Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live

Kaka wa Wa Lissu Kujibu Barua ya Bunge Kuhusu Stahiki za Lissu

$
0
0
Kaka wa Wa Lissu Kujibu Barua ya Bunge Kuhusu Stahiki za Lissu
Alute Mughwai,kaka wa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, amesema anatarajia kujibu barua iliyoandikwa kwake na Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai ikihoji stahiki ambazo chombo hicho kinapaswa kumpatia ndugu yake.

Akizungumza na MCL Digital, Mughwai amesema ameipata barua ambayo ataijibu na baadaye atazungumza na waandishi wa habari.

“Nilikuwa Nairobi (Kenya) ndiyo nimerejea, nitaijibu barua hiyo na nitaiwasilisha kabla ya Alhamisi halafu ndani ya siku mbili hizi nitawaeleza kila kitu kuhusu suala hilo na maendeleo ya afya ya Lissu,” amesema.

MCL Digital ilipotaka kujua ni stahiki zipi ambazo Bunge linataka kujua kwamba ndizo anazotakiwa  kupewa Lissu, Mughwai alijibu, “Hizo ndizo danadana ila nitawajibu.”

Katibu wa Bunge, Kagaigai alimwandikia barua Mughwai Novemba 27,2017 akimtaka alieleze ni stahiki zipi ambazo ndugu yao anastahili apewe na Bunge.

Kagaigai alieleza kuhusu barua hiyo siku mbili baada ya Lissu kuhoji sababu za Bunge kutojihusisha na matibabu yake tofauti na sheria zinavyotaka.

Lissu anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alikopelekwa tangu Septemba 7,2017 aliposhambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana akiwa ndani ya gari kwenye makazi yake eneo la Area D mjini Dodoma.

Kauli ya Lissu ilikuwa mwendelezo wa ya awali iliyotolewa na Mughwai aliyesema alishaiandikia ofisi ya Bunge kutaka ilipie gharama za matibabu ya mbunge huyo.

Katika mahojiano na Mwananchi hospitalini jijini Nairobi, Lissu alisema alimweleza Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan alipokwenda kumjulia hali kuwa, “Bunge liko wapi” kutokana na kutofanya juhudi za kwenda kumuona tangu alazwe.

Pia, alieleza kushangazwa na kitendo cha chombo hicho kutogharimia matibabu yake licha ya kuwa ni stahili yake kisheria iwe anatibiwa ndani au nje ya nchi.

NEC Yajibu Kauli ya Mbowe "NEC Haiwezi Kuahirisha Uchaguzi"

$
0
0
NEC Yajibu Kauli ya Mbowe "NEC Haiwezi Kuahirisha Uchaguzi"
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Kailima Ramadhani amesema chama cha siasa kutangaza kugomea uchaguzi hakuwezi kuifanya Tume iuahirishe kwa kuwa haiko kumshawishi mtu au chama kushiriki.

Akizungumza leo Jumanne Desemba 12,2017 jijini Dar es Salaam, Kailima amesema chama kushiriki uchaguzi ni jambo la hiari na NEC ipo kwa ajili ya kuweka na kutengeza mazingira yatakayofanya vyama vya siasa kushiriki uchaguzi.

Kailima katika taarifa iliyotolewa na NEC amesema iwapo kuna chama kitaamua kutoshiriki uchaguzi, kitakachoshiriki hata kama ni kimoja mgombea wake atapita bila kupingwa.

“Ikitokea vyama vikasusa vyote kushiriki kwenye uchaguzi hapo ndipo unaweza kuahirishwa kwa kuwa hakutakuwa na mgombea,” amesema alipozungumza na waandishi wa habari waliotaka ufafanuzi wa NEC kuhusu tamko lililotolewa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

Kailima ameviasa vyama vya siasa vinavyotishia kutoshiriki uchaguzi mdogo wa ubunge katika majimbo matatu na kata sita Januari 13,2018 kufuata mifumo ya kisheria ya kushughulikia malalamiko ya uchaguzi.

Juzi Mbowe alitishia kuwa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) havitashiriki uchaguzi iwapo changamoto zilizojitokeza wakati wa uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 43 Novemba 26,2017 hazitafanyiwa kazi na NEC.

Akizungumzia hoja hiyo, Kailima amesema katika orodha ya vyama vilivyopo NEC, Ukawa si moja ya vyama vya siasa.

