Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

Young Dee Azawadiwa Gari, Amedai Bongo Hakuna

$
0
0

Young Dee Azawadiwa Gari, Amedai Bongo Hakuna
Tazama Hapa Video:


Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumatatu

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
HARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670 

Rais Aiyefungwa Miaka 12 Aachiwa Huru Kwa Msamaa wa Rais Mwenzake

$
0
0
Rais wa zamani wa Peru, Alberto Fujimori ameachiwa huru kwa msamaha wa Rais wa sasa wa nchi hiyo, Pedro Pablo Kuczynski baada ya kutumikia kifungo chake kwa miaka takribani 12 (tangu 2005).

Fujimori alifungwa kwa kukutwa na hatia ya kupokea Rushwa na kukiuka haki za binadamu. Akiwa hoi kutokana na presha, Fujimori mwenye umri wa miaka 79 amewahishwa hospitali kwa matibabu ya kina.

Duru za siasa nchini humo zinadai kuwa msamaha huo umechochewa na vuguvugu la kisiasa kutoka kwa wapinzani wa Rais aliye madarakani ambao walidhamiria kuwasilisha hoja ya kumng’oa madarakani kwa tuhuma kupokea rushwa kutoka kwa kampuni ya ujenzi ambapo amejitetea kuwa fedha hizo ni malipo ya ada ya ushauri wa kitaalamu.

Wafanyabiashara Wafunguka Ugumu wa Biashara Msimu Huu wa Sikukuu

$
0
0
Wafanyabiashara Wafunguka Ugumu wa Biashara Msimu Huu wa Sikukuu
Leo ni sikukuu ya Krismas ambayo huadhimishwa na Wakristo duniani kote kila ifikapo Disemba 25 kila mwaka, ikiwa ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo, kwa upande wa biashara mambo yamekuwa tofauti, wafanyabiashara wamelia hali kuwa ngumu.


Wafanyabiashara katika Soko la Mwenge wameeleza kuwepo kwa ugumu katika biashara zao wakilalamikia ugumu wa biashara na upatikanaji wa wateja katika sikukuu hizi za mwisho wa mwaka.

Akiongea na kipindi cha Supa Mix cha East Africa Radio leo, mfanyabiashara wa nguo za mitumba katika soko la Mwenge jijini Dar es Salaam Dokta J Pamba, amesema hali ya biashara sio nzuri kwa mwaka huu.

“Hali ni mbaya kibiashara, zamani msimu wa sikukuu watu walikuwa wanakuja na familia zao lakini saivi anakuja mmoja mmoja, watoto wanakuwa nyumbani na mauzo yanakuwa kidogo kwasababu wananunua nguo moja, kiujumla biashara ni ngumu”, amesema Dokta J.

Kwa upande wa wateja waliozungumza na Supa Mix wamesema bei za bidhaa ziko juu na wamekiri kuwepo kwa upandishwaji wa bei katika kipindi hiki cha sikukuu lakini wamedai haiwazuii kufanya manunuzi kutokana na uhitaji walionao.

Hivi Ndivyo Kajala Alivyomshinda Shetani

$
0
0
Hivi Ndivyo Kajala Alivyomshinda Shetani
MKALI wa Bongo Movies mwenye figa matata, Kajala Masanja ‘Kay’ amemshinda shetani kwa kuweza kukaa mwaka mmoja bila kugusa pombe ‘ulabu’ kwani aliamua kufanya uamuzi huo mgumu ambao huwashinda mastaa wengi.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Kajala alisema kuwa, kuna umuhimu wa kujipongeza kwa sababu ndani ya mwaka 2017, hicho ni miongoni mwa mambo makubwa aliyofanikiwa.

“Watu wengi wanajaribu kufanya kama nilivyofanya, lakini inashindikana hivyo kwa kufanikisha hili, ninajipongeza sana kwani nimefanikiwa kumshinda shetani,” alisema Kajala.

