Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live

Izzo B Afunguka Sababu ya Kumwaga Chozi Wakati Akitambulisha Ngoma Yake Mpya Kwenye XXL

$
0
0
Izzo B Afunguka Sababu ya Kumwaga Chozi Wakati Akitambulisha Ngoma Yake Mpya
Mwanamuziki wa Hip Hop Izzo Bizness kazungumzia ishu iliyosababisha yeye kutoa machozi kwenye kipindi cha XXL, Clouds FM siku ya jana December 20, 2017 wakati alipokuwa akitambulisha wimbo wake mpya aliomshirikisha mkongwe Juma Nature wimbo unaoitwa “Baraka”.

Izzo Bizness ameleezea sababu na kusema alikuwa yupo kwenye emotion na wakati alipokuwa akitaka kujibu maswali aliyokuwa akiulizwa anapata kumbukumbu ya hustle alizokuwa akizipitia kwenye maisha alafu kuipigania ndoto yake…

"Nilikua kila nikitaka kujibu maswali nilikua yananirudisha nyuma na kukumbuka nilivyokuwa nafanya zile haso katika maisha yangu ya  nyuma na ilikuja automaticall sikutegemea kama ingetokea vile" Izzo B

Klabu ya Soka ya Ajax Amsterdam ya Uholanzi Yatimua Benchi la Ufundi

$
0
0
Klabu ya Soka ya Ajax Amsterdam ya Uholanzi Yatimua Benchi la Ufundi
Klabu ya soka ya Ajax Amsterdam ya Uholanzi imelitimua benchi lake lote la ufundi likiongozwa na kocha mkuu Marcel Keizer baada ya kufanya vibaya kwenye ligi ya nyumbani na ligi ya Mabingwa Ulaya.


Ukiacha kocha mkuu Marcel Keizer, wengine waliofutwa kazi ni wasaidizi wake Dennis Bergkamp pamoja na Hennie Spijkerman.

Meneja mkuu wa timu hiyo ambaye ni golikipa wa zamani wa Manchester United Edwin Van De Sar amefutwa kazi pia, huku mkurugenzi wa ufundi Marc Overmars naye akitupiwa vilago.

Ajax inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na alama 38 nyuma ya PSV yenye alama 43. Mlinzi wa zamani wa kimataifa wa uholanzi Michael Reiziger, na Winston Bogarde wamekabidhiwa timu kwa muda.

Makocha wanaotajwa kuchukua nafasi katika timu hiyo ni Ronald Koeman na Frank De Boer ambao wanatajwa huenda wakapewa timu kwa mkataba mrefu.

Picha: Ilivyokuwa Kwenye Usiku wa wa Zari All White Party Uganda

$
0
0
Picha: Ilivyokuwa Kwenye Usiku wa wa Zari All White Party Uganda
Zari All White Party ni moja kati ya show zinazofanya vizuri katika ukanda wa Afrika Mashariki kutokana na watu wanaohudhuria show hizo kuwa nadhifu zaidi. Usiku wa kuamkia Ijumaa hii moja ya show hizo ambazo huandaliwa na Zari The Bosslady, imefanyika katika ukumbi wa Guvnor nchini Uganda.



Japo Zari alikutana na upinzani mkali kutoka kwa hasimu wake Hamisa Mobetto ambaye na yeye alikuwa na show yake kwa upande wa pili lakini hilo halikuweza kuzuia watu kumiminika katika party hiyo ambapo DJ wa Diamond, Romy Jones alihudhuria pia.










Rugemalila Aleta Mapya Mahakamani Anataka Kumtaja Mwizi wa Fedha za ESCROW

$
0
0
Rugemarila Aleta  Mapya Mahakamani  Anataka Kumtaja Mwizi wa Fedha za ESCROW
Mfanyabiashara James Rugemalila anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa anahitaji kuonana na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) ili ampe ushahidi wa nani anayepaswa kukamatwa katika kesi hiyo.

December 8, 2017 Rugemarila aliieleza mahakama hiyo kuwa unahitajika ushirikiano baina yake na upande wa mashtaka ili kumbaini mwizi wa Sh.Bil 309 za Serikali.

