Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live

Rais wa Zimbabwe Awaonya Wananchi Wake

$
0
0
Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa ametaka wanachama wa Chama cha Zanu-PF kuachana na nyimbo za kumsifu na kuwataka watilie mkazo wimbo wa Taifa na nyingine zinazozungumzia ukombozi.

Mnangagwa amesema hayo katika mkutano wa chama hicho ambapo amewataka wanachama kutambua kuwa yeye ni Rais wa watu wote na wala si wa kikundi fulani.

Mkutano huo umemwidhinisha  Mnangagwa kuwa Mkuu Mpya wa chama na mgombea urais katika uchaguzi wa mwaka 2018. na kumvua rasmi uongozi aliyekuwa kiongozi mkongwe wa chama na Serikali ya Zimbabwe, Rais Robert Mugabe.

Rais Mnangagwa amesema wanachama wanapaswa kurekebisha uchumi ikiwa wanataka wawe na nafasi ya kushinda uchaguzi mkuu utakaofanyika mwakani.

“Huu si wakati wa kutambiana kuwa kundi gani limeshinda bali kila mwanachama anapaswa kuzingatia mahitaji ya wananchi ambao wanataka maendeleo” amesema

Kwa Mara Nyingine Tena..Mama Ashura Amrushia Dongo Ali Kiba..."Yeye ni Nani Asiambiwe?"

$
0
0
Usiku wa Desemba 15, 2017, katika ukumbi wa MLIMANI CITY, Jijini Dar es Salaam, kulifanyika uzinduzi wa filamu kubwa ya ‘FROM NIGERIA’, kutoka katika Kampuni ya JUMO ENTERTAINMENT, uzinduzi huo ulihudhuriwa na wasanii wengi kutoka katika tasnia mbalimbali, wakiwemo wachekeshaji wanaounda kundi la TIMAMU, Ebitoke, Mama Ashura na Bwana Mjeshi.

Katika mahojiano yake na Global TV, Mama Ashura ambaye kwa mara kadhaa amekuwa akimkosoa staa wa Bongo Fleva, Ally Kiba ‘King Kiba’, kutokana na kazi yake ya muziki, amesema kuwa hata kama akizindua wimbo wake, bado atahudhuria na atamkosoa vilevile, huku akidai kuwa hamjui mchekeshaji, Mkali Wenu ambaye waliwahi wakifanya kazi kwa pamoja. VIDEO:

Historia inaibeba Z’bar fainali Challenge Cup

$
0
0
Leo Jumapili December 17, 2017 wadau wengi wa soka wanasubiri kuona Zanzibar Heroes watafanya nini nchini Kenya kwenye mchezo wa fainali ya CECAFA Senior Challenge Cup mwaka 2017 ambapo watacheza dhidi ya wenyeji Kenya.

Rekodi zinaonesha kwamba, Zanzibar wameshinda ubingwa wa Challenge mara moja tu, ilikuwa mwaka 1995 walipowafunga wenyeji wa michuano hiyo mwaka huo timu ya taifa ya Uganda kwa bao 1-0. Miaka 22 baadaye, Zanzibar wamefika hatua ya fainali jambo zuri na la kuvutia wanacheza dhidi ya mwenyeji wa mashindano (Kenya) Je watarudia walichofanya mwaka 1995 dhidi ya timu mwenyeji?

Historia inaendelea kutukumbusha kwamba, Zanzibar inatafuta ubingwa wake wa pili kwenye mashindano hayo wakati Kenya wakitaka kuweka rekodi ya kutwaa kombe hilo kwa mara ya saba. Mra ya kwanza Zanzibar kushinda taji hilo ilikuwa ni 1995 wakati Kenya wameshatwaa kombe hilo mara sita (nafasi ya pili nyuma ya Uganda ambao wameshinda ubingwa huo mara 14)

Makundi CECAFA 2017
Group A: Kenya (wenyeji), Rwanda (Guest), Libya, Tanzania bara, Zanzibar (mechi zilichezwa Machakos) Group B: Uganda, Burundi, Ethiopia, Sudan Kusini (mechi zilichezwa Kakamega)
Kumbuka timu ambazo zimefuzu kucheza fainali (Kenya vs Zanzibar) zote zimetoka Group A, ambapo Kenya waliongoza kundi wakifuatiwa na Zanzibar waliomaliza katika nafasi ya pili.

Road to final

Kenya
Kenya 2-0 Rwanda
Kenya 0-0 Libya
Kenya 0-0 Zanzibar
Kenya 1-0 Tanzani

Zanzibar
Zanzibar 3-2 Rwanda
Tanzania 1-2 Zanzibar
Kenya 0-0 Zanzibar
Libya 1-0 Zanzibar

Nusu Fainali
Kenya 1-0 Burundi
Uganda 1-2 Zanzibar

Failani
Kenya ?? Zanzibar

Kocha wa Zanzibar Heroes Hemes Suleiman ‘Morocco’ amesema, timu yake ipo tayari kwa mchezo wa fainali huku akiamini watapata matokeo bora.

