza mechi zikiwemo za Kombe la dunia ikiwa atakutwa na hatia ya kumng’ata mchezaji mwenzake wa Italia Giorgio Chiellini.
Shirikisho la soka duniani limeanzisha uchunguzi dhidi ya mchezaji huyo  baada ya kuonekana akimng’ata mchezaji wa Italia, Giorgio Chiellini wakati wa mechi yao ya kombe la dunia.

Chiellini amedai Suarez amemng’ata katika bega lake la kushoto lakini Suarez amejitetea kuwa mchezaji huyo alijigonga kwake.
Refari wa mechi hiyo hakuchukua hatua yoyote dhidi ya Suarez.
Ikiwa atapatikana na hatia, Suarez huenda akazuiwa kucheza mechi 24 au kwa miaka miwili.
Suarez mwenyewe tayari amejitetea katika vyombo vya habari nchini Uruguay.
Suarez anasema Kuna mambo fulani ambayo hutokea uwanjani na hadhani ni vyema kuanza kuzua kashfa kutokana na mambo kama hayo.

Msekwa: Hatuhitaji Katiba Mpya, Kitu Chochote Kinachotakiwa Kingeweza Kuingizwa Katika Katiba iliyopo.

$
0
0
Spika mstaafu, Pius Msekwa amesema haoni haja wala sababu ya msingi ya Tanzania kuandika Katiba Mpya kwa sasa kwani hakuna matukio makubwa ya kisiasa nchini yanayolazimisha kufanya hivyo.

Katika mahojiano maalumu na Mwananchi nyumbani kwake Oysterbay, Dar es Salaam jana, Msekwa alisema hata hivyo, anakubaliana na uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete kuruhusu kufanyika kwa mchakato wa Katiba Mpya kwa sababu alikuwa na sababu zake na alikwishazieleza wazi.

Alisema, “Sioni haja ya kuwa na Katiba Mpya. Mnatunga Katiba Mpya kama kuna mabadiliko makubwa ya kisiasa, yaani mabadiliko ya kiutawala,” alisema.

Alifafanua Katiba ya Tanganyika na hata ya Tanzania ilibadilishwa pale palipokuwa na matukio makubwa ya kiutawala, lakini pia kuna matukio mengine ambayo hayakulazimisha kuandikwa upya kwa Katiba.

Msekwa aliyeshiriki michakato yote ya katiba zilizotangulia ikiwamo hii ya sasa, alisema kwa kawaida Katiba Mpya inaweza kuandikwa panapokuwa na mabadiliko makubwa ya kisiasa nchini kama ilivyotokea mwaka 1962 baada ya Tanganyika kupata uhuru wake, lakini Malkia wa Uingereza akaendelea kuwa mkuu wa nchi.

“Katika mazingira hayo Watanzania hawakujua maana ya uhuru ni nini, ikaleta sintofahamu, ikabidi Mwalimu (Julius Nyerere) na wenzake waamue kufanya mabadiliko makubwa ya kisiasa kutoka kuwa chini ya Malkia kwenda kwa uongozi wa wananchi,’’ alisema.

Pia, alieleza kuwa kuanzishwa kwa Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964 na kuzaliwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lilikuwa tukio jingine kubwa na la msingi lililosababisha kuandikwa kwa Katiba Mpya ya mwaka 1977.

“Mfano wa pili tulipoingia katika Muungano mwaka 1964, hapa kulikuwa na nchi mbili ambazo ni sovereignty (nchi zenye utawala kamili) tukaziunganisha, mazingira kama hayo yalidai Katiba Mpya.

Hata hivyo, Msekwa alisema hata mabadiliko kama ya mwaka 1965 kutoka mfumo wa vyama vingi vya siasa kuingia chama kimoja licha ya kuwa tukio kubwa, hayakulazimisha kuandikwa kwa Katiba Mpya, bali iliyokuwepo ilifanyiwa marekebisho.

Alisema tukio jingine ni la mwaka 1984 ambako mabadiliko mengine yalifanyika katika Katiba kwa kuingiza kipengele cha haki za binadamu na ukomo wa kipindi cha urais kuwa wa vipindi viwili vya miaka mitano kila kimoja ambalo halikuhitaji Katiba Mpya.

