Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live

JE Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo ya Kiume?

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?
Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

WASILIANA OSTADHI JUMA KWA SIMU NO,0784002216 AU 0769597778

Imebainika...Polisi, Mahakama vinara wa Rushwa Tanzania

$
0
0
Utafiti wa shirika lisilo la kiserikali la Twaweza umebaini kuwa Idara za Polisi na Mahakama bado zinaongoza kwa rushwa, licha ya kuwa ni taasisi zinazohudumia idadi kubwa ya watu.

Hayo yamebainishwa kwenye uzinduzi wa ripoti ya utafiti huo iliyopewa jina "Hawashikiki" uliofanyika leo jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau kutoka sekta za umma na kibinafsi.
Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti huo, wananchi wanaripoti kuwa licha ya viwango vya rushwa kupungua nchini kwa mwaka huu, bado idara za polisi na mahakama zimeendelea kuwa na kiwango kikubwa cha rushwa ambapo kati ya 36% na 39% ya wananchi waliohojiwa, wameiambia Twaweza kuwa waliombwa rushwa mara ya mwisho walipofika katika taasisi hizo.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Utetezi wa Twaweza Bi. , Anastazia Lugaba, amesema kuwa wananchi walitoa rushwa ili kupata huduma ya uhakika katika sekta hizo lakini kwa sauti za wananchi zinazoonesha matumaini katika mapambano dhidi ya rushwa.

Ndani ya utafiti huo pia wananchi wamezungumzia sakata maarufu la kampuni ya madini ya Acacia wakiliweka katika kundi la rushwa kutumika kwa kiasi kikubwa, huku Mamlaka ya Mapato ya Tanzania pamoja na Mamlaka ya Bandari nazo zinaonekana kushughulikiwa ipasavyo na Taasisi ya Kuuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru huku wakitaja vyama vya upinzani vingelifanya vizuri zaidi katika kupambana na rushwa endapo vingepata nafasi ya kuwa madarakani .

Chadema, CCM Waanza Vita Mapema...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Novemba 23

$
0
0


Chadema, CCM Waanza Vita Mapema...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Novemba 23

Godbless Lema Ampiga Dongo David Kafulila...ni Kuhusu Mkewe Ambaye Bado yupo Chadema

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini kupitia CHADEMA Godbless Lema, amefunguka kuhusu kitendo cha David Kafulila kuhama CHADEMA na kusema ana amini atamshauri mke wake naye afuate nyayo zake.

Kwenye ukurasa wake wa twiter Godbless Lema ameandika ujumbe akisema Kafulila ni rafiki yake wa karibu, lakini kwa namna alivyoamua hana shaka atamshauri mke wake ambaye ni mbunge kupitia chama cha CHADEMA, kufanya kama yale aliyoyafanya.
"David Kafulila ni rafiki yangu, nafikiri kwa namna hii alivyoamua ataweza bila shaka kumshauri Mbunge wa Chadema, Jesca Kishoa (mke wake) kufikiri kama yeye, hii inaweza kusaidia maoni yake juu ya uamuzi aliouchukua leo na kuthibitisha ukweli huu kama hupo", ameandika Godbless Lema.
Hii leo David Kafulila ametangaza kukihama chama cha CHADEMA akidai vyama vya upinzani havina nia ya kupambana dhidi ua ufisadi, lakini mke wake Jesca Kishoa ambaye ni mbunge wa viti maalum kupitia CHADEMA bado hajazungumza chochote.

