Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Akamatwa Akisafirisha Mabomu Kwenye Madumu ya Maji

$
0
0
Askari walimshtukia kijana huyo baada ya kupita kwenye vituo vitatu bila kusimama huku gari hilo likielekea kwenye kambi ya majeshi ya Umoja wa Mataifa kwa spidi kali.
Polisi mjini Kabul wamesema walitumia nguvu kubwa kumsimamisha kwa kulishambulia gari lake kwa risasi.

Wanajeshi wa UN nchini humo wamesema kuwa mabomu hayo yalichanganywa na mbolea na kuwekwa kwenye madumu huku mengine yakiwa kwenye maboksi ya nyanya hii ni baada ya kufanyiwa ukaguzi.

Hata hivyo, mpaka sasa hakuna kundi lolote la kigaidi lilitoa tamko juu ya tukio hilo.
Kwa mujibu wa UN nchini Afghanistan mamia ya raia wanauawa kila mwezi na makundi ya kigaidi ambapo kuanzia mwezi Januari hadi Septemba watu 1,584 wameshauawa kwenye matukio mbalimbali ya mashambulizi ya kigaidi.

Pendeza na Products za Kessy...Kutengeneza Shape, Kutoa Mvi na Mengine

$
0
0
PENDEZA NA KESSY PTODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA  MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA 

1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK (B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _90,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _80,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_90,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MILINI _90,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI_80,000/(B)VIDONGE MAX MAN_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_120,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_90,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA     MGUU_80,000/🍍🍉🍊                                                                                     TUNAPATIKAN DAR W SALAAM: NAKWA MIKOAN KOTE UTAPATA PIGA CM                                         (+255) 0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product
Delivery  POPOTE ULIPO,

TFF Yamteua Ndimbo Kuwa Msemaji wao Mpya

$
0
0
Clifford Marion Ndimbo ndiye atakuwa msemaji wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Taarifa kutoka ndani ya TFF zinaeleza, Ndimbo ameanza kazi leo rasmi.

“Ndimbo ameanza kazi leo na atashirikiana na Alfred Lucan katika majukumu katika kitengo cha usemaji,” kilieleza chanzo.

"Unajua kitengo cha habari cha TFF sasa kimetanuka kwa kiwango kikubwa. Kuna usemaji na masuala mengine kama mitandaoni na kadhalika. Hivyo hawa mabwana inabidi wasaidiane."

Ndimbo aliwahi kuwa msemaji wa Simba lakini ni mtangazaji mkongwe ambaye mara ya mwisho alisikika akiwa na Times FM.

Zitto Kabwe athibitisha kupokea barua ya kujiuzuru Mwigamba

$
0
0
Chama cha ACT- Wazalendo kitakutana Ijumaa Oktoba 20, 2017 kujadili masuala kadhaa, likiwemo la kujizulu kwa mwenyekiti wake wa Kamati ya Kampeni na Uchaguzi Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu, Samson Mwigamba.

Mwigamba leo Jumatatu, Oktoba 16 ameandika barua ya kujizulu uongozi na kueleza atabaki kuwa mwanachama wa kawaida ili aweze kupata fursa ya kuwahoji kwa matendo viongozi.

"Nimeamua kukaa kando kwa kuwa tumekuwa hatukubaliani na baadhi ya mambo ndani ya chama na hasa kiongozi wetu… wacha nikae pembeni niwe mwanachama ili niwe na nafasi ya kuwahoji vizuri viongozi wetu masuala mbalimbali na nitabaki kuwa mwanachama mwema,’’ amesema alipozungumza na Mwananchi.

Akizungumzia uamuzi huo, Kiongozi wa chama hicho, Zitto Kabwe amesema, “Nimepokea barua yake. Tutatafakari suala hilo na masuala mengine yanayohusiana na hayo kwenye kikao cha Kamati ya Uongozi wa chama Ijumaa.”

“Ndugu Mwigamba ataalikwa kwenye kikao hicho. Ninamshukuru sana kwa utumishi wake uliotukuka kwenye chama na ninamtakia kila la kheri. Mchango wake na kujitoa kwake kwa hali na mali hakutasahaulika kwenye chama chetu,” amesema  Zitto.

Uhuru Kenyatta na Willim Ruto Wayaonya Mataifa ya Kigeni

$
0
0
Rais Uhuru Kenyatta na Makamu wake William Ruto wametoa onyo kali kwa mataifa ya nje wakiyashutumu kwa kujaribu kuingilia mambo ya ndani ya Kenya.