“Niwasihi vyama vya siasa watumie mifumo iliyopo ya kawaida ya kuwasilisha malalamiko kwenye kamati za maadili; kujaza fomu namba 14 kabla ya kura kuanza kupigwa; fomu 16 wakati kura zinapigwa; na kuwasilisha malalamiko mahakamani baada ya kura kuhesabiwa,” amesema Kailima.

Amesema hiyo ndiyo mifumo iliyowekwa kisheria katika kushughulikia changamoto za uchaguzi zinapojitokeza na kuhoji wanayotaka wao ni ipi.

“Kama kuna mgombea hakuridhika mahakama zipo aende maana wamepewa siku 30 za kufungua kesi,” amesema.

Amesema NEC haiwezi kuahirisha uchaguzi kwa kuwa sheria inatamka kuwa uchaguzi unaweza kuahirishwa iwapo tu kuna mgombea amefariki; kutokuwepo mgombea; zikitokea ghasia na fujo au wagombea wakifungana kwa kura.

“Je kuna mgombea amefariki? Haya mambo yote manne hayajatokea, sasa tutaahirishaje uchaguzi?” amehoji Kailima.

Kuhusu jimbo la Longido ambalo Mbowe alidai shauri la uchaguzi bado liko mahakamani na wameiandikia NEC kuhusu suala hilo na barua kutojibiwa, Kailima amesema madai hayo si ya kweli kwa kuwa barua zote walizoandikiwa wamezijibu.

Amesema jimbo hilo liko wazi kwa kuwa Mahakama ndiyo imeiandikia NEC kuitaarifu kumalizika kwa kesi iliyokuwepo mahakamani.

Kailima amesema NEC itasimamisha uchaguzi wa jimbo hilo iwapo tu Mahakama itawaeleza wasimamishe mchakato huo.

“Nimesikitishwa na kauli kwamba eti wametuandikia barua sisi Tume ya kusimamisha uchaguzi wa Longido eti hatujawajibu. Tulipata barua kutoka kwa ole Nangole (Onesmo) tukamjibu, tukapata barua kwa wakili wa Ole Nangole nikamjibu; tukapata barua kutoka kwa katibu wa Chadema tukamjibu na nikaongea naye kwenye simu, sasa leo wanaposema hatujawajibu kwa kweli kauli hiyo imenisikitisha,” amesema.

Polisi Yachukua Magari Yake Yaliyokwama Bandarini

$
0
0
Polisi Yachukua Magari Yake Yaliyokwama Bandarini
Hatimaye magari 50 ya Jeshi la Polisi yalikuwa yamekwama Bandari ya Dar es Salaam tangu mwaka 2015 yamechukuliwa wiki iliyopita.

Novemba 26 mwaka huu, Rais John Magufuli alitembelea Bandari ya Dar es Salaam na kukuta magari ya polisi yakiwa yamekaa bandarini kwa muda mrefu wakati yalitakiwa kukaa hapo kwa siku 21.

Rais Magufuli alimwagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi, (IGP) Simon Sirro kuyachukua ili yakafanye kazi iliyokusudiwa.

Leo Jumanne, Msemaji wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Janeth Ruzagi amesema magari hayo yameshachukuliwa na polisi.

Alisema mamlaka hiyo na polisi wamefikia makubaliano na kuyachukua magari hayo na sasa yameshaondolewa bandarini.

Akizungumzia magari ya polisi, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa amesema ni kweli wameyachukua magari hayo.

Amesema walitii agizo la Rais na kufanya mazungumzo na bandari na sasa wameshayachukua kwa ajili ya kazi mbalimbali za polisi.

Pendeza na Kessy Products..Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Safi Kwa Products za Asilia Zisizo na Madhara

$
0
0

PENDEZA NA KESSY PRODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA* 🍇🌾🌳
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATAKS)KUNADAWA AINA TATU (@)JELI KUPAK_100,000/(B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI NA MAPAJAN_80,000/
5)TOA KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE NA MANYAM YOTE
@) DAW YA MAJINI_100,000/NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME BILA KUVAA SIDIRIA_80,000/
8)KUONGEZA MAZIWA NA SAIZI NZURI_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA (kifaru)_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO YAKAWAIDA NA UZAZ_80,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_70,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA KWA DAW(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MWLINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA JELI PAMOJA NA VIDONGE VYAAIN ZOT _100'000
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_ 120,000 /
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_80,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _80,000/
20)ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA MGUU_80,000/🍍🍉🌾 *TUNAPATIKAN DAR E SALAAM* *NAKWA *MIKOANKOTE* UTAPATA *PIA* *NA NCHI ZOTE PIGA CM* (+255)0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product*
*Delivery POPOTE ULIPO,*

