Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live

JE, Dada Unapenda Kuwa Mrembo? Kaka Kuwa Mtanashati na Kurudisha Heshima Katika Ndoa?

$
0
0

BAADA YA UTAFITI TULIOFANYA MARKSON BEAUTY KWA KUSHIRIKIANA NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (W.H.O) TUMEGUNDUA KUWA WANAUME WENGI DUNIANI HUSUMBULIWA NA MATATIZO KAMA👇👇
☆Kukosa hamu ya tendo.
☆Kuwahi kufika kileleni na kushindwa kurudia tendo.
☆Maumbile madogo ya uume.
☆Kuchoka sana wakati wa tendo na uume kusinyaa nk.
@natural2162 tumeandaa tiba bora kabisa kama ifuatavyo:-
1.HANDSOME UP OG_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @250,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 6.5 hadi 8 (wiki 2-3) @200,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @150,000/=
5.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @150,000/=
PIA KWA WANAWAKE WANAOPENDA KUWA NA MUONEKANO MZURI ZIPO ZA👇👇👇
☆Kuongeza hips, makalio na mapaja @200,000/=
☆Kushepu mguu (CHUPA YA BIA) @150,000/=
☆Kuwa mweupe bila sugu @150,000/=
☆Kurefusha nywele na kutokukatika ovyo @150,000/=
☆Kupunguza au kuongeza maziwa kuyasimamisha @130,000/=
*Kubana uke na kuzuia uchafu ukeni @130,000/=
*Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
BIDHAA HIZI NI ZA MIMEA NA MATUNDA NA ZIMEPIMWA KTK MAMLAKA NA KUPATA KIBALI HIVYO NI SALAMA KWA 100%

Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 au
0714335378
UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON BEAUTY CO pamoja na
garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Follow us
WEBSITE:- www.markworldbeauty.og
INSTAGRAM PAGE:-
@markson_beauty_pr

Download Application ya MCHAMBUZI Kwenye Simu yako Kusoma Habari za Siasa Kila Baada ya Lisaa Limoja

$
0
0
Maswala ya Siasa na Matamko ya kila siku ya Wanasiasa Hakikisha Umedownload App ya Mchambuzi Kwenye simu yako
Bonyeza HAPA

Kama we ni Mpenzi wa Habari za Siasa Usipitwe na Hii Application ya Mchambuzi..... 
Bonyeza HAPA Kudownload kwenye Simu yako

UVCCM yaomba Wanasiasa Wanaohubiri Udini, Ukabila Wakamatwe

$
0
0
Moshi. Kaimu Katibu mkuu wa Umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Shaka Hamdu Shaka, amevitaka vyombo vya usalama kuwashughulikia wanasiasa wanaohubiri udini na ukabila.

Shaka ameyasema hayo leo Novemba 4  wakati wa uzinduzi wa kampeni za udiwani kata ya Bomambuzi katika Manispaa ya Moshi, na kusisitiza kuwa vipo vyama vya siasa ambavyo vinataka kuwagawa watanzania.

“Tunu kubwa ya taifa letu ni upendo na amani kwa hiyo vyombo vya ulinzi na usalama viwashughulikie wanaohubiri udini, ukabila na ukanda ili kujipatia umaarufu wa kisiasa,” amesema.

Shaka aliwaambia wananchi waliofurika katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya soko la Pasua kuwa, alisema pamoja na yote yaliyojitokeza katika mkoa huo, bado wana imani na CCM.

Katika mkoa wa Kilimanjaro, upinzani unashikilia majimbo saba kati ya tisa huku CCM kikishikilia majimbo mawili tu ya Mwanga na Same Mashariki huku upinzani pia ukishikilia Halmashauri tano.

“Pamoja na yote yaliyojitokeza katika mkoa Kilimanjaro na kata mbalimbali bado mmeonyesha imani kubwa kwa Serikali ya CCM. Nawasihi sana katika uchaguzi huu msifanye makosa,” amesisitiza.

Pia ametumia mkutano huo kuwasihi wana CCM kutowabagua wala kuwatenga wanaorudi CCM wakitokea upinzani ambapo katika mkutano huo, baadhi ya wafuasi wa Chadema walijiunga na CCM.

Kwa upande wake, Katibu wa CCM mkoa Kilimanjaro, Jonathan Mabihya, amewaomba wananchi kumchagua mgombea Udiwani wa CCM, Juma Raibu akisema amejipanga vyema kuwatumikia.

Katika mkutano huo, aliyekuwa mmoja wa marafiki wa Waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Fred Mushi, alipewa fursa ya kuhutubia, na kusema huko upinzani alikoenda alikutana na moto.

Mushi ambaye alikuwa mwenyekiti wa UVCCM mkoa Kilimanjaro kati ya 2012 hadi 2015 alipojiuzulu na kumfuata Lowassa, alirejea tena CCM wiki mbili zilizopita akisema anamuunga mkono Rais John Magufuli.

