Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Mzee wa Miaka 85 Aliyepata Msamaa wa Rais Anene Haya

$
0
0
Mzee wa Miaka 85 Aliyepata Msamaa wa Rais  Anene Haya
Rais John Magufuli alishangaza wengi alipotaja jina la mfungwa aitwaye Mganga Matonya, mwenye umri wa miaka 85, wakati akitangaza msamaha kwa watu 61 waliohukumiwa kunyongwa na mmoja aliyekuwa na kifungo cha maisha.

Haikuwa kitu cha kawaida kwa mkuu wa nchi kutaja jina la mfungwa, lakini ni mwendelezo wa maajabu yaliyowahi kumkuta Matonya katika maisha yake ya gerezani. Mara ya kwanza alifutiwa adhabu ya kunyongwa hadi kufa na Rais wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere.

“Namshukuru sana  Rais Magufuli,” alisema Matonya alipoongea na mwandishi wetu jana akiwa kijijini kwake Wiliko mkoani Dodoma.

“Sikutegemea kama nitatoka gerezani. Naomba salamu zimfikie kwani sijui namna ya kuonana naye. Ningebahatika kuonana naye siku ile nilipotoka gerezani, ningemkumbatia kwa furaha.”

Matonya alipata taarifa za msamaha akiwa gereza la Kingolwira mkoani Morogoro, lakini awali alikuwa Gereza la Isanga mkoani Dodoma akiwa mahabusu baada ya kufanya kosa akiwa na umri wa miaka 39. Aliishi Isanga hadi Mei 10, 1980 wakati alipohukumiwa.

“Hakimu aliamuru ninyongwe mpaka kufa. Wakati nasubiri utekelezaji wa hatua hiyo mwaka 1984, rais wa  wakati huo, Julius Nyerere alinibadilishia adhabu kutoka kunyongwa hadi kifungo cha maisha,” alisema Matonya.

Baada ya kuhukumiwa kunyongwa, Matonya na mwenzake walisubiri kifo kwa miaka mitano, lakini mabadiliko ya tabia waliyoonyesha wakiwa gerezani yalishawishi wasimamizi wao wapendekeze majina yao ili wabadilishiwe adhabu.

Baada ya Rais Nyerere kuwapunguzia adhabu hiyo, wawili hao walihamishwa kutoka Gereza la Isanga mkoani Dodoma na kwenda Kingolwira mkoani Morogoro.

Anasema hakuwahi kufikiria kuwa kuna siku angetoka gerezani, zaidi ya kujipa matumani na kumuomba Mwenyezi Mungu amnusuru na adhabu ya kufia ndani ya kuta za majengo hayo.

Jana ilikuwa siku ya furaha kwa Matonya, familia yake, ndugu na wanakijiji wa Wiliko, kijiji ambacho kiko takriban kilomita 85 kutoka Dodoma Mjini.

Akizungumza na Mwananchi jana, Matonya alionyesha furaha, mwenye kutafuta maneno asijue la kusema zaidi ya shukrani nyingi kwa Rais Magufuli kwa uamuzi wake wa kumsamehe adhabu ambayo ni nadra kunusurika isipokuwa kwa kushindana kisheria.

“Natamani kuonana na Rais Magufuli na kuongea naye mambo mbalimbali, lakini sina uwezo,” alisema Matonya.

“Lakini kupitia gazeti hili naamini ujumbe utamfikia. Kwa kweli, namshukuru sana kwa hili.”

Pamoja na Rais kumtaja jina, Matonya anasena hakuwa anafahamu lolote kuhusu msamaha huo.

“Taarifa zilinifikia ghafla,” alisema.

“Siku hiyo nilikuwa nimepumzika gerezani na wenzangu walikuwa wanaangalia televisheni. Mara nikasikia wenzangu wakiniita. ‘Mzee Matonya, Mzee Matonya. Njoo uone huku jina lako limetajwa na Rais Magufuli kuwa umeachiwa huru’.

“Sikuamini na sikula chakula kwa furaha niliyokuwa nayo.”

Kosa mpaka kufungwa

Matonya na mwenzake anayeitwa Myeya Nyagalo walikamatwa Oktoba 1974 wakati walipoenda kuuza ng’ombe wa wizi kwenye mnada katika Kijiji cha Nyang’oro kilichopo kati ya Iringa na Dodoma. Walikuwa wamemuua mwenye mifugo hiyo kwa mkuki wakati wakiiba na hivyo walikuwa wanasakwa hadi walipoibuka mnadani.

Matonya na Nyagalo walikuwa miongoni mwa watu 12 walioorodheshwa kuwa walihusika katika mauaji hayo.

Akikumbuka tukio hilo, Matonya alisema wakati huo alikuwa kijana na mwenye tabia ya wizi wa mifugo.

Anasema siku alipofanya kosa hilo, alikuwa na Nyagalo na vijana wengine wawili wa kabila la Kimasai walioshirikiana kuiba ng’ombe hao.

“Tuliandaa mpango wa kujiongezea mifugo. Baada ya kujiridhisha wapi tunaenda kuiba mifugo hiyo, tuliamua kwenda,” alisema Matonya.

“Haikuwa mara yetu ya kwanza. tulishafanya matukio kama hayo maeneo mengine. Lakini, kwa hili, arobaini za mwizi zilikuwa zimefika. Tulipata upinzani mkubwa uliosababisha mapigano na kifo cha mwenye mali.

“Mimi na mwenzangu Nyagalo hatukufahamu kama mtu yule amefariki. Tulijua tumemjeruhi tu.”

Alisema wenzao walifahamu kwamba mwenye mali hangepona. Alisema tofauti na matukio ya awali, wenzao walitaka wagawane mifugo waliyoiba na kila mmoja ashike njia zake.

