Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

Mwanamuziki Jordin Sparks Afiwa na Mdogo Wake

$
0
0
Mwanamuziki Jordin Sparks Afiwa na Mdogo Wake
Mwanamuziki Jordin Sparks afiwa na mdogo wake wa kambo mwenye umri wa miaka 16 Bryanna Jackson-Frias.
Marehemu Bryanna Jackson amefariki siku ya Jumanne jioni kwa ugonjwa ambao alikuwa akipambana na nayo maisha yake yote uitwayo Sickle cell anemia.



Sickle cell Anemia ni ugonjwa wa kurithi wa kupungukiwa damu, ambapo mgonjwa hua hana damu ya kutosha kwa sababu ya seli zake za mwili sio imara kubeba hewa ya oksijeni kupeleka sehemu mbalimbali za mwili. ukosefu wa oksijeni unaweza kuharibu viungo na kusababisha maumivu makubwa sana ambayo husabibisha binadamu kulazwa hospitali.

Mama wa Jordin Sparks, Jodi Jackson alitumia akaunti yake ya Facebook kutoa ujumbe huo siku ya Jumatano ambapo alituma picha ya binti yake.


Dar Yashindwa Kuingia 10 Bora Ufaulu Kimkoa

$
0
0
Dar Yashindwa Kuingia 10 Bora Ufaulu Kimkoa
Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetoa mpangilio wa ubora wa ufaulu kimikoa wa matokeo ya kidato cha nne mwaka 2017, huku Dar es Salaam ukikosekana katika mikoa 10 iliyofanya vizuri.

Hata hivyo, mkoa huo umepanda kutoka nafasi ya 18 mwaka juzi, hadi nafasi ya 16 mwaka jana. Katika orodha hiyo mkoa wa Kilimanjaro umepanda kutoka nafasi ya tano mwaka 2016 hadi nafasi ya kwanza mwaka jana.

Mkoa wa Pwani nao umepanda kutoka nafasi ya saba mwaka juzi hadi nafasi ya pili mwaka jana. Katika orodha hiyo Tabora imeshika nafasi ya tatu kutoka nafasi ya 10 mwaka 2016.

Mikoa mingine iliyofuata na nafasi iliyoshika ni Shinyanga (nafasi ya nne kutoka nafasi ya tisa), Mwanza (nafasi ya tano kutoka nafasi ya sita).

Mkoa wa Njombe uliokuwa kwa kwanza mwaka 2016, mwaka jana umeporomoka hadi nafasi ya 15.

Mkoa wa Iringa ulishika nafasi ya pili mwaka 2016, lakini mwaka jana umeporomoka hadi nafasi ya 17 huku Kagera ulioshika nafasi ya tatu, ukishuka hadi nafasi ya tisa.

Mkoa ulioshika mkia katika mpangilio huo ni Kaskazini Unguja uliotoka nafasi ya 29 mwaka juzi hadi nafasi ya 31 mwaka jana, ukifuatiwa na Kusini Unguja ulioshika nafasi ya 30 ambayo pia uliishika mwaka juzi.

Mikoa mitano iliyoshika mkia ni Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Kaskazini Pemba, Kusini Pemba na Lindi.   


Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) Champongeza Rais Magufuli

$
0
0
Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) Champongeza Rais Magufuli
 Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Godwin Ngwilimi amepongeza Rais  John Magufuli kwa kutekeleza matarajio ya watanzania.

 Ngwilimi ametoa kauli hiyo leo Februari mosi jijini Dar es Salaam wakati wa kilele cha Maadhimisho ya 22 ya siku ya Sheria na uzinduzi wa mwaka mpya wa kimahakama.

Pia, ameomba uwezeshaji wa rasilimali fedha katika muhimili wa mahakama ili kushughulikia changamoto zinazoikabili. "Kama chama cha mawakili, tunakuunga mkono na tunaahidi kutoa ushirikiano kwa mahakama pale inapostahili."

Ametoa wito akisema, watumishi wa mahakama, majaji, wasajili, watendaji , makarani  na watumishi wengine, mawakili, wanasheria popote walipo wanatakiwa  kutambua mwelekeo wa nchi unabadilika kwa kasi, matarajio ya wananchi , kuondokana na utamaduni wa kuendelea kufanya kazi kimazoea, kutumia fursa zilizopo ikiwamo Tehama ili kuboresha huduma kwa wananchi.