Mwananchi:

Sarakasi za Uwoya za Kubadili Wanaume Zalichefua Kanisa

$
0
0
Baada ya ku­vuja kwa picha za staa wa filamu Bongo, Irene Uwoya (pichani) akiwa na staa wa Bongo Fleva, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ kuonesha wamefunga ndoa kisha mumewe Hamad Ndiku­mana ‘Katauti’ kuanika kifaa chake kipya, padri wa kanisa moja lililopo jijini Dar, ameibuka na kuwalipua wanandoa hao kwa kuishi kinyume na matakwa ya Kikristo.

ISHU ILIVYOANZA…
Hivi karibuni habari ya mjini kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na mitaani gumzo ilikuwa ni Uwoya kafunga ndoa na Dogo Janja lakini baadaye ilibainika kwamba ilikuwa ni kiki kwani walikuwa wanashuti video ya muziki.

NDIKUMANA AJIBU
Kutokana na hali hiyo Ndikumana au Ndiku naye aliamua kujibu mapigo ambapo aliweka picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa kima­haba na mrembo mmoja ambaye alitambulika kwa jina la Asma anayedaiwa kuwa ni Mrundi mwen­ziye.

Ili kuonyesha kwamba amedhamiria, Ndikumana alisindikizia picha hizo na maneno ‘sina habari na mtu nadeka zangu’. Baadaye akaongeza: ‘kata mti, panda mti.’

Baadhi ya mashabiki wal­ionekana kumuuliza kwamba anamjibu Uwoya baada ya kusemekana ameolewa ambapo aliwajibu: ‘aolewe, asiolewe mimi nina msimamo wangu na maisha yangu muda mrefu sana, mnataka kunipangia? Sijali mnayofikiria kwa sababu binadamu siku zote ndiyo tu­livyo, mimi ninafanya kinachouridhisha moyo wangu’.



NDUGU WA MWANAMKE WAJA JUU
Hata hivyo, baada ya kuanika picha hizo akiwa kimahaba na mwanamke huyo, tetesi zinadai kwamba ndugu zake mwanamke walikuja juu kwamba ni kwa nini ameamua kupiga picha na mwanaume huyo na kuzi­achia.
“Yaani unaambiwa ndugu wa Asma walikuja juu sana baada ya Ndikumana kuachia picha hizo mitandaoni, hali si shwari kabisa katika familia yao huku Burundi,” kilisema chanzo.

AMANI LATHIBITISHA FAMILIA KUTIBUKA
Amani liliingia mzigoni na kufanikiwa kuzungumza na mmoja wa marafiki wa Asma aliyeko jijini Dar ambaye alithibitisha kuwa mrembo huyo ame­charukiwa vibaya na wazazi wake baada ya kuona picha hizo za kimahaba zilizopostiwa na Ndiku­mana.


TUJIUNGE NA PADRI SASA…
Akizungumzia suala hilo kiimani, padri wa kanisa moja jijini Dar ambaye hakupenda jina lake li­chorwe gazetini, alisema, kitendo anachokifanya Uwoya na Ndikumana hakileti picha nzuri kwani ndoa ya Kikristo ambayo imefungwa kanisani, haivunjiki kirahisi.

KANISA LINAITAMBUA NDOA
Aliendelea kusema kuwa, hata kama wawili hao walitengana na kila mmoja kuwa na maisha yake siyo kwamba ndiyo ndoa imevunjika bali wao kan­isa linawatambua kama wanandoa, hivyo vitendo vyao vya kujiachia hovyo na wanawake au na wanaume ni kinyume kabisa na imani ya kanisa.
“Huyo Uwoya nimekuwa nikisoma kwenye mitandao ya kijamii mara utasikia yupo na mwa­naume huyu mara kabadilisha, kwa kweli dini hairuhusu mambo hayo.

“Ndoa yao ipo hai kanisani kwa sababu kwa dini yetu hakuna talaka, labda itokee kuna tatizo kubwa kama utagundua kwamba mmojawapo anazini na ushahidi ukawepo au ana tatizo la kinyumba ambalo halitatuliki ndiyo ndoa in­aweza kubatilishwa lakini kimsingi kanisa halitambui talaka.
“Kanisa linakataza kabisa uzinzi. Wanachokifanya kwa sasa ni zinaa. Kitendo hicho hakimpen­dezi Mungu kwa kuwa ni kinyume na imani na Biblia inavyosema, wanatakiwa wabadilike na wakae pamoja wamalize tofauti zao,” alisema padri huyo.

TUJIKUMBUSHE
Uwoya na Ndikumana walifunga ndoa mwaka 2009 katika Kanisa Katoliki, Mt. Joseph jijini Dar lakini walitengana na mpaka sasa Ndikuma­na bado hajatoa talaka rasmi kwa kile alichodai kuwa yupo kwenye harakati za kushughulikia mahakamani kwani ameshamtuma mtu jijini Dar.

Samatta Acheza Mechi ya 70 Akiwa na KRC Genk

$
0
0
NAHODHA wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta jana amecheza mechi yake ya 70 KRC Genk ikilazimishwa sare ya 0-0 na Lokeren katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A Ubelgiji Uwanja wa Luminus Arena, Genk.

