Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Hospitali Zinazowatoza Fedha za Matibabu Mama Wajawazito Kukiona

$
0
0
Hospitali Zinazowatoza Fedha za Matibabu Mama Wajawazito Kukiona
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto imewataka wananchi kutoa taarifa kwa hospitali yeyote inayotoza fedha kwa ajili ya matibabu ya wajawazito wanaokwenda kupatiwa matibabu kwa kuwa huduma hizo zinatolewa bure.


Tamko hilo limetolewa na Naibu wa Waziri wa wizara hiyo Dkt. Faustine Ndugulile,  katika mkutano wa 10 kikao cha tano cha Bunge kinachoendelea mjini Dodoma wakati alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Hawa Mchafu Chakoma alipotaka kujua serikali ili kuwa ina maana gani kusema matibabu kwa wamama wajawazito ni bure.

"Mama wajawazito ni moja ya makundi maalum wanaopaswa kupata huduma za matibabu bure kama ilivyoainishwa katika muongozo wa uchangiaji wa huduma za afya mwaka 1997. Wakina mama wajawazito ni haki yao kupewa huduma zote bila ya malipo na sio zile tu zinazohusu ujauzito", amesema Dkt. Ndugulile.

Pamoja na hayo, Dkt. Ndugulile ameendelea kwa kusema "katika muungozo uliopitiwa mwaka 2009-2010 imetamkwa bayana huduma ya afya kwa mama wajawazito ni bure ikiwa inamaana mara tu mwanamke anapokuwa mjamzito huduma zote kuanzia kliniki ya wajawazito, pale atakapougua maradhi yeyote pamoja na huduma ya kujifungua sanjari na kumuona daktari, kupatiwa vipimo, kupatiwa dawa, kufanyiwa upasuaji pale itakapo hitajika kufanyika hivyo".

Aidha, Dkt. Ndugulile amesema wizara ya afya imeandaa bajeti ya kununua vifaa wanavyotakiwa kutumia wanawake wajawazito ili kuwaondolea adha wafika hospitalini.

"Wizara imeandaa bajeti kutumika kwa ununuzi wa vifaa vinavyohitajika wakati wa kujifungua kwa maana 'delivery parts'. Vifaa hivyo watapewa wakina mama wajawazito wanapokaribia kujifungua ili wawe wanatembea na vifaa hivyo na kupunguza kero kwa kina mama kujinunulia vifaa vyao wao wenyewe", amesisitiza Dkt. Ndugulile.

Kwa upande mwingine, Dkt. Ndugulile amesema serikali inazikumbusha halmashauri kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sera hiyo ili wakina mama wajawazito wapate huduma ya kujifungua bure kama muongozo wa uchangiaji wa mwaka 1997 na sera ya afya  ya mwaka 2007 inavyoelekeza.

Damu ya Msanii Radio Yazidi Kufanya Kazi ...... Polisi Yamsaka Producer Washington Ambaye Amehusishwa Kifo cha

$
0
0
Damu ya Msanii Radio Yazidi Kufanya Kazi ...... Polisi Yamsaka Producer  Washington Ambaye Amehusishwa Kifo cha
Jeshi la Polisi nchini Uganda leo linakusudia kumkamata producer wa muziki nchini Uganda maarufu kwa jina la Washington, ambaye amehusishwa na kifo cha msanii Radio.


Kwa mujibu wa msemaji wa kundi hilo amesema Washington ndiye mtu aliyemchukua Radio kutoka nyumbani na kwenda naye club ambako alipigwa hadi kupelekea kifo chake, kutokana na kutoa maelezo yasiyoeleweka.

“Tunaenda kumkamata Washington leo, Washington ndiye alimchukua Radio na kwenda naye mahali ambako aliuawa, kutokana na maelezo anayoyatoa kuwa ya kuchanganya yasiyoeleweka”, amesema msemaji huyo.

Pia Polisi wa Uganda tayari wamemkamata mtu aliyempiga Radio hadi kupekea kifo chake anayejulikana kwa jina la Troy, ambaye ametajwa na producer Washington aliyekuwa naye siku ya tukio mpaka anapigwa.

Mpaka Radio anakutwa na umauti Troy alikuwa amejificha kwenye nyumba ya rafiki yake iliyopo Entebe Uganda.

Zuma Amekataa Kuachia Madaraka- Malema

$
0
0
Zuma Amekataa Kuachia Madaraka- Malema
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ameendelea kusisitiza kwamba amekwisha zingatia maelekezo yote ya kisheria na hawezi kuachia madaraka hayo. kwa mujibu wa viongozi wa upinzani Julius Malema na Bantu Holomisa.