“Tulishangaa, lakini mwisho wa siku tuligawana, tukaachana,” alisema.

Alisema baada ya muda hawakuwa na njia nyingine zaidi ya kupeleka mifugo mnadani kuiuza bila kujali kama Jeshi la Polisi lilikuwa linawatafuta. Ndio maana walikamatwa kirahisi.

Familia ya Matonya

Leo hii, Matonya amerejea mtaani ambako ana watoto sita, wajukuu 33 na vitukuu ambao idadi yake haikuweza kupatikana mara moja. Lakini alimuacha mkewe akiwa na watoto wawili na ujauzito wa miezi nane, hivyo watoto waliozaliwa wakati akiwa jela wanahesabika kuwa wake.

Kama ilivyokuwa kwa Nguza Mbangu Vicking na mwanae Papii Kocha waliotoka gerezani saa chache baada ya kutangaziwa msamaha, ndivyo ilivyokuwa kwa Matonya na mwenzake waliotoka gerezani juzi.

Mzee Matonya alisema anaangalia uwezekano wa kujikita kwenye kilimo, shughuli aliyokuwa akiifanya kabla ya kuhukumiwa, lakini anasema umri ushaenda.

Baada ya kuishi gerezani mwezi mmoja, alizaliwa mtoto ambaye mkewe alimuita Aron (45) ambaye akiwa shule ya msingi, alikuwa akipokea barua za baba yake kutoka kwa wafungwa waliokuwa wanamaliza kutumikia adhabu zao au mahabusu walioshinda kesi.

Aron ambaye kwa sasa ni baba wa watoto wanne na wajukuu, alisema alijisikia furaha baada ya kupata taarifa za kuachiwa kwa baba yake kwa kuwa hakuamini kama angekuwa huru tena.

“Tulikataa tamaa kama Mzee angetoka gerezani,” alisema Aron.

“Niliwahi kwenda kumuona mara nne na mwisho ilikuwa ni mwaka 2014. Ninapozungumza naye. Najisikia furaha iliyopitiliza. Kila mtu hapa kijijini haamini kilichotokea,” alisema Aron.

Baada ya kuongezeka kwa mzee wao, Aron anasema watu hawakauki nyumbani kwao kwa kuwa kila mtu anataka kumuona na kumshika mkono. Hapo nyumbani, anasema watu hawalali, wanashangilia huku wengine wakifanya maombi  ya kumshukuru Mungu na Rais Magufuli aliyempa msahama.

           

Shamsa Ford Amfunda Shilole "Kuwa Mke Bora kwa Mumeo Ustar Weka Pembeni"

$
0
0
Shamsa Ford Amfunda Shilole "Kuwa Mke Bora kwa Mumeo Ustar Weka Pembeni"
STAA wa Filamu nchini, Shamsa Ford amefungukia uamuzi wa msanii mwenzake wa Muziki, Zuwena Mohammed maarufu kama Shilole kwa kuamua kufunga ndoa tena ya Kidini na mpenzi wake, Uchebe ndoa iliyoshuhudiwa hivi karibuni na kutikisa kwenye mitandao na vyombo vya habari huku ikiwaacha midomo wazi kwa wale walidhani kuwa angerudiana na mpenzi wake wa zamani, Nuh Mziwanda.
Shamsa ambaye pia alifunga ndoa mwaka huu na mpenzi wake, Chidi Mapenzi ametumia ukurasa wake wa Instagram kumsihi Shilole atulie, aweke umaarufu pembeni, aitunze ndoa yake na hatimaye atafaidi matunda ya ndoa iliyo bora.
Shamsa ameandika;
“Hongera sana mamy. Umefanya maamuzi sahihi ya kumpendeza Mwenyezi Mungu.Cha muhimu uwe mke bora wa Kitanzania kwa mumeo na ustar uweke pembeni.
“Mumuweke Mungu mbele, uvumilivu na kuheshimiana inshaallah mtazikana.Karibu kwenye Chama mama….Sasa nyie mnao subili matajiri wawaoe wakati hao matajiri wana wake zao wameanza nao moja mtasubili sana mpaka uso uote sugu.Uzuri na Ustar una mwisho wake. Iitafika muda hata inzi hakusogelei……HONGERA MAMA @shilolekiuno_badgirlshishi,” ameadika Shamsa.


Msagasumu Awakata Ngebe Wanawake Wanaomshobokea " Nina Mke Wangu Acheni Shobo"

$
0
0
Msagasumu Awakata Ngebe Wanawake Wanaomshobokea " Nina Mke Wangu Acheni Shobo"
NGULI wa Muziki wa Singeli, Selemani Jabir ‘Msaga Sumu’, amewakata ngebe wanawake ambao wamekuwa wakimshobokea wakati yeye ana mke na watoto wawili.

Akizungumza na Full Shangwe, Msaga Sumu anayebamba na Ngoma ya Mwanaume Mashine alisema kuwa hana mpango na wanawake wanaomshobokea na haitakuja kutokea kwani ana ndoa yake anayoipenda.

“Imekuwa kero sasa, ninachoweza kuwaambia ni kwamba wanawake waache kunishobokea, Kwanza watambue kuwa ninaipenda familia yangu na kwa sasa ninatimiza miaka nane ya ndoa yangu, na nina watoto wawili, inshallah Mungu kanijalia,”alisema Msaga Sumu na kuongeza;

“Kwa sasa najipanga kuzindua rasmi Mwanaume Mashine ndani ya Dar Live hivyo soon nitatangaza.

Ukawa Wasusia Jimbo la Nyalandu

$
0
0
Ukawa Wasusia Jimbo la Nyalandu
VYAMA vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vimetishia kutoshiriki uchaguzi mdogo wa ubunge katika majimbo matatu, likiwamo la Singida Kaskazini la aliyekuwa mwakilishi Lazaro Nyalandu, endapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) haitotangaza kuuahirisha na kuupangia tarehe nyingine.

