Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Unaambiwa Hii Ndio Nguo Atakayo Vaa Diamond Kwenye BET Awards...Imetengenezwa Kwa Ajili Yake Tuu

$
0
0
BET Awards zinakaribia kufanyika na Diamond Platinumz anaelekea huko kwasababu amekuwa nominated kwenye kipengele cha Best African Act. Diamond atapita kwenye Red Carpet itakayo tumiwa na wasanii mbalimbali siku ya tukio. 

Hii ni sehemu ya nguo ambayo atavaa siku ya tukio na imetengenezwa na Sheria Ngowi, sehemu moja imeandikwa Mr Diamond Platnumz.

Haya ni maneno aliyoandika alipo-share hii picha.


Tabia za Mama Mkwe Ndio Tabia za Mkeo..Chukua hiyo Kubali Au Kataaa

$
0
0
Kwa utafiti wangu mdogo niliofanya nimegundua kwamba tabia za mama mkwe ndio tabia za mkeo upende usipende.kwahiyo kama una mpango wa kuoa usiishie kumchunguza mchumba wa kike ambaye wakati wa uchumba anakuwa anaishi maisha ya kuigiza bali pia angaika kumchunguza mama mkwe.
kwanini mama mkwe?
1. Mama mkwe ndie aliyemlea mkeo mtarajiwa kwahiyo mchumba wako atakuwa ameiga na kufundishwa kuwa na tabia kama mama yake
2.Mara mwanamke anapoolewa Mshauri mkuu ni mama yake mzazi(napenda uamini hili) kwahiyo maisha yake kwenye ndoa yatategemea ushauri wa mamaye
3.ikitokea mfarakano kwenye ndoa na kama mwanamke ndio tatizo mama mkwe ndie mtu pekee anayeweza kumbadilisha mkeo katika njia sahihi.

Kenya Airways Reports Second-Half Loss as Attacks Scare Visitors

$
0
0
Kenya Airways Ltd., sub-Saharan Africa’s third-biggest carrier, posted a second-half loss after attacks by Islamist militants in the country and a fire at the main airport in the capital scared off visitors.

The loss totaled 3.77 billion shillings ($43 million) in the six months through March, compared with 3.08 billion shillings in the same period a year earlier, according to Bloomberg calculations using Kenya Airways’ published financial results.

For the full-year, the loss was 3.38 billion shillings, compared with 7.86 billion shillings in 2012, the company said in a statement. Profit in the first half was 384 million shillings, according to results published in November.

“During the second half, the company made a loss largely driven by reduced passenger revenues,” the company said. It cited a fire at Jomo Kenyatta International Airport in August that burned down the international arrivals terminal, an attack on the Westgate Mall in Nairobi that killed at least 67 people, and travel advisories by foreign countries including the U.S.

Kenya has faced a growing number of attacks since it deployed troops in neighboring Somalia to fight al-Shabaab, the al-Qaeda-linked group that’s trying to overthrow the government and establish an Islamic state. The raids have dented Kenyan tourism, with arrivals to the East African country falling to 1.4 million last year from 1.7 million in 2012. The industry is the nation’s second-biggest source of foreign currency, generating $1.1 billion in 2013.

Kenya Airways shares fell 5.6 percent to 10.90 shillings by the close in Nairobi, the biggest decline in a year. The stock has fallen 16 percent this year, underperforming the Nairobi Securities Exchange All-Share Index (NSEASI), which has gained 9.7 percent over the same period.
Security Concern

“The security situation in Kenya remains a concern and this has negatively impacted on traffic, especially from Europe,” the company said. “Measures are being taken by management to rationalize capacity in affected markets.”

The carrier plans to focus on developing its markets in Africa to capitalize on increasing trade within the continent and tap growing tourist demand in Asian countries including China, Chief Executive Officer-designate Mbuvi Ngunze said in an interview at the results presentation.


Kenya Airways will also take delivery of five more Boeing Co. (BA) Dreamliner aircraft by October as part of a fleet-renewal program, which the company expects will “improve the customer experience.”


Jaji Werema Adaiwa Kumtishia kifo Kafulila Bungeni Dodoma

$
0
0
Mwanasheria mkuu wa serikali jaji Fredrick Werema ametuhumiwa kumtishia kifo mbunge wa Kigoma Kusini mh David Kafulila,Imedaiwa kuwa jaji Werema alimtolea maneno hayo ya vitisho mh Kafulila jana asubuhi kwenye viunga vya bunge mjini Dodoma baada ya bunge kuahirishwa.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii,mh Werema alimtolea maneno hayo ya kitisho mbele ya mwenyekiti wa Bunge Mussa Hassan Zungu,mwandishi wa habari mmoja alietajwa kwa jina moja la Butare,akiwa na waandishi wa habari wenzake ambao hawakutajwa majina yao ,wakiambatana na mpiga picha ambaye pia ametajwa kwa jina la moja la Edwin na baadhi ya wabunge kadhaa waliokuwa wanapita,mh Werema amanukuliwa akimwambia mh kafulila kwamba "I will take your head,unless you apologize"ikimaanisha atamkata kichwa iwapo hatamwomba msamaha,

Kufuatia sakata hilo mh Kafulila amemthibitishia ukweli wa madai hayo mwandishi wa Bloghii ya " http://nicholauskilunga.blogspot.com/" na kwamba tayari ameshachukua hatua kwa kuiandikia barua ya madai ya kutishiwa maisha ofisi ya spika wa bunge,huku nakala ya barua hiyo akiipeleka kwa mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Mangu na nakala nyingine ameipeleka kwa kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma(RPC Dodoma)mh Kafulila aliendelea kuongea na mwandishi wa habari hii akisema"ni kweli nimetishiwa maisha na mwanasheria mkuu wa serikali leo asubuhi kwenye viunga vya bunge,na nimekwisha chukua hatua tayari,lakini watanzania wakumbuke kwamba nilipokuwa nikichangia hoja ya ufisadi huu wa Escrow wakati wa bajeti ya wizara ya nishati,nilisema,hata kifo cha Mgimwa kilipaswa kuchunguzwa, kwasababu aliugua na kufariki kipindi ambacho kulikuwa na pressure kubwa ya kuzitoa pesa hizi za Escrow na hivyo kuna mashaka sana kuhusu kifo cha waziri huyo hasa ikizingatiwa makosa yaliyofanywa na Hazina na BOT kwa kushirikiana na wizara ya nishati na madini na jaji Werema alihakikisha hizo Bilioni 200 zinatolewa"alimaliza kuongea mh Kafulila.