Pia  kuendelea kusimamia maadili ya kitaaluma na uadilifu , hata Mungu anapenda uadilifu na imeandikwa katika vitabu vitakatifu, kulinda na kuhifadhi misingi ya kitaaluma na kujifunza kwa kufuata makosa yaliyotokea hapo nyuma

Ngwilimi ametoa  wito akisema: " Kama sehemu ya watanzania, tusitumie mahakama vibaya, kusumbua wengine, kuonea wengine, kama sehemu ya majaribio, siyo maabara , kama jumba la kamari.



Serikali Yafunguka Kuhusu Vipodozi Vilivyosajiliwa Kuingiza Nchini

$
0
0
Serikali Yafunguka Kuhusu Vipodozi Vilivyosajiliwa Kuingiza Nchini

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema kuwa TFDA imesajili jumla ya vipodozi 3179 ambavyo vinavyoruhusiwa kuingiza na kutumika nchini.



Akizungumza leo bungeni mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndungulile amesema kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/217 maeneo 3648 yalikaguliwa ambapo kati ya hayo maeneo 120 yalikutwa na vipodozi ambavyo havina viwango.

“TFDA imekuwa ikichukua hatua zifuatazo kudhibiti uingiaji na utumiaji wa vipodozi. Vipodozi vyote vinatakiwa kusajiliwa kabla ya kibali cha kuingiza nchini kutolewa mpaka sasa TFDA imesajili jumla ya vipodozi 3179 ambavyo ndivyo vinavyoruhusiwa kuingiza na kutumika nchini, TFDA imefungua ofisi 7 za Kanda kwa maana Arusha, Dar es salaam, Dodoma, Mbeya, Mtwara, Mwanza, Tabora kwa lengo la kuimarisha ukaguzi,” amesema Dkt. Ndungulile.

“Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/017 maeneo 3648 yalikaguliwa ambapo kati ya hayo maeneo 120 yalikutwa na vipodozi ambavyo havina viwango vinavyofaa kwa matumizi ya binadamu na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.”

Hatua ya ufafanuzi huyo imekuja baada ya Mbunge Mata ally salum Mbunge wa Shauri Moyo aliyeuliza “wananchi wengi hapa nchini hasa wanawake hutumia vipodozi ambavyo havina viwango vinavyofaa kwa matumizi ya binadamu pamoja na jitihada za serikali kuzuia bidhaa hizo Je serikali ina mpango gani madhubuti ya kuzuia vipodozi hivyo.?

Mnyika- Mtulia Alianza Usaliti Toka Alivyotangazwa Kuwa Mbunge Kwahiyo Msaliti na Hawezi Kuacha Hiyo Tabia

$
0
0
Mnyika-Mtulia Alianza Usaliti Toka Alivyotangazwa Kuwa Mbunge Kwahiyo Msaliti na Hawezi Kuacha Hiyo Tabia
Mbunge wa Kibamba kupitia Chama cha Kidemokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Mnyika amewatahadharisha wananchi wa jimbo la Kinondoni kwa kutomchagua mgombea wa CCM, Maulid Mtulia kwa madai ni msaliti na hawezi kuacha hiyo tabia.

Mnyika ametoa kauli hiyo ikiwa yupo katika muendelezo wa kumpigia kampeni mgombea wa Ubunge wa jimbo hilo Salum Mwalimu kupitia tiketi ya CHADEMA chini ya mwamvuli wa UKAWA.

"Mtulia alianza usaliti tangu siku ya kwanza alipotangazwa kuwa Mbunge mwaka 2015, maana siku ile matokeo yalipokuwa yanatangazwa na tume, aliposikia jina lake tu kuwa ameshinda alikimbia na kuwaacha watu waliokuwa wakipigania atangazwe na hakutaka kusikia matokeo ya Urais", alisema Mnyika.

Pamoja na hayo, Mnyika aliendelea kwa kusema "msaliti huwa haachi usaliti, hivyo kama wananchi wakikosea na kumpa Mtulia ridhaa ya kuwa Mbunge basi atakuja kuwasaliti tena".

Kwa upande mwingine, mpaka sasa zimebakia takribani siku 16 ili wananchi wa jimbo la Kinondoni  na Siha kuweza kushiriki kupiga kura katika majimbo hayo ambayo yapo wazi kwa sasa.