Video MPYA: Roma na Stamina Ft. Maua Sama na Dr. Shika Kafunga Kazi Mwishoni

$
0
0
Ni zamu ya ROSTAM (Roma na Stamina) kwenye nyingine tena ambayo time hii wamemshirikisha Mwimbaji Staa Maua Sama, itazame mwenyewe hapa chini

 VIDEO:

Ukomo wa Mifuko Mitano Tanzania Bara ni Machi, 2018; PSPF na NSSF pekee kubaki

$
0
0
Ukomo wa Mifuko Mitano ni Machi, 2018 na Mifuko miwili kuimarishwa au kudumishwa na ambapo idadi ya wanachama, madeni, makesi au madudu yeyote kutoka mifuko mitatu hiyo kukabidhiwa kuridhiwa na mifuko miwili yaani PSPF na NSSF. Kwani Tarehe 6 Novemba 2017 mifuko hiyo mitatu imepewa amri ya kupeleka idadi ya wanachama, mali zote, madeni na makesi zote kwa utayari wa umiliki.

Sasa utitili wa mifuko Tanzania Bara sasa unafikia kikomo ambapo SSRA atapumua na kufanya kazi kwa ufanisi Zaidi kuanzia Mwezi wa Machi 2018 kutoka mitano (PSPF, NSSF, PPF, LAPF na GEPF) kufikia miwili kwani awamu ya Tano imefanya maamuzi magumu na yenye busara kabisa.

Awamu ya Nne ya Jakaya ilikuwa na huo mpango wa kuunganisha mifuko lakini zoezi lilikuwa linasusua kwa safari zake Mzee wa Kaya kwenda Ulaya kila kukicha.

Kuna sekta mbili ambapo mifuko miwili itaimalishwa na mitatu kumezwa. Mfuko wa PSPF utachukua wanachama wote wa public sector kutoka mifuko ya PPF, GEPF na LAPF.

Mfuko wa NSSF utachukua wanachama wote wa private sector kutoka PPF, GEPF na LAPF. Wakati NHIF itaendelea kusajili wanachama kutoka public na private sector pasipo kikwazo cha umri na utaendelea kupata huduma ya kiafya mpaka ukomo wa maisha yako.

Angalia mchakato wa Chati.

Waziri Kalemani apiga marufuku TANESCO na REA kuagiza transfoma kutoka nje

$
0
0
Waziri wa Nishati Dk Medard kalemani amepiga marufuku shirika la umeme TANESCO na wakala wa umeme vijijini REA kuacha kuagiza transfoma nguzo na vifaa vingine kutoka nje ya nchi ili kudhibiti uingizwaji holela wa vifaa visivyo na ubora ambavyo vinaathiri uchumi na kukandamiza viwanda vya ndani.

Waziri Kalemani ametoa taarifa hiyo alipotembelea kiwanda cha kutengeneza trasfoma tanalec kilichopo jijini Arusha amesema serikali imepata hasara kubwa kwa uingizwaji wa transfoma kutoka nje ambapo hivi karibuni ziliingizwa zaidi ya trasfoma ishirini zilizogundulika kuwa chini ya kiwango.

Mkurugenzi wa ufundi na huduma wakala wa umeme vijijini REA Bengiel Msofe amesema wamepokea agizo la serikali na wataanza kununua vifaa vya ndani kama walivyo agizwa na waziri mwenye dhamana.

Mkurugenzi wa TANALEC Zahri Salehe anasema wamejipanga kuzalisha transfoma elfu kumi ili kumudu soko la ndani na mkuu wa mkoa wa arusha mrisho gambo anasema kama serikali ya mkoa watahakikisha wanasimamia utekelezezaji wa agizo hilo.

Chanzo: ITV

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Alhamisi

$
0
0

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
MIUJIZA YA SHARIFU SEIF MOHAMED KUTOKA BAGAMOYO.

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,
(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Omog Aanika Wachezaji Watakaotemwa

$
0
0
Omog Aanika Wachezaji Watakaotemwa
KUSHUKA kiwango na kuwa majeruhi wa muda mrefu ni moja ya sababu ambazo Kocha wa Simba, Joseph Omog, amesema zitachangia kufanya uamuzi wa "kutema" baadhi ya wachezaji wake katika kipindi cha dirisha dogo la usajili wa wachezaji linaloendelea nchini.