Samatta alicheza kwa dakika 40 tu kwenye mchezo wa jana, kabla ya kumpisha Nikolaos Karelis aliyekuwa anacheza kwa mara ya pili tangu arejee uwanjani baada ya kuwa nje kwa muda mrefu kutokana na kuwa majeruhi.

Katika mechi hizo 70, Samatta, mshambuliaji wa zamani wa Mbagala Market, African Lyon na Simba za Tanzania, amefunga mabao 22 kwenye mechi za mashindano yote tangu alipowasili Genk Januari mwaka jana akitokea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Katika mechi hizo, Samatta ambaye ni mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora Anayecheza Afrika mwaka jana alipokuwa na Mazembe, 41 ameanza na mechi 24 ametokea benchi.

Na baada ya mchezo huo, Samatta aliyetajwa katika orodha ya wachezaji 30 ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) wanaowania tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika, anarejea nyumbani kujiunga na timu yake ya taifa kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Benin wiki ijayo.

Baada ya kucheza nyumbani mfululizo mechi za kirafiki za kimataifa, Taifa Stars sasa itatoka mwezi huu kwenda Benin kucheza na wenyeji Novemba 11, mwaka huu na kikosi cha wachezaji 24 kitaingia kambini leo  mjini Dar es Salaam kabla ya kusafiri Novemba 9 kwenda Benin tayari kwa mchezo huo.

Kikosi cha KRC Genk kilikuwa: Vukovic, Uronen, Colley, Aidoo, Mata/Maehle dk84, Heynen, Malinovskyi, Pozuelo, Writers/Benson dk79, Samatta/Karelis dk40 na Ingvartsen.

Sporting Lokeren : Verhulst, Maric, Skulason, De Sutter/Enoh dk74, Kehli/Söder dk90, Ticinovic/Marzo dk79, Rassoul, De Ridder, Filipovic na Mpati.

Wema Sepetu Aliamsha Dude Kwa Marafiki wa Bwana Ake

$
0
0
Siku chache baada ya picha za muigizaji Wema Sepetu na bwana’ke mpya aitwaye Bakari Kila akiwa bafuni kuvuja, mrembo huyo amedaiwa kulianzisha kum­saka ‘snichi’ aliyezivujisha.


Picha za Wema na Kila wakiwa bafuni zilivuja wiki kadhaa zilizo­pita katika gazeti ndugu na hili la Ijumaa Wikienda ambapo kwenye picha hizo, Wema alionekana akiwa amevalia kanga moja huku akimpiga busu motomoto Kila.
Mara baada ya ubuyu huo kuanikwa gazetini, chanzo makini kimeeleza kuwa, kuliibuka tafrani la aina yake wakati Wema alipokuwa akihaha kumtafuta mchawi.

“Unajua Madam (Wema) ni kama alichanganyikiwa. Alishindwa kung’amua hasa nani ni mdudu mtu ambaye alivujisha picha hizo. Maz­ingira ya picha hizo walipiga wakiwa wawili, yeye na mpenzi wake tena kimahaba zaidi.


“Anajiuliza sasa kama aliyepiga ni yeye na picha hizo alikuwa nazo yeye na mpenzi wake, ni nani kazivujisha? Sasa kwa sababu hana uhakika, an­ampigia tu kila mtu ili kumpa msala. Yani marafiki wa jamaa yake wana­koma sasa hivi,” kilisema chanzo hicho cha uhakika.


Kikizidi kumwaga ubuyu, chanzo hicho kiliweka bayana kuwa, mrem­bo huyo hakumaindi sana zilipovuja zile picha za awali akiwa amekaa kwenye kochi lakini zilipovuja hizo mpya za chumbani, alichanganyiki­wa sana kumsaka mchawi.

“Unajua hizi mpya ziko romantic sana. Walikuwa nazo wao wawili tu, yeye na bwana wake sasa anajiuliza ni nani amezitoa hadi zikawafikia Global?,” kilisema chanzo hicho.

Kuonesha kwamba amekerwa na kuvuja kwa picha hizo, Wema alione­sha masikitiko yake kupitia kwenye mtandao wa Instagram ambapo alilalamika kuwa mtu aliyemuamini ndiye aliyevujisha hizo picha.

Licha ya Amani kuona povu la Wema mitandaoni akimlaumu aliye­vujisha picha hizo (si ambaye amezi­vujisha Global), lilijaribu kumvutia waya Wema ili kumsikia kama ana lolote kuhusiana na picha hizo, simu yake iliita bila kupokelewa.

GPL

Simba inahitaji Ushindi Kuliko kitu Chochote Kulinda Heshima

$
0
0
Mchezo kati ya Mbeya City dhidi ya Simba unasubiriwa kwa shauku kubwa na wadau wa soka nchini kwa sababu ni mchezo utakaoamua kinara wa ligi kuu Tanzania bara baada ya mechi za mwisho wa juma hili.

