Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live

Mgombea Mwingine Aruhusiwa Kuwania Urais Kenya

$
0
0
Mgombea Mwingine Aruhusiwa Kuwania Urais Kenya
Mahakama Kuu nchini Kenya imeamuru mgombea urais wa chama cha Thirdway Alliance Ekuru Aukot aliyekuwa ameshiriki uchaguzi mkuu tarehe 8 Agosti ashirikishwe kwenye uchaguzi mkuu mpya unaopangiwa kufanyika tarehe 26 Oktoba.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi IEBC ilikuwa imetangaza kwamba ni wagombea wawili pekee, Rais Uhuru Kenyatta wa chama cha Jubilee na Raila Odinga wa muungano wa National Super Alliance (Nasa) wangewania kwenye uchaguzi huo.
Bw Odinga alijiondoa kwenye uchaguzi huo Jumanne.
Dkt Aukot amesema amefurahia uamuzi huo na kwamba sasa watakuwa kwenye uchaguzi kwani mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alikuwa amejaribu kuwafungia nje
Hata hivyo, amesema chama chake bado kina masuala ambayo kilitaka yashughulikiwe na tume hiyo ya uchaguzi tangu mwezi Agosti na bado hayajashughulikiwa.

Amesema kukubaliwa kwao kuwania kutawafungulia mlango kufanya mashauriano na viongozi wa IEBC.
Dkt Aukot amesema chama chake kitatoa maelezo ya kina kuhusu msimamo wao katika kipindi cha siku mbili hivi baada ya mashauriano zaidi.
Maafisa wakuu wa IEBC walikutana jana kutafakari kuhusu hatua za kuchukua baada ya hatua ya Bw Odinga lakini kufikia sasa bado hawajatoa tamko.
Kujumuishwa kwa mgombea huyo kuna maana kwamba IEBC haiwezi kumtangaza Bw Kenyatta kuwa mshindi wa moja kwa moja hata baada ya kujiondoa kwa Bw Kenyatta.

Wafuasi wa muungano wa upinzani Nasa wamekuwa wakiandamana Mombasa kushinikiza mageuzi katika tume ya uchaguzi
Ekuru Aukot ni nani?
Dkt Aukot ni mtaalamu wa masuala ya katiba ambaye alikuwa mkurugenzi na afisa mkuu mtendaji wa wa Kamati ya Wataalamu iliyohusika katika kuandika rasimu ya ya Katiba ya Kenya iliyoanza kutekelezwa mwaka 2010.
Alikuwa amesema awali kwamba anataka kuwa rais wa taifa la Kenya kutokana na kile anachosema ni kutoheshimiwa na kuhujumiwa kwa Katiba aliyosaidia kuwepo kwake.
Dkt Aukot alizaliwa miaka 45 iliyopita katika eneo la Kapedo, katika kaunti ya Turkana kaskazini magharibi mwa Kenya.
Alianzisha chama cha Thirdway Alliance katika juhudi za kutoa uongozi mbadala na uongozi wa mageuzi kwa Wakenya.
Anaamini Wakenya hawawezi kuwategemea tena viongozi ambao wamekuwa madarakani kufikia sasa kumaliza ufisadi na ukabila.
Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na IEBC, Dkt Aukot alipata kura 27,311 sawa na 0.18%, nafasi ya tano kati ya wagombea wanane walioshiriki, katika uchaguzi uliofanyika tarehe 8 August ambao matokeo yake yalifutiliwa mbali na Mahakama ya Juu

Jaguar, Babu Owino Watwangana Makonde Bungeni

$
0
0
Jaguar, Babu Owino Watwangana Makonde Bungeni
Wabunge vijana wawili wa Kenya jana wamepigana bungeni  kutokana na tofauti ya vyama vyao na viongozi wanaowaunga mkono.

Wabunge hao ni msanii maarufu Charles Njagua maarufu kama Jaguar na Paul Ongili maarufu kama Babu Owino.


Ilikuwa hivi kabla ya kikao cha jioni kuanza Babu Owino aliingia kwenye chumba cha waandishi wa habari na kuwasalimia kisha akaenda kwenye ofisi ya ofisa uhusiano wa bunge.

Muda mfupi baadaye Jaguar akaingia kwenye chumba cha waandishi na kuuliza “Huyu Babu yuko wapi?”

Babu Owino akatokea na wakaanza kurushiana makonde na kutoleana maneno makali kabla ya kutenganishwa na maofisa wa bunge.

“Tutakufundisha adabu Babu, lazima umuheshimu Rais,”alisema Jaguar ambaye ni Mbunge wa Starehe.