Baadhi ya nyota wanaoonekana kukalia kuti kavu kwa kuzingatia sababu zilizotolewa na Omog ni pamoja na majeruhi Saidi Mohammed (kipa), Shomari Kapombe (beki) na straika Nicholas Gyan ambaye ameshindwa kuonyesha makali yake kama alivyokuwa kwao Ghana.

Omog aliliambia gazeti hili kuwa anatarajia kukutana na viongozi wa Simba mwishoni mwa wiki ili kuwasilisha mapendekezo yake ambayo yanalenga kuimarisha kikosi chake.

"Tutakuwa na kikao na viongozi wikendi hii, sisemi ni idara gani ninataka kuiimarisha, lakini kwanza nitaanza na wachezaji ambao hawajaonyesha viwango vizuri na wale majeruhi wa muda mrefu," alisema Omog.

Alisema kuwa mbali na kusaka ubingwa wa Ligi Kuu Bara, Simba inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubahatisha ya Matokeo Michezoni ya SportPesa, inatakiwa pia ifanye vizuri katika mashindano ya Kombe la FA na michuano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho Afrika watakayoshiriki kuanzia mapema Februari mwakani.

"Tunatakiwa tuwe imara kila idara, tunaelekea kwenye hatua ngumu zaidi, tunahitaji kuwa na wachezaji ambao wanauwezo na uzoefu wa kuisaidia timu," Omog aliongeza.

Dirisha dogo la usajili lililofunguliwa tangu Novemba 15 na litafungwa ifikapo Desemba 15, mwaka huu, siku chache kabla ya Yanga na Simba zitakazochuana kwenye mashindano ya CAF kutakiwa kupeleka majina ya nyota wake iliyowasajili.

Simba ambayo msimu huu imefanikiwa kuondoka na pointi sita Mbeya, inaendelea na mazoezi kwa ajili ya kuwakaribisha Lipuli FC katika mechi ya Ligi Kuu itakayopigwa Jumapili kwenye Uwanja wa Azam Complex uliyopo Chamazi jijini Dar es Salaam.


Mama Kanumba Amtetea Hamissa Mobetto " Wote ni Watoto Wangu Hamisa Sio Mnafki"

$
0
0
Mama Kanumba Amtetea Hamissa Mobetto " Wote ni Watoto WanguHamisa Sio  Mnafki"
MAMA wa aliyekuwa nguli wa filamu Bongo marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa amemkingia kifua mwanadada Hamisa Mobeto, baada ya mrembo huyo kuonekana mnafiki kwa kumsikitikia muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ kisha kuonekana akiwa beneti na mama huyo.

Hivi karibuni, Mobeto alionekana kwenye uzinduzi wa filamu ya Zero Player aliyoshirikiana na mdogo wa Kanumba, Seth Bosco akiwa na mama huyo ndipo watu mitandaoni walipoanza kumnanga kwa kumuita msaliti wakidai ni hivi karibuni tu, aliposti picha ya kumsikitikia Lulu aliyehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela ambaye hapatani na mama Kanumba.

Ishu hiyo ilimuibua mama Kanumba ambapo alimtetea Mobeto: “Sioni haja ya watu kumsema vibaya Hamisa, wote ni watoto wangu tatizo liko wapi, wasimuite mnafiki bwana,” alisema mama Kanumba.

Mama wa Marehemu Ndikumana Awataja Waliohusika Kusababisha Kifo cha Mwanaye

$
0
0
Mama wa Marehemu Ndikumana  Awataja Waliohusika Kusababisha Kifo cha Mwanaye
Wakati muigizaji nyota wa filamu nchini, Irene Uwoya akiwa nchini Rwanda kuhani msiba wa aliyekuwa mumewe, Hamad Ndikumana ‘Ndiku’, mama mzazi wa mwanasoka huyo wa zamani wa kimataifa, amewataja watu waliohusika kusababisha kifo cha mwanaye.