Simba inahitaji ushindi kuliko kitu chochote kwenye mchezo huo ili kuendelea kuongoza ligi hasa baada ya matokeo ya mechi za jana (Jumamosi November 4, 2017) ambapo wapinzani wa Simba kwenye nafasi ya kwanza Yanga na Mtibwa zilibanwa na kulazimishwa sare huku Azam ikishinda na kuongoza ligi baada ya kufikisha pointi 19 pointi mbili zaidi ya Yanga na Mtibwa ambazo zilicheza jana.

Pointi tatu pekee ndio zitaifanya Simba kurejea kwenye nafasi yake, matokeo tofauti na hayo maana yake ‘Mnyama’ atapoteza uongozi wa ligi kwa kuiacha Azam itawale kileleni. Endapo Simba itashinda itafikisha pointi 19 sawa na Azam lakini wastani mzuri wa magoli utaipeleka kwenye nafasi ya kwanza, matokeo ya sare yoyote yataifanya ibaki nafasi ya pili kwa wastani wa magoli kwa sababu  italingana pointi na Mtibwa pamoja na Yanga. Ikipoteza mbele ya City itaendelea kusalia katika nafasi ya nne ambayo ipo sasa ikiwa na pointi 16.

Matokeo ya Mbeya City kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya

Wameshinda mechi tatu kati ya nne walizocheza kwenye uwanja wao wa nyumbani, hawajashinda mechi yoyote nje ya Mbeya matokeo yao ya ushindi yamepatikana kwenye uwanja wa Sokoine. Mbeya City tayari imecheza mechi nane, imeshinda michezo mitatu, sare mbili huku ikiwa imepoteza michezo mitatu.

‘Wana-koma kumwanya’ wamepoteza mchezo mmoja wakiwa uwanja wa Sokoine huku mechi nyingine mbili wakidondosha pointi sita kwenye viwanja vya ugenini.

Mbeya City 1-0 Majimaji
Mbeya City 0-1 Ndanda
Mbeya City 1-0 Njombe Mji
Mbeya City 2-0 Ruvu Shooting
Katika magoli tisa waliyofunga kwenye mechi zao nane, manne kati ya hayo wamefunga wakiwa kwenye uwanja wa Sokoine na magoli matano yakifungwa kwenye viwanja vya ugenini.

Matokeo ya mechi za Simba nje ya uwanja wa Uhuru

Simba hawana rekodi nzuri wanapocheza viwanja vya ugenini, wameshinda mechi mmoja kati ya tatu walizocheza nje ya uwanja wa Uhuru. Ushindi pekee wa Simba katika mechi walizocheza nje ya uwanja wa Uhuru ni dhidi ya Stand United ya Shinyanga. Mchezo wa Yanga vs Simba haujahesabiwa kama wa ugenini kwa sababu uwanja huo ni wa nyumbani kwa vilabu vyote viwili kinachobalika ni zamu ya timu ipi kuwa nyumbani na nyingine kuwa ugenini kwenye uwanja huohuo.

Azam 0-0 Simba
Mbao 2-2 Simba
Stand United 1-2 Simba
Simba imefunga magoli manne tu nje ya uwanja wa uhuru kati ya magoli 20 iliyofunga katika mechi nane zilizopita za ligi kuu.

Matokeo ya Mbeya City vs Simba uwanja wa Sokoine, Mbeya

Mbeya City imecheza mara nane (mechi zote nyumbani na ugenini) mechi za VPL dhidi ya Simba tangu timu hiyo ya jijini Mbeya ilipopanda kucheza ligi kuu Tanzania bara msimu wa 2013/2014. Katika mechi nne ambazo Mbeya City imekutana na Simba kwenye uwanja wa Sokoine, Simba imeshinda mara mbili, imefungwa mara moja na kuambulia sare mara moja.

12/10/2016 Mbeya City 0-2 Simba
17/10/2015 Mbeya City 0-1 Simba
18/04/2015 Mbeya City 2-0 Simba
15/02/2014 Mbeya City 1-1 Simba

Aslay afunguka kuhusu Dogo Janja na Irene Uwoya

$
0
0
Msanii wa muziki wa Bongo fleva Aslay amefunguka na kusema kuwa msanii Dogo Janja yeye ndiye alikuwa anamvia Irene Uwoya na kusema ni kweli sasa wameoana na wanaishi kama mume na mke.

Aslay amesema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Frida Night Live (FNL) na kusema kuwa yeye anachojua watu hao saizi ni mume na mke na si kweli kuwa Irene Uwoya kwamba alikuwa anamvizia sana Dogo Janja bali yeye anaamini kuwa huenda Dogo Janja ndiye alikuwa anavizia penzi la Irene Uwoya.


Madee Aibua Jipya Kuhusu Dogo Janja na Uwoya

$
0
0
Msanii wa muziki wa Bongo fleva Madee amefunguka na kusema kuwa msanii Dogo Janja ambaye amemlea na kumtambulisha katika ulimwengu wa muziki alimficha sana kuhusu mahusiano yake na Irene Uwoya.