Akijibu kwa hasira Babu Owino ambaye ni Mbunge wa Embakasi Mashariki alimuuliza Jaguar “Rais yupi? Rais pekee ninayemjua ni Raila Odinga.”

Hata hivyo maofisa wa bunge walifanikiwa kuwatenganisha na wabunge hao watafikishwa kamati ya bunge ambapo wanaweza kuzuiwa kuhudhuria baadhi ya vikao vya bunge.

Sheik Ponda Aelea Alivyoguswa na Hisia za Tundu Lissu Wakati Walipokuwa Wanabadirishana Mawazo

$
0
0
Sheik Ponda Aelea Alivyoguswa na Hisia za Tundu Lissu Wakati Walipokuwa Wanabadirishana Mawazo
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda amesema ameguswa na hisia za Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu.

Ponda amesema hayo leo Jumatano akizungumzia safari yake ya Nairobi nchini Kenya alikokwenda kumjulia hali Lissu hivi karibuni.

“Tulipokuwa tunabadilisha mawazo, niliguswa na hisia kubwa, badala ya mimi kumpa matumaini yeye ndiye alinipa matumaini,” amesema Ponda.

Amesema madhumuni ya safari yake yalikuwa kumjulia hali Lissu, kumwombea dua, kumjengea matumaini ya afya na kujenga mazingira mapana yanayotosha kulizungumza jambo lililomfika.

Mtuhumiwa Hatari wa Uporji na Mauaji Auwawa kwa Kupigwa Risasi na Polisi

$
0
0
Mtuhumiwa Hatari wa Uporji na Mauaji Auwawa kwa Kupigwa Risasi na Polisi
Mkazi wa Dar es Salaam, Robert Massawe (51) ambaye polisi wanadai ni mtuhumiwa hatari wa uporaji na mauaji ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wanaodaiwa kuwa ni wenzake.

Kabla ya kuuawa katika majibizano ya risasi, mtuhumiwa huyo anadaiwa kukamatwa na bunduki aina ya SMG ikiwa na risasi 24, simu 19 zilizoporwa maeneo mbalimbali na laini za simu 58. Taarifa iliyotolewa jana na kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Hamisi Issah ilisema mtuhumiwa huyo aliuawa juzi saa tisa alfajiri wilayani Rombo na watu wanaodaiwa kuwa watuhumiwa wenzake.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mtuhumiwa huyo pamoja na mkewe walikamatwa jijini Dar es Salaam na baada ya kuhojiwa na polisi anadaiwa kueleza matukio mbalimbali ya ujambazi aliyoshiriki.

Kamanda Issah alisema baada ya kukamatwa jijini humo na kuwaeleza polisi ushiriki wake katika matukio mbalimbali ya ujambazi alikubali kuwaonyesha mahala alipoficha bunduki hiyo.

Polisi waliandamana naye chini ya ulinzi mkali hadi Moshi kwenye dampo lililopo karibu na kiwanda cha ngozi ambapo bunduki ilipatikana ikiwa imefukiwa ardhini ikiwa na risasi 24. “Muda wote alitoa ushirikiano mkubwa kwa polisi na alivyokuwa akisimulia matukio aliyoyafanya mwili unaweza kusisimka. Simu tatu kati ya 19 tumegundua ziliporwa hapa Moshi,” alisema.

Katika mahojiano hayo inadaiwa mtuhumiwa huyo aliwaeleza polisi juu ya mpango uliokuwapo wa kufanya tukio la ujambazi katika kijiji cha Chilio, kata ya Holili wilayani Rombo juzi alifajiri.“Akiwa chini ya ulinzi wa askari kanzu alikubali kuwapeleka polisi katika eneo hilo, sasa walipofika alipowaona wenzake alipiga kelele ya kuwajulisha wenzake kuwa polisi walikuwapo eneo hilo,” alisema.

Kamanda Issah alisema hali hiyo iliwafanya watuhumiwa wenzake kukimbia huku wakipiga risasi ovyo na baadhi zilimpiga Massawe mkono wa kushoto, mgongoni na mguuni na kufariki. “Tuonavyo sisi wale wenzake walikuwa na nia ya kupoteza ushahidi au kumpoteza mwenzao. Wahalifu ndio walimpiga risasi mwenzao na pale hata polisi wetu wangedhurika kama si kujihami,” alisema.

Kamanda Issah alisema kati ya simu 19 alizokutwa nazo, moja alikuwa nayo mkewe ambaye anashikiliwa Dar es Salaam.