Hata hivyo, tume hiyo imesema itaendelea kutekeleza majukumu yake ikibainisha kuwa katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya kikatiba, haitalazimika kufuata amri au maagizo ya mtu yeyote au idara yoyote ya serikali au maoni ya chama chochote cha siasa.

Nyalandu, waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii, alitangaza kuachia ubunge wa Sindiga Kaskazini na kuihama CCM Oktoba 30, mwaka huu kisha kujiunga na Chadema kutokana na kile alichodai kutoridhishwa na mwenendo wa sasa wa chama tawala.

Ukawa umeitaka tume hiyo kuusogeza mbele uchaguzi huo ili kwanza kuwe na majadiliano baina ya tume, vyama vya siasa na wadau wengine wa uchaguzi kuepuka ilichodai kasoro zilizojitokeza wakati wa uchaguzi mdogo wa madiwani wa kata 43 uliofanyika Novemba 26, mwaka huu.

Umoja huo unaundwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chama cha Wananchi (CUF), NCCR-Mageuzi na NLD.

Hata hivyo, CUF kwa sasa imegawanyika katika makundi mawili - moja likimuunga mkono Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba na jingine likiwa upande wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad.

Mapema mwezi huu, Makamu Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Hamid Mahmoud Hamid, alitangaza kuwa uchaguzi mdogo katika majimbo matatu ya Singida Kaskazini, Longido na Songea Mjini, na kata sita za Tanzania Bara utafanyika Januari 13.

Hata hivyo, zikiwa zimebaki siku 32 kabla ya kufanyika kwake, Ukawa jana ulitangaza tishio la kutoshirika katika uchaguzi huo endapo NEC haitauahirisha na kupanga tarehe nyingine na pia kutoa nafasi kwa vyama vyote na wadau husika kukaa pamoja kujadili na kuzipatia majibu "kasoro" zilijitokeza katika uchaguzi mdogo uliopita.

Ukawa umedai uchaguzi huo ambao chama tawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilitangazwa mshindi katika kata 42 kati ya 43 zilizoshindaniwa, haukuwa huru na wa haki hivyo kuna haja kuitishwa mkutano wa wadau kutatua changamoto zilizojitokeza wakati wa uchaguzi huo na kuzitafutia utatuzi kabla ya kuingia kwenye uchaguzi mwingine.

Wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, viongozi wa Ukawa walidai tayari wameshaiandikia barua NEC kuomba uchaguzi huo usogezwe mbele inagawa bado hawajajibiwa, hata hivyo.

Katika mkutano huo na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Ukawa, Freeman Mbowe, akizungumza kwa niaba ya viongozi wenzake, alibainisha mambo kadhaa ambayo yamewalazimu waombe uchaguzi huo usogezwe mbele ikiwa ni pamoja na kutangaza uchaguzi katika Jimbo la Longido ilhali bado kuna kesi kwenye Mahakama ya Rufani inayolihusu.

"Jimbo la Longido Kaskazini kwa mujibu wa sheria za uchaguzi haliko wazi," Mbowe alisema, "bado halijaiva kwa ajili ya uchaguzi kwa sababu rufani yake bado iko mahakama ya rufani na imekatwa kwa kufuata utaratibu, inakuwaje utangaze uchaguzi wakati rufani imekatwa?"

Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Taifa na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alisema sababu ya pili ni kasoro zilizojitokeza katika uchaguzi mdogo katika kata 43 mwezi uliopita, akidai kuwa pamoja na mambo mengine, NEC ilishindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kusababisha uchaguzi huo kutokuwa huru na wa haki.

Mbowe alisema sababu ya tatu iliyoulazimu Ukawa kuomba kusogezwa mbele kwa uchaguzi mdogo wa majimbo matatu ni kutumika kwa nguvu kubwa ya vyombo vya dola katika uchaguzi mdogo uliopita, huku wanachama, viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na wabunge wakikamatwa ovyo.

“Tumeona umwagaji wa damu katika uchaguzi huo mdogo na mambo hayo yanafanyika ikiwamo kwa kutumia silaha za asili na za moto," Mbowe alisema na kueleza zaidi:

"Tumeona viongozi wa mikoa wakifanya kampeni na wakati mwingine kuwaamrisha polisi nini cha kufanya katika uchaguzi huo japokuwa hawaruhusiwi kufanya hivyo, wasimamizi wa uchaguzi nao hawakubaki nyuma, Nec wamejidhihirisha kushindwa kutekeleza wajibu wao.

“Katika nchi hii tukiendelea tunavyoendelea, hakuna uchaguzi utakaofanyika kwa kufuata sheria na kanuni zilizopo. Mazingira ambayo sheria haziheshimiwi, tukishajenga tabia hiyo hakutakuwa tena na uchaguzi huru."

'Kigogo' huyo wa Ukawa alidai kukimbia moja kwa moja kwenda katika uchaguzi katika mazingira hayo kunaweza kuleta mpasuko na pia umoja huo ukifanya hivyo, hautakuwa unalitendea haki taifa.

“Kwa mantiki hiyo, uchaguzi huo unastahili kuahirishwa," Mbowe alisema, "ni rai yetu kwa serikali na NEC kuona umuhimu wa kuahirisha kwanza uchaguzi huo ili wadau mbalimbali wa vyama vya siasa na washiriki wa shughuli hizo, kutafakari wamepata funzo gani katika uchaguzi wa kata 43.

"Kuna mazingira gani ya kufanya siasa katika nchi  yetu inayotupa 'justification‘ (uhalali) ya kwenda kwenye kufanya chaguzi, kuendelea kushiriki chaguzi za kuumiza watu, kufunga watu, za kuvunja amani, hazitujengi kama taifa isipokuwa tunaongeza mpasuko na ufa kati yetu.