TUJIUNGE KWANZA NA UWOYA
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko kutoka Kigali aliko msibani, Uwoya alisema awali alipata taabu ya kufanya mawasiliano na ndugu na jamaa wa mumewe huyo wa zamani na baada ya kuwakosa, akaamua kuwasiliana na Asma, mwanamke ambaye siku chache nyuma, Ndikumana aliposti picha zake katika mtandao wa kijamii, akimnadi kama mpenzi wake.

Mama mzazi wa Ndikumana.

“Nilipompata huyo, nikajitambulisha na kumwambia juu ya nia yangu ya kutaka kuja huku, katika namna ya kufurahisha, akanikubalia na tangu wakati huo ndiye nilikuwa nawasiliana naye na hata nilipofika hapa, yeye ndiye alinipokea na kunipeleka nyumbani kwa wazazi wa Ndikumana,” alisema muigizaji huyo. APELEKWA KWA

WAZAZI, WAMKUBALI
Uwoya ambaye alizaa na marehemu mtoto mmoja wa kiume aitwaye Krish, alisema baada ya kufikishwa nyumbani kwa wazazi wake, alipokelewa vizuri na ndugu na jamaa ambao walimweleza kuwa hawana kinyongo naye kwa sababu mambo yote yaliyotokea huko nyuma ni mapito ya duniani.

Irene Uwoya akiwa na Ndikumana enzi za uhai wake.
“Yaani huwezi kuamini, walinipokea vizuri sana, tofauti kabisa na huko nyumbani jinsi wanavyonizungumzia. Nimekaa nao na wao ndiyo walioniambia kitu ambacho kilinishangaza sana kuhusu chanzo cha kifo cha Ndikumana,” alisema Uwoya.

SIKU YA TATU MAMA MKWE AMDUWAZA

Uwoya alisema ilipofika siku ya tatu ya msiba, ambayo kwa kawaida ndiyo siku ya kuanua matanga, mama huyo alimweleza wazi juu ya watu ambao wanahusika na kifo cha mtoto wao, ambao familia inawatambua na inajua namna ya kushughulika nao.

Ndugu wa Ndikumana akilia kwa uchungu.
“Mama Ndiku alisema anawafahamu waliomuua mtoto wao, alisema ni wachezaji wenzake sijui, wale watu wake wa mpira, wanasema chanzo ni kuwa yeye alikuwa mtu anayependwa na viongozi wa timu, hicho ndicho kilichowafanya wenzake wawe na wivu naye.

“Alinishtua sana, anasema wamegundua kuwa Ndiku aliwekewa sumu na wenzake na suala hilo linashughulikiwa na familia yao, sijajua watachukua hatua gani, lakini hicho ndicho kinachoendelea huku msibani,” alisema.

MANENO HAYO YAMEMFARIJI

Uwoya ambaye baadhi ya wadau wanamtaja kama mtu aliyesababisha msongo wa mawazo kwa mumewe baada ya hivi karibuni msanii Dogo Janja kung’ang’ania amefunga ndoa na muigizaji huyo, alisema kwa maneno hayo, amefarijika, kwani angalau mzigo wa lawama atautua.

Baba mzazi wa Ndikumana
“Maneno yalikuwa ni mengi sana kwa kweli huko nyumbani, kila mtu Uwoya Uwoya, afadhali mama amekata mzizi wa fitina, kifo chake wala siyo msongo wa mawazo, ni mchezo aliochezewa na wenzake huko kwenye mambo yao ya mpira,” alisema.

KWA NINI ALITAJWA UWOYA?

Kifo hicho cha ghafla cha Ndikumana, aliyefariki usiku wa Novemba 14 mwaka huu, kilisababisha baadhi ya watu kumtaja Uwoya kuwa huenda akawa chanzo kutokana na mtiririko wa matukio tangu ndoa ya wawili hao ilipovunjika miaka michache iliyopita.