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0

DAWA BORA ZA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za FULL POWER

Full Power dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin e pamoja na madini aina ya zinc

Itakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30 ZAT 50

Inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende

Tunapatikana Dar es Salaam  na mikoan wasiliana na DR Oshinda no 0755505099 au 0714126118  Karibuni kwa hunduma bora

Njoo Ushuhudie Miujiza ya Kamgambile na Bi Khadija, Wana Uwezo Mkubwa Katika Kutiba Magonjwa na Kurudisha Wapenzi

$
0
0

NJOO USHUHUDIE MIUJIZA YA KAMGAMBILE NA BI KHADIJA WANA UWEZO MKUBWA KATIKA KAZI ZAO JE? UMEACHWA NA MPENZI WAKO JE? NA HUJUI NAMNA YAKUMRUDISHA? WAONE HARAKA WAKUSAIDIE KAMGAMBILE NA BI KHADIJA HURUDISHA MAHUSIANO NDANI YA MASAA (12) TU

DAWAZAO NI NZURI ZENYE KUONYESHA MAFANIKIO KWAHARAKA ANATIBU KWAMITI SHAMBA NAKITABU CHA QUR AN TUKUFU WANA UWEZO MKUBWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE UVIMBE TUMBONI KIFAFA VIDONDA VYATUMBO TEZI PUMU KISUKARI MIGUU KUWAKA MOTO NAKUFA GANZI WANA UWEZO MKUBWA WAKURUDISHA MTU ALIE POTEA KIMAZINGIRA ( MSUKURE) KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (72) TU PATA UTAJIRI USIOKUWA NAMASHARITI KWAYULE ANE TAKA DAWA YA LIMBWATA KUMTAWALA MPEZI WAKO UNAVYO TAKA DAWA YA NGUVU ZAKIUME WANAYO KUONGEZA UUME SAIZI UPENDAYO NCHI 5-6-7-8-9 NIWEWETU UNAVYOTAKA WANAKUSAIDIA KUSAFISHA NYOTA NAKUPATA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NANYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA MALI BILA YA MASHARITI HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO DUNIANI ACHAKUTESEKA

CALLING +255719866726

WHATSAPP CALLING +255768455841 KARIBUNI WOTE WANAO TAKA HUDUMA HII

Polisi Wakamata Machungwa Yaliyoibiwa

$
0
0
Polisi Wakamata Machungwa Yaliyoibiwa
Polisi wa huko jijini Seville nchini Hispania wakamata watu watano jana baada ya kufukuzana nao kwa kasi na ndipo hapo polisi waligundua tani hizo za machungwa zilizoibiwa ambazo watuhumiwa walikuwa wameyajaza ndani ya magari.

polisi walipatwa na shaka wakati walipoona magari matatu yakikunja kona ya haraka kutokana na Ripoti ya Europa Press. Baada ya kukimbizana nao, polisi waliweza kusimamisha magari mawili. Walipofungua mlango wa nyuma wa gari mamia ya machungwa yalidondoka chini.

Machungwa hayo yalirudishwa katika mji wa Carmona, ambayo ndiyo mji uliotoa ripoti za wizi masaa machache tu kabla ya tukio hilo.

Polisi walisema kuwa karibu poundi 9,000 za matunda yalipatikana na uchunguzi wa wizi unaendelea.

Mabeste Amwaga Sifa Lukuki kwa Mkewe

$
0
0
Mabeste Amwaga Sifa Lukuki kwa Mkewe
Msanii wa muziki Bongo, Mabeste amemwaga sifa lukuki kwa mke wake Lisa Fickenscher ikiwa leo ni siku ya kumbukumbu yake ya kuzaliwa (birthday).

Mabeste amemueleza Lisa moja ya vitu ambavyo hajutii ni kumuoa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

Happy Birthday My Love, Sina cha kusema Zaidi ya Kusema nakupenda Saana Mama Wa Watoto wangu … Wewe Ni Mvumilivu Saaana, Unaupendo Saana, Unahuruma pia.