Rais Kenyatta Kutia Saini Miswada ya Sheria Itakaporipotiwa na Bunge

$
0
0
Ras Kenyatta Kutia Saini Miswada ya Sheria Itakaporipotiwa na Bunge
Rais Uhuru Kenyatta amesema atatia saini kuwa sheria miswada ya sheria ya uchaguzi mara itakaporidhiwa na Bunge.

Akiwahutubia wananchi katika kituo cha mabasi cha Kaloleni katika kaunti ya Kilifi jana Rais Kenyatta amesema haoni tatizo lolote kuhusu miswada hiyo kwa sababu masuala yaliyoibuliwa na wapinzani yamezingatiwa pia.

Kenyatta ametoa kauli hiyo wakati Bunge lenye wabunge wengi wa chama cha Jubilee linahaha kukamilisha mchakato wa kujadili miswada miwili na kuipitisha kabla ya siku ya mwisho ya kufanya hivyo Alhamisi.

Mabunge yote mawili yaani Bunge la Taifa na Seneti yanajadili miswada inayolenga Sheria ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka, na Sheria ya Uchaguzi na Makosa ya Uchaguzi kuelekea uchaguzi wa marudio.

Hata hivyo wabunge wa Nasa wamekataa kushiriki mjadala wa mabadiliko ya sheria ya uchaguzi yaliyowasilishwa katika vikao vya Bunge la Taifa na Baraza la Seneti. Wabunge hao walisisitiza pia kwamba kiongozi wao Raila Odinga hatashiriki uchaguzi huo.

Uamuzi wa kutoshiriki mjadala huo ulifikiwa Jumatano iliyopita katika vikao vya wabunge wa Nasa.

Kiongozi wa wachache bungeni katika Bunge la Taifa, Mbunge wa Suba Kusini John Mbadi alisema hatua yao ya kutoshiriki mjadala huo imelenga kukwepa kuhalalisha “mchakato uliokosewa.”

“Baada ya kupitia miswada yote miwili, tumejiridhisha kwamba ni miswada hatari. Miswada hii haiku kikatiba na iko katika msingi uliokosewa kwa maudhui yake na mchakato mzima,” alisema Mbadi.

Akipinga miswada miwili kujadiliwa kwa pamoja na mabunge mawili, Seneta wa Makueni Mutula Kilonzo Jnr alisema, “Hatutashiriki katika uchaguzi ambao Jubilee wanatoka jasho kubadili magoli. Tunataka kuwaambia Jubilee hatutaruhusu hilo kutokea.”

Lakini Rais Kenyatta ameweka msimamo akisema; "Binafsi sioni tatizo lolote katika sheria hii na ikiwa Bunge litapitisha (miswada), nitatia saini, sina tatizo nayo kwa sababu imebeba mambo yaliyoibuliwa na upande wa upinzani.”

Rais, ambaye aliongozana na Makamu wake William Ruto amesema wako tayari kushiriki uchaguzi wa marudio kwa kura ya urais Oktoba 26.

Kenyatta alisema mgombea urais kwa tiketi ya muungano wa upinzani (Nasa), Raila Odinga anajishughulisha na mipango ya kutaka kuhakikisha uchaguzi huo unafutwa jambo alilosema halitatokea kama anavyotaka.

Soma: Mbunge ataka mahakama imzuie Raila kususia uchaguzi

"Sisi tunahaha kutafuta kura na leo tuko Kaloleni wakati yeye ameamua kuitisha mkutano na waandishi wa habari,” amesema.

"Kwa nini hayuko tayari tena kwenda kwenye sanduku la kura baada ya hukumu ya Mahakama ya Juu, ikiwa ana uhakika aliibiwa uchaguzi? Ikiwa hatashiriki uchaguzi huu basi sisi tutaendelea kuwatumikia wananchi,” amesema.

Katika mwendelezo wa kampeni zake, Rais amesema ukanda wa pwani kwamwe hauwezi kutengwa kimaendeleo.

"Nafahamu kwamba hata mtu aliyepigia upande wa upinzani ni Mkenya, ambaye anataka Rais anayewajibika. Nitatimiza hayo na miradi yote iliyoanzishwa na utawala wangu haitatelekezwa,” amesema.

SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Jeshi la Polisi Lavamia Mkutano waSeik Ponda Waanishi wa Habari Wakamatwa

$
0
0
Jeshi la Polisi Lavamia Mkutano waSeik Ponda Waanishi wa Habari Wakamatwa
Jeshi la Polisi nchini limevamia mkutano wa Sheikh Issa Ponda ambao ulikuwa unatakiwa kufanyika katika hoteli ya Iris, Kariakoo jijini Dar es Salaam ambapo alikuwa amepanga kuzungumzia sakata la Tundu Lissu kupigwa risasi.

