Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

Jeshi la Zimbabwe: Tunawalenga Wahalifu Sio Mugabe

$
0
0
Jeshi la Zimbabwe limesoma taarifa kwenye kituo cha runinga cha serikali ZBC, likisema kuwa linachukua hatua ya kuwalenga wahalifu.
Hata hivyo limesema kuwa hayo sio mapinduzi ya kijeshi na Rais Mugabe yuko salama.
Milio mikubwa ya risasi ilisikika katika maeneo ya kaskazini mwa mji mkuu Harare mapema leo.
Taarifa hiyo ya jeshi ilikuja saa kadhaa baada ya jeshi kudhibiti kituo cha ZBC.
Mwanamume mmoja ambaye alikuwa amevaa sare za jeshi alisema kuwa jeshi linataka kukabiliana na watu ambao wanatenda uhalifu unaoleta madhara ya kijamii na kiuchumi nchini Zimbabwe.
"Wakati tutakapomalzia wajibu wetu, tunatarajia kuwa hali itadudi kuwa sawa."
Taarifa hiyo ilisema kuwa Mugabe 93, na familia yake wako salama.
Image caption
Wanajeshi wakiwa na silaha nzito wameoneakana wakirandaranda mjini Harare
Haijulikani ni nani anaongoza hatua hiyo ya kijeshi.
Magari ya wanajeshi waliojihami kwa silaha yameonekana maeneo ya mjini Harare.
Hali hiyo ya wasi wasi wa lolote kuweza kutokea, imeanza hapo jana jioni, ambapo wanajeshi wakiwa na silaha walionekana wakijipanga katika maeneo kadhaa pamoja na kuzingira ofisi za shirika la utangazaji la Zimbabwe ZBC.
Rais Robert Mugabe amemfuta kazi Makamu wa Rais
Hata hivyo taarifa zinasema kuwa wafanyakazi wa shirika hilo la utangazaji ZBC, waliambiwa na wanajeshi hao kwamba hawapaswi kuwa na wasiwasi na kwamba uwepo wa vikosi hivyo ni kwa lengo la kulinda eneo hilo.
Milipuko mizito imeendelea kusikika pia.
Image caption
Mkuu wa jeshi la Zimbabwe Constantino Chiwenga alitahadharisha uwezekano wa jeshi kuchukua nchi
Chama tawala nchini Zimbabwe kimemtuhumu mkuu wa majeshi Constantino Chiwenga, kwa hatua yake ya madai kuwa jeshi lipo tayari kuingilia mzozo huo wa kisiasa kwa lengo la kulinda wapigania uhuru wa taifa hilo.
Bi Grace Mugabe ataka makamu wa rais afutwe kazi
Hakuna kauli yoyote iliyotolewa na Rais Robert Mugabe kutokana na hali ya sasa nchini mwake.
Marekani imesema kuwa inafuatilia kwa karibu hali ya Zimbabwe na kutoa rai pande zote kutatua mzozo huo kwa njia ya amani.
Image caption
Grace Mugabe anaonekana kukaribia kukirithi kiti cha mumewe
Naye Balozi wa Marekani nchini Zimbabwe kupitia ukurasa wake wa Tiwtter amesema kuwa leo watasitisha shughuli za kiofisi ubalozini hapo kutokana na halisi ya sasa mjini Harare.
Balozi wa Zimbabwe nchini Afrika Kusini Isack Moyo ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa serikali ipo imara katika jambo hilo na kuzuia uwezekano wowote wa kufanyika kwa mapinduzi.

Bilionea wa Nyumba za Lugumi Afunguka Kuhusu Siku 28 za Mateso Aliyopata Baada ya Kutekwa Urusi

$
0
0
Bilionea wa Nyumba za Lugumi Afunguka Kuhusu Siku 28 za Mateso Aliyopata Baada ya Kutekwa Urusi
Dk Louis Shika ‘bilionea’ aliyejitokeza kununua majumba ya kifahari ya mfanyabiashara maarufu Said Lugumi ameelezea siku 28 za mateso aliyodai kuyapata baada ya kutekwa nyara nchini Urusi miaka 13 iliyopita.

Dk Shika, ambaye jana aliachiwa kwa dhamana na polisi amesema haikuwa rahisi kujinasua kwa sababu alipata mateso makali na alijua ndiyo mwisho wa maisha yake, lakini kwa uhodari na nguvu za Mungu alifanikiwa kutoroka kutoka mikononi mwa watekaji hao.

Hata hivyo aliendelea kusisitiza kuwa mpango wake wa kununua nyumba za Lugumi haujabadilika na kwamba ataishangaza dunia.

Alisema hayo jana jioni katika mahojiano maalumu na Mwananchi nyumbani kwake Tabata Mawenzi baada ya kurejea kutoka mahabusu ya Kituo Kikuu cha Polisi alikoshikiliwa kwa siku sita akituhumiwa kuvuruga mnada huku leo akitakiwa kuripoti kituoni hapo saa tatu asubuhi.

