Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Mchezaji Aomba Barua kwa Uongozi wa Timu Kuondoka Simba

$
0
0
Mchezaji Aomba Barua kwa Uongozi wa  Timu Kuondoka Simba
MSHAMBULIAJI wa Simba, Jamal Mnyate, ameomba barua kwa uongozi wa timu hiyo itakayomruhusu kuondoka na kwenda kwenye klabu nyingine kucheza soka.

Awali, kulikuwepo na taarifa za mshambuliaji huyo kuwepo kwenye orodha ya wachezaji watakaoachwa kwenye usajili huu wa dirisha dogo lililofunguliwa Novemba 15, mwaka huu.

Mchezaji mwingine anayetajwa kuachwa ni mshambuliaji Juma Liuzio ambaye yeye uongozi wa Simba umepanga kumtoa kwa mkopo.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo Championi Jumatatu limezipata, mshambuliaji huyo anaomba barua hiyo ya kuachwa ili aende zake akaichezee Lipuli FC inayonolewa na Selemani Matola.

Aliongeza kuwa, mshambuliaji huyo tayari amekutana na mabosi wake huku akiahidiwa kupatiwa barua hiyo ya kuondoka Simba baada ya kukosa nafasi ya kucheza.

“Mnyate hatutakuwa naye katika mzunguko wa pili wa ligi kuu, kwani yeye mwenyewe ameomba barua ya kuachwa baada ya kuwepo taarifa za kutolewa kwa mkopo.
“Hivyo, yeye mwenyewe ameomba aachwe moja kwa moja na siyo kwa mkopo kama wanavyotaka wenyewe Simba na maamuzi hayo ameyatoa baada ya kuona anakosa nafasi ya kucheza,” alisema mtoa taarifa huyo.

Alipotafutwa Kocha Mkuu wa Lipuli FC, Selemani Matola kuzungumzia hilo juu ya mshambuliaji huyo kuomba aende huko, alisema: “Ni kweli kabisa hizo taarifa, kama mambo yakienda vizuri basi Mnyate tutakuwa naye katika mzunguko wa pili wa ligi kuu.

“Kwani yeye mwenyewe ameonyesha nia ya kuja kuichezea Lipuli, hivyo ninamkaribisha na kama unavyojua timu yangu ina tatizo katika safu ya ushambuliaji, ninaamini kama akija yeye basi timu itaimarika zaidi.”

Beka Afunguka Kuhusu Kutoa Albamu" Sina Uwezo kwa Sasa"

$
0
0
Beka Afunguka Kuhusu Kutoa Albamu" Sina Uwezo kwa Sasa"
Msanii wa muziki Bongo, Beka Flavour amesema kwa sasa hana uwezo wa kutoa albamu kutokana na mazingira ya soko kutokuwa rafiki.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Sarafina’ ameiambia Dj Show ya Radio One kuwa sasa amejikita katika vitu vingine ambavyo anaona vitamuingizia fedha kwa urahisi kupitia muziki wake kuliko kuwaza kutoa albamu.

“Albamu ni kitu ambacho kipo tunakiweka pembeni kwa sababu sina uwezo wa kutoa albamu leo nikauza kwa sababu mauzo ya albamu magumu sana sasa hivi tofauti na kipindi cha nyuma ambacho wasanii walikuwa wanatengea mauzo ya albamu na inawalipa” amesema Beka.

“Kwa hiyo mimi sasa hivi natoa muziki mzuri, na target show, YouTube lakini albamu bado kwa sababu sina uwezo wa kupambana na wezi huko mtaani” ameongeza.

Licha ya kauli hiyo ya Beka kwa mwaka huu katika Bongo Flava    wasanii kadhaa wameweza kutoa albamu, miongoni mwao ni Lady Jaydee na Navy Kenzo

Jambazi Sugu wa Matukio ya Uporaji wa Pikipiki Akamatwa na Bastora Feki Iliyotengenezwa Kienyeji

$
0
0
Jambazi Sugu wa Matukio ya Uporaji wa Pikipiki Akamatwa na Bastora Feki Iliyotengenezwa Kienyeji
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam, tarehe 30, Novemba mwaka huu maeneo ya Buza Sigara lilifanikiwa kukamata silaha moja aina ya Bastola ambayo imetengenezwa kienyeji (bastola feki) iliyokuwa inatumiwa na jambazi sugu katika matukio ya uporaji wa pikipiki.