“Karibu wachezaji wote wako vizuri isipokuwa mchezaji mmoja tu (Kassim) na tuliweza kucheza mechi ya nusu fainali bila yeye, tuko vizuri na tayari kwa ajili ya mchezo wa fainali dhidi ya Kenya.”

“Watu waendelee kutupa support kama ambavyo walifanya kwenye mechi nyingine na sisi tutajitahidi kuhakikisha tunapata matokeo bora.”

Nimemsomesha, Nimegharamika, Leo Kaniacha Anaolewa na Mtu Mwingine

$
0
0
Wakuu nilikutana na huyu binti miaka kadhaa iliyopita mimi nikiwa nimepangiwa kazi mkoa fulani katika mihangaiko yangu nikakutana na huyu binti nilitokea kumpenda, mzuri kisura na kitabia very innocent niliamini kwake nimefika baada ya kash kash nilizopitia katika mahusiano ya nyuma.

Wanasema usiusemee moyo ila najua yule binti alinipenda kidhati tena moyoni kabisa na mimi kwangu she was a queen na niliapa kumuoa baada ya yeye kumaliza masomo yake. Binti huyu kwao ni familia maskini nikisema familia maskini ni familia maskini kisawasawa. Baba yake alifariki miaka kadhaa nyuma kabla sijaonana nae hivyo aliishi na mama yake na wadogo zake ni story ndefu kuhusu familia yao. Mimi nikawa ndio kama msaada katika familia yao, sikua na hiyana na nilisaidia niwezavyo kwani binti yule nilimpenda kutoka moyoni.

Yule binti alimaliza shule na kuhitajika kwenda chuo lakini familia ikawa haina uwezo wa kumsomesha na mkopo alikosa. Akakosa raha na ikawa kama jukumu ni langu. Mama yake aliniita tushauriane kwasababu kwao nilikua nafahamika. Kwakuwa mimi nilisema nitamuoa binti wakashauri nimsomeshe kama nina nia yakweli. Uwezo wa kumsomesha nilikua nao nikakubaliana na tukaandikishana kwamba namsomesha mimi lakini mwisho wa siku yeye atakuja kuwa mke wangu na hata mahari sintolipa kwani itakua imeingia huko.

Familia ilinishukuru sana kwani waliamini kusoma kwa binti itakua afadhali katika ukombozi wa maisha yao. Binti alikuwepo wakati maandikishano yanafanyika na mashahidi walikuwepo nakumbuka binti alilia yule akiapa kunipenda milele na mapenzi tuliyofanya siku hiyo siwezi kusahau ilikua best sex ever.

Wakuu nifupishe binti alianza chuo kila kitu nililipa nauli hosteli ada matumizi kila kitu ilikua mimi,mwaka wa kwanza ukaisha vizuri mapenzi yanachanua.Likizo naenda likizo zao anakuja, mama mtu alinishukuru sana. Mwaka. Mwaka wa pili matatizo yakaanza nikipiga simu naambiwa yuko library mara assignment nikiuliza zaidi anakua mkali nikasema labda labda kweli shule lakini hata mimi nilisoma muda wa kuongea na mwenzi wangu nilikua nao nikasema labda shule ya sasa ni ngumu. Binti akabadilika majibu ya jeuri nikaenda kuongea na mama yake amkanye naona akajirekebishe na kweli akatulia maisha yakaendelea. Upside zikiwa chache. Mahusiano yalitawaliwa na migororo

Kufupisha Miezi kadhaa imepita binti kaniandikia meseji eti "NAKUSHAURI UTAFUTE MWANAMKE MWINGINE MIMI SIKO TAYARI KUWA NA WEWE NIKUTAKIE MAISHA MEMA"

Naandika huu uzi wakuu acha nikipiga simu haipokelewi mara haipatikani. Nikampigia mama yake kumuuliza kama anajua lolote akasema hafahamu. Nikaomba likizo kazini nifatilie sikuamini siku naambiwa ana mimba na anaishi na mwanaume mwingine. Nilitamani ardhi ipasuke kumbe ndio maana niliandikiwa ule ujumbe nikajiuliza maswali bila majibu,basi angefanya nisijue na mimba juu kapata inauma sana. Kumuuliza mama yake hana analonijibu, kumbe chuo kapostpone sijui anaishi na huyo mwanaume moja ya mitaa Dar, yote hiyo nafatilia kwa baadhi ya marafiki zake na kibaya zaidi huyo mwanaume alishamlipa tena huyo mama pesa nyingine. Na ndio kamchukua binti yake.