Kikubwa Zaidi Unaakili saaana, OooH Thanks God Kwa Zawadi Hii,
Kuna Msemo Unasema Bora Ukosee Kujenga Nyuma But Sio Kuowa, Yaniii Daah Nakupenda Saana Saaana. Kitu kingine kizuri Ulicho Barikiwa kikubwa Saana ,Unapenda Kazi Yangu ya Music Na Unajuwa Music Nzuri Ukisikia tu..Japo kuimba Ujui.

Leo ni siku Kubwa saana Kwako na Kwangu Pia..Coz Leo ndio Naachia New Track #SIJUI …Leo Mama Wa Watoto wangu Umezaliwa Upya katika Bwana Yesu ,& Hata Kipaji Changu Leo Kimezaliwa Upya Katika Jina LA Bwana wetu Yesu … Kwenye Upendo Sana Mungu Yuko Muda Wote..Coz Mungu Ni Upendo..Tutafika Safari yetu Japo Changamoto ni Nyingi..I Love u Saana.

Mabeste na mkewe, Lisa Fickenscher walifunga ndoa mwaka 2016 na hadi sasa wamejaliwa watoto wawili, Kendrick na Kaylyn.

"Sitalalamika Tena Najua Nitakavyofanya"-Rais JPM

$
0
0
"Sitalalamika Tena Najua Nitakavyofanya"-Rais JPM
Rais John Magufuli amewapa pole Majaji kwa changamoto wanazokumbana nazo pindi wanapo shughulikia mashitaka yanayopelekwa na serikali na kuahidi kulifanyia kazi jambo hilo kabla ya mwezi Februari kuisha kwa madai ameshajifunza vya kutosha.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo wakati alipohudhuria kilele cha maadhimisho ya 22 ya siku ya Sheria na uzinduzi wa mwaka mpya wa kimahakama yaliyofanyika jijini Dar es Salaam ambapo yeye binafsi ndio alikuwa mgeni rasmi katika shughuli hizo akiongozana na viongozi wengine wa serikali.

"Kwa kuadhimisha siku hii ya sheria maana yake ni kwamba nchi yetu inatambua umuhimu wa sheria katika kusimamia haki, kudumisha amani na kuleta maendeleo ya nchi. Maadhimisho haya ya siku ya sheria ni muhimu kwa vile yanatoa fursa kwa vyombo vinavyohusika na masuala ya sheria na utoaji haki", alisema Rais Magufuli.

Aidha, Rais Magufuli alisema bado kuna tatizo kubwa katika ofisi ya DPP (Mkurugenzi wa Mashtaka) na AG (Mwanasheria Mkuu), na ndio maana muda mwingine inawapelekea kuwapa changamoto kubwa Majaji.

"Najua mnapata shida sana mnapo-dili na mashitaka yanayoletwa na serikali mnauona kabisa ushahidi upo lakini watetezi hawajitokezi hadharani kuutetea. Mwaka jana nililalamika lakini mwaka huu nitalishughulikia vizuri. Sitalalamika tena ninajua nitakavyofanya kwa sababu nimeshajifunza vya kutosha na nimejua wapi kuna 'weakness' na wala huu mwezi wa Februari hautoisha", alisisitiza Rais Magufuli.

Kwa upande mwingine, Rais Magufuli amewataka viongozi wengine wanaosimamia vyombo vya sheria kufuata mfano mzuri aliyouanzisha Profesa Ibrahimu Juma kwa kutowafumbia macho wahalifu wa aina yeyote ile.

Mbunge CUF Aeleza Wabunge Wanavyotelekeza Watoto Wao

$
0
0
Mbunge CUF Aeleza Wabunge Wanavyotelekeza Watoto Wao
Mbunge wa Konde (CUF), Khatib Said Haji leo Februari 1, 2018 ameibua tuhuma bungeni, akidai baadhi ya wabunge wenzake wamewatelekeza watoto wao.

Amesema katika mkutano wa Bunge uliopita,  mmoja wa mtoto aliyetelekezwa na wawakilishi hao wa wananchi, aliletwa bungeni na mama yake.

Akizungumza katika kipindi cha maswali na majibu bungeni, Khatibu amesema sasa chanzo cha watoto wa mitaani kimethibitika kwa sababu wanaume wengi wanashindwa kutunza familia zao.

“Mheshimiwa mwenyekiti Bunge lililopita nilishuhudia wanawake wengi wakija na watoto wao pale nje (ya viwanja vya Bunge) wakidai kutelekezwa na wazazi wenzao ambao ni wabunge wanaume. Tabia  hii itakwisha lini na wabunge waanze kutunza watoto wao," amesema Khatibu.