Akizungumza na wana habari leo, Kamanda wa Kanda Maalum hiyo, Lazaro Mambosasa amesema kuwa awali jambazi huyo alimkodi dereva pikipiki ili ampeleke maeneo ya msitu huko Buza.

Kamanda Mambosasa amesema kuwa ghafla walipofika eneo hilo jambazi huyo alitoa bastola yake iliyotengenezwa kienyeji ikiwa na baruti na kumuamuru dereva ashuke na kumuachia pikipiki. Baada ya kushuka dereva alipiga kelele kuomba msaada na ndipo wananchi walijitokeza na kuanza kumpiga kwa mawe huku wengine wakimkata mapanga jambazi huyo.

Alieleza kuwa askari walipopata taarifa walipofika eneo hilo walimkuta jambazi huyo akiwa na majeraha sehemu mbalimbali za mwili wake na ndipo walimkimbiza katika hospitali ya Temeke kwa ajili ya matibabu na muda mfupi baadae alifariki dunia.

Hata hivyo marehemu huyo anakadiriwa kuwa na umri kati ya miaka (25-30) na mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya Temeke kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa kitaalamu.

Wasiliana na The Great Maalim Hussein Mtaalam wa Kutatua Matatizo Yaliyoshindikana Kwa Kutumia Nyota na Dua

$
0
0

THE GREAT MAALIM HUSSEIN
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
Maalim Hussein ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)

MAALIM HUSSEIN ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)

Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.

Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
Maalim Hussein Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..
Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
+255 674 835 107 WhatsAPP tu. 

Mume, Mke Wafikishwa Mahakamani kwa Kosa la Kusafirisha Dawa za Kulevya

$
0
0
Mume, Mke Wafikishwa Mahakamani kwa Kosa la Kusafirisha Dawa za Kulevya
Wafanyabiashara watatu kati yao wawili wakidaiwa kuwa mume na mke, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi wa kusafirishaji dawa za kulevya aina ya Heroin ya gram 375.20.

Washtakiwa hao ni Minda Mfamai, Fatuma Mpondi na Oswini Mango. Kwa pamoja wamesomewa makosa yao na Wakili wa serikali, Adolf Mkini mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri.

Wakili Mkini alidai washtakiwa wanakabiliwa na kosa la usafirishaji wa dawa za kulevya aina Heroin zenye uzito wa gram 375.20. Inadaiwa walitenda kosa hilo November 22, 2017 maeneo ya Chamazi kwa Mkongo jijini Dar es Salaam.

Baada ya kusomewa kosa hilo, Hakimu Mashauri alisema washtakiwa hawapaswi kujibu chochote kwa kuwa kesi hiyo ni ya uhujumu uchumi na mahakama hiyo haina mamlaka na kwamba kesi hiyo inapaswa kusikilizwa Mahakama Kuu, au hadi Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) atoe kibali ndipo itaweza kusikilizwa.

Hata hivyo, mshtakiwa Mfamai aliiomba mahakama itoe amri akatibiwe kwa sababu amepigwa na polisi wakati akiwa kituo cha Polisi. Kutokana na hatua hiyo, Hakimu Mashauri aliagiza mshtakiwa huyo na wenzake wakatibiwe ambapo aliahirisha kesi hiyo hadi December 19, 2017.

Lukuvi Atoa Onyo kwa Wamiliki wa Nyumba Ataka Kodi ya Nyumba Kutozwa kwa Kila Mwezi

$
0
0
Lukuvi Atoa Onyo kwa  Wamiliki wa Nyumba  Ataka Kodi ya Nyumba Kutozwa kwa Kila Mwezi
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewaonya wamiliki wa nyumba wanaopangisha na kudai kodi ya mwaka mzima.

Akizungumza leo Jumanne Desemba 5,2017 akifungua jengo la makao makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) jijini Dar es Salaam na sanamu ya Mwalimu Julius Nyerere, amesema kodi ya nyumba inatakiwa kutozwa kila mwezi.