Wakizungumza wakati wa mikutano ya kampeni za kisiasa wakiwa Nyahururu na Karatina, viongozi hao walisema nchi haikuwa katika mgogoro wowote hata kustahili kuingiliwa kati na mataifa ya kigeni.

“Nataka kuiambia Jumuia ya kimataifa kwamba Kenya hakuna tatizo. Tatizo pekee tulilonalo ni mtu mmoja anayeitwa Raila Odinga (kiongozi wa Nasa),” alisema Rais Kenyatta.

Mkuu huyo wa nchi alisema nchi yake haitaruhusu mazungumzo kati yake na Odinga yatakayoongozwa na mataifa ya kigeni.

Huku akisisitiza kuwa Kenya ni nchi huru alisema: “Hatutaruhusu wazungu kuja na kutuambia nini cha kufanya. Kama watakuja Kenya, waacheni waje kama watalii. Waacheni waende Wamasai Mara, waje Laikipia na maeneo mengine, lakini wasije hapa na kutuambia nini cha kufanya,” alisema Rais Kenyatta.

Pia alimlaumu Odinga kwa maandamano na uharibifu wa mali katika maeneo mbalimbai ya nchi, akisema mtu yeyote aliyeshiriki katika maandamano lazima ashughulikiwe ipasavyo. Rais aliwaomba wapigakura nchini kujitokeza kwa idadi kubwa ili kupigakura zao kwenye uchaguzi wa marudio wa Oktoba 26.

Aidha, Makamu wa Rauis Ruto alimshutumu Odinga kwa kuiomba Jumuia ya Kimataifa kulazimisha mazungumzo ya upatanishi kwa lengo la kuunda Serikali ya Muungano.

“Analialia mbele ya mataifa ya kigeni ili yamuonee huruma na iundwe timu ya kusimamia upatanishi. Lakini hata kama atakwenda Ulaya, Washington apite hadi Mexico au arudi Casablanca, haitakuwepo Serikali ya Nusu Mkate,” alisema Ruto.

Ruto amemtaka Odinga kusitisha maandamano, kuacha uchokozi na vitisho dhidi ya Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) Wafula Chebukati na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Tume Ezra Chiloba na akamtaka ajiandae kwa uchaguzi.

“Kama Jubilee tungetaka kumwapisha Kenyatta kuwa Rais, tungekwisha fanya hivyo, lakini kamwe hatukutaka kuingiza nchi katika machafuko kwa sababu sisi ni wapenda amani. Hivyo tuliamua kurudi kupigakura. Hivyo naye pia asitishe maandamano, aache maonyesho na ajiandae kwa uchaguzi,” alisema Ruto

Akizungumza katika mkutano wa kampeni Karatina, Rais Kenyatta alisisitiza kuwa suala la kugawana madaraka na wapinzani halipo.

Pia aliwatetea polisi kutokana na madai ya kutumia nguvu kupita kiasi dhidi ya waandamanaji waliokuwa wakiandamana dhidi yaIEBC.

Katiba inaruhusu maandamano yenye amani, lakini huwezi kuita maandamano ya amani wakati unawatuma watu wako kurushia mawe vituo vya polisi. Unatarajia kupata nini pale unapokirushia mawe kituo cha polisi?”alihoji rais.

Mwananchi:

Mbowe Kuelezea Maendeleo ya Tundu Lissu Leo

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe leo Jumanne Oktoba 17, 2017 atazungumzia maendeleo ya afya ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Lissu aliyeshambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi akiwa katika makazi yake Area D mjini Dodoma Septemba 7, amelazwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya akiendelea na matibabu.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu, baada ya kuulizwa kuhusu hali ya Lissu, Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni amesema:

“Kesho saa 5:00 asubuhi nitakuwa na mkutano na waandishi wa habari, nitazungumzia hali ya Lissu na mambo mengine yanayoendelea.”

Baadaye katika taarifa ya Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha chama hicho, Tumaini Makene amesema mkutano huo utafanyika makao makuu ya Chadema Kinondoni jijini Dar es Salaam.

“Kupitia Mwenyekiti, Freeman Mbowe chama kitatoa taarifa kwa Taifa kuhusu maendeleo ya Tundu Lissu, mrejesho wa michango, gharama za matibabu,” amesema Makene.

