Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Polepole Awatupia Dongo Chadema..."Watani Wanakutana Leo Agenda ni Kutoshiriki Uchaguzi"

$
0
0
Polepole Awatupia Dongo Chadema..."Watani Wanakutana Leo Agenda ni Kutoshiriki Uchaguzi"
Katibu wa itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole amesema  CHADEMA wamefanya kikao cha dharura  kususia uchaguzi wa marudio wa majimbo na kata unaotarajiwa kufanyika January 13 mwakani.

Polepole amewatuhumu  CHADEMA  kuwa wanatumia mgongo wa kuminywa kwa Demokrasia nchini kususia uchaguzi huo wakati ukweli ni kwamba wamefulia baada ya kutumia vibaya hela ya mfuko wa chama chao.

"Watani wanakutana leo, agenda ni kutoshiriki uchaguzi unaokuja wa marudio kwa kisingizio cha demokrasia lakini ukweli ni matumizi mabaya ya fedha yamefuja mfuko wa chama. Tafuteni visingizio vingine lakini sio demokrasia. Watu wamechoka siasa za matukio. Kikao chema!" Ameandika polepole katika ukurasa wake wa Twitter.


Wolper Amuunga Mkono Faiza Kuweka Picha Akiwa Leba Anajifungua " Wabongo ni Washamba"

$
0
0
Wolper Amuunga Mkono Faiza Kuweka Picha Akiwa Leba Anajifungua " Wabongo ni Washamba"
STAA wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper amesema kuwa, anamuunga mkono muigizaji Faiza Ally kwa kitendo chake cha kuweka picha inayomuonyesha akiwa mtupu katika chumba cha kujifungulia (leba).


Wolper alisema anawashangaa watu wanaomponda Faiza aliyeposti picha hiyo hivi karibuni katika ukurasa wake wa Instagram, wakati yeye amevutiwa sana na kitendo hicho na ipo siku atamuiga.

“Wabongo ni washamba, ushamba unawasumbua sio kingine. Sioni ubaya wa hiyo picha hata kidogo, eti katudhalilisha, kamdhalilisha nani sasa pale, mimi nimefurahi mno tena nitamuiga nikijaaliwa kupata mtoto,”alisema Wolper.

Jacqueline Wolper, Leo Kusheherekea Sherehe Yake ya Kuzaliwa

$
0
0
Jacqueline Wolper, Leo Kusheherekea Sherehe Yake ya Kuzaliwa
STAA wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper, leo anatarajia kufanya sherehe ya siku yake ya kuzaliwa huko Masaki katika ukumbi wa Buckets ambapo atazindua ‘Application’ ambayo itapatikana kwenye Google Play Store ya duka lake la nguo kuwawezesha wateja wake kupata huduma kwa ukaribu.

Msanii atakayepiga shoo katika hafla hiyo ni Barnaba Classic  kuanzia saa moja mpaka saa sita usiku.  Wolper amemchagua Barnaba kupiga shoo hiyo kwa kuwa ni msanii anayempenda na kumsapoti kwa ukaribu akisema nyimbo zote alizoimba zinaelezea maisha yake aliyoyapitia.
Staahuyo amewaomba mashabiki zake kufika kwa wingi katika ukumbi wa Buckets kumsapoti na amesema kiingilio ni shilingi 10,000/- tu.
Wasanii mbalimbali wengine  watakuwepo kumsapoti Wolper leo.  Pia amesema shangwe za siku yake ya kuzaliwa zitaendelea kesho mjini Dodoma katika klabu ya usiku ya burudani ya Maisha.  Amewaomba pia mashabiki zake wa mji huo kujitokeza kwa wingi kumsapoti.
Kampuni ya Global Group tunamtakia Wolper kila la heri katika siku yake ya kuzaliwa.

Download Application ya MCHAMBUZI Kwenye Simu yako Kusoma Habari za Siasa Kila Baada ya Lisaa Limoja

$
0
0
Maswala ya Siasa na Matamko ya kila siku ya Wanasiasa Hakikisha Umedownload App ya Mchambuzi Kwenye simu yako

Kama we ni Mpenzi wa Habari za Siasa Usipitwe na Hii Application ya Mchambuzi.....