Khatibu ameungwa mkono na mbunge wa Kavuu (CCM), Dk Pudensiana Kikwembe, aliyetaka jambo hilo kuwekwa wazi ili kujua kama wabunge hao wamezaa na wabunge wenzao au wamezaa na watu wengine lengo likiwa ni kujua jinsi ya kuwasaidia.

Katika ufafanuzi wake, Naibu Waziri wa Afya, Dk Faustine Ndugulile amesema kitendo cha kutelekeza watoto ni kinyume na sheria za nchi, kuwataka wananchi, hasa wanaume kuacha tabia hizo.

Hata hivyo, Naibu Waziri huyo amesema Bunge halina taarifa za wabunge kutelekeza watoto..

Kuhusu hoja kama wamezaa na wabunge wenzao ama la, Dk Ndugulile ameomba kiti cha Spika kufuatilia suala hilo kwa maelezo kuwa yeye hawezi kulijibu.

Serikali ya Kenya Yashtakiwa kwa Kufungia Vituo vya TV kwenye ‘kuapishwa’ Raila

$
0
0
Serikali ya Kenya Yashtakiwa kwa Kufungia Vituo vya TV kwenye ‘kuapishwa’ Raila
Mwanaharakati nchini Kenya Okiya Omtatah amefungua mashtaka dhidi ya serikali katika Mahakama Kuu kutokana na uamuzi wake wa kuzima vituo vya televisheni vya Citizen TV, NTV na KTN pamoja na Inooro TV siku ya ‘kujiapisha’ Kiongozi wa Upinzania NASA Raila Odinga.

Omtatah ameeleza kuwa kufungiwa kwa vyombo hivyo vya habari  ni kinyume cha sheria na hakuna sheria yoyote iliyowapa mamlaka ya kutekeleza suala hilo.

Amedai kuwa serikali hiyo lazima izuiwe katika kudharau utawala wa sheria jambo ambalo ni msingi mkuu wa thamani ya taifa na kanuni ya utawala.

Ameongeza kuwa anahitaji mahakama iamuru serikali ilipe fidia vyombo hivyo vya habari vilivyofungwa na kusababishiwa hasara kutokana na jambo hilo.

Kiongozi wa Upinzani DRC, Tshisekedi Yupo Mochwari Mwaka Mmoja Sasa

$
0
0
Kiongozi wa Upinzani DRC, Tshisekedi Yupo Mochwari Mwaka Mmoja Sasa

Mwaka mmoja baada ya kifo cha aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Upinzani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Etienne Tshisekedi wa Mulumba, mwili wake haujarejeshwa nchini humo kwa ajili ya kuzikwa.

Etienne Tshisekedi alifariki February 1, 2017 katika mji mkuu wa Ubelgiji, Brussels. Kutokana na kukosekana kwa makubaliano kati ya chama cha UDPS na serikali mjini Kinshasa, mwili wa Tshisekedi bado upo katika chumba cha kuhifadhi maiti mjini Brussels.

Kwa upande wa kambi ya Tshisekedi mjini Brussels, kipaumbele cha kwanza ni kurejeshwa kwa mwili wa Waziri Mkuu wa zamani nchini DRC, ambako anapaswa kuzikwa, katika moja ya sehemu ya familia yake katika eneo la N’Sele, mjini Kinshasa. Familia tayari imelipa Euro 16,000 kwa ajili ya kuendelea kuhifadhiwa kwa mwili wa Tshisekedi katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Brussels.

Mitch Katumba, kiongozi wa chama cha UDPS mjini Brussels, amekua akikutana na viongozi wa Ubelgiji, Ufaransa pamoja na Ulaya, ili kuwezesha kurejeshwa kwa mwili wake nchini DRC. Mpaka sasa jambo hilo halijawezekana.

“Kabila, haipaswi kuwa na hofu, sio mwili wa Tshisekedi ambao utamuondoa madarakani, hakuna hoja yoyote kwa Tshisekedi kuzikwa nje ya nchi, Tshisekedi atazikwa DRC, katika mji wa Kinshasa. Tutajitahidi kusafirisha mwili wake,” -Katumba

“Sisi ni Waafrika, na sisi ni watu kutoka jamii ya Bantu. Kuna desturi, tuna maadili yetu. Mjane hawezi kukaa hivyo kwa mwaka mzima, wakati ambapo hatujamzika mumewe … Yuko hapo, analala chini, anaumia, ni mgonjwa, “ -Katumba.

