Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Mange Kimambi Avujisha Siri Nzito ya Ruge, Diamond, Kusaga na Mameneja wa Diamond

$
0
0

By Mange Kimambi

Story iko hivi. Mnaonijua toka enzi za uturn I think mtakuwa mnakumbuka kuwa nilishawahi kuwaambia kuwa meneja wa Diamond ni Ruge sio hao mashankupe kina Sallam.Hii ilikuwa ni siri kubwa mnoo. Ruge ndie aliekuwa meneja wa Diamond tangu Diamond anaanza mziki. Ruge ndio the brains behind success ya Diamond Platnumz. He is the mastermind ya career ya huyo mtoto.Ruge ndie aliewaomba Salaam na BabuTale wajifanye wao ndo mameneja wa Diamond. Si mnajua ingejulikan Diamond meneja wake Ruge Maneno yangekuwa mengi kuwa anabebwa na clouds and so forth. Ndo maana mnaona Diamond alikuwa anapata connection za collabo na wasaniii wa nje wengiii wakawa wanajifanya eti Sallam ndo anaetafuta hizo deals no it was all Ruge sabbau Ruge anajuana na hao watu wooote.Sasa miaka yoooote hii, Cut ya meneja aliekuwa anaila ni Ruge. Yani kila kazi aliyokuwa anafanya Diamond cut alikuwa anabeba Ruge then Ruge ndo anawapa chao kina Salaam na Babutale..

Hata Yamoto band meneja wao alikuwa Ruge sio BabuTale. Kama Aslay ataweza kuongea ukweli atawaambia Babutale alikuwa cover tu. Na ndo maana Yamoto Band waliblow up, na ndo maana Diamond aliblow up, It was all Ruge behind the scenes. Hata Lady Jaydee meneja wake alikuwaga Ruge.

Ngojeni niwaambieni kitu Ruge ana matatizo tena makubwa most ya matatizo la Ruge ni kwenye kuwanyenga wasaniii pesa. Hilo ndo tatizo la Ruge.Ila jamani naomba niwaambie Tanzania nzimaaaa kwenye entertainment industry hakuna kichwa kama Ruge. Jamani yule kaka sio mtu wa nchi hiii. Anajua entertainment.Na ndo maana Diamond alitulia na Ruge miaka yote hii, yawezekana Ruge alikuwa anamuonea cut yake ila mwisho wa siku alim-manage vizuri mnoo. Mimi nna ushahidi wa Ruge kumnyenga Diamond pesa. Mnakumbuka Diamond alisemaga kuwa Show kubwa aliyowahi kulipwa maisha yake yooote ni Diamonds are forever , jamani muongo ile show Diamond hakupewa hata senti na Ruge. Ile show mi mwenyewe kidogo ninyonyane macho na Ruge sababu alitaka kuniingiza mjini.Niliandaa ile show na Ruge Ila Diamond sababu Ruge meneja wake na anaona anapoifikisha career yake akawa anasema ile show ndo alillipwa sana.hayo ndo matatizo ya Ruge


Ila baadae Diamond alikuja kuwa mjanja akawa hakubali kabisa Ruge kumnyenga, wakawa wanaenda sawa. Anyways Diamond makes a lot of money so Ruge definitely alikuwa hamwibiii kihivyo. Na nawaambia 100% bila Ruge Diamond asingekuwa hapo alipo.

Okay nishawapa historia fupi ya Ruge na Diamond. Sasa tuende mbele kidogo.

Hii story ntakayotoa hapa nahisi hata Ruge na clouds nzima leo watapa msiba mkubwaaaa mnoooo.Joseph Kusaga ameamua kuivest pesa yake sehemu ingine. Na hiyo sehemu ni Diamond. Apparently ni kwamba Clouds kuna matatizo makubwa, na Ruge amekuwa dizaini kama anamsumbua Kusaga kuhusu ownership. Ukweli ni kwamba hakuna clouds FM bila Ruge Mutahaba. Ruge is the brains behind clouds. Ruge akiondoka cloudsleo, kesho tutawasahau . Jamani tumchukie tunavyotaka, hafai kuwa boyfriend wala mume wa mtu ila kwenye entertainment lets give credit where its due, the man is a fucking genius. Na kuna issue ya ownersship pale na Ruge nae anataka more sababu anaona ni kazi yake. As much as Ruge anawanyenga wasanii chao na yeye Clouds hawampi anachostahilo bila yeye Hakuna kitu. Ndo hivyo Kusaga slowly ana walk away from clouds. pia nimeambiwa kuna a lot of financial issue na clouds, madeni sijui kodi, na dadake Joseph .

Jamani ni hivi Hiyo Wasafi Radio and Wasafi TV Joseph Kusaga ndio owner by 80%, Diamond ana own 20%. All the investment ya Wasafi Radio na Wasafi TV amefanya kusaga. Hiyo wasafi online 95% owned by Joseph Kusaga. Diamond Karanga 100% owned by Joseph Kusaga. Chibu Perfume 100% owned by Johaina Kusaga, mke wa Joseph Kusaga. .
.
Clouds na Ruge sijui why wanagombana na Wasafi? Hapa Tatizo ni Joseph Kusaga. Bila Joseph Kusaga kusingekuwa na wasafi radio wala Wasafi TV. Ruge mwenyewe hii leo atapata shock na clouds nzima nahisi watapa msiba. Sababu they don’t know anaewafuck ni MD wao ambae ana believe while heartedly kuwa Clouds is going down. .

Jamani mpaka hiyo ofisi mpya ya wasafi Joseph Kusaga ndo kalipia kodi yoooote. .

Na ndo maana mnawaona kina Sallam wanamchokonia Ruge lakini kwa Kusaga wanatuliza pumbu zao. Ni sababu Kusaga ndo money roller.


At the end of the day, Jospeh Kusaga ndio anaeiletea completion clouds kisirisiri na ndio anaeiua clouds. .

Kwa hiyo wala tusidhani kuwa wasafi TV and Radio zitakuwa za mchezo mchezo, they will be biig. .

Alafu mnaambiwa Kusaga na Bashite wamekuwa mabesti balaaaaaaa. Yani Bashite hana Issue na clouds Issue yake ni Ruge na wake Shilawadu sababu Shilawadu ni watoto wa Ruge wale. So hii project mpya Bashite anaipongeza kwa mikono minne. Kawahakikishia vibalo and everything else.