Mwananchi:

Kaimu Katibu Mkuu Ammwagia Sifa Rais Magufuli

$
0
0
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana  wa UVCCM Taifa Shaka Hamidu, amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli kwa kurejesha mwamko ndani ya chama.

Shaka amesema kuwa katika uongozi wa Rais Magufuli kama Mwenyekiti wa Chama cha CCM, UVCCM imeweka rekodi ya kupokea maombi mengi zaidi ya watu wanaowania nafasi ya Uenyekiti Taifa kwenye uchaguzi wa mwaka huu. Jumla ya vijana 113 kutoka Tanzania bara na Zanzibar wamejitokeza kuwania nafasi hiyo.

“Katika uongozi wa Dkt, Magufuli akiwa Mwenyekiti wa chama limekuwa ni jambo la historia inaonyesha jinsi gani vijana wamekuwa na mwamko na hamu ya kukitumikia chama, kwakweli anastahili pongezi na hizi ni dalili nzuri kwa Chama”, amesema Shaka.

Kwa upande mwingine Shaka amesema hivi sasa zoezi linaloendelea ni usaili wa wagombea wote walioonesha nia ya kuwania uongozi ili kuwabaini na kuwapitisha wenye sifa sitahiki. Moja ya sifa kuu ya kugombea uongozi ndani ya UVCCM ni kuwa na miaka 30 au chini ya hapo ili katika uongozi wako usizidi miaka 35 kwani kila awamu ni miaka mitano.

Nafasi zinazowaniwa katika uchaguzi huo ambao mchakato wake umeanza tangu mwezi April kwa ngazi za Shina na Tawi ni Mwenyekiti, na Makamu wake, Wajumbe watano wa Halmashauri kuu ya Taifa (NEC), wajumbe watano wa baraza kuu la umoja huo Taifa na wawakilisha wa Jumuiya hiyo katika Jumuiya nyingine ndani ya chama.

SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumanne


Mfuko wa Kimataifa Umesitisha Msaada fedha za UKIMWI

$
0
0
Mfuko wa Kimataifa Umesitisha Msaada fedha za UKIMWI
Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria wa Umoja wa Mataifa umesitisha msaada wake wa kifedha kwa nchi ya Burundi.

Mfuko huo umetoa zaidi ya dola za Marekani milioni 275 kwa nchi hiyo katika kipindi cha miaka 14, na kueleza kuwa hatua ya kusimamisha msaada huo ni kutokana na matumizi mabaya ya fedha hizo.
Kwa mujibu wa barua ya mfuko huo kwa Waziri wa Afya wa Burundi, Josiane Nijimbere, pamoja na mambo mengine inatuhumu kuajiri kinyume cha sheria, maamuzi ya kufukuza wafanyakazi kiholela, kuingiliwa kwa usimamizi, na gharama za magari.

Sheik Ponda Akanusha Tuhuma za Kutoa Maneno ya Uchochezi

$
0
0
Sheik  Ponda Akanusha Tuhuma za Kutoa Maneno ya Uchochezi
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda amekanusha tuhuma kuwa alitoa maneno ya uchochezi alipozungumza na waandishi wa habari wiki iliyopita.

Badala yake, Ponda amesema alitoa tahadhari kwa matukio yanayojitokeza na jinsi ya kuyakabili kwa mustakabali wa amani ya nchi.

Sheikh Ponda alishikiliwa na polisi kwa takriban siku mbili baada ya kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu safari yake ya Nairobi, Kenya alikokwenda kumjulia hali mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Katika mkutano huo alizungumzia utekaji, kuokotwa kwa miili ya watu na mazungumzo aliyofanya na Lissu

Polisi walimhoji na kupekua nyumbani kwake wakituhumu kuwa alitoa maneno ya uchochezi.

Akizungumza na Mwananchi baada ya kuripoti polisi, Sheikh Ponda alisema: “Nilizungumza kwa nia nzuri kwa masilahi ya Taifa na umma. Nilikuwa nakumbushia vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwamba vina wajibu wa kusimamia amani na usalama.

“Kile nilichozungumza nimewaeleza nilikuwa sahihi na sikuwa na nia mbaya hata kidogo. Leo (jana) saa 3:00 asubuhi nimeripoti na nimeelezwa niondoke na watakaponihitaji muda wowote watanipigia simu.”