"Mpangaji anatakiwa kulipa kodi kila mwezi labda atake mwenyewe kulipa kwa miezi zaidi ya mmoja," amesema.

Lukuvi amesema hata NHC inatoza kodi kwa wateja wake kwa mwezi. "Acheni tamaa wenye nyumba chukueni kodi kila mwezi," amesema.

Amesema kuna vijana wanaoajiriwa wanashindwa kukaa jirani na mjini kutokana na kutozwa kodi ya nyumba kwa mwaka.

Mbali ya kauli hiyo, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula Novemba 17,2017 akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Halima Bulembo bungeni alisema Serikali iko katika mchakato wa maandalizi ya muswada wa sheria ambayo itasimamia sekta ya nyumba, hivyo kuondoa changamoto ya wamiliki kudai kodi ya pango ya zaidi ya mwezi mmoja.

Halima katika swali lake alisema vijana ambao ni kati ya asilimia 56 na 60 nchini, wanashindwa kutimiza ndoto zao kutokana na gharama kubwa ya kodi ambayo hutakiwa kulipa kwa kipindi cha mwaka mmoja au miezi sita.

Akijibu swali hilo, Mabula alisema Serikali imeliona tatizo hilo na ipo katika mchakato wa kuandaa muswada wa sheria utakaosimamia sekta hiyo.

Mabula alisema baada ya kukamilika kwa sheria ambayo itaunda chombo cha kusimamia sekta hiyo, wapangaji hawatalipa kodi ya mwaka wala miezi sita tena bali watalipa kwa mwezi na kuweka amana ya miezi mitatu.

Mourinho Apingana na Mashabiki Kuhusu De Gea

$
0
0
Mourinho Apingana na Mashabiki Kuhusu De Gea
Kocha wa Manchester United Jose Mourinho amekwenda tofauti na mashabiki wa soka kwa kusema, golikipa namba moja wa klabu hiyo David De Gea anashika namba tatu kwa ubora duniani.

Akiongea na wanahabari kwenye mkutano kuelekea mchezo wa UEFA leo ambapo Manchester United itaikaribisha CSKA Moscow, Mourinho amesema golikipa namba moja duniani ni Sergio Romelo ambaye ni golikipa namba mbili kwenye kikosi chake.
Alipoulizwa iwapo amewahi kufanya kazi na mlinda mlango bora zaidi ya De Gea Mournho amejibu, “Ndio, Sergio Romelo, kwasababu atacheza dhidi ya CSKA Moscow, magolikipa wangu wote huwa ni bora duniani”.

Mourinho ameongeza kuwa kwasasa golikipa namba mbili duniani ni Joel Castro Pereira ambaye ni golikipa namba tatu kwenye kikosi cha Man United wakati David De Gea anashika nafasi ya tatu kwa ubora duniani.
Kocha huyo Mreno amekuwa tofauti na mashabiki wengi wa soka duniani ambao hivi karibuni wamekuwa wakimtaja De Gea kama golikipa namba moja duniani kutokana na uwezo wake alioonesha kwenye mchezo dhidi ya Arsenal wikiendi iliyopita.

Mwanachuo wa UDSM Aliyepiga Picha Hosteri za UDSM Aachiwa Baada ya Kuachiwa na Polisi

$
0
0

Mwanachuo wa UDSM Aliyepiga Picha Hosteri za UDSM Aachiwa Baada ya Kuachiwa na Polisi
Mbunge wa serikali ya wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso), Kumbusho Dawson ameachiwa baada ya kuhojiwa na polisi wa kitengo cha makosa ya mtandao.

Kumbusho alipelekwa Kituo Kikuu cha Polisi leo Jumanne Desemba 5,2017 akitokea Oysterbay alikokwenda kuripoti asubuhi baada ya kuachiwa kwa dhamana jana usiku.

Wakili Alex Masaba anayewakilisha Kumbusho amesema polisi wamemuachia baada ya mahojiano na wanaendelea na upelelezi hivyo wakimuhitaji watamwita.