Masogange Afunguka Kuhusu Misukosuko Aliyokumbana Nayo Mwaka 2017 "Sitousahau Mwaka Huu"

$
0
0
Masogange Afunguka Kuhusu Misukosuko Aliyokumbana Nayo Mwaka 2017 "Sitousahau Mwaka Huu"
MUUZA nyago mwenye jina kubwa Bongo, Agness Gerald ‘Masogange; amefunguka kuwa, hakuna mwaka aliopata misukosuko kama 2017 na kujikuta akishindwa kufanya vitu vyake vingine.

Akizungumza na Ijumaa wikienda, Masogange alisema kuwa, muda mwingi alishindwa kwenda kufuata biashara zake kutokana na kukabiliwa na kesi mahakamani hivyo kufanya dili zake nyingi kubuma.

“Bora tu 2017 uishe na mambo mengine yaendelee. Ulikuwa ni mwaka mgumu sana kwangu kwa kila kitu kutokana na kesi inayonikabili (ya matumizi ya madawa ya kulevya), labda mwaka mpya ukianza na mambo mengine yataenda vizuri,” alisema Masogange

Bashe Awaangukia Wananchi wa Nzega Awaomba Radhi Aliowakwaza 2017

$
0
0
Bashe Awaangukia Wananchi wa Nzega Awaomba Radhi Aliowakwaza 2017
Mbunge wa Nzega Mjini, kwa tiketi ya (CCM) Hussein Bashe amefunguka na kuwaomba radhi baadhi ya wananchi wa Nzega na Watanzania mbalimbali ambao kwa namna moja au nyingine amewakwaza mwaka huu katika utekelezaji wa majukumu yake.


Bashe amesema hayo kupitia mitandao yake ya kijamii ambapo anatuma salamu za heri ya sikukuu kwa wananchi na watanzania na kudai kuwa wamsamehe pale ambapo amewakosea katika utekelezaji wa majukumu yake ya kibunge.

Ruby Afunguka Mikakati Yake kwa Mwaka 2018

$
0
0
Ruby Afunguka Mikakati Yake kwa Mwaka 2018
BAADA ya kukaa kimya kwa muda mrefu, sexy lady kunako Bongo Fleva, Hellen George ‘Ruby’ amefunguka kuwa, katika mwaka ujao wa 2018 amejipanga kupambana katika gemu.

Ruby alisema kuwa, alikuwa kimya kwa sababu ya kujipanga na mwakani ndiyo ataanza rasmi mapambano ya kimuziki.

“Sijatoa ngoma kwa muda mrefu, lakini mwakani (2018) mashabiki wangu wategemee mambo mazuri sana, kwani ndiyo rasmi nitajikita kwenye gemu maana nilikuwa ninajipanga,” alisema.

Muuza bangi Aingia kimakosa Ndani ya Gari la Polisi Akidhani ni Teksi

$
0
0
Muuza bangi aingia kimakosa ndani ya gari la polisi akidhani ni teksi
Mtu anayeshukiwa kuwa muuza madawa ya kulevya alijipa krismasi asiyoitaka wakati aliingia kwenye teksi akiwa na karibu misokoto 1000 ya bangi na kugundua kuwa alikuwa ameingi kwenye gari la polisi nchini Denmark.

Polisi nchini Denmak walisema kuwa mwanamume huyo alikuwa akirudi nyumbani wakati alifanya makosa hayo mabaya.

Makosa hayo yalitokea katika eneo la Christiana, wilaya moja ya mji mkuu Copenhagen iliyo maarfu kwa biashara ya madawa ya kulevya.

Polisi wanasema kuwa mwanamume huyo atafunguliwa mashtaka, Polisi walisema kuwa walifurahi kumuona, kwani alikuwa amebeba misokoto 1,000 ya bangi.

Bangi ni haramu nchini Denmark.

Polisi wamefanya uvamizi mara kadhaa katika wilaya ya Christiana miezi ya hivi karibuni waliwatafuta wauza madawa ya kulevya .

