Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live

RPC Kagera: Hali ya Shabiki Aliyepigwa na Nyoso Bado ni Mbaya Yupo Mikononi mwa Madaktari

$
0
0
RPC Kagera: Hali ya Shabiki Aliyepigwa na Nyoso Bado ni Mbaya  Yupo Mikononi mwa Madaktari
Kufuatia tukio la beki wa klabu ya Kagera Sugar, Juma Nyoso kudaiwa kumpiga shabiki hadi kuzimia baada ya mchezo wao na timu ya Simba hali iliyopelekea kukamatwa na Jeshi la Polisi Mkoani Kagera.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Agustine Ollomi amesema hali ya majeruhi anaye fahamika kwa jina la Shabani Hussein mwenye umri wa miaka 33 bado ni mbaya na yupo mikononi mwa madaktari huku mtumuhimiwa akiwa sero hado hapo upelelezi utakapo kamilika.

Kamanda Ollomi ameyasema hayo hapo jana mbele ya waandishi wa habari mara baada ya tukio hilo.

Leo kulikuwa na hiyo mechi ya ligi kuu kati ya Simba SC na Kagera Sugar, mechi ilikwenda salama hadi kumalizika kwa timu ya Simba kupata ushindi wa magoli 2-0.

Sasa wa kati wanatoka uwanjani mashabiki walikuwa ni wengi , yuko mmoja anaonekana kama wa Simba alikuwa anapuliza vuvuzela kwahiyo katika kupuliza kwake akawa anampulizia Juma Nyoso mchezaji wa Kagera Sugar ambaye ameshindwa.

Ilikuwa ni katika hali ya ushabiki lakini huyu mchezaji wa Kagera Sugar, Juma Nyoso aligeuka na kumshika yule shabiki akawa amemkunja akampiga futi la mguu akawa amepata jeraha kwenye paji la uso akazimia.

Majeruhi amechukuliwa na kukimbizwa kwenye hospitali ya Mkoa hapa Bukoba kwaajili ya matibabu haliyake bado siyo nzuri kwasababu alipoteza fahamu palepale madaktari wapo wanaendelea kuweka haliyake sawa.



Kamanda Ollomi amesema kuwa kitendo alichofanya mchezaji Juma Nyoso ambaye kwa sasa yupo sero kimevuruga raha ya mchezo huo huku akisema kuwa majeruhi wa tukio hilo anaitwa Shabani Hussein mwenye umri wa miaka 33.

Bata Hili la Alikiba Katika Mbuga za Wanyama Serengeti Balaa Tupu

$
0
0
Bata Hili la Alikiba Katika Mbuga za Wanyama Serengeti Balaa Tupu
Msanii wa muziki Bongo, Alikiba ameitembelea mbuga ya wanyama ya Serengeti National Park.

Alikiba ame-share picha kadhaa katika mtandao wake wa Instagram zikimuonyesha akiwa Serengeti, hata hivyo haijafahamika iwapo matembelezi hayo ni kwa ajili ya kazi au matunuzi pekee.

Si mara ya kwanza kwa Alikiba kufanya jambo kama hilo, mwaka 2015 yeye pamoja na team yake ya RockStar4000 walitembelea hifadhi ya Tarangire, Pia mwaka 2016 alikuwepo Serengeti kwa ajili ya kusherekea birthday  yake.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.


NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.


MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA.


MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.


NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,


Je unamali yako unauza hupati wateja?

Wasiliana nami 0716-263605


DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale

Aunt Ezekieli:Sina Kawaida ya Kuweka Maisha Yangu Kwenye Mitandao Ila Huku Tunakoendea Dah! Wanaume!

$
0
0
Aunt Ezekieli Yamemfika Hapa..... "Dah!wanaume!"
Muigizaji kutoka Bongo Movie Aunty Ezekiel amechukua headlines  katika mitandao ya kijamii baada ya kupost caption ambayo imeacha maswali kwa baadhi ya mashabiki kupitia ukurasa wake wa instagram na wengi kutafsiri hueda akawa kwenye migogoro na baba mtoto wake Mose Iyobo.