Masaba amesema mteja wake amekamatwa kwa kosa la kusambaza picha zinazoonyesha nyufa kwenye jengo la  mabweni ya chuo hicho. Hata hivyo, amesema anaamini kilichofanyika si jinai.

"Kosa la kusambaza picha zilizopigwa si jinai hata polisi nimewaeleza kwa kitendo kilichofanyika inabidi apongezwe," amesema Masaba.

Jambazi Komando Raia wa Burundi na Wengine Watatu Wauawa na Polisi

$
0
0
Jambazi Komandoo Raia wa Burundi na Wengine Watatu Wauawa na Polisi
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema limewauwa majambazi watatu akiwemo raia wa Burundi ambao walikuwa wakifanya uhalifu katika maeneo mbalimbali  ya jiji hilo na nchini kwa ujumla.

Hayo yameelezwa leo na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam ambapo amesema kuwa katika majambazi hao watatu waliouwawa kwenye oparesheni maalum ya jeshi hilo, iliyofanyika kuanzia Novemba 11 hadi 30, 2017 alikuwepo raia mmoja wa Burundi aliyejulikana kwa jina la Fanueli Luchunda Kamana ambaye ana mafunzo ya kijeshi na kufikia ngazi ya Komando.
“Baada ya kuwakamata na kuwafanyia mahojiano walikubali kuonyesha silaha moja aina ya AK 47 pamoja na Magazine mbili zenye jumla ya risasi 57 ambazo zote walikuwa wameficha kwenye vichaka maeneo ya Ubungo Mawasiliano” amesema Kamanda Mambosasa.
Aidha Mambosasa ameeleza kuwa raia huyo wa Burundi ndio alikuwa kiongozi wa kundi hilo ambapo alikuwa anakwenda Burundi kila baada ya kufanya tukio. Ameongeza kuwa baada ya kwenda kuonesha silaha walizokuwa wameficha katika eneo jingine, Mburundi huyo alimvamia askari kwa lengo la kumshambulia ili wajinasue.
“Baada ya kumvamia askari wetu majambazi wale wawili walianza kukimbia lakini askari wetu walifanikiwa kuwadhibiti kwa kuwafyatulia risasi na baadae kuwafikisha katika hospitali ya Mwananyamala ambapo walibainika kuwa wamefariki”, amesema Mambosasa.

Jeshi la JWTZ Laandaa Mazoezi ya Pamoja Kwa Maofisa Wanachama EAC

$
0
0
Jeshi la JWTZ Laandaa Mazoezi ya Pamoja Kwa Maofisa Wanachama EAC
 Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limeandaa mazoezi ya pamoja ya kijeshi kwa maofisa kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Mazoezi hayo yaliyopewa jina ‘Ushirikiano imara’ yanawashirikisha wanajeshi na maofisa wa Serikali kutoka Tanzania, Uganda, Burundi, Kenya na Rwanda.

Mkuu wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi, Brigedia Jenerali Alfred Kapinga amesema leo Jumanne Desemba 5,2017 kuwa watu 300 wanashiriki wakiwamo makamanda wa jeshi na maofisa wa juu kutoka wizara zaidi ya tatu ikiwamo ya Katiba na Sheria.

Amesema kwa Tanzania wanaoshiriki ni makamanda na maofisa watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Brigedia Jenerali Kapinga amesema kwa upande wa Tanzania washiriki ni 107 na kwamba, mazoezi yameanza jana Desemba 4,2017 na yatazinduliwa Desemba 7,2017 na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi.

“Mazoezi yanafanyika katika Kituo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani cha Kunduchi, Dar es Salaam na yamejikita katika mambo makuu manne,” amesema.

Ameyataja mambo hayo kuwa ni operesheni katika ulinzi wa amani; kupamba na ugaidi; kupambana na uharamia wa aina yoyote ndani ya Bahari ya Hindi; na majanga na maafa.

Amesema lengo la mazoezi hayo ni kuwaandaa na kuwapa uwezo washiriki katika kupanga na kutekeleza majukumu ya operesheni za ulinzi wa amani katika kupambana na ugaidi, uharamia na kukabiliana na maafa.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi amtembelea Tundu Lissu hospitalini

$
0
0
Rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi amemtembelea mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu aliyelazwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya.