Kwa muda wote ambao wawili hao walikuwa tofauti, Uwoya amekuwa akidai apewe talaka yake ili awe huru kuolewa na mtu mwingine, kitendo ambacho kinadaiwa kumuumiza mchezaji huyo wa zamani wa Stand United ya Shinyanga.
Chanzo: Global Publishers

Mastaa wa Bongo: Bora Lulu Atumikie Kifungo Cha Miaka Miwili Jera Asikate Rufaa

$
0
0
Mastaa wa Bongo: Bora Lulu Atumikie Kifungo Cha Miaka Miwili Jera Asikate Rufaa
Siku chache baada ya muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ kuhukumiwa kwenda jela miaka miwili, kwa kosa la kumuua bila kukusudia Steven Kanumba, mastaa mbalimbali wameibuka na kumshauri asikate rufaa. Wakizungumza na Risasi Mchanganyiko kwa nyakati tofauti mastaa wa filamu pamoja na wanamuziki wameeleza sababu zao za kwa nini wanafikiri kuwa ni vyema Lulu akatumikia kifungo hicho.

Wengi wao wamesema kwamba miaka miwili sio mingi na kutokana na jinsi alivyokuwa akiishi bila kujua hatma yake, ni vyema akatumikia kifungo hicho ili akimaliza awe huru.


Msanii wa Bongo, Lulu Diva.
LULU DIVA: Nikipata nafasi ya kumshauri ama kuzungumza na Lulu ningemshauri bora atumikie tu kifungo chake ili awe huru, ana kila sababu ya kutumikia adhabu hiyo ili kupoza machungu ya mashabiki wa Kanumba na familia ya msanii huyo ambayo imekuwa na mtazamo tofauti kuhusu yeye.

SNURA Japo upo uwezekano wa kukata rufaa lakini mimi ninachoweza kumshauri kikubwa, anatakiwa kumwachia Mungu, aijuaye kesho yake ni Mungu peke yake.

SANDRA: Asikate rufaa kwa sababu kesi inayohusiana na mauaji ni kesi kubwa, hata kama ataamua kukata rufaa kuna kuwa na mlolongo mrefu, hivyo uwezekano wa kutofanikiwa kwa rufaa yake ni mkubwa. Ni kheri atumikie kifungo ili baadaye awe mtu huru katika maisha yake mapya.

DAVINA: Asikate rufaa kwa sababu kuna watu ambao wanaona alifanya kosa, hivyo ni vema akatumikia hiyo miaka miwili kisha maisha yaendelee kama kawaida na Mungu atamsimamia. Asikate ili mambo yaishe atengeneze tu usawa!


MLELA: Mimi namshauri akabiliane na jaribu ili awe huru. Japokuwa jela sio pazuri lakini midomo ya watu na maneno mabaya yanatesa zaidi. Kila linalomtokea binadamu Mungu ndio hupanga kumpitisha katika jaribu hilo ili ampeleke mahali anapotaka awe.

PRETY CANDY: Ni vyema akatumikia tu kifungo maana kwa kweli mtazamo wa baadhi ya watu katika jambo hilo ni tofauti. Atumikie kifungo, akimaliza sidhani kama kuna mtu atakuwa na kinyongo naye tena.

MARY MAWIGI
Kwa upande wangu mimi namshauri tu amuombe Mungu atamfanyia wepesi maana ni miezi 18 tu atakaa Jela. Asikate tama, Mungu yu pamoja naye. Aidha, baadhi ya mastaa akiwemo Nuh Mziwanda, walionekana kumshauri tofauti Lulu kwa kumwambia akate tu rufaa kama anaona inafaa: “Binafsi naona ni haki yake ya msingi kukata rufaa, kwa kuwa sheria inampa haki hiyo namshauri akate rufaa kuliko kuendelea kuishi jela, ifahamike eneo lile siyo zuri kabisa. “Kama Lulu mwenyewe anaamini rufaa inaweza kumsadia juu ya msala huo ni bora akachukua hatua kuliko kuendelea kuteseka.”