“Kwa sisi, rai yetu kama viongozi wakuu wa kitaifa wa Ukawa ni kwamba, muda uliotolewa na kutangazwa uchaguzi huu bila kufanya ‘consultation’ (majadiliano) na vyama vya siasa japo NEC wanaweza kujitetea kwamba sheria inawapa mamlaka hayo, lakini tunaamini kwa upande wa pili uongozi ni pamoja na kusoma ‘between the line’ (kutafakari kwa makini) kwamba kuna viashiria vyote vya kupoteza amani katika taifa.

"Kwa hiyo, tunaiomba serikali chaguzi hizi zisogezwe mbele, wadau tukae kwanza, vyama vya siasa na wadau wengine tukae tuzungumze. Hivi kweli tumechagua uchaguzi ukawe ni wa mapanga, visu na rungu? Hivi kweli tumekubaliana kwamba mawakala watolewe vituoni?

“Na tukishakubaliana juu ya haya, maadili na kwanini yalikiukwa? Kwa sababu si kila jambo lazima liende mahakamani japo wao wanasema mkiona hamjaridhika muende mahakamani, ila wakumbuke kwamba mahakamani pia ni kuchelewesha haki na mambo ya kisiasa hayako hivyo.

"Ni vema wakaangalia namna uchaguzi huu uahirishwe ili wahusika wakae na kutafakari tulikotoka na tuliko na tunakotaka kwenda, kama Tume na serikali itapuuza rai yetu, sisi kama umoja wetu wa vyama hivi hatutakuwa tayari kushiriki uchaguzi huo."

Katibu Mkuu wa NLD, Toz Matwanga, aliyekuwa amefuatana na Mbowe kwenye mkutano huo, alisema sheria inavipa haki vyama vya siasa vyote kufanya siasa kwa amani, hivyo kuvinyima haki hiyo ni kosa.

Katika mkutano huo, mbali na Matwanga, Mbowe pia alifuatana na viongozi wa NCCR-Mageuzi na CUF kutoka upande wa Maalim Self.

MTU YEYOTENipashe ilimtafuta kwa simu Mkurugenzi wa Uchaguzi Ramadhan Kailima ambaye hakutaka kupokea simu, lakini akaomba atumiwe ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) na mwandishi.

Baada ya kutumiwa ujumbe juu ya ombi la Ukawa, Mkurugenzi huyo alimtaka mwandishi asome Ibara ya 74(11) cha Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977.

Kwa mujibu wa katiba hiyo, kifungu hicho kinasema: "Katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii, Tume ya Uchaguzi haitalazimika kufuata amri au maagizo ya mtu yeyote au idara yoyote ya serikali, au maoni ya chama chochote cha siasa".

Vilevile, katika majibu yake kwa njia ya SMS, mkurugenzi huyo alisema NEC huzingatia matakwa ya kifungu cha 37(1)(b) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura ya 343.

Kifungu hicho kinasema: "Unapotokea uchaguzi mdogo, tume itafanya uteuzi wa kujaza nafasi hizo si chini ya siku 20 na si zaidi ya siku 50 tangu nafasi hiyo kuwa wazi".

Katika ufafanuzi huo, Kailima pia alieleza Kifungu cha 46(2) cha Sheria ya Uchaguzi kinasema kampeni za uchaguzi mdogo zifanyike si zaidi ya siku 30.

"Ibara hiyo na vifungu hivyo, havijabadilika," alisisitiza mkurugenzi huyo.


Maneno ya Haji Manara Baada ya Kilimanjaro Stars Kufungwa "Tumerogwa na Nani? Wapi Tunakosea Kama Nchi?”

$
0
0
Maneno ya Haji Manara Baada ya Kilimanjaro Stars Kufungwa "Tumerogwa na Nani? Wapi Tunakosea Kama Nchi?”
Timu ya taifa ya Tanzania bara maarufu kama Kilimanjaro Stars iliyopo nchini Kenya katika michuano ya Kombe la CECAFA Senior Challenge Cup leo imecheza mchezo wake wa kukamilisha ratiba wa michuano hiyo dhidi ya timu ya taifa ya Kenya ambao ndio wenyeji wa michuano hiyo.

Kilimanjaro Stars leo imepoteza kwa goli 1-0 dhidi ya Kenya ikiwa ni mchezo wake wa tatu kupoteza wa hatua ya makundi katika michezo yake minne ikiwa imeambulia sare mchezo mmoja dhidi ya Libya katika mchezo wao wa kwanza.



Afisa habari wa Simba Haji Manara ni miongoni mwa watanzania ambao hawajafurahishwa na matokeo na perfomence ya Kilimanjaro iliyoionesha katika michuano ya Challenge msimu huu na katika ukurasa wake wa instagram akaamua kuandika hivi.

“Why always us?tumerogwa na nani?wapi tunakosea kama nchi?hatuna talents au programs?nn tufanye ili tuepuke fedheha hz?Serikali, TFF vilabu na wadau wote lazma tutafute suluhisho la aibu hii @harrisonmwakyembe @tanfootball @azamtvtz”>>> Haji Manara

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670 

Hili ndilo Kombora jipya la korea Kaskazini Linaloweza Kuitandika Marekani

$
0
0
Korea Kaskazini imetoa picha za jaribio la kombora lake jipya ambalo inadai kuwa linaweza kushambulia popote pale nchini Marekani.

Picha hizo zinaonyesha kiongozi wa Korea Kaskazini Ki Jong un na maafisa wengine kadha ya ngazi za juu jeshini wakisherehekea kombora la Hwasong-15 wakati likipaa.