Dk Shika, ambaye alidai kuwa alikwenda Urusi kwa masomo na baadaye kufanya kazi nchini humo alisimulia kuwa alitekwa na watu wasiojulikana Juni mwaka 2004 huku ‘watekaji’ wakimtaka awape Dola1.5 milioni za Marekani (Sh3 bilioni kwa sasa) ambazo hakuwa tayari kuzitoa licha ya kuwa na uwezo wa kuwapa.

“Nilipokamatwa walinipeleka sehemu huku nikipigwa, nikiteswa kwa siku 28 na nilijua ndio itakuwa kifo changu. Nilipigwa ngumi, niliteswa vikali, walitumia nyaya za umeme kunitesa, walinikata vidole kimoja kwa nyundo na viwili kwa panga, yote wakitaka niwape dola milioni moja na nusu,” alisema Dk Shika, ambaye mwandishi wa habari hizi alishuhudia kuona mkono wake wa kushoto ukiwa umekatwa vidole viwili na kidole kimoja mkono wa kulia.

“Sikuwa tayari kutoa, uwezo huo nilikuwa nao, siku 28 zilikuwa ngumu kwani chakula nilikula kile ambacho walibakiza wao, mwili wangu ulijaa damu, wale Warusi walinitesa sana kwani hata sikio langu (la kushoto, anamuonyesha mwandishi) limebondwabondwa, ni tofauti na hili la kulia hadi nafika Tanzania ni Mungu pekee anajua.”

Dk Shika alisema mateso hayo yalimsababishia maumivu makali ikiwamo kuvunjika mbavu tatu upande wa kulia na mbili kushoto ambazo bado hazijaunga vizuri.

Aliuhusisha mkakati wa kumteka na mmoja wa wafanyakazi katika kampuni yake aliyodai inaitwa Ralcefort ili kujipatia kiasi hicho cha fedha, lakini hawakufanikiwa baada ya kuwazidi ujanja na kutoroka.

Mwananchi lilipotaka kujua alitumia mbinu gani kutoroka ikiwa alikuwa hana nguvu na ndani ya jumba asiloweza kujua mlango ulipo, Dk Shika alidai, “ilikuwa siku moja wale watu walitoka na kumwacha mwenzao, akaanza kunywa pombe aina ya vodka na kujidunga unga, mimi nilipoona hivyo wakati huo nimefungiwa katika pipa la maji nilianza kufikiria mbinu za kumtoka.”

“Nilimhesabia tu muda, kuna muda ulifika nikamwona amelala na kwa kawaida mtu akilala ukimwangalia usoni anaweza kuamka, kwa hiyo mimi nikalibinua lile pipa na nikatoka, kule nje nilipotoka nilikutana na binti ambaye hakunisaidia.”

Dk Shika, ambaye huongea kwa kujiamini alisema baada ya kutoroka alipata msaada kutoka kwa wasamaria wema ambao walimchukua na kumpatia huduma ya kwanza wakati huo mwili wake ukiwa umeloa damu.

Alisema watu waliomsaidia walitaka awapeleke eneo alipotekwa, lakini siku ya kwanza hawakufanikiwa kwa sababu alikuwa hapajui vizuri ila siku ya pili walifanikiwa kupaona.

“Tulipofika mle ndani tulikuta damu imetapakaa chumba chote, kumbe wale watu walimuua yule mwenzao niliyemtoroka baada ya kudhani nilimpa fedha ili aniachie, wakadhani amewasaliti.

Kuhusu familia yake kumtenga kama alivyosema kaka yake anayeitwa Pelanya Lunyalula (84), katika mahojiano na Mwananchi, Dk Shika alisema, “mawasiliano mabaya, kama hatuwasiliani ni ukosefu wa mawasiliano, yawezekana mwenzangu akawa hana simu, sasa tutawasilianaje na sidhani kama nitakwenda (Simiyu) kwani kama wazazi wamekufa hata nikienda haitasaidia. Sasa ninachokiangalia ni kumaliza kwanza hili la kuzipata nyumba zangu.”

“Siku nikipeleka fedha nataka Yono (Kampuni ya Udalali iliyoendesha mnada huo) na TRA (Mamlaka ya Mapato Tanzania) waite waandishi wa habari waone na wautangazie umma,” alisema kwa kujiamini.

Polisi wamwachia kwa dhamana

Awali, kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alilieleza Mwananchi kuwa wamemwachia Dk Shika kwa kujidhamini mwenyewe baada ya kukosa mtu wa kumdhamini ila atakuwa akiripoti kila siku saa tatu asubuhi.

“Uchunguzi wa tuhuma dhidi yake unaendelea, lakini mpaka sasa hakuna mtu aliyefika kutaka kumuwekea dhamana, anaishi kama mtu wa nyikani. Nimeagiza watendaji wangu wamwachie kwa dhamana ajidhamini yeye mwenyewe na awe anakuja kuripoti kila siku,” alisema.

Njiani wakati akielekea kituo cha daladala cha Mnazi Mmoja baada ya kuachiwa na polisi, Dk Shika alikuwa kivutio kwa watu aliokuwa akipishana nao.