Madee amesema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Friday Night Live (FNL) na kudai kuwa awali kabla ya kupewa taarifa ya msanii huyo kuoa walikaa karibu siku mbili wakijifikiria wanapelekaje taarifa hizo kwake na kusema siku alipoambiwa hakuamini hivyo ilibidi ampigie simu Irene Uwoya kwanza kutaka kujua kama kweli au Dogo Janja anataka kumpiga mzinga.

CCM Arusha yampa ushauri wa bure Godbless Lema

$
0
0
Chama cha mapinduzi (CCM) Arusha kupitia kwa katibu Elias Mpanda kimefunguka kuhusu Wafuasi wanaodaiwa kuwa wa CHADEMA kuwashambulia watu watatu wa CCM akiwemo Mgombea Udiwani kata ya murieti Fransis Mbise.

Mpanda amesema “Sisi CCM kwakweli ni Wastaarabu na ninataka niwahakikishie kati ya kata zote 8 ambazo nimesema tutashinda, tutashinda kwasababu tuna hoja za kusema juu ya Wananchi“

“Nashukuru Wananchi wa Arusha na kama sio Tanzania nzima wameshatambua dhamira kubwa ya CHADEMA kwamba dhamira yao sio kuwaletea Wananchi maendeleo bali kuwatumia kwa maslahi yao binafsi”

“Ushauri wa bure kwa ndugu Godbless Lema, kwanza Wafuasi wa CHADEMA niwaombe sana wasitumike vibaya kwasababu hata jana walioleta fujo wote walikamatwa na wako polisi lakini Godbless alikimbia pamoja na katibu wa chama wa Wilaya”

Wakili Msomi Atinga Mahakamani Kudai Wanaume Wafutiwe Mahari

$
0
0
Wakili msomi nchini Zimbabwe, Bi. Priccilar Vengesai ameanzisha kesi mahakamani ya kufutilia mbali mahari zinazotolewa na wanaume pale wanapooa akidai kuwa ni mila iliyopitwa na wakati.

Tokeo la picha la pete ya ndoa

Wakili huyo amewasilisha malalamishi yake katika mahakama juu nchini humo akitaka kusikilizwa kwa kesi yake huku akilalamika kuwa utamaduni huo unakiuka haki za kibinaadamu.

Bi. Priccilar Vengesai anaamini kuwa endapo utamaduni huo utaendelea ,familia zote za mume na mke zinatakiwa kulipa mahari kwa maslahi ya usawa wa kijinsia.

Akizungumza na gazeti la serikali nchini Zimbabwe la Herald, Wakili huyo amesema kuwa anataka kuolewa upya baada ya ndoa yake ya kwanza kuvunjika kwani hakuwa na sauti ya kuhoji kiasi cha mahari iliyotolewa na kujiona kama bidhaa.

“Nataka kuolewa tena sitaki kupitia kama niliyopitia kwenye ndoa yangu kwani sikushiriki katika kuuliza gharama ya mahari. Sikupewa fursa ya kuuliza kwa nini mahari ilitolewa wala kujua hata ni kiasi gani.“amesema Bi. Vengesai na kuendelea kusimulia kisa hicho.

“Hali yote hiyo ilinifanya mimi kuonekana kama bidhaa ambapo kiwango cha thamani yangu kilipendekezwa na wajomba zangu na mume wangu akalipa. Hatua hiyo ilinivunja moyo kwani ilinifanya nijione mnyonge mbele ya mume wangu na kujihisi kama nimenunuliwa.“amesema Wakili huyo.

Hata hivyo, Bi. Vengesai ambaye anatoka katika kabila la washona amesema kuwa anatamani kuingia kwenye ndoa mapema baada ya mahakama kutoa tamko juu ya madai yake.

Nchini Zimbabwe mahari hutolewa na upande wa familia ya mwanaume na kama haitatoka basi mwanamke hataruhusiwa kuishi na mwanamme kwa namna yoyote ile

Kutana na Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed Kutoka Bagamoyo...Ana Dawa za Kurudisha Mapenzi na Zingine Nyingi

$
0
0
MIUJIZA YA SHARIFU SEIF MOHAMED KUTOKA BAGAMOYO.

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,
(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

USHAURI: kama unahitaji msaada ni  bora kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate  msaada kwa haraka.

Nay wa Mitego Awatosa Alikiba na Diamond

$
0
0
Nay wa Mitego amefunguka na kuzitaja ngoma kubwa ambazo zimepata umaarufu mkubwa zaidi nchini na kusema ni ngoma ya Muziki ya Darassa, Moyo Mashine ya Ben Pol, Bongo Bahati mbaya ya Young D na Wapo ya Ditto huku akizitosa ngoma za Alikiba na Diamond.

Ney wa Mitego amesema hayo kwenye kipindi cha Friday Night Live (FNL) na kudai hizi ndiyo ngoma kali ambazo zilitoka na kuwa kubwa kila kona nchini na kuleta mpaka misemo mtaani huku akidai zipo nyimbo nyingine zilikuwa kubwa lakini hazikuwa na matokeo makubwa kama ngoma hizo alizozitaja.
Mtazame hapa akifunguka zaidi.