Kuhusu upekuzi uliofanyika nyumbani kwake Ubungo - Kibangu, Sheikh Ponda alisema hawakukuta chochote.

“Walidai wanatafuta kama kuna nyaraka zozote za uchochezi, lakini hawakuzikuta. Tuliporudi polisi dhamana ilishindikana kwa kuwa wakubwa hawakuwepo.”

Sheikh Ponda, mwanaharakati wa haki za Waislamu, alijisalimisha Kituo Kikuu cha Polisi Oktoba 13 asubuhi kwa wito wa kamanda wa Jeshi la Polisi wa Kanda ya Dar es Salaam ambaye alimpa saa 72 kufanya hivyo.

Baada ya kujisalimisha alishikiliwa kwa mahojiano na baadaye askari walikwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake na aliachiwa Oktoba 14 akitakiwa kuripoti jana.

Upinzani Waahirisha Maandamano Dhidi ya Tume ya Uchaguzi Kenya

$
0
0
Upinzani Waahirisha Maandamano Dhidi ya Tume ya Uchaguzi Kenya
Muungano wa upinzani nchini Kenya National Super Alliance (Nasa) umefutilia mbali maandamano ambayo yalikuwa yamepangiwa kufanyika nchini humo leo kushinikiza mageuzi katika tume ya uchaguzi.
Muungano huo, kupitia taarifa, umesema umechukua hatua hiyo kupata fursa ya kuomboleza watu ambao wameuawa kwenye maandamano ya awali.
Nasa, muungano unaoongozwa na waziri mkuu wa zamani Raila Odinga, ulikuwa umeahidi kufanya maandamano kila siku kushinikiza mageuzi katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa marudio.
Taarifa iliyotumwa na msemaji wa Bw Odinga, Dennis Onyango, imesema maandamano hayo yatarejelewa tena Jumatano.

Uchaguzi mkuu umepangiwa kufanyika tarehe 26 Oktoba baada ya Mahakama ya Juu kufuta matokeo ya uchaguzi wa tarehe 8 Agosti na kuagiza uchaguzi mpya wa urais ufanyike katika kipindi cha siku 60.
"Hii ni hatua ya muda ya kuuwezesha muungano huu kuwazuru na wafuasi wake waliokumbana na ukatili wa polisi na jamaa za waliojeruhiwa au kuuawa," taarifa hiyo ilisema.
Jumatatu, kijana wa miaka 18 aliuawa kwa kupigwa risasi wakati wa maandamano kati ya polisi na wafuasi wa upinzani mjini Kisumu.

Zaidi ya Bilioni 330 Zatengwa Kujenga Kituo cha Ubungo

$
0
0
Zaidi ya Bilioni 330 Zatengwa Kujenga Kituo cha Ubungo
Wakati ujenzi wa flyover ya makutano ya Ubungo ukiendelea, Kampuni ya Linghang Group imetenga zaidi ya Sh330 bilioni kukibadili Kituo cha Mabasi Ubungo (UBT) kuwa cha biashara.

Makubaliano yaliyofanywa kati ya kampuni hiyo, Wakala wa Barabara (Tanroads) na Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart) yamekamilika na kinachosubiriwa ni vibali vya ujenzi pamoja na tathmini ya athari za mazingira.

Meneja mkuu wa Linghang Group, Cathy Wang alisema endapo kila kitu kitaenda kama kinavyotakiwa basi ujenzi wa kituo hicho cha biashara kitakachojulikana kama East Africa Commercial and Logistic Centre utaanza mapema Januari.

“Tutajenga kwa miezi 15. Kitakapokamilika, kitakuwa na maduka 3,550 pmoja na eneo la kuegesha magari 5,000. Wafanyabiashara kutoka mikoani wataweza kumaliza mahitaji yao hapa hivyo kupunguza foleni ya kwenda Kariakoo,” alisema Cathy.

Wateja

Akielezea muongekano wa kituo hicho kitakachokuwa kwenye eneo la mita 124,000 za mraba na kutoa zaidi ya ajira 20,000, Cathy alisema kutakuwa na maduka ya wauzaji wa jumla na litatengwa eneo kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo pia.

Kuimarisha usalama wa wateja na mali zao, alisema kutakuwa na kituo cha polisi na eneo zima litafungwa kamera za ulinzi (CCTV) huku kukiwa na nafasi za kuegesha magari chini na juu ya jingo hilo litakalokuwa la ghorofa tano.