Mbunge Kafulila ambaye pia ni mbunge Kigoma kusini kupitia chama cha NCCR na waziri kivuli wa wizara ya Viwanda na Biashara,aliendelea kumweleza mwandishi wa habari hii kwamba jaji Werema anajua kila kitu kilichotokea kwenye mchakato huo,anasema jaji Werema ndiye aliyetoa ushauri wa kisheria na kuelekeza bank kuu kuruhusu utolewaji wa fedha hiyo na aliruhusu hayo akiwa kama mwansheria wa mkuu wa serikali,na hatua yake yake hiyo ya kuruhusu utolewaji wa fedha hiyo kufuatia wizara ya nishati na madini kuwa tayari ilikwisha saini makubaliano na kampuni aliyoiita ya kitapeli inayomilikiwa na mtu alieitwa na mh Kafulila kuwa Singasinga ijulikanayo kama PAP iliyopewa fedha hizo kama mmiliki halali wa wa fedha hizo wakti haikuwa na sifa hiyo.

Nae mh Werema alipopigiwa simu na mwandishi wetu na kutakiwa kuthibitisha ukweli wa taarifa hizi za madai ya kutishia kumwua mh Kafulila alijibu"Hilo jambo si jambo la kitaifa,tafadharini sana msilifanye kuwa la kitaifa,mimi nilifikiri umenipigia kwa ajili ya kuzungumzia mambo ya kitaifa,kwa hili sina majibu naomba uniache nipumzike"alimaliza kuongea mh Werema huku akikwepa swali la msingi alilokuwa ameulizwa na mwandishi hii,

Sakata hili liliibuka jana bungeni mjini Dodoma,kufuatia mwongozo uliokuwa umeomba na mh Kafulila kuhusiana na majibu ya waziri wa nishati na madini aliedai kwamba alilidanganya Bunge na kusema uwongo ndani ya bunge tena mbele ya waziri mkuu,pale alipokuwa akijibu hoja juu ya madai ya ufisadi kwenye akaunti ya Escrow na kusema kwamba fedha hizo zilitolewa baada ya kesi kuamuliwa,ndipo alipotaka muongozo katika suala hilo hali iliyomlazimisha mwanasheria wa serikali jaji Werema kuingilia kati na kujibu swala hilo kwa kusema taratibu zote zilifuatwa wakati wa utolewaji wa fedha hizo, na ni kweli kesi ilikuwa imekwisha amuliwa,wakati akiendela kuongea mh Werema alienda mbali zaidi kwa kulitolea mfano wa kabila lake kwamba wanamsemo mmoja kwamba Tumbili hana maamuzi ndani ya msitu hali iliyotafsiriwa kumlenga Kafulila ambaye nae alimjibu kwamba ni mwizi hali iliyompandisha hasira zaidi jaji Werema huku akivuka mstari na kutaka kwenda kumpiga mh Kafulila kabla wabunge kumzuia jaji Werema na baadae kutolewa nje na askari wa bunge.


Mheshimiwa Kafulila alisema kinachofanywa na serikali ni sawa na kile kilichotokea mwanzoni mwa miaka ya 2006 na 2007 pale katibu mkuu wa CHADEMA na aliekuwa mbunge wa jimbo la Karatu Dr Wilbroad Slaa pale alipoibua ufisadi mkubwa kwenye akaunti ya madeni ya nje yaani EPA,alisema mwanzoni mwa sakata lile serikali na chama cha mapinduzi walilipinga sana na kusema madai yale yalikuwa ya uzushi mtupu na kwamba hayana ukweli wowote,lakini baadae yalibainika kuwa madai ya kweli,

Tulijaribui kuwasiliana na ofisi ya spika kuthibitisha madai ya kupokea barua hiyo,lakini ilishindikana mpaka tunakwenda mtamboni,lakini tunawaahidi wasomaji wetu wapendwa kwamba kesho tutaweka hapa nakala ya barua hiyo,hivyo endelea kutusoma na kutufuatilia.

Ukiwa na Mpenzi Mwenye Haiba hii, Kujenga Uhusiano Imara ni Mashaka

$
0
0
Wataalamu wa tabia na mienendo ya binadamu wanasema, kuna Makundi kadhaa ya haiba. Wana maana kwamba, binadamu wamegawanyika katika Makundi kitabia.

Je, wewe uko kwenye kundi lipi?

Hiki ndicho ninachotaka kuwasaidia siku ya leo.

Lakini leo ningependa kuwazungumzia watu wenye haiba ya ukamilifu. Hawa ni wale watu ambao wanaamini kwamba, hawapaswi kukosea. Kwao, wanaamini kuwa, mtu anatakiwa afanye kwa usahihi na ukamilifu na kukosea kuna maaana ya udhaifu mkubwa na unyonge.

Nguvu kubwa ya watu hawa iko kwenye usahihi, ukamilifu na kurekebisha makosa. Iko kwenye kufanya ambavyo mtu angetakiwa kufanya, na kufanya mambo kwa usahihi.

Watu hawa wenye haiba ya usahihi huko ndani mwao kuna sauti (little voices) ambazo zina nguvu sana kwao, zenye kuwaamuru wafanye mambo bila kukosea. Lakini, sauti hizi zinakosoa na kuwadhibiti wahusika kwa njia yenye kuwaumiza. Huwa ni sauti zenye kuzalisha mashaka. Kushtakiwa na dhamira na hofu.

Kwa sababu ni watu wanaoamini katika “nzuri na sahihi,” inakuwa ni vigumu sana kwao kuishi na watu wengine kwa amani. Mbaya zaidi ni kwamba, wapenzi wao hupata shida sana kuendana nao. Hii ni kwa sababu, wanataka mambo yaende kwa njia yao, yawe sahihi. Kuna, “ingetakiwa iwe hivi,” nyingi sana.

Watu hawa huwafanya wengine wanaohusiana nao kuhisi kama vile wanatembea juu ya maganda ya mayai.

Kwa nini?