Bonyeza HAPA Kudownload kwenye Simu yako



Nishaurini: Nimegundua Pesa Ninazompa Anahonga Mwanaume Mwingine

$
0
0
Mimi ni kijana wa kiume nna miaka 27, kuna msichana nimekutana nae miezi minne iliopita, kiukweli ni mzuri sana pia ni mwanachuo hapa Dar, kiukweli nimemuhudia sana ndani ya miezi hiyo minne.

Nimemnunulia hadi kiwanja Chanika, simu nzuri, pesa za matumizi nampa nyingi tuu nimemwambia boom lake awasaidie wazazi nyumbani kwani aliniambia wako vibaya sana (maskini wa kutupwa)

Sasa juzi nimegundua kumbe pesa ninazompa ana kamwanamme kake nae anakahonga anasoma nako chuo.

Gharama nilizomgharamia nimecalculate ni zaidi ya M8, nikimuulza analeta kiburi anadai kama vipi tuachane.

Je, nifanyaje? Juzi washikaji zangu wamenishauri tuwateke wote tukawatese nje ya mji ikiwezekana tumuue huyo jamaa.

Mnanishauri nini?

Inauma sana

Mke Wangu Ana Mimba; Katokea Kunichukia na Kampenda Mume wa Mtu Jirani na Chumba Tulichopanga

$
0
0
Aman iwe nanyi wapendwa katika bwana

Husika na kichwa cha habari hapo juu

Mimi kijana mwenzenu nasikitika sana na hii tabia ya mke wangu, kwakweli ana nichanganya sana jaman

Ana mimba ya miez sita lakin katokea kunichukia sana jaman hatak hata kunisogelea wala kula chakula mezan pamoja na mimi

Lakin katokea kumpenda mme wa mtu ambaye ni jiran wa chumba hapa tulipopanga

Mke wangu ni mama wa nyumban na hana kaz lakin mimi huondoka asubuh sana kwenda job lakin hurud usiku wa saa tatu

Nikifika nyumban get had nije nifunguliwe na mtu mwingine mke wangu yeye kalala tu na hata kama nikifika mlangon huwa hafungui upes yaan nitagonga mlango had bas na atakuja kufungua mda atakao taka yeye

Mfano jana nimefika nyumban saa tatu lakin alikuja kunifungulia saa tano usiku

Na kama nikiingia ndan anaanza kutema tema mate et kuna kitu ndan kinanuka shombo ya samak hasa mimi nikiingia

Yaan nakuwa naambiwa mda mwingine yule jamaa huwa anaingia had ndan mwangu kupiga story na mke wangu

Ina niuma sana mimi jaman

Nateseka sana jaman

Naomben usaur wenu

London baby/JF

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Disemba 8

$
0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Disemba 8

Mvutano waibuka kesi ya Madabida na wenzake....Mahakama kutoa uamuzi Kesho

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kesho Ijumaa inatarajiwa kutoka uamuzi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida na wenzake watano  kama ina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo ama la.

Uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa.

Utatolewa baada ya kusikilizwa hoja zilizowasilishwa na upande wa mawakili wa Serikali, Pius Hilla na Shedrack Kimaro na mawakili wa utetezi, Denis Msafiri, Makaki Masatu na Nehemia Nkoko.

Wakili wa Serikali, Kimaro akiwasilisha hoja zao leo Alhamisi alidai kuwa hoja ya mawakili wa utetezi kuwa Mahakama ya Kisutu ina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo kwa sababu ipo chini ya Sh 1 bilioni siyo sahihi.

Amedai kuwa ni dhahiri kuwa makosa hayo ni ya uhujumu uchumi na mamlaka yenye mamlaka ya kuisikiliza ni Mahakama Kuu Kitengo cha Rushwa na Uhujumu Uchumi maarufu Mahakama ya Mafisadi.

“Hivyo mahakama za chini kama Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo labda kuwepo na kibali cha kulipa mamlaka ya kuisikiliza kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).”

Kutokana na hilo aliiomba Mahakama kutupilia mbali hoja za upande wa utetezi.

Wakili wa utetezi, Msafiri alidai kuwa ameusikia upande wa mashtaka, ila ni rai yao kuwa marekebisho ya sheria ya uhujumu uchumi ya 2016 yanaipa moja kwa moja Mahakama ya Kisutu kuisikiliza kesi hiyo.

Alidai kuwa kosa lolote lililopo chini ya Sh 1 bilioni haliwezi kusikilizwa na Mahakama Kuu Kitengo cha Rushwa na Uhujumu Uchumi ni Mahakama za chini ikiwamo Mahakama ya Kisutu.