Rais Mwinyi akiambatana na mke wake na maofisa wa ubalozi wa Tanzania nchini Kenya, wamemtembelea Lissu hospitalini hapo alipolazwa tangu Septemba 7  anakotibiwa baada ya kuuguza majeraha ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 akiwa nyumbani kwake mjini Dodoma.

Rais Mwinyi anakuwa miongoni mwa viongozi wa juu wa Serikali waliomtembelea Lissu ambaye ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) ambaye hivi karibuni Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan naye alifika hospitalini hapo kumjulia hali.

Wabunge Tisa UKAWA Watajwa Kuhamia CCM...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Disemba 6

$
0
0


Wabunge Tisa UKAWA Watajwa Kuhamia CCM...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Disemba 6

Hatima ya Dhamana ya Wabunge Wawili wa CHADEMA Kujulikana Leo.....Ni Baada ya Jana Kurudishwa Rumande

$
0
0
Wabunge Susan Kiwanga na Peter Lijualikali waliofikishwa jana  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro pamoja na washtakiwa wengine 36 walirejeshwa rumande.

Mahakama iliyokuwa itoe uamuzi wa dhamana jana  Jumanne Desemba 5,2017 ilikwama kufanya hivyo kutokana na kuibuka hoja za kisheria.

Upande wa mashtaka na ule wa utetezi unavutana kuhusu hati ya kiapo ya kupinga dhamana iliyowasilishwa mahakamani hapo.

Kutokana na mvutano wa kisheria, hakimu Ivan Msack aliahirisha kesi hiyo hadi leo Jumatano Desemba 6,2017 ili kutoa fursa kwa pande zote mbili kujibu hoja kuhusu hati hiyo.

Washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka nane likiwamo la kuchoma moto ofisi ya Kata ya Sofi iliyopo wilayani Malinyi.

Washtakiwa wanatetewa na mawakili Peter Kibatala, Ignas Punge, Fredrick Kiwelo na Bartholomew Tarimo.

Upande wa mashtaka unawakilishwa na mawakili wa Serikali, Edga Bantulaki na Sunday Hyera.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho, Frederick Sumaye walihudhuria mahakamani.

Wengine waliofika mahakamani ni mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche na wa Viti Maalumu, Devota Minja.

Mwanafunzi Aliyesambaza Picha za Nyufa Hostel za UDSM Aachiwa.......Jeshi la Polisi Limetaja Sababu za Kumkamata

$
0
0
Mbunge wa serikali ya wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso), Kumbusho Dawson ameachiwa baada ya kuhojiwa na polisi wa kitengo cha makosa ya mtandao.

Kumbusho alipelekwa Kituo Kikuu cha Polisi jana Jumanne Desemba 5,2017 akitokea Oysterbay alikokwenda kuripoti asubuhi baada ya kuachiwa kwa dhamana juzi usiku.

Wakili Alex Masaba anayewakilisha Kumbusho amesema polisi wamemuachia baada ya mahojiano na wanaendelea na upelelezi hivyo wakimuhitaji watamwita.

Masaba amesema mteja wake alikamatwa kwa kosa la kusambaza picha zinazoonyesha nyufa kwenye jengo la mabweni ya chuo hicho. Hata hivyo, amesema anaamini kilichofanyika si jinai.

"Kosa la kusambaza picha zilizopigwa si jinai hata polisi nimewaeleza kwa kitendo kilichofanyika inabidi apongezwe," amesema Masaba.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alieleza kuwa polisi ilimkamata na kufanya mahojiano na mwanafunzi huyo ili kujua lengo hasa la yeye kusambaza picha hizo pasipo kutoa taarifa kwa wamiliki wa majengo pamoja na wakala wa majengo husika.

“Huyo mwanafunzi alikamatwa na kufikishwa katika kituo cha polisi lakini alihojiwa na kuachiliwa kwa dhamana.

"Kilichopelekea akamatwe ni ule uzushi awa kuzunguka kwenye kwenye mitando.