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano yya Disemba 13

$
0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano yya Disemba 13

CCM yafuta mchakato wa kumpata mrithi wa Lazaro Nyalandu

Mbunge Wa CHADEMA Amkumbuka Kikwete.....Ni Baada ya Askofu Kanisa Katoliki Aliyetaka Katiba Mpya Kuhojiwa

$
0
0
Baada ya kuwepo kwa taarifa za kuhojiwa kwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenga, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, Severine Niwemugizi (61) na Idara ya Uhamiaji kuhusu uraia wake, Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche amesema utawala wa Rais Kikwete,makanisa yalisimama na kukosoa.

Heche amesema kwamba utawala wa Kikwete Kanisa lilisimama imara kukosoa mambo kadhaa  ya serikali na wala hakuwahi kushuhudia viongozi wa dini wakihojiwa na kususitiza kwamba watu wasimame imara kupinga kuporwa kwa uhuru

"Kanisa lilisimama imara kukosoa mambo kadhaa wakati wa utawala wa Kikwete, sikuona kiongozi anahojiwa uraia wake naamini ingekuwa kipindi hiki kanisa lingefutwa wangesema sio kanisa la Kitanzania, tusimame imara kupinga uhuru wetu kuporwa, hakuna alie salama" Heche.

Taarifa zinadai kwamba Askofu Niwemugizi alihojiwa mara 2 na Idara ya Uhamiaji kuhusiana na Uraia wake kati ya mwezi Novemba na Disemba

 “Mara ya kwanza niliitwa na kufika ofisi za uhamiaji Ngara, Novemba 28 na mara ya pili niliitwa Desemba 4.

“Niliombwa kibali kinachoniruhusu kuwa nchini, nikashangaa, nikasema mimi ni Mtanzania, nikaambiwa nilete document (nyaraka).

“Nilipeleka hati ya kusafiria, kitambulisho cha kupigia kura na cheti cha kuzaliwa, wakasema wataniita tena.

“Baada ya kuitwa mara ya pili, nilipewa fomu ya kujaza ambayo bado naendelea kuijaza hadi sasa.

“Waliniita tena wakasema bado wanataka kujiridhisha ndio maana wanataka nijaze fomu, ninaendelea kuifanyia kazi mpaka nitakapokuwa nimeikamilisha yote,” anasema Askofu Niwemugizi ambaye amewahi kuwa Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu wa Katoliki (TEC).

Mwishoni mwa mwezi Septemba , Askofu Niwemugizi alisema kuwa  imefika wakati nchi inahitaji kuwa na dira nzuri ambayo pia italetwa na Katiba Mpya .

Msemaji Mkuu Idara ya Uhamiaji, Mrakibu Ally Mtanda, amekiri askofu huyo kuhojiwa na kusema;

“Ni kweli anahojiwa na ofisi yetu ya Wilaya ya Ngara, ni suala tu la tuhuma si kwamba ni kweli au la, hivyo itakapothibitika basi itajulikana,” alisema Mtanda.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670 

Wakati Naoa Sikuwa na Uhakika na Uamuzi Wangu- Tunda Man

$
0
0
Wakati Naoa Sikuwa na Uhakika na Uamuzi Wangu- Tunda Man
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Tunda Man ambaye mwaka huu aliuaga ukapera, amesema alipofanya uamuzi wa kuoa hakuwa na uhakika na uamuzi huo, kwani alihisi kama mwanamke wake hana mapenzi ya dhati na yeye.

Tunda Man ameyasema hayo alipokuwa akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kusema kwamba kutokana na umaarufu alionao, alikuwa na mashaka iwapo mpenzi wake huyo alikuwa anampenda au alikuwa anafuata umaarufu.
“Kwenye kuoa nilikuwa mguu ndani mguu nje nikijuliza huyu anampenda nani, Tundaman au Khalid, baada ya kukaa naye ndio nimegundua anampenda Khalid na sio Tunda Man, nilikuwa sina uhakika kabisa na ile ndoa”, amesema Tunda Man.
Hivi sasa msanii huyo ameachia kazi mpya inayoitwa 'toto', ambaye mwenyewe amedai ni moja ya kazi bora ambazo amewahi kuzifanya tangu aanze muzik

Steve Nyerere Atokwa Povu Kisa Wema Kukutana na Makonda

$
0
0
Steve Nyerere Atokwa Povu Kisa Wema Kukutana na Makonda
Siku tatu baada ya muigizaji maarufu wa filamu, Wema Sepetu kumuangukia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, mchekeshaji nyota, Steve Mengere ‘Steve Nyerere’ amebwatuka vibaya kuhusiana na ishu hiyo.