Ondoa Nyama Uzembe na Kupunguza Mwili Kwa Kutumia Virutubisho vya Edmark

$
0
0
NI VIRUTUBISHO AU CHAKULA MBADALA
ZIMEHAKIKIWA NA TFDA
Ni uhakika kwa afya yako,👉 kupunguza uzito na sumu mwilini,mafuta/lehemu mbaya, Kitambi na nyama uzembe na kutibu MAGONJWA Mbali mbali
@looseweight_trainer ni msaada wako text WhatsApp 0713 777 470 upate suluhisho la afya yako KARIBU
@looseweight_trainer

Mashinji: Wezi wa Mali za Nchi na Waliolipelekea Nchi Hapa ni CCM si Wazungu

$
0
0
Mashinji: Wezi wa Mali za Nchi na Waliolipelekea  Nchi Hapa ni CCM si Wazungu
Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), DR.Vincent Mashinji amefunguka na kusema kuwa watu ambao ni wezi wa mali za nchi na waliolipelekea nchi hapa ilipofika kwa mambo mabaya ni baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).


Mashinji amesema hayo kupitia mtandao wake wa kijamii wa twitter na kusema kuwa Wazungu hawapaswi kulaumiwa kwani wao walikuja na mapendekezo mbalimbali na viongozi wa CCM ndiyo waliyoyapokea huku akidai chama chake cha CHADEMA kilikuwa kikipinga na wakabezwa. 

"Eti Wazungu, wakati wezi ni CCM. Hawa Wazungu wamekuja na mapendekezo CCM ikayapokea kwa mbwembwe na vifijo. Hawakulazimisha, waliridhiana na MaCCM. CHADEMA ikaomba mikataba iletwe bungeni, CCM wakabeza. Mwizi ni nani? Wazungu au CCM?  Amkeni Watanzania, adui yupo hapa hapa na si Wazungu" alisisitiza Mashinji 

Kadinali Pengo Amewataka Wakristo na Watanzania kwa Ujumla Kudumisha Amani

$
0
0
Kadinali Pengo Amewataka Wakristo  na Watanzania kwa Ujumla Kudumisha Amani
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo amewataka wakristo wote na watanzania kwa ujumla kudumisha amani kwa sababu ni tunu inayoliliwa na mataifa yote ulimwenguni.


Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo

Amesema amani haiwezi kuja bure bali kila mtanzania anatakiwa kufanya kazi inayompendeza Mungu usiku na mchana ndipo amani itapatikana. “Kila mtanzania anatakiwa kufanya kazi inayoleta utukufu kwa Mungu kwani ndiyo kazi pekee inayoweza amani na utulivu,” amaesema Pengo.

Askofu Pengo ameyasema hayo katika Mkesha wa Krismasi katika Kanisa la Mtakatifu Maurus Kurasini jijini Dar es Salaam wakati akitoa salamu za Mkesha wa Krismas ambapo alizaliwa Mwokozi Yesu Kristo.

Amesema hakuna njia ya makato ya kuleta na kudumisha amani Tanzania na duniani kwa ujumla zaidi ya kufanya mambo yenye kumpendeza na kumtukuza Mungu. Amemshukuru Rais John Magufuli kwa kuifanya nchi kuwa na amani na mshikamano na amewataka watanzania kila mtu na imani yake kumwombea Rais ili aendelee kuiongoza nchi katika maendeleo anayohitaji Mungu.

Aidha Askofu Pengo amesema kuwa anatambua juhudi zinazofanywa na mataifa mbalimbali na watu mashuhuri kuleta amani duniani lakini akawakumbusha watanzania kuwa ni bora amani inayojengwa na watanzania wenyewe kuliko amani ya kuletewa.

Kwa upande wake Father John Sembuyagi wa Kanisa la Anglikana Tanzania ambaye alikuwa Mgeni Mwalikwa kutoka Jimbo Kuu Dodoma, Dawati la Theolojia amewataka wakristo Tanzania kujenga mazoea ya kuwapeleka watotowao kanisani ili kuwaweka karibu na Mungu. Sembuyagi ameyasema hayo wakati akitoa salamu za mkesha wa Krismasi katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Albano jijini Dar es Salaam.

Amesaema njia pekee ya kuwafanya watoto wetu waseme na Mungu ni kupitia mafundisho kanisani hali inayowasaidia kumjua Mungu na yale yote yanayompendeza na yale yote aliyokataza.