Mbali ya Rugemarila, Mshtakiwa mwingine ni mmiliki wa IPTL Harbinder Singh Sethi ambapo kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi, utakatisha fedha na kuisababishia Serikali hasara ya USD 22, 198,544.60 na Sh.Bil 309.

Rugemarila ameyaeleza hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Leornad Swai kudai upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, hivyo anaomba ahirisho.

Baada ya kueleza hayo, Rugemarila alinyoosha mkono ambapo amesema kuwa anaushukuru upande wa mashtaka ulimchukua gerezani na kumpeleka Upanga kwa mahojiano na kumrudisha salama gerezani.

“Leo nimekuja na ushahidi, hivyo naomba nikutane na DPP ili niweze kumsaidia kumjua mwizi anayepaswa kukamatwa, kwani lengo letu ni kuonyesha kuwa tupo Innocent,” alieleza Rugemarila.

Kutokana na maelezo hayo, Hakimu Shaidi alimtaka Rugemarila kuwasiliana na mawakili wake ili waandike barua ya kuwasilisha kwa DPP kuhusu suala hilo la ushahidi wake, ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi January 5, 2018.

ACT-Wazalendo Yafunguka Sababu ya Zitto Kabwe Kukutana na Viongozi wa Upinzani

$
0
0
ACT-Wazalendo Yafunguka Sababu ya Zitto Kabwe Kukutana na Viongozi wa Upinzani
Baada ya kuenea kwa picha za Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe kuwa na baadhi ya viongozi wengine wa vyama vya upinzani hatimae chama hicho kimeeleza kuwa kiliazimia kuanza kufanya mazungumzo na viongozi wengine wa vyama vya upinzani ili kuunganisha nguvu kwenye mapambano ya demokrasia.

Akiongea na Bongo5 leo, Katibu Itikadi na Uenezi wa Chama hicho, Ndugu.Ado Shaibu amesema kuwa ingawa kila Chama kina Itikadi, sera na programu zake, yapo mambo ambayo Chama cha upinzani hakiwezi kufanya peke yake.

“Kamati Kuu ya Chama chetu iliazimia kuwa Uongozi wa juu wa Chama uanze mazungumzo na viongozi wengine wa Vyama vya upinzani ili kuunganisha nguvu kwenye mapambano ya demokrasia. Ingawa kila Chama kina Itikadi, sera na programu zake, yapo mambo ambayo Chama cha upinzani hakiwezi kufanya peke yake. Moja ya mambo hayo ni mapambano ya kidemokrasia kwa hiyo, Zitto amekwishafanya mazungumzo na Mbowe na Rungwe na atafanya mazungumzo na viongozi wa Vyama vingine,” amesema Ado.

Mambo Yazidi Kuwa Magumu Bunge la Afrika Mashariki

$
0
0

Mambo Yazidi Kuwa Magumu Bunge la Afrika Mashariki
Katika hali inayozidi kuleta mkanganyiko kuhusu ushiriki wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (Eala), wabunge wawili wamechaguliwa wajumbe wa Tume ya bunge bila ya ridhaa yao.

Wabunge hao ni Fancy Nkuhi na Mariam Ussi Yahya ambao Jumatano Desemba 20,2017 walichaguliwa wajumbe wa tume licha ya umoja wa wabunge wa Tanzania katika Eala kutaka majina yao yaondolewe.

Kila mmoja alipata kura 35 katika uchaguzi uliosusiwa na wabunge wote kutoka Burundi.

Habari kutoka ndani ya Bunge zilizothibitishwa na msemaji wa Eala, Bobi Odiko zimesema wabunge wa Tanzania sasa ni wajumbe halali wa Tume licha ya Taifa hili kususia vikao tangu Jumatatu wiki hii.

Taarifa kutoka Eala zinasema wabunge hao walichaguliwa kwa kishindo kuwa wajumbe katika kikao kilichofanyika Jumatano ambacho kilihudhuriwa na wabunge watatu tu kutoka Tanzania.