Akizungumza na Risasi Mchanganyiko kwa njia ya simu juzi akiwa njiani kurejea Dar es Salaam akitokea Dodoma, msanii huyo anayedhaniwa kufanikisha kwa kiwango kikubwa kurejea CCM kwa Wema Sepetu, alikiri wawili hao kumaliza tofauti zao kwa njia ya amani, nyumbani kwa bosi huyo wa mkoa.

Wakiagana.
“Hakuna uadui wa kudumu katika haya maisha, isitoshe wale wote ni vijana, wamekutana wameombana msamaha na mambo yamebakia kuwa historia. Wanaangalia maisha mengine ya huko mbele kwa sababu safari bado ni ndefu,” alisema mchekeshaji huyo ambaye pia ni mmoja wa viongozi wa kundi linalohamasisha uzalendo kwa watanzania.

Kuhusu kama kuna ahadi yoyote iliyo nyuma ya makubaliano baina ya wawili hao ambao kabla ya kutofautiana wanaripotiwa kuwa marafiki, Steve alisema hakuna kitu chochote zaidi ya wao kuamua kuachana na mambo ya zamani na kufungua ukurasa mpya.

“Hili ni funzo kubwa sana kwa wapambe, hasa wasanii, watu wakikorofishana wawe na akiba ya maneno, kuna watu walikuwa wanatoa maneno ya ovyo kwa mkuu wa mkoa kupitia kwa Wema, sasa leo hawa wamepatana, hivi sura zao wanazipeleka wapi?

“Haya mambo ya maisha, ukiona kuna jambo limewatokea watu, ni vizuri mtu ukawa na kiasi cha maneno, au wengine walikuwa wanamponda Wema kwa kupitia kwa mkubwa, sasa leo hii wanajisikiaje?” alisema.

Alipoulizwa kuhusu kutoonekana kwa mama mzazi wa msanii huyo, Miriam Sepetu nyumbani kwake Sinza Mori, ikidaiwa kuwa huenda amefichwa sehemu kwa malengo maalum, Steve Nyerere alisema kada huyo wa Chadema yupo nyumbani kwake.

“Nani amekuambia mama hayupo? Yupo palepale nyumbani kwake na mambo yanaenda vizuri tu, wala watu hawana haja ya kumtafuta popote,” alisema Steve, akipinga habari za kutokuwepo nyumbani hapo kwa siku kadhaa sasa, ambako kumeripotiwa na magazeti ya Global Publishers.

Uhusiano wa Makonda na Wema uliingia dosari baada ya mkuu huyo wa mkoa kumtaja katika orodha ya kwanza ya watu wanaojihusisha na madawa ya kulevya, Februari mwaka huu.
STORI: Mwandishi Wetu, Risasi Mchanganyiko
Chanzo: Global Publishers

Bashe, Zitto Watoa Kauli Nzito Askofu Niwemugizi Kuhojiwa Uraia Wake

$
0
0
Bashe, Zitto Watoa Kauli Nzito Askofu Niwemugizi Kuhojiwa Uraia Wake
MBUNGE wa Nzega Mjini, Hussein Bashe ameelezwa kusikitishwa kwake baada ya Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge, Wilaya ya Ngara, mkoani Kagera, Severine Niwemugizi (61), kuhojiwa na Idara ya Uhamiaji kuhusiana na uraia wake.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Bashe ameandika;
I know how it feels unapo ambiwa AMA kuanza kujazishwa Fomu na kuhojiwa juu ya Uraia Wako its like kujazishwa fomu kuambiwa huyu sio Mama yako or Baba yako Pole Askofu Severine Niwemugizi wanaofanya haya hawana hata Khofu ya Mungu.



Askofu Niwemugizi aliehojiwa na Idara ya Uhamiaji kuhusiana na uraia wake kwa mara ya kwanza Novemba 28 mwaka huu na mara ya pili alihojiwa Desemba 4, mwaka huu.