 “Sina kawaida ya kuweka Maisha yangu kwenye Mitandao ila huku tunakoendea 🙌 Dah!wanaume!!!!👍“

Ingawa Aunt Ezekiel ni miongoni mwa waigizaji kutoka Bongo Movie ambao hawapendelei kuweka maisha ya mahusiano yao ya kimapenzi katika mitandao ya kijamii.

Breaking News: Nabii Tito Akamatwa na Polisi Mkoani Dodoma

$
0
0
Breaking News: Nabii Tito Akamatwa na Polisi Mkoani Dodoma
JESHI la Polisi Mkoa wa Dodoma inadaiwa limemtia mbaroni mkazi mmoja wa mkoani humo anayejitangaza kama nabii, Tito Machija, ambaye amekuwa akionekana mitandaoni akifanya mambo yasiyoendana na maadili ya dini na injili anayodai kuihubiri.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro,  amezungumza na ‘mhubiri binafsi’ huyo licha ya jeshi hilo kutotoa taarifa rasmi ya kilichojiri na utaratibu unaoendelea iwapo ni kumhoji au kumfikisha mahakamani.

Nabii huyo ambaye video zake zimesambaa akihamasisha kuoa mke zaidi ya mmoja, ikiwa ni pamoja na kutembea na wafanyakazi wa ndani,  anatumia pombe kunasa waumini na anadai hataki nyimbo za injili kwenye ‘ibada’ zake, ambazo nyingi hufanyikia baa.

Aidha ameonekana akicheza nyimbo za Bongo Fleva akiwa ‘madhabahuni’ badala ya kwaya na huku akieleza kuwa wafadhili wake wanatumia pombe,  hivyo na yeye lazima waumini wake watumie pombe ambazo amezifanyia upako.

Jaji Mkuu Awaonya Wanasiasa na Viongozi wa Serikali

$
0
0
Jaji Mkuu Awaonya Wanasiasa na Viongozi wa Serikali
Jaji Mkuu wa Tananzania, Profesa Ibrahimu Juma amewataka viongozi wa serikali na vyama vya siasa kuacha mara moja vitendo vya kuingilia mhimili wa Mahakama na kuvunja amri zake.

Jaji Profesa Juma ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wiki ya Sheria inayotarajiwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi ujao (Februari mosi), siku ambayo ndio itakayoashiria kuanza rasmi kwa shughuli za Mahakama kwa mwaka huu 2018 yatakayofanyika katika viwanja vya Mahakama vilivyopo mtaa wa Chimala jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi atakuwa Rais John Magufuli.

"Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania mamlaka ya utoaji haki ni ya Mahakama tu, nawasihi viongozi wote wa serikali wenye mamlaka za kikatiba na kisheria wabaki ndani ya maeneo yao ya Kikatiba na wajiepushe kuingilia maeneo yaliyo ndani ya haki, hadhi na Mamlaka ya Kikatiba ya Mahakama", alisema Jaji Profesa Juma.

Kwa upande mwingine, Jaji Profesa Juma ametoa rai kwa wananchi na wadau wote wa sheria kutembelea Mnazi Mmoja kwa ajili ya kujifunza na kupata huduma mbalimbali za Kisheria kutoka kwa Majaji, Mahakimu, Wasajili, Watendaji, Mawakili wa serikali na Mawakili wanaojitegemea ambao watakuwa tayari kuwasikiliza na kuwahudumia ipasavyo.

Matumizi ya Bangi Yahalalishwa na Gavana Bila Kupiga Kura Marekani

$
0
0
Matumizi ya Bangi Yahalalishwa na Gavana Bila Kupiga Kura Marekani
Kwa mara ya kwanza, jimbo la Marekani limehalalisha bangi kwa kuweka saini na si kwa kupiga kura.

Gavana wa jimbo la Vermont, Phil Scott amesaini muswada wa sheria namba 511 (House Bill 511) ambao unahalalisha kumiliki bangi za uzito usiopungua wakia moja na kuondoa adhabu za makosa ya kumiliki mimea iliyokomaa isiyozidi miwil au miine ambayo haijakomaa.