Mwakimu Mkuu Avuliwa Madaraka Kwa Kosa la Kubaka Mwanafunzi

$
0
0
Mwakimu Mkuu Avuliwa Madaraka Kwa Kosa la Kubaka Mwanafunzi
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Abdalah Malela amemvua madaraka Mwalimu Mkuu Masunga Ng’waya wa Shule ya Msingi Mwashagata, iliyopo kijiji hicho kata ya Ihusi kwa kosa la ukosefu wa maadili.



Akizungumza na mwandishi wa gazeti Habarileo, mkurugenzi huyo alisema tukio hilo lilitokea hivi karibuni la baada ya mwalimu mmoja wa shule yake kumrubuni mwanafunzi wake kwa kufanya mapenzi naye tena kwenye nyumba yake, kitendo ambacho ni cha kukosa maadili.

“Imebainika hili ni tukio la nne kwa mwalimu huyo kutuhumiwa kufanya mapenzi na wanafunzi tofauti tofauti lakini amekuwa hachukuliwi hatua, lakini mimi kwa mujibu wa sheria nimemvua madaraka mwalimu mkuu huyo ili awe mwalimu wa kawaida, sababu amekosa maadili ya kuendelea kushika wadhifa huo,” alisema mkurugenzi huyo.

Aidha, alisema kesi hiyo tayari imefikishwa polisi na wakati wowote mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani. Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga alisikitishwa na kitendo hicho na kumtaka mkurugenzi wa halmashauri hiyo kumchukulia hatua na kuwashauri wazazi wamuache mwanafunzi huyo aendelee na masomo yasije yakampita huku hatua za kisheria kwa mtuhumiwa zikiendelea.

Mlezi wa mwanafunzi huyo, alisema mwanae alisimama masomo kwa muda wa wiki mbili kutokana na tukio hilo. Mwalimu Ng’waya alipozungumza na mwandishi wa habari kwa njia ya simu alikiri kuvuliwa madaraka na kueleza amekuwa mwalimu wa kawaida huku akiendelea kufundisha katika shule hiyo

Zimbabwe Kushuhudia Demokrasia Mpya

$
0
0
Zimbabwe Kushuhudia Demokrasia Mpya
Kiongozi mpya wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa amesema nchi yake kwa inashuhudia mwanzo wa demokrasia mpya.
Mnangagwa, ambaye anatarajia kuapishwa kushika wadhfa wa Urais wa nchi hiyo siku ya Ijumaa, amesema kipaumbele chake ni kujenga upya uchumi wa nchi hiyo na kuunda ajira mpya kwa idadi ubwa ya watu wasio na ajira.
Katika hotuba yake hiyo, aliyokolezwa na maneno yaliyokuwa yakitumika wakati wa vita vya uhuru wa nchi hiyo, Bwana Mnangagwa alilishukuru jeshi la nchi hiyo, ambalo liliingilia kati baada ya yeye kufukuzwa na Rais Robert Mugabe na kuweza kufanikisha hali iliyopo sasa kwa amani.
Makamu huyo wa Rais wa zamani anayesubiri kuapishwa kuwa Rais wa nchi hiyo alirejea nchini Zimbabwe mapema jana.
Aidha alifahamisha kuwa aliikimbia nchi hiyo baada ya kutishiwa maisha yake baada ya kufukuzwa katika nafasi yake hiyo

Hudda Amtetea Mtoto wa Mugabe

$
0
0
Hudda Amtetea  Mtoto wa Mugabe
Kuna nini kati ya mtoto wa aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zimbabwe, Chatunga Bellarmine Mugabe na Huddah Monroe.

Mrembo huyo wa Kenya ameandika ujumbe kupitia mtandao wa Snapchat, kumkingia kifua mtoto huyo ambaye anaonekana kuchukiwa na watu wengi kutokana na kauli yake aliyowahi kuitoa hivi karibuni kabla ya Rais Mugabe kutangaza kujiuzulu.

Huu ni ujumbe wa Huddah ambao ameandika kwenye mtandao huo.