So mnafki hapa ni Joseph Kusaga, yeye ndio ambae cause balaa lote hili alafu kakaa pembeni watu wanadhani hii ni vita ya wasafi na clouds. .

Sasa jiulize je Kina Salaam na BabuTale wanapata nini jinsi wanavyomtia upepo Diamond hili bifu na Ruge. Kumbukeni kina Sallam hawakuwa wanapata Cut ya umeneja. Cut ilikuwa ya Ruge then Ruge ndo anawapa wao.Na walikuwa wanaona kama Ruge anawalalia, ila wanashindwa kuelewa kuwa Ruge ndo aliewatoa, ruge ndo aliemfundisha Salaam kazi yooote ya umeneja Ruge ndo kafanya tunajua kwa kuwafanya mameneja hewa wa Diamond na Yamoto Band. Sasa kina Sallam wanamchochea Diamond sababu Diamond akiachana na Ruge jiulize Nani atakaekuwa Real manager wa Diamond na atakuwa anapokea cut yooote ya umeneja?? You guess it right? Salaam na BabuTale.... So huu ugomvi ni mzuri kwa mifuko yao, now hawatokuwa chini ya Ruge Tena watakuwa wanapokea chao choooote..

Anyways, Sijui Why Diamond nae anakubali kumpampiwa labda ndo hivyo madili ya Kusaga, huku Bashite, lakini Diamond ajue pia ana risk career yake. Mimi personally nimeona wanamuziki woooote waliokuwa managed na Ruge walipoachana na Ruge they went down!!! Anyways, labda Diamond itakuwa tofauti kwake. Alafu ni bora angeachana na Ruge kibinadamu, Diamond akumbuke Ruge alimpotoa na alipo leo. Hakufikishwa hapo na Sallam, BabuTale, Bashite wala Joseph Kusaga, alifikishwa hapo na Ruge Mutahaba.

Ruge anaboa na simpendagi sababu ya mambo yake ya Magufuli Ila Diamond anaweza kuja kujutia baadae... Na hapo mjue LiBashite ndo linampapu Diamond zaidi.... Sasa jiulize Bashite ataweza kum-manage Diamond in his career? Au wanadhani now Salaam ataweza kum-manage wakati before Salaama alikuwa anatumwa na Ruge

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba, Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521 

Diamond Amponza Askari Magereza

$
0
0
Diamond Amponza Askari Magereza
STAA wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, anadaiwa kumtia matatani askari magereza mmoja ambaye jina halikupatikana mara moja, Ijumaa Wikienda lilishuhudia mkanda mzima.

Ndani ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu katika Kitengo cha Ustawi wa Jamii, askari huyo alisahau kofia yake ya kazi yenye Krauni ya Bibi na Bwana kwenye kiti aina ya ‘benchi’ ambapo Diamond alipofika aliikalia, jambo ambalo ilielezwa kuwa si sawa kwa sheria za kiaskari.


Ijumaa Wikienda lilimshuhudia askari huyo akinyanyuka haraka kwenye benchi hilo kisha kumpisha Diamond na mwanasheria wake ambao walikaa na kuendelea na mazungumzo yao wakati mlinzi wa msanii huyo, Mwarabu Fighter akichukua sendoz za Diamond zilizokuwa zimekatika na kwenda kuzishona.

Wakati Mwarabu akichukua sendoz hizo, Diamond alishuhudiwa akirudi nyuma na kuikalia kofia hiyo yote bila kujua huku askari huyo akihaha kuitafuta kofia hiyo.

Hata hivyo, askari huyo alikuja kuiona na kofia hiyo baada ya Diamond kusimama, jambo ambalo liliwasababisha askari wenzake akiwemo mkuu wao kumuita na kumuonya mwenzao kuwa alikuwa amefanya kosa kubwa la kisheria za kipolisi.

Ijumaa Wikienda lilipotaka kujua kosa alilolifanya askari huyo lilimuuliza mmoja wa maafisa hao ambaye hakutaka kutajwa kwa kuwa siyo msemaji wa jeshi hilo ambapo alisema kuwa, kofia za askari ni sehemu ya sare na ni kosa kubwa kutoka mwilini mwa askari na kuchezewa kwa kujua au kutojua na raia wa kawaida.

“Kimaadili ya kazi ni sawa na bunduki ndiyo maana kijeshi ukiona askari amevuliwa kofia na mkuu wake, ujue huo ndiyo mwisho wa kazi yake. Maana yake anakuwa amepoteza sifa za kulitumikia jeshi.


“Huyo askari amshukuru Mungu kwa kupewa tu onyo, lakini angeweza kupoteza kabisa sifa ya kulitumikia jeshi la magereza,” alisema mmoja wa maafisa wa jeshi la magereza aliyeeonekana kuwa na cheo kikubwa tofauti na wengine.

"Nchi Yetu Imefika Mahali Pa Hovyo"- Msigwa

$
0
0
"Nchi Yetu Imefika Mahali Pa Hovyo"- Msigwa
Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini (CHADEMA), Peter Msigwa amefunguka na kudai nchi ya Tanzania imefika mahali pa hovyo kutokana na watawala kuiendesha nchi kwa mtazamo wao na sio kufuata sheria na kanuni zilizopo.

Msigwa ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa akimuombea ridhaa mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni Salum Mwalimu ili aweze kupata kura za ndio kwa wananchi hao siku ya kupiga kura ambapo mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Waziri Mkuu mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA, Mhe. Edward Lowassa , huku akisindikizwa na mameya na Wabunge mbalimbali kutoka UKAWA.

"Watawala wanaendesha nchi kwa 'personality' na badala ya sheria na kanuni. Kwa bahati mbaya sana wale ambao wanategemewa kusema, kukemea pamoja na kuonya wamekaa kimya. Lakini baadhi yetu tumeamua iwe mvua, jua, iwe mabomu ya polisi, vituo vya polisi hata gereza tutazungumza hatutoogopa mtu yeyote", amesema Msigwa.

Pamoja na hayo, Msigwa ameendelea kwa kusema "nchi ya Tanzania imefika mahali ambako kiongozi hawezi kusemwa, Mkuu wa Mkoa hata Spika wa Bunge".

Kwa upande mwingine, Msigwa amewaambia wananchi wa Jimbo la Kinondoni kwamba wakimuona Mbunge anajikomba komba serikalini basi watambue mtu huyo hatambui wajibu wake anaopaswa kuutekeleza au kuufanya.