Hata hivyo, sheria hiyo haizungumzii lolote kuhusu kuanzishwa kwa soko kwa ajili ya mmea huo. Sheria hiyo itaanza kufanya kazi Julai, imeandika yahoo.com ikikariri tovuti ya HuffPost.

“Leo, kwa hisia tofauti, nimesaini H. 511,” alisema Scott katika taarifa aliyoituma kwa Bunge la jimbo hilo.

"Binafsi naamini kwamba ambayo ambayo watu wazima wanafanya ndani na kwenye nyumba zao ni chaguo lao, ili mradi tu hayana athari hasi kwa afya na usalama kwa wengine, hasa watoto.”

Kwa saini hiyo ya Scott, Vermont itaungana na majimbo mengine nane yaliyohalalisha bangi, ikiwa ni pamoja na Washington, D.C., katika wimbi linaloendelea kukua kufanya maamuzi yanayopingana na serikali ya shirikisho.

Serikali ya Marekani bado inaiweka bangi  katika jedwali la kwanza la madawa, ikiwa pamoja na dawa ya kulevya aina ya heroin na LSD.

Vermont ilihalalisha matumizi ya bangi kwa matibabu mwaka 2004, na sasa ni miongoni mwa majimbo 30, pamoja na nchi za Guam na Puerto Rico, na Wilaya ya Columbia, zilizohalalisha bangi kwa ajili ya matibabu.

Ingawa majimbo mengine yamehalalisha bangi kwa kutumia kura ili wananchi waamue, Vermont hairuhusu mchakato kama huo, badala yake wabunge wa jimbo hilo wamekuwa wakishughulikia suala hilo kwa kutaka mabadiliko ya sheria.

Muswada kama huo uliwasilishwa mezani kwa Scott mwaka jana, lakini alikataa kuupitisha, akisema kulikuwa na matatizo katika lugha iliyotumika katika adhabu kwa watakaobainika kuuza bangi kwa watoto na uanzishwa wa kamisheni kwa ajili ya kutafiti jinsi sheria sheria za kusimamia soko la bangi zitakavyofanya kazi katika jimbo hilo.

WhatsApp Waruhusu Video za Youtube Kucheza Kwenye Programu Yao

$
0
0
WhatsApp Waruhusu Video za Youtube Kucheza Kwenye Programu Yao
Baada ya muda mrefu WhatsApp kutangaza kuwa itafanya maboresho makubwa matano kwa mwaka huu tayari, Program hiyo imeanza maboresho hayo kwa kuanza kuruhusu video za YouTube kucheza moja kwa moja kwenye Programu wezeshi yao.

Program hiyo ilianza kuruhusu kwanza kwa watumiaji wa iOS mwanzoni mwa mwezi Januari mwaka huu lakini kwa sasa imeruhusu kwa watumiaji wa Android ambapo mtumiaji kama bado hujaona maboresho hayo itakubidi u-update kifaa chako ili uweze kupata huduma hii mpya.

Awali WhatsApp ilikuwa inaruhusu link tu kwenye programu hiyo ambapo mtumiaji alikuwa analazimika kubofya Link na kupelekwa moja kwa moja kwenye App ya YouTube.

Maneno ya Mwigulu Nchemba Baada ya Nabii Tito Kukamatwa na Polisi "“Udhalilishaji wa Aina Yoyote Ile Haukubaliki ''

$
0
0
Maneno ya Mwigulu Nchemba Baada ya Nabii Tito Kukamatwa na Polisi " “Udhalilishaji wa Aina Yoyote Ile Haukubaliki (Kijinsia,Dini n.k)”
Mchana wa leo January 23, 2018 Jeshi la Polisi mkoani Dodoma linamshikilia mkazi mmoja wa Dodoma Tito Machibya maarufu kama Nabii Tito, ambaye amekuwa akionekana mitaani kuhubiri huku akiwa anakunywa pombe hivi sasa maelezo yake yanachukuliwa .