Mbunge Chadema Ahoji Madhara ya Kuongeza Maumbile

$
0
0
Mbunge Chadema ahoji madhara ya kuongeza maumbile
Mbunge wa viti maalumu (Chadema) , Suzan Lyimo leo Februari 1, 2018 ameibua mjadala bungeni baada ya kuhoji kama wanawake wanaochoma sindano kwa lengo la kuongeza maumbile yao wanapata madhara yoyote.

Ametoa kauli hiyo wakati akiuliza swali la nyongeza bungeni, kubainisha kuwa miaka ya hivi karibuni kumekuwa na wimbi la wanawake kutumia sindano hizo, kwamba kama Serikali inalijua jambo hilo imechukua hatua gani.

“Naomba kujua iwapo serikali ina taarifa kwamba wapo wanawake wanaotumia sindano kwa ajili ya kuongeza maumbile yao, kama wanapata madhara  Serikali imechukua jukumu gani kukomesha jambo hilo,” amesema Lyimo.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Afya, Dk Faustine Ndugulile amesema sindano hizo zina madhara makubwa mwilini.

Amesema mwili wa binadamu umeumbwa kwa namna ya asili kwa lengo la kujikinga na mambo mengi ikiwemo mionzi.

Amebainisha kuwa Serikali hairuhusu jambo hilo, dawa zote ambazo hazijasajiliwa zinapingwa vita  kwa kuwa zina madhara kwa watumiaji.

Nyangumi Muuaji Anayeweza Kuongea

$
0
0
Nyangumi Muuaji Anayeweza Kuongea

Nyangumi Muuaji anayeweza kutamka maneno kama "hello" anadhaniwa kuwa wa kwanza wa aina yake kuigiza kauli ya binadamu.

Nyangumi huyo wa jinsia ya kike alijifunza''kuzungumza" baadhi ya maneno ya binadamu kwa kunakili mwalimu wake katika eneo la hifadhi wa nyama wa baharini nchini Ufaransa.

Matamshi anayoweza kuyatamka mnyama huyo ni pamoja na jina "Amy" na "one, two, three".

Nyangumi na pomboo ni miongoni mwa wanyama wachache kando na binadamu wanaoweza kujifunza kutoa sauti za matamshi kwa kuyasikia tu.

"Katika wanyama ni nadra sana ," alisema Dkt. Josep Call wa Chuo Kikuu cha St Andrews, mtafiti mwenza katika uchunguzi.

"Ni kawaida kwa binadamu bila shaka ... la kushangaza, wanyama wanaoweza kufanya vizuri ni wanyama wa baharini."

Watafiti wanataka kubaini ikiwa nyangumi hujifunza sauti kwa kuigiza wengine. Walimfanyia uchunguzi nyangumi wa kike aliyepatiwa jina la Wikie katika sehemu ya ardhi baharini katika eneo la Antibes nchini Ufaransa.

Alifundishwa kuongea maneno ya binadamu kupitia shimo lake la kupumua na anaweza kusikilizwa kwenye sauti yake iliyorekodiwa akirudia maneno kama vile "hello" na "Amy", na kuhesabu "one, two, three", kwa sauti ya kelele ,ya kunong'oneza ama sauti laini.

Nyangumi muuaji alifahamika kuishi katika makundi yenye lafudhi za kipekee "dialects". Wanaweza kuwanakili wajumbe wengine wa aina yake nyikakani, licha ya kwamba hili linahitaji uchunguzi zaidi.

Kwa mwanadamu ana kikomo cha matamshi katika uzungumzaji wa lugha, lakini kwa wanyama wengine ni nadra sana.

Pomboo na nyangumi wa beluga ni miongoni mwa wanyama wanaoweza kuigiza sauti kutoka kwa viumbe wengine ama wao kwa wao. Baadhi ya ndege pia wanaweza kuigiza sauti za binadamu.