Alisisitiza kuwa Mahakama ya Kisutu ina mamlaka kamili ya kuisikiliza kesi hiyo kwa vile shtaka halizidi Sh 1 bilioni na kwamba mahakama hiyo ndiyo yenye mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo na siyo Mahakama Kuu.

Pia alidai kuwa kibali cha DPP cha kuipa mamlaka mahakama kusikiliza kesi kinapaswa kipelekwe mahakamani pamoja na hati ya mashtaka.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi kesho Ijumaa ambapo mahakama itatoa uamuzi na washtakiwa waliamuliwa wapelekwe polisi.

Hata hivyo, Wakili wa Serikali, Pius Hilla aliomba wapelekwe magereza kwa sababu washtakiwa hao kuendelea kuwa mikononi mwa polisi kuna suala la gharama na polisi hawana fungu.

Baada ya kutolewa kwa ombi hilo, Wakili Nkoko aliomba Mahakama kusimamia amri yake kama ilivyoitoa.

Wakili Masatu naye aliiomba mahakama iendelee na oda yake ilivyoitoa jana Jumatano.

Hakimu Nongwa amesema suala la gharama hawawezi kulikwepa pale haki inapotafutwa na kuamuru washtakiwa wapelekwe polisi hadi kesho Ijumaa atakapotoa uamuzi kama mahakama hiyo ina mamlaka ama la.

Madabida na wenzake wanakabiliwa na mashtaka sita ya uhujumu uchumi ikiwamo kusambaza dawa bandia za kufubaza virusi vya Ukimwi ' ARV’s ' na kusababisha hasara ya Sh 148 milioni.

CHADEMA chawataka wabunge wake kujiondoa michuano ya mabunge EAC

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeazimia kuwa wabunge wake wote wanaoshiriki Michezo ya Mabunge ya Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wanatakiwa kuondoka mara moja kwenye kambi ya timu ya Tanzania.

CHADEMA kimefikia uamuzi huo katika kikao chake cha dharura kinachoendelea ambacho kiliitishwa kwa lengo la kutafakari kwa kina maendeleo ya hali ya siasa nchini.

Chama hicho kimesema kuwa maagizo hayo yameanza kutekelezwa usiku wa Jumatano, Disemba 6 mwaka huu baada ya kupitishwa kwa azimio hilo ambapo Kamati Kuu ilimuagiza Katibu wa Bunge kuwafikishia wabunge wahusika mara moja

Baada ya kupokea tathmini ya kina ya Uchaguzi wa marudio katika Kata 43 uliofanyika hivi karibuni CHADEMA kimebaini kuwa ulitawaliwa na uvunjifu Mkubwa wa Haki za binadamu.

Aidha CHADEMA kimesema kuwa maazimio mengine ya kikao cha Kamati Kuu ambacho kinaendelea jijini Dar yatatolewa katika hatua ya baadae ambapo umma utaarifiwa rasmi.

Gigy Money Atokwa Povu 'Kama Nina Mimba au Sina Haimhusu Mtu'

$
0
0
MSANII wa filamu Bongo Gift Stanford ‘Gigy Money’ amefunguka kutokana na uvumi uliopo kwamba amenasa kibendi na kusema watu waache kumjadili juu ya ishu hiyo sababu mimba si kitu cha matangazo na wala haina kificho.

Akipiga stori na Star Mix, mwanadada huyo ambaye kitumbo chake kinaonekana kimeshiba tofauti na kawaida yake huku mwili wake ukianza kunawiri wakati alikuwa amepungua na kuzua mjadala, alisema suala hilo halimhusu mtu yeyote sababu iwe kweli au si kweli hakuna atakayemsaidia kulea.

“Kama nina mimba au sina haimhusu mtu, sababu mimba si kitu cha matangazo, kama ni kweli ninayo mtajua tu maana hainaga kificho, kuhusu mwili wangu kuanza kuongezeka kipindi cha nyuma nilikuwa na ‘stress’ sasa hivi niko sawa ndiyo maana nimeanza kunenepa,”alisema.
Stori: Mayasa Mariwata

Mzazi Mwenzie Barnaba 'Mama Steve' Amtambulisha Mpenzi Wake Mpya

$
0
0
Mzazi Mwenzie Barnaba 'Mama Steve' Amtambulisha Mpenzi Wake Mpya
Unamkumbuka mama Steve wa Barnaba Classic? Alhamisi hii amemtambulisha mpenzi wake mpya aitwae, Brown ambapo katika usiku wa Birthday Party ya Jack Wolper iliyofanyika Buckets Masaki Jijini Dar es salaam akikuja naye na kuonana na Barnaba ambaye siku hiyo alikuwa anatoa burudani kwenye party hiyo.