Mwenyekiti wa kamati ya uongozi ya CUF, Julius Mtatiro amethibitisha polisi kuzuia mkutano huo na kusema kuwa baadhi ya waandishi wa habari ambao walikuwepo kwenye ukumbi huo wamekamatwa na polisi.
"Polisi wamevamia mkutano wa Sheikh Issa Ponda katika hoteli ya Iris, Kariakoo. Taarifa za awali zinasema baadhi ya waandishi wamekamatwa. Sheikh Ponda alikuwa azungumze na vyombo vya habari kuhusu suala la Kupigwa risasi kwa Tundulissu asubuhi hii, mara baada ya kurejea kutoka Nairobi ambako alizungumza na Lissu" alisema Mtatiro.

Sheikh Issa Ponda alikwenda kumtembelea, Tundu Lissu hospitali Nairobi nchini Kenya ambako anapatiwa matibabu kufuatia kushambuliwa kwa risasi Septemba 7, 2017 mjini Dodoma na baadaye kupelekwa Kenya kwa matibabu zaidi.

Mtukufu Agha Khan Awaasili Nchini kwa Mwaliko wa Rais Magufuli

$
0
0
Mtukufu Agha Khan Awaasili Nchini kwa Mwaliko wa Rais
Kiongozi wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani, Mtukufu Aga Khan amewasili nchini kwa mwaliko wa Rais John Magufuli.

Mtukufu Aga Khan amewasili leo Jumatano saa nne asubuhi na amepokewa na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa,  Dk Hussein Mwinyi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako.

Baada ya kushuka kwenye ndege, Mtukufu Aga Khan alikagua gwaride lililoandaliwa na Jeshi la Polisi na kutazama burudani ya vikundi vya ngoma.

Kiongozi huyo atakuwa na mazungumzo na Rais Magufuli baadaye mchana na kesho atahitimisha ziara nchini.

Mtukufu Aga Khan pia ni kiongozi mwasisi wa Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan ambao unatoa huduma mbalimbali duniani.

Kwa Tanzania mtandao huo unatoa huduma za afya, bima, elimu, mikopo kwa wajasiriamali, kusaidia kilimo na hasa kwa wakulima wa vijijini.

Ziara ya Mtukufu Aga Khan inalenga kuimarisha ushirikiano baina ya Serikali na taasisi yake ambayo ina uwekezaji mkubwa nchini.

Chadema Yakomaa Yasema Kama Chama Pinzani Wataendelea Kukosoa

$
0
0
Chadema Yakomaa Yasema  Kama Chama Pinzani Wataendelea Kukosoa
Chama cha Demokrasi na Maendeleo (Chadema) kimesema kuwa kama chama kikuu cha upinzani wana wajibu wa kuwazungumzia wananchi na kukosoa Serikali.

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zanzibar, Salum Mwalimu amesema hayo leo Jumatano wakati akizungumza na waandishi wa habari.

“Kumekuwapo na juhudi nyingi za kutuzima midomo, hatutakubali mitutu wala nini, tumezaliwa siku moja tutakufa siku moja,” amesema Mwalimu.

“Tutasema, tutakosoa na kukemea na hatutakubali kurudi nyuma hata siku moja na tunawahakikishia Watanzania hatutarudi nyuma,”

“Wako waliodhani matukio haya yataturudisha nyuma, hakuna jambo jema kama mshindani wako anapokuwa hoi na kweli wako hoi,” amesema Mwalimu.

Amesema mwaka jana walizungumza kuhusu Ukuta, kueleza kile walichokiona ambacho kinakuja siku za usoni na ndicho kinachotokea

“Tuliwaambia Watanzania harufu hii ya kutokuheshimu Katiba, sheria na ilianza kwa kuzuia mikutano, kamata weka ndani saa 48 wakasema si wanasiasa na tukawaambia ukiukwaji huu wa kisheria hautaishia kwa wanasiasa na ndicho kinaonekana,” amesema Mwalimu

Chadema Wamjia Juu IGP Sirro Kutekeleza Majukumu Yake Ikiwemo Upelelezi na Kuacha Kukataza Kujadili Suala la Lissu