Wengi wameshangazwa na ukubwa wa kombora hilo. Picha hii ambayo haijulikanai ilichukuliwa lini na iliyotolewa na vyombo vya habari vya taifa inaonyesha Kim akilikagua kombora hilo.

Michael Duitsman, mtafiti katika kituo kimoja alisema kuwa kombora hilo ni kubwa kuliko kombora la kwanza la Hwasong-14 "ni nchi chache tu zinaweza kuunda kombora kama hilo na Korea Kaskazini imejiunga nazo."

Pia linaonekana kuwa na kichwa kikubwa ikimaanisha kuwa linaweza kubeba bomu zito la nyuklia kwenye kichwa chake.

Yote haya yanaashiria kuwa kombora hilo lina uwezo kwa kusafirisha bomu la nyuklia kwa muda mrefu.

Lilisherehekewa kwa sigara

Kim mwenye furaha anaonekana akicheka kwa furaha  wakati kombora hilo linapaa. Linaaminiwa kuwa kombora la kwanza la Korea Kaskazini lililopaa mbali zaidi katika kilomita 4,475.

Bw Kim na wenzake walionekana wakisherehekea  mafanikio ya jaribio hilo kwa sigara.

Credit: BBC

Kufa Kimuziki Kwa Baraka Da Prince Wapi Alikosea?

$
0
0
Habari wakuu,

Kufa kimuziki kwa Baraka da prince wap alikosea?

Kama nlivyotangulia hapo awali swala la anguko la baraka kimuzik alilisababisha mwenyewe kwa haya machache ambayo aliyafanya;-

1. Ku-side team kati ya upande wa kiba na diamond, hii ilikua ishara mbaya sana kwake kwa siku za usoni, kwan msanii wa level zake hakupaswa kuwagawa mashabiki zake..
Badala yake hakupaswa kujionyesha wazwaz yuko upande gan ijapokua kikawaida ilikua inajulikana yuko upande wa kiba kwa kua walikua 'lebel mates'
Lakini kitendo cha kujinasibu hadharan kupitia mitandao ya kijamii ndo alikua anapanda mbegu ya anguko lake pasi na kujua.

2. Kupishana na upande wa team ambayo alikua anachezea..
yan kuznguana na kiba pamoja na rockstar kwa ujumla, mbegu nyingne akaotesha kwenye mgongo wa dunia..
Kwan pale awali wakat yuko upande wa kiba team diamond karibia wote hawakua wakimpenda so, ni kama alikua na mashabik wa upande wa kiba plus wale ambao hawana team..
Hivyo kitendo cha kukorofishana na kina kiba kukamfanya apoteze kotekote'

Yaani neither team Diamond nor team Kiba..na ukiacha hao jamaa wawili mashabiki wanaobak kimuziki hawana nguvu sana kwan muzik wa sasa ni wa promotions sana na mashabiki wa hzo team mbili wako vzur kwenye hilo (hapo nazungumzia mitandao ya kijamii) na bila trending ya kwenye social media muzik wa leo hutoboi.

3. Hili swala la tatu ndo lililompa sana baraka kiburi..
Alikua anaamini sana kuwa ukiwa na kipaji hakuna atakaekusumbua..so kipaji chake ndo kilichomfanya avimbe (bila shaka ni kweli he's talented) tena sana..
Akasahau kua:-

Bongo hatu-HIT kwa vipaji
Bali nani anabeba FLASH ya singo yako kupeleka kwenye Media houses.
Lakini pia hakujua kama mashabiki wanalamishwa kuamin flan anafanya muzik mzur hata kama siyo kweli na mifano tunayo tena hai kabisa..

Na laiti kama wananchi ndo wangekua waamuzi wa kuwaweka kileleni wasanii wenye talanta basi mtu kama Belle9, Rubby, mayunga na wengine kibao wasingepotea..

Yawezekana hayo yote hakuyajua' mfano saiz katoa nyimbo zaidi ya moja lakini zmepotelea studio2 "sometimes" ni bonge la wimbo ambao hauna hata miezI miwili lakini umepotea kwenye mzunguko..

Karibu umshauri huyu kijana kipaji kisipotee huku kinaonekana..

Nini afanye..

By Limited Edition

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Afande Sele Atoa Kauli Nzito Kwa Mrisho Mpoto ‘Ulistahili Kupigwa Risasi Tano Kichwani’

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Afande Sele amemvaa vikali msanii mwenzie, Mrisho Mpoto kufuatia madai kuwa alihusika kutoa baadhi ya wasanii katika wimbo maalum uliotungwa kwa ajili ya uzalendo na kumuweka Christian Bella wakati si raia wa Tanzania.

Afande Sele amedai kitendo hicho ni kuwakosea heshima wasanii wa Tanzania na Watanzania wenyewe. Msikilize hapo chini akifunguka zaidi pia Mrisho ajibu.

VIDEO:

Punguza Unene na Kutibu Magonjwa Kwa Kutumia Dawa za Edmark...Bonyeza Hapa

$
0
0
TUNA DAWA AMBAZO NI VIRUTUBISHO NA CHAKULA MBADALA ZIMEHAKIKIWA NA TFDA

Ni uhakika kwa afya yako, kupunguza uzito na Sumu mwilini, Mafuta/Sehemu Mbaya, Kitambi na Nyama Uzembe na kutibu MAGONJWA Mbali mbali yaliyoshindikana

Loose Weight Trainer ni Msaada wako Wasiliana Nasi Kwa WhatsApp 0713 777 470

Upate Suluhisho la Afya yako Bila Madhara pia unaweza kujiunga nami ili ufanye Biashara hii Nicheki


Intagram napatikana kwa jina @looseweight_trainer

Nyalandu Amtumia Rais Magufuli Ujumbe Huu

$
0
0
Nyalandu Amtumia Rais Magufuli Ujumbe Huu
ALIYEKUWA Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, lazaro Nyalandu, jana Disemba 11, 2017 alituma salamu za pole kwa Rais na Amri Jeshi Mkuu, Dkt. John Pombe Magufuli kufuatia vifo vya askari 14 wa JWTZ waliouawa nchini DR Congo walikokuwa wakilinda amani.