Wapalestina Wakataa Mazungumzo na Marekani

$
0
0
Wapalestina Wakataa Mazungumzo na Marekani
Marekani imeionya Palestina dhidi ya maamuzi yake kutotaka kukutana na makamu wa rais Marekani ,Mike Pence katika kikao ambacho kilipangwa kufanyika mapema mwezi huu ili kujadili uamuzi wa rais Trump wa kuhamishia Yerusaleam kuwa mji mkuu wa Israel.
Ikulu ya Marekani imesema, uamuzi huo uliofikiwa na Palestina utakuwa hauna maana kwa kuwa hawataweza kupata suhulu ya mgogoro huo.
Makamu wa rais wa Marekani ana mpango wa kwenda katika ukanda huo wa mashariki ya kati lakini kiongozi wa ngazi za juu wa Palestina ,Jibril Rjoub amesema kuwa kiongozi huyo hakaribishwi Palestina.

Hatua hiyo imekuja mapema baada ya rais Trump kutangaza kuwa anautambua mji wa Yerusaleum kuwa mji mkuu,
Ambapo mpaka sasa Wapalestina takriban 31 wamejeruhiwa katika makabiliano yaliyozuka Ukanda wa Gaza na maeneo ya Ukingo wa Magharibi yanayotawaliwa na Israel kuhusu mji wa Jerusalem.

Wolper Ajiongeza Kwenye Birthiday Yake kwa Afanya Sherehe na Kuzindua App

$
0
0
Wolper Ajiongeza Kwenye  Birthiday Yake kwa Afanya Sherehe na Kuzindua App
Msanii wa wa filamu, Jacqueline Wolper Alhamisi hii amefanya sherehe ya kusherekea birthday yake ambapo pia ametumia sherehe hiyo kuzindua App yake itwaayo, Wolper Stylish.

Party hiyo ilihudhuriwa na mastaa mbalimbali wa muziki akiwemo Diamond Platnumz.

Muigizaji huyo alisema app hiyo itawasaidia mashabiki wake kupata taarifa mbalimbli zinazohusu maisha yake, kazi pamoja na kampuni yake ya ubinifu wa nguo.

Wolper siku jana mchana alianza kusherekea ziku yake ya kuzaliwa kwa kula chakula cha mchana na watoto yatima.

Nuh Mziwanda Afunguka Kuhusu Mistari ya Nyimbo Aliyoandika Baada ya Kuolewa Shilole

$
0
0
Nuh Mziwanda Afunguka Kuhusu Mistari ya Nyimbo Aliyoandika Baada ya Kuolewa Shilole
Aliyekuwa mpenzi wa zamani wa Shilole, Nuh Mziwanda amefunguka kuzungumzia mistari ya wimbo wa Mwana FA, ‘Bado Nipo Nipo’ aliyoipost muda mchache baada ya aliyekuwa mpenzi wake huyo wa zamani kuolewa na kijana anayetambulika kwa jina na Uchebe.

Mapema Alhamisi hii muimbaji huyo aliandika “Aliyelala na bibi harusi wiki moja kabla ya harusi na wala sio bwana harusi bado mnanishauri harusi’ kauli ambayo ilitafsiriwa na wadau wa mambo kwamba dongo hilo linaenda kwa Shilole na Uchebe.

Ile post mimi nimeweka kwasababu ni msemo ambao nimeupenda na sipangiwi cha kukiposti na nimeandika si kwa ubaya na sijamtagi mtu hivyo nisinukuliwe vibaya coz niliandika na wala sikufikiria watu wangeusisha na harusi ya shilole ila ninavyojua hivi vitu vipo vinatokea kwa watu unamkuta bibi harusi kesho no harusi yake na analala na mwanamume mwingine.

Mimi na Shilole toka tuachane hatujawahi kurudiana ila uwa tunasaidiana pale inapoitajika kama kafiwa siwezi kuacha kwenda kumfariji kwakuwa tumeachana haipo hivyo na hata ngoma yangu ya sasa kuna baadhi ya vitu amenisaidia kuingiza.