Nyumba za Dkt Shika Kuuzwa kwa Mara Nyingine Kesho

$
0
0
 Nyumba za Dkt Shika Kuuzwa kwa Mara Nyingine Kesho
NYUMBA mbili za Lugumi ambazo hazikufanikiwa kuuzwa katika minada iliyopita, zitauzwa kwenye mnada utakaofanyika kesho jijini Dar es Salaam maeneo ya JKT Mbweni na Upanga.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya udalali ya Yono, Scolastica Kevela, alipozungumza na vyombo vya habari ambapo alitoa onyo pia kwamba watu wasiokuwa na nia ya kununuanyumba hizo wasifike sehemu hizo kwani watachukuliwa hatua.

Alirudia kusisitiza kwamba watu watakaofanikiwa kununua nyumba hizo ni lazima watangulize asilimia 25 ya bei husika na iliyobaki ilipwe ndani ya siku 14 la sivyo fedha iliyotangulizwa haitarudishwa.

Johari Afunguka Marehemu Ndikumana " Ndiku Enzi za Uhai Wake Alitupa Bata za Kutosha"

$
0
0
Johari Afunguka Marehemu Ndikumana " Ndiku Enzi za Uhai Wake Alitupa Bata za Kutosha"
BLANDINA Chagula ‘Johari’ amemfungukia aliyekuwa mume wa muigizaji Irene Uwoya, marehemu Hamad Ndikumana kuwa enzi za uhai wake, aliwapa bata za kutosha.

Akizungumza na mwanahabari wetu hivi karibuni, mkongwe huyo wa sinema za Kibongo, alisema Ndiku alipokuwa anakuja nchini akitokea nchini Cyprus alikokuwa akiishi, alikuwa akiwaletea zawadi na kujirusha naye sana.

Irene Uwoya akiwa na aliyekuwa mume wake, Ndikumana enzi za uhai wake.
“Kama unavyojua mimi na Irene ni damudamu, alikuwa anatupa raha hatari. Kuna wakati tulienda naye hadi Cyprus tukala raha sana, kwa kweli Ndiku ana roho ya peke yake, Mungu amlaze mahali pema peponi, amina,” alisema Johari.

Ndikumana ambaye alibahatika kuzaa mtoto mmoja na Uwoya kabla hawajatengana, alipatwa na umauti wiki iliyopita nchini kwao Rwanda kwa maradhi ya moyo.

Wanaoshikilia Bombardier Wafuatwa Huko Huko na Serikali

$
0
0
 Wanaoshikilia Bombardier Wafuatwa Huko Huko na Serikali
Tanzania imeiomba Mahakama ya Jimbo la Columbia kutupilia mbali ombi la Stirling Civil Engineering la kutaka kusajili hukumu mbili za Mahakama ya Kimataifa Usuluhishi ili kampuni hiyo ya Uingereza ikamate mali nyingine za Serikali zilizopo nchini Marekani.

Stirling, ambayo ni kampuni ya ujenzi iliyokatishwa zabuni ya kujenga Barabara ya Bagamoyo kutoka eneo la Wazo Hill kutokana na kutekeleza mradi huo chini ya kiwango, ilishinda ksi iliyofungua kupinga kitendo hicho msuluhishi akaagiza ilipwe dola 38 milioni za Kimarekani.

Kampuni hiyo ilisajili uamuzi huo wa msuluhishi nchini Uingereza na Uholanzi na kufanikiwa kushikilia ndege aina ya Bombardier Q400 iliyonunuliwa na Serikali na sasa inataka mahakama isajili hukumu mbili za mwaka 2015 na 2016 zisajiliwe Marekani ili ipate nguvu ya kushikilia mali nyingine.

Lakini Serikali ya Tanzania imeamua kupambana na kampuni hiyo mahakamani kuizuia isiendelee kukamata mali zake.

Kwa mujibu wa tovuti ya Law360, ambayo ni maalum kwa ajili ya habari za kisheria, Tanzania imewasilisha pingamizi, ikitaka mahakama hiyo isisajili hukumu hiyo ya Mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi.