Nyalandu alitumia ukurasa wake wa Facebook kutuma salamu zake za pole kwa Rais Magufuli na familia za askari hao waliouwawa na wale waliojeruhiwa katika mapigano makali yaliyotokea nchini humo Disemba 7 na 8 kati ya askari wa Tanzania na Waasi wa Allied Democratic Forces (ADF) yaliyopelekea askari hao 14 wa Tanzania kupoteza maisha huku wengine 44 wakiwa wamejeruhiwa na wawili wengine kutojulikana walipo.

“Natoa pole kwa Mhe. Rais Magufuli na wanafamilia wote kufuatia kuuawa kwa maaskari 14 wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)” alindika Nyalandu.

Miili ya wanajeshi hao iliwasili jijini Dar es Salaam jana kwa ndege maalum ya Umoja wa Mataifa, ambapo ilipelekwa kwenye Hospitali ya Jeshi Lugalo kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi ambapo Desemba 14 itaagwa.
Taarifa ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dkt. Augustine Mahiga akihojiwa na moja ya vituo vya redio alisema askari wote waliokuwa hawaonekani wamepatikana na uchunguzi unaendelea kwani inaonyesha mmoja wao kama alikuwa ameshikiliwa mateka.

Msigwa Awavaa Viongozi wa CCM

$
0
0
Msigwa Awavaa Viongozi wa CCM
Mbunge wa Iringa Mjini  CHADEMA, Peter Msigwa amewavaa baadhi ya viongozi wa CCM ambao wamekuwa wakisema upinzani Tanzania unakufa na kuwahoji kuwa endapo upinzani ukifa ndiyo maendeleo ya nchi yatapatikana.

Msigwa amesema hayo jana kupitia ukurasa wake wa Facebook baada ya juzi baadhi ya viongozi wa CCM waliokuwepo kwenye Mkutano Mkuu UVCCM wa 9 ambao ulifanyika mjini Dodoma Disemba 10, 2017 ambapo wapo baadhi ya wanachama na viongozi wa chama hicho walikuwa wakisema kuwa kwa sasa upinzani nchini unakufa.
"Mkutano wa UVCCM ulibebwa na kibwagizo cha upinzani kuwa unakufa ! Fine, tukubaliane kuwa upinzani unakufa! Ukifa upinzani zitaongezeka ajira ngapi! Umaskini utapungua kwa kiwango gani? Haki za binadamu zitalindwa kwa kiwango gani? Utawala bora utaimarika kwa kiwango gani ? Demokrasia itaimarishwa kwa kiwango gani? Uhuru wa kutoa mawazo na vyombo vya habari utaimarika kwa kiwango gani! Haya yote hayana chama! Nilitegemea CCM mje na majibu ya haya sio upinzani unakufa" alisisitiza Msigwa

Bright Aonyesha Hisia Zake kwa Vanessa Mdee "Kumpenda Siyo Dhambi"

$
0
0
Bright Aonyesha Hisia Zake kwa Vanessa Mdee "Kumpenda Siyo Dhambi"
Baada ya hapo awali Bright kueleza hisia zake kwa Vanessa Mdee kisha kufuatia ukimya, Bright amejibu kinachoendelea.

Muimbaji huyo amesema mipango yake kwa Vanessa ameisitisha kwanza kwa sababu anahitaji kujikita zaidi katika muziki wake.

“Sasa hivi sifirii hicho kitu lakini watu wanasema unaweza ukafa na dream, kwa hiyo kwangu mimi kumpenda mtu siyo dhambi. Wazo lipo lakini sasa hivi nime-keep busy kwenye muziki, Bright anatakiwa akue, afanye kolabo za kimataifa” amesema.

“Tushaonana na tunapiga story kawaida, hatujawahi kuzungumzia mapenzi tunaongea ishu za kazi kwanza tu” Bright ameiambia Bongo5.

Shilole Amtolea Povu Dada Yake " Hakutaka Mimi Niolewe Sijui Ananiona Mimi Bado Bikra"

$
0
0
Shilole Amtolea Povu Dada Yake " Hakutaka Mimi Niolewe Sijui Ananiona Mimi Bado Bikra"
Mwimbaji wa Bongofleva Shilole amefunguka kwa  mara ya kwanza toka alipofunga ndoa na Uchebe ambapo moja ya vitu alivyozungumzia ni dada yake kutotaka yeye aolewe.

Shilole amesema “Dada yangu hakukubali mimi niolewe na nilimwambia nimefika muda wa kuolewa sijui ananiona Bikra mpaka leo, mimi nina maamuzi yangu, mimi mkubwa ujue nina watoto wawili alafu bado niamuliwe? nilimwambia nina mtu nampenda usinichagulie mtu wa kuwa nae“