Badiliko jingine kubwa ambalo halihitaji katiba mpya, Msekwa alisema ni lile la mwaka 1992 la kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini … “Tuliporejea mfumo wa vyama vingi hatukutunga katiba kwa kuwa haikuwa lazima. Unaondoa vile vifungu vinavyoondoa chama kimoja na vingine vinaendelea kama kawaida.

Kwa hiyo hata sasa hakuna haja ya kuandika Katiba Mpya, kitu chochote kinachotakiwa kingeweza kuingizwa katika Katiba iliyopo.

Mtoto wa Mjomba Ananitega Sana ...Je ni Sawa Kula Tunda?

$
0
0
Mimi na dada yangu mtoto wa mjomba tumekuwa pamoja na kuzoeana sana, hadi wakati mwengine hutaniana kupita kiasi, Binti huyo yani binamu anaishi moshi na mjomba ambako mimi huenda mara kwa mara pindi nikiwa likizo.
Mjomba angu ni mkali sana, na huchunga sana watoto wake wakike, hivyo binamu yangu huyo ni mtoto wa geti kali ile mbaya hakuna kwenda popote zaidi ya kwenye bustani tu iliyopo nje hapo nyumbani.
Mjomba angu huniamini sana hata wakati mwengine husafiri na mke wake na kuniacha nyumbani hapo na binamu yangu huyo. Siku moja mjomba alipata safari ya kwenda nairobi na kuniacha mimi binamu na dada wa kazi. Hiyo siku binti huyo alivaa nguo ambao sijawahi kuona amevaa toka nimjue alikuwa akizunguka hapo ndani huku akijiachia bila wasi wala kujali mimi nipo. Kwakweli ni msichana mwenye mvuto yani kama una moyo mwepesi unaweza kuomba tunda. Ilifika wakati mpaka akaanza kuja na chumbani kwangu akiwa amevaa nusu uchi nakutaka ni mfanyie massage akidai mgongo unamuuma, sikuweza kufanya hivyo mpaka akaniuliza kwanini unanifanyia hivyo, na mimi nikamuuliza kwani hujui mi ni nani yako akajibu kwa unyonge sina jinsi naumia nisaidie hatojua mtu, daah basi nilimuelewa nikamfanyia massage na nikamuacha aende kwakweli ulikuwa ni wakati mgumu sana kwangu mpaka pale mjomba alivyorudi na nikaaga nikaondoka zangu. ila nashukuru sikutegeka.. Japo Niliwahi kusikia Kuwa Eti binamu ni Nyama ya Hamu ..Je Ukweli? 

Niatwa Vena Naishi Kijitonyama Nimemaliza chuo Natafuta Rafiki Mmoja wa Ukweli wa Kuniliwaza

$
0
0
Niatwa vena naishi mwenye maeneo ya kijitonyama nimemaliza chuo cha ustawi mwaka jana, natafuta rafiki mmoja wa ukweli wa kuniliwaza, kama uko serious andika comment

VIDEO: FLORA MBASHA akomba kila kitu ndani ya Nyumba na kutokomea na Mtoto

$
0
0
MACHOZI upya! Habari halali kwa ubongo wako zinaeleza kwamba wakati mumewe, Emmanuel Mbasha (32) alipokuwa mahabusu, Dar kati ya Juni 15 hadi 17, mwaka huu, staa wa Gospo Bongo, Flora Mbasha (31) anadaiwa kwenda nyumbani na kukomba vitu vya ndani kuvipeleka kusikojulikana.


Ilisemekana kwamba wakati hayo yakiendelea, Mbasha alikuwa nyuma ya nondo za Mahabusu ya Keko jijini Dar es Salaam ambako alishikiliwa.

Kwa mujibu wa mtu aliyeambatana na Mbasha alipopata dhamana dhidi ya kesi yake inayomkabili ya ubakaji wa shemejiye mwenye umri wa miaka 17, alipofika nyumbani kwake Tabata-Kimanga, Dar alipigwa butwaa kukuta hakuna vitu ndani!

Habari zilidai kwamba alipowauliza majirani kama walimuona mtu akiingia ndani walimwambia mkewe (Flora) ndiye alikuwa akiingia na kutoka mara kwa mara.