“Tusimfanye Mungu akae kimya juu ya watoto wetu, tusimfanye Mungu akae kimya juu ya familia zetu, tusimfanye Mungu akae kimya juu ya nchi yetu tumfanye Mungu aseme na watoto wetu na familia zetu ili tuwe na viongozi mahiri wa kanisa hapo baadaye,” amesema Sembuyagi.

WCB na Member wa Mafikizolo W alivyotokea party ya Nillan

$
0
0
WCB na Member wa Mafikizolo W alivyotokea party ya Nillan
Siku ya jana December 24, mtoto wa pili wa Diamond Platnumz, Prince Nillan alikuwa akisherekea siku yake ya kuzaliwa ambapo aliandaliwa party nchini Afrika Kusini na kuhudhuriwa na wasanii wa WCB kama Harmonize, Rich Mavoko, Maromboso, Queen Darleen na wengineo, hata hivyo si wao pekee bali na member wa kundi la Mafikizolo, Nhlanhla Nciza alihudhuria. Msanii hayo alikuwepo kwenye party hiyo kutokana na mwaliko alioupata kutoka kwa wazazi
wa Prince Nillan, Diamond na Zari. Kupitia ukurasa wake wa Instagram  Nhlanhla Nciza
ameandika;

A day well spent , Thank You fam ❤️@zarithebosslady@diamondplatnumz for inviting me to @princenillan ‘s birthday party. My son and I had such an awesome time ❤️🎂🎉🎊
#PrinceNillanTurnsOne

Utakumbuka Diamond alishawahi kushirikishwa na Mafikizolo katika ngoma yao iliyokwenda kwa jina Colors of Africa, hivyo hivyo kwa upande wa Harmonize katika ngoma iitwayo Don’t Go.

Taarifa y a Uokoaji Miili ya Watu Walizama Ziwa Tanganyika

$
0
0
Taarifa y a Uokoaji  Miili  ya Watu  Walizama Ziwa Tanganyika
Baada ya kuokoa miili 19 ya watu waliozama katika Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma, Jeshi la Polisi kupitia kwa Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo Switibert Njewike, limesema kazi ya uokoaji bado inaendelea.


Njewike ambaye ni Kamishina Msaidizi wa Polisi amesema wanatafuta miili mingine 3 ili kutimiza idadi ya watu 22 ambao wanakadiliwa kuwa walikuwemo kwenye mtumbwi ambao uligongwa na boti na kuzama majini.

“Kazi ya uokoaji inaendelea, hadi jana tumefanikiwa kuokoa miili 19 na tunaendelea kutafuta miili mingine mitatu ili kufikia idadi ya watu 22 kama ambavyo makadilio ya awali yalieleza kuwa mtumbwi huo ulibeba watu 22”, amesema Kamanda Njewike.

Kwa upande mwingine Kamanda Njewike amewataka madereva wa vyombo mbalimbali vya usafiri nchi kavu na majini ikiwemo Mitumbwi, bodaboda na magari ya abiria kuzingatia sheria za usafiri na usalama barabarani ili kuepusha ajali hususani kipindi hiki cha sikukuu.

Ajali hiyo ilitokea usiku wa kuamkia Ijumaa ikihusisha boti iliyokuwa inatoka Kigoma mjini kwenda Kalya na mtumbwi wa MV Pasaka uliokuwa ukitoka kijiji cha Kalilani kwenda Sunuka.

Moshi Pafulika Yaelemewa na Wageni

$
0
0
Moshi Pafulika Yaelemewa na Wageni
Mikate jana asubuhi iligeuka bidhaa adimu katika maduka makubwa mjini hapa, kutokana na wingi wa wateja uliosababishwa na utamaduni wa wenyeji wa Mkoa wa Kilimanjaro kusherehekea sikukuu za mwisho wa mwaka walikozaliwa.

Mbali ya wingi wa wageni waliorejea kusherehekea sikukuu, msongamano wa magari katikati ya mji na barabara ya njia panda ya Himo-Moshi jioni unaonekana kuvunja rekodi.