Zitto Kabwe Amtembelea Lissu Ubelgiji Wateta Mazito

$
0
0
Zitto Kabwe Amtembelea Lissu Ubelgiji Wateta Mazito
Mbunge Kigoma Mjini (ACT- Wazalendo), Zitto Kabwe amemtembelea Tundu Lissu nchini Ubelgiji anakoendelea na matibabu ya viungo na saikolojia tangu Januari 7, 2018.

Lissu ambaye ni mbunge wa Singida Mashariki anapata matibabu hayo baada ya kushambuliwa kwa risasi  Septemba 7, 2017 akiwa nje ya makazi yake mjini Dodoma. Awali mbunge huyo alipatiwa matibabu katika Hospitali ya Dodoma siku hiyohiyo kabla ya kuhamishiwa Hospitali ya Nairobi alikotobiwa hadi Januari 6, 2018 alipohamishiwa Ubelgiji.

Katika picha mbalimbali zilizotoka jana Februari 11, 2018  ziliwaonyesha wawili hao wakiwa kwenye mwonekano tofauti wa mazungumzo.

Akizungumza na Mwananchi leo Februari 12, 2018, Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Mawakili Tanzania (TLS) amesema, “Zitto amekuja kunijulia hali na kwa ajili ya kubadilishana mawazo kuhusu hali ya nchi yetu kisiasa, kiuchumi na kijamii.”

Hata hivyo, Zitto ambaye ni Kiongozi wa ACT- Wazalendo amesema hawezi kuzungumza zaidi kuhusu kile walichoteta na Lissu huku akiahidi baadaye kutoa taarifa.

Mzee Mwinyi Afuta Kauli yake Iliyodumu kwa Miaka 30

$
0
0
Mzee Mwinyi Afuta Kauli yake Iliyodumu kwa Miaka 30
Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi amekiri kufuta kauli yake iliyodumu kwa takribani miaka 30 kuwa Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu na haitakaa ifanye vizuri kwenye michezo.


Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya awali kati ya Simba SC dhidi ya Gendarmerie ya Djibouti, baada ya mchezo alisema kiwango cha mpira nchini kwasasa kimekua hivyo anafuta kauli yake.

''Mchezo umekuwa mzuri na sasa nafuta lile neno (Tanzania ni kichwa cha Mwendawazimu anayejifunza kunyoa atunyoe sisi) lakini sasa sisi ndio vinyozi'', alisema.



Katika mchezo wa jana Simba SC iliibuka na ushindi wa mabao 4-0 hivyo kujiweka vizuri kwenye mchezo wake wa marudiano huko Djibouti. Yanga pia ilishinda dhidi ya St. Louis ya Shelisheli.

Yanga inayocheza klabu bingwa Africa itasafiri kwenda Shelisheli kwaajili ya mchezo wake wa marudiano Februari 20 huku Simba inayoshiriki Kombe la Shirikisho nayo itasafiri kuelekea Djibouti kwaajili ya mchezo wa Februari 20 au 21.

Aslay, Nandy Kuburuzwa Mahakamani

$
0
0
Aslay, Nandy Kuburuzwa Mahakamani
Wasanii wa kizazi kipya Aslay pamoja na mwanadada Nandy wanaoendelea kufanya vizuri na kibao chao cha 'Subalkheri mpenzi' wanatarajiwa kuburuzwa Mahakamani kutoka na kuimba wimbo huo bila ya ridhaa ya wahusika.


Hayo yameibuka baada ya mmiliki wa wimbo huo, Kikundi cha Tarab Asilia visiwani Zanzibar (Culture Music  Club) kudai pesa zilizotolewa jumla ya Tsh. 800,000 kama fidia za kutumia kazi hiyo hawazitambui hivyo wanajipanga kuwapeleka mbele ya Mahakama.

Akizungumza Katibu Mtendaji wa kikundi hicho, Taimur Rukuni Twaha, amesema wasanii hao kabla ya kuimba tena upya wimbo huo walipaswa kuonana na uongozi huo ili kukubaliana jambo ambalo hawakufanya hivyo.

"Walichokifanya Aslay na Nandy kwenda kwa waimbaji wetu na kuwapa kiwango hicho cha fedha kwetu tunaona hakikubaliki na wametoa kama zawadi tu kwa sababu thamani ya wimbo wetu haulingani na kiwango hicho. Kwa mujibu wa katiba ya kikundi chetu, ibara ya sita inaeleza nyimbo zote zilizoimbwa na kikundi ni mali ya kikundi na kwamba muimbaji, mtunzi na muweka sauti watakuwa na haki zao kupitia kikundi hicho", amesema Twaha.

Kwa upande mwingine, Twaha amesema msimamo wao utabaki pale pale wa kuwafikisha Mahakamani wasanii hao endapo watashindwa kutimiza masharti waliyopewa na uongozi wa kikundi hicho.

Chanzo: Nipashe

Rais wa Zamani wa Liberia Ashinda Tuzo ya Mwaka ya Mo Ibrahim

$
0
0
Rais wa Zamani wa Liberia Ashinda Tuzo ya Mwaka ya Mo Ibrahim
RAIS wa zamani wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf ameshinda tuzo ya mwaka ya Mo Ibrahim kwa Uongozi wa Afrika – ambayo hupewa viongozi wa Afrika ambao wameonekana kuwa na utawala mzuri.

Ellen Johnson Sirleaf amekuwa mwanamke wa kwanza barani Afrika kushika nafasi ya Urais mwaka 2006 na kumaliza muda wake mwezi uliopita baada ya kuhudumu kwa mihula miwili.

Kamati ya Utendaji ya tuzo ya Mo Ibrahim imesema Ellen Johnson Sirleaf ameonesha uongozi wa kipekee katika kukabiliana na changamoto zisizowahi kutokea katika awamu zake mbili za uongozi alipokuwa Rais wa Liberia.



Wakati aliposhinda uchaguzi wa Rais nchini humo mwaka 2005, nchi hiyo ilikuwa imegawanyika kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa miaka kadhaa na tuzo hiyo ya amani ilikuwa ni kwa ajili ya kumpongeza kusaidia kuiimarisha nchi hiyo.

Wakosoaji wake wamekuwa wakimkosoa kwa kuwa na upendeleo, kutokana na kuwachagua watoto wake katika nafasi za ngazi za juu na pia wanadai kuwa hakuchukua hatua za kutosha kupambana na rushwa.