Ilielezwa kuwa vitu hivyo vilihamishwa Juni 16 ambapo Mbasha alitoka mahabusu Juni 17, yaani siku moja tu.

KITANDA CHA BEI MBAYA

Baadhi ya vitu vilivyodaiwa kuchukuliwa nyumbani hapo ni kitanda cha bei mbaya walichokuwa wakilalia kwenye chumba cha baba na mama huku akimwachia neti ikiwa inaning’inia.

SUTI ZA MAREKANI

Vingine ni makochi huku akibakisha sofa ndogo ya mtu mmoja, vitu vyote jikoni na nguo (suti za bei mbaya, walizonunua wakati wakiwa Marekani).
Pia alidaiwa kukomba vile vidani vyote vya dhahabu.

ZAIDI YA MIL. 13

Ukiacha zile hati za nyumba, viwanja na mashamba, gharama ya vitu vyote vilivyochukuliwa ndani ni zaidi ya Sh. milioni 13 za Kitanzania (kama zile ambazo Wema Isaac Sepetu alizomlipia Kajala Masanja asiende jela).

AMWAGA CHOZI

Baada ya kukutana na mazingira ya aina hiyo, lilikuwa ni pigo lingine zito kwa Mbasha ambaye alijikuta akimwaga chozi kwa mara nyingine kwa sababu ya mkewe Flora aliyedumu naye katika ndoa kwa takriban miaka 12.
Ilidaiwa kuwa, Mbasha aliumia kupita kiasi huku akiomba Watanzania waone ubaya aliotendewa.

AMANI LAPEKUWA CHUMBA HADI CHUMBA

Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, Amani lilifika nyumbani hapo ambapo lilipata mwanya wa kuingia ndani ya nyumba hiyo kisha kupekuwa chumba hadi chumba na kujionea kulivyokuwa kweupe huku madirishani mapazia yakiendelea kubembea kwa upepo mkali uliopo Dar kwa sasa.
Kimuonekano, nyumba hiyo ilikuwa kama kuna familia ilihama hivyo inahitaji kupangishwa au kuhamiwa na mwingine.

MBASHA ANASEMAJE?

Alipotafutwa Mbasha kuzungumzia ishu hiyo alikiri kukuta hali hiyo nyumbani kwake baada ya kupata dhamana.
“Nilipofika nyumbani kwangu nilikuta ufunguo wa nyumba kwa majirani. Niliwauliza kama kulikuwa na mtu anaingia nyumbani nikaambiwa ni Flora. Kama mnavyoona kuna vitu vingi vya ndani havipo,” alisema Mbasha.
Alipoulizwa kama ana uhakika kuwa mhusika ni Flora, Mbasha alisema  yeye alikuta nyumba nyeupe.
Jitihada za kumpata Flora hazikuzaa matunda kwani simu yake ya kiganjani haikuwa hewani juzi Jumanne mpaka gazeti hili linakwenda mitamboni.

TUMEFIKAJE HAPA?

Kabla ya Mbasha kukabiliwa na kesi hiyo ya madai ya ubakaji wa ndugu wa Flora, Mei 23 na 25, mwaka huu, tayari kulikuwa na mgogoro wa ndoa. Flora alishaondoka nyumbani na kwenda kuishi hotelini maeneo ya Sinza jijini Dar.

Video Hapo Chini:

Hali ya Afya ya JACK PATICK bado tete Gerezani…Ashindwa kuhudhuria Mahakamani

$
0
0
UNAWEZA kusema ni majanga juu ya majanga yanazidi kumkumba modo wa Bongo, Jacqueline Patrick ‘Jack’ baada ya wiki iliyopita kushindwa kupanda kortini kufuatia kutetereka kwa afya yake bila kufafanuliwa.

Mbali na kuwa na afya tete, pia Jack anadaiwa kulalamikia haki za msingi za kibinadamu ambazo anazikosa mahabusu kwa kuishi maisha kama ya mtu aliye kifungoni.

Akizungumza na Amani juzi jijini Dar, mtu anayejitolea kumpa msaada na kumtembelea Jack mahabusu, Macau, China alikoshikiliwa, Matilda  alisema Jack anaumia kwa kupewa maisha kama tayari amehukumiwa, anaona bora hukumu yake ipite ajue moja.