Katika hoja yake, Tanzania imesema mahakama hiyo haina mamlaka ya kisheria ya kushughulikia ombi hilo la Stirling.

Serikali inasema ina kinga dhidi ya hukumu mbili zilizotolewa na mahakamani nchini Uingereza na Uholanzi ambazo kampuni hiyo inaomba zitambuliwe pia Marekani, ikisema kuwa ondoleo hilo la kinga linalotolewa na Sheria ya Kinga ya Mataifa ya Kigeni, haiwezi kutumika.

Kwa mujibu wa tovuti hiyo, Sheria ya Kinga ya Mataifa ya Kigeni inasema taifa la kigeni halitakuwa na kinga dhidi ya mamlaka ya mahakama ya Marekani katika mashauri yanayowasilishwa kwa ajili ya kuthibitisha tuzo za mahakama ya usuluhishi zinazoongozwa na makubaliano yaliyoidhinishwa na nchi yanayotambuliwa nchini Marekani.

Serikaloi inasema Stirling inataka kutambuliwa kwa hukumu za mahakama ya nje ili ziwe na nguvu, badala ya kuomba kutekelezwa kwa hukumu hizo.

“Kuna tofauti inayotambulika vizuri kati ya kuthibitisha tuzo ya msuluhishi, kwa upande mmoja, na kutambua hukumu ya mahakama ya nje, kwa upande mwingine,” tovuti hiyo inakariri hoja hizo za Serikali.

“ingawa tuzo ya msuluhishi na hukumu ya mahakama zinalingana kwa kiasi kikubwa, hata hivyo zina tofautiana.”

Kwa hiyo, Serikali inasema Stirling haiwezi kutumia mwanya huo, kuomba utekelezaji wa hukumu hizo.

Kampuni hiyo inadai kuwa kitendo cha Serikali ya Tanzania kukubali kwenda kwenye Mahakama ya Usuluhishi, kiliondoa kinga hiyo na kuipa yenyewe haki ya kulipwa fidia hiyo.

Mwaka 1999 Serikali iliipa kandarasi kampuni ya Impresa Ing. Fortunato Federici SpA (IFF) ambayo baadaye ilinunuliwa na Stirling, kukarabati barabara ya Wazo Hill-Bagamoyo, lakini baadaye ikatimuliwa.

Mwaka 2004 kampuni hiyo ilifungua kesi Mahakama ya Usuluhishi wa Kimataifa na hukumu ilitolewa mwaka 2009 na 2010, lakini Serikali haikulipa fidia iliyopendekezwa na kuilazimu kukazia hukumu Uingereza na Uholanzi.

Novemba 2015, mahakama nchini Uingereza iliridhia utekelezaji wa hukumu hiyo na Uholanzi ilifanya hivyo Desemba 2016.

source: Mwananchi

Mashinji Naye Afunguka Kuhusu Kuhamia CCM

$
0
0
Mashinji Naye Afunguka Kuhusu Kuhamia CCM
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  Dkt. Vicent Mashinji amekanusha habari za kwamba anahamia Chama cha Mapinduzi na kusema kwamba yeye siyo mtu wa kuamini kwenye zidumu fikra za Mwenyekiti bali nguvu ya mamlaka ya umma.

Mashinji amesema kwamba yeye siyo mjamaa bali ni mlengo wa kipepari hivyo amewataka wananchi wawe na amani kuhusu hizo taarifa za yeye kuhamia CCM si za ukweli.
"Napokea simu nyingi eti nahamia CCM, mi si Mjamaa. Mi ni mlengo wa kibepari. Siamini kwenye “zidumu fikra za mwenyekiti” Ninaamini katika “nguvu na mamlaka ya umma”. Naomba ndugu zangu muwe na amani kabisa" Mashinji.
Dkt Mashinji ameongza kwamba "Nitaendelea kutumikia CHADEMA kwa makini na kutimiza ndoto za watanzania".
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live




Latest Images