$
0
0
Chadema Wamjia Juu IGP Sirro Kutekeleza Majukumu Yake Ikiwemo Upelelezi na Kuacha Kukataza Kujadili Suala la Lissu
CHAMA cha Demokrasia na Maendelo (Chadema) kimemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Nyakoro Sirro kutekeleza majukumu yake ikiwemo kufanya upelelezi na kuhakikisha wanawatia nguvuni walioshiriki katika tukio la kumshambulia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ambaye amelazwa jijini Nairobi akitibiwa.
Akizungumza na wanahabari leo katika ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA Kinondoni Dar es Salaam leo, (Jumatano), Oktoba 11, 2017, Mwanasheria wa chama hicho, John Mallya amesema:
“Wakati wanasiasa, wanasheria na wananchi wa Jimbo ambalo Tundu Lissu anatoka, wakijadili kuhusu mustakabali wa kiongozi wao aliyejeruhiwa, Sirro anapaswa kunyamaza na kufanya kazi ya upelelezi. Kitu tunachotaka kusikia kutoka kwake apeleke watu mahakamani, na si kuwaambia wananchi mitandaoni wanyamaze, kufanya hivyo anakiuka masharti ya ibara ya 18 ya katiba ya nchi,” alisema Mallya.
“Aliyepigwa risasi zaidi ya 30 pale Dodoma si mbuzi, ni binadamu, kwa nini tusimjadili?” alihoji Mallya na kuongeza, Sirro alipaswa achukue advantage (fursa) ya mijadala hiyo ya wanasheria kuifanyia upelelezi.
Aidha Mallya amewataka wananchi, wanansheria na wanasiasa kuendelea kujadili suala la Lissu huku akidai kuwa, kwa kufanya hivyo hawavunji sheria yoyote ya nchi na badala yake inaweza ikawa chanzo kizuri cha kuwapata watuhumiwa wa tukio hilo.
Kuhusu hali ya afya ya Lissu, Katibu Mkuu wa Chadema-Zanzibar, Salum Mwalimu, amesema hivi karibuni watatoa taarifa rasmi ya maendeleo ya mbunge huyo

Kairuki Amkaidhi Mkuchika Zigo la Vyeti Feki Afunguka Changamoto ya Vyeti Feki Ilivyomtesa

$
0
0
Kairuki Amkaidhi Mkuchika Zigo la Vyeti Feki Aeleza Changamoto ya Vyeti Feki Ilivyomtesa
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki amesema uhakiki wa vyeti ni changamoto aliyokumbana nayo alipokuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Amesema hayo leo Jumatano alipokabidhi ofisi kwa Waziri mpya wa Utumishi, George Mkuchika. Amesema changamoto ya uhakiki wa vyeti hawezi kuisahau.

"Nchi kama vile Afrika Kusini, India na Pakistan walifanya jambo kama hili kwa awamu na bado hawajamaliza, lakini sisi tumelifanya kwa jumla, haikuwa kazi nyepesi," amesema.

Kairuki amesema mbali ya uhakiki, baadhi ya watendaji alioshirikiana nao hawakuwa waaminifu ambao walipenyeza watu wasiokuwa na sifa.

"Waliopenya katika hatua hii naamini Mkuchika atapambana nao ipasavyo," amesema Kairuki.

Amesema uhakiki ulichukua muda mrefu kiasi cha kuwakatisha tamaa watumishi wa umma.

Masilahi ya watumishi wa umma amesema lilikuwa changamoto nyingine kwa sababu Serikali inatamani kuyaboresha lakini fedha inayokusanywa haikidhi mahitaji.

Amewatoa shaka watumishi ambao hawajapandishwa madaraja akisema fedha kwa ajili watumishi zaidi ya 163,000 zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza hilo.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa ofisi, waziri Mkuchika amesema mbali ya  kuendeleza mazuri aliyoyaacha Kairuki, ikiwemo kudumisha nidhamu katika utumishi wa umma, atasisitiza elimu ya kupiga vita rushwa.

Mkuchika amesema atazungumza na Waziri wa Elimu ili elimu ya kupiga vita rushwa ianze kutolewa kuanzia shule ya msingi.

Amesema nchi zilizofanikiwa kupiga vita rushwa ziliwekeza katika kutoa elimu juu ya madhara yake.

"Miaka ya nyuma ilikuwa hakuna mtu mwenye kuheshimika kama mtumishi wa umma. Wasomi wenye weledi na ujuzi walikuwa watumishi wa umma, hapa kati hali ikabadilika,” amesema.

Mkuchika amesema kazi iliyopo ni kuirudisha nidhamu hiyo na kuhakikisha watumishi wa umma wanakuwepo ofisini muda wote kutoa huduma kwa wananchi.

Rais Magufuli Akutana na Maseneta Kutoka Marekani

$
0
0
Rais Magufuli  Akutana na Maseneta Kutoka Marekani
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo amekutana na Seneta James Inhofe pamoja na Maseneta wengine wa Baraza la Marekani Ikulu jijini Dar es salaam.