Kurahisisha usafiri, kutakuwa na kituo cha kupakia na kushusha abiria wa mabasi ya mwendokasi huku barabara nyingine ikijengwa na Tanroads kutoka kituoni hapo mpaka Simu 2000.

Biashara

Kituo kitakuwa na huduma zote za msingi katika eneo moja. Cathy alisema kutakuwa na matawi ya benki za biashara ambayo yatawapa fursa wafanyabiashara kuweka fedha zao za mauzo hivyo kupunguza hatari ya kuvamiwa endapo wangezisafirisha kwenda kwingineko. Wateja pia wataweza kutoa fedha wanazozihitaji ndani ya jengo hilo. Kitakuwapo na ofisi za Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) ambazo zitakuwa na dirisha moja linalotoa huduma za Mamlaka ya Mapato (TRA) na Mamlaka ya Bandari (TPA) pamoja na nyinginezo muhimukatika kufanikisha biashara.

“Serikali itaweza kukusanya kodi na kusimamia uingizaji na usafirishaji wa bidhaa nje ya nchi,” alisema Cathy.

Mtandao

Ubungo haitakuwa peke yake. Itaunganishwa na vituo vingine muhimu ili kuongeza ufanisi wake. Meneja huyo alisema vituo vingine vitajengwa Kigoma Mjini na Mutukura ili kufanikisha usafirishaji wa bidha anje ya nchi.

Kufanikisha biashara, bidhaa zitapokelewa kutoka kituo cha viwanda na biashara kinachotarajiwa kujengwa Kurasini ambako wafanyabiashara watakaokuwa na maduka Ubungo watapewa kipaumbele cha kuwa na maghala ya kuhifadhia mizigo yao.

Kwa kutumia Reli ya Kisasa (SGR) inayojengwa kutoka jijini hapa kwenda mikoani, bidhaa hizo zitasafirishwa mpaka Kigoma au Mutukula kwa ajili ya masoko zilizopo ukanda huo.

Wakati Ubungo zikitarajiwa kutumika Dola 150 milioni za Marekani (zaidi ya Sh330 bilioni), Cathy alibainisha: “Kigoma Mjini tutatumia Dola 50 milioni (zaidi ya 1.1 bilioni). Miradi yote ikikamilika, Tanzania itakuwa kama Dubai au Singapore.”

Kitakapokamilika kituo cha Kigoma kitakuwa na maduka 500 yatakayokidhi mahitaji ya nchi za Burundi, Rwanda na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Alifafanua, chaguo la kujenga kituo hicho nchini ni kuiunganisha Tanzania na nchi zisizo na bahari kufanikisha biashara kati ya ukanda huo na dunia nzima na kwamba kwa jinsi ilivyo, Tanzania itakuwa na mafanikio kama au zaidi ya Dubai ambayo imepata mafanikio iliyonayo ndani ya miongo mitatu.

Alisema kwa utafiti walioufanya Dubai, fursa zilizopo huko zipo nchini pia hivyo anaamini kukamilika kwa mradi huo kutaongeza mchango wa sekta ya biashara kwenye Pato la Taifa (GDP) na kupunguza umaskini kwa kiasi kikubwa.

“Kwa sasa asilimia 40 ya uchumi wa Dubai unategemea biashara, hilo litakuwapo Tanzania pia. Ubungo na matawi yake ya Kigoma na Mutukula yatasaidia kufika huko,” alisema Cathy.

Alipotafutwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Makori ili kufahamu utaratibu utakaokuwapo kwa zaidi ya mabasi 500 yanayokitumia kituo hicho alisema ametingwa na kutaka atafutwe leo.

“Nipigie kesho nikupe majibu ya uhakika,” alisema kwa ufupi.

Katikati ya Machi, Rais John Magufuli aliweka jiwe la msingi kuzindua ujenzi wa barabara za juu (flyover) katika makutano ya Barabara ya Nelson Mandela inayoungana na ya Sam Nujoma, na Morogoro yaliyopo Ubungo utakaochukua miezi 30 kukamilika.