Odiko alisema ni kweli umoja wa wabunge wa Tanzania ulishamwandikia barua Katibu wa Bunge la Eala mapema wiki hii kuwa majina ya Nkuhi na Yahya yaondolewe katika orodha ya wagombea ujumbe wa Tume ya Eala.

Hata hivyo, alisema ilipofika siku ya uchaguzi wagombea hao walikuwa hawajaondoa majina yao kutokana na utaratibu na ndipo walipochaguliwa kuwa wajumbe wa Tume ambayo kazi yake kubwa ni kuratibu shughuli za Bunge.

"Licha ya Tanzania kususia vikao vya Eala tangu Jumatatu baada ya kukapishwa, kulikuwa na wabunge wasiopungua watatu wakati wa uchaguzi wa wajumbe wa Tume," amesema Odiko.

Wabunge wa Eala kutoka Tanzania na Burundi wamekuwa wakisusia vikao vya Bunge kutokana na utata juu ya uchaguzi wa Spika.

Martin Ngoga alichaguliwa kuwa Spika baada ya vuta nikuvute. Wabunge kutoka Tanzania na Burundi walisusia uchaguzi huo kwa madai kuwa haikuwa zamu ya Rwanda kuteua mgombea.

Huyu Hapa Bingwa wa Magonjwa Sugu Kama Vile Pumu, Vidonda vya Tumbo, Busha, Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa    dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SUPER POWER,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI
SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Rais wa Korea Kaskazini Apiga Marufuku Kuimba, Kunywa na Kufanya Mikusanyiko Wakati wa Kristmas

$
0
0
Rais wa Korea Kaskazini Apiga Marufuku Kuimba, Kunywa na Kufanya Mikusanyiko Wakati wa Kristmas
RAIS Kim Jong Un wa Korea ya Kaskazini amepiga marufuku kuimba, kunywa vileo na kufanya mikusanyiko ya aina yote nchini humo wakati wa Krismasi mwaka huu.

Kwa mujibu wa shirika la ujasusi la Korea ya Kusini (NIS), hatua hiyo inakazia amri ya kupiga marufuku sherehe za Krismasi ya mwaka jana (2016) ikilenga kuzuia nguvu za upinzani nchini humo hususan sasa ambapo vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya nchi hiyo vinaonyesha kuiumiza nchi hiyo.


“Korea ya Kaskazini imeanzisha mfumo wa jumuia za chama tawala kuripoti matatizo ya kiuchumi ya watu wanayokumbana nayo kila siku, na imepiga marufuku mikusanyiko inayohusiana na unywaji wa vileo, uimbaji na burudani nyingine, na imeimarisha udhibiti wa habari kutoka nje,” lilisema NIS.

Fursa za kuitumia sikukuu hiyo kueneza uelewano na furaha zinazidi kufifia katika taifa hilo linalodaiwa kutawaliwa kidikteta na ambalo limepiga marufuku dini zote isipokuwa maadhimisho ya familia iliyoasisi taifa hilo la kikomunisti. Mwaka jana, Kim aliwazuia Wakristo nchini humo kuadhimisha Krismasi na badala yake akawataka kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa bibi yake, Kim Jong-suk, aliyezaliwa siku ya mkesha wa Krismasi mwaka 1919.

Akiwa Mkomunisti aiyebobea, mke wa kwanza wa mwasisi wa taifa hilo la kikomunisti, Kim Il Sung, anafahamika kwa wananchi wa Korea ya Kaskazini kama “Mama Mtukufu wa Mapinduzi”. Miti yenye mapambo ya kuadhimisha Krismasi huonekana katika maduka makubwa ya bidhaa jijini Pyongyang, lakini hakuna alama zozote za kidini.

Lissu Atamani Kurudi Bungeni Afunguka Vitu Anavyovipenda Akiwa Bungeni

$
0
0
Lissu Atamani Kurudi Bungeni Afunguka Vitu Anavyovipenda Akiwa Bungeni
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amesema kuwa anapenda kazi ya ubunge kwasababu ya mapambano ya kisiasa na kiitikadi ndani ya Bunge huku akieleza kuwa una mkaba Waziri mpaka anashindwa kwa kukimbilia.