Aunt Ezekiel Awatolea Povu Wanayemsema Kuhusu Kuishi Nyumba za Kupanga

$
0
0
Aunt  Ezekiel Awatolea Povu Wanayemsema Kuhusu Kuishi Nyumba za Kupanga
BAADA ya kuandamwa mitandaoni kuwa tangu amekuwa staa bado anaishi nyumba za kupanga maeneo ya Kijitonyama jijini Dar, staa wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel amefungukia madai hayo kuwa wengi wanaongea bila kujua undani wa maisha yake.

Akizungumza na Star Mix, Aunt alisema ameamua kuishi maisha ya kupanga kwa sababu ya ukaribu na kazi zake na kama ni nyumba yake ipo maeneo ya Kigamboni.

“Nawashangaa sana wanaosema hivyo. Nimepanga katikati ya mji ili nifanye kazi zangu kwa wepesi na kama ni nyumba mbona ninayo Kigamboni?” Alihoji Aunt ambaye ni mzazi mwenza na Moze Iyobo.

Kampeni CCM Ngazi ya Taifa Zashika Kasi

$
0
0
Kampeni CCM Ngazi ya Taifa Zashika Kasi
Mshikemshike wa kampeni za uchaguzi ndani ya CCM ngazi ya taifa umeanza kushika kasi kwa wagombea kujinadi kupitia mitandao ya kijamii kabla ya Mkutano Mkuu wa Taifa utakaofanyika Desemba 18 na 19, mwaka huu.

Tangu mchakato wa uchaguzi huo uanze ngazi ya mashina, kata na mikoa wagombea waliokuwa wanateuliwa hawakuruhusiwa kufanya kampeni wala kusambaza vipeperushi na majina yao yalijulikana mbele ya mkutano wa uchaguzi.

Tofauti na ilivyokuwa kwa chaguzi hizo za chini, wagombea wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) na nyadhifa nyingine za juu kwenye jumuiya za chama wanaonekana kujinadi na kuomba kura kupitia vipeperushi kwenye mitando hasa kwenye makundi ya wanaCCM.

Nafasi ambayo inavuta wagombea wengi ni nafasi 15 za wajumbe wa NEC Tanzania Bara inayogombea na wanaCCM 50 na wengine 15 kutoka Zanzibar. Wengine wanawania uongozi wa Umoja wa Wanawake (UWT) na UV-CCM.

Baadhi ya wagombea ambao Mwananchi imeona vipeperushi vyao ni Stephen Wassira, Dk Fenella Mkangala, Angela Akilimali, Esther Baruti na Grace Kingalame.

Kwa kawaida nafasi hizo za NEC ndizo huwa na kinyang’anyiro kikali na safari kitambanisha sura nyingi mpya baada ya wale wakongwe kutokuwamo ama kutokana na kuwa na nafasi nyingine za uongozi, kutokuomba au kuenguliwa.

Katika mabadiliko kadhaa yaliyofanywa na chama hicho, wanachama wake hawaruhusiwi kuwa na kofia mbili kwa mtu mmoja.

Wakongwe waliokuwa wanashikilia nafasi hiyo na wanawania tena ni Wassira, Jackson Msome na Mkangala. Washindi wataungana na wenzao waliochaguliwa mikoani na kutimiza idadi ya wajumbe 162 wa NEC baada ya kupunguzwa kutoka 388 wa awali. Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole hakupatikana kuzungumzia hali hiyo iwapo ni ruksa kufanya hivyo, lakini Akilimali alilieleza Mwananchi kwamba kwa hatua ya sasa baada ya uteuzi wa majina kufanywa na Halmashauri Kuu ya Taifa wanaruhusiwa kujinadi.

Takukuru watia mguu

Mbali na wajumbe kujinadi, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) nayo imepiga kambi katika uchaguzi ili kukabiliana vitendo rushwa.

Mara kadhaa maofisa wa Takukuru katika mikoa mbalimbali wametoa taarifa za kufuatilia vitendo hivyo na wiki iliyopita mkoani Mwanza walilipekua gari la mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo, Anthony Diallo.