Maduka makubwa ya bidhaa (supermarkets), jana asubuhi yalikuwa hayana mikate kutokana na mingi kununuliwa juzi na wenyeji wanaoenda vijijini kwa ajili ya sikukuu.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kati ya saa mbili asubuhi hadi saa nne uliobaini upungufu wa mikate na wasambazaji walichelewa kuisambaza.

Katika baadhi ya maeneo mikate iliyokuwepo ni iliyokaa dukani kwa zaidi ya siku mbili.

“Hatuna kabisa mikate, ilimalizika jana (juzi) usiku kwenye saa tatu. Wateja walikuwa wengi na kila mmoja alinunua mkate mmoja au miwili kwa ajili ya kwenda nayo kijijini,” alisema mhudumu mmoja.

Katika maduka hayo, bidhaa nyingine iliyonunuliwa kwa wingi ni bia na pombe kali.

Vilevile kulikuwa na misururu mirefu ya wateja wakinunua bidhaa hizo na kupakia kwenye magari. Wateja pia walikuwa wengi kwenye masoko ya Mbuyuni na Kati.

Mji wa Moshi kwa siku tatu mfululizo hadi jana umeonekana kuelemewa na wingi wa magari.

Barabara Kuu ya Dar es Salaam -Moshi, ndiyo iliyotia fora kwa msongamano wa magari kuanzia saa kumi na moja jioni hadi saa tatu usiku. Nyingine iliyokuwa na msongamano ni ya kutoka stendi kuu hadi mzunguko wa magari wa YMCA.

Kutokana na msongamano huo, magari yalikuwa yakitumia hadi dakika 40 kutoka eneo la Stop and Shop karibu na Kiboriloni hadi katikati ya mji, wakati kwa siku za kawaida huchukua kati ya dakika tatu hadi tano.

Msongamano pia ulikuwepo barabara lilipo Kanisa Katoliki la Kristo Mfalme hadi masoko ya Mbuyuni na Kati na barabara ya kuelekea Arusha.

Askari wa usalama barabarani wamejikuta katika wakati mgumu wa kuongoza magari kuanzia barabara ya Polisi Majengo, mzunguko wa magari wa YMCA na soko la Mbuyuni.

Gazeti hili lilishuhudia waendesha pikipiki maarufu bodaboda wakihusika katika ajali wengi kwa kugonga magari kwa nyuma ikidaiwa hilo linachangiwa na kutokuwa wazoefu wa foleni kama ilivyo jijini Dar es Salaam.

Mmoja wa wenyeji wa Mkoa wa Kilimanjaro anayeishi Dar es Salaam ambaye jana alikuwa kijijini kwao Mwika, Moshi Vijijini, William Shao alisema kwa sasa kinachoendelea ni masuala ya kunywa na kula.

“Huku ni sherehe tu tunakula na kunywa, tena kuna ile Mbege (pombe ya asili kwa Wachaga) original (halisi) kabisa. Ni ndafu, mbege na kula. Huu ni utamaduni mzuri sana,” alisema Shao.

Ahadi Yangu Iko Palepale Nikitiza Miaka 30 Bila Kupata Mtoto Nitafunga Kizazi- Wema Sepetu

$
0
0
WEMA Isaac Sepetu amefunguka kuwa, kamwe hawezi kuvunja kiapo alichoweka kuwa akitimiza umri wa miaka 30 bila kupata mtoto atafunga kizazi.

Wema aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, kuwa alitoa ahadi kuwa atakapofikisha umri wa miaka 30 bila kunasa ujauzito, basi atafunga kizazi na kwenda kuasili mtoto.

“Mwaka ndiyo hivyo unaisha, lakini ahadi yangu iko palepale. Kama kweli sitanasa ujauzito hadi nagonga miaka 30 kamili, lazima nifanye nilivyoahaidi na nitaenda kuasili mtoto,” alisema Wema ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 29.