Kamati yab utendaji ya Mo Ibrahimu imearifu kwamba inafahamu mapungufu yake, lakini imeamua kwamba anastahili kupata tuzo ya dola za kimarekani milioni 5.

Mjasiriamali Mwingereza mwenye asili ya Sudan Mo Ibrahim alianzisha tuzo hiyo mwaka 2007 kwa ajili ya kuwatunukia viongozi walionesha kazi nzuri wakati wa kipindi cha uongozi wao ndani ya bara la Afrika, amballo madikteta na watawala wadhalimu wamerudisha nyuma maendeleo ya bara hili.



Tuzo hii ambayo inapaswa kutolewa kila mwaka , kwa mara sita mfululizo ilishindwa kupata mtu, kutokana na viongozi kukosa sifa za kushinda tuzo hiyo.

Ellen Johnson Sirleaf atapata dola za Kimarekani milioni tano zitakazogawanywa kwa miaka kumi, na dola laki mbili kwa maisha yake yote.


Wadau wa Sheria, Hakiza Binadamu Wasikitishwa na Hatua za RC Makonda Kuwawajibisha Hadharani Watumishi wa Umma

$
0
0
Wadau wa Sheria, Hakiza Binadamu Wasikitishwa na Hatua za RC Makonda Kuwawajibisha Hadharani Watumishi wa Umma
Wadau wa sheria, haki za binadamu na wafanyakazi wameeleza kusikitishwa na hatua ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuwawajibisha hadharani watumishi wa umma.

Pia, wamebainisha kuwa mkuu huyo wa mkoa hana mamlaka ya kusimamisha shughuli za mabaraza ya ardhi ya kata kwa sababu yameundwa kisheria na utaratibu wa kuyaondoa lazima uwe wa kisheria.

Juzi, Makonda alipokea ripoti kutoka kwa wanasheria waliosikiliza kero za wananchi kwa uratibu wa ofisi yake.

Katika mkutano huo, Makonda aliwaita jukwaa kuu, wakuu wa idara ya ardhi na nyinginezo kutoka manispaa zote tano na kuwahoji kuhusu idadi ya migogoro na changamoto katika maeneo yao ya kazi.

Mkutano huo wa Makonda wa kutoa mrejesho kwa wananchi baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wanasheria ulifanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee na kurushwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha TBC 1 na redio ya TBC Taifa.

Mkuu huyo wa mkoa aliwahoji maswali mbalimbali maofisa waliokuwa wakiitwa mbele yake, ikiwa ni pamoja na kuwauliza ni vipi walipanda madaraja na kufikia wadhifa walionao.

Ni katika kuwahoji huko, mkuu wa idara ya ardhi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Paul Mbembela alianguka na kupoteza fahamu.

Kutokana na Mbembela kushindwa kutoa idadi ya migogoro ya ardhi iliyopo, Makonda aliagiza apangiwe kazi nyingine na aondolewe katika nafasi yake ya sasa.

Hata hivyo, mkutano huo wa Makonda haujapita hivi hivi kwani kuna baadhi ya wanasheria na wadau wametoa mtazamo wao.

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), Tumaini Nyamhokya amesema hakupendezwa na kitendo cha mtumishi kuitwa na kuulizwa maswali ya kitakwimu huku akizomewa na watu.

Alisema walishaionya Serikali kuhusu kuwadhalilisha wafanyakazi hadharani kwa sababu ni kinyume cha utaratibu. Alisema kama kuna makosa yamefanyika basi uchunguzi ufanyike kisha hatua ichukuliwe.

“Tucta tutalitolea tamko suala hili ndani ya siku mbili zijazo. Haya mambo hayakubaliki, mtu anaweza kupata magonjwa ya kudumu kwa sababu ya jambo dogo tu,” alisema kiongozi huyo wa Tucta.

Akizungumzia suala la kuwajibishwa hadharani kwa watumishi wa umma, Felix Kibodya aliyewahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) alisema (watumishi) wana mamlaka za kinidhamu za kuwawajibisha.

Alisema Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya mwaka 2004 imebainisha hatua za kinidhamu dhidi ya watumishi ambao wanakiuka maadili ya kazi.

Alisema watumishi wana haki pia ya kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa. “Haiwezekani jukwaani mtu akapewa adhabu palepale, vinginevyo utawala wa sheria hautakuwepo,” alisema Kibodya.

Alisema ipo mifumo rasmi ya kisheria ambayo inaruhusu mamlaka za kinidhamu kuchukua hatua.

Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRD), Onesmo Ole Ngurumwa alisema viongozi wanapaswa kuwa na maadili ya kuwawajibisha watu na kwamba jukumu hilo liko kwenye mamlaka ya kuajiri.

Ole Ngurumwa alisema mkuu wa mkoa alipaswa kuwasiliana na mkurugenzi wa halmashauri ili kumwadhibu mtu ambaye anadhani amekosea na si yeye mwenyewe jukwaani kuchukua hatua za kumwadhibu.

“Masuala ya kinidhamu yazingatie sheria ili kuepuka baadhi ya watu kuonewa. Mtumishi anatakiwa kupata muda wa kusikilizwa na kujitetea. Watumie mamlaka zinazoajiri ili zichukue hatua dhidi yao kama sheria inavyoelekeza,” alisema.

Mabaraza ya kata

Kuhusu kusimamishwa kwa mabaraza ya ardhi ya kata, Kibodya alisema yalianzishwa mwaka 1985 ili kushughulikia migogoro ya ardhi na halmashauri zilipewa jukumu la kuyasimamia.

Alisema mabaraza hayo yaliongezewa nguvu zaidi kwenye Sheria ya Ardhi ya Kijiji ya mwaka 1999 na Sheria ya Utatuzi wa Migogoro ya mwaka 2002, na mabaraza hayo yanasimamiwa moja kwa moja na Wizara ya Ardhi.

“Haiwezekani kesho mtu anakwenda kwenye Baraza la Kata anaambiwa mabaraza yamesimamishwa. Mambo ya kisheria hayawezi kuondolewa kwa matamko ya jukwaani,” alisema mwanasheria huyo.

Akizungumzia mabaraza hayo, Ole Ngurumwa alisema hizo ni taasisi ambazo zimeundwa kisheria na utaratibu wa kuzisimamisha ni lazima ufuate sheria hata kama watendaji wake hawatimizi wajibu wao.