Hata allipopanda daladala la kwenda Tabata Mawenzi, kondakta alimkaribisha kwa kumweleza, “karibu mzee Shika”, huku ndani ya gari hilo watu wakipiga naye picha na alipowasili nyumbani kwake aligonga geti na kujitambulisha “choka mbaya bin mlalahoi” jambo lililowafurahisha waliojitokeza kumpokea.

Haruna Niyonzima Afunguka Chanzo cha Kifo cha Ndikumana

$
0
0
Haruna Niyonzima Afunguka Chanzo cha Kifo cha Ndikumana
Mchezaji wa Klabu ya Simba raia wa Rwanda Haruna Niyonzima amefunguka na kusema kuwa kinachodaiwa kupelekea kifo cha Mchezaji mwenzake Hamadi Ndikumama ni maumivu ya kichwa.

Akizungumza na EATV Website, Niyonzima amesema kuwa taarifa za awali azilipotokea kutoka Rwanda, zimesema kwamba Ndikumana alianza kupata maumivu ya kichwa  jioni mara baada ya kumaliza mazoezi kwenye timu yake.
Haruna amesema kwamba "Ndikumana hakuwa mgonjwa bali kwa taarifa nilizopokea ni kwamba alianza kuumwa na kichwa baada ya kumaliza mazoezi jana jioni. Alidhani ni maumivu ya kawaida kwamba na baadae yatakwisha lakini baadae yalimzidia na kuamua kwenda hosipitali na ndipo alipofariki usiku wa kuamkia leo.
Ameongeza "Ninachofahamu mimi Ndikumana alikuwa na maradhi ya moyo lakini nikipata tarifa zaidi kutoka kwa watu walipo nyumbani nitajua zaidi nini chanzo"
Kabla ya kufikwa na umauti Katauti alikuwa kocha msaidizi wa kikosi cha Rayon Sports ya Rwanda, enzi za uhai wake aliwahi kuichezea klabu ya Stand United ya Shinyanga akitokea timu ya Cyprus.
Ndikumana amewahi kuwa Mume wa muigizaji Irene Uwoya ambapo walifunga ndoa mwaka 2009 na kujaaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume (Krish) kabla ya kutengana baadaye.

Mambo Yazidi Kuwa Magumu kwa Mugabe Anajiandaa Kuondoka Madarakani

$
0
0
Mugabe Anajiandaa Kuondoka Madarakani
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani saa chache baada ya jeshi la Zimbabwe kutwaa madaraka, kwa mujibu wa mtandao maarufu wa habari nchini Afrika Kusini.

"Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani," mtandao wa wa News24 uliandika bila ya kutoa taarifa zaidi.

Misukusuko ya kisiasa imekuwa ikiongezeka tangu Mugabe hivi majuzi amfute Emmerson Mnangagwa, mshirika wake wa miaka mingi kama makamu wa Rais.

Jeshi Lakanusha Kufanya Mapinduzi ya Kijeshi Zimbabwe Lasema Mugabe na Famia Yake Wapo Salama

$
0
0
Jeshi Lakanusha Kufanya Mapinduzi ya Kijeshi Zimbabwe Lasema Mugabe na Famia Yake Wapo Salama
Jeshi la Ulinzi la Zimbabwe limetupilia mbali uvumi ulioenea kupitia mitandao ya kijamii juu ya kufanyika mapinduzi nchini na limesisitiza Rais Robert Mugabe na familia yake wako salama.

"Kilichofanywa na vikosi vya ulinzi vya Zimbabwe ni kuleta amani kutokana na kushuka kwa hali ya kisiasa, jamii na uchumi nchini,” amesema msemaji wa jeshi katika matangazo ya moja kwa moja kupitia shirika la utangazaji la ZBC alfajiri leo.

"Kwa watu wote na ulimwengu nje ya mipaka yetu, tunapenda kuwafahamisha kwa uwazi kabisa kwamba serikali haijapinduliwa,” ameongeza.

Zimbabwe imekuwa katika hali ya sintofahamu baada ya jeshi kudaiwa kuteka majengo kadhaa ya serikali yakiwemo ya shirika la utangazaji la ZBC.

Mashuhuda walisikia milio ya milipuko maeneo mbalimbali ya jiji la Harare alfajiri hali iliyozidisha hofu katikati ya ripoti za kuwepo kutoelewana kati ya serikali ya Rais Robert Mugabe na vikosi vya ulinzi.

Vyombo vya habari vya hapa nchini vimeripoti kwamba jeshi limeteka majengo ya makao makuu ya ZBC.

Hata hivyo, msemaji wa jeshi amesema Rais Mugabe na familia yake “wako salama na wana afya njema na ulinzi wao ni wa uhakika.”

Shuhuda mmoja aliliambia shirika la habari la AFP kwamba alisikia milio ya bunduki karibu na makazi binafsi ya Rais Mugabe alfajiri ya Jumatano.

"Kutoka kwenye uelekeo wa nyumba yake tumesikia milio ya bunduki 30 au 40 katika muda wa dakika tatu au nne majira ya saa 8:00 usiku,” mkazi mmoja wa jirani alinukuriwa akisema.