Mradi huo unajengwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia ukigharimu Sh188.71 bilioni unatarajiwa kukamilika Septemba ya mwaka 2019 na kupunguza msongamano wa magari katika barabara hizo kwa kiasi kikubwa

Huu Umaarufu Unani 'cost' Unanifanya Nishindwe Kufanya Vitu Vingine Kama Binadam- Wema Sepetu

$
0
0

Huu Umaarufu Unani 'cost' Unanifanya Nishindwe Kufanya Vitu Vingine Kama Binadam- Wema Sepetu
MUIGIZAJI nyota wa filamu Bongo, Wema Sepetu, analia na umaarufu mkubwa alionao kwani umemfanya kushindwa kufanya vitu vingi ambavyo kama binadamu, na yeye alitamani kufanya.

Akiwa hajawahi kupanda daladala kwa miaka 11 sasa, tangu alipovikwa taji la Miss Tan- zania mwaka 2006, Wema al-isema akiwa ndani ya gari lake barabarani, hujisikia raha sana kuona watu wakiwa wamepanda usafiri huo, wakiwa wanazungumza na kucheka, kitu ambacho anakimiss sana, lakini hamna namna anayoweza kufanya.

“Unajua kiukweli kabisa natamani mno kupanda daladala, k w a sababu hata mimi ni binadamu, kuna kipindi natamani kupanda gari kutoka kwangu mpaka Kariakoo au mpaka Mbagala, lakini unafikiria utakapopanda itakuwa ni vurugu na siyo starehe tena, huu umaarufu kwa kweli unani-’cost’ sana wakati mwingine,” alisema Wema.

Malori ya Dangote Yaua Madereva Watatu

$
0
0
Malori ya Dangote Yaua Madereva Watatu
WATU watatu kati ya sita waliokuwa wakisafiri na malori yanayomilikiwa na kiwanda cha saruji cha Dangote mkoani Mtwara, wamekufa papo hapo na wengine kulazwa Hospitali ya Sokoine ya mkoa wa Lindi, baada ya magari hayo kugongana uso kwa uso.

Waliofariki ni Issa Rashidi Mbweso (28) ambaye ni dereva wa lori namba T 481 DJZ na mkazi wa mjini Mtwara, Haruni Nazir Mbonde (48) ambaye pia ni dereva wa lori la kiwanda hicho pamoja na utingo wake aliyefahamika kwa jina moja la Rajabu.

Majeruhi ni Ramadhani Nasoro (30) utingo na mkazi wa mjini Mtwara, Sophia Isumaili (35) na dada yake, Mawazo Omari (40) wakazi wa Kata ya Mandawa wilaya ya Kilwa.

Wakizungumza na Nipashe katika hospitali hiyo Lindi, majeruhi hao akiwamo utingo wa lori hilo namba T 481 DJZ lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Mtwara, walisema ajali hiyo ilitokea eneo la kitongoji cha Mihambwe, kwenye barabara kuu ya Kibiti-Lindi juzi mchana.

Sophia Isumaili na dada yake Mawazo Omari waliokuwa wameomba lifti kutoka Mandawa kwenda Newala mkoani Mtwara, walisema walipofika kitongojini hapo na kukuta barabara imezibwa na wingu la moshi mzito, alimuomba dereva Issa ambaye ni marehemu asimamishe gari wasubiri kupungua kwa moshi huo, lakini alikaidi na kujitosa.

“Tulipofika eneo lile na kukuta moshi mwingi nilimshauri dereva wetu tusimame ili kupisha moshi, lakini hakuwa tayari na kujibu atapita tu bila shida,” alisema Sophia.

Utingo Ramadhani Omari alisema kutokana na dereva kukaidi ushauri huo, walijikuta wakigongana uso kwa uso na lori lingine lililokuwa limebeba saruji likiwa limesimama kando ya barabara kupisha kupungua kwa moshi huo.

Alisema baada ya malori hayo kugongana, kulijitokeza cheche za moto na kuteketea kwa magari yote hayo wakiwamo madereva na utingo, kabla ya gari la Zimamoto kutoka Manispaa ya Lindi kwenda eneo la tukio Mihambwe kuuzima moto.

Mganga wa zamu katika Hospitali ya Sokoine, Dk. Edgal Mlawa, alithibitisha kupokea miili na majeruhi watatu, lakini hakuwa tayari kutoa maelezo zaidi akisema hadi mkuu wake wa kazi atakapofika.

“Licha ya kuwa nipo zamu muda huu, lakini siwezi kuelezea zaidi kwani mwenye mamlaka ya kuzungumza na vyombo vya habari ni mkuu wangu wa kazi,” alisema Dk. Mlawa.