Ni kwa sababu hawa watu wenye haiba hii, hujiona wanaweza kuliko wengine na wanastahili kuliko wengine. Watu hawa wana tabia ya kusema au kumwambia mtu ukweli moja kwa moja kwa njia yenye kukera sana. Hali hii huwasononesha watu wanaoambiwa ukweli.

Watu ambao wameoa au kuolewa na wenye haiba hii, huwa wanatamani kuona mambo yakiwa tofauti kidogo. Wanajihisi kufungwa pumzi, kukaliwa kooni, kufungiwa kwenye dema na kushindwa kuona nafasi yao kama watu huru. Huhisi kuwa wao ni watoto, wanaokosea kila kitu, kwani ndivyo sauti za wapenzi wao zinavyowaambia kila wakati.

Inabidi mtu wa haiba hii ajifunze kukubali makosa, kwamba, kukosea siyo udhaifu, bali kujifunza. Ajue kwamba, kuna njia nyingi za kujifunza mambo, siyo njia moja tu ya “usahihi.” Kuna ya kukosea na kujifunza makosa, halafu ndiyo usahihi ufuate.

Mzee wa Kanisa Aaibika, Kisa Vibinti Under 18, Achomoliwa Gesti Apelekwa Kanisani Mzombe Mzombe

$
0
0
Stori: Richard Bukos na Issa Mnally
Tumekwisha! Mzee wa kanisa la kiroho (jina linahifadhiwa kwa sasa), aliyetajwa kwa jina la Luca Pesa, mkazi wa Segerea, Dar, ameaibika baada ya kukurupushwa kwenye nyumba ya kulala wageni (gesti) akidaiwa kutaka kuvunja amri ya sita na binti ambaye ni msanii chipukizi wa filamu za Kibongo, Debora Jacob, Ijumaa lina kisanga cha aina yake.

HABARI KAMILI
Tukio hilo ambalo kamwe Luca hawezi kulisahahu maishani mwake, lilijiri kwenye gesti hiyo iliyopo karibu na Kituo Kikuu cha Mabasi cha Segerea, Dar, Jumanne iliyopita huku mzee huyo akishushiwa tuhuma nzito ya rushwa ya ngono kwa vibinti chini ya miaka 18.

Katika tukio hilo, mzee huyo wa kanisa na msanii huyo wa Kundi la Maigizo la Vivif lenye maskani yake maeneo hayo walikuwa wamejichimbia kwenye gesti hiyo katika chumba ambacho mlangoni kilikuwa kimeandikwa Rombo kabla ya kuchomolewa na kufikishwa kanisani kisha polisi.

TUHUMA NZITO
Timu ya Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers, ikiwa kwenye mingo zake, ilipokea simu kutoka kwa dada aliyejitambulisha kwa jina moja la Diana na kujieleza kuwa anatoka kundi la sanaa za maigizo la Vivif lililopo Segerea jijini Dar.

OFM: Ndiyo hujakosea unazungumza na
OFM, tukusaidie nini?
Diana: Kuna mzee wa kanisa la kiroho la (anataja jina la kanisa hilo) lililopo maeneo ya Segerea, aliomba kuwa mfadhili wa kundi letu.


Tulimkubalia na baada ya muda alianza kutumia fedha zake vibaya kwa kufanya vitendo visivyofaa.
OFM: Vitendo gani visivyofaa?
Diana: Anawarubuni mabinti wadogo anawaweka kambini na kula nao tunda tamtam eti ndiyo tiketi ya kuchezeshwa kwenye maigizo.
OFM: Tiririka!

Diana: Yaani hadi muda huu ninapozungumza na ninyi mzee huyo wa kanisa anachati na msanii mwingine wa kundi hilo. Anaitwa Debora anataka waende kwenye gesti fulani wakanogeshane, wahini tayari mtego umewekwa utafyatuka muda wowote.

UDHALILISHWAJI?
Diana alisema baada ya Debora kuombwa ‘mambo’ ndipo akawataarifu wasanii wenzake na kuwataka wote kwa pamoja waungane kuikomesha tabia hiyo chafu ya Luca anayelichafua kanisa la kiroho na kulidhalilisha kundi lao la sanaa.

OFM MZIGONI
Baada ya kuseti kila kitu, Diana aliiomba OFM iambatane nao kwani muda huo tayari Debora alishatangulia kwenye gesti hiyo kumfuata mzee huyo wa kanisa ambaye alishachukua chumba.


Taarifa hiyo ilipokelewa kwa mikono miwili na kiongozi wa OFM ambaye aliwaagiza vijana wake makini ambao walisitisha kazi nyingine za kiintelijensia kisha kuelekeza nguvu zao eneo la tukio.
Vijana hao walitumia pikipiki zao ziendazo kasi ambapo baada ya muda usiozidi dakika ishirini walikuwa wamefika kwenye gesti hiyo.

ENEO LA TUKIO
OFM walipofika eneo la tukio, walikuta kundi la wasanii hao wakimchomoa gesti mzee huyo wa kanisa ambaye aliruka ukuta na kudondokea kwenye matuta ya viazi.

Akiwa anajizoazoa kwenye matuta hayo, kundi la wasanii hao lilimuunganishia ambapo kabla ya kumnasa aliingia kwenye chumba cha nyumba iliyopo jirani na gesti hiyo ili kujisalimisha.
Hata hivyo, zoezi lake lilifeli baada ya wasanii hao kumtahadhalisha mwenye nyumba hiyo kuwa wanamtaka mtuhumiwa wao la sivyo wangeichoma moto.

Baada ya kuzingirwa na wasanii hao huku akihatarisha maisha yake kwa kuwa wasanii hao walikuwa na hasira, aliona yasiwe makuu akaamua kuwaruhusu wamtoe mtuhumiwa wao wakamalizane naye kanisani.

KABANG!
Alipotiwa mikononi, mzee huyo wa kanisa aliomba apelekwe kanisani ambapo hapakuwa mbali na eneo la tukio ili akahifadhi vitu vyake muhimu pamoja na kuomba ushauri.

APELEKWA MSOBEMSOBE KANISANI
Kundi hilo la wasanii lilimpeleka kanisani msobemsobe ambapo baada ya hatua kadhaa polisi walitokea na kuwadhibiti wananchi wenye hasira na wasanii waliotaka kumdhuru mzee huyo wa kanisa wakati akipelekwa kanisani.