Pamoja na maelezo hayo, Jumanne watu walishuhudia magari ya kijeshi vikiwemo vifaru nje ya jiji la Harare, siku moja baada ya mkuu wa majeshi Jenerali Constantino Chiwenga kutishia kuingilia kati kukomesha ufukuzwaji kwenye chama cha Zanu PF na serikalini washirika wa Rais Mugabe.

Balozi wa Zimbabwe nchini Afrika Kusini, Isaac Moyo, amepuuza uvumi wa mapinduzi dhidi ya utawala wa miaka 37 wa Rais Mugabe.

"Hakuna kitu kama hicho. Hayo ni madai ya kwenye mitandao ya kijamii,” Moyo aliliambia shirika la Reuters.

Wabunge, Viongozi Chadema Wafunguka Baada ya Lawrence Mahsa Kujivua Uanachama

$
0
0
Wabunge, Viongozi Chadema Yafunguka Baada ya Lawrence Mahsa Kujivua Uanachama
Baadhi ya wabunge na viongozi wa CHADEMA wametoa maoni yao baada ya mwanachama wao Lawrence Mahsa kujivua uanachama na kujibu tuhuma alizozitoa zikiwa kama sababu za kujivua kwake.

Kwenye kurasa zao mbali mbali za mitandao ya kijamii Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema, ameandika ujumbe akisema safari ya kupigania usawa na haki ni safari ndefu, kwa yeye mwanaume kushindwa kuhimili safari hiyo ni aibu kwani kuna wananwake ambao bado wanaendelea kuhimili ugumu wa safari.
“Lawrence Masha , struggle ya kupigania usawa,haki na demokrasia, ni safari ndefu na ngumu ,wavulana wengi wameendelea kushindwa vile vile wanaume na wanawake imara wanaendelea na safari,sio uamuzi mbaya uliochukua ila ni uamuzi wa aibu . Utajua baadaye na sio sasa”, ameandika Godbless Lema.
Naye Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari ameandika ujumbe wake akisema wanajua sababu za Masha kuondoka CHADEMA na sio zile ambazo amezitaja, na hata hivyo wanaheshimu mamuzi yake.
“Tunaojua sababu za Masha kutoka CHADEMA zile kwenye barua yake tunajua ni danganya toto, tunajua sababu na tunaziheshimu. Kuthibitisha kuwa CHADEMA imejipanga kuingia ikulu, angalia takwimu za ushindi wa madiwani na wabunge nchini kuanzia 1995 hadi sasa. Ikulu ni suala la muda, tena si mrefu”, ameandika Joshua Nasari.
Pia Katibu Mkuu wa chama hiko Vicent Mashinji aesema Masha kuondoka CHADEMA ni haki yake kisheria, lakini ni vyema akaweka wazi ukweli wa sababu za yeye kuondoka.
“Mheshimiwa Masha ana haki kisheria, namtakia heri, lakini lazima auambie umma nini hasa kilichotokea”, ameandika Mashinji.
Lawrence Masha hapo jana ametangaza kujivua uanachama wa CHADEMA akisema chama hiko hakina malengo ya kushika dola, kama ambavyo malengo ya vyama vya upinzani huwa.


Mahakama Yamuhukumu Mwaka Mmoja na Nusu Jela au Faini ya Milioni Tano Bob Wangwe

$
0
0

Mahakama Yamuhukumu Mwaka Mmoja na Nusu Jela au Faini ya Milioni Tano Bob Wangwe
Mtoto wa marehemu Chacha Wangwe, Bob Wangwe ahukumiwa kifungo cha mwaka 1 na nusu jela au faini ya Sh. Milioni 5 kwa makosa ya mtandao.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu Bob kifungo cha mwaka mmoja na nusu jela au kulipa faini ya Shilingi Milioni 5 baada ya kupatikana na hatia kwenye kosa la kuchapisha taarifa za uongo kwenye mtandao wa FACEBOOK.

Hukumu hiyo imesomwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambapo amesema katika kesi hiyo upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi 6 na vielelezo 5 dhidi ya Bob ambae pia ni Mwanaharakati.

Alisema kuwa Mei 7, 2016 polisi walipata taarifa ya chapisho la Bob ambapo walianza kumfatilia na kumkamata kisha walichukua simu na kuipeleka maabara ya Polisi ili kuikagua.

“Kimsingi Bob hukupinga kuandika maneno hayo lakini umedai kuwa hukuyachapisha katika jamii bali yalikuwa ni siri kwenye akaunti yako“.

Hakimu Shaidi alisema kuwa wakati wa ushahidi simu yake ilipokaguliwa ilionekana ilitumika kuchapisha ujumbe huo kwa jamii na watu walimjibu, ikiashiria ujumbe uliwafikia.

“Hivyo ni dhahiri ulikuwa na nia ya kuchapisha taarifa hiyo, kueleza kile ambacho ulikiona sahihi kama ingekuwa ni ujumbe wako binafsi basi Polisi wasingeweza kukutafuta na watu wasingekujibu“

Hakimu Shahidi amesema kutokana na hatua hiyo Bob amekutwa na hatia chini ya kifungu cha 16 cha sheria ya makosa ya mitandao ya mwaka 2015 ambapo katika utetezi wake, Bob aliomba apunguziwe adhabu kwa sababu ni Mwanafunzi wa masomo ya Sheria na pia ni kijana mdogo na ni kosa lake la kwanza kulitenda.