Kamanda wa Polisi mkoani Lindi, Renatha Mzinga, alipoulizwa kupitia simu yake ya mkononi, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza taarifa kamili ataitoa baada ya kupelekewa na vijana wake waliokuwapo eneo la tukio.

Amber Lulu; Vituko Tunavyovifanya na Kukaa Nusu Utupu kwa Ajili ya Kutafuta Maisha si Vinginevyo.

$
0
0
MUUZA nyago maarufu kwenye video mbalimbali Bongo, ambaye kwa sasa amejitumbukiza kwenye muziki, Lulu Euggen ‘Amber Lulu’, amefunguka kuwa vituko wanavyofanya hasa kwa kukaa nusu utupu ni kwa ajili ya kutafuta maisha na si vinginevyo.

Amber Lulu ameiambia Kilinge kuwa, mtu anaweza akamuona ni msichana mhuni au ana wanaume wengi, kitu ambacho siyo kweli, bali akifanya hivyo ni moja tu ya kusaka pesa kwa ajili ya kuendesha maisha yake ya kila siku na si kwamba ana tabia mbaya kama watu wanavyomchukulia.

“Jamani mfano mimi nikipiga picha nimevaa nguo ya ndani tu utakuta ni kwa ajili ya kutangaza nguo hiyo lakini siyo kwamba najinadi au kujiuza kwenye mitandao kama watu wanavyochukulia,” alisema Amber Lulu.

Waziri wa Kilimo Awatumbua Watatu

$
0
0
Waziri wa Kilimo Awatumbua Watatu
Waziri wa Kilimo, Dkt Charles Tizeba amemuagiza katibu mkuu wa wizara hiyo mkoani Geita, Mhandisi Mathew Mtigumwe kuwafukuza kazi maafisa watatu wa wizara hiyo kutokana na kufanya jaribio la kutaka kuiibia serikali zaidi ya sh. bilioni 29.

Akizungumza na waandishi wa habari, Dkt Tizeba ambaye yuko mkoani Geita kwaajili ya siku ya maadhimisho ya Chakula duniani. watumishi watatu waliosimamishwa kazi ni Mkurugenzi wa maendeleo ya Mazao, Mkurugenzi wa kitengo cha ununuzi na ugavi, Aliekuwa akikaimu kitengo cha pembejeo

“Hawa sio tu wafukuzwe kazi lakini pia wakamatwe huko popote walipo, watafutwe wakamatwe kwa kuisababishia serikali hasara nimuombe tu IGP nani wawatafute hawajaa watatu hawa, wawatie mbaroni wakatusaidie kusema hizo pesa walifanya mpango gani na hawa watu waliokuwa wanashirikiana nao huko mikoani na wilayani kuuibia umma,” alisema Dkt Tizeba.

“Lakini pia naomba vyombo vya dola vya uchunguzi kuchunguza zaidi na kuchukua hatua stahiki za kisheria dhidi ya watu wote waliohusika katika mpanngo wa ruzuku na katika hili nina maanisha mambo yafuatayo kwasababu ripoti ipo tutawakabidhi wakuu wa mikoa wote nchini ambako mpango wa ruzuku ulikuwa unafanyika.”

Yanga Yabadirisha Upepo Yawafata Watani Wao Simba

$
0
0
Yanga Yabadirisha Upepo Yaafanya Maamuzi ya Kuwafata Simba
Yanga imefanya uamuzi wa kubadili upepo baada ya kubadili kambi yao kutoka Mwanza na kukimbilia Tabora kama ilivyokuwa kwa watani wao Simba walipojiandaa na mchezo dhidi ya Stand United.

Uamuzi huo wa Yanga ulichukua muda mfupi baada ya kutua Mwanza na kuamua kwenda Tabora kujiandaa na mechi dhidi ya Stand United ni njia iliyotumia na Simba na kufanikiwa kupata ushindi dhidi ya wapiga debe hao wa Shinyanga.

Simba baada ya kutoka sare 2-2 dhidi ya Mbao pale CCM Kirumba iliamua kupiga akili ndefu kwa kukimbilia mkoani Tabora waipoweka kambi kabla ya kurudi Shinyanga na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji wao Stand United.