Rais Magufuli Awanyooshea Kidole Ma- Video Qeen Wacheza Utupu

$
0
0
Rais Magufuli Awanyooshea Kidole Ma- Video Qeen Wacheza Utupu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amewataka watanzania kukemea vitendo vinavyodhihirisha mmomonyoko wa maadili, ikiwemo mabinti wanaocheza utupu kwenye video za muziki.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye mkutano wa Jumuiya ya Wazazi mjini Dodoma, na kusema kwamba huwa anashangazwa kila anapowasha Television kutazama muziki, na kukutana na mabinti wakicheza utupu huku wanaume wakiwa na mavazi ya staha, na kusema kwamba ni aibu kubwa kwa wazazi kuangalia mambo hayo.
“Mimi ni shabiki mzuri wa muziki, kila ukifungulia mziki wanaocheza utupu ni wanawake wanaume hapana., nyinyi kama jumuiya ya wazazi umefika wakati wa kukemea mambo haya, tunawafundisha nini watoto wetu, tunapenda mziki, lakini je, hiyo ndio muziki tunayocheza, tumeingiliwa na mdudu gani, saa nyingine unapoangalia TV na watoto wetu ni aibu kubwa, yanayofanyika pale ni aibu, si kwa sababu sitaki watu wastarehe, kama ni kwenye klabu kavue huko, lakini kwa nini uwavulie hata wasiohitaji kuona uc**? Tena kwa muda usio muafaka?”, amesema Rais Magufuli.
Rais Magufuli ameendelea kwa kuitaka jumuiya hiyo na watu wote kusimamia maadili, huku akivinyooshea mkono vyombo husika vinavyopaswa kushughulika na masuala ya utamaduni wa Mtanzania.
“Ifike mahali sisi kama watanzania, bila kujali vyama vyetu, tulinde maadili yetu, ninyi kama wazazi, sifahamu kama enzi za akina Fatma Karume au kina Maria Nyerere huo ndio ulikuwa mtindo, lakini nina uhakika enzi zile haikuwa hivyo, lakini vyombo vyetu vya habari, wasimamizi wa maadili haya wako wapi, wizara inayosimamia haya wako wapi, je, TCRA wako wapi, Niwaombe ndugu zangu Jumuiya ya wazazi kuikosoa hata serikali kwenye kusimamia maadili ya Tanzania”, amesema Rais Magufuli.

Mwana FA Afunguka A-Z Chanzo cha Beef Lake na J Dee

$
0
0
Mwana FA Afunguka A-Z Chanzo cha Beef Lake na J Dee
Msanii Mwana FA ambaye hivi karibuni amemaliza tofauti zake na msanii mwenzake lady Jaydee, ameweka wazi jibu la kitendawili ambacho wengi walikuwa wakijiuliza, juu ya chanzo cha ugomvi wao uliowapelekea kuwa mahasimu.

Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Mwana FA amesema chanzo kikubwa cha ugomvi wao ilikuwa ni kupangwa kwa show zao kwa siku moja, kitu ambacho kilionekana kumkwaza mmoja wapo.
“Sababu kubwa ilikuwa ni show yake na yangu zilianguka tarehe moja , nilikuwa na mipango ya show yangu na nilimwambia, hakuwa na neno, sasa mipango inavyoenda haiendi kwa kalenda yako inaenda kwa kalenda ya wadhamini, bahati mbaya Mangwea akafariki, wote tukaghairisha tukapeleka tarehe 31 na yeye na team yake wakasogeza mpaka 31, na wala haikupangwa kwa sababu yeye alipanga tarehe hiyo hiyo, mimi sikuona kitu kibaya kwa sababu Dar es salaam ina watu zaidi ya milioni 6, mimi nilikuwa nahitaji watu 400 tu nikaona haina tatizo, unajua tumeumbwa binadamu tuko tofauti tutachukulia ubaya, baada ya hapo maneno yakawa yameanza, ila hakukuwa na sababu nyingine zaidi ya hiyo”, amesema Mwana FA.
Kwa muda mrefu wasanii hao walikuwa hawapikiki chungu kimoja, huku wengi wakiwa wanajiuliza nini chanzo cha wawili hao kutoelewana ilhali walikuwa marafiki wakubwa wa kupika na kupakua, na kuja kumaliza tofauti zao mwaka huu.

Emmanuel Okwi Amgomea Mzambia Simba

$
0
0
Emmanuel Okwi Amgomea Mzambia Simba
Zikiwa zimebaki siku tatu kabla ya dirisha dogo la usajili kufungwa, Emmanuel Okwi ndiye mchezaji pekee katika kikosi cha Simba hajatikiswa na ujio wa mchezaji wa kigeni Jonas Sakuhawa kutoka Zambia.

Lakini, mshambuliaji John Bocco ‘Adebayor’ na Juma Luizio wanaweza kutikiswa na usajili wa Sakuwaha kutokana na nafasi zao wanazocheza.

Klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara zimeingia vitani kuwania saini za nyota wapya katika dirisha dogo la usajili lililofunguliwa Novemba 15 na linatarajiwa kufungwa Desemba 15.

Miongoni wa klabu hizo ni Simba ambayo inataka kuongeza mchezaji mmoja wa kigeni ambaye ni Sakuhawa aliyetua nchini hivi karibuni kumalizana na vigogo wa miamba hiyo ya soka nchini.

Usajili wa Mzambia huyo umekuwa gumzo kwa kuwa klabu hiyo italazimika kumtema mchezaji mmoja wa kigeni ili apate fursa ya kusajiliwa katika dirisha dogo.

Lakini, usajili wa Sakuwaha unaonekana kutokumtisha Okwi, raia wa Uganda ambaye ana uhakika wa kuendelea kupata namba katika kikosi cha kwanza chini ya kocha Joseph Omog.

Mabao manane aliyofunga Okwi kwenye Ligi Kuu yanamuweka salama na hatakuwa na presha kubwa ya kupoteza nafasi katika kikosi cha kwanza Simba mbele ya Mzambia huyo ambaye rekodi yake kwenye soka ya Afrika ni moto wa kuotea mbali.

Sakuwaha aliyetua nchini wiki iliyopita kufanya majaribio ya kujiunga na Simba, anaonekana kulikosha benchi la ufundi la timu hiyo ambalo kwa sasa linasimamiwa na kocha msaidizi Masoud Djuma ambaye anashika kwa muda mikoba ya Omog ambaye yupo kwenye mapumziko.