“Kiukweli Jack anaumwa, alishindwa hata kwenda mahamani, mbaya zaidi hata wakili wake naye hakutokea siku hiyo.
“Halafu kule mahabusu anafanyishwa kazi ngumu ambazo hastahili kama mahabusu na amesema hata watu wake wa karibu ambao anaamini kwa kipindi hiki wangekuwa wanampa faraja hawaoni, anatamani angekamatiwa Bongo labda kuna watu wanapenda kwenda kumtembelea kule Macau lakini hawana uwezo.

“Wabongo wengi ambao wako Macau kwa ajili ya sanaa ya sarakasi ndiyo kidogo wanakwenda kumtembelea siku mojamoja,” alisema Matilda.

Juni 20, mwaka huu, Amani lilizungumza na Mbongo Fleva anayedaiwa ni mtu wa karibu na Jack, Juma Khalid ‘Jux’ na kumuuliza kwa nini hajawahi kwenda kumtembelea ‘bebi’ wake mahabusu kama wanavyofanya Wabongo ambao wako Macau, akajibu:

“Sipendi kusikia ishu yoyote inayomuhusu Jack kwani nina mambo mengi ya kuongelea na si ishu za Jack kila kukicha.

“Kwa kipindi hiki sitahitaji mtu aniulize ishu za Jack, zinanitibua sana na kama kuongelewa zimeshaongelewa hivyo sioni kipya.”

Hii ni mara ya tatu kwa Jack kupanda mahakamani, mara ya kwanza ilikuwa Aprili 10, mwaka huu kosa likiwa kukutwa na madawa ya kulevya tumboni aina ya heroin kete 57 au kilo 1.1 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 223. Mara ya pili ilikuwa Mei 23, mwaka

Miujiza: Mwanamke Ajifungua Baada ya Kuwa Mjamzito kwa Miaka 14

$
0
0
Mwanamke wa Nigeria aliyejitambulisha kwa jina la Mercy James amesimulia tukio la ajabu la kujifungua salama mtoto wa kike baada ya kuwa mjamzito kwa kipindi cha miaka 14. Mtoto aliyeamua kumuita ‘Miracle’

Kwa mujibu wa Vanguard, Mercy alieleza kuwa alianza kujisikia dalili za ujauzito miaka 14 iliyopita lakini awali dalili hizo zilikuwa zinabadilika na mara nyingine anaingia katika hedhi kwa siku moja, lakini hali ilianza kuwa serious miaka miwili baadae alipoenda hospitali na kuhakikishiwa kwa vipimo kuwa ni mjamzito.

“Nilienda tena kwa tabibu miaka miwili baadae na kumlalamikia kuhusu maumivu niliyokuwa nayapata, aliniambia tena kuwa sina tatizo la tumbo na kwamba huo ulikuwa ujauzito. Alinishauri niendelee na maombi ili Mungu aniepushe na mikono ya shetani.” Mercy alisimulia.

Anaeleza kuwa alikuwa anatumia madawa mengi ya kutibu magonjwa ya tumbo lakini hali yake haikubadilika.

Hali iliendelea hivyo hadi ilipofika June 7 mwaka huu ambapo alienda tena katika hospitali hiyo akiwa analalamika na kusikia kila dalili za kitu kutaka kutoka mwilini mwake, lakini hakufahamu kuwa hiyo ingekuwa siku ambayo angejifungua mwanae wa kike, ‘Miracle’.

“Kisha Mungu aliamua kunifuta machozi. Katika siku niliyojifungua mwanangu wa kike, mwanzo nilihisi ni minyoo inataka kutoka kwenye mwili wangu bila kufahamu kuwa yule alikuwa mtoto. Hivi ndivyo nilivyomwambia mkunga. Lakini baada ya kunipima alianza kuniambia nisukume. Nilimpotezea. Baadae nikaishiwa fahamu kama dakika 15 na nilipopata fahamu, nilisikia mtoto Analia. Nilishangaa sana na kuchanganyikiwa nilipomuona mwanangu. Sikuweza kuamini macho yangu.” Mercy aliendelea kusimulia tukio hilo.