Nimechukia kuuziwa mbuzi kwa gunia.Love is blind inakuwaje sikuona yote hayo? Why me..Why.. Najiuliza sipati majibu, sikuwahi kupenda kama nilivyompenda huyo binti. Nilimpenda kutoka moyoni na kujitoa kwake sijawahi kumfanyia mwanamke yoyote niliyomfanyia leo ameniacha kwenye mataa na nyodo juu, kuna muda natamani ningekuwa na bastola nimsambaratishe ila that is not me. Juzi nimeona whatsup kaweka picha yake tumbo kule na namba yake nikafuta.

NILICHOFANYA;

Nimepeleka hii kesi Mahakamani kwasababu tuliandikishana kama mke nimekosa basi nilipwe gharama zangu najua haiwezi kuziba pengo kufuta maumivu naona is the least i can do for my self. Wakuu nifanyaje au nimekosea kupeleka shtaka polisi tumeshaitwa mara mbili hakuna mtu aliyetokea upande wao. Nimetokea kuwachukia wanawake sana. Kwanini mnatufanyia hivi jamani tuwapende vipi. Nimekaa hapa kitandani nimewaza mawazo mengi moyo wangu kama barafu naishia kusononeka.

Sijui nimfanyie kisasi gani aumie kama mimi nilivyoumia.

Waziri Mwakyembe Achimba Mkwara ‘Mazoea’ Taifa Stars

$
0
0
Waziri mwenye dhamana ya michezo Tanzania Dr. Harrison Mwakyembe amesema suala la uwakilishi kwenye timu ya Taifa kwa mazoea inabidi liangaliwe kwa makini kwa sababu kuna wachezaji wamekuwa na uhakika wa kuitwa kwenye timu hata kama hawajitumi wakiwa kwenye timu hiyo.

Waziri Mwakyembe amesema hata yeye ameumizwa na matokeo yaKilimanjaro Stars kwenye Challenge Cup kufuatia mfululizo wa matokeo mabovu ambapo timu hiyo haikushinda hata mechi moja kati ya nne ilizocheza hatua ya makundi huku ikitupwa nje ya mashindano ikiwa na pointi moja iliyoipata baada ya suluhu dhidi ya Libya kwenye mechi ya kwanza.

“Sasa uwakilishi kwenye Taifa Stars kwa mazoea hili suala lazima tuliangalie kwa makini sana. Sio mchezaji anakuwa anauhakika wa kuitwa kwenye timu, tunataka tuone kwa kujituma”-Mwakyembe.

Mwakyembe pia amesema kutokana na wachezaji wa Zanzibar Heroes wanavyojituma kwenye michuano ya Challenge Cup 2017, anaamini watarudi na kombe hilo.

“Kwa mchezo wanaouonesha vijana wa Zanzibar Heroes nina uhakika hili kombe tunalipata, litakuja Tanzania. Wanacheza kwa kujituma, sio mtu anacheza kwa kujituma nusu kwa sababu atajituma zaidi akiwa kwenye klabu, nafiri nimejifunza vizuri sana kama Waziri katika sekta hii.”

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
MHULI: Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.


Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na Nasi kwa Namba; 0783140065

Kama Unaogopa Kufanya Kitu Hiki, Sahau Kuhusu Mafanikio Katika Maisha Yako Yote

$
0
0
Fikiria kila unachokijua na kukikumbuka kuhusu mabadiliko unayotaka yawe katika maisha yako, halafu  uone ukweli huu  kama kweli nawe ni mmoja kati ya watu wanaotaka mafanikio au uko nje ya mstari wa mafanikio na pengine tu wewe hujijui. Kama kweli unataka mafanikio, ni kwanini  mara kwa mara umekuwa ukisita au kuogopa kufanya jambo ambalo lingeweza kubadili maisha yako na kukuletea mafanikio mkubwa? Hili ndilo tatizo walilonalo watu wengi wanahofia sana kufanya mabadiliko kwa namna moja au nyingine hata kwenye yale malengo waliojiwekea wao wenyewe kuna wakati huwa wanaogopa pia.

Kimaumbile, kila binadamiu anahofia mabadiliko, lakini hofu ya mabadiliko inapozidi kuwa kubwa na kukuzuia kufanya mambo ya maana kwako, hofu hii  sasa hugeuka kuwa ni maradhi yanayokuzuia wewe kufanikiwa. Hebu fikiria tena, ni mara ngapi umekuwa ukitaka kufanya mabadiliko Fulani  katika maisha yako, lakini umekuwa ukijikuta ukishindwa kufanya hivyo kutokana na kuogopa kufanya vitu Fulani? Ni mara ngapi umekuwa ukitaka kuingia kwenye biashara lakini umekuwa na hofu nyingi zinakuzuia? Hivi ndivyo ilivyo mabadiliko huogopwa, wakati mwingine bila sababu ya msingi.