Rais Magufuli ameupokea ugeni huo na kufanya nao mazungumzo mbalimbali ndani ya Ikulu. Hata hivyo bado taarifa rasmi za nini haswa wameongea viongozi hao baada ya kukutana hazijatoka.
Pia leo Rais Dkt. John Pombe Magufuli amempokea kiongozi wa Jumuiya ya Ismailia H.H.Prince Karim al-Hussayni Aga Khan alipotembelea Ikulu na kuteta mambo na mheshimiwa Rais.

Aidha Rais Dkt. Magufuli amepokea kitabu cha Seneta James Inhofe kilichoonyesha picha za maeneo mbalimbali ya Tanzania alipotembelea mwaka mmoja na nusu uliopita.

Jaguar Amuomba Msamaha Babu Owino Ila Amtaka Kumuheshimu Rais

$
0
0
Jaguar Amuomba Msamaha Babu Owino Ila Amtaka Kumuheshimu Rais
Mbunge jimbo la Starehe jijini Nairobi Kenya kupitia chama cha Jubilee, Charles Njagua Kanyi maarufu kama Jaguar, ameomba msamaha kwa mbunge mwenzake kupitia NASA, Paul Ongili (Babu Owino), baada ya kupigana bungeni hapo jana.

Akiongea na waandishi wa habari leo katika eneo la Bunge, Jaguar amesema kitendo hicho kilitokea kwa bahati mbaya, huku akiendelea kusisitiza kuwa mbunge huyo (Babu Owino) ni lazima aonyeshe heshima kwa Rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta.
"Kilichotokea jana bungeni ni bahati mbaya, nakusamehe Babu Owino lakini pia namuomba anisamehe, hata hivyo nasisitiza kwamba Babu Owino lazima amuheshimu Rais, asipofanya hivyo nitashughulika naye", amesema Jaguar.
Hapo jana Mbunge Jaguar na Babu Owino walipigana wakiwa bungeni, baada ya Babu Owino kutamka maneno ya kumvunjia heshima Uhuru Kenyatta, kitendo kilichomchukiza Jaguar na kupelekea kukunjana bungeni na video zao kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Ali Kipa Ndani ya Helkopta Akila Bata na Gavana wa Mji wa Mombasa

$
0
0
Ali Kipa Ndani ya Helkopta Akila Bata na Gavana wa Mji wa Mombasa
Huu unaweza ukawa ni muda muafaka wa Alikiba kusherehekea mafanikio ya ngoma yake ya Seduce Me.

Msanii huyo ameonekana katika picha ya pamoja ambayo ameiweka katika mtandao wa Instagram wakiwa kwenye Helkopta na rafiki yake wa karibu ambaye pia ni Gavana wa mji wa Mombasa, Hassan Joho.

“My brother thank you for hosting me and my team in Mombasa. @joho_001 #KingKiba,” ameandika Alikiba kwenye picha hiyo.


Alikiba (katikati) akitumbuiza katika kampeni za Gavana Joho

Kiba pia alikuwa akimfanyia kampeni kiongozi huyo ya kugombea katika mji huo wa Mombasa kabla ya uchaguzi uliofanyika August 8 ya mwaka huu na Joho ambaye ni mfanyabiashara maarufu nchini Kenya kushinda katika uchaguzi huo kwa takribani asilimia 90.

Katika uhaguzi huo Joho aliwabwaga wagombea wengine akiwemo Awiti Bolo, Suleiman Shabahal na wengine.

Shuhudia Maajabu ya Chief Sultan Mzee...Mtaalamu wa Nyota za binadamu

$
0
0

ONA MAAJABU YA CHIEF SULTAN MZEE

 Mtaalamu wa Nyota za binadamu Africa Mashariki na dunia nzima,
Amewasaidia watu wengi kujua nyota zao na jinsi ya kuzing'arisha,
Anarudisha Mpenzi,Mume,Mke mliyeachana NDANI ya masaa manne(4) tu,
Anaweza kuongeza ROMANCE na MAHABA kwa Mwenzi wako
Anatoa pete ya BAHATI pamoja na kukupa uwezi wa Kupata faida kubwa katika biashara yako,
Kwa wale mnaosumbuliwa na Chuma ulete tatizo hilo analiondoa kabisa,
Anakuwezesha kushinda kesi iliyodumu siku nyingi nk.
KWA USTAA,UMARUFU UTAPATA UTAJIRI WA MAISHA NA BILA MASHARTI YOYOTE, UTAPEWA NGUVU ZA KUJILINDA NA UTAJIRI, MALI NA AFYA YAKO,Karibu kwa CHIEF SULTAN MZEE akupatie Pete za Bahati na utajiri.Wachungaji wengi duniani, Wanasiasa na Wasanii Maaarufu duniani Tayari wamejiunga pia wamefaidika na wamebadirisha  Maisha yao toka umasikini mpaka utajiri,kujua mengi zaidi na kutatuliwa Matatizo yako yoote kwa usiri na Uaminifu piga simu namba 0762-846979 au 0672-202509

Diamond Platnumz Afanya Kolabo Rick Ross

$
0
0
Mkali wa bongo fleva Diamond Platnumz ameendelea kupeleka mbali muziki wake kwa kufanya kolabo za kimataifa.