Alisema wakuu wa mikoa na wilaya hawana jukumu katika mfumo wa utoaji haki na kwamba mahakama zinatakiwa kuwa huru bila kuingiliwa na mamlaka nyingine ya nje.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la CUF, Julius Mtatiro katika andiko lake juzi alisema huenda Makonda ana nia njema ya kutatua matatizo ya watu wa Dar es Salaam. Hata hivyo, alisema matatizo na migogoro ya ardhi ni masuala mtambuka yaliyoshindwa ndani ya mfumo wa uendeshaji wa nchi.

“Matatizo hayo na migogoro ya ardhi ni tatizo la nchi nzima na kwa kweli njia ya utatuzi wake bado ni Mahakama na njia za kisheria,” alisema.

Mtatiro alisema, “Hakuna namna mkuu wa mkoa au wilaya au waziri akawa na mamlaka ya kutoa haki ya ardhi kwa mtu fulani aliyeonewa, hilo likitokea bado wasioridhika watakimbilia mahakamani. Kwa hiyo Mahakama hazikwepeki.”

Alisema amri ya mkuu wa mkoa ya kusimamisha shughuli za mabaraza ya ardhi ya kata mkoani Dar es Salaam inakiuka sheria na Katiba na haitatui matatizo ya ardhi yaliyopo.

Alisema mkuu wa mkoa angeweza kutumia nafasi yake na kuishauri Serikali ipeleke mabadiliko ya sheria mbalimbali bungeni ili kufuta mabaraza ya ardhi ya kata na kuweka vyombo vingine ambavyo vitaonekana ni kufanya kazi.

Mtatiro alisema migogoro ya ardhi maeneo ya mijini na vijijini ni tatizo la sheria, mifumo na taasisi zilizopo.

“Ili utatue matatizo hayo, unahitaji Katiba Mpya ambayo itajenga misingi thabiti ya utoaji haki kwenye sekta zote, ikiwemo ardhi,” alisema.

Shigongo Ajipa Madaraka Ajiteua Kuwa Balozi wa Hospitali ya Muhimbili

$
0
0
Shigongo Ajipa Madaraka Ajiteua Kuwa Balozi wa Hospitali ya Muhimbili
Mjasiriamali, Mtunzi wa vitabu mashuhuri nchini Tanzania na mmiliki wa kampuni ya Global Publishers, Erick James Shigongo amefunguka na kujiteua mwenyewe kuwa balozi wa hospitali ya Muhimbili.


Shigongo amefikia maamuzi hayo baada ya kujionea mabadiliko makubwa katika utoaji huduma katika hospitali hiyo na kusema kuwa awali alikuwa anaichukia hospitali hiyo kutokana na mambo mbalimbali ya hovyo ambayo yalikuwa yakitokea kipindi cha nyuma kitu ambacho kwa sasa hakipo tena.

"Mimi Eric Shigongo James, Leo Februari 12, 2018, nimeamua kujiteua kuwa Balozi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, iliyopo Muhimbili jijini Dar es Salaam. Uamuzi huu nimeufikia kwa hiari yangu, bila kushinikizwa wala kuteuliwa na mtu yeyote, kwa sababu sina chembe ya shaka kwamba huduma zinazotolewa na taasisi hii ni bora, za kimataifa na zinaliletea sifa kubwa taifa letu. Nakiri kwa kinywa changu, Mungu shahidi yangu, kuwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na vitengo vyake vyote, imebadilika! Kwa hili nimshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli kwa kufanikiwa kupandikiza uzalendo, uadilifu na nidhamu ya kazi ndani ya mioyo ya Watanzania"

Aidha Shigongo amemuomba Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuendelea kuisaidia hospitali hiyo ya Muhimbili kwa ruzuku na vitendea kazi ili izidi kutoa huduma bora zaidi na kuokoa maisha ya Watanzania.

"Nimuombe, kwa mikono yote miwili, aiwezeshe hospitali hii kwa ruzuku, vifaa vya kutendea kazi na motisha kwa wafanyakazi ili iendelee kuokoa maisha ya Watanzania ambao wengi walikuwa wakifa kwa magonjwa ambayo yaliweza kutibika tu katika mataifa ya nje na si hapa nyumbani, jambo ambalo kwa hivi sasa halipo tena; kwani magonjwa makubwa ya moyo yanatibiwa hapahapa nyumbani na madaktari wetu wa Kitanzania"

Mbali na hilo Shigongo aliweka wazi jambo kuu lililomfanya yeye mwenyewe kujiteua kuwa Balozi wa Muhimbili

"Niliyoyashuhudia ndugu zangu ndiyo yamenifanya niamue kujiteua mimi mwenyewe kuwa Balozi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete pamoja na Hospitali ya Muhimbili, ndugu zangu Muhimbili imebadilika, si ile ya zamani, madaktari wanafanya kazi zao vizuri, wauguzi wanahudumia kwa kauli nzuri, dawa zipo ilimradi uwe na kadi yako ya bima, hakuna mbu Muhimbili kama ilivyokuwa zamani"

Sifanyi Kazi na Msanii Nisiyeendana Nami- Rosa Ree

$
0
0
Sifanyi Kazi na Msanii Nisiyeendana Nami- Rosa Ree
Msanii wa muziki Rosa Ree amesema ni vigumu kwa yeye kufanya kazi na msanii endapo haendani naye.

Rapper huyo anayetamba na ngoma yake mpya ‘Marathon’ amesema hayo wakati akieleza sababu ya kumshirikisha Bill Nass katika ngoma hiyo.

“Bill Nass kabisa ni mshakaji wangu, ni mtu ambaye tuna-vibe pamoja sana as person yeye ni poa sana na mimi napenda watu ambao wapo OG, cha pili mimi siwezi kufanya kazi na mtu ambaye sina vibe naye, mtu ambaye hana positive vibe,” Rosa Ree ameiambia Bongo5.

Ameongeza kuwa kuzaliwa kwa ngoma hiyo kulitokana na idea aliyokuwa nayo hapo awali na Bill Nass alipokuja na yake ikawa kazi rahisi kuikamilisha.