Wengi wetu kutokana na kuogopa mabadiliko, hujikuta ni watu wa kutoa sababu ambazo hata hazina mashiko zinazosababisha wao washindwe kutekeleza malengo na mipango waliojiwekea. Utakuta mtu anakwambia  hawezi kufanya biashara ni kwa sababu hana mtaji, ukija kuchunguza kidogo utagundua kuwa hiyo ni sababu ambayo amekuwa akiitoa kwa muda mrefu, iweje kila siku mtu huyohuyo awe hana mtaji tu. Kama uko hivi una hofu tu hata kwa vitu vidogo ambavyo ungeweza kuvifanyana , tambua kuwa kuanzia sasa unaye adui mkubwa ndani mwako anayekuzuia kufanikiwa. Na unapoogopa kufanya mabadiliko ambayo unaahitaji sasa ili ufanikiwe, sahau kuhusu mafanikio katika maisha yako yote.

Tatizo kubwa utakalokuwa nalo linalosababishwa na hofu hii ya kuogopa kufanya mabadiliko ni lazima utakuwa mtu wa kutaka mafanikio ya harakaharaka. Watu wengi wenye mawazo ya kutaka kufanikiwa leoleo hata kama wameanza biashara leo, wengi wao huwa wana hofu hii kubwa ya mabadiliko ndani mwao, unaweza  kufanya utafiti mdogo utagundua ukweli huu ulio wazi. Hawa ni watu ambao kiuhalisia hawaijui wala kuiamini subira ndani mwao, bali ni watu wakutaka mfumo wa maisha uwe ambao unaanza leo biashara na wiki ijayo uwe tajiri ni kitu ambacho hakiwezekani kabisa.

Hivi ndivyo walivyo watanzania wengi wanaogopa mabadiliko na kuamini katika miujiza, sio katika wao wenyewe kutenda na kuona matokeo.  Hebu jaribu kukagua maisha ya walio wengi utakuja kugundua ukweli huu ni watu wanaofikiria sana leo, sasa hivi, siyo baadaye. Hata malengo yao ni ya karibu sana na hawataki shida, wanataka wafanye leo, wamudu leo na kila kitu kimalizike leo. Sijui kesho watafanya kitu gani? Ukimwambia mtanzania aanzishe mradi ili aje faidi baada ya miaka 10 kutoka sasa kwanza atakushangaa, kisha atakucheka we hadi mbavu zimuume. Anataka leo hata kama ni kwa miujiza.

Ndiyo maana wengi kati ya Watanzania hawana malengo, wanaishi tu na kutawaliwa na hofu za mabadiliko. Kuweka malengo siyo sehemu ya maisha yao, kwani malengo yanataka mtu mwenye subira, mtu anayeamini kwamba maisha ni kuanguka na kusimama. Wanachojua kikubwa ni kulalamika na kulaumu, kuponda na kukejeli, kwa sababu wao wamekata tamaa bila kujijua. Ndiyo maana ni watanzania wanne tu kati ya kumi ambao wanafanya kazi, wanatoka jasho na wanaweza kusubiri bila kukata tamaa, wengine waliobaki wanasubiri ujanja ujanja tu ilimradi wafanikiwe hata kama ni kwa kufanya uhalifu wa aina yoyote.

Ni watu ambao wanataka kuishi kihadithi, wawe na pete ambayo wanaweza kuiamuru iwape wakitakacho na wakipate. Maisha ni ya kibunuasi- abunuasi tu, watu hawa kwao mabadiliko ni kitu kigumu sana kwao na kinaogopwa kweli. Kama unataka mafanikio ya kweli yawe kwako, unatakiwa kubadilisha fikra za zako na kuamua kukubali kuwa mafanikio yanahitaji mabadiliko makubwa sana ambayo wewe mwenyewe unatakiwa uyafanye kwa kujitoa hasa. Acha kuwa na hofu zisizo na maana zinazokuzuia wewe usifanikiwe, chukua hatua katika maisha yako, kuyafikia maisha unayoyataka.

Salam za JK Baada ya Z’bar Heroes Kufuzu Fainali Challenge Cup

$
0
0
Baada ya timu ya taifa ya Zanzibar ‘Zanzibar Heroes’ kufuzu kucheza fainali ya michuano ya CECAFA Senior Challenge Cup 2017, Rais mstaafu wa serikali ya awamu ya nne Dr. Jakaya Kikwete ‘JK’ ametuma salam za pongezi kwa timu hiyo.