Bila Kuondoa CCM hakuna Kitakachobadilika - Sumaye

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye amefunguka na kusema kuwa bila kukiondoa Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani basi hali ngumu za maisha za wananchi kwa wananchi wa chini haziwezi kubadilika kamwe.

Sumaye aliyasema hayo jana akiwa katika uzinduzi wa kampeni za Udiwani katika Kata ya Kijichi jijini Dar es Salaam na kusema kuwa amezunguka nchi nzima na kuona jinsi watu ambavyo wanaishi katika mazingira magumu kutoka na hali ngumu ya maisha.

"Tusipoipiga CCM chini Watanzania tutaendelea kuteseka, hali ya maisha itaendelea kuwa ngumu mtapigwa maneno ya hapa na pale lakini ukweli ni kwamba bila kuwaondoa hawa watu madarakani hali za maisha ya Watanzania hazitakuja kubadilika hata siku moja, tutaendelea kupondea mitumba, miguu ya kuku na utumbo, mtaendelea kukondeana, mtaendelea kupauka na ukiona mtu amenenepa ni kwashakoo tu si afya kwa sababu maisha ni magumu" alisema Sumaye

Sumaye amedai ili Watanzania waepukane na maisha hayo ya hovyo ambayo sasa wanaishi wanapaswa kukipiga chini Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho kimeshindwa kuboresha maisha ya Watanzania toka nchi imepata uhuru mpaka leo.

Godbless Lema Ampa Salamu Mrisho Gambo

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA) Godbless Lema amefunguka na kumpa salamu Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo na kumwambia kuwa akijaribu kufanya wizi katika uchaguzi wa udiwani unaotarajiwa kufanyika mwisho wa mwezi huu basi kutakuwa na mambo mawili

Lema amesema hayo jana katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo katika Kata ya Muriet Arusha mjini na kusema endapo Mkuu huyo wa Mkoa na Mkurugenzi wataiba uchaguzi huo basi kutatokea makundi mawili ya watu.
Mtazame hapa akifuguka zaidi.

Watu 26 Wauawa kwa Kupigwa Risasi Kanisani Texas, Marekani

$
0
0
Watu 26 wameuawa kwa kupigwa risasi na mtu mwenye silaha aliyewafyatulia risasi waumini katika kanisa moja jimbo la Texas wakati wa ibada, maafisa wanasema.

Shambulio hilo lilitekelezwa katika kanisa la First Baptist Church katika mji wa Sutherland Springs, mji mdogo katika wilaya ya Wilson, Texas.

Mshambuliaji, ambaye anadaiwa kuuawa baada ya kutekeleza mauaji hayo, aliingia kanisani na kuanza kuwafyatulia risasi watu mwendo wa saa tano unusu asubuhi (17:30 GMT).

Gavana Greg Abbott amethibitisha idadi ya waliofariki na kusema ndicho kisa kibaya zaidi cha mauaji ya kutekelezwa kwa kutumia bunduki katika historia ya texas.

"Kutakuwa na majonzi na masikitiko mengi kwa wale walioathiriwa," aliambia wanahabari.

Mkuu wa idara ya usalama wa Texas Freeman Martin amesema waathiriwa walikuwa na umri wa kati ya miaka 5 na 72

Maafisa wamesema watu zaidi ya 20 pia walijeruhiwa na wamelazwa hospitalini.

Bw Martin amesema mshukiwa ni mwanamume mzungu wa umri wa miaka 20 ambaye alikuwa amevalia mavazi meusi na fulana ya kujikinga dhidi ya risasi pamoja na kuwa na bunduki yenye uwezo mkubwa.

Alianza kufyatua risasi nje ya kanisa kabla ya kuingia ndani na kuendelea kufyatulia watu risasi.

Mwenyeji "litwaa bunduki yake na kuanza kumfyatulia " risasi mshukiwa kabla ya mshukiwa huyo kutoroka akitumia gari.

Raia huyo alimwandama mshukiwa huyo ambaye aliendesha gari lake na kisha kuliangusha katika barabara wilaya ya Guadalupe.

Polisi waelimpata mshukiwa akiwa amefariki ndani ya gari lake.

Haijabainika iwapo alifariki kutokana na majeraha ya risasi aliyojisababishia mwenyewe au kutokana na mejaraha kutoka kwa raia huyo, Martin ameongeza.

Mshukiwa ametajwa kuwa Devin P Kelley, 26, kwa mujibu wa vyombo vya jhabari Marekani.

Polisi bado hawajathibitisha jina lake.

Mhubiri wa kanisa hilo la First Baptist Frank Pomeroy, ameambia ABC News kwamba binti yake wa miaka 14 kwa jina Annabelle ni miongoni mwa waliouawa.

Sutherland Springs ni mtaa mdogo wenye wakazi wasiozidi elfu moja ambao hupatikana kilomita 50 hivi kusini mashariki mwa mji wa San Antonio mjini Texas.