Habari Njema Kwako Dr. Kessy Nawaletea Products za Asili Zisizo na Chemikali

$
0
0


*PENDEZA NA KESSY PRODUCT* : WEKA MUONEKANO WAKO VIZUR SASA, NIWAUZA WA PRODUCT ZA ASILI NA MAFUTA YASIO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI KWA MATUMIZI NA MATOKEO NI KWAARAKA KUANZIA WEEK (2) HADI (4)🍌🍍🥑

1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 100,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK 100,000/(B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _100,000/
5)TOA KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _90,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_90,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_80,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_80,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MWILINI _100,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI AINAZOTE 100,000/(B)VIDONGE MAX MAN NA AINA NYINGI_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_130,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_100,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_80,000/(21) ENGEZA MGUU_100,000/ 21) TUDISH NYELE KWENYE KIPARA 150,000/ 22) DAW YA NGIRI YAKUVIMBA NA KULEGEA 100,000/🍍🍉🥑

TUNAPATIKAN DAR E SALAAM:PIA NJE YA NCHI TUNATUMA MIZIGO,NA KWA MIKOAN KOTE UTAPATA *KESSY* NI WAAMINIFU WA KUTUM MIZIGO NA KUFIKA KWA WAKATI PIGA CM (+255) 0719955528
0756259180
0785371237
@ *Pendeza_kessy_product*
Delivery POPOTE ULIPO,

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU.

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..
na mengi zaidi

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Kamishna wa Polisi wa Zanzibar Aapishwa Leo na IGP Sirro

$
0
0
Kamishna wa Polisi wa Zanzibar Aapishwa Leo na IGP Sirro
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro leo Februari 12, 2018 amemuapisha Kamishna wa Polisi (CP) Mohamed Hassan Haji kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar.

CP Haji aliyeteuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli hivi karibuni, pia amekula kiapo cha maadili ya uongozi wa umma mbele ya Katibu wa Viongozi wa Utumishi wa Umma, John Kaole. Akizungumza baada ya kumuapisha, IGP Sirro amemtaka CP Haji kushughulikia matukio yenye viashiria vya ugaidi na rushwa.

“Viashiria vya ugaidi maana yake, kuna matukio kwa ndani ukiangalia kuna muelekeo wa ugaidi, unyang’anyi kwa kutumia sialaha kama ujambazi kama viashiria, ili tatizo ni la dunia nzima, kwa sababu haya yana tutia mashaka, ndio maana ninamuagiza hilo nalo aliangalie akiwa kule, haya matukio ya ujambazi ya ugaidi yakoje ili tuyashughulikie kwa pamoja,” amesema.

Naye Katibu wa Viongozi wa Sekretarieti ya Maadili ya Utumishi wa Umma, John Kaole amemtaka CP Haji ajiepushe na vitendo vya ukiukwaji wa maadili ya utumishi wa umma ili kusitokee mgongano wa masilahi.

“Kazi zenu ni nyingi uwezekano wa kutokea kwa mgongano wa masilahi ni mkubwa, inabidi mjiepushe sana na ukiukwaji wa maadili kwa sababu unaweza kuleta mgongano wa masilahi lakini sina wasiwasi sababu mtazingatia kwa ukamilifu kwa sababu ni sehemu ya maadili ya maadili ya jeshi la Polisi,” amesema.

Kwa upande wake CP Haji ameahidi kutekeleza maagizo ya IGP Sirro na kusema, “IGP ndiyo kiongozi wa juu kwenye jeshi letu ametoa maelekezo ya vipaumblele kwa hivyo vipaumbele hivyo mimi nitashughulikia yale maelekezo yaliyotolewa pale ili watanzania kwa ujumla na wazanzibar waishi kwa amani wapate haki zao wanavyostahili.”

CP Haji alijiunga na Jeshi la Polisi mwaka 1991 na kupandishwa vyeo mbalimbali ikiwemo Mkaguzi wa Polisi, Mrakibu wa Polisi, Mrakibu Msidizi wa Polisi na Kamishna Msaidizi wa Polisi.

Zitto Aanika Mambo Waliyoteta na Tundu Lissu Ubelgiji

$
0
0
Zitto Aanika Mambo Waliyoteta na Tundu Lissu Ubelgiji
Jana Jumapili Februari 11, 2018 Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Mhe. Zitto Kabwe alimtembelea Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Mhe Tundu Lissu ambaye yupo kwenye matibabu nchini Ubelgiji.

Zitto Kabwe amesema kuwa walipokutana waligusia mambo makubwa matatu ambayo ni juu ya Gharama za matibabu yake, Suala la uchunguzi wa shambulio lake na maendeleo ya afya yake na mbinu za kuleta mabadiliko nchini.

Kuhusu suala la matibabu Mhe. Zitto Kabwe amesema Lissu anasikitika kuwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mpaka leo sio tu halimhudumii Lakini pia hata stahili zake za msingi kama Mbunge hapewi. Licha ya kutibiwa kwa misaada ya wasamaria wema, lakini ana mahitaji mengine kama mwanadam na wajibu kama mzazi. Sheria ya Bunge imeweka wazi kuwa Mbunge anapokuwa ametibiwa nje ya nchi Bunge humgharamia maisha yake.

“Suala la Gharama za matibabu yake.,Lissu anasikitika kuwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mpaka leo sio tu halimhudumii Lakini pia hata stahili zake za msingi kama Mbunge hapewi. Licha ya kutibiwa kwa misaada ya wasamaria wema, lakini ana mahitaji mengine kama mwanadam na wajibu kama mzazi. Sheria ya Bunge imeweka wazi kuwa Mbunge anapokuwa ametibiwa nje ya nchi Bunge humgharamia maisha yake.

Tangu Septemba, 2017 Bunge halijampa Mbunge wa Singida Mashariki haki zake za kisheria. Bunge limesukuma wajibu huo kwa Serikali, Wizara ya Afya na linasema kuwa linasubiri urasimu wa Serikali. Inasikitisha sana. Ikumbukwe kuwa mmoja wa wataalamu waliosaidia Lissu kupata huduma ya kuokoa maisha yake katika Hospitali ya Mkoa ya Dodoma, mara tu baada ya kupigwa risasi, ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya.

Mzunguko ambao unafanywa na Bunge kuhusu suala lililo wazi kabisa la kugharamia maisha ya Mbunge aliye kwenye matibabu linatia simanzi sana. Ninamsihi Spika wa Bunge, achukue hatua kwenye jambo hili, Bunge litimize wajibu wake kwa Mbunge wake kwa mujibu wa sheria. Kuendelea kuvuta miguu katika suala hili kunaleta hisia mbaya, na kunajenga taswira mbaya ya Bunge letu.“ameeleza Mhe. Zitto Kabwe kwenye taarifa yake kwa Vyombo vya Habari.