MTAANI WERAAA!
Wakiwa mitaani, njiani mabinti walikuwa wakipiga kelele ‘weraaa…ukomeee…’ huku wakifurahia kufunga mitaa kwa madai kwamba mzee huyo wa kanisa alizidi.
Katika sekeseke hilo, polisi hao walimtia pingu mzee huyo wa kanisa na kuongoza safari ya kuelekea kanisani.

Wakiwa kanisani hapo polisi walijitambulisha na kuwauliza wachungaji pamoja na waumini wa kanisa hilo kama walimfahamu mzee huyo wa kanisa.

BREKI YA KWANZA POLISI
Kundi la wazee pamoja na vijana wa kanisa hilo walikiri kuwa Luca ni mmoja wa wazee wa kanisa hilo ndipo polisi hao wakamruhusu kuwakabidhi baadhi ya vitu vyake ikiwemo simu na fedha kisha breki ya kwanza ikawa Kituo cha Polisi cha Tabata-Shule ambapo alifunguliwa jalada la kesi namba RB/3843/2014 -RUSHWA YA NGONO, KUWAWEKA KAMBI KINYUME CHA SHERIA WASICHANA WENYE UMRI CHINI YA MIAKA 18 NA KUWADHALILISHA KIJINSIA.

Hadi OFM wanaanua jamvi kituoni hapo kanisa lilikuwa likihaha kumchomoa kwa dhamana akisubiri sheria kuchukua mkondo wake.

Wakati Hata Arobaini Bado Mke wa Marehemu George Tyson Ataka Mali zake

$
0
0
Stori: ShanI Ramadhani na Mayasa Mariwata
Wakati hata siku arobaini hazijatimia, mke wa marehemu George Otieno ‘Tyson’, Beatrice Shayo juzi alicharukia mali zake baada ya kuamua kutinga nyumbani kwa marehemu, Mbezi Makonde jijini Dar kwa lengo la kuchukua kila kinachomhusu.

Mdada huyo aliyefunga ndoa na Tyson Agosti 9, 2012 nchini Kenya na kujaaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume aitwaye Eugene, alishuhudiwa na gazeti hili Juni 24, mwaka huu saa sita usiku akiwa na ndugu zake na kuanza kugonga geti la nyumba hiyo.

Katika kujua kilichokuwa kikiendelea, mmoja wa mapaparazi wetu aliwasogelea na kuzungumza na Beatrice ambaye alieleza kuwa, lengo lake lilikuwa ni kuchukua mali zake zilizomo mle ndani.
“Ulidhani mimi nataka kuingia kwenye nyumba hii nikae, la hasha! Nimefuata mali zangu tu basi,” alisema Beatrice huku akiendelea kugonga geti hilo.

Wakati Beatrice na nduguze wakionekana kukata tamaa ya kufunguliwa, mara alitokea mwanamke anayedaiwa alikuwa akiishi na marehemu mpaka kifo kilipomkuta na kuuliza aliyegonga geti ni nani, alipotajiwa jina la Beatrice alisema: “Eee, Beatrice, usiku huu umekuja kutafuta nini?”
Beatrice: Nina shida, naomba ufungue tuongee.

Mwanamke: Hatuwezi kuongea usiku huu, uje kesho asubuhi.
Beatrice: Nakuomba ufungue tu, nimekuja kuchukua mali zangu nilizoacha humo ndani na nimekuja na gari kabisa la kubebea.

Mwanamke: Mali gani, humu hamna chako na kama una kitu chako humu, fuata taratibu.
Beatrice: Nimefuata taratibu, nipo na mjumbe hapa.
Mwanamke: Ndiyo nasema mje kesho asubuhi na mapema mtanikuta.
Baada ya mwanamke huyo kugoma kufungua, mjumbe wa eneo hilo aliyefahamika kwa jina la Sabina Mawanda aliwashauri waondoke na kurudi tena asubuhi lakini inadaiwa walipofanya hivyo walikuta nyumba imefungwa na hakukuwa na mtu.
GPL

'Mwezi Mtukufu Huu ni Kutulia na Kujipodoa tu, Mkorogo Utanikoma' Maimartha Jesse

$
0
0
Mtangazaji ambaye pia ni mjasiriamali, Maimartha Jesse amesema anafurahia ujio wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwani kazi yake itakuwa ni kutulia na kujipodoa tu.Akipiga stori na Ijumaa Mai alisema mwezi huo huwa mishemishe zake zikiwemo za u-MC anaziweka kando na kwamba atatumia muda mwingi kutengeneza mwili wake.

“Yaani mkorogo utanikomaje, nakuambia hadi Mwezi wa Ramadhani unaisha nadhani nitakuwa kama mwarabu, sitakuwa na la kufanya, nitakuwa ni mtu wa kujipodoa tu,” alisema Mai.

Diva Loveness'Huwa Mnahisi niko na Fimbo nini? Nina Mguu, Nina Hilo Tako saizi yangu, Nina Tattoo na Mengine Malizia

$
0
0

DIVA Shows Off Her  Body Mtakoma Mwaka Huu.....Team Nanilii Mpo? Hakuna kuedit Hapo kitu kipo real Kabisa...

Hali ya Jack Gerezani Macau Nchini China Siyo Nzuri

$
0
0
UNAWEZA kusema ni majanga juu ya majanga yanazidi kumkumba modo wa Bongo, Jacqueline Patrick ‘Jack’ baada ya wiki iliyopita kushindwa kupanda kortini kufuatia kutetereka kwa afya yake bila kufafanuliwa. Mbali na kuwa na afya tete, pia Jack anadaiwa kulalamikia haki za msingi za kibinadamu ambazo anazikosa mahabusu kwa kuishi maisha kama ya mtu aliye kifungoni.

Akizungumza juzi jijini Dar, mtu anayejitolea kumpa msaada na kumtembelea Jack mahabusu, Macau, China alikoshikiliwa, Matilda- alisema Jack anaumia kwa kupewa maisha kama tayari amehukumiwa, anaona bora hukumu yake ipite ajue moja. “Kiukweli Jack anaumwa, alishindwa hata kwenda mahamani, mbaya zaidi hata wakili wake naye hakutokea siku hiyo.

“Halafu kule mahabusu anafanyishwa kazi ngumu ambazo hastahili kama mahabusu na amesema hata watu wake wa karibu ambao anaamini kwa kipindi hiki wangekuwa wanampa faraja hawaoni, anatamani angekamatiwa Bongo labda kuna watu wanapenda kwenda kumtembelea kule Macau lakini hawana uwezo.