Maafisa wa FBI kutoka San Antonio wametumwa kufanya uchunguzi lakini kufikia sasa lengo la mshambuliaji halijabainika.

FBI pia wamesema mshambuliaji alikuwa mmoja pekee, lakini bado wanachunguza uwezekano wa iwapo kuna mtu mwingine aliyehusika.

Rais Donald Trump, ambaye yumo ziarani Asia, ameshutumu kisa hicho na kusema ni "kitendo cha uovu" na kusema kwamba Wamarekani watajikwamua na kusalia na umoja.

"Na kupitia kwa machozi na kupitia huzuni hii, tunasalia imara, imara zaidi," ameongeza.

Mauaji hayo yametokea mwezi mmoja tu baada ya mshambuliaji mwingine kufyatulia risasi watu waliokuwa wakihudhuria tamasha ya muziki Las Vegas na kuwaua watu 58 pamoja na kujeruhi mamia wengine, katika kisa kibaya zaidi cha mauaji ya kutumia bunduki katika historia ya Marekani nyakati za karibuni.

Hii ya Irene Uwoya Kuolewa Mara Mbili Tuiite Bahati au??

$
0
0
Helo wana nzengo wa humu jukwani. Hii tuite ni bahati kwa mwana dada Irene uwoya kuolewa mara mbili tena kihalali kabisa. Ya mwanzo kanisani na sherehe ya kufa mtu na hii sasa ya kiislamu. Kwa wadada ambao hawajapata bahati ya kuolewa huko bongo movie wanajisikiaje mwenzao kuolewa mara mbili wakati wao hata ya mkeka tuu hawajawahi. Hii inaonyesha mwanadada anamvuto sana au ndo vyuma vimekaza watu wanatafuta pa kujisitiri. Karibuni

Saudi Arabia yawasweka Ndani Bilionea Maarufu, Watoto 10 wa Kifalme na Mawaziri Wastaafu Kwa Tuhuma za Rushwa

$
0
0
Saudi Arabia Jumamosi imetangaza kuwakamata bilionea na muwekezaji maarufu Mwanamfalme Awaleed bin Talal pamoja na wanawafalme wengine wasiopungua 10 mawaziri wanne na makumi ya mawaziri wastaafu kwa tuhuma za rushwa

Kukamatwa kwa Mwanamfalme Alwaleed kumetikisa Saudi Arabia pamoja na vituo vya uwekezaji duniani

Anamiliki kampuni za za uwekezaji nchini humo na ni mmoja wa watu matajiri zaidi duniani akiwa anamiliki au ameshawahi kumiliki hisa nyingi katika mashirika ya habari, Citigroup, Twitter pamoja na makampuni mengine makubwa. Mwanamfalme huyo pia anamiliki mtandao wa televisheni unaotazamwa kwa eneo kubwa la Uarabuni

Kampeni hiyo ya kukamatakamata inaonekana kama njia ya kujiimarishia mamlaka ya mfalme mtarajiwa Mohammed bin Salman, mtoto wa Mfalme Salman

Akiwa na umri wa miaka 32 tu tayari mtoto huyo ana sauti kubwa kwenye jeshi la Saudi sera za kiuchumi, kijamii na za nje jambo linaloleta malalamiko katika familia ya kifalme kuwa amaejilimbikizia nguvu kubwa akiwa katika umri mdogo

Vituo vya ndege binafsi vilifungwa kwa ajili ya kuzuia wanawafalme wengine wasitoroke kabla ya kukamatwa

Ukosefu wa Elimu kwa Bongo Movie ndo Chanzo Kikubwa cha Tasnia Hiyo Kushuka- Shamsa Ford

$
0
0
Ukosefu wa Elimu kwa Bongo Movie ndo Chanzo Kikubwa cha Tasnia Hiyo Kushuka- Shamsa Ford
Msanii wa filamu nchini Shamsa Ford amewaponda baadhi ya wasanii wa Bongo movie na kusema ukosefu wa elimu kati yao chanzo kikubwa tasnia hiyo kushindwa kuendelea na kupiga hatua kubwa na kudai wamekalia umbea, chuki, ushirikina na roho mbaya.

Shamsa Ford amesema hayo kupitia mtandao wake wa Instagram na kudai kuwa anatamani muda ungekuwa unarudi nyuma ili aweze kubadili maamuzi yake na kuweza kusoma ili kupata maarifa zaidi kwani anaamini wasanii wengi wa filamu nchini wanashindwa kusonga kwenda Kimataifa kwa kukosa elimu.