Kitu hichi kilitokea baada ya mkutano ambao ulifanyika kati ya Zuma na viongozi 6 waliochaguliwa kwenye chama cha ANC siku ya Jumapili.

“Alikataa kujiuzulu na amewaambia wafanye uamuzi wa kumtoa kama watapenda kufanya hivyo kwa sababu hakuwa na hakuna kitu chochote kibaya alicho kifanya kwenye nchi hiyo. Analalamika kuwa alikubali maelekezo yote ya kisheria ikiwa ni pamoja ya kulipa fedha, Je, wanataka nini zaidi kutoka kwake.” Malema wa EFF aliandika katika akaunti yake ya Twitter.


Julius Sello Malema

@Julius_S_Malema
He refused to resign and he told them to take a decision to remove him if they so wish to do so because he didn’t do anything wrong to the country. He’s arguing that he complied with all legal instructions including paying back the money, what more do they want from him

12:25 AM - Feb 5, 2018
 962 962 Replies   4,304 4,304 Retweets   4,640 4,640 likes
Twitter Ads info and privacy
Watu wamependekeza kwamba Cyril Ramaphosa, aliyechaguliwa kuwa rais wa ANC mwezi Desemba 2017, kuchukua nafasi ya urais wa nchi kabla ya uchaguzi mkuu ujao mwaka 2019. maandamano dhidi ya Zuma yanatarajiwa katika kufanyika makao makuu ya ANC yaliyopo huko Johannesbur, South Africa.

kulingana na taarifa za hivi punde ni kwamba Kamati ya wanachama wa ANC wanatarajia kufanya mkutano maalum mchana huu.

Okwi Alishindwa Kupumua Baada ya Kupigwa Ngumi ya Koo- Haji Manara

$
0
0
Okwi Alishindwa Kupumua Baada ya Kupigwa Ngumi ya Koo- Haji Manara
Mshambuliaji Emmanuel Okwi alipigwa kwenye koo baada ya kupigwa ngumi.

Hali hiyo ilisababisha ashindwe kupumua na kulazimisha mwalimu wake Kocha Pierre Lechantre kulazimika kumpumzisha.

Okwi alipigwa ngumi na beki wa Ruvu Shooting ambaye alitolewa kwa kadi nyekundu.

Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema mchezaji huyo anaendelea vizuri ingawa alishindwa kupumua baada ya tukio hilo.

“Alipata maumivu baada ya kupigwa ngumi, unajua ngumi ya kisukusuku kwenye koromeo si jambo dogo.

“Lakini tunashukuru anaendelea vizuri na tunatarajia tutakuwa naye kambini maandalizi dhidi ya Azam,” alisema.


Okwi alitolewa baada ya kupigwa kwa makusudi na beki huyo na Ruvu Shooting walicheza kindava wakionekana walikuwa wamepania kuwaumiza wachezaji wa Simba kama ambavyo walicheza kindava katika mechi dhidi ya Yanga ambayo walilala kwa bao 1-0 lakini mshambuliaji Yohana Nkomola naye alitolewa baada ya kuumizwa na hadi sasa ni majeruhi.

Kilichotokea Mechi Dhidi ya Lipuli, Yanga Kuadhibiwa?

$
0
0
Kilichotokea Mechi Dhidi ya Lipuli, Yanga Kuadhibiwa?
Viongozi wa Yanga, juzi Jumamosi waligoma kuwaruhusu wachezaji wao kuingia katika vyumba vya kubadilishia nguo kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa ambapo timu hiyo ilipambana na Lipuli FC.

Sababu kubwa ya viongozi hao kuwazuia wachezaji wao kuingia kati vyumba hivyo ni kile walichodai kuwa kimepuliziwa dawa za kuwapunguza nguvu.

Jambo hilo lilizua mvutano mkubwa baina ya viongozi hao na wale wa Lipuli ambao walikuwa wakiwataka wawaruhusu wachezaji wao waingie vyumbani humo wakidai hiyo ni dawa ya mbu, jambo ambalo halikufanikiwa.

Viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) waliokuwa uwanjani hapo walishindwa kutoa maamuzi yao mara baada ya kwenda kukagua vyumba hivyo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Hussein Nyika, alisema kuwa hata kama ni dawa ya mbu ndiyo iliyokuwa imepuliziwa vyumbani humo wasingeweza kuwaruhusu wachezaji wao kuingia na bora wapigwe faini lakini siyo kuwaangamiza wachezaji wao.