Katika mazoezi ya Simba yanayoendelea katika kipindi hiki cha mapumziko ya ligi, Sakuhawa ameonyesha kiwango bora katika kufunga, kutengeneza nafasi za mabao, kumiliki mpira na kupiga chenga. Mzambia huyo anabebwa na umbo la miraba minne jambo linalompa nafasi kubwa ya kuziba nafasi ya mshambuliaji Laudit Mavugo anayehusishwa na mpango wa kutimkia Gor Mahia ya Kenya.

“Nimemtazama vizuri Sakuhawa baada ya kumsimamia katika majaribio ambayo ameendelea kufanya. Binafsi nimeridhika na kiwango chake kwa sababu ana sifa zote ambazo mimi kama kocha ninazihitaji kuziona kwa mshambuliaji wa kati ambazo ni kufunga na kutengeneza nafasi.

Kama ningekuwa mimi ndiye mwenye mamlaka ya mwisho kumsajili, ningekuwa nimeshafanya hivyo lakini viongozi wangu ndio wenye mamlaka hayo hivyo ni vyema kusubiri uamuzi wao,” alisema Djuma katika mazoezi ya jana asubuhi Coco Beach, Dar es Salaam.

Endapo Sakuhawa atamwaga wino, nafasi za kina Bocco, Liuzio, Mohammed Ibrahim ‘Mo’, Shiza Kichuya na Nicholas Gyan na wanapaswa kukaza buti kwani huenda Mzambia huyo akapangua kikosi cha Simba ili kuingia kwenye kikosi cha kwanza endapo ataendeleza makali.

Bocco na Luizio wanaocheza nafasi ya mshambuliaji wa kati wako kwenye hatari zaidi kwani wamekuwa wakipoteza idadi kubwa ya nafasi za mabao katika mechi mbalimbali ambazo Simba walicheza hivyo huenda wakajikuta wanarithi nafasi ya Mavugo benchi na kumpisha Mzambia huyo anayeonekana sio mchezaji wa kuanzia benchi.

Kichuya na Gyan wanaoshambulia kutokea pembeni wanaweza kuathirika pia na ujio wa mshambuliaji huyo hasa pale Simba itakapoamua kutumia mfumo wa 4-3-3 au 4-2-3-1 kwa kuwa Sakuhawa anaweza kusimama kama mshambuliaji wa kati na Okwi kusogezwa pembeni ambako ndipo anacheza mara kwa mara.

Ibrahim anaonekana hayuko kwenye presha kubwa analindwa na uwezo wa kucheza nafasi tatu tofauti uwanjani, lakini ile anayoipendelea ya kucheza nyuma ya mshambuliaji wa kati katika mfumo wa 4-4-2 inaweza kuathirika kwa kuwa Omog na benchi lake la ufundi wanaweza kumrudisha Okwi kwenye nafasi hiyo na Sakuhawa akacheza namba tisa.

Sakuhawa mwenye miaka 34 ambaye ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na Zesco United ana uzoefu katika ligi tofauti za soka duniani.

Baada ya kutamba kwa miaka mitatu kwenye kikosi cha Zesco iliyomuibuka kuanzia 2006 hadi 2009, alicheza Ligi Kuu Ufaransa kwenye klabu ya Lorient aliyoichezea mechi 14 kuanzia 2009 hadi 2010 kabla ya kujiunga na Le Havre ambapo hakufanya vizuri akicheza mechi nne tu.

Mwaka 2011 alijiunga na El Merreikh ya Sudan aliyocheza mechi 33 na kufunga mabao 22, alidumu miaka miwili kabla ya kutua TP Mazembe Englebert aliyoifungia mabao 14 na baadaye mwaka 2014 alirejea Zesco United.

Akizungumzia usajili wa Sakuhawa, meneja wa Simba, Robert Richard alisema unasubiri ripoti ya kocha Omog.

“Kuna mahitaji ambayo kocha ameupatia uongozi ambayo ndio yatakayofanyiwa kazi, hivyo ndani ya kipindi hiki, kamati ya usajili itakutana kufanyia kazi ripoti.

Kama kapendekezwa atasajiliwa kama hajapendekezwa hatasajiliwa,” alisema Richard.

Rais Magufuli Aahidi Kulinza Alichokianzisha Nyerere "Nikifuta Jumuhiya ya Wazazi wa CCM Nitalaaniwa"

$
0
0
Rais Magufuli Aahidi Kulinza Alichokianzisha Nyerere "Nikifuta Jumuhiya ya Wazazi wa CCM Nitalaaniwa"
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema hawezi kuifuta Jumuiya ya wazazi ya Chama hicho katika kipindi chake cha kuwa Mwenyekiti.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati anafungua mkutano wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM ambao ni mwendelezo wa mikutano ya uchaguzi wa Jumuiya mbalimbali za Chama hicho.
“Jumuiya hii ilianza mwaka 1955 ikiwa inaitwa Tanganyika African Parent Associations (TAPA), na aliyeianzisha ni Baba wa taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na anafahamu kwanini ilianza nikiifuta nitakuwa nimekosa busara na nitalaaniwa”, amesema Rais Magufuli.
Aidha Rais Magufuli ameongeza kuwa “Napenda niwahakikishie Jumuiya hii itaendelea kusimama kama zilivyo Jumuiya zingine ndani ya Chama”, ameongeza.
Aidha Rais magufuli amesifu mafanikio mbalimbali ambayo yamekuwa yakifanywa na Jumuiya hiyo ikiwemo kumiliki shule mbalimbali pamoja na Chuo cha sanaa cha Kaole kilichopo Pwani. Mkutano huo unatarajiwa kufanya uchaguzi wa viongozi wa taifa.

Soma Nafasi za Kazi Mbali Mbali Zilizotangazwa Leo

Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images