"Mama yangu alinikazania sana nisome kwa bidii wakati nipo shule ila nilipomaliza form 6 nikaona inatosha. COUNTER BOOK la shule nikaona zito ila SCRIPT ya movie nikaona jepesi..Natamani ningerudisha siku nyuma ningesoma kwa bidii hata kama ningetaka kuwa muigizaji basi ningekuwa muigizaji wa kimataifa mwenye maarifa. Moja ya vitu vikubwa vinavyoturudisha nyuma bongo movie ni elimu. Mtu aliyesoma na asiyesoma ni vitu viwili tofauti. sasa sisi wenge wetu hatuna elimu kabisaa" aliandika Shamsa Ford
aliendelea kusisitiza kuwa "wengi wao darasa 7,5,2,6 wengine ndiyo kabisaa alijifunza kusoma na kuandika tu. Nakumbuka mwaka juzi nilimuona msanii wa Nigeria Genevieve akiojiwa CNN nikatamani niwe mimi. Wenzetu wamesoma ndiyomaana wametupita vitu vingi sana. Huku bongo movie kumejaa umbea, chuki, roho mbaya, ushirikina, mtu hata kama hujawahi kumkosea lakini akikaa na watu wanaokuchukia atakusema vibaya, Lakini pia ukijitenga useme uishi kivyako utaambiwa unalinga na vikao utaekewa. Yote haya ni kwasababu ya ukosefu wa elimu ndomaana watu wanaweza kupoteza muda kwa vitu vya kijinga" alisisitiza Shamsa Ford


Jike Shupa Yamkuta Atolewa Vyombo Nje Usiku wa Manane

$
0
0
Jike Shupa Yamkuta Atolewa Vyombo Nje Usiku wa Mnane
UBUYU wa leo ni wa moto na hauna bei kwani upo kwenye punguzo maalum kutokana na hali ya sasa kifedha kuwa siyo shwari! Muuza nyago aliyeinogesha video ya mwanamuziki Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’, Zena Abdalah ‘Jike Shupa’ yamemkuta. Ubuyu mtamumtamu wa mjini unamung’unywa kwamba, wiki iliyopita Jike Shupa alitolewa vyombo vyake nje kwenye nyumba aliyopanga maeneo ya Mwanyamala, Kwa-Manjunju jijini Dar, kisa kikidaiwa kuwa ni picha chafu anazotupia kwenye mitandao ya kijamii. Msambaza ubuyu huo alilitonya Ijumaa Wikienda kuwa, nyumba aliyopanga Jike Shupa inamilikiwa na watu walioshika Dini ya Kiislam.

KISA PICHA ZA UTUPU
Ilidaiwa kuwa, Jike Shupa ana tabia ya kutupia picha na video za utupu mitandaoni, jambo ambalo watu anaokaa nao hawalipendi na hata wapangaji wenzake hawataki mtu anayekwenda kinyume na maadili.
Habari zinazidi kudai kuwa, juzkati Jike Shupa alitupia video kwenye ukurasa wake wa Mtandao Kijamii wa Instagram, ikionesha wanawake wakicheza wakiwa utupu, jambo ambalo liliwakera mno watoto wa mwenye nyumba anayoishi. “Yaani ile nyumba anayoishi Jike Shupa ni ya watu walioshika dini sana, hawapendi kuona mtu anakiuka maadili, hata wapangaji waliowapangisha,” alisema mpashaji wetu huyo.

KUMBE ALISHAONYWA Mtoa Ubuyu huyo alizidi kubainisha kuwa, baada ya watoto hao kuona picha hizo walikereka kwa sababu mara kadhaa walishamuonya Jike Shupa kuwa hawapendi kupangisha mtu mwenye tabia kama hizo hivyo walipandwa na hasira na kumuomba aondoke, akatafute sehemu nyingine Chanzo hicho kilizidi kutiririka kuwa, baada ya watoto wa mwenye nyumba hiyo kutoa amri hiyo, Jike Shupa alianzisha timbwili akiwavimbia hivyo kuzidi kuwapandisha hasira na kuanza kurusha vitu vyake nje usiku wa manane. “Jike Shupa alikuwa akibishana nao huku wakirushiana maneno makali, jambo ambalo liliwakera watoto wa mwenye nyumba na kuamua kumtolea vyombo nje,” kilizidi kumwaga ubuyu chanzo hicho.
HUYU HAPA JIKE SHUPA
Baada ya gazeti hili kupata Ubuyu huo lilifanya jitihada za kumtafuta Jike Shupa ambaye alilielekeza Ijumaa Wikienda limfuate kwa rafiki yake. Alipoulizwa kuhusu ishu yake hiyo alikiri na kusema kuwa, mtu anapopanga nyumba na kumlipa mwenye nyumba fedha zake za pango, hapaswi kufuatiliwafuatiliwa. “Yaani wale watu walinizingua sana, mtu nimepangisha na fedha nimetoa, nini shida, nisitangaze shoo yangu? Sasa mimi nitakula wapi? Au fedha ya kodi nitapata wapi? Wala hawajaniumiza kabisa na nimeshapata nyumba nyingine,” alisema Jike Shupa.
NENO LA MHARIRI Jike Shupa ni staa hivyo anapaswa kuwa kioo cha jamii hivyo tukio lililomkuta linapaswa kuwa findisho kwa mwingine yeyote.
Viewing all 104793 articles
Browse latest View live




Latest Images