"Hujuma kama hizi siyo za kiungwana kwa hiyo kama TFF watatupiga faini sawa lakini itakuwa ni ya uonevu kwani hata wao wamejionea hilo.

"Kama ni dawa ya mbu kwa nini wasipulizie siku nyingine mpaka wapulizie leo?" alihoji Nyika.

SOURCE: CHAMPIONI

Sheik Mkuu Amtolea Uvivu Mange Kimambi "Huu Ndio Mwaka Wake wa Mwisho"

$
0
0
Sheik Mkuu Amtolea Uvivu Mange Kimambi "Huu Ndio Mwaka Wake wa Mwisho"
Sheik Mkuu Mkoa wa Dar es Salaam Al Haji Mussa Salimu amtolea uvivu mwanadada maarufu mitandaoni mange Kimambi amwambia huu ndio mwaka wake wa mwisho  kutumia mdomo wake kuwatukana watu haswa viongozi.

"Kuna watu wanatafuta umaarufu  kupitia midomo michafu , mimi siwezi kupigia kampeniCCM sasa tunamwambia huyu anayeitwa @mangekimambi acjeze na watu wengine na si viongozi wa dini huu ndio mwisho wake tutasema na mwenyezi mungu na Majibu Mtayaona

Sheikh huyo amesema kwamba kutokana na kitendo hicho cha Mwanadada huyo kumuanika mtandaoni na kumtolea maneno machafu yeye kama kiongozi wa dini atarudi kwenda kushtaki katika mahakama ya mbinguni ambayo haina rushwa.

Kauli hiyo ya Sheikh Mkuu imekuja ikiwa ni siku moja tangu ianze kusambaa picha yake mitandaoni na kuanza kutuhumiwa kuwa anashiriki katika kampeni za uchaguzi mdogo kukisaidia Chama Cha Mapinduzi

"Tutarejea katika mahakama ya mbinguni kwani mahakama ya Mwenyezi Mungu haina rushwa na tutamuuliza  Mwenyezi Mungu kama alimpa Huyu Mange Kimambi ulimpa mikono kwa ajilli ya kudhalilisha na kuvunja heshma za watu. Amekuwa akiwatukana viongozi wa serikali lakini kwa hekima zao wamemnyamazia kimya" Al Haji Mussa Salimu .

Ameongeza kwamba "Tunamuonya acheze na namba nyingine lakini siyo viongozi wa dini kwani wao wana mahakama ya kushatakia. Huu utakuwa mwaka wake wa mwisho kutumia ulimi au mikono yake kudhalilisha watu".

Hata hivyo Sheikh huyo amesema kwamba wapo watu wengi waliompa rai ya kutomjibu Mange Kimambi  na kwamba kumjibu kwake kutamfanya atukanwe sana laki amesema kwamba mwanadada huyo aendelee kutukana kwani dua ya mwenye kudhulumiwa haina kizuizi na kama anaishi hapa duniani basi afahamu kwamba hataendelea kuwa salama na amejihalalishia mwenyewe kwa ulimi wake na mikono yake.

Auwawa kwa Kuchomwa Visu Akijaribu Kumtetea Mpenzi Wake

$
0
0
Auwawa kwa Kuchomwa Visu Akijaribu Kumtetea Mpenzi Wake
Mwanaume mmoja mwenye umri wa makamo chini Kenya katika eneo la Tudor Mombasa, ameuawa kwa kuchomwa na visu akijaribu kuwasuluhisha wapenzi waliokuwa wakigombana nyumbani kwao.

Kwa mujibu wa mjumbe wa nyumba 10 wa eneo hilo Benson Okello. Marehemu alichomwa visu mara kadhaa baada ya kujaribu kumuokoa mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 25 aliyekuwa akipigwa na mume wake, akimtuhumu kutumia dawa za kupanga uzazi ili asimzalie mtoto.

Okello amesema tukio hilo limewaacha pia wenza hao wakiwa wamejeruhiana vibaya na kupelekea kukimbizwa hospitali, ambako wamelazwa katika vyumba vya wagonjwa mahututi.

Kwa mujibu wa majirani wamesema wawili hao wamekuwa watu wa kugombana mara kwa mara, kwa sababu hiyo hiyo ya kutumia njia za uzazi wa mpango.