Kupitia ukurasa wake wa instagram Waziri wa Mambo ya Ndani Dr. Mwigulu Nchemba amesema ni kwa tuhuma za udhalilishaji, Namnukuu Dr. Mwigulu >>>  “Udhalilishaji wa aina yoyote ile haukubaliki(Kijinsia,Dini n.k)”

Tulijipanga Ila Makosa Mawili Ndio Yametugharimu -Mexime

$
0
0
Tulijipanga Ila Makosa Mawili  Ndio Yametugharimu -Mexime
Baada ya timu ya Kagera Sugar kupoteza point tatu nyumbni kufuatia mechi yao dhidi ya Simba Sports Club iliyochezwa katika uwanja wa Kaitaba ndani ya manispaa ya Bukoba, Kocha wa timu hiyo Mecky Mexime ameeleza walipokosea.

Mexime amesema kuwa kikubwa walijipanga vizuri lakini wamefanya mistake mbili na hizo ndo zimewaadhibu na ameongeza kuwa bado wanajipanga hawajakata tamaa na wanaamini watapata tu matokeo.

Jeshi la PolisiYadai Nabii Tito Ana Matatizo ya Akili Apelekwa Kupimwa Milembe

$
0
0
Jeshi la Polisi: Nabii Tito Anamatatizo ya Akili
JESHI la Polisi mkoani Dodoma,  baada ya kumkamata na kumfanyia mahojiano Onesmo Machija (44) anayejiita ‘nabii’ Tito, kutokana na mahubiri ya kidini anayoyafanya, limesema mtu huyo ana  matatizo ya akili.

 Akizungumza na wanahabari mjini Dodoma leo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Gillesi Muroto, amesema mnamo Juni 23, 2014, mtu huyo aliwahi kulazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu ya akili chini ya daktari aliyejulikana kwa jina moja la William ambapo aliporuhusiwa alitakiwa kurejea hospitalini hapo Julai 9 mwaka huohuo lakini hakurejea.

Kamanda Muroto aliendelea kusema kwamba baada ya hapo, Machija ambaye kanisa lake halijasajiliwa popote,  aliibukia mkoani Dodoma katika kijiji cha Nong’ona kilicho karibu na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) akifanya  mahubiri ya kidini yaliyodaiwa kuwa hayakuwa na maadili ya kidini.

Kwa msingi huo, alisema jeshi la polisi limempeleka Hospitali ya Rufaa ya Mirembe iliyoko mkoani Dodoma  kwa ajili ya kumpima tena matatizo hayo ya akili na baada ya majibu kutolewa,  Dkt. Dixon Philipo aliyemshughulikia alithibitisha kwamba bado ana matatizo hayo.

Pamoja na hayo, Muroto alisema jeshi la polisi mkoani humo  bado linaendelea kumshikilia kutokana na matendo yake aliyoyafanya ili kufanya uchunguzi zaidi.

TFF Yasubiria Ripoti ya Kamishna wa Michezo Ili Kumuadhibu Nyoso

$
0
0
TFF Yasubiria Ripoti ya Kamishna wa Michezo Ili Kumuwajibisha Nyoso
Baada ya beki wa Kagera Sugar, Juma Nyoso kudaiwa kumpiga shabiki wa Simba hapo jana, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema linasubiri ripoti ya kamishina wa mchezo huo ili kumchukulia hatua za kinidhamu.

Nyoso alishikiliwa jana na polisi kwa kosa la kumpiga shabiki huyo wa Simba aliwahi kufungiwa kwa miaka miwili kwa makosa ya utovu wa nidhamu.

Afisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo alisema ripoti wa kamishina iteleza kama beki huyo alifanya kitendo hicho cha utovu wa nidhamu.

"Kanuni zipo wazi hivyo hiyo ripoti itafikishwa kwa kamati ya saa 72 ambayo na wenyewe watafanya kazi yao na baadaya hapo tamati itakuwa kwa kamati ya nidhamu," alisema Ndimbo.