Hakimu Shaidi alisema anakubaliana na hoja za Bob kwani Mahakama inamuona bado ni mdogo na anapaswa kufanya mambo mengi mazuri katika jamii ambapo pia amesema kama yeye ni mwanafunzi wa masomo ya sheria anapaswa kufanya mambo mema katika jamii vitu ambavyo wengine watamuiga.

“Hivyo Mahakama inakuhukumu kulipa faini ya Sh.milioni 5 ama uende jela mwaka mmoja na nusu na pia milango ya dhamana ipo wazi“

Katika kesi hiyo namba 167, Chacha Wange anatuhumiwa kwa kosa la kuchapisha taarifa za kupotosha katika ukurasa wake wa mtandao wa FACEBOOK March 15,2016 ambapo aliandika maneno yafuatayo hapa chini.

“….Tanzania ni ambayo inajaza chuki wananchi.… matokeo ya kubaka Demokrasia Zanzibar ni hatari zaidi ya Muungano wenyewe…. Haiwezekani nchi ya Zanzibar kuwa koloni la Tanzania Bara kwasababu za kijinga.”

Serikali:Tozo Iliyowekwa Katika Daraja la Kigamboni Imefuata Utaratibu wa Kisheria Hivyo Itaendelea Kuwepo

$
0
0
Serikali:Tozo Iliyowekwa Katika Daraja la Kigamboni Imefuata Utaratibu wa Kisheria Hivyo Itaendelea Kuwepo
Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na wenye ulemavu imesema kuwa tozo iliyowekwa katika daraja la kigamboni imefuata utaratibu wa kisheria, kanuni na hivyo itaendelea kuwepo .

Akizungumza leo bungeni mjini Dodoma, Waziri wa Wizara hiyo Jenista Muhagama, baada ya mbunge Zainabu Ndolwa kuhoji,

Je ni lini serikali itasitisha tozo za daraja la Kigamboni ili liweze kutumika kama madaraja mengine Ruvu na Wami?

“Daraja la kigamboni limejengwa na mfuko wa jamii wa NSSF ni kivuko ambacho kinachofanya kazi kama vivuko vingine tulivyo navyo nchini na vivuko vingine pia vimeweka mfumo wa utozaji wa Tozo kidogo ili kuhakikisha kwamba vivuko vile vinaendela kulindwa na kukarabatiwa ili kuendelea kufanya kazi kwahiyo nisema kwamba Tozo iliyowekwa katika Daraja la Kigamboni imefuata utaratibu wa Kisheria na Kikanuni na hivyo itaendelea kuwepo,” amesema Jenista.

Lulu Akubali Kufungwa Miaka Miwili Jela Aikatalia Familia Yake Kukata Rufaa

$
0
0
Lulu Akubali Kufungwa Miaka Miwili Jela Aikatalia Familia Yake Kukata Rufaa
Imeelezwa kuwa baada ya msanii  Elizabeth Michael kusomewa hukumu ya kifungo cha miaka miwili jela, aliwaambia ndugu zake wasikate rufaa kwa kuwa kilichotokea ni mipango ya Mungu na yupo tayari kukabiliana nayo.

Msanii , Muhsin Awadh maarufu Dk Cheni ambaye amekuwa karibu na mwigizaji huyo katika kipindi chote amesimulia hali ilivyokuwa  muda mfupi  baada ya jaji kutoa hukumu hiyo.

“Kusema ukweli Lulu alijua lolote linaweza kutokea ila la kufungwa ni kama hakulipa kipaumbele sana, jaji alipomaliza kusoma hukumu alishtuka kama sisi wengine wote lakini ajabu alikuwa wa kwanza kurudi katika hali ya kawaida na kutoa kauli za ujasiri,” anasimulia Dk Cheni

 Lulu alisema: "Sipingani na maamuzi ya Mungu, haya ni maamuzi yake na nimekubaliana nayo. Ana makusudi yake kunipa hiki kilichotokea leo".

Anasema kingine alichowaambia ni kuachana na masuala ya kukata rufaa kwa sababu bado hatakuwa huru: "Acheni miaka miwili siyo mingi, sitaki kupingana na mahakama , naheshimu maamuzi ya mahakama, acheni nitumikie kifungo changu. "

Mapema wiki hii mwigizaji huyo alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia mwigizaji mwenzake Steven Kanumba, Aprili 7,2012.

Video: Dkt Shika Alivyowasili Nyumbani Kwake Baada ya Kuachiwa kwa Dhamana Polisi

$
0
0
Video hii imekuwa gumzo mitandaoni ya bilionea Dkt. Shika aliyepata umaarufu mkubwa baada ya mnada wa kununa nyumba za Lugumi.

Hivi ndivyo alivyorudi nyumbani kwake baada ya kutimiza masharti ya kujidhamini polisi na kuachiwa na kufafanua kilichomsibu hadi kukamatwa na polisi.