Huu Mwaka Una Mambo Mazuri Utakuwa Mwaka wa Kumbukumbu

$
0
0
Huu Mwaka Una Mambo Mazuri Utakuwa Mwaka wa Kumbukumbu
February 5, 2018 Staa wa Bongofleva na President wa WCB  Diamond Platnumz azidi kuwaahidi mashabiki zake vitu vikubwa kuhusu muziki wa Bongo Fleva kufanya vizuri zaidi kwa mwaka huu wa 2018 ameyasema haya kupitia account yake ya instagram.

Ambapo mwanzoni wa mwaka huu wa 2018 ameanza kwa kumtambulisha rasmi Mbosso WCB pamoja na kazi yake mpya ambapo mashabiki wameupokea vizuri wimbo huo

Kupitia instagram yake ameaandika caption inayosema “Matangazo ya siku 4 Mitandaoni na #WATAKUBALI ikiwa inasiku sita tu tangu itoke, Dah!….sio kwasababu eti tunaakili na kujua sana Hapana! ni kwasababu Mnatupenda na kutusapoti sana…Baraka za Mwenyezi Mungu, lakini pia Mnaridhika na kuvipokea vidogo vyetu tunavyowapatia.”

“Kwakweli Tunawashukuru na tunawapenda sana huu mwaka una mengi sana mazuri juu ya hii sanaa mengi sana naamini utakuwa ni mwaka wa kumbukumbu kwenye hii nchi ni mwaka ambao utaleta nyuso ya furaha kwa Wasanii, Mashabiki, na wadau wote wa sanaa tuseme InshaAllah”

Ukiachilia mbali na utambulisho alioufanya kwa Mbosso, Diamond Platnumz ametuonyesha jengo la Headquaters mpya za WCB ambapo pia zitapatikana ofisi za Wasafi Tv na Wasafi FM ikiwa ni moja ya kumbukumbu za mwaka huu wa 2018.

Viongozi Wengi Wajitokeza Kwenye Mazishi ya Kingunge

$
0
0
 Viongozi Wengi Wajitokeza Kwenye Mazishi ya Kingunge
Viongozi wa Serikali walio madarakani na wastaafu wakiongozwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan wamejumuika na waombolezaji wengine kuaga mwili wa mwanasiasa mkongwe nchini, marehemu Kingunge Ngombale Mwiru.

Shughuli ya kuaga mwili wa Kingunge imefanyika leo Jumatatu Februari 5,2018 katika viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam.

Viongozi wengine walioaga mwili wa Kingunge ni marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa aliyeambatana na mkewe Anna; Makamu wa Rais mstaafu, Dk Mohamed Gharib Bilal; mawaziri wakuu wastaafu Dk Salim Ahmed Salim, Frederick Sumaye, Edward Lowassa na mkewe Regina; na Jaji mstaafu Joseph Warioba.

Wengine ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula na mtangulizi wake Pius Msekwa; Jaji Mkuu mstaafu Mohamed Othman Chande; Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad na mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba.

Pia, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole; Mama Maria Nyerere; Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye; na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba.

Mwanamke Aliyeiba Mtoto Mchanga Hospitali Akamatwa

$
0
0
Mwanamke Aliyeiba Mtoto Mchanga Hospitali Akamatwa
Jeshi la Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya wamemkamata mwanamke mmoja mkazi wa 'Airport' ya zamani akiwa na mtoto mchanga jinsia ya kike aliyemuiba katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya.

Hayo yamebainishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi Mohamed .R. Mpinga wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari na kusema mnamo Februari 3, 2018 kwa kushirikiana na viongozi wa hospitali hiyo walifanikiwa kumshika kijana huyo aliyefahamika kwa jina la Happy Charles (24) ambae anajishughulisha na kazi ya Mama lishe.

Aidha, Kamanda Mpinga amesema mnamo Februari mosi mwaka huu majira ya saa 4:00 usiku katika wodi ya watoto Hospitali ya Mkoa wa Mbeya iliyopo Kata ya Forest Mpya, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya, mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Sarah Mwasanga Mkazi wa Iganzo akiwa katika wodi ya wazazi Hospitalini hapo baada ya kujifungua mtoto wa kike aligundua kuibiwa kwa mtoto huyo na mtu asiyefahamika.

Kutokana na tukio hilo, uongozi wa Hospitali hiyo ulitoa taarifa kituo kikuu cha Polisi na ndipo upelelezi kuhusiana na tukio hilo ulianza kufanyika.