Kupitia ukurasa wake wa twitter JK ameandika: “Nawapongeza Zanzibar Heroes kwa kututoa kimasomaso na kutinga fainali. Nawatakia kila la kheri katika mechi ya fainali waibuke na kombe na watupe raha ambayo Watanzania tumeikosa kwa muda mrefu.”

Zanzibar waliifunga 2-1 timu ya taifa ya Uganda ‘The Cranes’ kwenye mchezo wa nufu fainali, ikumbukwe Uganda ndio walikuwa mabingwa watetezi wa kombe hilo walilolitwaa mwaka 2015. Mwaka huohuo Uganda waliifunga Zanzibar 4-0 katika mchezo wa hatua ya makundi.

Mchezo wa fainali utachezwa Jumapili December 17, 2017 kati ya wenyeji Kenya dhidi ya Zanzibar.

Waziri asema asilimia 33 ya jamii inaviashiria vya ugonjwa wa figo

$
0
0
Waziri wa afya wa Zanzibar Mahmud Thabit kombo amesema asilimia 33 ya jamii ya Zanzibar inaviashiria vya ugonjwa wa figo huku akisitiza kuwa sera ya serikali  kutoa huduma bila malipo iko pale pale na tayari wagonjwa wa figo na magonjwa mengine wanapata huduma hizo bila malipo.

Akizungumza na wandishi wa habari  baada ya kupokea msaada wa madawa kutoka kwa  ubalozi mdogo wa Oman hapa Zanzibar Mhe Mahmud amesema ugonjwa huo ni tishio na serikali imelazimika kuhakikisha ina mashine za kusafisha figo .

Naye Mkuruegnzi wa kinga na elimu ya afya Dr Fadhil Abdullah amesema utafiti uliofanywa hadi sasa unaonyesha ugonjwa huo wa figo unawagusa asilimia 33 ya jamii na hii inatokana na wagonjwa wengi wa shinikizo la damu na sukari kuongezeka Zanzibar ambayo ndio chanzo kikubwa cha ugonjwa huo,huku balozi mdogo wa Oman Dr Ahmed Hamood  Al Habshi ambaye alikabidhi dawa hizo amesema serikali yao Oman iko  tayari  kusiaiida Zanzibar katika kupamabana na ugonjwa huo na mengine kwa kutoa utaalamu na vifaa.

Wizara ya afya kupitia vitengo mbali mbali vikiwemo vya saratani,sukari na magonjwa yasiyoambukiza vimekuwa vikitoa elimu ya afya kwa wakazi wa Zanzibar wabadilike katika ulaji wa vyakula na kuanza kufanaya  mazoezi kutokana na ongezeko la magonjwa hayo.

Hizi Hapa Taarifa Kuhusu Kukamatwa na Takukuru Kwa Aliyekuwa Mkurugenzi wa NHC Peter Mchechu...Mwenyewe Afunguka

$
0
0

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa(NHC), Nehemiah Mchechu amekanusha taarifa zilizosambaa mapema leo kuwa amekamatwa na TAKUKURU na kuhojiwa. Asema yupo kwenye msiba wa mama yake huko Ukonga.
-
Awali, zilisambaa taarifa zinazoeleza kuwa Mkurugenzi huyo aliyesimamishwa kazi jana kupisha uchunguzi, amekamatwa na TAKUKURU kwa mahojiano na angefikishwa mahakamani siku ya Jumanne kujibu mashtaka, taarifa ambazo si za kweli.

Rushwa Yazidi Kuwamaliza Vigogo...Takururu Yamshikilia Kigogo Huyu Mwingine Kwa Rushwa

$
0
0

TAKUKURU inamshikilia Mwanasheria wa Baraza la Taifa la Hifadhi ya Mazingira(NEMC), Bernard Kongola na Polisi wawili wa kituo cha Mbweni kwa madai ya kuomba Rushwa ya Shilingi milioni 1 kutoka kwa Mkalimani binafsi wa Kiwanda cha Yong Long Plastic

Huyu Sasa Kazidi...Kijana Aliyetoka Jela Kwa Msamaha wa Rais Aiba Tena na Kukamatwa.

$
0
0

Kijana Gerald Deus (30), aliyetoka jela kwa msamaha wa Rais Magufuli, amehukumiwa tena kifungo cha miaka 15 jela kwa tukio la wizi alilolifanya siku ya nne baada ya kuachiwa huru
-
Deus alihukumiwa kifungo hicho juzi na Mahakama baada ya kukiri kosa la kupora pesa shilingi laki 3 kutoka kwa Dina Mwende, mfanyabiashara wa soda za jumla.
-
Kwa mujibu wa Hakimu, kosa hilo adhabu yake ni kifungo cha miaka 30 lakini kutokana na mtuhumiwa kukiri kosa na kutoisumbua mahakama, amepunguziwa adhabu hivyo atatumikia miaka 15 na kazi ngumu.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tundu Lissu Afunguka Makubwa na Kumjibu Job Ndugai

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu amefunguka na kumjibu Spika wa Bunge, Job Ndugai kuhusu kauli yake ya kusema kuwa utaratibu uliotumika kumsafirisha Tundu Lissu kwenda Nairobi kuwa ulikwenda kinyume na mfumo wa serikali na kibunge.