Naye tabibu wa hospitali ya kanisa la ‘Celestial Church Of Christ, Parokia ya Kadoso ambapo Mercy alijifungulia, aliyetajwa kwa jina la Ajegunle aliliambia Vanguard kuhusu hatua zote alizopitia hadi kujifungua mwanae huyo na jinsi yeye binafsi kama mkunga alivyohusika.

Marafiki na ndugu wa mwanamke huyo walitoa ushuhuda pia kwa gazeti la Vanguard la Nigeria kuhusu tukio hilo la kushangaza.

Video: Bomu Lalipuka na Kuua 21 Katika Duka Kubwa la Manunuzi Abuja, Nigeria

$
0
0
Shambulizi baya la bomu limesababisha vifo vya watu 21 na kujeruhi mamia katika duka kubwa la manunuzi ‘Mall’ jijini Abuja, Nigeria.

AFP imeripoti kuwa bomu hilo limeripuka katika duka la manunuzi la Emab Plaza lililo karibu na Banex Plaza, maduka ambayo huwa na wateja wengi kuliko maduka yote (mall) katika jiji hilo.

“Unaona moshi mkubwa unafuka angani. Ni sehemu ya watu wengi.” Msemaji wa kitengo cha dharura cha Abuja aliiambia AFP.

Ripota wa Vanguard aliyekuwa kwenye eneo la tukio alisikika akiripoti kuwa anaona vipande vya miili ya watu katika eneo hilo na kwamba bado kuna watu wafanyabiashara wengi na watu waliotembelea Mall hiyo wamenasa kwenye jumba hilo.

Zaidi ya ambulance 6 zilionekana zikitoka kwenye eneo la tukio likiwa limejaza majeruhi.

Diamond Azungumzia Tuhuma za Kuiba nyimbo ikiwemo Kitorondo (MdogoMdogo)

$
0
0
Karibu kila mwaka kumekuwa na malalamiko ya wasanii kuhusu kuibiwa nyimbo au idea za nyimbo zao na Mkali wa Ngololo Style, Diamond Platinumz, madai ambayo huzua hisia tofauti kwa watu wengi.

Hivi karibuni, mshiriki wa BSS Wababa naye alijitokeza na kudai kuwa Diamond amemuibia wimbo wake wa Kitorondo na kwamba baadae aliubadilisha jina na kuuita MdogoMdogo.

Diamond amezitolea majibu tuhuma hizo jana (June 25) wakati akifanya mahojiano na Jabir Saleh katika kipindi cha The Jump Offf cha 100.5 Times Fm.

“Unapokuwa mkubwa sana kunakuwa kuna faida yake na madhara yake. Na madhara yake yalivyo, unapokuwa mkubwa sana kitu ambacho hakina maana watu wanajaribu kukifanya kuwa na maana, either kionekane kizuri au kibaya.”Amesema Diamond.

 Mfano nilipotoa Moyo wangu nyimbo nyingi sana zilitoka zinaitwa Moyo Wangu. Lakini hujawahi kusikia hata siku moja nikasema kuna mtu kaniibia. Kwa sababu lile ni neno ambalo wewe unavyojua wewe na mimi nikatumia ninavyojua mimi kwa sababu hakuna mwenye maneno yake duniani.” Alifafanua.

Akizungumzia tuhuma zilizotolewa na msanii Wababa hivi karibuni kuwa alimuibia wimbo wake wa Kitorondo na baadae akaubadili kuwa Mdogo Mdogo, Diamond amesema huo ni wimbo wa Asili ambao ulikuwa unaimbwa na bendi ya Tandale Modern Taarabu, na pia ni ngoma ya mdundiko wa zamani.

“Sitaki niongee kwa sababu nitampa Kick…anyways nilisikia kuna mtu anasema eti hii nyimbo yangu ya MdogoMdogo kuna mtu kaibiwa kwa neno la Kitorondo. Sasa mimi nikuadithie story fupi...mimi nimezaliwa Tandale nimekulia Tandale, kuna bendi ilikuwa inaitwa Tandale Modern Taarab nyimbo yao ya kwanza inaitwa Tandale (anaimba kidogo). Ukiacha hivyo, Kitorondo ni jina ambalo ni ngoma ambayo wanaimba hivyo (anaimba). Yaani hii ni nyimbo.