Msikilize hapa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi Mohamed .R. Mpinga pamoja na mzazi wa aliyeibiwa mtoto wakifafanua vizuri juu ya tukio hilo.

Timu ya Azam Yaweka Kambi Chamanzi

$
0
0
Timu ya Azam Yaweka Kambi  Chamanzi
Klabu ya soka ya Azam FC imesema haina mpango wa kuweka kambi nje ya uwanja wake wa Azam Complex kwaajili ya kujiandaa na mchezo wake dhidi ya Simba SC.


Msemaji wa klabu hiyo Jaffary Idd amesema kuwa timu imeanza kambi jana Jumapili kwenye makao makuu ya klabu hiyo Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam ikiwa ni maandalizi ya mwendelezo wa mechi za ligi ikiwemo ya Simba jumatano.

''Sisi kama Azam hatuna pakwenda, wala hatutaenda Bagamoyo au Zanzibar zaidi tutakuwepo hapahapa Azam Complex  tutajiandaa na kuondokea hapa kuelekea uwanja wa taifa kwaajili ya mechi'', amesema.

Simba na Azam zinakutana katika mchezo wa raundi ya 17 ya ligi kuu soka Tanzania Bara ambapo mchezo wa kwanza utapigwa kwenye dimba la taifa jiji Dar es salaam. Katika mchezo wa raundi ya kwanza kwenye uwanja wa Azam Complex timu hizo zilitoka sare.

Kwa upande mwingine Jaffary Idd amesema kwasasa timu yao ina kikosi kipana licha ya kuwa na majeruhi kadhaa lakini wanaamini waliopo watafanya vizuri. Pia amesema walimu wamelifanyia kazi suala la ufungaji na ndio mana katika mechi zao mbili za mwisho wamefunga mabao nane.

Mgombea Udiwani Ajitoa Chadema Ajiunga na CCM

$
0
0
Mgombea Udiwani Ajitoa  Chadema  Ajiunga na CCM
Chadema kimepata pigo baada ya mgombea wake wa udiwani Kata ya Manzase wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma, Mashaka Chalo kujiunga na CCM pamoja na wanachama wengine 131.

Chalo amehama Chadema siku ya tatu tangu chama hicho kikuu cha upinzani nchini kuzindua kampeni katika Kata hiyo na kunadiwa jukwaani na mbunge wa viti maalum, Kunti Majala.

Uchaguzi wa ubunge jimbo la Siha, Kinondoni na katika Kata 10 nchini utafanyika Februari 17, 2018. Uchaguzi katika Kata hiyo unafanyika baada ya aliyekuwa diwani, Peter Madanya (CCM), kufariki dunia mwishoni mwa mwaka jana.

Mgombea huyo amehamia CCM jana Februari 4, 2018 katika kijiji cha Manzase wakati wa uzinduzi wa kampeni za chama hicho na kupokewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Rodrick Mpogolo.

Mbunge wa Mtera (CCM),  Livingstone Lusinde amesema uamuzi wa Chalo kujiuzulu ni ushindi kwa chama tawala.

“Mpogolo unaweza kufungua kampeni hizi na kisha kuzifunga maana kazi imekwisha. Tulikuwa na  wagombea watatu, lakini kuondoka kwa huyu,  CCM tunaona kazi imekwisha. Wagombea wengine waliobaki  hata tukilala usingizi hakuna kitu ushindi ni wetu,” amesema.

Mgombea wa CCM katika Kata hiyo ni Amosi Mloha.

Lusinde amesema Chadema walimpitisha Chalo dakika za mwisho kuwania udiwani bila kujua kuwa alikuwa pandikizi la CCM.

Akizungumza katika mkutano huo Chalo amesema amerejea CCM kwa sababu ni chama chake na kimemlea.

Klabu ya Simba: Okwi Yuko Fiti Leo Ataungana na Wenzake Kwenye Mazoezi

$
0
0
Klabu ya Simba:  Okwi Yuko Fiti Leo Ataungana na Wenzake Kwenye Mazoezi
Uongozi wa Klabu ya Simba umesema hali ya mchezaji wao Emmanuel Okwi unaendelea vizuri huku wakidai kuwa jioni ya leo ataungana na wenzake kufanya mazoezi katika uwanja wa Boko Jijini Dar es Salaam.

Tarifa hiyo imekuja baada ya mchezaji huyo jana (Jumapili) kushindwa kumaliza mchezo dhidi ya Ruvu Shooting kutokana na kupata majeruhi kwenye shingo yake kwa kuchezewa ndivyo sivyo na mchezaji Mau Bodi.