“Wabongo wengi ambao wako Macau kwa ajili ya sanaa ya sarakasi ndiyo kidogo wanakwenda kumtembelea siku mojamoja,” alisema Matilda.
Juni 20, mwaka huu, Mbongo Fleva anayedaiwa ni mtu wa karibu na Jack, Juma Khalid ‘Jux’ na kumuuliza kwa nini hajawahi kwenda kumtembelea ‘bebi’ wake mahabusu kama wanavyofanya Wabongo ambao wako Macau, akajibu: “Sipendi kusikia ishu yoyote inayomuhusu Jack kwani nina mambo mengi ya kuongelea na si ishu za Jack kila kukicha.

“Kwa kipindi hiki sitahitaji mtu aniulize ishu za Jack, zinanitibua sana na kama kuongelewa zimeshaongelewa hivyo sioni kipya.” Hii ni mara ya tatu kwa Jack kupanda mahakamani, mara ya kwanza ilikuwa Aprili 10, mwaka huu kosa likiwa kukutwa na madawa ya kulevya tumboni aina ya heroin kete 57 au kilo 1.1 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 223. Mara ya pili ilikuwa Mei 23, mwaka huu

Picha: Jokate na Pozi Lenye Utata..Shanga na Kiuno

$
0
0
Mwanamitindo maarufu na mbunifu wa mavazi nchini, Jokate mwegelo (pichani) akiwa kwenye pozi lenye utata..Watu na Viuno vyao Shanga pale kati

Samuel Misago(EA Radio/TV) vs B-Dozen(Cloudz FM) nani zaidi?

$
0
0

1.SAM MISAGO vs B-TWELVE

2.ADAM MCHOMVU vs ABDALA(dulla wa planet bongo)

*hawa jamaa wanaendana sana kiutangazaji bila kusahau 'swaga' na wote wako hot kiukweli(wanajua),yupi anakukosha zaid kati yao katika kila kipengele?

NB:kama huwa huwasikilizi/huwajui usicomment

Ni Watanzania Wangapi Wamefungwa Brazil Mwaka Huu kwa ishu za Dawa za Kulevya? Vigogo Waliokamatwa Je?

$
0
0
January 2014 balozi wa Tanzania nchini China aliongea kwenye exclusive interview na millardayo.com na kusema Watanzania wanaoshikiliwa kwenye magereza mbalimbali nchini humo hawazidi 200 lakini idadi yao ni zaidi ya 100 ambapo asilimia kubwa kilichowapeleka huko ni kesi za dawa za kulevya.
Ilipofika March 25 2014 katibu mkuu wa wizara ya mambo ya nje John Haule alitaja idadi ya Watanzania waliokamatwa kwa ishu ya dawa za kulevya China na nikamkariri akisema ‘Katika Magereza ya China mpaka February 2014, tumepewa taarifa na mamlaka za China kwamba wapo Magerezani Watanzania 177 ambapo 15 kati yao wamehukumiwa kunyongwa kutokana na biashara hiyo ya dawa lakini niseme tu wenzetu wa Serikali ya China wanatuthamini sana kama sisi tunavyowathamini’
Alimalizia kwa kusema ‘wenzetu wa China wanathamini zaidi uhusiano wetu na ndiyo maana hata wale wachache Watanzania waliohukumiwa kunyongwa hawajanyongwa mpaka leo na hatutegemei kama watanyongwa, yani sanasana watafungwa kifungo cha maisha gerezani’

Sasa taarifa iliyotoka June 25 2014 kutoka tume ya kudhibiti dawa za kulevya imesema wamekamata zaidi ya tani 2.3 za dawa za kulevya na vilevile vigogo 12 wa biashara hiyo wamekamatwa.
Kingine ni kwamba kwa mwaka huu wa 2014 pekee idadi ya Watanzania waliofungwa nchini Brazil kwa kesi za dawa za kulevya ni 113 ambapo taarifa hiyo haikufafanua zaidi kuhusu hukumu zao na mengine yanayoambatana.

Msikilize Nuhu Mziwanda na Shilole Wakiongea Kuhusu Penzi leo na Kuhusu Ndoa

$
0
0
Wapenzi wanaotoka kiwanda cha muziki Tanzania Nuh Mziwanda na Shilole leo walikua kwenye kipindi cha Leo tena ambapo walikua kama wageni kwenye kipengele cha Hekaheka,sasa yameibuka mengi ambayo mengine hatuyafahamu kuhusu uhusiano wao.

Bonyeza play kusikiliza.

Dk Salim: Sina Mpango na Urais 2015, Sifikirii Tena, Hii ni Zamu ya Kizazi Kingine

$
0
0
Asema alipogombea 2005 alibaini kwamba mbali na rekodi ya utendaji, kuna mambo mengine yanayohitajika katika kinyang’anyiro hicho

Dar es Salaam. Waziri Mkuu mstaafu, Dk Salim Ahmed Salim amesema hana mpango na hafikirii tena kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili nyumbani kwake Masaki, Dar es Salaam jana, Dk Salim alisema alipowania nafasi hiyo mwaka 2005, hakuwa na ufahamu mzuri kuhusu mchakato huo lakini baadaye alibaini kwamba, mbali na rekodi ya utendaji, kuna mambo mengine yanayohitajika katika kinyang’anyiro hicho na kwamba hata watu wanaomfikiria na kutaja jina lake miongoni mwa wanaoweza kuwania tena nafasi hiyo, wanakosea.

“Sifikirii tena, hii ni zamu ya kizazi kingine. Ila nitaendelea kuisaidia nchi yangu katika nyanja mbalimbali kadri ya uwezo wangu,” alisema.

Dk Salim ambaye mbali na uwaziri mkuu amewahi kushika nafasi nyingine mbalimbali kitaifa na kimataifa, alisema uzoefu alioupata katika kinyang’anyiro cha urais unatosha.

Alipoulizwa kama uzoefu huo ni mbaya au mzuri kwake, alisema ni mchanganyiko.

Dk Salim aliwahi kugombea nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) na kushindwa kutokana  na kura ya veto ya Marekani, pia aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), sasa Umoja wa Afrika (AU). Pia aliwahi kuwa Rais wa Bunge Kuu la UN mwaka 1979 na 1980.