Tundu Lissu anadai kuwa kauli hiyo haina ukweli hata kidogo kwani kitendo cha yeye kusafirishwa kwa ndege mnamo Septemba 7, 2017 majira ya usiku kuelekea kwa matibabu nchini Kenya ni wazi kuwa kibali kilitolewa na serikali pamoja na Bunge kwani bila hivyo yeye asingeweza kusafirishwa.

"Mimi sikuamua kuja Nairobi sikuwa najitambua, watu walioamua mimi kuja Nairobi ni pamoja na Spika Ndugai mwenyewe watu wameniambia kwenye hicho kikao cha nipelekwe wapi Ndugai alikuwepo, Naibu wake alikuwepo, Katibu wa Bunge wakati huo Kashilila alikuwepo, Mwenyekiti wa chama changu alikuwepo ile ndege iliondoka saa sita usiku sasa ingerukaje kama haikuruhusiwa na serikali ya Tanzania kuruka kuja Nairobi? Kwa hiyo hii habari ya kwamba amepelekwa wapi ni mambo ya kujishikiza shikiza tu ni Bunge kujaribu kukwepa wajibu wake wa kisheria" alisema Tundu Lissu

Aidhaa Tundu Lissu aliendelea kufafanua kuwa "Nimesema mimi siombi fadhila, hakuna mtu anaomba kufadhiliwa hapa mimi naomba haki ambayo anatendewa mtu aliye Mbunge anayeumwa ambaye amelazwa nje ya kituo chake cha kazi hicho tu.

Mbali na hilo Tundu Lissu amesikitishwa na upelelezi unaofanywa na jeshi la polisi kuhusu shambulio lake la kutaka kuuawa na kusema anashangaa mpaka leo jeshi la polisi halijasema linamshuku nani kuhusika na shambulio hilo na mpaka leo jeshi la polisi halijaweza kumhoji japo aweze kutoa maelezo yake.

Tundu Lissu alishambuliwa na risasi mnamo Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma na baadaye kupelekwa nchini Kenya jijini Nairobi kupatiwa matibabu ambapo mpaka sasa yupo huko kwa matibabu.

Zanzibar Heroes yafa kiume Kenya, Yatoa somo kwa ‘vibonde’ Kilimanjaro Stars

$
0
0
Timu ya mpira wa miguu ya Zanzibar Heroes imefanikiwa kushika nafasi ya pili ya michuano ya CECAFA baada ya kukubali kichapo cha goli 3-2 kwa changamoto ya mikwaju ya penati baada ya kwenda sare ya goli 2-2 kwa kwa dakika 120.
 

Licha ya kupoteza fainali hiyo ninaweza kusema Zanzibar imekufa kiume kwanza kuanzia maandalizi, Zanzibar Heroes ilitumia usafiri wa basi kutoka Dar es salaam hadi Kenya kwa ajili ya kushiriki michuano hiyo wakati Timu ya taifa ya Tanzania Bara ambao wanastahili kuitwa ‘vichwa vya Wendawazimu’ hao walitumia pesa nyingi za Watanzania kusafiri kwa ndege, ambapo hata hivyo licha kuondoka kwa mbwembwe wametolewa mapema kwenye michuano hiyo.

Zanzibar imetoa somo kubwa kwa Timu ya Kilimanjaro Stars ikiwemo uzalendo na Kujituma kwa ajili ya taifa, leo hii ukiangalia jinsi Wachezaji wa Kilimanjaro Stars walivyokuwa wanacheza uwanjani unaamini kabisa kuwa hawakuwa tayari kulitumikia taifa lao.

Ukiangalia kikosi cha Zanzibar Heroes kilichoshiriki kwenye michuano ya CECAFA huwezi kulinganisha uwezo wa mchezo mmoja mmoja na kikosi cha Kilimanjaro Stars kilichojaa majina makubwa na yenye uzoefu wa michuano mikubwa.

Watanzania wamechoka kunung’unika kila siku huu ni muda wa Serikali kupitia wizara yake ya Michezo na TFF kukaa chini kutafakari kwa kina ni jinsi gani wataziokoa timu zetu za taifa kutoka kwenye aibu hii kwenye soka.

Hongereni Zanzibar Heroes kupoteza kwenu ni matokeo tu ya mpira wa miguu bila shaka ingekuwa jambo la kheri kurudi nyumbani kwa ndege na kupokelewa kwa shangwe kwani mlichotumwa mmekifanikisha kwa 50%.