Lissu akiongea na Azam News amesema kuwa kuna watu wanapenda ubunge kwasababu unapesa au kutokaa foleni.

“Mimi napenda kazi ya ubunge, kuna watu wanapenda ubunge kwasababu una pesa una manufaa unaitwa muheshimiwa hukai kwenye foleni kwanza hukai kwenye foleni mimi napenda ubunge mule ndani ya hasa yale mapambano ya kiitikadi, na kisiasa mule ndani ya bunge, unamkaba waziri mpaka anakosa pakukimbilia, hiyo ndiyo kazi naipenda mimi, hivyo hakuna kazi ninayoimisi mimi kama kazi ya ubunge bungeni,”amesema Tundu Lissu.

Mbunge Lissu alishambuliwa kwa kupigwa risasi eneo la ‘area D’ mjini Dodoma na watu wasiojulikana.

Zitto Aingilia Kati Sakata la Airtel, TTCL Ataka Ukaguzi Maalumu Ufanyike

$
0
0
Zitto Aingilia Kati Sakata la Airtel, TTCL Ataka Ukaguzi Maalumu Ufanyike
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe ameshauri kutazamwa mchakato mzima wa ubinafsishaji kwa kufanya ukaguzi maalumu wa sera ili kutoa mapendekezo ya kurekebisha makosa yaliyofanyika.

Amesema katika kufanya hivyo, suala la Airtel linaweza kushughulikiwa na kupata matunda mazuri zaidi.

Zitto katika taarifa kwenye mitandao ya kijamii leo Ijumaa Desemba 22,2017 amesema Serikali inaweza kuunda tume kutazama namna ubinafsishaji ulivyofanyika na kuchukua hatua za kisayansi baada ya matokeo ya kazi hiyo.

Amesema akiwa kiongozi wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) walifanyia kazi sera ya ubinafsishaji.

“Katika kila taarifa yetu ya mwaka tulikuwa na sehemu maalumu iliyoeleza ufuatiliaji wetu wa utekelezaji wa sera ya ubinafsishaji,” amesema.

Zitto amesema ubinafsishaji wa iliyokuwa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) ni suala walilolitolea taarifa mara kadhaa bungeni na ya mwisho ilikuwa Januari 2015.

“Ni ukweli usio na shaka kuwa kampuni ya Celtel (sasa Airtel) haikulipa chochote kuwezesha kumiliki hisa kwenye Celtel Tanzania na pia uuzwaji wa Celtel kwenda Zain na kisha Airtel ulisababisha Tanzania kupoteza mapato ya kodi ya ongezeko la mtaji (capital gains tax),” amesema.

Hata hivyo, amesema kunahitajika kushughulikia suala la Airtel kwa muktadha wa kazi nzima ya ubinafsishaji nchini.

Zitto amesema PAC iliagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya uchunguzi baada ya ubinafsishaji wa mashirika kadhaa, ikiwemo Benki ya NBC na matokeo waliyawasilisha bungeni.

“Uuzwaji wa NBC nao ulikuwa ni wa bure na huwezi kushughulika na kampuni mojamoja bila kutazama muktadha mzima wa ubinafsishaji wa mashirika ya umma,” amesema.

Yanga SC Yateua Wanachama 28 Kuunda Kamati Mpya ya Mashindano.

$
0
0
Yanga SC Yateua Wanachama 28 Kuunda Kamati Mpya ya Mashindano.
Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara klabu ya Yanga SC imeteua wanachama 28 kwaajili ya kuunda kamati mpya ya mashindano.

Taarifa ya klabu hiyo imeeleza kuwa kamati hiyo itakuwa chini ya Mwenyekiti Hussein Nyika, Makamu wake Mustapha Ulungo na Katibu Mkuu Samuel Lukumay.

Uteuzi huo umefanyika jana katika kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam huku.

Yanga inakamata nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi 21 baada ya mechi 11, ikizidiwa pointi mbili na vinara Simba na Azam FC.

Yanga itasafiri Desemba 31 hadi jijini Mwanza ambapo itakwaana na Mbao FC kwenye uwanja wa CCM Kirumba, ikiwa ni mwendelezo wa mechi za ligi kuu msimu wa 2017/18.