Licha ya kujitokeza mara moja kuomba uteuzi wa CCM kuwania urais 2005, nyota yake katika nafasi hiyo ilianza kuwaka tangu mwaka 1985 akiwa Waziri Mkuu pale aliposhindanishwa katika Kamati Kuu ya CCM na aliyekuwa Waziri Mkuu, Rashidi Kawawa pamoja aliyekuwa Makamu wa Rais wakati huo, Ali Hassan Mwinyi ambaye alipitishwa kiitifaki na kushinda kiti hicho.

Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, Makamu mwenyekiti mstaafu wa CCM, Pius Msekwa alisimulia jinsi Mwinyi alivyopita, kwa sababu alikuwa Makamu wa Rais, hivyo wajumbe wa Kamati Kuu walikosa hoja na sababu za kumwacha na kumchukua Waziri Mkuu aliyekuwa chini yake kiitifaki.

“Makamu wa Rais ukimruka maana yake hatoshi, wakaona hawana maelezo hayo, ikabidi wamteue Mwinyi,” alisema Msekwa.

Wanachama 34 CUF wawakataa Seif, Lipumba

$
0
0
Wanachama 34 wa Chama cha Wananchi (CUF), wamepiga kura za kuwakataa Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu wake, Maalim Seif Sharif Hamad.

Hata hivyo, pamoja na idadi hiyo ndogo kuwakataa, Profesa Lipumba na Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, walipata ushindi wa kishindo. Katika uchaguzi huo, Maalim Seif ambaye alikuwa mgombea pekee kwa nafasi ya katibu mkuu, alichaguliwa kwa kura 675 kati ya 678 sawa na asilimia 99.5 na Profesa Lipumba alichaguliwa kuwa mwenyekiti baada ya kupata kura  659 kati ya 690 zilizopigwa sawa na asilimia 95.7.

Wanachama wa CUF ambao walipiga kura kuanzia saa tisa alasiri, walibaki ukumbini hadi saa tatu usiku kusubiri matokeo hayo ambayo baada ya kutangazwa yaliamsha hoihoi, nderemo na vifijo.

Akitangaza matokeo hayo, msimamizi wa uchaguzi huo, Awadhi Said alisema Profesa Lipumba alimshinda Lutayosa Yemba aliyepata kura 30 sawa na asilimia 4.3. Mgombea mwingine, M’bezi Adam Bakari alijitoa muda mfupi kabla ya wajumbe hao kuanza kupiga kura akisema: “Nilikuwa naonja demokrasia ndani ya chama chetu lakini nimeona mzigo mzito ni bora nimpe Mnyamwezi.” Licha ya kufafanua ilionekana alikuwa akimlenga Profesa Lipumba ambaye ni wa kabila hilo. Hii ni mara ya nne kwa Profesa Lipumba kushinda nafasi hiyo.

Msimamizi huyo pia alimtangaza Waziri wa Afya wa Zanzibar, Dk Juma Duni Haji kuwa makamu mwenyekiti wa chama hicho baada ya kupata kura 662 kati ya kura 667 zilizopigwa sawa na asilimia  99.25.

Ahadi

Akitoa shukrani, Maalim Seif alishukuru kwa kuchaguliwa na akawaahidi Watanzania katiba yenye maoni ya wananchi... “Mmenipa heshima kubwa lakini ili kulipa fadhila nitahakikisha napigania kupata Katiba Mpya yenye maoni ya wananchi. Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ndiyo tumaini letu tutapambana hadi tupate katiba yenye maoni ya wananchi.”

Alisema CUF hakitakubali kuburuzwa katika mchakato wa Katiba na kitakuwa mtetezi wa masilahi ya wananchi wote.

Profesa Lipumba aliwashukuru wajumbe wa mkutano huo kwa kumchagua na kusema kupitia Ukawa, Watanzania watapata katiba iliyo bora.

“Tutapambana hadi kieleweke kwa kuwa Ukawa ndiyo tumaini letu. Watanzania wafahamu kwamba tuko pamoja tutawapigania ili wapate katiba wanayoitaka,” alisema.

Mgombea wa uenyekiti aliyeshindwa, Yemba alisema uchaguzi huo ulikuwa huru na haki na akawapongeza waliochaguliwa... “Nimeshindwa uchaguzi huu lakini nitaendelea kuwa mwanachama mwaminifu katika chama chetu.”

Werema: Nina watoto halafu natukanwa?

$
0
0
TAFRANI iliyojitokeza bungeni juzi kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Frederick Werema kumuita Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila(NCCR Mageuzi) tumbili, naye kumjibu kwa kumuita mwizi imeingia katika hatua nyingine ambapo wawili hao wamekataa kusuluhishwa. Jana asubuhi baada ya Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuahirisha shughuli za Bunge, Mwenyekiti wa Bunge, Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan ‘Zungu’, aliwakuta Werema na Kafulila wakiendeleza mzozo nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma.

Kutokana na hali hiyo, Zungu alijitolea kuwapatanisha huku akijaribu kukaa katikati awashikishe mikono ili yaishe, lakini hakufanikiwa. Lawama Wakati Zungu akifanya jitihada hizo, Werema alilalamika.

“Mimi nina watoto na wajukuu unanitukana… kwani ninyi hamkusikia akinitukana?” Alihoji huku baadhi ya waandishi wakishuhudia.

Wakati Werema akilalamika kutukanwa huku Zungu akiwa katikati yao, Kafulila naye alilalamika: “Wewe uliniita mimi mnyama(Tumbili) kumbuka vizuri.”

Werema akijibu malalamiko ya Kafulila, alisema yeye hakuwa na nia ya kumtukana bali alikuwa akielezea msemo wa Wanyankole kuwa tumbili hawezi kuamua kesi ya msituni na kukataa kushikana mkono na Kafulila akisisitiza aombe radhi.

Kutokana na hali hiyo, Kafulila aliondoka kutoka nje ya uzio wa ukumbi wa Bunge bila kuomba radhi huku akimnyooshea kidole Werema, ambaye naye aliingia katika ofisi za Bunge huku akilalamika kutukanwa na Kafulila.

Chanzo Juzi kabla ya kutoa kauli hiyo, Werema alikuwa akitoa ufafanuzi wa muongozo ulioombwa na Kafulila kuhusu fedha zilizokuwa katika akaunti ya Escrow iliyokuwa Benki Kuu (BoT), ambazo zimelipwa kampuni ya PAP, inayomiliki mitambo ya Kampuni ya Independent Power limited(IPTL).