“Kuna msanii kaichukua kaiimba kama ilivyo ile nyimbo ya mdundiko. Halafu baada ya kusikia neno la Kitorondo kwenye nyimbo yangu akasema yeye kaibiwa nyimbo. Mimi nimepata taarifa nikasema ana akili kweli. Yeye ndio kaenda kuiba. Mimi nimetumia neno la Kitorondo kwa taaluma zangu za kimuziki naliingiza kwa namna gani kama neno, yeye anasema nimemuibia yeye. Sikujisikia vizuri…halafu nikaulizwa kila sehemu nikienda nawaambia msiniulize maswali hayo kabisa.”

Diamond alizungumzia masuala mengi ikiwa ni pamoja na maandalizi ya Tuzo za BET ambapo anategemea kuwa na mkutano wa kimataifa kwa ajili ya tuzo hizo huko Marekani, mkutano utakaowajumuisha wasanii wengi wa kimataifa kama project ya dunia nzima.

Nando Atangaza Kuacha Kutumia Dawa za Kulevya..Kumbe Alikuwa Teja Mkubwa

$
0
0
Mshiriki wa shindano la Big Brother Africa ‘The Chase’, Ammy Nando ameweka wazi kuwa alikuwa mmoja kati ya waathirika wa dawa za kulevya.

Akiongea katika kipindi cha Hatua Tatu ha 100.5 Times Fm, Nando amesema alikuwa anatumia dawa hizo za kulevya kwa muda mrefu na kwamba hadi leno ni wiki ya 16 tangu afanye uamuzi wa kuacha.

Akizungumzia sababu zilizompelekea kutumia dawa za kulevya, amesema ujana na maisha ya starehe aliyoishi vilichochea.

“Sababu ya kuingia huko, ni ujana tu mwanangu…unajua ujana ni maji ya moto kama watu wanavyosema. Na pia pressure na watu nilokuwa nao wakati ule, na life nililoishi mimi…ni yale maisha ya kujiachia.” Amesema Nando.

Hata hivyo, Nando ameeleza kuwa ameachana na dawa za kulevya (unga) lakini bado anatumia bangi kwa hivi sasa japo amepunguza idadi.

“kuhusu bangi…sisi tunaitaga stock, natumia moja au mbili kwa siku.”

Ameongeza kuwa yeye ni mmoja kati ya watu wenye kibali cha kuvuta bangi  kwa maelezo ya daktari kuwa anafanya hivyo kwa lengo la kuacha kutumia unga.

Timbwili lazuka baada ya Jaji Werema kumfananisha Mbunge Kafulila na TUMBILI

$
0
0
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, ameteleza ulimi tena na mara hii amejikuta akimuita Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) tumbili.

Kabla ya kutoa kauli hiyo, Werema alikuwa akitoa ufafanuzi wa mwongozo ulioombwa na Kafulila, kuhusu fedha zilizokuwa katika akaunti ya Escrow iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ambazo zimelipwa kwa kampuni ya PAP, inayomiliki mitambo ya kampuni ya umeme ya Independent Power Tanzania Limited(IPTL).

Werema alisema fedha hizo si za Serikali, kama inavyodaiwa na Kafulila, kwa kuwa fedha za Serikali, hazikai katika akaunti hiyo.

Alifafanua kuwa taarifa zinazotolewa, zinapotosha umma kuwa serikali imetoa fedha kuilipa IPTL, wakati ukweli ni kuwa fedha hizo ziliwekwa katika akaunti hiyo, kutokana na misuguano baina ya wanahisa wawili, waliokuwa wamiliki wa IPTL

Werema alibainisha kuwa mmoja wa wanahisa hao, alikuwa akitaka IPTL ifilisiwe, huku mwingine akipinga jambo hilo mpaka walipouza hisa zao na kumaliza mgogoro huo, ambapo Mahakama iliruhusu mali za kampuni hizo,  apewe mwanahisa mpya, PAP.

Werema alisema kuna watu walileta bungeni  vipeperushi, wakidai ni ushahidi kuhusu utoaji wa fedha hizo za akaunti ya Escrow na kuhusisha na rushwa.

“Kafulila ni miongoni mwa  wanaoeneza taarifa potofu…kama ni tuhuma au kuna rushwa, itakuja kujulikana, tusubiri uchunguzi wa vyombo husika,” alisema.