Wikie alitoa sauti alipokuwa ndani ya maji huku mkia wake ukionekana juu nje ya maji. Sauti zinazotolewa chini ya maji zinaweza kuwa tofauti. Japo huyu anaweza kuwa ni nyangumi mmoja tu, watafiti hawana uhakika ikiwa kuna nyangumi wengine wanaoweza kuigiza sauti za matamshi.

Kampuni ya TTCL Yafutwa

$
0
0
Kampuni ya TTCL Yafutwa
Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Makame Mbarawa, amesema kuwa anamshukuru sana Rais Magufuli kwa kuona umuhimu wa kuona wa kuwa na shirika la mawasiliano madhubuti kwa ajili ya kuleta maslahi mapana ya nchi, huku akitoa shukrani pia kwa Wabunge wote kwa kukubali kupitisha muswada huo.

Aidha Prof Mbarawa, amesema uwepo wa sheria ya shirika la mawasiliano unatoa fursa ya kuboresha sekta kwa kuweka mazingira mazuri ya usimamizi wa miundombinu ya mikakati chini ya shirika hilo.

Profesa Mbarawa pia amewajulisha Watanzania wote kuwa mabadiliko ya kuhama kutoka kampuni kuwa shirika la mawasiliano hayatawaathiri kwa namna ya utoaji wa huduma mbalimbali ambazo zilikuwa zinatolewa na kampuni ya simu ya (TTCL) huku akielezwa kuwa wanaodaiwa na iliyokuwa kampuni hiyo watatakiwa kulia madeni yao kama mikataba yao inavyosema na wanaoidai watalipwa pia.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo?

$
0
0
Matatizo haya yame kuwa yakiwaathiri watu wengi sana kisaikolijia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wenzao kwa kawaida mwanaume ana takiwa awe na uume kuanzia inch(6_8)vinginevyo mtu huyo atakuwa na matatizo.

Zipo sababu nyingi zinazo sababisha tatizo hilo baadhi ni upungufu wa vichocheo (Hormones za Getrogen) Ambazo mwanaume akisha balehe vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume, chango husababisha NEVA ambayo huathiri misuri ya uume. Ngiri ambayo Huleta maumivu ya tumbo kuunguruma na kujaa guess, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri , miguu kufa ganzi, maumivu ya kiuno,upigaji wa punyeto sababu hizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembaba na mara kwa mara hipelekea kupunguka kwa nguvu za kiume na ham ya tendo la ndoa hukosekana na kuisha kabisa

NSUMBU:__Ni dawa dawa inayo zalisha hormones za Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.

NZAGI :--Ni dawa bora ya kurudisha nguvu za kiume na kukupa hamu ya kurudia tendo la ndoa mara dufu utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara nne
(4)bila hamu kuisha (kuchoka) dawa hii ni tiba kamili kwa matatizo hayo. Dawa hii pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk(15_30)kwa tendo moja la ndoa dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji kuanzia miaka(18_90)wana ruhusiwa kuzitumia Pia tunatibu KISUKARI, PRESHA, PUMU, MALARIA SUGU, MIMBA KUHARIBIKA(Chango)

POWER :__Ni dawa ya mitishamba inaongeza hips, (makalio), miguu, ina punguza maziwa (chuchu). Ina toa harufu mbaya sehem za siri Nk.

Pia anazo dawa za mvuto wa mapenzi,biashara, kurudishwa kazini, kumuita aliye mbali kwa mda mfupi tu

OSTADH JUMA ANAPATIKANA MBANGALA ZAKHIEM SIMU: 0769-597778 au 0784-002216 au 0627457957 Wote mnakaribishwa

JE, Unaupungufu wa Nguvu za Kiume, Hamu ya Tendo la Ndoa au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0
JE DADA, UNAPENDA KUWA NA SHEPU KAMA HII? KAMA JIBU NI NDIYO SOMA HAPA MWAKA MPYAMAMBO MAPYA

Katika kusherekea miaka kumi na nane (18) ya kampuni hii, @markson_beauty_pr imezindua bidhaa zake mpya. Bidhaa hizi mpya zimefanyiwa maboresho makubwa hivyo zina nguvu na matokeo ya haraka kuliko ilivyokuwa.