Werema alisema fedha hizo si za Serikali kama inavyodaiwa na Kafulila kwa kuwa fedha za Serikali hazikai katika akaunti hiyo.

Aliendelea kufafanua kuwa taarifa zinazotolewa zinapotosha umma kuwa serikali imetoa fedha kuilipa IPTL, wakati ukweli ni kuwa fedha hizo ziliwekwa katika akaunti hiyo kutokana na misuguano baina ya wanahisa wawili waliokuwa wamiliki wa IPTL. Werema alibainisha kuwa mmoja wa wanahisa hao, alikuwa akitaka IPTL ifilisiwe huku mwingine akipinga juu ya jambo hilo mpaka walipouza hisa zao na kumaliza mgogoro huo, ambapo Mahakama iliruhusu mali za kampuni hizo zipewe kwa mwanahisa mpya, PAP. Werema alisema kuna watu walileta bungeni vipeperushi wakidai ni ushahidi kuhusu utoaji wa fedha hizo za akaunti ya Escrow na kuhusisha na rushwa.

“Kafulila ni miongoni wanaoeneza taarifa potofu…, kama ni tuhuma au kuna rushwa itakuja kujulikana, tusubiri uchunguzi wa vyombo husika,” alisema.

Tumbili Wakati akizungumza, Werema alitumia mfano wa kabila la Wanyankole, aliosema kuwa wana usemi unaosema kwamba tumbili hawezi kuamua kesi ya msituni. Kabla ya kufafanua maana ya msemo huo, Kafulila bila kuwasha kipaza sauti alikuwa akipiga kelele kumuita Werema kuwa ni mtuhumiwa hivyo atangaze maslahi yake.

“Naomba nisikilize hata kama ni mtuhumiwa nina fursa ya kusikilizwa …nisikilize wewe tumbili,” alijikuta akisema Werema.

Baada ya kusema hivyo, Kafulila hakukubali na yeye bila kuwasha kipaza sauti alisema:

“wewe (Werema) ni mwizi tu.” Zungu Kutokana na hali hiyo, Mwenyekiti wa Bunge, Zungu alimuomba Jaji Werema kukaa chini ili atoe ufafanuzi, huku Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Chadema) na Kafulila wakitaka kuzungumza.

Zungu alisema kwa kuwa Bunge lilishaamua kuwa suala hilo lipelekwe Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) na kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ni vyema kama Kafulila ana ushahidi wowote, apeleke huko.

Baada ya kutoa muongozo huo, ambao ulisitisha malumbano, Mwenyekiti Zungu alisitisha shughuli za Bunge mpaka jioni na kuondoka huku akisindikizwa na makatibu wa Bunge na wapambe kama kawaida.

Tafrani Hatua ya Mwenyekiti wa Bunge kuondoka katika ukumbi baada ya kusitisha shughuli za Bunge, ilimpa fursa Jaji Werema kuweka sawa makabrasha yake na kutoka katika kiti chake, ambapo alionekana kama vile anakwenda kumkabili Kafulila.

Wakati hilo likitokea, Mbunge wa Maswa Mashariki, Sylvester Kasulumbai (Chadema), alihama katika kiti chake na kukimbilia alipokuwa amekaa Kafulila. Katika hali isiyokuwa ya kawaida, baadhi ya mawaziri walimzunguka Jaji Werema kabla hajamfikia Kafulila na Kasulumbai.

Mawaziri hao ni pamoja na Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Stephen Wassira, Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Asha- Rose Migiro, Naibu Waziri wa Afrika Mashariki, Dk Abdullah Juma Saadalla na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Simbachawene.

Nje ya Bunge, Kafulila na Mnyika waliitisha mkutano na waandishi wa habari, ambapo walidai kuwa na ushahidi wa kutuhumu baadhi ya mawaziri kusema uongo bungeni kuhusu fedha hizo za Escrow.

Serikali yapiga Marufuku tabia ya Trafiki kujificha Vichakani kuvizia magari barabarani

$
0
0
Serikali imepiga marufuku tabia ya askari Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani, kuvizia magari katika barabara kuu wakiwa na kifaa cha kupima mwendo kasi wa magari.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Peraira Silima, alisema tabia hiyo ya trafiki ni kinyume cha sheria na zinaweza kusababisha ajali.

 Hata hivyo, Silima aliwataka madereva kutii Sheria za Barabarani ikiwemo kupunguza mwendokasi na kufafanua kuwa, wakati mwingine askari hutafuta kivuli na hatua hiyo isichukuliwe kuwa wanavizia magari.

Katika swali lake, Ngoye alitaka Serikali ieleze ni hatua gani zimekuwa zikichukuliwa kuhakikisha madereva wanafuata sheria zilizowekwa kama inavyofanyika katika nchi nyingine.
Ngoye pia alitaka Serikali ieleze kwa nini madereva wameendelea kutumia magogo, mawe na majani yenye miba barabarani kuashiria kuwa kuna gari limeharibika, na wakiondoka wanayaacha na wengine wameendelea kuendesha magari huku wakisikiliza simu.

 Naye Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema), alihoji kama ni sahihi kwa trafiki kuvizia magari na kifaa cha kupima mwendo kasi.


Akifafanua majibu ya maswali hayo, Silima alisema trafiki kujificha na chombo hicho na kujitokeza kusimamisha  gari ni kinyume cha sheria  kwa kuwa tabia hiyo inaweza kusababisha ajali.

 Kuhusu matumizi ya magogo, majani na mawe, alisema ni kinyume na Sheria na kutaka madereva watumie alama za pembe tatu ambazo ni nzito na kuachana na alama hizo ambazo ni nyepesi ambazo hupeperushwa na upepo.

 Silima pia alionya kuwa Serikali iko mbioni kuanza kuwanyang’anya leseni za udereva madereva wote ambao watathibitika kukithiri kwa makosa ya usalama barabarani, na kuzuiwa kabisa kufanya kazi hiyo.

 Hatua hiyo itaanza kuchukuliwa mara baada ya kukamilika na kuanza kwa Mfumo mpya wa Nukta, ambao utaweka kumbukumbu za makosa ya madereva ambayo itatumika kuwachukulia hatua hiyo.