Baba Aaswa Gest na Mwanaye wa Kumzaa

$
0
0
Baba Aaswa Gest na Mwanaye wa Kumzaa
KIMENUKA! Fadhil Mshamu, mkazi wa Kibaha mkoani hapa anakula Krismasi na Mwaka Mpya wa 2018, akiwa na stresi kufuatia kusomewa shitaka la kumdhalilisha binti yake wa kumzaa jina linahidhiwa kwa sababu za kimaadili.

Kesi hiyo ilitajwa wiki iliyopita ambapo itaanza rasmi kusikilizwa mapema Mwezi Januari, mwakani katika Mahakama ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani.



Mshamu alikutwa na kasheshe hilo baada ya miezi kadhaa kunaswa akiwa na binti yake wa kumzaa kwenye nyumba moja ya kulala wageni (gesti) huko Kibaha huku kukiwa na madai ya kumtaka kingono.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, Mshamu alinaswa akiwa na binti yake huyo baada ya kuwekewa mtego kufuatia taarifa za kumsumbua kwa muda mrefu akidaiwa kumtaka kimapenzi.

Kwa mujibu wa chanzo chetu kutoka ndani ya familia ya Mshamu, baada ya kunaswa kwenye mtego huo uliowashirikisha polisi na ndugu wa familia hiyo, Juni 26, mwaka huu, Jeshi la Polisi lilimfungulia Mshamu jalada la uchunguzi ambalo lilipelekwa kwa Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Serikali (DPP) ambapo naye baada ya kuiona kesi hiyo, aliamuru ipelekwe mahakamani.

Ndugu huyo wa familia alilieleza gazeti hili kuwa, kufuatia sakata hilo, wiki iliyopita Mshamu alifikishwa mahakamani hapo na kusomewa shitaka la kutaka kumdhalilisha binti yake huyo ambaye ni mwanaye wa kumzaa kisha kutajwa tarehe ya kuanza kusikilizwa.

Kesi hiyo inatarajiwa kusikilizwa mahakamani hapo Januari 2, mwakani ambapo waandishi wetu wataendelea kufuatilia sakata hilo mahakamani hapo na kukuletea habari kamili.



AMA kweli mastaa hawaishiwi vimbwanga! Hayo yalidhihirika usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita baada ya staa wa kike wa Bongo Fleva, Esterlina Sanga ‘Linah’ kudaiwa kutelekeza mwanaye mchanga na kunaswa akibanjuka na jamaa ambaye ni meneja wa wasanii wa Bongo Fleva, Petit Man.

Tukio hilo lililonaswa na Ijumaa Wikienda lilijiri ndani

Breaking News;Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Kilimba Amepata Ajali na Familia Yake

$
0
0
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Juma Kilimba amepata ajali ya gari lake kupinduka leo akiwa na familia yake, wamepelekwa katika hospital ya Wilaya ya Kiomboi kwa ajili ya matibabu.

Barnaba Classic Atangaza Kuachana na Mziki

$
0
0
Barnaba Classic Atangaza Kuachana na Mziki
Ikiwa zimebaki siku sita tu kabla ya kuumaliza mwaka 2017 na kuingia 2018, staa wa Bongofleva Barnaba Classic ametangaza kuwaaga mashabiki wake kwa mwaka huu na atakuwa kimya kimziki kwa muda.


Mkali huyo wa sauti na uandishi kwenye kiwanda cha mziki Bongo, ameweka wazi kuwa ukimya wake utaanzia kwenye mitandao ya kijamii ikiwa ni sehemu ya kujiandaa na kujipanga namna ya kuuanza kwa kishindo mwaka 2018.

“Nikiwa najitoa kwenye mitandao ya kijamii kidogo, ningependa kuwatakia mashabiki, marafiki na familia yangu Heri ya Christmas na Mwaka Mpya”, amefunguka Barnaba kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Pamoja na kujitoa kwake nyota huyo anayetemba na ngoma yake ya Mapenzi Jeneza ameongeza kuwa anajiweka vizuri kuanzia mwonekano mpaka sound ya hit zake zijazo.

“Ninapumzika kidogo ili kuweka mipango yangu vizuri kwaajili ya mwaka 2018. Nitawaletea Barnaba mpya mwenye kila jipya kimuziki na hata Sound” ameongeza.
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live




Latest Images