Askofu Niwemuzi aliingia kwenye headlines baada ya kueleza kuwa serikali itoe kipaumbele kwa katiba mpya ya nchi ili iweze kukamilika.

Kwa upande wake Zitto ameandika;














Hashim Rungwe Atinga Nairobi Kumjulia Hali Tundu Lissu

$
0
0
Hashim Rungwe Atinga Nairobi Kumjulia Hali Tundu Lissu
Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Hashim Rungwe Spunda, amemtembelea na kumjulia hali mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu Hospitali Nairobi alikolazwa baada ya kushambuliwa kwa risasi nyumbani kwake Area D, Mjini Dodoma.

Akiwa Nairobi, Rungwe ambaye alikuwa miongoni mwa wagombea Urais Mwaka 2015, ametoa wito kwa Watanzania kuwa na moyo wa upendo huku akiliomba Jeshi la Polisi na vyombo vya Dola kufanya kila njia kuwapata waliomshambulia Lissu.

Lissu alikimbizwa katika hospitali hiyo baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 na watu wasiojulikana nyumbani kwake, Area D, Mjini Dodoma, Septemba 7 mwaka huu ambapo amefanyiwa upasuaji mara kadhaa na anaendelea na matibabu.

Babu Seya Apata Pigo Apata Msiba Mzito

$
0
0
Babu Seya Apata Pigo Apata Msiba Mzito
MUDA mfupi baada ya Babu Seya na Papii Kocha  kuachiwa huru kutokana na kupewa msamaha wa rais Magufuli, familia hiyo imepata pigo baada ya mdogo wa Babu Seya aitwaye Crizo Chimbukizi kufariki dunia. Kwa mujibu wa msemaji wa familia hiyo, King Kikii, Crizo alifariki dunia jana kutokana na mshtuko wa moyo baada ya kupewa taarifa ya kuachiliwa huru kwa wawili hao  na kwamba taratibu za mazishi zinafanywa.

Marehemu anatarajiwa kuzikwa mkoa wa Katanga Kongo nyumbani kwa familia ya Nguza.

Mume, Mke Wauawa Kikatili kwa Kukatwa na Mapanga Shingoni na Watu Wasiojulikana

$
0
0
Mume, Mke Wauawa Kikatili kwa Kukatwa na Mapanga Shingoni na Watu Wasiojulikana
Mume na mke wakazi wa kitongoji cha Kidogue wilayani Mkalama wamefariki dunia kwa madai ya kukatwa mapanga shingoni na kichwani na watu wasiojulikana.

Mauaji ya wanandoa hao, Kija Kitundu (53) na mkewe Mwajuma Ramadhan (59) yalitokea Desemba 10 saa sita usiku nyumbani kwao.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Debora Magiligimba alisema watoto wa wanandoa hao, Ramadhani (14) na Namagalu (12), wamepelekwa hospitali kwa matibabu baada ya kujeruhiwa katika tukio hilo.

Magiligimba alisema siku ya tukio wauaji hao walitumia ngazi kupanda juu ya paa la nyumba ya Kija kisha kuingia chumbani kwa wanandoa hao na kuwacharanga mapanga.

Alifafanua kuwa kabla ya tukio hilo, kuna mtu alikwenda nyumbani kwa Kija kuomba pampu lakini aliponyimbwa ndipo ugomvi ukaanza baina yao.

Hatima ya Scopion Kujulikana Mwakani Hukumu Yake Kusomwa Januari 10

$
0
0
Hatima ya Scopion KUjulikana Mwakani Hukumu Yake Kusomwa Januari 10
Kesi ya kumjeruhi mpaka kumtoboa macho kinyozi, Said Mrisho inayomkabili mwalimu wa sanaa ya kujihami, ‘Martial Arts’ na msanii wa filamu za kibongo, Salum Njwete maarufu Scorpion hatimaye imefikia tamati ambapo hukumu inatarajiwa kusomwa januari 10 mwakani.

Kesi hiyo iliendelea jana katika mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Ilala jijini Dar ambapo Scorpion alikuwa akibanwa maswali na wakili wa utetezi, Nassoro Katuga kufuatia utetezi wake alioutoa kipindi kilichopita akiongozwa na wakili wake, Juma Nassoro.

Katika utetezi wake wa awali Scorpion alisema alishurutishwa kutoa maelezo katika kituo cha polisi cha Buguruni ambapo wakili Katuga alimuuliza kwanini alisaini.

Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Flora Haule aliifunga kwa kuahidi kuitolea hukumu Januari 10 mwakani ambapo kabla ya hukumu hiyo kesi hiyo itatajwa tena mahakamani hapo Desemba 27 mwaka huu.

Anapoishi Gigy Maney Mmmh....... Hatare Tupu

$
0
0
Anapoishi Gigy Maney Mmmh....... Hatare Tupu
LICHA ya hivi karibuni kujinadi kuwa ametupia wigi la bei mbaya alilodai kulinunua kwa shilingi milioni sita, msanii wa Bongo Fleva anayefanya poa na ngoma yake ya Nampa Papa, Gift Stanford ‘Gigy Money’ anadaiwa kuishi kwenye nyumba ambayo haina hadhi ya hilo wigi hivyo kuibua miguno.

Kufuatia madai hayo, gazeti hili lilifika kwenye nyumba hiyo anayoishi Gigy maeneo ya Sinza-Kwaremi jijini Dar na kushuhudia inavyoonekana kwa nje kuwa haina hadhi, lakini kwa ndani ni bonge la nyumba.

Chanzo makini kilieleza kwamba, mwanadada huyo anaishi maeneo hayo kwenye nyumba hiyo yenye muonekano kama banda ambapo siyo hadhi yake, hali inayowashangaza wengi kutokana na umachachari wake hivyo kujiuliza inakuwaje ashindwe kuishi kwenye mjengo wenye hadhi yake.

“Yaani Gigy anaishi kwenye banda maana muonekano wa nyumba anayoishi kwa kweli unashangaza na hapa mtaani watu wamekuwa wakimsema sana na kumshangaa kwamba inakuwaje aishi hivyo wakati ni staa mkubwa ambaye anafanya shoo na kupata fedha?” kilihoji chanzo hicho.

Akizungumzia ishu hiyo katika mahojiano maalum na gazeti hili, Gigy alisema hawezi kuwakataza watu kuongea kwa sababu nyumba hiyo alijilipia kodi mwenyewe kwa mapenzi yake na wala hakulazimishwa na mtu.

“Ninawashangaa sana watu wanavyochonga wakati kwa ndani nyumba hii ni nzuri kabisa. Nadhani ninyi wenyewe mnajionea hii nyumba ilivyo kubwa.
“Kwanza hapa nimepanga nyumba nzima, ina sebule, jiko, chumba, choo, sehemu ya kuweka nguo na bado ina uwanja mkubwa wa magari hata matano.

“Sasa kwa nini nisiridhike kukaa hapa? Wasanii wengi wamepanga chumba kimoja, waliopanga nyumba nzima kama mimi ni wachache mno. Kwa nini nikapange jumba la kifahari wakati sina hata kibanda? Si ni bora hiyo pesa nijenge nyumba yangu!” aliwaka Gigy.

Hata hivyo, katika kile kinachoonesha Gigy anakerwa na maneno hayo, aliwataka mapaparazi wetu wakague nyumba nzima kujiridhisha anachoongea ambapo walibaini muonekano wa nje wa nyumba hiyo ndiyo hauvutii, lakini kwa ndani hakuna tofauti ya makazi anayoishi na umaarufu alionao.

Rosa Ree Afunguka Kuhusu Uwezo wa Harmorapa Kimuziki

$
0
0
Rosa Ree Afunguka Kuhusu  Uwezo wa Harmorapa Kimuziki
Msanii wa muziki Bongo, Rosa Ree amefunguka juu ya wale wanaoponda uwezo wa Harmorapa katika muziki.

Rapper huyo amesema ni vigumu kusema Harmorapa hana uwezo wa kimuziki ila kinachotakiwa ni yeye kuonyesha uwezo.

“Ni yeye kuendelea kuonyesha uwezo, huwezi kum-judge mtu kwa sababu ana sifa fulani mtaani au kwa sababu na muonekano fulani, kwa hiyo we can’t judge uwezo wa kipimo cha uwezo wa mtu ni bidii yake” Rosa Ree ameiambia Bongo5.

“Akitia bidii ndio inawezekana, mimi siwezi nikaja nikajiita rapper Rap Goddess wakati nyimbo ninazotoa ni mbovu, you have to call yourself what is your real hear, kwa hiyo ni yeye kuweka bidii anaweza kufika ninapotaka” amesisitiza Rosa Ree.