Aliyekuwa Makamo wa Rais Emmerson Mnangagwa Atangazwa Kuwa Rais wa Mpito Zimbabwe

$
0
0
Aliyekuwa Makamo wa Rais Emmerson Mnangagwa Atangazwa Kuwa Rais wa Mpito Zimbabwe
Aliyekuwa Makamo la Urais Zimbabwe Emerson Mnangagwa atangazwa kuwa Rais mpya wa chamacha ZANU-FP.

Mapema leo ametua uwanja wa ndege wa jeshi wa ManyameAkaunti ya chama cha Zanu PF inasemama kuwa Emmerson Mnangagwa amefanywa kuwa rais wa mpito.

Mnangawa mwenye umri wa miaka 75 alifutwa kama makamuu wa rais kutokana na kile serikali ilisema kuwa kutokuwa mtiifu.

Kufutwa kwake kulionekana kama nia ya kumwezesha mke wa Rais Mugabe, Grace, kufuata nyayo za mumewe na kuwa kiongozi wa Zimbabwe.

Awali alikuwa ametoa wito kwa mumewe kumfuta makamu wa rais.

Bw. Mnangagwa ambaye ni mku wa zamani wa ujasusi amekuwa mtu ambaye alitarajiwa kumrithi Rais Mugabe 93.

Kufutwa kwake kulimaanisha kuwa Grace Mugabe anatarajiwa kuteuliwa kuwa makamu wa rais wakati wa mkutano maalum wa chama tawala cha Zanu-PF mwezi ujao.. 

Wakati huo huo jeshi linamshikilia waziri wa fedha Ignatius Chombo, Waziri wa Elimu Prof. Jonahan Moyo Afisa Mwandamizi ndani ya chama cha ZANU-PF Savior Kasukuwere

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

JE Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo ya Kiume?

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?
Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

WASILIANA OSTADHI JUMA KWA SIMU NO,0784002216 AU 0769597778

CCM Wampuuza Lowassa.....Wawataka Wananchi Wasidanganyike na Ahadi

$
0
0
Wakazi wa Kata ya Moita wameombwa kumchagua mgombea wa CCM ili wapate maendeleo na kuachana na ahadi alizowapa, Waziri Mkuu mstaafu na mjumbe wa kamati kuu, Chadema, Edward Lowassa.

Lowassa aliyewahi kuwa mbunge wa Monduli ndiye aliyezindua kampeni za udiwani za Chadema katika kata hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita na kuwaahidi wananchi kuwa hatawasahau na ataendelea kushirikiana nao, kwani aliwaacha wakiwa tayari wana umeme, maji na shule mbili za kata.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Arusha, Shaban Mdoe akizungumza katika kampeni eneo la Moita Bwawani, alisema wananchi wasidanganyike.

Mdoe alisema kwamba wakimchagua mgombea wa CCM, Prosper Meyani kero zao zitapatiwa ufumbuzi, ikiwamo kero ya maji na barabara.

“Msidanganywe na Chadema, hawawezi kutatua kero zenu, alikuwepo diwani wao, hadi amejiuzulu, mbunge wa zamani Lowassa hivi sasa hawezi tena kuwasaidia,” alisema.

Awali, aliyekuwa diwani wa kata hiyo na kujiuzulu, Edward Sapunyo alisema aliamua kujiuzulu baada ya kunyimwa ushirikiano na madiwani wa Chadema.

Alisema kila mradi ambao alikuwa anaomba katika kata hiyo alinyimwa na hivyo akaona hana sababu ya kubaki bali arejee CCM.

Kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, Sapunyo ambaye alikuwa mwenyekiti wa halmashauri ya Monduli kupitia CCM, alisema chaguo sahihi katika kata hiyo ni mgombea wa CCM.

Halmashauri ya Monduli hadi sasa inaongozwa na Chadema kutokana na kuwa na madiwani 18 na CCM madiwani tisa.

Sina Uwezo wa Kulipa Milioni 250 Kilichobaki ni Kujiandaa Kisaikolojia Kufungwa Jela- Babu Tale

$
0
0
Mimi Sina Uwezo wa Kulipa Milioni 250 Kilichopaki ni Kujiandaa Kisaikolojia Kufungwa Jela- Babu Tale
Wakati siku 14 zilizotolewa na kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart & Co Ltd, kwa wakurugenzi wa kampuni ya Tip Top Connection Limited kutekeleza amri ya Mahakama zikikaribia kuisha, Hamis Taletale (Babu Tale), amejitetea huku akidai kuwa anajiandaa kisaikolojia kwa kifungo.

Babu Tale ambaye pia ni meneja wa msanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya, Diamond Platnum, pamoja na nduguye Iddy Taletale ni wakurugenzi na pia wanahisa wa kampuni hiyo.

Februari 18, 2016, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam iliiamuru kampuni hiyo kumlipa fidia ya Sh250 milioni Mhadhiri wa Dini ya Kiislam Sheikh Hashim Mbonde, kwa kutumia kibiashara mahubiri yake bila ridhaa wala makubaliano.