Akielezea mambo mengine waliyonena na Mwanasheria Lissu, Mhe. Zitto Kabwe amesema waligusia pia kuhusu kucheleweshwa kwa hatua za kiuchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana mnamo mwaka Septemba 7, 2017. Ambapo Lissu amewataka Watanzania waendelee kupaza sauti ili uchunguzi ufanyike na kuwakamata wahusika waliomshambulia.

“Suala la uchunguzi wa shambulio lake. Mpaka sasa ni miezi mitano imepita tangu Lissu ashambuliwe kwa risasi, na hakuna taarifa yeyote kuwa mamlaka za uchunguzi zimewakamata wahusika au kuonyesha tu juhudi za kuwatafuta wahusika. Jambo hili linatoa taswira mbaya sana juu ya vyombo vyetu vya uchunguzi, linajenga chuki na linaondoa imani ya wananchi kwa vyombo hivyo.

Ombi la Lissu kwangu ni kuwa tuendelee kupaza sauti ili uchunguzi ufanyike na kuwakamata wahusika waliomshambulia. Iwapo watu hawa hawatachukuliwa hatua wataendelea kuumiza watu wengine. Jeshi la Polisi linapaswa kueleza umma limekwama wapi kwenye uchunguzi wa tukio hili baya kabisa kuwahi kutokea katika nchi yetu, la mbunge kushambuliwa kwa risasi katika eneo la Bunge, akihudhuria vikao vya bunge.

Ni jambo la aibu kubwa kwa nchi yetu kuwa Mbunge anashambuliwa mchana kweupe na vyombo vya uchunguzi vinashindwa kufanya uchunguzi wa tukio hilo na kuwakamata wahusika. Kitendo cha Serikali kukataa kuchunguza shambulio hili ni ishara kuwa Serikali inawajua waliomshambulia Lissu, na hivyo imeamua kuwalinda. Jambo hili ni baya sana kwa ustawi wa haki katika nchi yetu.“ameeleza Zitto Kabwe.

Jambo lingine walilozungumzia ni kuhusu mbinu za kuleta mabadiliko nchini ambapo Zitto amesema ameambiwa na Mhe. Lissu kuwa Watanzania wapo tayari kwa mabadiliko ila kikwazo ni viongozi tu.

“Tulibadilishana mawazo na juu ya mbinu za mapambano ya kuleta mabadiliko nchini kwetu. Lissu ameniambia maneno yafuatayo “Wananchi wanajua wanataka nini, sisi Viongozi ndio tupo nyuma na Wananchi wapo mbele kimawazo. Jambo moja lipo wazi sana kwangu nalo ni kuwa sikati tamaa na Watanzania“amemaliza kwa kunukuu Zitto Kabwe.

Mnamo Januari 6, 2018 Mhe. Tundu Lissu alipelekwa nchini Ubelgiji akitokea Kenya alikokuwa anapatiwa matibabu hapo awali kwa ajili ya matibabu zaidi.

Tazama baadhi ya picha za Mhe. Zitto Kabwe alipomtembelea Mhe. Tundu Lissu hospitalini nchini Ubelgiji.



Wakili wa Maarufu wa Haki za Binadamu Akishwa Mahakamani

$
0
0
Wakili wa Maarufu wa Haki za Binadamu Akishwa Mahakamani
Moja ya habari zilizotufikia kutoka nchini Kenya ni pamoja na inayomhusu Wakili maarufu wa Haki za Binadamu Haron Ndubi ambaye amefikishwa Mahakamani asubuhi ya leo February 12, 2018.

Wakili Ndubi amefikishwa Mahakamani baada ya kubishana na Maaskari wa barabarani baada ya kukataa kufuata maelekezo aliyopewa na askari hao, tukio ambalo limetokea katika Barabara ya Jakaya Kikwete.

Inaelezwa kuwa Maaskari hao walimwagiza kupumua kwenye kifaa maalumu cha kupima dereva ana kiwango gani cha pombe mwilini kutokana na kuhisi kuwa Wakili huyo alikuwa akiendesha gari akiwa amelewa.

Hata hivyo ameachiwa kwa dhamana ya Ksh 30000 sawa na Tshs 67000.

Bashe Ajiweka Mtegoni Uchaguzi 2020

$
0
0
Bashe Ajiweka Mtegoni Uchaguzi 2020
Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Hussein Bashe amesema ikiwa atashindwa kutatua kero ya maji katika jimbo hilo hawezi kusimama na kuwaomba wananchi wamchague tena kuwa mbunge katika uchaguzi wa mwaka 2020.

Bashe ametoa kauli hiyo leo Februari 12, 2018 wakati akihojiwa katika kipindi cha 360 kinachorushwa na Kituo cha Televisheni ya Clouds.

Amesema Nzega Mjini tayari  miradi mbalimbali ya maji imeanza kutekelezwa na kwamba, hali ni tofauti tatizo lililopo hivi siyo kama ilivyokuwa miaka iliyopita.

Ameitaja miradi hiyo kuwa ni  mradi wa Ziwa Victoria ambao utawezesha kuwa na mtandao mpya wa maji wa kilomita 45 katika mji wa Nzega.

Amesema aliomba Sh460 milioni kwa Rais John Magufuli kwa ajili ya maji, kati ya hizo tayari amepatiwa Sh250 milioni.

Amebainisha kuwa fedha hizo zimetumika kufanya ukarabati wa chujio la maji na kufufua bwawa la maji la Uchami, hivyo kuwawezeaha wananchi kupata maji kwa mgawo mara mbili kwa wiki.

Pia, amesema Rais alipeleka Nzega Sh260 milioni nje ya bajeti ya halmashauri, ambazo zimetumika kujenga tangi lililopo Shule ya Msingi Nyasa na kujenga vituo vya maji katika maeneo mbalimbali ya Nzega.

Amesema miradi mingine ni ya visima 13 vinavyotumia umeme jua katika maeneo ambayo mradi wa maji wa Ziwa Victoria hautafika.

"Tunaamini miradi yote hii hadi 2020 itakuwa imekamilika, kwani mbali na hiyo  nilishaomba msaada Japan wa uchimbaji wa visima sita. Kama miradi hii yote haitakamilika sina haja ya kwenda kuwaomba kura wananchi wa Nzega,” amesema Bashe.

Haya Hapa Mapya ya Lulu Akiwa Gerezani

$
0
0
Haya Hapa Mapya ya Lulu Akiwa Gerezani
IKIWA ni takriban siku 85 tangu staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ aswekwe lupango katika Gereza la Segerea, Dar kwa kesi ya kumuua bila kukusudia msanii mwenzake, Steven Kanumba, mapya akiwa gerezani yameanikwa.