"Bob Junior Anaogopa Kusema Ukweli" - Amber Lulu

$
0
0
"Bob Junior Anaogopa Kusema Ukweli" - Amber Lulu
Msanii Amber Lulu hapo jana alikanwa kuwahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msanii Bob Junior, amefunguka na kudai kuwa msanii huyo anaogopa kusema ukweli.


Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv Amber Lulu amesema tukio hilo lilitokea siku nyingi akiwa mdogo, hivyo huenda Bob Junior anaogopa kukiri kwa kuwa lilikuwa kosa kisheria.

"Sasa kwa nini nimsingizie, labda anaogopa lakini ilikuwa siku nyingi na nilikuwa mdogo, sina sababu ya kumsingizia kweli nilikuwa naye, labda uoga wake, nimsingizie mimi na yeye nani ana kiki!", amesema AMber Lulu.

Hapo jana Bob Junoir alikana kuwahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msanii AMber Lulu akiwa mwanafunzi wa kidato cha pili, baada ya Amber Lulu kutoa siri hito huku akisema ndiye aliyemleta Dar es salaam.

Msimamizi wa Uchaguzi Kinondoni Atupilia Mbali Mapingamizi ya Wagombea Katika Jimbo Hilo

$
0
0

Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Kinondoni ambaye pia mkurugenzi wa manispaa hiyo, Aron Kagurumjuli ameyatupilia mbali mapingamizi matatu yaliyowasilishwa na wagombea wa vyama vya Chadema, CCM na CUF.

Mapingamizi hayo ni kwa mgombea wa CUF, Rajab Juma kumwekea mgombea wa Chadema, Salumu Mwalimu, wakati Mwalimu yeye alimwekea Maulid Mtulia wa CCM na mgombea huyo wa chama tawala alimwekea mgombea wa SAU, Johnson Mwangosi.

Baada ya jana ofisi ya msimamizi wa uchaguzi kutoa barua ya utetezi kwa wagombea waliowekewa mapingamizi leo Jumanne imetoa majibu ya kuyatupilia mbali mapingamizi hayo.

Akizungumza na Mwananchi leo, Jumanne Januari 23, 2017, Kagurumjuli amesema “Tumeyatupilia mbali mapingamizi yao kwa sababu hayana mashiko, kilichobaki ni wagombea kwenda uwanjani wakapambane,” amesema msimamizi huyo.

RPC Aweka Wazi Sababu Kukamatwa Msigwa

$
0
0
RPC Aweka Wazi Sababu Kukamatwa Msigwa
Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa, (RPC) Julius Mjengi amefunguka na kuweka wazi sababu zilizopelekea kumkamata Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa na kudai kuwa walimkamata wakimtuhumu kuratibu kuchoma na kubomoa nyumba.


Mjengi amesema hayo leo Januari 23, 2018 wakati akiongea na www.eatv.tvna kudai kuwa Mbunge huyo jana alipokamatwa alihojiwa na baadaye aliachiwa kwa dhamana hivyo yupo huru kwa dhamana toka jana majira ya saa tano usiku.

"Jana Msigwa alijisalimisha baada ya kusikia tunamtafuta hivyo tulimuhoji na usiku alipata dhamana, hivyo sisi tulikuwa tunamtafuta kwa tuhuma za kuratibu matukio mawili ya uhalifu hapa Iringa Mjini ambapo kuna nyumba ya diwani mmoja ambaye alijiuzulu na kuhama CHADEMA na kuhamia CCM nyumba yake pagale lilibomolewa"

Kamanda aliendelea kusema kuwa 

"Lakini pia usiku wa kuamia tarehe 17 kuna nyumba moja Kihesa ilichomwa moto ikateketea na ndani mle katika wapangaji mmoja alikuwa ni Katibu wa UVCCM Wilaya ya Iringa Mjini kwa hiyo Msigwa ana tuhuma za kuratibu matukio haya, kwa hiyo tulimuhoji na kudhamini ila tunaendela naye" alisisitiza Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa, (RPC) Julius Mjengi 

Kenya Yatengeneza Setilaiti Yake ya Kwanza

$
0
0
Kenya Yatengeneza Setilaiti Yake ya Kwanza
Kenya imetengeneza setilaiti yake ya kwanza kabisa ambayo imepangiwa kurushwa anga za juu Machi mwaka huu.