Mbali na hilo, Emmanuel Okwi mpaka sasa ndio anayeongoza kwa ufungaji wa magoli kwa kupata 12 akifuatiwa na John Boco kwa mabao 9, nafasi ya tatu kushikwa na Habibu Kiyombo kutokea Mbao FC kwa magoli  8 huku wapinzani wao wajadi wakiwa nafasi ya tano kwa kuwakilishwa na Obrey Chirwa kwa magoli 7 pekee katika msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2018.

Kwa upande mwingine, timu ya Simba SC inatarajia kukichapa na Azam FC siku ya Jumatano (Februari 7, 2018) katika dimba la Taifa.

Viongozi wa CCM Bagamoyo Wamtupia Lawama Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze

$
0
0
Viongozi wa CCM Bagamoyo Wamtupia Lawama Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze
Ikiwa ni kipindi cha maadhimisho ya miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama cha mapinduzi ccm, viongozi wa chaa hicho wilayani Bagamoyo wamelalamika juu ya kutoridhishwa na utendaji kazi wa mkurugenzi wa halmashauri ya Chalinze na kwamba amekua kikwazo katika kuharakisha miradi ya maendeleo.

Akitoa malalamiko hayo mbele ya mwenyekiti wa Ccm wilaya ya bagamoyo ndugu Abdulzahoro Rashid katika sherehe za maadhimisho ya miaka 41 ya ccm zilizofanika katika ukumbi wa shule ya sekondari Lugoba,  diwani wa kata ya Lugoba bi Rehema Mwene amesema kumekua na hali ya sintofahamu kwenye mradi wa upanuzi wa kituo cha afya Lugoba uliotengewa shilingi milioni 400 ambazo zilitakiwa kutumika tangu mwezi januari redha ambazo mpaka sasa haijafahamika nini kimekwamisha .

   "Nimejitahidi kwa kushirikiana na uongozi wa kijiji cha lunga kuwahamasisha waanchi kujitolea kusafisha eneo la ujenzi huo na tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa sambamba na kushiriki kuchimba msingi lakini cha ajabu fedha ambazo zilishaletwa halmashauri bado hazifahamiki nini kimekwamisha kufika mahali husika" alisema diwani huyo

Mradi huo ambao umelenga kuongeza majengo ya Wodi ya mama na mtoto, nyumba ya mganga wa kituo, chumba cha kuhifadhia miili ya marehemu, Wodi ya wazazi pamoja na wodi ya watoto

Kwa upande wake mwenyekiti wa Ccm wilaya ya Bagamoyo ndugu Abdulzahoro Rashid amesema vitendo vya kuchelewesha miradi ya maeneleo sio vya kufumbia macho na yeye kama msimamizi wa ilani ya chama atahakikisha anakutana na mkurugenzi huyo kujua sababu za kuchelewa kwa kuanza kwa ujenzi huo lakini pia atamtaka mkurugenzi huyo kujitathmini juu ya malalamiko mengi yanayomkabili kutoka kwa viongozi na wananchi wa chalinze juu ya utendaji wake na ikibidi aombe kujiuzuru

"kuna haja gani ya kuendelea kumnyamazia kiongozi anayerudisha nyuma jitihada za Mh rais Magufuli kwa kuchelewesha miradi ya maendeleo kwa kweli hili ni bomu " alisema ndugu Zahoro

Aidha kwa upande mwingine mwenyekiti huyo ametangaza kuunda kamati maalum itakayohusika na kukagua mali zote za chama pamoja na kupitia mikataba yote iliyosainiwa na viongozi wasio wazalendo na atakayebainika atafikishwa katika mikono ya sheria

"chama kimekua kama shamba la bibi kila mtu anachuma na kujinufaisha mwenyewe, kuna watu tangu mwaka 2000 mpaka leo mikataba yao haijaisha na wanaangaliwa tu" aliongeza mwenyekiti ndugu Zahoro

Kamati hiyo inaongozwana mwenyekiti ndugu yahya Msonde pamoja na katibu wake ndugu boubakar Mlawa huku wajumbe wa kamati hiyo wakiwa ni Bolizozo (Mwenezi wa wilaya), Mkwayu Makota (M/kiti Uvccm), Latifa Kizota ambao mpaka sasa tayari wameanza kazi hiyo na wanaendelea na uchunguzi na baada ya siku 10 wanatarajia kukabidhi ripoti kwa mwenyekiti



Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo?