Wajumbe wa Kamati hiyo ni kama inavyoonekana hapo chini.

Wolper Afunguka Kuhusu Kurudiana na Harmonize "Yule ni Njiwa Wangu Nampata Muda Wowote"

$
0
0
Wolper Afunguka Kuhusu Kurudiana na Harmonize "Yule ni Njiwa Wangu Nampata Muda Wowote"
Msanii wa Filamu Bongo, Jacqueline Wolper amefunguka taarifa za kurudiana na Harmonize.

Kauli hiyo inakuraja mara baada ya Wolper kumjibu shabiki mmoja katika mtandao kuwa anaweza kumpata Harmonize kwa wakati wowote.

“Kwanini nimejiaminisha?, sasa yule si njiwa wangu kabisa au hamjui Harmonize njiwa wangu,” amesema.

Hata hivyo amesema kuwa kauli hiyo aliitoa kutokana mtu huyo alimkera hivyo akaamua kutoa neno la kumuumiza pia.

Mabinti Wawili wa Miaka 19 Wadakwa na Polisi kwa Mizi wa Pikipiki Dar

$
0
0
Mabinti Wawili wa Miaka 19 Wadakwa na Polisi kwa Mizi wa Pikipiki
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata watu watatu, wakiwemo mabinti wawili wa miaka 19,  kwa tuhuma za kujihusisha na  wizi wa pikipiki jijini humo.

Hayo yamesemwa leo na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar alipokuwa akitoa taarifa ya oparesheni maalum katika kukabiliana na uhalifu.

“Tumekamata watu watatu kwa tuhuma za wizi wa pikipiki lakini miongoni mwao ni mabinti wawili wa miaka 19 ambao wanatuhumiwa kutumika kama chambo ili kufanikisha mazoezi ya wizi na matukio mengine ya uhalifu.

“Pia tumefanikiwa kuwakamata watu wawili wanaodaiwa kuiba sare za jeshi, ambapo wanatuhumiwa kutumia sare hizo kufanya wizi na matukio mbalimbali ya uhalifu,” alisema Mambosasa.

Aidha jeshi hilo litawafikisha mahakamani watuhumiwa hao pindi litakapokamilisha uchunguzi wake.

Akizungumzia kuhusu Sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya, Kamanda Mambosasa amesema:

“Kuelekea msimu huu wa Sikukuu, tumejipanga vizuri kufanya doria, mpaka sasa jiji la Dar liko salama. Niwaonye wahalifu msijidanganye kujaribu kufanya mabo ya ajabu, tuko imara kuhakikisha Sikukuu zinamalizika salama.”

Mambosasa amepiga marufuku  ‘disko toto’ kwa kuwa disko hizo nyingi hazijakidhi vigezo.  Pia amewataka wazazi kufuata njia salama ya kuwafurahisha watoto wao katika siku hiyo ya Sikukuu.

“Tumeamua eneo la Tanganyika Packers, Kawe,  kuwa ni eneo maalum la kusheherekea kipekee Siku ya Mwaka Mpya. Pia ni marufuku mtu kufyatua fataki siku ya Mwaka Mpya. Tutatoa nusu saa tu katika eneo la Tanganyika Packers kuwa sehemu maalum  ya kupiga hizo fataki,” alieleza Mambosasa.

Waziri Jafo Atoa Agizo Mkurugenzi wa Halmashauri Kuchunguzwa

$
0
0
Waziri Jafo Atoa Agizo Mkurugenzi wa Halmashauri Kuchunguzwa
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Morogoro Vijijini,  Sudi Mussa Mpiri atafanyiwa uchunguzi kutokana na utendaji wake kutoridhisha ikiwemo kushindwa kutekeleza miradi ya maendeleo.

Agizo hilo la kufanyiwa uchunguzi limetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jafo, ameagiza kufanyika uchunguzi wa haraka kwa mkurugenzi huyo baada ya kutoridhishwa na miradi ya maendeleo aliyoitembelea.