Akili hiyo sasa ndiyo iliyotumiwa na Yanga ambao jana alfajiri kikosi chao badala ya kuingia Mwanza kuweka kambi kwa muda ya kujiandaa kuwafuata Stand waliamua kubadili njia na kwenda  Tabora.

Akizungumza na tovuti ya Mwanaspoti (www.mwanaspoti.co.tz), Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh amesema wameamua kuweka kambi Tabora ikiwa ni maelekezo ya benchi la ufundi lililokubaliana na uongozi wa klabu hiyo.

Hafidh alisema wakiwa mkoani Tabora watakuwa na kambi hiyo fupi itakayoambatana na mchezo mmoja wa kirafiki kisha kurudi Shinyanga kuwafuata Stand.

"Tumekubaliana timu inakwenda kuweka kambi Tabora hayo ndiyo  uamuzi ya mwisho yaliyotoka kwa uongozi na kuungwa mkono na benchi la ufundi," alisema Hafidh.

"Tunataka kupata sehemu itakayokuwa na utulivu ili tujiandae na huo mchezo muhimu kama unavyoona ligi ni mbichi, lakini pia ni ngumu lazima uwe na maandalizi ya maana kwa kila mchezo tukitoka huko tutarudi Shinyanga kucheza mechi yetu dhidi ya Stand."

Nigeria yakosoa Sanamu ya Rais Jacob Zuma

$
0
0
Serikali ya jimbo moja nchini Nigeria imempa heshima rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, kwa kumjengea sanamu kubwa ya shaba na kuipa barabara moja jina lake.

Wakati akifanya ziara katika jimbo lililopo kusini mashariki la Imo siku ya Jumamosi na Jumapili, Bw. Zuma alipewa cheo cha kiongozi wa kitamaduni ambacho ndicho cha juu zaidi kinachotolewa eneo hilo.

Muungano wa mashirika ya kupambana na ufisadi (CSNC) ambao ni wa zaidi ya mashirika 150 ya kupambana na ufisadi nchini Nigeria, umemlaani gavana wa jimbo Rochas Okorocha, kwa kumtambua Zuma kama mtu shujaa mbele ya kundi la vijana wa Afrika, wakati anakabiliwa na shutuma nyingi za ufisadi nchini mwake.

"Ni kama Gavana Okorocha hafahamu kuwa watu wa Afrika Kusini kwa sasa, wanamtaka rais wao ajuzulu kwa kuleta aibu kwenye nchi ya Nelson Mandela?" uliandika katika taarifa.

Pia taarifa hizo zimekosolewa vikali katika mtandao wa twitter.

Install Application ya MCHAMBUZI Kwenye Simu yako Kusoma Matamko ya Wanasiasa Kila Siku

$
0
0
 Maswala ya Siasa na Matamko ya kila siku ya Wanasiasa Hakikisha Umedownload App ya Mchambuzi Kwenye simu yako
Bonyeza HAPA

Kama we ni Mpenzi wa Habari za Siasa Usipitwe na Hii Application ya Mchambuzi..... Bonyeza HAPAKudownload kwenye Simu yako

Breaking News: Takukuru Yampa Onyo Nassari Kuhusu Ushahidi wa Rushwa wa Madiwani

$
0
0
Breaking News: Takukuru Yampa Onyo Nassari Kuhusu Ushahidi wa Rushwa wa Madiwani
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU imeita Waandishi leo Dar es salaam na kutoa onyo kwa Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari ambae alipeleka ushahidi wa rushwa kwa taasisi hiyo dhidi ya Mkuu wa Wilaya Arumeru Alexander Mnyeti.

TAKUKURU imesema “Ni kama Mh. Nassari na wenzie wanataka kulifanya hili swala kama la kisiasa badala ya kuwa la kisheria, namuonya Mh. Nassari ameshaleta taarifa yake kwetu, atuachie tufanye kwa mujibu wa sheria na sio kutushinikiza kama kauli aliyoitoa jana….. ‘nitaendelea kutoa series’ “

“Hii Taasisi haishinikizwi na mtu yeyote na hapaswi hata mara moja kutushinikiza…. natoa onyo jingine, endapo ataendelea na utaratibu huu tutachukua hatua za kisheria dhidi yake”

Unaweza kutazama tamko zima lililotolewa na TAKUKURU ikiwemo kwanini hawajaenda Mahakamani kwa haraka kwa kubonyeza play kwenye hii video hapa chini
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images