Mapya hayo yamebainika baada ya gazeti hili kutaka kujua kinachoendelea kwa sasa kwenye maisha ya Lulu ambapo Jumapili iliyopita, saa 6 mchana mwandishi wetu alitinga katika gereza hilo kwa lengo la kumuona na kuzungumza naye lakini alikumbana na vizingiti.



Akizungumza na mwandishi wetu, mmoja wa maafisa wa magereza aliyekutwa eneo la getini na kugoma kutaja jina lake akidai si msemaji alisema:

“Kwani wewe ni miongoni mwa wale wana familia wanaokuja kumuona? Hapa wanaoruhusiwa ni wale tu ambao ni wanafamilia vinginevyo labda uje nao.”



Hata hivyo, mwanahabari wetu alijaribu kumlainisha afisa huyo na kumuweka wazi nia yake ya kufika gerezani hapo ambapo ulifika wakati akafunguka mambo mbalimbali mapya kuhusu Lulu.

Alisema mrembo huyo kwa sasa ni shavu dodo, anaendelea vizuri na kifungo chake na tangu aingie gerezani, hajawahi kuugua.

“Yani kwa kweli amenenepa kabisa tofauti na hata alivyokuja. Anaendelea vizuri na hajawahi kuugua ugonjwa wowote tangu afike,” alisema ofisa huyo.



AWASHANGAZA WANAOMTEMBELEA

Chanzo hicho kiliendelea kufunguka kuwa, mbali na kutoumwa na kunenepa, muda wote mrembo huyo amekuwa mtu wa kutabasamu na kuwatia moyo wanaokwenda kumsalimia, jambo ambalo linawashangaza kwa sababu huwa wanahuzunika huku yeye akijiamini na kuwafariji.



“Anawashangaza kwa kweli ndugu zake ambao wanakuja kila wiki kumuona, yani yeye anakuwa na furaha, anawapa moyo utafikiri yeye ndio yupo sehemu nzuri kuliko ndugu zake,” alisema ofisa huyo na kuongeza:

“Huyu binti kwa kweli sasa hivi anasali sana. Na mara nyingi huwa namsikia akiwaambia ndugu zake kuwa wasihuzunike, wachukulie kama tu yupo shule ya boarding atatoka tu.”


Muna.

MUNA AFUNGUKA

Amani lilimtafuta na kufanikiwa kukutana na rafiki ambaye ni kama ndugu kwa familia ya Lulu, Rose Alphonce ‘Munalove’ ambaye alipoulizwa kuhusu mabadiliko hayo makubwa ya Lulu na kwamba amekuwa akiwafariji wanapokwenda kumtembelea, alikiri kuwa ni kweli.

“Ni kweli anatushangaza hata sisi, kwanza kanenepa na anaonekana mwenye furaha maana wakati mwingine tukienda kumuona tunakuwa na simanzi lakini yeye anakuwa mfariji wetu akisema kwamba ipo siku atatoka na kuwa huru tena,” alisema Muna ambaye inadaiwa kila wiki lazima amtembelee Lulu gerezani.



MSIKIE MAMA LULU

Alipopigiwa simu mama Lulu, Lucresia Kalugira ili kueleza juu ya hali halisi ya mwanaye huyo, alitokwa povu huku akidai kwamba hataki kusikia magazeti.

“Sitaki kusikia habari za magazeti au waandishi wa habari maana mimi siyo supastaa na kuhusu mwanangu naombeni mmuache maana tayari yupo gerezani,” alisema mama Lulu.



TUMEFIKAJE HAPA?

Itakumbukwa kuwa hukumu ya Lulu kutumikia kifungo cha miaka miwili ilitolewa Novemba 13, mwaka jana na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Sam Rumanyika baada ya mahakama kujiridhisha kuwa aliua bila kukusudia.



CHANZO CHA KESI YAKE

Lulu alihukumiwa baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kumuua bila kukusudia, muigizaji Kanumba aliyepoteza maisha Aprili 7, 2012, baada ya kutokea ugomvi kati yao majira ya usiku wakiwa nyumbani kwa marehemu, Sinza-Vatican, jijini Dar es Salaam.

Mchezaji wa Azam Augua Ghafla Atolewa Kwenye Kikosi

$
0
0
Klabu ya Mabingwa Afrika Mashariki na Kati, Azam FC imemuondoa mchezaji wake Yahya Zayd kwenye kikosi kinachotarajiwa kucheza leo dhidi ya Kagera Sugar FC baada ya kuugua ghafla mchana huu.

Hayo yamebainishwa na taarifa iliyotolewa na klabu hiyo na kusema nafasi yake itachukuliwa na mshambuliaji Mbaraka Yusuph ambaye alipaswa kuanzia kutokea benchi.

Mechi hiyo ya Azam FC ni muendelezo wa michuano ya VPL mzunguko wa 18 ambao utapigwa katika dimba la Kaitaba mkoani Kagera.

Uwanja wa London Wafungwa Baada ya Bomu la Vita vya Pili vya Dunia Kupatikana

$
0
0
Uwanja wa London Wafungwa Baada ya Bomu la Vita vya Pili vya Dunia Kupatikana
Uwanja wa ndege wa mjini London umefungwa baada ya bomu la vita vya pili vya dunia kupatikana kwenye mto ulio karibu wa Thames.

Uwanja huo utafungwa siku nzima na safari zote za ndege kufutwa, na kuwaathiri hadi abiria 16,000.

Bomu hilo liligunduliwa siku ya Jumapili eneo la George V wakati wa shughuli ya kikazi mashariki mwa London.

Uwanja huo ukafungwa na polisi wanasema kuwa wanashirikiana na jeshi la wanamaji kuondia bomu hilo.

Abiria wameambiwa wasisafiri kwenda uwanja huo na kushauriwa kuwasiliana na mashirika yao ya ndege.

"Uwanja wa ndege unashirikiana kabisa na polisi wa Met na jeshi la wanamaji kuliondoa bomu hilo kwa njia salama na kutatua suala hilo haraka iwezekanavyo," alisema Robert Sinclair, mkurugenzi mkuu wa uwanja huo.

Ndege zinazotumia uwanjai huo wa London City ni pamoja na British Airways, Flybe, CityJet, KLM na Lufthansa kwa safari za ndani na kwenda nchi zingine zaUlaya.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images