Babu Tale amekiri kupokea taarifa hiyo ya Yono, lakini akasema kuwa yeye hajui chochote kuhusu madai hayo, kwani hakuwahi kujihusisha  na kampuni hiyo na kwamba hana cha kufanya bali anawasubiri kuona Yono hizo siku walizopewa ili waone hatua zitakazofuata.

“Lakini mimi nasema sijamdhulumu huyo mzee wala sijawahi kufanya naye biashara. Kwa kuwa hiyo ni amri ya Mahakama sawa sina cha kufanya, kama watasema tulipe nitaeleza uwezo wangu maana mimi sina uwezo huo wa kulipa hizo Sh250 milioni,” amesema na kuongeza:

“Kwa hiyo cha kufanya ni kujiandaa tu kisaikolojai hata kama ni kufungwa, kwani hata kina Mandela (Nelson) walifungwa jela hivyo hivyo.”

Amesema kuwa kampuni hiyo ilifunguliwa na ilikuwa ikimilikiwa na kaka yao Abdul Taletale (marehemu kwa sasa) kwa asilimia miamoja na kwamba baada ya kufariki kampuni hiyo haikuendelea na mali zake zote zilipotea kwani zilidhulumiwa.

Amesema kuwa japo anatajwa kama mhusika lakini hakuwahi kuwa mkurugenzi, mwanahisa wala kujihusisha kwa namna yoyote na kampuni hiyo na kwamba  hakuona taabu kwani hakujua kama kuna siku yatatokea matatizo kama haya.

Ameongeza kuwa alifahamu kuwepo kwa kesi hiyo baada ya kaka yao kufariki, ambapo wakili wa mdai alimpigia simu akimtaka afike mahakamani, lakini yeye alipuuza kwa kuwa alijua si mhusika.

Kwa mujibu wa hukumu ya kesi ya msingi ya madai namba 185 ya mwaka 2013, Juni 6, 2013 Sheik Mbonde aliingia makubaliano na kampuni hiyo, kutumia kazi zake za mawaidha, kwa kuzalisha, kurekodi na kuzisambaza na kugawana faida ya mauzo.

Hata hivyo, baada ya kukamilisha kurekodi masomo saba, kampuni hiyo ilimkatia mawasiliano hadi alipobahatika kukutana na ofisa mmoja wa kampuni hiyo,  Adam Waziri ambaye alimweleza kuwa wamesitisha mpango huo.

Lakini Agosti 9, 2013, wakati mdai akiendesha mhadhara Bahi Dodoma, alibaini kuwa DVD za masomo yake zilikuwa zikiuzwa sokoni Dodoma na katika  mikoa mbalimbali, bila ridhaa yake wala makubalino ndipo akafungua kesi hiyo.
Chanzo:Mwananchi

Jeshi Lamkamata Mugabe na Kumuweka Kizuizini

$
0
0
Jeshi Lamkamata Mugabe na Kumuweka Kizuizini
Rais Robert Mugabe aliyetawala Zimbabwe kwa miaka 37 amekamatwa na jeshi na kuwekwa kizuizini, chama tawala cha Zanu-PF kimesema.

Taarifa zinasema mawaziri kadhaa ambao wamekuwa wakitajwa kuwa ni “wahuni” na “wahalifu” wamekamatwa katika kile jeshi limeita ni “mapito yasiyo ya umwagaji damu.”

“Hakuna mapinduzi, ila kuna mapito yasiyo ya umwagaji damu ambapo baadhi ya mafisadi na wahuni wamekamatwa na mzee ambaye alitumika na mkewe kujinufaisha ametiwa ndani,” Zanu PF wamesema kupitia ujumbe wa Twitter.

“Milio kadhaa ambayo tuliisikia ilikuwa kutoka kwa wahuni ambao walikuwa wanagoma kukamatwa, lakini sasa wamewekwa ndani.”

Akaunti hiyo haikuwa imethibitishwa lakini si jambo la kawaida kwa ujumbe halali wa Twitter wenye uhusiano na serikali ya Zimbabwe na chama tawala kutothibitishwa na mitandao ya kijamii.

Hata hivyo, maswali mengi yameibuka juu ya nani anayesimamia akaunti zenye uhusiano na chama tawala na kambi hasimu.

Chama tawala kimeonekana kutetea hatua ya Mugabe kuwekwa kizuizini kikisema ilikuwa lazima “kwa msingi wa Katiba na usafi wa taifa ".

Mugabe amewekwa kizuizini muda mfupi baada ya makamu wa rais aliyefutwa kazi wiki iliyopita Emmerson Mnangagwa kurejea nchini kutoka uhamishoni. Mnangagwa, ambaye alikimbilia Afrika Kusini amerejea asubuhi na kutua kwenye kambi ya Jeshi la Anga ya Manyame, limeandika gazeti la The Guardian.

Kuna fununua kwamba jeshi linaweza kumsimika jenerali huyo wa zamani kuwa mkuu wa serikali huku Mugabe akibaki mtu mwenye cheo asiye na mamlaka.