"Sisi tulikuwa tunakitegemea kama angekuwa na taarifa yoyote, wamiliki wa majengo wapo, mkandarasi aliyefanya kazi ile yupo, kwa hiyo mtu ambaye angepaswa kuwa wa kwanza kulalamika angekuwa ni mmiliki wa majengo na sio yeye.

"Sasa yeye amefikia mahali akarusha, sijui alikuwa na maana gani, hatujaielewa vizuri..,” alisema Kamanda Mambosasa.

Waziri Lukuvi Awaonya Wamiliki wa Nyumba Wanaowatoza Wapangaji Kodi ya Mwaka Mzima

$
0
0

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewaonya wamiliki wa nyumba wanaopangisha na kudai kodi ya mwaka mzima.

Akizungumza jana Jumanne Desemba 5,2017 akifungua jengo la makao makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) jijini Dar es Salaam na sanamu ya Mwalimu Julius Nyerere, alisema kodi ya nyumba inatakiwa kutozwa kila mwezi.

"Mpangaji anatakiwa kulipa kodi kila mwezi labda atake mwenyewe kulipa kwa miezi zaidi ya mmoja," alisema.

Lukuvi alisema hata NHC inatoza kodi kwa wateja wake kwa mwezi. "Acheni tamaa wenye nyumba chukueni kodi kila mwezi," alisema.

Alisema kuna vijana wanaoajiriwa wanashindwa kukaa jirani na mjini kutokana na kutozwa kodi ya nyumba kwa mwaka.

Mbali ya kauli hiyo, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula Novemba 17,2017 akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Halima Bulembo bungeni alisema Serikali iko katika mchakato wa maandalizi ya muswada wa sheria ambayo itasimamia sekta ya nyumba, hivyo kuondoa changamoto ya wamiliki kudai kodi ya pango ya zaidi ya mwezi mmoja.

Halima katika swali lake alisema vijana ambao ni kati ya asilimia 56 na 60 nchini, wanashindwa kutimiza ndoto zao kutokana na gharama kubwa ya kodi ambayo hutakiwa kulipa kwa kipindi cha mwaka mmoja au miezi sita.

Akijibu swali hilo, Mabula alisema Serikali imeliona tatizo hilo na ipo katika mchakato wa kuandaa muswada wa sheria utakaosimamia sekta hiyo.

Mabula alisema baada ya kukamilika kwa sheria ambayo itaunda chombo cha kusimamia sekta hiyo, wapangaji hawatalipa kodi ya mwaka wala miezi sita tena bali watalipa kwa mwezi na kuweka amana ya miezi mitatu.

Zari Aamua Kuchunga Mzigo Wake Amdhibiti Mobeto kwa Diamond Aweka Kambi Dar

$
0
0
Zari Aamua Kumzibiti Mobeto Aamua Kuweka Kambi Dar
Wakati kukiwa na figisufigisu kuhusu uhusiano kati ya wadada wawili waliozaa na mwanaume mmoja, Zarina Hassan ‘Zari’ na Hamisa Mobeto, mwanamke huyo mama wa watoto watano anayeishi Afrika Kusini, anadaiwa kutua jijini na kuweka kambi maalum kulinda kitumbua chake, Risasi Mchanganyiko limeambiwa.

Kwa mujibu wa chanzo chetu kilicho karibu na Zari, inadaiwa kuwa mjasiriamali huyo alikuwa jijini Dar es Salaam ambako alihudhuria shughuli mbili za watu wake wa karibu, lakini inadaiwa kuwa hiyo ilikuwa ni geresha tu, kwani ziara yake ya kushtukiza ilikuwa na lengo maalum.

“Unajua kuna mambo kidogo kama hayaeleweki ambayo Mobeto anafanya, sasa Zari amepiga hesabu na kuamua kujiongeza, amekuja mjini na kupiga kambi Madale kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa, katika matukio yote mawili alihudhuria na mzazi mwenzake, kitu ambacho kilimnyima kabisa nafasi Mobeto ya kusogelea,” alisema mtoa habari wetu.

Hamisa Mobeto.
Kumekuwa na uvumi kuwa Mobeto ameongea na kumalizana na mzazi mwenzake nje ya vyombo vya kisheria na baadhi wakidai kuwa wamerejesha hata uhusiano wao, kitu ambacho kinamfanya Zari kuishi kimachalemachale.