1.Kuongeza hips, makalio na mapaja @200,000/=
2.Kushepu mguu (CHUPA YA BIA) @150,000/=
3.Kuwa mweupe bila sugu kwa:-
(a)mafuta @150,000/=
(b) Vidonge @170,000
4.Kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @150,000/=
 5.Kuongeza hips, makalio na mapaja kwa vidonge (YODI PILLS ORIGINAL) @250,000/=
6Kupunguza au kuongeza maziwa kuyasimamisha @150,000/=
7.Kubana uke na kuondoa uchafu ukeni @130,000/=
8.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
9.Kufungua mirija ya uzazi na kupata ujauzito haraka @250,000/=

  NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri na garantii ili kukuhakikishia ubora na usalama wa bidhaa za MARKSON BEAUTY LTD

    Wasiliana nasi Popote
  ulipo duniani kwa (+255)
          0767447444 au
             0714335378
    Bei hizi ni of a hadi tar 31/01/18

JB Amekaa Kupigwa Pigwa - Dude

$
0
0
JB Amekaa Kupigwa Pigwa - Dude
Mwigizaji Kulwa Kikumba maarufu zaidi kama Dude amefunguka na kudai ameshawahi kumuingiza mjini msanii mwenzake Jacob Stepheni (JB) kwa kumtapeli laki moja na thelathini japokuwa mwenyewe alifahamu.


Dude ameeleza hayo kwenye Big Chawa ndani ya kipindi cha Planet Bongo ya East Afrika Radio baada ya kuulizwa ni msanii gani amekaa kizembe zembe ambaye anaweza akatapeliwa kiurahisi.

"JB si unamuona amekaa kupigwa pigwa hivi, anachelewa kukumbuka kwanza mimi nimeshawahi kumpiga kiukweli kabisa kama shilingi laki 1 na thelathini. Anajua JB lakini alitoa kwa sababu mimi ni ndugu yake pia ni rafiki yake", alisema Dude.

Pamoja na hayo, Dude aliendelea kwa kusema "JB ni mtu mmoja poa sana yani yule unaweza kumuingia wakati wowote ule ukiwa na shida za haraka haraka ukimdanganya tu umemuingiza mkenge".

Halima Mdee Aliamsha Dude Bungeni Awavuruga Mawaziri

$
0
0
Halima Mdee Aliamsha Dude Bungeni Awavuruga Mawaziri
Naibu Waziri wa Afya,  Dkt. Ndugulile leo Februari 1, 2018 amefunguka na kusema Serikali haijazuia wanafunzi wa kike kutoendelea na masomo baada ya kupata ujauzito bali ilizuia mwanafunzi kurudi shule aliyokuwa akisoma awali kabla ya kupata ujauzito.

 Ndugulile amesema hayo leo Bungeni wakati akijibu swali ambalo liliulizwa na Mbunge wa Kawe kwa tiketi ya CHADEMA, Halima Mdee ambaye alitaka kujua juu ya utekelezaji wa sera ya 're entry policy' ambayo ilianzishwa katika kipindi cha awamu ya nne ya Serikali kuwawezesha wanafunzi waliopata ujauzito kurudi shule baada ya kujifungua kupata haki yao ya kimsingi ya kusoma.

Akijibu swali hilo Ndugulile alisema kuwa "Ni kweli kulikuwa na maandalizi ya 're entry policy' lakini utekelezaji wake sasa umepitwa na wakati kutokana na agizo lililotolewa na Serikali kwamba mtoto ambaye amepata ujauzito hataruhusiwa kurudi katika shule ambayo alikuwa anasoma lakini maagizo haya hayajazuia mtoto wa kike ambaye amepata ujauzito kutoendelea na masomo hapo naomba tuelewane vizuri. Serikali imezuia mtoto wa kike kurudi shule aliyokuwa akisoma ila haijazuia mtoto wa kike kuendelea na masomo" alisema Ndugulile

Mbali na hilo Naibu Waziri huyo amesema kuwa sasa Serikali inaangalia njia mbadala ambayo itawawezesha watoto wa kike ambao wamepata ujauzito ili waweze kuendelea na masomo.

Baada ya kauli ya Naibu Waziri aliibuka Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa. Joyce Ndalichako na kuweka msimamo wa Serikali kuwa mwanafunzi ambaye amepata ujauzito hawezi kurudi shule kama ambavyo Naibu Waziri wa Afya amesema.

Mwezi June 23, 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli alisema serikali yake haitoruhusu mwanafunzi aliyepata ujauzito kuendelea na masomo.
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live




Latest Images