Zitto Kabwe aivaa TAKUKURU, Adai wanavunja sheria na kutumika kisiasa

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini na kiongozi wa ACT Wazalendo, Mhe. Zitto Kabwe ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) kujisafisha kwanza yenyewe na kuepuka kutumika kisiasa.

Mhe. Zitto amesema TAKUKURU ina miaka mitano haijakaguliwa na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) na kila mwaka inapewa kiasi cha tsh bilioni 85 lakini mpaka sasa ni miaka mitano haijafunga hesabu wala kukaguliwa na CAG.

Zitto Kabwe amedai kuwa TAKUKURU kitendo cha kutokufunga hesabu za kila mwaka wanavunja kifungu chao wenyewe cha sheria namba 13 ya mwaka 2007 kifungu 47(2) kinachowataka kufunga hesabu za kila mwaka.

“TAKUKURU ni moja ya taasisi nyeti za uwajibikaji nchini Lakini inatumika kisiasa. Inatumwa na wanasiasa wa CCM kufanya mambo yao. Kukamatwa kwa Mwalimu Mukoba jana ni moja ya ushahidi wa kutumika kwa TAKUKURU kisiasa. Serikali Ina lengo ya kudhibiti Chama cha Walimu nchini na kina Mukoba walionekana ni vikwazo. Sitaki kusema la Nehemia Mchechu wa NHC Lakini nina hakika ya dhati amekuwa fixed sababu ya chuki, visasi na roho mbaya. TAKUKURU wanatumika kwenye hayo. Lakini Watanzania wajue kuwa TAKUKURU sio wasafi. Sheria yao inawataka wafunge hesabu kila mwaka na wakaguliwe na CAG. Licha ya kupewa tshs 84 bilioni kila mwaka, TAKUKURU hawana mahesabu ( annual accounts ) na hawajakaguliwa na mkaguzi yeyote. Jeshi letu JWTZ lina kaguliwa na CAG na kuitwa mbele ya PAC Lakini TAKUKURU hata hesabu hawafungi.”amesema Zitto Kabwe.

Kwa upande mwingine Zitto Kabwe ameitaka TAKUKURU kuacha kutumika kisiasa na kuionya kuwa isipokuwa makini huenda ikawa jumuiya ya nne la CCM.

“Nimepata kumwambia Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU uso kwa uso kuwa taasisi yake inatumika kisiasa. Narudia kumwambia hadharani kuwa taasisi yake inatumika. Wamejifanya wanamchunguza DC Mnyeti ambaye sasa ni RC hawajafanya na wala hawatafanya. Mimi simpendi Sadifa, Lakini najua Sadifa kakamatwa kisiasa tu. Watanzania tutoke tuiambie TAKUKURU iache kutumika kisiasa. Isafishe nyumba yake kwa kufunga vitabu vya hesabu na kukubali kukaguliwa na CAG. Iachie watu inaowakamata kwa siasa na ikamate watoa rushwa wa Kweli kama Mnyeti nk. Mlowola ajue kuwa TAKUKURU sio na haitakuwa Jumuiya ya 4 ya CCM baada ya Vijana, Wanawake na Wazazi. Kwa sasa tuwatake TAKUKURU kwanza wasafishe nyumba yao. Wanapewa tshs 84bn kila mwaka na Bunge. Sheria yao inawataka kila mwaka wafunge hesabu na zikaguliwe. Wana miaka 5 hawajafunga hesabu wala hawajakaguliwa na CAG. Nashangaa sana donor countries zinazowapa fedha bila ukaguzi.”amesema Zitto Kabwe.

Soma taarifa yake kamili aliyoiweka kwenye ukurasa wake wa Facebook.

TAKUKURU ni moja ya taasisi nyeti za uwajibikaji nchini Lakini inatumika kisiasa. Inatumwa na wanasiasa wa CCM kufanya mambo yao. Kukamatwa kwa Mwalimu Mukoba jana ni moja ya ushahidi wa kutumika kwa TAKUKURU kisiasa. Serikali Ina lengo ya kudhibiti Chama cha Walimu nchini na kina Mukoba walionekana ni vikwazo. Sitaki kusema la Nehemia Mchechu wa NHC Lakini nina hakika ya dhati amekuwa fixed sababu ya chuki, visasi na roho mbaya. TAKUKURU wanatumika kwenye hayo.

Lakini Watanzania wajue kuwa TAKUKURU sio wasafi. Sheria yao inawataka wafunge hesabu kila mwaka na wakaguliwe na CAG. Licha ya kupewa tshs 84 bilioni kila mwaka, TAKUKURU hawana mahesabu ( annual accounts ) na hawajakaguliwa na mkaguzi yeyote. Jeshi letu JWTZ lina kaguliwa na CAG na kuitwa mbele ya PAC Lakini TAKUKURU hata hesabu hawafungi.