Wakati akizungumza, Werema alitumia mfano wa kabila la Wanyankole, aliosema kuwa wana usemi unaosema kwamba ‘Tumbili hawezi kuamua kesi ya msituni’.

Kabla ya kufafanua maana ya msemo huo, Kafulila bila kuwasha kipaza sauti, alikuwa akipiga kelele kumuita Werema kuwa ni mtuhumiwa, hivyo atangaze maslahi yake.
“Naomba nisikilize, hata kama ni mtuhumiwa, nina fursa ya kusikilizwa …nisikilize wewe tumbili,” alijikuta akisema Werema.

Baada ya kusema hivyo, Kafulila hakukubali ;na yeye bila kuwasha kipaza sauti, alisema: “Wewe (Werema) ni mwizi tu.”

Kutokana na hali hiyo, Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azan ‘Zungu’ alimuomba Jaji Werema, kukaa chini ili atoe ufafanuzi, huku Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Chadema) na Kafulila wakitaka kuzungumza.

Zungu alisema kwa kuwa Bunge, lilishaamua kuwa suala hilo, lipelekwe Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) na kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ni vyema kama Kafulila ana ushahidi wowote, apeleke huko.

Baada ya kutoa mwongozo huo, ambao ulisitisha malumbano, Mwenyekiti Zungu alisitisha shughuli za Bunge mpaka jioni na kuondoka, huku akisindikizwa na makatibu wa Bunge na wapambe kama kawaida.

Hatua ya Mwenyekiti wa Bunge kuondoka katika ukumbi, baada ya kusitisha shughuli za Bunge, ilimpa fursa Jaji Werema kuweka sawa makabrasha yake na kutoka katika kiti chake, ambapo alionekana kama vile anakwenda kumkabili Kafulila.

Wakati hilo likitokea, Mbunge wa Maswa Mashariki, Sylvester
Kasulumbayi (Chadema), alihama katika kiti chake na kukimbilia alipokuwa amekaa Kafulila.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, baadhi ya mawaziri  walimzunguka Jaji Werema, kabla hajamfikia Kafulila na Kasulumbayi.

Mawaziri hao ni Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Stephen Wassira, Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Asha Rose Migiro na Naibu Waziri wa Afrika Mashariki, Dk Abdullah Juma Abdullah Saadalla.

Nje ya Bunge, Kafulila na Mnyika waliitisha mkutano na waandishi wa habari, ambapo walidai kuwa na ushahidi wa kutuhumu baadhi ya mawaziri, kusema uongo bungeni kuhusu fedha hizo za Escrow.

Confirmed Suarez Kafungiwa Mechi Tisa za Word Cup Baada ya Kumg'ata Mchezaji Mwenzake

$
0
0
Habari za hivi punde breaking news zinasema kuwa FIFA imemuadhibu Suarez kwa kumfungia mechi tisa au miezi 4 na kulipa faini ya franc laki moja. Kwa kipindi chote hicho hataruhusiwa kujihusisha na shughuli zozote za mpira wa miguu

Ally Kiba kwenye Planet Bongo, Sasa nimeelewa kwanini hakui kimuziki

$
0
0


Katika segment ya KITENGO, leo katika Kipindi cha Planet Bongo Kinachorushwa EATV: Host Abdallah Ambua Alimtembelea Msanii Wa Muziki wa B'flava, Ally Salehe Kiba, nyumbani kwao anapoishi yeye na familia yake kwa ujumla::

Nilikuwa na shauku ya kusikia nini ambacho Ally K angekizungumza kuhusiana na Muziki wake kwa ujumla na hii ''Backwardness'' yake licha ya kuwa msanii mkubwa na anayependwa zaidi Bongo; After Interview Nilijifunza vitu vifuatavyo:

Kitu Cha kwanza ambacho kilinistua ni Kuona Setup ya Location ambayo waliichagua kufanyia Interview, Lazima niseme wazi haikuwa Kwa Hadhi yake - Hata km ni usimple, that was too much... Kwa ufupi ilikuwa ni Unprofessional !! Walikaa on a rough and shabby set mpaka nikawa naichungulia mara mbili mbili.