Kwa sasa Rosa Ree anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Dow’ baada ya kufunika vilivyo na ngoma ‘Up In The Air’.

Uteuzi wa Makocha Ndio Chanzo cha Kufanya Vibaya kwa Kilimanjaro Stars- Julio

$
0
0
Uteuzi wa Makocha Ndio Chanzo cha Kufanya Vibaya kwa Kilimanjaro Stars- Julio
BAADA ya timu ya Taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’ kufanya vibaya kwenye michuano ya Chalenji inayoendelea nchini Kenya, baadhi ya makocha nchini wametoa maoni yao kufuatia kuondolewa kwa timu hiyo.

Kilimanjaro Stars iliwasili nchini jana ikitokea Kenya ambapo katika michezo minne iliyocheza ilijikuta ikiambulia pointi moja baada ya kufungwa michezo mitatu na kutoka sare mchezo mmoja.

Kocha wa Dodoma FC, Jamhuri Kiwhelu ‘Julio’ alisema kufanya vibaya kwa Kilimanjaro Stars kumetokana na maandalizi duni pamoja na uteuzi wa kocha.

“Mimi niseme tu ukweli, Kilimanjaro Stars ilihitaji kocha ambaye anawajua wachezaji vizuri na anazijua vyema changamoto za soka letu, namuheshimu Ninje (kocha wa Kilimanjaro Stars), lakini hakuwa na jipya,” alisema Julio, alipokuwa akizungumza na kituo kimoja cha Radio.

Alisema kuwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), halikufanya chaguo sahihi kumpa timu Ninje ambaye alitumia michuano hiyo kuingiza mfumo mpya wa uchezaji.

“Wachezaji ni walewale, chini ya Salum Mayanga, timu ilikuwa inacheza, huwezi kuingiza mfumo mpya kwenye mashindano na matokeo yake ndio haya tumetia aibu,” alisema Julio.

Kwa upande wake, Kocha Abdallah Kibadeni, alisema wachezaji wa Kilimanjaro Stars wameshindwa kuona thamani ya kuvaa jezi za Taifa.

“Lakini pia ni lazima kujua changamoto za wachezaji, kufanya vibaya kwa Kilimnajaro Stars iwe chachu ya kujipanga upya na kuwa makini katika maandalizi ya michuano mingine,” alisema Kibadeni.

Naye nyota wa zamani wa klabu ya Yanga na timu ya Taifa ‘Taifa Stars’, Ally Mayai, alisema kocha Ninje alifanya makosa kuanzisha staili mpya ya uchezaji wakati wa michuano hiyo.

“Inawezekana alikuwa na lengo zuri, lakini huwezi kutambulisha mfumo mpya wakati wa mashindano au siku chache kabla ya mashindano hili limetugharimu,” alisema Mayai.

Akiwasili nchini jana asubuhi pamoja na kikosi hicho, Kocha wa Kilimanjaro Stars, Ninje, mbali na kuomba radhi kwa Watanzania kutokana na kufanya vibaya kwenye michuano hiyo, alisema kuwa timu yake haikuwa na bahati kwenye michuano hiyo.

Aidha, alikiri mfumo mpya aliouanzisha kwenye kikosi cha timu hiyo umewagharimu, lakini akatetea kuwa kama utafanyiwa kazi utaifanya timu hiyo ya taifa kuwa moto.




Zari Amkumbuka Marehemu Ivan Don Amtumie Ujumbe Mzito "Maisha Hayapo Sawa Tena"

$
0
0
Zari Amkumbuka Marehemu Ivan Don Amtumie Ujumbe Mzito "Maisha Hayapo Sawa Tena"
Miezi saba toka mzazi mwenzake Zari, Ivan Ssemwanga kufariki dunia ambapo kama angekuwa hai siku ya leo December 12, 2017 angekuwa akisherekea siku yake ya kuzaliwa na hivyo Zari kuamua kuadhimisha siku hii kwa kupost maneno yenye majonzi kupitia mtandao wake wa snapchat.




Na huu ndio ujumbe wa Zari kwa marehemu Ivan Don“heri ya siku ya kuzaliwa Don, umeondoka lakini kamwe hautosahaulika, tunakukumbuka, maisha hayako sawa tena,watoto wanakukumbuka, tunakuombea kila siku, endelea kupumzika kwa amani”

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Viewing all 104808 articles
Browse latest View live




Latest Images