Katika mabadiliko yaliyoasisiwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais John Maguf

Watu zaidi ya Thelathini Wajeruhiwa Palestina

$
0
0
Watu zaidi ya Thelathini Wajeruhiwa Palestina
Vurugu zimeendelea huko ukanda wa gaza na ukingo wa magharibi ambapo zaidi ya wapalestina thelathini wamejeruhiwa katika makabiliano na polisi wa Israel
Hii ni kufuatia Rais Donald Trump kutangaza kuutambua mji wa Yerusalemu kuwa mji mkuu wa Israel.

Wakati huo huo Marekani imeionya Palestina dhidi ya maamuzi yake kutotaka kukutana na makamu wa rais marekani ,Mike Pence katika kikao ambacho kilipangwa kufanyika mapema mwezi huu.
Waandamanaji wamechoma matairi na kurusha mawe huku maafisa usalama wa Israel wakifyatulia wandamaanaji hao hewa ya kutoa machozi na risasi za mpira.

Israel wakifyatulia wandamaanaji hao hewa ya kutoa machozi na risasi za mpira
Huko Gaza kundi la kiislamu la Hamas limeitisha intifada au mapambano. Omary Shakir mkuu wa shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch katika eneo la Isreal na Palestina yupo mjini Ramala.
Ameiambia BBC kuwepo baada ya Israel katika eneo hilo kwa miongo kadhaa sasa wapelestina wengi wamekuwa na hasira na tangazo la Rais Trump.

Kwa upande wake Naibu waziri anayehusika na masuala ya Diplomasia wa Israel Michael Oren ameimbia BBC kuwa tangazo la Rais Trump limeleifanya iwe siku ya furaha kwa kwa taifa la Israel ameseema mamlaka ya Israel ilitarajia vurugu kutoka kwa wapalestina.
Vurugu zaidi zinatarajia kuendelea hii leo huku kikao cha dharara baraza la usalama la umoja wa mataifa kinatarajiwa kutoa maamuzi mazito kuhusu tamko hilo la rais Donald Trump.

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Zijue Maana za 'TICK' Katika Mtandao wa Whats App

$
0
0
Mtandao wa kijamii wa WhatsApp umekuwa ni moja kati ya mitandao maarufu sana inayotumiwa na watu wengi duniani. Siyo vijana tu kama ilivyozoeleka kuwa ndiyo wapenzi wa mitandao ya kijamii, bali hata watu wazima na wazee.

WhatsApp imekuwa ikijitahidi kuborosha mtandao wake kadiri siku zinavyokwenda ili uweze kukidhi mahitaji ya watumiaji wake katika maeneo mbalimbali duniani.

Tangu mtandao huu ulipopata maboresho ambayo yanamwezesha mtumiaji kugundua kama ujumbe wake umefanikiwa kutumwa, umepokelewa na kusomwa na mpokeaji, jambo hili kwa baadhi ya watu limekuwa la kufurahisha huku wengine wakipata maudhi kutokana na kuona jumbe zao zimesomwa na hawajibiwi.

Wengine nao ili kuepuka adha hii, wamefikia uamuzi wa kuficha vema (ticks) zinazoonyesha kuwa ujumbe umesomwa.

Hizi hapa ni maana na vema (tick) katika mtandao wa whatasapp.

Unapotuma ujumbe kupitia ‘whatsApp’ ikitokea alama moja ya vema yenye rangi ya kijivu hiyo huwa na maana kuwa ujumbe wako umefanikiwa kwenda lakini bado haujamfikia mlengwa au mpokeaji.



Wakati mwingine unaweza kutuma ujumbe halafu ukaona alama kama ya duara, alama hiyo huwa inamaanisha kuwa ujumbe wako bado haujafanikiwa kutumwa na inawezekana ikawa ni ubovu wa mawasiliano au hauna kifurushi cha data kitakachokuwezesha kuutuma ujumbe huo.



Pale ambapo ujumbe utafika katika simu ya mpokeaji ile alama ya vema itabadilika na kuwa vema mbili za rangi ya kijivu.



Ujumbe unapoingia katika simu ya mpokeaji na kusomwa ama tu kufunguliwa, basi alama ile ya vema mbili hugeuka na kuwa ya rangi ya bluu.



Hapa kama uliyemtumia ujumbe hatokujibu, siyo kwamba hajaupata na kuusoma ujumbe wako, bali yawezekana hataki kukujibu au anafanya vitu vingine ambavyo vinamzuia yeye kukujibu kwa wakati huo.

Njia rahisi ya kuzisoma meseji za WhatsApp za mpenzi wako bila yeye kujua
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live


Latest Images