$
0
0

Matatizo haya yame kuwa yakiwaathiri watu wengi sana kisaikolijia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wenzao kwa kawaida mwanaume ana takiwa awe na uume kuanzia inch(6_8)vinginevyo mtu huyo atakuwa na matatizo.

Zipo sababu nyingi zinazo sababisha tatizo hilo baadhi ni upungufu wa vichocheo (Hormones za Getrogen) Ambazo mwanaume akisha balehe vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume, chango husababisha NEVA ambayo huathiri misuri ya uume. Ngiri ambayo Huleta maumivu ya tumbo kuunguruma na kujaa guess, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri , miguu kufa ganzi, maumivu ya kiuno,upigaji wa punyeto sababu hizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembaba na mara kwa mara hipelekea kupunguka kwa nguvu za kiume na ham ya tendo la ndoa hukosekana na kuisha kabisa

NSUMBU:__Ni dawa dawa inayo zalisha hormones za Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.

NZAGI :--Ni dawa bora ya kurudisha nguvu za kiume na kukupa hamu ya kurudia tendo la ndoa mara dufu utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara nne
(4)bila hamu kuisha (kuchoka) dawa hii ni tiba kamili kwa matatizo hayo. Dawa hii pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk(15_30)kwa tendo moja la ndoa dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji kuanzia miaka(18_90)wana ruhusiwa kuzitumia Pia tunatibu KISUKARI, PRESHA, PUMU, MALARIA SUGU, MIMBA KUHARIBIKA(Chango)

POWER :__Ni dawa ya mitishamba inaongeza hips, (makalio), miguu, ina punguza maziwa (chuchu). Ina toa harufu mbaya sehem za siri Nk.

Pia anazo dawa za mvuto wa mapenzi,biashara, kurudishwa kazini, kumuita aliye mbali kwa mda mfupi tu

OSTADH JUMA ANAPATIKANA MBANGALA ZAKHIEM SIMU: 0769-597778 au 0784-002216 au 0627457957 Wote mnakaribishwa

Kenya: Vituo viwili vya matangazo vya televisheni vyarejea hewani

$
0
0

Matangazo ya vituo viwili vya televesheni Kenya, KTN na NTV yamerejea hewani baada ya kufungiwa siku 7 na serikali.

Lakini bado haviwezi kutazamwa na Wakenya wengi ambao hawana king'amuzi.

Kupitia mtandao wao wa Twitter, NTV wamesema wamerudi hewani kwenye ving'amuzi vya "Dstv, GoTV and Zuku baada ya kufungiwa na serikali."

Stesheni ya iliyokuwa mmojawapo zilizoathirika na hatua ya serikali ,Citizen TV bado haijafunguliwa.

Serikali ilizifunga stesheni tatu za televisheni NTV, Citizen na KTN kwa madai kuwa vilipanga kupeperusha moja kwa moja matangazo sherehe ya kumuapisha kiongozi wa upinzani Raila Odinga kama rais licha ya onyo kutofanya hivyo.

Tutaendelea kuwaletea habari kadri zinavyotufikia.

Vanessa Mdee: Mimi na Diamond ndio tunaosikika Nigeria

$
0
0

Msanii wa muziki Bongo, Vanessa Mdee amesema muziki wa Afrika Mashariki haupewi nafasi kubwa nchini Nigeria kama inavyokuwa ikitazamiwa.

Muimbaji huyo ambaye yupo nchini humo kwa ajili ya kutangaza albamu yake ‘Money Mondays’ ameiambia Clouds Fm kuwa katika moja club alizopita alikuta ngoma zinazochezwa ni ya Patoranking na Diamond ‘Love You Die’ na ile aliyoshirikiana na Reekado ‘Move’.

“Hapa Nigeria haupo kabisa muziki wa Tanzania, haupo kwa nguvu ambayo unatakiwa kuwepo kwa sababu tunaelewa muziki wetu ni mkali, wasaniii wetu ni wakali. Kidogo wanauzito wa kupokea muziki wa East Africa, jana nilikuwa club nilisikia nyimbo za Tanzania ambazo zinapigwa ni ile Diamond na Patoranking na ya kwangu  na Reekado ‘Move’ hakuna nyimbo nyingine inapigwa hata ya Afrika Mashariki,” amesema.

Pia Vanessa amesema si kwamba hawatambui muziki kutoka Afrika Mashariki ni mzuri ila wameamua kuupa kipaumbele muziki wao na kutokana na idadi kuwa wasanii walionao inakuwa ni vigumu kwa muziki kutoka sehemu nyingine kupata nafasi.