Wahandisi kutoka chuo kikuu cha Nairobi, wakisaidiwa na maafisa kutoka shirika la anga za juu la Japan walitenengeza chombo hicho katika mradi uliogharimu zaidi ya dola milioni moja.

Setlaiti hiyo itatumika kuchunguza mienendo ya kilimo, pamoja na kuchunguza maeneo ya pwani ya taifa hilo.

Mwandishi wa BBC Tomi Oladipo anasema setilaiti hiyo ni ya umbo la mchemraba na ina ukubwa wa sentimita 10 mraba - hujulikana kama nano-setilaiti.

Setlaiti hiyo itatumwa hadi Kituo cha Kimataifa cha Anga za Juu (ISS) mnamo mwezi Machi na kuzinduliwa rasmi kuizungukza dunia na roboti mwezi mmoja baadaye.

Hatua hiyo itaifanya Kenya kuwa miongoni mwa mataifa sita barani Afrika yaliyo na setilaiti zinazoizunguka dunia.

Kundi la wahandisi kutoka chuo kikuu cha Nairobi walioitengeza walikuwa kundi la kwanza kufaidika kutokana na mradi wa pamoja kati ya Umoja wa Mataifa na shirila la anga za juu la Japan unaolenga kuzisaidia taasisi za elimu kutoka mataifa yanayostawi kutengeneza setilaiti zao.

Wenger Aweka Wazi Kuhusu Aubamayeng

$
0
0
Wenger Aweka Wazi Kuhusu Aubamayeng
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amesema usajili wa nyota wa klabu ya Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang, hauko kwenye hatua nzuri za kukamilika na ataendelea kutumia washambuliaji waliopo.


Wenger amesema hayo mchana huu wakati akiongea na wanahabari kuelekea mchezo wa kesho wa nusu fainali ya kombe la ligi EFL dhidi ya Chelsea.

''Hatujakamilisha usajili wa Aubameyang wala mchezaji mwingine, lakini tunaendelea na maongezi hivyo siwezi kusema kama tutampata au tutamkosa, tuna washambuliaji wengine na tutaendelea nao'', amesema Wenger.

Aubameyang raia wa Gabon mwenye umri wa miaka 28 anatajwa kuwa na thamani ya € 65 milioni takribani shilingi bilioni mbili.

Kuhusu mchezo wa kesho Wenger amesema washambuliaji wake Danny Welbeck na Olivier Giroud bado hawako vizuri hivyo hajajua kama watacheza au hawatacheza.

Arsenal itaelekea darajani katika mchezo wa kesho ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Chelsea kwenye mchezo wa kwanza uliopigwa Emirates wiki iliyopita.

Man Fongo Atokwa na Povu

$
0
0
 Man Fongo  Atokwa na Povu
Msanii wa miondoko ya singeli Man Fongo amewaomba wasanii wenzake kama kuna yeyote yule anahisi amemuibia kazi yake ya sanaa kwa namna moja ama nyingine basi asisite kwenda kumshtaki Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) ili waweze kuhakiki haki miliki.

Man Fongo amebainisha hayo baada ya kusakamwa takribani wiki moja sasa kwa kudaiwa kutumia kazi ya wasanii wenzake bila ya makubaliano ya aina yoyote waliyowekeana.

"Ni kweli nimepigiwa simu na watoto wa Baraka Mwishee wakitaka kufuatilia hati miliki ya ule muziki. Kwa hiyo hata kama kuna mtu mwingine anaona mimi nimemuibia muziki wake asiogope kufuatilia hati miliki kwa sababu huu muziki wetu tunausajili BASATA. So ukiwa unaongea ongea mimi najua ni 'blah blah' tu hizo wanaotafuta kiki kutoka kupitia mgongo wangu", alisema Man Fongo pindi alipohojiwa katika kipindi cha eNewz kutoka EATV.