Amina Maige akana Shitaka la kumchoma Pasi na Kumng’ata Hausigeli wake..Arudishwa Rumande Zamana yaKataliwa

$
0
0
Mkazi wa Mwananyamala, Amina Maige(42) anayetuhumiwa kumng’ata mfanyakazi wake wa ndani,  amepandishwa kizimbani kusomewa maelezo ya awali baada ya upelelezi wa kesi hiyo kukamilika.
 
Amina  alisomewa maelezo hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni mbele ya Hakimu Yohana Yongolo.
 
Wakili wa Serikali Tumaini Msikwa alidai kati ya Januari na Juni mwaka huu, maeneo ya Mwananyamala Wilaya ya Kinondoni, Maige alimng’ata Yusta Kashinde(20) sehemu  mbalimbali za mwili wake na kumsababishia maumivu.

Mshitakiwa alikana maelezo aliyosomewa na kwamba aliiomba mahakama kumpatia dhamana.

Wakili Msikwa aliiambia mahakama kuwa dhamana ya mshitakiwa imezuiliwa kama awali kwa kuwa bado  wananchi wana hasira hivyo kuhofia usalama wake.

Hakimu Yongolo alisema shauri hilo litaanza kusikilizwa  Julai 10 mwaka huu.

Mungu Hashindwi Hatimaye Flora Mbasha na Mumewe Wapatana

$
0
0
HAKUNA neno zuri la kusema zaidi ya Mungu mkubwa! Ule mtafaruku ndani ya ndoa ya mwimba Injili mahiri Bongo, Flora na mumewe, Emmanuel Mbasha umedaiwa kumalizika kwa wawili hao kupatana, Risasi Jumamosi linakuwa nambari wani kukuhabarisha.
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika, wawili hao walikalishwa kikao cha upatanishi mapema wiki hii kilichokuwa chini ya familia.

MANENO YA CHANZO
“Kikao cha familia kilikaa, Mbasha aliitwa akafika, Flora naye aliitwa akatokea, mazungumzo yalikuwa marefu lakini kimsingi waliamua kuweka kando mtafaruku wao na kuijenga upya ndoa yao,” kilisema chanzo.

Chanzo kiliongeza kuwa katika kikao hicho cha mwanzoni mwa wiki hii, miongoni mwa adidu za rejea ilikuwa kutokumbushia vikao vilivyopita ambapo hakukupatikana muafaka.

VIKAO VILIVYOPITA
Katika vikao vilivyopita, wahusika wakuu walikuwa wazazi wa Mbasha (mzee Maneno Mbasha, Zulfa Maneno), ndugu wa Flora na Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.

VIKAO VYA BAADAYE
Kwa mujibu wa chanzo, vikao vilivyofuata, wawili hao wakawa tayari kila mmoja ametema nyongo yake pembeni na kufikia makubaliano kwamba, ndoa yao isimame tena wakitumia maandiko kwenye Biblia kutoka kitabu cha Waebrania yanayosema:    Ndoa na iheshimiwe na watu wote na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.

WAKORINTHO YAFUNGA KAZI
Kwa mujibu wa chanzo hicho, maneno mengine ya Biblia yaliyotumika kwenye kikao hicho mpaka wawili hao wakaamua kurudiana ni 1 Wakorintho 7:1-10 ambapo maandiko yanasema:
Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe. Mume na ampe mkewe haki yake vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake
Mke hana amri juu ya mwili wake bali mumewe vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake bali mkewe. Msinyimane, isipokuwa mmepatana kwa muda ili mpate faragha kwa kusali, mkajiane tena shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.

Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza, wala hapo si mimi, ila Bwana (Mungu), mke asiachane na mumewe, lakini ikiwa ameachana naye na akae asiolewe au apatane na mumewe, tena mume asimwache mkewe.

KIKAO CHA JUMAMOSI KUMALIZIA
Chanzo kilisema kuwa, kikao cha mwisho ambacho kitamalizia kuweka mambo sawa ili wawili hao waanze ngwe ya pili ya ndoa yao ambayo inaaminika itakuwa ya mwisho mpaka kifo kiwatenganishe, kinatarajiwa kufanyika leo jijini Dar es Salaam mahali ambapo hapakutajwa.

MWANASHERIA ATAJWA
Mwanasheria wa Flora aliyejulikana kwa jina moja la Ado ametajwa kusimamia kikao hicho ili wawili hao waanze maisha mapya baada ya safari fupi ya mvurugano uliowafanya kuwa mbalimbali.

AONGEA NA RISASI JUMAMOSI
Juzi, Risasi Jumamosi lilimsaka mwanasheria huyo kwa njia ya simu yake ya mkononi ili kumsikia anasemaje kuhusu kutajwa kwenye usuluhishi wa ndoa hiyo ambapo alipopatikana alisema:
“Niko Arusha, Ijumaa nitarudi Dar. Kuhusu kikao cha usuluhishi siwezi kukwambia lakini suala la kuwapatanisha nalifahamu, nawaomba na ninyi msaidie kufanikisha jambo hilo zuri.”

VIPI KUHUSU KESI YA MADAI YA KUBAKA?
Hata hivyo, Wakili Ado hakutaka kugusia kuhusu kesi ya Mbasha iliyopo Mahakama ya Wilaya ya Ilala ambapo anadaiwa kumbaka shemejiye mara mbili (jina tunalo) ambayo kwa mujibu wa mahakama, upelelezi umekamilika na itasikilizwa Julai 17, mwaka huu.

KWA UPANDE WAKE FLORA
Risasi Jumamosi lilimwendea hewani, Flora ili kumsikia anasemaje kuhusu kuwepo kwa upatanishi kati yake na mumewe, Emmanuel.

Huyu hapa: “Ongea na wakili wangu atakwambia kila kitu.” Ambapo majibu ya wakili yalikuwa: ”Ninachojua mimi ni kwamba Flora ameshamsamehe mumewe na yuko tayari kuanza ukurasa mpya.”

MBASHA SASA
Kwa upande wake, Mbasha alipozungumza na gazeti hili juzi alisema kurejea upya kwa ndoa yake ni jambo la kuupendeza moyo wake.

“Mimi sina neno nipo tayari, nimeshasamehe yaliyotokea, Flora ni mke wangu jamani, nampenda sana kutoka moyoni.”


Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images