Nimepata kumwambia Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU uso kwa uso kuwa taasisi yake inatumika kisiasa. Narudia kumwambia hadharani kuwa taasisi yake inatumika. Wamejifanya wanamchunguza DC Mnyeti ambaye sasa ni RC hawajafanya na wala hawatafanya. Mimi simpendi Sadifa, Lakini najua Sadifa kakamatwa kisiasa tu.

Watanzania tutoke tuiambie TAKUKURU iache kutumika kisiasa. Isafishe nyumba yake kwa kufunga vitabu vya hesabu na kukubali kukaguliwa na CAG. Iachie watu inaowakamata kwa siasa na ikamate watoa rushwa wa Kweli kama Mnyeti nk. Mlowola ajue kuwa TAKUKURU sio na haitakuwa Jumuiya ya 4 ya CCM baada ya Vijana, Wanawake na Wazazi.

Mkuu wa Mkoa Aitaka Takururu Ichunguze Ofisi yake

$
0
0
Serikali Mkoani Mara imeiagiza Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru) kufanya uchunguzi wa upotevu wa fedha zaidi ya Tsh 3.5bn katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na miradi ya maji mkoani humo.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima katika kikao cha pamoja cha watendaji wa TAKUKURU, Mahakama na Jeshi la Polisi. Kikao hicho kiliitishwa kwa malengo ya ofisi hizo kujitathimini katika utendaji kazi.

Malima ambaye aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa huo mwishoni mwa mwezi wa Oktoba amesema katika ofisi yake pekee, amebaini ubadhirifu wa zaidi ya Shilingi milioni 500.

“Kwenye miradi ya maji ya mkoa huo, kuna zaidi ya Shilingi bilioni tatu hazionekani. Kila ninapokwenda katika mkoa wa Mara, kila ninapokanyaga watu wanalia na shida ya maji. Tena ni aibu zaidi kwetu hapa maana tupo hapa na ziwa lipo lakini watu hawana maji. Hatuwezi kuvumilia haya, lazima hatua kali zichukuliwe,” amesema Malima.

Kabla ya 40 ya Marehemu Ndikumana...Irene Uwoya Achafua Hali ya Hewa na Picha za Faragha

$
0
0
WHY? Hata kabla ya siku 40 baada ya kifo cha aliyekuwa mumewe, Hamad Ndikumana ‘Katauti’ au ‘Ndiku’, staa wa sinema za Kibongo, Irene Uwoya, anadaiwa kuchafua hali ya hewa na kuwafanya watu wake wa karibu kushindwa kuamini alichokifanya.

Jana, Jumapili, picha za Uwoya akiwa kimahaba kitandani na mwanaume, zilichafua upepo kwenye mitandao ya kijamii ambapo mwanamama huyo alinangwa kuwa, angalau angesubiri mumewe huyo aliyezaa naye mtoto mmoja wa kiume, atimize siku 40 kaburini ndipo ajiachie.

Picha hizo zilisambaa wakati Ndikumana akitimiza mwezi mmoja na siku mbili tu kaburini kwani alifariki dunia usiku wa kuamkia Novemba 15, mwaka huu akiwa Kocha Msaidizi wa Timu ya Rayon ya Rwanda. Gazeti hili lilifanya uchunguzi juu ya picha hizo ambapo kwa mujibu wa mtu wa karibu wa Uwoya, picha hizo zilisambaa ikiwa ni mwendelezo wa ‘kutafuta kiki’ ya tamthiliya mpya ya msanii huyo baada ya ile kiki yake na msanii wa Bongo Fleva, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ ya kufunga ndoa kudaiwa kubuma.

Jana, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Uwoya ‘fizikali’ kwa kufika nyumbani kwake maeneo ya Sinza-Mori, Dar, lakini likamkosa. Alipoendewa hewani, simu yake iliita bila kupokelewa na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno (SMS) hakujibu
STORI: Imelda Mtema, Dar

Ondoa Nyama Uzembe na Kupunguza Mwili Kwa Kutumia Virutubisho vya Edmark

$
0
0

NI VIRUTUBISHO AU CHAKULA MBADALA
ZIMEHAKIKIWA NA TFDA
Ni uhakika kwa afya yako,👉 kupunguza uzito na sumu mwilini,mafuta/lehemu mbaya, Kitambi na nyama uzembe na kutibu MAGONJWA Mbali mbali
@looseweight_trainer ni msaada wako text WhatsApp 0713 777 470 upate suluhisho la afya yako KARIBU
👉@looseweight_trainer

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa leo Jumatatu

$
0
0
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live




Latest Images