Mussa Mpiri anadaiwa kushindwa kutoa ufafanuzi wa fedha zilizopokelewa na Halmashauri hiyo kiasi cha sh.milioni 1.6 ya mapato ya ndani. Imeelezwa pia zaidi ya asilimia 90 ya matumizi ya pesa hizo hayafahamiki hivyo kutia shaka juu ya utendaji wake.



Kufuatia hatua hiyo Waziri Jafo, ameagiza kitengo cha uchunguzi na ufuatiliaji kilichopo Ofisi ya Rais TAMISEMI kufika haraka ndani ya Halmashauri hiyo kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini mwenendo wa Mkurugenzi huyo.

Jafo amewataka madiwani wa Halmashauri hiyo kufahamu kwamba wao wapo kwa niaba ya wananchi wanyonge hivyo wanapaswa kulinda na kusimamia  rasilimali za Halmashauri hiyo.

Aliyekatwa Sikio kwa Kosa la Kulawiti Mtoto wa Miaka Mitatu Akamatwa na Polisi

$
0
0
Aliyekatwa Sikio kwa Kosa la Kulawiti Mtoto wa Miaka Mitatu Akamatwa na Polisi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga  Simon Haule amethibitisha kuwa Jeshi la Polisi Mkoani kwake linamshikilia kijana Msigala Salum (24) kwa tuhuma za kumlawiti mtoto  mwenye umri wa miaka mitatu.


Kamanda Haule  amesema Kijana  huyo aliyejulikana kwa jina la Msigala Salum (24) amekatwa masikio yote mawili na wananchi wenye hasira kali baada ya kumlawiti mtoto huyo mwenye umri wa miaka mitatu katika eneo la Majengo Mapya Kata ya Lubaga Manispaa ya Shinyanga mkoani Shinyanga.

"Tukio hilo limetokea Disemba 20, 2017 majira ya saa tatu asubuhi ambapo kijana huyo anayejishughulisha na shughuli ya kuosha magari mkazi wa Ndala, alimdanganya mtoto huyo wakati akicheza na wenzake nyumbani kwao, kutokana na tukio hilo mtuhumiwa alishambuliwa na wananchi kabla ya Jeshi la polisi kufika eneo la tukio na kumuokoa", amesema Kamanda Haule.

Aidha kamanda Haule ameongeza kwa kusema kuwa mara baada ya tukio hilo baba mzazi wa mtoto huyo alimkamata mtuhumiwa na kumkata masikio yote mawili kwa kutumia kisu na kukimbia, na jeshi la Polisi bado linaendelea kumtafuta.

Aliyekamatwa na Bilioni Mbili Uwanja wa Ndege Apandishwa Kizimbani

$
0
0
Aliyekamatwa na Bilioni Mbili Uwanja wa Ndege Apandishwa Kizimbani
Siku chache baada ya Rais John Magufuli kubainisha kukamatwa kwa kiasi kikubwa cha fedha katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA) aliyekamatwa na fedha hizo amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Mshtakiwa huyo ni Raia wa Uganda, ambaye ni Kalani wa Kampuni ya Ulinzi ya SGA, Winfred  Businge  (33).

Busige amefikishwa mahakamani akikabiliwa na kosa la kushindwa kuelezea kwa mamlaka ya forodha fedha alizokamatwa nazo Airpot ambazo ni USD Milioni moja(takribani Sh.Bil 2).

Wakili wa serikali Mwandamizi, Awamu Mbagwa amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa mshtakiwa anakabiliwa na kosa moja.

Amedai kuwa kosa hilo amelitenda kinyume na kanuni za sheria za utakatishaji fedha, ambayo haimnyimi mshtakiwa dhamana.

Wakili Mbagwa amedai kuwa Businge ametenda kosa hilo December 11, 2017 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Inadaiwa akiwa ndani ya jiji la Dar es Salaam alikutwa ameingia nchini akiwa na USD Milioni 1 (zaidi ya Sh.Bil 2) ambazo alishindwa kuzitolea maelezo kwa wakala wa forodha.