Tangu Nimtongoze Zari, Hadi Sasa Sijawahi Kutongoza Msichana Mwingine- Diamond

$
0
0
Tangu Nimtongoze Zari, Hadi Sasa Sijawahi Kutongoza Msichana Mwingine- Diamond
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ameweka wazi kuwa tangu amtongoze mzazi mwenzie, Zari mwaka 2014 ndio ilikuwa mara yake ya mwisho kufanya hivyo hajawahi tena kutongoza mwanamke mwingine.

Diamond Platnumz amesema kuwa hawajahi kutongoza mwanamke mwingine kwa sababu yupo na Zari tofauti na kipindi cha nyuma kabla ya kuwa maarufu.

Akijibu swali kwenye mahojiano yake na Kituo cha Radio cha Kiss FM cha nchini Rwanda, swali lililohoji kuwa alishawahi kukataliwa na mwanamke kabla ya umaarufu wake? Diamond alijibu kwa kusema ‘ndio tena wengi tu kwanini isitokee“.

Na alipoulizwa ni lini mara yake ya mwisho kukataliwa na mwanamke au kusikia neno hapana kutoka kwa mwanamke Diamond Platnumz amesema “tangu nimtongoze Zari, hadi sasa sijawahi kutongoza msichana mwingine“.

Diamond Platnumz wikiendi iliyopita alikuwa nchini Rwanda ambapo akiwa huko alitembelea kituo cha Jordan Foundation kinacholea watoto wenye ulemavu wa macho (Vipofu).

Mume hanifikishi kisawasawa, Akimaliza yeye mimi nabaki bado na hamu

$
0
0
Mimi ni msichana wa miaka 27 nimeolewa miaka minne iliyopita na nina watoto wawili wote wa kike. Mwanzoni mwa mahusiano yetu na mume wangu (wakati tukiwa wachumba) na hata kama mwaka mmoja na nusu hivi kwenye ndoa yetu, baba watoto alikuwa ananiweza kweli....yaani nikikutana nae...aaah, allahmdullillah, nilikuwa naiona anga kwa uhalisia kabisa....na akiwa amechoka sana, basi hata mbili nitapata na kweli nilikuwa najisikia nime.....! Na kwa wiki nilikuwa napata kama siku nne hivi, yale mapigo ya sawa sawa.

Sasa kwa kipindi kama cha mwaka mmoja hivi...da, baba watoto kwa kweli ana underperform kabisa....wakati mwingine inapita wiki nzima, sionji na mm mwanamke huwa nahitaji...nikimwambia anasema nimechoka sana kazini. Kwa heshima niliyo nayo kwa mume wangu, huwa namwambia sawa, lakini moyoni huwa nabaki na maswali mengi kuliko majibu. Huwa nahisi moja kati ya mambno haya:

1) Huenda mume wangu ameanza mambo ya nyumba ndogo, so akitoka kazini huenda anamalizia huko huko then akirudi nyumbani anakuwa hoi

2) Labda umbile langu limemchosha, coz kabla hatujaoana nilikuwa na bambataa ya wastani na kiuno chembamba, lakini now sio utani, nyonga imebaki vile vile lakini makalio yameongezeka mara-dufu, so huwa hafikii pale "Dar es Salaam" kisawasawa kama tunado ile style ya chuma mboga.

Haya yoye ni mawazo yangu ambayo ninayo moyoni. Sasa sijajua kama nimuulize au na mimi nianze kupiga show za nje kwani wanaonitongoza nikiwapanga kuanzia Dar, basi watafika hadi morogoro......tatizo nampenda baba watoto na nimempa muda wa kama miezi 6 hivi, kama hatobadilika, basi nita-confirm namba (1) ya hapo juu....so na mm nitaanzia humuhumu jamii formu kutafuta kurusha nae roho.

Naomba mnisadies what to do at the moment
Viewing all 104808 articles
Browse latest View live




Latest Images