Safari hii Diamond ameonekana kuvuka mipaka akitarajia kuachia ngoma mpya aliyoshirikiama na rapa wa Marekani Rick Ross.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Meneja wa Diamond, Babu Tale ameweka video inayomuonyesha msanii huyo akiwa na Rick Ross wakirekodi video.

Soma: Diamond aeleza sababu za kuachana na Vevo

Tale aliandika, "Kuthubutu ni sehemu ya kufanya,dhamira yetu ni kuupeleka muziki wa bongo fleva mbele, kikubwa dua zenu."

Video hiyo inaonekana kutengenezwa Miami, Marekani.

Siku chache zilizopita nyota huyo alipata tuzo ya mwanamuziki bora wa Afrika Mashariki zilizotolewa na Afrimma

Kutana na The Great Maalim Hussein Aweze Kutatua Matatizo yako Kwa Tiba za Asili, Dua na Nyota..

$
0
0
THE GREAT MAALIM HUSSEIN
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
Maalim Hussein ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)

MAALIM HUSSEIN ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)

Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
Maalim Hussein Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..

Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
+255 674 835 107

Waziri Jafo Aagiza Wanafunzi Kufanya Mitihani ya Mchujo Kabla ya Kuvuka Darasa

$
0
0
Waziri Jafo Aagiza Wanafunzi Kufanya Mitihani ya Mchujo Kabla ya Kuvuka Darasa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo ameagiza wanafunzi wa shule za Serikali kufanya mtihani wa mchujo kabla ya kupandishwa vidato.

Pia, amesema hatapanga ada elekezi kwa shule binafsi bali watapunguza wenyewe.

Jafo ametoa kauli hiyo leo Jumatano mjini Dodoma alipozungumza na wafanyakazi wa Tamisemi.

Ametoa kauli hiyo akisema shule kongwe za Serikali zimekuwa ‘zikikimbizwa’ na za binafsi.

"Naagiza kuanzia leo, lazima wanafunzi wa shule za Serikali wafanye mitihani mara mbili, mwezi wa sita na mwisho wa mwaka ili kuwachuja wa shule zenye vipaji maalumu na kuwarudisha shule za kawaida za Serikali, vinginevyo ndiyo maana tunafanya vibaya wakati wote," amesema.

Amesema katika mchujo huo, wanafunzi watatolewa kutoka shule kongwe na kupelekwa za vipaji maalumu na vivyo hivyo kutoka vipaji maalumu kwenda shule kongwe.

Kuhusu ada kwa shule binafsi amesema si jukumu la Serikali bali wanataka kuboresha shule zake ili watu na taasisi binafsi zikose wanafunzi.

"Mheshimiwa Kakunda (Joseph –Naibu Waziri Tamisemi) nakuagiza kuanzia leo maana wewe ndiyo nimekukabidhi jukumu la elimu, nataka mtihani wa 2019 shule za vipaji zote 22 ziongoze mtihani wa Taifa na shule binafsi ziwe nyuma, lakini tuongoze kwa halali si ubabaishaji hapo ndipo shule binafsi za makanjanja zitajifuta zenyewe," aliagiza Jafo.

Wakati huohuo, Jafo amewaagiza watendaji katika idara ya elimu kushughulika na wakuu wa shule kongwe zote ili kuona kama bado wana sifa za kuendelea kuwa wakuu wa shule au kuwaondoa wanaoonekana kushindwa kazi.

Kuhusu watendaji wa Tamisemi amesema hataki mambo matatu wizarani hapo ambayo ni ulegevu, mazoea na kutojali muda ambayo amesema ni adui wa mafanikio.

Naibu waziri, Kakunda amesema hana shaka na kazi aliyopewa akiahidi kuifanya kwa kutumia weledi na uzoefu wake ili kuibadilisha Tamisemi.

Kakunda ambaye kabla ya kuwa mbunge alikuwa mkurugenzi Wizara ya Maji amesema mipango mingi anaijua lakini akaomba ushirikiano kwa watumishi.