“Si Wazimbabwe wala Zanu-PF wanaomilikiwa na Mugabe na mkewe. Leo inaanza zama mpya na komredi Mnangagwa atatusaidia kuipa maendeleo Zimbabwe,” ulisema ujumbe mwingine wa Twitter.

Zuma: Nimewasiliana na Mugabe na Yuko Salama

$
0
0
Zuma: Nimewasiliana na Mugabe na Yuko Salama
Rais Robert Mugabe "yuko salama", rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesema.

Bw Zuma amesema amezungumza na kiongozi huyo wa miaka 93 kwa njia ya simu.

Amesema Mugabe amemjulisha kwamba yupo nyumbani kwake ambapo amezuiwa kuondoka, kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka kwa afisi ya rais wa Afrika Kusini.

Zuma amesema kwamba amewasiliana pia na Majeshi ya Ulinzi ya Zimbabwe (ZDF), taarifa hiyo imesema.

Afrika Kusini inapanga kuwasiliana na pande zote mbili.

Bw Zuma amekariri wito wake wa awali kwamba kuwe na "utulivu"

Dkt Shika Atii Amri ya Polisi Aripoti Kama Kama Alivyotakiwa

$
0
0
Dkt Shika Atii Amri ya Polisi Aripoti Kama Kama Alivyotakiwa
'Bilionea' Dk Louis Shika aliyeibuka mshindi wa kununua nyumba za mfanyabiashara Said Lugumi leo Novemba 15  ameripoti kituo kikuu cha Polisi Dar es Salaam kama alivyotakiwa.

Dk Shika ameripoti kama alivyotakiwa jana na Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa mara baada ya kuachiwa kwa kujidhamini yeye mwenyewe.

Kabla ya kwenda kuripoti, Dk Shika ambaye amekuwa maarufu kila anapopita, alipata kifungua kinywa maeneo ya Posta.

Saa 2.24 asubuhi, Dk Shika alikuwa amewasili kituoni hapo na ilipofika Saa 3.36 asubuhi aliondoka na kesho atarejea tena kituoni hapo.

Akizungumza na Mwananchi lililokuwapo tangu anaingia hadi anatoka amesema hana tatizo na ataendelea kuitikia wito wa polisi bila tatizo.

Mke wa Rais wa Zimbabwe Grace Mugabe Adaiwa Kutorokea Namibia

$
0
0
Mke wa Rais wa Zimbabwe Grace Mugabe Adaiwa Kutoroka Nchini
Mbunge wa upinzani nchini Zimbabwe Eddie Cross ameambia BBC kwamba anaamini mke wa Rais Mugabe, Grace, ametorokea Namibia.

Mwanasiasa huyo wa chama cha Movement for Democratic Change (MDC) amesema anafahamu kwamba Grace aliruhusiwa kuondoka nchini humo usiku wa kuamkia leo na jeshi.

Ameongeza kwamba alikuwa hana kwingi kwa kwenda kutafuta hifadhi baada yake kudaiwa kumdhalilisha mwanamitindo Afrika Kusini jambo lililomaanisha kwamba hawezi kuwa salama huko.

Hata hivyo, taarifa hizi hazijathibitishwa na jeshi.

Nick Mangwana, mwakilishi wa chama tawala cha Zanu-PF nchini Uingereza ameambia BBC kwamba mwenyewe pia amepokea taarifa kwamba Grace hayupo tena nchini Zimbabwe.

Lakini Bw Mangwana amesema katika siasa za Zanu-PF, Bi Mugabe ni mtu wa chini sana na hana usemi wowote.

Amesema ana mamlaka tu kwa sababu ya kuwa ni mke wa Rais Mugabe.

„Alichukua wadhifa wa juu kuliko ule anaostahiki kuwa nao,” amesema.

Napokea Idadi Isiyo ya Kawaida ya Vitisho Tangu Kutoka CCM Tafadhali Niombeeni Pamoja na Familia Yangu- Nyalandu

$
0
0
Napokea Idadi Isiyo ya Kawaida ya Vitisho Tangu Kutoka CCM Tafadhali Niombeeni Pamoja na Familia Yangu- Nyalandu
Aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini. Mh. Lazaro Nyalandu ameomba kuombewa yeye pamoja na familia yake kwa kudai kwamba  amekuwa akipokea vitisho visivyo na idadi baada ya kuondoka ndani ya Chama Cha Mapinduzi.

Usiku wa kuamkia leo Nyalandu ametumia ukurasa wake wa twittter ambao ameonyesha hofu yake na kudai kwamba njia zote zinatumika kuhakikisha ananyamazishwa.
"Napokea  idadi isiyo ya kawaida ya vitisho tangu kuondoka CCM chama cha tawala. Ni ajabu kuwa kuna hofu kubwa kutoka kwa wasomi, ambao wanatumia njia zote zinazowezekana kuninyamazisha" Nyalandu
Ameongeza "Tafadhali niombeeni mimi pamoja na familia yangu wakati wa majaribu haya tunayopitia".
Kabla ya kuhamia Chadema mapema mwanzoni mwa mwaka huu, Nyalandu alikuwa Mbunge wa Singida Kaskazini na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images