Kingine ni the way anavyojichukulia: Ni mtu ambae anaonesha kama ndoto zake zote kimuziki zimeshatimia, Especially kufanya kazi na msanii mkubwa duniani , R kelly: He sounded like Nani kama mimi in Tz... HAKUNA !

Pia; Namna alivyokuwa anazungumza na kujibu maswali, Haonekani kuwa na strategy zozote za kuukuza Muziki wake na kufanya kitu ambacho mashabiki wake wengi wanakitarajia Aidha ni kwa kutopenda kuanika mambo yake (maybe) lakini as an artist hakuwa na ile promising attitude..

Mengineyo:

Hakuvaa vizuri, Hakuwa na ile starlook kabisa, He looked more of An Underground artist:


My Take:

Inakatisha tamaa kuwa mshabiki wa msanii ambae hana hata dalili za kukata kiu yako kama mshabiki. Ni kwa vile anajua kwamba we are addicted to his music au ni nini?

Ifikie hatua mshkaji ajiongeze kidogo, Music is Business, Na luckily he's on a high demand, Ningefurahi kama angejikagua tena na kufanya kitu ambacho shabiki zake wanapenda.

Nisingependa kumtaja; Lakini Diamond is a nice mirror to look at : Sio dhambi Kuiga vitu vizuri.


NAISAPOTI..................... .......

#BringBackOurArtistCampaigne
#ALLYKIBA

Diamond Adhamiria Kumtoa Wema Kimataifa Amtafutia Madeal Makubwa Nje ya Nchi

$
0
0
Wema Sepetu anatarajia kufanya filamu mpya na wasanii kutoka Ghana ili kutanua wigo wake filamu pamoja na kwenda kimataifa zaidi.

Akizungumza na 225 ya XXL ndani Clouds FM, mpenzi wake na Wema, Diamond Platnumz amesema tayari ameshamfanyia mawasiliano na wasanii wa filamu wa Ghana ili kuhakikisha mwaka huu anafanya filamu ya kimataifa.

“Hapa juzi kati kulikuwa na mazungumzo, kuna mtu mmoja anaitwa Frank yupo huko Ghana, ni mtu mkubwa sana, na yeye ndio anaandaaga zile tuzo za Ghana, kwasababu kuna movie anataka kuifanya baby. Hiyo movie wajue kabisa eeh Sepetunga kaachia mashine mpya. So jamaa yule ana link na watu wengi nikajaribu kuzungumza kuwapata actors na actress ambao anaweza kushirikiana nao kwa sababu namna pekee ya kuweza kutanua market yako katika kazi yoyote ni kushirikiana na mtu ambae yupo katika nchi nyingine ili kuweza wewe kupenyeza bidhaa yako wewe na yeye apenyeze bidhaa yake kwako,” alisema Diamon.

“Kama akina Van Vicker sijui akina nani, nimefanya mazungumzo nao kuangalia namna gani wanaweza kufanya movie na movie ifanyike Tanzania au ifanyike Nigeria au ifanyike Ghana. Ghana, Nigeria ni nchi ambazo zina nguvu kwenye soko la movie Afrika. Wakati nazungumza nao pia uzuri ilikuwa ni rahisi hivi baby kamlink sehemu yoyote ni rahisi sana kwa sababu kwanza ana content nyingi za movie zake. CV zake ni rahisi kumwambia mtu hiki na hiki, kwahiyo mtu akiona anashtuka, yaani mtu anakuwa excited kufanya naye kitu. So na wao pia kuna movie wanataka ashiriki uzuri pia wakasifika Kiingereza chake ni rahisi zaidi kufanya naye kazi. Kwahiyo mwenyezi Mungu akisaidia kuna mipango itakaa sawa basi mwaka huu utakuwa ni mwaka wake mzuri na zaidi nafikiri hata kabla hata mwaka haujaisha hii project itakuwa imekamilika labda inaweza kuwa out sijui yeye ndiyo anajua zaidi lakini. Wajibu wangu ni kutekeleza kuona kwamba baby amefanya movie na fulani na fulani kutoka nchi fulani na movie imekuwa fulani na kulingana alivyokuwa mwanzo na sasa hivi aonekane ame advance kutoka pale alipokuwa mwanzo.”
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images