Vigogo wa Chuo cha Uhasibu Wapandishwa Kizimbani kwa Kuisababishia Hasara Serikali ya Zaidi ya Bilioni Moja

$
0
0
Vigogo wa Chuo cha Uhasibu Wapandishwa Kizimbani kwa Kuisababishia Hasara Serikali ya Zaidi ya Bilioni Moja
VIGOGO wawili wa Chuo cha Uhasibu (TIA) jijini Dar es Salaam, leo wamepandishwa kizimbani Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Shilingi bilioni moja.

Akisoma hati ya mashtaka, Wakili wa Serikali kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leornad Swai, amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Shaha Mussa Hanzuruni na Onesphory Ambangile Luhungu.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, imedaiwa kuwa kati ya Januari Mosi 2012 na Desemba 30 2014, katika chuo hicho kilichopo Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, washtakiwa walitenda makosa hayo.

Imedaiwa, washtakiwa, walitumia vibaya madaraka yao kwa kutofuata taratibu za manunuzi katika ununuzi wa ardhi wa chuo hicho (TIA) kampasi uya Mwanza na kimsababishia Vedasto Lupungo kupata manufaa ya Sh.1,097,681,107/=

Katika shtaka la pili imedaiwa siku na mahali hapo washtakiwa hao kwa ridhaa zao na matendo yao waliisababishia TIA hasara ya Sh. 1,097,681,107/- kwa kutofuata sheria za manunuzi wakati wa kusaini mkataba wa ardhi wa eneo la TIA kampasi ya Mwanza.

Kwa kuwa DPP ameipa mamlaka mahakama ya Kisutu kusikiliza kesi hiyo ya uhujumu uchumi, washtakiwa walipata nafasi ya kujibu tuhuma hizo ambapo wote wamekana kutenda makosa hayo na mahakama ikawasomea masharti ya dhamana kwa kuwa kesi hiyo inadhaminika.

Akisoma masharti ya dhamana, Hakimu Simba amewataka washtakiwa kuwa na wadhamini wawili watakaoweka bondi ya Sh. milioni 250 kila mmoja, pia amemtaka mdhamini mmoja kati ya hao kuweka mahakamani pesa taslimu, Sh. milioni 250 au hati ya mali isiyohamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha ambayo ipo ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Aidha wametakiwa kuwasilisha pasipoti zao na kwamba hawaruhusiwi kusafiri nje ya mkoa huo bila ruhusa ya maandishi kutoka mahakamani.

Polisi Watawanya Maandamano ya Upinzani Kenya

$
0
0
Polisi Watawanya Maandamano ya Upinzani Kenya
Polisi nchini Kenya wamerusha mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya wafuasi wa muungano wa upinzani National Super Alliance ambao wamekuwa wakiandamana mjini Kisumu, magharibi mwa nchi hiyo.
Maandamano pia yamefanyika katika miji mingine mikuu ingawa hali imekuwa tulivu.
Mwandishi wa BBC David Wafula anasema maandamano ya leo jijini Nairobi, ukilinganisha na maandamano ya awali, yalikuwa na utulivu zaidi na idadi ya waliojitokeza walikuwa wengi.
Muungano wa Nasa umekuwa ukifanya maandamano kila Jumatatu, Jumatano na Ijumaa kushinikiza mageuzi katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (IEBC) kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu mpya.
Uchaguzi ambao umepangiwa kufanyika tarehe 26 Oktoba umeingiwa na utata baada ya mgombea wa Nasa Raila Odinga kutangaza kujiondoa rasmi Jumanne.

Mapema leo, Mahakama Kuu pia iliagiza mgombea wa Thirdway Alliance Dkt Ekuru Aukot ajumuishwe kwenye uchaguzi huo.
Muungano wa Nasa unataka uchaguzi mpya ufanyike katika kipindi cha siku 90 na wagombea wateuliwe upya.

Huyu alijitokeza na mbwa kuandamana
Kando na maandamano mijini, Nasa wameandaa pia mkutano wa kisiasa katika uwanja wa Uhuru Park katikati mwa jiji la Nairobi.
Shirika la habari la AFP linasema waandamanaji mjini Kisumu, ambayo ni ngome ya upinzani, wamekuwa wakichoma matairi kwenye barabara.
Mahakama yafutilia mbali ushindi wa Kenyatta
Baadhi wameonekana kwenye picha wakiwa na manati ambazo mara kwa mara wamezitumia kuwarushia polisi mawe.
Bw Odinga aliwahimiza wafuasi wake kuendelea kuandamana kushinikiza mageuzi katika tume ya uchaguzi IEBC ambayo inatarajiwa kutangaza msimamo wake baada ya kujiondoa kwa mgombea huyo wa Nasa wakati wowote.
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live




Latest Images