Baada ya kusomewa kosa hilo, mshtakiwa alikana kosa, ambapo wakili Mbagwa alieleza kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na anaomba tarehe kwa ajili ya kumsomea mshtakiwa maelezo ya awali.

Hata hivyo, wakili wa utetezi Emmanuel Safari alimuombea dhamana mteja wake.

Hakimu Shaidi alimuachia mshtakiwa huyo kwa masharti ya dhamana ya mdhamini mmoja bila kusaini bondi.

Hakimu Shaidi amesema amemuachia kwa dhamana bila bondi kwa sababu fedha zilizokamatwa zitakuwa kama dhamana yake. Kesi imeahirishwa hadi January 18,2018.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Haipiti Wiki Bila Kukwaruzana, Nikikaa Kimya Malalamiko

$
0
0
Jamanii mi nna mama mtoto wangu ambaye tunaishi mbalimbali japo sio sana na tupo kwenye uhusiano almost 5 years now

Labda nielezee tabia zetu nikianza kwa upande wangu nna tabia zifuatazo

  • Sipendi kusikia/kuona mwanamke ananikoromea.
  • Ni mwepesi kukasirika Lakini ni mwepesi kurudi katika hali ya kawaida 
  • Nina huruma na Nina jishusha pale ninapokumbuka wapi tumetoka na huyo mzazi mwenzangu/Mke wangu( hatujafunga ndoa)


Huyu mwenzangu ana tabia hizi:-

  • Mbishi sana sometimes hashauriki kwa yale ninayomshauri
  • Mkimya,ila sometimes ana majibu ya ovyo kwangu
  • Mgumu kupiga simu kutuma msg,hadi nimuanze Mimi


Sasa katika mawasiliano na kulingana na tabia zetu nlizozieleza hapo juu huwa tunakwaruzana kwaruzana Mara kwa Mara

Sometimes nikikaa kimya bila kumtafuta atapiga simu atatoa lawama nami najikuta nampandishia kwa hiyo tumekuwa watu wa migogoro ya Mara kwa Mara hadi najiuliza je huyu mwanamke hii kazi yake na mshahara wake unampa kiburi hadi awe na jeuri ya kunipandishia/kunijibu ovyo!?anajua nampenda ndo mana ananifanya mtumwa wa kuanza kumpigia simu kila siku!? , nashindwa kuelewa

N.B Nyie wanawake hata kama mna Mali na kuwapa waume zenu vitu mbalimbali ,kama umeshindwa kumpa heshima yake ni sawa sawa na bure,Mwanaume anahitaji KUHESHIMIWA

By Sigara Kali

IGP Sirro: Malalamiko Yatolewayo na Viongozi wa Upinzani dhidi ya Polisi Katika Uchaguzi Mdogo si ya Kweli

$
0
0
Mkuu wa jeshi la polisi nchini(IGP) Simoni Sirro, amesema tuhuma zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani kuwa polisi walihusika kuwatoa nje wasimamizi wa uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika hivi karibuni si za kweli kwa sababu hajawahi kupokea barua ama malalamiko ndani ya ofisi yake kutoka kwa viongozi hao.

IGP Sirro ameyasema hayo mkoani Lindi, wakati akizungumza na waandishi wa habari na kueleza kwamba tuhuma hizo zinazotolewa na viongozi hao si za kweli kwani hajawai kupata malalamiko hayo na kusema kuwa kama kuna mtu ana ushahidi na tukio hilo atoe taarifa mara moja ndani ya jeshi la polisi ili waweze kupeleleza na kuchukua hatua.

Chanzo; ITV

Ondoa Nyama Uzembe na Kupunguza Mwili Kwa Kutumia Virutubisho vya Edmark

$
0
0
NI VIRUTUBISHO AU CHAKULA MBADALA
ZIMEHAKIKIWA NA TFDA
Ni uhakika kwa afya yako,👉 kupunguza uzito na sumu mwilini,mafuta/lehemu mbaya, Kitambi na nyama uzembe na kutibu MAGONJWA Mbali mbali
@looseweight_trainer ni msaada wako text WhatsApp 0713 777 470 upate suluhisho la afya yako KARIBU
@looseweight_trainer
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>