Kuapishwa Kwa Raila Odinga Kenya Bado Kizungu zungu, Polisi Washindwa Kumpandisha Mahakamani Aliyeandaa Kuapisha

$
0
0

KENYA: Polisi wameshindwa kumfikisha Mahakamani kiongozi wa kundi la NRM, Miguna Miguna licha ya Mahakama Kuu kuamuru afikishwe leo saa nane mchana kufuatia kukamatwa kwake tangu siku ya Ijumaa
-
Aidha, Mahakama imewaamuru Mkuu wa Jeshi la Polisi(Joseph Boinnet) na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai(George Kinoti) kwenda Mahakamani hapo kesho saa tatu asubuhi na kueleza sababu za kutokufikishwa kwa kiongozi huyo
-
Miguna Miguna alikamatwa nyumbani kwake huko Runda kutokana na kushiriki kwake kuapishwa kwa kiongozi wa Upinzani, Raila Odinga.

Watumishi Wasiyoiunga Mkono CCM Kufukuzwa Kazi

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti amefunguka na kuwataka watumishi mbalimbali mkoani kwake ambao hawaiungi mkono Serikali ya awamu ya tano iliyopo chini ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuondoka mapema katika nafasi zao hizo.

Mnyeti amesema kuwa siku zote Chama Cha Mapinduzi ndiyo kimekuwa kikihangaika kuomba kura majukwaani huku viongozi mbalimbali wa chama hicho wakiwa si wanufaika wakubwa kulinganisha na watumishi, hivyo watumishi wanapaswa kutambua na kuiunga mkono Serikali ya CCM na kama hataki waondoke kwenye nafasi hizo. 

"Wanaoumia kuomba kura majukwaani ni CCM anayekuja kula ugali na familia yake ni wewe mtumishi, unanufaika wewe na familia yako. Sasa tumejipanga vizuri wale wote ambao siyo wenzetu watupishe mapema kabla ya uchaguzi, mimi ndiyo Mkuu wa Mkoa huu wa Manyara nasema hivi kama wewe huungi mkono Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ondoka mapema" alisisitiza Mnyeti

Offer ya Valentine Day..Ongeza Hips, Makalio na Imarisha Uume na Ongeza Hamu na Markson Products

$
0
0

OFFER YA VALENTINE DAY🎁
ONGEZA HIPS, MAKALIO, UUME, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA SASA.
KATIKA KUSHEREHEKEA MSIMU WA SIKUKUU (Valentine day) TUNA PUNGUZO LA 20% KWA BIDHAA ZETU ZOTE, IKIWA NI SHUKRANI KWA KUTUUNGA MKONO.
BIDHAA ZETU ZOTE ZIMETENGENEZWA KWA MIMEA NA MATUNDA HAZINA KEMIKALI WALA MADHARA.
KWA WANAUME TUNATIBU👇👇
☆Kukosa hamu ya tendo.
☆Kuwahi kufika kileleni na kushindwa kurudia tendo.
☆Maumbile madogo ya uume.
☆Kuchoka sana wakati wa tendo na uume kusinyaa nk.
@markson_beauty_pr tumeandaa tiba bora kabisa kama ifuatavyo:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @240,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 6.5 hadi 8 (wiki 2-3) @180,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @150,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @250,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @150,000/=
PIA KWA WANAWAKE WANAOPENDA KUWA NA MUONEKANO MZURI ZIPO ZA👇👇👇
1.Kuongeza hips, makalio na mapaja @200,000/=
2.Kushepu mguu (CHUPA YA BIA) @150,000/=
3.Kuwa mweupe bila sugu kwa:-
(a)mafuta @150,000/=
(b) Vidonge @170,000
4.Kurefusha nywele na kutokukatika ovyo @130,000/=
5.Kuongeza hips, makalio na mapaja kwa vidonge (YODI PILLS ORIGINAL) @230,000/=
6Kupunguza au kuongeza maziwa kuyasimamisha @150,000/=
7.Kubana uke na kuondoa uchafu ukeni @130,000/=
8.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri na garantii ili kukuhakikishia ubora na usalama wa bidhaa za MARKSON BEAUTY CO

Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444
na
0714335378
UTAPATA HUDUMA.
👉🏻OUR WEBSITE:- www.marksnbeuty.org
👉🏻INSTAGRAM PAGE:-
@markson_beauty_pr
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images