Katika video vilizowekwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ilimuonyesha Zari akiwa na furaha tele, tofauti na mzazi mwenziye aliyeonekana kama kuna jambo ambalo hafurahishwi nalo. Zari raia wa Uganda, anaishi Afrika Kusini pamoja na watoto wake watano, wakiwemo watatu aliozaa na mumewe, Ivan Ssemwanga aliyefariki mapema mwaka huu.

Mwinyi Amtembelea Tundu Lissu Nairobi Kumjulia Hali

$
0
0
Mwinyi Amtembelea Tundulissu Nairobi Kumjulia Hali
RAIS Mstaafu wa awamu ya pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi leoDesemba 5, 2017 amemtembelea Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema) na Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika, Tundu Lissu katika Hospitali ya Nairobi anakotibiwa baada kushambuliwa kwa risasi nyumbani kwake Area D, Mjini Dodoma.

Lissu alikimbizwa katika hospitali hiyo baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 na watu wasiojulikana nyumbani kwake, Area D, Mjini Dodoma, Septemba 7 mwaka huu.

Rufaa ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Yafanyiwa Kazi

$
0
0
Rufaa ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Yafanyiwa Kazi
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza orodha yenye wanafunzi 2,679 ambao wamepata mikopo ya elimu ya juu yenye thamani ya TZS 9.6 bilioni kufuatia kukamilika kwa uchambuzi wa rufaa zilizowasilishwa.

Kati ya wanafunzi hao 1,847 ni wa mwaka wa kwanza ambao mikopo yao ina thamani ya TZS 6.84 bilioni. Wengine 832 ni wale wanaoendelea na masomo lakini hawakuwa na mikopo katika miaka iliyopita. Wanafunzi hao wanaoendelea na masomo wamepata mikopo yenye thamani ya TZS 2.76 bilioni.
Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru amesema orodha ya wanafunzi hao na fedha zao zimetumwa katika vyuo walipo wanafunzi hao hivi sasa
“Hatua hii inafanya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza kuwa wamepangiwa mikopo yenye thamani ya zaidi ya TZS 108 bilioni kwa mwaka wa masomo 2017/2018 hadi sasa”, amesema Badru na kufafanua kuwa Serikali imetenga jumla ya TZS 427.54 bilioni kwa ajili ya mikopo hiyo kwa mwaka 2017/2018.
HESLB ilifungua dirisha la rufaa kwa siku saba kuanzia tarehe 13 Novemba, 2017 hadi tarehe 19 Novemba, 2017 ili kuwapa fursa waombaji wote ambao hawakuwa wameridhika na upangaji wa mikopo na kuwasilisha rufaa kupitia vyuo walivyopata udahili.

Mtanzania Afa Ndani ya Ndege Akiwa Anasafirisha Dawa za Kulevya Kupeleka China

$
0
0
Mtanzania Afa Ndani ya Ndege Akiwa Anasafirisha Dawa za Kulevya Kupeleka China
Mtanzania aliyekuwa anasafirisha madawa ya kulevya kupeleka nchini China amefariki kwenye ndege ya Shirika la Ethiopia baada ya kuzidiwa na dawa hizo.

Akithibitisha taarifa hizo, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA), Rogers Sianga amesema amepokea taarifa hizo jana Desemba 4, 2017, ila bado wanafanya uchunguzi zaidi kujua jina lake na wapi alizitoa dawa hizo.

“Ni kweli kuna Mtanzania amekutwa amekufa kwenye ndege ya Shirika la Ethiopia akiwa amemeza dawa za kulevya. Tunaendelea kufuatilia kujua jina lake na amezitoa wapi hizo dawa.” amesema Sianga kwenye mahojiano yake na gazeti la Mwananchi.

Kwa upande mwingine Sianga amesema Watanzania wengi wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya  wanatumika kwa kupokea mizigo hiyo na kuisafirisha kunakohitajika kitu ambacho bado serikali inapambana nacho ili kuweza kutokomeza kabisa biashara hiyo haramu..
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images